Showing posts with label siasa. Show all posts
Showing posts with label siasa. Show all posts

DKT.SAMIA SULUHU HASSAN AZUNGUMZA NA WANANCHI WA MISUNGWI MKOANI MWANZA

October 07, 2025 Add Comment

Mgombea wa nafasi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Taifa Ndugu Dkt. Samia Suluhu Hassan akizungumza na wananchi wa Misungwi katika muendelezo wa muendelezo wa Kampeni za Uchaguzi kwa CCM, mkoani Mwanza tarehe 07 Oktoba, 2025.



Matukio mbalimbali katika mkutano wa hadhara wa Kampeni wa Mgombea wa nafasi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Taifa Ndugu Dkt. Samia Suluhu Hassan uliofanyika Misungwi mkoani Mwanza tarehe 07 Oktoba, 2025.

Shamra shamra za mapokezi ya Mgombea wa nafasi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Taifa Ndugu Dkt. Samia Suluhu Hassan mara baada ya kuwasili Misungwi mkoani Mwanza tarehe 07 Oktoba, 2025.


.






DKT.SAMIA SULUHU HASSAN AZUNGUMZA NA WANANCHI WA BUHONGWA,NYAMAGANA JIJINI MWANZA

October 07, 2025 Add Comment
Mgombea wa nafasi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Taifa Ndugu Dkt. Samia Suluhu Hassan akizungumza na wananchi wa Kata ya Buhongwa, katika muendelezo wa Kampeni za Uchaguzi kwa CCM, Nyamagana mkoani Mwanza tarehe 07 Oktoba, 2025.
Mgombea wa nafasi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Taifa Ndugu Dkt. Samia Suluhu Hassan akizungumza na wananchi wa Kata ya Buhongwa, katika muendelezo wa Kampeni za Uchaguzi kwa CCM, Nyamagana mkoani Mwanza tarehe 07 Oktoba, 2025.
KATIBU Mkuu wa CCM Dkt Asha Rose Migiro akizungumza katika muendelezo wa Kampeni za Uchaguzi kwa CCM, Nyamagana mkoani Mwanza tarehe 07 Oktoba, 2025.

 Sehemu ya Wananchi wa Kata ya Buhongwa waliohudhuria mkutano wa hadhara wa Kampeni wa Mgombea wa nafasi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Taifa Ndugu Dkt. Samia Suluhu Hassan mkoani Mwanza tarehe 07 Oktoba, 2025.

Shamra shamra za mapokezi ya Mgombea wa nafasi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Taifa Ndugu Dkt. Samia Suluhu Hassan mara baada ya kuwasili Buhongwa mkoani Mwanza tarehe 07 Oktoba, 2025.
Shamra shamra za mapokezi ya Mgombea wa nafasi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Taifa Ndugu Dkt. Samia Suluhu Hassan mara baada ya kuwasili Buhongwa mkoani Mwanza tarehe 07 Oktoba, 2025.

Shamra shamra za mapokezi ya Mgombea wa nafasi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Taifa Ndugu Dkt. Samia Suluhu Hassan mara baada ya kuwasili Buhongwa mkoani Mwanza tarehe 07 Oktoba, 2025.

Shamra shamra za mapokezi ya Mgombea wa nafasi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Taifa Ndugu Dkt. Samia Suluhu Hassan mara baada ya kuwasili Buhongwa mkoani Mwanza tarehe 07 Oktoba, 2025.



DKT.SAMIA SULUHU HASSAN AWASILI JIJINI MWANZA

October 07, 2025 Add Comment

 

Mgombea wa nafasi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Taifa Ndugu Dkt. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na viongozi mbalimbali mara baada ya kuwasili kwenye uwanja wa Ndege wa Mwanza katika muendelezo wa Kampeni za Uchaguzi kwa CCM mkoanI Mwanza tarehe 07 Oktoba, 2025.



Mgombea wa nafasi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Taifa Ndugu Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasalimia wananchi waliofika kumpokea katika uwanja wa Ndege wa Mwanza tarehe 07 Oktoba, 2025.
Mgombea wa nafasi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Taifa Ndugu Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasalimia wananchi waliofika kumpokea katika uwanja wa Ndege wa Mwanza tarehe 07 Oktoba, 2025.
Mgombea wa nafasi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Taifa Ndugu Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasalimia wananchi waliofika kumpokea katika uwanja wa Ndege wa Mwanza tarehe 07 Oktoba, 2025.
Shamra shamra za mapokezi ya Mgombea wa nafasi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa  Tanzania na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Taifa Ndugu Dkt. Samia Suluhu Hassan mara baada ya kuwasili katika uwanja wa Ndege wa Mwanza tarehe 07 Oktoba, 2025.


