HABARI

SIASA

ELIMU

Recent Posts

MBUNGE ULENGE KUWAFUTA MACHOZI WENYE ULEMAVU TANGA: KUTOA MIGUU BANDIA 100, VITI MWENDO NA FIMBO

July 09, 2026 Add Comment



Na Mwandishi wa diGOtv, Tanga

WATU wenye ulemavu mkoani Tanga wamepata tabasamu jipya kufuatia Ofisi ya Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Tanga, Mhandisi Mwanaisha Ulenge, kutangaza neema ya kugawa miguu bandia 100, viti mwendo (wheelchairs), na fimbo kwa wasioona, sambamba na kuwafungulia fursa za kiuchumi kupitia mafunzo maalum.

Hatua hii ni mwendelezo wa mikakati thabiti ya Mbunge huyo katika kuwajali, kuwainua kiuchumi, na kurudisha matumaini kwa wananchi wenye mahitaji maalum mkoani hapa ili waweze kushiriki kikamilifu katika ujenzi wa Taifa na kujikwamua kimaisha.

Ugawaji wa Viti Mwendo na Fimbo (Kesho Ijumaa)

Katika kuhakikisha makundi yote yanafikiwa, Mhe. Ulenge kesho *Ijumaa (Julai 10, 2026)* anatarajia kugawa vifaa saidizi vifuatavyo kwa walengwa:

* *Viti Mwendo (Wheelchairs):* 20

* *Fimbo za watu wenye uoni hafifu:* 25


*MUHIMU KWA WENYE UHITAJI:* Watu wote wenye uhitaji wa viti mwendo na fimbo hizo wanaombwa kuwasiliana haraka kupitia namba ya simu *0753 210 211* ili kupewa maelekezo ya namna ya kuvipata.


*Zoezi la Kujaribisha Miguu Bandia (Limeanza Leo)*

Akitoa taarifa rasmi kwa umma kuhusu miguu bandia 100, Mhe. Ulenge amebainisha kuwa zoezi la kitabibu la kujaribisha miguu hiyo (*fittings*) kwa walengwa ambao tayari walishapimwa hatua ya awali na wataalamu kutoka *Taasisi ya Kamal Foundation*, *limeanza rasmi leo Alhamisi, Julai 9, 2026.*


Zoezi hili litaendelea hadi *Jumatatu, Julai 13, 2026*, kuanzia saa 2:00 asubuhi kila siku katika ukumbi wa *Regal Naivera* uliopo Tanga Mjini. Walengwa wote wanasisitizwa kufika bila kukosa.


*Matembezi ya Hisani na Hafla Kuu ya Makabidhiano*

Baada ya kukamilika kwa hatua ya kujaribisha viungo hivyo, kilele cha tukio hilo la kihistoria linatarajiwa kuwa *Jumanne ya Julai 14, 2026*. 


Siku hii muhimu itatanguliwa na *matembezi makubwa ya hisani* yatakayozunguka mitaa mbalimbali ya Jiji la Tanga kuhamasisha jamii, na kisha kuhitimishwa katika ukumbi wa Regal Naivera. Hapo ukumbini ndipo hafla kubwa ya kukabidhi miguu hiyo bandia kwa walemavu wote 100 itakapofanyika rasmi. Hatua hiyo inatarajiwa kuwasaidia walengwa wengi kurudisha uwezo wao wa kutembea na kufanya shughuli zao za uzalishaji mali kwa urahisi tofauti na ilivyokuwa awali.


*Mafunzo ya Sheria ya Asilimia 30 (Fursa za Kiuchumi)*

Ili kuhakikisha kundi hilo linapata ukombozi kamili wa kiuchumi badala ya kutegemea misaada pekee, hafla hiyo itaambatana na utoaji wa mafunzo maalum ya uwezeshaji.


Mhe. Ulenge alisema washiriki watapatiwa elimu ya kina kuhusu namna ya kunufaika na fursa za kisheria zinazoelekeza Mamlaka za Serikali kutenga asilimia 30 ya zabuni kwenye manunuzi ya umma kwa ajili ya vijana, wanawake, na watu wenye ulemavu. Mafunzo haya yanalenga kuwapa ujasiri wa kuomba zabuni na kufanya biashara rasmi na taasisi za Serikali.

