HABARI

SIASA

ELIMU

Recent Posts

MWENGE WAPITA NYASA,MRADI WA REA WA BILIONI 4 WAZINDULIWA

May 16, 2026 Add Comment


*📌Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa aridhishwa na miradi ya REA*


📍Nyasa - Ruvuma


Wananchi wa Kitongoji cha Ndecha Wilaya ya Nyasa mkoani Ruvuma wameanza kushuhudia mwanga wa matumaini baada ya kuzinduliwa rasmi kwa mradi wa REA kwa gharama ya zaidi ya shilingi bilioni 4.17 wa kusambaza umeme unaotekelezwa kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA), mradi ambao unatarajiwa kuleta mageuzi makubwa ya kiuchumi na kijamii kwa wananchi wa eneo hilo.


Mradi huo umezinduliwa leo tarehe 16 Mei, 2026 na Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa, Ndugu  Wazo Michael Mwang’onda, ambaye amesema kuwa dhamira ya Serikali ni kuhakikisha wananchi wa vijijini wanapata huduma bora za nishati ili kuboresha maisha yao na kuchochea maendeleo ya Taifa.


Halikadhalika Bw. Mwang'onda  amewataka wananchi kutumia nafasi hiyo ya mradi kulipa shilingi 27,000 tu ili waweze kuwekewa umeme huo. 


“Tunataka kuona wananchi wanalipia 27,000 ili wawekewe umeme hata ukiuza kuku mmoja 27,000 unaenda kuweka umeme kwenye nyumba yako sio 300,000 kama ilivyokuwa hapo zamani'' amesema Kiongozi wa Mwenge kitaifa. 

Kwa upande wake, Msimamizi wa Miradi ya REA Mkoa wa Ruvuma, Mha. Hamisi  Mrope, amesema mradi wa kusambaza umeme vijijini (REDP2C) katika Wilaya ya Nyasa unalenga kufikisha huduma ya umeme katika vitongoji vyote ili kuinua maisha ya wananchi na kuchochea maendeleo ya kiuchumi na kijamii.

Aidha, Mha. Mrope amesema mradi huo ulianza rasmi tarehe 16 Novemba 2023 na unatarajiwa kukamilika  ifikapo mwezi Oktoba, 2026, huku ukihusisha vitongoji 30, mashine umba 30 pamoja na wateja 1,247 kwa gharama ya zaidi ya shilingi bilioni 4.17.

Katika Kitongoji cha Ndecha pekee, mradi umehusisha ujenzi wa kilomita 8.43 za njia ya umeme, ufungaji wa mashine umba mbili pamoja na kuunganisha wateja 94 kwa gharama ya zaidi ya shilingi milioni 307.6. Hadi sasa, miundombinu imekamilika kwa asilimia 100 huku wananchi 56 tayari wakiwa wameunganishiwa huduma ya umeme kwa gharama nafuu ya shilingi 27,000 kwa kila mteja.


Mradi huo unatekelezwa na Mkandarasi mzawa MF Electrical Engineering Ltd chini ya usimamizi wa TANESCO.

Naye, Mbunge wa jimbo  la Nyasa Mhe. John Nchimbi amesema miradi ya REA imesaidia kwa sasa vijiji vyote 84 vya wilaya Nyasa kupata huduma ya umeme huku Tanzana ikijivunia kuwa ya pili Afrika Mashariki kwa kusambaza umeme.


Kwa upande wake, Mkandarasi wa mradi huo MF Electrical Engineering Ltd mhandisi Mussa David amesema mradi huo kwa kitongoji cha Ndecha 1 wameshafikisha umeme na wameshawasha nyumba 56.

Wananchi wa Ndecha wameeleza furaha yao kutokana na ujio wa umeme ambapo mwenyekiti wa kijiji cha Linda Antony Nkoma amesema  sasa wataweza kufanya shughuli zao za kiuchumi kwa ufanisi zaidi tofauti na zamani walipotegemea taa za vibatari na vyanzo vya nishati visivyo salama.


