Showing posts with label siasa. Show all posts
Showing posts with label siasa. Show all posts

MABALOZI WA MASHINA NI NGUZO YA KUKIPAMBANIA CHAMA-DKT MIGIRO.

January 20, 2026 Add Comment




*Atoa wito kwa viongozi wa ngazi zote za Kitaifa, kuhudhuria vikao vya Chama kwenye ngazi za Mashina.


*Asema ni mahala pa kuikusanya jamii pamoja, kutangaza kazi nzuri inayofanywa na Rais Dkt. Samia.


*Ala chakula na Mabalozi wa mashina


Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt Asha-Rose Migiro, amesema Mabalozi wa Mashina ndiyo nguzo ya kukipambania Chama, kwa kuwa ni macho, masikio na daraja la kuunganisha Chama na kuendelea kulinda umoja kama nguvu ya kusonga mbele ili kuwatumikia wananchi.

Akizungumza leo, tarehe 20.1.2026 katika mkutano na Mabalozi wa Mashina Mkoa wa Dodoma, Katibu Mkuu wa CCM, Dkt Migiro, amesema Mashina ni ngome ya ulinzi wa chama, kwani yataendelea kuwa Walezi, na kuwaunganisha wananchi pamoja, na kwamba siasa lazima iende sambamba na uchumi ndio maana Mashina yana tija kwa Chama.

Amesema ni mahala pa kuikusanya jamii pamoja, kutangaza kazi nzuri inayofanywa na Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan, huku akiwataka kufanya vikao vya mara kwa mara na kufikisha maadhimio ngazi za juu, ambapo kupitia Chama wanaweza kuishauri serikali iliyoko madarakani.

Aidha, Dkt. Migiro ametoa wito kwa viongozi wa ngazi zote za Kitaifa, kuhakikisha wanahudhuria vikao vya Chama kwenye ngazi za Mashina, ili kujadili kwa pamoja na kutatua au kueleza ahadi walizoahidi watakaposhika dola zimefikia wapi utekelezaji wake, ili kulinda umoja wa Chama na kuwa nguvu ya kusonga mbele kuwatumikia wananchi.

Awali, akitoa shukrani kwa niaba ya Wabunge waliohudhuria mkutano huo, Mbunge wa Jimbo la Mtumba na Waziri wa Madini, Anthony Mavunde, amesema katika miaka mingi iliyopita hakuna kipindi ambacho Chama kimewaangalia Mabalozi vizuri kama awamu hii ya sita chini ya Rais Samia Suluhu Hassan, ambaye ni Mwenyekiti wa CCM, akitoa rai kwa Mabalozi na viongozi wote kuyafanyia kazi maelekezo yote yaliyotolewa na Katibu Mkuu wa CCM.



DKT. MIGIRO: MAENDELEO YA JAMII NA SIASA HAVIWEZI KUTENGANISHWA

January 13, 2026 Add Comment


*Asisitiza mabalozi kupandisha bendera za chama kwenye maeneo yao.


* Asema chama kinawajali na kuwathamini mabalozi.

Mahusiano kati ya maendeleo ya jamii na maendeleo ya kisiasa hayawezi kutenganishwa, kwani maendeleo ya kweli huanzia katika misingi imara ya uongozi wa wananchi wenyewe. 

Kauli hiyo imesisitizwa na Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dkt. Asha-Rose Migiro, alipobainisha kuwa injini ya maendeleo ya chama na Taifa kwa ujumla ipo katika mashina ya CCM.

Dkt. Migiro amesema maendeleo ya kweli kwa wananchi huanzia katika mashina ya Chama hicho, akisisitiza kuwa jitihada zote za maendeleo ya kijamii na kiuchumi hupata nguvu kupitia uongozi wa ngazi za chini.

Katibu Mkuu huyo, ambaye ni mwanamke wa kwanza kushika wadhifa huo tangu chama kianzishwe, ameyasema hayo katika mkutano wake na Mabalozi wa Mashina wa CCM Wilaya ya Ilala, ikiwa ni hitimisho la ziara yake katika Mkoa wa Dar es Salaam yenye lengo la kuimarisha uhai wa CCM kuanzia mashinani, kwa kauli mbiu ya “Shina lako linakuita.”

