SERIKALI imesema hivi karibuni inatarajia kusaini kuwa Sheria miongozo Wa kima cha chini Cha mshahara kwa TaasisiI binafsi zinazofanywa kazi nchini.
Imesema katika miongozo huo inatarajia kuainisha viwango vipya vya mshahara ambapo wafanyakazi Wa sekta binafsi watakuwa wanalipwa.
Waziri Wa Nchi,Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi,Ajira Vijana Na Wenye Ulemavu ,Ridhiwan Kikwete amesema hayo jijini Arusha katika uzinduzi wa jengo la biashara Shirikisho La Vyama Vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA) lililoko mkabala na soko kuu.
Kuhusu miongozo huo amesema mazungumzo yameshafanyika baina ya wadau ambao ni Taasisi binafsi na wasimamizi wa sera lakini pia uongozi wa timu Ya Wizara iliyopewa jukumu la kusimamia marekebisho hayo.
Amesema kikao kilichobakia ni Cha mashauri ambapo watashauriana na wenzao juu ya viwango vilivyowekwa na baada ya hapo mapema mwezi ujao huenda wakasaini marekebisho hayo.
“Hivyo nawaambia Wafanyakazi kuwa Rais Dkt Samia anathamini sana maslahi yenu,” amesema Ridhiwan na kuongeza kuwa serikali Itaendelea kuboresha sheria za Wafanyakazi Ili ziendane na mahitaji ya wafanyakazi.
Amesema Serikali itaendelea kushirikiana na Wafanyakazi bega kwa bega katika:Kutekeleza mikakati ya kuongeza ajira;Kulinda haki za wafanyakazi;Kuimarisha mifumo ya utatuzi wa migogoro kwa njia ya mazungumzo.
EmoticonEmoticon