HABARI

SIASA

ELIMU

Recent Posts

MWENYEKITI WA CCM MKOA TANGA AINGILIA KATI KUINUSURU KLABU YA AFRICAN SPORTS ISISHUKE DARAJA

April 12, 2026 Add Comment

 

Na Oscar Assenga,Tanga

Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Tanga, Rajab Abdurhaman  ameanza jitihada za kuinusuru Klabu ya African Sports ambayo ipo hatarini kushuka daraja kufuatia matokeo mabaya katika Ligi ya Championship.

Rajab aliyasema hayo baada ya kukutana na wachezaji pamoja na viongozi wa klabu hiyo, ambapo alieleza kuwa hali ya timu si ya kuridhisha, akifananisha na mgonjwa aliye katika chumba cha mahututi.

Alibainisha kuwa kwa sasa African Sports inashika nafasi ya 15 kati ya timu 16, hali inayoiweka katika hatari kubwa ya kushuka daraja endapo haitafanya vizuri katika mechi zilizobaki.

Akizungumzia historia ya klabu hiyo, alisema ni moja ya timu zenye heshima kubwa nchini na mshindani wa jadi wa Coastal Union, hivyo ni muhimu kurejesha ushindani wa soka la Tanga.

Katika hatua ya kuokoa timu hiyo, Mwenyekiti huyo  alitangaza kuchangia Shilingi milioni 20 ambazo tayari alikwisha kuziweka kwenye akauti, huku Mbunge wa Jimbo la Tanga akiahidi kutoa milioni tano na mdau mwingine kuahidi milioni 20, ikiwa ni sehemu ya kufikia lengo la kukusanya milioni 45 zinazohitajika kuiwezesha timu kumaliza msimu salama.

Alisema atahakikisha fedha hizo zinapatikana ili kutatua changamoto zinazoikabili klabu hiyo na kuwawezesha wachezaji kucheza kwa utulivu.

Aidha, aliwataka wachezaji kujituma katika mechi zilizobaki ili kuinusuru timu, akisisitiza kuwa wana dhamana ya kulinda heshima ya klabu hiyo.

Kwa upande mwingine, aliwashauri viongozi wa klabu kuweka mikakati ya muda mfupi na mrefu, ikiwemo kutovunja kambi mara baada ya msimu kumalizika ili kuboresha maandalizi ya msimu ujao.

Aliongeza kuwa mabadiliko ya mara kwa mara ya kikosi na maandalizi hafifu yamekuwa yakichangia kushuka kwa kiwango cha timu, na kusisitiza kuwa kwa mipango madhubuti wanaweza kurejea Ligi Kuu katika msimu ujao.






BARAZA LA WAFANYAKAZI INEC LAKUTANA

April 12, 2026 Add Comment

 

Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na wenye Ulemavu), Dkt. James Henry Kilabuko (wapili kulia) akishiriki kuimba Wimbo wa Wafanyakazi wakati wa ufunguzi wa Barala la Wafanyakazi wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi lililokutana leo Aprili 11, 2026 mkoani Morogoro. Wengine pichani ni Mwenyekiti wa Baraza hilo na Mkurugenzi wa Uchaguzi wa INEC, Ramadhani Kailima (wapili kushoto), Katibu wa Baraza, Livini Avith (kulia) na Kulia ni mtumishi wa Tume, Rose Tengu. (Picha na INEC).
Sehemu ya wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi la Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi wakishiriki kuimba Wimbo wa Wafanyakazi wakati wa ufunguzi wa Kikao cha Barala la Wafanyakazi  INEC lililokutana leo Aprili 11, 2026 mkoani Morogoro. (Picha na INEC).

DC SUMAYE - NMB KIJIJI DAY NI HATUA MUHIMU YA KUWAFIKIA WANANCHI WA VIJIJINI KUWAPATIA ELIMU YA FEDHA

April 12, 2026 Add Comment



Na Oscar Assenga, Lushoto

Mkuu wa Wilaya ya Lushoto, Zephania Sumaye, ameishukuru Benki ya NMB Bank Plc kwa kuandaa tukio la kipekee la Kijiji Day, akisema ni hatua muhimu katika kuwafikia wananchi vijijini na kuwapatia elimu ya kifedha.

Akizungumza kwa niaba ya Waziri wa TAMISEMI, Prof. Riziki Shemdoe ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Lushoto (CCM), alisema kuwa wizara ina malengo mahsusi ya miaka mitano, likiwemo kuhakikisha wananchi wanapata uhuru wa kiuchumi.

