CHABATA yaanza mikakati ya kuandaa timu ya Mkoa

March 30, 2013
Na Mwandishi Wetu, Tanga.

CHAMA cha mchezo wa Baiskeli Mkoa wa Tanga (Chabata) kimeanza mikakati ya kuandaa timu ya mkoa kwa ajili ya kushiriki mashindano ya mchezo huo taifa ambayo mwaka huu yatafanyika mwezi wa saba mkoani Dodoma.

Mwenyekiti wa Chama hicho mkoa wa Tanga, Dege Masoli aliliambia gazeti hili kuwa timu ya mkoa itachaguliwa kutokana na mashindano ya mchezo huo ngazi ya mkoa ambayo yataanza mwezi mei ambapo pia katika watayatumia kwa ajili ya kuwachuja wachezaji ambao wataunda timu ya mkoa.

Masoli alisema licha ya kuwa na mikakati hiyo lakini pia chama chao kinakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo uhaba wa fedha hali ambayo inapelekea timu ya mchezo huo kushindwa kuanza maandalizi mapema.

  “Tatizo la uhaba wa fedha katika chama chetu limekuwa suala kubwa sana hivyo tunawaamba wadau mbalimbali kuweza kujitokeza kwa ajili ya kutusapoti ili tuweze kushiriki vema mashindano ngazi ya Taifa “Alisema Masoli.

Aliongeza kuwa wanawaomba wadau kutoka maeneo mbalimbali,wakiwemo viongozi wa serikali,makampuni, na taasisi binafsi kuangalia namna gani wanaweza kuisaidia timu hiyo iweza kufikia malengo yake.

Mwenyekiti huyo alisema wachezaji 5 ndio ambao watachaguliwa ili kwenda kuuwakilisha mkoa katika mashindano ya Taifa ambapo kwa sasa timu ya mkoa wa Tanga ilianza mazoezi .

Mwisho.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »