Showing posts with label elimu. Show all posts
Showing posts with label elimu. Show all posts

HESLB INAVYOSHIRIKIANA NA WADAU KUWAWEZESHA WANAFUNZI KUJITEGEMEA KIUCHUMI

February 23, 2026 Add Comment

 Na: Dk. Reubeni Lumbagala, Tanga



Elimu ni haki muhimu ya binadamu. Elimu ni nyenzo muhimu ya kumsaidia binadamu kumudu maisha yake. Kwa kutambua hilo, ndiyo maana wazazi na walezi wanapambana sana kusomesha watoto na vijana wao ili kuwawezesha kupata elimu bora ya kuwasaidia katika maisha yao na kutimiza ndoto zao za kimaendeleo walizonazo.

Kazi kubwa na nzuri zimefanyika nchini katika kuboresha sekta ya elimu katika ngazi zote za elimu kuanzia elimu ya awali, msingi, sekondari, vyuo vya kati na vyuo vikuu Ili watoto na vijana wa Kitanzania waweze kupata elimu bora ya kuwasaidia maishani mwao. Mitaala ya ujifunzaji imeboreshwa ili kuwajengea wanafunzi umahiri wa kujitegemea pindi wanapohitimu ngazi mbalimbali za masomo yao.

Ikumbukwe kuwa mabadiliko haya mazuri ya mitaala yamekuja kipindi hiki ambacho wahitimu wengi wana changamoto ya kukosa stadi na ujuzi stahiki wa kuwawezesha kuajiriwa au kujiajiri katika sekta mbalimbali. Ndiyo maana wengi tunapongeza mabadiliko haya ya mitaala kwa ustawi mwema wa wahitimu. Katika elimu ya juu, serikali kupitia Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) inaratibu zoezi la utoaji mikopo kwa wanafunzi huku wanufaika wa mikopo hiyo wakiwajibika kuirejesha mikopo hiyo baada ya kuhitimu na kuwa na kipato katika sekta rasmi au isiyo rasmi.

Kwa kutambua changamoto iliyopo kwa baadhi ya wahitimu kukosa ujuzi na stadi mbalimbali, HESLB inashirikiana na taasisi mbalimbali zikiwemo taasisi ya kifedha katika kuhakikisha wanawajengea uwezo wahitimu ili waweze kuajiriwa au kujiajiri ambapo kufanikiwa kwao kunaiwezesha HESLB kukusanya fedha kutoka kwa wahitimu hao lakini pia nchi kupata wataalamu kwa maendeleo.

Mathalani, Februari 18, 2026, katika Ofisi za CRDB Makao Makuu Jijini Dar es Salaam, HESLB iliingia makubaliano ya kushirikiana na CRDB Bank Foundation na kampuni ya Basil Link ili kuwawezesha wanafunzi wa vyuo vikuu kupata ujuzi wa kidigitali, elimu ya ujasiriamali na elimu ya fedha.

Kwa hakika makubaliano haya ni mwelekeo mzuri katika kuwaandaa wanafunzi wa vyuo vikuu kujitegemea kutokana na mafunzo muhimu watakayoyapata kupitia uwezeshaji utakaofanywa hasa katika kuwa na jicho la kuona fursa za kiuchumi zilizopo.

Kupitia programu hiyo lijulikanalo kwa jina la "Imbeju - SmartElite," wanafunzi wa vyuo watapata mafunzo ya ujasiriamali ili kuweza kujiajiri wenyewe. Aidha, watapata pia elimu ya fedha ambayo ni muhimu sana katika ulimwengu huu wa sasa. Sanjari na hilo, wanafunzi watapata mikopo nafuu na ushauri elekezi wa namna bora ya kuwekeza mikopo hiyo ili ilete tija kiuchumi.

Katika hafla hiyo, Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB Foundation, Tully Mwambapa alisema "Tunataka kuona vijana wanachangamkia fursa, wanabuni, wanaanzisha biashara na hata kuajiri wengine. Hii si tu kuwasaidia kumaliza chuo, bali kuwaandaa kuingia katika uchumi wa kidigitali wakiwa tayari na ujuzi pamoja na raslimali."

