HABARI

SIASA

ELIMU

Recent Posts

WAZIRI MKUU MSTAAFU JOHN MALECELA TULINDE AMANI YETU KUKUZA SEKTA YA UTALII

April 11, 2026 Add Comment

 


SAME. 

MAKAMU wa Rais na Waziri Mkuu mstaafu, John Samuel Malecela amesema kuwa, swala la Utalii kokote Duniani linaenda sambamba na swala la Amani na Utulivu na kuwaomba wananchi kuhakikisha wanalinda Amani ili kukuza Utalii nchi na kuendelea kujinufaisha kupitia sekta hiyo. 

Malecela alitoa kauli hiyo jana wakati wa Uzinduzi wa tamasha la Same Utalii festival lililofanyika katika viwanja vya stendi wilayani Same mkoani Kilimanjaro ambapo alisema kuwa, utalii ni kite ambacho huchangia kuleta fedha za kigeni. 

Alisema kuwa, baadhi ya nchi ulimwenguni serikali zinaendeshwa kwa fedha za Utalii na kuwataka kulichukulia swala hilo kwa umakini mkubwa. 

Kiongozi huyo alidai kuwa, misingi ya Utalii ni ukarimu kwa wageni na kuwataka wananchi wa wilaya ya Same kuwa mfano katika ukarimu ili kukuza Utalii wa wilaya ya Same. 

"Hata sehemu kukiwa na njiwa 10,000  wamejaa lakini jiwe likigonga tu wote wanakimbia kwa hiyo na sisi utalii wetu uanze na sisi wenyewe Watanzania kuwa na Amani ni jambo la msingi sana kwani Amani ndio italeta na kuwakaribisha watalii na ndio itatufanya tuendelee kukua kiuchumi" Alisema Malecela. 

Na kuongeza "Swala la ukarimu kwa wageni ni kitu muhimu sana mahali pengine watu hawaendi kwa sababu hakuna moyo wa kuwapokea wageni lakini kwetu same tuwe na moyo wa kuwapokea wageni ili kukuza utalii wetu".

Alisema kuwa, kinachotuunga pamoja ni Amani na kuwasihi Watanzania kuendelea kuitunga na mambo mengine yatafuata. 

"Ili Utalii wa same uweze kukua ni lazima uanze na sisi wenyewe wanasama kuwa na moyo dhabiti wa ukarimu ili wanapokuja na kurudi wakatoe sifa ni kweli wataenda kuona wanyama lakini mkiwakaribisha kwa moyo upande hawatarudi tena" Alisema Malecela.






KIKWETE STEPS IN: AU ENVOY OFF TO A PROMISING START IN SOUTH SUDAN PEACE EFFORT

April 11, 2026 Add Comment

 

 Former Tanzanian President Dr. Jakaya Mrisho Kikwete, now serving as High Representative of the African Union Chairperson to the Horn of Africa and the Red Sea, on Friday met with President Salva Kiir Mayardit of South Sudan in Juba as he wrapped up a high-level two-day mission to the country engaging key national, regional and international actors in efforts to restabilize the country. He also met with other key Ministers to assess progress and challenges in implementing the Revitalized Agreement on the Resolution of Conflict in South Sudan (R-ARCSS) signed in 2018.



Special Reporter, JUBA, South Sudan

 

In a significant diplomatic push to revive momentum in South Sudan’s fragile peace process, former Tanzanian President Jakaya Mrisho Kikwete has wrapped up a high-level two-day mission to Juba, engaging key national, regional and international actors in efforts to restabilize the country.

 

Kikwete, now serving as High Representative of the African Union Chairperson to the Horn of Africa and the Red Sea, met with President Salva Kiir Mayardit and other key Ministers to assess progress and challenges in implementing the Revitalized Agreement on the Resolution of Conflict in South Sudan (R-ARCSS) signed in 2018.

 

At the State House, President Kiir reassured the envoy that the peace agreement remains on track, dismissing claims of its collapse. He outlined ongoing efforts by the Revitalised Government of the National Unity (RTGoNU) to encourage and advance inclusive dialogue among various parties, both signatories and non-signatories to the R-ARCSS in order to reach consensus on critical issues leading up to the elections scheduled for December 2026, as declared in the communique by the African union High Level Ad Hoc Committee for South Sudan (C5) Plus Summit held in the margins of the 39th Ordinary AU Summit Addis Ababa, Ethiopia in February 2026.

 

The government also used the occasion to express gratitude for continued African Union support while calling on the international community to allow space for homegrown solutions to take root.

 

In a statement issued by the State House in Juba following the meeting betwee President Kiir and the experienced Envoy, a key takeaway highlighted was the commitment by the Govermnent to proceed with the election process so that to not only avoid yet another extension to the December deadline, but also to heed the desire by the Sudanese people to finally go to the ballot for the first time since the country attained its independence in 2011.

