HABARI

SIASA

ELIMU

Recent Posts

MIRADI 19 YA MAENEO MAALUM YA KIUCHUMI (SEZ) YAZALISHA AJIRA ZAIDI YA 11,700 NCHINI

MIRADI 19 YA MAENEO MAALUM YA KIUCHUMI (SEZ) YAZALISHA AJIRA ZAIDI YA 11,700 NCHINI

April 16, 2026 Add Comment

Waziri Wa Nchi, Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, Prof. Kitila Mkumbo akiwasilisha Hotuba ya Bajeti kwa Mwaka wa Fedha 2026/2027.

Na.Alex Sonna,Mzalendo blog-Dodoma

Serikali imeandika historia mpya katika sekta ya uwekezaji baada ya kusajili miradi 915 yenye thamani ya dola za Marekani bilioni 10.95 mwaka 2025, ikiwa ni kiwango cha juu zaidi kuwahi kufikiwa tangu kuanzishwa kwa mfumo wa usajili wa miradi ya uwekezaji mwaka 1996.

Hayo yameelezwa leo Aprili 16,2026 bungeni jijini Dodoma na Waziri Wa Nchi, Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, Prof. Kitila Mkumbo akiwasilisha Hotuba ya Bajeti kwa Mwaka wa Fedha 2026/2027.

Prof.Mkumbo amesema kuwa  mafanikio hayo yanaakisi ukuaji mkubwa wa sekta ya uwekezaji nchini, ambapo katika kipindi cha miaka mitano iliyopita, idadi ya miradi imeongezeka kutoka 256 mwaka 2021 hadi 915 mwaka 2025—sawa na ongezeko la asilimia 257.4.

Amesema  hatua hiyo ni ishara ya kuimarika kwa mazingira ya biashara na uwekezaji, sambamba na juhudi za makusudi za kuvutia wawekezaji wa ndani na nje ya nchi.

"Tanzania pia imeanza kupanua uwekezaji wake nje ya mipaka. Takwimu za awali zinaonyesha kuwa kampuni za Kitanzania zimewekeza zaidi ya dola bilioni 3.1 katika nchi mbalimbali zikiwemo Kenya, Uganda, Rwanda, Afrika Kusini, Japan na Qatar. Uwekezaji huo unalenga kupanua masoko, kuongeza ushindani na kuchochea uhamishaji wa teknolojia."amesema Prof.Mkumbo

Hata hivyo amesema kuwa Sekta zinazoongoza katika uwekezaji huo wa nje ni pamoja na viwanda vya chakula na vinywaji, nishati, usafirishaji, huduma za kifedha na vyombo vya habari.

Katika hatua nyingine, Serikali imekamilisha mapitio ya Sera ya Taifa ya Uwekezaji ya mwaka 1996 na kuandaa sera mpya ya mwaka 2026 inayosubiri kuidhinishwa. Sera hiyo inalenga kuboresha mazingira ya uwekezaji kwa kuweka mkazo kwenye upatikanaji wa ardhi, vivutio vya uwekezaji, ubunifu na ushirikiano kati ya sekta ya umma na binafsi.

Sambamba na hilo, Mkakati wa Taifa wa Uwekezaji wa mwaka 2026–2031 umeandaliwa ili kutafsiri sera hiyo katika vitendo, kwa kuainisha vipaumbele na hatua mahsusi za kukuza uwekezaji wenye tija kwa uchumi wa taifa.

Katika kuimarisha ulinzi wa uwekezaji, Tanzania imeendelea kusaini mikataba ya kimataifa ya uwekezaji, ambapo hadi Machi 2026 jumla ya mikataba 20 ilikuwa imesainiwa, huku mingine ikiendelea kujadiliwa na nchi mbalimbali ikiwemo Japan, Canada na Umoja wa Falme za Kiarabu.

