Showing posts with label michezo. Show all posts
Showing posts with label michezo. Show all posts

MCC RAJAB AWAKABIDHI AFRICAN SPORTS BASI JIPYA, AHAIDI KUENDELEA KUISAPOTI IREJEE LIGI KUU

January 25, 2026 Add Comment


Na Oscar Assenga,TANGA

MJUMBE wa Kamati Kuu ya CCM Taifa na Mwenyekiti wa  Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Tanga  Rajabu Abdurhaman amesema ana dhamira ya dhati kurejesha timu ya mpira wa miguu, African Spots ya jijini humo ili kurejesha heshima ya timu hiyo kongwe pamoja na Daby ya Tanga iliyokuwa na upinzani mkubwa hapa nchini.



Alisema timu hiyo imekuwa ikisuasua kupanda daraja kwa muda mrefu kutokana na changamoto mbali mbali ikiwemo basi la kuwasafirisha wachezaji pamoja na benchi la ufundi hivyo uwepo wa basi hilo utasaidia kuwawezesha kuondokana nazo


Aliyasema hayo Januari 24 mwaka huu katika hafla ya kuukabidhi uongozi wa timu hiyo gari Jipya aina ya TATA lililogarimu takribani shilingi Milioni 170, katika hafla iliyofanyika Makao Makuu ya Klabu hiyo barabara 12 Jijini Tanga .

Rajabu ambaye  pia ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Taifa (MCC) alisema kwamba kurudi kwa timu hiyo  kongwe hapa nchini ambayo ilianzishwa mwaka 1936 kutarejesha heshima ya Mkoa wa Tanga kutokana na kwamba bila African Spots hakuna Coastal Union inayochangiwa na utani wa  jadi timu hizo kama ilivyokuwa Simba na Yanga za Jijini Dar es Salaam.


Mbali ya kununua basi na kukabidhi, Mwenyekiti ameahidi kusaidia timu hiyo na kuiinua hadi kufikia kucheza ligi kuu ambapo ataipambania na kujenga Jengo la Ofisi la Gorofa tatu ikiwa ni pamoja na kununua gari kubwa zaidi wakati gari iliyokabidhiwa kubaki kuwa ya kuwapeleka wachezaji mazoezini.


Sambamba na kukabidhi gari hilo mwenyekiti huyo pia alitoa kiasi cha shilingi Milioni 30 na kukabidhi kwa uongozi wa timu ya Coastal Union kwa ajili ya kutatua changamoto kadhaa zinazowakabili.


Awali akizungumza katika Halfa hiyo Rais wa TFF  Walles Karia aliwasihi wanachama kushirikiana na vionhozi ili kufanya maamuzi pamoja na kujitokeza uwanjani pindi timu zitakapokuwq zancheza kwani ndio jambo sahihi la kuvuta wawekezaji.


Lakini pia aliwasihi viwanja vya michezo vilivyopo Myanjani Technically Center, "kile kituo kipo na kinafanya vizuri sana lakini kinanufaisha vijana walioko nje ya Tanga, niwasiji kwamba mpeleke vijana pale ili timu zetu zipate wachezaji bora" alisema Karia.

Katika hafla hiyo alikuwepo Naibu Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Hamisi Mwinjuma (Mwana FA) ambaye alisisitiza suala la wanachama kushirikiana na vionhozi wa timu hiyo na kuchangia kipato kwenye timu matokeo yataonekana.

"Kama tutakuwa na timu mbili (2) zinazoenda ligi kuu, hata uchumi wa Tanga utaimarika kupitia michezo, tuchangie timu kwa kwenda uwanjani na hata kununua jezi, kwa kufanya hivyo kutaimarisha timu zetu na wachezaji kuwa na ari uwanjani" alisema.

Katika kuinua timu hizo Naibu Waziri Mwana FA alitoa kiasi cha shilingi Milioni 10 ambapo kila timu imekabidhiwa kwa vionhozi wa timu zote mbili kiasi cha shilingi Milioni 5.