 

Going beyond the government corridors, Kikwete’s visit also provided a valuable platform to voices from across the South Sudanese political spectrum. He held consultations with leaders of the ruling Sudan People's Liberation Movement (SPLM - IG), opposition parties including representatives of the Sudan People's Liberation Movement - in Opposition (SPLM - IO), and the South Sudan Opposition Alliance (SSOA) - which is an umbrella for various smaller political parties in the country. He also met with members from the civil society, faith-based organizations, and the academia - underscoring the inclusive approach employed by the envoy and which is commended by many as what was missing to ensure all voices are heard and no one is left behind in the process of rebuilding the conflict ridden youngest country in the continent.

 

In a voice note recorded and widely circulated by Edmund Yakani, Executive Director of Community Empowerment for Progress Organization (CEPO), the South Sudanese civil society activist and human rights advocate applauded the appointment of Former President Kikwete to the role as the envoy and urged him to work with all parties to ensure inclusive political dialogue, including bringing on board those with contentious positions who are inside and outside of South Sudan.

 

“Our people have paid a very expensive price through loss of life and property. We are confident of the Envoy through his experience in mediation and his knowledge of the South Sudanese issues. We hope that he will take up this responsibility wholeheartedly, embrace everyone and bring everyone to the table so that to nurture a pathway to transition and to sustainable peace” he said. He added that “ if some people and some parties are isolated, that will mark the beginning of yet another failure of the implementation of the resolution of the AU C5 Summit to empower the South Sudanese people to resolve their differences amicably”

 

Underscoring the desire of the international community and regional bodies to see peace and stability in South Sudan, the envoy also met with key international and regional stakeholders, including the Intergovernmental Authority on Development (IGAD), the United Nations Mission in South Sudan (UNMISS), and the Reconstituted Joint Monitoring and Evaluation Commission (RJMEC), as well as Ambassadors from of the European Union, Canada, Germany and the Troika countries of the United States of America,  United Kingdom and Norway.

 

The envoy also met with Vice President Rebecca Nyandeng De Mabior Garang, a prominent leader in the transitional government and a symbol of national unity who is a widow of Dr. John Garang De Mabior, the founder of the Sudan People’s Liberation Army (SPLA) and considered as Father of the South Sudanese Nation.

 

Kikwete’s return to the South Sudan peace file carries historical weight. In 2015, he played a pivotal role in brokering intra-party dialogue among various faction in the SPLM Party that led to the Arusha Peace Agreement - a foundation for subsequent peace efforts. His visit to Juba is preceded by visits to the President Cyril Ramaphosa of South Africa and President Yoweri Kaguta Museveni who are key guarantors to the peace process.

 

As South Sudan edges toward a critical electoral milestone, Kikwete’s mission signals renewed continental commitment to steering the young nation away from instability and toward a more durable peace.

NYASI BANDIA SULUHISHO LA KUDUMU UWANJA WA CCM MKWAKWANI

April 11, 2026 Add Comment



Na Oscar Assenga, Tanga

Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Tanga kimeeleza kuwa suluhisho la kudumu la kuboresha eneo la kuchezea katika Uwanja wa CCM Mkwakwani ni uwekaji wa nyasi bandia, huku wakipanga kushirikiana na wadau wa soka kufanikisha mpango huo.

Akizungumza wakati wa ziara ya kukagua uwanja huo, Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Tanga, Rajab Abdurahman, alisema uwekaji wa nyasi bandia unakadiriwa kugharimu kati ya shilingi milioni 400 hadi 500.

Ziara hiyo ni sehemu ya ukaguzi wa miradi mbalimbali ya maendeleo mkoani humo, ikiwemo ile inayotekelezwa kwa fedha zinazotolewa na Serikali chini ya uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa lengo la kupunguza kero kwa wananchi.

Abdurahman aliwataka viongozi wa CCM, ambao ni wamiliki wa uwanja huo, kutumia ubunifu na kushirikiana na wadau wa soka ili kuhakikisha wanapata fedha za kuweka nyasi bandia.

“Tutawaomba wadau wa soka nchini watakapohitajika kutusaidia, kwani dhamira yetu ni njema. Kama ambavyo wamekuwa wakitusaidia hapo awali, tunaamini watashiriki nasi kuhakikisha tunakuwa na uwanja wa kisasa zaidi,” alisema.

Alieleza kuwa maboresho ya uwanja huo yatasaidia kuinua uchumi wa Mkoa wa Tanga, kwani utaweza kutumika kwa mashindano ya kitaifa na kimataifa, ikiwemo CECAFA na michuano mingine ya Afrika.

“Tunapokuwa na uwanja mzuri, hata timu za nje zitakuja kucheza hapa Tanga. Hii itaongeza mzunguko wa fedha na kukuza uchumi wa mkoa wetu,” aliongeza.

Aidha, alikumbusha kuwa uwanja huo uliwahi kufungiwa kutokana na kutokidhi vigezo, hasa ubora wa eneo la kuchezea, akisisitiza kuwa hatua zinazochukuliwa sasa zinalenga kuhakikisha viwango vinazingatiwa kwa usalama wa wachezaji na ubora wa mchezo.

“Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) linapofungia uwanja si kwa kupenda, bali kuhakikisha viwango vinazingatiwa. Ndiyo maana tumekuwa wepesi kuchukua hatua za maboresho,” alisema.

Katika hatua nyingine, Abdurahman alieleza kuridhishwa na maendeleo ya ufungaji wa viti 6,500 vilivyotolewa na TFF chini ya Rais wake, Wallace Karia, licha ya kuwepo kwa ucheleweshaji mwanzoni.

Amesema tayari ameagiza kazi hiyo ikamilike ndani ya mwezi mmoja, na kwa sasa inaendelea vizuri chini ya usimamizi wa Mjumbe wa Kamati ya Siasa ya Mkoa, Nasoro Makau.

Kwa mujibu wa mpango huo, maeneo ya kipaumbele ni jukwaa kuu pamoja na sehemu za mashabiki wa klabu za Coastal Union na African Sports. Pia wameomba viti vingine 2,500 ili kukamilisha uwanja mzima.

Abdurahman aliishukuru Serikali kupitia Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, inayoongozwa na Waziri Paul Makonda na Naibu wake Hamisi Mwinjuma, pamoja na Rais wa TFF Wallace Karia, kwa ushirikiano wao katika kuboresha uwanja huo.

Alisisitiza kuwa maboresho hayo yanalenga kuhakikisha klabu za Coastal Union na African Sports zinaendelea kucheza mechi zao za nyumbani mkoani Tanga badala ya kuhamishiwa maeneo mengine.

Aidha, aliwataka mashabiki wa soka kujitokeza kwa wingi uwanjani kuunga mkono timu zao.

“Haileti maana kuwa na uwanja mzuri halafu mashabiki wanabaki nyumbani kuangalia mechi,” alisisitiza.

Kwa upande wake, Meneja wa Uwanja wa Mkwakwani, Nasoro Makau, alisema hadi sasa wamefikia asilimia 40 ya ufungaji wa viti na wana uhakika wa kukamilisha kazi hiyo ndani ya mwezi mmoja.

SAME UTALII FESTIVAL YACHANGIA KUONGEZA WATALII HIFADHI YA MKOMAZI..

April 11, 2026 Add Comment

 

TAMASHA la Utalii la Same festival linalofanyika kila mwaka wilayani Same mkoani Kilimanjaro limetajwa kuwa chanzo cha kuchochea idadi ya wageni wanaotembelea hifadhi ya Taifa ya Mkomazi.

Hayo yamebainishwa na Kaimu Mhifadhi wa hifadhi hiyo, Kamishna Emmanuel Sisiya katika uzinduzi wa tamasha hilo uliofanyika wilayani Same, ambapo alisema kuwa hapo nyuma wageni waliokuwa wakitembelea hifadhi hiyo walikuwa wachache.

Alisema kuwa, tamasha hilo limekuwa chachu na hamasa kubwa ya kutangaza hifadhi ya Taifa ya Mkomazi ambapo kabla ya kuanzishwa tamasha hilo idadi ya wageni waliokuwa wakitembelea hifadhi walikuwa wachache lakini kwa sasa wameongezeka ambapo kwa mwaka wa fedha uliopita walipokea wageni 7700 na katika wageni hao 4000 ni Watanzania.

"Wageni wengi wamechangiwa na hamasa kubwa inayofanywa kupitia tamasha hili la Same Utalii festival na kila anayekuja anakiri kuwa yeye ameifahamu Mkomazi kupitia matamasha mbalimbali ambayo yamekuwa yakifanyika kuitangaza Mkomazi hivyo nirudishe pongezi kwa Mkuu wa wilaya Kasilda Mgeni kwa kuanzisha tamasha hili " Alisema Kumishna Sisiya.

Aliongeza kuwa, kwa sasa hifadhi hiyo ina fursa ya uwekezaji ambapo yapo maeneo kwa wageni kuja kuwekeza maeneo ya malazi na hoteli kwani wageni wengi wanaofika Same hudai eneo la malazi hayatoshi.

Alisema kuwa, ndani ya hifadhi maeneo ya malazi yaliyopo hayatoshi hivyo sasa ni fursa kwa Watanzania kuwekeza ndani ya hifadhi hiyo.

"Hifadhi ya Mkomazi katika Kanda ya Kaskazini ni ya pili ambapo ukifika utaweza kuwaona wale wanyama wakubwa watano tofauti na hapo katika Kanda ya Kaskazini utaweza kuwaona Serengeti na Ngorongoro lakini kwa urahisi na kwa ukaribu ukitaka kumwona faru mweusi utamwona ndani ya hifadhi ya Mkomazi" alisema.






SHINYANGA YAJIPANGA KUPOKEA MAONESHO YA KITAIFA YA SIDO

April 11, 2026 Add Comment

Shirika la Maendeleo ya Viwanda Vidogo (SIDO) limetangaza kuwa Maonesho yake ya Tano ya Kitaifa yanatarajiwa kufanyika Oktoba 21 hadi 30, 2026 katika Uwanja wa Magufuli uliopo Manispaa ya Kahama, mkoani Shinyanga, yakilenga kuinua uchumi wa wajasiriamali wadogo nchini.

SERIKALI YAKUTANA NA MJUMBE MAALUM WA KATIBU MKUU WA JUMUIYA YA MADOLA

April 10, 2026 Add Comment

 

Na Mwandishi wetu

Ujumbe wa Serikali ya Tanzania ukiongozwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu, Mhe. Profesa Palamagamba Kabudi, umekutana na Mjumbe Maalum wa Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Madola na Rais wa zamani wa Malawi, Mhe. Dkt. Lazarus McCarthy Chakwera, na kujadiliana kuhusu namna Tanzania ilivyojidhatiti katika kudumisha umoja, amani na mshikamano miongoni mwa Watanzania.

FCC YATILIA MKAZO USHIRIKIANO KATIKA KUFIKIA MALENGO YA TAASISI

April 10, 2026 Add Comment
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Ushindani (FCC) Bi. Khadija Ngasongwa amewataka watumishi wa FCC kufanya kazi kwa ushirikiano, bidii, upendo pamoja na ubunifu katika utendaji ili kuboresha utoaji huduma kwa wananchi.

MWANAMKE CHUMA MAENDELEO GROUP YAWAKUMBUKA WAFUNGWA WANAWAKE GEREZA LA KAHAMA

April 10, 2026 Add Comment

Na Kadama Malunde - Kahama

Katika kuendeleza jitihada za kijamii na kuonesha mshikamano wa dhati kwa wanawake wenzao, Kikundi cha wanawake maarufu kinachojulikana kama Mwanamke Chuma Maendeleo Group kimetoa msaada wa vifaa mbalimbali kwa wafungwa wanawake katika Gereza la Kahama Mkoani Shinyanga, ikiwa ni sehemu ya maandalizi kuelekea kilele cha Tamasha la Mwanamke Chuma 2026 litakalofanyika Aprili 11, 2026 Mjini Kahama.

DORIS MOLEL UMESTAHILI TUZO YA WHO,UMEOKOA MAISHA YA WENGI

April 10, 2026 Add Comment

 



Na: Dk. Reubeni Lumbagala


Nakumbuka mwalimu wangu wa somo la Uraia (Civics) alipokuwa akitufundisha mada (topic) ya "Haki za "Binadamu" (Human Rights) tulipokuwa Kidato cha Kwanza, alituambia mengi kuhusu haki za binadamu. 


Miongoni mwa mikazo yake, alituambia hivi: Haki ya kuishi (Right to life) ndiyo haki kubwa kuliko zote maana mtu anapokuwa hai ndipo anakuwa na uwezo wa kupata haki nyingine zote. Nilimwelewa vizuri sana.


Kimsingi, uhai ni muhimu katika maisha ya mwanadamu, ndiyo maana inapotokea mtu ameugua, na akawa hana uwezo wa kumudu gharama za matibabu yake, basi familia, ndugu, jamaa na marafiki hushikamana kwa kuchangishana fedha kunusuru uhai wa ndugu yao huyo.


Watoto ni kundi ambalo lipo hatarini kukabiliwa na magonjwa mbalimbali. Ni kutokana na msingi huo, serikali inajitahidi sana kutoa chanjo za magonjwa mbalimbali ili kuimarisha na kujenga afya zao ili kuwa na kinga ya kutosha ya kuweza kupambana na magonjwa.


Taasisi ya Doris Mollel (DMF) ni wadau muhimu hapa nchini katika suala la afya ya mama na watoto. Ni taasisi inayopambana sana kuhakikisha maisha ya mama na watoto yanakuwa salama dhidi ya vifo hasa vitokanavyo na uzazi.


Taasisi hii chini ya uongozi wa Mkurugenzi Mtendaji wake, Doris Mollel, imejikita katika kusaidia vifaa vya kuweza kuokoa maisha ya watoto wanaozaliwa kabla ya muhula (njiti) katika vituo vya afya na hospitali mbalimbali nchini.


Bi. Mollel alipata msukumo wa kuanzisha taasisi hii kwani yeye ni miongoni mwa watoto waliozaliwa kabla ya muhula na alizaliwa mama yake alipokuwa na ujauzito wenye wiki  27 huku akizaliwa na uzito wa gramu 900 tu. Kupona kwake kumempa msukumo wa kutetea maisha ya wanawake na watoto ili wawe salama katika suala zima la uzazi kwa  kuwezesha upatikanaji wa vifaa vya afya. 


Kupitia taasisi hii, vituo vya afya na hospitali nyingi zimepata msaada wa vifaa, jambo linalosaidia kuokoa maisha ya maelfu ya wanawake na watoto. Hata mtoto anapozaliwa na uzito pungufu, anapata wasaa wa kuwekewa kwenye wodi maalum ya uangalizi wa watoto njiti (NICU).


Aidha, kutokana na vifaa vilivyopo humo na unyonyeshaji unaoendelea kutoka kwa mama yake, uzito wa mtoto huongezeka. Na pale wataalamu wanapojiridhisha juu ya kuimarika kwa afya ya mtoto, mtoto huyo hutolewa katika wodi hiyo na kuendelea na maisha mengine ya kunyonya kutoka kwa mama yake.


Mwezi Machi, 2026, Shirika la Afya Duniani (WHO) limetambua kazi kubwa na nyingi zinazofanywa na DMF, na hivyo kumpa tuzo ya heshima Doris Mollel kama njia ya kutambua mchango wake katika kuboresha na kukuza afya mama na mtoto nchini Tanzania.


Tuzo hiyo ilitolewa na Mkurugenzi Mkuu wa WHO, Dk. Tedros Ghebreyesus katika Makao Makuu ya WHO, Geneva, Uswisi. Binafsi, nampongeza Bi. Mollel kwa tuzo hiyo kwani jitihada zake za kupigania afya ya mama na watoto zimezaa matunda, na maisha ya wengi yameokolewa kupitia juhudi zake. 


Harakati za Bi.Mollel zinaongozwa na kauli yake isemayo "Nikiacha kupigana, watoto njiti watafariki". Hakika, tuzo hii ni heshima kwa Bi.Mollel na Tanzania kwa ujumla.



Maoni; 0620 800 462.

JAFO KUJA NA HOJA BINAFSI KUPENDEKEZA MPANGO MAALUM WA AJIRA ZA MUDA MFUPI KWA VIJANA

JAFO KUJA NA HOJA BINAFSI KUPENDEKEZA MPANGO MAALUM WA AJIRA ZA MUDA MFUPI KWA VIJANA

April 09, 2026 Add Comment

Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo,akichangia makadirio ya mapato na matumizi ya Ofisi ya Waziri Mkuu na taasisi zake kwa mwaka wa fedha 2026/27  leo Aprili 9,2026 bungeni jijini Dodoma.

Na.Alex Sonna-DODOMA

Mbunge wa Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo, amedhamiria kuwasilisha hoja binafsi bungeni itakayolenga kuishauri Serikali kuanzisha mpango maalum wa mikataba ya ajira za muda mfupi kwa vijana ili kupunguza changamoto ya ukosefu wa ajira nchini.

Akichangia makadirio ya mapato na matumizi ya Ofisi ya Waziri Mkuu na taasisi zake kwa mwaka wa fedha 2026/27 bungeni, Jafo alisema mpango huo unaweza kuwa na mfumo wa Ajira za muda (part time employment) utakaodumu kwa kipindi cha miaka mitatu mitatu hadi ifikapo mwaka 2050  ambapo vijana watapata ajira za mikataba na kujipatia uzoefu wa kazi.

Alimpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, kwa juhudi kubwa za kuongeza fursa za ajira kwa vijana tangu aingie madarakani, akisema serikali imefanya kazi kubwa katika kuwawezesha wananchi, lakini bado kuna haja ya kuja na mikakati mipya ya kukabiliana na wimbi la vijana wasio na ajira.

Jafo alibainisha kuwa changamoto ya ajira bado ni kubwa, huku akitoa mfano wa vijana wengi waliopo kwenye shughuli zisizo rasmi kama bodaboda, baadhi yao wakiwa na elimu ya juu ikiwemo stashahada,  shahada na kuendelea. Alipendekeza mpango maalum utakaolenga wahitimu hao ili kuwapa nafasi ya kupata ajira za muda na mikataba ya miaka mitatu.

Kwa mujibu wa mapendekezo yake, kila mwaka vijana 50,000 wanaweza kuingizwa kwenye mpango huo, ambapo asilimia 20 wawe wahitimu wa stashahada na asilimia 80 wawe wahitimu wa shahada na kuendelea. Aidha, alipendekeza malipo ya kujikimu ya Shilingi 500,000 kwa wenye stashahada na Shilingi 700,000 kwa wahitimu wa shahada.

Alisema gharama ya utekelezaji wa mpango huo inakadiriwa kufikia Shilingi bilioni 396, huku akisisitiza kuwa mpango huo utasaidia kukuza ujuzi wa vijana, kuongeza uzoefu wa kazi na kupunguza tatizo la ajira nchini.

Pia alipendekeza asilimia 10 zitoke katika mapato ya ndani ya kila Halmashauri, 10 ya gawio la Serikali kutoka kwenye mashirika ya umma, na fedha zingine zitokane na kubana maeneo mengine ya matumizi ya kawaida ya serikali(Recurrent Expenditure) ili zitumike kufadhili mpango huo. Aidha, alishauri mpango huo usimamie kupitia serikali za mitaa na Taasisi za Umma ili kurahisisha upatikanaji wa ajira katika halmashauri mbalimbali na Taasisi hizo za Umma.

Jafo alisisitiza kuwa mpango huo, kama utapitishwa, utaisaidia Serikali kuongeza wigo wa ajira na kuwawezesha vijana wengi zaidi kunufaika na fursa za kiuchumi nchini.

NGORONGORO NI NYUMBANI KWA KILA BINADAMU - KAMISHNA BADRU.

