Showing posts with label afya. Show all posts
Showing posts with label afya. Show all posts

DKT. BITEKO AZINDUA TEKNOLOJIA YA KUONDOA UVIMBE MWILINI BILA UPASUAJI

August 27, 2025 Add Comment




📌 Ni kwa mara ya kwanza kufanyika Afrika Mashariki na Kati


📌 Aipa kongole Hospitali ya Kairuki kwa kutoa punguzo la asilimia 50 kwa wagonjwa 50 wa kwanza


📌 Asema Serikali itaendelea kuweka msukumo ushirikiano na Sekta binafsi


📌 Awaasa Watendaji Wizara ya Afya kutoogopa kujifunza pale Sekta binafsi inapofanya vizuri


📌 Wagonjwa 300  wanufaika na teknolojia ya utoaji uvimbe bila upasuaji


Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati


Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko ameziindua teknolojia ya kuondoa uvimbe mwilini bila upasuaji inayofahamika kama High-Intensity Focused Ultrasound (HIFU) katika Hospitali ya Kairuki ikiwa ni mara ya kwanza kwa huduma hiyo kuzinduliwa katika nchi za Afrika Mashariki na Kati.

Akizindua huduma hiyo Agosti 27, 2025 jijini Dar es Salaam, Dkt. Biteko amepongeza Watendaji wa hospitali ya Kairuki pamoja na muasisi wake Hubert Kairuki na Mkewe kwa uthubutu wao katika masuala mbalimbali ikiwemo utoaji wa huduma hiyo ya HIFU ambayo imeiweka Tanzania katika rekodi ya kutoa uvimbe bila kufanya upasuaji  barani Afrika suala ambalo pia litaongezea nchi mapato.

Ameeleza kuwa awali huduma ya HIFU barani Afrika likuwa ikipatikana katika nchi tatu tu ambazo ni Misri, Nigeria na Afrika Kusini.

Aidha, ameipongeza Hospitali ya Kairuki kwa kutoa punguzo la asilimia 50 la gharama za matibabu ya utoaji uvimbe bila upasuaji kwa wagonjwa 50 wa kwanza ndani ya kipindi cha mwezi mmoja kuanzia leo ikiwa ni kielelezo cha Watendaji wa hospitali hiyo kuonesha utu kwa Watanzania, kuacha alama njema na kuunga  mkono dhamira ya Serikali ya kutoa huduma kwa watanzania kwa gharama nafuu.

Dkt. Biteko amesema kuwa kufanyika kwa tukio hilo muhimu  ni kielelezo cha Serikali ya Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan kuipa msukumo sekta binafsi na kuikuza ili kutoa huduma za matibabu kwa wananchi kwa ufanisi na kusogeza karibu huduma ambazo hapo awali zilikuwa hazipatikani ndani ya nchi hivyo ameahidi kuwa Serikali itaendelea kuunga mkono Sekta binafsi.

·Aidha, ameipongeza Hospitali ya Kairuki kwa kuanzisha Idara ya huduma za dharura ambayo ina uwezo wa kuhudumia wagonjwa zaidi ya 9,000 kwa mwaka. 

Katika hatua, nyingine, Dkt. Biteko amewataka Watendaji katika Wizara ya Afya kutoogopa kujifunza kutoka Sekta binafsi pale inapofanya vizuri na wawape ushirikiano wakati wote siyo nyakati za ukaguzi tu kwani lengo la Serikali ni kufikisha huduma bora kwa wananchi kwa ushirikiano wa Serikali na sekta hiyo.


Kuhusu ombi la Hospitali ya Kairuki la kujengewa barabara ya lami ya mita 300 kuelekea kwenye hospitali hiyo ili kurahisisha utoaji huduma kwa wananchi ameelekeza Manispaa ya Kinondoni kufanyia kazi ombi hilo.

Dkt. Mwinyikondo Amir, kutoka Wizara ya Afya akimwakilisha Waziri wa Afya, amesema kuwa tukio hilo ni ishara ya ushirikiano uliopo kati ya sekta binafsi na Serikali katika kutoa huduma bora kwa wananchi.

Amesema Wizara ya Afya imekuwa na ushirikiano mkubwa na Hospitali ya Kairuki katika masuala mengi ikiwemo matumizi ya Bima ya Afya na kwamba pande zote mbili zinatambua kuwa zina wajibu wa kutekeleza dira ya maendeleo ya 2050 inayoelekeza uwepo wa jamii yenye afya bora.


Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Afya na Elimu Kairuki, Kokushubila Kairuki ameishukuru Serikali kwa kutambua mchango wa sekta binafsi katika kuboresha huduma za afya nchini.


Amesema sekta ya afya imekuwa na maendeleo makubwa chini ya uongozi wa  Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan na kwamba  hospitali hiyo itaendelea kuunga  mkono juhudi hizo hasa ikiwa ni utekelezaji wa Dira 2050 inayolenga kujenga Taifa lenye uchumi imara na afya bora.


Amesema gharama za kuweka teknolojia hiyo ya HIFU ni shilingi Bilioni 12 na milioni 300.

 

Aidha amesema kutoka huduma ya HIFU ianze kutolewa tayari wananchi 300 wamepata huduma za uchunguzi huku 298 wakipata matibabu.


 Awali, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Hospitali ya Kairuki,  

Dk. Onesmo Kaganda alisema uzinduzi wa HIFU ni tukio la kihistoria kwakuwa ni mara ya kwanza kwa huduma hiyo  kuzinduliwa  katika nchi za Ukanda wa Afrika Mashariki na Kati.


Amesema teknolojia hiyo barani Afrika  imeanzishwa katika nchi tatu tu ambazo ni Misri, Nigeria na Afrika Kusini.


Ameeleza kuwa HIFU ni Teknolojia ya kisasa inayotumia Mawimbi Sauti (Sound Waves) b kutibu aina mbalimbali za uvimbe mwilini bila upasuaji, ikiwemo uvimbe wa saratani na usiokuwa wa saratani katika maeneo kama Matiti, Kongosho, Kizazi kwa Wanawake, na Tezi Dume kwa wanaume.


Ameeleza  faida za huduma hiyo kuwa ni pamoja na kutokuwa na kovu kwa kuwa hakuna upasuaji, mgonjwa hawekewi nusu kaputi na mgonjwa hupona kwa muda mfupi na kurejea katika shughuli zake, matibabu hayahitaji kumwongezea damu mgonjwa hata kwa wagonjwa wenye upungufu wa damu, pia kupunguza gharama za kwenda nje ya nchi kutafuta matibabu.


Ameongeza kuwa, faida nyingine ya HIFU ni pamoja na tiba shufaa ambayo husaidia dawa za saratani kufanyakazi vizuri mwilini, kufubaza kukua kwa saratani mwilini (slowdown disease progression) na kupunguza maumivu kwa wagonjwa wa saratani. 


Amesema mtambo huo ulianza kufanya kazi desemba 2023 ambapo mpaka sasa wagonjwa 303 wamefanyiwa uchunguzi na 298 kupatiwa matibabu na kumekuwa na matokeo chanya ya wagonjwa hao.

Amesema kuwepo kwa teknolojia hiyo ni sehemu ya kuunga mkono juhudi za Serikali ya Tanzania kupitia Wizara ya Afya za kuifanya  Tanzania kuwa kitovu cha utalii Tiba Kusini mwa jangwa la Sahara.

Pia, amemshukuru Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan kuweka mazingira wezeshi ya ushirikiano kati ya Serikali na Taasisi Binafsi.

Kuhusu Idara ya Huduma za Dharura iliyozinduliwa katika Hospitali ya Kairuki amesema itakuwa  na uwezo wa kuhudumia wagonjwa zaidi ya 9000 kwa mwaka na pia imejizatiti kwa magonjwa ya dharura pindi yatakapotokea.


Mwisho

GIZ YATOA MSAADA WA VIFAA TIBA VYENYE THAMANI YA SHILINGI MILIONI 975 KATIKA HALMASHAURI ZA MKO WA TANGA

May 01, 2025 Add Comment



Na Oscar Assenga, TANGA

SERIKALI ya Ujerumani kupitia shirika la  ufadhili wa kimataifa nchini humo (GIZ) limetoa msaada wa  vifaa tiba vyenye thamani ya shilingi Milion 975 vitakavyotumika katika hospitali 20 zilizopo kwenye hamashauri mbalimbali Mkoani Tanga hii ikiwa ni  utekelezaji wa programu yake ya  kusaidia na kuimarisha sekta ya afya hapa nchini.

GIZ ambayo inashirikiana na  Wizara ya afya pamoja ofisi ya Rais tawala za mikoa na Serikali za mitaa (TAMISEMI)kwa lengo la kuboresha utoaji wa huduma  bora kwa mama na mtoto pamoja na afya ya uzazi  utekelezaji wake umeleta mabadiliko chanya  katika vituo vya afya vilivyoguswa na mpango huo ambao umeanzishwa muda mrefu.



Akipokea vifaa hivyo Mkuu wa mkoa wa Tanga Balozi Dkt Batilda Buriani ameipongeza Serikali ya Ujerumani  kupitia shirika la GIZ  ambapo kupitia msaada huo unakwenda kuongeza juhudi za Serikali katika kupambana kupunguza na kuondoa kabisa vifo vya wajawazito, wakinamama pamoja na watoto wachanga waliopo chini ya miaka mitano.

Alisema lengo kubwa la Rais ni kupunguza vifo vya wakina mama wajawazito na watoto wachanga chini ya miaka mitano na wameona mafanikio vifo vimepungua kwa kiasi kikubwa sana sasa wamewasaidia kupata vifaa hivyo ili kuongeza vifaa tulivyonavyo na kuhakikisha kwamba watoto wetu wanaozaliwa njiti , wanaozaliwa  na manjano , wanaozaliwa na changamoto ya upumuaji , wanakuwa salama wanapongeza na kuwashukuru kwa msaada huo



Aliongeza kuwa licha ya vifaa hivyo vilivyotolewa bado kuna uhitaji kutokana na idadi kubwa ya wananchi wanaohitaji kupatiwa huduma mbalimbali ambapo ametumia nafasi hiyo kuwaomba shirika la GIZ kuangalia uwezekano wa kuendelea kuwezesha upatikanaji wa wa vifaaa vingine.

" Tumekuwa na mazungumzo na tumekubaliana kwamba waongeze vifaa hivi ni kweli tumepata vingi lakini bado uhitaji ni mkubwa  tunaomba hivi vifaa vilivyopo viongezeke zaidi kutokana na idadi kubwa ya wahitaji tulionao katika vituo na hospitali zetu za halmashauri tuna imani kuwa tutaongezewa ili kuhakikisha kwamba huduma za wakina mama na watoto zinakwenda karibu zaidi na wananchi ikiwemo huduma za kibobezi" aliongeza.



Awali alizungumza Meneja wa  mradi huo hapa nchini Kai Strahler-Pohl  alipongeza juhudi za Serikali katika kuendelea kukabiliana na kupunguza  vifo vya watoto wachanga , kuboresha matokeo ya afya wakina mama na watoto, sambamaba na kuimarisha miundombinu ya vituo vya afya.

Alisema mpango huo umelenga katika  kuwezeshwa uwepo wa  vifaa tiba vya kutosha kwaajili ya kuanzisha vitengo vipya vya utoaji wa huduma  za utunzaji wa watoto wachanga (NCU) katika hospitali za wilaya zote zilizopo Mkoani Tanga .



