HABARI MPYA
HABARI
SIASA
ELIMU
Recent Posts
SERIKALI KUENDELEA UBORESHA NA KUJENGA MIUNDOMBINU YA UVUVI
habariNA MWANDISHI WETU – SONGEA
Serikali inaendelea kuboresha na kujenga Miundombinu ya uvuvi ikiwemo masoko ,maghala ya kuhifadhia mazao ya uvuvi, vichanja vya kukaushia samaki maghala ya kuifadhia mazao ya uvuvi na viwanda vya kuchakata mazao ya uvuvi na teknolojia rafiki za ukaushaji ili kubadilisha sekta hii kutoka ufugaji na ukulima mdogo kuelekea katika kuimarisha lishe na uchumi wa wakulima wadogo wanaojikita katika uzalishaji na ukuzaji wa viumbe maji nchini ambapo matokeo hayo yanatarajia kuchochea uchumi wa wananchi na taifa kwa ujumla.
Hayo yameelezwa na Bw. Jumanne Mwankoo Kaimu katibu Tawala Mkoa wa Ruvuma wakati wa tukio la kuhakiki taarifa ya matokeo ya mwisho ya mradi wa kuimarisha lishe kwa wakuzaji wadogo wa viumbe maji (ARNSA) uliokuwa ukiratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge Uratibu wenye Ulemavu kwa msaada wa Shirika la NORAD kupitia Mfuko wa Kimataifa wa Maendeleo ya Kilimo Duniani IFAD tarehe 5 Juni 2026.Bw. Mwankoo alisema kuwa Mradi huo wa kikanda uliokuwa katika Nchi za Tanzania, Kenya na Msumbiji na kutekelezeka katika Mikoa ya Lindi Mtwara na Ruvuma nchini,
Ambao umetoa mchango mkubwa katika sekta ya uvuvi ambayo imechangia takribani asilimia 69% ya protini katika lishe bora, uzalishaji wa mazao ya viumbe maji sambamba na ongezeko la ajira kwa vijana na wanawake na kuimarisha lishe kwa wakuzaji wadogo wa viumbe maji, hususan wakulima wa mwani na wafugaji wa samaki katika Halmashauri za Mtama, Ruangwa Songea na Mbinga
Akiongea wakati wa kufunga mradi huo wa Lishe, Mratibu wa Programu ya Kuendeleza Kilimo na Uvuvi (AFDP) kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Uratibu na wenye Ulemavu Bw. Salimu Mwinjaka Alisema kuwa, mradi huo wa miaka miwili ulijikita zaidi katika katika kilimo cha mwani na uzalishaji wa viumbe maji ulifanikiwa kwa kiasi kikubwa kwani wanufaika wa mdari huo bado wanaendelea na shughuli hizo za uzalishaji kwa kutumia teknolojia za kisasa na ubunifu waliojijengea.

Kwa pande wake Mkurugenzi wa Ukuzaji viumbemaji toka Wizara ya Mifugo na Uvuvi Dkt Nazaeli Madala alieleza kuwa, Serikali imeweka msisistizo katika kukuza uchumi na mikoa iliyotekeleza mradi huo imeweza kukuza uchumi.
‘Mkoa hiyo imebahatika kupata ardhi nzuri na imekuwa fursa ya kuweza kufuga na kupata chakula na kuwauzia wengine chakula, kupata uzalishaji ulio na tija pamoja na uzalishaji Ajira na huu ndo msukomo wa Serikali.” Alibainisha Dkt Madala.
Mmoja wa wanufaika wa Mradi huo mwakilishi wa vijana Bw. Innocent Kikiwa Amesema kuwa mradi huo umemuwezesha yeye kama kijana kuweza kupata uzoefu katika eneo la Ufugaji Viumbemaji na kilimo cha mwani, kuweza kujiajiri kukuza mnyororo wa thamani kwa kuuza mazao yatokanayo na zao la mwani, kuuza samaki anaowafuga pamoja na kutafuta masoko.
KATIBU MKUU WA CCM AKUTANA NA BALOZI WA UINGEREZA KUJADILI USHIRIKIANO WA MAENDELEO NA DIRA 2050
siasa
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Ndugu Asha-Rose Migiro, leo Ijumaa Juni 5,2026 amefanya mazungumzo na Mheshimiwa Marianne Young, Balozi wa Uingereza nchini Tanzania, katika Makao Makuu ya CCM, Dodoma.

