Na Oscar Assenga, Tanga
MKUU wa Mkoa wa Tanga Balozi Batilda Burian amefanya ziara
ya kutembelea Jengo la Kitega Uchumi la Shirika la Taifa la Nyumba (NHC) “Mkwakwani Plaza” ambalo litagharimu
kiasi cha Bilioni 8.6 huku akiwapongeza kwa
usimamizi imara na ubora mkubwa.
Akizungumza akiwa katika eneo la mradi huo RC Batilda
alisema kwamba ubunifu ambao wameutumia shirika hilo kuanzia hatua ya ujenzi
mpaka usimamizi wanafanya wenyewe kupitia wataalamu wao jambo ambalo
litawezesha kuwepo kwa ubora.
Alisema kwamba kutokana na uwepo wa fursa hiyo watu wa Tanga
wanapaswa kuichangamkia sasa na wasisubiri bali waanze sasa kujiitokeza
kuchukua nyumba katika Jengo hilo la kitega Uchumi la NHC
“Nitumie fursa hii kuwahimiza wananchi kuchangamkia fursa
zilizopo katika Jengo hili wale ambao wana fedha za mitaji waweze kuzungumza na
Meneja wa NHC na leo tumekuja kwenye ziara hapa na kamati ya usalama ya mkoa kukagua
ujenzi wa jengo hilo niendelee kuwapongeza NHC kazi inaendelea vizuri na ya viwango
vya hali ya juu hongereni sana”Alisema
Aidha alimpongeza Rais Dkt Samia Suluhu kwa kuendelea kusukuma
mbela maendeleo katika sekta mbalimbali ikiwemo miundombinu na makazi
Awali akizungumza Menej awa Shirika la Taifa la Nyumba (NHC)
Mhandisi Mussa Kamendu alisema kwamba Jengo hilo litakuwa na maeneo ya maduka
,ofisi za kupangisha katika sehemu ya Biashara huku likiwa na Gorofa nne za
makazi.
Alisema kwamba katika Jengo hilo eneo la makazi nyumba ya
vyuma viwili itakuwa inauzwa kwa kiasi cha Milioni 178 na za vyumba vitatu
zitauzwa kwa shilingi Milioni 240 bei zote zikijumuisha VAT.
Aidha alisema kwamba wanawakaribisha wananchi kuchangia fursa
ya kuweza kununua vyumba hizo huku akiwashukuru ambao wamekwisha kujitokeza na
wapangaji wamepata wengi.
Naye kwa upande wake Mhandisi wa Ujenzi huo Mhandisi Ephahim
Fanuel Msigwa alisema kwamva jengo hilo
lilianza mwaka 2025 na kwa mujibu wa mkataba wanatakiwa kumaliza mwezi Juni 2027.
Mhandisi Ephahim aliongeza kwamba kupitia mradi huo wametengeneza
ajira za kazi 189 na wanawashukuru watu wa Tanga wamejitokeza kwa asilimia
kubwa .
Mradi wa jengo hilo la Mkwakwani Plaza ni mradi wa Kisasa
ambalo linajumisha sehemu za biashara na makazi na kwamba utajkapokamilika
utaongeza thamani ya mji wa Tanga na kutoa fursa zaidi ya ajira na uwekezaji
kwa wananchi.
EmoticonEmoticon