CHADEMA YAPANIA KUCHUKUA KATA ZOTE SITA KANDA YA KASKAZINI.

December 04, 2013


KATIBU WA CHADEMA KANDA YA KASKAZINI,AMANI GOLUGWA KATIKAI AKIMKABIDHI VIFAA VYA AWALI MWENYEKITI  WA CHADEMA KATA YA SUNGA JIMBO LA MLALO EDWARD NGEREZA ANAYESHUHUHIA NI KATIBU WA CHADEMA MKOA WA TANGA,JONATHAN BAWEJE.



KATIBU WA CHADEMA KANDA YA KASKAZINI,AMANI GOLUGWA KATIKATI AKISISITIZA JAMBO KABLA YA KUKABIDHI VIFAA KWA MWENYEKITI WA CHADEMA KITONGOJI CHA LUANDE KATA YA KIOMONI  MWANAMTAMA BAKARI KUSHOTO NA KULIA NI KATIBU WA CHADEMA MKOA WA TANGA,JONATHAN BAHWEJE.

WANACHAMA WA CHAMA HICHO MKOANI TANGA WAKIMSIKILIZA KATIBU WA KANDA YA KASKAZINI,AMANI GOLUGWA AMBAYE HAYUPO PICHANI LEO

KATIBU WA CHADEMA KANDA YA KASKAZINI,AMANI GOLUGWA AKISISITIZA JAMBO LEO.
CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)kimesema kuwa licha ya kuwepo msuguano wa ndani lakini kimetamba kuwa kitachukua kata zote sita zilizopo kanda ya kaskazini katika uchaguzi utakaofanyika hivi karibuni hapa nchini. 

Uchaguzi huo wa marudio unatokana na kata za Kiomoni,Mtae mkoani Tanga na Sombetini mkoani Arusha,Kiborolioni mkoani Kilimanjaro na Karachimbi Kiteto mkoani Manyara kutokuwa na madiwani wake kutokana na baadhi yao kujiuzulu na wengine kufariki dunia.


Tambo hizo zilitolewa na Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini,Amani Golugwa wakati akizungumza na viongozi wa chama hicho mkoani hapa kwenye mafunzo ya Chadema ni msingi ambayo yalikuwa na lengo la kuwajengea uwezo pamoja na kukabidhi vifaa vya awali vya kampeni kwa kata zinazokabiliwa na uchaguzi huo ambazo ni Kiomoni na Mtae

Golugwa alisema vifaa hivyo vimetolewa kwa awamu ambapo awamu ya pili watakabidhi pikipiki ili viongozi wa chama hicho waweze kutimiza wajibu wao ipasavyo na hatimaye kuweza kupata ushindi kwenye chaguzi hizo.



Alisema chama hicho kitaingia kwenye mchakato huo kwa kuangalia wanachama ambao watakao kuwa na uwezo wa kuipeperusha bendera yao kwa kuweka wagombea wanaokubalika kwa wananchi kwenye kata zao.



Katibu huyo alisema kuelekea kwenye mchakato huo aliwataka wanachama kuwa na mshikamano wa dhata ambao utakiwezesha chama hicho kupata ushindi na kuacha kutengeneza makundi yasiyo na tija.

  

   “Tunataka kutengeneza historia kwa madiwani wawili kwenye jimbo la Tanga na kata nyingine zilizopo mikoa ya kanda ya kaskazini “Alisema Golugwa.



Akizungumzia mafunzo hayo,Golugwa alisema mafunzo hayo ya siku mbili yana lengo la kuwajengea uwezo wanachama wake mkoani Tanga pamoja na kukiimarisha chama hicho kuelekea uchaguzi ujao.



Waliopokea vifaa hivyo ni Mwanamtama Bakari ambaye ni Mwenyekiti wa Chadema kitongoji cha Luande kata ya Kiomoni Jimbo la Tanga na Edward Ngereza wa Kata ya Mtae Jimbo Mlalo wilayani Lushoto


Share this

Related Posts

Previous
Next Post »