HABARI

SIASA

ELIMU

Recent Posts

Ushirikiano wa Oryx Gas Tanzania na Doris Mollel Foundation Waimarisha Afya na Mazingira Kwimba

March 01, 2026 Add Comment
WATUMISHI wa sekta ya afya katika Wilaya ya Kwimba wamepatiwa nishati safi ya kupikia ya mitungi mikubwa ya gesi ya Oryx na majiko yake pamoja na kupatiwa elimu ya matumizi sahihi na salama ya nishati hiyo.

SERIKALI YA AWAMU YA SITA YASISITIZA UWEZESHWAJI WA WATU WENYE ULEMAVU

March 01, 2026 Add Comment

  

Na mwandishi wetu, Arusha.

Naibu Waziri katika Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu), Mhe. Ummy Nderiananga, amesisitiza dhamira ya Serikali ya kuendelea kuwawezesha kiuchumi watu wenye ulemavu kupitia mikopo ya asilimia 10 ya mapato ya Halmashauri, ikiwemo asilimia 2 inayotengwa mahsusi kwa kundi hilo.

KIKUNDI CHA AMANI NCHINI WAFANYA MKUTANO MAALUMU ULIOLENGA KUHAMASISHA UZALENDO NA KUELEZEA MAFANIKIO YA SERIKALI

March 01, 2026 Add Comment



Na Oscar Assenga,Tanga

KIKUNDI cha Amani nchini kimefanya mkutano maalumu leo katika Jiji la Tanga  uliolenga kuhamasisha uzalendo, kuelezea mafanikio ya Serikali na kupongeza utekelezaji wa ahadi za siku 100 za Rais tangu alipochaguliwa 2025.

Akizungumza wakati wa mkutano huo Maalumu Mwenyekiti wa Kikundi hicho nchini Hassan Kubebelwa alitoa wito kwa watanzania hususani vijana wametakiwa kuwa wazalendo kwa nchi na kuacha kukubali kushawishiwa na watu wanaoshinda kwenye majukwaa ya mitandao ya kijamii kueleza mabaya pekee na kuficha mazuri mengi yanayofanywa na Serikali

Katika kulitilia mkazo jambo hilo aliiomba Serikali kupitia Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) na Jeshi la Polisi, kuongeza kasi ya kuwafuatilia na kuwachukulia hatua kali watu wanaojiita wanaharakati wa mitandaoni wanaotumia majukwaa hayo kupotosha ukweli na kuichafua Serikali

"Lengo la kuja Tanga ni kuwahamasisha wanakikundi wenzetu wasimame kidete kuelezea maendeleo ya miundombinu mkoani hapa na nchi nzima. Tuache kusikiliza upotoshaji wa mitandaoni; Serikali imaleta fedha za mikopo ya asilimia 10 kwenye halmashauri, watu wakope na kujiendeleza badala ya kulalamika," alisisitiza Kubebelwa.

Awali akisoma riskala ya kikundi hicho, Mjumbe wa Kikundi hicho, Rehema Manyama alieleza katika kipindi cha siku 100, Rais ameonyesha dira kwa kufanikisha utoaji wa Bima ya Afya kwa wote, kuzalisha ajira kwa vijana ikiwemo kutoa mikopo.

Aidha alitoa ushauri wake kwa ngazi za mikoa ziendelee kutoa elimu ya uzalendo na kuimarisha elimu ya amali ili vijana wajiajiri na kuingiza kipato

 

Naye Mjumbe Zuberi Gogo, alibainisha kuwa ingawa hitilafu ndogo ndogo haziwezi kukosekana, changamoto kubwa inatokana na baadhi ya watendaji wanaopindisha taratibu na kuigombanisha Serikali na wananchi. Alitoa wito kwa wananchi kuelewa taratibu za kiserikali ili wasipotezwe na upotoshaji.

