HABARI MPYA
HABARI
SIASA
ELIMU
Recent Posts
REA KUSAMBAZA MAJIKO BANIFU 10650 MKOANI PWANI
Nishati*📌RC Kunenge aipongeza REA kwa kuhamasisha matumizi nishati safi*
*📌Mifumo ya umeme jua kuchochea upatikanaji wa umeme
kwa asilimia 100 ifikapo mwaka 2030*
📍Pwani
Wakala wa Nishati Vijijini (REA), imetoa jumla ya Majiko Banifu 10,650 Mkoani Pwani ikiwa ni mwendelezo wa jitihada za Serikali za kuhakikisha kila mwananchi anatumia Nishati Safi ya kupikia nchini.
Akizungumza leo tarehe 18 Agosti, 2025 ofisini kwa Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Meneja wa Teknolojia za Nishati kutoka REA, Mha. Michael Kyessi amesema mradi huo unalenga kuuza na kusambaza Majiko Banifu kwa bei ya ruzuku ambapo mwananchi atachangia asilimia ishirini (20%) za gharama ya jiko huku asilimia themanini (80%) zikitolewa na Serikali.
“Mwananchi wa kawaida atachangia 20% tu za gharama za jiko ambapo bei ya jiko ni 56,000 na mwananchi atagharamika kuchangia shilingi 11,200 tu baada ya ruzuku kutolewa na Serikali” amesema Mha. Kyessi.
Sambamba na hilo Mha. Kyessi amebainisha thamani ya mradi huo kwa ujumla ni milioni 596,400,00 ambapo Serikali kupitia REA imetoa ruzuku ya shilingi milioni 477,120,00 ambayo ni sawa na asilimia themanini.
Katika hatua nyingine, REA inatekeleza lengo la Serikali ya Tanzania kufikia mpango wa Umoja wa Mataifa wa "Nishati Endelevu kwa Wote" (SE4ALL) wa upatikanaji wa nishati
kwa asilimia 100 ifikapo mwaka 2030. Mradi huu utatumia nishati Jadidifu ili kuweza kufikia wananchi wa maeneo ya visiwani na utekelezaji wake ni kwa kupitia mradi wa Ufadhili unaotegemea Matokeo (RBF) kupitia Benki ya Dunia.
"Serikali ya Tanzania kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umetenga fedha kwa ajili ya utekelezaji wa mradi wa kufunga mifumo ya umeme jua maeneo ya visiwani kwa
kutoa ruzuku kwa bei ya mwisho ya mtumiaji wa mfumo wa Umeme Jua ili kufanikisha upatikanaji wa umeme katika maeneo hayo yaliyo mbali na Gridi ya Taifa, " Amesema Mha. Kyessi.
Mha. Kyessi amesema katika Mkoa wa Pwani mradi wa umeme jua unategemea kuhudumia visiwa 13 na jumla ya watoa huduma wawili (2) wanategemea kuhudumia visiwa hivyo kupeleka jumla ya mifumo 2,243 ndani ya kipindi cha miaka miwili (2) na gharama za mradi kwa mkoa wa Pwani ni shilingi bilioni 1.372 ambapo ruzuku ni shilingi milioni 935.7 sawa na asilimia 69 ya gharama zote ya mradi na shilingi milioni 436.6 ni fedha toka kwa wanufaika.
Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhe. Abubakar Kunenge ameipongeza REA kwa mkakati wa kuendelea kuongeza matumizi ya Nishati safi na kuondoa kero kwa wananchi kuhusu matumizi ya kuni na mkaa ambayo ni hatarishi kwa afya zao.
Mradi huo utatekelezwa kwa muda wa miezi 15 katika mkoa wa Pwani na jumla ya Majiko Banifu 10,650 yatasambazwa kwa wananchi.
HAMADI –NITAFANYA KAZI KWA UADILIFU KUHAKIKISHA WANANCHI WANAPATA MAENDELEO
siasaKADA ya Chama cha Mapinduzi (CCM) Hamadi Shamisi Hamadi leo amechukua fomu ya kuwania Udiwani Kata ya Msambweni Jijini Tanga huku akihaidi kufanya kazi kwa uadilifu.
Hamadi aliyasema hayo leo mara baada ya kuchukua fomu katika Ofisi ya Mtendaji Kata ya Msambweni huku akiwa amesindikizwa na wanachama wa chama hicho wakiwemo wananchi.
Alisema kwamba lengo lake ni kuhakikisha anawatumikia wananchi wa kata hiyo na kuwa kiungo cha maendeleo ya wananchi na hivyo kuchochea ukuaji wa maendeleo.
“Nawaambia tutafanya kazi kwa dhati na kutanguliza uaminifu na uadilifu kuhakikisha wananchi wanapata maendeleo na shahidi ni Baba yangu mzazi ambaye ananisindikiza hapa”Alisema
Awali akizungumza Mwenyekiti wa CCM kata ya Msambweni alisema kwamba hicho ni kishindo cha kwanza ila Agosti 28 wanaanza kampeni zao na wanafungua kwenye tawi la Msambweni B eneo la Komesho watakuwa na Mbunge wa Tanga Jijini kampeni za wilaya zitafunguliwa hapo.
Alisema Agosti 29 utakuwa uzinduzi wa kampeni wa Diwani wa Kata ya Msambweni na zitazinduliwa Mtaa wa Madina eneo la Mabanda ya Papa huku akiwataka wananchi kujitokeza kwa wingi katika uzinduzi huo.
TARURA MUSOMA WAPONGEZWA UJENZI WA MIRADI KULINGANA NA THAMANI YA FEDHA
habari
Na Mwandishi Wetu, Mara.
Kiongozi wa Mbio za Mwenge Kitaifa Ndugu Ismail Ali Ussi amewapongeza wafanyakazi wa TARURA wilaya ya Musoma kwa kufanya kazi kwa weledi na kuhakikisha wanajenga miradi ya miundombinu ya barabara kulingana na thamani halisi ya fedha.
Ndugu Ussi ameyasema hayo wakati akiweka jiwe la msingi kwenye ujenzi wa barabara ya Nyabisarye Mahakama kuu Kanda ya Musoma yenye urefu wa Mita 700 kwa kiwango cha lami .
Ussi amesema kuwa Serikali imekuwa ikitumia fedha nyingi katika ujenzi wa miundombinu ya barabara kwa lengo la kuwarahisishia wananchi huduma katika maeneno yao ili waweze kufanya shughuli zao za kiuchumi na kujiingizia kipato.
Kwa upande wake Kaimu Meneja Wilaya ya Musoma Mhandisi Mohamed Etanga amesema jumla ya shilingi Milioni 600.97 zimetengwa kwaajili ya ujenzi wa barabara ya Nyabisarye- Mahakama Kuu yenye urefu wa Mita 700 kwa kiwango cha lami .
Amebainisha kuwa ujenzi wa barabara hiyo ulianza Oktoba mwaka jana na unatarajiwa kukamilika ifikapo Septemba, 2025.
Mhandisi Etanga ameongeza kusema kuwa barabara hiyo endapo itakamilika itakuwa kiunganishi cha Kata ya Bweri na Kata ya Rwamlimi na kuwa kiungo kikubwa kwa wananchi katika kupata mahitaji ya kijamii kwa wepesi.





WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA AKISAFIRI KWA TRENI YA UMEME YA KIWANGO CHA KIMATAIFA (SGR) KUTOKA DODOMA KUELEKEA DAR ES SALAAM LEO AGOSTI
habariKIKWETE : SERIKALI KUSAINI MUONGOZO WA KIMA CHA CHINI CHA MSHAHARA KWA SEKTA BINAFSI
SERIKALI imesema hivi karibuni inatarajia kusaini kuwa Sheria miongozo Wa kima cha chini Cha mshahara kwa TaasisiI binafsi zinazofanywa kazi nchini.
Imesema katika miongozo huo inatarajia kuainisha viwango vipya vya mshahara ambapo wafanyakazi Wa sekta binafsi watakuwa wanalipwa.
Waziri Wa Nchi,Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi,Ajira Vijana Na Wenye Ulemavu ,Ridhiwan Kikwete amesema hayo jijini Arusha katika uzinduzi wa jengo la biashara Shirikisho La Vyama Vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA) lililoko mkabala na soko kuu.
Kuhusu miongozo huo amesema mazungumzo yameshafanyika baina ya wadau ambao ni Taasisi binafsi na wasimamizi wa sera lakini pia uongozi wa timu Ya Wizara iliyopewa jukumu la kusimamia marekebisho hayo.
Amesema kikao kilichobakia ni Cha mashauri ambapo watashauriana na wenzao juu ya viwango vilivyowekwa na baada ya hapo mapema mwezi ujao huenda wakasaini marekebisho hayo.
“Hivyo nawaambia Wafanyakazi kuwa Rais Dkt Samia anathamini sana maslahi yenu,” amesema Ridhiwan na kuongeza kuwa serikali Itaendelea kuboresha sheria za Wafanyakazi Ili ziendane na mahitaji ya wafanyakazi.
Amesema Serikali itaendelea kushirikiana na Wafanyakazi bega kwa bega katika:Kutekeleza mikakati ya kuongeza ajira;Kulinda haki za wafanyakazi;Kuimarisha mifumo ya utatuzi wa migogoro kwa njia ya mazungumzo.
DKT. TULIA AKOSHWA NA CRDB BANK MARATHON IKIKUSANYA BILIONI 2 KUSAIDIA AFYA NA UWEZESHAJI JAMII
michezo


Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Tulia Ackson Mwansasu, aliongoza maelfu ya washiriki kwenye msimu huu wa sita wa CRDB Bank Marathon.

“Ushiriki wetu katika CRDB Bank Marathon ni tendo la huruma linaloleta faraja kwa watoto na wakinamama na familia zao. Ni ushahidi kwamba tukishirikiana, tunaweza kubadilisha maisha,” alisema.

Alisema, “CRDB Bank Marathon si tu imekuwa ikikuza afya na mshikamano wa kijamii, bali pia imekuwa ikifungua milango ya ajira na fursa za kiuchumi kwa vijana wetu. Michezo ni sekta inayoweza kubadili maisha, na ninapongeza sana kitendo cha kuweka zawadi nono kwa washindi. Hizi ni fursa ambazo zinaweza kuwa mtaji wa kuanzisha biashara na kuimarisha maisha ya vijana wetu. Serikali itaendelea kushirikiana na wadau kama CRDB Bank Foundation kuhakikisha michezo inakuwa chachu ya maendeleo ya taifa.”

Nsekela alisema kuwa mbio za mwaka huu zimeweza kuvutia zaidi ya washiriki 16,000, na kufanikisha lengo la kukusanya shilingi bilioni 2 ambapo pamoja na kusaidia maandalizi ya mbio hizo, shilingi milioni 450, zimeelekezwa kusaidia wenye uhitaji katika jamii.
Kati ya hizo shilingi milioni 100 zimekwenda hospitali ya CCBRT kusaidia wakinama wenye ujauzito hatarishi kujifungua salama, shilingi milioni 100 zimekwenda Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) kusaidia upasuaji wa Watoto wenye matatizo ya moyo, na shilingi 250 zitaelekezwa katika uwezeshaji wa vijana.

Mwambapa alisisitiza kuwa mafanikio haya ni matokeo ya mshikamano wa kipekee wa serikali za nchi shiriki, wadhamini na washiriki, akiwashukuru wadau wote waliotoa jitokeza kuchangia ikiwamo kampuni za bima za Sanlam Life na Alliance Life ambao wamekuwa sehemu ya mbio hizi tangu kuanzishwa kwake.

Washindi wa mbio za mwaka huu upande wa Tanzania kwa Kilometa 42 upande wa wanawake ni Joyloyce Kemuma kutoka Kenya, upande wa wanaume mshindi ni Abraham Kiptum kutoka Kenya. Kilometa 21 upande wa wanawake ni Catherine Syokau kutoka Kenya, na upande wa wanaume ni Joseph Panga kutoka Tanzania. Kilometa 10 upande wa wanawake ni Silia Ginoka kutoka Tanzania, na upande wa wanaume ni Boayi Maganga kutoka Tanzania.
Joseph Panga mshindi wa mbio za Kilometa 21 upande wa wanawake ameeleza furaha yake kushiriki katika mbio hizo na kusema kuwa ushindi wake ni sehemu ya kusaida matibabu ya watoto wenye matatizo ya moyo na matibabu ya wakinamama wenye ujauzito hatarishi hospitali ya CCBRT.
“Mimi kama Mtanzania najisikia fahari kubwa kushiriki kusambaza tabasamu kwa watoto na wakinamama. Ni muhimu watu kufahamu kuwa afya bora ni haki ya kila mtoto, na hakuna mama anayestahili kupoteza maisha wakati wa kujifungua. Tunawashukuru CRDB Bank Foundation kwa kutuleta pamoja katika harakati hizi za kuokoa maisha,” amesema.

