HABARI

SIASA

ELIMU

Recent Posts

TANZANIA NA OMAN KUIMARISHA USHIRIKIANO MASUALA YA KAZI NA AJIRA

TANZANIA NA OMAN KUIMARISHA USHIRIKIANO MASUALA YA KAZI NA AJIRA

January 28, 2026 Add Comment

Tanzania na Oman zimeendelea kuonyesha dhamira ya kuendelea kuimarisha ushirikiano katika masuala ya kazi na ajira ili kuongeza ajira zenye staha, kulinda haki za wafanyakazi na kukuza uchumi wa mataifa yote mawili.

Hayo yamebainishwa wakati wa kikao cha Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Clement Sangu na Waziri wa Kazi wa Oman, Dkt. Mahad bin Said bin Ali Baawain walipokutana katika Mkutano wa Mawaziri wa Kazi Duniani (Global Labour Market Conference) uliofanyika Jijini Riyadh, Saudi Arabia.

Aidha, katika kikao hicho Waziri Sangu alielezea umuhimu wa kukamilishwa na kutiwa saini kwa Hati ya Makubaliano ya Ushirikiano wa masuala ya Kazi na Ajira (MoU) kati ya nchi hizo mbili, ili kuweka mfumo rasmi na endelevu wa usimamizi wa masuala ya ajira, ulinzi wa haki za wafanyakazi na utatuzi wa changamoto za kiutendaji zinazojitokeza.

Vilevile, Waziri Sangu ameishukuru Serikali ya Oman kwa kuendelea kutoa fursa za ajira kwa Watanzania katika sekta mbalimbali. Pia, amesema idadi ya Watanzania wanaofanya kazi nchini Oman imeendelea kuongezeka , jambo linaloonesha kuimarika kwa mahusiano ya ajira kati ya mataifa hayo mawili.

Kwa upande mwingine, nchi hizo zimekubaliana kuendeleza ushirikiano kwa kuendelea kupanua wigo wa ajira zenye staha, kulinda haki za wafanyakazi na kuimarisha mahusiano ya kiuchumi na kijamii kati ya mataifa yetu mawili.

MUCOHAS,WIZARA YA AFYA,MUHAS ZATEKELEZA MRADI WA AFUA JUMUISHI KUBORESHA HUDUMA RAFIKI KWA WAGONJWA WA VVU NA WATUMIAJI DAWA ZA KULEVYA

January 28, 2026 Add Comment


Chuo cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUCOHAS) kwa kushirikiana Wizara ya Afya na Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi (MUHAS), zinaendelea kutekeleza mradi wa Afua Jumuishi (Total Facility Approach) unaolenga kuondoa unyanyapaa na ubaguzi miongoni mwa watoa huduma za afya kwa wagonjwa wanaoishi na Virusi vya Ukimwi (VVU) pamoja na watumiaji wa dawa za kulevya. 

Kikao cha siku tano kinafanyika mkoani Morogoro, kikilenga kuandaa nyenzo za  kufundishia ili kuwajengea uwezo walimu  na wanafunzi wa vyuo vya kati, juu ya unyanyapaa na ubaguzi.

Akizungumza kuhusu utekelezaji wa mradi huo, Mkuu wa Chuo cha MUCOHAS, Dkt. Bonny Betson, amesema mradi huo umejikita katika kuboresha uelewa, mitazamo na ujuzi wa watoa huduma ili kuhakikisha huduma za afya zinazotolewa ni jumuishi, rafiki na zenye kuzingatia utu wa kila mteja.

“Huu ni mwaka wa tatu tangu tulipoanza mradi huu, na kwa sasa tumetekeleza awamu ya kwanza hapa MUCOHAS kwa wanafunzi na walimu, baada ya hapo tunapitia mtaala mdogo tulioutengeneza mahsusi kwa ajili ya kuendesha mafunzo haya,” amesema Dkt. Betson.

