


Mgombea Ubunge Jimbo la Mbinga Vijijini kupitia tiketi ya CCM *Wakili.Judith Kapinga leo tarehe Oktoba 21,2025 ameendelea na Ziara yake ya Kampeni Kijiji kwa Kijiji-Kata ya Mapera.Ambapo *Ndugu.Kapinga* ameomba Kura za CCM katika Vijiji vya Kihongo,Mkinga na Lukanzauti.Akiwa katika Vijiji hivyo amepokea baadhi ya Changamoto mbalimbali za Maendeleo kama vile Changamoto za Barabara na ameahidi kuzishughulikia na kusimamia iwapo atachaguliwa kuwa Mbunge.
Kwa Upande wa CCM kupitia Mwenyekiti wake wa Timu ya Kampeni Jimbo la Mbinga Vijijini ambaye pia ni Katibu Mwenezi wa CCM Wilaya ya Mbinga, *Ndugu.Johnbosco Mkandawile* amenadi Ilani ya CCM ya Mwaka 2025-2030 inayotoa majawabu na Uelekeo wa Maendeleo ya Miaka 5.CCM imewaombea Kura Mgombea Urais, *Ndugu.Dkt.Samia Suluhu Hassan* ,Mgombea Mwenza, *Ndugu.Balozi.Dkt.Emmanuel Nchimbi* ,Mgombea Ubunge Jimbo la Mbinga Vijijini, *Wakili.Judith Kapinga* na Mgombea Udiwani Kata ya Mapera, *Ndugu.Amos Komba.*
Aidha, *Ndugu.Judith Kapinga* ameshiriki Mazishi ya *Ndugu.Belta Ndunguru* yaliyofanyika Kijiji cha Mkinga,pia katika hatua nyingine *Ndugu.Kapinga* amewaomba Kura Wananchi Mnadani Kijiji cha Unyoni sambamba na kununua Bidhaa.
Imetolewa na Ofisi ya Mgombea Ubunge Jimbo la Mbinga Vijijini,Leo tarehe 21.10.2025