Alisisitiza kuwa uhuru huo hauwezi kupatikana bila wananchi kujihusisha na taasisi za kifedha, ikiwemo benki kama NMB.

Alieleza kuwa tukio la Kijiji Day ni sehemu ya utekelezaji wa malengo hayo, kwani linawawezesha wananchi kupata elimu ya kifedha pamoja na huduma mbalimbali za kibenki moja kwa moja walipo.

Tukio hilo lilifanyika katika Kata ya Magamba, ambapo wananchi walipata fursa ya kujifunza na kunufaika na huduma zinazotolewa na benki hiyo.

Aidha, alisema moja ya malengo ya serikali ni kuhakikisha jamii ya Lushoto inaunganishwa na kuwa kitu kimoja.

Alibainisha kuwa njia mojawapo ya kuimarisha mshikamano huo ni kupitia michezo na mabonanza, kama ilivyofanyika katika tukio hilo ambapo NMB ilitumia siku nzima kushirikiana na wananchi wa Kijiji cha Magamba.

Alisisitiza umuhimu wa elimu kwa maendeleo ya mwanadamu, akieleza kuwa hata katika mafundisho ya dini mbalimbali, elimu imepewa kipaumbele kikubwa.

Alifananisha juhudi za NMB na msemo usemao: “Usimpe mtu samaki, mfundishe kuvua.” Akasema benki hiyo inafanya kazi kubwa kwa kuwafundisha wananchi namna ya kutumia huduma za kifedha kwa ufanisi, badala ya kuwapatia msaada wa moja kwa moja bila uelewa.

Aliongeza kuwa kama benki zingetoa mikopo bila elimu ya matumizi sahihi, matokeo yasingekuwa endelevu,Hivyo, matukio kama Kijiji Day yanafungua njia ya kuwafikia wananchi, kuwapa elimu na kuwasogezea huduma za kifedha karibu zaidi.

Aliwahimiza NMB kuendelea na juhudi hizo pamoja na kuandaa mabonanza yatakayoongeza furaha, mshikamano na uelewa wa wananchi kuhusu huduma zao, jambo litakalosaidia kujenga imani na umiliki wa wananchi kwa benki hiyo.

Katika tukio hilo la Kijiji Day lililofanyika Magamba, shughuli mbalimbali zilifanyika ikiwemo mbio za marathon, huduma ya chakula, pamoja na mabonanza mengine. Lengo kuu lilikuwa ni kuwafikia wananchi, kuwapa elimu ya kifedha na kuwajengea uelewa mpana kuhusu huduma za benki.

Awali akizungumza Meneja wa Kanda ya Kaskazini wa NMB Bank Plc, Baraka Ladislaus, amesema benki hiyo inaendelea kusogeza huduma za kifedha karibu na wananchi kupitia matamasha ya Kijiji Day yanayofanyika vijijini.

Alisema lengo la mpango huo ni kuwafikia wananchi walipo, kuwapatia elimu ya kifedha na kuwaunganisha na huduma mbalimbali za kibenki ili kuwawezesha kiuchumi.

Alieleza kuwa pamoja na elimu ya kifedha, tukio hilo linaambatana na shughuli za kijamii ikiwemo upandaji miti kwa kushirikiana na Taifa Gas, ikiwa ni sehemu ya juhudi za kuhifadhi mazingira na kuifanya Tanzania kuwa ya kijani.

Aidha, alisema NMB ina mtandao mpana wa mawakala zaidi ya 80,000 nchi nzima wanaotoa huduma karibu asilimia 60 ya mahitaji ya kifedha ya wananchi, sambamba na matumizi ya magari maalum ya kibenki yanayowafikia wananchi vijijini.

Aliongeza kuwa benki hiyo imeboresha huduma zake za kidijitali ikiwemo programu ya NMB Mkononi, inayorahisisha upatikanaji wa huduma kwa wateja popote walipo.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Lushoto Whitney Mwinzagi aliwataka wananchi kutumia vyema elimu wanayoipata na kuelekeza mikopo wanayoipata kuitumia shughuli za uzalishaji mali badala ya matumizi yasiyo na tija.











FEDHA ZA CSR ZA BARRICK BULYANHULU KUENDELEA KULETA MAENDELEO HALMASHAURI YA WILAYA YA NYANG’HWALE

April 12, 2026 Add Comment

Meneja wa Mahusiano ya Jamii na Mazingira wa Mgodi wa Barrick Bulyanhulu , Bw Agapiti Paul (kushoto) akibadilishana mkataba wa utekelezaji wa miradi ya maendeleo kupitia (CSR) Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Nyang’hwale, John Isack (kulia) wengine pichani ni maofisa waandamizi wa halmashauri hiyo.
Meneja wa Mahusiano ya Jamii na Mazingira wa Mgodi wa Barrick Bulyanhulu , Bw. Agapiti Paul akiongea katika hafla ya kusaini mkataba wa utekelezaji wa miradi ya maendeleo kupitia (CSR) katika Halmashauri ya Wilaya ya Nyang’hwale.
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Nyang’hwale, John Isack akiongea katika hafla ya kusaini mkataba wa utekelezaji wa miradi ya maendeleo kupitia (CSR) katika Halmashauri ya Wilaya ya Nyang’hwale.
Meneja wa Mahusiano ya Jamii na Mazingira wa Mgodi wa Barrick Bulyanhulu , Bw Agapiti Paul akisaini mkataba.

#Mgodi kutoa shilingi milioni 900 kwa utekelezaji wa miradi ya mwaka huu

Uwekezaji wa kampuni ya Barrick nchini yenye ubia Serikali nchini kupitia kampuni ya Twiga unazidi kuleta manufaa kwa wananchi ambapo mgodi wa Barrick Bulyanhulu uliopo wilayani Msalala na Nyang’hwale umesaini mkataba na Halmashauri ya Wilaya ya Nyang’hwale ambapo katika kipindi cha mwaka huu utatoa kiasi cha shilingi milioni 900 za uwajibikaji kwa jamii (CSR) kwa ajili ya kufanikisha miradi mbalimbali ya maendeleo.

RC MBONI MHITA AONGOZA TAMASHA LA MWANAMKE CHUMA 2026, ASISITIZA UJASIRI NA UMOJA

April 12, 2026 Add Comment


Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Mboni Mhita akikata keki katika  Tamasha la Mwanamke Chuma Msimu wa Tano
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Mboni Mhita akikata keki na kuzindua kikundi cha Wanawake Chuma katika Tamasha la Mwanamke Chuma Msimu wa Tano -Picha - Malunde


Mamía ya wanawake wamejitokeza kushiriki Tamasha la Mwanamke Chuma Msimu wa Tano lililofanyika Aprili 11, 2026 katika Ukumbi wa Malex uliopo Kahama, mkoani Shinyanga, huku wito ukitolewa kwa wanawake kushirikiana na kuinua wenzao ili kufikia mafanikio ya pamoja.

Mgeni rasmi katika tamasha hilo alikuwa Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Mboni Mhita, aliyesisitiza umuhimu wa mshikamano, uthubutu na kujiamini kwa wanawake katika harakati za maendeleo binafsi na ya jamii.

Akizungumza katika tamasha hilo, Mhita amewataka wanawake kuacha hofu ya maneno ya watu na badala yake kuzingatia malengo yao kwa vitendo.

DKT AKWILAPO AKUTANA NA MTENDAJI MKUU WA SHELTER AFRIQUE

April 12, 2026 Add Comment

 Na Munir Shemweta, WANMM Nairobi


Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Dkt Leonard Akwilapo, amekutana na kufanya mazungumzo na Afisa Mtendaji Mkuu wa Shelter Afrique Bw. Thierno-Habib Hann jijini Nairobi, nchini Kenya.

Viongozi hao wawili wamekutana pembezoni mwa Kongamano la Miji Afrika (2nd Africa Urban Forum) lililofanyika kuanzia Aprili 8 hadi 10, 2026 nchini Kenya, na kukutanisha mataifa mbalimbali Barani Afrika kwa lengo la kubadilishana uzoefu na suluhisho bunifu katika kukabiliana na changamoto za maendeleo ya miji na makazi.

Dkt Akwilapo na Bw.Thierno-Habib Hann katika kikao chao walijadili masuala mbambali yanayohusu uimarishaji wa upatikanaji wa makazi nafuu kwa wananchi pamoja na ushirikiano kati ya serikali na taasisi za kifedha katika kufanikisha azma hiyo.