" Tunafurahi sana kuimarisha  huduma katika halmashauri zote za mkoa wa Tanga hasa kuweza kuzipatia hospital vitengo  vya utunzaji wa watoto wachanga vinavyofanya kazi kikamilifu takribani wakazi 870,000 sasa wanaweza kuwa na uhakika  kwamba Kila mtoto mchanga mvulana na msichana atatunzwa  vizuri karibu na makazi yao"

" Tunathamini ushirikiano wa Serikali kupitia Wizara ya afya  , TAMISEMI, mikoa halmashauri za wilaya zote  pamoja na Serikali ya Ujerumani kukamilisha hili" alisema Meneja huyo.


Awali akizungumza Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga Bombo Dkt. Frank Shega alilishukuru shirika la GIZ kwa msaada huo ambao pia umeenda sambamaba na utoaji wa mafunzo ya utendaji wa kazi kwa baadhi ya watumishi kwa lengo la kuwaongezea maarifa na ujuzi katika utoaji wa huduma.



"Tunawashukuru na kuwapongeza sana wenzetu wa GIZ kwa  kutupatia msaada wa vifaa  hivi ambavyo vinakwenda kutusaidia kuhakikisha kuwa tunakuwa na vizazi hai na vyenye afya bora wamekuwa pia wakitoa mafunzo kwa watumishi kwaajili ya kuongeza weledi tumekuwa nao kwa muda mrefu na wamekuwa wadau wetu ambao wamwtusaidia sana" alisema Dkt Shega

Mwisho.

PAC YAIPONGEZA MSD KWA KUJENGA GHALA LA KISASA LA KUHIFADHIA BIDHAA ZA AFYA

March 14, 2025 Add Comment

 

 

Na Mwandishi Wetu.

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) chini ya Mwenyekiti wake, Mhe. Naghenjwa Kaboyoka (pichani) imetembelea  na kukagua maendeleo ya ujenzi wa mradi wa ghala la kisasa la kuhifadhia bidhaa za afya linalojengwa na Bohari ya Dawa (MSD) katika eneo la Kizota, Mkoani Dodoma.

Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Mhe. Kaboyoka ameipongeza MSD kwa kazi kubwa inayoifanya ya ujenzi wa ghala kubwa na kisasa ambalo litakwenda kutatua changamoto za utunzaji wa bidhaa za afya kwa kiasi kikubwa. 

"Kazi mnayoifanya inaonekana, leo tumeona uwekezaji mkubwa wa ghala la hili kubwa na la Kisasa ambalo lina Ubora wa kimataifa, serikali imewekeza hapa zaidi ya Bilioni 23.7 kujenga ghala hili lenye mita za mraba 7,200 sisi kama kamati tunategemea kuona changamoto za utunzaji wa bidhaa za afya zinapungua”.
Aidha pamoja na kupongeza ujenzi wa maghala Mhe. Kaboyoka amepongeza namna MSD inavyosambaza mashine za kusafisha damu kwa wagonjwa wa Figo ambazo zimepelekea kupunguza ghalama za huduma hiyo kwa wananchi. “Siku izi magonjwa ya figo yamekuwa mengi hadi watoto wadogo wanapata ugonjwa huo tunaishukuru MSD kwa kupunguza gharama ya huduma hii baada ya MSD kuanza kusambaza mashine za kusafisha damu sasahivi tunaona huduma hiyo imepungua gharama kwa kiasi kikubwa. 

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Bodi ya MSD Bi. Rosemary Silaa amesema MSD itaendelea na ujenzi wa Maghala mapya kwa lengo la kutatua changamoto za utunzaji wa bidhaa za afya ambapo baada ya ujenzi huu wa Dodoma na Mtwara MSD itaanza ujenzi wa maghala mapya mkoani Chato, Kilimanjaro, Dar es Salaam, Mwanza na Ruvuma.   MSD kwasasa inauwezo wa kutunza bidhaa hizo kwenye mita za mraba 56,000 huku MSD ikiwa na uhitaji wa mita za mraba 100,000 kukidhi mahitaji yake ya utunzaji.

PAC imetembelea  na kukagua maendeleo ya ujenzi wa mradi wa ghala la kisasa la kuhifadhia bidhaa za afya linalojengwa na Bohari ya Dawa (MSD) katika eneo la Kizota, Mkoani Dodoma.