Uzinduzi wa mradi huo umeonekana kuwa hatua muhimu katika safari ya kuwaletea wananchi maendeleo endelevu huku ukiunga mkono kaulimbiu ya Mwenge wa Uhuru 2026 isemayo:


“Tanzania ni Yetu Sote, Tushikamane kwa Pamoja Kuleta Maendeleo.”


Mwisho

SERIKALI KUIMARISHA NISHATI YA UMEME WILAYANI KONDOA

May 16, 2026 Add Comment




Katika jitihada za kuendeleza ustawi wa wananchi na kuchochea uchumi wa maeneo ya vijijni na vitongojini, Serikali inaendelea kuimarisha upatikanaji wa umeme wilayani Kondoa kupitia mpango wa kusambaza umeme katika vitongoji vyote vya wilaya hiyo.


 Mpaka sasa vitongoji 113 vina umeme huku kukiwa na mradi unaoendelea wa kupeleka umeme katika vitongoji 60.


Hayo yameelezwa leo Mei 16, 2026 na Naibu Waziri wa Nishati Mhe. Salome Makamba wakati wa ziara ya kikazi ya Waziri Mkuu Mhe. Dkt Mwigulu Nchemba wilayani Kondoa, Dodoma.

Mhe. Salome ameeleza kwamba katika mradi wa umeme unaotekelezwa sasa wa kusambaza umeme katika vitongoji 60 zaidi ya shilingi billion 21 imetengwa kuhakikisha mradi huo unakamilika ambapo kukamilika kwake kutafanya  Kondoa kubakiwa na vitongoji 88 tu ambavyo havina umeme  vitakavyofikiwa na huduma hiyo ifikapo mwaka 2030.


Pia Mhe Salome ameeleza kwamba Serikali imetenga zaidi ya shilingi milioni 752 kwa ajili ya  kuhakikisha wananchi ambao miradi ya umeme inapita karibu na nyumba zao  wanafikiwa na huduma ya umeme katika kaya zao.


Ameongeza kuwa katika Wilaya ya Kondoa,  Wizara ya Nishati ina mpango wa kubadilisha nguzo zote chakavu na kupeleka nguzo za zege ili kuhakikisha wilaya hiyo inakuwa na nishati ya umeme ya uhakika ili wananchi waendelee kufanya shughuli zao za kiuchumi kama vile uendeshaji wa viwanda vidogo na shughuli za kijamii.

Vilevile amesema Serikali ina mpango mahsusi kujenga laini kubwa ya umeme ili kuimarisha na kutatua changamoto ya nguvu ya umeme (Low Voltage katika Jimbo la Kondoa).


Katika hatua nyingine, Mhe. Salome amewaasa wananchi kuendelea kutumia nishati safi ya kupikia akieleza kuwa pamoja na jitihada zinazofanywa na Wananchi Kondoa  kutunza misitu bado wanatakiwa kuilinda kwa kuachana na matumizi ya Kuni na mkaa na kuhamia katika matumizi ya nishati safi ya kupikia kama vile gesi, umeme na mkaa mbadala 


“Niwahakikishie wanakondoa sasa hivi Serikali imeweka ruzuku katika mitungi ya gesi, hivyo niwaombee sana tuanze kutumia Nishati safi kwa ajili ya kulinda  afya, mazingira na kuokoa muda wa kukaa jikoni ili tuweze kujiendeleza kiuchumi lakini pia tutumie nishati nyingine kama mkaa mbadala usiotoa moshi ambapo utatumia mkaa kidogo kupika chakula kingi na katika hali iliyo bora zaidi." Amesisitiza  Mhe Salome.

TANZANIA NI NCHI YA PILI AFRIKA KUWA NA HADHI YA UTALII WA JIOLOJIA (GEOPARK MUSEUM)

May 16, 2026 Add Comment
-Ni kutokana na kuwa na hadhi ya Ngorongoro Lengai UNESCO Global Geopark;

DKT. KOMBA: TEHAMA NI MSINGI WA ELIMU YA KISASA

May 16, 2026 Add Comment
NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

TAASISI ya Elimu Tanzania (TET) imezindua maabara za kompyuta katika Shule ya Sekondari Kimara pamoja na Shule ya Msingi Mkwawa jijini Dar es Salaam ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 50 ya taasisi hiyo na jitihada za kuimarisha matumizi ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) katika sekta ya elimu.

DKT.MIGIRO AIMARISHA USHIRIKIANO KIMATAIFA NA MABALOZI WA CUBA, VIETNAM, NA UN

May 16, 2026 Add Comment
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi, Dkt. Asha-Rose Migiro, kwa nyakati tofauti amekutana na kufanya mazungumzo na mabalozi wawili wanaoziwakilisha nchi zao katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

KAPINGA: SERIKALI YA RAIS SAMIA INAENDELEA KUBORESHA ELIMU, AFYA NA KILIMO MBINGA VIJIJINI

May 16, 2026 Add Comment
Mbunge wa Jimbo la Mbinga vijijini na Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe. Judith Kapinga amesema Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan, inaendelea kuleta mageuzi makubwa katika sekta za elimu na afya hasa maeneo ya Jimbo hilo kupitia utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo.

BODI YA TVLA YARIDHISHWA NA KASI YA UJENZI WA MAABARA YA KISASA DODOMA

May 16, 2026 Add Comment
Daudi Nyingo – DODOMA

Bodi ya Ushauri ya Wakala ya Maabara ya Veterinari Tanzania (TVLA) imeeleza kuridhishwa kwake na maendeleo ya mradi mkubwa wa ujenzi wa jengo la ofisi na maabara ya kisasa unaotekelezwa katika Kituo cha Kanda ya Kati jijini Dodoma ambapo Mradi huo wenye ghorofa nne unategemewa kuwa mradi kielelezo nchini utakapokamilika.

TBS inaadhimisha nusu karne,Inajivunia mafanikio ya utekelezaji wa majukumu yake kwa ufanisi

May 15, 2026 Add Comment
NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Viwango Tanzania (TBS), Dkt. Ashura Katunzi, amesema katika kipindi cha miaka 50 Shirika hilo limefanikiwa kujenga na kusimamia mifumo ya udhibiti ubora na usalama wa bidhaa nchini hatua iliyosaidia kuongeza tija katika uchumi na sekta ya Viwanda na Biashara kwa ujumla.

SERIKALI YAISIFU CRDB KWA KUKUZA UWEKEZAJI WA VIJANA

May 15, 2026 Add Comment

 



Na Mwandishi Wetu, Arusha.

Serikali imeipongeza Benki ya CRDB Bank Plc kwa juhudi zake za kuhamasisha uwekezaji nchini kupitia elimu ya fedha, uwekezaji wa hisa na uwezeshaji wa kiuchumi unaolenga kuwajenga vijana kuwa wawekezaji wa baadaye.

Pongezi hizo zimetolewa jana jijini Arusha na Waziri wa Fedha, Khamis Mussa Omar wakati akifungua Semina ya Wanahisa wa Benki ya CRDB iliyofanyika sambamba na Mkutano Mkuu wa 31 wa mwaka wa benki hiyo katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Arusha (AICC).

Semina hiyo ilikuwa na kaulimbiu isemayo “Vijana na Uwekezaji kwenye Hisa” na iliwakutanisha viongozi wa serikali, wanahisa, wataalamu wa masoko ya mitaji pamoja na vijana kutoka maeneo mbalimbali nchini.

Akizungumza katika semina hiyo, Waziri Omar alisema vijana wanapaswa kushiriki kikamilifu katika umiliki wa uchumi kupitia uwekezaji badala ya kutegemea ajira pekee.