Akizungumzia suala la mikopo, Mjumbe Zainabu Salim Ugata, alifafanua kuwa mikopo ya asilimia 10 inayotolewa na halmashauri haina upendeleo, bali inatolewa kwa vikundi vilivyofuata taratibu zote zilizowekwa. Alisema kikundi hicho kitaendelea kuzunguka mikoa yote nchini kutoa elimu kwa umma ili kuongeza uelewa wa mambo ya Serikali.





Washiriki wa mkutano huo waliazimia kuwa ni wajibu wa kila mzalendo kuilinda taswira ya nchi na kuhakikisha kuwa fursa za kiuchumi zinazotolewa na Rais zinawafikia walengwa bila vikwazo.



LUHAGA MPINA ALIVYOSHIRIKI MAZISHI YA MWADHAMA KARDINALI PENGO

March 01, 2026 Add Comment

Waziri Mkuu Mstaafu, Majaliwa Kassim Majaliwa akisalimiana na Aliyekuwa mgombea wa Urais wa Tanzania kupitia ACT Wazalendo mwaka 2025, Luhaga Joelson Mpina (baadae alienguliwa na Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi )  walipokutana katika mazishi ya Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo katika Kituo cha Hija Pugu jijini Dar Es Salaam tarehe 28 Februari 2026
 Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Yuda Thadei Ruwaichi akisalimiana na 
Aliyekuwa mgombea wa Urais wa Tanzania kupitia ACT Wazalendo mwaka 2025(baadae alienguliwa na Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi), Luhaga Joelson Mpina walipokutana katika mazishi ya Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo katika Kituo cha Hija Pugu jijini Dar Es Salaam tarehe 28 Februari 2026
 Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Mwanza, Mhashamu Renatus Nkwande akisalimiana na 
Aliyekuwa mgombea wa Urais wa Tanzania kupitia ACT Wazalendo mwaka 2025,(baadae alienguliwa na Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi Luhaga Joelson Mpina walipokutana katika mazishi ya Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo katika Kituo cha Hija Pugu jijini Dar Es Salaam tarehe 28 Februari 2026

Aliyekuwa mgombea wa Urais wa Tanzania kupitia ACT Wazalendo,(baadae alienguliwa na Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi) Luhaga Joelson Mpina pamoja na Maaskofu Katoliki katika mazishi Mwadhama Askofu Mstaafu Polycarp Kardinali Pengo katika Kituo cha Hija Pugu jijini Dar Es Salaam tarehe 28 Februari 2026
Aliyekuwa mgombea wa Urais wa Tanzania kupitia ACT Wazalendo mwaka 2025 (baadae alienguliwa na Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi), Luhaga Joelson Mpina pamoja na Mwenyekiti wa Zamani wa Chama cha NCCR Mageuzi, James Mbatia  katika mazishi ya Askofu Mkuu  Mstaafu Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo katika Kituo cha Hija Pugu jijini Dar Es Salaam tarehe 28 Februari 2026
Aliyekuwa mgombea wa Urais wa Tanzania kupitia ACT Wazalendo mwaka 2025 (baadae alienguliwa na Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi), Luhaga Joelson Mpina akisalimiana na Waziri Msaafu wa Ardhi, Nyumba na Makazi, Profesa Anna Kajumulo Tibaijuka mara baada Adhimisho la Misa Takatifu ya Kumuombea Askofu Mkuu Mstaafu wa Jimbo Kuu Katoliki Dar es Salaam, Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Yosefu jijini Dar Es Salaam tarehe 27 Februari 2026

Aliyekuwa mgombea wa Urais wa Tanzania kupitia ACT Wazalendo mwaka 2025 (baadae alienguliwa na Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi), Luhaga Joelson Mpina akisalimiana na Mwenyekiti wa Baraza la Wazee  wa CHADEMA, Suzan Lyimo mara baada Adhimisho la Misa Takatifu ya Kumuombea Askofu Mkuu Mstaafu wa Jimbo Kuu Katoliki Dar es Salaam, Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Yosefu jijini Dar Es Salaam tarehe 27 Februari 2026