Ameongeza kuwa kabla ya kuandaa mtaala huo, utafiti wa awali ulifanyika kwa wanafunzi na walimu waliopata mafunzo ili kubaini mahitaji halisi na changamoto zilizopo katika utoaji wa huduma na matokeo ya utafiti huo yalitumika kutengeneza mtaala unaolenga kutumika pia katika vyuo vingine vya afya nchini, ikiwa ni hatua muhimu ya kupunguza unyanyapaa na ubaguzi miongoni mwa watoa huduma za afya.

Utekelezaji wa mradi wa Afua Jumuishi unaendana na malengo ya Serikali kupitia Wizara ya Afya ya kuboresha huduma za afya kwa wananchi, hususan katika kuondoa unyanyapaa unaodhorotesha upatikanaji  na utumiaji wa huduma kwa watu wanaoishi na VVU Pamoja na watumiaji wa madawa ya kulevya.


Hili litachangia katika mikakati ya Serikali iliyowekwa  ili kutokomeza maambukizi ya VVU ifikapo mwaka 2030, kwa kuimarisha utoaji wa huduma rafiki, jumuishi na zenye usawa kwa wote.




VYANZO VYA MAJI KUENDELEA KUTUNZWA KUONGEZA UHAKIKA WA HUDUMA YA MAJI.

VYANZO VYA MAJI KUENDELEA KUTUNZWA KUONGEZA UHAKIKA WA HUDUMA YA MAJI.

January 28, 2026 Add Comment

Waziri wa Maji Mhe. Jumaa Aweso,akizungumza wakati wa Mkutano wa Tisa wa mwaka wa Bodi  za Maji za Mabonde nchini uliofanyika leo Januari 28,2026  Jiji la Dodoma.

.....

Waziri Wa Maji Mhe. Jumaa Aweso  amewataka wakurugenzi wa bodi za maji za mabonde nchini kuonyesha umuhimu wa taasisi hizo kwa wananchi kwa vitendo kwa kutoa huduma sahihi.

Waziri Aweso ametoa maelekezo hayo katika kikao cha Bodi za maji za mabonde nchini katika ukumbi wa Jiji la Dodoma.

Aweso ambaye ndiye mgeni rasmi katika kikao hicho amewataka viongozi wa mabonde hayo kutambulika kwa utoaji wa huduma na si kutambulika kwa sifa mbaya kwa wananchi na serikali ikiwemo utozaji wa Kodi zisizi halali.

Aidha Serikali bado inaendelea na mpango mkakati iliyojiwekea katika kujenga mabwawa ya kimkakati kuendelea kupanda miti rafiki wa maji kwa mazingira Ili kuboresha vyanzo vya maji na kutoa huduma ya uhakika kwa wananchi.

Nae Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji Mhandisi Mwajuma Waziri amewataka wakurugenzi na wenyeviti wa Bodi za maji za mabonde nchini kuendelea kutunza vyanzo vya maji Ili kuwa na uhakika wa huduma ya Maji kwa mwananchi.

Ameeleza kuwa vyanzo vya maji nchini ni muhimu katika kikao mabonde yanakuwa na maji ya kutosha kutoa huduma kwa wananchi.

Kadhalika Ili kuwe na uhakika wa utunzwaji wa vyanzo vya maji, amezitaka Bodi hizo kushirikiana na jamii na wadau wa mazingira ikiwemo Ofisi ya Waziri Mkuu TAMISEMI pamoja na taasisi zinazojihusisha na mazingira, Ili kuweka mipango mikakati ya Pamoja katika utunzwaji wa vyanzo vya maji.

Waziri wa Maji Mhe. Jumaa Aweso,akizungumza wakati wa Mkutano wa Tisa wa mwaka wa Bodi  za Maji za Mabonde nchini uliofanyika leo Januari 28,2026  Jiji la Dodoma.

Waziri wa Maji Mhe. Jumaa Aweso,akizungumza wakati wa Mkutano wa Tisa wa mwaka wa Bodi  za Maji za Mabonde nchini uliofanyika leo Januari 28,2026  Jiji la Dodoma.

TANESCO YAFANYA UKAGUZI WA MITA KITAALAMU KUBAINI UKWELI MALALAMIKO YA UMEME KUISHA HARAKA YAGUNDUA MITA ZIPO SAWA

January 28, 2026 Add Comment







Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) limefanya ukaguzi wa kitaalamu wa mita za umeme kwa baadhi ya wateja waliowasilisha malalamiko hayo kwa njia za mitandao katika maeneo ya Tabata Kimanga na Kimara Suka jijini Dar es Salaam.

