.jpg)
Na Oscar Assenga, MKINGA
WAVUVI na Wakulima wa Mwani 800 wilayani Mkinga mkoani Tanga wanatarajiwa kupatiwa elimu ya utendaji wa shughuli zao kwa usalama ili kuwaepusha na changamoto za baharini zinazotokana na uwepo wa mwigiliano wakati wa utekelezaji wa majukumu yao.
.jpg)
Hayo yalisemwa na Mkurugenzi wa Shirika la Uwashem Hussein Msagati wakati wa kikao cha wavuvi na wakulima wa mwani katika kata ya Boma wilayani humo ikiwa ni kutambulisha mradi wa kujenga uwezo kwa matumizi bora ya rasilimali za bahari ngazi ya Kata .
Mradi huo unaendeshwa na Shirika la Umoja wa Wasaidizi wa Sheria wilayani Mkinga (Uwashem) ukifadhiliwa na Shirika la 4 H Tanzania pamoja na We World ambapo sasa utasaidia kuwaweka kwenye hali ya amani ili waweze kushirikiana kwa pamoja kufanya kazi zao na kutokuwepo kwa mivutano ya hapa na pale.

Alisema kwamba umuhimu wa elimu hiyo ni mkubwa kutokana na changamoto za baharini zinazotokana na kuwepo kwa mwingiliano wa maeneo kwa sababu wavuvi wanaotumia makokoro wanaingia kwenye maeneo yanayolimwa mwani kufanya shughuli za uvuvi.
Aidha alisema kwamba hatua hiyo inapelekea kuharibu mazao ya mwani jambo ambalo sio zuri hivyo ikiwezekana washirikiane kwa pamoja ili kuepusha migongano katika shughuli zao za kila siku.
Awali akizungumza Kaimu Afisa Maendeleo ya Jamii wilaya ya Mkinga Hilda Muro alilipongeza Shirika hilo kwa kuandaa vikao kati ya wavuvi na wakulima wa mwani akieleza kwamba itasaidia kuleta tija kwa kuwaepusha na migogoro au kuitatua pindi inapotokea baina yao wakati wa utekelezaji wa majukumu yao baharini.
Alisema kwamba wanapotokea wadau kama hao kuwaletea elimu ya kutatua migigoro kwa njia za mazungumzo inapendeza zaidi hivyo wanalishukuru shirika hilo kuwapelekea elimu na wanaamini kupitia elimu hiyo kwa wananchi itakuwa ni mwanzo wa amani kwa jamii za pwani.
“Kutokana na kila mtu atafanya shughuli zake bila kukutana na vikwazo au kubuguziwa na mtu mwengine yoyote na hivyo kutengeneza amani na mazingira ya uzalishaji kuwa bora kuanzia sasa”Alisema
Hata hivyo alisema kwamba elimu itasaidia uzalishaji mwani na wavuvi kutokana na kwamba watakuwa wakitekeleza majukumu yao wakiwa kwenye hali ya usalama baharini.
Hata hivyo mmoja wa Wavuvi wilayani humo Yasin Baraza alisema kwamba midahalo hiyo inayoendeshwa na Shirika hilo itawasaidia kuweza kutatua migogoro kati ya wavuvi na wakulima wa mwani na tatizo hilo liweze kuondoka moja kwa moja .
Mwisho.




.jpg)




























.jpg)