Aliyekuwa mgombea wa Urais wa Tanzania kupitia ACT Wazalendo mwaka 2025 (baadae alienguliwa na Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi), Luhaga Joelson Mpina akisaini kitabu cha Maombolezo kufuatia Kifo cha Askofu Mkuu Mstaafu wa Jimbo Kuu Katoliki Dar es Salaam, Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Yosefu jijini Dar Es Salaam tarehe 27 Februari 2026



RAIS SAMIA AWASILI KILIMANJARO AKIELEKEA MKOANI ARUSHA KWA ZIARA YA KIKAZI

March 01, 2026 Add Comment


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Mhe. Nurdin Babu pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. CPA. Amos Makalla na viongozi mbalimbali mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA) kwa ajili ya Ziara ya kikazi mkoani Arusha, tarehe 01 Machi, 2026.



JK AKABIDHI TUZO KWA VIONGOZI BORA BARANI AFRIKA

JK AKABIDHI TUZO KWA VIONGOZI BORA BARANI AFRIKA

March 01, 2026 Add Comment




Mwanasheria Mkuu na Waziri wa Katiba wa Ghana Dominic Akuritinga Ayine akipokea Tuzo kwa niaba ya Rais John Mahama wa Ghana

Kanali Chris Magezi, Msemaji wa Jeshi la Wananchi la Uganda akipokea Tuzo kwa niaba ya Mkuu wa Majeshi wa Uganda, Jenerali Muhoozi Kainerugaba

Rais Mstaafu Dkt. Jakaya Kikwete akikabidhi Tuzo kwa Waziri Mkuu wa Lesotho, Samuel Matekane

Rais Mstaafu Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akihutubia wakati wa Hafla hiyo ya kukabidhi Tuzo kwa Viongozi Bora wa Mwaka wa Afrika kwa Mwaka 2026

Rais Mstaafu Dkt. Jakaya Kikwete akisalimiana na mwigizaji maarufu Moses Nyarko aliyeshiriki katika Hafla hiyo ya utoaji wa Tuzo kwa Viongozi Bora barani Afrika kwa Mwaka 2026

……………

Rais Mstaafu Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete amekabidhi Tuzo za Viongozi Bora barani Afrika kwa Mwaka 2026 katika Hafla iliyofanyika Accra, Ghana tarehe 28 Februari 2026.

Tuzo hizo zinatolewa na Jarida la Africa Leadership Magazine linaloandaliwa na Taasisi ya Uongozi Afrika (Africa Leadership Organisation) ambayo Rais Mstaafu Dkt. Kikwete ni Mwenyekiti wa Bodi yake ya Ushauri.

Mshindi wa Jumla wa Tuzo hizo ni Rais John Dramani Mahama wa Ghana, ambaye ametunukiwa Tuzo ya Mwafrika wa Mwaka kwa Mwaka 2026 kwa kutambua mchango wake katika kukuza demokrasia na uchumi nchini Ghana pamoja na kuwa kinara katika kuimarisha utengamano wa kikanda kupitia Eneo Huru la Biashara Afrika (AfCFTA).

Akihutubia kabla ya kukabidhi Tuzo hiyo ya mshindi wa jumla, Rais Mstaafu Dkt. Kikwete ameeleza kuwa “kila kizazi za uongozi hukutana na changamoto za kipekee za wakati wake na hivyo hulazimika kubuni njia za kipekee za kuzitatua”. Akaongeza kuwa “kipimo mojawapo cha mafanikio katika uongozi ni kuweza kukuza kipato cha mtu mmoja mmoja na kuboresha hali ya jumla ya kimaisha kwa watu unaowaongoza kutoka hali ya chini kwenda hali ya juu zaidi”.

Mbali na Rais Mahama, miongoni mwa watu mashuhuri waliiopata Tuzo hizo ni pamoja na Waziri Mkuu wa Ufalme wa Lesotho, Samuel Matekane aliyepata tuzo kwa kutambua mchango wake katika kuimarisha ushirikiano kati ya Serikali na Sekta Binafsi nchini Lesotho pamoja na Mkuu wa Majeshi wa Uganda, Jenerali Muhoozi Kainerugaba aliyepata tuzo kwa kutambua mchango wake katika kuliimarisha jeshi la Uganda na kukuza diplomasia ya kijeshi katika ukanda wa maziwa makuu.

