Showing posts with label Nishati. Show all posts
Showing posts with label Nishati. Show all posts

TANZANIA YATAJA MAFANIKIO YAKE YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA KATIKA JUKWAA LA KIMATAIFA LA IRENA -ABU DHABI

January 11, 2026 Add Comment





ABU DHABI, UAE


Imeelezwa kuwa, Tanzania inaendelea kufanya jitihada mbalimbali ili kuhakikisha wananchi wanaendelea kupata nishati safi, salama na nafuu ya kupikia, kwa kuhakikisha fedha za kuwezesha miradi ya nishati safi ya kupikia zinapatikana kutoka Serikalini, Sekta Binafsi, Wadau na Mashirika ya Kimataifa yanayounga mkono jitihada za matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia duniani.

Akizungumza katika Mkutano wa pembeni wa Baraza la Kimataifa Nishati Jadidifu (IRENA), uliohusu suala la upatikanaji wa fedha kwa ajili ya miradi ya Nishati Safi ya Kupikia, Abu Dhabi katika Falme za Kiarabu, Mhandisi Anita Ringia kutoka Wizara ya Nishati, amesema Tanzania imeendeelea kutenga na kutafuta fedha kwa ajili ya utekelezaji wa Ajenda ya Nishati Safi ya Kupikia na matokeo yake yanaonekana kupitia upatikanaji wa nishati safi ya kupikia.

Amesema.upatikanaji wa Nishati Safi ya Kupikia umeongezeka kutoka asilimia 6.9 mwaka 2021 hadi asilimia 23.2 mwaka 2025, ikiwa ni zaidi ya mara tatu ndani ya kipindi cha miaka minne pekee.

Amesema mafanikio hayo yametokana na uongozi thabiti wa Serikali chini ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, ambaye ameifanya nishati safi ya kupikia kuwa kipaumbele cha kitaifa na nguzo muhimu ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.

Katika hatua nyingine, Ringia amesema Tanzania katika mwaka wa fedha 2025/26 inaendelea na miradi mbalimbali ikiwemo usambazaji wa majiko banifu 200,000 yenye ruzuku, kulipia majiko ya umeme 480 kupitia bili ya umeme kwa kushirikiana na TANESCO katika mradi wa majaribio, na kusambaza mitungi zaidi ya 450,000 ya gesi ya LPG kwa bei ya ruzuku.

Ameongeza kuwa Serikali pia imepiga marufuku matumizi ya kuni na mkaa katika taasisi zinazohudumia zaidi ya watu 100 kwa siku, hatua iliyolenga kuhamasisha matumizi ya nishati safi katika zaidi ya taasisi za umma 31,000 uwekezaji unaohitaji zaidi ya bilioni 1 za kimarekani, sambamba na kuimarisha kampeni za uhamasishaji na kusaidia biashara ndogo na za kati katika sekta hiyo.

Mhandisi Ringia amebainisha kuwa mafanikio hayo yameungwa mkono pia Sekta binafsi nchini kupitia ongezeko la uwekezaji wa taasisi za kifedha za ndani, zikiwemo Benki ya NMB na CRDB, ambazo zimeanza kutoa mikopo kwa riba nafuu kwa wajasiriamali wa nishati safi ya kupikia ili kupanua mitandao ya usambazaji nchi nzima.

Katika Mkutano huo, Mhandisi Ringia ametangaza fursa mbalimbali za uwekezaji katika ujenzi wa miundombinu ya kupokea, kuhifadhi na kusambaza nishati safi ya kupikia, ujenzi wa viwanda vya ndani vya kutengeneza majiko, vifaa, na mitungi na uwepo wa fursa bunifu za kuwezesha wananchi kulipia nishati kupitia mifumo ya kulipia kidogo kidogo (PAYGO), kulipia kwa riba nafuu na kulipia kupitia bili za umeme.