Mazungumzo hayo yalihusu maeneo ya ushirikiano wa maendeleo kati ya Tanzania na Uingereza, kwa kuzingatia vipaumbele vilivyobainishwa katika Ilani ya CCM ya Uchaguzi ya mwaka 2025–2030, Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 pamoja na Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDGs).
Viongozi hao walijadili fursa za kuendeleza ushirikiano kwenye maendeleo ya kijamii na kiuchumi, hususan katika kuwawezesha vijana na wanawake kupitia elimu, ujuzi, ubunifu na uwekezaji.

CCM inaendelea kuthamini ushirikiano wa kimataifa unaochangia maendeleo endelevu na ustawi wa wananchi wa Tanzania.
JUKWAA LA BIASHARA LA VIWANGO LAHAMASISHA USALAMA WA CHAKULA NCHINI
habariNEMC YATUNUKU TUZO SHULE BORA ZA UHIFADHI WA MAZINGIRA DAR ES SALAAM
habariJAB KUPUNGUZA VIKWAZO VYA ITHIBATI KWA WAHITIMU WA HABARI
habariKaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amewashauri Waandishi wa Habari nchini kuipa thamani na heshima taaluma ya habari kwa kuzingatia nadhifu ya mavazi na mienendo yao wanapotekeleza majukumu ya kitaaluma.
Wakili Kipangula ametoa ushauri huo leo Juni 5, 2026 wakati akiwasilisha mada kuhusu “Uhuru wa Vyombo vya Habari katika Enzi ya Kidijiti: Wajibu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari” kwenye Kongamano la Uhuru wa Vyombo vya Habari lililoandaliwa na Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) kupitia Idara ya Sanaa na Taaluma za Habari.
Amesema uandishi wa habari ni taaluma muhimu inayotambulika kama muhimili wa nne usio rasmi katika jamii, hivyo ni wajibu wa waandishi wenyewe kuhakikisha wanaijengea heshima kupitia mwenendo, maadili na namna wanavyojiwasilisha mbele ya jamii.
Wakili Kipangula amesema mwonekano wa mwandishi wa habari unaweza kuwa sehemu ya kujenga imani kwa jamii na vyanzo vya habari vinavyotoa taarifa mbalimbali kwa vyombo vya habari.
“Kwa hiyo hata mtu unavyoenda kumhoji mtu akikuona jinsi ulivyo anajua huyu mtu ataeleza kitu cha msingi na huyu mtu anaeleweka na ni wa maana,” amesema Wakili Kipangula.
Amesisitiza kuwa pamoja na kuzingatia maadili, sheria na weledi katika ukusanyaji na uchakataji wa habari, Waandishi wa Habari wanapaswa kutambua kuwa taswira wanayoijenga mbele ya jamii ni sehemu muhimu ya kuimarisha hadhi ya taaluma hiyo na kuongeza imani ya wananchi kwa vyombo vya habari.
TADB YAPOKEA TUZO KWA KUENDELEZA KILIMO ENDELEVU NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
habariKatibu Mkuu wa CCM akutana na Balozi wa Uingereza Kujadili Ushirikiano wa Maendeleo na Dira 2050”
habariTPDC YAKABIDHI KARAKANA YA KISASA YA CNG KWA CHUO KIKUU CHA DAR ES SALAAM.
habariDKT. KIJAJI: NYUMBA ZA IBADA ZIWE CHANZO CHA MSHIKAMANO NA AMANI KWA TAIFA
habariKONDOA, DODOMA
Mbunge wa Jimbo la Kondoa ambaye pia ni Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (Mb), amesisitiza kuwa nyumba za ibada zinapaswa kuwa sehemu ya kuimarisha mshikamano, umoja na amani miongoni mwa wananchi na si kuwa chanzo cha migawanyiko katika jamii.
Dkt. Kijaji ametoa kauli hiyo leo alipokuwa akifungua rasmi Msikiti wa Filimo uliopo Kata ya Mnenia, Halmashauri ya Wilaya ya Kondoa mkoani Dodoma.
Akizungumza katika hafla hiyo, Dkt. Kijaji amesema kuwa nyumba za ibada zina nafasi kubwa katika kujenga maadili mema, kuimarisha upendo na kukuza mshikamano wa kijamii, hivyo zinapaswa kutumika kwa malengo hayo kwa manufaa ya Taifa.
