HABARI

SIASA

ELIMU

Recent Posts

EWURA YADHIHIRISHA NIDHAMU NA BIDII KATIKA SIKU YA WAFANYAKAZI DUNIANI

EWURA YADHIHIRISHA NIDHAMU NA BIDII KATIKA SIKU YA WAFANYAKAZI DUNIANI

May 01, 2026 Add Comment

Wafanyakazi wa EWURA wakishiriki maandamano ya Mei Mosi mbele ya Rais, Mhe. Samia Suluhu Hassan.

...

Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) leo, Mei 1, 2026, imeungana na wafanyakazi wengine duniani kuadhimisha Siku ya Wafanyakazi Duniani (Mei Mosi), maadhimisho yaliyofanyika kitaifa mkoani Njombe.

Sherehe hizo zilihudhuriwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, ambaye alikuwa mgeni rasmi. Katika hotuba yake, Rais Samia amewahimiza waajiri na waajiriwa kote nchini kuendeleza ushirikiano, kuaminiana, na kutanguliza maslahi ya taifa katika utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku.

Amesisitiza kuwa Serikali itaendelea kuboresha mazingira na ustawi wa wafanyakazi, huku akiwataka kuongeza bidii na ufanisi kazini. Aidha, alibainisha wazi kuwa Serikali inathamini mchango wa wafanyakazi na itaendelea kuwaunga mkono katika juhudi za maendeleo ya nchi.

Katika maadhimisho hayo, EWURA imewakilishwa na wafanyakazi wake bora kutoka idara na vitengo mbalimbali. Wafanyakazi hao walichaguliwa kwa kura za wenzao kwa kuzingatia vigezo muhimu kama vile utendaji uliotukuka, nidhamu ya kazi, ubunifu pamoja na kujituma kazini.

Wawakilishi hao walishiriki katika maandamano rasmi yaliyopita mbele ya mgeni rasmi, wakibeba mabango yenye ujumbe wa kuhamasisha mshikamano na uwajibikaji kazini.

Ushiriki wao umeonesha dhamira ya EWURA kuendelea kutoa huduma bora kwa wananchi na kuchangia maendeleo ya taifa kwa ujumla.

Wafanyakazi wa EWURA wakishiriki maandamano ya Mei Mosi mbele ya Rais, Mhe. Samia Suluhu Hassan.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwapungia mkono wafanyakazi wa EWURA, wakati wa maandamano ya Maadhimisho ya Sherehe za Meimosi leo.

WAHITIMU 12 NIT WAHITIMU MAFUNZO YA AWALI YA LUGHA YA KIJAPANI

May 01, 2026 Add Comment

NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

Wahitimu 12 wa Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT) wamehitimu mafunzo ya awali ya lugha ya Kijapani, hatua inayolenga kuongeza ujuzi na ushindani wao katika soko la ajira la ndani na kimataifa.

WMA YASHIRIKI MAADHINISHO YA SIKU YA WAFANYAKAZI DUNIANI MEI MOSI

May 01, 2026 Add Comment


Wakala wa Vipimo (WMA) imeungana na wafanyakazi kutoka katika taasisi na mashirika mbalimbali nchi nzima kuadhimisha siku ya Wafanyakazi Duniani.

Siku ya Wafanyakazi Duniani huadhimishwa kila Mwaka tarehe 1 Mei na kaulimbiu ya Siku ya Wafanyakazi Duniani Mwaka 2026 ni *"Kazi zenye Staha ni Nguzo Imara kwa Maendeleo Endelevu katika Utekelezaji wa Dira ya Taifa 2050".

Wakala imeshiriki katika maadhimisho hayo Kitaifa Mkoani Njombe ambapo watumishi wa Mkoa huo wameongozwa na Afisa Mtendaji Mkuu wa WMA Bw. Alban Kihulla.

Pamoja na ushiriki wa Kitaifa kadharika, WMA imeshiriki kuadhimisha siku ya Wafanyakazi katika ngazi za Mikoa kupitia ofisi za Mikoa za Kivipimo.

