Showing posts with label habari. Show all posts
Showing posts with label habari. Show all posts

KWA NINI MARUBANI WANAVAA MISTARI YA DHAHABU MABEGANI?

August 17, 2026 Add Comment

      

Ukiwa uwanja wa ndege, huenda umewahi kumuona rubani akitembea kuelekea kwenye ndege akiwa amevalia sare nadhifu, kofia maalum na mistari ya dhahabu mabegani. Muonekano huo umekuwa sehemu inayotambulika sana ya taaluma ya urubani duniani.

TBS YABANA BIDHAA HATARISHI, YATAKA MAENEO YA BIASHARA YA CHAKULA NA VIPODOZI KUSAJILIWA

TBS YABANA BIDHAA HATARISHI, YATAKA MAENEO YA BIASHARA YA CHAKULA NA VIPODOZI KUSAJILIWA

August 17, 2026 Add Comment

Meneja wa Usajili wa Bidhaa na Majengo wa TBS, Bw.Habakuki Kalebo,akiwasilisha mada wakati wa kikao kilichoandaliwa na BRELA cha Maafisa Biashara pamoja na Wakuu wa Idara za Viwanda na Biashara kinachofanyika kwa siku mbili jijini Dodoma.

Na.Mwandishi Wetu-DODOMA 

Shirika la Viwango Tanzania (TBS) limesisitiza umuhimu wa kusajili maeneo yote yanayohusika na uuzaji, usambazaji na uhifadhi wa bidhaa za chakula na vipodozi, likieleza kuwa hatua hiyo ni muhimu katika kuhakikisha wananchi wanapata bidhaa salama na bora, kulinda afya zao.

Meneja wa Usajili wa Bidhaa na Majengo wa TBS, Bw.Habakuki Kalebo, amesema hayo wakati wa kikao kilichoandaliwa na BRELA cha Maafisa Biashara pamoja na Wakuu wa Idara za Viwanda na Biashara, akieleza kuwa TBS inashirikiana na Ofisi ya Rais–TAMISEMI kupitia mamlaka za serikali za mitaa katika kusimamia usajili wa maeneo hayo.

Kalebo amesema usajili huo unalenga kuhakikisha bidhaa zinazouzwa, kusambazwa au kuhifadhiwa ni salama, bora na zimethibitishwa na TBS, huku mazingira yanayotumika kuhifadhi na kuuza bidhaa yamekidhi masharti ya usalama na usafi. Amesema kwa bidhaa za chakula, hatua hiyo inasaidia kuzuia uchafuzi kwa kuhakikisha chakula hakihifadhiwi au kuchanganywa na bidhaa nyingine zinazoweza kuhatarisha ubora wake.

Aidha, amesema usajili huo unasaidia kudhibiti usalama wa vipodozi vinavyoingizwa sokoni, kwa kuhakikisha havina viambata vyenye madhara kwa watumiaji. Ameongeza kuwa ukaguzi katika maeneo hayo pia husaidia kubaini na kuondoa bidhaa zilizomaliza muda wake kabla hazijawafikia wananchi, hivyo kupunguza hatari zinazoweza kujitokeza kutokana na matumizi ya bidhaa zisizofaa.

 "Mfumo wa usajili pia una umuhimu katika ufuatiliaji wa bidhaa sokoni, kwani pale changamoto inapojitokeza, TBS inaweza kubaini bidhaa husika zilipo, kiasi kilichopo na kuchukua hatua za haraka za kuziondoa sokoni. Amesema utaratibu huo unaimarisha udhibiti wa bidhaa na kuongeza uwezo wa Serikali kulinda afya na usalama wa wananchi."amesema Bw.Kalebo 

Amesema ushirikiano kati ya TBS, Maafisa Biashara na Mamlaka za serikali za mitaa ni muhimu katika kuhakikisha wafanyabiashara wanaelewa na kutekeleza matakwa ya Sheria na Viwango vya bidhaa. 

Kalebo amesisitiza kuwa ulinzi wa afya ya wananchi unapaswa kuwa sehemu muhimu ya usimamizi wa biashara, akieleza kuwa mtu mwenye afya njema ana uwezo mkubwa wa kushiriki katika shughuli za uzalishaji na kuchangia uchumi wa taifa.

Amesema matumizi ya bidhaa salama hupunguza hatari za magonjwa na gharama za matibabu, hivyo usajili na udhibiti wa maeneo ya biashara ya chakula na vipodozi ni hatua muhimu katika kulinda afya ya jamii na kuongeza tija ya Taifa.

RAIS DKT SAMIA SULUHU AKUTANA NA KUZUNGUMZA NA MKURUGENZI MKUU WA SHIRIKA LA KIMATAIFA LA UHAMIAJI (IOM) BI. AMY E. POPE

August 17, 2026 Add Comment

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Kimataifa la Uhamiaji (IOM) Bi. Amy E. Pope, tarehe 17 Agosti,2026 Ikulu Ndogo, Zanzibar.


 

TBS YATEKETEZA BIDHAA ZA CHAKULA ZISIZOKIDHI VIWANGO ZENYE THAMANI YA SH. MILIONI 149

August 17, 2026 Add Comment
SHIRIKA la Viwango Tanzania (TBS) Kanda Maalum ya Dar es Salaam limeteketeza tani 39 za bidhaa za chakula zisizokidhi matakwa ya viwango, zenye thamani ya takribani Sh milioni 149, ikiwa ni hatua ya kuwalinda wananchi dhidi ya matumizi ya bidhaa zisizo salama.

TOL GASES YAWEKA WAZI UWEZO WA TANZANIA KUZALISHA OKSIJENI YA TIBA

August 17, 2026 Add Comment
Na Mwandishi Wetu

SERIKALI imeombwa kuzipa kipaumbele kampuni binafsi zenye uwezo wa kuzalisha oksijeni ya tiba kwa ajili ya matumizi hospitalini, badala ya kuwekeza zaidi katika uzalishaji wake, ili kutumia kikamilifu uwezo uliopo nchini.

DAWASA YAWASISITIZIA WANAWAKE NAFASI YAO KATIKA ULINZI WA HUDUMA ZA MAJI

August 17, 2026 Add Comment
Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es salaam (DAWASA) imewakumbusha Jamii juu ya umuhimu wa kulinda miundonbinu ya Maji ili kujenga jumuiya inayothamini huduma ya Maji kwa vizazi vya sasa na vizazi vijavyo.