Malalamiko hayo yaliibuliwa na baadhi ya wananchi mitandaoni na kwenye vyombo vya habari kuhusu madai ya umeme kuisha haraka bila sababu ya msingi.


Zoezi hilo lilifanyika Januari 27, 2026, likiongozwa na Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano na Huduma kwa Wateja wa TANESCO, Bi. Irene Gowelle, akiambatana na timu ya wataalamu wa Shirika, kwa lengo la kubaini chanzo halisi cha changamoto hiyo na kujiridhisha kuhusu ufanisi wa utendaji wa mita za wateja.


*Matokeo ya Ukaguzi*


Baada ya kufanyiwa vipimo vya kitaalamu, TANESCO imebaini kuwa mita zote zilizokaguliwa zilikuwa salama na zinafanya kazi kwa usahihi, kinyume na madai yaliyokuwa yakitolewa kuwa mita hizo zina kasoro ya kiutendaji.

Hata hivyo, ukaguzi umeonesha kuwa vyanzo vilivyopelekea wateja waliokaguliwa kulalamika umeme kuisha kwa haraka ni uchakavu wa mtandao wa nyaya za umeme (wiring) ndani ya nyumba, hali iliyosababisha umeme kuvuja bila mtumiaji kugundua.


Aidha, matumizi holela ya umeme yameonekana kuchangia kwa kiasi kikubwa changamoto hiyo.

Akizungumza kuhusu zoezi hilo, Bi. Gowelle amesema
“Baada ya kuona malalamiko yanaongezeka, tuliona ni muhimu kufika moja kwa moja kwa baadhi ya wateja waliolalamika. Tulifanya ukaguzi wa kitaalamu, tukazima vifaa vya umeme na kufuatilia usomaji wa mita, lakini bado uniti ziliendelea kupungua. Hii ilithibitisha kuwepo kwa hitilafu katika mfumo wa wiring za ndani ya nyumba na sio mita."


Katika nyumba moja iliyopo Tabata, ukaguzi ulibaini kuwa uchakavu wa mtandao wa nyaya (wiring) ulisababisha upotevu wa takribani uniti mbili za umeme, hali iliyomfanya mteja kutumia zaidi ya shilingi 30,000 za ziada kwa mwezi kuliko matumizi yake halisi.


Kwa upande mwingine, katika nyumba ya mteja mmoja eneo la Kimara Suka, timu ya ukaguzi ilishuhudia matumizi yasiyo bora ya umeme, ikiwemo kuwasha taa wakati wa mchana, hali iliyotajwa kuweza kuchangia kuisha kwa umeme kwa.


Wateja Waliokaguliwa


Miongoni mwa wateja waliokaguliwa ni Devotha Kihwelo, mwandishi wa Gazeti la Mwananchi na mkazi wa Tabata, ambaye taarifa yake iliifanya TANESCO kuwajibika kwa kuchukua hatua ya kufanya ukaguzi huo ambapo Baada ya uchunguzi, ilibainika kuwa nyumba aliyokuwa akiishi ilikuwa na hitilafu kwenye wiring ambayo ilikua ya muda mrefu hali iliyosababisha umeme kupotea.


Wateja wengine waliokaguliwa ni John Vincent wa Tabata Kimanga na Crispin Mizambwa wa Kimara Suka.


Kwao, ukaguzi umebaini kuwa mita zao zilikuwa hazina changamoto yoyote, na matumizi yao ya wastani wa uniti 2–3 kwa siku yaliendana na vifaa walivyokuwa wakitumia.


Kutokana na matokeo hayo, TANESCO ilijiridhisha kuwa madai ya kuisha kwa umeme bila sababu ya msingi hayakusababishwa na ubovu wa mita na kwamba mita zilikua salama na sawa kiutendaji.


