BITEKO ATEMBELEA BANDA LA GGML MAONESHO YA OSHA, AIPONGEZA KUDHIBITI VIFO MAHALI PA KAZI

April 29, 2024

 Na Mwandishi Wetu


NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko ameipongeza Kampuni ya Geita Gold Mining Limited (GGML) kwa kufanikiwa kudhibiti matukio ya vifo na majeruhi katika shughuli za uchimbaji mgodini na kuwasisitiza waajiri wengine kuhakikisha wakati wote wanalinda usalama wa waajiriwa wao.

Biteko ametoa kauli hiyo jana Jumapili baada ya kutembelea banda la GGML katika maonesho ya afya na usalama mahali pa kazi yanayoendelea kwenye viwanja vya General Tyre jijini Arusha.

Biteko ambaye pia alikuwa mgeni rasmi katika kilele cha maonesho hayo, ameeleza kufurahishwa na elimu ya afya na usalama mahali pa kazi inayotolewa na washiriki wa maonesho hayo.

“Niwapongeze wale mliofanya maonesho hapa, mmetoa elimu kubwa kwangu na kwale ambao tumepita lakini tumejifunza bado zipo kazi za kufanya,” alisema.

Alisema waajiriwa wanatakiwa kuzingatia usalama na afya mahali pa kazi kwani kifo cha mtu mmoja kwa takwimu ni sawa na asilimia 100 kwa wategemezi wake ambao ni mke, watoto, ndugu na hata majirani.

“Kifo cha mtu mmoja ni kikubwa kinatakiwa kisitokee. Wito kwa waajiri wote wakati wote nataka mhakikishe mnarekod ziro katika matukio haya ya vifo mahali pa kazi.

“Kwa waajiriwa wito wangu kwenu ni kwamba mtu wa kwanza kulinda usalama ni muajiriwa mwenyewe, ukiona mtambo unaopaswa kuundesha na una kasoro huku ukiwa umelazimishwa na muajiri kuuendesha, uwe wa kwanza kusema mtambo huu haupo salama na usihesabike kuwa mtu uliyegoma kwa sababu pia una wajibu kulinda usalama wako,” alisema.

Alidha alitoa wito kwa kila mtu kuthamini maisha yake kwamba pindi anapokuja kazini anarejea salama bila kuwa na madhara yoyote.

Awali akimkaribisha Dk. Biteko katika banda la GGML, Meneja Usalama wa kampuni hiyo Isack Senya kwa kipindi cha zaidi ya miaka 15 hapajawahi kutokea tukio la vifo kwa mfanyakazi akiwa kazini.

“Tuna miaka zaidi ya sita hakuna mtu aliyeumia akashindwa kurudi kazini siku inayofuata. Suala la msingi tunajitahidi kujifunza kwa wenzetu na kuendelea kuboresha maingira ya afya na usalama mahali pa kazi,” alisema.

Aidha, Senya pia alimueleza Dk. Biteko namna GGML inavyotumia mfumo wa rada kuangalia mienendo ya miamba au kuta katika maeneo ya uchimbaji.

Pia alimueleza kuwepo kwa chumba maalumu cha uokozi ambacho huwepo chini ya ardhi katika migodi ili kufanya uokozi pindi kunapotokea dharura yoyote.

Naye Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Afya na Usalama mahali pa kazi (OSHA), Hadija Mwenda alisisitiza kuwa wataendelea kusimamia majukumu yao ipasavyo kwa mustakabali wa maendeleo ya taifa.

“Tutaendelea kuhamasisha kuwezesha maeneo ya kazi yawe salama. Suala la usalama na afya ni suala la kujenga tabia na ujengaji tabia ni jambo linatokana na kuelimishwa,” alisema.
 

Meneja Usalama kutoka GGML, Isack Senya (kushoto) akimuelezea Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Doto Biteko namna kampuni hiyo inavyotumia vifaa vyenye teknolojia ya kisasa katika shughuli za uchimbaji ili kuzingatia afya na usalama mahali pa kazi. Anayefuata kulia ni Naibu Waziri ,Ofisi ya Waziri Mkuu(Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Patrobas Katambi pamoja na viongozi wengine waliotembelea banda la GGML katika maonesho ya Afya na usalama mahali pa kazi yanayoendelea jijini Arusha.