Akizungumza na mabalozi hao, amesema mashina ndiyo ngazi ya kwanza inayowawezesha wananchi kushiriki kikamilifu katika mchakato wa maendeleo, kwa kuwa ndiko wanakotoka wananchi wenyewe na ndiko changamoto zao halisi zinapojadiliwa na kutafutiwa ufumbuzi.

Ameeleza kuwa mashina imara huwezesha utekelezaji wa miradi ya maendeleo kwa uwazi, ushirikishwaji na uwajibikaji, jambo linaloongeza imani ya wananchi kwa Chama Cha Mapinduzi na kuimarisha mshikamano wa kisiasa na kijamii.

Ameongeza kuwa viongozi wa mashina wana wajibu mkubwa wa kusimamia utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika maeneo yao, akisisitiza kuwa uangalizi wa karibu wa miradi hiyo ndio msingi wa maendeleo yenye tija na yanayogusa maisha ya wananchi moja kwa moja.

Aidha, Mwanadiplomasia huyo amesema Mwenyekiti wa CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amepongeza kazi kubwa inayofanywa na Mabalozi wa Mashina, huku akibainisha kuwa chama kitaendelea kuwajali, kuwathamini na kuwatambua kama mhimili muhimu wa uhai na ushindi wa CCM kuanzia ngazi ya chini.


DOYO AONGOZA KIKAO CHA TATHIMINI YA UCHAGUZI MKUU WA OCTOBA 2025.

January 07, 2026 Add Comment

 


Na Mwandishi Wetu,TANGA

KATIBU MKUU wa Taifa wa Chama cha NLD Doyo Hassan Doyo leo January 6 mwaka huu 2026 ameongoza kikao cha Tathimini ya Uchaguzi Mkuu uliofanyika Octoba mwaka 2025 cha Watendaji wa Makao Makuu na Afisi Kuu pamoja na Wagombea Wote.

Wagombea hao ni waliogombea nafasi mbalimbali katika uchaguzi huo, ikiwa ni maandalizi ya vikao vya kikatiba vinavyotarajia kufanyika mwishoni mwa mwezi huu.

Katika kikao hicho kimepitisha pia Taarifa ya maandalizi ya kugombea Ubunge Jimbo la Peramiho mkoani Ruvuma wakati tume itapotangaza rasmi kuanza mchakato wa kumpata mwakilishi wa Jimbo hilo .

Katibu Mkuu huyo aliwashukuru  wananchi wote waliokiunga mkono chama chetu katika kampeni zake nchin kote wakati wa uchaguzi mkuu.

Hata hivyo alitumia nafasi hiyo kuwashukuru  wagombea wote waliogombea nafasi mbalimbali kote nchini nakuwataka wasife moyo na kujipanga kisawasawa katika chaguzi zijazo katika nchi yetu kwani hiyo ndyo njia pekee ya kuweza kushika Dola.

KATA ZA KIRUA VUNJO,MINDU KUPIGA KURA KESHO KUCHAGUA MADIWANI

January 04, 2026 Add Comment


Na Mwandishi wetu, Dar es Salaam

Jumla ya Wapiga Kura 20,851 walioandikishwa katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura watashiriki katika uchaguzi wa kuchagua madiwani katika Kata ya Kirua Vunjo Magharibi iliyopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Moshi Mkoa wa Kilimanjaro na Kata ya Mindu iliyopo katika Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro Mkoa wa Morogoro.


Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Jaji wa Rufaa Mhe. Jacobs Mwambegele leo Januari 04, 2026 wakati akisoma risala maalum kuhusu uchaguzi katika Kata hizo utakao fanyika Januari 05,2026 na kusema kuwa jumla ya vituo 55 vya Kupigia Kura vitatumika.


Aidha, amesema jumla ya wagombea watano (5) kutoka katika vyama vya siasa vinne (4) wanawania nafasi wazi za udiwani katika maeneo hayo na kuvipongeza vyama vya siasa na wagombea waliojitokeza kushiriki katika uchaguzi huo. 


