Showing posts with label michezo. Show all posts
Showing posts with label michezo. Show all posts

BARRICK BULYANHULU YAENDELEA KUDUMISHA UHUSIANO MZURI NA JAMII KUPITIA JUKWAA LA MICHEZO

October 15, 2025 Add Comment

 


Mchezo kati ya timu ya Mgodi wa Barrick Bulyanhulu na Sixers ukiendelea 

Mchezo kati ya timu ya Mgodi wa Barrick Bulyanhulu na Sixers ukiendelea
Mchezo kati ya timu ya Mgodi wa Barrick Bulyanhulu na Sixers ukiendelea
Wachezaji timu ya Mgodi wa Barrick Bulyanhulu na Sixers wakiwa katika picha ya pamoja kabla ya mchezo

***
Mgodi wa Barrick Bulyanhulu uliopo katika halmashauri ya wilaya ya Msalala mkoani Shinyanga, umeendelea kujenga uhusiano mzuri na jamii za maeneo yanaozunguka mgodi kupitia jukwaa la michezo ambapo Oktoba 14,2025 timu ya mpira wa kikapu inayoundwa na wafanyakazi wa mgodi iliikaribisha timu ya Sixers kutoka Kahama katika mechi ya kirafiki ambapo Bulyanhulu imeibuka na ushindi wa vikapu 33-30.

MASHINDANO YA NGALAWA YATUMIKA KUHAMASISHA USALAMA WA CHAKULA

October 13, 2025 Add Comment


Na Mwandishi Wetu, TANGA


MBIO za ngalawa baharini, zikijumuisha timu 12, zimekuwa kivutio katika Maadhimisho ya 44 ya Siku ya Chakula Kimataifa, ambapo hapa nchini, yanafanyika mkoani Tanga.


Mashindano hayo yaliyoratibiwa na Serikali kwa kushirikiana na Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa (FAO) na wadau wengine, yamefanyika jana kwenye ufukwe wa Deep Sea jijini Tanga.

Kwenye shindano hilo lililofanyika kwenye umbali wa jumla ya kilomita 12 majini, nafasi ya kwanza ilichukuliwa na timu namba 010 iliyoongozwa na Idd Kileo na kusafiri kwa dakika 48:30.


Timu namba 012 iliyoongozwa na Amir Seleman ilichukua nafasi ya pili kwa kutumia dakika 48:49 wakati nafasi ya tatu ilichukuliwa na timu namba 009, ikiongozwa na Mahamud Rashid na ilitumia dakika 49:20.

Washindi hao watatunukiwa zawadi za ushindi kwenye kilele cha Siku ya Chakula Kimataifa Oktoba 16, 2025 na Mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Waziri Mkuu, Mhe Kassim Majaliwa. 


Timu nyingine zilizoshiriki na viongozi wake kwenye mabano ni  namba 002 (Halfan Mnyeto), 007 (Mohamed Salim), 003 (Hamza Nguzo), 008 (Hussein Seif), 011 (Veso Kileo), 005 (Akida Koja), 001 (Kassim Abdi) na 006 (Jumaa Kibao).


Kaimu Mkurugenzi wa Mifugo kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Nankondo Senzira, amesema mashindano hayo ni kilelezo cha ukweli kuwa uvuvi una mchango mkubwa katika ajira, lishe bora, kipato na fedha za kigeni.

Hivyo, amesema muhimu kuwepo ubunifu kama kufanyika kwa mashindano na kuwazawadia wavuvi ili kuonesha thamani na kuongeza tija katika shughuli zao.


Ametoa mfano kuwa mwaka 2024, uvuvi ulichangia asilimia 1.8 ya pato la taifa huku ikitoa ajira kwa Watanzania takribani milioni 6.


Mwakilishi Msaidizi wa FAO, Charles Tulahi, alisema mashindano hayo yanaendelea mpango wa kuzitafakari changamoto dhidi ya uzalishaji wa chakula ikiwemo mabadiliko ya tabia nchi, migogoro, gharama za maisha na kupungua kwa rasilimali kama ardhi, maji na bioanuai.