RAIS DKT. SAMIA ASHIRIKI MKUTANO WA WAKUU WA NCHI ZA AFRIKA JIJINI NAIRONI NCHINI KENYA.

April 29, 2024

 


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha ya pamoja na Rais wa Kenya Mhe. Dkt. William Ruto mara baada ya kuwasili katika ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Kenyatta (KICC) Jijini Nairobi nchini Kenya tarehe 29 Aprili, 2024 kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Afrika wenye lengo la kuainisha vipaumbele vya Nchi hizo ili viweze kuzingatiwa kwenye mzunguko wa 21 wa IDA.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Mkuu wa Mawaziri wa Kenya Musalia Mudavadi mara baada ya kuwasili katika ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Kenyatta (KICC) Jijini Nairobi nchini Kenya tarehe 29 Aprili, 2024 kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Afrika wenye lengo la kuainisha vipaumbele vya Nchi hizo ili viweze kuzingatiwa kwenye mzunguko wa 21 wa IDA. 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa amesimama pamoja na Viongozi mbalimbali wakati wa Wimbo wa Taifa wa Kenya pamoja na ule wa Umoja wa Afrika (AU) ukiimbwa kabla ya kuanza Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Afrika wenye lengo la kuainisha vipaumbele vya Nchi hizo ili viweze kuzingatiwa kwenye mzunguko wa 21 wa IDA. Mkutano huo umefanyika katika ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Kenyatta (KICC) Jijini Nairobi nchini Kenya tarehe 29 Aprili, 2024    

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa pamoja na Viongozi mbalimbali kwenye Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Afrika wenye lengo la kuainisha vipaumbele vya Nchi hizo ili viweze kuzingatiwa kwenye mzunguko wa 21 wa IDA katika ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Kenyatta (KICC) Jijini Nairobi nchini Kenya tarehe 29 Aprili, 2024. IDA ni Mfuko Maalum wa Benki ya Dunia ambao unatoa mikopo nafuu na misaada kwa nchi zinazoendelea.

Migodi ya Barrick Tanzania yatoa elimu ya usalama kazini na utunzaji wa Mazingira kwenye maonesho ya OSHA.

April 28, 2024
Baadhi ya Wafanyakazi wa Barrick wakishiriki zoezi la kupanda miti katika hospitali ya jiji la Arusha.
Wafanyakazi wa Barrick wakiwa na wafanyakazi wa hospitali ya Arusha baada ya kushiriki zoezi la kupanda miti kwenye hospitali hiyo baada ya kushiriki zoezi la kupanda miti.
Mwenyekiti wa Bodi ya OSHA, Dk. Adelhelm Meru alipotembea banda la maonesho la Barrick.
Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda, akitembelea banda la Barrick Tanzania kupitia migodi ya Bulyanhulu, North Mara na Buzwagi.

Na Mwandishi Wetu.

Elimu ya afya na usalama mahali pa kazi inaendelea kuwafikia wananchi mbalimbali ambao wanatembelea banda la maonesho ya kampuni ya dhahabu ya Barrick kupitia migodi yake ya Bulyanhulu, North Mara na Buzwagi kwenye maonesho ya Wakala wa Usalama na Afya Mahala pa Kazi (OSHA) yanayoendelea mkoani Arusha.

Mbali na elimu hiyo pia wafanyakazi wa Barrick wameshiriki katika programu za kupanda miti maeneo mbalimbali kwa ajili ya utunzaji wa mazingira kwendana na kauli mbiu ya maonesho ya mwaka huu inayohimiza utunzaji wa mazingira kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi.

Mratibu wa Mazingira wa Barrick (Safety Coordinator), Hassan Kallegeya ameeleza baada ya kuongoza zoezi la kupanda miti kuwa katika maonesho ya mwaka huu mbali na kutoa elimu ya usalama mahali pa kazi wameshiriki pia kupanda miti kwendana na kauli mbiu ya OSHA ya maonesho hayo mwaka huu isemayo athari za mabadiliko ya tabia nchi katika usalama mahali pa kazi.

