WENYE MAHITAJI MAALUM WAKUMBUKWA UDOM

November 29, 2023


Na Dotto Kwilasa,Dodoma

Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM)kimezindua Harambee ya kuwachangia wanafunzi wenye mahitaji maalum wanaosoma chuoni hapo ili kuchochea ari ya mafanikio yao ikiwa ni pamoja na kuongeza ushawishi kwa wanafunzi wengine wa kundi hilo kutokata tamaa ya kusoma. 

Hayo yamejiri November 29,2023 Jijini hapa kwenye Mkutano wa 14 wa Baraza la wahitimu wa Chuo hicho (UDOM) ambapo fedha zitazopatikana kupitia Harambee hiyo zitasaidia kukidhi mahitaji ya ada, magongo,vifaa wezeshi na mengineyo. 

Akizungumza kwenye Baraza hilo, Waziri wa Madini nchini Peter Mavunde ameipongeza hatua hiyo huku akitoa maelekezo kwa Uongozi wa UDOM kuandaa orodha ya wadau wa Chuo hicho na kuwaomba kuchangia ili kufikia malengo kwa kuwa kila mwenye ulemavu ana haki ya kuishi maisha mazuri.

Kwa kutambua umuhimu wa wenye mahitaji maalum Mavunde kwa upande wake amechangia shilingi milioni tano za kitanzania ambazo zitasaidia kuboresha baadhi ya mahitaji kwa wanafunzi hao.

"Mnatambua hapa nimemwakilisha Naibu Waziri Mkuu ambaye hajaweza kufika hapa kutokana na kuwa na majukumu mengine, yeye kwa upande wake ameahidi kutoa shilingi milioni kumi,na mimi binafsi natoa milioni tano naamini kabisa hii itaweza kusaidia kwa kiasi fulani," amesema

Kwa upande wake Naibu Makamu Mkuu wa UDOM anayeshughulikia Mipango,Fedha na Utawala Prof.Winesta Anderson ameeleza kuwa Chuo hicho kina jumla ya wanafunzi 160 wenye mahitaji maalumu . 

Amefafanua kuwa kati yao wenye uoni hafifu ni 12,walemavu wa ngozi 28,wenye ulemavu wa kutosikia ni 70 na wengine 46 waliosalia wapo kwenye kundi la ulemavu mwingine. 

"Amesema msingi wa jumuiya ya Tanzania unamtaka kila mwananchi kupata elimu bila kujali hali yake na kwamba kwa kulitambua hilo wao kama wadau wana mpango mkakati wake ambao utakamilika 2026 ukiwa umezingatia kwa undani mahitaji ya wanafunzi hao" amesema na kuongeza;

"UDOM kupitia convocation hii tumesema tulilete hili kama kampeni ya kuwasaidia wenye uhitaji kusoma na kufika chuo Kikuu,Wizara yetu mama ya elimu imeendelea kitusapoti kwa kutupatia bajaji nane,laptop 26, mafuta na bado tunaendelea kunapambana kuhakikisha kila sehemu inapitika ili wanafunzi wetu wawe salama,"amesema

Naye Mlezi wa wanafunzi wenye mahitaji maalum chuoni hapo kupitia Kurugenzi ya huduma za wanafunzi    Florida  Chambi ameeleza kuwa ili kufanikiwa katika kampeni hiyo,kiasi cha shilingi milioni 300 kinahitajika ambacho kitakusanywa kwa kipindi cha miezi 12 kuanzia sasa. 

Amesema fedha hizo zitasaidia pia kuboresha hali ya miundombinu ya wanafunzi hao ikiwa ni pamoja na kuboresha mazingira ya vyumba wanavyolala kuendana na hali yao. 

"Tunaishukuru Serikaki na Chuo hiki kwa jitihada zake mfano, Chuo kimeendelea kuwajali wanafunzi hawa kwa kuajiri madereva maalum wanaweza kuendesha bajaji na kuwarahisishia usafiri, Chuo pia kimetoa motisha kwa wanafunzi wanaowasaidia wenye mahitaji maalum kama Shukrani kwa kuwawekea mazingir wezeshi, "amesema

Chambi amesema Chuo hicho kinajali kuwatengea wanafunzi wenye mahitaji maalumu chumba cha mtihani na kueleza kuwa kupitia kurugenzi hiyo wanaendelea kuboresha zaidi kila eneo ili kuwawezesha wanafunzi hao kusoma kwa bidii kufikia malengo yao. 

Pamoja na hayo baadhi  ya wadau wa UDOM wameweza kuchangia harambee hiyo akiwemo Mkuu wa Mkoa wa Mbeya ambaye amemwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Rosemary Senyamule ambaye ameahidi milioni mbili,Ridhiwan Kikwete milioni mbili,Kituo cha uwekezaji million mbili huku Makamu mkuu wa Chuo hicho Prof.Lughano Kusiluka akiahidi kuchangia shilingi milioni mbili. 

WANASAYANSI WATAKIWA KUFIKISHA TAARIFA ZA UTAFITI KWA JAMII ILI ZIWAFIKIE WALENGWA.

November 29, 2023

 


Naibu katibu Mkuu Wizara ya Afya Dkt. Grace Maghembe amewataka wana sayansi nchini na wadau wa afya kufanya tafiti zitakazosaidia kuleta suluhisho juu ya changamoto mbalimbali zinazoikabili sekta ya afya hasa changamoto kubwa ya unyanyapaa katika jamii jambo linalochangia kwa kiasi kikubwa kuzorotesha juhudi za serikali na wadau wa maendeleo katika mapambano dhidi ya VVU na UKIMWI nchini.

Hayo yamesemwa na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Afya Dkt.Grace Maghembe wakati akifunga Kongamano la Kitaifa la Kisayansi lililofanyika katika Hoteli ya Nashera Mkoani Morogoro ambapo wadau na wataalamu wa masuala ya sayansi na tafiti walikutana kwa siku mbili kujadiliana kwa pamoja juu ya tafiti mbalimbali walizofanya zenye lengo la kutoa mwelekeo dhidi ya Maambukizi mapya ya virusi vya UKIMWI.

‘’Serikali itaendelea kujivunia wanataaluma wetu hasa wanaofanya tafiti za ndani zitakazoleta suluhisho katika jamii hasa kwenye sekta ya afya,na hakikisheni hizo tafiti mnazofanya ziwekwe kwenye lugha rahisi ambayo kila mtanzania ataelewa nini kimeandikwa na mzisambaze hadi ngazi ya chini kabisa ya serikali za Mitaa ilikusudi kila mtanzania aweze kunufaika na hayo machapisho yenu ya kitaalamu’’.AlisemaDkt Grace Maghembe Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Afya.

Aidha aliipongeza TACAIDS kwa uratibu wa kongamano hilo lililokutanisha wataalam na kujadili masuala muhimu yenye lengo la kutatua changamoto katika sekta ya afya hasa namna ya kujikinga na maambukizi mapya ya VVU na UKIMWI,alipongeza pia uwepo wa kongamano la vijana na wadau kusaidia uwezeshaji wa makongamano hayo yenye tija kubwa kwa vijana pia ni sehemu muhimu ya kupata maoni yao ili kujua ni namna gani serikali inaweza kuwekeza katika afua zinazowalenga. Hivyo kwa kufanya kungamano la vijana wa vyuo vikuu na hili lililofanyika hapa hoteli ya Nashera kwa siku mbili ambalo limekutanisha wataalamu na wadau mbalimbali wa masuala ya kisayansi katika kujadiliana kwa pamoja juu ya tafiti zilizofanywa zinatoa taswira gani kama taifa kwenye mapambano dhidi ya VVU na UKIMWI.

Dkt Grace Maghembe amesema kongamano hili lilikuwa na lengo la kukaa kwa pamoja kwa wadau na kujitathimini tunafanya kazi serikali pamoja na wadau wamaendeleo kutekeleza afua mbalimbali lakini pia na kufanya tafiti kwa wakati ilikuona namna ya kutekeleza afua mbalimbali katika kudhibiti maambukizi ya virusivya UKIMWI.

Amongeza kuwa, kupitia kongamano hili litasaidia serikali kuona kazi zilizofanyika mambo gani yaliyofanyika vizuri na mambo gani ambayo haya kufanyika vizuri na kutuonyesha mambo gani ya kujifunza kutoka taasisi mbalimbali,Aidha kupitia majadiliano haya yatatuwezesha kuandaa sera itakayotekelezwa kwa jamii kwasababu tayari tumeshafahamu nini jamii inahitaji huko ngazi za chini na kwakuwa tayari tumeshapata taarifa za kitaalamu za kitafiti.

Aidha ameongeza kwa kusema kuwa lazima tupambane kuhakikisha ili kufikia malengo ya 20/30 lazimatuangalietumefikiawapikwenyejitihadazamapambanokuanzialeolakini pia kuna changamoto kubwa kuhusiana na changamoto ya kukabiliana maambukizi kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto lazima iende kwa vitendo na amesema tumepiga hatua kubwa kwenye unyanyapaa lakini bado kuna changamoto kubwa ya unyanyapaa hadi leo watu wanaogopa kujitokeza kujitangaza kuwa anamaambukizi wa na kuwa hawako huru kuzungumza kwa familia na marafiki na waathirika wanavyokaa kimya ndio kunasababisha kuongezeka kwa maambukizi mapya jambo ambalo linahitaji tafiti za kina kuhusu suluhisho la kupambana na unyanyapaa katika Jamii.

POLISI SHINYANGA WAJIWEKA TAYARI KUKABILIANA NA UHALIFU KUELEKEA CHRISMAS NA MWAKA MPYA... BUNDUKI YAKUTWA SHULENI

November 29, 2023

 

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga ACP Janeth Magomi akionesha silaha aina ya Pistol Browning ikiwa na risasi 12 ambayo ilitelekezwa au kusahauliwa na mmiliki wake katika  moja ya shule ya Mjini Shinyanga kutokana na uzembe katika kumiliki silaha hiyo.

Na Mwandishi wetu - Malunde 1 blog

Kuelekea kipindi cha Sikukuu za Krismas na Mwaka mpya, Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga limeendelea kujiweka katika hali ya utayari ili kukabiliana na vitendo mbalimbali vya kihalifu, na kuhakisha ulinzi na Usalama wa raia na mali zao unaendelea kuimarika.

Akizungumza na vyombo vya habari leo Jumatano Novemba 29,2023 Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga ACP Janeth Magomi amesema  Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga limeendelea kufanya doria na misako katika maeneo yote ya Mkoa wa Shinyanga, kuimarisha vikundi vya ulinzi shirikishi ambapo hadi sasa kuna jumla ya vikundi hai 209 vinavyoshirikiana na Jeshi la Polisi. 