“Kaulimbiu ya mwaka huu imebeba ujumbe mkubwa wa kimkakati kwa taifa letu. Vijana hawapaswi kuishia kutafuta ajira pekee, bali wanastahili kushiriki katika umiliki wa uchumi kupitia uwekezaji,” alisema Waziri Omar.

Aidha, aliipongeza benki hiyo kwa hatua ya kufungua Ofisi ya Uwakilishi Dubai, akisema hatua hiyo imeongeza hadhi ya Tanzania katika sekta ya fedha na uwekezaji kimataifa.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela alisema benki hiyo itaendelea kuwawezesha vijana kupitia huduma za kifedha, ubunifu na programu za maendeleo ya ujasiriamali.

Alisema kupitia CRDB Bank Foundation na programu ya IMBEJU, maelfu ya vijana na wafanyabiashara wadogo wamefikiwa kwa mafunzo, mitaji na ushauri wa biashara.

“Tunaamini vijana wa leo si wateja tu wa benki yetu, bali ni wawekezaji, wabunifu na viongozi wa uchumi wa kesho,” alisema Dkt. Nsekela.

Naye Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya CRDB, Neema Mori alisema uwekezaji katika hisa ni njia muhimu ya kujenga ustawi wa kifedha wa muda mrefu kwa vijana na familia za Kitanzania.

Profesa Mori alisema mafanikio ya Benki ya CRDB yanaonyesha namna uwekezaji wa muda mrefu unavyoweza kuleta matokeo chanya kwa wanahisa.

Alibainisha kuwa ndani ya miaka mitatu iliyopita thamani ya hisa za benki hiyo imeongezeka kwa zaidi ya asilimia 253, huku bei ya hisa ikifikia wastani wa Sh2,800 kutoka Sh460 mwaka 2023.

Aidha, alisema bodi ya wakurugenzi inapendekeza gawio la Sh90 kwa kila hisa kutokana na matokeo mazuri ya kifedha ya mwaka 2025, ikiwa ni ongezeko la asilimia 38 ikilinganishwa na mwaka uliopita.

Profesa Mori aliwahamasisha wazazi kuanza kuwawekezea watoto wao hisa mapema ili kuwajengea msingi imara wa maisha ya kifedha ya baadaye.

Benki ya CRDB ni miongoni mwa taasisi kubwa za kifedha Afrika Mashariki na Kati, ikiwa na zaidi ya wateja milioni sita katika nchi za Tanzania, Burundi na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo pamoja na ofisi ya uwakilishi Dubai, Falme za Kiarabu.
Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), akizungumza wakati akifungua Semina ya Wanahisa wa Benki ya CRDB katika Mkutano Mkuu wa 31 wa Wanahisa, uliobeba kauli mbiu ya “Vijana na Uwekezaji kwenye Hisa”, semina inayofanyika katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Arusha (AICC), ambapo alitoa wito kwa Taasisi za Fedha nchini kupunguza riba na gharama nyingine za mikopo ili kuwawezesha wananchi wakiwemo vijana kupata mitaji ya kuwekeza kwenye shughuli zao za kiuchumi.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dkt. Abdulmajid Nsekela, akizungumza wakati wa hafla ya ufunguzi wa Semina ya Wanahisa wa Benki ya CRDB katika Mkutano Mkuu wa 31 wa Wanahisa hao, uliobeba kauli mbiu ya “Vijana na Uwekezaji kwenye Hisa”, uliofunguliwa na Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb) (hayupo pichani), uliofanyika katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Arusha (AICC).
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya CRDB, Prof. Neema Mori, akizungumza wakati wa hafla ya ufunguzi wa Semina ya Wanahisa wa Benki ya CRDB katika Mkutano Mkuu wa 31 wa Wanahisa hao, uliobeba kauli mbiu ya “Vijana na Uwekezaji kwenye Hisa”, uliofunguliwa na Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb) (hayupo pichani), uliofanyika katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Arusha (AICC).









