Showing posts with label habari. Show all posts
Showing posts with label habari. Show all posts

RAIS MUSEVENI ABARIKI KUREJEA KWA SHUGHULI ZA NATION MEDIA GROUP NCHINI UGANDA

July 28, 2026 Add Comment

 

Kampuni ya Taifa Group leo Julai 28,2026 imetangaza kurejea kwa shughuli za kampuni yake tanzu ya Nation Media Group nchini Uganda kufuatia idhini iliyotolewa na Mheshimiwa Rais Yoweri Kaguta Museveni.

RAIS MUSEVENI ABARIKI KUREJEA KWA SHUGHULI ZA NATION MEDIA GROUP NCHINI UGANDA

July 28, 2026 Add Comment



Kampuni ya Taifa Group leo imetangaza kurejea kwa shughuli za kampuni yake tanzu ya Nation Media Group nchini Uganda kufuatia idhini iliyotolewa na Mheshimiwa Rais Yoweri Kaguta Museveni.


Uamuzi huu ni hatua muhimu katika uwekezaji wa kikanda, maendeleo ya sekta ya habari na ustawi wa ushirikiano wa Afrika Mashariki. Kupitia kampuni tanzu yake, Taarifa Limited, Taifa Group ndiyo mbia mkuu wa Nation Media Group na inaendelea kujitolea katika uwekezaji wenye uwajibikaji, utawala bora wa kampuni na maendeleo endelevu kote katika kanda hii.


Akizungumzia hatua hiyo, Mwenyekiti wa Taifa Group, Bw. Rostam Azizi, alitoa shukrani zake za dhati kwa Mheshimiwa Rais Yoweri Kaguta Museveni kwa kuruhusu kurejea kwa shughuli za Nation Media Group nchini Uganda. Pia alitoa shukrani kwa Jenerali Muhoozi Kainerugaba, Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi ya Uganda (UPDF), kwa uungaji mkono wake katika mchakato mzima uliopelekea matokeo haya chanya akisema,


“Ningependa kutoa shukrani zangu za dhati kwa Mheshimiwa Rais Yoweri Kaguta Museveni kwa uamuzi huu muhimu, na kwa Jenerali Muhoozi Kainerugaba kwa uungaji mkono wake katika mchakato mzima uliopelekea matokeo haya chanya.


Tunajivunia uamuzi huu na tunadumisha azma yetu thabiti ya kuchangia maendeleo ya kijamii na kiuchumi ya Uganda kupitia uwekezaji wenye uwajibikaji, ushirikiano wa muda mrefu na ujenzi wa thamani endelevu.


Kama mbia mkuu wa Nation Media Group, tunaunga mkono kikamilifu dhamira ya Kampuni hiyo ya kufuata misingi ya uandishi wa habari wa haki, uwiano, uhuru na uwajibikaji, unaotoa taarifa, kuelimisha na kuchangia vyema katika mijadala ya umma. Tunashiriki dhima kuu ya Kampuni hiyo ya kuleta athari chanya katika jamii, na tunaamini kuwa vyombo vya habari imara, vya kitaalamu na vinavyozingatia uwajibikaji vina jukumu muhimu katika kusaidia maendeleo ya taifa, utawala bora na ushirikiano wa kikanda.”


"Uamuzi huu unaonyesha thamani ya mazungumzo, kuheshimiana na ushirikiano wa kikanda. Taifa Group itaendelea kuwekeza katika fursa zinazozalisha ajira, kuimarisha taasisi na kuendeleza ustawi wa pamoja katika Afrika Mashariki."


Mwenyekiti wa Nation Media Group, Bw Joe Muganda, alisema Kundi hilo sasa litazingatia kujenga upya uwepo wake, kuungana tena na watazamaji na kuimarisha mchango wake katika sekta ya vyombo vya habari nchini Uganda.


"Tunakaribisha fursa ya kurejesha shughuli nchini Uganda na kuunganishwa tena na watazamaji wetu, wafanyakazi, washirika wa kibiashara na jumuiya.


