TIRA YAPAZA SAUTI BIMA ZA VYOMBO VYA MOTO KWENYE WIKI YA NENDA KWA USALAMA BARABARANI

August 26, 2024

 



Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania (TIRA) imeshiriki katika ufunguzi rasmi wa Wiki ya Nenda kwa Usalama Barabarani 2024 ambayo inaadhimishwa kitaifa mkoani Dodoma katika Viwanja vya Jamhuri. 

Maadhimisho haya yamezinduliwa rasmi leo Agosti 26, 2024 na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Philip Isidor Mpango ambaye pia alitembelea banda la TIRA.

Kamishna wa Bima Tanzania Dkt. Baghayo Saqware amemueleza Mhe. Dkt. Mpango alipotembelea banda la TIRA kuwa Mamlaka inahakikisha kuwa watoahuduma za bima ya vyombo vya moto wanawafikia watanzania kwa ufanisi zaidi ili kuhakikisha huduma na bidhaa za bima zinawafikia walengwa na zinatumiwa ipasavyo kwa maendeleo endelevu na kuleta ustahimilivu wa soko na sekta ya bima kwa ujumla. 

Aidha, Dkt. Saqware ametumia fursa hiyo kuwakumbusha watanzania kutumia vyombo vya moto vilivyokatiwa bima kwa ajili ya usalama wao. 

Kupitia kaulimbiu ya mwaka huu ambayo ni “Endesha Salama, Ufike Salama” inayolenga kuhamasisha na kuchochea kila mmoja kuchukua tahadhari awapo kwenye chombo cha moto, Mamlaka pia imeendelea kutoa elimu ya bima na kuwahamasisha watanzania kuhusu masuala mbalimbali ya bima ikipaza sauti kupitia maadhimisho haya juu ya umuhimu wa bima ya vyombo vya moto na fidia wanazopata watumiaji wa bima hiyo.




Share this

Related Posts

Previous
Next Post »