ZIARA YA MAKAMU WA RAIS MKOA WA KASKAZINI PEMBA

April 06, 2018


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na mjasiriamali wa kazi za sanaa za mikono katika ufukwe wa Nungwi Ndugu Rabinson Mungule wakati wa ziara ya Makamu wa Rais ya kukagua miradi ya CCM ikiwa sehemu ya kuhamasisha Chama Cha Mapinduzi kujitegemea kwa kutumia rasilimali zake katika mkoa wa Kaskazini Unguja.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiangalia urembo wa wanawake unaouzwa katika fukwe za Nungwi Ndugu Rabinson Mungule wakati wa ziara ya Makamu wa Rais ya kukagua miradi ya CCM ikiwa sehemu ya kuhamasisha Chama Cha Mapinduzi kujitegemea kwa kutumia rasilimali zake katika mkoa wa Kaskazini Unguja.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Waziri wa Zamani Mambo ya Ndani ya Nchi, Ali Ameir Mohammed, alipomtembelea nyumbani kwake, Kichaviani, Jimbo la Donge, Makamu wa Rais alikuwa kwenye ziara katika mkoa wa Kaskazini Unguja.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na viongozi wa CCM mkoa wa Kaskazini Unguja ikiwa sehemu ya ziara yake ya kuhamasisha shughuli za maendeleo ya Chama Cha Mapinduzi.

Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu amesikitishwa sana na uharibifu wa mazingira unaoendelea katika machimbo ya mchanga Donge.

Makamu wa Rais ambaye yupo kwenye ziara Visiwani Unguja na leo alikuwa na ziara katika mkoa wa Kaskazini Unguja.

Makamu wa Rais amesema hatua za haraka zichukuliwe ili kuokoa mazingira yasiendelee kuharibiwa.

Makamu wa Rais pia amewataka Viongozi wote wa CCM kuhakikisha kuwa Chama kinajitegemea kwenye maeneo yao, Makamu wa Rais aliyasema hayo mara baada ya kukagua shughuli za kiuchumi za CCM katika ufukwe wa Nungwi ikiwa sehemu ya ziara yake aliyoifanya kwenye mkoa wa Kaskazini Unguja.

Makamu wa Rais pia alifungua ofisi mbili za CCM moja ikiwa ya jimbo la Donge na nyingine ikiwa Ofisi ya CCM mkoa wa Kaskazini ambapo inahistoria ya kipekee kutokana na kuwekwa jiwe la msingi mwaka 1986 na Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »