HABARI MPYA
HABARI
SIASA
ELIMU
Recent Posts
RAIS WA ZAMANI WA LIBERIA AWASILI NCHINI KWA ZIARA YA KIKAZI
habariTUMUOMBEE RAIS, TULIOMBEE TAIFA-MASHILI
habariTANZANIA INAENDELEA KUIMARISHA MATUMIZI YA GESI ASILIA KUZALISHA UMEME-WAZIRI NDEJEMBI
O
Tanzania inaendelea kuimarisha na kuongeza matumizi ya gesi asilia katika uzalishaji wa nishati ya umeme nchini, hatua inayolenga kuiwezesha kufikia lengo la kuzalisha megawati 8,000 za umeme ifikapo mwaka 2030. Katika mpango huo, gesi asilia ni miongoni mwa vyanzo muhimu vitakavyotumika kuimarisha uzalishaji wa umeme wa uhakika na wa kutosha nchini.
Hayo yameelezwa na Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratus Ndejembi, katika Mikutano ya Kipupwe ya Benki ya Dunia na Shirika la Fedha la Kimataifa (World Bank – IMF Spring Meetings 2026) inayoendelea jijini Washington D.C, nchini Marekani.
Akizungumza katika mjadala kuhusu uzalishaji wa umeme kupitia gesi asilia uliofanyika chini ya mada isemayo “Gas in Sub-Saharan Africa’s Energy Sector”, Waziri Ndejembi amesema Tanzania ni miongoni mwa nchi zilizoweka kipaumbele kikubwa katika kutumia gesi asilia kama chanzo cha kuzalisha umeme.
Ameeleza kuwa hadi sasa, Tanzania inazalisha zaidi ya megawati 1,200 za umeme kupitia gesi asilia, ambazo tayari zimeunganishwa katika Gridi ya Taifa, hatua inayochangia kuimarika kwa upatikanaji wa umeme wa uhakika nchini.
Aidha, Waziri Ndejembi amebainisha kuwa serikali inaendelea kuimarisha uzalishaji wa gesi asilia, ambapo kazi ya uchimbaji wa visima vipya vitatu katika Kitalu cha Mnazi Bay mkoani Mtwara inaendelea. Hatua hiyo inatarajiwa kuongeza upatikanaji wa gesi na hivyo kuimarisha zaidi uzalishaji wa nishati nchini.
Pia, amesisitiza kuwa Tanzania inaendelea kuwakaribisha wawekezaji katika sekta ya nishati, hususani katika eneo la matumizi ya gesi asilia, ambalo lina fursa kubwa za kiuchumi na maendeleo ya taifa.
Katika mkutano huo, Benki ya Dunia imezitaka nchi za Afrika kuendelea kuongeza uzalishaji wa umeme kwa kutumia gesi asilia, huku Tanzania ikitajwa kuwa miongoni mwa nchi zilizopiga hatua muhimu katika matumizi ya nishati hiyo.
Katika Mkutano huo, Waziri Ndejembi ameambatana na Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati anayeshughulikia Mafuta na Gesi, Dkt. James Mataragio pamoja na wataalam kutoka taasisi zilizo chini ya Wizara ya Nishati.
BARRICK BULYANHULU YAKABIDHI TREKTA WILAYA NYANG’WALE KUFANIKISHA USAFI WA MAZINGIRA
habariJAB: Uandishi Usiozingatia Maadili Wahatarisha Umoja wa Kitaifa na Amani
habari

Na Mwandishi Wetu.
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula , amesema uandishi wa habari usiozingatia maadili unaweza kuhatarisha umoja wa kitaifa, amani na utulivu wa jamii.
Akizungumza na waandishi wa habari ambao ni wanachama wa JUMIKITA, TADIO na TBN, Aprili 17, 2026 jijini Dar es Salaam, Kipangula alisema waandishi wa habari wanapaswa kutambua uzito wa nafasi yao katika jamii, hasa katika kipindi hiki cha mabadiliko ya kijamii, kisiasa na kiuchumi, ambapo taarifa wanazozitoa zina athari kubwa kwa mwenendo wa jamii.