Uongozi wa WMA unaendelea kuwahimiza watumishi wake kufanya kazi kwa weledi na kuhakikisha wanatoa huduma sahihi kwa wananchi kwa kusimamia matumizi sahihi ya Vipimo katika sekta mbalimbali.





CRJE–UDSM PARTNERSHIP PUTS STUDENTS TO THE TEST IN REAL-WORLD BRIDGE CHALLENGE

May 01, 2026 Add Comment

  

Mr. Zhang Cuishan, Deputy General Manager of CRJE

By Prosper Makene 

CRJE (East Africa) Ltd opened the gates of its Mbezi Beach project site on Thursday to host faculty and students from the University of Dar es Salaam’s College of Engineering and Technology (CoET) for a full-day Site Open Day and Youth Bridge Skills Challenge. 

MZUMBE YAUNGANISHA WATAFITI NA JAMII KUKABILI ATHARI ZA TABIANCHI NA CHANGAMOTO ZA MAJI

April 30, 2026 Add Comment
Farida Mangube Morogoro

Juhudi za kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi na changamoto za upatikanaji wa maji zimepata msukumo mpya kufuatia kuimarishwa kwa ushirikiano kati ya watafiti na jamii kupitia mradi wa kimataifa wa ICP Connect na Lab to Life.

Oryx Gas Tanzania Yaimarisha Upatikanaji wa Nishati Safi Kupitia Maduka Maalum

April 30, 2026 Add Comment
Na Mwandishi Wetu

KAMPUNI ya Oryx Gas Tanzania imesema mkakati wake ni kuendelea kuunga mkono juhudi za Serikali kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia huku pia ikisisitiza umuhimu wa elimu ya mara kwa mara kwa watumiaji ili wawe na uelewa namna bora ya kutumia nishati safi ya kupikia.

TANZANIA NA JAPAN KUFUNGUA MILANGO MIPYA YA UWEKEZAJI KATIKA SEKTA YA NISHATI

April 30, 2026 Add Comment


Ushirikiano kati ya Tanzania na Japan katika sekta ya nishati unaingia hatua mpya, huku juhudi zikielekezwa zaidi katika kuvutia uwekezaji wa sekta binafsi na teknolojia za kisasa za uzalishaji umeme.

Hatua hiyo imebainishwa jijini Dar es Salaam leo tarehe 30 Aprili,2026 wakati Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati anayeshughulikia Mafuta na Gesi Asilia,Dkt.  James Mataragio alipokutana na Mwakilishi Mkuu mpya wa Japan International Cooperation Agency, Dkt. Kuge Katsuya.

Katika kikao hicho Dkt. Mataragio ameweka wazi Mkakati wa Serikali kuifanya sekta ya nishati kuwa kivutio kikubwa cha mitaji ya kimataifa hususan kutoka Japan.

Amesema  kuwa pamoja na historia ndefu ya ushirikiano kati ya nchi hizo mbili, hatua inayofuata inapaswa kulenga uwekezaji mkubwa zaidi unaoweza kuongeza uzalishaji na upatikanaji wa nishati nchini.

“Huu ni wakati wa kuhamasisha kampuni binafsi na taasisi za kifedha kutoka Japan kuja kuwekeza moja kwa moja katika miradi ya nishati Tanzania,” amesisitiza.

Akizungumzia ushirikiano wa Tanzania na Japan Dkt. Mataragio amesema JICA imekuwa mdau wa muda mrefu katika sekta ya nishati nchini na wameshiriki katika miradi ya  Uandaaji wa Mpango kabambe wa Matumizi ya Gesi Asilia Nchini (Natural Gas Utilization Master Plan -NGUMP),  wametoa fursa za kuwajengea uwezo wataalamu katika Matumizi ya gesi asili pamoja na utekelezaji wa Miradi mbalimbali ya umeme.

Aidha Dkt. Mataragio amembushia ahadi ya muda mrefu ya Japan ya kuwezesha Mradi wa umeme wa megawati 300 mkoani Mtwara.

