TAKUKURU TANGA YAWAPANDISHA KIZIMBANI WATUHUMIWA WA MAKOSA YA RUSHWA NA UHUJUMU UCHUMI

June 30, 2023





TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa TAKUKURU mkoani Tanga imewapandisha kizimbani watuhumiwa wane(8)kwa makosa ya rushwa na uhujumu uchumi na kuisababisha Serikali matumizi batili ya zaidi ya shilingi milioni 28.

Waliopandishwa kizimbani ni William Nguluko Mwalimu Mkuu Shule ya Msingi Mabokweni jijini Tanga ambaye anakabiliwa na ashitaka la ubadhirifu na ufujaji kinyume na kifungu cha 28(1)(2) sharia na kuzuia na kupambana na rushwa sura ya 329 marejeo ya mweka 2022.

Kosa jingine ni kula njama , kutenda makossa ya rushwa kinyume na kifungu na kifungu 32 sheria ya kuzuia na kupambana na rushwa , kuisababishia hasara serikali kinyume na aya ya 10(1) ya jedwali la kwanza na kifungu cha 57(1) na 60(2) sharia ya uhujumu uchumi sura ya 200 marejeo ya mwaka 2002.

Mshitakiwa wa pili ni Sudi Mshamu, mwalimu wa fedha katika shule hiyo , ambaye yeye anakabilwa na na makosa 31 likiwemo kosa la kughushi kinyume na kifungu cha 333,335(111) na 338,340(2)A sharia ya kanuni ya adhabu sura ya 16 marejeo ya mwaka 2022.

Kosa jingine ni kula nyama kinyume na kifungu cha 32 sheria ya kuzuia na kupambana na rushwa sura ya 329 marejeo ya mwaka 2022 ikisomwa pamoja na aya ya 21 jedwali la kwanza na kifungu cha 57 (1) na kifungu cha 60(2) sharia ya uhujumu uchumi sura ya 200 marejeo ya mwaka 2020.

Mtuhumiwa wa tatu, Mwanabakari Adhumani aliyekuwa mwenyekiti wa kamati ya shule hiyo anashitakiwa kwa tuhuma ya kula njama kifungu cha 32 ,sheria ya kuzuia na kupambana na rushwa sura ya 329 marejeo ya mwaka 2022.

Kosa jingine ni kuisababishia hasara serikali kinyume na aya ya 10(1) jedwali la kwanza na kifungu cha 57(1) na 60(2) sharia ya uhujumu uchumi sura ya 200 marejeo ya mwaka 2022.

Mshitakiwa wa nne ni Yusuph Mushi mwalimu wa shule ya sekondari Saruji ambaye kati ya makossa yanayomkabili ni kula nyama kinyumea na kifungu cha 32 sheria ya kuzuia na kupambana na rushwa sura ya 329 marejeo ya mwaka 2022 ikisomwa pamoja na aya ya 21 jedwali la kwanza na kifungu cha 57 (1) na 60(2) sharia ya uhujumu uchumi sura ya 200 ya mwaka 2022,mshitakiwa alikiri kutenda kosa hilo.

Mbele ya hakimu wa Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Kakimu Mkazi Tanga Sophia Masati mtuhumiwa wa kwanza amekataa kutenda kosa hilo,wakati wa pili mwalimu wa fedha amekiri kutenda kosa hilo na mshitakiwa wa tatu naye amekataa kutenda kosa hilo wakati mshitakiwa wa nne amekiri kutenda kosa hilo.Washitakiwa hao wamerudishwa rumande na kesi yao itawajwa tena Julay 7 mwaka huu.

CCM TANGA- WANAOPINGA UWEKEZAJI WA DP WORLD KATIKA BANDARI YA DAR ES SALAAM NI MAADUI WA MAENDELEO NCHINI

June 30, 2023
 Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Tanga Comred Rajabu Abdurhaman akizungumza  wakati wa dua maalumu iliyofanywa na waumini dini ya Kiislamu katika Taasisi ya Tamta kwa ajili ya kumuombea Rais Dkt Samia Suluhu iliyodhuriwa pia na Mkuu wa Mkoa wa Tanga Waziri Kindamba.
Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Tanga Comred Rajabu Abdurhaman akizungumza  wakati wa dua maalumu iliyofanywa na waumini dini ya Kiislamu katika Taasisi ya Tamta kwa ajili ya kumuombea Rais Dkt Samia Suluhu iliyodhuriwa pia na Mkuu wa Mkoa wa Tanga Waziri Kindamba.

MKUU wa Mkoa wa Tanga Waziri Kindamba akizungumza wakati wa dua hiyo maalumu
Mkuu wa Mkoa wa Tanga Waziri Kindamba katika akiwa kwenye dua hiyo wa kwanza kushoto ni Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Tanga Rajab Abdurhaman
Waumini wa dini ya Kiislamu katika Taasisi ya Tamta wakimsikiliza Mwenmyekiti wa CCM Mkoa wa Tanga Rajab Abdurhaman mara baada ya kumalizika Dua Maalumu ya Kumuombea Rais Dkt Samia Suluhu
Na Oscar Assenga, TANGA

CHAMA cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Tanga kimesema kwamba watu wanaopinga uwekezaji wa Kampuni ya DP World katika Bandari ya Dar es Salaam  ni maadui wakubwa wa maendeleo ya watanzania hivyo wanatakiwa kupuuzwa.