Alisema athari za mabadiliko ya tabia nchi, zinamuathiri kila mmoja hivyo mbali na kufundisha usalama pia wanazo programu za utunzaji wa mazingira kwa kupanda miti kwa kushirikiana na wadau mbalimbali ili kukabiliana na majanga yatokanayo na mabadiliko hayo.

Barrick imekuwa ikitekeleza kampeni ya ‘Journey to zero’ ambayo inalenga kuhamasisha afya na usalama kwa wafanyakazi wake ambayo sasa inapelekwa kwa wadau wengine wote kwenye jamii.

“Kampeni yetu ya 'Journey to Zero' inalenga kuhakikisha wafanyakazi wote wa kampuni wanakuwa salama wakati wote wanapokuwa kazini hadi wanaporudi nyumbani hivyo tumehakikisha kampeni hii inavuka mipaka hadi nje ya kampuni kuhakikisha jamii nzima inakuwa salama na ndio maana tunaendelea kuendesha mafunzo ya usalama kwa jamii ili kuhakikisha jamii yote inakuwa salama”. alisema.

Wakati huohuo banda la maonesho la Barrick limekuwa likitembelewa na viongozi mbalimbali na Serikali na wananchi ambao wameweza kuona vifaa mbalimbali vya kisasa vya usalama na udhibiti wa majanga mbalimbali ikiwemo moto pia kupata mafunzo kutoka kwa wataalamu mbalimbali wa usalama.

Mkuu wa Mkoa wa Arusha,Paul Makonda ni miongoni mwa wageni walioteembelea banda la Barrick katika maonesho hayo na kupongeza kampuni kwa kuwekeza katika vifaa vya usalama vya teknolojia ya kisasa sambamba na kuwa na programu za kutoa elimu ya Afya na Usalama Mahali pa Kazi kwenye jamii nje ya migodi yake.

Usalama ni sehemu muhimu ya DNA ya Barrick.Katika kudhihirisha hilo migodi yake nchini Imekuwa ikishinda tuzo mbalimbali zinazotolewa na taasisi za nchini na za nje.Mwaka jana Barrick Tanzania ilinyakua tuzo sita za OSHA.) Mgodi wa Dhahabu wa Barrick Bulyanhulu, ulishinda tuzo kubwa ya mshindi wa jumla.

Mbali na ushindi huo mkubwa, Bulyanhulu, pia ilinyakua tuzo ya uandaaji Ripoti Bora ya Tathmini ya Hatari katika uchimbaji madini na mshindi Bora wa tuzo ya Usalama na afya (OHS) katika sekta ya madini.

Kwa upande wake, Barrick North Mara, ilishinda tuzo za juu katika: Kujali zaidi Wafanyakazi wenye Mahitaji Maalum na utekelezaji sera bora ya Usalama mahali pa kazi (OHS). Pia ilikuwa mshindi wa pili kwa washindi wa jumla wa sekta ya Madini. Mgodi wa Buzwagi pia ulishiriki maonesho hayo na kunyakua tuzo ya utekelezaji Mpango Kazi Bora wa Usalama na Afya mahali pa kazi.

KAMPENI YA USALAMA BARABARANI YA AMEND YAWAFIKIA WAENDESHA BODABODA HALE WILAYA YA KOROGWE

April 28, 2024




Na Oscar Assenga,KOROGWE.

KAMPENI ya Usalama barabara inayotolewa na Jeshi la Polisi kwa kushirikiana an Shirika la Amend Tanzania kupitia Ubalozi wa Uswis nchini imewafikia waendesha pikipiki maarufu kama bodaboda eneo la Hale wilaya ya Korogwe huku ikielezwa zaidi ya waendesha Bodaboda kati ya 5 mpaka 10 wanapoteza maisha kwa siku katika Mkoa wa Tanga kutokana na ajali za barabarani.

Chanzo kikubwa kikitajwa ni kuchangia wa na kutokuzingatia sheria za usalama wanapokuwa wakiendesha vyombo vya moto pamoja na kuendesha mwendokasi.

Hayo yalisemwa na Kaimu Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Tanga (RTO) Hamis Mbilikila wakati wa utoaji wa elimu katika kampeni ya usalama barabarani iliyokuwa ikitolewa na Jeshi la Polisi kwa kushirikiana na Shirika la Amend kupitia ufadhili wa Ubalozi wa Uswis Tanzania iliyofanyika Hale wilayani Korogwe .

