SERIKALI YATOA BARAKA SHINDANO LA MISS TANZANIA,SASA RASMI KUBEBA SURA YA NCHI

March 31, 2018


Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk. Harrison Mwakyembe (kulia) akipokea mpango mkakati wa Mashindano ya urembo nchini (Miss Tanzania) kutoka kwa Mkurugenzi wa Kampuni ya The Look, Basilla Mwanukuzi ambaye sasa ndiye muendeshaji wa Mashindano hayo. Serikali imetoa baraka zake kwa uongozi wa The Look Company Limited kwa nia yake ya kurudisha heshima, hadhi na mvuto wa tasnia ya urembo hapa nchini kupitia Mashindano hayo.

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk. Harrison Mwakyembe (kulia) na Naibu wake, Juliana Shonza (kushoto) wakifurahi jambo na Mkurugenzi wa Kampuni ya The Look, Basilla Mwanukuzi baada ya mazungumzo yao, jana katika ofisi za Ukombozi wa bara la Afrika, zilizopo Garden avenue, Jijini Dar es salaam.

MAASKOFU,WACHUNGUJI KANDA YA ZIWA WABARIKI TAMASHA LA PASAKA 2018,WAMPONGEZA MSAMA PROMOTIONS.

March 31, 2018


Mkurugenzi wa Kampuni ya Msama Promotion Bw. Alex Msama akifafanua jambo mbele ya Maaskofu na Wachungaji wa mkoa wa jiji la Mwanza mapema leo jijini humo kuhusu upokeo na maandalizi ya tamasha la Pasaka linalotarajiwa kufanyika hapo kesho Aprili Mosi,ndani ya uwanja wa CCM Kirumba mkoani humo.
MKurugenzi wa Kampuni ya Msama Promotion Bw. Alex Msama akizungumza na Maaskofu na Wachungaji wa mkoa wa jiji la Mwanza mapema leo kwenye moja ya hoteli jijini humo,akieleza kukamilika rasmi kwa maandalizi ya tamasha la pasaka,linalotarajiwa kufanyika hapo kesho Aprili Mosi katika uwanja wa CCM Kirumba mkoani humo.

Msama amewashukuru Maaskofu hao na Wachungaji kwa kujitoa na kuunga mkono Tamasha la Pasaka 2018,ambalo kwa mara ya kwanza linaanzia kufanyika jijini Mwanza na baadae kuhamia mkoa wa Simiyu ndani ya mji wa Bariadi April 2 ndani ya uwanja wa Halmashauri,aidha tamasha hilo litakuwa na waimbaji lukuki ambao tayari wameishatangazwa kushiriki,kuhakikisha tamasha hilo linafana.

Kwa upande wa Maaskofu wameipongeza Kampuni ya Msama Promotions,chini ya Mkurugenzi wake Alex Msama kwa kuupa mkoa wa Mwanza kipaumbele kwa kuleta tamasha hilo mkoani humo,Wameongeza kuwa tamasha hilo litawavuta waumini wengi na wapenzi wa muziki wa injili na kuwaleta pamoja ili kupata neno la mungu na uponyaji kwa njia ya uinjilisti wa nyimbo za injili .





katika picha kutoka kushoto ni Askofu Charles Sekelwa Mwenyekiti wa Umoja wa Makanisa Mwanza na Askofu Zenobius Isaya kutoka kanisa la Philadephia Gospel Asembly na mlezi wa Msama Promotion Kanda ya Ziwa.


Askofu Zenobius Isaya kutoka kanisa la Philadephia Gospel Asembly na mlezi wa kampuni ya Msama Promotion Kanda ya Ziwa,akitoa ufafanuzi wa namna tamasha hilo la Pasaka 2018 lilipofikia na maandalizi yake kwa ujumla,mbele ya kikao cha Maaskofu na Wachungaji kilichofanyika mapema leo jijini humo,kulia ni Mkurugenzi wa Msama Promotion Bw. Alex Msama na kushoto ni Askofu Charles Sekelwa Mwenyekiti wa Umoja wa Makanisa Mwanza.



Mmoja wa maaskofu akitoa mchango wake katika kikao hicho kilichofanyika jijini Mwanza leo.
Askofu Joyce Mangu wa kanisa la Calvary Assemblies Of God Mjini Kati jijini Mwanza akizungumza wakati akitoa mchango wake katika kuboresha tamasha hilo siku za usoni na kwamba amefurahishwa sana na ujio wa tamasha hilo kwa jiji la Mwanza.




Baadhi ya maaskofu na wachungaji wakifuatilia kikao hicho.
-- Ahmad Issa Michuzi Editorial Director P.O BOX 9033, DAR ES SALAAM. issamichuzi.blogspot.com www.michuzijr.blogspot.com othmanmichuzi.blogspot.com Phone:0713 422 313/ 0783 422 313 Tanzania- East Africa.

RC SHIGELLA MGENI RASMI TANGA CITY MARATHON JUMAMOSI WIKI HII MJINI TANGA

March 30, 2018


Mratibu wa Mashindano ya Riadha ya Tanga City Marathon, Juma Mwajasho kulia akitetea jambo na waandishi wa habari kuhusu maandalizi ya kuelekea mashindano hayo Jumamosi wiki hiikushoto ni Meneja wa Mkwabi Super Market ya Jijini Tanga ambao niwaandaaji wakuu wa mbio hizo,Kawkab Hussein na Katibu wa Chama cha Riadha Mkoani Tanga (RT) Hassan Mwagomba
Katibu wa Chama cha Riadhaa Mkoa wa Tanga (RT) Hassan Mwagomba akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na uwepo wawashiriki kutoka Visiwa vya Shelisheli, Unguja na Pemba ambao watapat afursa ya kuonyesha umahiri wao kulia ni Meneja wa Mkwabi Super Marketya Jijini Tanga ambao ni waandaaji wakuu wa mbio hizo,Kawkab Hussein,

Meneja wa Mkwabi Super Market ya Jijini Tanga ambao ni waandaaji wakuu wa mbio hizo, Kawkab
Hussein akizungumza na waandishi wa habari kwenye mkutano huu kuhusiana na zawadi zitakazotolewa msimu huu

Sehemu ya medali zitakazotolewa kwenye mashindano hayo

MKUU wa mkoa wa Tanga, Martine Shigella ametarajiwa kushuhudia mashindano ya riadha ya Tanga City Marathon msimu wa piliyanayotazamiwa kufanyika Jumamosi wiki hii mjini hapa.

Akizungumza na waandishi wa habari, Mratibu wa Mashindano hayo, Juma Mwajasho alisema maandalizi yamekamilika kwa asilimia kubwa huku baadhi ya washiriki wakithibitisha kushiriki.

Alisema katika mashindano hayo msimu huu watazamia washiriki zaidi ya600 ambapo washindi watakabidhiwa zawadi mbalimbali zikiwemo medali ambazo zimeandaliwa na wadhamini wa mashindano hayo.

Aidha alisema mashindano hayo yatashirikisha wakimbaji kwenye umbali wa kilomita 21,10 na 5 ambapo wataanzia mbio hizo kwenye eneo la Mkwabi Super Market kuzunguka maeneo mbalimbali Jijini Tanga na kuishia eneo hilo.

“Lakini kwa mara ya kwanza washiriki wote watakaoshiriki mashindano hayo watapewa medali na mgeni rasmi kwenye mashindano hayo.

Kwa upande wake, Katibu wa Chama cha Riadhaa Mkoa wa Tanga (RT) Hassan Mwagomba alisema mashindano hayo pia yatashirikisha washiriki kutoka Visiwa vya Shelisheli, Unguja na Pemba ambao watapata fursa yakuonyesha umahiri wao.

Alisema njia zitakazopitia mashindano hayo zimeboreshwa zaidi kiusalama kwa wakimbiaji ili kuweza kuepukana na adhari zinazoweza kujitokeza wakati yakiendelea.

Naye kwa upande wake,Meneja wa Mkwabi Super Market ya Jijini Tanga ambao ni waandaaji wakuu wa mbio hizo,Kawkab Hussein alisema msimu huo wameboresha mashindano hayo kwa kutoa zawadi kwa mshindi wa kwanza hadi wa kumi.

Alizitaja zawadi zinazotolewa kuwa ni mshindi wa kwanza km 21 atapata700,000 wa pili 500,000, huku mshindi wa tatu akipata 300,000 huku wengine kuanzia wa nne hadi wa kumi watapata kifuta jasho cha 50,000.

Hata hivyo alisema katika kilomita 10 mshindi wa kwanza atapata 250,000, wa pili 150,000 na wa tatu 100,000 huku washindi wa kuanzia nafasi ya nne mpaka 10 watapewa 30,000 pia kutakuwa na vituo maalumu kwaajili ya kutoa huduma ya maji kwa wakimbiaji.

WATALII WENGI WAZIDI KUTEMBELEA TANZANIA - WAZIRI KIGWANGALLA

March 30, 2018


Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Dkt. Hamisi Kigwangalla (kushoto) akipokelwa na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Maj. Gen. Gaudensi Milanzi mjini Dodoma jana ambapo alikuwa mgeni rasmi katika Mkutano wa 25 wa Baraza la wafanyakazi wa Wizara hiyo.
.............................................................................

Tanzania imefanikiwa kuongeza idadi ya watalii kutoka 1,284,279 mwaka 2016 hadi kufikia 1,327,143 mwaka 2017 hali iliyopelekea kuongezeka kwa mapato ya Serikali.

Akizungumza wakati wa Mkutano wa 25 wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara ya Maliasili na Utalii uliofanyika mjini Dodoma, Waziri wa Wizara hiyo, Dkt. Hamisi Kigwangalla amesema Wizara yake itaendelea kuvutia watalii wengi zaidi ili kukuza utalii na kuongeza pato la Taifa.

“Mapato yanayotokana na utalii yameongezeka kutoka Dola za Kimarekani Bilioni 2.1 mwaka 2016 hadi Dola za Kimarekani Bilioni 2.2 mwaka 2017” alisema Dk. Kigwangalla.

Akifafanua Dkt. Kigwangala amesema lengo la Serikali ni kuona mafanikio haya yanazidi kuimarika, hivyo kila mtumishi katika Wizara hiyo lazima atimize wajibu wake ipasavyo katika kutimiza lengo la Wizara hiyo ambalo ni kuhifadhi na kusimamia maliasili, malikale na kuendeleza utalii.

Aliongeza kuwa ili kufanikisha majukumu ya Wizara hiyo ipasavyo ni muhimu kuwa na bajeti ambayo itawezesha kushughulikia changamoto za migogoro ya mipaka katika maeneo ya hifadhi, kufanya mapitio ya Sera, Sheria na Kanuni mbalimbali, upungufu wa watumishi, uhaba wa vitendea kazi, kutoa elimu ya maadili na kusimamia watumishi.

Alisema Wizara yake itaendelea na mapambano dhidi ya ujangili, biashara haramu ya nyara, magogo na kuwachukulia hatua kali za kinidhamu na kisheria kwa watumishi wote watakaogundulika kukiuka maadili ya utumishi wa umma kwa kushiriki katika vitendo hivyo.

Kwa upande wake Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Meja Jenerali Gaudensi Milanzi amesema kuwa Wizara hiyo itazingatia ushauri utakaotolewa na Baraza la Wafanyakazi wa Wizara hiyo ili kuongeza tija katika kutatua changamoto zinazojitokeza.

“Wizara itaendelea kupambana dhidi ya ujangili, biashara haramu ya nyara na magogo na kuwachukulia hatua kali watumishi wote watakaogundulika kukiuka maadili ya utumishi wa umma kwa kushiriki katika vitendo hivyo “ Alisisitiza Meja Jenerali Milanzi.

Wizara kwa mwaka wa fedha 2017/2018 iliendelea na utaratibu wa kuendeleza watumishi katika mafunzo ya aina mbalimbali kama ifuatavyo:-Jumla ya watumishi wanne (4) wanahudhuria mafunzo ya muda mrefu nje na ndani. Aidha, mtumishi mmoja(1) yupo nje ya nchi.

Watumishi wengine kumi na moja (11) walihudhuria mafunzo ya muda mfupi. Mafunzo haya yalihusu watumishi wa kada mbalimbali.

Jumla ya watumishi saba (7) wamehudhuria mafunzo ya ujasiliamali unaohusiana na maandalizi ya kustaafu. Aidha, Wizara bado inaendelea na utaratibu wa kuwaandaa watumishi wote wanaokaribia kustaafu kuhakikisha wanapata mafunzo hayo.

Akifunga mkutano huo wa siku moja Naibu Waziri wa Wizara hiyo, Mhe. Japhet Hasunga aliwataka watumishi wa Wizara hiyo kufanya kazi kwa bidii, juhudi na maarifa ili kufikia lengo lililokusudiwa la uhifadhi wa maliasili, malikale na kuendeleza Utalii.

Waziri wa Mali Asili na Utalii Mhe. Dkt. Hamisi Kigwangalla akihutubia Wafanyakazi wa Wizara hiyo wakati wa Mkutano wa 25 wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara hiyo uliofanyika mjini Dodoma jana.

Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii Maj. Gen. Gaudensi Milanzi akizungumza na Wafanyakazi wa Wizara hiyo wakati wa mkutano huo.


Baadhi ya wajumbe wa mkutano huo wa baraza wakisikiliza hotuba ya mgeni rasmi, Mhe. Dk. Hamisi Kigwangalla.


Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Dkt. HamisI KigwangalLa (katikati) akiimba wimbo wa mshikamano pamoja na Katibu Mkuu Wizara hiyo, Maj. Gen. Gaudensi Milanzi pamoja na viongozi wengine wa Shirikisho la Wafanyakazi.


Baadhi ya ya Wakurugenzi na Wakuu wa Taasisi wa Wizara ya Maliasili na Utalii Wakiimba wimbo wa mshikamano wa wafanyakazi wakati wa mkutano huo uliofanyika mjini Dodoma.


Naibu Waziri wa Malisili na Utalii, Mhe. Japhet Hasunga (kushoto) akisalimiana na Katibu Mteule wa Tughe Tawi la Wizara ya Maliasili na Utalii, William Mwita muda alipowasili kufunga mkutano huo wa baraza. Katikati anayemtambulisha kwake ni Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii, Maj. Gen. Gaudence Milanzi.


Naibu Waziri wa Malisili na Utalii, Mhe. Japhet Hasunga (kulia) akiteta jambo na Katibu Mkuu Wizara wizara hiyo, Utalii, Maj. Gen. Gaudence Milanzi muda mfupi kabla ya kufunga mkutano huo wa baraza la wafanyakazi wa wizara hiyo.


Naibu Waziri wa Malisili na Utalii, Mhe. Japhet Hasunga (kulia) akizungumza na watumishi wa wizara hiyo wakatika akifunga mkutano huo wa baraza la wafanyakazi wa wizara hiyo.



Baadhi ya Wakurugenzi na Wakuu wa Vitengo wa Wizara hiyo walioshiriki baraza hilo.

Baadhi ya watumishi wa Wizara na wajumbe wa baraza hilo.

WANAFUNZI UTUMISHI WATOA MISAADA KWENYE KITUO CHA KULELEA WAZEE WASIOJIWEZA CHA MWANZANGE

March 29, 2018


Kaimu Mkurugenzi wa Chuo cha Utumishi wa Umma Jijini Tanga Elibariki Mushi wa pili kutoka k ulia ni akimkabidhi vyakula na vifaa Afisa Mfawidhi Makao ya Wazee Wasiojiweza Mwanzange Jijini Tanga Otilia Chilumba kutoka kwa wanafunzi wa chuo cha utumishiwa Umma tawi la Tanga ikiwa ni mkakati wa kusaidia jamii isiyojiweza kulia ni mratibu wa zoezi hilo Dastan Kingalu

Kaimu Mkurugenzi wa Chuo cha Utumishi wa Umma Jijini Tanga Elibariki Mushi wa pili kutoka kulia ni akimkabidhi mbuzi mmoja wa wazee wanaoishi kwenye kituo hicho kwa niaba ya wenzake


CHUO cha Utumishi wa Umma Tawi la Tanga kimetoa msaada kwenye kituo cha kulelea wazee wasiojiweza cha Mwanzange Jijini Tanga ikiwa ni mpango wao wa kuona namna ya kusaidia jamii inayokabiliwa na changamoto mbalimbali.

Msaada uliokabidhiwa ni mchele kg 500, unga kg 300, sukari mifuko 2 kg100,sabuni ya unga mifuko 3,sabuni ya maji box 10,sabuni ya kuogeakatoni 2,maharagwe kg 100,chumvi katoni 10,mbuzi wawili.

Vitu vyengine ambazo vilikabidhiwa ni majani ua chai katoni 2,dagaa kg10,ngano kg 50,miswaki katoni 5,dawa za meno katoni nne,mafuta yakula ndoo tatu na mafuta ya kupikia katoni 10 vyote vina thamani yash.milioni 2.2.

Akizung umza wakati wakikabidhi msaada huo ,Kaimu Mkurugenzi wa Chuo cha Utumishi wa Umma JijiniTanga Elibariki Mushi aliwataka wanafunzi wajifunze taaluma hiyokatika mtazamo mpana ambao utawasaidia kuwajenga katika nyanja yakutatua changamoto zinazozikabili jamiihusika.

Mushi alisema mbali na wanafunzi hao ku jifunza mambo mbalimbali yauga vi na utawala pia wanaowajibu wa kuona umuhimu wa kujali jamii hasazile zinazoishi katika mazingira magumu.

“Tunaimani wanafunzi wetu wanajifunza masuala ya kuutumikia um ma lakini lazima wajikite kuangalia uhalisia halisi katika jamii zetuzinazotuzunguka na tukifanya hivyo tunaweza kuzifikia malengo yakuzisaidia jamii zilizo katika maisha duni”Alisema.

Aidha alisema swala la maadili lipo katika mitaala ya masomo yao hivyolazima wanafunzi hao wajifunze kivitendo kusaidia jamii h itajikaambapo walijitolea kupitia michango yao kwa kujitolea vyakula.

Awali kziungumza mara baada ya kupokea msaada huo,Afisa Mfawidhi Makao ya Wazee Wasiojiweza Mwanzange Jijini Tanga Otilia Chilumba aliwashukuru huku akiwataka kuwa makini kwa kuzingatia masomo ili waweze kupata manufaa kwenye maisha yao
“Ndugu zangu niwaambieni kuwa ujana ni maji ya moto tuutumie vizuri lakini pia acheni kukataa mimba mnazowapa wasichana mtoto utakayemzaandie anaweza kuja kukuokoa baadae “Alisema.

“Wapo baadhi ya wazee walishawahi kunililia walikwisha kuwate lekeza watotowao ndio sababu za kuwepo kwenye kambi za kulea wazee hivyo niwasihiacheni kuwakataa kwani mnaweza kukumbana na changamoto mbeleni

Alieleza pia sababu za baadhi ya wazee wengi kuishi maisha ya t a bu na kulazimika kulelewakwenye vituo maalumu imeelezwa kuchangiwa na baadhi yao kuwakanawatoto wao jambo ambalo linawapelekea kujikuta wakiingia kwenyechangamoto za namna hiyo.

Hatua hiyo inat ajwa kuwapa majukumu mazito wasichana ambao wamekuwaw akikumbana na kadhia hiyo ambao kwa asilimia kubwa wanakuwa wakiishikwa manunguniko.

MZUKA WA SOKA NA COKA YAWAFIKIA KANDA YA KASKAZINI

March 29, 2018


Baadhi ya shehena ya zawadi za pikipiki watakazojishindia wateja.



Mkuu wa Mauzo na Masoko wa kampuni ya Bonite Bottlers, Chris Loiruk akiongea na wafanyakazi wakati wa uzinduzi wa promosheni.