April 09, 2026 Add Comment

 Kamishna wa Uhifadhi wa Mamlaka ya Hifadhi ya Eneo la Ngorongoro Bw. Abdul-Razaq Badru leo tarehe 9 Aprili, 2026 amepuliza rasmi Kipenga cha shindano la mwezi mmoja la Safari Field Challenge akisisitiza kwamba Ngorongoro ni nyumbani kwa kila binadamu kutokana na chimbuko la historia linalobainishwa kisayansi.


Akizindua shindano hilo Kamishna Badru amewashukuru washiriki nane (8) wa shindano hilo kwa kuitika wito wa Ngorongoro na kuwaeleza kuwa Hifadhi ya Ngorongoro ni zaidi ya Kreta hasa kutokana na kuwa na utamaduni, asili, chimbuko la binadamu wa kale, siri ya Binadamu na maisha yake, Nyayo za Laetoli zenye umri za zaidi ya miaka milioni 3.6, mchanga unaohama, kushuhudia pumzi ya kwanza ya Nyumbu eneo la Ndutu, kuona Wanyama wakubwa watano katika eneo moja, mlima Lolmalasian ambao wa tatu kwa urefu Tanzania, misitu, mimea na ndege mbalimbali.

“Karibuni Ngorongoro ambapo ni nyumbani kwa sisi sote, mtapata uzoefu ya maajabu mbalimbali, kuyahisi, kuyaishi, kufurahia, kuyahadithia na kuwasaidia kupata ujuzi ambao utawafanya muwe mabalozi wazuri kuwaelezea watu wengine mkusanyiko wa maajabu yaliyoko Ngorongoro” Alisema Kamishna Badu.

Kamishna Badru amewapa changamoto washiriki wa shindano hilo kuwa watundu wa kuifahamu Ngorongoro, kuisemea Ngorongoro kwa mtazamo mpya wa sauti moja ambapo kwa kushirikiana na Azam Media hadithi, historia, maajabu ya Ngorongoro itasimuliwa na kufika pembe nne za dunia kuwa Ngorongoro sio kivutio cha utalii pakee bali ni Nyumbani kwa kila Binadamu ambapo historia yao ilianza.

Kamishna Msaidizi Mwandamizi anayesimamia Huduma za Utalii na masoko Mariam Chuma Kobelo amewaeleza washiriki wa Safari Field Challenge kuwa Tanzania ina vitu vingi vya Kujivunia,lakini Ngorongoro kuna vingi zaidi na kuwasisitiza washiriki wa shindano hilo kwenda kujifunza, kuifahamu na kuisimulia Ngorongoro kuwa ni zaidi ya Kasoko ya Ngorongoro.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Tanzania Tour Guide Fondation (TTGF) Mosses Njole ameleza kuwa washiriki wote 8 wako timamu na wamejiandaa kikamilifu kushiriki shindano hilo na kuwapongeza Ngorongoro kwa kuwa wadhamini wakuu na wadau wengine wakiwepo Azam Media ambayo imekuwa sehemu ya kusimulia maajabu ya Ngorongoro.







SERIKALI YAZINDUA KUKOSI KAZI CHA TAIFA CHA UFUATILIAJI,TATHMINI NA UTOAJI TAARIFA

April 09, 2026 Add Comment


Na  OWM-SBUU -Morogoro


Serikali imezindua Kikosi Kazi cha Taifa cha Ufuatiliaji, Tathmini na Utoaji Taarifa (ME&R National Task Force) kwa lengo kuratibu utekelezaji wa Mwongozo Jumuishi wa Ufuatiliaji na Tathmini katika kusimamia utendaji wa shughuli za Serikali.


Kauli hiyo imetolewa leo tarehe 09 Aprili, 2026 na Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu Dkt. James Kilabuko  wakati akifungua Kikao Kazi Cha Kikosi Kazi cha Taifa cha Ufuatiliaji, Tathmini na Utoaji Taarifa (ME&R National Task Force) kilichofanyika mkoani Morogoro.

Dkt. Kilabuko amesema, Ufuatiliaji na Tathmini ni dhana muhimu ya usimamizi inayotumika kwa lengo la kuhakikisha uwajibikaji na uwazi katika utekelezaji wa afua za maendeleo.

“Kikosi Kazi hiki kitakuwa chombo cha kitaalamu cha kusaidia kuratibu utekelezaji wa Mwongozo Jumuishi wa U&Tc, kuoanisha mifumo ya kitaifa ya utendaji, kuimarisha ubora wa takwimu na taarifa za Serikali na  kuandaa mapendekezo ya sera na maboresho ya kiutendaji” alisema Naibu Katibu Mkuu huyo.

Ameeleza kuwa, kikao kazi hicho ni fursa ya kipekee ya kujifunza, kubadilishana uzoefu na kuweka mikakati ya pamoja ya namna bora ya kutekeleza majukumu ya  Ufuatiliaji na Tathmini nchini.