Kwa upande wa Dk. Peter Mmari ambaye ni Mkurugenzi na Upangaji Mikopo wa HESLB amesema "Kupitia mpango huu, wanafunzi wataongeza uwezo wa kutumia mifumo ya kidijitali na watapata fursa ya kujiajiri wakiwa vyuoni au baada ya kuhitimu. Tunaamini wataweza pia kutoa mchango katika kuwainua Watanzania wengine kielimu na kiuchumi."

Kimsingi, vijana wenye vipaji na mawazo bunifu watanufaika na mpango huu huku wakiwezeshwa mitaji na vitendea kazi kama kompyuta. Kwa hakika programu ya Imbeju - Smart Elite, ni mkombozi kwa vijana hasa katika ulimwengu wa uchumi wa kidijitali na biashara.












MBUNGE MAKUBEL AANZA NA ELIMU AGAWA MADAFTARI SHULE ZA MSINGI KUUNGA MKONO JUHUDI ZA SERIKALI

February 19, 2026 Add Comment


Na Oscar Assenga, TANGA

MBUNGE wa Jimbo la Tanga (CCM) Kassim Amar Makubel ameanza kugawa madaftari kwa wanafunzi wa shule za Msingi ikiwa ni sehemu ya kuunga mkono juhudi za Serikali katika kuinua sekta ya elimu hapa nchini.

Makubel aliyasema hayo wakati wa halfa ya kuzindua zoezi la kugawa Madaftari kwa wanafunzi wa Shule za Msingi Pongwe kupitia Mpango wa Daftari la Mama Samia kwa kushirikiana na Taasisi ya Watoto Foundation ambapo mpango huo utazifikia shule zote kwenye Jimbo hilo.

Mbunge huyo alisema kwamba mpango huo ni sehemu ya kuunga mkono juhudi za Serikali na Rais Dkt Samia Suluhu katika sekta ya elimu kutokana na mabadiliko na mageuzi makubwa yaliyofanyika.

Alisema kwamba wakati alipoingia madarakani alikaa na kubaini vijana wengi wa shule ya msingi wanapitia changamoto nyingi hivyo akaona ni bora kila kila mzazi wa mtoto wa Jimbo hilo anayesoma shule ya msingi walau aguse maisha yake kwa kutoa madaftari matano 5 ili kuwapunguzia makali kwenye baadhi ya mahitaji.


Alieleza madaftari hayo ni sehemu ya mchango wake kurejesha shukrani kwa kumchagua katika uchaguzi mkuu uliopita na wameanza rasmi uzinduzi ambapo wataanza kugawa madaftari hayo Tarafa ya Pongwe na kasha kuelekea kwenye kata nyengine.

Aidha alisema kwamba Tarafa hiyo inayojumuisha Kata za Marungu,Kirare na Pongwe na baadae wataenda kwenye Tarafa nyengine ili kuhakikisha shule zote za misngi zinafikiwa na kuwagusa.



Alisema keamba mabadiliko hayo yaliyofanywa na Rais Dkt Samia Suluhu katika sekta ya elimu wakati alipoingia madarakani ni kuona elimu walionayo haikizi mahitaji ya sasa na wanatakiwa kuendana na mabadiliko kwenye mitaa ya elimu ya sasa na sasa watoto watasoma darasa la kwanza mpaka la sita.



Aidha alisema mabadiliko hayo machache ikiwemo mkondo wa amali ambao ni muhimu kwa ajili ya kuwapatia ujuzi watoto wanapomaliza shule jambo ambalo litasaidia kuongeza wataalamu mbalimbali ambao watakuwa na mchango mkubwa wa kuweza kujiajiri na kuweza kujiendeleza kwenye vyuo vya kati

“Kutokana na mabadiliko hayo makubwa ya kielimu hapa nchi na hakuna malipo hivyo tuwahimize watoto waende shule pamoja na kufuatilia maendeleo yao na tuhudhurie vikao”Alisema .



Awali akizungumza Mwalimu Mkuu Msaidizi wa shule ya Pongwe Mchanganyiko Abubakari Sadik alimshukuru Mbunge huyo kwa kuwapelekea msaada huo madaftari ambayo yamekuja kutatua changamoto ya watoto ambao hawana uwezo wa kununua madaftari kwa wakati .

