HABARI

SIASA

ELIMU

Recent Posts

OFISI YA WAZIRI MKUU YAINOA TIMU YA KUKABILIANA NA MAAFA MKOA WA DODOMA

April 27, 2026 Add Comment





Na Mwandishi wetu- DODOMA

Katibu Tawala Mkoa wa Dodoma, Dkt. Khatibu Kazungu, amesema Ofisi yake ikishirikiana na Ofisi ya Waziri Mkuu Idara ya Menejimenti ya Maafa ipo katika hatua ya kuanzisha Kituo cha Operasheni ya Dharura katika Mkoa ikiwa ni utekelezaji wa Sera ya Taifa ya Usimamizi wa Maafa ya mwaka 2004.

Dkt. Kazungu ameyasema hayo leo tarehe 27 Aprili,2026 jijini Dodoma kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma wakati akifungua mafunzo ya siku nne ya kujiandaa na kukabiliana na maafa kwa Timu ya kukabiliana na dharura ya Mkoa ambayo yameandaliwa na Ofisi ya Waziri Mkuu kupitia Idara ya Menejimenti ya Maafa pamoja na uanzishaji wa kituo cha Operesheni na Mawasiliano ya Dharura cha Mkoa.

NEMC, ZEMA WABADILISHANA UZOEFU KATIKA TATHMINI ZA ATHARI ZA MAZINGIRA

April 27, 2026 Add Comment
Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) na Mamlaka ya Usimamizi wa Mazingira Zanzibar (ZEMA) wamekutana Aprili 27,2026 katika ziara ya mafunzo, kwa lengo la kubadilishana uzoefu katika utekelezaji wa majukumu ya kimazingira, hasa mchakato wa ufanyaji wa Tathmini ya Athari kwa Mazingira na jamii katika miradi mikubwa na mchakato wa kupata vyeti vya kimazingira ili kuhakikisha maendeleo yanaendana na uhifadhi wa mazingira.

MIGODI YA BARRICK TANZANIA YAFIKISHA ELIMU YA USALAMA KWENYE JAMII MAONESHO YA OSHA NJOMBE

April 27, 2026 Add Comment

 


Mkuu wa Mkoa wa Njombe , Mhe. Anthony Mtaka akipokea moja ya mitungi ya gesi uliotolewa na Barrick
Mkuu wa Mkoa wa Njombe , Mhe. Anthony Mtaka akipokea Zawadi ya begi kutoka Afisa Mifumo ya Usalama wa Barrick, Beatrice Amos.
Afisa wa Usalama kutoka Mgodi wa Barrick Mgodi North Mara, Maisori Mniko akizima moto kwa vitendo katika mafunzo ya siku moja ya kupambana na majanga ya moto.
Afisa Msimamizi wa Usalama kutoka Barrick North Mara, Athanas Mtenga akitoa elimu ya usalama mahala pa kazi kwa wajasiriamali wa Mkoani wa Njombe.
Baadhi ya timu ya wafanyakazi wa Barrick kwenye maonesho
Majaji wa OSHA wakipita katika banda la maonesho la Barrick.

CCM NA CPC MAANDALIZI YA KUPOKEA UGENI

April 27, 2026 Add Comment

Katibu wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (NEC), Siasa na Uhusiano wa Kimataifa (SUKI), Ndugu Rabia Abdalla Hamid akiwa kwenye kikao kazi na Kansela wa Chama cha Kikomunisti cha China (CPC) wa Ubalozi wa China nchini Tanzania, Ndugu Xu Sujiang, leo Jumatatu tarehe 27 Aprili 2026, Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba, jijini Dar Es Salaam, ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya kupokea ugeni wa Mjumbe wa Kamati Kuu ya CPC na Waziri wa Mambo ya Nje wa China, Mhe. Liu Haixing, anayetarajiwa kufanya ziara rasmi nchini Tanzania, mwezi Mei 2026.

#KazinaUtuTunasongaMbele



BARRICK YAWEZESHA WANAFUNZI VYUO VIKUU MOROGORO KUPATIWA UTAMBUZI WA FURSA KUPITIA AIESEC 2026

April 27, 2026 Add Comment

  

Picha ya pamoja ya wadhamini na viongozi wa AIESEC Tanzania
Wanafunzi na wageni waalikwa wakifuatilia mada mbalimbali wakati wa kongamano la AIESEC lililofanyika katika Chuo Kikuu cha Mzumbe mkoani Morogoro
Wafanyakazi wa Barrick katika kongamano hilo

***
Wanafunzi wa vyuo vikuu mkoani Morogoro wamepata fursa ya kupata elimu ya kuchangamkia fursa za kupata mafanikio kupitia elimu yao katika kongamano lililoandaliwa na taasisi ya AIESEC lililodhaminiwa na Barrick kwa kushirikiana na wadau mbalimbali.

