HABARI

SIASA

ELIMU

Recent Posts

MAKATIBU WAKUU VYAMA VYA UKOMBOZI WAJADILI HALI YA KISIASA KUSINI MWA AFRIKA

March 05, 2026 Add Comment


Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimeongoza Kikao cha 12 cha Makatibu Wakuu wa Vyama vya Ukombozi Kusini mwa Afrika, ambapo, pamoja na mambo mengine, vimejadili hali ya siasa, ukombozi wa kiuchumi na kuboresha hali za wananchi katika nchi zao. 

Kikao hicho kilichofanyika leo tarehe 5 Machi 2026, Kibaha, mkoani Pwani, kilihusisha Makatibu Wakuu wa Vyama 6 vya Ukombozi Kusini mwa Afrika, ambavyo ni ANC (Afrika Kusini), CCM (Tanzania), FRELIMO (Msumbiji), SWAPO (Namibia), ZANU-PF (Zimbabwe) na MPLA (Angola).

Akizungumza na vyombo vya habari baada ya mkutano huo, Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi, Asha-Rose Migiro, amesema kuwa katika kikao hicho wamepitia maazimio ya Mkutano Mkuu wa Wakuu wa Vyama hivyo uliofanyika mwaka jana, nchini Afrika ya Kusini. 

Alisema mijadala ilijikita kuangalia hali ya kisiasa katika ukanda wa Kusini mwa Afrika, hususan kulinda uhuru wa kisiasa na kiuchumi, kutathmini malengo ya harakati za ukombozi pamoja na kuendelea kulinda na kuimarisha uhuru uliopatikana.


Dkt. Migiro amesema jukumu kubwa la vyama hivyo ni kuimarisha mshikamano na umoja wao pamoja na kujadili changamoto mbalimbali zinazoikabili kanda hiyo ikiwemo mabadiliko ya tabianchi. Aidha, walijadili namna ya kutatua migogoro katika nchi wanachama na kuchochea maendeleo ya kiuchumi, kisiasa na kijamii.


Katika kikao hicho pia walifanya mapitio ya maendeleo yaliyopatikana katika nchi zao, ikiwa ni pamoja na kuimarisha huduma za jamii, kuboresha miundombinu pamoja na kuweka mikakati ya kujenga uchumi stahimilivu na kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi.

Masuala mengine yaliyojadiliwa ni pamoja na umuhimu wa kuongeza ajira kwa vijana, kuwawezesha wanawake pamoja na kujenga uchumi jumuishi na stahimilivu kwa maendeleo ya Ukanda wa Kusini mwa Afrika.


#Ends

EWURA KANDA YA KASKAZINI YAWANOA VIONGOZI WA WILAYA YA KOROGWE

EWURA KANDA YA KASKAZINI YAWANOA VIONGOZI WA WILAYA YA KOROGWE

March 05, 2026 Add Comment

Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) kupitia Kanda ya Kaskazini, leo tarehe 5 Machi 2026 imetoa elimu kwa viongozi wa Wilaya ya Korogwe katika semina iliyofanyika katika ukumbi wa GMCC.

Akimkaribisha Mgeni Rasmi, Meneja wa EWURA Kanda ya Kaskazini, George Mhina, alisema lengo ni kuwajengea viongozi uelewa kuhusu majukumu ya EWURA na maeneo inayoyadhibiti ili kuboresha utoaji wa huduma kwa wananchi.

Katika semina hiyo, washiriki walipatiwa elimu kuhusu umuhimu wa uvunaji wa maji ya mvua, matumizi ya nishati safi ya kupikia, leseni za mafundi umeme, ujenzi wa vituo vya mafuta vijijini pamoja na namna ya kutatua migogoro katika sekta za maji na nishati.

Akizungumza katika kikao hicho, Mkuu wa Wilaya ya Korogwe Mhe. William Mwakilema amewasisitiza viongozi hao kuwa mabalozi wa elimu waliyoipata kwa kuhakikisha wanaifikisha kwa wananchi ili kuongeza uelewa na matumizi sahihi ya huduma za maji na nishati.