RAIS DKT SAMIA SULUHU AHUDHURIA HALFA YA UWASILISHWAJI TAMKO LA PAMOJA LA MARIDHIANO YA KISIASA ZANZIBAR KATIKA VIWANJA VYA IKULU ZANZIBAR

July 09, 2026 Add Comment
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi wakati wakiwasili katika viwanja vya Ikulu Zanzibar kwa ajili ya kuhudhuria hafla ya uwasilishaji wa Tamko la Pamoja la Muafaka wa Kisiasa baina ya Chama cha Mapinduzi (CCM) na ACT-Wazalendo, tarehe 09 Julai, 2026. 







Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi akiwa na Mwenyekiti wa Chama cha ACT-Wazalendo Taifa Mhe. Othman Masoud Othman pamoja na Marais Wastaafu wa Zanzibar, Mhe. Dkt. Ali Mohamed Shein, Amani Abeid Karume wakishuhudia utiaji saini wa ajenda zilizokubaliwa na pande zote mbili kwa ajili ya kufanyiwa kazi baada ya Tamko la Pamoja la Muafaka wa Kisiasa baina ya Chama cha Mapinduzi (CCM) na ACT-Wazalendo, katika viwanja vya Ikulu Zanzibar, tarehe 09 Julai, 2026. Kushoto anaye saini ni Naibu Katibu Mkuu wa ACT-Wazalendo- Zanzibar Omary Ally Shehe pamoja na Naibu Katibu wa Chama cha Mapinduzi CCM- Zanzibar Dkt. Mohammed Said Dimwa


TANZANIA YAITAKA WIPO KUJENGA MFUMO JUMUISHI WA MILIKI UBUNIFU ILI NCHI ZINAZOENDELEA ZINUFAIKE NA AKILI MNEMBA

July 09, 2026 Add Comment
-Geneva, Julai 2026

Tanzania imelitaka Shirika la Miliki Ubunifu Duniani (WIPO) kujenga mfumo wa kimataifa wa miliki bunifu unaowezesha nchi zinazoendelea kunufaika na maendeleo ya akili mnemba (Artificial Intelligence–AI), huku ikisisitiza umuhimu wa kuhamasisha matumizi ya teknolojia na kujengea watu uwezo.

WAZIRI SANGU AKUTANA NA MTENDAJI MKUU WAMOWASALAT QATAR

July 09, 2026 Add Comment
- Wajadili Fursa za Ajira kwa Madereva wa Kitanzania

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Sangu amekutana na kufanya mazungumzo na Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Usafirishaji ya MOWASALAT, Ahmad Hassan Al Obaidly, alipofanya ziara katika kampuni hiyo tarehe 8 Julai, 2026, jijini Doha, nchini Qatar.

WAZIRI SANGU AHIMIZA NIDHAMU NA UWAJIBIKAJI KWA WAFANYAKAZI WA KITANZANIA NCHINI QATAR

July 09, 2026 Add Comment
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Sangu akizungumza na Wafanyakazi Madereva wa Kitanzania wanaofanya kazi katika kampuni ya MOWASALAT iliyopo nchini Qatar alipofanya ziara katika kampuni hiyo, tarehe 8 Julai, 2026.

TEA YAIMARISHA ELIMU YA AMALI KWA VIFAA VYA KISASA VYA USHONAJI

July 08, 2026 Add Comment
Na Mwandishi Wetu

WANAFUNZI wanaosoma mkondo wa elimu ya amali katika Shule ya Sekondari Dar es Salaam wameeleza kuwa ufadhili wa vifaa vya ushonaji uliotolewa na Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA) umeleta mapinduzi makubwa katika utoaji wa mafunzo ya vitendo, hatua inayowajengea uwezo wa kujiajiri na kuanzisha biashara mara baada ya kuhitimu masomo yao.

BANDARI YA FUMBA YATAJWA KUWA LANGO LA FURSA MPYA ZA BIASHARA AFRIKA MASHARIKI

Kajunason July 08, 2026 Add Comment
Na Mwandishi Wetu.

Zanzibar. Equity Group, kwa kushirikiana na Mamlaka ya Kukuza Uwekezaji Zanzibar (ZIPA), imeongoza ujumbe wa viongozi na wadau kutoka Tanzania Bara na Zanzibar kutembelea mradi wa Bandari ya Fumba, hatua inayolenga kuhamasisha uwekezaji na kuonyesha fursa za maendeleo ya kiuchumi zilizopo visiwani humo.

Ziara hiyo ni sehemu ya juhudi za kuwaleta pamoja wawekezaji na taasisi za Serikali ili kuimarisha mazingira ya biashara na kuongeza uwekezaji katika miradi ya kimkakati itakayochochea ukuaji wa uchumi.
Equity Bank, ambayo ni mmoja wa wafadhili wakuu wa mradi wa Bandari ya Fumba, imesema itaendelea kuunga mkono uwekezaji katika miundombinu yenye uwezo wa kuchochea biashara, kuongeza ajira na kuimarisha ushindani wa Zanzibar na Tanzania katika soko la kikanda na kimataifa.

Benki hiyo imeeleza kuwa dhamira yake inaenda zaidi ya utoaji wa huduma za kifedha, kwa kuwezesha ushirikiano kati ya wawekezaji wa ndani na wa kimataifa pamoja na mamlaka za udhibiti ili kujenga mazingira rafiki ya uwekezaji.

Aidha, juhudi hizo zinaunga mkono utekelezaji wa Eneo Huru la Biashara la Afrika (AfCFTA), kwa lengo la kuimarisha biashara ya kikanda, kuvutia mitaji mipya na kufungua fursa zaidi za maendeleo ya uchumi endelevu nchini Tanzania na barani Afrika.

TFS YAPOKEA WAGENI WA OFA YA SABASABA

July 08, 2026 Add Comment
Na Mwandishi wetu Bagamoyo

Wakala wa Misitu nchini (TFS) wamepokea wameanza kupokea wageni kutokana na Punguzo la Msimu huu wa sabasaba katika kutembelea vituo vyao vya utalii.

WAZIRI SANGU AKUTANA NA KUZUNGUMZA NA WAZIRI WA KAZI QATAR

July 08, 2026 Add Comment
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Sangu, akiwa kaitika mazungumzo na Waziri wa Kazi wa Qatar, Mhe. Dkt. Ali bin Samikh Al Marri, leo Julai 8, 2026, jijini Doha, nchini Qatar.

WANANCHI, WADAU WAALIKWA TAMASHA LA KIZIMKAZI 2026 VISIWANI ZANZIBAR

July 08, 2026 Add Comment
Na Said Mwishehe,Michuzi TV-Zanzibar

KIZIMKAZI Kumenoga! Hiyo ndio kauli mbiu iliyobeba Tamasha la Kizimkazi 20226 linatarajiwa kufanyika kuanzia Agosti 12 hadi Agosti 14 mwaka huu likiwa limesheheni fursa lukuki .

WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA DKT. HOMERA ATEMBELEA BANDA LA OFISI YA WAKILI MKUU WA SERIKALI SABASABA

July 08, 2026 Add Comment
Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Juma Homera akisaini kitabu cha wageni alipotembelea banda la Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali wakati wa Maonesho ya Sabasaba yaliyofanyika Jijini Dar es Salaam.

NAIBU WAKILI MKUU WA SERIKALI ATEMBELEA MAONESHO SABASABA

July 08, 2026 Add Comment
Naibu Wakili Mkuu wa Serikali Bi. Alice Mtulo (aliyesimama katikati) akiwa pamoja na watumishi wa Ofisi ya Wakili Mkuu wakati wa Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba) yanayoendelea Jijini Dar es Salaam.

KAMANDA MULIRO AIPONGEZA NEMC KWA JUHUDI ZA USIMAMIZI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA

July 08, 2026 Add Comment
-Aipongeza NEMC kwa juhudi za Usimamizi na Uhifadhi wa Mazingira

SAT, I AM ORGANIC WATUMIA SABASABA KUHAMASISHA KILIMO HAI NA AFYA BORA

July 08, 2026 Add Comment

Meneja miradi wa Shirika la kilimo Endelevu Tanzania (SAT), Bw. Peter Mwangalo, akiwaonyesha wananchi na waandishi wa habari (hawapo pichani) bidhaa mbalimbali zinazotokana na kilimo hai, ambacho huzalisha mazao bila matumizi ya kemikali na mbolea zenye madhara, katika Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara (Sabasaba) yanayoendelea katika Viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere, Dar es Salaam, chini ya uratibu wa Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TANTRADE).
Meneja miradi wa Shirika la kilimo Endelevu Tanzania (SAT), Bw. Peter Mwangalo, akitoa maelezo kwa waandishi wa habari kuhusu bidhaa zinazozalishwa kwa njia ya kilimo hai katika Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara (Sabasaba), yanayofanyika Dar es Salaam chini ya uratibu wa TANTRADE.
Meneja miradi wa Shirika la kilimo Endelevu Tanzania (SAT), Bw. Peter Mwangalo akitoa maelezo kwa waandishi wa habari kuhusu bidhaa zinazozalishwa kwa njia ya kilimo hai katika Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara (Sabasaba), yanayofanyika Dar es Salaam chini ya uratibu wa TANTRADE.
Meneja wa Duka la I AM ORGANIC, Bi. Dainess Sunday, akitoa elimu kwa wakazi wa Dar es Salaam waliotembelea banda la I AM ORGANIC kuhusu bidhaa za kilimo hai katika Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara (Sabasaba), yanayoendelea katika Viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere, Dar es Salaam.
Baadhi ya wakazi wa Dar es Salaam wakitembelea banda la SAT na I AM ORGANIC katika Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara (Sabasaba), yanayoendelea katika Viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere, Dar es Salaam.
Meneja miradi wa Shirika la kilimo Endelevu Tanzania (SAT), Bw. Peter Mwangalo, akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusu kilimo hai katika Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara (Sabasaba), Dar es Salaam.

***

#SAT na I AM ORGANIC waendelea kuhamasisha kilimo hai kwa Watanzania

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam

Takribani wakulima 1,000 kutoka maeneo mbalimbali nchini pamoja na wajasiriamali na wafanyabiashara wadogo na wa kati (SMEs) 50 wamejengewa uwezo kuhusu kilimo hai, ambacho hakitumii kemikali na kinachochangia kukuza mnyororo wa thamani kupitia masoko ya bidhaa zinazozalishwa kwa njia salama kwa afya na mazingira.

TANZANIA NA QATAR KUENDELEA KUSHIRIKIANA KUFUNGUA FURSA ZA AJIRA KWA VIJANA

July 07, 2026 Add Comment
Na: OWM (KAM) – Doha, Qatar

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Sangu, amesema Tanzania na Qatar zimeendelea kushiurikiana kwa karibu katika sekta mbalimbali, ikiwemo masuala ya ajira ambapo tangu nchi hizo ziliposaini makubaliano ya ushirikiano wa ajira mwaka 2018 mafanikio makubwa yameonekana katika kuongezeka kwa fursa za ajira kwa Watanzania.

UTPC YAWAWEZESHA WAANDISHI WA HABARI WANAWAKE KUKABILIANA NA VITISHO VYA KIDIJITALI

July 07, 2026 Add Comment


Mkurugenzi wa Umoja wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC), Kenneth Simbaya, akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya Usalama wa Kidijitali na Ukatili wa Kijinsia Mtandaoni kwa Waandishi wa Habari Wanawake yaliyofanyika mjini Morogoro.
Mkurugenzi wa Umoja wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC), Kenneth Simbaya, akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya Usalama wa Kidijitali na Ukatili wa Kijinsia Mtandaoni kwa Waandishi wa Habari Wanawake yaliyofanyika mjini Morogoro.
Washiriki wa mafunzo ya usalama wa kidijitali kwa waandishi wa habari wa kike wakipiga picha ya pamoja

Na Elizabeth Cosmas, Morogoro

Umoja wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC) umeendesha mafunzo maalumu ya Usalama wa Kidijitali na Ukatili wa Kijinsia Mtandaoni kwa Waandishi wa Habari Wanawake, yakilenga kuimarisha uwezo wao wa kutumia mazingira ya kidijitali kwa usalama, kujiamini na ufanisi katika kutekeleza majukumu yao ya kitaaluma.

MMS ATEMBELEA WADAU MAONESHO YA SABASABA 2026

July 07, 2026 Add Comment
Mkemia Mkuu wa Serikali, Dkt. Fidelice Mafumiko, akisaini kitabu cha wageni alipowasilikwemye viwanja vya maonyesho vya Mwalimu Nyerere vilivyopo Barabara ya Kilwa Dar es Salaam Julai 6, 2026.

