Showing posts with label siasa. Show all posts
Showing posts with label siasa. Show all posts

CCM YAMNG’OA KIGOGO UWANJA WA MKWAKWANI

March 11, 2026 Add Comment



Na Oscar Assenga,TANGA

KAMATI ya Siasa ya Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Tanga imeagiza kusimamishwa kazi Meneja wa Uwanja wa Mkwakwani Akida Machai kutokana na mapungufu mbalimbali yaliyobainika wakati wa ziara ya kamati hiyo kwa ajili ya kujionekana maendeleo yake.

Akizungumza kuhusu maamuzi hayo ,Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Tanga Rajab Abdurhaman ambapo alisema kwamba ukiangalia mapato yanayopatikana na gharama ambazo zinatumika zikitolewa sawasawa na CCM hakuna chochote kinachopatikana lakini maji yanalipwa na CCM ,Umeme unalipwa na CCM.

Alisema wanafanya hivyo kuhakikisha wananchi waendelee kupata burudani ya michezo sasa wanapotoa fedha na kuona mambo bado hawaendi kama wanavyotarajia ni jambo ambalo limekuwa likiwaumiza.


“Mimi Binafsi nilitoa milioni 50 inawezekana fedha hamtafiti nyie ndio maana hamuoni uchungu wake mimi natayetafutaa fedha kwa wadau anawawaomba anajua uchungu wake lakini wao kwa sababu hawajui uchungu wake na walimuweka yeye kama meneja wakiamini angeweza kutusaidia kuhakikisha uwanja huo muda wote unaweza kuwa bora unatumika”Alisema

“Lakini ukija wakati wote uwanja umekuwa kama Mbuga za Wanyama haiwezekani sio sawa mpaka leo viti vimeletwa havijafungwa na mmeviacha mpaka vimeota majani”Alisema

Aidha alisema kwamba wao wamekaa kama viongozi waliochaguliwa ili uwanja uweze kufikia vigezo lakini mpaka kufikia wakati uwanja kufungiwa na TFF hivyo hawawezi kukubali.

“Nilisema kwa hali ilivyo muda wowote TFF wangeweza kuja kutufungia uwanja hivyo nitoe maelekezo kwa Kamati ya Siasa mkoa kaeni Mtafute Meneja mwengine ili changamoto hizo ziweze kuondoka”Alisema

Hata hivyo alisema kwamba kwa mpangaji Yule mwenye baa pale nje ambayo haijakidhi vigezo na Shirikisho la Soka nchini (TFF) walishasema ile baa inazuia washabiki kuingia uwanjani wakati wa mpira na inatakiwa kuondoka lakini mpaka leo haijaondoka.

“Maanake huyo mtu ana mapembe kiasi gani yeye ni mpangaji kwenye eneo letu lakini anakigomea CCM hivyo nahitaji hii baa leo iondoke ili maelekezo na maagizo ya TFF tuweze kuyatimiza na apatikane Meneja mwengine haraka ili aweze kushirikina na vongozi wa CCM kufungwa viti hivyo na nanatoa mwezi mmoja”Alisema

Awali akizungumza aliyekuwa Meneja wa uwanja wa CCM Mkoa wa Tanga Akida Machai alisema changamoto ya uhaba wa nguvu kazi ndio imepelekea kukwamisha viti hivyo kufungwa .

Alisema kwamba walikuwa wakihitaji kuongezewa nguvu kazi yeye anashukru CCM kwa nafasi waliompatia na wanamtakia kilala heri Meneja Mpya huku akieleza wakati viti vilipokuja walipeleka Bajeti ya kufunga viti CCM na vitu vinavyohusika na hawezi kutoa fedha zake kufungwa viti.

Mwisho.

WANAWAKE WA UWT KIBAHA MJI WAANZA KUTEMA CHECHE BAADA YA USHINDI WA KISHINDO KATIKA UCHAGUZI MKUU

March 11, 2026 Add Comment


NA VICTOR MASANGU,KIBAHA

Jumuiya ya umoja wa wanawake (UWT) Wilaya ya Kibaha mjini katika kukiimarisha chama imeamua kufanya ziara maalumu yenye lengo la kuwashukuru na kuwapongeza wanawake kwa umoja wao na mshikamao waliouonyesha katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2025 na kupelekea chama cha mapinduzi (CCM) kuweza kushinda kwa kishindo katika nafasi za Udiwani, Ubunge pamoja na Urais.

Akizungumza katika ziara hiyo ambayo imefanyika katika Kata mbili za Visiga pamoja na Misugusugu Mwenyekiti wa (UWT) Wilaya ya Kibaha Elina Mgonja amesema kwamba wameamua kufanya ziara hiyo ambayo itaweza kuwapa fursa ya kukutana na wanawake hao ambao ndio walikuwa mstari wa mbele katika kukipigania chama kiweze kushinda na kupata viongozi wa CCM katika nafasi mbali mbali.'