Ushauri kwa Wateja


TANESCO imetoa elimu ya sababu zinazoweza kuchangia umeme kuisha haraka kuwa ni pamoja na ;
• Uchakavu wa mtandao wa nyaya za ndani ya nyumba (wiring)


• Matumizi holela ya umeme
• Matumizi ya vifaa vya zamani ,vilivyokaa muda mrefu au visivyo na ufanisi wa matumizi ya umeme kidogo


• Kutotumia vifaa vyenye teknolojia ya matumizi fanisi (energy efficiency)



Bi. Gowelle amewashauri wateja kufanya jaribio rahisi la kujitathmini kabla ya kulalamika “Wateja wazime vifaa vyote vya umeme, wasome kiwango cha uniti, wakae kwa muda usiopungua saa nne, kisha wasome tena. Endapo uniti zitakuwa zimepungua, wawasiliane na TANESCO kwa ukaguzi. Ikiwa hazijapungua, basi changamoto sio mita bali ni matumizi ya vifaa vyao au mfumo wa wiring zao za ndani umechoka.”


TANESCO imetoa wito kwa wateja wote wanaokumbana na changamoto za umeme kuisha haraka kuwasiliana na Shirika moja kwa moja kwa msaada badala ya kuamini au kusambaza taarifa zisizothibitishwa , ili kufanyiwa ukaguzi na kupata ufumbuzi wa kitaalamu unaolenga kupunguza gharama zisizo za lazima kwa wateja wake.



TANESCO YAFANYA UKAGUZI WA MITA KITAALAMU KUBAINI UKWELI MALALAMIKO YA UMEME KUISHA HARAKA YAGUNDUA MITA ZIPO SAWA

TANESCO YAFANYA UKAGUZI WA MITA KITAALAMU KUBAINI UKWELI MALALAMIKO YA UMEME KUISHA HARAKA YAGUNDUA MITA ZIPO SAWA

January 28, 2026 Add Comment

 **


📌 Ni kufuatia malalamiko ya baadhi ya wateja kwenye mitandao ya kijamii na vyombo vya habari


📌 Chanzo cha tatizo kwa mita zilizokaguliwa chatajwa kuwa ni uchakavu wa wiring za ndani ya nyumba na tabia holela za matumizi ya umeme


📌 Shirika kuongeza kasi ya utoaji wa elimu ya matumizi bora ya umeme kwa wananchi.


Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) limefanya ukaguzi wa kitaalamu wa mita za umeme kwa baadhi ya wateja waliowasilisha malalamiko hayo kwa njia za mitandao katika maeneo ya Tabata Kimanga na Kimara Suka jijini Dar es Salaam.


Malalamiko hayo yaliibuliwa na baadhi ya wananchi mitandaoni na kwenye vyombo vya habari kuhusu madai ya umeme kuisha haraka bila sababu ya msingi.


Zoezi hilo lilifanyika Januari 27, 2026, likiongozwa na Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano na Huduma kwa Wateja wa TANESCO, Bi. Irene Gowelle, akiambatana na timu ya wataalamu wa Shirika, kwa lengo la kubaini chanzo halisi cha changamoto hiyo na kujiridhisha kuhusu ufanisi wa utendaji wa mita za wateja.


*Matokeo ya Ukaguzi*


Baada ya kufanyiwa vipimo vya kitaalamu, TANESCO imebaini kuwa mita zote zilizokaguliwa zilikuwa salama na zinafanya kazi kwa usahihi, kinyume na madai yaliyokuwa yakitolewa kuwa mita hizo zina kasoro ya kiutendaji.


Hata hivyo, ukaguzi umeonesha kuwa vyanzo vilivyopelekea wateja waliokaguliwa kulalamika umeme kuisha kwa haraka  ni uchakavu wa mtandao wa nyaya za umeme (wiring) ndani ya nyumba, hali iliyosababisha umeme kuvuja bila mtumiaji kugundua. 


Aidha, matumizi holela ya umeme yameonekana kuchangia kwa kiasi kikubwa changamoto hiyo.


