TASAC YATOA ELIMU KWA WANANCHI KATIKA MAONESHO YA TANO YA TEKNOLOJIA YA MADINI GEITA

September 29, 2022

 

Afisa Masoko Mwandamizi wa Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC)  Martha Kalvin (wa kwanza kulia) akikabidhi zawadi Kwa  Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Madini Bw. Msafiri  Mbibo  alipofanya ziara katika kutembelea Banda la Shirika hilo kwenye maonesho ya tano  Teknolojia ya madini yanayofanyika mkoani Geita.


 Afisa Masoko Mwandamizi wa TASAC Martha Kalvin akiwa kwenye picha ya pamoja na watumishi wengine wa Taasisi hiyo kwenye Banda lao.



SHIRIKA LA Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC) limebainisha kwamba katika kutekeleza majukumu yake limejikita kwenye kutoa elimu kwa wananchi kufahamu namna linavyotekeleza majukumu yake kwa mujibu wa sheria

Hayo yalisemwa na Afisa Masoko Mwandamizi wa  Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC) Martha Kelvin wakati wa mahojiano maalumu na mtandao huu katika Maonesho ya tano ya Teknolojia na Uwekezaji kwenye Sekta ya Madini yanayofanyika Mkoani Geita.

Amesema kuwa licha ya majukumu makubwa waliyonayo pia Shirika hilo limeendelea kutoa elimu kwa wananchi katika Maonesho hayo ili kufahamu namna  linavyotekeleza majukumu yake kwa mujibu wa Sheria.

Alisema kwamba wanashiriki maonesho hayo ya teknolojia na uwekezaji kwenye sekta ya madini yanayofanyika mkoani Geita ili kuweza kutoa elimu kwa wananchi juu ya majukumu yanayotekezwa Kisheria. 

“Lakini kama mdhibiti wa shughuli za usafiri kwa njia ya maji tunasimamia huduma zinazotolewa na Bandari, tunadhibiti na kusimamia ulinzi, usalama na utunzaji wa mazingira na kuratibu shughuli za uokoaji na utafutaji pale panapotokea dhoruba katika vyombo vya usafiri kwa njia ya maji”

Aidha pia alisema katika maonesho kutoa elimu kwa wananchi wa Geita hususani wadau wa Madini katika jukumu letu la kipekee kwenye biashara ya Meli ambapo kwa sasa wanafanya uondoshaji wa shehena kwa makinikia na mashine zinazotumika katika migodi hivyo wanawakaribisha waweze kupata elimu zaidi itakayowasaidia kujua nini cha kufanya wanapotaka kuagiza mashine zao kuziingiza hapa nchini na kuzitoa pia na usafirishaji wa Makinikia

Kwa mujibu wa Sheria, TASAC ina wajibu wa kusimamia kazi mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuhimiza usimmizi na shughuli za uwakala wa meli wenye ufanisi, kuhimiza shughuli za bandari na huduma za meli zenye ufanisi, kuhakikisha kunakuwepo usalama na ulinzi wa shehena, kuhimiza na kutunza mazingira, usalama na ulinzi wa bahari, maziwa na mito.

Aidha Shirika hilo pia lina wajibu wa kuhimiza ufanisi, uchumi na uaminifu, kuendeleza upanuzi wa sekta ya usafirishaji kwa njia ya maji, kuhimiza ushindani katika biashara ya uwakala wa meli, na kuingia kwenye majukumu ya kimkataba na watu wengine au kikundi cha watu.

Maonesho hayo ya Teknolojia ya Madini ni maonesho ya tano kufanyika Mkoani Geita yakiwa na lengo la kuwaleta pamoja wadau mbalimbali katika Sekta hiyo ili kubadilishana uzoefu wa kitaalamu na kujifunza Teknolojia za kisasa katika sekta hiyo pamoja na Taasisi nyingine ikiwemo TASAC.

