Showing posts with label michezo. Show all posts
Showing posts with label michezo. Show all posts

BARRICK YAPONGEZWA KWA KUWEKA MIUNDOMBINU YA KITUO CHA MICHEZO BUZWAGI

February 28, 2026 Add Comment

    

Baadhi ya wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Taifa wa shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) wakiwa katika picha ya pamoja na Rais wa shirikisho hilo Wallace Karia na Meneja wa Ufungaji wa Mgodi wa Barrick Buzwagi, Mhandisi Zonnastraal Mumbi.
Meneja wa Ufungaji wa Mgodi wa Barrick Buzwagi, Mhandisi Zonnastraal Mumbi akitoa maelezo kwa Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) Wallace Karia na ujumbe wake walipotembelea kituo cha michezo cha Buzwagi.

RAIS WA CAF AWASILI TANZANIA

February 13, 2026 Add Comment


Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF), Dkt. Patrice Motsepe, amewasili rasmi nchini Tanzania asubuhi ya leo kwa ajili ya kuhudhuria Mkutano wa Kamati Tendaji ya Shirikisho hilo.

Mutsepe amepokelewa na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere International Airport, Terminal 1, jijini Dar es Salaam.

Dkt. Motsepe ataongoza mkutano huo unaotarajiwa kufanyika leo katika Hoteli ya Hyatt Regency Dar es Salaam, The Kilimanjaro.

Mkutano huo unatarajiwa kukutanisha viongozi mbalimbali wa soka barani Afrika kwa ajili ya kujadili masuala muhimu yanayohusu maendeleo ya mpira wa miguu.

Kuwa mwenyeji wa mkutano huo ni ishara ya nafasi ya Tanzania katika ramani ya soka barani Afrika, hususan katika kipindi hiki cha maandalizi ya mashindano ya AFCON 2027.




AKWILAPO ATEMBELEA ENEO UNAPOJENGWA UWANJA WA AFCON ARUSHA

February 12, 2026 Add Comment


§ Atoa siku kumi na tano wasiokamilisha malipo ya viwanja vinavyozunguka uwanja kukamilisha

 Asisitiza waliomilikishwa viwanja kufanya maendelezo

Na Munir Shemweta, WANMM ARUSHA

Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Dkt Akwilapo tarehe 11 Februari 2026 ametembeleo eneo unapojengwa uwanja wa kisasa wa mpira kwa ajili Mashindano ya Fainali za Mataifa ya Afrika (AFCON 2027) mkoani Arusha.

Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi imetekeleza Mradi wa Kupanga, Kupima na Kumilikisha Ardhi katika eneo lililopo pembezoni unapojengwa Uwanja wa mpira wa Afcon katika kata ya Olmoti Jiji la Arusha, mkoani Arusha.

Hata hivyo, pamoja na viwanja kuuzwa kwa ajili ya matumizi mbalimbali lakini kuna baadhi ya waliochukua viwanja kushindwa kukamilisha malipo ndani ya muda huku baadhi waliomilikishwa wakishindwa kuendeleza maeneo yao.

Akiwa katika eneo la uwanja huo, Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Dkt Leonard Akwilapo alijionea maendeleo ya ujenzi wa uwanja huo ambapo alipongeza jitihada zinazofanyika za kuhakikisha uwanja huo unakamilika kwa wakati na hatimaye kutumika katika mashindano hayo makubwa ya Afrika.

Akigeukia wananchi waliochukua viwanja na kushindwa kukamilisha malipo kwa wakati, Mhe Akwilapo amewataka kuhakikisha wanafanya malipo ndani ya siku kumi na tano kuanzia tarehe 12 Februari 2026.

"Kuna wananchi walioomba viwanja katika maeneo yanayozunguka uwanja wa AFCON 2027 na kushindwa kukamilisha malipo ya viwanja hivyo, wanatakiwa kulipa ndani ya siku kumi na tano na baada ya hapo tutawanyang'anya na kuwapatia wengine". Amesema Akwilapo

Aidha, amesisitiza wananchi wenye hati milki za ardhi katika eneo linalozunguka uwanja huo kuhakikisha wanafanya maendelezo kwenye maeneo yao huku akiweka bayana kuwa, kama kuna mtu anayedhani hawawezi kufanya maendelezo katika muda wa kuelekea Mashindano ya AFCON 2027 basi airejeshe hati ili kupatiwa wale wanaoweza kufanya maendelezo.

Ujenzi wa mradi wa uwanja wa AFCON Arusha kwa sasa umefikia asilimia 74 na unatarajiwa kukamilika Julai, 2026.
Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Leonard Akwilapo akipata maelezo ya maendeleo ya ujenzi wa uwanja wa mpira unaotarajiwa kutumika katika mashindano ya mataifa ya afrika (AFCON 2027) jijini Arusha jana

Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Leonard Akwilapo (Kushoto) na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi Bi. Lucy Kabyemera wakipata maelezo ya mradi wa viwanja vinavyozunguka uwanja wa AFCON Arusha jana alipofanya ziara katika eneo hilo.

Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Leonard Akwilapo (wa tatu kulia) na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi Bi. Lucy Kabyemera (kushoto) wakielekea katika uwanja wa AFCON wakati wa ziara ya siku moja katika maeneo ya uwanja huo jana. (PICHA NA WIZARA YA ARDHI)

AMBONI ADVENTURE RUN, FURSA YA KUTANGAZA MAPANGO YA AMBONI TANGA

January 31, 2026 Add Comment



Na Kassim Nyaki, Amboni Tanga.

Mamlaka ya hifadhi ya Ngorongoro imeshiriki na kudhamini mbio za AmbonI Adventure run zilizofanyika leo tarehe 31 Januari 2026 jijini Tanga kwa lengo la kutangaza vivutio vya utalii hususan mapango ya Amboni yanayosimamiwa na Mamlaka yah ifadhi ya Ngorongoro

Mbio hizo za umbali wa kimomita 6, 10 na 20 ambazo zimehudhuriwa na wakimbiaji zaidi ya 500 kutoka maeneo mbalimbali nchini zimeanzia katika viwanja vya Shule ya Sekondari Galanos hadi Mapango ya amboni ambapo washiriki wa mbio hizo wamepata fursa ya kufanya utalii wa ndani katika mapango hayo.

Kaimu meneja uhusiano wa Ngorongoro Hamis Dambaya ambaye ameshiriki mbio hizo kwa kukimbia kilomita 10 ameeleza kuwa Ngorongoro imeamua kuungana na wadau mbalimbali kuendelea kutangaza vivutio vilivyoko katika mapango ya Amboni ili yaendelee kujulikana kitaifa na kimataifa na kuvutia wageni wengi kutembelea na kuona vivutio vinavyopatikana katika mapango hayo na kupataa taarifa mbalimbali ikiwemo historia ya wapigania uhuru. 

Msimamizi wa Mapango ya Amboni Afisa Uhifadhi Daraja la kwanza Ramadhan Rashid ameeleza kuwa baadhi ya vivutio vinavyopatikana katika Mapango ya Amboni  ni pamoja na maumbo ya asili ya kijiolojia, vivutio vilivyochongwa na maji kama meli, mlima Kilimanjaro, kanisa, msikiti, shughuli za kimila na mataambiko, ndege ndani ya mapango, pango la jinsia, Pango la fatuma ambalo watu hulitumia kuomba mchumba wa kuoa, mimea ya aina mbalimbali, mto pamoja na mazingira asilia yanayopaambwa naa upepo mwanana wa bahari ya hindi.

Mkuugenzi wa Kale Amboni Caves Sophia Mulamula ameeleza kuwa Mbio za Amboni Adventure Run ambazo zimefanyika kwa msimu wa tatu na kuhudhuriwa na wakimbiaji takriban 500 zinatendelea kuboreshwa ili kuvutia wakimbiaji wengi zaidi mwaka ujao 2027 


“Tumefanya tathmini kwa miaka hii miwili tumeona mbio hizi zinavutia watu wengi, tunaamini mwakani tunaboresha vitu vingi zaidi ili tupate wakimbiaji wengi kwa lengo la kutangaza vivutio vya utalii, kutangaza nchi yetu lakini kuendelea kuhamasisha utalii wa michezo” alilisitiza Mulamula.






WANAFUNZI 500 JIJINI TANGA WASHIRIKI BONANZA LA MICHEZO LA MICHEZO PLUS .

January 30, 2026 Add Comment



Na Oscar Assenga, TANGA



BONANZA la Michezo maarufu kama Michezo Plus limekuwa na mvuto wa aina yake huku likifanyika kwenye viwanja vya Shule ya Sekondari Tanga Ufundi kwa kushirkisha wanafunzi zaidi ya 500.


Wanafunzi hao kutoka shule 50 Jijini Tanga ambao walishiriki katika Michezo ya Mpira wa Miguu,Pete na Wavu huku wakionyesha vipaji vya hali ya juu hatua iliyoshangiliwa na wadau wa michezo ambao walijitokeza kushuhudia bonanza hilo


Akizungumza baada ya kumalizika kwa Bonanza hilo Afisa Michezo wa Jiji la Tanga na Mratibu wa Michezo Plus katika mradi unaotekelezwa na Jiji hilo ukifadhiliwa nan a Botnar Foundation chini ya Programu ya Tanga Yetu Lucy Michael alisema kwamba waliliandaamaalumu kwa ajili ya kujenga mahusiano na kuwajenga kiakili.

Alisema kwamba bonanza hilo litakuwa linafanyika kila mwaka mara mbili ambapo hilo limeanza kwa kufungua mwaka na kukaribisha wanafunzi na watafanya bonanza la vijana.



Awali akizungumza Mratibu wa Bonanza hilo Haji Milao alisema kwamba nia na madhumuni yake ni kuwaweka watoto sawa kwa ajili ya michezo ya Umistashumta mwaka huu 2026 ikiwemo kutengeneza afya za watoto ili waweze kuwa sawa na watoto wakiwa vizuri kwenye michezo hata darasani watakuwa vizuri.



Naye kwa upande wake Mwanafunzi wa Shule ya Msingi Makorora Zuhuru Ally alisema michezo hiyo ina faida kubwa sana kwao kutokana na kwamba inawafanya wakutana na wenzao na kubadilisha mawazo jambo ambalo linawapa fursa.