Akizungumza kuhusu zoezi hilo, Bi. Gowelle amesema

“Baada ya kuona malalamiko yanaongezeka, tuliona ni muhimu kufika moja kwa moja kwa baadhi ya wateja waliolalamika. Tulifanya ukaguzi wa kitaalamu, tukazima vifaa vya umeme na kufuatilia usomaji wa mita, lakini bado uniti ziliendelea kupungua. Hii ilithibitisha kuwepo kwa hitilafu katika mfumo wa wiring za ndani ya nyumba na sio mita."


Katika nyumba moja iliyopo Tabata, ukaguzi ulibaini kuwa uchakavu wa mtandao wa nyaya (wiring) ulisababisha upotevu wa takribani uniti mbili za umeme, hali iliyomfanya mteja kutumia zaidi ya shilingi 30,000 za ziada kwa mwezi kuliko matumizi yake halisi.


Kwa upande mwingine, katika nyumba ya mteja mmoja eneo la Kimara Suka, timu ya ukaguzi ilishuhudia matumizi yasiyo bora ya umeme, ikiwemo kuwasha taa wakati wa mchana, hali iliyotajwa kuweza kuchangia kuisha kwa umeme kwa.


*Wateja Waliokaguliwa*

Miongoni mwa wateja waliokaguliwa ni Devotha Kihwelo, mwandishi wa Gazeti la Mwananchi na mkazi wa Tabata, ambaye taarifa yake iliifanya TANESCO kuwajibika kwa kuchukua hatua ya kufanya ukaguzi huo ambapo Baada ya uchunguzi, ilibainika kuwa nyumba aliyokuwa akiishi ilikuwa na hitilafu kwenye wiring ambayo ilikua ya muda mrefu hali iliyosababisha umeme kupotea.


Wateja wengine waliokaguliwa ni John Vincent wa Tabata Kimanga na Crispin Mizambwa wa Kimara Suka. 


Kwao, ukaguzi umebaini kuwa mita zao zilikuwa hazina changamoto yoyote, na matumizi yao ya wastani wa uniti 2–3 kwa siku yaliendana na vifaa walivyokuwa wakitumia.


Kutokana na matokeo hayo, TANESCO ilijiridhisha kuwa madai ya kuisha kwa umeme bila sababu ya msingi hayakusababishwa na ubovu wa mita na kwamba mita zilikua salama na sawa kiutendaji.


*Ushauri kwa Wateja*


TANESCO imetoa elimu ya sababu zinazoweza kuchangia umeme kuisha haraka kuwa ni pamoja na ;

Uchakavu wa mtandao wa nyaya za ndani ya nyumba (wiring)

Matumizi holela ya umeme

Matumizi ya vifaa vya zamani ,vilivyokaa muda mrefu au visivyo na ufanisi wa matumizi ya umeme kidogo

Kutotumia vifaa vyenye teknolojia ya matumizi fanisi (energy efficiency)


Bi. Gowelle amewashauri wateja kufanya jaribio rahisi la kujitathmini kabla ya kulalamika “Wateja wazime vifaa vyote vya umeme, wasome kiwango cha uniti, wakae kwa muda usiopungua saa nne, kisha wasome tena. Endapo uniti zitakuwa zimepungua, wawasiliane na TANESCO kwa ukaguzi. Ikiwa hazijapungua, basi changamoto sio mita bali ni matumizi ya vifaa vyao au mfumo wa wiring zao za ndani umechoka.”


*Wito kwa Umma*

TANESCO imetoa wito kwa wateja wote wanaokumbana na changamoto za umeme kuisha haraka kuwasiliana na Shirika moja kwa moja kwa msaada badala ya kuamini au kusambaza taarifa zisizothibitishwa , ili kufanyiwa ukaguzi na kupata ufumbuzi wa kitaalamu unaolenga kupunguza gharama zisizo za lazima kwa wateja wake.

TANZANIA YAVUTIA WAWEKEZAJI KATIKA JUKWAA LA WIKI YA NISHATI INDIA

January 28, 2026 Add Comment




Na Mwandishi Wetu

Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba, ameshiriki katika mdahalo wa Mawaziri kuhusu uwekezaji na uimarishaji wa ushirikiano wa kimataifa katika sekta ya mafuta na gesi, ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Wiki ya Nishati ya India (India Energy Week – IEW 2026) yanayoendelea kufanyika Goa, India.