"Kipaumbele chetu cha haraka kitakuwa kurejesha majukwaa yetu kwa uwajibikaji, kuimarisha maudhui ya ndani na kuwapa Waganda uandishi wa habari wa kuaminika, muhimu na wa ubunifu katika magazeti, matangazo na njia za digital.


"Nation Media Group itatumia uwezo wake wa kikanda na uzoefu ili kusaidia tasnia ya habari yenye uthabiti, yenye mtazamo wa mbele nchini Uganda, huku ikitengeneza fursa za talanta, biashara na ushiriki wa umma."


Kurejeshwa kwa shughuli hizo kunaonyesha uhusiano wa kudumu kati ya Uganda na Tanzania na dhamira pana ya serikali za Afrika Mashariki na sekta binafsi ya kukuza utangamano wa kikanda, uwekezaji wa mipakani na ushirikiano wa kiuchumi.


Nation Media Group inapojenga upya shughuli zake nchini Uganda, itaendelea kutumia uwepo wake kote nchini Kenya, Uganda, Tanzania na Rwanda ili kuunganisha watazamaji, kuimarisha mazungumzo ya kikanda na kusaidia maendeleo ya kijamii na kiuchumi ya Afrika Mashariki. Taifa Group itaendelea kushirikiana na serikali, taasisi, wafanyabiashara na jumuiya kote kanda ili kupanua fursa za kiuchumi endelevu na kusaidia ustawi wa muda mrefu wa Afrika Mashariki.

RAIS SAMIA AAPISHA VIONGOZI WAPYA, ATOA MAELEKEZO MAZITO YA UADILIFU, USHIRIKIANO NA UWAJIBIKAJI

July 28, 2026 Add Comment


Na Mwandishi wetu


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, amewaapisha Naibu Makatibu Wakuu wawili na kushuhudia viongozi wanne wakila Kiapo cha Uadilifu kwa Viongozi wa Umma, huku akiwataka kutekeleza majukumu yao kwa uadilifu, ushirikiano, uwajibikaji na kuzingatia maslahi ya wananchi.

Akizungumza katika hafla iliyofanyika Ikulu, Tunguu, Zanzibar, Rais Samia amesema uteuzi wa viongozi hao unaonesha imani ambayo Serikali imewawekea, hivyo wanapaswa kuhakikisha wanatoa huduma bora, kufanya kazi kwa weledi na kuleta matokeo yanayogusa maisha ya Watanzania.

Rais Samia ameielekeza Ofisi ya Makamu wa Rais kuendelea kuimarisha usimamizi wa masuala ya Muungano kwa kushughulikia changamoto zinazojitokeza kupitia ushirikiano, ili kuendelea kuulinda na kuuimarisha Muungano wa Tanzania. Pia amesisitiza umuhimu wa kusimamia kwa karibu programu za uhifadhi wa mazingira na hatua za kukabiliana na changamoto zinazotishia ustawi wa Taifa.

Aidha, ameagiza Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kuendelea kuboresha usimamizi wa watumishi wa umma kwa kuweka mazingira yatakayowawezesha kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi na kuongeza ubora wa utoaji wa huduma kwa wananchi.

Katika sekta ya uchukuzi, Rais Samia amesisitiza kuongezwa kasi ya utekelezaji wa miradi ya reli, barabara, bandari na meli, pamoja na kutathmini fursa za kupanua biashara ya anga ya Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) ili kuongeza mchango wake katika maendeleo ya uchumi.

Kwa upande wa sekta ya sheria, ameitaka Wizara ya Katiba na Sheria kuendelea kuimarisha upatikanaji wa haki kwa wananchi kupitia kampeni za msaada wa kisheria, ili huduma hizo ziweze kuwafikia wananchi wengi zaidi kwa wakati.

Vilevile, Rais Samia ameitaka Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TANTRADE) kuongeza juhudi katika kukuza biashara na kuboresha usimamizi wa maonesho ya biashara nchini. Pia ameliagiza Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) kuimarisha ulinzi na usimamizi wa hifadhi za taifa na rasilimali za utalii, akieleza kuwa sekta hiyo ni nguzo muhimu ya uchumi wa Taifa.

Kwa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC), Rais Samia amesisitiza umuhimu wa kuendelea kuimarisha nafasi yake kama chombo cha Serikali na sauti ya Taifa kwa kuongeza ubora wa maudhui, weledi wa watumishi na ufanisi katika utoaji wa huduma za habari.

Walioapishwa ni Dkt. Latifa Mohammed Khamis, aliyeteuliwa kuwa Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Makamu wa Rais anayeshughulikia masuala ya Muungano, pamoja na Bi. Prisca Burton Lwangili, aliyeteuliwa kuwa Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora.

Viongozi wengine walioapa Kiapo cha Uadilifu ni Bw. Ephraim Balozi Mafuru, Mkurugenzi Mkuu wa TANTRADE; Bw. Salum Nassor Mnuna, Mkurugenzi Mkuu wa EWURA; Bw. Massana Gibril Mwishawa, Kamishna wa Uhifadhi wa TANAPA; na Bi. Asha Dachi Mbaruk, Mkurugenzi Mkuu wa TBC.


RC DKT BATILDA -MIKOKO NI UHAI WA PWANI ISIHARIBIWE

July 28, 2026 Add Comment



Na Oscar Assenga,TANGA

 Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Balozi Dkt. Batilda Burian, amewataka wananchi kuacha ukataji holela wa mikoko na kushiriki kikamilifu katika uhifadhi wake, akisema misitu hiyo ni muhimu kwa kulinda fukwe, kuhifadhi viumbe wa majini na kuimarisha uchumi wa jamii za pwani.

Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Balozi Dkt. Batilda Burian, ameitaka jamii kuachana na tabia ya ukataji holela wa miti ya mikoko katika maeneo ya mwambao wa Bahari ya Hindi, akionya kuwa endapo vitendo hivyo vitaendelea vinaweza kuhatarisha makazi ya viumbe wa majini, maisha ya wananchi wanaotegemea rasilimali za bahari pamoja na usalama wa fukwe.



Dkt. Burian alitoa kauli hiyo Juni 28 wakati wa Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Uhifadhi wa Ikolojia ya Mikoko yaliyofanyika katika eneo la Donge Mnyanjani, Jijini Tanga. 

Alisema Mkoa wa Tanga umebarikiwa kuwa na ukanda mpana wa pwani pamoja na misitu ya mikoko yenye umuhimu mkubwa wa kiikolojia na kiuchumi katika wilaya za Mkinga, Pangani, Muheza na Jiji la Tanga.

Alieleza kuwa mikoko ni ngao muhimu inayolinda mwambao wa bahari dhidi ya mmomonyoko wa ardhi, huku pia ikiwa mazalia ya samaki na makazi ya viumbe wengine wa majini wanaochangia kuimarisha sekta ya uvuvi na kipato cha wananchi wa maeneo ya pwani.


"Mikoko ya Tanga si tu inalinda mwambao wa bahari dhidi ya mmomonyoko wa ardhi, bali ni chanzo muhimu cha maisha ya wavuvi na jamii nyingi za pwani. Kwa miaka ya hivi karibuni Mkoa wa Tanga umeendelea kuwa mfano wa uhifadhi wa mazingira unaokwenda sambamba na maendeleo ya utalii wa ikolojia," alisema Dkt. Batilda Burian.

Mkuu huyo wa Mkoa alisisitiza umuhimu wa kurejesha maeneo yaliyoharibiwa kwa kupanda mikoko mipya ili kurejesha mazingira katika hali yake ya awali kwa manufaa ya kizazi cha sasa na kijacho.

Aidha, aliwataka viongozi wa serikali za mitaa, vikundi vya wavuvi, wanawake, vijana, wanafunzi pamoja na wadau mbalimbali wakiwemo Scouts kuendelea kushiriki kikamilifu katika juhudi za uhifadhi wa mikoko huku wakizingatia sheria na taratibu za usimamizi wa misitu.