Rais wa Namibia Netumbo Nandi-Ndaitwah alipata Tuzo ya Kiongozi Bora wa Kisiasa Afrika huku Makamu wa Rais wa Angola Esperança da Costa, Makamu wa Rais wa Angola akioata Tuzo ya Kiongozi Bora Mwanamke barani Afrika.

Tuzo ya Rais Mahama ilipokelewa kwa niaba yake na Mwanasheria Mkuu wa Ghana, ambaye pia ni Waziri wa Sheria wa Ghana, Dominic Akuritinga Ayine wakati tuzo ya Jenerali Kainerugaba ilipokelewa na Msemaji wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Uganda, Kanali Chris Magezi.

Kila mwaka Jarida la Africa Leadership Magazine huratibu mchakato wa wazi unaojumuisha kupokea mapendekezo ya viongozi mbalimbali wenye sifa ambao hupigiwa kura kwa njia ya mtandao ili kupata washindi. Viongozi wa tasnia mbalimbali zikiwemo uongozi wa kisiasa, diplomasia, biashara na uwekezaji, ujasiriamali, habari, ulinzi na usalama, nk., wanaoshinda hupokea Tuzo hizo kwa kutambua mchango wao katika kusimamia vizuri tasnia zao pamoja na kulea na kuwaandaa vijana wanaowaongoza ili kuja kuwa viongozi bora wa baadaye.

Katika hafla hiyo, jumla ya Tuzo 36 zilitolewa.

BARRICK YAENDELEZA MKAKATI WAKE WA KUJENGA KIZAZI KIPYA CHA WATAALAMU WA SEKTA YA MADINI NCHINI

March 01, 2026 Add Comment

 

Mkufunzi kutoka Kampuni ya Barrick Dkt. Yann Mpaka akiwa kwenye mafunzo hayo ya weledi kwa wanafunzi wa Shule ya Madini ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM)
Mkufunzi wa kampuni ya Barrick, Dkt. Yann Mpaka akifundisha nadharia na vitendo mbalimbali ya jinsi ya kusoma ramani ya miamba kwenye mafunzo ya siku ya pili yaliyoratibiwa na Barrick kwa kushirikina na Shule ya Madini na Jiolojia (School of Mining and Geoscience) ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.
Mkufunzi kutoka Kampuni ya Barrick Dkt. Yann Mpaka akiwa kwenye mafunzo hayo ya weledi kwa wanafunzi wa Shule ya Madini ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM)
Mkuu wa Idara ya Shule ya Madini na Jiolojia (School of Mining and Geoscience SOMG), Dkt. Emmanuel Kazimoto (wa pili kulia) akifungua mafunzo hayo ya siku ya pili ya kuwajengea uwezo wa wanafunzi wa mwaka wa nne wa chuo hicho kuhusu masuala ya madini na Jiolojia
Mtaalamu kutoka Barrick, Ibrahim Kamage ambaye alihitimu katika shule hiyo mwaka 2023 akitoa mada kwenye mafunzo hayo yaliyofadhiliwa na kampuni ya Barrick nchini
Mtaalamu kutoka Barrick , Ibrahim Kamage ambaye alihitimu katika shule hiyo mwaka 2023 akitoa mada kwenye mafunzo hayo yaliyofadhiliwa na kampuni ya Barrick nchini
Baadhi ya wanafunzi wa mwaka wa nne wa Shule ya Madini na Sayansi ya Jiolojia (School of Mining and Geoscience) ya Chuo kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) wakifuatilia mafunzo kwenye semina hiyo ya kitaaluma iliyokuwa ikitolewa na watalaamu kutoka Kampuni ya Barrick nchini.
Sehemu ya wanafunzi wa mwaka wa nne wakifuatilia mafunzo hayo ya mambo ya madini na Jiolojia na hasa teknolojia inavyotumika kwenye migodi duniani , mafunzo hayo yalifadhiliwa na kampuni ya Barrick hapa nchini.
Baadhi ya wanafunzi waliohudhuria masomo katika picha ya pamoja na wakufunzi.
**