"Pia tunaendelea kutoa elimu kwa watumiaji wa barabara katika msimu huu wa sikukuu ili kuimarisha usalama barabarani, na kuwapeleka mahakamani wale wote wanaovunja sheria za usalama barabarani",amesema.

 Amefafanua kuwa, kwa kipindi cha mwezi mmoja uliopita, jumia ya madereva 06 wa magari walipelekwa mahakamani kwa makosa ya usalama barabarani, madereva 6,499 wa vyombo vya moto walitozwa fine na pia madereva 03 walifungiwa leseni zao. 

Hata hivyo amesema, kwa kipindi hicho cha mwezi mmoja uliopita, hakukuwa na ajali mbaya iliyojitokeza katika mkoa wa Shinyanga.


 "Kwa upande wa mahakama, jumla ya kesi 19 ziliweza kufanikiwa ambapo kesi 03 za makosa ya kubaka zilihukumiwa kifungo cha kati ya miaka 30 hadi kifungo cha maisha, kesi 01 ya kulawiti ilihukumiwa kifungo cha maisha jela, kesi 01 ya shambulio la aibu ilihukumiwa kifungo cha miaka 20 jela na fidia ya shilingi millioni moja, kesi 03 za wizi zilihukumiwa kifungo cha mwaka 01 jela, kesi 01 ya ukatili dhidi ya mtoto ilihukumiwa kifungo cha miaka 03 jela pamoja na fine ya shilingi laki tano, pia kesi 01 ya kumtorosha mwanafunz ilihukumiwa kifungo cha miaka 30 jela",ameeleza Kamanda Magomi.

"Vilevile kesi 01 ya kughushi nyaraka ilihukumiwa kifungo cha miaka 05 jela, kesi 01 ya wizi wa mtoto ilihukumiwa kifungo cha miaka 03 jela, kesi 02 za wizi wa mifugo zlihukumiwa kifungo cha mwaka 01hadi 05 jela na pia kesi 02 za kujeruhi zilihukumiwa kifungo cha mwaka 01 hadi 05 jela. Kesi zingine 02 za wizi wa Pikipiki ziliyohukumiwa kifungo cha miaka 02 na nyingine ya wizi ilihukumiwa kifungo cha miezi 06 jela na kulipa fidia ya shilingi milioni nane na kesi 01 ya kupatikana na bangi ilihukumiwa miaka 02 jela",ameongeza.

Ameongeza kuwa, katika mafanikio ya misako na doria wamefanikiwa kukamata jumla ya gramu 2205 pamoja na kete 61 za dawa za kulevya aina ya bangi, Pikipiki 11, mifuko 24 ya Cement, Ndoo 04 na makopo 04 ya rangi za majumba, Gypsum Powder na vifaa mbalimbali vya ramli chonganishi. 

Aidha kutokana na ushirikiano mwema kati ya Polisi na Jamii, amesema wananchi waliweza kutoa taarifa ya uwepo wa silaha aina ya Pistol Browning ikiwa na risasi 12 ambayo ilitelekezwa au kusahauliwa na mmiliki wake katika moja ya shule mjini Shinyanga kutokana na uzembe katika kumiliki silaha hiyo. 

Amesema jumla ya watuhumiwa 29 walikamatwa huku baadhi yao wakifikishwa mahakamani na wengine kupewa dhamana wakisubiri upelelezi wa kesi zao kukamilika.

 "Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga linatoa wito kwa wananchi wake kufuata Sheria na kutojihusisha na vitendo vya kiuhalifu, Madereva na watumia barabara kufuata sheria za Usalama barabarani ili kuepusha ajali zisizo za lazima, na litaendelea kuchukua hatua kali za Kisheria kwa yeyote atakayejihusisha na vitendo vya uhalifu",amesema.


GPE And CAMFED Host Roundtable On Education With Tanzanian CSOs

November 29, 2023

 Dar es Salaam, 29th November 2023 - The Chair of the Board of Directors of the Global Partnership for Education (GPE), H.E. Dr. Jakaya Mrisho Kikwete, Retired President of the United Republic of Tanzania, along with GPE’s Chief Executive Officer, Ms. Laura Frigenti, are set to participate in a significant roundtable discussion today at the Campaign for Female Education (CAMFED) Tanzania offices in Dar es Salaam.


According to Ms. Anna Sawaki, CAMFED Tanzania’s Director of Programs and Partnership, the primary objective of the roundtable is to collectively emphasise the importance of prioritising education on the political agenda.

Additionally, she said, the event aims to recognise the pivotal role of Civil Society Organisations (CSOs) in advocating for education and actively contributing to policy dialogue within local education groups.

“The roundtable will also provide an opportunity for CSO representatives to share their successful practices and experiences in supporting the transformation of education systems”, Ms Sawaki explained.

Among the CSOs expected to attend the roundtable are HakiElimu, PESTALOZZI, Shule Direct, UWEZO, Ubongo Kids, Lyra in Africa, World Vision, Binti Salha Foundation, TEN/MET, TEM/MET, CAMFED, CAMFED Tanzania, Transforming Life Tanzania, and Gender Networking (TGNP).

The Global Partnership for Education (GPE) is the largest global fund exclusively dedicated to reshaping education in lower-income countries. Operating as a unique, multi-stakeholder partnership, GPE works towards delivering quality education to ensure that every child, regardless of gender, has access to hope, opportunity, and agency.

For the past two decades, GPE has been actively disbursing funds and providing support to develop robust and resilient education systems in countries marked by extreme poverty or conflict. The focus is on enabling more children, particularly girls, to receive the education necessary for personal growth and contribution to building a more prosperous and sustainable world.

