Showing posts with label elimu. Show all posts
Showing posts with label elimu. Show all posts

SHULE ZINAZOTUMIA KUNI KAMA NISHATI YA DHARURA ZAELEKEZWA KUTUMIA NISHATI SAFI YA KUPIKIA

October 09, 2025 Add Comment


📌 *Mkurugenzi Nishati Safi ya Kupikia apongeza jitihada za Shule zilizohamia kwenye nishati salama na rafiki kwa afya na Mazingira.*


📌 *Atoa wito kwa Wadau kuwekeza katika uzalishaji wa kuni/mkaa mbadala kutokana na kuhitajika kwake*

Mkurugenzi wa Nishati safi  ya kupikia, Wizara ya Nishati, Bw. Nolasco Mlay, ametoa wito kwa shule zote nchini  kuhakikisha zinaachana na matumizi ya kuni na badala yake kuhamia kwenye matumizi ya nishati safi ya kupikia, ikiwemo gesi, majiko banifu, na mkaa mbadala.

Akizungumza wakati wa kuhitimisha  ziara yake ya ukaguzi wa miradi ya nishati safi ya kupikia inayotekelezwa chini ya mpango wa CookFund katika Mkoa wa Mwanza, Mlay amesema kuwa shule nyingi bado zinategemea kuni kama nishati ya dharura, hali inayochangia uharibifu wa mazingira na madhara kwa afya ya watumiaji.

“Katika ziara hii nimebaini Shule nyingi zinatumia kuni kama nishati ya dharura hivyo nitoe wito kwa uongozi wa shule mkishirikiana na Afisa Elimu kuanza kutumia mkaa mbadala ambao ni rafiki kwa mazingira na unachangia katika kupunguza uzalishaji wa hewa ukaa." Amesema Mlay

Aidha, Bw. Mlay amepongeza baadhi ya shule ambazo tayari zimeanza kutumia nishati safi, ambazo hazifadhiliwi na mradi wa Cookfund ikiwemo shule ya Sekondari ya wavulana Musabe pamoja na Shule ya Msingi Buhongwa A akizitaja kuwa mfano bora kwa taasisi nyingine nchini.

Amesema matumizi ya nishati safi huchangia kwa kiasi kikubwa kulinda afya ya wanafunzi na walimu dhidi ya magonjwa ya mfumo wa upumuaji, yanayosababishwa na moshi kutoka kwa kuni na mkaa wa kawaida.

“Tunapongeza juhudi za shule zinazohamia kwenye nishati safi ya kupikia kwani hii hatua ni kubwa katika kulinda afya, mazingira na hata kuongeza ufanisi wa shughuli za kila siku shuleni hivyo nitoe wito kwa shule zote ambazo bado hazijaanza kutumia nishati safi ya kupikia, kuanza kutumia nishati safi kwani ni nafuu na zinaokoa muda." Ameongeza Bw. Mlay

vilevile, Mlay amehimiza Serikali za Mitaa, Wakuu wa Shule na wadau wa elimu kushirikiana kwa karibu katika kuhakikisha taasisi za elimu zinapata vifaa vya kisasa vya kupikia kwa kutumia nishati safi.

 Amesisitiza kuwa mradi wa CookFund na mipango mingine ya kitaifa iko tayari kusaidia shule zinazotaka kuhamia kwenye mfumo huo wa kisasa wa kupikia ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa Mkakati  wa Taifa wa Nishati Safi ya Kupikia 2024 - 2034 ambao unalenga kuhakikisha kuwa ifikapo mwaka 2034, asilimia 80 ya wananchi wanatumia nishati safi ya kupikia.

Mlay  ametoa wito kwa wawekezaji mbalimbali kujitokeza kuwekeza katika uzalishaji wa kuni na mkaa mbadala ili kufanikisha azma ya nchi kuhamia kwenye nishati safi na kulinda mazingira.