RAIS DKT SAMIA ATOA MAELEKEZO KWA WAZIRI MCHENGERWA

February 23, 2025 Add Comment


Na Oscar Assenga, HANDENI.

RAIS Dkt Samia Suluhu amemuagiza Waziri wa Tamisemi Mohamed Mchengerwa kuhakikisha wanapeleka kiasi cha Milioni 240 kwa ajili ya kujenga eneo maalumu la Upasuaji wa Mifupa katika Hospitali ya Halmashauri ya wilaya ya Handeni.

Dkt Samia aliyasema hayo leo mara baada ya kufungua Hospitali ya Halmashauri ya wilaya ya Handeni eneo la Mkata ikiwa ni ziara ya siku saba katika Mkoa wa Tanga yenye lengo la kukagua miradi ya maendeleo, kuweka mawe ya msingi na kuzungumza na wananchi.

Alisema kwa sababu wanataka Handeni kuwa eneo maalumu kwa ajili ya Hospitali ya Mifupa pamoja na kuwepo na tiba mbalimbali lakini libaki kuwa maalumu kwa ajili ya mifupa

Aidha alisema kwamba mpaka sasa Hospitali hiyo imeshapokea wajawazito 900 na 300 walijifungua kwa upasuaji na iwapo isingekuwepo lazima kungekuwa na Rufaa na hivyo uwepo wa hospitali hiyo umeokoa maisha ya watu wengi.

Alisema hospitali hiyo ipo barabarani na wakiweka lami kipande kinachotoka Barabarani kwenda hosputali itakuwa karibu na wameamua kujenga aeneo la kufanya upasuaji wa mifupa na ameilekeza Waziri Tamisema aleta fedha milioni 240 ili kujenga eneo la mifupa likamilike,

“Ukiangalie kuna maeneo ya upasuaji mawili eneo la upasuaji ,upauaji wa jumla na mifupa na hakuna wodi na wanalazwa na wagonjwa wengine hivyo ni vema sehemu ya mifupa ikabakia pekee yake na Handeni ikiwa Hospitali maalumu kwa ajili ya mifupa na mambo mengine na watu wengine wake na wagonwa wengine wa mifupa na maeneo mengine waje kupata huduma”Alisema

Rais Dkt Samia aliawapongeza wana kijiji na uongozi wa kijiji cha Mkata Mashariki kwa kutoa eneo la ekari 32 kwa ajili ya ujenzi wa Hospitali hiyo huku akieleza jambo hilo ni la kuigwa kwani kama wangesubiri Serikali itoe eneo pengine mradi ungeweza kuchelewa.

“Mbali na hayo awamu ya sita Serikali katika wilaya ya Handeni wamepeleka Bilioni 4.37 kwa ajili ya Hospitali hiyo na fedha walizipeleka kwa ajili ya kujenga vituo vya afya na zahanati 16 kwa hiyo ni dhamira ya serikali kuwakinga wananchi wasipatwe na magonjwa .

“Ikitokea wanahitaji matibabu wapate huduma za uhakika zilizokaribu nao ndio maana wameendelea ujenzi wa Hospitali hiyo na kuleta vifaa vya kisasa kwa mkoa wa mzima “Alisema

Alisema kwamba wananchi wa handeni wanamshukuru kwa kazi kubwa anayoifanya ya kuliunganisha Taifa na wannachi ikiwemo kuwapeleka wadau ambao waliwashika mkono wakajenga majengo mbalimbali na kuifanya hospitali hiyo kwa bora na yenye viwango vya hospitali ya mkoa.

Mchengerwa alisema ujenzi wa jengo hilo ni mpango wa Serikali kuendelea kusogeza huduma karibu na wananchi na maelekezo ya Rais Dkt Samia Suluhu ya kuelekeza kwamba yajengwe majengo kwa ajili ya kuwahudumia wananchi wa handeni na hiyo ni kazi kubwa ya kuunganisha Taifa na mahusiano na watu mbalimbali duniani.

“Wananchi walipata bahati ya kupata wadau wa maendeleo kutushika mkono na kujenga majengo mbalimbali na kuifanya Hospitali yetu kuwa bora na yenye viwango vya Hospitai ya mkoa na kazi hiyo imekwenda kuokoa maisha ya watoto, wakina mama wanaokwenda kujifungua na maisha ya wapiti njia”Alisema

Hata hivyo alisema kwamba Serikali imewezesha ujenzi wa Majengo 15 ya huduma za maabara, majengo muhimu za huduma za nje, huduma za dharura, huduma za mionzi,jingo la huduma za wuzazi ,jengo la dawa na kipindi cha muda mfupi umweza kuokoa maisha ya wakina mama na watoto.

“Mhe Rais Sekta ya Afya inafanya kazi kubwa ya kuokoa maisha ya wakina mama na watoto na wilaya ya Handeni hakuna kifo cha mama na mtoto na wahudumu katika sekta hii wamebadilika na wanafanya kazi kwa bidii kuhakikisha wanaokoa maisha ya watanzania.

Hata hivyo alisema katika Mkoa wa Tanga fedha ambazo zilitolewa na Serikali kwenye sekta ya afya wametoa Bilioni 65.6.


RAIS DKT SAMIA KUPOKEA TUZO YA "THE GATES GOALKEEPERS AWARD

February 03, 2025 Add Comment


Na WAF - Dar Es Salaam

 

Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan anatarajia kupokea tuzo ya “The Gates Goalkeepers Award” kama kielelezo cha matokeo makubwa ambayo yamepatikana kwenye uongozi wake kufuatia ripoti ya utafiti wa demografia na afya ya mwaka 2022 inayoonesha kupungua kwa vifo vitokanavyo na uzazi kwa asilimia 80.

 

Waziri wa Afya Mhe. Jenista Mhagama amesema hayo  Februari 3, 2025 wakati akitoa taarifa ya upokeaji wa tuzo hiyo ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan zinazoandaliwa na taasisi ya The Gates Foundation, mbele ya waandishi wa habari kwenye ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam.


Waziri Mhagama amesema tukio hilo linafanyika nje ya Marekani nchini ya Tanzania kwa mara ya kwanza na Rais Samia ndiye kiongozi wa kwanza kupokea tuzo hiyo kwa bara la Afrika jambo lililochochewa na uongozi wake mahiri ulioleta mafanikio makubwa nchini hususani ni sekta ya afya kwa kuitendea haki na kusababisha mataifa makubwa duniani kutambua mchango wake.

 

Amesema kuwa mafanikio haya yametokana na mikakati mbalimbali iliyotekelezwa na inayoendelea kutekelezwa kutokana na utashi wa kisiasa chini ya uongozi wa Rais Dkt. Samia kuweka mazingira wezeshi kisera pamoja na  kuimarisha rufaa za akina mama na watoto. 

 

“Rais Samia ameongeza bajeti ya kuimarisha huduma ikiwemo upatikanaji wa dawa na vifaa tiba, kusogeza huduma za dharula za uzazi karibu na wananchi kwa kujenga zaidi ya vituo 530 vya upasuaji wa kutoa mtoto tumboni,” amesema Waziri Mhagama

 

Waziri Mhagama ameipongeza Taasisi ya The Gates Foundation kwa kutambua na kuunga mkono juhudi za serikali kwenye kupambana na vifo vitokanavyo na uzazi, Watoto wachanga na walio na umri chini ya miaka mitano (5).

 


“Kwa namna ya kipekee, tunatambua jitihada za kipekee za Amiri jeshi Mkuu Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mapambano ya vifo vya kina mama vinavyotokana na uzazi, vifo vya Watoto wachanga na Watoto walio chini ya miaka mitano, hivyo wananchi wenzangu tunayo kila sababu ya kumpongeza na kutembea kifua mbele kwa jinsi Mheshimiwa Rais anavyotung’arisha nchi yetu nje ya mipaka ya nchi yetu,” amesema Waziri Mhagama