Aidha, Serikali imeongeza kasi ya maendeleo ya Maeneo Maalum ya Kiuchumi (SEZ), ambapo miradi 19 yenye thamani ya dola milioni 331.51 imesajiliwa na kutarajiwa kuzalisha ajira zaidi ya 11,700 pamoja na kuongeza mauzo ya nje.

Katika maeneo hayo, uwekezaji umeelekezwa kwenye viwanda vya kuchakata mazao ya kilimo, uzalishaji wa bidhaa za chuma, dawa na hata uunganishaji wa magari kwa kutumia teknolojia za kisasa.

Serikali pia imeendelea kuboresha huduma kwa wawekezaji kupitia Kituo cha Pamoja cha Uwezeshaji Uwekezaji (OSFC), ambapo idadi ya taasisi zinazotoa huduma imeongezeka na kurahisisha upatikanaji wa vibali na nyaraka muhimu kwa wawekezaji.

Katika jitihada za kuimarisha uchumi, mapato yasiyo ya kodi kutoka mashirika ya umma yameongezeka na kufikia shilingi bilioni 773.37 hadi Machi 2026, ikiwa ni asilimia 85 ya lengo la kipindi hicho. Serikali pia imeongeza uwekezaji wake katika mashirika ya umma hadi kufikia shilingi trilioni 90.61.

Pamoja na mafanikio hayo, Serikali imeendelea kufanya mageuzi ya kimuundo kwa kufuta na kuunganisha baadhi ya mashirika ya umma ili kuongeza ufanisi na tija.

Hatua nyingine muhimu iliyochukuliwa ni kuboresha mazingira ya biashara kupitia mpango wa MKUMBI, ambapo sheria 28 zimefanyiwa mapitio na tozo 245 zimeondolewa au kupunguzwa ili kupunguza gharama kwa wafanyabiashara.

Serikali imesisitiza kuwa mageuzi haya yanalenga kujenga mazingira rafiki, yenye ushindani na yanayovutia uwekezaji zaidi, huku yakichochea ukuaji wa uchumi na ajira kwa Watanzania.

Amesema kuwa mwelekeo wa sasa unaonyesha kuwa Tanzania inaendelea kujijenga kama kitovu muhimu cha uwekezaji barani Afrika, huku mikakati mipya ikiweka msingi imara wa kufikia malengo ya maendeleo ya muda mrefu ifikapo mwaka 2050.

JUMLA YA WANANCHI 25 WA MBEZI JOGOO WAKOPESHWA MAJIKO SANIFU YA UMEME

April 16, 2026 Add Comment


📌Ni sehemu ya jitihada za TANESCO za kuhamasisha matumizi ya umeme kupikia


📌Diwani wa Mbezi juu aipongeza TANESCO kwa kuibeba ajenda ya nishati safi kwa vitendo.


Diwani wa Kata ya Mbezi Juu, Bi. Anna Lukindo, ameipongeza TANESCO chini ya uongozi wa Mkurugenzi Mtendaji, Bw. Lazaro Twange, kwa jitihada  za kutekeleza ajenda ya Serikali ya kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia nchini.

Pongezi hizo zimekuja kufuatia utekelezaji wa mpango wa pili wa ugawaji wa majiko ya umeme kwa mkopo nafuu kwa wakazi wa Mbezi Jogoo, ambapo jumla ya wananchi 25 tayari wamenufaika na mpango huo.

Akizungumza kuhusu hatua hiyo, Bi. Lukindo amesema mpango huo ni ushahidi wa dhamira ya TANESCO katika kuboresha maisha ya wananchi kupitia nishati salama na rafiki kwa mazingira.

“Naipongeza sana TANESCO kwa kuendelea kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia. Zoezi hili linaakisi dhamira  ya kuboresha maisha ya wananchi, kuongeza ufanisi wa matumizi ya umeme, na kuendeleza ajenda ya maendeleo endelevu,” alisema.

Aidha, Diwani huyo amewataka wakazi wengine wa kata hiyo kuchangamkia fursa hiyo ya kupata majiko ya umeme kwa mkopo nafuu.