Alifafanua kuwa amani ni hali ya kutokuwepo kwa migogoro au vurugu, huku utulivu ukimaanisha usalama na uhakika wa maisha ya wananchi bila hofu, akibainisha kuwa hali hizi mbili haziwezi kudumu bila uwepo wa umoja wa kitaifa unaojengwa juu ya mshikamano wa wananchi bila kujali tofauti zao.


“Pale ambapo uandishi hauzingatii maadili, unaweza kuchochea migawanyiko, kupotosha ukweli na hatimaye kuvuruga mshikamano wa kitaifa. Hivyo, ni muhimu kwa waandishi wa habari kutekeleza majukumu yao kwa weledi, uadilifu na uwajibikaji,” alisema Kipangula.
Alibainisha kuwa waandishi wa habari wana wajibu wa msingi wa kukusanya, kuchakata na kusambaza taarifa sahihi, pamoja na kusaidia kuunda mitazamo ya wananchi kwa njia inayochangia maridhiano na maendeleo ya jamii.
Aidha, alisisitiza umuhimu wa kuzingatia Kanuni za Maadili ya Taaluma ya Uandishi wa Habari, akibainisha kuwa maadili hayo yanahimiza ukweli, usawa, uwazi na heshima kwa haki za binadamu, mambo ambayo ni msingi wa kulinda amani, kuimarisha utulivu na kukuza umoja wa kitaifa.







TANESCO YATOA ZAWADI YA MAJIKO KWA WALIMU WA SEKONDARI YA WASICHANA MKOA WA MANYARA
📌Ni katika Kuhamasisha matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia kwa umeme
📌Waishukuru TANESCO kwa zawadi hiyo, wapongeza kazi kubwa inayofanywa na Shirika
📌Waahidi kwenda kuwa mabalozi wazuri wa Nishati Safi ya Kupikia kwa Umeme
Na. Mwandishi Wetu, Manyara
Katika Kuhamasisha matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia kwa umeme hapa nchini Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) Bw. Lazaro Twange ametoa Majiko zaidi ya 30 kwa Walimu wa Shule ya Wasichana Mkoa wa Manyara ili kuwapa hamasa kwa kazi wanayoifanya.
Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Manyara Mhe. Queen Sendiga, Mkuu wa Wilaya ya Simanjiro Mhe. Fakii Lulandala amempongeza Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) Bw. Lazaro Twange kwa kutoa majiko hayo kwa walimu yanayolenga kuhamasisha matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia kwa umeme.
Amesema Bw. Twange anaunga mkono kwa vitendo ajenda ya Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuhamasisha matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia kutokana na jitihada kubwa zinazofanywa na TANESCO katika maeneo mbalimbali hapa nchini.
Amesema majiko hayo yanakwenda kutoa motisha kubwa kwa walimu wa shule hiyo na kuchochea ari ya ufundishaji kwa wanafunzi kwani sasa watatumia muda mchache wakati wa kupika hali ambayo itasaidia kuongeza ufaulu zaidi kwa wanafunzi hao.
Amesema licha ya kutoa Majiko hayo Bw. Lazaro Twange anamchango Mkubwa katika ujenzi wa Shule hiyo ya Wasichana kwani alihakikisha anaisimamia kikamilifu wakati akiwa Mkuu wa Wilaya ya Babati na kufanikisha ujenzi wake kutokana na kujitoa kwakwe usiku na mchana ili kuhakikisha ujenzi wa shule hiyo unakamilika.
“Bw. Lazaro Twange ndiye kinara wa ujenzi wa Shule hii na leo ametoa majiko ya kisasa yanayotumia umeme kidogo sana kwa ajili ya kuwagawia walimu, na hii inakwenda kuwa motisha kubwa kwa walimu wa shule hii hasa katika matumizi ya Nishati Safi ya umeme “
Kwa upande wake, Meneja wa TANESCO Mkoa wa Manyara Mhandisi Regina Mvungi amesema kwa Niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) Bw. Lazaro Twange wamekabidhi majiko 30 kwa walimu wa shule hiyo kama zawadi kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO.
Amesema majiko hayo yamekabidhiwa kwa walimu wote wa Shule hiyo na sasa wanakwenda kuwa mabalozi wa kuhamasisha matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia kwa umeme kwa vitendo kwa jamii inayowazunguka wakiwemo wanafunzi wao na wananchi kwa ujumla.