Kwa upande wake, Dkt. Kuge ameashiria mwelekeo mpya wa ushirikiano utakaojikita katika Mafunzo ya teknolojia ya nishati ya nyuklia, Uzalishaji wa umeme kupitia gesi asilia kwa ufanisi mkubwa zaidi na Kuunganisha Tanzania na wawekezaji binafsi kutoka Japan

Ahadi hiyo inaashiria uwezekano wa Tanzania kunufaika na teknolojia za kisasa zaidi za nishati kutoka Japan, moja ya nchi zinazoongoza duniani katika ubunifu wa nishati.

Mkutano huo umeonesha wazi kuwa ushirikiano kati ya Tanzania na Japan hauishii katika misaada, bali sasa unaelekea kwenye uwekezaji mkubwa na ubadilishanaji wa teknolojia  hatua inayoweza kubadilisha kabisa sekta ya nishati nchini

RAIS SAMIA ATAMBULIWA KUWA KINARA WA NISHATI SAFI YA KUPIKIA AFRIKA

April 30, 2026 Add Comment




📌 Mawaziri wa nchi wanachama wa Umoja wa Afrika wapendekeza Rais Samia kutangazwa rasmi

Umoja wa Afrika umetambua juhudi za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, katika kuendeleza na kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia ndani na nje ya nchi, na kumpendekeza kutangazwa rasmi kuwa kinara wa Umoja wa Afrika wa ajenda hiyo.

Hatua hiyo imefikiwa katika Mkutano wa 5 wa Mawaziri wa Nchi wanachama wa Umoja wa Afrika wanaoshughulikia Nishati na Uchukuzi uliofanyika jijini Johannesburg, Afrika Kusini, tarehe 30 Aprili 2026. Katika mkutano huo Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi, ameongoza ujumbe wa Tanzania katika ngazi ya Mawaziri.

Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan ametambuliwa na kupendekezwa kuwa kinara wa Afrika kutokana na mchango wake mkubwa katika kusukuma sera, mikakati na ushirikiano wa kimataifa unaolenga kupanua upatikanaji wa nishati safi ya kupikia, kupunguza athari za kiafya na kimazingira, pamoja na kuboresha maisha ya waafrika, hususan wanawake na watoto.

Akizungumza katika mjadala kuhusu Programu ya Nishati Safi ya Kupikia Afrika, Waziri Ndejembi amesema kuwa mafanikio ya Tanzania katika sekta hiyo yametokana na uongozi madhubuti wa Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kusukuma ajenda ya nishati safi ya kupikia ndani na nje ya nchi.

Amesema kuwa chini ya uongozi wa Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, nishati safi ya kupikia imepewa kipaumbele cha kitaifa na kuingizwa katika Dira ya Taifa ya 2050, ikiwa ni sehemu muhimu ya maendeleo ya kijamii na kiuchumi.

Katika juhudi za kimataifa, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan ameendelea kuhamasisha agenda ya nishati safi ya kupikia kupewa kipaumbele katika mipango ya mataifa mbalimbali kupitia majukwaa ya kimataifa ikiwemo mkutano wa COP28 mwaka 2023, pamoja na Mkutano wa Nishati Safi ya Kupikia Barani Afrika uliofanyika Paris mwaka 2024, ambapo zaidi ya dola za Marekani bilioni 2.2 ziliahidiwa kusaidia sekta hiyo.

Kutokana na hatua hiyo ya mapendekezo ya Mawaziri yaliyoanzia katika ngazi ya wataalamu wa Umoja wa Afrika, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan anatarajiwa kuthibitishwa na kutangazwa rasmi kuwa Kinara wa Umoja wa Afrika wa Nishati Safi ya Kupikia katika Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Umoja wa Afrika utakaofanyika.




WATUMISHI PBPA WAHAMASISHWA KUPIMA AFYA NA KUPATA CHANJO YA HOMA YA INI

April 30, 2026 Add Comment

 

Daktari Johnson Katanga kutoka Taasisi ya Saratani Ocean Road (OCR) amewahimiza watumishi wa Wakala wa Uagizaji Mafuta kwa Pamoja (PBPA) kujitokeza kupima afya zao na kupata chanjo ya kujikinga na maambukizi ya *ugonjwa wa Homa ya Ini* (Hepatitis B).


