DKT. NCHEMBA AWAAGIZA WATAALAM WA UCHUMI WA KITAIFA NA KIMATAIFA KUTAFUTA SULUHU YA UPUNGUFU WA DOLA ZA MAREKANI KATIKA SOKO LA FEDHA
Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb) akifungua kikao cha wataalamu wa Wizara hiyo na Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) kuhusu tathmini ya Program ya Huduma za Mikopo (EFC), jijini Dodoma. |
Na Farida Ramadhani-Dodoma
BWAWA LA KIDUNDA KULETA AHUENI DAR NA PWANI KIPINDI CHA KIANGAZI
Serikali kupitia Mamlaka ya Maji safi na Usafi wa Mazingira Dar es salaam (DAWASA) imeanza utekelezaji wa mradi wa ujenzi Bwawa la Kidunda litakalojengwa Mkoani Morogoro na kugharimu Tsh Bilioni 335 na litakalokuwa na uwezo wa kuhifadhi maji kwa yatakayotumika kwa miaka mitatu mfululizo.
PSSSF YAPEWA TUZO YA KIMATAIFA
NA
K-VIS BLOG/KHALFAN SAID, DAR ES SALAAM
MFUKO
wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) Umepewa tuzo na Taasisi ya
Kimataifa ya Hifadhi ya Jamii (International Social Security Association-ISSA)kutokana
na mafanikio iliyoyapata katika kipindi kifupi baada ya kuunganishwa (Merge)
kwa mifuko minne ya Hifadhi ya Jamii ya PSPF, PPF, GEPF NA LAPF na kuwa PSSSF.
Akizungumzia
tuzo hiyo, Mkurugenzi Mkuu wa PSSSF, CPA. Hosea Kashimba alisema sababu nyingine
iliyoifanya ISSA kutoa tuzo kwa Mfuko huo ni pamoja na jinsi Mfuko ulivyoweza
kupunguza gharama za uendeshaji na ulipaji wa mafao kwa wakati.
“Kwenye
suala la kuunganisha mifuko yapo mambo manne ambayo ISSA imeyaona na kuona ni
mafanikio ambayo ni pamoja na kupunguza gharama za uendeshaji, kutoa mafao
yanayofanana kwa wanachama wa Mfuko licha ya kutoka kwenye mifuko tofauti,
kukabiliana na madeni kabla ya mifuko kuunganishwa na pia suala la uwekezaji
hususan katika viwanda.” Alisema
CPA
Kashimba aliishukuru Bodi ya Wadhamini kwa usimamizi mzuri na hivyo kuufanya
Mfuko huo kufanya vizuri.
“Kazi
kubwa ya kusimamia zoezi hili la kuunganisha mifuko mmeifanya ninyi Bodi kwa
maelekezo ya serikali, sehemu nyingi duniani wanasema karibu asilimia 85 ya
kampuni zilizoungana huwa zinashindwa lakini muunganiko wetu sisi umeendelea
kufanya vizuri hadi kuivutia taasisi hii kubwa kuifanya PSSSF kuwa mfano wa
kuigwa.” Alisema CPA Kashimba.
Alisema
tayari Mfuko umeanza kupokea wageni KUTOKA sehemu mbalimbali wakihitaji kujifunza kutoka PSSSF.
“Juzi
kamati ya bunge ya Uganda wao wanaanzisha Mfuko wa Watumishi wa Umma na walikuja
kujifunza na wameridhishwa na elimu tuliyowapatia.” Alifafanua.
Alisema
tuzo hiyo ni zawadi kwa Bodi na sio Menejimenti pekee na mfuko uko kwenye
mikakati ya kuhakikisha unaendelea kutoa huduma bora kwa Wanachama na Wastaafu
kwa ujumla.
Awali Mkurugenzi wa Uendeshaji PSSSF, Bw. Mbarouk Magawa alidokeza kuwa eneo lingine ambalo liliwavutia watoa tuzo ni jinsi mfukoulivyofanya maboresho makubwa katika utoaji wa huduma kwa wastaafu na wanachama.
"Suala la Huduma kwa wananchama, jinsi tunavyokusanya michango, tunavyolipa mafao, kutoka kwenye matumizi ya hundi kulipa mafao, lakini jinsi tunavyohakiki wastaafu wetu, haya yote yaliwavutia." Alifafanua Bw. Magawa.
Aidha Meneja Uhusiano na Elimu kwa Umma (PSSSF) Bw. James Mlowe alisema PSSSF
ilikabidhiwa tuzo hiyo jijini Abidjan Ivory Coast Mei 17, 2023 na kwamba ifikapo
Agosti Mosi, 2023 PSSSF itafikisha miaka mitano tangu kuundwa kwake baada ya
kuunganishwa kwa mifuko (merge), Agosti Mosi, 2018.