GPE's distinctive model has played a pivotal role in helping partner countries make significant strides in enhancing access, learning outcomes, and equity, resulting in improved educational opportunities for millions of boys and girls.

On the other hand, CAMFED, a pan-African movement, is leading a revolutionary approach to delivering girls' education. Through a gold-standard system of accountability to the young people and communities they serve, CAMFED has established a model that significantly improves the prospects of girls becoming independent and influential women.

CAMFED's work is driven at the grassroots level by local committees and teams comprising graduates, teachers, parents, government officials, and other volunteers who dedicate their time and expertise to ensure more girls successfully complete their education. The organisation’s governance structures include the boards of each national entity.

The roundtable represents a significant collaboration between GPE and CAMFED, bringing together key stakeholders and CSOs to reinforce the collective commitment to advancing education, particularly in regions facing the most pressing needs. This collaborative effort aligns with GPE's mission of transforming education systems and CAMFED's dedication to revolutionising girls' education across Africa.

The Chair of the Board of Directors of the Global Partnership for Education (GPE), H.E. Dr. Jakaya Mrisho Kikwete, Retired President of the United Republic of Tanzania, along with GPE’s Chief Executive Officer, Ms. Laura Frigenti, participate in a roundtable discussion with CSOs today at the Campaign for Female Education (CAMFED) Tanzania offices in Dar es Salaam.


The Chair of the Board of Directors of the Global Partnership for Education (GPE), H.E. Dr. Jakaya Mrisho Kikwete, Retired President of the United Republic of Tanzania, along with GPE’s Chief Executive Officer, Ms. Laura Frigenti, in a group photo with members of CSOs after their roundtable today at the Campaign for Female Education (CAMFED) Tanzania offices in Dar es Salaam.

FAO LA HUDUMA YA UTENGEMAO KUONGEZA FARAJA: PROFESA NDALICHAKO

November 29, 2023

 

 NA K-VIS BLOG/KHALFAN SAID

SERIKALI kupitia Mfuko wa Fidia kwa Wafanmyakazi (WCF) imetangaza Fao jipya la Huduma ya Utengemao wa Kijamii (Social Rehabilitation) kwa wafanyakazi wanaopata ulemavu na magonjwa yatokanayo na kazi na hivyo litawaongezea faraja, Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Mhe. Profesa Joyce Ndalichako, amesema.

Akizungumza jijini Dar es Salaam,  Novemba 29, 2023, alipokutana na wanufaika wa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) kuelekea Maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Watu wenye Ulemavu Duniani inayotarajiwa kufanyika kitaifa jijini Dodoma, Desemba 2, 2023. 

Profesa Ndalichako mesema, “Ndugu zangu hivi karibuni tutaanza kutoa Fao la Huduma ya Utengamao wa Kijamii na kutoa mafunzo ya kujenga ujuzi kwa wafanyakazi wanaopata ulemavu wakiwa kazini na aina ya ujuzi tutakaotoa utategemea uhitaji.” Alisema

Alisema lengo la Serikali ni kumpatia mfanyakazi ujuzi ambao utaendana na hali ya ulemavu wake, mfano alikuwa dereva na akapata ajali iliyopelekea ulemavu wa miguu, huyu anaweza kubadilisha ujuzi na kusomea kazi nyingine. 

Sambamba na kuwajengea ujuzi, fao hilo pia litatoa fursa ya kumjengea miundombinu inayoendana na hali yake, na hivyo kumuwezesha kumudu maisha katika mazingira anayoishi.” Alifafanua Profesa Ndalichako.

Kwa upande wao, wanufaika wa WCF wameishukuru Serikali kwa huduma wanazopokea kutoka katika Mfuko huo licha ya kupata ulemavu na wengine kuondokewa na wapendwa wao.

“Naomba kuhamasisha waajiri kuweza kuwachangia wafanyakazi wao, kwani viwango vya uchangiaji ni vidogo, tunaishukuru Serikali imepunguza viwango vya uchangiaji hadi kufikia asilimia 0.5” Alisema Norbert Tesha, ambaye amepata ulemavu wa kudumu baada ya kupata ajali akiwa kazini mwaka 2016.

“Hatuwezi kujua kesho yetu, lakini kama kuna misingi mizuri iliyowekwa leo, basi kesho yetu itakuwa njema, kila mtu ni mlemavu mtarajiwa.” Alisema, Bw. Tesha.

Mnufaika mwingine Bi. Emmaculet Nhigula, ambaye alimpoteza mumewe kwa ajali ya gari, amesema, “Mimi na watoto wangu wanne, tunanufaika sana na Mfuko huu, rafiki yetu kwa sasa ni WCF, huwa nikipita kwenye barabra hii na kuliona jengo lenu, ninasema hawa ni rafiki zangu wanaotembea na mimi nyakazi ngumu." Alisema

Alisema yale mafao ya kila mwezi yamekuwa na msaada mkubwa sana, yamesaidia kusomesha watoto wangu na sikuweza kuwahamisha kutoka shule walizokuwa wanasoma kabla ya kufariki baba yao.” Alisema Bi. Emaculate. 

Maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Watu Wenye Ulemavu, yanalenga kuwahamasisha viongozi wa taasisi za kibiashara Duniani kutambua mchango maridhawa wa watu wenye ulemavu.

Kwamujibu wa Shirika la Afya Duniani (WHO), kwasasa inakadiriwa kuwa watu bilioni 1.3 duniani wanaishi na changamoto ya ulemavu, hii ni sawa na asilimia 16% ya Watu wote duniani.

Kauli mbiu ya maadhimisho ya mwaka huu ni “ Tuungane katika hatua za Kuokoa na kufikia Malengo ya SDGs kwa Watu wenye Ulemavu”.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Mhe. Profesa Joyce Ndalichako (wapili kushoto) akiwa na Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF), Dkt. John Mduma (wakwanza kushoto), wakati akizungumza na wanufaika wa Fidia inayotolewa na WCF, kwenye Ofisi za Mfuko huo, jijini Dar es Salaam. 

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Mhe. Profesa Joyce Ndalichako akizunguzma kwenye mkutano na waandishi w ahabari jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Mhe. Profesa Joyce Ndalichako, akizungumza kwenye mkutano na waandishi w ahabari jijini Dar es Salaam. Kulia ni Mkurugenzi Mkuu wa WCF, Dkt. John Mduma.
 Mkurugenzi Mkuu wa WCF, Dkt. John Mduma, akizungumza mwanzoni mwa mkutano huo.
Bw. Norbert Tesha (kushoto), Mnufaika wa WCF, akitoa ushuhuda mbele ya waandishi wa habari jinsi anavyonufaika baada ya kupata ulemavu wa kudumu kufuatia kuumia katika ajali iliyotokana na kazi
Bw. Kelvin Cameroon,  mnufaika wa WCF, akitoa ushuhuda mbele ya waandishi wa habari jinsi anavyonufaika baada ya kupata ulemavu wa kudumu kufuatia kuumia katika ajali iliyotokana na kazi
Bi. Emmaculat Nzigula, Mtegemezi anayenufaika na mafao yanayotolewa na WCF baada ya kumpoteza mumewe aliyefariki katika ajali ya gari wakati akitekeleza majukumu ya mwajiri wake.
Profesa Ndalichako, akisalimiana na mmoja wa wategemezi wanaonufaika na mafao ya Fidia. Kulia ni Mkurugenzi Mkuu wa WCF.
Profesa Ndalichako, akizungumza na waandishi wa habari kwenye ofisi za WCF jijini Dar es Salaam. Katikati ni Mkurugenzi Mkuu wa WCF, Dkt. John Mduma na Bw. Rasheed Maftah, Mkurugenzi wa Kitengo cha Huduma kwa  Wenye Ulemavu, Ofisi ya Waziri Mkuu.

Picha ya pamoja.

POLISI TANGA YAWAKAMATA WATUHUMIWA 107, WAMO WA MAUAJI, WIZI WA MIFUGO NA UNYANG’AJI WA KUTUMIA SILAHA

November 28, 2023

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Almachius Mchunguzi akizungumza na waandishi wa habari ambao hawapp pichani mapema leo wakati akitoa taarifa kwa vyombo vya habari Jijini Tanga kwa kipindi cha mwezi mmoja kuanzia Octoba hadi Novemba 27, 2023.


Na Oscar Assenga, TANGA





JESHI la Polisi Mkoani Tanga limefanikiwa kuwakamata watuhumiwa 107 kwa makosa mbalimbali yakiwemo ya Mauaji,Wizi ya Mifugo,Unyang’anyi wa kutumia silaha ,kuingia nchini bila kibali pamoja na kupatikana dawa za kulevya aina mbalimbali.

Hayo yalisemwa leo na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Almachius Mchunguzi wakati akitoa taarifa kwa vyombo vya habari Jijini Tanga kwa kipindi cha mwezi mmoja kuanzia Octoba hadi Novemba 27, 2023.

Kamanda Mchunguzi alisema kwamba kati ya watuhumiwa hao 21 wamekamatwa na Bhangi kilogramu 43, Mirungi Kilogramu 124,

Heroin Gramu 242 huku wanne (4) wakikamatwa kwa kosa la kusafirisha wahamiaji haramu na watuhumiwa saba (7) raia wa Ethiopia kuingia nchini bila kibali.

Aliwataja wengine ni mtuhumiwa 01 kupatikana na kosa la unyang’anyi kwa kutumia silaha aina ya Panga na watuhumiwa wengine 74 wamekamatwa huku upelekezo ukiwa bado unaendelea.

Aidha Kamanda Mchunguzi alisema pia katika kuimarisha doria za nchi kavu na baharini Novemba 21 mwaka huu huko maeneo ya Kisiwa cha Jambe wilaya ya Tanga walifanikiwa kukamata boti aina ya Fibre yenye rangi nyeupe na bluu isiyokuwa na usajili ikiwa na injini ya Yamaha HP 15.

Alisema vitu nyengine vilivyokuwepo kwenye boti hiyo ni Chupa za Hewa ya Oxygen 02,(Diving Cylinder),mipira ya kupumulia 02 (regulator),Tega ya kuokotea Samaki,Kiberiti 01 na Samaki aina mbalimbali Kilogramu 30 waliovuliwa kwa kutumia baruti ambao walithibitishwa na Afisa Uvuvi kuwa hawafai kwa matumizi ya Binadamu.



Aliongeza kwamba watuhumiwa wamekimbia na kutelekeza boti hiyo baada ya kugundua wanafuatiliwa na Polisi wa Kikosi cha Wanamaji Tanga huku Upelelezi unaendelea kwa kuwatafuta watuhumiwa wa tukio hilo.

