WATALI 54 KUTOKA CHINA WASHIRIKI TAMASHA LA KUPANDA MLIMA KILIMANJARO

December 28, 2023

 Pamela Mollel ,Arusha


Watalii zaidi 54 kutoka nchini China wamewasili Mkoani Arusha kwaajili ya kushiriki Tamasha la kupanda Mlima Kilimanjaro

Akizungumza katika hafla ya kuwapokea watalii hao,Mkuu wa Mkoa wa Arusha John V.K Mongella alisema ujio huo umetokana na mahusiano mazuri kati ya Tanzania na China

Alisema kuwa msimu wa mwisho wa mwaka ni msimu mzuri zaidi kwa kupanda mlima Kilimanjaro hali itakayowafanya wafurahi zaidi lakini pia kutangaza Tanzania kupitia mlima huo

Pia Mh.Mongella aliwatunuku vyeti vya pongezi kwa uamuzi mzuri wa kuja kupanda mlima Kilimanjaro ambao ni mlima mrefu zaidi Duniani

"Nawapongeza sanaaa kwa ujio wenu naamini mtafurahia sanaaa tamasha la kupanda mlima Kilimanjaro lakini pia niwapongeze kampuni ya kitalii ya Gosheni Safari kwa kuandaa tamasha hili"alisema Mongella

Ikumbukwe kuwa ujio wa watalii hao ni matokeo ya Filamu ya Royal Tour iliyoongozwa na Rais MaMa Samia Suluhu Hassan




 

 

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »