WAZIRI WA AFYA AANZA ZIARA MKOANI KILIMANJARO

October 04, 2024

Waziri wa Afya Mhe. Jenista Mhagama ameanza ziara yake ya siku Sita leo Oktoba 4, 2024 katika Mkoa wa Kilimanjaro kwa kukagua miradi mbalimbali ikiwemo ya Sekta ya Afya iliyotolewa fedha na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Katika ziara yake Waziri Mhagama amekagua ujenzi wa jengo la wagonjwa wa nje (OPD) katika kituo cha Afya Masama Kati na kuweka jiwe la msingi, ametembelea na kukagua jengo la kuhifadhia maiti pamoja na kuweka jiwe ka msingi katika kituo cha Afya Longoi, ametembelea na kukagua jengo la Zahanati ya Kimashuku na kuizindua.









Share this

Related Posts

Previous
Next Post »