Kauli hiyo ilitolewa leo na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Tanga Comred Rajabu Abdurhaman wakati wa dua maalumu iliyofanywa na waumini dini ya Kiislamu katika Taasisi ya Tamta iliyodhuriwa pia na Mkuu wa Mkoa wa Tanga Waziri Kindamba.

Aliisema kwamba siri za uadui huo wanazo wenyewe na waliyoyatamka ni sehemu ya uadui wao hivyo wao kama viongozi wa dini ni wajibu wao kuendelea kumuombea Rais Dkt Samia Suluhu kila mmoja kwa wakati wake mpaka maadui wote waweze kuteketea.

Aidha alisema lengo la Rais ni nzuri katika kuisaidia nchi hivyo hizo kelele wanazozisikia kila kona ni za maadui kuhusu uwekezaji wa Bandari ya Dar ambako viongozi wenyewe pia hufafanua kwamba hakuna Bandari inayouzwa na uwekezaji haufanyika kwenye Bandari zote.

Mwenyekiti huyo alisema uwekezaji huo unafanyika sehemu tu na awali pia waliokuwepo wazungu wa kampuni ya TICTS walifanya shughuli zao kwa muda wa miaka 22 lakini viongozi wa ngazi za juu ikiwemo Rais, Makamu, Waziri Mkuu na wengine waliona hapana lazima kufanyike uwekezaji mkubwa kwenye Bandari.

Alisema uwekezaji huo unafanyika ili ziweze kupatikana fedha nyingi za kuendesha nchi kama alivyofanya TICTs ndio wanakuja kuyafanya DP World isipokuwa wao wanakuja kuboresha zaidi ili manufaa yapatikane hivyo tatizo lipo wapi huo ni aadui ni mkubwa kwa Rais kwa watu wachache.

Mwenyekiti huyo alisema ila watanzania wengi humuombea Rais ili aweze kutimiza lengo la kusaidia nchi ili kila mtu aishi kwa amani na hivyo kupata maendeleo makubwa katika maendeleo nchini ikiwemo barabara mzuri,dawa pamoja na huduma nyengine za msingi.

“Nimefarijika sana kwa mwaliko huo tulioupata kwenye dua maalumu ya kumuombea Rais Dkt Samia Suluhu na tunamuomba Mwenyezi Mungu amuweke mbali na mahasidi na maadui wasioitakia mema nchi yetu”Alisema

Alisema kwamba uongozi ni dhamana kubwa sana wanaona rais juhudi kubwa kuisaidia jamii waislamu na wasio wasilamu hivyo ni wajibu wetu sote kumuombea dua kweli kweli wao waislamu wajitahidi kumombea Rais na wanafahamu lengo lake ni nzuri.

Hata hivyo alisema lakini wapo watu ambao wamethubutu wanadiriki kumbagua kwa sababu katokea visiwani lakini hawajui huko ni sehemu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Rais yupo kwa mujibu wa Katiba ya Tanzania,

Awali akizungumza Mkuu wa Mkoa wa Tanga Waziri Kindamba alisema kwamba wanamuombea Rais Samia kutokana na juhudi kubwa anazofanya za kimaendeleo hapa nchini.

Alisema kwamba mkoa wa Tanga ni miongoni mwa mikoa ambayo inamatumkizi ya dawa za kulevya hivyo katika majumba yetu hakuna mtu hata mmoja ambaye hajaathiriwa na dawa za kulevya kama sio ndugu itakuwa ni jamaa au rafiki.

Mkuu huyo wa mkoa alisema mapambano ya madawa ya kulevya wataendelea nayo kuhakikisha yanakoma na mkoa huo hauendelei kuwa na historia ya dawa hizo kupita mkoani hapa.

Mwisho.