Akizungumza kuhusu suala la mchango wa kimataifa katika kuwezesha fedha za kutekeleza Ajenda ya Nishati Safi ya Kupikia, Mhandisi Anita amesema Tanzania inaunga mkono wito wa kuimarisha ushirikiano kati ya Serikali, sekta binafsi, taasisi za kifedha, na washirika wa maendeleo ili kuziba pengo la ufadhili wa nishati safi ya kupikia, hususan barani Afrika ambako karibu watu bilioni moja bado hawana huduma hiyo.

Wataalam wengine wakiongozwa na Kamishna Msaidizi anayeshughulikia Nishati Jadidifu, Imani Mruma walishiriki vikao vya awali vilivyohusu masuala ya utungaji wa sheria, udhibiti, uandaaji wa mipango na uwekezaji wa miradi ya Nishati Jadidifu.

Katika vikao hivyo Tanzania ilieleza kuhusu juhudi inazochukua katika kuhakikisha Nishati Jadidifu inakuwa na mchango wa kutosha katika gridi ya Taifa ili kuendana na maendeleo endelevu ya matumizi ya nishati jadidifu duniani (SDG 7) .

Katika Nishati Jadidifu Tanzania imeeleza kuwa inazidi kupiga hatua ambapo mchango wake unaoingizwa kwenye gridi ya taifa ni asilimia 68 huku juhudi nyingine zikiendelea.ikiwemo ya ujenzi wa mradi wa umeme Jua wa Kishapu wa MW 150 ambao ifikapo Februari mwaka huu utakuwa umeanza kuzalisha umeme kiasi cha MW 50.

Aidha vyanzo vingine vya Nishati Jadidifu vinavyoendelezwa ni pamoja na vyanzo vya Jotoardhi katika ziwa Ngozi (70MW) Songwe (5MW) kiejombaka (60MW), Natron (60MW) na Luhoi (5MW).

Akifungua Mkutano wa IRENA katika siku yake ya kwanza, Naibu Mkurugenzi Mkuu wa IRENA, Gaun Singh amehimiza kila nchi wanachama kuzidi kuwekeza kwenye miradi ya nishati jadidifu ambapo lengo la kidunia ni kuwa na umeme wa GW 11,000 zinazotokana na nishati jadidifu ifikapo 2030.


Mkutano wa IRENA 2026 unaongozwa na kaulimbiu ya “Matumizi ya Nishati Jadidifu kwa manufaa ya pamoja kwa kila binadamu” yaani “Powering Humanity: Renewable Energy for Shared Prosperity”.

     

HIMIZENI WANANCHI, VIJANA NA WANAFUNZI KUTEMBELEA MRADI WA BOMBA LA MAFUTA- WAZIRI NANKABIRWA

January 07, 2026 Add Comment




📌*Lengo ni makundi hayo kuwa sehemu ya miradi na kupata ufahamu*


📌*Aipongeza Tanzania kwa kasi ya utekelezaji wa mradi wa bomba la EACOP*


📌 *Ahitimisha ziara yake mkoani Tanga kwa kutembelea kambi namba 16 wilaya ya Muheza*


TANGA


Waziri wa Nishati na Maendeleo ya Madini wa Uganda, Dkt. Ruth Nankabirwa, ametoa wito kwa nchi zinazotekeleza mradi wa bomba la mafuta ghafi la Afrika Mashariki (EACOP) kuhimiza wananchi, vijana na wanafunzi kutembelea mradi huo akisema kuwa hatua hiyo itasaidia kuongeza uelewa wao, hasa ikizingatiwa kuwa wao ndio wanufaika wakubwa wa mradi.

Dkt. Nankabirwa ametoa wito huo leo tarehe 7 Januari, 2026 jijini Tanga, wakati wa ziara yake katika Kambi namba 16, ambayo ni kipande cha mwisho kutoka upande wa Uganda katika mchakato wa uunganishaji wa mabomba yatakayosafirisha mafuta ghafi kutoka Hoima nchini Uganda hadi eneo la Chongoleani mkoani Tanga.

Akiwa katika kambi hiyo, Waziri Nankabirwa alijionea shughuli za uunganishaji wa mabomba katika eneo lenye urefu wa kilomita 2.5, na kueleza kuridhishwa kwake na ubora wa kazi inayotekelezwa na upande wa Tanzania, akisema ni ya kupongezwa sana.


Aidha, alipata fursa ya kutembelea mmoja wa wanufaika wa mradi kupitia utekelezaji wa huduma za kijamii, ambaye amejengewa nyumba ya kuishi kama sehemu ya manufaa ya mradi huo kwa jamii zinazozunguka mradi.

Hadi sasa, ujenzi wa bomba la mafuta ghafi la EACOP umefikia asilimia 79. Mradi huo unahusisha ujenzi wa bomba lenye urefu wa takribani kilomita 1,445 kutoka Hoima nchini Uganda hadi Chongoleani mkoani Tanga, ambapo jumla ya vipande vya mabomba 86,000 vinatumika katika utekelezaji wake.

Ujenzi wa bomba la mafuta ghafi la Afrika Mashariki ulianza mwaka 2022 na unatarajiwa kukamilika mwezi Julai, 2026.


#NishatiTupoKazini

#TanzaniaNchiYetuSote

#NchiYetuKwanza

#MaendeleoEndelevu

BILIONI 10 ZALIPWA FIDIA KWA WANANCHI WALIOPISHA UJENZI WA MIUNDOMBINU YA MRADI WA BOMBA LA MAFUTA

January 07, 2026 Add Comment


Na Oscar Assenga,TANGA

BILIONI 10 zimelipwa kama sehemu ya fidia kwa wananchi ambao wameweza kupisha maeneo yao kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu ya Bomba la Mafuta Ghafi kutoka Hoima nchini Uganda hadi Chongeleani Tanga,Tanzania.


Hayo yalibainishwa na Naibu Waziri wa Nishati Salome Makamba wakati wa ziara ambayo aliambatana na Waziri wa Nishati na Maendeleo ya Madini wa Uganda, Dkt. Ruth Nankabirwa ya kujionea hatua ambayo imefikiwa ya ujenzi wa mradi huo katika eneo la Chongoleani Jijini Tanga.

Ambapo pia katika mradi huo zaidi ya wananchi 9800 waliopo katika mkoa wa Tanga wameweza kushiriki kwenye shughuli za ujenzi wa bomba la mafuta ghafi.

Naibu Waziri huyo alisema mradi huo kwa upande wa Tanzania umeweza kufikia asilimia 86 ya utekelezaji wake ukihusisha maeneo ya ulazaji wa mabomba,ujenzi wa matankiya kuhifadhia mafuta ghafi sambamba na eneo la gati ya kushushia mafuta hayo.


Aidha alisema kuwa mpaka sasa mradi huo upo katika hatua nzuri ya utekelezaji wake na unatarajiwa kukamilika ifikapo mwezi Julai mwaka huu.

Makamba alisema kuwa mradi huo utaongeza usambazaji wa mafuta nchini na kupunguza gharama za usafirishaji, na kuufanya uwe na tija kwa wananchi wa mkoa wa Tanga na Tanzania kwa ujumla.



Mradi huu umewanufaisha kwa kiasi kikubwa wananchi wa Tanzania tofauti na wenzetu wa uganda kutokana na eneo kubwa kuwa upande wa nchi yetu"alisema Naibu Waziri Makamba.


Hata hivyo Makamba alisema kwamba dhamira ya dhati ya Rais Dkt Samia Suluhu na Rais wa Uganda Yoweri Kaguta Museveni imewezesha utekelezaji mzuri wa mradi huo unaotarajiwa kuleta mabadiliko makubwa katika Nyanja za kiuchumi ,kijami,ajira na uboreshaji wa huduma za jamii


Kwa upande wake Waziri wa Uganda Nankabirwa alisema kuwa mradi huo umeweza tekelezwa katika viwango bora vya usalama huku ukizingatia ulinzi wa athari za kimazingira


"Tayari wananchi wetu wameweza wameweza kunufaika na sehemu ya kurudisha kwa jamii kwa kuwekewa miundombinu ya maji safi,ujenzi w barabara sambamba na shughuli za michezo kwa wananchi wanaoishi karibu na maeneo ya mradi huo"alisema Waziri huyo.

Aidha aliwataka wananchi wa nchi hizo mbili kuutunza na kuulinda mradi huo kwani utakapoanza kazi utaweza kuketa manufaa makubwa ya kiuchumi baina ya nchi hizi mbili.


Ziara hiyo ililenga kuona hatua za utekelezaji wa mradi huo na kuhakikisha kuwa unatekelezwa kwa viwango vya juu vya ubora na usalama.





MRADI WA BOMBA LA MAFUTA GHAFI AFRIKA MASHARIKI KUFUNGUA FURSA ZA KIUCHUMI NA AJIRA

January 05, 2026 Add Comment








Mradi wa ujenzi wa bomba la kusafirisha mafuta ghafi Afrika Mashariki (EACOP) unaendelea kufungua fursa za kiuchumi na ajira kwa wananchi wa Tanzania na Uganda, huku ukiendelea kuchochea ukuaji wa uchumi wa nchi hizo mbili.

Hayo yameelezwa wakati wa ziara rasmi ya Waziri wa Nishati na Maendeleo ya Madini wa Uganda, Dkt. Ruth Nankabirwa, aliyeko nchini kwa ajili ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa bomba la mafuta ghafi kutoka Hoima nchini Uganda hadi Chongoleani mkoani Tanga. Waziri huyo yuko nchini sambamba na mwenyeji wake, Waziri wa Nishati wa Tanzania, Mhe. Deogratius Ndejembi.

Akizungumza na waandishi wa habari, Mhe. Ndejembi amesema kuwa utekelezaji wa mradi wa EACOP umeendelea kuleta manufaa makubwa, hususan katika eneo la ajira, ambapo jumla ya ajira 12,000 zimetolewa kwa vijana na wananchi wa Tanzania na Uganda tangu kuanza kwa mradi huo.

Ameeleza kuwa hadi sasa ujenzi wa bomba la mafuta ghafi Afrika Mashariki umefikia asilimia 79 ya utekelezaji, na unatarajiwa kukamilika mwezi Julai 2026. Aliongeza kuwa mradi huo utaongeza mapato ya nchi na kuchochea ukuaji wa uchumi, sambamba na kuwa na uwezo wa kusafirisha mapipa 246,000 ya mafuta ghafi kwa siku pindi utakapokamilika.

Kwa upande wake, Waziri wa Nishati na Maendeleo ya Madini wa Uganda, Dkt. Ruth Nankabirwa, amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa dhamira na ushirikiano mkubwa unaooneshwa katika utekelezaji wa mradi huo wa kimkakati kwa ukanda wa Afrika Mashariki.

Dkt. Nankabirwa amesema mradi wa EACOP umeleta mapinduzi makubwa ya kiuchumi kwa nchi za Tanzania na Uganda, na kusisitiza umuhimu wa kuwepo kwa utaratibu wa kuwatambua watumishi na wataalamu wanaoshiriki katika miradi mikubwa ya kimkakati ili waweze kupewa kipaumbele katika miradi mingine ijayo kulingana na uzoefu na uadilifu wao. Ameitaja miradi ya gesi na umeme inayotarajiwa kutekelezwa na nchi hizo mbili kuwa miongoni mwa miradi itakayonufaika na uzoefu huo.

Mradi wa bomba la mafuta ghafi kutoka Hoima nchini Uganda hadi Chongoleani mkoani Tanga una urefu wa kilomita 1,443, ambapo kilomita 296 zipo nchini Uganda na kilomita 1,147 zipo nchini Tanzania. Kwa upande wa Tanzania kutakuwa na jumla ya vituo vinne vya kusukuma mafuta, huku Uganda ikiwa na vituo viwili, na kufanya jumla ya vituo vya kusukuma mafuta kuwa sita.