Akizungumza katika mdahalo huo uliofanyika leo Januari 28, 2026, Mhe. Makamba ameeleza kuwa Tanzania inaendelea kuweka mazingira wezeshi ya uwekezaji kwa kuzingatia fursa mbalimbali zilizopo katika sekta ya mafuta na gesi.

Amebainisha kuwa tafiti za kuchukua taarifa za mitetemo zinaendelea kufanyika katika vitalu vya Eyasi–Wembere, Lindi na Mtwara, sambamba na kukamilisha majadiliano na wawekezaji mbalimbali kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mikubwa ikiwemo Mradi wa Gesi Asilia Kimiminika (LNG).

Aidha, amesema Serikali inaendelea kuwekeza katika miradi ya usambazaji wa gesi kwa matumizi ya viwandani, uzalishaji wa umeme, matumizi ya majumbani pamoja na kuendesha magari.

“Sekta ya mafuta na gesi ni sekta muhimu na wezeshi katika kukuza uchumi wa taifa. Tanzania, kama zilivyo nchi nyingine zenye rasilimali za gesi asilia na mafuta, imeweka msisitizo mkubwa katika ushirikiano na sekta binafsi ili kunufaika na teknolojia na mitaji,” amesema Mhe. Makamba.

Amefafanua kuwa mahitaji ya nishati nchini yanaendelea kuongezeka kutokana na ukuaji wa kasi wa uchumi, hali inayoongeza uhitaji wa nishati ya uhakika na endelevu.

Pia, amesema jiografia ya Tanzania inaipa nchi fursa ya kuhudumia nchi jirani kupitia bandari zake pamoja na kuunganisha mifumo ya umeme na nchi za Afrika Mashariki na Kusini mwa Jangwa la Sahara, huku ikizingatia ulinzi wa mazingira.

Vilevile, Mhe. Makamba amesema Serikali inasisitiza kuwa mpito kuelekea matumizi ya nishati safi na rafiki kwa mazingira lazima uwe wa haki, usiomwacha mwananchi yeyote nyuma, kwa kuhakikisha upatikanaji wa nishati ya gharama nafuu, salama na ya uhakika.

Maadhimisho ya Wiki ya Nishati ya India (IEW 2026) yanaendelea kutoa fursa kwa Tanzania kujitangaza katika majukwaa ya kimataifa, kuvutia wawekezaji zaidi na kuchochea ukuaji wa uchumi unaoendana na maendeleo ya teknolojia.


&&&&

MRADI WA BILIONI 15.3 WA KUSAMBAZA UMEME VITONGOJI 175 WAPOKELEWA KWA SHANGWE MTWARA

January 28, 2026 Add Comment
-Zaidi ya Kaya 5,600 kunufaika

Wananchi wa vitongoji vya Msokole na Funguni Kijiji cha Mnazi Kata ya Nalingu Mkoani Mtwara wameishukuru Serikali kwa kuwapelekea mradi wa Umeme unaotekelezwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA) ambao wamesema unakwenda kubadili maisha yao.

NGORONGORO YAPANDA MITI AINA YA OLORIEN, MITI MAARUFU WAKATI WA TOHARA KWA VIJANA WA KIMASAI.

January 28, 2026 Add Comment

 


Na Mwandishi Wetu, Ngorongoro.

Tofauti na vijana wa mjini hasa wa Dar es Salaam ambao wengi wao hutahiriwa wakiwa wadogo hospitalini tena kwa ganzi, tohara kwa vijana wa kimasai hufanyika wakiwa mabarobaro na mashabaro na tena bila ganzi na hivyo kusikia maumivu makali ya kitendo hicho.

Katika kuadhimisha siku ya kuzaliwa kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro imeungana naye kwa kupanda miti aina ya Olorien katika kijiji cha Oloirobi Wilayani Ngorongoro.

Miti hiyo hukatwa na hutumika mara baada ya vijana wa kimasai kufanyiwa Jando/kutahiriwa, kijana akishatahiriwa miti huo huwekwa mlangoni wa nyumba yenye kijana aliyetahiriwa kisha akina mama huzunguka ulipowekwa mti husika huku wakiimba kwa furaha na vigelegele kuashiria kwamba zoezi la tohara limefanyika na kukamilika.

