Pamela Mollel ,Arusha
Watalii zaidi 54 kutoka nchini China wamewasili Mkoani Arusha kwaajili ya kushiriki Tamasha la kupanda Mlima Kilimanjaro
Akizungumza katika hafla ya kuwapokea watalii hao,Mkuu wa Mkoa wa Arusha John V.K Mongella alisema ujio huo umetokana na mahusiano mazuri kati ya Tanzania na China
Alisema kuwa msimu wa mwisho wa mwaka ni msimu mzuri zaidi kwa kupanda mlima Kilimanjaro hali itakayowafanya wafurahi zaidi lakini pia kutangaza Tanzania kupitia mlima huo
Pia Mh.Mongella aliwatunuku vyeti vya pongezi kwa uamuzi mzuri wa kuja kupanda mlima Kilimanjaro ambao ni mlima mrefu zaidi Duniani
"Nawapongeza sanaaa kwa ujio wenu naamini mtafurahia sanaaa tamasha la kupanda mlima Kilimanjaro lakini pia niwapongeze kampuni ya kitalii ya Gosheni Safari kwa kuandaa tamasha hili"alisema Mongella
Ikumbukwe kuwa ujio wa watalii hao ni matokeo ya Filamu ya Royal Tour iliyoongozwa na Rais MaMa Samia Suluhu Hassan
EmoticonEmoticon