 

SHEIKH MKUU WA TANZANIA AWAHAMASISHA WANAWAKE KUMILIKI ARDHI BAADA YA KUPATA HATI SAMIA ARDHI KLINIKI

March 05, 2026 Add Comment
Dar es salaam –
Mufti na Sheikh Mkuu wa Tanzania, Abubakar Zubeir, ametoa wito kwa Watanzania kujitokeza kwa wingi kutumia fursa ya huduma za ardhi zinazotolewa kupitia Samia Ardhi Kliniki, akisisitiza umuhimu wa wanawake kumiliki ardhi kama njia ya kujikomboa kiuchumi.
Mufti Zubeir alitoa kauli hiyo baada ya kufika katika Kliniki ya Ardhi inayofanyika katika Ofisi za Ardhi za Mkoa wa Dar es Salaam, ambapo alipata hati ya ardhi huku akishuhudia namna wananchi wanavyohudumiwa katika kliniki hiyo ambayo inaendelea nchi nzima.
Akizungumza mara baada ya kupata huduma hiyo, Mufti Zubeir alisema hatua ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kuandaa Samia Ardhi Kliniki yenye kulenga kuwapa kipaumbele wanawake ni jambo muhimu linalosaidia kuongeza usawa katika umiliki wa rasilimali muhimu kama ardhi.
Alisema wanawake wanapaswa kutumia kikamilifu fursa hiyo ili waweze kupata hati za ardhi na kujiimarisha kiuchumi.
“Wanawake wana haki ya kumiliki mali mbalimbali ikiwemo magari na mali nyingine, hivyo hakuna sababu ya kuwanyima nafasi ya kumiliki ardhi. Ni muhimu jamii, hususan wanaume, kuachana na mila kandamizi zinazowazuia wanawake kumiliki rasilimali,” alisema Mufti Zubeir.
Aidha, aliwataka wanaume kuwapa nafasi wanawake kumiliki ardhi ili kuongeza idadi ya wanawake wenye umiliki rasmi wa ardhi nchini, jambo ambalo litasaidia kuimarisha ustawi wa familia na jamii kwa ujumla.
Katika hatua nyingine, Mufti Zubeir alipongeza maandalizi mazuri yaliyofanywa na Ofisi ya Mkoa wa Dar es Salaam katika uendeshaji wa kliniki hiyo, kuanzia mapokezi hadi utoaji wa huduma kwa wananchi.
Alisema namna wateja wanavyohudumiwa kwa ufanisi ni jambo jema lenye manufaa kwa jamii na lina thawabu kubwa mbele za Mwenyezi Mungu, hususan katika kipindi hiki cha mwezi mtukufu wa Ramadhani.
Mufti Zubeir pia aliwaombea heri watumishi wanaotoa huduma katika kliniki hiyo ili waendelee kuwahudumia wananchi kwa uadilifu na bidii.
Samia Ardhi Kliniki zinaendelea kufanyika katika maeneo mbalimbali nchini kwa lengo la kurahisisha upatikanaji wa huduma za ardhi, hususan kwa wanawake, ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya kuelekea Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani yanayoadhimishwa Machi 8 kila mwaka.
 
 
SERIKALI, SEKTA BINAFSI KUIMARISHA HUDUMA ZA DHARURA KUCHOCHEA AJIRA NCHINI

SERIKALI, SEKTA BINAFSI KUIMARISHA HUDUMA ZA DHARURA KUCHOCHEA AJIRA NCHINI

March 05, 2026 Add Comment






Na Abduly Iddy, Dar es Salaam

Serikali imesema ushirikiano kati yake na Sekta binafsi utaendelea kuwa chachu muhimu ya kuimarisha huduma za afya nchini, hususan katika kuboresha huduma za dharura kupitia mpango wa kuanzisha uzalishaji wa magari ya wagonjwa (ambulance) mkoani Tanga.