DC TANGA ATOA NENO KWA WASTAAFU KUHUSU MATAPELI

June 30, 2023
MKUU wa wilaya ya Tanga Hashim Mgandilwa akizungumza wakati akifungua Semina kwa Wanachama wanaotarajia kustaafu Jijini Tanga iliyoandaliwa na Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF)
MKUU wa wilaya ya Tanga Hashim Mgandilwa akizungumza wakati akifungua Semina kwa Wanachama wanaotarajia kustaafu Jijini Tanga iliyoandaliwa na Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF)
Meneja wa Mafao wa Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) Makao Makuu James Oigo akizungumza wakati wa semina hiyo kulia ni Mkuu wa wilaya ya Tanga Hashim Mgandilwa akifuatia na Meneja wa Pensheni wa NSSF Makao Makuu Nancy  Mwangamilo na Afisa na kushoto ni Meneja wa Huduma kwa Wateja wa Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) Cosmas Kadeghe na wa kwanza kulia ni  Afisa Mkuu wa Idara ya Matekelezo wa NSSF Mkoa wa Tanga Abubakari Mshangama 
Meneja wa Mafao wa Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) Makao Makuu James Oigo akizungumza wakati wa semina hiyo kulia ni Mkuu wa wilaya ya Tanga Hashim Mgandilwa akifuatia na Meneja wa Pensheni wa NSSF Makao Makuu Nancy  Mwangamilo na Afisa na kushoto ni Meneja wa Huduma kwa Wateja wa Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) Cosmas Kadeghe na wa kwanza kulia ni  Afisa Mkuu wa Idara ya Matekelezo wa NSSF Mkoa wa Tanga Abubakari Mshangama
Afisa Mkuu wa Idara ya Matekelezo wa NSSF Mkoa wa Tanga Abubakari Mshangama akizungumza wakati wa semina hiyo kushoto ni Meneja wa Pensheni wa NSSF Makao Makuu Nancy  Mwangamilo akifuatiwa na Mkuu wa wilaya ya Tanga Hashim Mgandilwa ,Meneja wa Mafao wa Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) Makao Makuu James Oigo na  Meneja wa Huduma kwa Wateja wa Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) Cosmas Kadeghe  
Meneja wa Pensheni wa NSSF Makao Makuu Nancy  Mwangamilo akisisitiza jambo wakati wa semina hiyo
Meza kuu wakifuatilia matukio mbalimbali

Sehemu ya wanachama wanaotarajiwa kustaafu Jijini Tanga wakiwa kwenye semina hiyo  
Sehemu ya wanachama wanaotarajiwa kustaafu Jijini Tanga wakiwa kwenye semina hiyo
Meneja wa Benki ya NMB tawi la Ngamiani Elizaberth Chawinga kulia akifuatilia semina hiyo
Picha ya Pamoja 



Na Mwandishi Wetu, Tanga

MKUU wa wilaya ya Tanga Hashim Mgandilwa amefungua Semina kwa Wanachama wanaotarajia kustaafu Jijini Tanga iliyoandaliwa na Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) huku akitoa wito kwa wastaafu hao kuhakikisha wanafanya uwekezaji mapema ikiwemo kuepukana na magenge ya matapeli

Mgandilwa aliyasema mwishoni mwa wiki wakati akifungua semina hiyo kwa wanachama wanaotarajiwa kustaafu Jijini Tanga iliyoandaliwa na mfuko ambapo pia aliwataka kuepukana na magenge ya matapeli ambao wanahaingaika kuwashawishi kufanya biashara ambazo mlengo wao ni kwenda kuwaibia

Alisema kwamba kuna tabia ambayo imeibuka kwamba wafanyakazi wanapokaribia kustaafu lipo genge la matapeli ambalo limekuwa likijitokeza na kuwashawishi kufanya biashara ambazo mwisho wa wiki zinapelekea kuwaibia fedha ambazo wanakuwa wamezipata kama mafao yao.

“Katika Jambo hilo niwaase wastaafu tuweni makini sana na watu wa namna hii maana tunaweza kujikuta tunapoteza fedha zetu na mwisho wa tukajuta hivyo niwaase katika kipindi cha kuelekea kustaafu ni vema tukaanza maandalizi ikiwemo uwekezaji wenye tija”Alisema Mkuu huyo wa wilaya.

“Niwapongeze NSSF kwa kazi nzuri changamoto zinazowakumba watu wanaokaribia kustaafu kuna watu ambao ni genge la matapeli wanahaingaika kuwashawishi kufanya biashara ambazo mlengo wake ni kwenda kuwaibia hivyo niwasihi hakikisheni mnakuwa makini na watu wa namna hii”Alisema

Mkuu huyo wa wilaya pia alitumia wasaa huo kuwaasa kuhakikisha wanafanya maandalizi ya kustaafu kabla ya muda wa kustaafu lakini pia ni vema kuendelea kukumbushana kuna biashara ambazo zinaibuka kwenye msimu wa watu wanapokuwa wakitaka kustaafu hivyo nitoe rai kwa wastaafu kuona umuhimu wa kuhifadhi fedha wanazozipata.

Alisema licha ya kuhifadhi fedha hizo ni vema wawekeze kwenye maeneo yenye tija kwenye fedha lakini wakumbuke kuchagua marafiki kwenye kipindi hicho kutokana na kwamba wakati huo wapo ambao wanaweza kuibuka wakiwa na nia mbaya.

Awali akizungumza wakati wa semina hiyo Meneja wa Mafao wa Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) Makao Makuu James Oigo alisema kwamba semina hiyo ni muhimu kutokana na kwamba ni maandalizi ya kustaafu kwa wafanyakazi ambao wanatarajiwa kustaafu lengo kubwa kuwaandaa kueleza dhana nzima ya hifadhi ya Jamii nafasi ya mfuko wa (NSSF) katika maisha yao baada ya kustaafu.