Wafanyakazi wa Bonite wakisherekea kuzinduliwa kwa promosheni.
Baadhi ya wafanyakazi wa Bonite wakiandamana katika mitaa ya mji wa Moshi wakati wa uzinduzi *Kuangalia mashindano ya kombe la Dunia wakiwa majumbani kwao Wakati mashindano makubwa na maarufu ya soka ya Kombe la Dunia 2018 yanakaribia kuanza, kampuni ya Coca-Cola kupitia kampuni kiwanda cha Bonite Bottlers, imezindua promosheni kubwa itakayowawezesha watumiaji wa vinywaji yake kujishindia luninga bafa za kisasa (flat screen TV sets) zinakazowawezesha kufurahia mashindano ya soka ya Kombe la Dunia wakiwa wakiwa na familia zao majumbani kwao. Promosheni hii mpya inajulikana kama “Mzuka wa Soka na Coka” na itanufaisha watumiaji wa vinywaji vinavyotengenezwa na kampuni ya Coca-Cola ambavyo ni Coca-Cola, Sprite, Fanta, Sparletta, Schweppes Stoney Tangawizi katika mikoa ya Kilimanjaro, Arusha, Manyara na Singida. Mbali na kujishindia luninga bapa za kisasa watumiaji wa vinywaji vya Coca-Cola kupitia promosheni hii wanayo fursa ya kujishindia zawadi kubwa ya pikipiki, fedha taslimu kuanzia shilingi 5,000/- hadi shilingi 100,000/- ikiwemo pia kujishindia soda za bure. Mkuu wa Mauzo na Masoko wa kampuni ya Bonite Bottlers, Chris Loiruk, amesema kampuni ya Coca-Cola ikiwa ni mdhamini mkuu wa mashindano yajayo ya Kombe la Dunia ,imewaandalia promosheni hii wakazi wa kanda ya Kaskazini ili kuhakikisha wanafurahia “Mzuka wa Soka na Coka” wakiwa majumbani kwao kupitia luninga za kisasa wakati huohuo wakiburudika na vinywaji vya Coca-Cola. “Tukiwa wadhamini wakuu wa mashindano ya Kombe la Dunia yatakayoanza mwezi June mwaka huu tumeona kuna umuhimu wa kuwaletea wateja promosheni itakayowaunganisha na kufurahia mashindano haya makubwa duniani kupitia kunywa zetu.Zawadi za ushindi zitakuwa zinapatikana katika ganda lililopo chini ya kizibo” Kwa upande wa zawadi kubwa za pikipiki,alisema anachotakiwa kufanya mywaji wa soda ni kukusanya maganda matatu ya chini ya vizibo yanayoonyesha sehemu 3 za pikipiki, yapo yanayoonyesha sehemu ya mbele, sehemu ya kati na sehemu ya nyuma ambayo yakiungaishwa yanaonyesha picha halisi ya pikipiki “Katika promosheni hii zawadi ya soda za bure zitatolewa madukani na zawadi za fedha taslimu, luninga na pikipiki zitakabidhiwa kwa washindi kutoka ofisi za kampuni ya Bonite,” Alisema, Chris Loiruk. Meneja wa chapa ya Coca-Cola nchini Tanzania, Sialouise Shayo, alisema promosheni hii imelenga kuwaandaa washabiki wa soka nchini kujiandaa kufurahia mzuka wa kombe la Dunia na kufurahia mashindano haya pindi yatakapoanza.

MAXCOM AFRICA PLC - Maxmalipo Kuendelea kutoa Huduma za Malipo Kielektroniki, kupitia Mfumo wa serikali wa malipo Kielektroniki (GePG) Ikiwamo huduma ya LUKU

March 29, 2018


photo Best Regards Krantz Mwantepele|Managing Director KONCEPT ROGECH ANIMATIONS STUDIO Mikocheni B, House No 58. Adjacent Clouds Media. Dar es Salaam, Tanzania | M: + 255 624053989 / +255 658123310 Blog: www.mwanaharakatimzalendo.blogspot.com W: www.koncept.co.tz IMAGINE INSPIRE INFLUENCE

AGPAHI YAKUTANA NA WADAU WA VVU NA UKIMWI MKOA WA MWANZA

March 29, 2018



Shirika la Ariel Glaser Pediatric AIDS Healthcare Initiative (AGPAHI) limeendesha kikao cha wadau wanaohusika katika mapambano ya VVU na Ukimwi mkoani Mwanza kwa ajili ya kujadili na kupanga mikakati ya kupambana na Virusi Vya Ukimwi (VVU) na Ukimwi mkoani humo.

Kikao hicho cha siku mbili kilichoandaliwa na shirika la AGPAHI kwa ufadhili wa Watu wa Marekani kupitia Centres for Disease Control (CDC), kimefanyika Machi 27,2018 hadi Machi 28,2018 katika ukumbi wa Gold Crest jijini Mwanza.

Miongoni mwa wadau waliohudhuria kikao hicho ni waratibu wa Ukimwi ngazi ya mkoa na wilaya,wakuu wa wilaya,wakurugenzi wa halmashauri,waganga wakuu wa wilaya,waratibu wa afya ya uzazi na mtoto,waratibu wa kifua kikuu,mashirika,taasisi na wadau mbalimbali wanaofanya shughuli za kupambana na VVU na Ukimwi.

Akifungua kikao hicho,Mkuu wa mkoa wa Mwanza,John Mongella alisema mapambano dhidi ya VVU na Ukimwi yatafanikiwa tu endapo kila mdau atashiriki

“Sisi kama mkoa wa Mwanza ni wa pili kwa idadi kubwa ya watu baada ya Dar es salaam,lakini pia tupo wa pili kwa shughuli za uchumi, takwimu za mwaka 2011/2012 zinaonesha kuwa tulikuwa na maambukizi ya asilimia 4.2 lakini mwaka 2016/2017 maambukizi yamepanda hadi kufikia asilimia 7.2”,alieleza.