“Matarajio yangu ni kwamba, baada ya kikao hiki tutaboresha uratibu na kuoanisha viwango vya kitaifa vya Ufuatiliaji na Tathmini (M&E) katika Wizara, Idara na Wakala (MDAs), Sekretarieti za Mikoa (RSs) na Mamlaka za Serikali za Mitaa (LGAs) ni hatua muhimu katika kuhakikisha uwiano na ufanisi wa utekelezaji wa shughuli za maendeleo” amefafanua.

 


Vilevile, Dkt. Kilabuko amebainisha kuwa ipo haja ya  kuoanisha viashiria vya taasisi na maeneo muhimu ya matokeo ya Kitaifa ili kuhakikisha kuwa juhudi za taasisi mbalimbali zinaendana na vipaumbele vya Taifa.

 


“ Katika hili, ni muhimu kuimarisha mwingiliano na utangamano wa Mfumo wa Kupima Utendaji Kazi wa Watumishi wa Umma na Taasisi (PEPMIS), PIPMIS na Mfumo wa Kitaifa wa Usimamizi wa Miradi ya Maendeleo na Programu (NPMIS) ili kuwezesha mtiririko mzuri wa taarifa na matumizi ya data kwa ufanisi” ameeleza.

 



Aidha, amebainisha kuwa Serikali ya Awamu ya Sita inataka kuona taarifa za U&T zikitumika kufanya maamuzi,  miradi inakamilika kwa wakati na kwa thamani halisi ya fedha na maisha ya wananchi yanaboreshwa kutokana na kazi zinazotekelezwa.

 


“Haya yote yatawezekana ikiwa tutazingatia misingi ya Ufuatiliaji na Tathmini kama inavyoelekezwa katika Mwongozo Jumuishi. Tumieni muda huu vizuri kujadili masuala yatakayokuwa na maslahi mapana kwa nchi yetu na kuwa na Ufuatiliaji na Tathmini wenye tija” ameongeza Dkt. Kilabuko.



*MWISHO*

CCM YATAKA MAENEO YA KUKUSANYIA TAKA SOKO LA MGANDINI YABORESHWE

April 09, 2026 Add Comment

 


Na Oscar Assenga, TANGA

Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Tanga kimetoa maelekezo kwa Halmashauri ya Jiji la Tanga kuhakikisha maeneo ya kukusanyia taka katika soko la Mgandini yanaboreshwa kwa kujazwa kifusi ikiwemo kurekebisha barabara za ndani ili kuimarisha usafi.

Agizo hilo lilitolewa na Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Tanga Rajab Abdurhaman wakati wa ziara yake ambapo alisisitiza umuhimu wa kuhakikisha maji ya mvua yanaelekezwa ipasavyo kwenye mifereji ili kuepusha mafuriko na uharibifu wa miundombinu.

Ziara hiyo ilikuwa ni kufuatilia utekelezaji wa maagizo aliyoyatoa awali kuhusu kuboresha usafi wa soko hilo ambapo viongozi wa Jiji hilo walianza kuyafanyia kazi ikiwemo kuondosha uchafuzi uliokuwepo awali.

Awali, wakati wa ziara yake ya kukagua hali ya usafi, Mwenyekiti huyo hakuridhishwa na mazingira ya soko hilo na kutoa muda wa mwezi mmoja kwa uongozi wa Jiji kuhakikisha hali ya usafi inaboreshwa.

Akizungumza baada ya kufanya ziara ya ufuatiliaji, Rajab aliwapongeza Mstahiki Meya pamoja na viongozi wa Jiji kwa kuchukua hatua na kuanza kutekeleza maelekezo hayo ya CCM.

“Hatuhitaji viongozi wa kulalamika, tunahitaji viongozi wanaochukua hatua kutatua changamoto za wananchi. Mlichokifanya ni kutimiza wajibu wenu,” alisema.

Alisema kuwa hali ya uchafu iliyokuwepo awali haikuwafurahisha viongozi wala wafanyabiashara, hivyo hatua zilizochukuliwa zinaonesha uwajibikaji wa uongozi.

Hata hivyo Mwenyekiti Rajab alisisitiza kuwa atarejea kukagua maendeleo hayo baada ya wiki mbili na kuonya kuwa hataki kusikia visingizio badala ya utekelezaji.

“Ndani ya mwezi mmoja kuanzia Aprili 9 hadi Mei 9, tunatarajia kuona kazi imeanza. Hatutaki hadithi, tunataka vitendo,” alisisitiza.

Aidha, alieleza kuwa Jiji la Tanga ni taswira ya mkoa huo, hivyo linapaswa kuwa safi na lenye mpangilio mzuri.

Alikumbusha kuwa zamani Tanga ilikuwa mji unaojulikana kwa usafi na ustaarabu, hivyo ipo haja ya kurejesha hali hiyo.

Kuhusu huduma za vyoo katika soko hilo, Mwenyekiti alieleza kutoridhishwa na hali iliyopo, akibainisha kuwa choo kilichopo hakitoshelezi mahitaji kutokana na idadi kubwa ya watumiaji.