VIONGOZI NA WATUMISHI WA TRA WASIMAMA NA KUPIGA MAKOFI KWA DAKIKA 1 KUWASHUKURU WALIPAKODI

July 07, 2026 Add Comment

 

Viongozi na watumishi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) wamesimama na kupiga makofi kwa muda wa dakika moja wakati wa kikao cha tathmini ya utendaji kazi kwa mwaka wa fedha 2025/2026 ikiwa ni ishara ya kuwapongeza na kuwashukuru Walipakodi kote nchini kwa kuendelea kulipa kodi kwa hiari.

TBS YATOA ELIMU YA UTHIBITISHAJI WA BIDHAA KWA WAJASIRIAMALI SABASABA

July 07, 2026 Add Comment
SHIRIKA la Viwango Tanzania (TBS) limeendelea kutumia Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba) kutoa elimu na kuwahamasisha wajasiriamali kuthibitisha ubora wa bidhaa zao ili kukidhi matakwa ya sheria za viwango na kuongeza ushindani wa bidhaa hizo katika soko la ndani na nje ya nchi.

TIRDO YAWAWEZESHA WAJASIRIAMALI KWA TEKNOLOJIA YA KUCHAKATA NGOZI

July 07, 2026 Add Comment
NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

Matumizi ya kemikali katika uchakataji wa ngozi yanatarajiwa kupungua kufuatia ubunifu wa Shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania (TIRDO) wa kubuni dawa ya asili inayotokana na mimea, teknolojia inayolenga kulinda mazingira, afya za watumiaji na kuongeza ushindani wa bidhaa za ngozi za Tanzania katika masoko ya ndani na kimataifa.

BODI YA UTALII TANZANIA IMETAKIWA KUZINGATIA UBUNIFU, UWAJIBIKAJI NA UZALENDO KATIKA KUTEKELEZA MAJUKUMU YAKE PIA KUISHIRIKISHA SEKTA BINAFSI*

July 07, 2026 Add Comment

 



Bodi ya Wakurugenzi ya Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) imetakiwa kuisimamia ipasavyo Taasisi hiyo na kuishirikisha sekta binafsi ili kufikia malengo ya Taifa yaliyokusudiwa katika sekta ya Utalii.


Maelekezo hayo yametolewa na Waziri wa Maliasili na Utalii Dkt. Ashatu Kijaji (Mb) alipokutana na kufanya mazungumzo na Wajumbe Bodi hiyo Jijini Dar es Salaam kwa lengo la kufanya tathmini, kushauri na kuboresha ili kuiwezesha TTB kufikia malengo yaliyokusudiwa. 

Ameongeza kuwa ili kufikia malengo ya kuwa na watalii milioni nane ifikapo 2030 ni lazima Sekta binafsi ishirikishwe ipasavyo ili kukuza utalii na kuongeza ushindani wa Tanzania katika soko la kimataifa.

"Tushirikishe sekta binafsi ili tuweze kufikia malengo. Hata jumbe tunazozipeleka kwenye masoko tuwashirikishe sekta binafsi ili tuweze kufanikiwa kufikisha watalii milioni 8 na zaidi ifikapo mwaka 2030. Sekta binafsi iwe sehemu ya maisha yetu ya kila siku," amesema Dkt. Kijaji.

Aidha, ameitaka Bodi hiyo kuweka malengo yanayopimika yatakayowezesha kutathmini utendaji wake na kuongeza ufanisi katika kufikia azma ya Serikali ya kuongeza idadi ya watalii nchini.

Pia, amesisitiza umuhimu wa TTB kuendelea kufanya tafiti na kufuatilia mwenendo wa masoko mbalimbali ya utalii duniani ili kubaini mahitaji ya watalii na kuishauri Serikali pamoja na taasisi zake kuhusu maboresho yanayohitajika.

"Sisi ndio tuliopewa jukumu la kuiuza nchi huko nje, hivyo tunapaswa kuzishauri taasisi nyingine kuhusu mahitaji ya soko la kimataifa. Kwa mfano, TFS na taasisi nyingine zinapaswa kufahamu kwa wakati mahitaji ya watalii ili ziweze kuboresha huduma na bidhaa za utalii," amesema.

Akizungumzia matukio makubwa yanayotarajiwa kufanyika nchini, ikiwemo AFCON na Mkutano wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU), Dkt. Kijaji ameitaka Bodi ya Utalii kuhakikisha inajiandaa kikamilifu kutumia matukio hayo kama fursa ya kuitangaza Tanzania na vivutio vyake vya utalii katika masoko ya kimataifa.