Hali hiyo inachangia kwa asilimia kubwa kupelekea kupoteza nguvu kazi kubwa ya vijana kutokana na asilimia kubwa kujiajiri kupitia sekta hiyo bila kuwa na elimu ya sheria za usalama barabarani wakati wakitekeleza majukumu yao ya kila siku.

Alisema ajali hiyo zinatokana na asilimia kubwa kutokuzingatia sheria za usalama barabarani hivyo uwepo wa mafunzo hayo ambayo yanatolewa na Shirika hilo kwa mkoa huo utasaidia kwa kiasi kikubwa kupunguza ajali zinazotokana na madereva hao wa pikipiki maarufu kama bodaboda.

Aidha alisema kwamba mafunzo hayo wanaamini yatakuwa na tija ka madereva hao ambao huku akiwataka pia kuacha kujichukulia sheria mkononi pindi ajali zinazopotekea kweye maeneo yao badala yake watoe taarifa kwenye mamlaka husika.

“Ndugu zangu bodabda ajali zinapotkea msijichukulie sheria mkonono mtoe taarifa mkoa wa Tanga ni wa kimkakati tumeona mambo mengi yanafanyika kuna bomba la mafuta kuna wageni wengi Bandari yetu imefunguka kuna njia inaunganisha nchi jirani na Kenya na hapa hale ni barabara kuu kuna watu wengi wanapita hivyo ni lazima tufuate sheria za usalama barabara”Alisema

Aidha aliwataka waendesha pikipiki maarufu kama bodaboda kuacha kujichukulia sheria za usalama barabarani kutokana na kwamba hawawezi kujua watakumbana na jambo gani lakini pia madhara ya ajali ni kupoteza maisha na vifo .

“Vijana wengi wanapoteza maisha kupitia vyombo hivyo pikipiki zimekuja kutusaidia na asilimia kubwa kwenye vijiji pikipiki ni muhimu hivyo kutokana na adhari hivyo Jeshi la Polisi kwa kushirikiana na Shirika la Amend kwa ufadhili wa Ubalozi wa Uswis wameona wawape mafunzo hayo ili tuweze kujua sheria za usalama barabarani”Alisema

Awali akizungumza katika mafunzo hayo Afisa Miradi kutoka Shirika la Amend Tanzania Scolastica Mbilinyi alisema lengo lao ni kupeleka mafunzo kwenye maeneo mbalimbali ili kuwafikia watu wengi sana kwenye kampeni ya usalama barabarani na sasa wanayafikia maeneo ya pembezoni ambao ni mpango kazi wa dunia kupunguza ajali angalau kwa asilimia 50 ifikapo mwaka 2030.

“Tulianza wilaya ya Tanga na baadae Mkanyageni wilaya ya Muheza walianza leo tupo Hale wilaya ya Korogwe na tumepanga kupeleka elimu hii kwenye maeneo mengi kwa sababu wengi hawana elimu ya usalama barabarani na itasaidia kuokoa maisha ya watu wengi zaidi baada ya kupata elimu hii”Alisema

Afisa Mradi huyo aliwataka bodaboda wafuata sheria za usalama barabarani ikiwemo wahakikishe wanatembea spidi inayotakiwa na sehemu kwenye matuta waweze kupunguza mwendo ikiwemo kuhakikisha pikipiki walizokuwa nazo zimekamilika kwa sabababu itawasaidia kupunguza ajali kwa asilimia kubwa .

“Lakini sisi tunatoa elimu ya usalama barabarani kwa shule za Sekondari,Msingi na kwenye Jamii pamoja na madereva wa pikipikimaarufu kama bodabda na tumekua tukishirikiana na Jeshi la Polisi na mafunzo hayo yanaratibiwa na Jeshi hilo”Alisema

Naye kwa upande wake Mratibu wa Shirika la Amend Tanzania Ramadhani Nyanza –aliwashukuru kwa bodaboda kwa mwitiko mzuri wao waliojitokeza kwa wingi huku akieleza mikakati yao baada ya kutoka Hale watakwenda Korogwe,Mombo, Segera, Handeni na Kilindi kwani hilo ni kundi kubwa lipo kwenye hatari kwa ajali ni bodaboda.