"Ukosefu wa daftari ni kwamba wanafunzi asipokuwa na madaftari anakosa kumbukumbu ya kusoma kipindi anapofikia kwenye mtihani yake hivyo msaada huu umeenda kutatua changamoto ya kila mmoja kutokana na wazazi wa watoto wengine wako mbali na inakuwa vigumu kuwa na madaftari kila wakati”Alisema

Alisema kwamba shule hiyo imekuwa ikifanya vizuri katika taaluma na wamekuwa na mwendelezo mzuri wa wanafunzi katika madarasa ya mitihani ya darasa la nne.

Aliongeza kwamba changamoto ambazo zinawakabili ni upungufu wa madarasa unaotokana na ongezeo la uandikishaji wanafunzi kila mwaka na wale wanaohamia kutoka maeneo mengine huku akieleza jambo linguine ni bima za afya kwa wanafunzi wenye mahitaji maalumu.

“Tunamshukuru Mhe Mbunge Wetu kwa kutupelekea wadau wenye kuwasaidia madaftar mchango huo umewapa faraja kubwa na matumaini motisha mpya kwa watoto wao kuonyesha dhamira ya kweli kujenga jamii inayojali na kuthamini kila mtoto bila ubaguzi”Alisema

Hata hiyo alitoa shukrani zake kwa Rais Dkt Samia Suluhu katika kukuza na kutoa kipaumbeme kwenye elimu jumuishi na kupitia uongozi wake fursa za elimu zinaendelelea kuimarishwa na kuwafikia hata wenye mahitaji maalumu.

Naye kwa upande wake Mkurugenzi wa Taasisi ya Watoto Foundation Ally Yakub Pingizi alisema taasisi hiyo imezindua mpango unaoitwa Daftari la Mama Soma na Samia ikiwa ni kipaumbele kuhakikisha wanafunzi hawana sababu ya kutoroka shule ikiwa hana vitendea kazi cha shule.

Alisema kwamba wao wamekuja na mpango wa daftari la mama soma na samia ikiwa ni kuunga mkono juhudi zinazofanywa na Rais Dkt Samia Suluhu katika kuboresha sekta ta elimu na amefanya maboresho makubwa kwa kujenga miundombinu ya elimu, nyumba za walimu,mabweni na vyoo.


Alisema kwamba taasisi hiyo kupitia mpango huo wameona wao waunge mkono kwa kutoa vifaa hivyo vitendea kazi na kuwatia moyo watoto wa kike waweze kusoma kwa hari na moyo ili kuepuka kujiingiza kwenye vishawishi na watoto wa kike na hivyo kusoma kwa bidii pamoja na kupunguza utoro shuleni hatua itakayochochea ufaulu.
 






WAZIRI MKUU AZINDUA UJENZI WA CHUO KIKUU MZUMBE TANGA

WAZIRI MKUU AZINDUA UJENZI WA CHUO KIKUU MZUMBE TANGA

February 15, 2026 Add Comment


Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba, leo tarehe 15 Februari, 2026 akiweka jiwe la msingi la ujenzi wa miundombinu ya Chuo Kikuu Mzumbe kampasi ya Tanga ambayo hadi kukamilika kwake utagharimu zaidi ya shilingi bilioni 12. Pembeni yake ni Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Wanu Hafidh Ameir. PICHA NA OFISI YA WAZIRI MKUU

Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba, akipanda mti katika eneo la Chuo Kikuu Mzumbe kampasi ya Tanga mara baada ya kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa Chuo hicho leo tarehe 15 Februari, 2026. PICHA NA OFISI YA WAZIRI MKUU



Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba, akizungumza na wananchi wa Tanga mjini mara baada ya kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa miundombinu ya Chuo Kikuu Mzumbe kampasi ya Tanga ambayo hadi kukamilika kwake utagharimu zaidi ya shilingi bilioni 12 leo tarehe 15 Februari, 2026. PICHA NA OFISI YA WAZIRI MKUU

