Showing posts with label elimu. Show all posts
Showing posts with label elimu. Show all posts

CRDB Bank Foundation, StartHub Africa zaungana kuwawezesha wanafunzi wa vyuo vikuu

June 13, 2025 Add Comment

 

Meneja Uendelezaji Biashara Changa wa CRDB Bank Foundation, Sharron Nsule akitoa elimu ya ujasiriamali kwa wanafunzi walioshiriki semina katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.
Dar es Salaam, Tanzania – June 2025: Katika kuendeleza jitihada za kuinua ujasiriamali na kuwawezesha wanafunzi wabunifu, Taasisi ya CRDB Bank Foundation kwa kushirikiana na StartHub Africa imevitembelea vyuo vikuu vitatu nchini na kutoa mafunzo ya elimu ya fedha kwa wanafunzi wanaopenda kumiliki biashara baada ya masomo yao.

Ushirikiano huo unaotekelezwa kupitia programu ya “Uni Launch and Scale” tayari umewafikia zaidi ya wanafunzi 1,000 katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Chuo Kikuu cha Iringa na Taasisi ya Uhasibu Arusha (AIA) na kuwapa fursa ya kupata walezi wa kibiashara na mitaji wezeshi kutoka CRDB Bank Foundation.

Akizungumzia mafunzo hayo, Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB Bank Foundation, Tully Esther Mwambapa amesema vyuo hivi vitatu ni mwanzo tu kwani lengo lililopo ni kuwafikia wanafunzi wengi zaidi na kuwawezesha ili wanapohitimu au wakai wanaendelea na masomo yao waanze kushiriki shughuli za kuujenga uchumi baada ya kuwapa elimu ya fedha, mafunzo ya ujasiriamali na uhakika wa kupata mtaji wezeshi.

“Lengo letu ni kuamsha ari ya ujasiriamali iliyomo ndani ya wanafunzi wetu wa vyuo vikuu na kutoa mazingia rafiki kwao kuanzisha biashara zitakazoajiri vijana wenzao badala ya wao wenyewe kuwa waombaji wa kazi wakihitimu. Kupitia ushirikiano huu tunajenga kizazi cha vijana waliowezeshwa kushiriki kuujenga uchumi wa taifa letu,” anasema Tully.

Katika vyuo vitatu ambako wataalamu wa CRDB Bank Foundation na StartHub Africa wamepita, jumla ya biashara 30 zinazomilikiwa na kuendeshwa na wanafunzi zitachaguliwa baada ya kukaguliwa ili kuingizwa kwenye mpango maalumu wa mafunzo ya usimamizi na uendeshaji biashara, utayari wa kifedha na utimamu wa bidhaa.

“Kwa kushirikiana na StartHub Africa pamoja na vyuo vikuu hivi, tunaamini tunaendeleza juhudi za kukuza ubunifu hasa wa kidijitali miongoni mwa wanafunzi wetu hivyo kujenga msingi imara wa biashara zinazoweza kukua na kuwanufaisha wananchi wengi,” amesema Tully.

Programu ya Uni Launch and Scale ambayo CRDB Bank Foundation inashirikiana na StartHub Africa kuitekeleza inalenga kuwawezesha wanafunzi wa vyuo vikuu kutekeleza uwekezaji wanaoukusudia kwa kuwapa mafunzo, ulezi wa kibiashara na uwezeshaji wa mitaji kupitia Programu ya Imbeju iliyojielekeza kuwainua vijana, wanawake na makundi maalumu.

Meneja Programu wa StartHub Africa, Zagaro Emanuel anasema katika ushirikiano huu wanakusudia kuwawezesha vijana wengi wabunifu kupitia mafunzo ya ujasiriamali na elimu ya fedha hivyo kuchangia kuujenga uchumi na kusukuma mbele maendeleo ya Tanzania.

“Tunawahamasisha wanafunzi na wahitimu wa vyuo vikuu, tunawandaa waanzilishi wapya wa biashara watakaosaidia kuleta mapinduzi ya kiuchumi na kuimarisha ujasiriamali nchini kwa kushirikiana na vyuo vikuu, wawekezaji na wawezeshaji. Tukiwa pamoja na Taasisi ya CRDB Bank Foundation, tunaamini tutafika mbali na kuwajumuisha wanafunzi wengi zaidi nchini,” anasema Emanuel.