“Barabara zetu mnaziona kila siku mnaingia barabarani hakuna njia za waendesha pikipiki ni hiyo hiyo moja kisheria kama kuna sehemu wanatembea 50 nao wanatembea hivyo hivyo wanapiga honi muwapishe kwa hiyo mkijiweka kwenye hali ya kudharaulika na watu wanawafanya hivyo wao mnapoamua kuwatoa huko ni kampeni ya usalama barabarani hao wakiwa salama askari watakuwa salama na abiria wao”Alisema

Akizungumza na mmoja wa washiriki wa mafunzo hayo Isa Juma ambaye ni bodaboda kituo cha Hale alisema wanashukuru wamepata elimu hiyo nzuri na kuna mambo mengi wamejifunza ambayo watayatumia ili kuondokana na ajali za barabarani.

Alisema pia mafunzo hayo yamewapa mwanga wa kuona namna nzuri ya kutumia sheria za usalama barabarani kwani kuna vitu vingi walikuwa hawavijui na wameelezwa hivyo vitakuwa chachu kwao kuepukana na ajali .

CRDB BANK KUWAWEZESHA WANACHAMA WA TAPIE KUBORESHA ELIMU KATIKA SHULE BINAFSI

April 28, 2024

 

Dar es Salaam. Tarehe 27 Aprili 2024: Katika kuunga mkono juhudi za kuboresha elimu nchini, Benki ya CRDB imeasaini mkataba wa ushirikiano na Chama cha Wawekezaji katika Elimu Tanzania (TAPIE) utakaowawezesha wanachama wake kupata mikopo nafuu ya kuboresha miundombinu na kuwezesha uendeshaji wakati wote.

Mkataba huo umesainiwa tarehe 27 Aprili 2024 kwenye mkutano mkuu wa 5 wa mwaka wa TAPEI uliofunguliwa na Naibu Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Waziri wa Nishati, Mheshimiwa Dkt Doto Biteko na kuhudhuriwa na wadau wa elimu nchini.
Akizungumza na wajumbe waliohudhuria mkutano mkuu huo, Afisa Mkuu wa Biashara wa Benki ya CRDB, Boma Raballa amesema Benki inatambua changamoto wanazokutana nazo wamiliki binafsi wa shule hivyo imechukua hatua za kusaidia kuzitatua ili kuwa na mazingira rafiki kwa wanafunzi kusoma na kujifunza.

“Ni ukweli usiopingika kuwa elimu ndio msingi wa maendeleo ya Taifa lolote lile duniani kwani husaidia kujenga maarifa, ujuzi na kuongeza ufanisi hivyo kuwa kichocheo muhimu katika ukuaji wa uchumi. Kwa kuyatambua haya yote, Benki ya CRDB imeiweka sekta ya elimu katika moja ya vipaumbele vyake vya uwezeshaji. Tunafanya hivi ikiwa ni sehemu za kusaidia jitihada za Serikali pamoja na wadau wa sekta hii kutoa elimu bora itikayozalisha rasilimali watu bora katika nyanja mbalimbali,” amesema Raballa.

Kwa kuzitambua changamoto zilizopo ukiwamo ukweli kwamba uendeshaji wa shule unategemea mapato yatokanayo na ada ambayo mara nyingi hukusanywa shule zinapofunguliwa hivyo kuwa na uhaba pindi zinapofungwa, Benki ya CRDB imewaletea mkopo wa uendeshaji ili kukidhi mahitaji yanayopaswa kulipiwa wakati mapato mengine yakisubiriwa indi muhula mpya utakapoanza.
Raballa pia amesema shule nyingi zipo kwenye maeneo ambayo hayajarasmishwa jambo linalowanyima wamiliki uwezo wa kukopa kutokana na kutokidhi vigezo vya dhamana hivyo Benki ya CRDB imewaletea suluhisho kwa kuwaruhusu kukopa fedha zitakazowezesha urasmishaji wa maeneo yao ili kupata hati ya wizara itakayowaruhusu kukopa ili kuimarisha biashara zao.