Muonekano wa Chuo Kikuu Mzumbe kampasi ya Tanga ambayo hadi kukamilika kwake utagharimu zaidi ya shilingi bilioni 12 ambao umewekwa jiwe la msingi na Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba leo tarehe 15 Februari, 2026.
WAZIRI MKUU AONGOZA KIKAO KAZI NA WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA NA TIMU YA WATAALAM

WAZIRI MKUU AONGOZA KIKAO KAZI NA WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA NA TIMU YA WATAALAM

January 15, 2026 Add Comment



Waziri Mkuu, Dkt Mwigulu Nchemba akizungumza katika kikao cha kazi na Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Adolf Mkenda (kushoto) na Timu ya Wataalam kwenye ukumbi wa Ofisi ya Waziri Mkuu, Mlimwa jijini Dodoma, Januari 15, 2026. Kulia ni Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Wanu Hafidh Ameir. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

Waziri Mkuu, Dkt Mwigulu Nchemba akizungumza katika kikao cha kazi na Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Adolf Mkenda na Timu ya Wataalam kwenye ukumbi wa Ofisi ya Waziri Mkuu, Mlimwa jijini Dodoma, Januari 15, 2026. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu).

Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba akiteta na Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Wanu Hafidh Ameir katika kikao cha kazi na Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Adolf Mkenda na Timu ya Wataalam kwenye ukumbi wa Ofisi ya Waziri Mkuu, Mlimwa jijini Dodoma, Januari 15, 2026. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu).

Waziri Mkuu, Dkt.Mwigulu Nchemba akizungumza na Waziri wa Elimu , Sayansi na Teknolojia, Profesa Adolf Mkenda (wa pili kulia), Naibu Waziri wa Elimu , Sayansi na Teknolojia, Wanu Hafidh Ameir (kulia ) na Katibu Mkuu Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia, Profesa Carolyne Nombo katika kikao cha kazi na Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia na Timu ya Wataalam kwenye ukumbi wa Ofisi ya Waziri Mkuu, Mlimwa jijini Dodoma, Januari 15, 2026. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu).

Baadhi ya washiriki wa kikao cha kazi cha Waziri Mkuu na Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia na Timu ya Wataalam wakimsikiliza Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba alipozungumza kwenye ukumbi wa Ofisi ya Waziri Mkuu, Mlimwa jijini Dodoma, Januari 15, 2026. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

RAIS SAMIA: MAGEUZI YA ELIMU NA SAYANSI KUJENGA UCHUMI ENDELEVU

January 09, 2026 Add Comment


NA EMMANUEL MBATILO, ZANZIBAR

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesema Serikali imedhamiria kufanya mageuzi makubwa katika sekta za elimu, sayansi, utafiti na ubunifu ili kujenga uchumi imara, shindani na endelevu.

Mhe. Rais ameyasema hayo Januari 8, 2026, Buyu visiwani Zanzibarbaada ya kuzindua Jengo la Taaluma na Utawala la Taasisi ya Sayansi za Bahari Zanzibar (UDSM–IMS), akisisitiza kuwa taasisi hiyo ni mdau muhimu wa Serikali katika kukuza uchumi shirikishi, hususan uchumi wa buluu.

Amesema uwepo wa taasisi hiyo ya kimkakati utaimarisha uvuvi endelevu, utalii wa baharini pamoja na ulinzi na matumizi bora ya rasilimali za bahari.

Mhe. Samia ameipongeza Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kwa kusimamia kwa ufanisi Mradi wa HEET, ambao umeleta matokeo chanya katika miundombinu na ubora wa elimu ya juu, huku akiwahimiza vijana kutumia fursa hiyo kusoma na kupata elimu pamoja na ujuzi unaohitajika katika soko la ajira.

MAHAFALI YA 6 YA LAVENDER DAY CARE CENTER YAFANA KITUNDA MASAI

December 24, 2025 Add Comment

 


Na. Mwandishi Wetu, Dar

Mahafali ya sita (6) kwa Watoto wa darasa la Awali ya Kituo cha Lavender Day Care Center kilichopo Kitunda Masai, yameweza kukonga nyoyo Wazazi na viongozi waliofika kushuhudia tukio hilo la kipekee katika kuhitimisha Wanafunzi hao.