“Natumia fursa hii kuvikumbusha Vyama vya Siasa vinavyoshiriki uchaguzi kesho Januari 05,2026 kuzingatia wajibu wao wa kuweka mawakala katika vituo vyote vya zoezi la kupiga, kuhesabu na kujumlishia kura. Wasimamizi wa uchaguzi katika Majimbo na Kata husika, wamekamilisha taratibu zinazoweka mazingira yanayowawezesha mawakala wa vyama vya siasa kufuatilia mchakato mzima wa uchaguzi,”alisema Jaji Mwambegele.


Amesema, mawakala hao, wanawajibika katika kulinda maslahi ya vyama na wagombea wao. Hivyo, wanapaswa kuzingatia Sheria, Kanuni, taratibu za Uchaguzi na maelekezo ya Tume katika utekelezaji wa majukumu yao vituoni.


Jaji Mwambegele amesema vituo vitafunguliwa saa 01:00 asubuhi na kufungwa saa 10:00 jioni. Ifikapo muda wa kufunga kituo saa 10:00 kamili jioni, kama wapiga kura bado wapo kwenye mistari, mlinzi wa kituo atasimama nyuma ya mtu wa mwisho na zoezi la upigaji kura litaendelea hadi wapiga kura walio kwenye mstari watakapomalizika.


“Baada ya kumaliza kupiga kura, mpiga kura anatakiwa kuondoka eneo la kituo cha kupigia kura; na Mpiga kura awapo kituoni, anatakiwa kufuata maelekezo yote atakayopewa na karani mwongozaji wapiga kura,”alisema Jaji Mwambegele.


Kwa mpiga kura ambaye ameandikishwa katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura na taarifa zake zipo katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura lililopo katika kituo husika, lakini amepoteza kadi yake au kadi yake imeharibika, ataruhusiwa kupiga Kura kwa kutumia moja wapo ya vitambulisho cha Taifa NIDA, Leseni ya udereva au Pasi ya kusafiria (Passport).


MWISHO

MBUNGE MAKBEL AWATAKA MADIWANI KUSIMAMIA KWA WALEDI FEDHA ZA MIRADI YA MAENDELEO

December 03, 2025 Add Comment





Na Oscar Assenga, TANGA

Mbunge wa Jimbo la Tanga (CCM) Kassim Amary Mbaraka Makbel amewataka madiwani kuhakikisha wanasimamia kwa waledi halmashauri ikiwemo fedha zote za miradi ya maendeleo zinazotolewa na Serikali ziende kwenye miradi husika.

Makbel aliyasema wakati akizungumza na waandishi wa vyombo vya habari wakati wa mchakato wa kumpitisha Mgombea nafasi ya Umeya na Naibu Meya wa Jiji hilo ambapo alisema kwamba wanawashukuru vongozi wa CCM na kamati kuu kwa kumteua na kumpendekeza kuwa miongoni mwa wagombea.

Alisema kwamba lazima madiwani wahakikishe wanasimamia vema halmashauri kuhakikisha fedha zote za miradi ya maendeleo ya Serikali ziende kwenye miradi husika ikiwemo kutokuwa na ubadhirifu wa aina yote kuhakikisha miradi inakamilika na hilo jambo ambalo watalisimamia kwa ukaribu.

Alisema kwamba hatataka kuona matumizi mabaya ya Fedha za Umma bali ni kuhakikisha kila fedha zinatumika kulingana na taratibu zake ili ziweze kuleta matokeo yaliyokusudiwa

“Katika hili niwaambie Madiwani kwamba sitataka kuona matumizi mabaya ya fedha zaa umma ambazo zinaletwa katika Halmashauri hivyo lazima tuwe makini “Alisema

Awali akizungumza Mbunge wa Viti Maalumu (CCM) Mhandisi Mwanaisha Ulenge alisema kwamba watakwenda bungeni kusukuma kwa nguvu kuhakikisha fedha zinakuja pamoja na kuhakikisha matumizi mazuri ya fedha zinazoletwa kwa ajili ya maendeleo ya watu kama ilivyo dhamira ya Rais Dkt Samia Suluhu ili kupeleka tabasamu kwa wananchi.