"Tunayo matukio kadhaa makubwa yanayokuja mbele yetu. Tujipange vya kutosha kabla ya matukio hayo ili tuyatumie kama fursa ya kuitangaza Tanzania na kuongeza idadi ya watalii," amesema.

Ameongeza kuwa utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 unahitaji taasisi zote kupanga na kutekeleza mikakati kwa pamoja ili kuhakikisha malengo yaliyowekwa yanafikiwa kwa wakati.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya TTB, Mhe. Balozi Dkt. Ramadhani Kitwana Dau, amesema Bodi hiyo imeweka mikakati madhubuti ya kuhakikisha inafikia malengo ya Serikali katika sekta ya utalii. Amesisitiza kuwa moja ya malengo makuu ni kufikisha idadi ya watalii zaidi ya milioni 8 ifikapo mwaka 2030, sambamba na kuvuka lengo lililowekwa katika Ilani ya Chama Cha Mapinduzi.

Kikao hicho cha Dkt. Kijaji na Bodi ya Wakurugenzi ya TTB kimehudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Wizara, akiwemo Katibu Mkuu wa Wizara, Dkt. Hassan Abbas, Mkurugenzi wa Utawala, Benard Marcelline; Mkurugenzi wa Idara ya Utalii, Dkt. Theresa Mugobi, Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Emmanuel Buhohela, Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Utalii Tanzania (TTB),  Ephraim Mafuru; pamoja na wajumbe wa Bodi hiyo.






DKT. MWIGULU AALIKA WAFANYABIASHARA WA UFARANSA KUWEKEZA TANZANIA

July 06, 2026 Add Comment
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba, amewaalika wafanyabiashara wa Ufaransa kuwekeza Tanzania, akisisitiza kuwa mazingira mazuri ya uwekezaji yaliyopo nchini yanatoa fursa kubwa za kukuza biashara, kuzalisha ajira, kuhamisha teknolojia na ujuzi, pamoja na kuharakisha ujenzi wa uchumi wa viwanda wenye manufaa kwa Tanzania na Ufaransa.

TEA YAONGEZA JUHUDI ZA KUTAFUTA RASILIMALI KUSAIDIA MAGEUZI YA ELIMU

July 06, 2026 Add Comment
NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

MAMLAKA ya Elimu Tanzania (TEA) imeeleza kuwa imejikita katika kutafuta rasilimali zitakazowezesha utekelezaji wa Sera ya Elimu na Mafunzo ya mwaka 2023, kwa kuwekeza nguvu katika maeneo matatu ya kipaumbele ambayo ni ujenzi wa miundombinu kwa elimu ya lazima ya miaka 10, maendeleo ya mkondo wa amali pamoja na matumizi ya nishati safi na uhifadhi wa mazingira shuleni.

FCC YAIMARISHA ELIMU YA USHINDANI KWA WAFANYABIASHARA SABASABA

July 06, 2026 Add Comment
NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

WAFANYABIASHARA na wananchi kwa ujumla wametakiwa kutumia Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba) kutembelea banda la Tume ya Ushindani (FCC) ili kupata huduma mbalimbali za papo kwa papo pamoja na elimu kuhusu ulinzi wa mlaji, ushindani wa biashara na udhibiti wa bidhaa bandia.

WAZIRI WA ULINZI ATEMBELEA BANDA LA WIZARA YA NISHATI SABASABA

July 06, 2026 Add Comment




Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Mhe. Dkt. Rhimo Nyansaho ametembelea banda la Wizara ya Nishati katika Maonesho ya Kimataifa ya Biashara (Sabasaba) yanayoendelea katika viwanja vya Mwl. Nyerere jijini Dar es Salaam.


Katika Banda la Wizara amepata maelezo kuhusu Sera ya Nishati ya Mwaka 2015 pamoja na mikakati mingine inayosimamiwa na Wizara ya Nishati ukiwemo Mkakati wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia, Mkakati wa Matumizi Bora ya Nishati na Mkakati wa Taifa wa Mawasiliano wa Nishati Safi ya Kupikia.




WAZIRI NDEJEMBI AJADILI AWAMU YA PILI YA MRADI WA UMEME WA JUA KISHAPU NA WASHIRIKA WA MAENDELEO.

