Showing posts with label siasa. Show all posts
Showing posts with label siasa. Show all posts

WAKILI,JUDITH KAPINGA AENDELEA NA KAMPENI KIJIJI KWA KIJIJI

October 22, 2025 Add Comment



📌 *CCM yaendelea Kunadi Ilani ya Uchaguzi ya Mwaka 2025-2030*

📌 *Ndugu.Kapinga ashiriki Mazishi Kijiji cha Mkinga*

📌 *Ndugu.Kapinga aomba Kura Mnadani Kijiji cha Unyoni sambamba na kununua Bidhaa*

Mgombea Ubunge Jimbo la Mbinga Vijijini kupitia tiketi ya CCM *Wakili.Judith Kapinga leo tarehe Oktoba 21,2025 ameendelea na Ziara yake ya Kampeni Kijiji kwa Kijiji-Kata ya Mapera.Ambapo *Ndugu.Kapinga* ameomba Kura za CCM katika Vijiji vya Kihongo,Mkinga na Lukanzauti.Akiwa katika Vijiji hivyo amepokea baadhi ya Changamoto mbalimbali za Maendeleo kama vile Changamoto za Barabara na ameahidi kuzishughulikia na kusimamia iwapo atachaguliwa kuwa Mbunge.

Kwa Upande wa CCM kupitia Mwenyekiti wake wa Timu ya Kampeni Jimbo la Mbinga Vijijini ambaye pia ni Katibu Mwenezi wa CCM Wilaya ya Mbinga, *Ndugu.Johnbosco Mkandawile* amenadi Ilani ya CCM ya Mwaka 2025-2030 inayotoa majawabu na Uelekeo wa Maendeleo ya Miaka 5.CCM imewaombea Kura Mgombea Urais, *Ndugu.Dkt.Samia Suluhu Hassan* ,Mgombea Mwenza, *Ndugu.Balozi.Dkt.Emmanuel Nchimbi* ,Mgombea Ubunge Jimbo la Mbinga Vijijini, *Wakili.Judith Kapinga* na Mgombea Udiwani Kata ya Mapera, *Ndugu.Amos Komba.*

Aidha, *Ndugu.Judith Kapinga* ameshiriki Mazishi  ya *Ndugu.Belta Ndunguru* yaliyofanyika Kijiji cha Mkinga,pia katika hatua nyingine *Ndugu.Kapinga* amewaomba Kura Wananchi Mnadani Kijiji cha Unyoni sambamba na kununua Bidhaa.

Imetolewa na Ofisi ya Mgombea Ubunge Jimbo la  Mbinga Vijijini,Leo tarehe 21.10.2025




DAKIKA ZA LALA SALAMA,DKT NCHIMBI ATUA KILWA KUSAKA KURA ZA USHINDI WA CCM

October 20, 2025 Add Comment


Mgombea mwenza wa Urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi mapema leo Oktoba 20, 2025 amewasili katika uwanja wa ndege wa Kilwa mkoani  Lindi,ikiwa ni muendelezo wa mikutano ya Kampeni ya kusaka kura za ushindi wa kishindo kwa Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Dkt.Samia Suluhu Hassan,Wabunge na Madiwani.

Ikiwa zimebaki siku 9  za lala salama kufikia uchaguzi mkuu,Dkt. Nchimbi anatarajia kufanya mkutano wake wa hadhara wa kampeni wa kunadi Sera na Ilani ya CCM (2025-2030) katika kata ya Tingi, jimbo la Kilwa  Kaskazini na kuomba  ridhaa ya wananchi kukipigia kura za ndio chama hicho kupitia wagombea wake katika nafasi zote kwenye uchaguzi mkuu unaotarajia kufanyika Oktoba 29, 2025.