Akizungumza Machi 5, 2026 jijini Dar es Salaam katika kikao cha maandalizi ya kuanzisha uzalishaji wa magari hayo, Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mhe.Batilda Burian, amesema Serikali inakaribisha uwekezaji huo unaofanywa kwa kushirikiana na SO Company Limited kwani utaimarisha upatikanaji wa huduma za dharura za afya nchini hususan magari ya wagonjwa.

Amesema uzalishaji wa ambulance ndani ya nchi utaongeza upatikanaji wa magari ya kisasa ya kuwahudumia wagonjwa na kupunguza muda wa kuwafikia wananchi wanaohitaji msaada wa haraka wa kitabibu, hatua itakayosaidia kuokoa maisha ya watu.

“Mradi huu ni hatua muhimu tunapoimarisha mfumo wetu wa huduma za afya. Kupatikana kwa ambulance zinazozalishwa hapa nchini kutarahisisha usambazaji wake katika maeneo mbalimbali, hususan ya pembezoni,” amesema, RC Batlida.

Aidha, amesema mradi huo pia utaleta manufaa ya kiuchumi kwa kufungua fursa za ajira kwa vijana, kukuza wazalishaji wa ndani wa vipuri na kuchochea maendeleo ya sekta zinazohusiana na uzalishaji wa vifaa vya magari na huduma za afya.

Kwa upande wake, Kaimu Mkurugenzi wa Huduma za Dharura na Maafa kutoka Wizara ya Afya, Dkt. Erasto Sylvanus, amesema Serikali itaendelea kuweka mazingira rafiki ya uwekezaji ili kuhakikisha mradi huo unatekelezwa kwa ufanisi na kuchangia maendeleo ya sekta ya afya pamoja na uchumi wa taifa.

Mradi huo unatarajiwa kuimarisha huduma za dharura za afya huku ukifungua fursa mpya za ajira na maendeleo ya kiuchumi nchini.

SENYAMULE AIPA KONGOLE WIZARA YA ARDHI KUANZISHA SAMIA ARDHI KLINIKI

SENYAMULE AIPA KONGOLE WIZARA YA ARDHI KUANZISHA SAMIA ARDHI KLINIKI

March 05, 2026 Add Comment

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Mhe. Rosemary Senyamule ameipongeza Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa kuendesha zoezi la Samia Ardhi Kliniki linalofanyika nchi nzima.

Mhe. Senyamule ametoa pongezi hizo leo Machi 5, 2026 alipotembelea kliniki hiyo inayoendelea katika viwanja vya Ofisi ya Kamishna wa Ardhi Msaidizi Mkoa wa Dodoma.

“Nimekaa sijawahi kuona ubunifu wa jambo hili, na nimeambiwa linafanyika nchi nzima ya Tanzania. Hiki ni kitu cha pekee sana,” amesema Senyamule.

Kwa mujibu wa Mkuu huyo wa mkoa wa Dodoma, awali aliposikia kuhusu kliniki hiyo alijiuliza kama kutapatikana wanawake wa kutosha kwenda kutatuliwa kero zao za ardhi, lakini hali imekuwa tofauti.

“Nilijiuliza kama wanawake watapatikana kwa wingi, lakini leo nimeshangaa kuona na kushuhudia kuwa sasa wanawake wengi wanamiliki ardhi,” amesema Senyamule.

Aidha, amesema kuwa kama jambo hilo lingefanyika miaka kumi au ishirini iliyopita, isingekuwa rahisi kupata wanawake wengi kwa sababu wengi hawakuwa na uelewa wa haki yao ya kumiliki ardhi.

“Kama ungelifanya jambo hili miaka kumi au ishirini iliyopita na kusema wanawake waje washughulikie kero zao za ardhi na kupata hati, usingewapata wengi kwa sababu wakati huo hatukuwa na uelewa kuwa sisi pia tunastahili kumiliki ardhi,” ameongeza.

