JOPO LA MAWAKILI WA SERIKALI 40 KUTUA TANGA KLINIKI YA KISHERIA

March 05, 2026



Na Oscar Assenga,TANGA

 JOPO la Mawakili wa Serikali 40 wanatarajiwa kutua mkoani Tanga mahususi kwa ajili ya kusikiliza kero sugu za kisheria ambazo zitatolewa ufafanuzi wa kisheria na hatimaye kufungwa na  kuweza kuzimaliza.

Hayo yalisemwa na Mkuu wa Mkoa wa Tanga Balozi,Batilda Burian wakati akieleza kuhusu uzinduzi wa Kamati ya Ushauri wa Masuala ya Kisheria ngazi wa Mkoa Bila Malipo itakayofanyika kwenye viwanja vya Tangamano Jijini Tanga ikianza Machi 9 hadi 15 mwaka huu huku akiwataka wananchi wote .

Alisema kamati hizo zinalenga kutoka huduma kwa wananchi na watuumishi wa umma ,viongozi wa umma na wengine bila kubagua ili kutatua changamoto za kisheria zinazojitokeza huku akieleza itasadia kupunguza mashauri au migogoro dhidi ya Serikali katika ngazi ya mikoa na wilaya.

“Lakini kama mtakumbuka Rais Dkt Samia Suluhu alituma jopo la wanasheria kutoa Wizara ya sheria wakiongozwa na Waziri kwa ajili ya kuzindua kliniki za sheria mkoa lakini ofisi ya Mwanasheria mkuu wa Serikali alituma jopo la wanasheria kutoka ofisi yake na waliopo kwenye mikoa kushirikiana na wanasheria wengine wa kujitolea hapa Tanga”Alisema .

“Kama mtakumbuka hivi karibuni Waziri Mkuu alianza ziara ameenda Arusha na Manyara migiogoro ni mingi wenzetu hawa wamekuja kusaidia kutoa  suluhu za kisheria na kuwasaidia wananchi na zitakutanaisha mawakili wa serikali na taasisi mbalimbali kuwasaidia wananchi wenye changamoto mbalimbali”Alisema

Hata hivyo alisema kwamba huduma hiyo itawezesha kupunguza malalamiko kwa wananchi na hata jopo hilo likiondoka utaratibu huo utaendelea na zoezi hilo  litafanyika bila malipo kwa hiyo wananchi wajitokeze kwa wingi wenye malalamiko ikiwemo mabando yenye malalamiko yawabebe na yawe na vielelezo vya kutosha.

Alieleza kwamba hiyo yote ni ni muendelezo wa kazi nzuri anayoifanya Rais Dkt Samia Suluhu  na wanaendelea kumpongeza kuweza kulinda,kukuza na kutetea haki za wananchi wanyonge na kupinga vitendo vya uvunjifu wa haki za binadamu na misingi ya utawala bora na kuhakikisha ukatili wa kijinsia unatokomezwa.

Mkuu huyo wa mkoa alisema pia  lakini kuheshimu utawala wa sharia ambao ndio msingi wa maendeleo kwenye mkoa huo wanaendeela kupongeza Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali kwa kuhakikisha kamati ya ushauiri wa kisheria kwenye mkoa wa Tanga inazinduliwa na kuanza kutioa huduma kwa wananchi wote bila kujali uwezo wao wa kifedha .



Mwisho.



Share this

Related Posts

Previous
Next Post »