“Mashindano haya ya ngalawa siyo tu burudani, yana ujumbe kuhusu umuhimu wa Bahari na sekta ya uvuvi katika kuhakikisha usalama za chakula, lishe bora na ajira kwa jamii zetu,” alisema.


Alisema, yamefanyika kwenye Bahari ya Hindi iliyo hazina kubwa ya maliasili kwa samaki na viumbe wengine ambavyo ni chanzo cha protini, mafuta yenye afya na madini yanayosaidia ukuaji wa mwili na ubongo.


Risala ya washiriki wa shindano hilo ilieleza kuwa, wavuvi walitumia mwelekeo wa upepo, mawimbi na mbinu za jadi, na hivyo kuwawezesha kumaliza salama kwa kila mmoja wao.


Kwa mujibu wa risala hiyo, mashindano hayo yameonesha azma ya Serikali na wadau wake kuwatambua, kuwathamini na kuwashirikisha wavuvi wanaojinasibu kuwa mashujaa wa chakula na afya za watu nchini.


MWISHO

CCM YAFANYA BONANZA KUHAMASISHA WANANCHI KUSHIRIKI UCHAGUZI KWA AMANI

October 07, 2025 Add Comment



Mgeni rasmi katika bonanza hilo alikuwa Mwenyekiti wa UWT Taifa, Mary Pius Chatanda,mgombea ubunge wa Jimbo la Segerea, Bonnah Kamoli na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa (MNEC) na Mratibu wa Kampeni za CCM Mkoa wa Dar es Salaam, Richard Kasesela kwa pamoja walihimiza kufanya mazoezi kila siku na kupiga kura siku ya uchaguzi mkuu kwa amani na utulivu

Mgeni rasmi katika bonanza hilo alikuwa Mwenyekiti wa UWT Taifa, Mary Pius Chatanda,mgombea ubunge wa Jimbo la Segerea, Bonnah Kamoli na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa (MNEC) na Mratibu wa Kampeni za CCM Mkoa wa Dar es Salaam, Richard Kasesela kwa pamoja walihimiza kufanya mazoezi kila siku na kupiga kura siku ya uchaguzi mkuu kwa amani na utulivu

Na Fredy Mgunda.


Chama cha Mapinduzi (CCM) kimeandaa Bonanza Maalum katika Jimbo la Segerea, mkoani Dar es Salaam, kwa lengo la kuhamasisha wananchi kujitokeza kwa wingi kushiriki Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Oktoba 29, kwa njia ya amani na utulivu.

Mgeni rasmi katika bonanza hilo alikuwa Mwenyekiti wa UWT Taifa, Mary Pius Chatanda, ambaye aliwataka wananchi kutumia haki yao ya kidemokrasia kwa kupiga kura kwa amani, akisisitiza kuwa kiongozi anayechaguliwa leo ndiye atakayekuwa na mamlaka ya kuleta maendeleo kwa miaka mitano ijayo.

“Kupiga kura ni haki ya msingi kwa kila Mtanzania. Tuchague viongozi wanaotuletea maendeleo ya kweli,” alisema Chatanda.

Akimnadi mgombea urais wa CCM, Dkt. Samia Suluhu Hassan, Chatanda alisema kuwa serikali ya awamu ya sita imeitekeleza ilani ya CCM ya mwaka 2020-2025 kwa asilimia 100, na hivyo anastahili kupewa tena ridhaa ya kuendelea kuongoza nchi.

Aidha, alitoa wito kwa wananchi kumchagua mgombea wa CCM katika nafasi ya urais, ubunge na udiwani ili kuimarisha juhudi za maendeleo nchini.

Kwa upande wake, mgombea ubunge wa Jimbo la Segerea, Bonnah Kamoli, alisisitiza kuwa mojawapo ya sera zake ni kuhamasisha mazoezi ya mara kwa mara kwa wananchi, ili kuboresha afya ya mwili na akili.

“Afya bora ni msingi wa maendeleo. Tukifanya mazoezi tutakuwa na nguvu za kushiriki kikamilifu katika ujenzi wa taifa,” alisema Kamoli.

Kamoli aliwaomba wakazi wa Segerea kumpigia kura nyingi pamoja na kumpa kura ya kishindo Dkt. Samia Suluhu Hassan, ili kuendeleza kasi ya maendeleo katika jimbo hilo.