Wito huo umetolewa leo wakati wa zoezi la utoaji elimu ya afya, upimaji wa hiari pamoja na utoaji wa chanjo dhidi ya *ugonjwa wa Hepatitis B* lililofanyika katika ukumbi wa PBPA jijini Dar es Salaam.

Akizungumza katika zoezi hilo, Dkt. Katanga alieleza kuwa chanjo ya Hepatitis B hutolewa kwa awamu tatu, ambapo dozi ya kwanza hutolewa *mara* baada ya mhusika kupimwa *na kuthibitika kuwa kuwa hana maambukizi* , dozi ya pili hutolewa baada ya mwezi mmoja, na dozi ya tatu hutolewa miezi sita tangu kupokea dozi ya kwanza.

Alifafanua kuwa chanjo hiyo ilianza kutolewa kwa watoto nchini tangu mwaka 2002 ikiwa sehemu ya chanjo za kawaida zinazotolewa mara baada ya kuzaliwa. Kutokana na hali hiyo, watu waliozaliwa mwaka 2001 na kurudi nyuma wanashauriwa kupata chanjo hiyo endapo hawajawahi kuipata.

Kuhusu dalili, Dkt. Katanga alisema *u* mgonjwa wa homa ya ini mara nyingi haoneshi dalili katika hatua za awali, hali inayosababisha watu wengi kugundua maambukizi wakiwa tayari wameathirika kwa kiwango kikubwa. Alitaja baadhi ya dalili zinazoweza kujitokeza baadaye kuwa ni pamoja na uchovu uliokithiri, maumivu ya tumbo upande wa juu kulia, *macho na ngozi kuwa na rangi ya njano* , kupoteza hamu ya kula, mkojo kuwa mweusi, kinyesi cheupe, pamoja na kuvimba kwa miguu au tumbo.

Aidha, alieleza kuwa maambukizi ya virusi hivyo yanaweza kutokea kupitia njia mbalimbali ikiwemo kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto, ~wakati wa kujifungua~ , kujamiiana bila kinga, kugusana na damu au majimaji ya mwili wa mtu mwenye ~yenye~ maambukizi, kushirikiana vitu vyenye ncha kali kama sindano, pamoja na kuongezewa damu iliyoathiriwa.

“Takwimu zinaonesha kuwa takribani watu milioni 254 duniani wanaishi na virusi vya homa ya ini, huku nchini Tanzania kiwango cha maambukizi kikikadiriwa kuwa asilimia 4. Hali hii ~Hii~ inaonesha umuhimu wa kuchukua hatua mapema,” alisisitiza.

Aliongeza kuwa endapo maambukizi hayatagunduliwa mapema, kati ya asilimia 5 hadi 6 ya waathirika huingia katika hatua ya ugonjwa sugu (chronic), hali inayoweza kusababisha madhara makubwa ikiwemo saratani ya ini.

Kwa upande wake, Kaimu Meneja wa Rasilimaliwatu~Utumishi~ wa PBPA, Bw. Matiko Sanawa, alisema kuwa utoaji wa elimu hiyo ni sehemu ya utekelezaji wa maelekezo ya Serikali kupitia Waraka wa Utumishi Na. 2 wa mwaka ~2024~2014 unaosisitiza umuhimu wa kulinda afya za watumishi kazini.

Alisema mwajiri ana jukumu la kuhakikisha watumishi wanakuwa na afya njema ili waweze kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi na kuchangia maendeleo ya taifa.

“Tumewaalika wataalamu kutoka Taasisi ya Saratani Ocean Road ili kutoa elimu, kufanya upimaji wa hiari na kutoa chanjo. Hii ni hatua muhimu katika kuhakikisha watumishi wanakuwa na afya bora,” alisema Bw. Sanawa.
Huu ni Mkakati wa Serikali wa kuimarisha huduma za kinga dhidi ya magonjwa yasiyoambukiza na ya kuambukiza, kwa kuhamasisha uchunguzi wa mapema na utoaji wa chanjo.