Shelter Afrique ni taasisi ya kifedha ya kimataifa inayolenga kusaidia maendeleo ya makazi Barani Afrika, huku makao makuu yake makuu yakiwa jijini Nairobi nchini Kenya.
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Dkt Leonard Akwilapo (Kulia) akizungumza na Mtendaji Mkuu wa Shelter Afrique Bw.Thierno-Habib Hann jijini Nairobi, Kenya walipokutana pembezoni mwa Kongamano la pili la Miji Afrika (2ND Africa Urban Forum) lilofanyika nchini humo.
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Dkt Leonard Akwilapo (Kushoto) na Mtendaji Mkuu wa Shelter Afrique Bw.Thierno-Habib Hann wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kikao chao jijini Nairobi, Kenya, walipokutana pembezoni mwa Kongamano la pili la Miji Afrika lilofanyika nchini humo.
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Dkt Leonard Akwilapo (Kulia) akitambulishwa baadhi ya maafisa wa taasisi ya Shelter Afrique alipokutana na Mtendaji Mkuu wa taasisi hiyo Bw.Thierno-Habib Hann pembezoni mwa Kongamano la pili la Miji Afrika (2nd Africa Urban Forum) lilofanyika jijini Nairobi nchini Kenya. (PICHA ZOTE NA WIZARA YA ARDHI)

AMAN NI MSINGI WA UTALII: JOHN MALECELA AWATAKA WANANCHI KUILINDA ILI KUKUZA SEKTA YA UTALII

April 12, 2026 Add Comment




MAKAMU wa Rais na Waziri Mkuu mstaafu, John Samuel Malecela amesema kuwa, swala la Utalii kokote Duniani linaenda sambamba na swala la Amani na Utulivu na kuwaomba wananchi kuhakikisha wanalinda Amani ili kukuza Utalii nchi na kuendelea kujinufaisha kupitia sekta hiyo. 


Malecela alitoa kauli hiyo jana wakati wa Uzinduzi wa tamasha la Same Utalii festival lililofanyika katika viwanja vya stendi wilayani Same mkoani Kilimanjaro ambapo alisema kuwa, utalii ni kite ambacho huchangia kuleta fedha za kigeni. 

Alisema kuwa, baadhi ya nchi ulimwenguni serikali zinaendeshwa kwa fedha za Utalii na kuwataka kulichukulia swala hilo kwa umakini mkubwa. 


Kiongozi huyo alidai kuwa, misingi ya Utalii ni ukarimu kwa wageni na kuwataka wananchi wa wilaya ya Same kuwa mfano katika ukarimu ili kukuza Utalii wa wilaya ya Same. 

"Hata sehemu kukiwa na njiwa 10,000  wamejaa lakini jiwe likigonga tu wote wanakimbia kwa hiyo na sisi utalii wetu uanze na sisi wenyewe Watanzania kuwa na Amani ni jambo la msingi sana kwani Amani ndio italeta na kuwakaribisha watalii na ndio itatufanya tuendelee kukua kiuchumi" Alisema Malecela. 


Na kuongeza "Swala la ukarimu kwa wageni ni kitu muhimu sana mahali pengine watu hawaendi kwa sababu hakuna moyo wa kuwapokea wageni lakini kwetu same tuwe na moyo wa kuwapokea wageni ili kukuza utalii wetu".


Alisema kuwa, kinachotuunga pamoja ni Amani na kuwasihi Watanzania kuendelea kuitunga na mambo mengine yatafuata. 


"Ili Utalii wa same uweze kukua ni lazima uanze na sisi wenyewe wanasama kuwa na moyo dhabiti wa ukarimu ili wanapokuja na kurudi wakatoe sifa ni kweli wataenda kuona wanyama lakini mkiwakaribisha kwa moyo upande hawatarudi tena" Alisema Malecela.

WAZIRI KOMBO KUTANA NA WAZIRI WA MAMBO YA NJE WA SEYCHELLES

April 12, 2026 Add Comment


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Mahmoud Thabit Kombo(Mb), amekutana na kuzungumza na Waziri wa Mambo ya Nje na Diaspora wa Jamhuri ya Seychelles Mhe. Barry Faure pembezoni mwa Mkutano wa Tisa Bahari ya Hindi jijini Port Louis, Mauritius Aprili 11,2026.

Kikao hicho, kililenga kuangalia njia za kuendelea kuimarisha uhusiano uliopo kati ya Tanzania na Seychelles ambapo viongozi hao pia walijadili masuala mbalimbali ya maslahi ya pamoja ikiwemo ushirikiano wa kisiasa, kiuchumi, na amani ya kikanda.