Naye Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa (MNEC) na Mratibu wa Kampeni za CCM Mkoa wa Dar es Salaam, Kasesela, aliwataka wananchi kupuuza wanasiasa na wanaharakati wanaotumia mitandao ya kijamii kuchochea vurugu na hofu wakati huu wa uchaguzi.

“Wachochezi wengi wapo nje ya nchi. Vurugu zikitokea, ni Watanzania waliopo hapa ambao watateseka. Amani ni tunu ya taifa letu,tuilinde,” aliongeza Kasesela.

Katika bonanza hilo, wananchi walishiriki katika michezo mbalimbali, burudani, na kupata elimu juu ya umuhimu wa kushiriki uchaguzi kwa njia ya amani.

MENEJA WA TRA DODOMA AONGOZA BONANZA LA MICHEZO KWA WATUMISHI

MENEJA WA TRA DODOMA AONGOZA BONANZA LA MICHEZO KWA WATUMISHI

October 05, 2025 Add Comment

 

 

Dodoma

Meneja wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Mkoa wa Dodoma, Bw. Pendolake Elinisafi, ameongoza watumishi wa mamlaka hiyo kushiriki katika bonanza maalum la michezo lililolenga kujenga na kuimarisha afya pamoja na kuongeza mshikamano miongoni mwao.

Bonanza hilo lililofanyika katika viwanja vya Kilimani Park jijini Dodoma, limehudhuriwa na watumishi kutoka vitengo mbalimbali vya TRA na lilipambwa na michezo ya kuvutia ikiwemo mpira wa miguu, kuvuta kamba, mbio za magunia, kukimbiza kuku, kutembea na yai kwenye kijiko, na mpira wa pete.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa bonanza hilo, Bw. Elinisafi alisisitiza umuhimu wa michezo katika kujenga afya bora na kuimarisha mahusiano kazini. “Michezo ni njia mojawapo ya kuimarisha afya ya mwili na akili, lakini pia huchangia katika kujenga mshikamano na ari ya kufanya kazi kwa pamoja kama timu,” alisema.

Watumishi walionekana kufurahia michezo hiyo ambayo iliibua ushindani wa kirafiki na kuongeza furaha, huku ikidhihirisha umuhimu wa matukio ya kijamii kazini. Washiriki walitunukiwa zawadi mbalimbali kama sehemu ya kutambua ushiriki wao na kuwahamasisha kuendelea na utamaduni wa kushiriki michezo kazini.

Bonanza hilo limeonesha kuwa, mbali na majukumu ya kikazi, TRA inatambua umuhimu wa shughuli za kijamii na kiafya kwa ustawi wa watumishi wake.

OSHA YAKABIDHI VIFAA CHUO CHA UFUNDI MIRONGO JIJINI MWANZA

September 19, 2025 Add Comment

 

Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana, Mhe. Amina Makilagi, akiwasilisha hotuba yake wakati wa Bonanza la OSHA la Huduma kwa Jamii (OSHA CSR BONANZA 2025) lililofanyika katika viwanja vya Shule ya Msingi Nyakabungo Jijini Mwanza akiwa ni Mgeni Rasmi wa Bonanza hilo. Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana, Mhe. Amina Makilagi na Mtendaji Mkuu wa OSHA, Bi. Khadija Mwenda wakimkabidhi Mkuu wa Chuo cha Ufundi cha Mirongo vifaa mbalimbali vya msaada vilivyotolewa na OSHA kukiwezesha chuo hicho. Vifaa vilivyotolewa ni pamoja na kompyuta, makoti ya usalama na vifaa vya michezo. 

Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana, Mhe. Amina Makilagi na Mtendaji Mkuu wa OSHA, Bi. Khadija Mwenda wakimkabidhi Mkuu wa Chuo cha Ufundi cha Mirongo vifaa mbalimbali vya msaada vilivyotolewa na OSHA kukiwezesha chuo hicho. Vifaa vilivyotolewa ni pamoja na kompyuta, makoti ya usalama na vifaa vya michezo.
Mwenyekiti wa timu ya OSHA Iliyoshiriki SHIMIWI mwaka 2025 Ndugu Charles Mhilu akimkabidhi kikombe  Mtendaji Mkuu wa OSHA Bi Khadija Mwenda, mara timu hiyo ya OSHA kuibuka timu Bora yenye nidhamu miongoni mwa timu 50 shindani kwenye mashindano yailyoshirikisha zaidi ya timu 50 toka taasisi,wakala za Serikali na Timu toka RAS mashindano yaliyofanyika hivi karibuni jijini Mwanza.

Na  Fredy Mgunda,Kwanza.


Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana, Mheshimiwa Amina Makilagi, amewataka waajiri na wafanyakazi kote nchini kuitekeleza kikamilifu Sheria ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi Na. 5 ya mwaka 2003 ili kupunguza au kuondoa kabisa ajali na magonjwa yanayotokana na mazingira duni ya kazi.


Mheshimiwa Makilagi alitoa wito huo jana wakati wa Bonanza la OSHA la Huduma kwa Jamii (OSHA CSR Bonanza 2025) lililofanyika katika viwanja vya Shule ya Msingi Nyakabungo, Wilaya ya Nyamagana, Jijini Mwanza. Bonanza hilo lilihusisha shughuli mbalimbali za kijamii na michezo kwa lengo la kuimarisha mshikamano kati ya OSHA na jamii inayohudumiwa, pamoja na kutoa msaada kwa wanafunzi wa Chuo cha Ufundi Mirongo, wakiwemo wenye ulemavu.


Katika tukio hilo, OSHA ilikabidhi vifaa mbalimbali kwa Chuo cha Ufundi Mirongo, vikiwemo kompyuta, vifaa kinga vya usalama kazini, pamoja na vifaa vya michezo kama mipira na jezi za michezo.


Akizungumza kama Mgeni Rasmi, Mheshimiwa Makilagi aliipongeza OSHA kwa juhudi zake za kuhakikisha mazingira salama na yenye afya sehemu za kazi na kuonesha moyo wa huruma kwa makundi maalum katika jamii.


“Nitoe rai kwa waajiri na wafanyakazi nchini kuisoma na kuitekeleza Sheria Na. 5 ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi ya mwaka 2003. Sheria hii ikitekelezwa ipasavyo, maeneo ya kazi yatakuwa salama, bila ajali wala magonjwa, hivyo kuongeza tija kazini,” alisema Mkuu wa Wilaya Makilagi.


Aidha, aliihakikishia OSHA ushirikiano wa Halmashauri na Ofisi yake katika kusimamia usajili na ukaguzi wa maeneo ya kazi, sambamba na kutoa ushauri wa kitaalamu juu ya maboresho ya mazingira ya kazi.


Kwa upande wake, Mtendaji Mkuu wa OSHA, Bi. Khadija Mwenda, alisema Bonanza hilo ni sehemu ya mpango wa taasisi hiyo wa kurudisha kwa jamii (Corporate Social Responsibility) na kwamba msaada uliotolewa kwa Chuo cha Mirongo umetokana na tathmini iliyofanywa na wataalam wa OSHA baada ya kutembelea chuo hicho.


“Tunaamini kuwa kwa kusaidia vyuo vya ufundi kama Mirongo, tunachangia kwa kiasi kikubwa maandalizi ya wataalamu wa baadaye katika fani muhimu za kiufundi na kazi,” alisema Bi. Mwenda.


Kaimu Mkuu wa Chuo cha Mirongo, Bi. Herieth Richard, pamoja na mwanafunzi wa fani ya ushonaji, Bi. Aneth Augustino, waliishukuru OSHA kwa msaada huo ambao wamesema umeongeza ari ya kujifunza na kushiriki katika shughuli za kijamii.


Bonanza hilo lilihusisha michezo ya mpira wa miguu, mpira wa pete, riadha, na michezo ya jadi kama kukimbia kwenye magunia, kukimbia na ndimu kwenye kijiko, rede na kukamata kuku. Washiriki walitoka OSHA na vyuo vya Ufundi vya Mirongo, Nyakato na Kisesa.


Chuo cha Ufundi Mirongo kinamilikiwa na Serikali chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), na hutoa mafunzo ya umeme, useremala, ushonaji na uchomeleaji kwa vijana wakiwemo wenye mahitaji maalum.