"Tunapanda mikoko leo, lakini bado tunakabiliwa na changamoto kubwa ya uchafuzi wa mazingira unaosababishwa na mifuko ya plastiki, chupa na taka nyingine zinazotupwa ovyo kwenye fukwe zetu. Ni wajibu wetu kuendelea kutoa elimu kwa watoto na vijana kuhusu umuhimu wa kuhifadhi mikoko, kwa sababu tunapohifadhi mikoko tunalinda maisha yetu, chakula chetu, uchumi wetu na mazingira ya watoto wetu," alisisitiza Dkt. Burian.

Kwa upande wake, Mwakilishi wa Kamishna wa Uhifadhi kutoka Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS), Husein Msuya, alisema Siku ya Kimataifa ya Uhifadhi wa Ikolojia ya Mikoko huadhimishwa kila mwaka ifikapo Juni 28, baada ya kuanzishwa na UNESCO mwaka 2015 kwa lengo la kuhamasisha jamii kuhusu umuhimu wa mifumo ya ikolojia ya mikoko na wajibu wa kuihifadhi.

Alisema Tanzania ina takribani hekta 158,100 za misitu ya mikoko iliyopo katika wilaya mbalimbali za ukanda wa pwani, zikiwemo Tanga, Pangani na Mkinga, ambapo misitu hiyo ina mchango mkubwa katika kuhifadhi bioanuwai, kuzuia mmomonyoko wa fukwe, kuhifadhi kaboni na kukuza uchumi kupitia uvuvi pamoja na utalii wa ikolojia.
Wananchi wahamasisha uhifadhi wa mikoko

Mkazi wa Jiji la Tanga, Abdalah Mwalimu, alisema wananchi wana wajibu wa kutunza mikoko kwa kuwa ndiyo kinga ya kwanza dhidi ya athari za mawimbi makubwa na mabadiliko ya tabianchi yanayoathiri maeneo ya pwani.


"Mikoko ni uhai wetu. Tukiiharibu, tutakuwa tumeharibu mazalia ya samaki, tumepunguza kipato cha wavuvi na kuhatarisha usalama wa fukwe. Kila mmoja wetu anapaswa kushiriki kupanda na kuitunza," alisema Abdalah Mwalimu.

Kwa upande wake, mkazi mwingine wa Jiji la Tanga, Fatuma Omari, alisema elimu ya uhifadhi wa mazingira inapaswa kuendelea kutolewa kwa wananchi wote ili kuongeza uelewa wa umuhimu wa kupanda mikoko na kulinda fukwe.


"Kupanda mikoko ni uwekezaji wa maisha ya baadaye. Tunapaswa kuwafundisha watoto wetu kupenda mazingira ili waendeleze jukumu hili na kuhakikisha fukwe zetu zinabaki salama kwa vizazi vijavyo," alisema Fatuma Omari.

Fatuma aliongeza kuwa ushirikiano kati ya wananchi, serikali na taasisi zinazoshughulika na uhifadhi wa mazingira ni muhimu katika kuhakikisha mikoko inaendelea kulindwa na kurejeshwa katika maeneo yaliyoharibiwa.

Abdalah naye alihimiza vijana kujitokeza kwa wingi kushiriki katika kampeni za upandaji wa mikoko na usafi wa fukwe, akisema hatua hiyo itasaidia kuhifadhi mazingira, kuongeza uzalishaji wa samaki na kukuza uchumi wa jamii za pwani kwa manufaa ya kizazi cha sasa na kijacho.









TBS YAKUTANA NA WADAU WA VIPODOZI, YASISITIZA VIWANGO NA USALAMA

July 28, 2026 Add Comment
NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

SHIRIKA la Viwango Tanzania (TBS) limekutana na wadau wa sekta ya vipodozi nchini kwa lengo la kutoa elimu kuhusu matakwa ya viwango, ubora na usalama wa bidhaa hizo zinazotumika kwa kiasi kikubwa na Watanzania.