Showing posts with label habari. Show all posts
Showing posts with label habari. Show all posts

SHIRIKA LA MASOKO YA KARIAKOO LAANZA KUANDAA MPANGO MKAKATI WA MIAKA MITANO 2026-2031

December 13, 2025 Add Comment
Shirika la Masoko ya Kariakoo limeanza rasmi maandalizi ya Mpango Mkakati mpya wa miaka mitano 2026-2031, hatua inayolenga kulifanya soko hilo la kimataifa kutoa huduma bora, kwa wakati na kuzingatia mabadiliko ya teknolojia yanayojitokeza duniani.
SHIRIKA LA MASOKO YA KARIAKOO LAANZA KUANDAA MPANGO MKAKATI WA MIAKA MITANO 2026-2031.

SHIRIKA LA MASOKO YA KARIAKOO LAANZA KUANDAA MPANGO MKAKATI WA MIAKA MITANO 2026-2031.

December 13, 2025 Add Comment

Meneja Mkuu wa Shirika la Masoko ya Kariakoo, CPA. Ashiraf Abdulkarim,akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya uchambuzi na uandaaji wa mpango Mkakati mpya wa miaka mitano 2026-2031 wa Shirika la Masoko ya Kariakoo.

....

Shirika la Masoko ya Kariakoo limeanza rasmi maandalizi ya Mpango Mkakati mpya wa miaka mitano 2026-2031, hatua inayolenga kulifanya soko hilo la kimataifa kutoa huduma bora, kwa wakati na kuzingatia mabadiliko ya teknolojia yanayojitokeza duniani.

Mpango huo unakuja baada ya baada ya mpango wa 2021-2025 kumaliza muda wake wa utekelezaji kwa mafanikio makubwa.

Akizungumza wakati wa ufunguzi mafunzo ya uchambuzi na uandaaji wa mpango huo, Meneja Mkuu wa Shirika la Masoko ya Kariakoo, CPA. Ashiraf Abdulkarim , amesema maandalizi ya mpango huo umeshirikisha wadau ikiwemo Ofisi Waziri Mkuu TAMISEMI, Wafanyabiashara wa Kariakoo, Wapangaji na wadau wengine ili kuwa na mpango mkakati bora, uliochukua mawazo ya wengi na unaojibu matamanio ya kila mmoja na hivyo kuwa rahisi katika utekelezaji wake.

CPA Abdulkarim ameongeza kuwa katika kuandaa mpango huo, Shirika litazingatia nyaraka mbalimbali ikiwemo Dira ya Maendeleo ya Taifa 2025-2050, hotuba ya Rais wakati akifungua Bunge la 13, Mpango wa Nne wa Maendeleo wa Taifa, Ilani ya Uchaguzi ya mwaka 2025-2030 pamoja na Sheria na miongozo mbalimbali iliyoanzisha Shirika la Kariakoo.

“Mafunzo haya yatafanyika kwa siku tano na yatakuwa endelevu. Lengo ni kuwa na mpango mkakati bora, unaotekelezeka na unaoweza kupimika kila mwaka kwa kipindi cha miaka mitano ambao utalifanya soko la kariakoo kuwa kinara na linalotoa huduma anuai na sio mazao pekee" amebainisha CPA Abdulkarim.

Amesema mpango huo ukikamilika utalibadilisha soko la Kariakoo kuwa kituo cha kisasa cha biashara, chenye mifumo ya kisasa ya uendeshaji na utoaji huduma.

CPA. Abdulkarim amesema kuwa Kariakoo mpya itakuwa na miundombinu ya kisasa kuanzia maeneo ya maegesho ya magari, mifumo ya kuzima moto, maeneo ya dharura, hewa ya kutosha na mifumo ya kiteknolojia ya uendeshaji. Tunataka kuwahudumia Watanzania katika mazingira bora na ya kisasa.

Kwa upande wake, Meneja wa Mipango na Biashara wa Shirika la Kariakoo, Bi. Mwinga Luhoyo amesema maandalizi ya mpango huo yanahusisha tathmini ya mpango uliopita wa 2021–2025 ili kubaini mafanikio, changamoto na maeneo yanayohitaji maboresho.

Meneja huyo ameongeza kuwa lengo ni kuhakikisha mpango huo unaendana na mikakati ya kitaifa na huku ukilenga kuongeza tija, kuimarisha biashara, na kukuza mchango wa Kariakoo katika uchumi wa taifa.

 WAZIRI  KAPINGA:MAZAO YAPANDA 120% KWENYE MFUMO WA STAKABADHI

WAZIRI KAPINGA:MAZAO YAPANDA 120% KWENYE MFUMO WA STAKABADHI

December 12, 2025 Add Comment

Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Judith Kapinga,akizungumza wakati akizindua Bodi mpya ya Wakurugenzi wa WRRB) hafla iliyofanyika leo Disemba 12,2025 jijini Dodoma.

.......

Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Judith Kapinga (Mb), amesema Bodi ya Usimamizi wa Mfumo wa Stakabadhi za Ghala (WRRB) imeleta mageuzi makubwa katika Biashara ya mazao nchini katika kipindi cha miaka mitano (2019–2025), hatua iliyoongeza tija kwa wakulima na mapato ya Serikali.

Mhe. Kapinga ameyasema hayo Disemba 12, 2025 jijini Dodoma wakati akizindua Bodi mpya ya Wakurugenzi wa WRRB alipobainisha kuwa mageuzi hayo yameongeza ufanisi, uwazi na matumizi ya TEHAMA katika minyororo ya biashara ya mazao nchini.

Aidha, kiasi cha mazao yanayopitia mfumo huo kimeongezeka kwa zaidi ya asilimia 120, kutoka chini ya tani 600,000 hadi zaidi ya tani 1.3 milioni kwa mwaka, huku bei za mazao zikiongezeka kwa wastani wa asilimia 15 hadi 35, na hivyo kuongeza kipato cha maelfu ya wakulima.

Pia amesema kuwa idadi ya maghala yaliyosajiliwa imeongezeka kutoka chini ya 300 hadi zaidi ya 500, huku mapato ya Serikali yakipanda kwa zaidi ya asilimia 140 kutokana na ushuru, kodi na tozo mbalimbali.

Waziri Kapinga ameielekeza Bodi mpya kuhakikisha mafanikio yaliyopatikana yanaimarishwa na kupanuliwa zaidi katika kipindi kijacho cha miaka mitano huku akiitaka bodi hiyo Mpya kuongeza ufanisi, uwajibikaji na ushindani katika biashara ya mazao nchini.

Kwa upande wake Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda na Biashara, Dkt. Hashil Abdallah, amesema kuwa wizara hiyo itaendelea kushirikiana kwa karibu na Wizara ya Kilimo ili kuboresha huduma za masoko na kuongeza tija kwa wakulima nchini pamoja na kuimarisha uwezo wa wakulima, kukuza ajira na kuunganisha kilimo na viwanda ili kuchochea maendeleo endelevu ya taifa.

Awali, Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Usimamizi wa Mfumo wa Stakabadhi za Ghala (WRRB), Asangye Bangu, amebainisha kuwa matumizi ya stakabadhi yameendelea kuongezeka mwaka hadi mwaka, ambapo idadi ya stakabadhi imepanda kutoka 33,100 hadi 53,107 kwa mwaka 2024/2025, hatua inayoonyesha kuongezeka kwa uelewa na mwitikio wa wakulima na wafanyabiashara.

Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Judith Kapinga,akisalimiana na Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Usimamizi wa Mfumo wa Stakabadhi za Ghala (WRRB), Asangye Bangu,wakati alipowasili kwa ajili ya kuzindua Bodi mpya ya Wakurugenzi wa WRRB) hafla iliyofanyika leo Disemba 12,2025 jijini Dodoma.

Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Judith Kapinga,akizungumza wakati akizindua Bodi mpya ya Wakurugenzi wa WRRB) hafla iliyofanyika leo Disemba 12,2025 jijini Dodoma.

Naibu Waziri Wa Kilimo Mh.David Silinde ,akizungumza wakati wa uzinduzi wa  Bodi mpya ya Wakurugenzi wa WRRB) hafla iliyofanyika leo Disemba 12,2025 jijini Dodoma.

Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda na Biashara, Dkt. Hashil Abdallah,akizungumza wakati wa uzinduzi wa  Bodi mpya ya Wakurugenzi wa WRRB) hafla iliyofanyika leo Disemba 12,2025 jijini Dodoma.

Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Judith Kapinga,akiteta jambo na Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda na Biashara, Dkt. Hashil Abdallah, wakati wa uzinduzi wa uzinduzi wa Bodi mpya ya Wakurugenzi wa WRRB) hafla iliyofanyika leo Disemba 12,2025 jijini Dodoma.

Sehemu ya washiriki wakisikiliza hotuba ya Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Judith Kapinga (hayupo pichani)  wakati akizindua Bodi mpya ya Wakurugenzi wa WRRB) hafla iliyofanyika leo Disemba 12,2025 jijini Dodoma.

Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Judith Kapinga,akiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kuzindua  Bodi mpya ya Wakurugenzi wa WRRB) hafla iliyofanyika leo Disemba 12,2025 jijini Dodoma.

WAKALA WA VIPIMO TANZANIA NA ZAMBIA KUSHIRIKIANA KUSIMAMIA MATUMIZI SAHIHI YA VIPIMO

December 12, 2025 Add Comment
Lusaka, Zambia

Taasisi za Wakala wa Vipimo kutoka nchini Tanzania (WMA) na Zambia (ZMA)zimesaini rasmi Mkataba wa kushirikiana katika usimamizi wa matumizi sahihi ya vipimo. Mkataba huo ni wa muda wa miaka mitatu (3) ambapo utekelezaji wake umeanza mara tu baada ya kusainiwa.

MHE. QWARAY ATOA WITO KWA VIONGOZI KUENDELEA KUJIFUNZA ILI KUBUNI MIKAKATI YA KUBORESHA UTENDAJI

December 11, 2025 Add Comment

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray akizungumza na Viongozi Chipukizi wakati wa uzinduzi wa Programu ya Mafunzo kwa Viongozi hao Awamu ya Kwanza yaliofanyika jijini Dar es Salaam. Sehemu ya Viongozi Chipukizi wakifuatilia hotuba ya Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray (hayupo pichani) wakati akizindua Programu ya Mafunzo kwa Viongozi hao Awamu ya Kwanza yaliofanyika jijini Dar es Salaam. Sehemu ya Viongozi Chipukizi wakifuatilia hotuba ya Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray (hayupo pichani) wakati akizindua Programu ya Mafunzo kwa Viongozi hao Awamu ya Kwanza yaliofanyika jijini Dar es Salaam. Wengine ni wageni waalikwa. Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray (wakwanza kulia) akimsikiliza Afisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya UONGOZI, Bw. Kadari Singo (hayupo pichani) wakati akitoa maelezo ya awali kuhusu taasisi hiyo kabla ya kumkaribisha Naibu Waziri huyo kuzindua rasmi Programu ya Mafunzo kwa Viongozi Chipukizi Awamu ya Kwanza yaliofanyika jijini Dar es Salaam. Sehemu ya Viongozi Chipukizi wakifurahia jambo wakati Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray (hayupo pichani) alipokuwa akizindua Programu ya Mafunzo kwa Viongozi hao Awamu ya Kwanza jijini Dar es Salaam. Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray (wapili kutoka kulia) akiwa katika uzinduzi wa Programu ya Mafunzo kwa Viongozi Chipukizi Awamu ya Kwanza yaliofanyika jijini Dar es Salaam. Kulia kwake ni Afisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya UONGOZI, Bw. Kadari Singo. Wengine ni Watendaji wa taasisi hiyo. Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray (katikati waliokaaa) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Viongozi Chipukizi mara baada ya Naibu Waziri huyo kuzindua Programu ya Mafunzo kwa Viongozi hao Awamu ya Kwanza yaliofanyika jijini Dar es Salaam. Sehemu ya Viongozi Chipukizi wakifuatilia hotuba ya Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray (hayupo pichani) wakati akizindua Programu ya Mafunzo kwa Viongozi hao Awamu ya Kwanza yaliofanyika jijini Dar es Salaam. Wengine ni wageni waalikwa. Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray (katikati waliokaa) akiwa katika picha ya pamoja na Watumishi wa Taasisi ya UONGOZI mara baada ya kuzindua Programu ya Mafunzo kwa Viongozi Chipukizi Awamu ya Kwanza yaliofanyika jijini Dar es Salaam. Kulia kwake ni Afisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya UONGOZI, Bw. Kadari Singo.

Na Veonica Mwafisi-Dar es Salaam

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray ametoa wito kwa Viongozi kuendelea kujifunza siku kwa siku ili kuendana na mabadiliko ya kiteknolojia na kitamaduni yatakayowezesha kubuni mikakati mbalimbali ya kuboresha utendaji kwa ustawi wa taifa.

Mhe. Qwaray ameyasema hayo leo tarehe 11 Disemba, 2025 jijini Dar es Salaam wakati akizungumza na Viongozi Chipukizi kabla ya kuzindua Programu ya Viongozi hao.

Amesema ili mtu aweze kuwa kiongozi mzuri, ni lazima aendelee kujifunza kila siku kwa lengo la kuweza kukabiliana na changamoto za kiuongozi ikiwemo kubuni mbinu mbalimbali za kusimamia mabadiliko ya kimfumo, kiutawala, kiuchumi, kiteknolojia na kitamaduni yanayojitokeza kila siku.

Mhe. Qwaray amewashukuru na kuwapongeza washirika kutoka Finland na HAUS kwa kukubali kushirikiana na Taasisi ya UONGOZI kubuni na kuandaa programu hii maalumu kwa viongozi na taifa kwa ujumla kwani ina umuhimu wa pekee katika kuendeleza viongozi nchini Tanzania na Afrika kwa ujumla.

Aidha, amewasisitiza Viongozi kushirikiana na watumishi walio chini yao kwa kuwaelekeza kazi badala ya kuwaacha na kuwaona ni tatizo katika utekelezaji wa majukumu yao.

Kiongozi usiwe mchoyo kufundisha walio chini yako, tuwafundishe, tunakua, tutengeneze viongozi wa baadae, tusishikilie madaraka, tutengeneze viongozi wengi kadri tuwezavyo, Kiongozi hutakiwi kushikilia kila kitu, shirikisha wenzio ili upate mawazo mapya, kuboresha utendaji na kufikia malengo mahususi yaliyowekwa kwa ustawi wa taifa, Mhe. Qwaray amesisitiza.

Amesema Tanzania inaendelea kutekeleza Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDGs 2030), Ajenda ya Maendeleo ya Afrika (Agenda 2063) na Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 na malengo hayo yameweka bayana kuwa mabadiliko ya kiuongozi ni muhimu kwani ndiyo nguzo kuu ya kufikia malengo yaliyowekwa huku akitolea mfano Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 kuwa imeweka malengo ya kuwa na uchumi wa dola trilioni moja ifikapo mwaka 2050.

“Ni dhahiri hatuwezi kufikia lengo hili kama tusipojipanga na kuweka mikakati madhubuti ya kutuwezesha kufikia malengo yetu.”

Ametaja moja ya mikakati hiyo ni pamoja na kuwa na nguvu kazi yenye uwezo na motisha pamoja na kuwajengea uwezo viongozi kupitia mafunzo kama haya.

Programu hii ni muhimu sana kwani itasaidia Serikali kuwa na viongozi watakaotimiza matarajio ya wananchi.

“Nina imani kuwa maarifa na ujuzi utakaotolewa kwa washiriki wa programu hii utawapa msingi bora na utayari kuongoza na kutoa huduma bora kwa wanachi.

Mhe. Qwaray amewashauri viongozi kujifanyia tathmini ili kutambua uwezo na udhaifu wao kwani kwa kufanya hivyo itasaidia kuboresha utendaji hasa kwenye eneo la mapungufu.

Akitoa neno la utangulizi kabla ya kumkaribisha Naibu Waziri kuzindua Programu hiyo, Afisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya UONGOZI, Bw. Kadari Singo amesema Taasisi yao imekuwa ikitoa mafunzo mbalimbali ya uongozi ili kuwa na viongozi bora katika taifa.

“Kunaweza kukawa na mifumo mizuri lakini viongozi sio wazuri, hivyo mafunzo tunayoyatoa yanasaidia kuwajenga viongozi kuendana na mifumo mizuri iliyopo, Bw. Kadari ameongeza.