 Amebainisha kuwa walengwa watalipa kwa utaratibu rahisi kupitia manunuzi ya umeme (LUKU) ndani ya kipindi cha miezi 12.

Kwa upande wake, Afisa Uhusiano na Huduma kwa Wateja, Bi. Winifrida Peter, ametoa elimu kwa wananchi mara baada ya kukabidhiwa majiko hayo, akisisitiza matumizi sahihi na salama ya vifaa hivyo ili kulinda afya zao pamoja na mazingira.



Mpango huo unaendelea kuwa chachu ya mabadiliko chanya kwa jamii,  ukihamasisha matumizi ya nishati safi kama sehemu ya safari ya kuelekea maendeleo endelevu.

TANZANIA NA BRAZIL ZAJIZATITI KUENDELEZA USHIRIKIANO WA KIDIPLOMASIA

April 16, 2026 Add Comment
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Ngwaru Maghembe (Mb.) ameongoza ujumbe wa Tanzania kwenye Mkutano wa Pili wa Mashauriano ya Kisiasa kati ya Tanzania na Brazili uliofanyika jijini Brasilia, Brazili Aprili 15, 2026.

JK AZINDUA HARAMBEE KUCHANGIA UJENZI WA MAABARA YA TEHAMA YA “DARASA JANJA” SHULE YA SEKONDARI KIBAHA

April 16, 2026 Add Comment





Na Issa Michuzi,

Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, Jumatano, Aprili 15, 2026, amehudhuria Mahafali ya 59 ya Shule ya Sekondari Kibaha (KSS) kama mgeni rasmi, katika hafla iliyofanyika shuleni hapo, Tumbi, Kibaha Mji, mkoani Pwani.

Akiwa katika mahafali hayo, Dkt. Kikwete amezindua harambee ya kuchangia ujenzi wa jengo la ghorofa la maabara ya TEHAMA na masomo mengine, ambalo linatarajiwa kugharimu shilingi bilioni 3.

Amesema ujenzi huo ni muhimu katika kuendeleza ubunifu na uwezo wa wanafunzi katika masomo ya sayansi, teknolojia, uhandisi na hisabati (STEM).

Aidha, Dkt. Kikwete amekubali kuwa mlezi wa kamati ya kukusanya michango kwa ajili ya mradi huo mkubwa ambao kwa sasa umefikia hatua ya msingi.


Pia, Rais Mstaafu ameishukuru jumuiya ya wanafunzi wa zamani (alumni) wa shule hiyo, wakiuongozwa na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA) Bw. Abdul Mombokaleo, kwa kuchangia kompyuta zenye thamani ya Shilingi Milioni 170 kwa ajili ya “Darasa Janja” (Smart Class) lililoanzishwa shuleni hapo.

Darasa hilo litakuwa ni kituo cha mafunzo kwa wanafunzi wa shule hiyo na shule nyingine zitakazounganishwa kupitia mfumo wa mtandao, ambapo mwalimu anaweza kufundisha madarasa yaliyoko nje ya Kibaha kwa wakati mmoja kwa njia ya kidigitali.

Katika ziara yake, Dkt. Kikwete alipata fursa ya kutembelea na kukagua Darasa Janja hilo, akipokea maelezo kutoka kwa Mkuu wa Shule kuhusu namna teknolojia hiyo inavyotumika kuboresha mbinu za ufundishaji na ujifunzaji shuleni hapo.

Shule ya Sekondari Kibaha, inayomilikiwa na Shirika la Elimu Kibaha na kusimamiwa na Kurugenzi ya Hud uma za Elimu, ilianzishwa mwaka 1965 kupitia ushirikiano kati ya Serikali ya Tanganyika ya wakati huo na nchi za Nordic – Denmark, Finland, Norway, na Sweden. Wakati inaanzishwa, shule ilikuwa na wanafunzi 110 wa Kidato cha Kwanza na 60 wa Kidato cha Tano.