Alisema pia na jinsi ambavyo wanatakiwa wajiandee kwa ajili ya kupata mafao yao na namna watakavyotumia mafao yao katika maisha yao baada ya kustaafu ikiwemo kuwaondolea hofu ambayo jamii inayofikiri hakuna maisha baada ya kustaafu.

Alisema kwamba wanataka kuwapa elimu na kuwajenga kisaikolojia kwamba maisha yapo na NSSF ina nafasi kubwa sana kwenye maisha yao kwa kila pensheni wanayoipata kila mwezi na elimu hiyo imekuwa ikitolewa kwa mikoa yote nchini .

Naye kwa upande wake Mwanachama Mstaafu wa Mfuko wa NSFF Mkoani Tanga Martha Kazala alisema kwamba wanaushukuru mfuko huo na kwamba wanapokea pensheni kila mwezi na haina matatizo yoyote.

Alisema kwenye ustaafu wake ana miaka saba na anafurahia maisha yake kwa sababu yanamsaidia katika maisha yao watu wanafikiria ukiajiriw ukitoka kazini wanadhani hakuna maisha yanayoendelea baada ya kustaafu maisha ni mazuri kubwa inatakiwa uwe mvumilivu wakati wa ajira ili uweze kufanikiwa kwenye masuala la ustaafu na malipo ya pensheni.

Hata hivyo aliwataka waajiriwa wanaotarajiwa kusfaafu wajipange ili wanapopata fedha wafanye maamuzi yaliyokuwa na busara ya mipangilio ikiwemo kuepukane na vishiwsihi sambamba na kufuata maelekezo ya mifuko ya hidadhi za jamii ili waweze kuishi vema



WAZIRI AWESO AAHIDI KUSHIRIKIANA NA MBUNGE SALIM KUMALIZA TATIZO LA MAJI ULANGA.

June 27, 2023

Mbunge wa Jimbo la Ulanga (CCM) Mhe Selim Alaudin kulia akizungumza na Waziri wa Maji Jumaa Aweso



Waziri wa Maji Jumaa Aweso(Mb) amemuahidi Mbunge wa Jimbo la Ulanga Mhe.Salim Alaudin Hasham kuwa atatoa ushirikiano wa kina yeye na ofisi yake katika mapambano ya kuhakikisha wilaya ya Ulanga inamaliza Changamoto ya upatikanaji wa maji safi na salama.


Waziri Aweso ameyasema hayo wakati alipotembelewa Ofisini kwake Dodoma na Mbunge Salim akiwa na wafadhili kutoka Uswisi ambao wamekuja kwa lengo la kuangalia Changamoto ya maji wilayani Ulanga ili kuona namna bora ya kuisaidia kuondokana na shida hiyo.


Naye mfadhili wa maswala ya maji kutoka nchini Uswisi Bi. Rubab Jawad Aziz amesema kilichomvutia kusaidia wilaya ya Ulanga kuondokana na tatizo la maji ni kwasababu wazazi wake waliishi hapo na yeye alilelewa hapo hivyo anajua Changamoto hizo tangu akiwa mtoto mdogo kabla ya kwenda nje ya nchi kutafuta maisha.


Kwa upande wake Mbunge Salim amesema lengo la kutafuta wafadhili kwa wingi ni kuona namna bora ya kuisaidia Serikali katika kutatua Changamoto mbalimbali.


Jimbo la Ulanga linazalisha kiasi cha lita 8000 hadi 9000 wakati mahitaji ya maji ikiwa ni lita 1,600,000.







MABAHARIA JIENDELEZENI KIELIMU ILI MPANUE WIGO WA AJIRA KIMATAIFA.

June 26, 2023


Mgeni Rasmi, Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Mwanza ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Ilemela Mhe.Hassan Masala akisisitiza jambo kwa wadau wa sekta ya Uchukuzi kwa njia ya maji na Wananchi kutoka maeneo mbalimbali ya Jiji la Mwanza na Mikoa ya Jirani(hawapo pichani) wakati wa kilele cha maadhimisho ya siku ya Mabaharia Duniani yaliyofanyika kwenye viwanja vya Furahisha vilivyopo katika Manispaa ya Ilemela Jijini Mwanza Tarehe 25 Juni,2023



Mkurugenzi wa Usalama na Mazingira kutoka Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi-Sekta ya Uchukuzi Bi Stella Katondo akisisitiza jambo kwa Mgeni Rasmi, Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Mwanza ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Ilemela Mhe.Hassan Masala na Baadhi ya Mabaharia, Wafanyakazi wa wizara, Taasisi na Wananchi kutoka maeneo mbali mbali ya Jiji la mwanza na Mikoa ya jirani (hawapo pichani) wakati wa kilele cha maadhimisho ya siku ya Mabaharia Duniani yaliyofanyika kwenye viwanja vya Furahisha vilivyopo katika Manispaa ya Ilemela Jijini Mwanza Tarehe 25 Juni,2023