#Yaja na programu ya kuwajengea uwezo wanafunzi wa sekta ya madini UDSM

Kampuni ya Barrick nchini inaendelea kufanikisha dhamira yake ya kujenga kizazi kipya cha wataalamu wenye maarifa ya kisasa katika sekta ya madini kupitia Programu ya kuwapatia mafunzo wanafunzi wanaosoma shahada ya kwanza ya fani ya madini na jiolojia katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kwa kutumia wataalamu wabobezi na wenye uzoefu kutoka ndani ya kampuni.

Kupitia programu hiyo kwa kushirikiana na Shule ya Madini na Jiolojia (SOMG) ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ,wataalamu kutoka Barrick wameendesha ya mafunzo ya kuwajengea uwezo katika tasnia ya madini na jiolojia wanafunzi wa mwaka wa mwisho kwenye shule ya madini.

Akizungumzia kuhusu mafunzo kupitia programu hii Mkuu wa Shule hiyo Profesa Elisante Mshiu, amesema yatakuwa ni endelevu kwa kubadilishana uzoefu na wataalamu katika tasnia kutoka Barrick kwa nia ya kuwapatia wanafunzi ujuzi , uelewa wa ndani na jinsi ya kukabiliana na changamoto katika sehemu za uchimbaji na utafiti wa madini kwenye miamba na chini ya ardhi.

Amesema progamu imelenga pia kuwaunganisha wanafunzi na wadau wakubwa katika tasnia ya madini kutoka sekta binafsi ili kuwajengea uwezo na kujiamini ili wanapomaliza masomo yao waweze kuhimili ushindani katika soko la ajira nchini na nje ya nchi na wengine kuweza kujiajiri kupitia taaluma walizosomea.

“Mafunzo haya zaidi yanawapa mwangaza wa aina ya kazi wanazotarajia kukutana nazo pindi wanapomaliza masomo yao , kujua ni kwa jinsi ya kufanya utafiti wa kujua kiasi cha madini kilichopo chini ya ardhi, miamba , namna bora ya kusoma ramani na kuwa na matarajio ya kitafiti na kisayansi zaidi kwenye fani ya Jiolojia,” ameongeza Profesa Mshiu.

Kwa upande wake , Mkuu wa Idara wa Shule hiyo ya Madini (SOMG) , Dkt Emmanuel Kazimoto amesema mafunzo hayo yanayoendeshwa kwa ufadhili wa kampuni ya Barrick ni fursa ya kipekee kwa wanafunzi wa mwaka wa nne katika shule hiyo katika kupanua uelewa wao kuhusu masuala ya madini , joto la ardhi na elimu ya miamba pamoja na matumizi ya teknolojia kwenye kufanya tafiti za madini chini ya ardhi.

Dkt. Kazimoto amesisitiza kuwa programu itaendelea kufungua milango zaidi wa wanafunzi wa chuo hapo kupenda zaidi masomo ya madini na Jiolojia kwa sababu ya kufundishwa na wadau ambapo wanatoka kweye makampuni makubwa ya uchimbaji madini hapa nchini kama vile Barrick.

“Muhimu ni kwamba wameshawaona wenzao ambapo wamepata kazi Barrick na wengine wamepata kazi nje ya nchini kwa hiyo ni muhimu waendelee kujifunza kwa vitendo zaidi jinsi ya kusoma ramani , ugunduzi wa kiasi ya hifadhi ya madini ambacho kipo chini ya ardhi , jinsi ya kupima joto chini ya ardhi na mambo mengine ya kitaalamu zaidi,” ameongeza Dkt. Kazimoto.

Amesema kwamba ni muhimu kuendelea kupanua wigo wa ushirikiano kati yao na wadau wa madini kama vile Barrick katika juhudi za kuifanya sekta hii ya madini si tu kwa ajili ya mapato ya nchini lakini pia kupanua mianya ya uelewa wa masomo haya kwa wanafunzi kutoka kizazi hadi kikazi kwa maslahi mapana ya nchini.