Katika mahafali hayo yaliyofanyika hivi karibuni Disemba 2025, Wahitimu hao wa darasa la awali wameweza kuonesha uwezo wao mkubwa wa yale waliofundishwa darasani kama masomo na michezo mbali mbali.




Awali mgeni rasmi katika mahafali hayo, Mdau wa Elimu Bi. Elly Kitaly ambaye ni Mkurugenzi wa taasisi ya Chadron's Hope Foundation amepongeza uongozi wa shule, Walimu pamoja kwa namna ya kipekee katika kumsaidia Mtoto kitaaluma sambamba na wazazi kwa kuichagua Lavender Day Care tawi la Kitunda Masai.




Amesema uwezo wa watoto hao ni mkubwa hivyo wanatakiwa kuendelea kusimamiwa katika malezi sahihi ya kielimu na kuendelea kujengwa katika mambo mema katika hatua ya Elimu ya Msingi.

Bi.Elly Kitaly amesema kuwa, Elimu ni muhimu lakini pia vitu vingine vya Msingi kabisa vinapaswa kufundishwa Watoto ilikuwajenga zaidi.

"Nimeona kuna watu wana elimu kubwa lakini hawafanyi mambo makubwa.Elimu ni pamoja na mambo ya msingi ni kwa kujifunza Hutu, kujifunza kuwa mkweli na kujifunza kusimama kwenye haki." Amesema Bi. Elly Kitaly.

Aidha, katika risala ya Kituo hicho, juu ya kuongeza majengo mengine, Bi. Elly Kitaly amesema kuwa anaamini Wazazi wanaweza kuchangia chochote ilikufanikisha ujenzi huo kwani itasaidia maendeleo ya watoto wengi.

"Nimesikia tunataka kujenga majengo mengine, moja ya changamoto ya kuendeshea shughuli kama hizi za taasisi za shule ni suala la kifedha, na nafahamu pesa ni changamoto hivyo tuungane kusaidia kituo cha Levender ili kiendelee kusaidia watoto wetu, Mimi na wewe tuungane tukatoa kilichopo mifuko ya cement, au matofali au hata kuchangia elfu moja (Tsh 1,000) inaweza kubadilisha mazingira ya Lavender.

Ameongeza "Utakuja hapa utakuta mazingira safi yame boreshwa, madarasa yame ongezeka, sehemu ya michezo ya watoto imeboreshwa hata utakuta na eneo la kuogelea (swimming pool) ya watoto.

Aidha amesema kuwa, 

Elimu ni muhimu, lakini pia lazima tujifunze mengine kama fani ya muziki, kuogelea na mengine katika vipaji ili kukabiliana na soko la ajira.

"Nimeona watoto wamefanya mambo makubwa hapa, niwapongeze Uongozi wa Lavender, na Walimu kwa kuwalea vyema watoto hawa, na wakawe mfano huko katika ngazi inayofuata.

Nae Mkurugenzi wa kituo cha Lavender Day Care, Bi.Vida Andrew Ngowi amewashukuru Wazazi na Walezi kwa kuendelea kuwaunga mkono na kwa sasa wanaendelea kuongeza majengo mengine ya Kituo hicho cha eneo la Kitunda Masai.

Aidha, kupitia risala ya msimamizi wa kituo hicho, amesema Lavender Day Care Center kilichopo Kitunda Masai ilianzishwa mwaka 2019 kwa lengo la kutoa huduma bora ya malezi, makuzi na maendeleo ya awali ya watoto. 

"Kituo kilianza na watoto wachache mwaka 2019 na hadi kufikia sasa tuna watoto wengi, tuna washukuru Wazazi na Walezi kutukimbilia Lavender kwa hapa eneo la Kitunda Masai, kwani kituo chetu "Mtoto ndiye kiini cha ujifunzaji ", lakini pia falsafa yetu kuu inasema"Tunajifunza kupitia michezo".

Kituo cha Lavender pia kina tawi katika eneo la Bunju A ambacho nacho kinafanya vizuri sana ikiwemo watoto wanajifunza kifaransa, kuogolea na muziki kama chaguo kwa wale wanaopenda.