
Na Oscar Assenga, TANGA.
MSHEHERESHAJI aliyeibuka kinara katika Tuzo za MC Bora wa Mkoa wa Tanga 2025 Giliad Kianda “MC Kianda” amesema kwa sasa malengo yake anayatazama kuwania tuzo bora za Taifa kutokana na umahiri wake na ubunifu katika utekelezaji wa kazi zake.
Kianda aliyasema hayo mara baada ya kumalizika kwa mashindano ya Tuzo la Tanga Awards na kufanikiwa kuibuka na Tuzo ya MC Bora kwa Mkoa wa Tanga baada ya kupigiwa kura na wadau mbalimbali.
Alisema kwamba wanawashukuru wana Tanga kwa kumsapoti mpaka akafanikiwa kuibuka na ushindi katika shindano hilo kwani bila wao asingeweza kupata mafanikio aliyoyapata huku akiwahaidi kile ambacho walikiona kwake wategemee makubwa zaidi.

“Niwaambie tu kwanza wadau wangu nawashukuru sana na niwahaidi wategemee kazi nzuri zinakuja kutokana na ubunifu ambao utakuwa kipaumbele lakini pia niwashukuru waandaaji wa tuzo hizo KEBI na timu yake nawashukuru”Alisema MC Kianda.

Aidha alisema utolewaji wa Tuzo katika Tasnia mbalimbali nchini ikiwemo washereheshaji wa matukio mnbalimbali ikiwemo Harusi imetajwa kuwa chachu ya kuwapa motisha kufanya kazi kwa kujituma na ubunifu.

Awali akizungumza mshindi wa Tuzo mbili za Uandaaji wa Video mwaka 2024/2025 na upigaji wa Picha Mwaka Production aliwashukuru wapiga kura maana watu wanaona kazi zao na wanapiga kura na juhudi zao na maarifa ndio zimewaweka kuwa namba moja.

Katika tuzo hizo zile ambazo zimeshindanishwa ni za Heshima pamoja na utambuzi wa mchango wa wasanii mbalimbali katika mkoa wa Tanga ambazo zinatajwa kwenye kuwa chachu katika kuongeza ubunifu na ufanisi zaidi katika kazi zao.

EmoticonEmoticon