COASTAL UNION:MCHAKATO WA KOCHA MPYA BADO UNAENDELEA

October 29, 2013


Na Oscar Assenga, Tanga.
UONGOZI wa Klabu ya Coastal Union ya Tanga umesema hivi sasa hauna mpango wa kutafuta kocha mpya badala yake wataendelea na kocha Joseph Lazaro mpaka kumalizika mzunguko wa kwanza.

Kauli hiyo ilitolewa leo na Mwenyekiti wa Klabu hiyo,Hemed Aurora “Mpiganaji”wakati akizungumza na mwandishi wa habari hizi kuhusu mikakati ya kumleta kocha mpya baada ya Hemed Morroco kubwaga manyanga.

Morroco alibwaga majanga baada ya mkataba wake kumalizika huku timu hiyo ikiwa inasuasua kufanya vizuri katika michezo yao ya ligi kuu Tanzania bara hali ambayo wakati mwengine ilikuwa ikimuweka kwenye wakati mgumu hasa kwa mashabiki.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »