WAZIRI UMMY APIGIA CHAPUO VIVUTIO VYA UTALII TANGA

March 26, 2022

 

WAZIRI wa Afya Ummy Mwalimu akizungumza mara baada ya Kufungua Tamasha la Tanga Utalii Festival leo Jijini Tanga lililofanyika viwanja vya Urith Jijini humo ambalo liliandaliwa na Mkuu wa wilaya ya Tanga Hashim Mgandilwa
MKUU wa wilaya ya Tanga Hashim Mgandilwa akizungumza wakati wa Tamasha hilo
Naibu Mstahiki Meya wa Jiji la Tanga Calvas Joseph akizungumza wakati wa Tamasha hilo
WAZIRI wa Afya Ummy Mwalimu kulia akipata maelezo kutoka kwa Bandari ya Tanga mara baada ya kutembelea banda lao
WAZIRI wa Afya akipata maelekezo kwenye Banda la Benki ya Tanzania Comercial Benki wakati alipotembelea Banda lao
WAZIRI wa Afya Ummy Mwalimu kulia akimsikiliza kutoka kwa Benki ya NMB wakati alipotembelea Banda lao
WAZIRI wa Afya Ummy Mwalimu kushoto akipata maelezo kwenda Banda la Magoroto
WAZIRI wa Afya na Mbunge wa Jimbo la Tanga (CCM) Ummy Mwalimu  kushoto akimkabidhi cheti cha ushiriki mshiriki kutoka Kivutio cha Utalii cha Magoroto kilichopo wilayani Muheza Aisiana Mero wakati alipofungua tamasha la Tanga Utalii Festival kushoto ni Mkuu wa wilaya ya Same Mkoani Kilimanjaro Edward Mpogolo katikati ni Mkuu wa wilaya ya Mwanga Abdallah Mwaipaya
WAZIRI wa Afya na Mbunge wa Jimbo la Tanga (CCM) Ummy Mwalimu  kushoto akimkabidhi cheti cha ushiriki mshiriki kutoka Kivutio cha Utalii cha Magoroto kilichopo wilayani Muheza Aisiana Mero wakati alipofungua tamasha la Tanga Utalii Festival kushoto ni Mkuu wa wilaya ya Same Mkoani Kilimanjaro Edward Mpogolo akifuatiwa na Katibu Tawala wa wilaya ya Tanga (DAS) katikati ni Mkuu wa wilaya ya Mwanga Abdallah Mwaipaya
WAZIRI wa Afya na Mbunge wa Jimbo la Tanga (CCM) Ummy Mwalimu  akipokea tisheti wakati wa tamasha hilo

NA OSCAR ASSENGA,TANGA

WAZIRI wa Afya Ummy Mwalimu amefungua Tamasha la Tanga Utalii Festival huku  akipigia chapuo vivutio vya utalii vilivyopo Jijini Tanga kwa kuwashauri watalii wanapokwenda kutembelea Hifadhi ya Taifa ya Mkomazi waunganishe na Tanga kuona vuvutio vingine ikiwemo Beach nzuri,Visiwa vya Toten na Mapango ya Amboni.

Amesema pia Tamasha hilo la Tanga Utalii Festival litafungua fursa na kuongeza za kipato kwa wananchi wa mkoa wa Tanga na hivyo kuchochoe ukuaji wa uchumi kwa mkoa huo.

Ummy ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Tanga (CCM) aliyasema hayo leo wakati akifungua Tamasha la Tanga Utalii Festival ambalo limefanyika kwa mara ya kwanza ambalo limeandaliwa na Mkuu wa wilaya ya Tanga Hashim Mgandilwa na kushirikisha wadau kutoka maeneo mbalimbali.

Alisema upo umuhimu wa watalii wanapokwenda kutembelea hifadhi ya Taifa ya Mkomazi wanapomaliza badala ya kurudi uwanja wa ndege Kia watumia fursa hiyo kuja mkoani Tanga ili kuweza kuona vivutio adimi vilivyopo ikiwemo beach,visiwa na eneo la magoroto lenye vipepeo ambavyo havipatikani mahali pengine popote duniani.

Waziri Ummy alisema kwamba wanaweza kutumia jukwaa hilo ambalo kwa sasa litakuwa likifanyika kila mwaka kuhakaikisha wakuza fursa za ajira na uchumi kwa watu wa Tanga.

“Tunataka kulifanya Jiji la Tanga kuwa la Mahaba watu wa Mwanga na Same wanapokuja kutalii Mkomazi tutakaa na maombi yetu watu wasiiishie mkomazi waje na Tanga tuwapeleke visiwa vya toten,beach Usongo Pangani ambapo kuna mchanga mzuri halafu waende Magoroto Muheza wanaona vipepeo”Alisema

Hata hivyo alisema jambo hilo ni nzuri na wao wataendelea kumuunga mkono Mkuu wa wilaya ya Tanga huku akieleza kwamba Rais Samia Suluhu ametoa Milioni 500 kwa Jiji la Tanga kwa ajili ya kujenga Machinga Complex.

“Kwa kweli nimpongeza Dc Mgandilwa kwa kuandaa Tanga Utalii Festival ni jambo nzuri lengo lake ni kutaka kuonyesha utamaduni wa Tanga uzuri mila za Tanga nitoe wito kwa wakazi wa Tanga na nje ya Tanga kutembelea vivutio vilivyopo katika mkoa wa Tanga yakiwemo Mapango ya Amboni tunashukuru Mamlaka ya Ngorongoro wanayaboresha kila siku”Alisema

“Lakini Tanga pia tuna kisima cha maji Moto,Beach nzuri za kutembelea,kisiwa cha Toten tunaposema tunataka kulifanya Jiji la Tanga kuwa la mahabaa ukarimu na maendeleo ni kuonyesha mambo mazuri tulionayo ni jambo nzuri na sisi viongozi wenye asili ya Tanga tutakuunga mkono kuhakikisha tunaliboresha kila mwaka”Alisema

Awali akizungumza wakati wa tamasha hilo Mkuu wa wilaya ya Tanga Hashim Mgandilwa alisema waliona watumie jukwaa hilo kutangaza fursa za utalii uliopo Jijini Tanga ikiwemo Visiwa,Mapango na Makaburi ya Shabani Robert kwani waliona bado hayajatangaza ipasavyo.

Alisema sambamba na kutangaza vivutio hivyo lakini pia kutangaza Utalii uliopo eneo la Magoroto wilayani Muheza ikiwemo na baadhi ya samaki silikant huku akieleza kuanzishwa kwa tamasha hilo ni kutangaza vivutio vilivyopo kwa wadau.

Mkuu huyo wa wilaya alisema lengo lengine ni kuhamasisha wananchi kupata chanjo na kuhamasisha sensa ya watu na makazi kwa wananachi na wanaamini tamasha hili litakuwa endelevu lengo ni kutangaza utalii .

Naye kwa upande wake Mkuu wa wilaya ya Same Edward Mpogolo alisema wamekuja kumuunga mkono Waziri Ummy kutokana na kazi nzuri anayoifanya nchi na jimbo na wilaya ya Same umekuja kufanya kazi kubwa na nzuri hivyo pia niwahamasisha wananchi kutembelea vuvutio vya utalii vilivyopo nchini.

Hata hivyo Mkuu wa wilaya ya Mwanga Abdallah Mwaipaya Alisema wao kama wakuu wa wilaya za mkoa wa Kilimanjaro wameona kuna umuhimu wa kuja kuunga mkono tamasha hilo.

Mwisho.


MTAFITI AISHAURI SERIKALI HATUA KUKABILIANA NA MABADILIKO YA TABIA YA NCHI

March 25, 2022

 



MTAFITI Mwandamizi kutoka Taasisi inayojihusisha na Tafiti katika Nyanja za Uchumi na Jamii (ESRF) Vivian Kazi akizungumza wakati wa kikao hicho



Mtafiti kutoka Chuo Kikuu cha Kilimo (SUA) Morogoro Dk Winifred Mbungu akizungumza



Sehemu ya washiriki wa kikao hicho wakifuatilia kwa umakini

Sehemu ya washiriki wa kikao hicho wakifuatilia kwa umakini 
NA OSCAR ASSENGA,TANGA

MTAFITI Mwandamizi kutoka Taasisi inayojihusisha na Tafiti katika Nyanja za Uchumi na Jamii (ESRF) Vivian Kazi ameishauri Serikali kuona namna nzuri ya kuweza kuchukua hatua kukabiliana na mabadiliko ya tabia ya nchi kwa kuhakikisha wakulima wanalima kilimo kinachostahimili ukame

Vivian aliyasema hayo wakati wa kikao chao cha kuwasilisha utafiti ambao ulifanywa na Taasisi hiyo na Chuo Kikuu cha Sokoine Morogoro (SUA) kwa awamu mbili mwaka 2019 na 2021 lengo kubwa wamechagua Tanga kama eneo lenye sifa ya hali ya hewa inayowakilisha maeneo mengi nchini hali ya hewa nzuri kwenye nyanda za juu na chini   

Vivian ambaye pia ni  Mkuu wa Idara inayojihusisha na tafiti za kimkakati na machapisho na ESFR kwa kushirikiana na Chuo Kikuu cha Leeds,Abadin vya Uingereza,Sua na Chuo cha Ku cha Nelson Mandara Arusha wamekuwa wakifanya kazi ya mradi unaojihusisha na mabadiliko ya Tabia ya nchi.