Mkurugenzi wa Usalama na Mazingira kutoka Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi-Sekta ya Uchukuzi Bi Stella Katondo akimuongoza Mgeni Rasmi, Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Mwanza ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Ilemela Mhe.Hassan Masala kukagua mabanda ya maonesho ya wadau wa usafiri kwa njia ya maji wakati wa kilele cha maadhimisho ya siku ya Mabaharia Duniani yaliyofanyika kwenye viwanja vya Furahisha vilivyopo katika Manispaa ya Ilemela Jijini Mwanza Tarehe 25 Juni,2023



Mgeni Rasmi, Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Mwanza ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Ilemela Mhe.Hassan Masala akigawa vyeti vya pongezi kwa Mabaharia waliofanya Vitendo vya kijasiri vya uokozi kwa nyakati mbalimbali wakati wa kilele cha maadhimisho ya siku ya Mabaharia Duniani yaliyofanyika kwenye viwanja vya Furahisha vilivyopo katika Manispaa ya Ilemela Jijini Mwanza Tarehe 25 Juni,2023



Baadhi ya Mabaharia, Wafanyakazi wa wizara, Taasisi na Wananchi kutoka maeneo mbali mbali ya Jiji la mwanza na Mikoa ya jirani wakiwa kwenye picha ya pamoja na Mgeni Rasmi, Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Mwanza ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Ilemela Mhe.Hassan Masala ( katikati kwa waliokaa) wakati wa kilele cha maadhimisho ya siku ya Mabaharia Duniani yaliyofanyika kwenye viwanja vya Furahisha vilivyopo katika Manispaa ya Ilemela Jijini Mwanza Tarehe 25 Juni,2023





Baadhi ya Mabaharia, Wafanyakazi wa wizara, Taasisi na Wananchi kutoka maeneo mbali mbali ya Jiji la mwanza na Mikoa ya jirani wakiwa kwenye picha ya pamoja na Mgeni Rasmi, Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Mwanza ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Ilemela Mhe.Hassan Masala ( katikati kwa waliokaa) wakati wa kilele cha maadhimisho ya siku ya Mabaharia Duniani yaliyofanyika kwenye viwanja vya Furahisha vilivyopo katika Manispaa ya Ilemela Jijini Mwanza Tarehe 25 Juni,2023




Baadhi ya Mabaharia, Wafanyakazi wa wizara, Taasisi na Wananchi kutoka maeneo mbali mbali ya Jiji la mwanza na mikoa ya jirani wakifuatilia mada kutoka kwa Mgeni Rasmi, Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Mwanza ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Ilemela Mhe.Hassan Masala wakati wa kilele cha maadhimisho ya siku ya Mabaharia Duniani yaliyofanyika kwenye viwanja vya Furahisha vilivyopo katika Manispaa ya Ilemela Jijini Mwanza Tarehe 25 Juni,2023



Kwaya ya Watumishi wa Jiji la Mwanza wakiwa katika picha ya pamoja na Mkurugenzi wa Usalama na Mazingira kutoka Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi-Sekta ya Uchukuzi Bi Stella Katondo walipotembelea banda la Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi wakati wa kilele cha maadhimisho ya siku ya Mabaharia Duniani yaliyofanyika kwenye viwanja vya Furahisha vilivyopo katika Manispaa ya Ilemela Jijini Mwanza Tarehe 25 Juni,2023




Baadhi ya Mabaharia, Wafanyakazi wa wizara, Taasisi na Wananchi kutoka maeneo mbali mbali ya Jiji la mwanza na Mikoa ya jirani wakiwa kwenye picha ya pamoja na Medali zao mara baada ya kumaliza kushiriki mbio za KM 7 za Seafarers Marathon zilizoanzia kwenye Mwalo wa Kirumba na kumalizikia kwenye viwanja vya Furahisha ikiwa ni kilele cha maadhimisho ya siku ya Mabaharia Duniani yaliyofanyika kwenye viwanja vya Furahisha vilivyopo katika Manispaa ya Ilemela Jijini Mwanza Tarehe 25 Juni,2023



Baadhi ya Mabaharia, Wafanyakazi wa wizara, Taasisi na Wananchi kutoka maeneo mbali mbali ya Jiji la mwanza na Mikoa ya jirani wakiwa kwenye picha ya pamoja na Medali zao mara baada ya kumaliza kushiriki mbio za KM 7 za Seafarers Marathon zilizoanzia kwenye Mwalo wa Kirumba na kumalizikia kwenye viwanja vya Furahisha ikiwa ni kilele cha maadhimisho ya siku ya Mabaharia Duniani yaliyofanyika kwenye viwanja vya Furahisha vilivyopo katika Manispaa ya Ilemela Jijini Mwanza Tarehe 25 Juni,2023




Na Mwandishi wetu Mwanza


Serikali imewataka Mabaharia kote Nchini kuzidi kujiendeleza kielimu na kuchapa kazi kwa bidii ili waaminike kwenye ajira hususan za kimataifa ili waweze kupata fursa zaidi za kufanya shughuri za ubaharia nje ya Nchi kwa manufaa yao na Nchi kwa ujumla.


Hayo yamesemwa leo na Mgeni Rasmi, Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Mwanza ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Ilemela Mhe.Hassan Masala wakati wa akihitimisha maonesho ya siku ya Mabaharia Duniani yaliyofanyika kwenye viwanja vya Furahisha vilivyopo katika Manispaa ya Ilemela Jijini Mwanza kuanzia Tarehe 22 Juni, 2023 na kufikia tamati Tarehe 25 Juni,2023.


Mhe.Masala amesema Mabaharia huendesha na kuwezesha uchumi wa nchi zao na Dunia kukua, kwa kulitambua hilo Serikali ya awamu ya sita ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayoongozwa na Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan na Serikali ya Awamu ya Nane ya Mapinduzi Zanzibar inayoongozwa na Mhe. Dkt Hussein Ally Mwinyi kwa kushirikiana na vyama vya Mabaharia, wamiliki wa vyombo vya usafiri majini na taasisi mbalimbali za kimataifa zimefanya kila liwezekanalo kuhakikisha kazi za Ubaharia na taaluma yake zinatambuliwa nchini na nje ya nchi sasa kuliko wakati mwingine wowote ule.

“Serikali imehakikisha Mabaharia wanapewa heshima inayostahili kama zilivyo taaluma nyingine sasa ni wakati wenu sasa Mabaharia kote Nchini kutumia fursa hii kujiendeleza zaidi kitaaluma ili mzidi kuaminika kwenye ajira za kimataifa” amesisitiza Masala

Mhe. Masala amesema Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inawajali sana Mabaharia kwani katika mkoa wa Mwanza imekarabati Meli za MV Victoria , MV Butiama,Mv Umoja na kujenga meli mpya ya MV Mwanza ambazo zitasaidia kuongeza upatikanaji wa ajira kwa Mabaharia

Akimkaribisha Mgeni rasmi kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi, Mkurugenzi wa Usalama na Mazingira kutoka Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi-Sekta ya Uchukuzi Bi.Stella Katondo amesema Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ilijiunga na Shirika la Bahari Duniani(IMO) lenye majukumu ya kukuza na kusimamia utendaji wa Sekta ya Usafiri majini, kusimamia ulinzi, usalama na uhifadhi wa mazingira ya maji tangu mwaka 1974 ambapo walikubaliana Kusherehekea Siku ya Mabaharia Duniani kila mwaka ifikapo tarehe 25 Juni,2023

Bi. Stella amesema Maadhimisho haya ya siku ya Mabaharia Duniani yanayoambatana na kauli mbiu
“Miaka 50 ya MARPOL uwajibikaji wetu unaendelea” yaliyofanyika Kitaifa Jijini Mwanza kuanzia tarehe 22 Juni,2023 na kufikia tamati tarehe 25 Juni,2023 yalikutanisha Taasisi, Wizara na wadau wote wa Sekta ya Uchukuzi kwa njia ya Maji Nchini kwa lengo la kutambua umuhimu wa kazi ya Mabaharia na kuwaenzi mabaharia ambao ni kiungo muhimu sana kwa uchukuzi kwa njia ya maji na kukuza uchumi wa Taifa na Dunia

Maonesho ya siku ya Mabaharia Duniani yaliyoanza tarehe 22 mpaka 25 Juni, 2023 na kufanyika kitaifa Jijini Mwanza yameandaliwa kwa ushirikiano kati ya Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi-Sekta Uchukuzi kwa Tanzania Bara kupitia Shirika la uwakala wa Meli Tanzania(TASAC) na Wizara ya Ujenzi,Mawasiliano na Uchukuzi Zanzibar kupitia Mamlaka ya Usimamizi wa Bahari Zanzibar(ZMA), Pamoja na wadau mbalimbali wa Uchukuzi kwa njia ya maji Nchini.

TSB KUTUMIA MCHEZO WA YOGA KUHAMASISHA ZAO LA MKONGE

June 26, 2023


Mkurugenzi wa Bodi ya Mkonge Tanzania (TSB) Saady Kambona wakati wa Shughuli ya Kimataifa ya Mchezo wa Yoga iliyofanyika kwenye Hotel ya Mkonge Jijini Tanga.