RC MGUMBA AWATAKA WAHITIMU WA MAFUNZO OPERESHENI MABEYO 2022 KUTUMIA MITANDAO YA KIJAMII KWA TIJA

September 28, 2022

 



MKUU wa Mkoa wa Tanga Omari Mgumba kulia  akikagua gwaride la vijana wahitimu wa mafunzo kwa mujibu wa sheria Operesheni Jenerali Venance Mabeyo kikosi cha 835 KJ cha Mgambo JKT wilayani  Handeni  Mkoani Tanga
 Gwaride la vijana wahitimu wa mafunzo kwa mujibu wa sheria Operesheni Jenerali Venance Mabeyo kikosi cha 835 KJ cha Mgambo JKT wilayani  Handeni  Mkoani Tanga wakipita mbele ya mgeni rasmi Mkuu wa Mkoa wa Tanga Omari Mgumba wakati wa ufungaji wa mafunzo hayo
 gwaride la vijana wahitimu wa mafunzo  kwa mujibu wa sheria Operesheni Jenerali Venance Mabeyo kikosi cha 835 KJ cha Mgambo JKT wilayani  Handeni  Mkoani Tanga wakati wa ufungaji wa mafunzo hayo 

Na Oscar Assenga HANDENI.

MKUU wa Mkoa wa Tanga Omari Mgumba amewataka vijana waliohitimu wa mafunzo ya Operesheni Mabeyo 2022 wanakwenda kujiunga na vyuo vikuu hapa nchini kuhakikisha wanatumia vizuri mitandao ya kijamii kwa faida badala ya kuhakikisha wanajiepusha na matumizi mabaya.
na sio vyenginevyo


RC Mgumba aliyasema hayo wakati akifunga mafunzo ya katika kambi ya JKT Kabuku 835 KJ wilayani Handeni wa mujibu wa Sheria Operesheni Jenerali Venance Mabeyo 2022,ambapo alisema kwa sababu vijana wengine waliopo vyuoni wamekuwa na uhuru uliopitiliza na kufanya mambo bila uwepo wa usimamizi.


Alisema lazima wazazi washirikiane katika kuwatembelea watoto wao mara kwa mara kwa maana unaweza kujua mtoto wao anasoma kumbe anasomeshwa jambo ambalo baadae linaweza kuwa na athari kwake na Jamii kwa ujumla.


"Niwasihi wazazi wenzangu muwe mnafanya kuwatembelea watoto wenu wanapokuwa vyuoni lakini wahitumu leo niwaase mkatumie vizuri mitandao ya kijamii kwa ajili ya faida na sio nyenginevyo maana vijana wengine waliopo vyuoni anaweza kudanganywa mwenye mitandao ya kijamii ukashurutishwa jambo ambalo unaweza kufanya kwa tamaa"Alisema


Mkuu huyo wa Mkoa alisema matokeo yake wanadhalilisha wazee wao Jamii na Ndugu na Taifa kwa ujumla hivyo hakikisheni suala la nidhamu wanalishikilia kweli hasa wale wanaoenda kuishi vyuoni.


"Kwa sababu mtakumbana na watu mbalimbali ikiwemo wanasheria wasije kuwapotosha nyie mmeiva na mmefundwa nidhami na uadilifu kaishini maisha hayo"Alisema Mkuu huyo wa Mkoa.


Awali akizungumza wakati wa ufunguji wa mafunzo hayo Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa nchini (JKT) Meja Jenerali Rajab Mabele aliwataka wahitimu wa mafunzo wasiende kutu mika vibaya katika maeneo mrakayokuwepo wakati wote mkumbuke kiapo mlichoapa.


Alisema kuwa kama wanavyofahamu majukumu ya JKT ni malezi ya vijana na uzalishaji wa mali na kufanya shughuli za ulinzi wa Taifa katika kutekeleza majukumu hayo ya kila siku.


Hata hivyo alisema hivyo kutolewa mafunzo hayo kwa vijana wa mujibu wa sheria na mafunzo ya mujibu wa sheria op Jenarali Mabeyo yamekuchukua muda wa majuma 12 mfululizo.


Mkuu wa Jkt alisema kwamba wahitimu hao wamejifunzamasomo mbalimbi yakiwemo ya uzalishaji mali,nadharia na vitendo kwa ujumla lengo kukuza moyo wa uzalendo kuwajengea nidhamu ,ukakamavu na ujasiri.


Alisema hiyo itawafanya wajitambue kuwa ni sehemu ya Jamhuri ya muungano wa Tanzania kuilinda,kuijenga na kuitetea nchi yao.



Naye kwa upande wake Mkuu wa Kikosi cha 835 KJ JKT Kabuku Luteni Kanali Raymond Mwanri alisema vijana hao wakiwa kwenye mafunzo hayo wamejifunza mambo mbalimbali ikiwemo ulinzi wa Taifa lao,Uzalendo na utii kwa mamlaka zilizowekwa kwa mujibu wa sheria .


Hata hivyo aliwataka wahitimu hao kuhakikisha wanakiishi kiapo hicho huku akieleza wamefaulu katika viwango mbalimbali vya kuhitimua mafunzo hayo.


Hata hivyo kwa upande Mkuu wa Mafunzo wa JKT Tanzania Kanali Aisha Matanza alisema mafunzo ya vijana ya kujitolea kwa mujibu wa sheria ya Jenero Mabeyo yamekuwa chachu kuweza kuwaimarisha vijana kuwafanya wakakamavu na wazalendo kwa nchi yao.

RAIS SAMIA AOMBWA KUIPA NGUVU ZAIDI SHERIA KWA WANAOFANYA VITENDO VYA UKATILI KWA WATOTO

September 25, 2022

 


Mkurugenzi wa Asasi ya Kiraia  ya Tanga Youth Talent Asociation( Tayota)  George Bwire akizungumza na waandishi wa habari wakati wa utekelezaji wa mradi wa kupiga vita ukatili wa kijinsia aina zote kwa  watoto na vijana wa rika balehe uliofanyika kwenye shule ya msingi na Sekondari kata ya Kirare ambapo Mradi huo unatekelezwa katika Kata zote za Jiji la Tanga na mitaa wenye lengo kupambana na ukatili ambao watoto wadogo na vijana wanaopitia na unafadhiliwa na Botnar Foundation kutoka Uswis.
Mkurugenzi wa Asasi ya Kiraia  ya Tanga Youth Talent Asociation( Tayota)  George Bwire akizungumza na waandishi wa habari wakati wa utekelezaji wa mradi wa kupiga vita ukatili wa kijinsia aina zote kwa  watoto na vijana wa rika balehe uliofanyika kwenye shule ya msingi na Sekondari kata ya Kirare ambapo Mradi huo unatekelezwa katika Kata zote za Jiji la Tanga na mitaa wenye lengo kupambana na ukatili ambao watoto wadogo na vijana wanaopitia na unafadhiliwa na Botnar Foundation kutoka Uswis.

Wanafunzi wa shule ya Msingi Kirare 


 Na Oscar Assenga,TANGA.


Rais Samia Suluhu ameombwa kuangalia namna ya kuipa nguvu zaidi sheria ya watu wanaofanya vitendo vya ukatili kwa watoto kuweza kushughulikiwa kikamilifu hatua itakayowezesha kukomesha vitendo hivyo kwenye Jamii.

Ombi hilo lilitolewa mwishoni mwa wiki  na Mkurugenzi wa Asasi ya Kiraia  ya Tanga Youth Talent Asociation( Tayota)  George Bwire wakati wa utekelezaji wa mradi wa kupiga vita ukatili wa kijinsia aina zote kwa  watoto na vijana wa rika balehe uliofanyika kwenye shule ya msingi na Sekondari kata ya Kirare.