Rais Karia amewahakikishia Watanzania kwamba timu ya African Spots ikismama imara kama awali na Coastal Union ndiyo timu pekee ambazo zina uwezo wa kusimamishana na Simba na Yanga na siyo timu nyingine.

Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Balozi, Dk. Batilda Buriani aliwataka vionhozi wa timu za mipira na wanamichezo wote kutumia fursa ambazo zipo mkoani humo katika kuimarisha timu na kuleta manufaa katika Mkoa.

"Mradi wa Bomba la mafuta nao una fursa katika michezo, kule Uganda wamesaidia kujenga uwanja wa mpira, na hata timu yetu ya Coastal Union imeshapeleka maombi yake tunasubiri utekelezaji mwengine uendelee" alisema

WAZIRI MAKONDA AKABIDHI BARUA YA RAIS DKT. SAMIA KWA RAIS WA CAF

January 20, 2026 Add Comment









WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mheshimiwa Paul Christian Makonda amekutana na Rais wa Shirikisho la Kandanda Barani Afrika (CAF) Dkt. Patrice Motsepe Jijini Rabat, Morocco na kukabidhi barua kutoka kwa Rais Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan.


Pamoja na kukabidhi barua hiyo Mheshimiwa Makonda aliyeongozana na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo na Msemaji Mkuu wa Serikali Bw. Gerson Msigwa amemhakikishia Dkt. Motsepe kuwa Rais Samia yupo tayari wakati wote kushirikiana na CAF katika utekelezaji wa mipango mbalimbali ya maendeleo ya kandanda ikiwemo mashindano mbalimbali.


Amesema Tanzania imepiga hatua kubwa katika maandalizi ya kuwa wenyeji wa AFCON 2027 sambamba na Kenya na Uganda na kwamba imedhamiria kuonesha tofauti kubwa na mashindano yaliyopita.


Aidha, Makonda amemuomba Dkt. Motsepe kuiangalia Tanzania kimkakati ili mipango inayowekwa na Serikali ipate mafanikio makubwa yanayotarajiwa.


Kwa upande wake Dkt. Motsepe amemshukuru Rais Samia kwa kumuandikia barua na salamu zake za upendo na ushirikiano kwa CAF na amemhakikishia kuwa CAF ipo tayari kufanya kazi bega kwa bega na Tanzania ili kufikia maendeleo makubwa katika kandanda.


Motsepe ameelezea kufurahishwa na jitihada kubwa zilizofanywa na Rais Samia na Serikali anayoiongoza katika maendeleo ya mpira ikiwemo ujenzi wa miundombinu, kufanya mashindano ya CHAN 2024 kwa mafanikio makubwa na maandalizi mazuri yanayoendelea kuelekea AFCON 2027.


Amesema CAF itatuma timu ya wataalamu kwenda Tanzania kushirikiana na Serikali na wadau mbalimbali katika kukamilisha maandalizi makubwa ya AFCON 2027 ambayo yanatarajiwa kushirikisha nchi 28 badala ya 24.


Motsepe ameahidi kuja Tanzania hivi karibuni kujionea maandalizi mbalimbali ya AFCON 2027 na kukutana na viongozi kwa mazungumzo.


MAGAMBA FOREST WALKATHON AND ADVENTURE SEASON III KUFANYIKA DESEMBA 17 HADI 20 MWAKA HUU

December 16, 2025 Add Comment



Na Oscar Assenga, LUSHOTO.

MATEMBEZI Maalumu ndani ya Hifadhi ya Misitu ya Mazingira Asilia Magamba (Magamba Forest Walkathon and Andventure Season 111) yenye lengo la kutangaza na kuhamasisha utalii zinatarajiwa kufanyika Desemba 17 -20 katika mji wa Lushoto mkoani Tanga huku maandalizi yakielezwa kukamilika kwa asilimia 85.

Akizungumza na Mtandao huo Mhifadhi Mkuu wa Hifadhi ya Misitu ya Mazingira Asilia Magamba, Christoganus Vyokuta amesema kwamba kuelekea mbio hizo wadau mbalimbali wa uhifadhi na utalii watapata fursa ya kujitangaza na kuonesha huduma na bidhaa zao mjini Lushoto.