MRADI WA BARRICK-TWIGA FUTURE FORWARD EDUCATION KUBORESHA SEKTA YA ELIMU TANZANIA

May 15, 2026 Add Comment

Meneja Mkazi wa Barrick nchini Dkt. Melkiory Ngido (kulia) akiweka Jiwe la Msingi la Ujenzi wa Mabweni mawili, vyumba vitano vya madarasa na vyoo matundu nane shule ya sekondari Nyang'hwale
Meneja Mkazi wa Barrick nchini Dkt. Melkiory Ngido (kulia) akiwa na viongozi mbalimbali wakati wa hafla ya uwekaji Jiwe la Msingi la Ujenzi wa Mabweni mawili, vyumba vitano vya madarasa na vyoo matundu nane shule ya sekondari Nyang'hwale.
Muonekano wa sehemu ya madarasa
Muonekano wa sehemu ya vyoo
Meneja Mkazi wa Barrick nchini Dkt. Melkiory Ngido (kulia) akizungumza wakati akiweka Jiwe la Msingi la Ujenzi wa Mabweni mawili, vyumba vitano vya madarasa na vyoo matundu nane shule ya sekondari Nyang'hwale.

TADB YATOA GAWIO LA BILIONI 8.38 KWA SERIKALI

May 15, 2026 Add Comment
Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) imetoa gawio la shilingi Bilioni 8.38 kwa serikali ikiwa ni ongezeko la Asilimia 50 kutoka shilingi Bilioni 5.58 ya mwaka 2024, katika Mkutano Mkuu wa wanahisa kwa mwaka ulioishia 31 Desemba 2025.

TBS YASHIRIKI MKUTANO WA 28 WA VIWANGO AFRIKA MASHARIKI

May 15, 2026 Add Comment
Shirika la Viwango Tanzania (TBS) limeshiriki Mkutano wa 28 wa Kamati ya Viwango Afrika Mashariki (EASC) uliofanyika Makao Makuu ya Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) jijini Arusha kuanzia Mei 12 hadi 14, 2026, kwa lengo la kutekeleza mpango kazi wa viwango, upimaji, metrolojia na ubora wa bidhaa (SQMT).

NAIBU KATIBU MKUU FEDHA AAGIZA UJENZI WA MCHAKATO WA UTEKELEZAJI WA MAJUKUMU (BUSINESS PROCESSES) ZA KIDIGITALI

May 15, 2026 Add Comment

Mkurugenzi wa Idara ya Usimamizi wa Mali za Serikali, Wizara ya Fedha, Bw. Chotto Sendo, akizungumza kwa niaba ya Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Fedha, Bw. Nsubili Joshua, wakati akifungua mafunzo kwa Menejimenti ya Wizara kuhusu Mwongozo wa Udhibiti wa Ndani wa Wizara ya Fedha, yaliyofanyika katika Hotel ya Morena mkoani Morogoro.

Meza Kuu ikiongozwa na Mkurugenzi wa Idara ya Usimamizi wa Mali za Serikali, Wizara ya Fedha, Bw. Chotto Sendo (katikati), Kaimu Mkaguzi wa Ndani Mkuu wa Serikali, Wizara ya Fedha, Bw. Kenneth Nindie (kushoto), na Mhasibu Mkuu Wizara ya Fedha Fungu 21 CPA. Sostheness Mafuru (kulia) wakifuatilia mawasilisho mbalimbali yaliyotolewa na Wawezeshaji kutoka Kampuni ya Ushauri (KPMG) wakati wa mafunzo ya Mwongozo wa Udhibiti wa Ndani wa Wizara ya Fedha, yaliyohusisha Menejimenti ya Wizara ya Fedha na Watumishi wa Wizara hiyo yaliyofanyika katika Hotel ya Morena mkoani Morogoro.