KAMISHNA LUOGA AONGOZA WATAALAMU KUTOKA TANZANIA KATIKA MKUTANO WA AU KUHUSU NISHATI NA UCHUKUZI

April 27, 2026 Add Comment




Wizara ya Nishati na Wizara ya Uchukuzi za Tanzania zimeshiriki katika Mkutano wa 5 wa mwaka wa Kamati Maalum ya Wataalamu ya Umoja wa Afrika kuhusu Uchukuzi na Nishati (Specialised Technical Committee (STC) on Transport and Energy), unaofanyika jijini Johannesburg, Afrika Kusini 


Ushiriki wa Tanzania kwa ngazi ya wataalamu unaongozwa na Kamishna wa Umeme na Nishati Jadidifu, Mhandisi Innocent Luoga, aliyeongoza ujumbe wa sekta kushiriki katika majadiliano ya kimkakati yanayolenga kuimarisha maendeleo ya miundombinu ya nishati na uchukuzi barani Afrika.

Wataalamu wengine walioshiriki mkutano huo ni Mkurugenzi wa Usalama wa Usafiri na Mazingira wa Wizara ya Uchukuzi, Bi. Stella Katondo, Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC), Bw. Mohamed Salum, pamoja na wataalamu wengine kutoka katika sekta husika.

Mkutano huo wa wataalamu umeanza Aprili 27 hadi 29, 2026, ambapo unajadili masuala mbalimbali ya sekta ya nishati na uchukuzi ikiwemo kuongeza uwekezaji katika nishati jadidifu, matumizi ya gesi asilia, pamoja na kuimarisha miundombinu ya umeme wa kuvuka mipaka.

Mkutano huo utafuatiwa na kikao cha Mawaziri kitakachofanyika Aprili 30, 2026, ambapo Tanzania pia itashiriki.

Katika majadiliano hayo, nchi wanachama zinaangazia mikakati ya kuboresha upatikanaji wa nishati ya uhakika na nafuu, pamoja na kuendeleza mifumo jumuishi ya uchukuzi ikiwemo reli, barabara, anga na usafiri wa majini ili kurahisisha biashara na usafirishaji barani Afrika



CBE YAENDELEZA MAZINGIRA JUMUISHI KUPITIA MIKAKATI YA KIJINSIA

April 27, 2026 Add Comment
NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

Imeelezwa kuwa usawa wa kijinsia unaendelea kuwa nguzo muhimu katika kufanikisha maendeleo endelevu, kuchochea ukuaji wa uchumi na kuimarisha utawala bora katika jamii na taifa kwa ujumla.

MKOA WA NJOMBE KUSHIRIKIANA NA OMR, WIZARA YA MALIASILI KUDHIBITI MAJANGA YA MOTO

April 27, 2026 Add Comment
Mkuu wa Mkoa wa Njombe, Mhe. Antony Mtaka akizungumza na Wanamichezo wanaoshiriki Mashindano ya Mei Mosi, 2026 Mkoani humo wakati waliofika katika Ofisiza Mkoa huo Aprili 27, 2026 kwa ajili ya zoezi la upandaji Miti kupitia kampeni ya 27 ya kijani, Mti wa Mama inayofanyika tarehe ya Kila mwezi.

OMR YATWAA USHINDI NAFASI YA TATU KARATA WANAWAKE

April 27, 2026 Add Comment


OFISI ya Makamu wa Rais imebuka mshindi wa nafasi ya tatu kupitia mchezo wa karata upande wa wanawake katika Mashindano ya Michezo ya Mei Mosi, 2026 yanayoendelea Mkoani Njombe.

KIKUNDI CHA WE ARE FAMILY CHAWAFIKIA WAGONJWA OCEAN ROAD CANCER INSTITUTE

April 27, 2026 Add Comment

NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

Kikundi cha We Are Family kinachowahusisha wenza wa majaji nchini, kimetembelea wagonjwa wa saratani katika Ocean Road Cancer Institute jijini Dar es Salaam, ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa dhamira yao ya kufanya matendo ya huruma kwa jamii.