Naye kwa upande wake Mstahiki Meya Mteule wa Jiji la Tanga Selebosi Mhina Mustafa amehaidi kusimamia kikamilifu suala la mapato katika Jiji hilo ikiwemo kuzuia mianya ya upotevu wake kwa njia moja ama nyengine ili kuhakikisha halmashauri inakuwa na mafanikio makubwa.

Selebosi aliyasema hayo jana wakati akizungumza na waandishi wa vyombo vya habari ambapo alisema kwamba wanawashukuru vongozi wa CCM na kamati kuu kwa kumteua na kumpendekeza kuwa miongoni mwa wagombea.

Alisema kwamba hiyo ni imani kubwa ambayo walikuwa nayo juu yake huku madiwani wenzake wa Jiji hilo wakimthibitishia kwa kumpitisha kuwa mgombea wa nafasi hiyo na ndio mteule hivyo atakwenda Halmashauri kushirikiana na madiwaniwenzake kuwa chachu ya maendeleo.

“Kwa kweli nawashukuru sana kwa kuniteua kuwa mgombea na nafasi hii lakini niwaambie kwamba kubwa nitakwend kuzuia mianya yote ya upotevu wa mapato kwa njia moja ama nyengine wanaijua ili kuhakikisha halmashauri isimame kama Halamshauri”Alisema

Alisema kwamba katika kufanikisha jambo hilo watahakikisha wanakuwa makini katika suala la ukusanyaji wa mapato huku akiwaomba ushirikiano ili kuweza kutekeleza majukumu yao kwa tija na kufikia malengo waliojiwekea.

Aidha alisema pia atakwenda kusimamia kutekeleza ilani ya CCM na ndio muongozo wao na dira yao ya kwenda kuifanyia pamoja na kuwa wasimamizi wakuu wa fedha za miradi mbalimbali ambazo Mhe Rais Dkt Samia Suluhu amekuwa akizielekeza Tanga kuhakikisha zinatumika kwenye malengo yaliyokusudiwa na sio vyenginevyo.

“Lakini niwaombe wana Tanga ushirikiano,umoja pamoja na ubunifu katika kutekeleza miradi ya maendeleo na kuwa na vyanzo vipya vya mapato ili kuifanya Halmashauri yao iweze kupiga hatua kubwa za kimaendeleo.

“Tanga ni Jiji hivyo kuhakikisha kusimamia Bilioni 22 kwa Jiji la Tanga lenye viwanda karibuni 7 hadi 5 bado kwake ni ni fedha ndogo ipo haja ya kwenda kuzuia mianya yote ambayo kwa njia moja ama nyengine ”Alisema

Katika hatua nyengine Selebosi alizungumzia kuhusu uwepo wa tishio la maandamano Desemba 9 mwaka huu ambako aliwaambia madiwani kwamba wao ndio wanakaa na wananchi lazima viongozi wachukua hatua ikiwemo viongozi wa mitaa na watendaji wa kata ambao ndio walinzi wa amani katika maeneo yao.

“Katika hili lazima kwenye maeneo yenu tuisaidie serikali na kumsaidia Rais kuhakikisha hakutakuwa na maandamano yasiyokuwa rasmi kutokana na kwamba hayana tija kwa maendeleo “Alisema

Alisema kwambaa wanaofanya maandamano hawazuki tu bali wapo kwenye maeneo wanakutana na wana maeneo wanatokea hivyo lazima ifike mahali waisaidie Serikali kuhakikisha viashiria vyovyote vya uvunjifu wa amani hawavipi nafasi.

Awali akizungumza na waandishi wa habari Katibu Itikadi,Mafunzo na Uenezi Mkoa wa Tanga (CCM) Mngazija alisema kwamba alisema kwamba katika mchakato wa nafasi ya Meya na Naibu Meya wamewapitisha Selebosi Mhina Mustapha kuwa mgombea wa CCM baada ya kupata kura 24 kwa 14 dhidi ya mpinzani wake Hamza Bwanga.

Alisema kwamba katika nafasi ya Naibu Meya walimpitisha Khalid Rashid Hamnza kuwania nafasi hiyo baada ya kumgaragaza mpinzani wake Mwanaidi Chombo kwa kura 21 dhidi ya 16 .


Mwisho.