Meneja huyo anaongeza kwamba programu hiyo inawapa wanafunzi jukwaa la kujitangaza katika soko la ndani, kitaifa na kimataifa na wanapowasilisha mawazo ya miradi yao, wanajiweka kwenye nafasi nzuri zaidi ya kuvutia mitaji huku vyombo vya habari vikiwarahisishia kujulikana kwa biashara zao hivyo kujiongezea umanifu kwa wadau ambalo ni jambo jema kwa kila biashara.

DKT.BITEKO AFURAHISHWA NA UTATUZI CHANGAMOTO ZA ARDHI MONDULI

April 24, 2025 Add Comment


📌 Azindua Shule ya Sekondari Migungani, awataka wanafunzi kutunza miundombinu


📌 Asema Serikali yajipanga kujenga mradi mkubwa wa umeme Monduli


Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati


Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko ameupongeza uongozi wa Wilaya ya Monduli kwa jitihada zao za kutatua migogoro ya ardhi wilayani humo ikiwa ni utekelezaji wa agizo la  Serikali la  kuwataka viongozi kutatua changamoto za wananchi katika maeneo yao.

Dkt. Biteko ametoa pongezi hizo Aprili 23, 2025 wilayani Monduli, mkoani Arusha wakati akihutubia wananchi mara baada ya kuzindua Shule Mpya ya Sekondari ya Migungani iliyopo wilayani humo.


“Naomba kuwapongeza tena uongozi wa Wilaya ya Monduli kwa kuendelea kufanya kazi nzuri sana hapa wilayani kwa maslahi mapana ya wananchi wa Monduli. Nimejulishwa kuwa, mmefanya mengi mno ikiwemo utatuzi wa changamoto na migogoro ya ardhi hapa wilayani. Nimejulishwa kuwa sehemu kubwa ya changamoto hizi mmefanikiwa kuzitatua hongereni sana,” amesema Dkt. Biteko.

Ameipongeza pia kamati ya kutatua kero za wananchi inayoongozwa na Mkuu wa Wilaya ikiwa na wataalamu mbalimbali ambayo imejiwekea utaratibu wa kupokea kero kutoka kwa wananchi na kuzipatia ufumbuzi, ambapo ameitaka pia iratibu zoezi la kutoa elimu kwa wananchi kuhusu masuala ya ardhi.

Akiwa shuleni hapo, Dkt. Biteko amewapongeza wananchi kwa kujenga shule hiyo ya Sekondari Migungani na kufikia asilimia 85 ya ujenzi huku Serikali ikichangia shilingi milioni 500.


“ Sote tunafahamu kuwa, elimu ni msingi mkubwa wa maendeleo. Sisi wana Monduli tayari tunayo shule yetu hii ambayo imeshakamilika. Hii ni miongoni mwa shule zilizopo Wilayani hapa ambazo zitaendelea kutupatia elimu kwa vijana wetu,” amesema Dkt. Biteko.

Ameongeza kuwa Shule hiyo itakuwa na uwezo wa kuwa na wananfunzi 400 na hivyo amewataka wanafunzi kutunza miundombinu sambamba na kujifunza kwa bidi ili wajiandae kuwa wazalendo na raia wema huku wakiwa na uwezo wa kutafuta majibu ya matatizo watakayokumbana nayo.


Kuhusu miradi ya umeme wilayani humo, amesema kuwa mwaka huu Serikali inatarajia kujenga mradi mkubwa wa umeme kwa lengo la kuuongezea nguvu umeme  unaopatikana ili uweze kufika  Loliondo na kusaidia wilaya hiyo kuwa na  umeme wa uhakika.

Aidha, Dkt. Biteko amezungumzia maadhimisho ya miaka 61 ya Muungano kwa kuwataka Watanzania kuenzi muungano huo kwa kujenga Taifa moja kwa kushikamana  na kufanyakazi kwa pamoja kwa kushirikiana.

Naye, Mkuu wa Wilaya ya Monduli, Mhe. Festo Kiswaga amesema kuwa Wilaya hiyo ni tegemeo kwa Chama Cha Mapinduzi na wamekuwa wakishirikiana na wananchi katika kutekeleza shughuli mbalimbali za maendeleo.

Pia, amesema Serikali imekuwa ikitoa fedha nyingi kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ikiwemo barabara, hospitali, shule na kuwa Wilaya hiyo ni kati ya wilaya zinazofanya vizuri katika elimu na huku akimshukuru Rais Samia kwa kuwekeza katika elimu nchini.