Alisema sheria zipo wazi ikiwemo zile ambazo zinawalinda watoto na utekelezaji wake unafanyika vizuri lakini kumekuwa na mapungufu ya kibinadamu kwa watu kwenye vyombo husika ikiwemo mahakamani na Jeshi la Polisi lakini kwa mujibu wa sheria zipo na zinajitosheleza na utekelezaji inabidi ufanyike kwa hali ya ukamilifu.

Mradi huo unatekelezwa katika Kata zote za Jiji la Tanga na mitaa wenye lengo kupambana na ukatili ambao watoto wadogo na vijana wanaopitia na unafadhiliwa na Botnar Foundation kutoka Uswis.

"Nikikuta na Rais Samia Suluhu nitamwambia azidishe nguvu sheria  watu wanaowatendea watoto ukatili waweze kushughukiwa kikamilifu na sio mtu anawafanya ukatili lakini anaonekana mitaani anazunguka hii sio sawa hivyo waweze kushughulikiwa bila upendeleo"Alisema


Mkurugenzi huyo alisema mradi huo kwa sasa unatekelezwa na asasi mbili ambazo  ni Tayota na Tree of Hope na wamefikia shule zote za Tanga 81 za msingi na 25 za Sekondari kwa ujumla wanafunzi waliofikiwa ni 49,000 huku akieleza lengo la mradi kwa awali  ni kuwafikia wanafunzi 10,000. 

Alisema  lakini wameenda mbali zaidi kuwafikia wanafunzi wote wanatoa elimu ya kuwajengea uelewa juu ya vitendo vya ukatili wa kijinsia maana wengine hawafahamu kwamba kuna vitu wanaweza kufanyiwa ni viashiria vya ukatili hivyo ni fursa nzuri kwao kufika shuleni kuweza kuwajengea uelewa.

"Lakini zaidi ya hapa tumekwenda  kwenye Jamii maana wengine wanaowafanyia vitendo vya ukatili ni wana Jamii wanashughu hivyo tunaungana nao  jioni kwenye mitaa kuhamasisha wawalinde watoto lakini kukomesha visa vya ukatili na Jamii za Tanga kulinda maana hilo jambo unakuta limefanywa na mjomba  baba mdogo kwa sababu wanataka kulindana kifamilia mtoto akakoshwa haki na hivyo vitendo vipi sana"Alisema Mkurugenzi huyo 

Hata hivyo alisema kwa sasa wapo kwenye harakati za kuundaa ripoti kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi na idara ya ustawi wa Jamii na Maendeleo ya Jamii ili waweze kufanya uchunguzi zaidi na ambao utasaus kywashughuloliwa wanaotumiwa kwa Mujibu wa sheria

Katika hatua nyengine Mkurugenzi huyo alisema asilimia 60 ya vitendo vya ukatili majumbani vinachangiwa na ndugu wa karibu na hivyo kushindwa kutoa taarifa kwenye mamlaka husika ili kuweza kuvikomesha vitendo hivyo kwenye Jamii .


"Kabla ya kuanza kutekeleza mradi huu tulifanya utafiti tatizo hilo tulipitia ripoti ya hivi karibuni kutoka Ofisi ua DCI kwamba Tanga ni mkoa wa Tatu kwenye ukatili na inaonyesha watoto wanapitia hali ngumu za mateso, watoto wadogo kuanzia darasa la Pili  na kuendelea wanaathirika sana na vitendo vya ukatili"Alisema 

Awali akizungumza wakati wa semina hiyo Emanuel Elias alisema wamefikia kutoa elimu ya kupiga vita ukatili kwa watoto namna ya kujua athari na aina ya namna ya kuweza kuepukana nayo pindi wanapokutana nayo.

Alisema wamelazimika kutoa elimu kutokana na matukio mengi yaliyoshamiri katika Jiji la Tanga shule nyingi walizotembelea mwanzl wamegundua upo ukatili wa aina  nyingi ambao watoto wanafanyiwa majumbani hasa wa kingono na kimwili.

Alisema lengo lao nikwenda shule zote bila kubagua ilo kupata visa mkasa na kupata elimu ya ukatili huku akiitaka Jamii hususani familia kutilia mkazo malezi Bora kwa watoto maana hayo yote chanzo chake ni kukosekana kwa malezi Bora kwenye Jamii.

Naye kwa upande wake Mwanafunzi wa Kidato cha nne katika shule ya Sekondari Kirare Erick Mzungu elimu walioipata itawasaidia pindi watakapoona vitendo vya ukatili vinafanyika ili waweze kutoa taarifa kwenye mamlaka husika kuweza kutatuliwa na Jamii iweze kubaki Salama dhidi ya vitendo hivyo.

Alisema kwamba kupitia elimu hiyo wamegundua namna wanaweza kutoa taarifa ya kuhusu vitendo hivyo vya ukatili ili wahusika waweze kuchukuliwa hatua ikiwemo kuvikomesha .

BILIONI 27 KUJENGA BWAWA LA KILIMO CHA UMWAGILIAJI MSAGALI MPWAPWA

September 21, 2022
Kushoto Mhandisi wa Umwagiliaji Mkoa wa Dodoma Raphael Laizer akizungumza wakati wa kukabidhi Mradi wa bwawa la Umwagiliaji Msagali, Wilayani Mpwapwa, kulia ni mwakilishi wa kampuni ya GNMS Contractors itakayofanya kazi ya ujenzi wa bwawa hilo.
Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule akiongea wakati wa kukabidhi mradi wa Ujenzi la bwawa la Msagali wilayani Mpwapwa.
Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule akimkabidhi Kablasha Mwakilishi wa Kampuni wa GNMS Contractors  Mhandishi Emmanuel Mponda itakayojenga bwala litakalotumika kwa Kilimo cha Umwagiliajia Msagali.
Aliyesimama meza kuu ni mkuu wa Wilaya ya Mpwapwa Mhe. Josephat Maganga akizungumza na wananchi wa kata ya Chunyu na Ng'ambi wilayani humo baada ya kukabidhi eneo la ujenzi wa mradi wa Bwawa la umwagiliaji.


Picha ikionesha wananchi wa kata ya Ng'ambi na Chunyu katika mkutano wa  hadhara na viongozi wa Mkoa wa Dodoma.





Na ,Mwandishi Wetu - Mpwapwa


KWA MARA NYIGINE TENA; Serikali kupitia Tume ya Taifa ya Umwagiliaji Iliyopo chini ya Wizara ya Kilimo, imekabidhi rasmi kwa makandarasi GNMS Contractors eneo la Ujenzi wa Bwawa litakalotumika kwa kilimo cha Umwagiliaji litakalojengwa kwa thamani ya shilingi Bilioni 27.

Mhandisi wa Umwagiliaji wa Mkoa wa Dodoma Raphael Laizer amesema wakati wa makabidhiano ya eneo hilo la umwagiliaji jana jioni kuwa,

Bwawa hilo litakalokuwa na ujazo wa lita milioni tisini, litapelekea kuendelezwa kwa eneo litakalotumika kwa kilimo cha umwagiliaji lenye ukubwa wa hekta elfu tatu na mia tano (3500), ambapo ujenzi wa bwawa hilo unaotegemewa kuchukua miezi kumi na nane, utahusisha eneo ya unyweshwaji maji mifugo, matumizi ya binadamu na shughuli nyingine za kimaendeleo.

Awali, Mkuu wa mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule amesema kuwa Mhe Rais Samia Suluhu Hassan, amedhamiria kusaidia kundi hili maalum la wakulima, wavuvi na wafugaji na kumuasa mkandarasi na wasimamizi wote wa mradi huu kufanya kazi hii kwa weledi na kwenda na wakati.

