




HABARI NA MATUKIO MBALIMBALI





Na Mwandishi wetu- Dodoma
Na Mwandishi Wetu- Dodoma
Kaimu Mkurugenzi wa Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania (TFNC) Bi. Debora Charwe amesema, Serikali ipo katika mchakato wa kuandaa Mpango wa Muda Mrefu wa Lishe wa Taifa (NN-LTP) ili kuongeza jitihada za sekta mtambuka katika kuboresha utekelezaji wa lishe kwa kipindi cha miaka 25 ijayo.
Bi. Debora ameyasema hayo leo tarehe 30 Juni, 2026 wakati akifungua Warsha ya mafunzo kuhusu kuandaa mpango wa muda mrefu wa lishe wa Taifa (National Nutrition Long Term Plan 2026-2050) ambayo inafanyika jijini Dodoma kwa siku tatu kuanzia Juni 30 hadi Julai 02, 2026
Amesema, mafunzo hayo yanatolewa kwa Wataalam kutoka ngazi ya Wizara mbalimbali kwa lengo la kuwajengea uwezo kuhusu uandaaji wa mipango ya muda mrefu wa lishe inayojumuisha sekta mtambuka pamoja na kubadilishana uzoefu kusaidia katika usanifu, muundo na taratibu za utekelezaji wa Mpango wa muda mrefu wa Lishe wa Taifa.
Vilevile Bi. Debora amefafanua kuwa, mpango huo unaandaliwa chini ya usimamaizi wa Ofisi ya Waziri Mkuu kwa kushirikiana na Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania (TFNC) na wadau wengine wa maendeleo kwa kuzingatia haja ya kuifanya lishe kuwa moja ya kichocheo na kipimo katika kufikiwa kwa malengo ya Dira ya Maendeleo ya Tanzania kufikia 2050.
Aidha, warsha hiyo imehusisha Afisa viungo wa lishe kutoka Wizara mbalimbali zikiwemo Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, Ofisi ya Rais Maendeleo ya Vijana, Ofisi ya Waziri Mkuu TAMISEMI, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Ajira na Mahusiano) pamoja na Wizara ya Kilimo, Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Wizara ya Viwanda, Wizara ya Maji na Wizara ya Mambo na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.
==MWISHO==

📌 Waziri Ndejembi amtaka mkandarasi kukamilisha ukarabati kwa wakati bila kuongezewa muda wa mkataba
📌 Kukamilika kwake kutaongeza ufanisi wa uzalishaji na kuimarisha upatikanaji wa umeme wa uhakika Mkoa wa Tanga na maeneo ya jirani
Na Mwandishi Wetu, Korogwe – Tanga
Serikali imeendelea kusimamia utekelezaji wa miradi ya ukarabati wa miundombinu ya umeme nchini, huku Mradi wa Ukarabati wa Kituo cha Kuzalisha Umeme cha Hale wilayani Korogwe, mkoani Tanga, ukifikia asilimia 83 ya utekelezaji.
Akikagua maendeleo ya Mradi huo tarehe 29 Juni, 2026 Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi (Mb), amemtaka mkandarasi kuhakikisha anakamilisha kazi ndani ya muda uliopangwa, akisisitiza kuwa Serikali haitakuwa tayari kuongeza muda wa mkataba wa utekelezaji wa mradi huo.
Waziri Ndejembi amesema kukamilika kwa ukarabati wa Kituo cha Hale kutaimarisha ufanisi wa uzalishaji wa umeme, kuongeza upatikanaji wa umeme wa uhakika na kuchochea shughuli za kiuchumi katika Mkoa wa Tanga na maeneo ya jirani.
“Mkandarasi ahakikishe anakamilisha mradi huu kwa muda uliopangwa ifikapo Julai 31 mwaka huu, ili wananchi waanze kunufaika na huduma ya umeme wa uhakika pamoja na kuimarisha maendeleo ya kiuchumi,” amesema Mhe. Ndejembi.
Kwa upande wake, Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa Usambazaji Umeme TANESCO, Mhandisi Timoth Mgaya, amesema mradi huo unagharimu dola za Kimarekani milioni 24.81, sawa na takribani shilingi bilioni 64, na hadi sasa umefikia asilimia 83 ya utekelezaji.
“Mradi huu unagharimu dola milioni 24.81 ambazo ni sawa na shilingi bilioni 64. Hadi sasa utekelezaji umefikia asilimia 83, na tunaendelea kushirikiana na mkandarasi kuhakikisha kazi zilizobaki zinakamilika ndani ya muda uliopangwa,” amesisitiza Mhandisi Mgaya
Mradi wa ukarabati wa Kituo cha Kuzalisha Umeme cha Hale unalenga kuongeza ufanisi wa kituo hicho, kuboresha utegemevu wa uzalishaji wa umeme na kuendelea kuimarisha upatikanaji wa huduma ya umeme wa uhakika kwa wananchi.
Kituo cha Kuzalisha Umeme cha Hale ni kituo cha kwanza cha kuzalisha umeme kwa kutumia maji nchini. Kilijengwa kati ya mwaka 1961 na 1964 na kina uwezo wa kuzalisha takribani megawati 21. Ukarabati unaoendelea unalenga kuongeza ufanisi wa kituo hicho ili kiendelee kutoa mchango mkubwa katika Gridi ya Taifa kwa miaka ijayo.

Morogoro, Tanzania – June 27, 2026_ — Dar es Salaam Merchant Group (DMG) has clinched the coveted _Best Maritime Technology Company of the Year_ award at the 2026 Morogoro Business Awards, cementing its position as a leader in Tanzania’s technological transformation of the blue economy.