“Kupitia Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) Bw. Lazaro Twange tumetoa zawadi ya majiko 30 kwa walimu wa shule hii ili wakawe mabalozi wa kupikia kwa umeme kuanzia shuleni na jamii zinazowazunguka”
Naye Mkuu wa Shule hiyo ya Sekondari ya Wasichana Mkoa wa Manyara Mwl. Gisela Msoffe amelishukuru Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO wakati akiwa Mkuu wa Wilaya ya Babati hasa kwa usimamizi uliotukuka wa ujenzi wa shule hiyo pamoja na kuwezesha kufikishiwa kwa huduma ya umeme katika majengo yote ya shule hiyo.
Zaidi ameshukuru kwa zawadi ya majiko ya kisasa ya umeme waliyopatiwa walimu kwani yanakwenda kuwa msaada mkubwa hasa katika kuokoa muda wakati wa kupika ili kuwawezesha kuwa na muda wa kutosha kufundisha wanafunzi.
“Nimshukuru kwa dhati Bw. Lazaro Twange watumishi wote wa shule hii hasa Walimu tumepewa majiko ya kisasa ya umeme yatatusaidia kuokoa muda wakati wa kupika na tutapata Muda mwingi wa kufundisha Wanafunzi” ameongeza Mwl. Gisela
Serikali Yapanga Mageuzi Makubwa ya Mafunzo kwa Watumishi wa Umma
habariSERIKALI YATENGA SH.BILIONI 3.2 KUSAMBAZA UMEME VIJIJI 9 LUDEWA
Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba amesema Serikali imetenga kiasi cha Sh Bilioni 3.2 kupitia kwa Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa ajili ya kusambaza umeme katika vitongoji vilivyopo ndani ya vijiji Tisa vya Kitewele, Kimata, Ndoa, Chanjale, Nkanda, Lumbila, Nsele na Kilondo vilivyopo wilayani Ludewa mkoani Njombe ambapo mradi huo unatarajiwa kukamilika ifikapo Septemba 2026.
Mhe. Salome ameyasema hayo leo Aprili 17, 2026 Bungeni jijini Dodoma wakati akijibu swali la Mbunge wa Ludewa, Mhe. Joseph Kamonga aliyehoji ni lini Vijiji hivyo vitawashiwa umeme.
" Kwa kutambua changamoto ya Jiografia na ugumu wa kufikisha vifaa katika maeneo hayo, tumempatia kazi hiyo Mkandarasi M/s SUMA JKT Electric Co. Ltd ambaye tumemuelekeza kufanya kazi kama Jeshi na kuhakikisha kuwa azma ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kufungamanisha nishati na maendeleo ya kiuchumi inatimia," Amesema Mhe. Salome.
Aidha Mhe. Salome ameiagiza REA kumsimamia Mkandarasi huyo ili aweze kutimiza majukumu yake ili kuhakikisha wananchi wa Ludewa wananufaika na uwepo wa nishati imara na uhakika.

TCDC YAICHALAZA KILIMO KWA BAO 2 – 1
michezo
Timu ya Mpira wa miguu ya TCDC Sports Club imechukua alama tatu (3) baada cha kuifunga Timu ya Mpira wa miguu ya Wizara ya Kilimo goli mbili (2) kwa moja (1) katika mechi iliyochezwa leo Aprili 17, 2026 saa 2:30 3:45 katika viwanja vya Venite mkoani Njombe.
Timu hizo zimekutana katika mashindano ya Michezo ya Wafanyakazi (Meimosi) yanayoyafanyika kitaifa mkoani Njombe.
Hapo Kesho Aprili 18, 2026 Timu ya Mpira wa miguu TCDC Sport Club inatarajia kukutana na Timu ya Mpira wa miguu ya TAMISEMI saa10:15 jioni katika viwanja vya Kibena mkoani humo.
KAMATI YA UCHUMI ZANZIBAR YARIDHISHWA NA MAENDELEO YA MIRADI YA GESI MTWARA
habariSERIKALI YABORESHA HUDUMA ZA KIDIJITALI : TAASISI 571 ZAPITIWA NA MABORESHO YA TEHAMA
habari
Na Okuly Julius, OKULY BLOG, DODOMA
Serikali kupitia Mamlaka ya Serikali Mtandao (e-GA) imepanga kuimarisha usalama wa mifumo ya TEHAMA, kuongeza ufanisi wa huduma za kidijitali na kuunganisha taasisi za umma katika mfumo mmoja jumuishi ili kurahisisha utoaji wa huduma kwa wananchi.