Kwa mujibu wa imani ya kabila hilo nyimbo za shangwe na faraja zinazoimbwa na kina mama kwa kuzunguka mti huo ukiwa kwenye nyumba humfanya kijana kuwa na faraja kutofikiria maumivu aliyoyapata wakati wa tohara.

Tohara katika kabila la wamasai inahusisha mafundisho yote ya msingi kwa mwanaume ikiwa ni pamoja na kuwafanya wawe majasiri na shujaa wanaoweza kukabiliana na changamoto zozote za kimaisha tofauti na vijana wanaozaliwa mjini maarufu kama vijana wa elfu mbili (2000) ambao wengi wao maumivu ya jando hawayafahamu kutokana na kutahiriwa wakiwa wadogo tena wengi wao wakifanyiwa tohara hospitali.

Akizungumza mara baada ya zoezi hilo la upandaji wa miti Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro anayesimamia Idara ya Maendeleo ya Jamii Gloria Bideberi amesema kuwa mamlaka itaendelea kuithamini miti hiyo na kushirikiana na jamii ya kabila hilo kuhakikisha miti hiyo haitoweki

Kiongozi wa kimila wa kata ya Ngorongoro bwana Sembeta Ngoidiko amempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa kuamua kusherehekea siku yake ya kuzaliwa kwa kupanda miti na kusema na wananchi wa kijiji cha Oloirobi kwa kushirikiana na Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro wameamua kupanda miti hiyo pamoja na miti mingine inayotumika kama miti dawa ili kuendelea kudumisha uhifadhi,mila na desturi.


















e-GA YASEMA MFUMO WA BARUA PEPE ZA SERIKALI UNAENDELEA KUIMARISHWA KITAIFA

January 28, 2026 Add Comment


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete, ametoa onyo kwa Watumishi wa Umma dhidi ya matumizi ya baruapepe binafsi katika mawasiliano ya shughuli za Serikali.

Amesema kuwa, watumishi wote wa Umma wanapaswa kutumia baruapepe rasmi za Serikali ili kulinda usalama wa taarifa Serikalini, kuongeza uwajibikaji, kuimarisha mifumo rasmi ya mawasiliano ya Serikali sambamba na kuzuia kuvuja kwa taarifa za Serikali.

Akizungumza mapema hivi karibuni wakati wa uzinduzi wa Bodi ya Pili ya Mamlaka ya Serikali Mtandao (e-GA), Mhe. Kikwete amesema, matumizi ya barua pepe zisizo za Serikali yamekuwa chanzo cha hatari ya uvujaji na upotevu wa taarifa nyeti za Serikali.

Alibainisha kuwa, Serikali imewekeza katika miundombinu ya TEHAMA inayokidhi viwango vya usalama na inapaswa kutumiwa ipasavyo katika mawasiliano ya shughuli zote za Serikali, ili kudhibiti na kulinda usalama wa taarifa muhimu za nchi.

“Kuanzia sasa, serikali itakuwa na jicho la karibu sana kuangalia namna watumishi wa Umma wanavyopeana taarifa za Serikali kupitia baruapepe rasmi za Serikali na si vinginevyo, nitoe wito kwa viongozi na watumishi wote wa umma kutumia anuani za baruapepe rasmi kwa ajili ya mawasiliano ya shughuli zote za Serikali, alisisitiza Waziri Kikwete.

Alibainisha kuwa, barua pepe za Serikali zinatoa mazingira salama ya kuhifadhi kumbukumbu, kudhibiti hatari ya kuvuja kwa taarifa za serikali, usalama na ulinzi wa taarifa hizo kwa mujibu wa sheria na miongozo mbalimbali inayohusu usalama na utunzaji wa taarifa za Serikali, sambamba na uwajibikaji kwa watumishi wa umma katika kuzingatia misingi ya utunzaji wa taarifa za Serikali.

