Showing posts with label burudani. Show all posts
Showing posts with label burudani. Show all posts

TANZANITE ROYAL GIN YAZIDI KUPAMBA MANYARA TANZANITE MARATHON 2026

Kajunason August 18, 2026 Add Comment

 

Na Mwandishi Wetu, Manyara

Manyara Tanzanite Marathon 2026 inatarajiwa kuwa na burudani ya aina yake baada ya wasanii maarufu nchini, Dully Sykes, Banana Zoro na Mr Blue, kuthibitisha kushiriki na kutumbuiza katika tukio hilo litakalofanyika Agosti 22, 2026 mjini Babati, mkoani Manyara.

Ushiriki wa wasanii hao umewezeshwa na kampuni ya Mati Super Brands Ltd kupitia kinywaji chake cha Tanzanite Royal Gin, hatua inayoongeza ushiriki wa sekta binafsi katika kufanikisha mbio hizo zinazolenga kuunganisha michezo, burudani na shughuli za kijamii.
Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Queen Sendiga, amekabidhi wasanii hao T-shirt rasmi za Manyara Tanzanite Marathon, ikiwa ni sehemu ya maandalizi kuelekea tukio hilo ambalo limeendelea kupata mwitikio kutoka kwa wadau mbalimbali.

Manyara Tanzanite Marathon 2026 imebeba kaulimbiu “Hatua Moja Okoa Maisha”, ikiwa na lengo la kukusanya Shilingi bilioni 1.5 kwa ajili ya ujenzi wa wodi maalumu ya kuwahudumia watoto njiti wanaozaliwa kabla ya wakati.
Ujio wa Dully Sykes, Banana Zoro na Mr Blue unatarajiwa kuongeza hamasa kwa wanariadha, vikundi vya jogging na wananchi watakaoshiriki au kujitokeza kushuhudia mbio hizo. Burudani hiyo pia inalenga kuwapa washiriki na watazamaji uzoefu wa kipekee huku ikihamasisha jamii kuunga mkono kampeni ya kuokoa maisha ya watoto njiti..
Mchango wa Mati Super Brands Ltd kupitia Tanzanite Royal Gin unaendelea kuonesha nafasi ya sekta binafsi katika kusaidia shughuli zenye manufaa kwa jamii. Ushiriki huo unatarajiwa kuongeza mvuto wa marathon na kuwafikia watu wengi zaidi kupitia michezo na burudani.

Kwa ujumla, Manyara Tanzanite Marathon 2026 inatarajiwa kuwa jukwaa linalounganisha michezo, burudani, utalii na uwajibikaji kwa jamii, huku kila hatua ya washiriki ikilenga kuchangia upatikanaji wa huduma bora kwa watoto njiti mkoani Manyara.

HALIMA – A CROSS-AFRICAN LOVE MELODY BY EKUNRAWO AND JUX

January 08, 2026 Add Comment

   



“HALIMA” brings together two vibrant voices from West and East Africa—Nigeria’s Ekunrawo and Tanzania’s Jux—in a collaboration that beautifully captures the heart of modern Afrobeat. The track glides on warm rhythms, smooth melodies, and heartfelt vocals, telling a romantic story that feels both intimate and universal.

Ekunrawo, also known as Timileyin Adeleke, is a fast-rising Nigerian artist recognized for blending Afrobeat grooves with deep storytelling and cultural authenticity. His music carries emotion and truth, and “HALIMA” continues this journey. By teaming up with Jux, one of Tanzania’s most beloved voices, the song bridges borders and celebrates unity through sound.

“HALIMA” stands out not only for its polished production but for its spirit—celebrating love, connection, and the synergy that happens when African artists come together. West African rhythm meets East African smoothness, creating a timeless feel that speaks beyond language and location.

This song is more than a collaboration—it’s a statement about African creativity, shared culture, and music’s power to connect people everywhere.



SERIKALI KUTOA MIRAHABA YA BILIONI 1 KWA WASANII MWAKANI

December 19, 2025 Add Comment


NA MASHAKA MHANDO


WIZARA ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, kupitia Taasisi ya Hakimiliki nchini (COSOTA), inatarajia kuweka historia mpya kwa kugawa zaidi ya shilingi bilioni moja kama mirabaha kwa wasanii wa makundi mbalimbali nchini ifikapo Januari 23, 2026.


Hatua hiyo inakuja baada ya majadiliano ya kimkakati kati ya Naibu Waziri wa sekta hiyo, Mhe. Hamis Mwinjuma (MwanaFA), na uongozi wa COSOTA, yaliyolenga kujibu kiu ya muda mrefu ya wasanii kuhusu malipo ya haki zao.


Akizungumza katika mahojiano maalum, MwanaFA alisema kuwa Serikali imejipanga kufanya ugawaji huo kuwa shughuli kubwa na ya kihistoria kutokana na kiwango kikubwa cha fedha kilichokusanywa.


"Kama msanii na kama Naibu Waziri, nimekuwa nikipokea maswali mengi kutoka kwa wasanii wenzangu wakitaka kujua hatma ya mirabaha yao. Nimefanya majadiliano (discussion) nzuri na COSOTA na tumekubaliana kuwa Januari 23 mwakani, tunakwenda kutoa zaidi ya shilingi bilioni moja na ushee. Hiki ni kiwango kikubwa ambacho hakijawahi kutokea nchini," alisema MwanaFA.

MwanaFA alibainisha kuwa mafanikio hayo yametokana na hatua ya Bunge kubadilisha sheria inayoruhusu kuanzishwa kwa Taasisi za Pamoja za Kusimamia Hakimiliki (Collective Management Organizations - CMOs). 

Alieleza kuwa hadi sasa, leseni mbili zimetolewa kwa kampuni za CMO ambazo zimeshirikiana na taasisi za kimataifa, ikiwemo Taasisi ya Afrika Kusini inayosimamia mirabaha ya kidijitali (CAPASSO) kupata fedha hizo zinazokwenda kutolewa Januari.


Aidha, alitaja kuwa miongoni mwa vyanzo vikuu vya fedha hizo ni pamoja na kodi ya vifaa vinavyobeba kazi za sanaa na ada zinazotokana na Vibali vya Jumla vya kupiga nyimbo kwenye Redio na Televisheni (Blanket License).


"Tumepata zaidi ya shilingi bilioni moja kupitia mfumo wa Blanket License. Fedha hizi zitawanufaisha wasanii, huku sehemu ikiongoza Mfuko wa Utamaduni na Sanaa, COSOTA, pamoja na kodi ya Serikali," aliongeza.


Alifafanua kuwa tofauti na zamani, safari hii wigo umepanuliwa ambapo wanufaika watatoka katika makundi ya Muziki, Filamu, Sanaa za Maonyesho, Sanaa za Ufundi, pamoja na Waandishi wa Vitabu.


Hata hivyo, MwanaFA alitoa rai kwa wasanii wote: "ili unufaike na fedha hizi, ni lazima usajili kazi zako COSOTA. Usajili ndio utambulisho pekee utakaorahisisha utaratibu wa wewe kupata mirabaha yako pindi kazi zako zinapotumika au kuchezwa."

Mwisho