CHUO Kikuu cha Eckenforde-Tanga
kinatarajia kufungua tawi la Chama cha Mapinduzi (CCM) chuoni hapo katika kuitikia azimio la Mkutano Mkuu wa CCM wa kuanzishwa matawi ya Chama kwenye Vyuo vya Elimu ya Juu hapa
nchini.
Akithibitisha habari hiyo,
Katibu wa muda wa Jumuiya hiyo chuoni hapo, Rehema Maclean alisema Jumuia ya
wananfunzi katika Chuo hicho wanatarajia kufungua tawi hilo baada ya kukidhi
kigezo cha kufikia wanachama wanaozidi 50.
Maclean aliliambia blog hii
jana kwamba sherehe za ufunguzi wa tawi hilo zinatarajiwa kufanyika mwezi
Januari 5, mwaka huu lakini zimesongezwa mbele kutokana na sababu mbalimbali.
Akifafanua zaidi, Katibu
huyo alisema kufunguliwa kwa tawi hilo Chuoni hapo kutaongeza idadi ya matawi
kuwa mawili, ambayo ni pamoja na Chuo Kikuu cha SEKOMU kilichoko wilayani
Lushoto.
Aidha, alisema kufunguliwa
kwa tawi hilo ni kutekeleza azma ya kuunda mkoa wa Vyuo Vya Elimu ya Juu kama ilivyoridhiwa na Mkutano Mkuu wa
CCM uliofanyika Dodoma mwaka huu.
Hivi karibuni, akihutubia mkutano wa Jumuiya
hiyo jijini hapa, Katibu wa Mkoa wa Vyuo vya Elimu ya Juu, Christopher Ngu
Ngubiagai alisema kufunguliwa kwa matawi ya Chama cha Mapinduzi katika Vyuo vya
Elimu ya Juu ni hatua iliyochukuliwa kwa maksudi kwa lengo la kukisogeza Chama
kuwa karibu zaidi na watu.
Alisema kuwa Chama kimedhamiria
kuleta mageuzi makubwa yatakayoendana na dhamira ya kuwaingiza vijana katika
safu ya uongozi wa nchi pamoja na mashirika na taasisi za umma.
Akasema vijana wana wajibu
wa kulelewa kulingana na maadili ya Kitanzania na kuongeza kuwa uzalendo
hauteremshwi kutoka mbinguni, bali hujengwa na moyo unaokataa rushwa.
"Vijana wakijengewa
uwezo wanaweza kuongoza kwani wengi wao
ni wazalendo wanaoipenda nchi yao kwa dhati”,alibainisha.
Kwa kutambua hilo, alisema,
tayari Mwenyekiti wa CCM Taifa ambaye pia ni Rais wa Jamhuri ya Muungano, J.K.
Kikwete ameanza kuwaingiza vijana katika
nafasii mbalimbali za uongozi wakiwemo Wakuu wa Wilaya ambao wanaongoza kwa wingi
katika safu hiyo.
Katibu huyo wa Mkoa wa Vyuo
Vya Elimu ya Juu alifafanua kuwa CCM mlango wa kujenga mahusiano ya karibu
baina ya wanafunzi hao wa Vyuo Vya Elimu ya Juu na CCM.
Alisema madhumuni ya
kuanzishwa kwa Mkoa wa Vyuo vya Elimu ya Juu ni kueneza itikadi ya CCM pamoja
na kujenga uzalendo na maadili ya kitaifa.
Hata hivyo Ngubiagai
alitahadharisha kwamba shughuli zote za kisiasa zitafanyika nje na maeneo ya
Vyuo na kwamba wanachama ni vanavyuo tu.
Katibu wa Muda wa Tawi hilo,Rehema
Maclean alisema wanachama hao tayari wamejiandaa kikamilifu tayari kwa ufunguzi
wa tawi lao ifikapo mwishoni mwa mwezi huu.
(Mwisho).
EmoticonEmoticon