Hata hivyo Kamanda Mchunguzi alitaja tukio lingine kuwa ni Novemba 18 mwaka huu Jeshi hilo lilifanikiwa kumkamata Hamisi Kombo (46) mkazi wa Kwediboma wilaya ya Kilindi akiwa na wenzake nane .

Alisema wenzake wote hao ni waganga wa kienyeji ambao wanajihusisha na rasmi chonganishi wakiwa katika kijiji cha Kivindani Kata ya Tongoni Tarafa ya Pongwe wilaya ya Tanga ambapo wananchi wa eneo hilo waliwaita waganga hao kwa ajili ya kufanya ukaguzi katika nyumba za kijiji hicho ambazo zinasadikiwa kuwa na uchawi.

Kamanda huyo alisema uchawi huo ambao wanajiji hao walilalamika kuwa wakitendewa vitendo vya kudhalilishwa kwa kuvuliwa nguo na kuachwa wakiwa watupu kimazingara wakati wakiwa wamelala usiku,ambao watuhumiwa hao wote wapo nje kwa dhamana wakati upelelezi wa shauri hilo ukiendelea.

Katika hatua nyengine Kamanda Mchunguzi alisema katika kipindi mwezi mmoja Jumla ya watuhumiwa 41 wamefikishwa mahakamani,kesi 11 zinaendelea mahakamani na kesi 27 zimetolewa hukumu mbalimbali ambapo watuhumiwa watatu ambao ni Justis Kunael(40),Saidi Adam (32) na Maliki Amiri (38) wote wakazi wa Handeni wamehukumiwa kifungo cha Maisha kwa kosa la kubaka.

Kwenye tukio la Mauaji,Kamanda Mchunguzi alisema watuhumiwa Rashid Mwalimu “Chidi Kiwangwa”(32),Siwajui Kigaa “Sahonelo” (27) na Zuberi Hassani (34) wote wakazi wa Kijiji cha Kwandugwa wilayani Handeni walihukumiwa kunyongwa hadi kufa kwa kosa la mauaji ya mtoto wa Kike mwenye umri wa miaka (9).

WAKANDARASI WABABAISHAJI WASIPEWE KAZI BASHUNGWA.

November 24, 2023




Na Oscar Assenga,TANGA

Waziri wa ujenzi Innocent Bashungwa amemtaka Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Barabara nchini (TANROADS), kuhakikisha kuwa wakandarasi wasumbufu na wababaishaji hawapewi kazi za ujenzi wa barabara nchini kote.


Akizungumza alipokagua Barabara ya Handeni-Mafuleta 20km Bashungwa amesema ni aibu kuwa na mkandarasi msumbufu anaechelewesha kazi na bado kupewa miradi mingine hali inachelewesha maendeleo kwa wananchi.


Alimuagiza Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Barabara nchini  kuhakikisha Mkandarasi huyu HHEG hapewi mradi nyengine ya km 30 mpaka watakapojiridhisha na kasi yake ya ujenzi wa km 20 alizonazo sasa ifikapo Januari mwakani

Alisema haiwezekani mkandarasi anapewa kazi ya mradi wa km 30 na hakamilishi kwa wakati na bado wanafikiria kumpa eneo nyengine suala hilo haliwezi kukubalika hata kidogo 

Aidha Waziri Bashungwa alimtaka  Mtendaji Mkuu wa Tanroad kuhakikisha wanajipanga  vizuri na kusimamia wataalam wake ili Barabara ziweze kukamilika kwa wakati

" Wana ujenzi wote tuwahudumie watanzania kwa kutanguliza uzalendo mbele," amesisitiza Waziri Bashungwa"

 Waziri huyo amezungumzia umuhimu wa wakandarasi kuwa na uhusiano mzuri na wananchi katika ni maeneo wanayofanyia kazi kwani kufanya hivyo ni sehemu ya ulinzi kwenye miradi wanayoitekeleza.


Katika hatua nyengine Waziri Bashungwa amemuagiza Meneja wa TANROADS Mkoa wa Tanga Eng. Eliazari Rweikiza kuhakikisha HHEG anayejenga Barabara ya Handeni-Mafuleta anaboresha barabara inayotumika kati ya Handeni na Kilindi ili kupunguza kero ya usafiri kwa wananchi.

"Lakini Mtendaji Mkuu wa TANROADS hakikisheni  katika vipaumbele  vya barabara zitakazojengwa kwa lami iwe ni pamoja na barabara za Handeni-Mziha -Turiani( KM 108.2), Kiberashi-Songe (KM 33.5)na Songe-Gairo ili kuufungua vizuri mkoa wa Tanga hususan wilaya za Handeni na Kilindi"Alisema 


Awali akizungumza katika ziara hiyo Mtendaji Mkuu wa TANROADS Eng. Mohammed Besta alimueleza Waziri huyo kwamba  tayari TANROADS wameshawapanga mameneja wa miradi katika miradi yote 69 inayoendelea nchini ili kuhakikisha inatekelezwa kwa ubora unaotakiwa.

Kwa upande wake Mbunge wa jimbo la Handeni mjini Mh.Ruben Kwagirwa amempongeza Waziri wa ujenzi kwa miradi mbalimbali ya barabara inayoendelea mkoani Tanga na kusisitiza kwamba kufunguka kwa barabara ya Mkata -Kwamsisi (Km 36), Handeni Turiani (KM 108.2), Handeni- Kiberashi- Singida, (KM434), Kiberashi- Songe ( KM 33.5) na Songe -Gairo kutaufungua vizuri mkoa wa Tanga na kuuunganisha na makao makuu ya nchi Dodoma kwa njia fupi.