Katika ziara hiyo ambayo imeongozwa na Mwenyekiti wa UWT Wilaya ya Kibaha pamoja na baadhi ya wajumbe wa kamati ya utekelezaji ambapo pia wametumia fursa ya kutembelea zahanati ya Misusugu pamoja na kuendesha zoezi la upandaji wa miti.

Mwenyekiti huyo amebainisha kwamba wameamua kufanya ziara hiyo kwa lengo la kuweza kutoa shukrani kwa wanawake ikiwa pamoja na kuhamasiha viongozi wa matawi mbali mbali kuwezaa kushikamana kwa pamoja ili kuimalisha uwahi wa jumuiya pamoja na chama kuanzia ngazi za chini.

"Tumeanza ziara yetu ya jumuiya ya wanawake Wilayaa ya Kibaha ambapo tumetembeleakata mbili za visiga pamoja na kata ya Misugusugu lakini kitu kikubwa ni kwa ajili ya kuwashukuru wanawake wote wa chama cha mapinduzi pamoja na jumuiya wa UWT kwa kuweza kuwachagua viongozi kwa kura nyingi za kishindo katika nafasi ya Udiwani, Ubunge, pamoja na nafasi ya Urais,"amebainisha Elina

Kadhalika Mwenyekiti huyo amempongeza kwa dhati Rais wa awamu ya sita kwa kuweza kutekeleza ilani ya cchama kwa vitendo ikiwemo kutenga fedha nyingi ambazo zimekwenda kutekeleza miradi mbali mbali ya maendeleo ikiwemo sekta ya afya, eilimu, maji, nishati ya umeme pamoja na huduma za kijamii.

Kwa upande wake Katibu wa UWT Wilaya ya Kibaha Cesilia Ndalu amesema kuwa ziara hiyo pia imelenga kuanzisha vikundi vya uchumi ambavyo vitaweza kuwasaidia kwa kiasi kukubwa kupambana na wimbii la umasikini.

Diwani wa kata ya Misugusugu Ally Simba amewahimiza wanawake wa UWT kuhakikisha wanachangamkia fursa za mikopo mbali mbali ambayo inatolewa na Halmashauri kwa lengo la kuweza kujikwamua kiuchumi pamoja na kuleta mabadiliko chanya ya kimaendeleo katika nyanja tofauti.

CCM NA FRELIMO KUIMARISHA USHIRIKIANO WA KIUCHUMI

March 06, 2026 Add Comment


Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dkt. Asha-Rose Migiro, amekutana na kufanya mazungumzo na Katibu Mkuu wa Chama cha FRELIMO, (Msumbiji), Ndugu Chakil Felizardo Passadas Aboobacar, ambaye ameanza ziara rasmi ya kikazi kwa siku mbili nchini. 

Katika mazungumzo hayo yaliyofanyika leo tarehe 6 Machi 2026, katika Ofisi Ndogo za Makao Makuu ya CCM, Dar Es Salaam, vyama hivyo viwili ambavyo vina urafiki na udugu wa kihistoria, vimekubaliana kuendelea kuimarisha uhusiano uliopo kati ya pande hizo mbili, hasa kushirikiana kiuchumi.



MABALOZI WA MASHINA NI NGUZO YA KUKIPAMBANIA CHAMA-DKT MIGIRO.

January 20, 2026 Add Comment




*Atoa wito kwa viongozi wa ngazi zote za Kitaifa, kuhudhuria vikao vya Chama kwenye ngazi za Mashina.


*Asema ni mahala pa kuikusanya jamii pamoja, kutangaza kazi nzuri inayofanywa na Rais Dkt. Samia.


*Ala chakula na Mabalozi wa mashina


Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt Asha-Rose Migiro, amesema Mabalozi wa Mashina ndiyo nguzo ya kukipambania Chama, kwa kuwa ni macho, masikio na daraja la kuunganisha Chama na kuendelea kulinda umoja kama nguvu ya kusonga mbele ili kuwatumikia wananchi.

Akizungumza leo, tarehe 20.1.2026 katika mkutano na Mabalozi wa Mashina Mkoa wa Dodoma, Katibu Mkuu wa CCM, Dkt Migiro, amesema Mashina ni ngome ya ulinzi wa chama, kwani yataendelea kuwa Walezi, na kuwaunganisha wananchi pamoja, na kwamba siasa lazima iende sambamba na uchumi ndio maana Mashina yana tija kwa Chama.

Amesema ni mahala pa kuikusanya jamii pamoja, kutangaza kazi nzuri inayofanywa na Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan, huku akiwataka kufanya vikao vya mara kwa mara na kufikisha maadhimio ngazi za juu, ambapo kupitia Chama wanaweza kuishauri serikali iliyoko madarakani.

Aidha, Dkt. Migiro ametoa wito kwa viongozi wa ngazi zote za Kitaifa, kuhakikisha wanahudhuria vikao vya Chama kwenye ngazi za Mashina, ili kujadili kwa pamoja na kutatua au kueleza ahadi walizoahidi watakaposhika dola zimefikia wapi utekelezaji wake, ili kulinda umoja wa Chama na kuwa nguvu ya kusonga mbele kuwatumikia wananchi.