Mkufunzi wa mafunzo hayo, Dkt. Yann Waku Mpaka , Mjiolojia kutoka kampuni ya Barrick amesema umuhimu wa mafunzo yanayotolewa kupitia programu hii ni jinsi ya kubadilishana na kupeana uelewa , taarifa , ujuzi na uzoefu wa uchimbaji , utafutaji na utafiti kwenye sekta ya madini.

Dkt. Mpaka ameongeza kwamba kuna umuhimu wa kuwajengea uwezo wanafunzi kwenye maeneo ya utafiti , usomaji wa ramani za miamba na jinsi ya kujua joto la ardhi na namna bora ya kufanya shughuli za uchimbaji na utafutaji wa madini kwa njia ya kitaalam zaidi ambayo ni salama pia,na masuala mbalimbali yanayohusiana na tasnia ya madini.

Amesema kuna umuhimu wa kuendelea kuweka mkazo kwenye sayansi na teknolojia nadharia ya uchimbaji na tafiti za madini duniani zimebadilika, uwekezaji mkubwa kwenye vifaa na teknolojia vinawalazimu vijana kwenye sekta hii kujua hasa teknolojia ya kisasa kwenye tafiti na uchimbaji wa madini.

Ibrahim Kamage ambaye ni mtalaamu kutoka Barrick na ni mhitimu wa shule hiyo ya chuo kikuu ya Madini na Jiolojia mwaka 2023 alisema kwamba ni muhimu kwa wanafunzi hao kukuza uelewa wao wa mawasiliano na mahusiano kwa jamii.

“Katika fani Jiolojia ni muhimu kwa mtaalamu kujifunza jinsi ya kuwasiliana na watu mbalimbali kuanzia mafundi hadi wanakijiji kwenye maeneo ya uchimbaji ili kupunguza migogoro kwenye jamii na kuondoa dhana potofu kwamba sehemu za migodi ina migogoro na wananchi wanaozunguka migodi hiyo,” ameongeza Kamage.

Akizungumza kwa niaba ya wenzake , Paul Maghembe ambaye naye ni mwanafunzi wa mwaka wa nne chuoni alisema kwamba mafunzo hayo yamewajengea uwezo wa jinsi ya kusoma ramani za miamba , matumizi ya teknolojia na ukusanyaji wa data (takwimu) kwenye shughuli za utafutaji na uchimbaji wa madini.

Sarah Nestory Musembele ambaye anachukua shahada ya sayansi ya Jiolojia chuoni hapo alisema kwamba ni ndoto zake kwamba anataka kuwa na weledi na kuzingatia maadili ya kazi ya Jiolojia na kuleta mabadiliko kwenye sekta hiyo hapa nchini.

BARRICK YAENDELEZA MKAKATI WAKE WA KUJENGA KIZAZI KIPYA CHA WATAALAMU WA SEKTA YA MADINI NCHINI

March 01, 2026 Add Comment
Mkuu wa Idara ya Shule ya Madini na Jiolojia (School of Mining and Geoscience SOMG), Dkt. Emmanuel Kazimoto (wa pili kulia) akifungua mafunzo hayo ya siku ya pili ya kuwajengea uwezo wa wanafunzi wa mwaka wa nne wa chuo hicho kuhusu masuala ya madini na Jiolojia
Mkufunzi kutoka Kampuni ya Barrick Dkt. Yann Mpaka akiwa kwenye mafunzo hayo ya weledi kwa wanafunzi wa Shule ya Madini ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM)
Mkufunzi wa kampuni ya Barrick, Dkt. Yann Mpaka akifundisha nadharia na vitendo mbalimbali ya jinsi ya kusoma ramani ya miamba kwenye mafunzo ya siku ya pili yaliyoratibiwa na Barrick kwa kushirikina na Shule ya Madini na Jiolojia (School of Mining and Geoscience) ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.
Mkufunzi kutoka Kampuni ya Barrick Dkt. Yann Mpaka akiwa kwenye mafunzo hayo ya weledi kwa wanafunzi wa Shule ya Madini ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM)

