HABARI MPYA
HABARI
SIASA
ELIMU
Recent Posts
REA YANG'ARA SABASABA 2026
🏆 *RAIS MWINYI ASHUHUDIA REA IKITWAA TUZO YA MUONESHAJI BORA WA TAASISI ZA SERIKALI*
🤝 *REA YAWASHUKURU WADAU KWA MCHANGO WAO KATIKA MAFANIKIO HAYO*
📍 Dar es Salaam
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, ameshuhudia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) ukitwaa Tuzo ya Muoneshaji Bora wa Taasisi za Serikali (*Government Institutions Exhibitor*) katika kilele cha Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba) 2026.
Tuzo hiyo imepokelewa na Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano na Mawasiliano kwa Umma wa REA, Bi. Martha Chassama, kwa niaba ya Wakala.
REA inawashukuru wadau wote waliotembelea banda lake, kujionea mafanikio na utekelezaji wa miradi ya nishati vijijini, pamoja na kuendelea kuunga mkono jitihada za Wakala za kupeleka nishati ya umeme kwenye vitongoji.
Mwisho
NEEC YALETA ELIMU YA MITAJI KARIBU NA WANANCHI RUKWA
MHANDISI MRAMBA ATEMBELEA BANDA LA TANESCO SABASABA
Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati (Umeme na Nishati Jadidifu), Mhandisi Felchesmi Mramba, ametembelea Banda la Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), na kampuni zake Tanzu katika Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam (Sabasaba), ambayo leo yanafikia kilele katika Viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere, jijini Dar es Salaam.
Mha.Mramba ametembelea banda hilo ili kuona huduma mbalimbali zinazotolewa kwa wananchi wanaotembelea banda hilo.
RAIS MWINYI ATEMBELEA BANDA LA NISHATI SABASABA
NishatiRais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, akisalimiana na Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati, Mhandisi Felchesmi Mramba mara baada ya kufika katika Banda la Wizara ya Nishati katika kilele cha Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam (Sabasaba), yanayofanyika katika Viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere, jijini Dar es Salaam.
Kushoto kwa Katibu Mkuu ni Mkurugezi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania ( TANESCO), Lazaro Twange.
MHANDISI MRAMBA ATEMBELEA BANDA LA WIZARA YA NISHATI SABASABA
Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati (Umeme na Nishati Jadidifu), Mhandisi Felchesmi Mramba, ametembelea Banda la Wizara ya Nishati katika Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam (Sabasaba), ambayo leo yanafikia kilele katika Viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere, jijini Dar es Salaam.
Akiwa katika banda la Wizara, Mhandisi Mramba amepata maelezo kutoka kwa wataalam wa Wizara ya Nishati kuhusu elimu inayoendelea kutolewa kwa wananchi wanaotembelea maonesho hayo.
Elimu hiyo inahusu huduma zinazotolewa na Wizara na Taasisi zake pamoja na fursa mbalimbali zilizopo katika sekta ya nishati, ikiwemo umeme, mafuta, gesi asilia, nishati jadidifu na nishati safi ya kupikia, sambamba na hatua zinazochukuliwa na Serikali kuboresha upatikanaji wa huduma za nishati nchini.
MHANDISI MRAMBA AVUTIWA NA KASI YA REA KUSAMBAZA UMEME KWENYE VITONGOJI
NishatiKatibu Mkuu wa Wizara ya Nishati (Umeme na Nishati Jadidifu) Mha. Felchesmi Mramba ameipongeza Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa utekelezaji wa miradi ya umeme vijijini pamoja na mafanikio ya usambazaji umeme kwenye vitongoji.
Mha. Mramba amesema hayo leo Julai 13, 2026 alipotembelea banda la REA kwenye Kilele cha maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba)
ELIMU YA UTOAJI WA MIKOPO KWA MAKUNDI MAALUM IONGEZEKE - RABIA
Viongozi wa Serikali wameshauriwa kuongeza Elimu ya utoaji na urejeshaji wa mikopo ya asilimia 10, ambayo katika bajeti ya mwaka 2026/2027 itakuwa asilimia 15.
Hayo yameelezwa leo Julai 12,2026 na Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, Idara ya Mambo ya Siasa na Uhusiano wa Kimataifa Ndg Rabia Abdalla Hamid katika muendelezo wa ziara yake ya Kusikiliza na kutatua changamoto za Makundi mbalimbali ya kijamii mkoani Rukwa.
“Nitoe rai kwa Viongozi wa serikali kuhakikisha Elimu ya utoaji na urejeshaji wa mikopo ya asilimia 10,ambayo katika bajeti ya mwaka 2026/2027 itakuwa asilimia 15 inatolewa kwa kasi ili wananchi wawe na uelewa mpana katika masuala ya fedha na walengwa waendelee kunufaika ”,amesema Ndugu Rabia.
.jpeg)


































.jpeg)


.jpeg)

.jpeg)