Katika hatua nyingine, Mhe. Senyamule amewaasa wanawake kutunza vizuri hati zao za ardhi, akieleza kuwa ardhi ya Dodoma ina thamani kubwa inayoongezeka kila siku.

“Ukishapata hati yako, itunze vizuri kwa sababu ardhi ya Dodoma ina thamani kubwa na thamani yake inaendelea kuongezeka kila siku,” amesema.

Sambamba na hilo, Mhe. Senyamule pia amekabidhi hati miliki kwa baadhi ya wanawake waliofika katika kliniki hiyo iliyofanyika katika viwanja vya Ofisi ya Kamishna Msaidizi wa Ardhi Mkoa wa Dodoma.

Samia Ardhi Kliniki ilianza rasmi tarehe 2 Machi 2026 katika mikoa yote nchini na inatarajiwa kuhitimishwa tarehe 7 Machi 2026 yenye Kauli Mbiu, Mwanamke; Haki Yako, Miliki Ardhi sasa.

RAIS MHE. DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AONGOZA KIKAO CHA BARAZA LA MAWAZIRI, IKULU JIJINI DAR ES SALAAM

March 05, 2026 Add Comment


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akiongoza kikao cha Baraza la Mawaziri, tarehe 5 Machi, 2026 Ikulu Jijini Dar es Salaam.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akiongoza kikao cha Baraza la Mawaziri, tarehe 5 Machi, 2026 Ikulu Jijini Dar es Salaam.

MARIAM CHUMA KOBELO, CHUMA CHA MJERUMANI NGORONGORO

March 05, 2026 Add Comment



“Kwa Mungu hakuna kubwa kwa kuwa hashindwi kitu, tusikate tamaa katika kuhamasisha watanzania kutembelea vivutio vya utalii, ipo siku watanzania wanaotembelea vivutio vya utalii Ngorongoro na maeneo mengine watakuwa wengi zaidi”.

Maneno kutoka kwa Mariam Chuma Kobelo, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Uhifadhi anayesimamia Huduma za utalii na Masoko Ngorongoro akielezea umuhimu wa utalii wa ndani kwa watanzania.

Ni jembe la Ngorongoro na katika maadhimisho ya siku ya wanawake duniani, Ngorongoro tunatambua mchango wake  kwa kubuni kampeni mbili za kuhamasisha utalii wa ndani na kuibua mazao mapya ya utalii kama *Wedding Tourism* 

Ubunifu wa kampeni za _Merry and Wild Ngorongoro Awaits_ na _Diko la Amboni_  ni mawazo yake yaliyosaidia kuongeza idadi ya watalii wa ndani na kuibua vivutio vipya vya utalii.

Chukua maua yako mama kuelekea maadhimisho ya siku ya wanawake Duniani tarehe 08 Machi, 2026.

TANZANIA IMEENDELEA KUIMARISHA USHINDANI WA HAKI ZA UDHIBITI WA BIDHAA BANDIA

March 05, 2026 Add Comment

 Na Maandishi Wetu, Dodoma.

Tanzania inaendelea kuimarisha ushindani wa haki na udhibiti wa bidhaa bandia kupitia Tume ya Ushindani (FCC) pia Sheria ya Alama za Bidhaa, 1963 inalinda biashara halali na watumiaji dhidi ya udanganyifu.

FCC inaidhinisha miungano 4 katika sekta ya fedha, ikilenga kuimarisha mfumo wa malipo ya kidijitali na huduma za benki. Aidha, udhibiti wa bidhaa bandia unaendelea kulinda biashara halali na kuchochea ukuaji wa uchumi.

Hayo yamebainishwa na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Ushindani (FCC),  Khadija Ngasongwa, akizungumza na waandishi wa habari kuhusu miradi ya maendeleo na fursa kwa vijana, leo Machi 05, 2026, katika ukumbi wa Idara ya Habari (MAELEZO), Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.