Kwa Upande wake Mwananchi kwa kata ya Chunyu, Bi Easther Zeavela alitoa ombi kwa mkuu wa mkoa kuwaasa wasimamizi wa miradi inayokwenda vijijini kuwa makini, kwani mradi mingi inakosa usimamizi mzuri. “Uongozi wa juu unapoleta miradi huku vijijini, wasimamizi wasimamie vizuri ili pesa za miradi zitosheleze, mambo mengi tunaona yanaanzishwa na hayakamiliki.” Alisema mwananchi huyo

Ujenzi wa bwawa la msagali unaelezwa kuleta mafanikio mengi pindi utakapokamilika kutokana na asili ya eneo hilo kukumbwa na mafuriko ya maramara, hivyo kingo za bwawa hilo linaweza kustiri miondombinu mingine kama vile ya marabara na umeme.



Mradi wa Bwawa la Msagali ni moja kati ya miradi 21 ya kilimo cha Umwagiliaji iliyosainiwa mbele ya Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan katika maadhimisho ya sikukuu ya wakulima nanenane yaliyofanyika kitaifa mkoani Mbeya mwaka huu.

WAZIRI MCHENGERWA AIPONGEZA SIMBA KWA KUENDELEZA USHINDI LIGI YA MABINGWA AFRIKA

September 18, 2022

 









Na John Mapepele


Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Mohamed Mchengerwa ameipongeza Timu ya Simba kwa kushinda kwenye mashindano ya Ligi ya Mabingwa Afrika.


Simba imeshinda mabao 2-0 dhidi ya timu Nyasa Big Bullet ya Malawi katika mchezo wa marudiani uliochezwa leo Septemba 18, 2022 kwenye uwanja wa Mkapa jijini Dar es Salaam.


Mhe. Mchengerwa ameambatana na Naibu Spika Mhe. Iddi Zungu, Katibu Mkuu wa Wizara yake Dkt. Hassan Abbasi na viongozi mbalimbali wa Serikali.


Amesema watanzania na wanachama wa Simba wanafurahi kuona wanafanya vizuri katika mashindano haya ambapo amefafanua kuwa Mhe. Rais pia anaipongeza timu hiyo.


Ameongeza kuwa timu hiyo imeonyesha uzalendo ambao unapaswa kuendelezwa ili kuitangaza Tanzania Kimataifa.


Ameitaka timu hiyo kutoridhika na ushindi walioupata leo na badala yake iendelee kufanya mazoezi zaidi ili kujinoa hatimaye timu hiyo iingie fainali na kuweza kurejesha kombe nyumbani.


"Ninatoa wito kwa timu yetu kutobweteka na ushindi tulioupata leo, watanzania wanakiu ya ubingwa wa kombe hili. Tunahitaji kujituma na kutanguliza uzalendo ili tuwape raha watanzania". Amesisitiza Mhe. Mchengerwa


Aidha, Mhe. Mchengerwa amesema kuwa dhamira ya Serikali ni kufanya uwekezaji katika michezo ili kuwasaidia wananchi kueluka na magonjwa hivyo kujenga afya zao.


Kapteni wa timu ya Simba John Boko amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano, Mhe. Samia Suluhu Hassan kwa kutoa kipaumbele kwenye michezo.

RC MGUMBA WANAOWEKA FEDHA KWENYE MAGODORO WAMEPUNGUA

September 15, 2022

 


MKUU wa Mkoa wa Tanga Omari Mgumba akizungumza wakati akifungua tawi la Benki hiyo eneo la Ngamiani Jijini Tanga


Afisa Mkuu na Wateja wakubwa wa Benki ya NMB Alfred Shayo akizungumza wakati wa halfa hiyo



MENEJA wa Benki ya NMB Kanda ya Kaskazini Dismas Prosper akizungumza wakati wa halfa hiyo



