IMEWEKWA DESEMBA 23
Na Oscar Assenga,Tanga.
Na Oscar Assenga,Tanga.
MWENYEKITI
wa Chama cha Mpira wa Kikapu Mkoa wa Tanga(TRBA)Hamisi Jaffary
amejitokeza kuchukua fomu za kuwania nafasi ya Umakamu wa Rais wa
Shirikisho la mpira wa Kikapu nchini (TBF) unaotarajiwa kufanyika
Desemba 29 mwaka huu.
Akizungumza
jana,Jaffary alisema ameamua kuchukua fomu za kuwania nafasi hiyo kwa
lengo la kuleta mabadiliko kwenye mchezo huo kwenye mikoa mbalimbali
hapa nchini.
Alisema
endapo atafanikiwa katika nafasi hiyo atahakikisha anajitahidi kuutoa
mchezo huo hatua moja kwenda nyengine pamoja na kufanya uhamasishaji wa
kuanzishwa mashindano ya kikapu ngazi ya mikoa na wilaya.
"Nimechukua fomu hii kwa nia na madhumuni ya kuhakikisha tunafanya
mabadiliko makubwa kwenye tasnia ya mchezo wa kikapu hapa nchni "Alisema
Jaffary.
Aidha
alihaidi kushirikiana na wenyeviti wa mikoa wa mchezo huo kuhakikisha
wanaufikia malengo makubwa kwa kurudisha hamasa yake kwa kuanzisha
mashindano mara kwa mara.
EmoticonEmoticon