Mradi huo wa miaka minne umefanyika na mapendekezo waliyoyatoa ni kuweza kulima kilimo stahimilivu na mabadiliko ya tabia ya nchi kuweza kutumia teknolojia ya chini au kati ili kuongeza kilimo tija na kuweza kulima mazao ambayo yataweza kustahimili mabadiliko ya tabia ya nchi.

Akizungumzia athari za mabadililo ya nchi,Vivian alisema mabadiliko ya tabia ya nchi yameathiri nchi nyingi tajiri na masiki ikiwemo kuathiri kwa kiasi kikubwa mabadilko ya mvua hatua ambayo inasababisha mazao kutokuua kwa wingi wakati wa mavuno.

 “Kwenye tafiti zenu tuliliona hilo na ifikapo mwaka 2050 kama zisipochukuliwa juhudi za makusudi athari zitakuwa kubwa kiasi huku wakishauri hatua zianze kuchukuliwa mapema kuweza kukabiliana nazo”Alisema

Alisema lengo la mkoa wa Tanga kuwepo miongoni mwa mikoa kwenye mradi huo unaojihusisha na mabadiliko ya tabia ya nchi kilimo stamilivu na usalama wa chakula kwa Tanzania kutokana na kuwa eneo lenye sifa ya hali ya hewa inayoweza kuwakilisha maeneo mengi nchini na kuna mpango wa kuongeza uwezo maafisa kilimo,maafisa ugavi.

Aidha alisema mradi huo ambao ulianza mwaka 2018 ambao ni wa miaka minne una lengo la mradi kushauri kwenye mambo ya sera kitu gani kifanyike kwa Tanzania kuhakikisha wanapambana na mabadiliko hayo ya tabia ya nchi.

Aliongeza namna ya kukabiliana nao ni kupunguza athari za mabadiliko ya tabia ya nchi kwa wakulima kulima kilimo stamilivu na kuangalia mazao yanayostahimili mabadilio hayo pamoja na usalama wa chakul,lishe na biashara kama watapata satras.

“Lakini kuna mafanikio mengi kwenye mradi mpango wa kuongeza uwezo maafisa kilimo,maafisa ugavi ,watafiti na wamefanya tafiti kwenye sera kwa kuhojiana na wadau mbalimbali  katika ngazi za wizara na ngazi za idara serikali na wakala mbalimbali”Alisema  

Hata hivyo aliwataka maafisa ugani mkoani Tanga kutumia vema elimu waliopewa  na taasisi hiyo ili kuweza kuwasaidia wakulima kuweza kulima kwa tija na kuondokana na kulima kimazoea ambapo wakati mwengine wanakosa mavuno.

Vivian aliyasema hayo wakati walikuwa na mkutano wao na watafiti na maafisa kilimo kutoka wilaya ya Muheza na Lushoto zilizopo mkoani Tanga kuweza kuwasilisha utafiti ambao

Awali akizungumza wakati wa mkutano huo Mtafiti kutoka Chuo Kikuu cha Kilimo (SUA) Morogoro Dk Winifred Mbungu  alisema ameshiriki kwenye utafiti na watalamu mwengine kutoka nchi za Afrika ambazo ni Malawi ,Zambia,Afrika Kusini na Tanzania  yeye pamoja na wengine wameshiriki kujaribu kuona mkusanyiko kufanya utafiti kwa ajili ya kuangalia athari diet na gesi.

Alisema katika utafiti huo ulikuwa shirikishi wao kama nchi walikwa wanaangalia wanapokwenda na kuangalia namna gani wanaweza kustahimili mabadiliko walilenga miaka 2050 ambapo mabadiliko yanatokea na maendelea yanatokokea.

Alisema miaka 2050 inakadiriwa joto linatarajiwa kuongezeka na linakwenda kuathiri mazao hasa ya wanayozalishwa lakini zao hilimilivu ni soya ambalo linaweza kuthimili na kwa Tanzania wana watu wanaokadiriwa milioni 60 na kwa mwaka 2050 inakadiriwa kutakuwa na watu milioni 100 sasa wanatakiwa wawe wanazalisha chakula ardhi hiyo hiyo hawataweza kwenda mbele kama hawatutaingiza teknolojia.

Kwa upande wake Kaimu katibu Tawala wa Mkoa wa Tanga Emigidius Kasunzu aliwataka maofisa kilimo kutumia elimu waliyoipata kuwaelekeza wakulima kulima mazao yanayohimili hali ya ukame .

Aliwataka wataalamu wa kilimo na waatafiti kufanya utafiti na ugunduzi wa mbegu bora pamoja na tekinolojia ya kisasa ili wakulima waweze kuwasaidia  kulima kulima kilimo chenye tija. 

" Uvunaji wa maji utunzaji wa mazinhira pamoja na upatikanaji wa mbegu bora utaweza kutusaidtia kujiepusha na baa la njaa kwa siku za mbeleni ' Amebainisha Kasunzu