Awali, akitoa shukrani kwa niaba ya Wabunge waliohudhuria mkutano huo, Mbunge wa Jimbo la Mtumba na Waziri wa Madini, Anthony Mavunde, amesema katika miaka mingi iliyopita hakuna kipindi ambacho Chama kimewaangalia Mabalozi vizuri kama awamu hii ya sita chini ya Rais Samia Suluhu Hassan, ambaye ni Mwenyekiti wa CCM, akitoa rai kwa Mabalozi na viongozi wote kuyafanyia kazi maelekezo yote yaliyotolewa na Katibu Mkuu wa CCM.



DKT. MIGIRO: MAENDELEO YA JAMII NA SIASA HAVIWEZI KUTENGANISHWA

January 13, 2026 Add Comment


*Asisitiza mabalozi kupandisha bendera za chama kwenye maeneo yao.


* Asema chama kinawajali na kuwathamini mabalozi.

Mahusiano kati ya maendeleo ya jamii na maendeleo ya kisiasa hayawezi kutenganishwa, kwani maendeleo ya kweli huanzia katika misingi imara ya uongozi wa wananchi wenyewe. 

Kauli hiyo imesisitizwa na Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dkt. Asha-Rose Migiro, alipobainisha kuwa injini ya maendeleo ya chama na Taifa kwa ujumla ipo katika mashina ya CCM.

Dkt. Migiro amesema maendeleo ya kweli kwa wananchi huanzia katika mashina ya Chama hicho, akisisitiza kuwa jitihada zote za maendeleo ya kijamii na kiuchumi hupata nguvu kupitia uongozi wa ngazi za chini.

Katibu Mkuu huyo, ambaye ni mwanamke wa kwanza kushika wadhifa huo tangu chama kianzishwe, ameyasema hayo katika mkutano wake na Mabalozi wa Mashina wa CCM Wilaya ya Ilala, ikiwa ni hitimisho la ziara yake katika Mkoa wa Dar es Salaam yenye lengo la kuimarisha uhai wa CCM kuanzia mashinani, kwa kauli mbiu ya “Shina lako linakuita.”

Akizungumza na mabalozi hao, amesema mashina ndiyo ngazi ya kwanza inayowawezesha wananchi kushiriki kikamilifu katika mchakato wa maendeleo, kwa kuwa ndiko wanakotoka wananchi wenyewe na ndiko changamoto zao halisi zinapojadiliwa na kutafutiwa ufumbuzi.

Ameeleza kuwa mashina imara huwezesha utekelezaji wa miradi ya maendeleo kwa uwazi, ushirikishwaji na uwajibikaji, jambo linaloongeza imani ya wananchi kwa Chama Cha Mapinduzi na kuimarisha mshikamano wa kisiasa na kijamii.

Ameongeza kuwa viongozi wa mashina wana wajibu mkubwa wa kusimamia utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika maeneo yao, akisisitiza kuwa uangalizi wa karibu wa miradi hiyo ndio msingi wa maendeleo yenye tija na yanayogusa maisha ya wananchi moja kwa moja.

Aidha, Mwanadiplomasia huyo amesema Mwenyekiti wa CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amepongeza kazi kubwa inayofanywa na Mabalozi wa Mashina, huku akibainisha kuwa chama kitaendelea kuwajali, kuwathamini na kuwatambua kama mhimili muhimu wa uhai na ushindi wa CCM kuanzia ngazi ya chini.


DOYO AONGOZA KIKAO CHA TATHIMINI YA UCHAGUZI MKUU WA OCTOBA 2025.

January 07, 2026 Add Comment

 


Na Mwandishi Wetu,TANGA

KATIBU MKUU wa Taifa wa Chama cha NLD Doyo Hassan Doyo leo January 6 mwaka huu 2026 ameongoza kikao cha Tathimini ya Uchaguzi Mkuu uliofanyika Octoba mwaka 2025 cha Watendaji wa Makao Makuu na Afisi Kuu pamoja na Wagombea Wote.

Wagombea hao ni waliogombea nafasi mbalimbali katika uchaguzi huo, ikiwa ni maandalizi ya vikao vya kikatiba vinavyotarajia kufanyika mwishoni mwa mwezi huu.

Katika kikao hicho kimepitisha pia Taarifa ya maandalizi ya kugombea Ubunge Jimbo la Peramiho mkoani Ruvuma wakati tume itapotangaza rasmi kuanza mchakato wa kumpata mwakilishi wa Jimbo hilo .

Katibu Mkuu huyo aliwashukuru  wananchi wote waliokiunga mkono chama chetu katika kampeni zake nchin kote wakati wa uchaguzi mkuu.

Hata hivyo alitumia nafasi hiyo kuwashukuru  wagombea wote waliogombea nafasi mbalimbali kote nchini nakuwataka wasife moyo na kujipanga kisawasawa katika chaguzi zijazo katika nchi yetu kwani hiyo ndyo njia pekee ya kuweza kushika Dola.