Alisema kilele cha mbio hizo kitafanyika Desemba 20 ambapo washiriki watashiriki katika matembezi maalumu ndani ya Hifadhi ya Misitu ya Magamba ikiwa ni sehemu ya kutangaza pia vivutio vya utalii vilivyopo ndani ya hifadhi ya Mazingira Asilia ya Magamba wilayani humo

Mhifadhi huyo alisema pia lengo jingine la mbio hizo za Magamba Forest Walkathon and Adventure Season III ni kuunga mkono juhudi za Serikali katika uhifadhi wa mazingira na kukuza utalii ikolojia ikiwemo kuhamasisha Watanzania kutembelea vivutio vya asili vilivyopo nchini.

Mhifadhi huyo amewataka wananchi na wadau wa sekta ya utalii kujitokeza kwa wingi kushiriki katika mbio hizo huku akisisitiza kuwa ushiriki wao ni muhimu katika kulinda rasilimali za asili na kuhakikisha uhifadhi endelevu kwa manufaa ya kizazi cha sasa na kijacho.

TIMU YA MPIRA WA WAVU (VOLLEYBALL) YA WANAUME YA REA YAANZA KWA KISHINDO MASHINDANO YA SHIMMUTA

TIMU YA MPIRA WA WAVU (VOLLEYBALL) YA WANAUME YA REA YAANZA KWA KISHINDO MASHINDANO YA SHIMMUTA

November 27, 2025 Add Comment

TIMU  ya mpira wa wavu ya wanaume ya Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imeanza mashindano ya Shirikisho la Michezo la Mashirika ya Umma, Taasisi na Makampuni Binafsi Tanzania (SHIMMUTA) kwa kishindo baada ya kuibuka na ushindi mkubwa dhidi ya timu ya Mamlaka ya Udhibiti wa Mbolea (TFRA).

Katika mchezo uliochezwa leo Novemba 27, 2025 katika viwanja vya Bwalo Mkoani Morogoro, wachezaji wa timu ya REA walionyesha kiwango cha juu cha mchezo na kasi iliyowaduwaza wapinzani wao, na hivyo kuweza kuwagaragaza TFRA kwa ushindi wa seti 2 kwa 1.

Ushindi huu wa mwanzo unatoa motisha kubwa kwa timu ya REA kuelekea michezo mingine, huku wakiwa na matumaini ya kutwaa ubingwa katika mashindano hayo yanayoendelea mkoani Morogoro.

Kocha wa timu hiyo alieleza kuridhishwa na juhudi za wachezaji wake na kuahidi kuendelea kuweka mikakati imara ili kuhakikisha REA inasalia kileleni mwa kundi hilo gumu.

Timu hiyo ambayo imeshiriki mashindano hayo kwa mara ya kwanza imeonekana kuwavutia mashabiki wengi waliokuwa katika viwanja hivyo.

BARRICK BULYANHULU YAENDELEA KUDUMISHA UHUSIANO MZURI NA JAMII KUPITIA JUKWAA LA MICHEZO

October 15, 2025 Add Comment

 


Mchezo kati ya timu ya Mgodi wa Barrick Bulyanhulu na Sixers ukiendelea 

Mchezo kati ya timu ya Mgodi wa Barrick Bulyanhulu na Sixers ukiendelea
Mchezo kati ya timu ya Mgodi wa Barrick Bulyanhulu na Sixers ukiendelea
Wachezaji timu ya Mgodi wa Barrick Bulyanhulu na Sixers wakiwa katika picha ya pamoja kabla ya mchezo

***
Mgodi wa Barrick Bulyanhulu uliopo katika halmashauri ya wilaya ya Msalala mkoani Shinyanga, umeendelea kujenga uhusiano mzuri na jamii za maeneo yanaozunguka mgodi kupitia jukwaa la michezo ambapo Oktoba 14,2025 timu ya mpira wa kikapu inayoundwa na wafanyakazi wa mgodi iliikaribisha timu ya Sixers kutoka Kahama katika mechi ya kirafiki ambapo Bulyanhulu imeibuka na ushindi wa vikapu 33-30.