Waziri Bashungwa yupo katika ziara ya kukagua athari za mvua za vuli mkoani Tanga na kukagua miradi ya ujenzi wa barabara na madaraja inayoendelea mkoani Tanga.

PSSSF YATENGA MUDA MAALUM WA MAJUMA MANNE KUSIKILIZA NA KUZIPATIA UFUMBUZI CHANGAMOTO ZA WANACHAMA NCHI NZIMA TANZANIA NA ZANZIBAR.

November 23, 2023

 

NA K-VIS BLOG/KHALFANS AID, ARUSHA

MFUKO wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) umetenga muda maalum wa majuma manne kuanzia Novemba 27 hadi Disemba 22, 2023, kwa lengo la kusikiliza na kuzipatia ufumbuzi changamoto mbalimbali za wanachama, Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko huo, CPA. Hosea Kashimba, amesema.

CPA. Kashimba amesema hayo kwenye banda la PSSSF katika Maadhimisho ya Wiki ya Huduma za Fedha Kitaifa, kwenye uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini Arusha Novemba 24, 2023.

“Iwapo kuna mwanachama yeyote mwenye changamoto yoyote inayohusu uanachama, michango na mafao, afike katika ofisi za PSSSF zilizo jirani naye Tanzania bara na Zanzibar, tutamsikiliza na kutatua changamoto yake.” Alisisitiza.

Alisema zoezi hilo litakuwa likifanyika kuanzia saa mbili asubuhi hadi saa kumi na moja jioni, Jumatatu hadi Ijumaa.

“Lakini hata baada ya kipindi hicho maalum kufikia ukomo, bado tutaendelea kuwapatia huduma wanachama wetu, lengo hasa ni kuhakikisha wanachama wetu wanafurahia huduma zetu wakati wote.” Alisema CPA. Kashimba.

Pia amerejelea angalizo kwa wanachama na wastaafu, kuwa wasikubali kupokea maelekezo yoyote kutoka kwa watu wasiowajua endapo wanahisi wanachangamoto yoyote kuhusiana na uanachama wao au mafao yao.

“Tunawaasa wanachama wetu hususan wale wanaokaribia kustaafu, watambue kuwa huduma zetu zinatolewa bure bila malipo yoyote, na kama wanachangamoto yoyote wapige simu namba ya bure 0800 110 040 au kupitia mitandao yetu ya kijamii kupitia anuani ya PSSSFTZ.” Alifafanua CPA. Kashimba.

CPA. Hosea Kashimba, Mkurugenzi Mkuu PSSSF,

KITANDULA ATOA MSAADA WA VYAKULA NA FEDHA KWA WALIOKUMBWA NA MAFURIKO JIMBONI KWAKE

November 23, 2023




Na Mwandishi Wetu, MKINGA.

MBUNGE wa Jimbo la Mkinga (CCM) Dastan Kitandula ametoa msaada wa Vyakula na Fedha kwa Kaya 36 zilizopo kwenye Kata ya Manza na Mtimbwani wananchi katika Kijiji cha Msimbazi ambao walikumbwa na kadhia ya mafuriko kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha maeneo mbalimbali hapa nchini

Kitandula ambaye pia ni Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii aliamua kutoa msaada huo wakati akiwa kwenye ziara ya Jimbo hilo  ili kuhakikisha wananchi hao wanaaondokana na changamoto ambazo wamekumbana nazo kutokana na uwepo wa mafuriko hayo

Akizungumza wakati akiwa kwenye ziara hiyo pamoja alipokwenda kushuhudia zoezi la ukoaji wa wananachi katika Kijiji cha Msimbazi Kata ya Manza kutokana na mvua kubwa zinazoendelea katika maeneo mbalimbali hapa nchini.

Kitandula aliwaeleza wananchi hapo kwamba yupo pamoja nao na kuhaidia kuendelea kuwasaidia kuhakikisha wanaondokana na changamoto mbalimbali ili kuweza kujikwamua kiuchumi

Katika hatua nyengine Mbunge Kitandula alitoa msaada wa Pikipiki kwa kikundi cha wafugaji kwa ajili ya kukusanya maziwa kutoka kwa wafugaji wadogo wilayani humo.

Baada ya kuwakabidhi Pikipiki hiyo alimshukuru Mkuu wa wilaya hiyo Kanali Maulid Surumbu kwa kumshirikisha kwenye jambo hili ni kazi kubwa na nzuri ambazo zimekuwa zikifanywa kwa ajili ya kuwakwamua kiuchumi wafugaji hao

 “Nimeona niwaunge mkono kwa kuwapatia pikipiki hii naamini utakuwa chachu kwenu lakini pia niwaambie kwamba tupo pamoja na tutaendelea kushirikiana “Alisema

Awali akizungumza mmoja wa wanakikundi hao Abdala Mwajasi alimshukuru Mbunge huyo kwa msaada aliowasaidia huku akieleza mbunge huyo ni mahiri sana kuwasaidia wananchi hasa wanapokuwa wamekumbana na changamoto mbalimbali.