“Tunawaruhusu wamiliki wa shule kukopa mpaka shilingi milioni 10 kwa ajili ya kurasmisha maeneo ya shule. Fedha hizi ni kwa ajili ya kutafuta hati ya wizara hivyo kuyatambulisha maeneo yao ya kisheria. Vilevile, tunayo mikopo kwa dhamana zisizo rasmi yaani maeneo ya shule ambayo hayana hati. Benki yetu inamruhusu mmiliki kuja kukopa mpaka shilingi milioni 100 kwa ajili ya kuimarisha miundombinu ya shule. Tunaamini kwa utaratibu huu rahisi na rafiki, tutasaidia kuwezesha uwekezaji wa shule katika sekta binafsi,” amesema Raballa.
Wakati wamiliki wakipewa mkopo wa uwekezaji wanaoweza kuurejesha mpaka kwa miaka 7, Raballa amesema walimu na wafanyakazi wa shule binafsi nao wanaweza kupata mkopo kwa ajili ya kufanikisha mambo yao binafsi. Mikopo ya wafanyakazi hawa, amesema inajumuisha ‘salary advance’ ambao ni mahsusi kwa wale ambao mishahara yao inapitia Benki ya CRDB ambao wanaweza kupata mpaka asilimia 50 ya mshahara wao na wakalipa ndani ya siku 30 pamoja na mkopo wa binafsi unaofika mpaka shilingi milioni 100 zinazoweza kurejeshwa kwa mpaka miaka 8. 
 
”Kwa miaka mitatu iliyopita, kiwango cha mikopo ya eimu tuliyoitoa kwa kundi hili imekuwa ikiongezeka. Mwaka 2021 Benki yetu ya CRDB ilikopesha zaidi ya shilingi bilioni 78.66 ambazo zilipanda mpaka shilingi bilioni 86 mwaka 2022 na mwaka jana zikawa shilingi bilioni 97.17. Nitumie fursa hii kuweka wazi kwamba mikopo hii tunayotoa kwa wamiliki wa shule binafsi hasa wanachama wa TAPIE, inaweza kurejeshwa mpaka kwa miaka 7,” amesisitiza Raballa.

Kwa upande wake, rais wa TAPIE, Mahmoud Mringo amesema hadi sasa kuna zaidi ya shule 6,362 zinazojumisha za awali 2,364, za msingi 2,270 na sekondari 1,728 zinazomilikiwa na watu binafsi, mashirika ya dini na yasiyo ya dini, majeshi, na jumuiya za wazazi ambazo zimedahili takriban wanafunzi 1,020,772 kuanzia elimu ya awali hadi kidato cha sita ambazo zimeajiri takribani walimu 59,445 na wataalamumwengine zaidi ya 100,000 wenye taaluma na ujuzi mbalimbali kama wahasibu, madereva, wasimamizi na walezi wa wanafunzi, walinzi na wapishi. Ajira hizi zimesaidia kuinua hali za kimaisha kwa watu husika na kupanua wigo wa kodi mbalimbali na hivyo kukuza uchumi wa taifa.

“Ukitaka kujenga darasa, maabara au kuboresha miundombinu mingine ya shule, ni lazima uende kukopa benki lakini tatizo ni riba kubwa. Kujenga shule ndogo tu kwa sasa unahitaji walau shilingi bilioni 2 lakini kuwa na shule yenye kila kitu basi unahitaji shilingi bilioni 10. Ukizikopa hizi kutoka benki na ukalipa kwa riba iliyopo, itakuchukua miaka 20 ya kumaliza deni ambalo ni lazima lilipwe na mwanafunzi. 
 
Bado kuna kodi na tozo 16 ambazo shule inatakiwa kulipa. Haya mambo yote yanaifanya elimu yetu kuwa ghali na kusoma shule zisizo za serikali inaonekana ni anasa,” amesema Mringo akiiomba serikali iangalie namna ya kupunguza riba ya mikopo tozo pamoja na kodi.
Akifungua mkutano huo, Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dkt Doto Biteko amepongeza juhudi za sekta binafsi kuchangia kuboresha elimu nchini kwamba zinaifanya jamii iwe na mchango zaidi katika kukuza uchumi. "Niwapongeze kwa ushirikiano na mkataba wa makubaliano mnayosaini leo na Benki ya CRDB. Ili kufanikisha mambo, ushirikiano na wadau wengine ni muhimu sana. Hivi mnavyofanya, ndio namna nzuri ya kukabiliana na changamoto zetu," amesema Dkt Biteko.