Mtaalamu kutoka Barrick, Ibrahim Kamage ambaye alihitimu katika shule hiyo mwaka 2023 akitoa mada kwenye mafunzo hayo yaliyofadhiliwa na kampuni ya Barrick nchini
Mtaalamu kutoka Barrick , Ibrahim Kamage ambaye alihitimu katika shule hiyo mwaka 2023 akitoa mada kwenye mafunzo hayo yaliyofadhiliwa na kampuni ya Barrick nchini
Baadhi ya wanafunzi wa mwaka wa nne wa Shule ya Madini na Sayansi ya Jiolojia (School of Mining and Geoscience) ya Chuo kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) wakifuatilia mafunzo kwenye semina hiyo ya kitaaluma iliyokuwa ikitolewa na watalaamu kutoka Kampuni ya Barrick nchini.
Sehemu ya wanafunzi wa mwaka wa nne wakifuatilia mafunzo hayo ya mambo ya madini na Jiolojia na hasa teknolojia inavyotumika kwenye migodi duniani , mafunzo hayo yalifadhiliwa na kampuni ya Barrick hapa nchini.
Baadhi ya wanafunzi waliohudhuria masomo katika picha ya pamoja na wakufunzi.
**



#Yaja na programu ya kuwajengea uwezo wanafunzi wa sekta ya madini UDSM

Kampuni ya Barrick nchini inaendelea kufanikisha dhamira yake ya kujenga kizazi kipya cha wataalamu wenye maarifa ya kisasa katika sekta ya madini kupitia Programu ya kuwapatia mafunzo wanafunzi wanaosoma shahada ya kwanza ya fani ya madini na jiolojia katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kwa kutumia wataalamu wabobezi na wenye uzoefu kutoka ndani ya kampuni.

Kupitia programu hiyo kwa kushirikiana na Shule ya Madini na Jiolojia (SOMG) ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ,wataalamu kutoka Barrick wameendesha ya mafunzo ya kuwajengea uwezo katika tasnia ya madini na jiolojia wanafunzi wa mwaka wa mwisho kwenye shule ya madini.

Akizungumzia kuhusu mafunzo kupitia programu hii Mkuu wa Shule hiyo Profesa Elisante Mshiu, amesema yatakuwa ni endelevu kwa kubadilishana uzoefu na wataalamu katika tasnia kutoka Barrick kwa nia ya kuwapatia wanafunzi ujuzi , uelewa wa ndani na jinsi ya kukabiliana na changamoto katika sehemu za uchimbaji na utafiti wa madini kwenye miamba na chini ya ardhi.

Amesema progamu imelenga pia kuwaunganisha wanafunzi na wadau wakubwa katika tasnia ya madini kutoka sekta binafsi ili kuwajengea uwezo na kujiamini ili wanapomaliza masomo yao waweze kuhimili ushindani katika soko la ajira nchini na nje ya nchi na wengine kuweza kujiajiri kupitia taaluma walizosomea.

“Mafunzo haya zaidi yanawapa mwangaza wa aina ya kazi wanazotarajia kukutana nazo pindi wanapomaliza masomo yao , kujua ni kwa jinsi ya kufanya utafiti wa kujua kiasi cha madini kilichopo chini ya ardhi, miamba , namna bora ya kusoma ramani na kuwa na matarajio ya kitafiti na kisayansi zaidi kwenye fani ya Jiolojia,” ameongeza Profesa Mshiu.

Kwa upande wake , Mkuu wa Idara wa Shule hiyo ya Madini (SOMG) , Dkt Emmanuel Kazimoto amesema mafunzo hayo yanayoendeshwa kwa ufadhili wa kampuni ya Barrick ni fursa ya kipekee kwa wanafunzi wa mwaka wa nne katika shule hiyo katika kupanua uelewa wao kuhusu masuala ya madini , joto la ardhi na elimu ya miamba pamoja na matumizi ya teknolojia kwenye kufanya tafiti za madini chini ya ardhi.