“Tunakushuru Mhe Mbunge Wetu kwa kutusaidia jambo hilo la umuhimu mkubwa kwa sababu sisi tauna uwezo wa kununua pikipiki “Alisema

WAZIRI BASHUNGWA ATOA MAAGIZO KWA TANROAD KUWASIMAMIA WAKANDARASI WANAOTEKELEZA MIRADI NCHINI

November 22, 2023
WAZIRI wa Ujenzi Inocent Bashungwa akikagua barabara inayotoka Kwamsisi kuelekea Pangani mkoa ni Tanga wakati wa ziara yake kulia ni Mkuu wa wilaya ya Handeni Albart Msando

Waziri wa Ujenzi Inocent Bashungwa akizungumza mara baada ya kuikagua barabara hiyo kushoto ni Mkuu wa wilaya ya Handeni Albarto Msando
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Handeni Saitoti Zelothe akizungumza wakati wa ziara hiyo kulia  ni Waziri wa Ujenzi Inocent Bashungwa





 Na Oscar Assenga,HANDENI




WAZIRI wa Ujenzi Inocent Bashungwa ameiagiza Wakala wa Barabara nchini (TANROAD) kuhakikisha wanawasimamia wakandarasi wanaotekeleza miradi ya barabara nchini kutokana na kusuasua na serikali kutoridhishwa na kasi ya ujenzi.



Sanjari na agizo hilo pia amesema iwapo miradi hiyo ya barabara itaendelea kusuasua atalazimika kumshauri Rais Dkt Samia Suluhu Hassan ambadilishe Mtendaji Mkuu wa Tanroad nchini Mohamed Besta kama ataendelea kucheka na wakandarasi hao bila ya kuwachukulia hatua.



Bashungwa aliyasema hayo leo wakati wa ziara yake ya siku moja wilayani Handeni na Pangani ambapo alikagua barabara ya kutoka Tanga-Pangani hadi Bagamoyo ambayo inatekelezwa na mkandarasi wa kampuni ya Kichina ya Railway 15, hakuridhishwa na kasi ya ujenzi wake.



Alisema kwamba kuna miradi mingi imekuwa ikisuasa suasua lakini bado wanaendelea kuiangalia bila kuchukua hatua jambo ambalo linakwamisha juhudi kubwa za Serikali kuifungua nchi kupitia miradi ya barabara ya kimkakati.



“Barabara hii nikuambie Mkurugenzi Mkuu wa Tanroad, kama hatutachukua hatua kwa muda unaotakiwa miradi kama hii inayoendelea kusuasua nitamshauri rais akubdilishe hatuwezi kuendelea namna hii”Alisema Waziri Bashungwa.



“Lakini pia Kaimu Mkurugenzi wa Miradi Tanroad tumemuamini tumekukaimisha ili usimamie hayo tumekuwa na wewe uone, Boniface Mkumbo yule aliyekuwa kabla yako nilipokuja kumtoa ilikuwa mbinde kwa sababu ya kulindana sasa Mkurugenzi Mtendaji baada ya wao utakuwa wewe kama usipobadilika”Alisema



Waziri huyo alisema haiwezekani anapokwenda kila kipande cha barabara nchini niwaamshe nyie hapana lazima mbadilike kama sijawaamsha na ile mipango mlioniambia naenda kukagua barabara lakini sitaki wakandarasi wa aina hii kule yule CR 7 hawa ni CR 15 wanaweza kukuta mtu na binadamu yake.



“Lakini yule CR 7 ni shida kwani miradi kama sita imesimama kwa sababu ya kurundikiwa miradi na nyie mnajiita CR 15 nyie mnauhusiana na C7 hii ni tatizo kila mradi mnaoufanya hii barabara wananchi mmesikia mipango ya Serikali ninakwenda kuikagua”Alisema



Aliwaambie wananchi tayari Serikali imeshaleta fedha lakini mkandarasi anawachelewesha wameona ni kwanini wanawachelewesha Mkurugenzi wa barabara hautakiwa kuwa ofisini unapaswa uzungumze maeneo mbalimbali nchini ili uweze kuona changamoto



Awali akizungumza wakati wa ziara hiyo Mtendaji Mkuu wa Tanroad alimueleza Waziri Bashungwa kwamba hatua ambazo wamechukua ni kumuelekeza mkandarasi aongeze vifaa na awe na mpango kazi ambao unaendana na wakati.



Alisema kwa sababu kwa sasa yupo nyuma ya asilimia 19 ya mpango wake ya kazi na Novemba 14 waliwaita makao makuu na kukaa kikao nao na baadae Novemba 28 wamewaita tena ili kuona kama yale maelekezo yametekelezwa.



Naye kwa upande wake Mkuu wa wilaya ya Handeni Albert Msando alisema kwamba wananchi wa eneo la Kwamsisi wameandika Historia kwa kuwa Waziri wa kwanza kufikia na kuzungumza nao na kutembelea barabara hii na wananchi walikuwa wamekata tamaa.



Alisema kwamba wanawaomba wanapokwenda kwa maofisi ya wakuu wa wilaya wasije na kuondoka na waache kujifungia ofisini wabadilike watumie ofisi zilizopo katika maeneo wanayotekeleza miradi.



“Mh Waziri sisi hapa leo tunapoteza tuna mazao mengi tunalima unaweza kukaa wiki nzima hautaja toa mazao na hivyo kupoteza mapato mengi ambayo serikali yangepatikana kwamsisi jana na juzi wamekusanya 0 hakuna gari zinaingia shambani kwa sababu ya ubovu wa barabara”Alisema



Alisema kwa sababu wao ni wazalishaji wengi ya muhogo barabara hii itakuwa mkombozi na wananchi hao watakukuyumbisha hivyo Tanroad lazima waangalie mahitaji ya wananchi na fedha imetengwa haenda hatua moja mbele.