MWISHO

WAISHUKURU TAASISI YA UMOJA WA WASAIDIZI WA SHERIA UWASHEM KUWAWEZESHA KUTATUA MIGOGORO BAINA YA WAVUVI NA WAKULIMA WA MWANI

April 07, 2025 Add Comment

 


WANANCHI wanaofanya shughuli za  Uvuvi na Wakulima wa Zao la Mwani wanaoishi katika kijiji cha Mwaboza wilaya ya Mkinga Mkoani Tanga wameishukuru taasisi ya Umoja wa wasaidizi wa Sheria 'UWASHEM' kwa kuwawezesha kutatua mgogoro baina yao kutokana na matumizi ya rasilimali bahari ambapo kupitia elimu waliyoipata imewawezesha kuwaunganisha.


Awali wakizungumza katika mdahalo wa pamoja  ulioandaliwa na taasisi hiyo kwa lengo la kutambua changamoto zilizopo baina yao Kila mmoja ameonekana kumshutumu mwingine kuwa chanzo cha mgogoro kwa kile walichoeleza kuwa wamekuwa wakigombania maeneo hali iliyopelekea kukosa maelewano na hatimaye kuwaingiza kwenye mgogoro.

Wakizungumza baadhi yao wamesema kuwa pamoja na elimu waliyoipata kupitia shirika la UWASHEM' ni vyema Serikali ikatenga maeneo maalum ili kuwasaidia wananchi hao kufanya shughuli zao bila bughuza  na hatimaye kuendelea kujipatia kipato Chao cha Kila siku

Mratibu wa miradi kutoka shirika la UWASHEM' Swalehe Sokolo amesema kuwa  kupitia mradi huo wanaoutekeleza imesaidia kwa kiasi kikubwa kutatua changamoto baina ya Wavuvi na Wakulima wa Zao la Mwani ambapo pia wameweza kuwaunganisha na viongozi wa Serikali.

Kwa upande wake mratibu wa mradi wa KUJENGA AMANI PAMOJA kutoka shirika la shirika la We World  Zacharia Msabila amesema wanafanya kazi na  taasisi zilizopo karibu na jamii ambapo kupitia ufadhili wanaoutoa itasaidia kufikia malengo waliyoyatarajia.

Diwani wa kata ya Moa Staruki Njama amekiri uwepo wa migogoro ya muda mrefu biana ya Wakulima wa Zao la Mwani na Wavuvi katika kijiji cha Mwaboza ambapo shirika la UWASHEM' limekuja kuleta suluhisho kupitia elimu waliyoitoa ambapo amewapongeza kwa jitihada walizozifanya huku akisisitiza  wananchi kuendelea kufuatia na kutekeleza Sheria zilizowekwa.

Shirika la umoja wa usaidizi wa Sheria Mkinga "UWASHEM'' linatekeleza mradi wa KUJENGA AMANI  PAMOJA katika wilaya hiyo kwa kushirikiana na shirika la 4H Tanzania  ukifadhiliwa na shirika la We World kwa lengo la kuleta amani baina ya wananchi kutatua changamoto mbalimbali ambazo zinaweza kupelekea uvunjifu wa amani.

VETA TANGA WAADHIMISHA MIAKA 30 YA KUANZISHA KWAKE KWA KUFANYA UKARABATI SHULE YA MSINGI CHANGA

March 16, 2025 Add Comment


Na Oscar Assenga,TANGA

CHUO cha Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) Jijini Tanga katika kuadhimisha miaka 30 ya kuanzishwa kwake wamefanya shughuli mbalimbali za kijamii ikiwemo kufanya ukarabati wa majengo ,Miundombinu ya Umeme ,Tehama pamoja na kwashonea sare wanafunzi wa Shule ya Msingi Changa ya Jijini Tanga.

Akizungumza kuhusu maadhimisho hayo Mkuu wa VETA kituo cha Tanga,Gideon Lairumbe alisema kwamba wameamua kuadhimisha katika shule hiyo kutokana na kwamba ni miongoni mwa wanufaika wa maadhimisho ya VETA ambayo kitaifa kilele chake kitafanyika Jijini Dar es salaam kuanzia Machi 17 hadi 21 mwaka huu mgeni rasmi anatarajiwa kuwa waziri Mkuu Kassim Majaliwa.

Alisema kwa ngazi ya kituo cha Tanga,VETA imefanya ukarabati darasa la awali kujenga sakafu ya nje ya shule,mfumo wa umeme,Tehama na kuziba maeneo hatarishi maeneo hatarishi ya mmomonyoko wa udongo wakati wa mvua .

Eneo jingine ambalo shule hiyo imenufaika na VETAni kuwashonea sare wanaf unzi 150,kupiga rangi na kukarabati mfumo wa jiko la kupikia zikiwamo sufuria.

