VIONGOZI MLIYOPEWA DHAMANA MSIBAGUE WATU KATIKA KUWATUMIKIA - GAVU

October 18, 2024

Katibu Wa Idara ya Oganazesheni CCM Ndg Issa Ussi Gavu akizungumza wakati wa kufungua kongamano la maombi ya kuliombea Taifa lililoandaliwa na Kanisa la Ufunuo lililopo Ubungo Dar Es Salaam (Picha na Fahadi Siraji)

Katibu Wa Idara ya Oganazesheni CCM Ndg Issa Ussi Gavu amewataka viongozi wa Serikali waliyopewa dhamana ya uongozi kuwatumikia wananchi bila kuwabagua.


Gavu aliyasema hayo hapo jana wakati alipofungua kongamano la kuliombea Taifa lililoandaliwa na Kanisa la Ufunuo lililopo Ubungo jijini Dar Es Salaam.


“Niwahakikishie tutaendelea kumuomba Mwenyezimungu aendelee kuwakumbusha na kuwasimamia viongozi wetu wa Serikali na kila aliyepewa dhamana, kwamba dhamana waliyopewa ni ya kuwatumikia watanzania waliyo wote, dini zote,rangi zote,makabila yote na jinsia zote” alisema.


Aidha amesema Viongozi wa dini ni watu muhimu sana kwani wamekuwa wakiliombea taifa pasipo wengine kufahamu .


"Lakini katika kila jambo unaloliona duniani wapo Viongozi wanaochukua jukumu kwa niaba ya wengine kwenye hili jukumu la kumuomba na kumlilia Mungu niwaombe Viongozi wetu wa kiroho Msichoke endeleeni kuliombea Taifa” alisema na kuongeza


“Maombi yenu Mungu akiyapokea ndio baraka na neema kwa Taifa lenu na Viongozi wetu wa kisiasa Viongozi wetu wa Serikali, Msichoke kutukumbusha pale ambapo panaondoka amani, upendo na utulivu hata shughuli za Ibada hazitapata nafasi ya kuwapa watu Muda wa kuabudu kwa utulivu".


Kongamano hilo ni la siku tano ambapo waumini zaidi ya elfu tatu wanakutana kuliombea taifa.




Share this

Related Posts

Previous
Next Post »