July 06, 2026 Add Comment




Na Mwandishi Wetu - Paris, Ufaransa

Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi, amekutana na kufanya mazungumzo na wawakilishi kutoka Wizara ya Fedha ya Ufaransa, Shirika la Maendeleo la Ufaransa (AFD) pamoja na kampuni ya SAGECOM, kwa lengo la kujadili utekelezaji wa awamu ya pili ya Mradi wa Uzalishaji Umeme wa Jua wa Megawati 100 unaotekelezwa katika Wilaya ya Kishapu, mkoani Shinyanga.


Mazungumzo hayo yamefanyika leo, Julai 6, 2026, katika Ofisi za Ubalozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania jijini Paris, Ufaransa.


Katika kikao hicho, Mhe. Ndejembi ameishukuru Serikali ya Ufaransa kupitia Wizara yake ya Fedha na Shirika la Maendeleo la Ufaransa (AFD) kwa kuendelea kuwa mshirika muhimu wa Tanzania katika utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo ya sekta ya nishati. Amesema ushirikiano huo umeendelea kuchangia kwa kiasi kikubwa katika kuimarisha upatikanaji wa nishati ya uhakika na kuchochea maendeleo ya kijamii na kiuchumi nchini.


Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa AFD, Bi. Sandra Kassab, ameipongeza Serikali ya Tanzania kupitia Wizara ya Nishati kwa hatua kubwa iliyofikiwa katika utekelezaji wa miradi ya nishati, hususan ile inayolenga kuongeza uzalishaji wa umeme na kuimarisha matumizi ya nishati safi. Aidha, ameahidi kuendeleza ushirikiano uliopo ili kuhakikisha miradi hiyo inatekelezwa kwa ufanisi na kuleta manufaa kwa wananchi wa Tanzania.




“WOMEN TAKING OVER” YA BARRICK YAWATIA MOYO WANAWAKE KUTOBAKI NYUMA SEKTA YA MADINI

July 06, 2026 Add Comment

  

Zoezi la kukata keki likiendelea wakati wa maadhimisho ya Siku ya Wanawake katika Sekta ya Madini, yaliyoandaliwa na Barrick North Mara chini ya kaulimbiu ya "Women Taking Over."
Baadhi ya wafanyakazi wanawake wa Barrick North Mara, Bulyanhulu pamoja na kampuni za wakandarasi wazawa wakiwa katika picha ya pamoja katika maadhimisho ya Siku ya Wanawake katika Sekta ya Madini yaliyofanyika katika Mgodi wa Dhahabu wa North Mara chini ya kaulimbiu ya "Women Taking Over"
Maonyesho ya mavazi na sare mbalimbali zinazotumika migodini yalikuwa miongoni mwa vivutio vilivyopamba maadhimisho ya Siku ya Wanawake katika Sekta ya Madini.
Meneja Mkuu wa Mgodi wa Barrick North Mara, Apolinary Lyambiko, akizungumza wakati wa maadhimisho ya Siku ya Wanawake katika Sekta ya Madini yaliyofanyika katika Mgodi wa Dhahabu wa North Mara.
Meneja Mahusiano Msaidizi wa Barrick North Mara, Nasieku Kisambu, akisoma risala kwa mgeni rasmi, akieleza mafanikio na shughuli mbalimbali zilizotekelezwa katika maadhimisho ya Siku ya Wanawake katika Sekta ya Madini yaliyofanyika Mgodi wa Dhahabu wa North Mara.

Baadhi ya washiriki walitunukiwa vyeti
Baadhi ya washiriki walitunukiwa vyeti
Baadhi ya washiriki walitunukiwa vyeti
Baadhi ya wanawake walioshiriki katika picha ya pamoja
Baadhi ya wanawake walioshiriki katika picha ya pamoja
Meneja Mkuu Apolinary Lyambiko akiwa na Maofisa waandamizi wa mgodi wa Barrick North Mara.

***

Katika kuendelea kuhamasisha usawa wa kijinsia na kuongeza ushiriki wa wanawake katika sekta ya madini, Kampuni ya Barrick imefanya maadhimisho makubwa ya Siku ya Wanawake katika Sekta ya Madini yaliyowakutanisha wafanyakazi wanawake kutoka migodi ya North Mara na Bulyanhulu pamoja na wanawake kutoka kampuni mbalimbali za wakandarasi wazawa wanaoshirikiana na migodi hiyo.