NISHATI

WAZIRI MKUU APONGEZA TPDC KWA UJENZI WA SHULE YA MSINGI LIKONG'O KUPITIA MRADI WA LNG

December 20, 2025 Add Comment


📌*Asema ni utimizaji wa majukumu ya kijamii kupitia miradi*

 

📌*Akumbusha shule kufungwa miundombinu ya Nishati Safi ya Kupikia kuunga mkono jitihada za Rais Samia*


📌*Mhe. Salome asema taasisi 52 zitasambaziwa nishati safi ya kupikia ndani ya siku 100 za uongozi wa Rais Samia*


Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.Dkt. Mwigulu Nchemba amepongeza Wizara ya Nishati kupitia Shirika la Maendeleo ya Petroli  Tanzania (TPDC) kwa ujenzi wa shule bora ya Awali na Msingi  katika Kijiji cha Likong'o mkoani Lindi inayojengwa kupitia mradi wa uzalishaji na usindikaji wa Gesi Asilia kuwa kimiminika ( LNG). .

Waziri  Mkuu ametoa pongezi hizo tarehe 20 Desemba 2025 wakati akikagua ujenzi wa shule hiyo  itakayokuwa na uwezo wa kuhudumia wanafunzi 400 katika Kijiji cha Likong'o, Kata ya Mbanja, Halmashauri ya Manispaa ya Lindi.

" Nawapongeza TPDC kwa hatua hii ya kutekeleza shughuli za uwajibikaji kwa jamii (CSR) kupitia mradi huu wa LNG, shule hii ni bora ya kisasa na imezingatia mahitaji mbalimbali ikiwemo kuwa na miundombinu inayokidhi watu wenye mahitaji maalum na watoto wa kike." Amesema Mhe. Nchemba

Katika hatua nyingine Dkt. Nchemba ametoa msisitizo kwa Wizara ya Nishati kuhakikisha kuwa shule hiyo inafungwa miundombinu ya Nishati Safi ya Kupikia kuunga mkono utekelezaji wa Ajenda ya Nishati Safi ya Kupikia ambayo kinara wake ni Rais, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Kutokana na uwepo wa shule hiyo, Waziri Mkuu amewaasa wananchi kuchangamkia fursa kwa kuwasomesha watoto wao na hivyo kuunga mkono jitihada anazofanya Rais Rais Samia za ujenzi  shule katika maeneo mbalimbali nchini ili kuwawezesha watoto wote kupata elimu.

Kwa upande wake Mhe. Salome Makamba ambaye ni Naibu Waziri wa Nishati, amesema mradi wa ujenzi wa Shule ya Msingi Likong'o unatekelezwa  kama sehemu ya kurudisha fadhila kwa wananchi waliotoa ardhi kwa ajili ya utekelezaji mradi wa LNG.

Ameeleza kuwa ujenzi wa Shule hiyo ambao umefikia asilimia 70  unaonesha jinsi kaulimbiu ya kazi na utu inavyotekelezwa kwa vitendo na Serikali ya Awamu ya Sita.

Katika hatua nyingine, Mhe. Salome ameeleza kuwa agizo la Waziri Mkuu la shule hiyo kuwekewa miundombinu ya nishati safi ya kupikia litatekelezwa na kuongeza kuwa  ndani ya siku 100 za uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan taasisi 52 zitasambaziwa miundombinu ya nishati safi ya kupikia.

Naye, Mbunge wa Lindi, Mohamed Utaly amemshukuru Rais Samia kwa uwekezaji huo wa mradi wa LNG  ambao amesema unaleta chachu ya elimu mkoani Lindi.


Amepongeza pia TPDC kwa kuhakikisha kuwa miradi ya uwajibikaji kwa jamii imeanza kutekelezwa mapema kupitia mradi huo wa LNG.

Awali, Mhandisi Msimamizi wa mradi wa shule ya Awali na Msingi Likong'o, Upendo Mahavanu kutoka TPDC  alisema mradi huo unagharimu Sh .bilioni 1.27 ambapo shule itakuwa na Madarasa 9;  saba yakiwa ni ya shule msingi na mawili ni ya awali. Pia  kutakuwa na ofisi na nyumba za walimu.