Khadija amesema Katika kipindi cha 2025/26, Tume ya Ushindani imeidhinisha miungano 4 katika sekta ya Fedha, Kuidhinishwa kwa miungano hii miwili (2) katika sekta ya fedha na malipo kunaweza kuleta mabadiliko chanya kwa Tanzania kwa kuimarisha mfumo wa kadi na malipo ya kidijitali kupitia uwekezaji wa Toppan Global Security Limited katika DZ Card (Africa) Limited, hivyo kuongeza usalama na ufanisi wa miamala ya kielektroniki.

Vilevile, muungano unaohusu kampuni ya Soren Investment Company Limited na Habib African Bank Limited unatarajiwa kuleta mtaji mpya na uwezo wa kibiashara ili kuimarisha huduma za benki, kutanua upatikanaji wa mikopo kwa wafanyabiashara na wananchi, na kuchochea ushindani katika sekta ya fedha ambao unaweza kupunguza gharama za huduma za kifedha na kuongeza kasi ya ukuaji wa uchumi kupitia ubunifu na uwekezaji katika teknolojia za kifedha.

Aidha amesema Udhibiti wa Bidhaa Bandia FCC imeendelea kusimamia kikamilifu Sheria ya Alama za Bidhaa, 1963 ambayo jukumu muhimu katika kuzuia uingizaji, uuzaji, na usambazaji wa bidhaa bandia au zile zenye maelezo potofu. 

"Bidhaa bandia huzuia ushindani wa haki, kuathiri vibaya biashara halali, na kuhadaa watumiaji, hivyo kuunda uwanja usio sawa wa biashara. Sheria hii inahakikisha kuwa biashara zinapewa fursa ya kufanikiwa kutokana na ubora, ubunifu, na kufuata sheria, badala ya udanganyifu"

Hata hivyo amesema hiyo inakuza soko lenye ushindani wa haki na uwazi, likilinda imani ya watumiaji na kuwezesha makampuni kuwekeza kwa kujiamini katika ukuaji na ubunifu.

Kudhibiti bidhaa bandia kwa mujibu wa sheria hii pia kunachangia ukuaji wa uchumi. Biashara halali zinabaki na mapato yao, jambo linalochochea uwekezaji zaidi, kuongeza ajira, na kuendeleza ubunifu. Watumiaji wanalindwa dhidi ya bidhaa zisizo salama au zisizo halisi, na hivyo kupunguza hasara za kiuchumi zinazotokana na udanganyifu. 

Aidha, jitihada za kuzuia bidhaa bandia zinaboresha sifa ya biashara kitaifa na kimataifa, kuwavutia wawekezaji, na kuongeza mauzo ya nje, Kwa kuunganisha utekelezaji madhubuti, ushirikiano wa sekta, na uhamasishaji wa Umma, Sheria hiyo inahakikisha kuwa ushindani wa haki na uthabiti wa kisheria unachochea ukuaji wa uchumi endelevu wa nchi. 




KIHONGOSI AIPONGEZA WIZARA YA NISHATI KWA MRADI WA UMEME JUA KAYENZE

March 05, 2026 Add Comment






📌Umegharimu bilioni 11 na kuingiza umeme gridi ya Taifa.

Katibu wa Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa, Kenan Kihongosi ameipongeza Wizara ya Nishati kwa utekelezaji wa mradi wa umeme jua wenye thamani ya shilingi bilioni 11 unaoingiza megawati tano (5) katika Gridi ya Taifa.

Kihongosi ametoa pongezi hizo mara baada ya kutembelea mradi huo uliopo katika Kijiji cha Kayenze, Jimbo la Ushetu wilayani Kahama, akiwa katika ziara yake ya kikazi mkoani Shinyanga.