“Majukumu
ya mfuko yanatekelezwa vizuri, uwezo wa mfuko unazidi kuimarika, watumishi
wanazidi kuwa kitu kimoja na kutekeleza majukumu yao ipasavyo na kwakweli mafanikio
haya ndiyo yamewavutia ISSA kuweza kutoa tuzo hii” Alisema
“Tunajisikia
faraja kwa tuzo hii na hii imekuwa chachu ya kuendelea kutekeleza majukumu yetu sawasawa
kuendelea kuwahudumia wanachama wetu na wastaafu kikamilifu.” Alitoa hakikisho.
Mkurugenzi wa Uendeshaji PSSSF, Bw. Mbarouk Magawa, akielezea mchakato uliopelekea PSSSF kupewa tuzo hiyo.
KLABU YA KWANZA YA MKONGE YAZINDULIWA
TETE FOUNDATION YAADHIMISHA SIKU YA HEDHI DUNIANI KATIKA KITUO NA SHULE YA AMANI, MVOMERO MOROGORO
Tarehe 28/5/2023 TETE FOUNDATION imeungana na jamii kuadhimisha Siku ya Hedhi Duniani, ambapo Taasisi hiyo imefanya maadhimisho hayo katika kituo na shule Amani iliyopo Mvomero - Mkoa wa Morogoro
Shule/ kituo cha Amani, ni kituo kinachojumuisha malezi ya kitaalam na kijamii Kwa Watoto Wanaoishi kwenye mazingira magumu, Uhitaji na wenye Ulemavu.
Ndani ya kituo hicho kuna Shule ya Msingi kuanzia darasa la awali Hadi darasa la saba na Shule ya Sekondari kuanzia kidato Cha kwanza hadi Cha Pili
Takwimu zinaonyesha kwamba mtoto wa kike anaeishi kwenye mazingira magumu, uhitaji na wenye ulemavu hukosa darasani siku 5 - 7 darasani kwa kukosa taulo za kike.
Katika maadhimisho hayo Mkurungezi wa TETE FOUNDATION, Bi. Suzana Senso amesema kutokana na takwimu hiyo, mwaka huu tumekuja na dhima "Sitakosa Shule Campaign" ambapo mwaka huu tumegawa taulo za kike za kutumia kwa muda wa miezi 6 kwa kila binti zaidi ya 50 waliopo kwenye shule ya Amani
Shukurani za kipekee kwa wadau walioshirikiana na TETE FOUNDATION kufanikisha hili zoezi ikiwemo UAP INSURANCE TANZANIA kwa kuwa sehemu ya kufanikisha zoezi hili bila kusahau wazalishaji wa taulo za kike za HQ PAD na Ministry ya “love of Christ Ministry” kwa kuwa sehemu ya kuhakikisha kila mtoto wa kike wa Shule ya Amani hakosi darasani kwa muda wa miezi 6 kutokana na kuwa kwenye hedhi
Asante kwa kuwa sehemu ya kurudisha tabasamu kwa mtoto wa kike 🙏🏾🙏🏾🙏🏾
@tete_foundation
TASAC YATOA ELIMU YA USALAMA, ULINZI NA UTUNZAJI WA MAZINGIRA MKOANI PWANI, KIBITI
Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC) limetoa elimu ya Usafiri Salama Majini kwa wadau mbalimbali wa Wilaya ya Kibiti katika mialo ya Nyamisati Mkoani Pwani tarehe 25 Mei, 2023.
Elimu hiyo iliyotolewa katika mialo iliyozunguka Nyamasati iliwajumuisha wavuvi, manahodha wa vyombo, wamiliki wa vyombo, wafanyabiashara na watumiaji wa vyombo vidogo vya usafiri majini.
Watoa mada mbalimbali kutoka TASAC, TPA na BMU walitoa elimu ya jinsi ya kutumia vifaa vya uokoaji pindi inapotokea dharura au ajali majini; utumiaji vifaa vya uokoaji pamoja na matumizi ya kizimia moto (fire extinguisher) na umuhimu wa kuwa na kifaa hicho kwenye vyombo vidogo vya majini.
TASAC imeendelea kushirikiana na wadau mbalimbali wa sekta ya usafiri majini kutoa elimu katika maeneo mbalimbali kwa lengo la kuwahamasisha wamiliki wa vyombo kuweka vifaa vya kujiokolea lakini pia manahodha na wavuvi kuvaa jaketi okozi wakati wote wawapo safarini au kuendesha shughuli za uvuvi.
