Na Oscar Assenga, Lushoto.
WANANCHI wa Kijiji cha Ungo
Kata ya Mlola wilaya ya Lushoto mkoani Tanga wamelazimika kumueleza Mkuu wa
wilaya hiyo, Alhaj Majid Mwanga kuwa diwani wa Kata hiyo, Shekallage Rashid
amekuwa akishindwa kusimamia miradi ya maendeleo na hivyo kumuomba
kumuajibisha.
Wakizungumza kwa nyakati
tofauti katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika uwanja wa shule ya msingi
iliopo kwenye kijiji hicho ikiwa ni ziara yake ya siku nne ya mkuu huyo wa
wilaya ya kukagua miradi ya maendelo na kusikiliza kero za wananchi zinazowakabili.
Wananchi hao walisema kuwa waliazimia
kujenga zahanati na waliamua kupanga kuwa wananchi wanaoishi katika kijiji
hicho wawajibike katika kutengeneza matofauti ambayo yatajengea zahanati hiyo.Akizungumza mmoja wa wananchi wa kijiji hicho,Rashid Mtangi alimueleza mkuu huyo wa wilaya kuwa baada ya kukubaliana hivyo walianza kazi hiyo mara moja na kufanikiwa kufetua matofali na kuyaweka karibu na eneo la shule kwa ajili ya ujenzi huo na kuchukua muda wa kipindi cha miaka miwili lakini ukashindwa kufanyika na matofauti hayo kuharibika.
Mtangi alisema kutokana na
kitendo hicho wananchi wa eneo hilo huenda wakashindwa kuchangia shughuli za
maendeleo katika maeneo yao kutokana na viongozi wazembe ambao wanashindwa
kusimamia majukumu yao na kusababisha nguvu za wananchi kupotea.
“Diwani wetu haitishi hata mikutano ya
wananchi kitendo ambacho kinawafanya wananchi kushindwa kuona umuhimu wao
katika nafasi wanazoziongoza kwani hawaelewi anafanya kazi gani kwao“Alisema
Mtangi.Aidha aliongeza kuwa kijiji hicho kimekuwa hakina mtendaji kwa muda mrefu hali ambayo inapelekea wananchi wanaoishi katika maeneo hayo kushindwa kuelezwa mapato na matumizi yao kwa muda mrefu na hivyo kuchangia kurudisha nyuma kasi ya maendeleo.
Akijibu tuhumu hizo,Diwani Rashid
alimueleza Mkuu wa wilaya kuwa hakuna
mahali popote alipokwamisha ujenzi za zahanati hiyo bali aliambiwa na mbunge wa
jimbo hilo,Henry Shekifu na mganga mkuu wa wilaya hiyo aliyehamia kilombero
mkoani Morogoro kuwa kuwa umbali wa kituo cha Afya cha Mlola na eneo ambalo
kulitakwa kujengwa zahanati hiyo ni karibu.
Kwa upande wake, Mkuu wa
wilaya hiyo, Alhaj Majid Mwanga alisema hatamuangalia tu kwa cheo chake wala
thamani aliyonayo katika jamii kutokana na kushindwa kusimamia miradi ya
maendeleo ya wananchi atahakikisha wachukulia hatua zinazostahili.
“Watu wanataka serikali ichukiwe kuwa
haikufanya kitu kutokana na watendaji wazembe hatutokubali hali hii iendelee
lazima wale wote ambao wanakwamisha miradi ya maendeleo ya wananchi wachukuliwe
hatua stahiki “Alisema DC Mwanga.
Mwanga aliwaomba wananchi
wampe muda aende akaangalie kuwa mradi huo wa zahanati hiyo na kuwataka
viongozi mbalimbali katika kata hiyo kuheshimu maamuzi ya serikali hasa za
vijiji.
Aidha alisema suala la
wananchi wao kutokuwa na mtendaji kwa muda mrefu alihaidi kulishughulikia na
kubwa baraza la madiwani walikumbushie ili liweze upata ufumbuzi haraka
iwezekanayo.
Akizungumzia suala la
wanafunzi ambao hawajaripoti mashuleni tokea shule hizo zilipofunguliwa
aliwaagiza watendaji wa vijiji na kata katika maeneo yote wilayani humo
kuhakikisha wanafunzi hao wanaripoti haraka iwezekanavyo na wampelekee taarifa
zao ofisini wake.
Mwisho.
EmoticonEmoticon