Meneja wa Uchumi na Takwimu wa Benki Kuu ya Tanzania BOT Tawi la Arusha Ernest Ndunguru akizungumza wakati wa halfa hiyo



MKUU wa wilaya ya Tanga Hashim Mgandilwa akizungumza wakati wa halfa hiyo



MENEJA wa Benki ya NMB tawi la Ngamiani Elizaberth Chawinga akizungumza wakati wa halfa hiyo








Na Oscar Assenga,TANGA


SERIKALI mkoani Tanga imesema kwamba kusogezwa karibu kwa huduma za kibenki kumesaidia kupunguza wananchi waliokuwa wakihifadhi fedha zao kwenye magodoro jambo ambalo ilikuwa ni athari kubwa ikitokea wizi inakuwa rahisi kuweza kuibiwa au kupotea lakini pia zimekuwa salama na hivyo kuepukana na matumizi yasiyokuwa ya lazima.


Hayo yalisemwa na Mkuu wa Mkoa wa Tanga Omari Mgumba wakati akifungua tawi jipya la Benki ya NMB Ngamiani lililopo barabara ya 20 Jijini hapa katika halfa iliyokwenda sambamba na utoaji wa mabati 250 kwa shule ya msingi Masiwani.


Alisema uwepo wa tawi hilo utawawezesha wananchi kupata sehemu ambayo yataweza kuhifadhi fedha zao walizozitolea jasho na kuondoa changamoto ya uhifadhi kwenye vyungu vya maji au kulalia kwenye magodoro ambapo ikitokea moto au wizi kuiba kwake inakuwa ni rahisi lakini pia fedha zina vishawishi ukiziweka ndani matumizi yake yanakiwa ni makubwa sana.


Mkuu huyo wa mkoa alisema lakini ikiziweka benki unaweza kuokoa matumizi yasiyokuwa yalazima na unaweza kutumia hapo baadae kwenye matumizi muhimu katika mahitaji na maisha yenu.


Alisema Serikali imeweka mazingira mazuri kuhakikisha jamii ya kitanzania inapata huduma Bora sa kibenki na nafuu huku akiishukuru benki hiyo ambayo imekuwa ikiunga mkono juhudi za Serikali na hivi karibuni mlitenga zaidi ya Bilioni 200 ya mikopo kwenye sekta ya kilimo kwa riba ya asilimia 9.


"Niwapongeze Benki ya NMB kwa kuendelea kubuni huduma mpya kwa kufungua matawi mapya na zaidi ya hapo kuwajali na kuwathamini wateja bila kujali kipato pia serikali inatambua juhudi zenu za kuwawezesha wananchi kupitia mikopo ya wafanyakazi,wakulima na wafanyabiashara wakubwa na wadogo" Alisema Mkuu huyo wa Mkoa



Alisema dunia kwa sasa inakwenda kasi hususani kwa upande wa teknolojia ambazo zimerahisisha huduma za kibenki kutokutegemea matawi rasmi ingawa haiondoi ukweli kwamba kufungua matawi mapya ni kusogeza huduma karibu zaidi na wananchi ambao hauwezi kupata nje ya tawi la benki.


Mkuu huyo wa mkoa alisema pamoja na mafanikio yaliyoyapata katika kubuni huduma bora na nafuu na za haraka ikiwemo huduma mpya ya Teleza Kidigitali ambayo kwa mara ya kwanza benki inatoa mikopo midogo midogo bila kufika kwenye tawi la benki bila kuwa na dhamana unakopa mwenyewe kupitia simu ya mkononi.


Alisema mikopo hiyo itaondoa adha kwa mama mntilie,babalishe na watu wengine wenye biashara ndogondogo ambao mitaji yao haizidi laki tano hiyo inafaida kubwa ya matumizi ya teknolojia kwani wananchi wengi hususani wafanyabiashara wadogo wadogo huduma hiyo itawanufaisha sana.


