HABARI

SIASA

ELIMU

Recent Posts

SERIKALI YAENDELEA KUTAMBUA MCHANGO WA BARRICK-TWIGA KWA UENDESHAJI WA SHUGHULI ZAKE KWA WELEDI

March 24, 2026 Add Comment

 



Waziri wa Fedha na Mipango, Balozi Khamis Mussa Omar (Mb) akiwa kwenye picha ya pamoja na wenyeviti wa Bodi na Wakurugenzi wa Mashirika na makampuni ambayo serikali ina hisa chache kwenye mkutano wa mwaka 2026 uliyofanyika jijini Arusha , waliosimama wa kwanza kulia , ni Meneja Mkazi wa Barrick nchini , Dkt. Melkiory Ngido
Waziri wa Fedha na Mipango, Balozi Khamis Mussa Omar (Mb) akiwa kwenye picha ya pamoja na wenyeviti wa Bodi na Wakurugenzi wa Mashirika na makampuni ambayo serikali ina hisa chache kwenye mkutano wa mwaka 2026 uliyofanyika jijini Arusha , waliosimama wa kwanza kulia , ni Meneja Mkazi wa Barrick nchini , Dkt. Melkiory Ngido.
**
Serikali imeendelea kutambua mafanikio yanayoendelea kupatikana kutokana na ubia baina ya kampuni ya Barrick na Serikali ya Tanzania kupitia kampuni ya Twiga ambapo katika mkutano wa Wakurugenzi wenye Hisa chache za Serikali (MIF 2026) uliomalizika jijini Arusha imetunukiwa tuzo ya mshindi katika kipengele cha uwakilishi bora wa Bodi za Wakurugenzi (MIF) Directors Forum 2026 Outstanding Board Representation) na ofisi ya Msajili wa Hazina.
MRAJIS AAGIZA MATUMIZI YA MIZANI ZA KIDIGITALI KULINDA WAKULIMA.

MRAJIS AAGIZA MATUMIZI YA MIZANI ZA KIDIGITALI KULINDA WAKULIMA.

March 24, 2026 Add Comment

Mrajis wa Vyama vya Ushirika, Dkt. Benson Ndiege amevitaka Vyama vya Ushirika vya Mazao nchini kutumia mizani za kidigitali katika kupima mazao ya wakulima ili kuondoa udanganyifu na kumlinda mkulima. Mrajis ametoa maelekezo hayo kupitia barua ya tarehe 13 Machi, 2026 aliyowaandikia Wenyeviti na Wajumbe wa Bodi wa Vyama vya Ushirika vya mazao Tanzania Bara kuhakikisha kuwa vinatumia mizani za kidigitali kwa lengo la kuondoa udanganyifu kwenye upimaji wa mazao ya wakulima na kurahisisha upatikanaji wa takwimu sahihi za makusanyo/mauzo ya mazao. Vyama vya Ushirika wa Mazao vitakavyobainika kuwa na Mizani ya kidijitali na havitumii Mizani hizo au kuzitumia kwa matumizi tofauti na malengo yaliyokusudiwa, vitachukuliwa hatua kwa mujibu wa Sheria; na wakulima wanatakiwa kuhakikisha mazao yao yanapimwa kwa kutumia Mizani zilizounganishwa na Mfumo wa Usimamizi wa Vyama vya Ushirika (MUVU) ili kuwawezesha kupata malipo stahiki ya mazao yao. Aidha, Dkt. Ndiege amevitaka Vyama vyote vya Ushirika wa Mazao ambavyo bado havijatekeleza maelekezo ya ununuzi wa Mizani za kidijitali kuhakikisha kuwa vinanunua Mizani hizo kwa kufuata utaratibu wa manunuzi na Mwongozo wa Ofisi ya Mrajis kuhusu Ununuzi wa Mizani hadi kufikia Juni 31, 2026. Tume ya Maendeleo ya Ushirika inaendelea na jitihada za kuimarisha Usimamizi wa Vyama vya Ushirika nchini ambapo kwa sasa moja ya kipaumbele kinachotiliwa mkazo ni kuratibu na kuhimiza Vyama vya Ushirika vya Mazao, kuweka utaratibu wa ununuzi wa Mizani za Kidijitali sambamba na matumizi sahihi ya mizani hizo.

MAFUTA YAIMARISHA UPATIKANAJI WA MAFUTA YA PETROLI NCHINI MALAWI

March 24, 2026 Add Comment


Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam


Serikali kupitia Bandari ya Dar es Salaam imeendelea kuwa nguzo muhimu ya upatikanaji wa mafuta kwa nchi jirani ya Malawi, hatua inayochochea shughuli za kiuchumi na kuboresha maisha ya wananchi wa nchi hizo mbili.


Akizungumza wakati wa ziara ya kukagua miundombinu ya mafuta katika Kituo cha Kurasini Oil Jet (KOJ-1), kilichopo katika Bandari ya Dar es Salaam, Waziri wa Nishati na Madini wa Malawi, Mhe. Dkt. Jean Mathanga, aliishukuru Serikali ya Tanzania kwa mchango wake mkubwa katika kuwezesha mtiririko wa mafuta kwenda nchini Malawi.

Alisema kuwa kutokana na Malawi kutokuwa na bandari, nchi hiyo inategemea kwa kiasi kikubwa miundombinu ya nchi jirani, hususan Tanzania, katika kuhakikisha upatikanaji wa mafuta unaendelea kuwa wa uhakika.


Alibainisha kuwa ziara hiyo imelenga kujionea kwa vitendo namna mafuta yanavyopokelewa na kusimamiwa bandarini ili kuboresha mipango ya ununuzi na usambazaji wa mafuta nchini Malawi. 

Kwa upande wake, Mwakilishi wa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Uagizaji Mafuta kwa Pamoja (PBPA), ambaye ni Mkurugenzi wa Uendeshaji wa Petroli PBPA, Mhandisi Bruno Tarimo, alifafanua kuwa sehemu kubwa ya mafuta yanayoingia Malawi hupitia Tanzania kupitia Mfumo wa Uagizaji Mafuta kwa Pamoja (BPS), huku wakati mwingine nchi hiyo ikiagiza moja kwa moja kutoka kwa wazabuni wake.



KUELEKEA UZINDUZI WA WAZOHURU APARTMENTS MATHIAS CANAL ACHANGIA VIFAA VYA MICHEZO VYA MIL 4 MANISPAA YA SINGIDA

March 24, 2026 Add Comment
Kuelekea uzinduzi wa WazoHuru Air BnB Apartments Mtaa wa Unyankae-Miembeni Manispaa na Mkoa wa Singida, Afisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Wazohuru Media Group Limited amechangia vifaa vya michezo kwenye shule za msingi katika Manispaa ya Singida vyenye gharama ya shilingi Milioni 4.2

MHANDISI MRAMBA ATEMBELEA OFISI ZA UBALOZI WA TANZANIA NCHINI INDIA

March 23, 2026 Add Comment


Katibu Mkuu Wizara ya Nishati anayeshughulikia masuala ya Umeme na Nishati Jadidifu, Mhandisi Felchesmi Mramba, ametembelea Ofisi za Ubalozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Jijini New Delhi, India, ambapo amekutana na Balozi wa Tanzania nchini India, Mhe. Anisa Mbega.


Akiwa nchini India, Mhandisi Mramba alihudhuria Mkutano wa Bharat Electricity Summit 2026, uliohitimishwa tarehe 22 Machi 2026, ambapo walijadili fursa mbalimbali za uwekezaji zilizopo kati ya nchi hizo mbili, hususani katika Sekta ya Nishati.



DKT. YONAZI AKUTANA NA KUFANYA MAZUNGUMZO NA MKURUGENZI MTENDAJI MPYA WA TACAIDS DKT. MRISHO

March 23, 2026 Add Comment



Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu Dkt. Jim Yonazi amekutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi Mtendaji mpya wa Tume ya Kudhibiti UKIMWI Tanzania (TACAIDS) Dkt. Adam Joseph Mrisho ambaye amefika kujitambulisha baada ya kuteuliwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.


Kikao hicho kimefanyika tarehe 23 Machi, 2026 katika Ofisi ya Waziri Mkuu iliyopo mtaa wa Reli jijini Dodoma na kudhuriwa na Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu) Dkt. James Kilabuko pamoja na Mratibu wa Masuala ya UKIMWI Bi. Adela Mpina.


Dkt.Yonazi ameahidi kumpa ushirikiano katika utekelezaji wa majukumu yake ya kila siku.
(PICHA ZOTE NA OFISI YA WAZIRI MKUU)




WAZIRI NDEJEMBI AITAKA EWURA KUKAGUA MAGHALA YA MAFUTA KUHAKIKISHA HAKUNA MAFUTA YANAYOFICHWA

March 23, 2026 Add Comment

 



📌*Asema nchi ina usalama mkubwa wa mafuta hivyo wananchi waendelee kupata huduma muda wote*


📌*Timu maalum kuundwa kufuatilia uingizaji wa mafuta nchini*


Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi ameitaka Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) kuhakikisha kuwa, hakuna mfanyabiashara anayeficha mafuta kwa kisingizio cha kusubiri bei za mafuta zipande kutokana na mgogoro unaoendelea katika eneo la Mashariki ya Kati ambao umepelekea baadhi ya nchi kukumbana na changamoto za upatikanaji wa mafuta.

Akizungumza jijini Dodoma katika kikao na Taasisi za Wizara zinazosimamia Sekta ya Mafuta, Mhe. Ndejembi ameeleza kuwa nchi ina usalama mkubwa wa mafuta na kwamba Serikali imejipanga vizuri kuhakikisha  wananchi katika maeneo yote wanapata huduma bila vikwazo hivyo EWURA anapaswa kuhakikisha hakuna mafuta yanayofichwa katika maghala ya kuhifadhi Mafuta.

Aidha, ili kuhakikisha mafuta yote yaliyoagizwa nje ya nchi yanafika nchini kwa mujibu wa mkataba, Mhe. Ndejembi ameelekeza kuundwa kwa timu maalum kufuatilia mwenendo wa uingizaji wa Mafuta nchini ambayo itahusisha Wataalam kutoka Wakala wa Uagizaji wa Mafuta kwa Pamoja (PBPA),  EWURA, Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) pamoja na Ulinzi na Usalama.

 " Timu hii itakuwa na jukumu la kufuatilia hatua kwa hatua  na kuhakikisha kuwa mafuta yote yaliyoagizwa ambayo yako njiani  kuja nchini yanafika kwa wakati bila kikwazo wala changamoto yoyote. Hali ya biashara ya mafuta huko duniani si ya kuridhisha, baadhi ya nchi bei ya mafuta imepanda maradufu na wafanyabiashara wengine wanaweza kuingia tamaa na kupeleka mafuta huko, katika hili sitarajii kuona mikataba tuliyoingia na waagizaji wa mafuta ikikiukwa." Amesisitiza Mhe. Ndejembi


Kwa upande wake, Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati anayeshughulikia Mafuta na Gesi Asilia, Dkt. James Mataragio, amewahakikishia Watanzania kuwa nchi ina akiba ya kutosha ya mafuta hadi mwezi Julai 2026. 


Amesema Serikali ilichukua hatua za mapema kwa kushirikiana na taasisi zake, ili kuhakikisha kunakuwa na uhakika wa upatikanaji wa mafuta na kwa gharama himilivu. 




Ameongeza kuwa Wizara itaendelea kusimamia Taasisi zake ili kuhakikisha mafuta yaliyopo njiani yanafika kwa wakati, pamoja na kuwadhibiti wauzaji ili wasitumie changamoto iliyopo kama fursa ya kupandisha bei.


Awali, Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Uagizaji wa Mafuta kwa Pamoja (PBPA) Bw. Erasto Simon alieleza kuwa hali ya upatikanaji wa mafuta nchini iko salama  ambapo ameeleza kuwa ukijumuisha mafuta yaliyopo nchini na yaliyopo njiani kuna petroli lita milioni 474 inayotosheleza siku 78, dizeli  lita milioni 392 inayotosheleza siku 50 pamoja na lita milioni 55 za mafuta ya ndege zinazotosheleza siku 91.


Naye, Mkurugenzi Mtendaji Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) Bw.Mussa Makame ameeleza kuwa kuna mafuta ya kutosha ndani ya nchi na ambayo yako safarini kwani Serikali ilishasaini mikataba na wazabuni mapema kwa ajili ya uingizaji wa mafuta.

Kwa upande wake,  Mkurugenzi Mkuu wa EWURA, Dkt. James Andilile ameeleza kuwa kwa sasa soko liko sawa hakuna mfumuko wa bei hivyo  EWURA itahakikisha watu hawafichi mafuta kusubiri mfumuko wa bei katika soko la dunia.


Amesema EWURA imeendela kushirikiana na wadau wa mafuta wakiwemo waagizaji na wauzaji ili kuhakikisha kama kuna changamoto zozote  zinatatuliwa kwa haraka ili wananchi wapate huduma kwa uhakika.

UJENZI WA BARABARA YA KAHAMA - BULYANHULU JCT - KAKOLA KWA UWEZESHAJI WA MIGODI YA BARRICK NI UWEKEZAJI ENDELEVU UTAKAOACHA ALAMA YA KUDUMU NCHINI

March 23, 2026 Add Comment

Mchakato wa kumwaga lami katika barabara ya Kahama-Kakola inayojengwa kwa uwezeshaji wa kampuni ya Barrick nchini ukiendelea
Mchakato wa kumwaga lami na kuisambaza ukiendelea
Msimamizi wa Ujenzi wa barabara ya Kahama-Kakola kutoka Wakala wa Barabara nchini (TANROADS) Mhandisi Marco Bee, akiongea kuhusu maendeleo ya ujenzi huo unaotekelezwa kwa ufadhili wa kampuni ya Barrick nchini.
Msimamizi Msaidizi kutoka kampuni ya Barrick, Mhandisi Ibahim Paul akielezea maendeleo ya ujenzi wa barabara hiyo.
**
#Wafikia hatua ya barabara kuwekwa lami

Mradi wa ujenzi wa barabara ya Kahama-Bulyanhulu JCT- Kakola kwa kiwango cha lami yenye kilomita 73 kwa uwezeshaji wa migodi ya Barrick nchini ya Bulyanhulu na North Mara yenye ubia na Serikali kupitia kampuni ya Twiga Minerals kwa gharama ya shilingi bilioni 101.2 umefikia hatua ya kuwekwa lami na kudhihirisha dhamira ya kampuni ya uwekezaji unaoenda sambamba na kufanikisha miradi mikubwa endelevu inayobadilisha maisha ya wananchi kuwa bora na itakayoacha alama ya kudumu hadi kwa vizazi vijavyo.

THPS YAKABIDHI KLINIKI YA MAT SHINYANGA KUIMARISHA MAPAMBANO DHIDI YA MATUMIZI YA DAWA ZA KULEVYA

March 23, 2026 Add Comment

  


MAHITAJi YA UMEME YAONGEZEKA KWA WASTANI WA ASILIMIA 10-15 KILA MWAKA

March 22, 2026 Add Comment


ONGEZEKO la idadi ya watu pamoja na kuimarika kwa shughuli za viwanda na biashara limeendelea kuchochea kasi ya mahitaji ya umeme nchini kwa wastani wa asilimia 10 hadi 15 kila mwaka.


Kutokana na mwenendo huo, Serikali imejipanga kuongeza jitihada za kuhakikisha upatikanaji wa umeme wa uhakika kwa wananchi wote, sambamba na kuimarisha miundombinu ya nishati.

Akizungumza katika mkutano wa Powering Africa Summit uliofanyika jijini Washington, DC, Machi 20, 2025, Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba, amesema kuwa ongezeko hilo la mahitaji linachochea uwekezaji mkubwa katika sekta ya nishati, ambayo ni mhimili muhimu wa ukuaji wa uchumi.

Amefafanua kuwa hadi kufikia Machi 2026, uwezo wa uzalishaji wa umeme nchini umefikia megawati 4,383, wakati kiwango cha juu cha mahitaji kikiwa takribani megawati 2,100.


Hata hivyo, ameonya kuwa kasi ya ongezeko la mahitaji inahitaji uwekezaji zaidi katika uzalishaji, usafirishaji na usambazaji wa umeme ili kuendana na mahitaji ya sasa na ya baadaye.

Kuhusu upatikanaji wa huduma hiyo, amesema Serikali imefanikiwa kufikisha miundombinu ya umeme katika vijiji vyote vya Tanzania Bara, ingawa kiwango cha uunganishaji wa umeme katika kaya bado ni cha chini, hali inayoonesha changamoto ya kuwafikia wananchi wote.


Mhe. Salome amesisitiza kuwa Serikali imelenga kufikia asilimia 100 ya upatikanaji wa umeme ifikapo mwaka 2030, huku ikikusudia kuongeza kiwango cha uunganishaji wa kaya hadi asilimia 75 ili kuchochea maendeleo ya kijamii na kiuchumi.

Aidha, ameeleza kuwa Tanzania ina vyanzo mbalimbali vya nishati ikiwemo gesi asilia, maji, jua, upepo na jotoardhi, ambavyo vina uwezo mkubwa wa kukidhi mahitaji yanayoongezeka.


Ameongeza kuwa Serikali itaendelea kuhimiza matumizi ya nishati jadidifu ili kuhakikisha upatikanaji endelevu wa umeme, huku ikiendeleza juhudi za kuhamasisha uwekezaji katika sekta hiyo.


Hatua hizo zinatarajiwa kusaidia kukidhi mahitaji ya nishati yanayoongezeka na kuiwezesha Tanzania kuwa kitovu cha nishati katika ukanda wa Afrika.

MAENEO YA UWEKEZAJI SEKTA YA NISHATI YATAJWA NCHINI INDIA

March 22, 2026 Add Comment


📌*Mhandisi Mramba asema Tanzania ina fursa nyingi na mazingira ya uwekezaji ni rafiki*


New Delhi, India


Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati anayeshughulikia Umeme na Nishati Jadidifu,  Mhandisi Felchesmi Mramba, ametangaza fursa mbalimbali za uwekezaji zilizopo katika sekta ya nishati nchini, akizialika kampuni na wawekezaji wa kimataifa kuchangamkia nafasi hizo ili kuchochea ukuaji wa sekta hiyo.


Akizungumza katika kikao maalum cha India–Africa Partnership kilichofanyika wakati wa mkutano wa Bharat Electricity 2026 unaoendelea nchini India, Mhandisi Mramba amesema Tanzania ina mazingira rafiki ya uwekezaji na inaendelea kujipambanua kama moja ya maeneo yenye fursa kubwa katika sekta ya nishati barani Afrika.


Ameeleza kuwa fursa hizo zinapatikana katika maeneo mbalimbali ikiwemo miradi ya kuzalisha umeme, kusafirisha na kusambaza umeme, pamoja na uwekezaji katika nishati jadidifu kama jua, upepo, jotoardhi na umeme wa maji. Aidha, ametaja pia uwekezaji katika nishati safi ya kupikia kuwa ni eneo muhimu linalopewa kipaumbele na Serikali. 


Mhandisi Mramba ameeleza kuwa Tanzania inaendelea kukuza sekta ya umeme ili kukidhi ongezeko la mahitaji linalochochewa na ukuaji wa viwanda na ongezeko la matumizi ya umeme mijini na vijijini, akibainisha kuwa uwezo wa uzalishaji umefikia takribani megawati 4,500 na unatarajiwa kufikia megawati 8,000 ifikapo mwaka 2030. 


Ameongeza kuwa Serikali kupitia Mpango wa Taifa wa Nishati ( National Energy Compact) inalenga kuongeza upatikanaji wa umeme, kuimarisha matumizi ya nishati jadidifu na kufikia matumizi ya nishati safi ya kupikia kwa asilimia 75 ifikapo mwaka 2030 hatua inayofungua zaidi fursa kwa wawekezaji kushiriki katika miradi yenye tija. 


Amesisitiza kuwa Tanzania iko tayari kushirikiana na wadau wa kimataifa katika kuendeleza miradi ya kimkakati kupitia ubia kati ya sekta ya umma na binafsi (PPP), akiwahakikishia wawekezaji uwepo wa mazingira wezeshi, sera thabiti na dhamira ya dhati ya Serikali katika kusimamia na kutekeleza miradi ya nishati.

EID AL-FITR AND THE NGORONGO CRATER REFLECTED IN THE HOLY QUR'AN ( SURAH 99 -AL-ZALZALAH

March 22, 2026 Add Comment




As Muslims and Tanzanians at large celebrate Eid al-Fitr, marking the end of the holy month of Ramadan, it is a fitting moment to reflect on the deeper spiritual truths that connect faith, nature, and existence. For those open to belief, there will come a final day when the earth is shaken and gathered together, and mountains are reduced to dust.


This philosophy, described in sacred teachings, mirrors what unfolded at the Ngorongoro Crater approximately 2.5 million years ago.


In the Holy Qur’an, Surah 99—Al-Zalzalah (The Earthquake), which consists of eight verses, vividly describes the events of the Day of Judgement. The earth will shake violently and release its burdens, and humanity will witness every deed: good or bad, even those as small as a particle.


These verses find a powerful parallel in the history and present state of the Ngorongoro Crater.


Scientists explain that over 2.5 million years ago, a massive volcanic mountain: believed to have been larger than Mount Kilimanjaro, erupted within what is now the Ngorongoro area. A series of intense eruptions destabilized the structure, and the volcanic cone could no longer support its own weight. It collapsed inward, forming the vast caldera we now know as the Ngorongoro Crater, one of the largest intact volcanic calderas in the world.


Today, the crater spans roughly 20 kilometers in diameter and reaches a depth of about 610 meters, forming a natural basin of extraordinary scale and beauty.


This geological event took place during the Pleistocene epoch, a time marked by significant volcanic activity across the Eastern Rift Valley, as the Great Rift itself continued to expand.


Over time, nature shaped this landscape into a self-contained ecosystem of remarkable diversity. The crater floor hosts a mosaic of habitats: freshwater and soda lakes, forests, open grasslands, rivers, springs, rocky outcrops, and rolling hills. These environments support an abundance of wildlife, with populations exceeding 25,000 animals throughout the year.


When you consider the formation of the Ngorongoro Crater alongside insights drawn from sacred texts and blend them with the region’s rich culture, traditions, and natural heritage, a profound narrative emerges. Ngorongoro reveals itself as a living testament often described as a “Garden of Eden” where humanity, nature, and the Creator’s design converge, and where every layer of its story continues to unfold.

RC BATILDA AWATAKA WAZAZI KUWA MAKINI NA WATOTO

March 22, 2026 Add Comment




Na Oscar Assenga, TANGA



MKUU wa Mkoa wa Tanga Balozi,Dkt Batilda Burian ametoa salamu za sikuu ya Eid El Fitri kwa wakazi wa mkoa huo huku akiwataka wazazi na walezi kuwa makini na watoto wanapotoka kwenda kutembea.



Dkt Batilda aliyasema hayo jana mara baada ya kumalizika kwa Swala ya Eid El Fitri iliyofanyika kwenye msikiti wa Ijumaa Jijini Tanga ambapo alisema ni muhimu wakati wa sikuuu wahakikishe watoto wanapokwenda kutembea wanakuwa na uangalizi.



Alisema kwamba kufanya hivyo kutawasadia kwenda kutembelea salama na kuweza kusheherekea sikuuu salama bila kadhia ambayo inaweza kuleta madhara mbalimbali ikiwemo majozi na msiba.



“Wazazi na walezi niwaombe Shehere ya Eid watoto wanakwenda kutembelea tuwe makini wawe na mtu mzima hata njiani wawe makini kuna vyombo vya usafiri bodabodoa na magari tuhakikishe tunakula sikuuu salama bila kadhia ambayo italeta msiba na majonzi”Alisema



Aidha aliwataka wakazi wa mkoa huo kuendelea kudumisha amani na utulivu kuendeleza mshikamano kwa upendo pamoja na kuendelea kumuombea Rais wetu Dkt Samia Suluhu .



Mkuu huyo wa Mkoa alisisitiza wana Tanga kuendelea kuwaombea waliotangulia mbele za haki na waliojaliwa kuendelea kumshukuru Mwenyezi Mungu ikiwemo kuwaombea viongozi wa dini.



“Nitoe mkono wa Eid Fitri kwa wana Tanga na watanzania tuendelee kama tulivelekezwa tuwatembelee wagonjwa ndugu na jamaa na tuzuru makaburi na tufanye amali njema na tuendelee kupendana na kutenda mema”Alisema



Akizungumza Mbunge wa Jimbo la Tanga Kassim Amary Makubel aliwatakia heri ya sikuu ya Eid El Fitri wakazi wa Jiji hilo huku akieleza kwamba hivi sasa Tanga imefunguka kimaendeleo na itaendelea kufunguka zaidi kutokana na uwekezaji mkubwa uliofanywa na Serikali.



Mbunge huyo aliwashauri watu wa Tanga wasiwe wepesi wa kuunza nyumba zao hata kama ni za urithi na kama ikitokea anataka kuja Mwekezaji kuwekeza ingieni ubia kwa miaka fulani kwani watakapouza wanaweza kuwa nje ya mji.



Awali akizungumza Diwani wa Kata ya Ngamiani Kaskazini, Fahadi Rished amesema umoja ulioonyeshwa wakati wa swala ya Eid uendelee kushikamana na waendelee kuwasaidia ndugu na jamaa wasiojiweze.



Alisema kwamba kata yao ipo salama kwa wananchi kusheherekea sikuu ya Eid hivyo wananchi washeherekee kwa salama .


Mwisho.








TANESCO YAGUSA MIOYO YA WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUMU

March 21, 2026 Add Comment




📌Ni sehemu ya uwajibikaji wake kwa jamii 


📌Yatoa misaada mbalimbali kwa vituo vitatu Dar es Salaam.


Katika kuendeleza dhamira ya uwajibikaji kwa jamii, Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), tarehe 19 Machi 2026, lilifanya ziara ya kutembelea vituo vitatu vya watoto wenye mahitaji maalum jijini Dar es Salaam, na kutoa misaada mbalimbali kwa lengo la kuleta faraja na matumaini.


Akizungumza wakati wa ziara hiyo kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji ,Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano na Huduma kwa Wateja wa TANESCO, Bi. Irene Gowelle, alisema kuwa lengo la ziara hiyo ni kushirikiana na jamii kwa vitendo kwa kutoa misaada hususan kwa makundi ya watoto yenye uhitaji .

Alieleza kuwa msaada huo haujalenga tu kukidhi mahitaji ya msingi, bali pia kuwajengea watoto hao imani, matumaini na ujasiri wa kuendelea kuamini katika ndoto zao licha ya changamoto wanazokabiliana nazo.


“Leo TANESCO tumeshiriki na watoto hawa wenye mahitaji maalum kwa kutoa misaada mbalimbali, ikiwa ni sehemu ya kurejesha kwa jamii na kuendeleza uwajibikaji wetu wa kijamii,” alisema Bi. Irene.

Aidha, alisisitiza kuwa TANESCO itaendelea kushirikiana na jamii inayowazunguka kama sehemu ya mchango wake katika kujenga taifa lenye mshikamano, upendo na ustawi wa pamoja.


Kwa upande wake, Mwanzilishi wa Kituo cha Umra Orphanage Center, Bi. Rahma Juma, aliipongeza TANESCO kwa hatua hiyo, akisema msaada uliotolewa umefika kwa wakati muafaka na umeleta faraja kubwa kwa watoto pamoja na walezi wao.


Alibainisha kuwa ujio wa TANESCO umeongeza furaha na kuwapa watoto motisha mpya, huku akieleza kuwa vituo vya aina hiyo bado vinakabiliwa na changamoto mbalimbali zinazohitaji ushirikiano wa wadau.



“Kazi hii iliyofanywa na TANESCO ni mfano wa kuigwa. Msaada huu umekuja kwa wakati mwafaka na utatusaidia sana katika malezi ya watoto tulionao hapa kituoni,” alisema Bi. Rahma.


"Napenda kuwashukuru TANESCO  kwa ujio wao kwetu tunashukuru

kwa sadaka ambazo wameleta hasa katika msimu huu  wa  sikukuu zimekuja  kwa wakati sahihi wametuletea  vitu ambavyo  ni mahitaji yetu ya kila siku "  Amesema Bi. Nuru Mwegoha

Aidha, alitoa wito kwa taasisi, makampuni na watu binafsi kujitokeza kusaidia makundi yenye mahitaji maalum ili kuhakikisha wanapata huduma bora na kuishi maisha yenye matumaini.



Vituo vilivyofikiwa katika ziara hiyo ni Umra Orphanage Center kilichopo Magomeni, Kituo cha Watoto Yatima cha CHAKUWAMA kilichopo Sinza Mori, pamoja na New Hope for Girls Organization kilichopo Kimara.