“Naipongeza Wizara ya Nishati kwa mradi huu wenye tija ambao ni sehemu ya vielelezo vya utekelezaji wa miradi ya nishati safi kwa ajili ya wananchi. Kupitia mradi huu tunaendelea kuona dhamira ya Serikali ya kupeleka maendeleo katika maeneo mbalimbali nchini,” amesema Kihongosi

Aidha, amemshukuru na kumpongeza Rais, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa maono yake yaliyowezesha kukamilika kwa miradi mbalimbali ya kimkakati ikiwemo mradi wa Julius Nyerere unaozalisha megawati 2,115 pamoja na mradi wa umeme jua wa Kishapu ambapo awamu ya kwanza imekamilika na kuanza kuzalisha megawati 50.

Kihongosi pia amempongeza Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi, Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba pamoja na viongozi wengine kwa usimamizi madhubuti unaoifanya sekta ya nishati kuwa imara na yenye utulivu, huku akisisitiza kasi ya utekelezaji wa miradi kuendelea.

Kwa upande wake, Naibu Waziri wa Nishati na Mbunge wa Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Salome Makamba amesema umeme unaozalishwa katika mradi huo unaingizwa kwenye Gridi ya Taifa kupitia njia ya msongo wa kilovolti 33 (33kV). Ameongeza kuwa mradi huo ulikamilika mwezi Mei 2025 na kuanza kufanya kazi mara moja.

Ameeleza pia kuwa pamoja na kusaidia kuimarisha hali ya upatikanaji wa umeme, mradi huo umechangia maendeleo ya jamii kwa kujenga jengo la zahanati katika Kijiji cha Kayenze kwa gharama ya shilingi milioni 130.

Kuhusu usambazaji wa umeme katika Jimbo la Ushetu, Mhe. Salome amesema Rais, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ametoa fedha kwa ajili ya kusambaza umeme katika vitongoji 136 jimboni humo, huku vitongoji takriban 100 vilivyosalia vitakuwa vimefikiwa na huduma hiyo ifikapo mwaka 2030.


































RC SENYAMULE ATEMBELEA BANDA LA TEMESA KATIKA MAONESHO YA MAFANIKIO YA SIKU 100 ZA UONGOZI WA RAIS DKT. SAMIA SULUHU

March 05, 2026 Add Comment


Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Mhe. Rosemary Senyamule, ametembelea banda la Wakala wa Ufundi na Umeme Tanzania (TEMESA) katika maonesho ya mafanikio ya siku 100 za uongozi wa Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania pamoja na utatuzi wa kero za wananchi.

Maonesho hayo ya siku tatu yamefunguliwa leo machi 5, katika viwanja vya Nyerere Square jijini Dodoma, yakishirikisha taasisi mbalimbali za Serikali ikiwemo TEMESA, ambapo imewasilisha mafanikio yao katika utoaji wa huduma kwa wananchi na kutoa elimu kuhusu majukumu yao.

Akiwa katika banda la TEMESA, Mhe. Senyamule alipata maelezo kuhusu shughuli mbalimbali zinazofanywa na TEMESA pamoja  na mafanikio ya Wakala kutoka kwa Meneja Masoko na Uhusiano kwa Umma, Bi. Martha Joachim.

Akitoa ufafanuzi huo, Bi. Martha amesema TEMESA imepiga hatua katika kuboresha utoaji wa huduma za kiufundi kwa taasisi za Serikali kupitia matumizi ya mifumo ya kisasa na ya kidijitali.

Ameeleza kuwa miongoni mwa mafanikio hayo ni matumizi ya Mfumo wa Usimamizi wa Kazi za Matengenezo (MUM), unaosaidia na kurahisisha ufuatiliaji wa shughuli za matengenezo kwa ufanisi zaidi.

“Mfumo huu umeongeza uwazi, ufanisi na kasi katika utoaji wa huduma za matengenezo, na kusaidia taasisi za Serikali kupata huduma bora zinazopelekea  kuwahudumia wananchi kwa ufanisi,” amesema.

Aidha, Bi. Martha ameongeza kuwa TEMESA inaendelea  kuboresha utendaji kazi wake, hasa katika huduma za matengenezo ya magari ya Serikali, usimamizi wa vivuko pamoja na miundombinu ya umeme katika taasisi mbalimbali za Umma.