“Matumizi ya baruapepe zisizo rasmi yamesababisha baadhi ya nyaraka za Serikali kupotea na wakati mwingine kuhatarisha usalama na usiri wa taarifa hizo ndani ya serikali, tukiwa kama watumishi wa umma sote tunawajibika kulinda usalama wa taarifa za Serikali kwa kutumia baruapepe rasmi za Serikali”, alisema Mhe.Kikwete.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Serikali Mtandao (e-GA) Eng. Benedict Ndomba, alisema kuwa e-GA itaendelea kutoa ushirikiano kwa taasisi za umma ili kuzijengea uwezo katika matumizi ya mfumo wa Buruapepe Serikalini (GMS).

Alisema kuwa, takriban zaidi ya miaka 10 sasa, tangu kuanza kutumika kwa mfumo wa GMS na kuleta matokeo chanya ikiwemo kurahisisha mawasiliano ndani na nje ya taasisi pamoja na kuwezesha utekelezaji wa maamuzi kwa wakati.

“e-GA tunatoa msaada wa kiufundi kwa saa 24 kwa watumiaji wa mifumo mbalimbali ukiwemo GMS na tutaendelea kufanya hivyo, ili kuhakikisha mawasiliano ya Serikali yanakuwa imara muda wote kupitia mfumo huu wa GMS”, alisema Ndomba.

MEYA TANGA ATOA WITO KWA VIJANA WANAOPATA FURSA YA AJIRA NJE YA NCHI

January 28, 2026 Add Comment





Na Oscar Assenga,TANGA

MSTAHIKI Meya wa Jiji la Tanga Seleboss Mustapha amewataka vijana wataopata fursa ya ajira nje ya nchi katika Falme za Kiarabu kufanya kazi kwa uadilifu na kuitangaza vizuri sifa na fursa ya nchi jambo ambalo litafungua milango kwa wengine kuendelea kuaminiwa.

Seleboss aliyasema hayo  wakati akizungumza na vijana zaidi ya 200 waliojitokeza kufanyiwa usaili kwa ajli ya kwenda nchi za falme za Kiarabu kwa shughuli za udereva wa pikipiki maarufu kama Bodaboda.

Alisema kufanya kazi kwa uaminifu sambamba na kuyaishi maadili ya kitanzania katika nchi za kigeni itasaidia kuleta taswra njema ya kutangaza nchi kwa mazuri badala ya kuwa kinyume chake.

Aidha alisema watakaofanikiwa kupita kwenye mchujo wakawe mabalozi wazuri kwa kufanya kazi lea ajil ya maendeleo yao ikiwemo kutokusahau kuwekeza nyumbani ikiwemo wawwe waaminifu

Meya huyo aliwataka kuhakikisha wanazingatia sheria na tararubu na miongozo ya nchi wanazokwenda ili waweze kufanya shughuli vizuri lakini kwa kujenga imani kwa wengine kuweza kuvutika na vijana kutoka nchni.

Awali akizungumza Ofisa Kazi Mkuu kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi,Ajira na Mahusiano Peter Ugata alisema kwamba Serikali imekuwa ikiendelea kuratibu fursa za ajira nje ya nchi kwa kuhakiisha wanawasimamia vijana wao kupata ajira zao.

Alisema kuwa hiyo ni dhamira ya Rais Dkt Samia Suluhu kukabiliana na ukosefu wa ajira kwa vijana na hivyo ni muhimu vijana kuchangamkia fursa hizo zinapojitokeza.

Alisema miongoni mwa majukumu yao ni kuhakikisha wanapata vijana wenye sifa na vigezo ambao wataweza kufanya kazi kwa mujibu wa taratibu za nchi husika.

Naye kwa upande wake mmoja wa vijana wanaoshiriki kwenye usaili huo ,Juma Haki waliishukuru Serikali kwa fursa hiyo kuweza kufika hadi ngazi ya mikoa na hivyo kuweza kushiriki nao.

Hata hivyo alisema kwamba wanaishukuru Serikali kwa fursa hiyo ambayo itasaidia kumaliza changamoto za ajira lakini itawapa mwamko wa kujipanga kwa ajili ya kuwa na sifa za kufanya kazi nje ya nchi .


Mwisho.