“Ili tushushe asilimia hizi kubwa za maambukizi lazima wadau wote tushirikiane katika mapambano dhidi ya Ukimwi kwa kuelekeza nguvu zaidi katika kundi la vijana ambalo linapata maambukizi ya VVU kwa kasi”,aliongeza Mongella.

Aidha alisema teknolojia na utandawazi inachangia kwa kiasi kikubwa kuongezeka kwa maambukizi kwani vijana wanatumia vibaya mitandao ya mawasiliano na kusababisha kujiingiza katika tabia hatarishi zinazochongia kuwepo kwa maambukizi.

Mkuu huyo wa mkoa aliwataka wadau wa afya mkoani humo likiwemo shirika la AGPAHI ambalo limekuwa msaada mkubwa katika sekta ya afya nchini,kuendelea kushirikiana na serikali katika mapambano dhidi ya VVU na Ukimwi.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa shirika la AGPAHI, Dk. Sekela Mwakyusa alisema mkoa huo una takribani watu 90,000 wanaokisiwa kuwa na maambukizi ya VVU na bado hawajafikiwa.
Aliongeza kuwa shirika hilo lina mpango wa kuwafikia watu wapatao 37,900 kwa ajili ya kuwapatia huduma za tiba na matunzo watu wanaoishi na maambukizi ya VVU na Ukimwi (kutokana na takwimu za utafiti wa Tanzania HIV Impact Survey (THIS) 2016 – 2017).
ANGALIA PICHA WAKATI WA KIKAO



Mkuu wa mkoa wa Mwanza,John Mongella akizungumza katika kikao cha wadau wa mapambano dhidi ya VVU na Ukimwi mkoa wa Shinyanga. Kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa shirika la AGPAHI, Dk. Sekela Mwakyusa. Kushoto ni Kaimu Mganga mkuu mkoa wa Mwanza Dk. Sylas Wambura. Picha zote na Kadama Malunde - Malunde1 blog

Mkuu wa mkoa wa Mwanza,John Mongella akiwasisitiza wadau wa afya kuungana katika mapambano dhidi ya VVU na Ukimwi.

Mkuu wa mkoa wa Mwanza,John Mongella akilishukuru shirika la AGPAHI na Watu wa Marekani kupitia CDC kwa kuendelea kushirikiana na serikali ya Tanzania katika mapambano dhidi ya VVU na Ukimwi.



Kaimu Mganga mkuu mkoa wa Mwanza Dk. Sylas Wambura akizungumza wakati wa kikao hicho. Kushoto ni Mkuu wa wilaya ya Nyamagana, Mary Tesha.

Wakuu wa wilaya na wakurugenzi wa halmashauri za wilaya mkoa wa Mwanza wakiwa ukumbini.

Mkurugenzi Mtendaji wa shirika la AGPAHI, Dk. Sekela Mwakyusa akizungumza wakati wa kikao hicho na kueleza kuwa shirika hilo litaendelea kutoa huduma za tiba na matunzo kwa watu wanaoishi na maambukizi ya VVU.


Mwakilishi wa Centres for Disease Control (CDC) nchini, Eva Matiko akizungumza katika kikao hicho. Wadau wa masuala ya VVU na Ukimwi wakifuatilia kilichokuwa kinaendelea wakati wa kikao hicho.


Wadau wakiwa ukumbini.

Wafanyakazi wa shirika la AGPAHI mkoa wa Mwanza wakiwa ukumbini.

Mratibu wa Ukimwi mkoa wa Mwanza, Dk. Pius Masele akizungumza katika kikao hicho.

Mkuu wa wilaya ya Magu, Hadija Nyembu akichangia hoja wakati wa kikao hicho kuhusu namna ya kupambana na maambukizi ya VVU.




Mratibu wa Ukimwi,Kifua Kikuu na Malaria kutoka TAMISEMI, Mbuuni akichangia hoja wakati wa kikao hicho.



Kikao kinaendelea...








Wadau wakiwa ukumbini. Picha zote na Kadama Malunde - Malunde1 blog