Hayo yameelezwa Aprili 17, 2026 Bungeni jijini Dodoma na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Ridhiwani J. Kikwete, wakati akiwasilisha hotuba ya bajeti ya Ofisi hiyo kwa mwaka wa fedha 2026/27.
Waziri Kikwete amesema katika mwaka huo wa fedha e-GA itafanya tathmini na usimamizi wa usalama wa mifumo na miundombinu ya TEHAMA katika taasisi 571 za umma, hatua inayolenga kuhakikisha mifumo hiyo inafanya kazi kwa ufanisi na usalama wakati wote.
Aidha, Serikali itaimarisha mifumo jumuishi ya TEHAMA pamoja na mifumo ya kisekta na kitaasisi ili kuhakikisha huduma za kidijitali zinaboreshwa na kuondoa urudufu wa mifumo isiyohitajika serikalini.
Katika hatua nyingine, e-GA itafanya uchambuzi, usanifu na ujenzi wa mifumo mipya ya kisekta kwa taasisi mbalimbali ili kupunguza wingi wa mifumo na kuongeza ushirikiano wa kiutendaji kati ya taasisi za umma.
Serikali pia itaunganisha mifumo ya taasisi zote kupitia Mfumo wa Serikali wa kubadilishana taarifa (GovESB), hatua inayolenga kurahisisha mawasiliano na ushirikiano wa kidijitali serikalini.
Vilevile, Mamlaka hiyo itaimarisha utafiti na ubunifu katika matumizi ya teknolojia mpya za TEHAMA ili kuibua huduma mpya kwa wananchi, sambamba na kuhakikisha matumizi salama ya teknolojia zinazoendelea kujitokeza duniani.
Katika kuboresha huduma, Serikali itaongeza wigo wa mtandao wa mawasiliano wa serikali hadi kufikia wilaya zote nchini, pamoja na kuimarisha mifumo kama e-Office na huduma nyingine za kidijitali.
Aidha, e-GA itaendelea kusimamia miundombinu ya TEHAMA ikiwemo vituo vya kuhifadhi taarifa za serikali na mifumo ya kujikinga na majanga ya kidigitali.
Kwa mwaka wa fedha 2026/27, Serikali pia itatoa mafunzo kwa watumishi wa umma na watumiaji wa mifumo ya TEHAMA ili kuhakikisha matumizi salama na yenye ufanisi wa teknolojia katika utumishi wa umma.
Hatua hizo zinalenga kuimarisha utawala bora wa kidijitali, kupunguza gharama za uendeshaji na kuongeza ufanisi wa huduma za serikali kwa wananchi.
RC MTANDA AAGIZA UKAGUZI MKALI WA MAZINGIRA MWANZA
habariRAIS MSTAAFU DKT JAKAYA MRISHO KIKWETE AKUTANA NA MHESHIMIWA RAIS WILLIAM RUTO WA KENYA JIJINI NAIROBI
Rais Mstaafu Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, ambaye ni Mwakilishi wa Ngazi ya Juu wa Mwenyekiti wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika kwenye Eneo la Pembe ya Afrika na Bahari ya Shamu jana amekutana na kufanya mazungumzo na Rais William Ruto wa Kenya, Nairobi.
Pamoja na mambo mengine, viongozi hao walipata fursa ya kuzungumzia mchakato wa kutafuta amani nchini Sudani Kusini, hususan kwa kuzingatia nafasi ya Kenya katika mgogoro wa nchini huo.
Moja ya jitihada za kuleta amani nchini Sudani kusini zimefanywa na Serikali ya Kenya kupitia Mpango wa Amani wa Tumaini ambao umelenga kuvijumuisha katika mazungumzo ya amani vikundi vyote vya kijamii na vya kijeshi ambavyo havikutia saini katika Makubaliano ya Amani nchini Sudani Kusini R-ARCSS yaliyosainiwa Mwaka 2018.
Ziara hii ya Rais Mstaafu Dkt. Kikwete ni sehemu ya kutekeleza kujumu lake jipya la kuwa mpatanishi wa amani nchini Sudani Kusini, ambapo tangu kuteuliwa kwake ameweza kukutana na Viongozi mbalimbali wenye ufuasi katika hali ya amani, ulinzi na usalama nchini Sudani kusini wakiwemo Rais Cyril Ramaphosa wa Afrika Kusini, Rais Yoweri Museveni wa Uganda na sasa Rais William Ruto wa Kenya.
Aidha, Dkt. Kikwete ameshafanya ziara nchini Sudani Kusini na kukutana na Makundi yote muhimu katika mgogoro huo kwa lengo la kukubaliana mkakati endelevu utakaohakikisha amani inarejea katika nchi hiyo changa kuliko zote barani Afrika

Rais Mstaafu Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, ambaye ni Mwakilishi wa Ngazi ya Juu wa Mwenyekiti wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika kwenye Eneo la Pembe ya Afrika na Bahari ya Shamu jana amekutana na kufanya mazungumzo na Rais William Ruto wa Kenya, Nairobi. Picha na IKULU, NAIROBI


KIKWETE AKUTANA NA MJUMBE MAALUM WA JUMUIYA YA MADOLA, RAIS MSTAAFU WA MALAWI DKT. LAZARUS CHAKWERA JIJINI DAR ES SALAAM
habariRais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, amemkaribisha Rais Mstaafu wa Malawi, Dkt. Lazarus Chakwera, ofisini kwake jijini Dar es Salaam Jumatano April 15, 2026, kwa mazungumzo yenye lengo la kuimarisha maridhiano ya kisiasa nchini.
Dkt. Chakwera yupo nchini kwa ziara rasmi ya kikazi kufuatia kuteuliwa kwake kuwa Mjumbe Maalum wa Jumuiya ya Madola (Commonwealth), chini ya uongozi wa Katibu Mkuu Bi. Shirley Ayorkor Botchwey.
Aliwasili Aprili 8, 2026, amepewa jukumu la kusaidia juhudi za kidiplomasia za kupunguza mvutano wa kisiasa uliotokana na uchaguzi mkuu wa Oktoba 29, 2025.
Katika kipindi cha ziara yake, Dkt. Chakwera amekutana na wadau mbalimbali wakiwemo viongozi wa serikali, vyama vya siasa, asasi za kiraia, viongozi wa dini pamoja na wanadiplomasia.
Amekutana pia na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan na kufanya naye mazungumzo yanayo lenga kuweka msingi wa majadiliano jumuishi ya kitaifa yatakayochochea maridhiano, maboresho ya mfumo wa utawala na kudumisha utulivu wa kisiasa wa muda mrefu nchini.
Ziara hii ni sehemu ya mfumo wa “Good Offices” wa Commonwealth, unaolenga kuhamasisha mazungumzo ya faragha na suluhu za amani miongoni mwa nchi wanachama.
Mhe. Dkt. Chakwera, ambaye amehitimisha ziara yake hiyo nchini, amepongeza ushirikiano unaoendelea na kueleza utayari wa Jumuiya ya Madola kuendelea kuisaidia Tanzania katika kuimarisha utawala wa sheria, ushirikiano wa kisiasa na mshikamano wa kitaifa.
Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, akiwa na Mjumbe Maalum wa Jumuiya ya Madola (Commonwealth), Rais Mstaafu wa Malawi, Dkt. Lazarus Chakwera, ofisini kwake jijini Dar es Salaam Jumatano April 15, 2026.
Balozi Waziri Salum Aridhishwa na Utendaji wa TBS
habariMNEC-SUKI RABIA HAMID,KANSELA WA CPC WAFANYA KIKAO KAZI JIJINI DAR
Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa - Mambo ya Siasa na Uhusiano wa Kimataifa (SUKI), Ndg. Rabia Abdalla Hamid, amefanya Kikao kazi na Kansela wa Chama Cha Kikomunisti (CPC), Ubalozi wa China nchini Tanzania Ndg. Xu Sujiang leo tarehe 16.04.2026, Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba, Dar es Salaam.
Lengo la kikao hicho ni kujadiliana kuhusu masuala mbalimbali yanayolenga kuimarisha uhusiano na itikadi za vyama hivyo.
















.jpeg)
.jpeg)


.jpeg)