Utekelezaji wa mradi wa LNG unatarajiwa kuwa na manufaa mbalimbali nchini ikiwemo mapato ya Serikali yatakayotokana na uuzaji wa LNG kwenye soko la kimataifa, fursa za ajira, fursa kwa wazawa kuuza bidhaa, uhaulishaji wa teknolojia mbalimbali ili kuwajengea uwezo wataalam wa ndani n.k

TUNAIMARISHA GRIDI YA UMEME YA TAIFA ILI WANANCHI WOTE MPATE UMEME WA UHAKIKA- DKT.NCHEMBA

December 19, 2025 Add Comment



📌*Asema baada miundombinu kufika hadi ngazi ya vijiji; kipaumbele ni kila mwananchi kuwa na umeme*


📌*Mhe. Salome asema Wizara ya Nishati inaendelea kuyatekeleza maono ya Rais Samia.*


 ðŸ“Œ*Ni ya kuifungamanisha Sekta ya Nishati na maendeleo*


Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba, amesema  baada ya Tanzania kuzalisha umeme wa kutosha kupitia miradi mbalimbali ukiwemo Mradi wa Umeme wa Julius Nyerere (JNHPP), hatua inayofuata ni kuhakikisha wananchi wote wanapata umeme wa uhakika kupitia uimarishaji wa Gridi ya Taifa.


Dkt. Nchemba ameyasema hayo tarehe 19 Desemba 2025 alipokuwa akizungumza na wananchi katika eneo la Somanga mkoani Lindi, baada ya kukagua miradi ya ujenzi wa madaraja, ukarabati wa barabara, pamoja na maendeleo ya ujenzi wa Bandari ya Uvuvi ya Kilwa.

 “Kulikuwa na masuala mawili makuu yaliyokuwa yakishughulikiwa na Serikali. Kwanza ilikuwa ni kufikisha miundombinu ya umeme  ngazi ya mikoa, wilaya, kata na vijiji. Sasa kazi inayoendelea ni kusambaza umeme kwa wananchi kutoka katika vyanzo vya uzalishaji kama vile Julius Nyerere. 

Ameeleza kuwa kwa sasa nchi ina ziada ya umeme, hivyo kazi iliyopo ni kuhakikisha umeme huo unawafikia wananchi kupitia uimarishaji wa Gridi ya Taifa.

Ameongeza kuwa, suala la kuwafikishia wananchi umeme limepewa pia kipaumbele katika Mpango wa Misheni 300, ambao Tanzania ilisaini mwezi Januari 2025. Kupitia mpango huo, Serikali inalenga kuwafikishia umeme wananchi wote ifikapo mwaka 2030.

Kwa upande wake, Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba, amesema Wizara ya Nishati inaendelea kuyatekeleza maono ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, ya kuifungamanisha sekta ya nishati na maendeleo ya kiuchumi kwa kuhakikisha kunakuwa na upatikanaji wa nishati ya uhakika kwa wananchi.

Kuhusu hali ya upatikanaji umeme katika mikoa ya Lindi na Mtwara, Mhe. Salome amesema  Serikali inaendelea kuboresha miundombinu ya umeme katika mikoa hiyo ili wananchi wapate umeme wa uhakika na endelevu.

Mhe. Salome pia amempongeza Rais Samia kwa kuendelea kuboresha miundombinu ya barabara mkoani Lindi, akieleza kuwa barabara hizo ni muhimu katika shughuli za uendelezaji wa rasilimali za mafuta na gesi asilia zinazopatikana katika  mikoa ya Lindi na Mtwara.


Ziara ya Waziri Mkuu mkoani Lindi pia inahusisha kutembelea mradi wa ujenzi wa Shule Mpya ya Msingi ya Likong’o, inayojengwa kupitia Mradi wa kuchakata Gesi Asilia  kuwa Kimiminika (LNG), unaotarajiwa kutekelezwa katika kijiji hicho.


Kutoka Wizara ya Nishati, ziara hiyo pia imehudhuriwa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati,  Dkt. James Mataragio.