Showing posts with label Nishati. Show all posts
Showing posts with label Nishati. Show all posts

WAZIRI NDEJEMBI AITAKA TPDC KUONGEZA KASI YA UPATIKANAJI WA MAENEO YA UCHIMBAJI WA GESI

March 01, 2026 Add Comment


Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi amelitaka Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) kuongeza kasi katika utafiti wa upatikanaji wa maeneo mapya ya uchimbaji wa visima vipya vya gesi asilia ili kuongeza upatikanaji wa gesi kwa matumizi mbalimbali pamoja na kufanikisha agenda ya matumizi ya nishati safi nchini.

Ndejembi ameeleza hayo tarehe 27 Februari 2026 mkoani Mtwara wakati akizindua mradi wa uchimbaji wa visima vitatu ambapo viwili ni kwa ajili ya kuongeza uzalishaji wa gesi asilia katika Kitalu cha Mnazi Bay na kimoja kwa ajili ya utafutaji huku utekelezaji umefikia asilimia 58.

“Rai yangu kwenu TPDC ni kuongeza kasi ya uchimbaji wa gesi katika maeneo mengine na kuhakikisha mashapo yaliyopo yanaanza kuzalisha tunapozindua kitalu hiki hapa mipango ya kuanza kuchimba sehemu nyingine ianze mara moja” amesisitiza Ndejembi.

Ndejembi ameeleza kuwa Serikali inayoongozwa na Mheshimiwa Rais Dkt Samia Suluhu Hassan iliamua kuwekeza fedha kupitia TPDC kwani mahitaji ya gesi yanaongezeka kutokana na nchi inavyoendelea kukua na kusababisha mahitaji ya gesi kuongezeka kwa ajili ya uzalishaji wa umeme matumizi ya viwandani na taasisi nishati kwenye vyombo vya usafiri pamoja na matumizi ya majumbani.

Ndejembi ameipongeza TPDC kwa kushirikiana na Kampuni ya Maurel & Prom katika kutekeleza mradi wa uchimbaji wa visima hivyo ambavyo vitaongeza uzalishaji wa gesi na kuchochea kwa kiasi kikubwa ukuaji wa uchumi.

Kadhalika Ndejembi ameitaka TPDC kuendelea kuyawezesha makampuni na wataalamu wazawa ikiwa ni pamoja na kuweka mpango wa kuendelea kuwajengea uwezo wataalamu waliopo katika maeneo ya utekelezaji wa miradi ili nao wanufaike na kuchangia ukuaji wa uchumi wa nchi yao.

Kwa upande wake, Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati anayeshughulikia Mafuta na Gesi Dkt James Mataragio ameeleza kuwa Serikali imewekeza fedha nyingi katika nishati ya gesi ambapo katika mradi huo pekee itatumika zaidi ya shilingi bilioni 235.

Awali, Mkurugenzi Mtendaji wa TPDC Mussa Makame amesema Serikali kupitia TPDC inamiliki Kitalu cha Mnazi Bay kwa asilimia 40 na Kampuni ya Maurel & Prom inamiliki asilimia 60 na kubainisha kuwa uzalishaji umeendelea kuongezeka ambapo kwa sasa uzalishaji katika kitalu hicho umefikia futi za ujazo milioni 100 kwa siku.

Mwisho.

KAMATI YA UONGOZI WA MRADI WA JNHPP YAKAGUA MAENDELEO YA BWAWA LA JULIUS NYERERE

February 27, 2026 Add Comment







📌Yasema mradi umesimamiwa na kutekelezwa kwa ufanisi

📌Yasisitiza ni kichocheo muhimu katika za fursa za kiuchumi na kijamii

Kamati ya Uongozi wa Mradi wa Bwawa la Julius Nyerere (JNHPP), tarehe 26 Februari 2026, imekagua maendeleo ya uzalishaji wa umeme katika mradi huo na kueleza kuridhishwa na usimamizi pamoja na utekelezaji wake, uliokidhi viwango vya ubora vinavyoendana na thamani ya fedha iliyowekezwa na Serikali.

Mwenyekiti wa Kamati hiyo, ambaye pia ni Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu), Dkt. Jim Yonazi , amesema kamati imefurahishwa na namna bwawa hilo linavyochochea ukuaji wa uchumi kwa kuongeza uzalishaji wa umeme unaosambazwa katika maeneo mbalimbali nchini, hatua inayochangia kuimarika kwa upatikanaji wa nishati ya umeme.