Alisema kuwa hali hiyo inasababisha baadhi ya watu kulazimika kujisaidia katika maeneo yasiyofaa, jambo linalohatarisha afya za wananchi na wafanyabiashara.

Alisisitiza umuhimu wa Jiji kutafuta suluhisho la kudumu, ikiwemo kuboresha mfumo wa maji taka ili kuendana na ongezeko la watumiaji.

Hata hivyo, aliwapongeza viongozi kwa kuanza mpango wa kujenga choo kipya chenye matundu 12 kitakachosaidia kupunguza changamoto hiyo, hasa katika kipindi hiki ambacho soko linatarajiwa kujengwa upya.

Pia alizungumzia changamoto ya msongamano wa magari yanayoleta bidhaa sokoni hapo, akielekeza kuwepo kwa utaratibu maalum wa magari kuingia na kushusha mizigo kwa mpangilio ili kupunguza msongamano na kuboresha usafi.

Alipendekeza magari yapaki katika maeneo maalum yaliyo nje ya soko, kisha yaingie kwa zamu kushusha bidhaa.

Katika hatua nyengine alisisitiza umuhimu wa kujenga mifereji ya maji ili kuzuia maji ya mvua kutuama au kuingia sokoni, hali inayochangia uchafu na uharibifu wa mazingira.

Alimalizia kwa kuwataka viongozi wa Jiji kuwa karibu na wananchi na kushughulikia changamoto zao kwa vitendo, akibainisha kuwa wananchi hao ndio chanzo cha mapato ya Jiji kupitia kodi.

Kwa upande wake, Naibu Meya Khalid Rashid alisema kuwa Jiji lina mpango wa kuboresha miundombinu ya ndani ya soko, ikiwemo njia za kupita ili kuondoa changamoto ya matope wakati wa mvua. Alibainisha kuwa kazi hiyo inatarajiwa kuanza ndani ya wiki moja.

Mwisho.

WATENDAJI OFISI YA WAZIRI MKUU WAKUMBUSHWA KUIMARISHA WELEDI KUTIMIZA DIRA YA TAIFA 2050

April 08, 2026 Add Comment




Na. MWANDISHI WETU -DODOMA



Watendaji wa Ofisi ya Waziri Mkuu wamekumbushwa kuendelea kutekeleza majukumu yao kwa weledi, ufanisi na kujituma ili kuhakikisha wanachangia kikamilifu katika kufanikisha malengo ya Dira ya Taifa 2050, hususan katika maeneo ya sera, uratibu na usimamizi wa utekelezaji wake.


Wito huo umetolewa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu), Mhe. Prof. Palamagamba J.A. Kabudi, wakati akizungumza na watumishi wa Ofisi hiyo mara baada ya kuwasili rasmi na kupokelewa na uongozi na watumjshi wa Ofisi hiyo katika Jengo la Ngome Jijini Dodoma tarehe 8 Machi, 2026

Prof. Kabudi alisisitiza umuhimu wa ushirikiano na ubunifu miongoni mwa watumishi ili kuongeza ufanisi wa utendaji kazi.

“Ni muhimu tushirikishane mawazo na kufanya kazi kwa pamoja ili kumsaidia Mheshimiwa Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kufanikisha adhima ya maendeleo yenye kuleta ustawi na furaha kwa Watanzania," alisema Prof. Kabudi


Aliongezea kuwa upo umuhimu wa kushikamana ili kuendelea kuimarisha utendaji wetu ili kumwezesha Mheshimiwa Waziri Mkuu kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi zaidi.


Aidha, Waziri Kabudi alibainisha kuwa mazingira ya kazi yenye mshikamano na mahusiano ya kifamilia hayapaswi kuwa chanzo cha uzembe au utovu wa nidhamu, bali yawe kichocheo cha kuongeza uwajibikaji na kufikia viwango vya juu vya utendaji.

Katika hatua nyingine, Waziri Kabudi aliwataka watumishi kuendelea kumuombea aliyekuwa Waziri wa Nchi katika Ofisi hiyo, Marehemu William Vangimembe Lukuvi, ili Mwenyezi Mungu amrehemu na kumpa pumziko la milele.

“Nitaendeleza, kadri nitakavyoweza, misingi na jitihada zilizoanzishwa na mtangulizi wangu katika kuijenga Ofisi hii,” aliongeza.

Awali, Naibu Waziri wa Ofisi hiyo, Mhe. Ummy Nderiananga, alimpongeza Prof. Kabudi kwa kuaminiwa na kuteuliwa na Mheshimiwa Rais kushika nafasi hiyo, akiahidi ushirikiano wa dhati kutoka kwa watumishi wote katika utekelezaji wa majukumu yake.

Kwa upande wake, Katibu Mkuu wa Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu), Dkt. Jim Yonazi, naye alimpongeza Waziri Kabudi kwa uteuzi huo na kusisitiza kuwa watumishi wako tayari kuongozwa na kushirikiana naye katika kuendelea kuwahudumia wananchi kwa ufanisi.



=MWISHO=