Kwa sasa, shule hiyo ya bweni kwa wavulana ina uwezo wa kuchukua zaidi ya wanafunzi 800 na imeendelea kuwa miongoni mwa taasisi kongwe na zenye heshima kubwa katika sekta ya elimu nchini.

Dkt. Kikwete ni miongoni mwa alumni mashuhuri wa Shule ya Sekondari Kibaha, alikosoma zaidi ya miaka 60 iliyopita. Wengine waliopitia shule hiyo ni pamoja na Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati, Mkurugenzi Mkuu wa ATCL Bw. Peter Ulanga, Balozi Lazaro Nyalandu, Katibu Mtendaji wa Tume ya Taifa ya UNESCO Nchini Prof. Hamisi Malebo, Mkurugenzi Mkuu wa Viwanja vya Ndege Bw. Abdul Mombokaleo, na Mwenyekiti Mstaafu wa CHADEMA Mhe. Freeman Mbowe, miongoni mwa wengine wengi.

Aidha, kwa kutambua mchango mkubwa wa alumni wake, Shule ya Sekondari Kibaha inaendelea kuimarisha ushirikiano na wadau wa elimu ili kuhakikisha inaendelea kuwa kinara katika utoaji wa elimu ya ubora nchini.

Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, Jumatano, Aprili 15, 2026, akikagua na kupewa maelezo juu ya maabara ya TEHAMA ambayoni ‘Smart Class” na Mkuu wa Shule hiyo alipokuwa Mgeni rasmi katika n Mahafali ya 59 ya Shule ya Sekondari Kibaha (KSS) kama mgeni rasmi, katika hafla iliyofanyika shuleni hapo, Tumbi, Kibaha Mji, mkoani Pwani.
Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, Jumatano, Aprili 15, 2026, akimpongeza na kumshukuru Mkurugenzi Mkuu wa Viwanja vya Ndege (TAA) Bw. Abdul Mombokaleo kwa kujitolea computer zenye thamani ya shilingi milioni 170 kama mchango wake yeye na Alumni wengine kwa kuboresha elimu ya Sayansi katika shule hiyo.
Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, Jumatano, Aprili 15, 2026, akupewa maelezo juu ya mradi wa jengo la maabara ya TEHAMA ambayo ni ‘Smart Class’ alipokuwa Mgeni rasmi katika Mahafali ya 59 ya Shule ya Sekondari Kibaha (KSS) kama mgeni rasmi, katika hafla iliyofanyika shuleni hapo, Tumbi, Kibaha Mji, mkoani Pwani.
Sehemu ya wahitimu wa kidato cha sita katika Mahafali ya 59 ya Shule ya Sekondari Kibaha (K katika hafla iliyofanyika shuleni hapo, Tumbi, Kibaha Mji, mkoani Pwani.
(Picha na Habari na Issa Michuzi)
BRELA YASUKUMA MAGEUZI YA KIDIGITALI KATIKA BIASHARA

BRELA YASUKUMA MAGEUZI YA KIDIGITALI KATIKA BIASHARA

April 15, 2026 Add Comment

Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Usajili wa Leseni (BRELA) Bw Godfrey Nyaisa,akitoa ufafanuzi kwa Madiwani wa Halmashauri ya Dodoma wakati wa mafunzo kwa madiwani hao juu ya Huduma zitolewazo na BRELA katika kuwezesha biashara nchini. Mafunzo hayo yametolewa na BRELA yaliyofanyika leo 15,2026 jijini Dodoma.

...

VIJANA nchini Tanzania wanaendelea kurasimisha shughuli zao za biashara kwa kasi, hali inayoashiria kuongezeka kwa ushiriki wao katika uchumi rasmi na mchango wao katika juhudi za maendeleo ya taifa.

Hayo yameelezwa leo Aprili 15,2026 na Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA), Bw.Godfrey Nyaisa, wakati wa Semina kwa madiwani wa halmashauri ya Dodoma .

Bw.Nyaisa amesema takwimu za BRELA zinaonesha kuwa maelfu ya kampuni, majina ya biashara na alama za biashara na huduma (trade and service marks) zilizosajiliwa katika kipindi cha mwaka mmoja uliopita zinamilikiwa na vijana. Hali hii inaonesha wazi kuongezeka kwa mchango wa vijana katika sekta za viwanda na biashara nchini.

"Kampuni 5,045 zimesajiliwa, ambapo 3,120 zinamilikiwa na vijana. Aidha, majina ya biashara 8,792 yamesajiliwa, kati ya hayo 4,938 ni ya vijana. Kwa upande wa alama za biashara, jumla ya 1,018 zimesajiliwa, nyingi zikiwa zinamilikiwa na vijana. Vilevile, leseni za biashara daraja la “A” 5,430 zimetolewa, ambapo takribani nusu yake zimekwenda kwa vijana."amesema Bw.Nyaisa

Amesema mafunzo hayo yanalenga kuwajengea uwezo madiwani kuhusu taratibu za usajili wa biashara, utoaji wa leseni pamoja na ulinzi wa haki miliki, ili waweze kuwasaidia wafanyabiashara katika kata zao kwa ufanisi zaidi.

Hata hivyo amempongeza Meya wa Jiji la Dodoma kwa kushiriki mafunzo hayo, hatua hiyo inaonesha dhamira ya dhati ya kuboresha mazingira ya biashara katika mji mkuu wa nchi. Pia ametambua mchango wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma chini ya uongozi wa Rosemary Senyamule kwa ushirikiano wake katika kutoa elimu ya biashara na msaada wa kitaalamu.

Ameeleza kuwa mafunzo hayo yanahusisha maeneo muhimu kama usajili wa kampuni, majina ya biashara, alama za biashara, hati miliki (patents), pamoja na utoaji wa leseni za viwanda na leseni za biashara daraja la “A”.

Aidha, amebainisha kuwa chini ya uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan, BRELA imefanya maboresho mbalimbali ya kurahisisha mazingira ya kufanya biashara, ikiwemo kuanzisha mifumo ya kidijitali inayowezesha huduma kupatikana mtandaoni kupitia simu za mkononi.

Hata hivyo, Nyaisa ametaja changamoto ya utofauti katika utoaji wa leseni za biashara katika ngazi za serikali za mitaa. Alieleza kuwa baadhi ya wafanyabiashara hupewa leseni daraja la “B” badala ya “A” kimakosa, hali inayosababisha mkanganyiko.

Amewataka madiwani kutumia mafunzo hayo kutatua changamoto hizo na kuwa mabalozi wa kuhamasisha urasimishaji wa biashara, hususan kwa vijana, wanawake na wajasiriamali wadogo.

“Baada ya mafunzo hayo, tunatarajia muwe mabalozi wazuri katika maeneo yenu na kusaidia kutatua changamoto zinazowakabili wananchi katika ngazi za chini,” amesema.

Kwa upande wake, Meya wa Jiji la Dodoma, Alimwona Chaula,amesema mafunzo hayo ni muhimu katika kuwajengea uwezo madiwani wanaofanya kazi kwa karibu na wananchi katika ngazi ya msingi. Aliongeza kuwa yatawasaidia kuelewa vyema taratibu za usajili na utoaji wa leseni za biashara ili waweze kuwasaidia wananchi katika shughuli zao za kila siku za kiuchumi.

Mafunzo hayo ni sehemu ya mkakati mpana wa BRELA wa kujenga uchumi shindani na jumuishi kwa kuongeza ushiriki wa wananchi katika shughuli rasmi za biashara nchini.

Mstahiki Meya wa Jiji la Dodoma, Mhe Alimwona Chaula,akizungumza wakati wa  ufunguzi wa mafunzo ya madiwani wa Halmashauri ya Dodoma yaliyoandaliwa na Wakala wa Usajili wa Leseni (BRELA) yakilenga kuwajengea elimu juu ya Huduma zitolewazo na BRELA katika kuwezesha biashara nchini yaliyofanyika leo Aprili 15,2026  jijini Dodoma

Mstahiki Meya wa Jiji la Dodoma, Mhe Alimwona Chaula,akizungumza wakati wa  ufunguzi wa mafunzo ya madiwani wa Halmashauri ya Dodoma yaliyoandaliwa na Wakala wa Usajili wa Leseni (BRELA) yakilenga kuwajengea elimu juu ya Huduma zitolewazo na BRELA katika kuwezesha biashara nchini yaliyofanyika leo Aprili 15,2026  jijini Dodoma

Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Usajili wa Leseni (BRELA) Bw Godfrey Nyaisa,akitoa ufafanuzi kwa Madiwani wa Halmashauri ya Dodoma wakati wa mafunzo kwa madiwani hao juu ya Huduma zitolewazo na BRELA katika kuwezesha biashara nchini. Mafunzo hayo yametolewa na BRELA yaliyofanyika leo 15,2026 jijini Dodoma.

Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Usajili wa Leseni (BRELA) Bw Godfrey Nyaisa,akitoa ufafanuzi kwa Madiwani wa Halmashauri ya Dodoma wakati wa mafunzo kwa madiwani hao juu ya Huduma zitolewazo na BRELA katika kuwezesha biashara nchini. Mafunzo hayo yametolewa na BRELA yaliyofanyika leo 15,2026 jijini Dodoma.

Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Usajili wa Leseni (BRELA) Bw Godfrey Nyaisa,akitoa ufafanuzi kwa Madiwani wa Halmashauri ya Dodoma wakati wa mafunzo kwa madiwani hao juu ya Huduma zitolewazo na BRELA katika kuwezesha biashara nchini. Mafunzo hayo yametolewa na BRELA yaliyofanyika leo 15,2026 jijini Dodoma.

Madiwani wa Halmashauri ya Dodoma wakisikiliza elimu juu ya Huduma zitolewazo na BRELA katika kuwezesha biashara nchini. Mafunzo haya yamelenga kuwajengea ufahamu juu ya masuala ya urasimishaji biashara ili kuleta chachu za mabadiliko katika Kata wanazoziongoza. Mafunzo hayo yametolewa na Wakala wa Usajili wa Leseni (BRELA) leo Aprili 15, 2026 jijini Dodoma

Madiwani wa Halmashauri ya Dodoma wakisikiliza elimu juu ya Huduma zitolewazo na BRELA katika kuwezesha biashara nchini. Mafunzo haya yamelenga kuwajengea ufahamu juu ya masuala ya urasimishaji biashara ili kuleta chachu za mabadiliko katika Kata wanazoziongoza. Mafunzo hayo yametolewa na Wakala wa Usajili wa Leseni (BRELA) leo Aprili 15, 2026 jijini Dodoma.

Madiwani wa Halmashauri ya Dodoma wakisikiliza elimu juu ya Huduma zitolewazo na BRELA katika kuwezesha biashara nchini. Mafunzo haya yamelenga kuwajengea ufahamu juu ya masuala ya urasimishaji biashara ili kuleta chachu za mabadiliko katika Kata wanazoziongoza. Mafunzo hayo yametolewa na Wakala wa Usajili wa Leseni (BRELA) leo Aprili 15, 2026 jijini Dodoma.

Mkurugenzi wa Kampuni na Majina ya Biashara Bw Isdor Nkindi, akitoa elimu kwa Madiwani wa Halmashauri ya Dodoma juu ya Huduma zitolewazo na Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA). Mafunzo hayo yametolewa na BRELA yaliyofanyika leo Aprili 15, 2026 jijini Dodoma

Mkurugenzi wa Kampuni na Majina ya Biashara Bw Isdor Nkindi, akitoa elimu kwa Madiwani wa Halmashauri ya Dodoma juu ya Huduma zitolewazo na Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA). Mafunzo hayo yametolewa na BRELA yaliyofanyika leo Aprili 15, 2026 jijini Dodoma

Mbunge wa Jimbo la Dodoma Mjini Mhe.Paschal Inyasi Chinyele,akichangia mada wakati wa semina ya madiwani wa Halmashauri ya Dodoma yaliyoandaliwa na Wakala wa Usajili wa Leseni (BRELA) yakilenga kuwajengea elimu juu ya Huduma zitolewazo na BRELA katika kuwezesha biashara nchini yaliyofanyika leo Aprili 15,2026  jijini Dodoma.