Mwalimu wa Yoga kwa upande wa Tanga Darshana Minesh akizungumza 

Mwalimu wa Yoga kwa upande wa Tanga Darshana Minesh kulia akiongoza mchezo wa Yoga 
Washiriki wa mchezo wa Yoga wakiendelea nao kwenye Ukumbi wa Hotel ya Mkonge Jijini Tanga 
Mchezo wa Yoga ukiendelea
Mchezo wa Yoga ukiendelea
Wageni mbalimbali wakifuatilia mchezo huo
Picha ya pamoja na kikundi cha Yoga cha Jijini Tanga
Mwenyekiti wa Klabu ya Waandishi wa Habari Mkoani Tanga (TPC) Lulu George ambaye ni miongoni mwa wachezaji wa mchezo huo 


Na Oscar Assenga,Tanga

BODI ya Mkonge Tanzania (TSB) imeweka bayana kwamba itatumia pia mchezo wa Yoga kuhamasisha Kilimo cha zao la Mkonge ili kuweza kupanua wigo mpana ili kuongeza idadi ya wakulima.

Kauli hiyo ilitolewa mwishoni mwa wiki na Mkurugenzi wa Bodi ya Mkonge Tanzania (TSB) Saady Kambona wakati wa Shughuli ya Kimataifa ya Mchezo wa Yoga iliyofanyika kwenye Hotel ya Mkonge Jijini Tanga.

Kambona ambaye alialikwa kwenye shughuli hiyo kama mgeni Alisema mashuhuri kwenye shughuli ya kimataifaa ya Yoga ambapo Tanga wana wanachama wengi ambapo aliweza kujionea shughuli zinazoendelea.

Alisema kwamba baada ya kuona shughuli hizo amejifunza kwamba mchezo wa Yoga ni mchezo muhimu kwa ajili ya afya ya akili na kuweza kuona namna mazoezi yanavyofanyika tumeshuhudia walimu kutoka nchini India wakifundisha kupitia videeo Conference akionyeha mazoezi yanavyokwenda.

Aidha alisema kwamba hivyo wameona ni hatua muhimu kwao kufika na kuna uwekezako wa kutumia mchezo wa Yoga kuhamasisha kilimo cha zao la mkonge kutokana na kwamba wao kila kila fursa wanaiutumia kuona namna ya kuiunganisha na zao la Mkonge.

Alisema kwamba na jambo hilo linafanyika hoteli ya Mkonge ambayo ni Brand kubwa ya zaio la Mkonge Tanga na amefurahi sana na Taasisi ya Yoga ni jambo nzuri sana.

Kwa upande wake Mwalimu wa Yoga kwa upande wa Tanga Darshana Minesh aliitaka jamii kutambua umuhimu wa Yoga kwa afya ya mwili,akili na roho na kwamba yatawasaidia katika kuleta mitazamo chanya kwenye mambo mbalimbali ya maisha yao.

"Yoga ni muhimu sana kwenye afya ya mwili ,akili na roho na mtu akifanya hatajutia maamuzi ya kujiunga kwani ataona mabadiliko makubwa kwenye maisha yake," alisisitiza Mratibu huyo wa Yoga kwa Mkoa wa Tanga.

DC TANGA AZINDUA MSIMU WA SITA WA TANGA WOMEN GALA, AWAFUNDA WAJASIRIAMALI TANGA

June 25, 2023

MKUU wa wilaya ya Tanga Hashim Mgandilwa kushoto akizundua msimu wa sita wa Tanga Women Gala Jijini Tanga linaloandaliwa na Kampuni ya Five Brother Intertainment kulia ni Mkurugenzi wa Kampuni hiyo Nasoro Makau na kulia ni Mratibu wa Matukio Five Brothers  Asma Makau akifuatiwa na Naibu Meya wa Jiji la Tanga Wakili Mwanaidi Kombo
MKUU wa wilaya ya Tanga Hashim Mgandilwa kushoto akimvalisha kofia mmoja wa wajasiriamali waliofika kwenye uzinduzi huo 
Mkuu wa wilaya ya Tanga Hashim Mgandilwa akizungumza wakati wa uzinduzi wa Tanaga Women Gala
Mkurugenzi wa Kampuni ya Five Brothers Intertainment ambao ndio waandaaji wa Tanga Women Gala  Nasoro Makau akizungumza wakati wa uzinduzi huo
Naibu Meya wa Jiji la Tanga (CCM) Wakili Mwanaidi Kombo akizungumza katika uzinduzi huo
Mwanzilishi wa Tanga Women Gala Latifa Shehoza akizungumza wakati wa uzinduzi huo 

Mwanzilishi wa Tanga Women Gala Latifa Shehoza  akiingia ukumbini wakati wa uzinduzi huo
Naibu Meya wa Jiji la Tanga Wakili Mwanaidi Kombo akiingia ukumbini 
Sehemu ya Wajasiriamali walioshiriki kwenye uzinduzi huo
Sehemu ya Wajasiriamali walioshiriki kwenye uzinduzi huo
Sehemu ya Wajasiriamali walioshiriki kwenye uzinduzi huo
Mkuu wa wilaya ya Tanga Hashim Mgandilwa kulia akiteta jambo na Naibu Meya wa Jiji la Tanga (CCM) Wakili Mwanaidi Kombo wakati wa uzinduzi huo

Na Mwandishi Wetu, TANGA


MKUU wa wilaya ya Tanga Hashim Mgandilwa amezindua msimu wa sita wa Tanga Women Gala huku akitumia jukwaa hilo kuwataka wajasiriamali ni vema watumie maonesho hayo kama sehemu ya kutangaza biashara zao na sio ya kufikia kuuza tu.