“Tumeridhishwa na jinsi mradi huu ulivyosimamiwa na kutekelezwa kwa ufanisi mkubwa.

Ukilinganisha na miradi mingine barani Afrika, mradi huu umejengwa kwa ubora wa hali ya juu na umeleta unafuu katika huduma ya umeme nchini. Haya ni mafanikio makubwa kwa Taifa,” alieleza Dkt. Yonazi.

Akizungumza kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati, Mkurugenzi wa Sera na Mipango, Bw. Petro Lyatuu, amesema mradi huo umekamilika kwa asilimia 100 na mchango wake tayari umeanza kuonekana.

Amefafanua kuwa mwaka 2021, gridi ya taifa ilikuwa na jumla ya megawati 1,600, lakini kwa sasa uwezo wa uzalishaji umefikia zaidi ya megawati 4,000, zaidi ya mara mbili ya kiwango cha awali.

“Kwa sasa bwawa linazalisha umeme na tija yake imeonekana wazi. Kuongezeka kwa uzalishaji kumeimarisha gridi ya taifa na tunaendelea kuongeza nguvu katika sekta ya nishati kwa ajili ya maendeleo ya nchi na ustawi wa wananchi,” alisisitiza Bw. Lyatuu.

Aidha kwa hatua nyingine Kamati hiyo ilitembelea kituo cha kupokea na kupoza umeme cha Chalinze, kinachopokea umeme kutoka Bwawa la Julius Nyerere na kusambaza katika maeneo mbalimbali ya nchi.

Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), Naibu Mkurugenzi Mtendaji Uzalishaji, Mhandisi Antony Mbushi, amesema kituo hicho kimekamilika na tayari kinafanya kazi.

Ameongeza kuwa ujenzi wa njia ya kusafirisha umeme kutoka Chalinze hadi Dodoma umefikia asilimia 71.58, huku mradi wa kusafirisha umeme kutoka Chalinze kupitia Kinyerezi hadi Mkuranga umefikia asilimia 59.76.

‘’Kamati imeridhishwa na maendeleo ya miradi hiyo na kusisitiza kuwa mpango uliopo ni kuendelea kuongeza uzalishaji ili kuhakikisha nishati ya umeme inakuwa ya uhakika na endelevu’,’Aliongeza Mha. Mbushi

Katika hitimisho la ziara hiyo, Kamati imeeleza kuwa utekelezaji wa miradi ya kimkakati ya umeme unaifanya Tanzania kuwa kivutio cha uwekezaji na kitovu cha usambazaji wa umeme katika ukanda wa Afrika Mashariki, Kati na Kusini.




















KAMATI YA UONGOZI WA MRADI WA JNHPP YAKAGUA MAENDELEO YA BWAWA LA JULIUS NYERERE

February 27, 2026 Add Comment




📌Yasema mradi umesimamiwa na kutekelezwa kwa ufanisi


📌Yasisitiza ni kichocheo muhimu katika  fursa za kiuchumi na kijamii


Kamati ya Uongozi wa Mradi wa Bwawa la Julius Nyerere (JNHPP), tarehe 26 Februari 2026, imekagua maendeleo ya uzalishaji wa umeme katika bwawa la Julius Nyerere na kueleza kuridhishwa na usimamizi pamoja na utekelezaji wake, uliokidhi viwango vya ubora vinavyoendana na thamani ya fedha iliyowekezwa na Serikali.

Mwenyekiti wa Kamati hiyo, ambaye pia ni Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu), Dkt. Jim Yonazi , amesema kamati imefurahishwa na namna bwawa hilo linavyochochea ukuaji wa uchumi kwa kuongeza uzalishaji wa umeme unaosambazwa katika maeneo mbalimbali nchini, hatua inayochangia kuimarika kwa upatikanaji wa nishati ya umeme.



“Tumeridhishwa na jinsi mradi huu ulivyosimamiwa na kutekelezwa kwa ufanisi mkubwa. Ukilinganisha na miradi mingine barani Afrika, mradi huu umejengwa kwa ubora wa hali ya juu na umeleta unafuu katika huduma ya umeme nchini. Haya ni mafanikio makubwa kwa Taifa,” alieleza Dkt. Yonazi.



Akizungumza kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati, Mkurugenzi wa Sera na Mipango, Bw. Petro Lyatuu, amesema mradi huo umekamilika  kwa asilimia 100 na mchango wake tayari umeanza kuonekana. 



Amefafanua kuwa mwaka 2021, gridi ya taifa ilikuwa na jumla ya megawati 1,600, lakini kwa sasa uwezo wa uzalishaji umefikia zaidi ya megawati 4,000, zaidi ya mara mbili ya kiwango cha awali.

“Kwa sasa bwawa linazalisha umeme na tija yake imeonekana wazi. Kuongezeka kwa uzalishaji kumeimarisha gridi ya taifa na tunaendelea kuongeza nguvu katika sekta ya nishati kwa ajili ya maendeleo ya nchi na ustawi wa wananchi,” alisisitiza Bw. Lyatuu.



Aidha, tarehe 25 Februari 2026, Kamati hiyo ilitembelea kituo cha kupokea na kupoza umeme cha Chalinze, kinachopokea umeme kutoka Bwawa la Julius Nyerere na kusambaza katika maeneo mbalimbali ya nchi.

Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), Naibu Mkurugenzi Mtendaji Uzalishaji, Mhandisi Antony Mbushi, amesema kituo hicho kimekamilika na tayari kinafanya kazi.

Ameongeza kuwa ujenzi wa njia ya kusafirisha umeme kutoka Chalinze hadi Dodoma umefikia asilimia 71.58, huku mradi wa kusafirisha umeme kutoka Chalinze kupitia Kinyerezi hadi Mkuranga umefikia asilimia 59.76.


‘’Kamati imeridhishwa na maendeleo ya miradi hiyo na kusisitiza kuwa mpango uliopo ni kuendelea kuongeza uzalishaji ili kuhakikisha nishati ya umeme inakuwa ya uhakika na endelevu’,’ Aliongeza Mha. Mbushi

Katika hitimisho la ziara hiyo, Kamati imeeleza kuwa utekelezaji wa miradi ya kimkakati ya umeme unaifanya Tanzania kuwa kivutio cha uwekezaji na kitovu cha usambazaji wa umeme katika ukanda wa Afrika Mashariki, Kati na Kusini.



RC MALIMA AIPONGEZA REA UTEKELEZAJI MIRADI MIKUBWA YA UMEME

February 26, 2026 Add Comment





Na Mwandishi Wetu - Morogoro




Mkuu wa mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Malima ameipongeza Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa utekekezaji wa miradi ya umeme maeneo ya Vijijini na Vitongoji hali iliyopelekea kuchochea uchumi wa wananchi na Taifa kwa ujumla.


RC Malima ametoa pongezi hizo leo Februari 26, 2026 mkoani humo wakati akizungumza na Bodi ya Nishati Vijijini (REB) pamona na Menejimenti ya Wakala wa Nishati Vijijini (REA) ilipomtembelea ofisini kwake kueleza utekelezaji wa miradi ya umeme vijijini inayoendelea na iliyokamilika mkoani humo.


"Nimeifahamu REA kwa mingi toka ilipoanzishwa rasmi. Hapa ilipofika leo hii lazima tujivunie sisi kama Watanzania kwa kuwa imeweza kufikisha umeme vijiji vyote na sasa utekekezaji unaendelea kwenye vitongoji vyote nchini," Amesema RC Malima.


Halikadhalika RC Malima ameipongeza Bodi ya REA na Menejimenti kwa kazi kubwa iliyofanyika kwa kusimamia miradi mbalimbali ya umeme katika mkoa huo ili Watanzania waweze kunufaika na nishati hiyo muhimu.


Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Bodi ya Nishati Vijijini (REB), Mhe. Balozi Meja Jenerali Mstaafu Jacob Kingu ameeleza kuwa REA itaendelea kutekekeza miradi ya umeme vijijini wa weledi huku ikiwasimamia wakandarasi wa miradi hiyo ili waweze kuikamilisha miradi hiyo kwa wakati.


"Sisi kama Bodi tunauhakika miradi inayoendelea tutaikamilisha kwa wakati kwa kuwa Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan tayari imetoa fedha nyingi ili kuwezesha na kukamilisha miradi hiyo, " Ameongeza Mhe. Balozi Kingu.




Naye, Mkurugenzi Mkuu wa REA Mha. Hassan Saidy ameeleza kuwa kwa mkoa huo Wakala ipo mbioni kuongeza miradi ya ziada katika maeneo ya miji ambayo bado hayajafikiwa na huduma ya umeme ambapo takribani maeneo 165 yatapatiwa huduma hiyo na wateja wa awali 1,750 watapatiwa huduma ya umeme ambapo Serikali imetoa takribani shilingi bilioni 7 kwa mkoa wa Morogoro kutekeleza miradi hiyo.



DKT. MATARAGIO: PURA ONGEZENI KASI UTAFITI WA MAENEO MAPYA YA MAFUTA NA GESI

February 26, 2026 Add Comment




Na Mwandishi Wetu, Morogoro


Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati anayeshughulikia Mafuta na Gesi, Dkt. James Mataragio, ameielekeza Mamlaka ya Udhibiti Mkondo wa Juu wa Petroli (PURA) kuongeza kasi ya utafiti wa awali katika maeneo mapya ya mafuta na gesi asilia ili kuvutia wawekezaji na kuongeza mapato ya taifa.


Akizungumza leo Februari 26, 2026, wakati wa Mkutano wa Tano wa Baraza la Wafanyakazi uliofanyika mkoani Morogoro, Dkt. Mataragio amesema juhudi hizo zitachochea uwekezaji, kupanua ushiriki wa wazawa na kuimarisha utekelezaji wa majukumu ya msingi ya taasisi hiyo.

Amesisitiza kuwa ni muhimu kwa PURA kuendelea kutambua na kuendeleza maeneo mapya ya miradi, kuyatangaza kwa wawekezaji pamoja na kusimamia kikamilifu majukumu yake kama yalivyoainishwa katika malengo ya kuanzishwa kwake.

Miongoni mwa majukumu hayo ni kusimamia na kufuatilia shughuli za utafutaji na uzalishaji wa mafuta na gesi asilia kwa kuzingatia sheria na taratibu, kuishauri Serikali kuhusu masuala ya mkondo wa juu wa mafuta na gesi, pamoja na kutangaza vitalu vilivyowazi kwa ajili ya uwekezaji ili kuongeza ugunduzi wa rasilimali hizo nchini.

Dkt. Mataragio amesema hatua hizo zitasaidia kuongeza mchango wa sekta ya mafuta na gesi katika ukuaji wa uchumi wa taifa na kuimarisha usimamizi wa rasilimali kwa manufaa ya Watanzania.



&&&

SADC YAVUTIWA NA MIKAKATI YA TANZANIA KATIKA AJENDA YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA.

February 26, 2026 Add Comment

 

Victoria Falls, Zimbambwe


Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika – SADC) imeeleza kuvutiwa na mikakati ya Tanzania katika kuharakisha matumizi ya nishati safi ya kupikia, hususan hatua ya kuondoa kodi na kutoa ruzuku kwa vifaa kama mitungi ya gesi na majiko banifu, pamoja na kampeni za uhamasishaji kwa wananchi.

Akizungumza katika mdahalo wa Mawaziri kuhusu Nishati endelevu katika maadhimisho ya Wiki ya Nishati Endelevu ya SADC inayofanyika Victoria Falls, Zimbabwe (23–27 Februari 2026), Naibu Waziri wa Nishati Mhe. Salome Makamba amesema Tanzania inalenga kufikia asilimia 80 ya matumizi ya nishati safi ya kupikia ifikapo mwaka 2034, huku Mpango Mahsusi wa Taifa wa Nishati ukilenga asilimia 75 ifikapo 2030.

Mhe. Salome amesema Serikali imeweka mkazo kwa taasisi zinazohudumia zaidi ya watu 100 zikiwemo magereza, kambi za jeshi, shule na masoko makubwa kwa kuzifungia mifumo ya nishati safi ya kupikia, hatua iliyotajwa kuwa ya ubunifu na yenye matokeo chanya.

Aliongeza kuwa Tanzania imefikisha umeme katika vijiji vyote 12,318 vya Tanzania Bara, na kuongeza upatikanaji wa umeme hadi asilimia 85.5. Uwezo wa uzalishaji umefikia megawati 4,437 na unatarajiwa kuongezeka hadi megawati 8,000 ifikapo 2030.

Kwa upande wake Katibu Mtendaji wa SADC, Mhe. Elias Magosi aliipongeza Tanzania kwa kuongoza juhudi za kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia katika Ukanda, hivyo kuchochea mabadiliko chanya ya kijamii, kiuchumi na kimazingira katika ngazi zote za maendeleo

Maadhimisho hayo yalifunguliwa rasmi na Makamu wa Rais wa Zimbabwe, Constantino Chiwenge amesisitiza umuhimu wa nchi za Afrika kutumia rasilimali za nishati jadidifu kama chachu ya maendeleo ya kiuchumi.