DKT.NCHIMBI ATIKISA TUNDURU,AMUOMBEA KURA DKT.SAMIA

October 19, 2025 Add Comment

PICHA mbalimbali za Mgombea mwenza wa Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) Dkt. Emmanuel John Nchimbi akiwa katika mkutano wake wa hadhara wa kampeni uliofanyika kata ya Nalasi,Jimbo la Tunduru Kusini,mkoa wa Ruvuma, leo Oktoba 19,2025, katika mwendelezo wa mikutano yake ya hadhara ya kampeni nchi nzima kusaka kura za ushindi wa kishindo za mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Dkt.Samia Suluhu Hassan,Wabunge na Madiwani.

Akiwa katika mkutano huo wa kampeni pamoja na kunadi sera na Ilani ya CCM ya 2025-30 ,Dkt.Nchimbi aliwashukuru wananchi wa Tunduru kwa kujitokeza kwa wingi kwenye mkutano wake huku akiwaomba kujitokeza kwa wingi ifikapo Octoba 29,2025 kuwapigia kura  za kishindo Wagombea wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) .

Katika hatua nyingine Dkt.Nchimbi alitumia nafasi hiyo kuwanadi wagombea Ubunge wa mkoa huo,akiwemo mgombea Ubunge wa jimbo la Tunduru Kusini,Mhandisi Fadhili Sandali CHILOMBE na Mgombea Ubunge wa Jimbo la Tunduru Kaskazini Ndugu Sikudhani Yassin CHIKAMBO pamoja na Madiwani







WAKILI JUDITH KAPINGA APIGA HODI ARDHI YA TARAFA YA HAGATI

October 18, 2025 Add Comment


📍 *Mbinga-Ruvuma* 🇹🇿🌍


📌 *Ndugu.Kapinga aendelea kuomba Kura za CCM Kipapa*


📌 *Ndugu.Kapinga aeleza umadhubuti na Uimara wa CCM katika Utekelezaji wa Maendeleo*


📌 *CCM yaendelea kusaka Kura,yasisitiza Wananchi Oktoba 29 kupiga Kura*

Mgombea Ubunge Jimbo la Mbinga Vijijini kupitia tiketi ya CCM Wakili Judith Kapinga Octoba 17 Oktoba,2025 ameanza Ziara yake rasmi ya Kampeni ya kuomba Kura za CCM katika Kata ya Kipapa-Tarafa ya Hagati ametembelea Vijiji vya Matuta,Kipapa na Mhilo.

Katika Ziara hiyo, Kapinga ameendelea kuwashukuru Wananchi kwa mapokezi mazuri na moyo wao wa Upendo katika Mikutano hiyo,ameendelea kusisitiza sera yake kubwa ya kupita Kijiji kwa Kijiji ili ajionee Changamoto mbalimbali.Akiwa katika Vijiji hivyo.

Wakili Kapinga amepokea baadhi ya Changamoto mbalimbali za Maendeleo ameahidi kuzishughulikia na kuzisimamia kupitia Ilani  ya CCM ya Uchaguzi ya mwaka 2025/2030.

Katika,hatua nyingine Kapinga amewaeleza Wananchi umadhubuti na uimara wa CCM katika kuwaletea Maendeleo,hivyo amewaomba Kura za Kishindo kwa mgombea Urais wa CCM Dkt Samia Suluhu Hassan pamoja na mgombea mwenza Balozi.Dkt.Emmanuel Nchimbi.

Ndugu.Judith Kapinga ambaye ni Mgombea Ubunge Jimbo la Mbinga Vijijini na Ndugu.Essau Z.Ndunguru -Mgombea Udiwani Kata ya Kipapa.

Kwa Upande wa CCM,chini ya Mwenyekiti wa Timu ya Kampeni Jimbo la Mbinga Vijijini ambaye ni Katibu Mwenezi wa CCM Wilaya ya Mbinga Johnbosco Mkandawile ameendelea kuomba Kura za CCM na kusisitiza Wananchi kupiga Kura Oktoba 29 mwaka huu




         *Imetolewa na Ofisi ya Mgombea Ubunge Jimbo la  Mbinga Vijijini,Leo tarehe 18.10.2025*