“Ni muhimu kuwekeza kwa dhati katika uzalishaji wa kuni na mkaa mbadala, hasa kwa ajili ya taasisi kwani kukosekana kwa wazalishaji hawa kunaweza kusababisha athari kubwa kiuchumi, kijamii na kimazingira hapo baadaye hivyo tunahimiza wadau wote kujitokeza, kushirikiana, na kuwekeza katika mabadiliko haya yenye tija kwa taifa na vizazi vijavyo”. Amesisitiza Bw. Mlay


Naye Afisa Elimu Taaluma Halmashauri ya Jiji la Mwanza Bw. Rodrick Kazinduki ameeleza kuwa  kupitia mkakati wa Nishati Safi ya kupikia, Tanzania itaondokana na changamoto za uharibifu wa mazingira na afya zinazotokana na matumizi ya nishati zisizo safi huku akieleza kuwa  kupitia ushirikiano wa Serikali, Mashirika ya Kimataifa na jamii kwa ujumla, kuna matumaini kuwa shule nyingi zaidi zitaweza kuhama kutoka kwenye kuni na mkaa wa kawaida, na kuingia katika zama mpya za nishati safi, salama na endelevu.

WALIMU NI NGUZO YA MAENDELEO -WAZIRI MKUU MAJALIWA

October 04, 2025 Add Comment











📌 Asema Walimu ni fahari ya nchi na chimbuko la uvumbuzi na ubunifu


📌 Dkt. Biteko asema ualimu ndio taaluma inayomtengeneza mtu awe bora kuliko hata ualimu wenyewe

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amesema kuwa walimu ni nguzo kuu ya maendeleo ya taifa lolote hapa duniani kwani ndio wanaotoa rasilimali watu yenye elimu ambayo ni muhimu zaidi kwa Taifa.

Amesema kuwa mafanikio ya kielimu, kijamii na kiuchumi yanatokana na juhudi za walimu kwani walimu ni fahari ya familia, jamii na nchi na kupitia mikono yao vijana wa kitanzania wanajengewa maarifa, stadi na maadili ya uzalendo.

Amesema hayo Oktoba 03, 2025 wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Mwalimu Duniani ambayo kiwilaya imeadhimishwa Bukombe mkoani Geita katika uwanja wa Shule ya Sekondari ya Ushirombo.

"Kila hatua ya ustawi wa kijamii na kiuchumi inaanzia darasani kupitia juhudi na maarifa ya walimu. bila walimu, hakuna taaluma, hakuna viongozi wa kesho na hakuna Taifa linaloweza kusimama imara, walimu ndio chimbuko la uvumbuzi na ubunifu wa kizazi kipya.".

Amesema kuwa kwa kutambua umuhimu wa kada ya ualimu hapa nchini, Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imeendelea kuboresha mazingira ya kada hiyo ikiwemo kwa kupandisha madaraja na kuimarisha mafunzo kwa walimu.

Ameongeza kuwa ili kukabiliana na upungufu wa walimu nchini Serikali ya Awamu ya Sita imeendelea kuthamini na kuwekeza katika kada ya ualimu kwa kuajiri walimu wapya kila mwaka. 

Kadhalika, Mheshimiwa Majaliwa ameziagiza Ofisi ya Rais - TAMISEMI na Ofisi ya Rais - UTUMISHI kufanya msawazo wa walimu ndani ya mikoa husika kwa kuhakikisha kila shule inapata walimu ili watoto wa Kitanzania wapate elimu bora.

"Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kwa kushirikiana na Vyuo vya Ualimu na Taasisi ya Elimu Tanzania (TET) imarisheni mafunzo ya kitaaluma na endelevu kwa walimu ili waendane na mabadiliko ya teknolojia na mahitaji ya dunia ya leo". Amesema Mhe. Majaliwa.

Naye, Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dkt. Doto Biteko amesema kuwa taaluma ya ualimu ndio taaluma pakee inayomtengeneza mtu awe bora kuliko hata ualimu wenyewe na wakati wowote hujinyima muda wake na nguvu zake zote kumtengeneza mtu kuwa mume au mke bora au hata mzazi bora.

"Taaluma ya ualimu humfanya mtu kuwa raia mwema kwenye nchi na zaidi sana humfanya kuwa mtumishi, mfanyakazi na mzalishaji mali bora, wakati wote wa maisha yake, hii ni taaluma ambayo tunaamini ni ya uumbaji wa pili baada ya mwanadamu kuzaliwa na wazazi wake, kazi ya pili huendelea hapa duniani na muumbaji huwa ni mwalimu," amesema Dkt. Biteko.

Ameongeza kuwa Mwalimu ndiye anayetoa mwelekeo wa maisha ya kila mtu na ukiona jamii yoyote yenye ustaarabu na kustaarabika huhitaji kupiga ramli kujua nani chanzo chake bali mwalimu ndio sababu yake.

Kwa upande wake Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Caroline Nombo amesema kuwa Serikali ya Awamu ya Sita imeendelea kufanya shughuli mbalimbali zinazowawezesha walimu kufanya kazi zao kwa ufanisi na kuleta matokeo chanya ikiwemo ujenzi wa miundombinu shuleni na lengo ni kukuza ujifunzaji na ufundishaji.

Ameongeza  “ Serikali inathamini jitihada zinazofanywa na walimu kwani wamekuwa kiini cha mafanikio. "Kila mmoja wetu amepita kwenye mikono ya walimu, tunawashukuru walimu wote wanaotoa nguvu na maarifa yao kuwawezesha Watanzania"


Mwisho

WAZIRI MKUU MGENI RASMI MAADHIMISHO YA SIKU YA MWALIMU DUNIANI

WAZIRI MKUU MGENI RASMI MAADHIMISHO YA SIKU YA MWALIMU DUNIANI

October 04, 2025 Add Comment






Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dkt. Doto Biteko alipowasili kwenye uwanja wa Shule ya Sekondari Ushirombo wilayani Bukombe ambapo alikuwa mgeni rasmi katika Maadhimisho ya Siku ya Mwalimu Duniani, Oktoba 3, 2025. Kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Geita, Martin Shigela. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)



Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dkt. Doto Biteko alipowasili kwenye uwanja wa Shule ya Sekondari Ushirombo wilayani Bukombe ambapo alikuwa mgeni rasmi katika Maadhimisho ya Siku ya Mwalimu Duniani, Oktoba 3, 2025. Kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Geita, Martin Shigela. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dkt. Doto Biteko wakiingia kwenye uwanja wa Shule ya Sekondari Ushirombo wilayani Bukombe ambapo Waziri Mkuu alikuwa mgeni rasmi katika Maadhimisho ya Siku ya Mwalimu Duniani, Oktoba 3, 2025. Kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Geita, Marten Shigella. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)



Walimu wakimsikiliza Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa alipozungumza katika Maadhimisho ya Siku ya Mwalimu Duniani yaliyofanyika kwenye uwanja wa Shule ya Sekondari Ushirombo wilayani Bukombe, Oktoba 3, 2025. Kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Geita, Marten Shigella. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza katika Maadhimisho ya Siku ya Mwalimu Duniani kwenye uwanja wa Shule ya Sekondari Ushirombo wilayani Bukombe, Oktoba 3, 2025. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)



Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiteta na Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dkt. Doto Biteko katika Maadhimisho ya Siku ya Mwalimu Duniani yaliyofanyika kwenye uwanja wa Shule ya Sekondari Ushirombo wilayni Bukombe, Oktoba 3, 2025. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)



Washiriki wa Maadhimisho ya Siku ya Mwalimu Duniani wakiwasha tochi za Simu zao kuashiria kuwa elimu ni mwanga katika Maadhimisho ya Siku ya Mwalimu Duniani kwenye uwanja wa Shule ya Sekondari Ushirombo wilayani Bukombe, Oktoba 3, 2025. Mgeni rasmi alikuwa Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)



Waziri Mkuu Kassim Majaliwa na Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dkt. Doto Biteko wakimsikiliza Mkurugenzi wa Makampuni ya Jembe, Sebastian Ndege walipotembelea mabanda ya maonesho ya makampuni hayo katika Maadhimisho ya Siku ya Mwalimu Duniani kwenye uwanja wa Shule ya Sekondari Ushirombo wilayani Bukombe, Oktoba 3, 2025. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

DC NYAMWESE ASISITIZA UJENZI WA BWENI  UPEWE KIPAUMBELE MRADI WA VETA HANDENI

DC NYAMWESE ASISITIZA UJENZI WA BWENI UPEWE KIPAUMBELE MRADI WA VETA HANDENI

September 26, 2025 Add Comment

 

Na Mwandishi Wetu, Handeni

MKUU wa Wilaya ya Handeni, Mhe. Salum Nyamwese, amekagua ujenzi wa Chuo cha Ufundi Stadi (VETA) wilayani humo na kuagiza maboresho mbalimbali kwenye utekelezaji wa mradi huo unaotarajiwa kugharimu Sh.Bilioni 1.6.

Miongoni mwa maboresho ni kuangalia namna ya kuhakikisha bweni linajumuishwa katika awamu ya kwanza ya ujenzi, ili wanafunzi waweze kuanza kupata mafunzo mara tu awamu hiyo itakapokamilika.

Akizungumza baada ya kukagua mradi huo, Nyamwese amewataka mshauri elekezi na msimamizi wa mradi kushirikiana kuhakikisha bweni linaingizwa katika mpango huo kutoka na awamu ya kwanza inayohusisha majengo tisa kutokuwa na bweni.

Vilevile, ameelekeza Jeshi la Zimamoto lishirikishwe mapema kutoa ushauri kuhusu vifaa vya usalama vinavyohitajika kabla ya mradi kukamilika.

Hata hivyo, amewapongeza wasimamizi wa mradi kwa kazi nzuri iliyofanyika, akisisitiza mapungufu yaliyojitokeza yashughulikiwe mara moja.

SERIKALI YAPANIA KUANDAA WALIMU USHIRIKIANO WA ATE NA WIZARA WAZAA MATUNDA KWA WATAFUTA AJIRA

SERIKALI YAPANIA KUANDAA WALIMU USHIRIKIANO WA ATE NA WIZARA WAZAA MATUNDA KWA WATAFUTA AJIRA

September 25, 2025 Add Comment

 

KATIKA  kuhakikisha mafunzo ya darasani yanaendana na mahitaji halisi ya soko la ajira, Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Carolyne Nombo, amekutana na Afisa Mtendaji Mkuu wa Chama cha Waajiri Tanzania (ATE), Bi. Suzzane Ndomba, kwa mazungumzo ya namna ya kuwawezesha vijana wahitimu kupata mafunzo ya vitendo sehemu za kazi.

Mkutano huo umefanyika  katika ofisi za ATE jijini Dar es Salaam, ambapo Prof. Nombo alisema Serikali imefanya mapitio ya Sera ya Elimu na kuboresha mitaala ya ngazi zote ili vijana wapate ujuzi unaowawezesha kujiajiri au kuajiriwa.

Aidha, Prof. Nombo alisisitiza kuwa Serikali inaendelea kutoa mafunzo kwa walimu walioko kazini ili kuboresha mbinu za ufundishaji, akieleza kuwa ufundishaji bora ndio msingi wa kuwajengea wanafunzi ujuzi wa maisha na ajira.

“Lengo la ziara hii ni kujadiliana na ATE kuhusu njia bora za kuwashirikisha waajiri katika kusaidia vijana waliopo vyuoni au waliomaliza masomo kupata mafunzo ya vitendo sehemu za kazi,” alisema Prof. Nombo.

Kwa upande wake, Afisa Mtendaji Mkuu wa Chama cha Waajiri Tanzania (ATE), Bi. Suzzane Ndomba, alisema ATE imekuwa ikisaidia wanafunzi kupata mafunzo kwa vitendo kupitia wanachama wake, wakiwemo viwanda na makampuni. Alitolea mfano wa Mradi wa Kukuza Ujuzi wa Vijana unaotekelezwa na ATE, uliowawezesha zaidi ya vijana 1,000 waliomaliza kidato cha nne kupata mafunzo ya miezi sita katika vyuo vya ufundi kabla ya kupelekwa makampuni kwa mafunzo ya vitendo, ambapo baadhi yao walipata ajira.

Aidha, alitoa wito kwa Watanzania kutumia Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) kujifunza ujuzi kwa gharama nafuu bila kujali kiwango cha elimu rasmi walichonacho.

Mazungumzo hayo yameonesha dhamira ya pamoja ya Serikali na sekta binafsi katika kuimarisha ujuzi wa vijana na kuandaa nguvu kazi yenye mchango katika maendeleo ya taifa.