Tanzania na Seychelles zinashirikiana katika maeneo ya biashara na uwekezaji. Bidhaa kuu zinazouzwa Nje ni pamoja na misumari, pini ndogo (tacks), pini za kuchomelea misumari ya bati vikolezo na bidhaa zinazofanana, bidhaa za chuma au chuma kigumu, nati nazi na korosho ambapo bidhaa kuu zinazoagizwa ni nguo, samaki wa jamii ya jodari, na jodari aina ya skipjack.

Kuhusu uwekezaji katika kipindi cha kuanzia 2014 hadi 2024 Tanzania na Seychelles zimekuwa zikishirikiana katika ujenzi wa majengo ya biashara na viwanda na hivyo kusababisha ajira nchini. Tanzania na Seychelles pia zimekuwa zikishirikiana katika eneo la ulinzi na usalama pamoja na masuala ya magereza.

Mawaziri hao walielezea dhamira ya kutumia matokeo ya kikao chao kuendelea kuimarisha ushirikiano katika maeneo ya biashara, utalii na usalama, kwa lengo la kukuza maendeleo na kudumisha amani, utulivu na usalama katika ukanda wa Bahari ya Hindi.



WAZIRI MKUU MSTAAFU JOHN MALECELA TULINDE AMANI YETU KUKUZA SEKTA YA UTALII

April 11, 2026 Add Comment

 


SAME. 

MAKAMU wa Rais na Waziri Mkuu mstaafu, John Samuel Malecela amesema kuwa, swala la Utalii kokote Duniani linaenda sambamba na swala la Amani na Utulivu na kuwaomba wananchi kuhakikisha wanalinda Amani ili kukuza Utalii nchi na kuendelea kujinufaisha kupitia sekta hiyo. 

Malecela alitoa kauli hiyo jana wakati wa Uzinduzi wa tamasha la Same Utalii festival lililofanyika katika viwanja vya stendi wilayani Same mkoani Kilimanjaro ambapo alisema kuwa, utalii ni kite ambacho huchangia kuleta fedha za kigeni. 

Alisema kuwa, baadhi ya nchi ulimwenguni serikali zinaendeshwa kwa fedha za Utalii na kuwataka kulichukulia swala hilo kwa umakini mkubwa. 

Kiongozi huyo alidai kuwa, misingi ya Utalii ni ukarimu kwa wageni na kuwataka wananchi wa wilaya ya Same kuwa mfano katika ukarimu ili kukuza Utalii wa wilaya ya Same. 

"Hata sehemu kukiwa na njiwa 10,000  wamejaa lakini jiwe likigonga tu wote wanakimbia kwa hiyo na sisi utalii wetu uanze na sisi wenyewe Watanzania kuwa na Amani ni jambo la msingi sana kwani Amani ndio italeta na kuwakaribisha watalii na ndio itatufanya tuendelee kukua kiuchumi" Alisema Malecela. 

Na kuongeza "Swala la ukarimu kwa wageni ni kitu muhimu sana mahali pengine watu hawaendi kwa sababu hakuna moyo wa kuwapokea wageni lakini kwetu same tuwe na moyo wa kuwapokea wageni ili kukuza utalii wetu".

Alisema kuwa, kinachotuunga pamoja ni Amani na kuwasihi Watanzania kuendelea kuitunga na mambo mengine yatafuata. 

"Ili Utalii wa same uweze kukua ni lazima uanze na sisi wenyewe wanasama kuwa na moyo dhabiti wa ukarimu ili wanapokuja na kurudi wakatoe sifa ni kweli wataenda kuona wanyama lakini mkiwakaribisha kwa moyo upande hawatarudi tena" Alisema Malecela.






KIKWETE STEPS IN: AU ENVOY OFF TO A PROMISING START IN SOUTH SUDAN PEACE EFFORT

April 11, 2026 Add Comment

 

 Former Tanzanian President Dr. Jakaya Mrisho Kikwete, now serving as High Representative of the African Union Chairperson to the Horn of Africa and the Red Sea, on Friday met with President Salva Kiir Mayardit of South Sudan in Juba as he wrapped up a high-level two-day mission to the country engaging key national, regional and international actors in efforts to restabilize the country. He also met with other key Ministers to assess progress and challenges in implementing the Revitalized Agreement on the Resolution of Conflict in South Sudan (R-ARCSS) signed in 2018.