Mkaguzi Mkuu wa Ndani wa Wizara ya Fedha CPA, Evalisto Mwalongo, akitoa utambulisho wakati wa mafunzo ya Mwongozo wa Udhibiti wa Ndani wa Wizara ya Fedha, yaliyohusisha Menejimenti ya Wizara ya Fedha na Watumishi wa Wizara hiyo yaliyofanyika katika Hotel ya Morena mkoani Morogoro.

Baadhi ya viongozi wa Idara, Vitengo na Watumishi wa Wizara ya Fedha, wakifuatilia hotuba ya mgeni rasmi (hayupo pichani), wakati wa mafunzo ya Mwongozo wa Udhibiti wa Ndani wa Wizara ya Fedha, yaliyohusisha Menejimenti ya Wizara ya Fedha na Watumishi wa Wizara hiyo yaliyofanyika katika Hotel ya Morena mkoani Morogoro.

Baadhi ya Watumishi wa Wizara ya Fedha wakifuatilia hotuba ya mgeni rasmi (hayupo pichani), wakati wa mafunzo ya Mwongozo wa Udhibiti wa Ndani wa Wizara ya Fedha, yaliyohusisha Menejimenti ya Wizara ya Fedha na Watumishi wa Wizara hiyo yaliyofanyika katika Hotel ya Morena mkoani Morogoro.

Meza kuu ikiongozwa na Mkurugenzi wa Idara ya Usimamizi wa Mali za Serikali, Wizara ya Fedha, Bw. Chotto Sendo (katikati), Kaimu Mkaguzi wa Ndani Mkuu wa Serikali, Wizara ya Fedha, Bw. Kenneth Nindie (kulia), na Mhasibu Mkuu Fungu 21 Wizara ya Fedha, CPA. Sostheness Mafuru (kushoto) wakiwa katika picha ya pamoja na Menejimenti ya Wizara ya Fedha baada ya kumalizika kwa mafunzo ya Mwongozo wa Udhibiti wa Ndani wa Wizara ya Fedha, yaliyohusisha Menejimenti ya Wizara ya Fedha na Watumishi wa Wizara hiyo yaliyofanyika katika Hotel ya Morena mkoani Morogoro.

Meza kuu ikiongozwa na Mkurugenzi wa Idara ya Usimamizi wa Mali za Serikali, Wizara ya Fedha, Bw. Chotto Sendo (katikati), Kaimu Mkaguzi wa Ndani Mkuu wa Serikali, Wizara ya Fedha, Bw. Kenneth Nindie (kulia), na Mhasibu Mkuu Fungu 21, Wizara ya Fedha CPA. Sostheness Mafuru (kushoto) wakiwa katika picha ya pamoja na Watumishi wa Wizara ya Fedha baada ya kumalizika kwa mafunzo ya Mwongozo wa Udhibiti wa Ndani wa Wizara ya Fedha, yaliyohusisha Menejimenti ya Wizara ya Fedha na Watumishi wa Wizara hiyo yaliyofanyika katika Hotel ya Morena mkoani Morogoro.

Meza kuu ikiongozwa na Mkurugenzi wa Idara ya Usimamizi wa Mali za Serikali, Wizara ya Fedha, Bw. Chotto Sendo (katikati), Kaimu Mkaguzi wa Ndani Mkuu wa Serikali, Wizara ya Fedha Bw. Kenneth Nindie (kulia), na Mhasibu Mkuu Fungu 21 Wizara ya Fedha CPA. Sostheness Mafuru (kushoto) wakiwa katika picha ya pamoja na Sekretarieti ya maandalizi, baada ya kumalizika kwa mafunzo ya Mwongozo wa Udhibiti wa Ndani wa Wizara ya Fedha, yaliyohusisha Menejimenti ya Wizara ya Fedha na Watumishi wa Wizara hiyo yaliyofanyika katika Hotel ya Morena mkoani Morogoro.