Mgandilwa aliyasema hayo wakati akizungumza na wajasiriamali hao kwenye uzinduzi huo ambapo alisema kwamba miongoni mwao wakifika kwenye maonesho wanafikiria kuuza mzigo walionao kwa siku hizo wakimaliza wanasema faida wamepata mwisho wa siku wanaendelea na maisha.

Tanga Women Gala ni Jukwaa la Wajasiriamali ambalo limekuwa likifanyika kila mwaka kwa lengo la kuhakikisha wanakua na kuinuka kiuchumi kwa kupanua wigo wa kuwakutanisha linaloandaliwa na Kampuni ya Five Brother Intertainment

Mkuu huyo wa wilaya aliwataka wabadilike na kuondokana na hali hiyo badala yake watumie kama jukwaa la kutafuta masoko muda wote kwa kujikita kutangaza biashata zao na sio kuuza tu wakati wa maoyesho.

Alisema kwamba ni matumaini yake kwamba katika msimu huo wa sita wa Tanga Women Wajasiriamali tunakwenda kutengeneza historia kubwa ambayo itakuwa chachu ya kuendelea kuwainua wajasiriamali mkoani humo kukua kiuchumi

“Niwashukuru Tanga Women Gala kwa kazi kubwa mnaoendelea kuifanya tunajua inawezekana wakawa hawana cha kuwalipa lakini dua za wajasiriamali ambao kila siku mnaendelea kuwainua ndio malipo yenu”alisema Mkuu huyo wa wilaya.

“Pamoja na Pongezi mimi kama DC wenu niwapongeza kwa mchango wenu kwa jamii ya wana Tanga ni mkubwa serikali yetu imetengeneza fursa nyingi ikiwemo kutoa wigo kwa wajasiriamali na wafanyabiashara kufanya biashara zao vizuri bila changamoto zozote niliona kama kiongozi wa wilaya niwapongeza niwatake muendeee kufanya hivyo hivyo siku zote”Alisema

Hata hivyo aliwataka kuendelea kupanua wigo kwa wajasiriamali ambao kimsingi hawana uwezo wa kufika kwenye maeneo yao kwa kutengeneza utararibu wa namna ya kuweza kuwafikia na kuwatambua ili kuona namna ya kuwasaidia.

“Lakini maonyesho yetu ni ya siku chache ni vema tukajikita kutengeneza masoko baada ya maonyesho sio wakati wa maonyesho ninasema hivyo kwa sababu kwenye wakati huo tunakuwa na siku tatu mpaka tano hivyo tunapaswa kutegeneza kuona mjasiriamali anafanya biashara siku zote za mwaka”Alisema DC Mgandilwa,

Awali akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Mkurugenzi wa Five Bothers Intertainment Nasoro Makau alisema kwamba Tamasha hilo la Tanga Women Gala la msimu wa sita linatarajiwa kuwa la aina yake kutokana na namna walivyojipanga

Alisema kwamba wamekuja kuzindua rasmi siku pendwa uzinduzi huo ambao ni msimu wa sita mfululizo kwa umri wa kuzaliwa ni sawa na mtoto anayeanza shule Tanga huku akieleza Tanga Women Gala ilianza kwa hali ya udogo lakini sasa inakwenda kukua.

“Tunawashukuru wadau mbalimbali ikiwemo Benki ya NMB,CRDB,Amana,Stanbic, Azania,TRA,Tanga Uwasana Prism Comunication ambao mwaka jana tuliokuwa nao hivyo tunaamini msimu huu pia watatushirika mkono tushirikiane nao”Alisema

Naye kwa upande wake Naibu Meya wa Jiji la Tanga (CCM) Wakili Mwanaidi Kombo alitoa wito kwa wakina mama kuendelea kuchangamkia fursa mbalimbali zilizopo ili waweze kujikwamua kiuchumi

Mwanaidi ambaye pia ni Mrartibu wa Tawla Kanda ya kaskazini aliwataka pia kuona namna yao kufanya biashara kwa waledi ili ziwezi kuleta tija kwa maisha yetu na jamii zinazowazunguka.

“Wakati tukichangamkia fursa hizo tusisahau majukumu mengine kama mwanamke changamoto nyingi za ukatili wa kijinsia kwa watoto na wanafunzi kwa sababu sisi wakinaa nana tumejikita kutafuta fedha badala ya majukumu yetu ya ndani”Alisema

Hata hivyo aliwataka wajiepushe na mikopo isiyokuwa na tija ya kausha damu riba zake hazieleki hivyo niwaombe kwamba iwapo wanataka kukua kiuchumi waende kwenye taasisi zilizosajiliwa za kifedha kwenye mabenki.

Mwisho.