Showing posts with label habari. Show all posts
Showing posts with label habari. Show all posts

MAKAMU WA RAIS BALOZI DKT .NCHIMBI AMTEMBELEA NA KUMJULIA HALI , MAKAMU WA RAIS MSTAAFU DKT.MOHAMED GHARIB BILAL

January 02, 2026 Add Comment

MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi, amtembelea na kumjulia hali, Makamu wa Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mohamed Gharib Bilal, katika makazi yake Masaki Jijini Dar es Salaam, leo tarehe 02 Januari 2026.




DKT. MWIGULU AKAGUA MAENDELEO MRADI WA BWAWA LA MAJI KIDUNDA

January 02, 2026 Add Comment


Waziri Mkuu Dkt Mwigulu Nchemba leo Januari 02, 2026 amekagua maendeleo ya ujenzi wa Bwawa la Maji Kidunda lililopo Mkoani Morogoro.

Akizungumza baada ya ukaguzi huo, Dkt. Mwigulu amesema kuwa mradi huo unaakisi maono ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuhakikisha nchi inakabiliana na changamoto ya upungufu wa maji hasa kutokana na mabadiliko ya tabia nchi.

Pia, ameiagiza Wizara ya Maji kuhakikisha mradi huo hausimami na unakamilika kwa wakati ili uanze kutoa huduma ya maji kwa wananchi.












WIZARA YA NISHATI KUSHIRIKIANA NA BODI YA NYAMA KUKUZA MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA

WIZARA YA NISHATI KUSHIRIKIANA NA BODI YA NYAMA KUKUZA MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA

January 02, 2026 Add Comment

 





*Lengo ni kuhakikisha wachomaji nyama katika minada wanatumia nishati safi na kupikia

*Wito watolewa kwa Benki kutoa mikopo yenye riba nafuu kwa wachomaji nyama

Wizara ya Nishati kwa kushirikiana na Bodi ya Nyama Tanzania imeandaa mpango maalum wa kuhamasisha wachomaji nyama katika minada mbalimbali nchini kutumia nishati safi ya kupikia kwa lengo la kupunguza matumizi ya nishati zisizo rafiki kwa mazingira pamoja na kulinda afya za wachomaji nyama na jamii kwa ujumla.

Akizungumza wakati wa ziara yake ya kumtembelea mdau wa Nishati safi ya kupikia, Matima Investment Wilayani Kibaha, Mkoani Pwani, Mkurugenzi wa Nishati Safi ya Kupikia kutoka Wizara ya Nishati, Bw. Nolasco Mlay, amesema mdau huyo anajihusisha na utengenezaji wa majiko maalum ya kuchomea nyama yanayotumia gesi, ambayo ni rafiki kwa mazingira na afya.

Katika ziara hiyo, Bw. Mlay alikutana na wataalamu kutoka Bodi ya Nyama Tanzania pamoja na Meneja wa Benki ya CRDB, ambapo walijadili mikakati mbalimbali ya kuhakikisha minada yote ya kuchomea nyama nchini inahamia katika matumizi ya majiko ya kisasa yanayotumia nishati safi.

“Matumizi ya nishati safi ya kupikia hayalindi mazingira pekee, bali pia yanaboresha afya na kuongeza ufanisi katika shughuli za wachomaji nyama. Kupitia ushirikiano na Bodi ya Nyama Tanzania, tutaendelea kuwahamasisha wachomaji nyama katika minada mbalimbali kutumia nishati safi, kwani bodi hiyo ina jukumu la kusimamia na kuwaendeleza wadau wa sekta ya nyama,” amesema Bw. Mlay.

Aidha, ametoa wito kwa wadau wa maendeleo hususani taasisi za kifedha na benki, kuwawezesha wachomaji nyama kwa kuwapatia mikopo yenye riba nafuu ili waweze kumudu gharama za ununuzi wa majiko ya kisasa. Hatua hiyo itawawezesha wajasiriamali hao kuachana na matumizi ya kuni na mkaa na badala yake kutumia teknolojia safi na rafiki kwa mazingira.

Kwa upande wake, Meneja wa Benki ya CRDB Mkoa wa Pwani, Bi. Rose Kazimoto, amesema benki hiyo iko tayari kushirikiana na wachomaji nyama pamoja na watengenezaji wa majiko ya nishati safi kwa lengo la kuongeza uzalishaji na matumizi ya nishati safi ya kupikia.

Amesema CRDB itaangalia namna bora ya kuwawezesha wachomaji nyama kupata mikopo, jambo litakalosaidia kulinda mazingira na kuboresha afya zao.

Hata hivyo, amewasisitiza wachomaji nyama kujisajili katika Bodi ya Nyama Tanzania na kufanya kazi katika mfumo uliopangwa (organized) ili kurahisisha ufuatiliaji na upatikanaji wa mikopo.

Bi. Kazimoto ameongeza kuwa kutokana na hali ya wachomaji nyama wengi kuhamahama, ni vyema wakaunda vikundi vinavyodumu kwa angalau miaka mitatu. Amesema Mnada wa Loliondo tayari umejipanga vizuri na una sifa za kupata mikopo kutoka CRDB Bank.

Naye Afisa Dawati wa Nishati Safi ya Kupikia kutoka Bodi ya Nyama Tanzania, Bi. Pendo Msaki, amesema bodi hiyo imeendelea kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia katika minada ya nyama nchini.

Ameeleza kuwa Bodi ya Nyama Tanzania iko katika hatua za mwisho za kuandaa waraka wa katazo la matumizi ya kuni na mkaa katika minada ya nyama, hatua inayolenga kulinda mazingira na kuboresha afya za wachomaji nyama.

Aidha, amewasisitiza wachomaji nyama wote kujisajili katika Bodi ya Nyama Tanzania ili wapate ithibati na kutambulika rasmi.

Ameongeza kuwa bodi hiyo itaanza kusambaza majiko ya nishati safi kwa mkopo katika minada ya Loliondo–Kibaha pamoja na Pugu jijini Dar es Salaam, kama sehemu ya utekelezaji wa mpango huo.    

ASANTE EWURA KWA ELIMU YA UDHIBITI WA HUDUMA

ASANTE EWURA KWA ELIMU YA UDHIBITI WA HUDUMA

December 31, 2025 Add Comment

Mwenyekiti wa Klabu ya Waandishi wa Habari mkoani Dodoma (DPC) Bw.Musa Yusuf,akitoa neno la shukrani kwa Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) mara baada ya waandishi wa klabu hiyo kupatiwa mafunzo kuhusu udhibiti wa huduma za nishati na maji yaliyofanyika leo Disemba 31,2025 jijini Dodoma.

Na.Mwandishi Wetu-Dodoma

Wanachama wa Klabu ya Waandishi wa Habari mkoani Dodoma, leo 31 Desemba 2025, wameishukuru Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) kwa kuwapa mafunzo kuhusu udhibiti wa huduma za nishati na maji.

Mwenyekiti wa klabu hiyo, Musa Yusuf, ameipongeza EWURA kwa hatua ya kutoa mafunzo hayo, akibainisha umuhimu wa mkataba wa huduma kwa wateja, uvunaji wa maji ya mvua, na utekelezaji wa mkakati wa kitaifa wa matumizi ya nishati safi ya kupikia. Amesisitiza kuwa elimu waliyoipata wataitumia kwa kuelimisha umma.

“Asanteni sana EWURA kwa elimu hii, hakika imetufungua macho. Wenzangu wote ni mashahidi. Tunaomba mafunzo kama haya yaendelee,” amesema Bw. Yusuf.

Kwa upande wake Kaimu Meneja Mawasiliano na Uhusiano wa EWURA, Wilfred Mwakalosi, amesisitiza umuhimu wa waandishi wa habari kuelewa masuala yanayodhibitiwa na EWURA, kwani yanagusa huduma ambazo kila mwananchi kwa namna moja au nyingine anazitumia.

“Ninyi waandishi wa habari ni daraja kati ya EWURA na wananchi, tuendelee kushirikiana katika kuelimisha umma ili kila mtumiaji wa huduma tunazodhibiti ajue haki na wajibu wake”. Amesisitiza Mwakalosi.

 

   

RC TANGA AWATAKA WALIOPANGA KUCHOMA MATAIRI MKESHA WA MWAKA MPYA WASITHUBUTU

December 31, 2025 Add Comment




Na Oscar Assenga, TANGA


MKUU wa Mkoa wa Tanga Balozi,Dkt Batilda Burian amewataka wananchi wa mkoa wa Tanga ambao wamepanga kutumia matairi kuchoma moto barabarani kama njia ya kusheherekea sikuuu ya mwaka mpya wasithubutu kufanya hivyo.

Dkt Batilda aliyasema hayo leo wakati akizungumza na waandishi wa habari kuelekea mkesha wa mwaka mpya ambao unatarajiwa kufanyika kwenye viwanja vya Urithi Jijini Tanga ambapo alisema kutokana huo ni uharibifu wa miundombinu ya barabara na hatari kwa Taifa.

Alisema kwamba ndio maana Ofisi ya Mkoa huo kwa kushirikiana na Uongozi wa Halmashauri ya Jiji la Tanga na Mbunge wa Jimbo la Tanga wameamua kufanya shughuli ya wana Tanga kwenye uwanja wa Burudani wa Uhuru Park.

Alisema kwamba kutakuwa na sanaa mbalimbali taarabu na miziki mbalimbali ikiwemo mashindano ya kupika maandazi ,vitumbua na watakaokuwa mabingwa wa kupika sambusa lakini watachoma samaki na mbuzi watu watakula bila gharama yoyote ili kuendeleza umoja,amani na ukarimu wa wana Tanga.