 


Benki ya CRDB yakabidhi madarasa Sekondari ya Kikilo, Shule ya Msingi Isabe, Kondoa

April 26, 2024

 

Benki ya CRDB kupitia sera yake ya uwekezaji kwa jamii, Aprili 24 - 25, 2024 ilikabidhi madarasa mawili katika Shule ya Sekondari Kikilo na madarasa mengine mawili katika Shule ya Msingi Isabe zote za wilayani Kondoa, mkoa wa Dodoma yaliyojengwa kwa ufadhili wa Benki hiyo.

Hafla ya kukabidhi madarasa hayo, iliyoongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Kondoa, Dkt. Khamis Mkanachi ambaye aliambatana na Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Kondoa pamoja na Maafisa Elimu Sekondari na Msingi.

Katika hafla zote mbili Dkt. Khamis Mkanachi ameishukuru Benki ya CRDB kwa kukubali maombi ya ujenzi wa madarasa katika Wilaya ya Kondoa, ambayo yapo katika vijiji vya Kikilo na Bukulu. Huku akitoa rai kwa wanafunzi kusoma kwa bidii kwani mazingira ya shule yanaendelea kuboreshwa.

Aidha, Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Kondoa, Mashauri Vicent aliyekabidhiwa madarasa hayo ameishukuru Benki ya CRDB kwa kuwa mstari wa mbele katika kuchangia maendeleo ya elimu pia kuahidi kuwa watahakikisha madarasa hayo yanakuwa ni sehemu ya kuchagiza ongezeko la wanufaika ambayo ni watoto kwenye jamii ya Kondoa.

Kwa upande wa Benki ya CRDB, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Benki ya CRDB, Dkt. Ally Laay aliyeongozana na Mkuu wa Kitengo cha Uwekezaji kwa Jamii pamoja na Kaimu Meneja wa Kanda ya Kati, amesema kuwa Benki ya CRDB imeweka sera ya uwekezaji kwa jamii inayolenga kuchangia maendeleo mbalimbali katika jamii hasa katika swala la Elimu, Mazingira, Afya, Vijana na Wanawake. Aidha, ametoa rai kwa wazazi wa shule hizo kuendelea kushirikiana kwa karibu na uongozi wa shule katika kuboresha miundombinu ya shule.
Mkuu wa Wilaya ya Kondoa, Dkt. Khamis Mkanachi na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Benki ya CRDB, Dkt, Ally Laay wakiwa pamoja na viongozi wengine pamoja na Wanafunzi katika moja ya madarasa mawili yaliyojengwa kwa ufadhili wa Benki ya CRDB yenye thamani ya shilingi Milioni 40 katika Shule ya Msingi Isabe, iliyopo katika kijiji cha Bukuru, Wilayani Kondoa, katika hafla  iliyofanyika Aprili 25, 202.
Mkuu wa Wilaya ya Kondoa, Dkt. Khamis Mkanachi (wanne kushoto) akimsikiliza Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Benki ya CRDB, Dkt, Ally Laay muda mfupi baada ya kukaidhi madarasa mawili yaliyojengwa kwa ufadhili wa Benki ya CRDB yenye thamani ya shilingi Milioni 40 kwa uongozi wa Halmashauri ya Kondoa.
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Benki ya CRDB, Dkt, Ally Laay (katikati) akiwa pamoja na viongozi wengine wa Benki ya CRDB pamoja na wa Halmashauri ya Kondoa wakiwa katika picha ya paamoja na Wanafunzi wa Shule ya Sekondari Kikilo, muda mfupi baada ya kukaidhi madarasa mawili katika shule hiyo
Mkuu wa Wilaya ya Kondoa, Dkt. Khamis Mkanachi akizungumza wakati wa hafla kukaidhi madarasa mawili yaliyojengwa kwa ufadhili wa Benki ya CRDB yenye thamani ya shilingi Milioni 40 kwa uongozi wa Halmashauri ya Kondoa.
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Benki ya CRDB, Dkt, Ally Laay akizungumza wakati wa hafla kukaidhi madarasa mawili yaliyojengwa kwa ufadhili wa Benki ya CRDB yenye thamani ya shilingi Milioni 40 kwa uongozi wa Halmashauri ya Kondoa.












