Na Oscar Assenga, Tanga.
MBUNGE wa Jimbo la Tanga,Omari Nundu amewapa muda wa
miezi mitatu wananchi waliochukua fedha katika mfuko wa Zindaba Fund wawe wamekwisha kuzirejesha la
sivyo watafikishwa kwenye vyombo vya sheria.
Akizungumza hivi karibuni katika mkutano wake na
wananchi wa kata za Marungu,Kirare,Tongoni na Tangasisi ziliyopo jijini Tanga
alisema wananchi hao wamechukua fedha hizo na kushindwa kuzirejesha licha ya
kuandikiwa barua za mara kwa mara kufanya hivyo bila kuwepo kwa mafanikio yoyote
yale.
Hatua ya mbunge huyo ameichukua kutokana na wananchi
hao mbalimbali jijini Tanga kuchukua fedha katika mfuko huo kiasi cha
sh.milioni 78 huku baadhi yao wakirudisha nusu nusu na wengine wapatao 33
wakishindwa kuzirudisha fedha hizo ili ziweze kuwasaidia na wananchi wengine
shughuli zao mbalimbali.
Alisema hata akichukiwa na mtu yoyote hatajali
badala yake ataendelea kufanya kazi ili kuweza kuwaletea maendeleo wananchi wa
jimbo lake na kuhakikisha huduma muhimu zinawafikia kwa wakati pamoja na kufanyia
kazi changamoto zinazowakabili.
Akizungumzia tatizo la usalama nchini,Nundu alisema
haiwezekani makanisa yakachomwa moto na serikali kuendelea kuyafumbia macho na
kuitaka serikali kuangalia uwezekano wa kuywazibiti wahalifu wa aina hiyo ili
kudumisha hali ya usalama na amani hapa nchini.
Aidha pia alitumia fuksa aliyoipata kuwaasa viongozi
wa vyama vya upinzani wanapokuwa kwenye mikutano yao waongelee sera na sio
mambo mengine yasiyo na tija kwa wananchi wao.
“Tunapotaka kuwaletea maendeleo wananchi wetu tusiangalie itikadi za
vyama vyetu bali tuangalie namna ya kufanya ili wananchi tunaowaongoza waweze
kupata unafuua wa maisha kwa kuangalia
jinsi gani tunaweza kutatua kero zao zinazowakabili “alisema Nundu.
Katika mkutano huo,mwananchi wa kata hiyo,Abdallah
Mnyamisi alimueleza mbunge huyo kuwa wanamatatizo kwenye ofisi yake hakuna
watendaji wazuri na kumuomba mbunge huyo kuwa fedha zake za mfuko wa jimbo
azipeleke katika kutatua kero mbalimbali za wananchi vijijini.
Akijibu swali hilo,Nundu alihaidi kuzifanyia kazi
changamoto zote zinazowakabili wananchi katika maeneo yao kwa kushirikiana na
viongozi wa ngazi ya vijiji na kata ili kuweza kuyapatia ufumbuzi kwa haraka
iwezekanavyo.
Awali akizungumza katika mkutano huo,Mwenyekiti wa
Chama cha Mapinduzi wilaya ya Tanga,Kassimu Mbuguni alisema pamoja na mbunge
huyo kufanya mkutano huo lakini pia walienda kusikiliza ilani ya chama hicho na
kuhaidi kuyafanyia kazi maneno yaliozungumzwa na wananchi katika mkutano huyo
ili yaweza kufikia malengo yao.
Mwisho
EmoticonEmoticon