CCM YABADILISHA MAISHA NAMONGE

October 01, 2025 Add Comment

Mgombea nafasi ya Ubunge wa Jimbo la Bukombe kwa tiketi ya CCM Dkt. Doto Biteko akinadi Ilani ya CCM kwa wananchi wa Kijiji cha Bwenda  Kata ya Namonge ikiwa ni sehemu ya muendelezo wa kampeni za Uchaguzi Mkuu kwa Chama hicho Wilaya ya Bukombe tarehe 01 Oktoba 2025.



Mgombea Ubunge wa Jimbo la Bukombe kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi (CCM), Ndugu Doto Mashaka Biteko amesema kuwa Serikali ya CCM inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imebadilisha maisha ya watu wa Kata ya Namonge  kwa kuleta miradi ya maendeleo ikiwemo kufungua barabara, maji na umeme.

Dkt. Biteko amesema hayo Oktoba 1, 2025 wakati wa mkutano wa kampeni katika Kijiji cha Bwenda, Kata ya Namonge wilayani Bukombe mkoani Geita ikiwa ni sehemu Kampeni za Uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani utakaofanyika Oktoba 29, mwaka huu.

Dkt. Biteko amesema kuwa awali Kata hiyo haikuwa na maji, umeme,barabara na hata walimu waliochaguliwa kufundisha katika shule za Kata hiyo hawakufurahia kazi zao kutokana na hali iliyokuwa.


“Kituo cha afya kimekamilika, gari la kubeba wagonjwa kesho litakuwepo, leo tuna shule 14 za msingi, shule tatu za sekondari na tutataka kujenga shule zingine za kidato cha tano na sita,” amesema Dkt. Biteko.

Ameendelea kusema ikiwa wananchi hao wanahitaji maendeleo zaidi amewaomba ifikapo Oktoba 29 mwaka huu wajitokeze kupiga kura huku akiwahimiza kuchagua viongozi wa CCM.


Amesema CCM ina mpango wa kukarabati Shule ya Bwenda, kupeleka umeme maeneo yote ambayo hayana umeme.


Pia, amewahimiza wananchi wa Kata hiyo kumpigia kura mgombea udiwani Mlalu ambaye mara zote ameyapa kipaumbele maendeleo ya wananchi.

“ Kura 31, 772 za wananchi waliojiandikisha kupiga kura katika Kata hii zimchague mgombea wetu wa Urais Dkt. Samia Suluhu Hassan, zinichague Mbunge Biteko na Diwani Mlalu kisha mtudai maendeleo,” amesisitiza Dkt. Biteko.


Pia amewaeleza wananchi hao kuwa Oktoba 12, Dkt. Samia atatembelea Jimbo lao hivyo wajitokeze kwa wingi ili kuashiria upendo na shukrani zao kwake.


Naye, Mgombea wa Udiwani Kata ya Namonge, Malalu Bundala amesema kuwa miradi yote iliyopo kwenye Kata hiyo imegharamiwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan.


Ametolea mfano wa miradi hiyo kuwa ni ujenzi wa nyumba mbili za walimu katika kijiji cha Nyamagana na Shule Shikizi Bwenda.


Kuhusu miradi ya maji amesema Kata hiyo imepata visima viwili ikiwa ni hatua ya Rais Samia ya kutatua changamoto ya maji na kusogeza karibu zaidi huduma huyo kwa wananchi kwa kuchimba visima vitano katika kila jimbo.


Pamoja na hayo amewaomba wananchi wa Kata hiyo kuwachagua wagombea wote wa CCM katika Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Oktoba 29.


Mwisho.

KURA ZOTE BUTINZYA TUMPIGIE DKT.SAMIA -DKT.BITEKO

October 01, 2025 Add Comment

Mgombea Ubunge wa Jimbo la Bukombe kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi (CCM), Ndugu Doto Mashaka Biteko amewahimiza wananchi wa Kata ya Butinzya, Wilayani Bukombe kumpigia kura mgombea wa Urais kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi (CCM)Dkt. Samia Suluhu Hassan ili aendelee kuongoza na kusimamia miradi ya maendele iliyokwishaanzishwa na hivyo kuwaletea maendeleo.


Dkt. Biteko amesema hayo Septemba 30, 2025 wakati wa mkutano wa kampeni katika Kata ya Butinzya wilayani Bukombe mkoani Geita ikiwa ni sehemu Kampeni za Uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani utakaofanyika Oktoba 29, mwaka huu.

Amesema wananchi wanalo jukumu la kujotokeza kwa wingi kupiga kura na watakapopiga kura maana yake ni kutimiza wajibu wao kidemokrasia ambao utawawezesha kutimiziwa mahitaji yao kwa kujengewa miradi ya maji, umeme, barabara, hospitali na shule.


Amesema katika miaka mitano iliyopita wananchi hao wakishiriki katika kutekeleza miradi ya maendeleo iliyolenga kutatua changamoto za Bukombe na sasa jukumu lililopo mbele ni kuboresha na kuongeza miundombinu kwa maslahi mapana ya wananchi wa Wilaya ya Bukombe na Taifa kwa ujumla.

“Kipindi kilichopita hapakuwa na barabara lakini leo tumeifungua miundombinu ya barabara kutoka Butinzya hadi Isemabuma na maeneo mengine. Changamoto ya maji tunaifanyia kazi na tutahakikisha yatapatikana katika umbali usiozidi mita 400, tunajenga zahanati nyingine na tunataka kuongeza madarasa na kukarabati shule,” amesema Dkt. Biteko.


Ameongeza maendeleo yaliyopatikana ni uwezeshaji kutoka kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan “ Haya yote anayoweza kuyafanya ni Dkt. Samia, mimi siwezi kufanya haya yote bila msaada na uwezeshaji wake. Hivyo, niwaombe wananchi wote 7,111 mliojiandikisha mjitokeze na kumpigia kura Dkt. Samia,” 


Akiendelea na kampeni zake katika Kata ya Igulwa, Dkt. Biteko amesema kuwa Rais Samia amedhamiria kuleta maendeleo katika Wilaya ya Bukombe kwa kuendelea kujenga barabara za lami ambapo barabara ya Ushirombo kwenda Katoro imeanza kujengwa.

Pia, amesema Rais Samia ametoa kibali kwa ajili ya kuchimba madini katika Pori la Kigosi ili kuwasaidia wananchi hapo kujipatia kipato.


Dkt. Biteko amebainisha kuwa katika Shule ya Sekondari Bukombe kupitia ufadhili wa Ubalozi wa India wanajenga kituo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano ili wanafunzi wa Bukombe waweze kuwa na elimu ya masuala ya teknolojia kwa manufaa yao.

 

Kwa upande wake, Naibu Katibu Mkuu Umoja wa Vijana Taifa wa Chama Cha Mapinduzi Tanzania Bara na Mjumbe wa Halmashauri Kuu, Mussa Mwakitinya amesema  Ilani ya CCM inaweka wazi malengo ya Serikali kukuza uchumi wa Mtanzania na kuongeza ustawi wa jamii.


“ Ilani yetu imeeleza hapa kuwa Dkt. Samia ana mpango wa kumuona kila Mtanzania ana maisha mazuri, anatenga bilioni 99 kwa ajili ya wanawake na shilingi bilioni 96 kwa ajili ya vijana. Hapa Bukombe CCM italeta shilingi bilioni 2 kwa ajili ya mikopo,” amesema Mwakitinya.


Naye, Mgombea wa Udiwani Kata ya Butinzya, Kwizi Mathias amewaeleza wananchi hao kuwa endapo watawachagua wagombea wa CCM Oktoba 29 watahakikisha wanafanyia kazi changamoto chache zilizopo katika Kata hiyo ikiwemo upatikanaji wa maji.


Kwa upande wake, Mgombea Udiwani  wa Kata ya Igulwa, Richard Mabenga amewaomba wananchi hao kuendelea kumuamini na kumchagua tena katika nafasi ya udiwani.


Aidha, amesema waichague CCM kwa kuwa    pamoja na miradi mingine wamejenga shule ya sekondari ya Dkt. Biteko, sekondari ya amali ya Igulwa iliyogharimu shilingi milioni 580.


Sambamba na hayo wameanza kujenga mtandao wa  barabara za lami , wamechimba kisima, wamejenga Chuo Kikuu hivyo Oktoba 29 wananchi wawachague wagombea wa CCM.


Mwisho.

 MUHEZA WAKO TAYARI OKTOBA 29, 2025, DKT. SAMIA AWAOMBA KURA

MUHEZA WAKO TAYARI OKTOBA 29, 2025, DKT. SAMIA AWAOMBA KURA

September 29, 2025 Add Comment



Mgombea wa nafasi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Taifa Ndugu Dkt. Samia Suluhu Hassan akizungumza na wananchi wa Muheza katika muendelezo wa Kampeni za Uchaguzi kwa CCM mkoani Tanga tarehe 29 Septemba, 2025.

Wananchi wa Muheza wamekuwa na shauku. kubwa kumsikiliza Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi ambaye alishangiliwa wakati wote wa hotuba yake wakati akizungumza na kuomba kupigiwa kura za ndiyo katika uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani utakaofanyika nchini kote



Mgombea wa nafasi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Taifa Ndugu Dkt. Samia Suluhu Hassan akimkabidhi Ilani ya Uchaguzi Mgombea Ubunge wa Jimbo la Muheza Ndugu Hamis Mwijuma ‘Mwana FA’ mara baada ya kuwahutubia wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika Muheza mkoani Tanga tarehe 29 Septemba, 2025.

Matukio mbalimbali katika mkutano wa hadhara wa Kampeni za Uchaguzi kwa Chama cha Mapinduzi (CCM) uliofanyika Muheza mkoani Tanga tarehe 29 Septemba, 2025.

Sehemu ya wananchi wa Muheza mkoani Tanga waliohudhuria mkutano wa hadhara wa Kampeni za Uchaguzi kwa Chama cha Mapinduzi (CCM) tarehe 29 Septemba, 2025.