Showing posts with label habari. Show all posts
Showing posts with label habari. Show all posts

WAANDISHI WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KUHUSU DAWA ZA KULEVYA

July 03, 2026 Add Comment
Na Mwandishi Wetu

MAMLAKA ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) imebainisha kuwa mwaka 2025 ilikamata tani 31.76 na lita 183,500 za kemikali bashirifu, huku ikizuia tani 734 kuingia nchini kinyume cha sheria, ikisema waandishi wa habari wanapaswa kuwa sehemu ya mapambano dhidi ya uhalifu huo kupitia utoaji wa taarifa sahihi kwa umma.

NEMC YAJA NA KIJIJI CHA MAZINGIRA MAONESHO SABASABA

July 03, 2026 Add Comment
Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) linashiriki Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam (Sabasaba) kwa kuanzisha Kijiji cha Mazingira, jukwaa maalum linalowakutanisha wananchi, wadau wa mazingira na taasisi mbalimbali kwa lengo la kutoa elimu, kuonesha ubunifu na teknolojia rafiki kwa mazingira, pamoja na kuhamasisha uhifadhi na usimamizi endelevu wa mazingira.

TANZANIA IPO TAYARI KUELEKEA AFCON 2027

July 03, 2026 Add Comment
Na. Mwandishi Wetu - Arusha

Tanzania ipo tayari kwa mashindano ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON 2027) ikiwa mwenyeji kwa kushirikiana na Kenya na Uganda ambapo maandalizi yamefikia hatua nzuri kwa kuzingatia viwango vya Shirikisho la Mpira wa Miguu Barani Afrika (CAF) vinavyotakiwa.

KIPANGULA ASISITIZA WELEDI WA UANDISHI WA HABARI SABASABA

Kajunason July 03, 2026 Add Comment

 

Na Mwandishi Wetu

Dar es Salaam. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea kutumia Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara (Sabasaba) kutoa elimu kwa wananchi kuhusu majukumu yake, huduma mbalimbali na umuhimu wa ithibati katika kuimarisha taaluma ya uandishi wa habari nchini.

Hatua hiyo imejidhihirisha leo baada ya Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa JAB, Wakili Patrick Kipangula, kuungana na maafisa wa Bodi katika banda la JAB lililopo Kijiji cha Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, kutoa elimu kwa wananchi, kujibu maswali mbalimbali na kuzungumza na waandishi wa habari waliotembelea banda hilo.

Akizungumza katika maonesho hayo, Wakili Kipangula alisema JAB imejipanga kuhakikisha wananchi na wadau wa sekta ya habari wanapata uelewa sahihi kuhusu majukumu ya Bodi pamoja na huduma zinazotolewa kwa mujibu wa Sheria ya Huduma za Habari.

Alisema ushiriki wa JAB katika maonesho ya Sabasaba unalenga kusogeza huduma karibu na wananchi, kuongeza uelewa kuhusu umuhimu wa ithibati kwa waandishi wa habari na kuhamasisha uzingatiaji wa maadili, weledi na uwajibikaji katika taaluma ya uandishi wa habari.

Mbali na kutoa elimu, JAB inaendelea kutoa huduma mbalimbali katika banda lake ikiwemo usajili wa waandishi wa habari, utoaji wa vitambulisho vya ithibati kwa waliokidhi vigezo, marekebisho ya taarifa za usajili pamoja na ushauri kuhusu huduma zinazotolewa na Bodi.

JAB imewahimiza waandishi wa habari, wadau wa sekta hiyo na wananchi kwa ujumla kutumia fursa ya Maonesho ya Sabasaba kutembelea banda lake ili kupata huduma, elimu na ufafanuzi kuhusu shughuli zake, huku ikisisitiza kuwa ithibati ni nyenzo muhimu katika kujenga taaluma ya uandishi wa habari yenye weledi, uwajibikaji na kuaminika.

WAZIRI SANGU: TAASISI ZA DINI NI NGUZO YA AMANI, MAADILI NA MALEZI BORA

July 02, 2026 Add Comment
Na: OWM (KAM), Manyoni - Singida

Serikali imesema inatambua mchango mkubwa wa taasisi za dini katika kuimarisha huduma za kijamii kudumisha amani na kukuza maadili nchini huku ikizitaka viongozi wa dini kuendelea kushirikiana na Serikali katika kukuza malezi bora kwa watoto na vijana ili kujenga taifa lenye ustawi na mshikamano.

BARRICK-TWIGA , SERIKALI WAZINDUA MRADI WA ‘BARRICK FUTURE FORWARD EDUCATION PROGRAM AWAMU YA PILI KIBAIGWA, DODOMA

July 02, 2026 Add Comment
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI), Profesa Riziki Shemdoe akizindua jiwe la msingi la ujenzi wa madarasa sita na mabweni mawili katika Shule ya Sekondari Kibaigwa, mkoani Dodoma. Kushoto ni Meneja wa Fedha wa Barrick nchini, Penina Kituku.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI), Profesa Riziki Shemdoe akizindua jiwe la msingi la ujenzi wa madarasa sita na mabweni mawili katika Shule ya Sekondari Kibaigwa, mkoani Dodoma.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI), Profesa Riziki Shemdoe, akiwa pamoja na ujumbe kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI) na viongozi wa Mkoa wa Dodoma, wakikagua maendeleo ya mradi wa ujenzi wa madarasa na mabweni katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Kibaigwa, mkoani Dodoma.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI), Profesa Riziki Shemdoe, akiwa pamoja na ujumbe kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI) na viongozi wa Mkoa wa Dodoma, wakikagua maendeleo ya mradi wa ujenzi wa madarasa na mabweni katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Kibaigwa, mkoani Dodoma.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI), Profesa Riziki Shemdoe, akiwa pamoja na ujumbe kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI) na viongozi wa Mkoa wa Dodoma, wakikagua maendeleo ya mradi wa ujenzi wa madarasa na mabweni katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Kibaigwa, mkoani Dodoma.
Muonekano wa sehemu ya majengo katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Kibaigwa, mkoani Dodoma.
Muonekano wa sehemu ya majengo katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Kibaigwa, mkoani Dodoma.
Muonekano wa sehemu ya majengo katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Kibaigwa, mkoani Dodoma.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI), Profesa Riziki Shemdoe, akiwa pamoja na ujumbe kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI) na viongozi wa Mkoa wa Dodoma, wakikagua maendeleo ya mradi wa ujenzi wa madarasa na mabweni katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Kibaigwa, mkoani Dodoma.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI), Profesa Riziki Shemdoe akizungumza wakati wa hafla ya uzinduzi wa awamu ya pili ya mpango wa Barrick–Twiga Future Forward Education Program katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Kibaigwa, mkoani Dodoma.
Meneja Mkazi wa Barrick nchini, Dkt. Melkiory Ngido akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya uzinduzi wa awamu ya pili ya mradi wa Barrick–Twiga Future Forward Education Program uliozinduliwa Kibaigwa, mkoani Dodoma, na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI), Profesa Riziki Shemdoe.
Meneja Mkazi wa Barrick nchini, Dkt. Melkiory Ngido (kulia) akipeana mkono na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI), Profesa Riziki Shemdoe, baada ya uzinduzi wa awamu ya pili ya mpango wa Barrick–Twiga Future Forward Education Program unaotekelezwa nchini kote kwa lengo la kuboresha miundombinu katika shule za sekondari zenye madarasa ya Kidato cha Tano na Sita.
Meneja wa Fedha wa Barrick nchini, Penina Kituku, akizungumza wakati wa hafla ya uzinduzi wa awamu ya pili ya mpango wa Barrick–Twiga Future Forward Education Program uliofanyika katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Kibaigwa, mkoani Dodoma.

***
Kampuni ya Barrick, inayofanya shughuli zake kwa ubia na Serikali kupitia Twiga Minerals, imeahidi kwamba kupitia programu yake ya Barrick-Twiga Future Forward Education Program itaendelea kufanya kazi na Serikali ya Awamu ya Sita kwenye sekta ya elimu kwa kuboresha miundombinu ya elimu, kuwezesha mazingira rafiki ya kusomea kwa ajili ya kuchochea maendeleo ya taifa kwenye sekta hiyo.