“Msikiti huu uwe chachu ya mshikamano ndani ya jamii yetu. Nawapongeza viongozi wa dini kwa kusimama katika haki na kuendelea kuhubiri amani na umoja miongoni mwa wananchi,” alisema Dkt. Kijaji.

Aidha, aliongeza kuwa kila mtu ana wajibu wa kutekeleza majukumu yake kwa uadilifu katika jamii na mbele za Mungu, akibainisha kuwa maendeleo yanayopatikana katika Jimbo la Kondoa yanalenga kuwanufaisha wananchi wote bila ubaguzi.
"Ninachokifanya ndani ya jimbo letu ni kwa ajili ya maendeleo ya Wakondoa wote. Tunapaswa kuendelea kushirikiana na kuishi kwa upendo ili kuleta maendeleo endelevu,” alisisitiza.
Vilevile , Dkt. Kijaji alitumia fursa hiyo kuwahamasisha waumini na wananchi wa eneo hilo kuendelea kujenga na kuendeleza nyumba za ibada ili zitumike katika kukuza maadili mema na kuimarisha imani katika jamii.
Katika hatua nyingine, amewataka vijana kujiepusha na matumizi ya dawa za kulevya na vitendo vingine vinavyohatarisha mustakabali wao, huku akiwataka viongozi wa dini kuendelea kuliombea Taifa pamoja na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan.
Pia amesisitiza umuhimu wa malezi bora kwa watoto na vijana, akiwataka wazazi na walezi kuwajenga katika misingi ya maadili mema ili kuwa raia wema na wenye mchango chanya kwa maendeleo ya Taifa.
SERIKALI YAZINDUA GRAND CHALLENGES TANZANIA KUCHOCHEA UBUNIFU WA KUTATUA CHANGAMOTO ZA TAIFA
habariSERIKALI YAENDELEA NA UANDAAJI WA KANUNI ZA BIMA ZA KILIMO KULINDA WAKULIMA
Na Jordan Mbwambo WF, Dodoma
Serikali imesema inaendelea kukamilisha mchakato wa uandaaji wa Kanuni za Bima za Kilimo ambazo zitasaidia kuongeza upatikanaji wa kinga kwa wakulima dhidi ya majanga yanayoathiri mazao, mifugo, misitu na sekta ya uvuvi nchini.
Hayo yamebainishwa bungeni jijini Dodoma na Naibu Waziri wa Fedha, Mhe.Laurent Luswetula (Mb), alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Ilemela, Mhe. Kafiti William Kafiti, aliyetaka kujua wakati ambao Serikali itakamilisha Kanuni hizo ili kuongeza na kupatikana kwa kinga kwa wakulima na mazao mbalimbali.
Mhe. Luswetula alisema kuwa, Serikali kupitia Wizara ya Fedha inaendelea na utafiti na maboresho katika Sekta ya Bima ya Kilimo ili kuhakikisha mfumo huo unakuwa shirikishi na wenye kuvutia uwekezaji kwa wadau wa ndani na nje ya nchi.
“Serikali inaendelea na utafiti kuhusu bima katika mnyororo wa kilimo (mazao, mifugo, misitu na uvuvi) ili pamoja na mambo mengine kuwa na Kanuni zinazovutia uwekezaji katika bima ya kilimo na kuweka mazingira wezeshi kwa wakulima ili kupata huduma za bima kwa urahisi na haraka”, alisema Mhe. Luswetula.
Aliongeza kuwa, Serikali inakusudia kuhakikisha kanuni hizo zinakuwa rafiki kwa wakulima na wakati huo huo zikichochea ushiriki wa sekta binafsi katika kutoa huduma za bima ya kilimo nchini.
Aidha, alisisitiza kuwa Serikali itaendelea kushirikiana na wadau wa sekta ya bima kuhakikisha mfumo huo unakuwa endelevu na unaonufaisha wakulima kwa upana zaidi.
DKT.SAMIA SULUHU HASSAN ATUNUKU SHAHADA KWA WATANZANIA ASEMA NI YAO
Na Beda Msimbe,TBN, Moscow
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ametunukiwa Shahada ya Udaktari wa Heshima (Honoris Causa) na Chuo Kikuu cha Urafiki wa Watu wa Urusi- (RUDN University) huku akiitoa shahada hiyo kwa Watanzania.
Shahada hiyo ilitolewa na Mkuu wa Chuo hicho Profesa Oleg Yastrebov kwenye hafla iliyofanyika Chuoni hapo Moscow nchini Urusi, tarehe 04 Juni,2026.
Rais Mhe. Dk Samia ametunukiwa Shahada hiyo ya Uzamivu kutokana na mchango wake katika Mageuzi ya sekta ya Elimu, juhudi zake za kuimarisha Diplomasia ya Tanzania,
pamoja na mchango wake katika kuimarisha hadhi ya Tanzania Kimataifa ikiwemo kupitia sekta ya Utalii,
Akizungumza baada ya kupewa shahada hiyo Rais Samia alisema kwamba heshima aliyopewa si ya mafanikio yake binafsi bali ni utambuzi wa juhudi na matarajio ya watanzania wote.
Alisema shahada hiyo ni ishara ya utambuzi wa dhamira ya pamoja ya Watanzania wote katika kuleta maendeleo,ushirikiano na ustawi wa binadamu.
“Nilipokea kwa furaha habari za kutunukiwa heshima hii,lakini mara moja nikatambua kwamba si yangu peke yangu. Ni heshima inayoitambua dhamira yetu ya pamoja ya maendeleo, ushirikiano na maendeleo ya binadamu” alisema Dk Samia.
Hii ni shahada yake ya nane kutolewa kwa Rais Samia .
Aidha alisema shahada hiyo aliyopewa leo ni ishara ya urafiki wa muda mrefu kati ya Tanzania na Urusi ikiwa ni uthibitisho wa nafasi muhimu ya elimu katika kuunganisha mataifa.
Aidha alisema heshima hiyo inaakisi uhusiano wa kudumu kati ya nchi za Tanzania na Urusi ambazo zimeendelea kushirikiana katika sekta mbalimbali hususani elimu kwa miongo kadhaa sasa.
Katika hotuba yake ambayo viongozi wa watanzania waliopo Urusi na vyuo vya Urusi walisema ni iluiyiojaa mamlaka makubwa, Rais Samia alisema kwa miaka mingi watanzania walikuwa wanapata elimu inayochangia maendeleo ya Tanzania katika Nyanja mbalimbali jambo ambalo pia limeimarisha mahusiano ya watu wa pande zote mbili,
“Mama amezungumza nchi yetuj ina sifa sana. Tena sifa njema kwa kupata mwaliko wa Rais Vladmir Putin kuja hapoa ni kutambulika kwa Tanzania ni ishara njema na hotuba ya mama imeakisi matarajio” alisema Jefrey Mashauri Mwenyekiti wa wanafunzi wa Tanzania shirikishoi la Urusi (TASCARU).
Naye Mwenyekit wa watanznaia wanaoishi Urusi Pascal Gura alisema watanzania 300 wanaosihi hapo wameona fahari kubwa kukutana na kumsikiliza Rais Samia akionesha ni kwa namna gani kama Taifa Tanzania linaendelea kuwika.
Rais Samia katika hotuba yake alionesha jinsi Tanzania inavyoweza kufanikisha mambo wanaposaidiana na kushirikiana kwa maendeleo ya taifa.
Pia alikumbusha vijana kujipatia elimu huku wakizingatia kauli ya baba wa taifa mwalimu Julius Nyerere ambaye alifundisha kwamba maendeleo lazima daima yaweke mwanadamu katikati ya kila jambo.
Aidha alitaka vijana kuangalia taifa lao na kwamba dokumentari iliyooneshwa kabla ya kutunukiwa shahada kuhusu maendeleo ya Tanzania inawaonesha dhamira ya watanzania na ni muhumu kwao watambue umuhimu wao kwa taifa huku huku wakiyaakisi maneno ya baba wa taifa katika utumishi wao.
Tangu kuanzishwa kwa chuo hicho miaka ya 1960 watanzania 1,100 wamepata utaalamu mbalimbali kupitia hucho hicho.Idadi hiyo ni kati ya wanafunzi 5000 ambao wamepata taaluma zao nchini Urusi katika Nyanja mbalimbali ikiwamo udaktari uhandisi na wataalamu wa sayansi.
Rais katika hotuba yake pia alizungumzia makubaliano kadhaa yaliyotiwa saini yenye lengo la kuleta ushirikiano wa aina yake katika utafiti na elimu na ufundishaji.
Mwisho
MWANZA KINARA KATIKA USIMAMIZI WA MAAFA
habariNa, mwandishi wetu - Mwanza
Mkoa wa Mwanza umetajwa kuwa Kinara kwa kuratibu na kusimamia ipasavyo shughuli za kukabiliana na maafa, majanga na mawasiliano ya dharura kutokana na hatua mbalimbali za kuimarisha mifumo ya utayari na mwitikio wa dharura.
Sifa hizo zimetolewa Juni 4, 2026 na wataalamu wa Ofisi ya Waziri Mkuu wakati wa mafunzo ya Kamati za Usimamizi wa Maafa yanayofanyika mkoani Mwanza kwa siku mbili yakilenga kuongeza uwezo wa kukabiliana na majanga.
Akifungua mafunzo hayo, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mheshimiwa Said Mtanda amesema maafa yameendelea kuwa tishio kubwa duniani kutokana na athari zake kwa maisha ya watu, uchumi na maendeleo ya jamii.
Ametaja baadhi ya majanga yanayoikabili Tanzania kuwa ni mafuriko, ukame, maporomoko ya ardhi, matetemeko ya ardhi, mioto ya misitu na magonjwa ya mlipuko.
Kutokana na kuongezeka kwa matukio hayo Mhe. Mtanda amezitaka Wilaya zote Mkoani humo kuwa na mipango kazi na mifumo imara ya usimamizi wa maafa ili kuhakikisha maandalizi, mwitikio wa haraka na urejeshaji wa hali unafanyika kwa ufanisi.
Aliongezea kuwa, Serikali kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu imeendelea kuimarisha usimamizi wa maafa kwa kutumia Sera ya Taifa ya Usimamizi wa Maafa ya mwaka 2024 pamoja na Sheria ya Usimamizi wa Maafa Na. 6 ya mwaka 2022.
Mkuu wa Mkoa ameeleza kuwa mafunzo hayo yatawajengea uwezo viongozi na wataalamu katika utekelezaji wa sera, sheria na miongozo ya usimamizi wa maafa katika maeneo yao.
Aidha, ameipongeza Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutoa msaada kwa waathirika wa mafuriko Wilayani Kwimba, uliojumuisha tani tisa za mahindi, mablanketi, ndoo na vifaa vya wanafunzi.
Kwa upande wake, Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Usimamizi wa Maafa eneo la utafiti kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu Bw. Vanvaco Luvanda amesema mafunzo hayo ya siku mbili yanaendelea kutolewa nchini kote kwa lengo la kuongeza utayari na uwezo wa kitaalamu wa kukabiliana na maafa yanapotokea.
Alifafanua kuwa, uwepo wa mafunzo hayo yamekuja kwa wakati muafaka ambapo uzoefu unaonesha kuwa athari za maafa zinaendelea kuongezeka kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo mabadiliko ya tabianchi, ongezeko la shughuli za kibinadamu na changamoto nyingine zinazoweza kusababisha maafa.
=MWISHO=
DCEA, VETA Kuibua Matumaini Mapya kwa Waraibu Waliopona
habariMAMLAKA ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) na Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) zimeingia makubaliano ya ushirikiano yatakayowezesha waraibu waliopona matumizi ya dawa za kulevya kupata mafunzo ya ufundi stadi, hatua inayolenga kuwajengea uwezo wa kujitegemea kiuchumi na kuzuia kurejea kwenye matumizi ya dawa hizo.
TIMU KUTOKA OFISI YA WAZIRI MKUU YAFANYA MAZUNGUMZO NA KATIBU TAWALA MWANZA KUHUSU MASUALA YA USIMAMIZI WA MAAFA
habariNa, mwandishi wetu - Mwanza
Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa Mwanza Bw. Henry Mwaijega amekutana na kufanya mazungumzo timu ya Idara ya Usimamizi wa Maafa kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu walipomtembelea ofisini kw
ake leo 04 Juni, 2026 Jijini Mwanza.
Timu hiyo ipo mkoani Mwanza kwa lengo la kuongoza mafunzo ya usimamizi wa maafa kwa Kamati za Usimamizi wa Maafa mkoa pamoja na wadau mbalimbali, ikiwa ni sehemu ya juhudi za kuimarisha utayari, uratibu na uwezo wa kukabiliana na majanga katika ngazi ya mkoa.
Pamoja na mafunzo hayo, wanatarajia kuzindua Kituo cha Operesheni na Mawasiliano ya Dharura cha mkoa wa mwanza tarehe 05 juni, 2026.
=MWISHO=





















.jpg)

.jpg)




