‘JOURNEY TO ZERO’ YA BARRICK YAVUTIA WENGI MAONESHO YA OSHA 2026

April 26, 2026 Add Comment

Kamishina wa Kazi Ofisi ya Waziri Mkuu , Kazi , Ajira na Watu Wenye Ulemavu , Suzan Mkangwa akipata maelezo kutoka kwa Afisa Usalama na Afya Mahali Pa Kazi  kutoka Mgodi wa Barrick North Mara, Michael Bernard (wa kwanza kulia) , alipotembelea banda la Barrick North Mara kwenye maonesho yanayoendelea kwenye viwanja vya Mji Mwema Mkoa wa Njombe
Baadhi ya wanafunzi wakipata mafunzo ya kudhibiti majanga ya moto katika maonesho haya yanayoendelea kwenye viwanja vya Mji Mwema Mkoa wa Njombe

***

KAFULILA ATOA WITO WA KUULINDA MUUNGANO

April 26, 2026 Add Comment

Katika kuadhimisha miaka 62 ya Muungano wa Tanzania, Mkurugenzi Mkuu wa Kituo cha Ubia kati ya Sekta ya Umma na Binafsi (PPPC), David Kafulila, amesema mafanikio ya Muungano huo yanatokana zaidi na mshikamano wa watu kuliko mifumo ya kiserikali.

DKT. MWIGULU AKAGUA MAENDELEO YA UJENZI WA MADARAJA YA MKWAJUNI NA KIGOGO, DAR ES SALAAM.

April 26, 2026 Add Comment

 Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba leo Aprili 26, 2026 anafanya ziara katika mkoa wa Dar es Salaam ambapo amekagua maendeleo ya ujenzi wa Daraja la Mkwajuni lenye urefu wa mita 20 na kimo cha mita 5.5 ambalo hadi kukamilika kwake litagharimu shilingi bilioni 11.6

Pia Mheshimiwa Dkt. Mwigulu amekagua mradi wa ujenzi wa Daraja la Kigogo lenye urefu wa mita 50 kimo cha mita 8.9 na barabara unganishi zenye jumla ya urefu wa mita 625 ambalo hadi kukamilika kwake litagharimu shilingi bilioni 17.7.









TAIFA GESI YATOA ELIMU YA MATUMIZI SALAMA YA GESI NJOMBE

April 26, 2026 Add Comment





Na Mwandishi Wetu

Kampuni ya Taifa Gesi imeendelea kutoa elimu kwa wananchi kuhusu matumizi sahihi na salama ya gesi, sambamba na kuhamasisha usalama mahali pa kazi katika maadhimisho ya Wiki ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi Duniani.

Akizungumza katika viwanja vya Shule ya Msingi Mji Mwema, Njombe, Mtaalamu wa Masuala ya Afya, Mazingira, Usalama na Ulinzi Mahali pa Kazi kutoka Taifa Gesi, Aurelius Marcus Mdemu, alisema kampuni hiyo imeshiriki maadhimisho hayo yanayoanza Aprili 24 hadi 29, 2026 kwa lengo la kutoa elimu kwa wateja na jamii kwa ujumla.




Alisema kupitia banda lao, wanaonesha vifaa mbalimbali vinavyotumika kazini ili kuimarisha usalama wa wafanyakazi, pamoja na kutoa elimu kuhusu matumizi sahihi ya gesi na faida zake. Aidha, alieleza kuwa wanajitahidi kuondoa hofu na dhana potofu zilizopo miongoni mwa watumiaji wa gesi.

“Tunawaonesha wananchi namna Taifa Gesi inavyoweka kipaumbele kwenye usalama wa wafanyakazi, ikiwa ni pamoja na matumizi ya vifaa kinga vinavyotakiwa kutumika muda wote wakiwa kazini,” alisema Mdemu.








Kwa upande wake, Afisa Masoko wa Chapa wa Taifa Gesi, Santina Ngaponda, alisema maonyesho hayo yameandaliwa na OSHA, yalianza Aprili 24 na yanatarajiwa kufikia kilele chake Aprili 29 mwaka huu.

Ngaponda aliwahimiza wakazi wa Njombe na maeneo ya jirani kutembelea banda la Taifa Gesi ili kupata elimu kutoka kwa wataalamu wa usalama, kujifunza matumizi sahihi ya gesi, pamoja na kuona vifaa vya usalama vinavyotumika kazini na umuhimu wake.


Aidha, aliongeza kuwa kampuni hiyo inatoa punguzo maalum la bei ya gesi na vifaa vyake, pamoja na zawadi mbalimbali kwa wateja watakaotembelea banda hilo.


Naye Meneja Mauzo wa Kanda ya Nyasa wa Taifa Gesi, Arnold Salewa, alisema wanaendelea kutumia maonyesho hayo kutoa elimu kuhusu matumizi sahihi ya nishati safi pamoja na kuuza bidhaa zao kwa bei ya promosheni.

Alisema kanda hiyo inajumuisha mikoa ya Njombe, Iringa na Ruvuma, na kwamba pia wanatoa fursa kwa wananchi wanaotaka kuwa mawakala wao, kwa kuwapatia elimu ya biashara na usimamizi salama wa mitungi ya gesi.

Salewa alisisitiza kuwa Taifa Gesi ipo mstari wa mbele kuhakikisha kaya, migahawa na taasisi mbalimbali zinaanza kutumia nishati safi ya kupikia kwa gharama nafuu, ili kupunguza athari za matumizi ya mkaa na kuni kwa mazingira na afya za Watanzania.

Aliongeza kuwa mwitikio wa wananchi umekuwa mkubwa, huku Taifa Gesi ikiendelea kuwa chaguo sahihi kwa watumiaji wengi nchini.

TRA KARIAKOO YASHIRIKI MKUTANO MKUU WA JWK, YASISITIZA UWASILISHAJI WA RITANI KWA WAKATI

April 25, 2026 Add Comment
Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Mkoa wa Kikodi Kariakoo imeshiriki kikamilifu katika Mkutano Mkuu wa Jumuiya ya Wafanyabiashara Kariakoo (JWK) uliofanyika katika ukumbi wa soko la Kariakoo, jijini Dar es Salaam.

DCEA YANUFAIKA NA TEKNOLOJIA YA KISASA KATIKA VITA DHIDI YA DAWA ZA KULEVYA

April 25, 2026 Add Comment
Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) imepokea vifaa vya kisasa vya uchunguzi wa kimaabara kutoka Ofisi ya Umoja wa Mataifa inayoshughulikia Dawa za Kulevya na Uhalifu (UNODC), ikiwa ni pongezi baada ya kutambua mafanikio yaliyofikiwa na Tanzania katika udhibiti wa dawa za kulevya nchini.

WAMILIKI WA HOTELI WATAKIWA KUJIANDAA KUNUFAIKA NA AFCON 2027

April 25, 2026 Add Comment
Waziri wa Maliasili na Utalii, Ashatu Kijaji (Mb), akiwa katikati katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa Hoteli ya Manyara’s Secret, iliyopo ndani ya Pori Tengefu la Mto wa Mbu, Wilaya ya Monduli, Mkoani Arusha.

GASCO YATOA ELIMU YA USALAMA KAZINI, YAVUTIA WANANCHI KATIKA MAADHIMISHO YA OSHA

April 25, 2026 Add Comment
Watumishi wa GASCO katika picha ya pamoja kwenye maonesho ya OSHA-mkoani Njombe

TALGWU TAWI LA RUWASA LAFANYA UCHAGUZI WA VIONGOZI WAPYA, MHANDISI RASHID ATETEA UENYEKITI

April 25, 2026 Add Comment

Chama cha Wafanyakazi Serikali za Mitaa (TALGWU), tawi la RUWASA, kimefanya mkutano mkuu wa uchaguzi wa viongozi wapya ambapo Mwenyekiti aliyemaliza muda wake, Mhandisi Rashid Abdallah, amefanikiwa kutetea nafasi yake ya uenyekiti.

Uchaguzi huo ulifanyika Aprili 24, 2026 jijini Dodoma, katika mazingira ya uwazi na ushirikishwaji mpana wa wanachama, waliotekeleza haki yao ya kidemokrasia kwa kuchagua viongozi watakaoongoza tawi hilo kwa kipindi cha miaka mitano ijayo.

Katika uchaguzi huo, viongozi waliochaguliwa ni pamoja na Mhandisi Rashid Abdallah (Mwenyekiti wa Tawi), Ibrahim Fungo (Katibu wa Tawi), Tumaini Gwatalile (Mwenyekiti wa Makundi Maalum – Wanawake), Ashura Nkunya (Katibu wa Makundi Maalum – Wanawake), Victoria Charles (Mjumbe wa Makundi Maalum – Vijana), na Adam Suleiman (Mjumbe wa Makundi Maalum – Watu wenye Ulemavu).

Uongozi huo mpya unatarajiwa kuimarisha mshikamano miongoni mwa wanachama, kulinda na kutetea maslahi yao, pamoja na kuendeleza maendeleo ya chama katika tawi la RUWASA.