Showing posts with label habari. Show all posts
Showing posts with label habari. Show all posts
TANZANIA NA OMAN KUIMARISHA USHIRIKIANO MASUALA YA KAZI NA AJIRA

TANZANIA NA OMAN KUIMARISHA USHIRIKIANO MASUALA YA KAZI NA AJIRA

January 28, 2026 Add Comment

Tanzania na Oman zimeendelea kuonyesha dhamira ya kuendelea kuimarisha ushirikiano katika masuala ya kazi na ajira ili kuongeza ajira zenye staha, kulinda haki za wafanyakazi na kukuza uchumi wa mataifa yote mawili.

Hayo yamebainishwa wakati wa kikao cha Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Clement Sangu na Waziri wa Kazi wa Oman, Dkt. Mahad bin Said bin Ali Baawain walipokutana katika Mkutano wa Mawaziri wa Kazi Duniani (Global Labour Market Conference) uliofanyika Jijini Riyadh, Saudi Arabia.

Aidha, katika kikao hicho Waziri Sangu alielezea umuhimu wa kukamilishwa na kutiwa saini kwa Hati ya Makubaliano ya Ushirikiano wa masuala ya Kazi na Ajira (MoU) kati ya nchi hizo mbili, ili kuweka mfumo rasmi na endelevu wa usimamizi wa masuala ya ajira, ulinzi wa haki za wafanyakazi na utatuzi wa changamoto za kiutendaji zinazojitokeza.

Vilevile, Waziri Sangu ameishukuru Serikali ya Oman kwa kuendelea kutoa fursa za ajira kwa Watanzania katika sekta mbalimbali. Pia, amesema idadi ya Watanzania wanaofanya kazi nchini Oman imeendelea kuongezeka , jambo linaloonesha kuimarika kwa mahusiano ya ajira kati ya mataifa hayo mawili.

Kwa upande mwingine, nchi hizo zimekubaliana kuendeleza ushirikiano kwa kuendelea kupanua wigo wa ajira zenye staha, kulinda haki za wafanyakazi na kuimarisha mahusiano ya kiuchumi na kijamii kati ya mataifa yetu mawili.

VYANZO VYA MAJI KUENDELEA KUTUNZWA KUONGEZA UHAKIKA WA HUDUMA YA MAJI.

VYANZO VYA MAJI KUENDELEA KUTUNZWA KUONGEZA UHAKIKA WA HUDUMA YA MAJI.

January 28, 2026 Add Comment

Waziri wa Maji Mhe. Jumaa Aweso,akizungumza wakati wa Mkutano wa Tisa wa mwaka wa Bodi  za Maji za Mabonde nchini uliofanyika leo Januari 28,2026  Jiji la Dodoma.

.....

Waziri Wa Maji Mhe. Jumaa Aweso  amewataka wakurugenzi wa bodi za maji za mabonde nchini kuonyesha umuhimu wa taasisi hizo kwa wananchi kwa vitendo kwa kutoa huduma sahihi.

Waziri Aweso ametoa maelekezo hayo katika kikao cha Bodi za maji za mabonde nchini katika ukumbi wa Jiji la Dodoma.

Aweso ambaye ndiye mgeni rasmi katika kikao hicho amewataka viongozi wa mabonde hayo kutambulika kwa utoaji wa huduma na si kutambulika kwa sifa mbaya kwa wananchi na serikali ikiwemo utozaji wa Kodi zisizi halali.

Aidha Serikali bado inaendelea na mpango mkakati iliyojiwekea katika kujenga mabwawa ya kimkakati kuendelea kupanda miti rafiki wa maji kwa mazingira Ili kuboresha vyanzo vya maji na kutoa huduma ya uhakika kwa wananchi.

Nae Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji Mhandisi Mwajuma Waziri amewataka wakurugenzi na wenyeviti wa Bodi za maji za mabonde nchini kuendelea kutunza vyanzo vya maji Ili kuwa na uhakika wa huduma ya Maji kwa mwananchi.

Ameeleza kuwa vyanzo vya maji nchini ni muhimu katika kikao mabonde yanakuwa na maji ya kutosha kutoa huduma kwa wananchi.

Kadhalika Ili kuwe na uhakika wa utunzwaji wa vyanzo vya maji, amezitaka Bodi hizo kushirikiana na jamii na wadau wa mazingira ikiwemo Ofisi ya Waziri Mkuu TAMISEMI pamoja na taasisi zinazojihusisha na mazingira, Ili kuweka mipango mikakati ya Pamoja katika utunzwaji wa vyanzo vya maji.

Waziri wa Maji Mhe. Jumaa Aweso,akizungumza wakati wa Mkutano wa Tisa wa mwaka wa Bodi  za Maji za Mabonde nchini uliofanyika leo Januari 28,2026  Jiji la Dodoma.

Waziri wa Maji Mhe. Jumaa Aweso,akizungumza wakati wa Mkutano wa Tisa wa mwaka wa Bodi  za Maji za Mabonde nchini uliofanyika leo Januari 28,2026  Jiji la Dodoma.

TANZANIA YAVUTIA WAWEKEZAJI KATIKA JUKWAA LA WIKI YA NISHATI INDIA

January 28, 2026 Add Comment




Na Mwandishi Wetu

Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba, ameshiriki katika mdahalo wa Mawaziri kuhusu uwekezaji na uimarishaji wa ushirikiano wa kimataifa katika sekta ya mafuta na gesi, ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Wiki ya Nishati ya India (India Energy Week – IEW 2026) yanayoendelea kufanyika Goa, India.

