Na Oscar Assenga,TANGA
MAMLAKA ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira (Tanga Uwasa) imeweka bayana mpango mkakati wao wa kuboresha uwezo wa uzalishaji wa maji kutoka Lita Milioni 45 mpaka kufikia Lita Milioni 60 pamoja na kuongeza mtandao wa bomba la usambazaji wa maji kwa umbali wa kilomita 60
Mpango huo uliwekwa bayana leo na Mkurugenzi wa Huduma kwa Wateja wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira (Tanga Uwasa) Alawi Ahmadi wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu maadhimisho ya wiki ya maji iliyoanza Machi 16 hadi Machi 22, 2025 yenye kauli mbiu “Uhifadhi wa uoto wa asili kwa uhakika wa Maji”
Alisema kwamba lengo la mipango hiyo ni kuhakikisha huduma inafika kwa wakazi wote pamoja na utekelezajii wa miradi mkubwa wa uboreshaji wa miundombinu kuanzia eneo la Bwawani,Mtambo wa kutibu maji pamoja na kuendeleza mtandao wa usambazaji maji katika maeneo mbalimbali .
“Tutaboresha uwezo wa kuzalisha maji kwa asilimia 25 ukilinganisha na mahitaji kwa sasa tunaweza kuzalisha maji lita milioni 45 tunataka kuzalisha maji lita milioni 60 kutakuwa na ongezeko la maji lita milioni 15 kwenye uwezo uliopo wa mtambo wetu”Alisema
Aidha alisema kwamba wataongeza pia mtandao wa bomba la usambazaji maji kwa kilomita 60 sasa hivi wana urefu wa kilomita 862 lakini wataongeza kilimota 60 ili kufikia watu wote waliopo kwenye eneo lao lka huduma,
Alisema kwamba mradi huo ulianza tokea mwezi Julai mwaka jana na unatarajia kuisha Desemba mwaka huu ambapao kwa sasa umefikia asilimia 15 kwa maana vifaa vyote vinayotakiwa kutekeleza mradi huo vimewasili eneo la mradi na wakandarasi wamekwisha kuanza kazi kwa maeneo mbalimbali.
“Mradi huu vifaa vyote vinavyotakiwa vimewasili na gharama za mradi huo ni Sh.Bilioni 53.12 ambazo walizipata kwa kuuza hati fungani na kwa sasa utoaji huduma umefikia asilimia 93 ya wakazi wa Jiji ya Tanga, Muheza na Pangani”Alisema
Alisema kupitia kauli mbiu hiyo Tanga Uwasa inapanga kufanya tathimini na kuweka vipaumbele kwenye mambo mbalimbali ikiwemo jitahida zinazofanyika na matokeo ya uhifadhi wa mazingira ili kufanikisha kutunza vyanzo vya maji ili viweze kuwa endelevu.
“Lakini kupunguza athari za uchafuzi wa vyanzo vya maji ili kupunguza athari zake kwa watumiaji na kupunguza gharama za kuyasafisha pamoja na utekelezaji wa miradi ya kuboresha hali ya huduma kwa upande wa maji safi na taka”Alisema
Alisema pia kuendelea na utatuzi wa kero za huduma zinazowapata wananchi kwa sasa katika maeneo mbalimbali ya huduma pamoja na kutoa elimu kwa wateja juu ya huduma kwa kutumia vyombo vya habari, madawati ya huduma kwa wateja.
“Katika wiki ya maadhimisho ya wiki ya maji Tanga Uwasa imejipanga kutoa elimu kwa wateja kuhusu masuala mtambuka ya maji kutumia vyombo vya habari, madawati maalumu ya huduma kwa wateja na kuwatembelea majumbani pamoja na kutoa msahama wa tozo ya kurejesha huduma kwa wateja ambao wamesitishiwa huduma ya maji pamoja na kuruhusiwa kuweka mikataba ya kulipa madeni yao kwa awamu yaani kidogo kidogo”Alisema
Awali akizungumza Kaimu Mkurugenzi wa Usambazaji wa Maji na Usafi wa Mazingira wa Tanga Uwasa Mhandisi Salum Hamis alisema wana mradi mkubwa wa hati fungani ambapo wana maeneo makubwa manne ambayo yatasaidia kumaliza shida ya maji katika Jiji la Tanga na miji ya Muheza na Pangani.
Alisema kwenye huo mradi wanakwenda kuupanua mtambo wa kusukuma maji mabayani kutoka uwezo wa sasa wa kusumua maji kutoka Lita 42,000 kwa siku mpaka kufika 60,000 kwa siku ikiwemo kujenga bomba linguine kubwa kutoka mabayani mpaka kituo chao cha kusafisha maji Mowe lenye kipenyo cha Milimita 600.
“Sasa hivi wana Bombo lenye milimita 600 na wanaongeza la pili na lingine ni kituo cha kusafisha na kutibu maji Mowe kwa sasa kina uwezo wa kusafisha na kutibu maji kwa uwezo wa mita za ujazo 45,000 kwa siku kwenye huo mradi tunakwenda kukiongeza kufikia uwezo wa mita za ujazo 60,000 kwa siku “Alisema
EmoticonEmoticon