Dkt. Kazimoto amesisitiza kuwa programu itaendelea kufungua milango zaidi wa wanafunzi wa chuo hapo kupenda zaidi masomo ya madini na Jiolojia kwa sababu ya kufundishwa na wadau ambapo wanatoka kweye makampuni makubwa ya uchimbaji madini hapa nchini kama vile Barrick.

“Muhimu ni kwamba wameshawaona wenzao ambapo wamepata kazi Barrick na wengine wamepata kazi nje ya nchini kwa hiyo ni muhimu waendelee kujifunza kwa vitendo zaidi jinsi ya kusoma ramani , ugunduzi wa kiasi ya hifadhi ya madini ambacho kipo chini ya ardhi , jinsi ya kupima joto chini ya ardhi na mambo mengine ya kitaalamu zaidi,” ameongeza Dkt. Kazimoto.

Amesema kwamba ni muhimu kuendelea kupanua wigo wa ushirikiano kati yao na wadau wa madini kama vile Barrick katika juhudi za kuifanya sekta hii ya madini si tu kwa ajili ya mapato ya nchini lakini pia kupanua mianya ya uelewa wa masomo haya kwa wanafunzi kutoka kizazi hadi kikazi kwa maslahi mapana ya nchini.

Mkufunzi wa mafunzo hayo, Dkt. Yann Waku Mpaka , Mjiolojia kutoka kampuni ya Barrick amesema umuhimu wa mafunzo yanayotolewa kupitia programu hii ni jinsi ya kubadilishana na kupeana uelewa , taarifa , ujuzi na uzoefu wa uchimbaji , utafutaji na utafiti kwenye sekta ya madini.

Dkt. Mpaka ameongeza kwamba kuna umuhimu wa kuwajengea uwezo wanafunzi kwenye maeneo ya utafiti , usomaji wa ramani za miamba na jinsi ya kujua joto la ardhi na namna bora ya kufanya shughuli za uchimbaji na utafutaji wa madini kwa njia ya kitaalam zaidi ambayo ni salama pia,na masuala mbalimbali yanayohusiana na tasnia ya madini.

Amesema kuna umuhimu wa kuendelea kuweka mkazo kwenye sayansi na teknolojia nadharia ya uchimbaji na tafiti za madini duniani zimebadilika, uwekezaji mkubwa kwenye vifaa na teknolojia vinawalazimu vijana kwenye sekta hii kujua hasa teknolojia ya kisasa kwenye tafiti na uchimbaji wa madini.

Ibrahim Kamage ambaye ni mtalaamu kutoka Barrick na ni mhitimu wa shule hiyo ya chuo kikuu ya Madini na Jiolojia mwaka 2023 alisema kwamba ni muhimu kwa wanafunzi hao kukuza uelewa wao wa mawasiliano na mahusiano kwa jamii.

“Katika fani Jiolojia ni muhimu kwa mtaalamu kujifunza jinsi ya kuwasiliana na watu mbalimbali kuanzia mafundi hadi wanakijiji kwenye maeneo ya uchimbaji ili kupunguza migogoro kwenye jamii na kuondoa dhana potofu kwamba sehemu za migodi ina migogoro na wananchi wanaozunguka migodi hiyo,” ameongeza Kamage.

Akizungumza kwa niaba ya wenzake , Paul Maghembe ambaye naye ni mwanafunzi wa mwaka wa nne chuoni alisema kwamba mafunzo hayo yamewajengea uwezo wa jinsi ya kusoma ramani za miamba , matumizi ya teknolojia na ukusanyaji wa data (takwimu) kwenye shughuli za utafutaji na uchimbaji wa madini.

Sarah Nestory Musembele ambaye anachukua shahada ya sayansi ya Jiolojia chuoni hapo alisema kwamba ni ndoto zake kwamba anataka kuwa na weledi na kuzingatia maadili ya kazi ya Jiolojia na kuleta mabadiliko kwenye sekta hiyo hapa nchini.