Special Reporter, JUBA, South Sudan

 

In a significant diplomatic push to revive momentum in South Sudan’s fragile peace process, former Tanzanian President Jakaya Mrisho Kikwete has wrapped up a high-level two-day mission to Juba, engaging key national, regional and international actors in efforts to restabilize the country.

 

Kikwete, now serving as High Representative of the African Union Chairperson to the Horn of Africa and the Red Sea, met with President Salva Kiir Mayardit and other key Ministers to assess progress and challenges in implementing the Revitalized Agreement on the Resolution of Conflict in South Sudan (R-ARCSS) signed in 2018.

 

At the State House, President Kiir reassured the envoy that the peace agreement remains on track, dismissing claims of its collapse. He outlined ongoing efforts by the Revitalised Government of the National Unity (RTGoNU) to encourage and advance inclusive dialogue among various parties, both signatories and non-signatories to the R-ARCSS in order to reach consensus on critical issues leading up to the elections scheduled for December 2026, as declared in the communique by the African union High Level Ad Hoc Committee for South Sudan (C5) Plus Summit held in the margins of the 39th Ordinary AU Summit Addis Ababa, Ethiopia in February 2026.

 

The government also used the occasion to express gratitude for continued African Union support while calling on the international community to allow space for homegrown solutions to take root.

 

In a statement issued by the State House in Juba following the meeting betwee President Kiir and the experienced Envoy, a key takeaway highlighted was the commitment by the Govermnent to proceed with the election process so that to not only avoid yet another extension to the December deadline, but also to heed the desire by the Sudanese people to finally go to the ballot for the first time since the country attained its independence in 2011.

 

Going beyond the government corridors, Kikwete’s visit also provided a valuable platform to voices from across the South Sudanese political spectrum. He held consultations with leaders of the ruling Sudan People's Liberation Movement (SPLM - IG), opposition parties including representatives of the Sudan People's Liberation Movement - in Opposition (SPLM - IO), and the South Sudan Opposition Alliance (SSOA) - which is an umbrella for various smaller political parties in the country. He also met with members from the civil society, faith-based organizations, and the academia - underscoring the inclusive approach employed by the envoy and which is commended by many as what was missing to ensure all voices are heard and no one is left behind in the process of rebuilding the conflict ridden youngest country in the continent.

 

In a voice note recorded and widely circulated by Edmund Yakani, Executive Director of Community Empowerment for Progress Organization (CEPO), the South Sudanese civil society activist and human rights advocate applauded the appointment of Former President Kikwete to the role as the envoy and urged him to work with all parties to ensure inclusive political dialogue, including bringing on board those with contentious positions who are inside and outside of South Sudan.

 

“Our people have paid a very expensive price through loss of life and property. We are confident of the Envoy through his experience in mediation and his knowledge of the South Sudanese issues. We hope that he will take up this responsibility wholeheartedly, embrace everyone and bring everyone to the table so that to nurture a pathway to transition and to sustainable peace” he said. He added that “ if some people and some parties are isolated, that will mark the beginning of yet another failure of the implementation of the resolution of the AU C5 Summit to empower the South Sudanese people to resolve their differences amicably”

 

Underscoring the desire of the international community and regional bodies to see peace and stability in South Sudan, the envoy also met with key international and regional stakeholders, including the Intergovernmental Authority on Development (IGAD), the United Nations Mission in South Sudan (UNMISS), and the Reconstituted Joint Monitoring and Evaluation Commission (RJMEC), as well as Ambassadors from of the European Union, Canada, Germany and the Troika countries of the United States of America,  United Kingdom and Norway.

 

The envoy also met with Vice President Rebecca Nyandeng De Mabior Garang, a prominent leader in the transitional government and a symbol of national unity who is a widow of Dr. John Garang De Mabior, the founder of the Sudan People’s Liberation Army (SPLA) and considered as Father of the South Sudanese Nation.

 

Kikwete’s return to the South Sudan peace file carries historical weight. In 2015, he played a pivotal role in brokering intra-party dialogue among various faction in the SPLM Party that led to the Arusha Peace Agreement - a foundation for subsequent peace efforts. His visit to Juba is preceded by visits to the President Cyril Ramaphosa of South Africa and President Yoweri Kaguta Museveni who are key guarantors to the peace process.

 

As South Sudan edges toward a critical electoral milestone, Kikwete’s mission signals renewed continental commitment to steering the young nation away from instability and toward a more durable peace.