Shule nyingine iliyonufaika na VETA katika maadhimisho hayo ni ya Msingi Juhudi wa mamambayo wanafunzi wenye mahitaji maalumu wameshonewa sare na kwa upande wa Mama lishe katika mitaa mbalimbali wamepewa kofia na vizibao vya kuwahudumia wateja.

“Tumefanya hivi ikiwa ni jithada za VETA kurejesha imani kwa jamii ambayo imekuwa ikiihudumia kwa kipindi cha miaka 30 tangu kuanzishwa kwake lakini pia kuwavuta vijana kujiunga katika mafunzo yake ambayo yamesaidia kwa kiasi kikubwa kutoa ajira”amesema Lairumbe.

Yussuph Ilias ambaye ni mzazi wa wanafunzi wawili wanaosoma shule ya Msingi Changa amesema ukarabati uliofanywa na VETA umesaidia kwani imebadilika na kuwa ya kisasa na kuwawezesha awanafunzi kusoma bila wasiwasi.

“Kwa mfano upande wa baharini shule ya Changa inapakana na bahari ya Hindi..kule chini kulikuw na mmompnyoko ambao ulikuwa ukitutia wasiwasi wazazi kuhusu usalama wa watoto,lakini VETA wameweka vifusi na hali imekuwa nzuri”amesema Ilias.

Makamu Mwenyekiti wa wanafunzi wa Chuo cha VETA Tanga,Mariam Hashim amewaomba wazazi kuwapeleka vijana wao waliohitimu shule za Sekondari na vyuo mbalimbali ili kupata mafunzo ya ufundi yatakayowasaidia kujiajiri.

“Mfano ni mimi nimehitimu chuo kikuu lakini nimeamua kuja VETA kupata ujuzi wa ufundi wa umakenika na kabla sijamaliza mwaka wangu wa pili tayari kuna mashirika matatu yamenifuata na yameahidi kunipa kazi”amesema Mariam.

KAMPUNI YA DNATA NA EMIRATES LEISURE ZATOA MSAADA WA VIFAA VYA SHULE ZANZIBAR

January 26, 2025 Add Comment



Wafanyakazi wa Kampuni za DNATA na Emirates Leisure za Zanzibar wakiwa katika picha ya pamoja na wanafunzi wa Shule za Msingi na Sekondari za Kijiji cha Kendwa baada ya kupatiwa vifaa vya shule Januari 23, 2025.

................................................ 

Na Dotto Mwaibale 

KAMPUNI ya DNATA na Emirates Leisure za Zanzibar zimetoa vifaa vya shule kwa Shule za Msingi na Sekondari za Kilindi  kwa ajili ya kusaidia jamii zenye uhitaji. 

Akizungumza katika hafla ya kukabidhi msaada huo Kijiji cha Kendwa kilichopo Wilaya ya Kaskazini A Mkoa wa Kaskazini, Mwakilishi wa kampuni ya Emirates Leisure  Msokolo Layya alisema wameamua kutoa sehemu ya fedha zao kwenye eneo la elimu ambayo ndio msingi wa maisha na kuwa msaada huo umewafikia wanafunzi 240. 

“Kampuni hizi zimeanzisha mpango wenye lengo la kutoa nyenzo muhimu za kujifunzia watoto ili kuwajengea uzoefu na kuwainua kitaaluma,” alisema Layya. 

Layya alitaja vifaa hivyo kuwa ni kalamu za kuandikia, vifutio, madaftari, mikebe yenye vifaa vya kucholea na vingine vinavyofanana na hivyo. 

Layya alisema kampuni hizo zitaendelea kusaidia wahitaji na kuwa mpango huo ni endelevu na tayari wamekwisha ratibu ratiba ya kufanya hivyo kwa mwaka mzima. 

Alisema kampuni hizo zinafanya hivyo ikiwa ni kuunga mkono jitihada za Serikali ya Mapinduzi Zanzibar inayoongozwa na Rais Dkt. Hussein Ali Mwinyi kwa kusaidia makundi yenye uhitaji na shughuli mbalimbali za kijamii. 

Akizungumza katika hafla hiyo Meneja wa Kampuni ya  Emirates Leisure, Paul Attallah alisisitiza kuendelea kudumisha ushirikiano baina ya kampuni hizo na Serikali ili kutoa huduma kwa wananchi wa Zanzibar hasa katika sekta ya elimu.

Wanafunzi hao wakiwa na vifaa vya shule walivyo kabidhiwa.
Vifaa hivyo vikikabidhiwa kwa wanafunzi hao. Kushoto ni Mwakilishi wa kampuni ya Emirates Leisure  Msokolo Layya.