Aidha alisema Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Samia Suluhu imaweka mikakati mizuri ya kupunguza umaskini kwa wananchi wake hivyo nitoe changamoto kwa ajili ya kuwasaidia na kukuza ajira kwa wananchi kuendelea kutoa mikopo kwa wakazi wa vitongoji vyote vya mkoa wa Tanga mijini na vijijini.


Awali akizungumza wakati wa halfa hiyo,Afisa Mkuu na Wateja wakubwa na Serikali wa Benki ya NMB Alfred Shayo alisema kwamba benki hiyo imekuwa ikiendeshwa kwa waledi na ufanisi na ndio maana wameweza kufikia hatua kubwa ya kimaendeleo hapa nchini


Alisema tokea Benki hiyo ilipoanzishwa mwaka 1997 imepiga hatua kubwa kwani awali ilikuwa na matawi 97 lakini sasa matawi yamefikia 227 na uzinduzi wa tawi hilo unaongezeka na kufikia 228 ni hatua kubwa imefanya ili kuweza kuwafikia wateja wake kwa karibu zaidi ambapo usogezaji karibu huduma kwa wananchi hatujaaachwa nyuma kidigitali.


" Benki ilipoanzishwa ilikuwa haina wakala wala ATM lakini kwa sasa ina na atm 762 na mawakala zaidi ya 15000 hii inaonyesha namna mnavyoishi ndoto zenu Benki ua NMB karibu yako na kujipanua kwenye mtandao na tunafanya kazi karibu na Serikali pamoja na wateja wetu kuhakikisha tunaboresha huduma na kutoa masuluhisho kwa wateja wetu"Alisema.


Alisema kwa mwaka jana wametoa trilioni 4.3 za mikopo kwa wateja wadogo wadogo kwa kilimo, biashara ndogondogo na wateja binafsi hiyo imetokana na ushirikiano mzuri walionayo kati yao na Serikali na wateja wao


"Kwa Tanga Benki wetu ya NMB ina matawi 10 kanda ya kaskazini tuna matawi 40 hii inaonyesha namna gani tupo karibu na serikali huku wananchi wanapata masuluhisho ya kuwasaidia kuendeleza shughuli za kuweza kujikwamua kiuchumi"Alisema


Alisema kwa upande wa Kilimo kama walivyosikia serikali ilitoa trilioni 1 kwa ajili ya kukopesha sekta ya kilimo kwa riba ambayo ni ya chini ya asilimia 10 huku akieleza kwamba hawakwenda kuchukua hela benki kuu Tanzania (BOT) hivyo walitenga fedha zao Bilioni 100 kwa ajili ya kukopesha kwa asilimia 10 ilipoisha na wakatenga nyengine bilioni 100 ambayo wanapokesha wakulima wadogo wadogo kwa riba ya asilimia 9.


Naye kwa upande wake Meneja wa Benki ya NMB Kanda ya Kaskazini Prosper kwa niaba ya Benki alisema kwamba wamefarijika sana kuona mwitikio kutoka kwa wananchi waliojumuika katika shughuli hiyo muhimu ya uzinduzi wa tawi hilo ambapo ni utekelezaji wa azma yao ya kusogeza huduma karibu na wana chi.


Naye kwa upande wake Meneja wa Uchumi na Takwimu Benki kuu ya Tanzania (BOT) tawi la Arusha Ernest Ndunguru alisema baadhi ya Benki zimekuwa na tabia ya kutokuweka fedha kwenye ATM mashine hususani nyakati za sikukuu na wikiendi jambo ambalo zimekuwa kero kwa wananchi wengi.


"Mimi ni moja ya wateja wa Benki hapa nchini lakini changamoto kubwa ambazo umekuwa tukikutana nazo ni kukosekana kwa fedha kwenye ATM Mashine hususani nyakati za sikukuu na wikiendi hili tatizo tunaomba lishughulikiwe "Alisema