MAKAMBA :MGOGORO WA KIWANDA CHA MPONDE SIO WA KISIASA.

November 27, 2013
RAISA SAIDI,BUMBULI.
Naibu  Waziri  wa  Mawasiliano  Sayansi na  Teknolojia  January  Makamba  amewataka  baadhi  ya watu  kuondokana  na dhana  ya  kusema  mgogoro  wa  kiwanda cha  chai  cha  Mponde   ni siasa   badala  yake amewataka  kuiacha  serikali  indelee na taratibu zake  za  kulitafutia  ufumbuzi  swala hilo.
Makamba  ambaye pia   ni  Mbunge  wa  jimbo  la  Bumbuli  alisema  yeye kama  mbunge  wa  eneo hilo  lazima  ashirikiane  na  wananchi  wake  na  si kikundi  cha  watu wachache  licha ya kutukanwa  kwa  kuwaunga mkono  wananchi  wake.

Naibu  waziri  huyo  alieleza  kusikitishwa  kwake  na  baadhi ya  watu  kusema  swala  hilo  ni  la  kisiasa na  kwamba  linamaslahi  binafsi  ambapo alisema  ni upambuvu   nakwamba  tangu  2010  wakati  wa  uchaguzi ulishapita  sasa  ni wakati  wa  kuleta  maendeleo  kwa  wananchi  waliomuamini  na  kumtuma  kuwa  muwakilishi wao  bungeni na   si vinginevyo.

“Siamini   kama  kuwaunga  mkono  wananchi  walionichagua yanatokana na tofauti za kisiasa kwani eneo hili linamilikiwa na Chama kimoja ambacho ni Chama cha Mapinduzi na wala sina  maslahi binafsi katika suala hilo” Alisema  Makamba  nakuongeza  kuwa  yeye  anawasimia  wakulima  wa zao la  chai  kupata  haki yao  ya  msingi .


Kiwanda cha Mponde  kimefungwa  takribani  miezi  mitano  sasa kufuatia wakulima kususa kupeleka majani mabichi ya chai kwa madai ya kutaka Uongozi wa Chama cha Wakulima wa Chai Usambara (UTEGA) uitishe Mkutano Mkuu na kuwasomea mapato na matumizi ya chama hicho ikiwa ni pamoja na mapato ya kiwanda ambacho kinamilikiwa na chama hicho.


Hivi  karibuni Makamba, alimwaga machozi hadharani katika kijiji cha Mponde Kweminyasa kutokana na taarifa za watu watano kujeruhiwa kwa risasi za moto kufuatia vurugu zilizotokea  kati ya wakulima wa zao la chai  na Jeshi la polisi.


Vurugu hiyo ilitokea kutokana na Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Luteni Mstaafu Chiku Gallawa kuamuru kiwanda cha chai cha Mponde kilichokuwa kimefungwa kwa mwezi mmoja na nusu wakati  huo kifunguliwe kwa nguvu chini ya usimamizi wa Polisi jambo  ambalo  zilisababisha  vurugu  kubwa  mpaka  watu  kujeruhiwa  kwa  risasi za  moto.



Makamba alisema kuwa kuna haja kubwa ya kuwepo maridhiano katika kufungua kiwanda hicho badala ya kutumia nguvu. “Unaweza kufungua kiwanda kwa bunduki lakini huwezi kukiendesha kwa bunduki,” alisema na kuwataka wakulima wa Chai wa Mponde kuwa na subira na uvumilivu kwa sababu haki yao haiwezi kupotea kwa sababu kiwanda hicho ni mali yao.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »