Showing posts with label habari. Show all posts
Showing posts with label habari. Show all posts
SERIKALI YAPANIA KUANDAA WALIMU USHIRIKIANO WA ATE NA WIZARA WAZAA MATUNDA KWA WATAFUTA AJIRA

SERIKALI YAPANIA KUANDAA WALIMU USHIRIKIANO WA ATE NA WIZARA WAZAA MATUNDA KWA WATAFUTA AJIRA

September 25, 2025 Add Comment

 

KATIKA  kuhakikisha mafunzo ya darasani yanaendana na mahitaji halisi ya soko la ajira, Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Carolyne Nombo, amekutana na Afisa Mtendaji Mkuu wa Chama cha Waajiri Tanzania (ATE), Bi. Suzzane Ndomba, kwa mazungumzo ya namna ya kuwawezesha vijana wahitimu kupata mafunzo ya vitendo sehemu za kazi.

Mkutano huo umefanyika  katika ofisi za ATE jijini Dar es Salaam, ambapo Prof. Nombo alisema Serikali imefanya mapitio ya Sera ya Elimu na kuboresha mitaala ya ngazi zote ili vijana wapate ujuzi unaowawezesha kujiajiri au kuajiriwa.

Aidha, Prof. Nombo alisisitiza kuwa Serikali inaendelea kutoa mafunzo kwa walimu walioko kazini ili kuboresha mbinu za ufundishaji, akieleza kuwa ufundishaji bora ndio msingi wa kuwajengea wanafunzi ujuzi wa maisha na ajira.

“Lengo la ziara hii ni kujadiliana na ATE kuhusu njia bora za kuwashirikisha waajiri katika kusaidia vijana waliopo vyuoni au waliomaliza masomo kupata mafunzo ya vitendo sehemu za kazi,” alisema Prof. Nombo.

Kwa upande wake, Afisa Mtendaji Mkuu wa Chama cha Waajiri Tanzania (ATE), Bi. Suzzane Ndomba, alisema ATE imekuwa ikisaidia wanafunzi kupata mafunzo kwa vitendo kupitia wanachama wake, wakiwemo viwanda na makampuni. Alitolea mfano wa Mradi wa Kukuza Ujuzi wa Vijana unaotekelezwa na ATE, uliowawezesha zaidi ya vijana 1,000 waliomaliza kidato cha nne kupata mafunzo ya miezi sita katika vyuo vya ufundi kabla ya kupelekwa makampuni kwa mafunzo ya vitendo, ambapo baadhi yao walipata ajira.

Aidha, alitoa wito kwa Watanzania kutumia Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) kujifunza ujuzi kwa gharama nafuu bila kujali kiwango cha elimu rasmi walichonacho.

Mazungumzo hayo yameonesha dhamira ya pamoja ya Serikali na sekta binafsi katika kuimarisha ujuzi wa vijana na kuandaa nguvu kazi yenye mchango katika maendeleo ya taifa.

TANZANIA YANG'ARA UWEKEZAJI KATIKQ ELIMU KWA RASILIMALI ZA NDANI

September 24, 2025 Add Comment


📌 *Dkt. Biteko asema tafiti zaonesha elimu bora huchangia asilimia 20-30 ya ukuaji wa uchumi*


📌 *Walimu milioni 17 wa shule za msingi na sekondari wahitajika Afrika ifikapo 2030*


📌 *Bajeti ya elimu yaongezeka kwa trilioni 1.44 tangu mwaka 2020/21*


*Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati*


Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema Tanzania ni miongoni mwa nchi zilizopiga hatua katika  matumizi ya rasilimali za ndani na kuwekeza katika sekta ya elimu kwa maendeleo endelevu.


Amesema hayo leo Septemba 24, 2025 jijini Dar es salaam wakati akifungua Kongamano la Tano la Kimataifa la Elimu Bora lililoongozwa na kauli mbiu inayosema “Kuimarisha mifumo na uwekezaji: Kusonga mbele katika Uhamasishaji wa Rasilimali za Ndani kwa ajili ya Elimu Jumuishi, Bora na Endelevu Barani Afrika”.

Dkt. Biteko ametaja hatua zilizochukuliwa na Serikali kuwa ni pamoja na kutunga na kuboresha Sera, Sheria na miongozo mbalimbali ya elimu, kuongeza kiwango cha bajeti ya elimu kutoka shilingi za trilioni 4.72 kwa mwaka wa fedha 2020/2021 hadi kufikia shilingi za trilioni 6.16   mwaka wa fedha 2024/2025.

Amesema ongezeko hilo la bajeti limeboresha mazingira na miundombinu mbalimbali ya elimu kwa maendeleo endelevu. Vile vile, Serikali imetanua wigo wa Sera ya Elimu bila malipo kwa elimu ya Sekondari ambapo mwaka 2020 kilitengwa kiasi cha shilingi za Kitanzania bilioni 312.08 na mwaka 2024 kilitengwa kiasi cha shilingi za Kitanzania bilioni 796.58 ikiwa ni sawa na ongezeko la shilingi bilioni 484.

“Ongezeko hili limeweza kupunguza changamoto za kifedha zinazorudisha nyuma sekta ya elimu na hivyo kuongeza idadi ya wanufaika wa elimu malipo kutoka wanafunzi 14,940,925 wa mwaka 2020 hadi kufikia wanufaika 16,155,282 wa mwaka 2024,” amesema Dkt. Biteko.


Ameongeza “Pamoja na mafanikio haya, Serikali inaendelea na mikakati mbalimbali kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo ili kutatua changamoto nyingine kadhaa katika sekta ya elimu kwa maendeleo endelevu.”

Amewahimiza wadau wa kongamano hilo kuifanyia kazi kauli mbiu ya mwaka huu ili kufikia utekelezaji wa matakwa ya kimataifa ya kutenga na kuelekeza asilimia 20 ya bajeti ya nchi katika maendeleo ya sekta ya elimu.


Aidha, amesema Afrika ikiwekeza katika elimu bora itaweza kutatua changamoto ya uhaba wa walimu bora hususan maeneo ya vijijini. Ambapo, hadi kufikia mwaka 2030 Bara hilo linahitaji kuwa na walimu milioni 17 ili kuwa na elimu bora ya  msingi na sekondari na kuwa na mifumo thabiti ya elimu ya kidigitali ambayo itasaidia kukabiliana na changamoto zilizopo nakuendana na mazingira tuliyonayo. 

Ambapo tafiti za Shirika la Ushirikiano wa Kiuchumi na Maendeleo (OECD) mwaka 2025 zinaonesha kwamba, elimu bora, kwa wastani, huchangia asilimia 20 hadi asilimia 30 ya ukuaji wa uchumi wa muda mrefu wa Taifa lolote. Tafiti hizo hizo pia zinaonesha kuwa, mtu mwenye elimu ya juu hupata kipato kwa wastani wa asilimia 50 hadi asilimia 100 zaidi ya mtu asiyekuwa na elimu hiyo ya juu.

Kwa upande wake, Naibu Waziri Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki anayeshughulikia masuala ya Afrika Mashariki, Mhe. Dennis Londo amesema suala la kugema raslimali fedha na watu vinaweza kuongeza ubora wa elimu na kupunguza changamoto za sekta ya hiyo kwa kushirikiana na wadau.


Naye, Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Carolyne Nombo amesema kuwa Kongamano hilo linalenga kuboresha sekta ya elimu nchini na kuwa Wizara yake ina jukumu la kuhakikisha elimu inayotolewa inakuwa katika viwango vya kimataifa. 


“ Kongamano hili limekuja katika wakati muafaka ambapo Serikali inaendelea kuwekeza raslimali fedha, hivyo mkutano huo utasaidia kugema raslimali fedha ili kuleta mabadiliko katika mfumo wa elimu,” amesema Prof. Nombo.

Meneja wa Kanda wa Global Partnership for Education (GPE), Belay Addise amesema kuwa Taasisi hiyo inajivunia ushirikiano wake mzuri uliopo kati yake na Serikali ya Tanzania tangu mwaka 2013. Ambapo kupitia ushirikiano huo Tanzania imepokea takribani dola za Marekani milioni 348 kupitia mashirika mbalimbali ikiwemo UNICEF, UNESCO na Swedish Development Agency (SIDA) kwa ajili ya kutekeleza miradi ya elimu.


Mratibu wa Mtandao wa Elimu Tanzania, Martha Makala ameishukuru Serikali kupitia Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia pamoja na wadau wa elimu kutoka ndani na nje nchi kwa kuwezesha Kongamani hilo na kuwa uwepo wa watunga sera katika Kongamano hilo utasaidia kufanya mijadala kuwa yenye tija itakayoleta matokeo chanya katika sekta ya elimu.

Mwisho.

TANZANIA YANG'ARA UWEKEZAJI KATIKA ELIMU KWA RASILIMALI ZA NDANI

September 24, 2025 Add Comment


📌 Dkt. Biteko asema tafiti zaonesha elimu bora huchangia asilimia 20-30 ya ukuaji wa uchumi


📌 Walimu milioni 17 wa shule za msingi na sekondari wahitajika Afrika ifikapo 2030


📌 Bajeti ya elimu yaongezeka kwa trilioni 1.44 tangu mwaka 2020/21


Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati


Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema Tanzania ni miongoni mwa nchi zilizopiga hatua katika  matumizi ya rasilimali za ndani na kuwekeza katika sekta ya elimu kwa maendeleo endelevu.


Amesema hayo Septemba 24, 2025 jijini Dar es salaam wakati akifungua Kongamano la Tano la Kimataifa la Elimu Bora lililoongozwa na kauli mbiu inayosema “Kuimarisha mifumo na uwekezaji: Kusonga mbele katika Uhamasishaji wa Rasilimali za Ndani kwa ajili ya Elimu Jumuishi, Bora na Endelevu Barani Afrika”.

Dkt. Biteko ametaja hatua zilizochukuliwa na Serikali kuwa ni pamoja na kutunga na kuboresha Sera, Sheria na miongozo mbalimbali ya elimu, kuongeza kiwango cha bajeti ya elimu kutoka shilingi za trilioni 4.72 kwa mwaka wa fedha 2020/2021 hadi kufikia shilingi za trilioni 6.16   mwaka wa fedha 2024/2025.

Amesema ongezeko hilo la bajeti limeboresha mazingira na miundombinu mbalimbali ya elimu kwa maendeleo endelevu. Vile vile, Serikali imetanua wigo wa Sera ya Elimu bila malipo kwa elimu ya Sekondari ambapo mwaka 2020 kilitengwa kiasi cha shilingi za Kitanzania bilioni 312.08 na mwaka 2024 kilitengwa kiasi cha shilingi za Kitanzania bilioni 796.58 ikiwa ni sawa na ongezeko la shilingi bilioni 484.

“Ongezeko hili limeweza kupunguza changamoto za kifedha zinazorudisha nyuma sekta ya elimu na hivyo kuongeza idadi ya wanufaika wa elimu malipo kutoka wanafunzi 14,940,925 wa mwaka 2020 hadi kufikia wanufaika 16,155,282 wa mwaka 2024,” amesema Dkt. Biteko.

Ameongeza “Pamoja na mafanikio haya, Serikali inaendelea na mikakati mbalimbali kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo ili kutatua changamoto nyingine kadhaa katika sekta ya elimu kwa maendeleo endelevu.”


Amewahimiza wadau wa kongamano hilo kuifanyia kazi kauli mbiu ya mwaka huu ili kufikia utekelezaji wa matakwa ya kimataifa ya kutenga na kuelekeza asilimia 20 ya bajeti ya nchi katika maendeleo ya sekta ya elimu.

Aidha, amesema Afrika ikiwekeza katika elimu bora itaweza kutatua changamoto ya uhaba wa walimu bora hususan maeneo ya vijijini. Ambapo, hadi kufikia mwaka 2030 Bara hilo linahitaji kuwa na walimu milioni 17 ili kuwa na elimu bora ya  msingi na sekondari na kuwa na mifumo thabiti ya elimu ya kidigitali ambayo itasaidia kukabiliana na changamoto zilizopo nakuendana na mazingira tuliyonayo. 

Ambapo tafiti za Shirika la Ushirikiano wa Kiuchumi na Maendeleo (OECD) mwaka 2025 zinaonesha kwamba, elimu bora, kwa wastani, huchangia asilimia 20 hadi asilimia 30 ya ukuaji wa uchumi wa muda mrefu wa Taifa lolote. Tafiti hizo hizo pia zinaonesha kuwa, mtu mwenye elimu ya juu hupata kipato kwa wastani wa asilimia 50 hadi asilimia 100 zaidi ya mtu asiyekuwa na elimu hiyo ya juu.

Kwa upande wake, Naibu Waziri Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki anayeshughulikia masuala ya Afrika Mashariki, Mhe. Dennis Londo amesema suala la kugema raslimali fedha na watu vinaweza kuongeza ubora wa elimu na kupunguza changamoto za sekta ya hiyo kwa kushirikiana na wadau.



Naye, Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Carolyne Nombo amesema kuwa Kongamano hilo linalenga kuboresha sekta ya elimu nchini na kuwa Wizara yake ina jukumu la kuhakikisha elimu inayotolewa inakuwa katika viwango vya kimataifa. 


“ Kongamano hili limekuja katika wakati muafaka ambapo Serikali inaendelea kuwekeza raslimali fedha, hivyo mkutano huo utasaidia kugema raslimali fedha ili kuleta mabadiliko katika mfumo wa elimu,” amesema Prof. Nombo.


Meneja wa Kanda wa Global Partnership for Education (GPE), Belay Addise amesema kuwa Taasisi hiyo inajivunia ushirikiano wake mzuri uliopo kati yake na Serikali ya Tanzania tangu mwaka 2013. Ambapo kupitia ushirikiano huo Tanzania imepokea takribani dola za Marekani milioni 348 kupitia mashirika mbalimbali ikiwemo UNICEF, UNESCO na Swedish Development Agency (SIDA) kwa ajili ya kutekeleza miradi ya elimu.


Mratibu wa Mtandao wa Elimu Tanzania, Martha Makala ameishukuru Serikali kupitia Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia pamoja na wadau wa elimu kutoka ndani na nje nchi kwa kuwezesha Kongamani hilo na kuwa uwepo wa watunga sera katika Kongamano hilo utasaidia kufanya mijadala kuwa yenye tija itakayoleta matokeo chanya katika sekta ya elimu.

Mwisho.

REA YASAMBAZA MAJIKO NA MITUNGI YA GESI KILO 15 KWA JESHI LA MAGEREZA MKOANI SHINYANGA

September 24, 2025 Add Comment

 

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) tarehe 24 Septemba, 2025 imesambaza kwa Watumishi wa Jeshi la Magereza 221 mkoa wa Shinyanga majiko ya gesi ya sahani (2) na mitungi ya kilo 15 kwa ajili ya Maafisa na Watumishi wa Jeshi hilo huku wito ukitolewa wa kuwataka wawe mabalozi wa nishati safi kwa mkoa huo.

Katika hafla hiyo ya ugawaji wa majiko na mitungi ya gesi, Mjumbe wa Bodi ya Nishati Vijijini (REB); Mhandisi, Ahmed Chinemba ametoa wito kwa Watumishi wa Jeshi hilo huku akieleza mkataba wa kusambaza teknolojia mbalimbali za nishati safi kati ya Wakala na Jeshi hilo, ulisainiwa mwezi Septemba, mwaka 2024 kwa gharama ya shilingi bilioni 35 kwa Magereza 129 Tanzania Bara.

Chinemba amesema Maafisa wa Magereza wanatakiwa kuwa mabalozi katika utumiaji wa teknolojia za nishati safi kama majiko ya gesi na kuongeza kuwa Wananchi wengi wa maeneo ya vijijini wanakata miti hovyo kwa ajili ya matumizi ya kuni na mkaa.

“Ninawapongeza Jeshi la Magereza kwani wamekuwa vinara wa matumizi ya nishati safi kwenye Magereza yote ukilinganisha na Taasisi nyengine sawa sawa na agizo la Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu kuzitaka Taasisi zinazohudumia Watu zaidi ya 100 kutumia nishati safi kama gesi; gesi vunde, mkaa na kuni mbadala”. Alisema Mhandisi, Chinemba.

Chinemba amesema katika utekelezaji wa Mradi huo, REA imechangia shilingi bilioni 26 na Jeshi la Magereza limetoa shilingi bilioni 8 ambapo ushirikiano huo umelenga katika maeneo kadhaa ikiwemo ujenzi wa miundombinu 126 ya bayogesi na majiko banifu 377; Ujenzi wa miundombinu 64 ya LPG na majiko banifu 256; Usambazaji wa mitungi ya gesi 15,126 ya kilo 15 pamoja na majiko ya gesi ya sahani mbili kwa watumishi wote wa Magereza; Usambazaji wa mkaa unaotokana na makaa ya mawe (Rafiki briquettes) tani 850 na majiko banifu 344 kwa kambi 129 za Magereza na maeneo mengineyo.

Naye, Mkuu wa Magereza mkoa wa Shinyanga, Kamishna Msaidizi Mwandamizi, Nobert Ntacho ameishukuru Serikali kupitia REA na kukiri kupokea mitungi ya gesi na majiko ya sahani mbili na kusema familia za Watumishi wa Jeshi hilo, wanakwenda kunufaika ambapo tayari wamepatiwa mafunzo ya matumizi ya nishati safi.

Kwa upande wake, Mkuu wa Gereza wilaya ya Shinyanga; Kamishina Msaidizi, Martin Kunambi amesema Gereza linahudumia mahabusi 263 na kuongeza kuwa walishajenga miundombinu ya kupikia tangu Rais Samia Suluhu Hassan atoe maelekezo ya kuzitaka Taasisi zenye kuhudumia Watu zaidi ya 100 kuacha matumizi ya nishati zisizo safi na salama kama kuni na mkaa na kuhamia kwenye matumizi ya nishati safi na salama

“Tunaipongeza na kuishukuru Serikali, leo tumepokea majiko na mitungi ya gesi ipatayo 221 sawa na idadi ya askari na Watumishi waliopo hapa mkoa wa Shinyanga” amesema Bwana Kunambi.



TEITI YASHIRIKI MAONESHO YA NANE YA UWEKEZAJI KATIKA SEKTA YA MADINI MKOANI GEITA

September 23, 2025 Add Comment




● Tanzania yaendelea kutekeleza Vigezo vya Kimataifa vya EITI kikamilifu



● Uwazi wa Mikataba katika sekta ya uziduaji waanza kutekelezwa.


📍 GEITA*

Katika maonesho hayo yaliyofunguliwa tarehe 22 Septemba, 2025 na Mhe. Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Kassim Majaliwa Majaliwa.Imeelezwa kwamba, tangu Tanzania ijiunge na Asasi ya Kimataifa ya EITI iliyopo nchini Norway, TEITI imeendelea kutekeleza kikamilifu vigezo vya Kimataifa vya EITI vya mwaka 2023 pamoja na Sheria ya TEITA, 2015 ambapo katika tathimini ya umoja wa EITI ulifanyika hivi karibuni Tanzania imeendelea utekelezaji wa vigezo vya EITI kikamilifu.

Hayo, yameelezwa leo Septemba 23, 2025 na Meneja Kitengo cha Uwazi na Uwajibikaji kutoka Taasisi ya TEITI - Bw. Erick Ketagory. 

Bw. Ketagory amesema kuwa, katika kipindi cha kuanzia 2009 hadi 2025 TEITI imetoa ripoti 15 za ulinganishi wa malipo ya Kampuni za Madini, Mafuta na Gesi Asilia na mapato ya Serikali ambapo ripoti ya 15 ya TEITI kwa mwaka 2022/2023 iliwekwa wazi  mwezi Juni, 30 mwaka 2025.

Kwa upande mwingine,  Bw. Ketagory amesisitiza kuwa utekelezaji wa Takwa la uwekaji wazi wa Mikataba ambayo Serikali imeingia na kampuni za sekta ya uziduaji imeanza kutekelezwa ambapo Mikataba hiyo imewekwa wazi kupitia tovuti ya TEITI.

Tunawakaribisha wananchi wote Mkoani Geita kutembelea banda la TEITI ili kujifunza majukumu ya TEITI na namna ya kutumia takwimu zinazotolewa na tipoti za TEITI, "alisisitiza Bw. Ketagory"


Taarifa na Ripoti za TEITI zinapatkana kupitia: www.teiti.go.tz

TRA Dodoma Yawataka Wafanyabiashara Kulipa Kodi Kabla ya Septemba 30

September 23, 2025 Add Comment
Na. Yahya Saleh, Dodoma

Meneja wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Mkoa wa Dodoma Bw. Pendolake Elinisafi amewataka wafanyabiashara kuhakikisha wanalipa kodi ya awamu ya tatu kwa wakati kabla ya tarehe 30.09.2025 ili kuepuka faini zisizo za lazima.