(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, WF, Morogoro)


Na. Chedaiwe Msuya, WF, Morogoro


Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Fedha, Bw. Nsubili Joshua, amekiagiza Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini cha Wizara ya Fedha kuratibu ujenzi wa mchakato wa utekelezaji wa majukumu (business processes) za kidigitali ili kuongeza ufanisi wa utekelezaji wa majukumu ya Wizara.

Maagizo hayo yametolewa kwa niaba yake na Mkurugenzi wa Idara ya Usimamizi wa Mali za Serikali, Wizara ya Fedha, Bw. Chotto Sendo, wakati akifungua mafunzo mafunzo ya Mwongozo wa Udhibiti wa Ndani wa Wizara ya Fedha, kwa
Menejimenti ya Wizara hiyo, yaliyofanyika katika Hotel ya Morena mkoani Morogoro.

Alisema business processes mpya zinazotakiwa ni pamoja na ufuatiliaji wa Mfumo wa Ununuzi (NeST), ufuatiliaji na udhibiti wa mapato kupitia big data analysis, ufuatiliaji wa miradi ya PPP, miradi ya alternative financing, ulipaji wa michango ya Serikali kwenye taasisi za kimataifa, na ufuatiliaji wa mapato yasiyo ya kodi.

Aidha, Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini (M&E) kimetakiwa kuhakikisha kuwa business processes hizo zinajengwa kwa mfumo wa kielektroniki ili kurahisisha ufuatiliaji na tathmini ya utekelezaji wa majukumu ya Wizara ili kuimarisha uwajibikaji, uwazi na ufanisi wa mifumo ya kiutendaji.

Bw. Sendo, alifafanua kuwa mafunzo hayo yataiwezesha Menejimenti na Watumishi wa Wizara kuelewa dhana na mbinu za udhibiti wa ndani, kujifunza namna ya kuchambua viashiria hatarishi, na kuimarisha business processes zilizopo.

“Mwongozo huu utakuwa na manufaa makubwa ikiwemo kuimarisha mifumo ya ufuatiliaji na tathmini kwa njia za kidigitali, kuwezesha Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani kufanya tathmini kwa mujibu wa Mwongozo wa Kimataifa wa Ukaguzi wa Ndani wa mwaka 2024, na kuweka vigezo vya kupima ufanisi wa mifumo ya kiutendaji”, alisisitiza Bw. Sendo.

Aliwasisitiza washiriki wa mafunzo hayo kufuatilia kwa umakini ili kuutumia Mwongozo huo kuboresha mfumo wa udhibiti wa ndani katika maeneo yao ya kazi ili kuimarisha uchumi wa taifa kupitia usimamizi bora wa rasilimali za umma.

Naye Kaimu Mkaguzi wa Ndani Mkuu wa Serikali, Wizara ya Fedha, Bw. Kenneth Nindie, alitoa rai kwa Idara zote za Serikali kuhakikisha wanatumia vizuri Mwongozo huo ili uweze kuwasaidia kuweka taratibu vizuri na malengo ya Wizara yanafikiwa kwa ufasaha.

Kwa upande wake, Mkaguzi Mkuu wa Ndani wa Serikali Msaidizi Bw. Abraham Msechu, amesema kuwa mafunzo yatasaidia Menejimenti ya Wizara kupata uelewa wa Mwongozo wa Udhibiti wa Ndani na kuimarisha mifumo ya udhibiti wa ndani.

Akizungumzia mafunzo hayo mmoja wa washiriki, Kamishna Msaidizi Idara ya Usimamizi wa Madeni, Wizara ya Fedha, Bw. Omary Khama, aliahidi kuyafanyia kazi mafunzo yote waliyopata katika Idara na Vitengo ili kufikia malengo ya Serikali katika udhibiti wa ndani.


Mafunzo hayo yamewajumuisha Menejimenti ya Wizara ya Fedha pamoja na Watumishi wa Wizara na Wawezeshaji kutoka Kampuni ya Ushauri (KPMG).