Benki ya CRDB kupitia sera yake ya uwekezaji kwa jamii, Aprili 24 - 25, 2024 ilikabidhi madarasa mawili katika Shule ya Sekondari Kikilo na madarasa mengine mawili katika Shule ya Msingi Isabe zote za wilayani Kondoa, mkoa wa Dodoma yaliyojengwa kwa ufadhili wa Benki hiyo.

Hafla ya kukabidhi madarasa hayo, iliyoongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Kondoa, Dkt. Khamis Mkanachi ambaye aliambatana na Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Kondoa pamoja na Maafisa Elimu Sekondari na Msingi.

Katika hafla zote mbili Dkt. Khamis Mkanachi ameishukuru Benki ya CRDB kwa kukubali maombi ya ujenzi wa madarasa katika Wilaya ya Kondoa, ambayo yapo katika vijiji vya Kikilo na Bukulu. Huku akitoa rai kwa wanafunzi kusoma kwa bidii kwani mazingira ya shule yanaendelea kuboreshwa.

Aidha, Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Kondoa, Mashauri Vicent aliyekabidhiwa madarasa hayo ameishukuru Benki ya CRDB kwa kuwa mstari wa mbele katika kuchangia maendeleo ya elimu pia kuahidi kuwa watahakikisha madarasa hayo yanakuwa ni sehemu ya kuchagiza ongezeko la wanufaika ambayo ni watoto kwenye jamii ya Kondoa.

Kwa upande wa Benki ya CRDB, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Benki ya CRDB, Dkt. Ally Laay aliyeongozana na Mkuu wa Kitengo cha Uwekezaji kwa Jamii pamoja na Kaimu Meneja wa Kanda ya Kati, amesema kuwa Benki ya CRDB imeweka sera ya uwekezaji kwa jamii inayolenga kuchangia maendeleo mbalimbali katika jamii hasa katika swala la Elimu, Mazingira, Afya, Vijana na Wanawake. Aidha, ametoa rai kwa wazazi wa shule hizo kuendelea kushirikiana kwa karibu na uongozi wa shule katika kuboresha miundombinu ya shule.
Mkuu wa Wilaya ya Kondoa, Dkt. Khamis Mkanachi na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Benki ya CRDB, Dkt, Ally Laay wakiwa pamoja na viongozi wengine pamoja na Wanafunzi katika moja ya madarasa mawili yaliyojengwa kwa ufadhili wa Benki ya CRDB yenye thamani ya shilingi Milioni 40 katika Shule ya Msingi Isabe, iliyopo katika kijiji cha Bukuru, Wilayani Kondoa, katika hafla  iliyofanyika Aprili 25, 202.
Mkuu wa Wilaya ya Kondoa, Dkt. Khamis Mkanachi (wanne kushoto) akimsikiliza Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Benki ya CRDB, Dkt, Ally Laay muda mfupi baada ya kukaidhi madarasa mawili yaliyojengwa kwa ufadhili wa Benki ya CRDB yenye thamani ya shilingi Milioni 40 kwa uongozi wa Halmashauri ya Kondoa.
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Benki ya CRDB, Dkt, Ally Laay (katikati) akiwa pamoja na viongozi wengine wa Benki ya CRDB pamoja na wa Halmashauri ya Kondoa wakiwa katika picha ya paamoja na Wanafunzi wa Shule ya Sekondari Kikilo, muda mfupi baada ya kukaidhi madarasa mawili katika shule hiyo
Mkuu wa Wilaya ya Kondoa, Dkt. Khamis Mkanachi akizungumza wakati wa hafla kukaidhi madarasa mawili yaliyojengwa kwa ufadhili wa Benki ya CRDB yenye thamani ya shilingi Milioni 40 kwa uongozi wa Halmashauri ya Kondoa.
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Benki ya CRDB, Dkt, Ally Laay akizungumza wakati wa hafla kukaidhi madarasa mawili yaliyojengwa kwa ufadhili wa Benki ya CRDB yenye thamani ya shilingi Milioni 40 kwa uongozi wa Halmashauri ya Kondoa.