Aidha alisema kwamba baada ya hapo usiku watawasha mafataki watakayowashwa na wataalamu maalumu ya viwango maalumu hivyo kuliko kuchoma matairi waje kwenye uwanja wa uhuru ili kuona burudani mbalimbali ikiwemo mafataki.

Mkuu huyo wa mkoa aliwataka wana Tanga kwenda uwanja wa Urithi ili kuweza kuomba dua kumshukuru Mungu kuuona mwaka na baada ya hapo mtu kurudi nyumbani ni eneo ambalo litakuwa salama.

.



RAIS SAMIA ATOA ZAWADI ZA MWAKA MPYA KWA WENYE UHITAJI, NAIBU WAZIRI UMMY AMUWAKILISHA

December 31, 2025 Add Comment


Na Mwandishi wetu- KILIMANJARO

Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Sera, Bunge, Uratibu na Watu wenye Ulemavu Mhe. Ummy Nderiananga ametoa wito kwa jamii kuwapenda, kuwajali na kuwahudumia makundi ya wenye mahitaji maalumu ili kukuza umoja na mshikamano katika Jamii.


Mhe. Nderiananga alisema hayo leo Disemba 31, 2025  akimuwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan katika utekelezaji wa utaratibu wa utoaji zawadi za sikukuu mbalimbali kuelekea Sikukuu ya Mwaka Mpya wa 2026, zawadi hizo  zimeenda kwa watoto 190 wakiwemo wenye ulemavu na wasio na ulemavu wanaolelewa na Shirika la The Creator Share Foundation lililopo Kata ya Kirua, Wilaya ya Moshi Vijijini mkoani  Kilimanjaro.




Alisema, ndani ya siku 100 za uongozi wake ameendelea kuleta faraja, upendo, tumaini na umoja kwa watanzania huku akisema kuwa kitendo hicho ni ishara ya upendo mkubwa kwa wananchi bila kujali hali zao.


“Naomba nitumie fursa hii kuwatakia kheri ya sikukuu ya mwaka mpya  wa  2026 twende tukasherehekee kwa amani  na tukiwa na faraja kwa sababu Mhe. Rais ametukumbuka sisi ni watoto wake hivyo tudumishe upendo huu miongoni mwetu kila mmoja amuone mwenzake ni wa muhimu katika jamii,” alisema Mhe. Nderiananga.

Akitaja vitu alivyovikabidhi kwa watoto hao alisema, ni pamoja na Mchele kilo 100, Ngano kilo 50, Mbuzi wawili, sabuni, mafuta ya kupikia, madaftari, sukari kilo 25 na vinywaji



" Nitoe wito kwa jamii kuwa, kila mmoja ana wajibu wa kuwahudumia watoto na watu wenye mahitaji maalum, siyo tu kwa siku za sikukuu, bali kwa muda wote ili kuwapa faraja na huo ndio upendo tunaotakiwa kuwaonesha," aliongeza.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Moshi Bw. Godfrey Mnzava  alibainisha kuwa,  ili kuwa na ustawi wa maisha ya kijamii ni lazima kuwajali watu wenye uhitaji  ili waweze kukidhi mahitaji muhimu ya kila siku.


Naye,Diwani wa Viti Maalum Tarafa ya Vunjo Magharaibi ambaye pia ana mtoto mwenye ulemavu anayelelewa katika Shirika hilo Bi. Pamela Chuwa alipongea hatua hiyo ya Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuwafikia watu wenye ulemavu hatua inayowaganya kujisikia kuwa ni sehemu ya jamii.



“Mimi kama mama mwenye mtoto wa mahitaji maalum nimejisikia furaha kwa kupewa kipaumbele na tumefurahi sana Naibu Waziri Ummy kutufikia ukizingatia baadhi yetu tumefukuzwa katika familia  tukionekana kama kuzaa watoto wenye ulemavu ni mkosi na laana katika familia,” alipongeza Bi. Diwani huyo.



Vilevile Afisa Rasilimali Watu katika Shirika hilo Bi. Judith Shio mara  baada ya kupokea zawadi hizo alimshukuru Mhe. Rais Dkt.  Samia  Suluhu Hassan kwa moyo wa upendo na kuwajali watu wenye mahitaji Maalum huku akitoa wito kwa wadau mbalimbali kujitolea ili kuendelezwa moyo wa upendo na faraja kwa makundi hayo.



“Kwa niaba ya Shirika tunatanguliza shukrani zetu za dhati kwa upendo huu na mwaka huu tunauanza kipekee sana na watoto wamefurahi hivyo kwetu imekuwa faraja kubwa na imegusa jamii,” alishukuru Bi. Judith.


 Nao baadhi ya watoto wanaolelewa katika Shirika hilo wameishukuru Serikali kwa kuwakumbuka wakisema ujio huo kwao umekuwa ni historia na furaha kubwa ya kuuanza mwaka mpya kwa matumaini huku wakimshukuru Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa upendo huo wa the kuwashika mkono watoto wenye mahitaji maalum.


MWISHO