MCHENGERWA, WANANCHI WA VIJIJI VYENYE MIGOGORO YA MIPAKA HIFADHI YA SERENGETI WAYAJENGA, WAIPONGEZA SERIKALI, WATAKA USHIRIKISHWAJI.
ALIYOYASEMA DC JOKATE BAADA YA KUFANYIKA MAMATHON KOROGWE
MHE UMMY AFANYA MKUTANO WA HADHARA WA JIMBO LA TANGA
MBUNGE wa Jimbo la Tanga (CCM) Ummy Mwalimu ambaye pia ni Waziri wa Afya akizungumza na wananchi wa Kata ya Makorora katika Jimbo hilo mwishoni mwa wiki wakati wa mkutano wake wa hadhara akielezea utekelezaji wa Ilani kwa miaka miwili
Mstahiki Meya wa Jiji la Tanga Abdurhaman Shillow akizungumza wakati wa mkutano huo
*Aanza na matembezi kuhimiza utunzaji wa mazingira na kufungua shina la vijana wa bodaboda Mikanjuni.
*Aelezea utekelezaji wa Ilani kwa miaka miwili.
*Amshukuru Mhe.Rais Dkt. Samia kwa kuendelea kumwaga mabilioni Tanga Mjini.
Mbunge wa Jimbo la Tanga Mjini Mhe Ummy Mwalimu ambae pia ni Waziri wa Afya tarehe 27/5/2023 amefanya mkutano wa hadhara kwa ajili ya kuelezea utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM kwa kipindi cha miaka miwili. Mkutano huo umefanyika katika viwanja vya Makorora Sokoni, Kata ya Makorora Jijini Tanga.
Katika mkutano huo uliofunguliwa na Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Tanga Meja Mstaafu Hamisi Mkoba, Mhe Ummy ameelezea utekelezaji wa yale yote yalioahidiwa na Mgombea uRais, ubunge na madiwani katika mikutano ya kuomba kura Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2020.
Mhe Ummy ameeleza mafanikio yaliyopatikana katika sekta za Elimu, Afya, Miundombinu ya Barabara, upatikanaji wa Maji na umeme hususani katika kata za pembezoni mwa jiji, maboresho ya Bandari ya Tanga, Masoko, Ongezeko la viwanda vya kati vitatu (3) na viwanda vidogo 21 na utoaji wa Mikopo yenye thamani ya shilingi bilioni 3,032,030,000 kwa vikundi 176 vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu.
Katika mkutano huo uliohudhuriwa na Mjumbe wa Kamati ya siasa Mkoa wa Tanga Ndugu Omari Ayoub, Mkuu wa Wilaya ya Tanga Mhe. Hashim Mgandilwa, Katibu wa CCM Wilaya ya Tanga, ndugu Selemani Sankwa, Katibu Itikadi na Uenezi ndugu Joel Mulenga, wajumbe wa Kamati ya Siasa ya Wilaya na sekretariet wilaya ya Tanga, Viongozi wa CCM Kata ya Makorora, wanaCCM na wananchi wa Jiji la Tanga, Mhe Ummy alirudia tena kuwashukuru wanatanga kwa kuendelea kumuamini na kuwaahidi hatawaangusha katika utekelezaji wa majukumu yake ya kibunge. Aidha alieleza kufurahishwa kwa jinsi wananchi walivyojitokeza kwa wingi kuhudhuria mkutano huo.
Imetolewa na;
Ofisi ya Mbunge, Jimbo la Tanga Mjini
28/5/2023
JIOPAKI PEKEE KUSINI MWA JANGWA LA SAHARA KUANZISHWA NGORONGORO - MHE MCHENGERWA
Na John Mapepele
Waziri wa Maliasili na Utalii - Mhe. Mohammed Mchengerwa amepokea timu ya wataalam saba kutoka nchini China ambao wamewasili nchini kwa ajili ya kuanza maandalizi ya utekelezaji wa mradi wa uendelezaji wa jiopaki ya Ngorongoro- Lengai, ambayo ndio jipaki pekee kusini kwa Jangwa la Sahara .
Pamoja na uimarishaji wa uhifadhi wa rasilimali za kijiolojia, mradi huu utaongeza vivutio vya utalii, ujenzi wa makumbusho ya kijiolojia, kuweka mitambo ya kufuatilia hatari za kijiolojia na kuwajengea uwezo wataalam wa kitanzania kuwezesha ukuaji utalii wa miamba na sura za nchi ( Geotourism and landscape tourism)
Mradi huu ambao utagharimu jumla ya dolla za kimarekani millioni 9.5 na kutarajiwa kukamilika baada ya miaka miwili na nusu, umefadhiliwa na Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China.