Madiwani wa Halmashauri ya Dodoma wakichangia mada juu ya Huduma zitolewazo na Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) katika kuwezesha biashara nchini katika semina iliyoandaliwa na BRELA leo tarehe 15 Aprili, 2026 jijini Dodoma

Madiwani wa Halmashauri ya Dodoma wakichangia mada juu ya Huduma zitolewazo na Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) katika kuwezesha biashara nchini katika semina iliyoandaliwa na BRELA leo tarehe 15 Aprili, 2026 jijini Dodoma

Madiwani wa Halmashauri ya Dodoma wakichangia mada juu ya Huduma zitolewazo na Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) katika kuwezesha biashara nchini katika semina iliyoandaliwa na BRELA leo tarehe 15 Aprili, 2026 jijini Dodoma

Madiwani wa Halmashauri ya Dodoma wakichangia mada juu ya Huduma zitolewazo na Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) katika kuwezesha biashara nchini katika semina iliyoandaliwa na BRELA leo tarehe 15 Aprili, 2026 jijini Dodoma

KATIBU MKUU CCM AKUTANA NA UJUMBE MAALUMU WA JUMUIYA YA MADOLA

April 15, 2026 Add Comment


Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Ndg. Asha-Rose Migiro, leo tarehe 15 Aprili 2026 amefanya mazungumzo na Mjumbe Maalum wa Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Madola na Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Malawi, Mhe. Lazarus Chakwera, katika Ofisi za CCM Lumumba, jijini Dar es Salaam.

Mazungumzo hayo yalijikita katika hali ya kisiasa nchini pamoja na matukio ya wakati na baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2025.

Mhe. Chakwera yupo nchini Tanzania kwa ziara maalum katika nafasi yake kama Mjumbe Maalum wa Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Madola, Mhe. Shirley Ayorkor Botchwey.

Kikao hicho ni sehemu ya mashauriano yake na wadau mbalimbali wa kitaifa kwa lengo la kubadilishana mawazo kuhusu maendeleo ya kisiasa baada ya Uchaguzi Mkuu wa tarehe 29 Oktoba 2025, pamoja na juhudi zinazoendelea za kuimarisha amani, demokrasia na mshikamano wa kitaifa nchini Tanzania.








MINISTER KOMBO MEETS TANZANIAN STUDENTS IN MAURITIUS; CALLS FOR DISCIPLINE AND PATRIOTISM

April 14, 2026 Add Comment

      

On 13th April, 2026, the Minister for Foreign Affairs and East African Cooperation, Ambassador Kombo, met and held discussions with Tanzanian students studying in Mauritius, where he used the opportunity to offer important guidance regarding their academic lives and their role as representatives of Tanzania abroad.

TCDC YAKABIDHI VIFAA VYA MICHEZO KWA WACHEZAJI

TCDC YAKABIDHI VIFAA VYA MICHEZO KWA WACHEZAJI

April 14, 2026 Add Comment

Mrajis na Mtendaji Mkuu wa Tume ya Maendeleo ya Ushirika Tanzania (TCDC) Dkt. Benson Ndiege kushirikiana na Uongozi wa TCDC Sports Club wanunua vifaa vya michezo kwa wachezaji 42 kuelekea mashindano ya Michezo ya Meimosi mjini Njombe.

Vifaa hivyo vimekabidhiwa leo Aprili 14, 2026 jijini Dodoma wakati wa kuwaaga wanamichezo wakielekea mjini Njombe.

Vifaa vilivyonunuliwa ni jezi za mprira wa miguu, viatu, mipira na vifaa vingine vya michezo.