Akizungumza katika mdahalo huo uliofanyika leo Januari 28, 2026, Mhe. Makamba ameeleza kuwa Tanzania inaendelea kuweka mazingira wezeshi ya uwekezaji kwa kuzingatia fursa mbalimbali zilizopo katika sekta ya mafuta na gesi.

Amebainisha kuwa tafiti za kuchukua taarifa za mitetemo zinaendelea kufanyika katika vitalu vya Eyasi–Wembere, Lindi na Mtwara, sambamba na kukamilisha majadiliano na wawekezaji mbalimbali kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mikubwa ikiwemo Mradi wa Gesi Asilia Kimiminika (LNG).

Aidha, amesema Serikali inaendelea kuwekeza katika miradi ya usambazaji wa gesi kwa matumizi ya viwandani, uzalishaji wa umeme, matumizi ya majumbani pamoja na kuendesha magari.

“Sekta ya mafuta na gesi ni sekta muhimu na wezeshi katika kukuza uchumi wa taifa. Tanzania, kama zilivyo nchi nyingine zenye rasilimali za gesi asilia na mafuta, imeweka msisitizo mkubwa katika ushirikiano na sekta binafsi ili kunufaika na teknolojia na mitaji,” amesema Mhe. Makamba.

Amefafanua kuwa mahitaji ya nishati nchini yanaendelea kuongezeka kutokana na ukuaji wa kasi wa uchumi, hali inayoongeza uhitaji wa nishati ya uhakika na endelevu.

Pia, amesema jiografia ya Tanzania inaipa nchi fursa ya kuhudumia nchi jirani kupitia bandari zake pamoja na kuunganisha mifumo ya umeme na nchi za Afrika Mashariki na Kusini mwa Jangwa la Sahara, huku ikizingatia ulinzi wa mazingira.

Vilevile, Mhe. Makamba amesema Serikali inasisitiza kuwa mpito kuelekea matumizi ya nishati safi na rafiki kwa mazingira lazima uwe wa haki, usiomwacha mwananchi yeyote nyuma, kwa kuhakikisha upatikanaji wa nishati ya gharama nafuu, salama na ya uhakika.

Maadhimisho ya Wiki ya Nishati ya India (IEW 2026) yanaendelea kutoa fursa kwa Tanzania kujitangaza katika majukwaa ya kimataifa, kuvutia wawekezaji zaidi na kuchochea ukuaji wa uchumi unaoendana na maendeleo ya teknolojia.


&&&&

MRADI WA BILIONI 15.3 WA KUSAMBAZA UMEME VITONGOJI 175 WAPOKELEWA KWA SHANGWE MTWARA

January 28, 2026 Add Comment
-Zaidi ya Kaya 5,600 kunufaika

Wananchi wa vitongoji vya Msokole na Funguni Kijiji cha Mnazi Kata ya Nalingu Mkoani Mtwara wameishukuru Serikali kwa kuwapelekea mradi wa Umeme unaotekelezwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA) ambao wamesema unakwenda kubadili maisha yao.

NGORONGORO YAPANDA MITI AINA YA OLORIEN, MITI MAARUFU WAKATI WA TOHARA KWA VIJANA WA KIMASAI.

January 28, 2026 Add Comment

 


Na Mwandishi Wetu, Ngorongoro.

Tofauti na vijana wa mjini hasa wa Dar es Salaam ambao wengi wao hutahiriwa wakiwa wadogo hospitalini tena kwa ganzi, tohara kwa vijana wa kimasai hufanyika wakiwa mabarobaro na mashabaro na tena bila ganzi na hivyo kusikia maumivu makali ya kitendo hicho.

Katika kuadhimisha siku ya kuzaliwa kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro imeungana naye kwa kupanda miti aina ya Olorien katika kijiji cha Oloirobi Wilayani Ngorongoro.

Miti hiyo hukatwa na hutumika mara baada ya vijana wa kimasai kufanyiwa Jando/kutahiriwa, kijana akishatahiriwa miti huo huwekwa mlangoni wa nyumba yenye kijana aliyetahiriwa kisha akina mama huzunguka ulipowekwa mti husika huku wakiimba kwa furaha na vigelegele kuashiria kwamba zoezi la tohara limefanyika na kukamilika.

Kwa mujibu wa imani ya kabila hilo nyimbo za shangwe na faraja zinazoimbwa na kina mama kwa kuzunguka mti huo ukiwa kwenye nyumba humfanya kijana kuwa na faraja kutofikiria maumivu aliyoyapata wakati wa tohara.

Tohara katika kabila la wamasai inahusisha mafundisho yote ya msingi kwa mwanaume ikiwa ni pamoja na kuwafanya wawe majasiri na shujaa wanaoweza kukabiliana na changamoto zozote za kimaisha tofauti na vijana wanaozaliwa mjini maarufu kama vijana wa elfu mbili (2000) ambao wengi wao maumivu ya jando hawayafahamu kutokana na kutahiriwa wakiwa wadogo tena wengi wao wakifanyiwa tohara hospitali.

Akizungumza mara baada ya zoezi hilo la upandaji wa miti Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro anayesimamia Idara ya Maendeleo ya Jamii Gloria Bideberi amesema kuwa mamlaka itaendelea kuithamini miti hiyo na kushirikiana na jamii ya kabila hilo kuhakikisha miti hiyo haitoweki

Kiongozi wa kimila wa kata ya Ngorongoro bwana Sembeta Ngoidiko amempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa kuamua kusherehekea siku yake ya kuzaliwa kwa kupanda miti na kusema na wananchi wa kijiji cha Oloirobi kwa kushirikiana na Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro wameamua kupanda miti hiyo pamoja na miti mingine inayotumika kama miti dawa ili kuendelea kudumisha uhifadhi,mila na desturi.