Makubaliano ya msaada huu yalisainiwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan alipofanya ziara ya kitaifa nchini China Novemba, 2022.
Mhe. Mchengerwa amefafanua kuwa dhamira ya Serikali kwa sasa ni kuimarisha uhifadhi wa raslimali na kutangaza vivutio mbalimbali vya utalii kimataifa na kutoa wito kwa wananchi kushirikiana kikamili kwa faida ya kizazi cha sasa na baadaye.
TAKUKURU DODOMA YAFUATILIA UTEKELEZAJI MIRADI 36 YA MAENDELEO
Na Dotto Kwilasa,DODOMA.
Taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa nchini (TAKUKURU)Mkoa wa Dodoma katika utekelezaji wa majukumu yake imepokea jumla ya malalamiko 138 ambapo kati yake, malalamiko 81 yalihusu rushwa na mengine 7 taarifa zake kuhamishiwa Idara nyingine kwa hatua zaidi.
Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Dodoma John Joseph amesema hayo leo Mei 26,2023 wakati akizungumza na Waandishi wa habari kuhusu ufuatiliaji utekelezaji wa miradi 36 ya maendeleo ya zaidi ya bilioni 16.8 ikiwa ni sehemu ya Utaratibu wake wa kutoa taarifa kwa kila kipindi cha miezi mitatu.
Amesema malalamiko 57 yalihusu rushwa ambapo yalipelekwa kufunguliwa majalada ya uchunguzi na kati ya hayo uchunguzi wa majalada 17 umekamilika ,mashauri mawili yamefunguliwa mahakamani na mengine 15 hatua mbalimbali za kisheria zinatarajiwa kuchukuliwa dhidi ya watuhumiwa.
Mkuu huyo wa TAKUKURU amefafanua kuwa Idara zinazo lalamikiwa Kutokana na taarifa 57 ni pamoja na Elimu (11), TAMISEMI (9),Sekta binafsi (9), Ardhi (7),Afya (7),Polisi(5),Kilimo(3),Manunuzi (2), Mahakama (1), Maji (1), Mazingira (1)na fedha (1).
"Mashauri mapya manne yametolewa maamuzi ambapo hadi sasa mawili tumeshinda na mawili tumeshindwa ,aidha jumla ya mashauri 31 yanaendelea kusikilizwa mkoani Dodoma na yako katika hatua mbalimbali,"amesema
Pamoja na hayo amesema katika kipindi cha miezi mitatu TAKUKURU Mkoa wa Dodoma wamefanya kazi za uzuiaji rushwa,uelimishaji wa jamii na uchunguzi.
Amefafanua kuwa katika jukumu la uzuiaji rushwa wamefanya tafiti 10 katika maeneo mbalimbali ya Mkoa wa Dodoma kwa Wilaya za Dodoma, Chamwino na Chemba na kufanya tafiti moja moja kwa kila Wilaya.
"Kwa Wilaya ya Bahi zilifanyika tafiti mbili na katika Wilaya ya Kongwa zilifanyika tafiti tano,tumeweza kufanya warsha tano ambazo zilitumika kuwasilisha matokeo ya chambuzi za mifumo zilizofanyika Kwa lengo la kushirikisha jamii kutafuta ufumbuzi dhidi ya mianya ya rushwa,"amefafanua.
Katika ufuatiliaji wa utejekezwaji miradi ya maendeleo, TAKUKURU Mkoa wa Dodoma imefuatilia miradi 36 yenye thamani ya zaidi ya bilioni 16 ambayo inatoka sekta mbalimbali ikiwemo elimu, afya, Ardhi, Kilimo, ujenzi, barabara na fedha .
Kwa mujibu wa Mkuu wa TAKUKURU Dodoma jumla ya miradi 22 ya elimu imefanyiwa ufuatiliaji, Kilimo miradi 5,fedha 3 na afya miradi 4 hali iliyosaidia kufikia fedha kiasi cha shilingi 1,050,000 katika Wilaya ya Chamwino.
"Miradi 21 imetolewa ushauri na elimu pia ufuatiliaji unaendelea, miradi 7 imekamilika ,miwili imetolewa maelekezo, chambuzi za mifumo ya warsha miradi miwili,miradi miwili inaendelea na ufuatiliaji nyaraka katika Wilaya ya Chamwino,"ameeleza