HABARI MPYA
HABARI
SIASA
ELIMU
Recent Posts
Kuelekea maadhimisho ya miaka 50 ya Shirika la Viwango TBS yawakaribisha wadau Viwango Marathon
habariRAIS SAMIA AUNDA TUME YA UCHUNGUZI WA KIJINAI VURUGU UCHAGUZI MKUU 2025 KUONGOZWA NA JAJI SHABANI LILA
habari 
Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameunda Tume ya Uchunguzi wa Kijinai wa Matukio ya Ghasia ya Wakati na Baada ya Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025.
Hatua hiyo imechukuliwa katika kutekeleza mapendekezo ya Tume ya Rais ya Kuchunguza Matukio ya Uvunjifu wa Amani yaliyotokea katika kipindi hicho cha uchaguzi.
Katika taarifa rasmi iliyotolewa leo tarehe 18 Mei, 2026 na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Dkt. Moses M. Kusiluka, Rais ameteua viongozi na wajumbe wa tume hiyo kwa kuzingatia mamlaka aliyonayo chini ya Sheria ya Tume za Uchunguzi, Sura ya 32.
Katika uteuzi huo, Jaji wa Mahakama ya Rufani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Shabani Ally Lila, ameteuliwa kuwa Kamishna na Mwenyekiti wa Tume hiyo.
Uzoefu wake katika mambo ya kisheria unatajwa kuwa nguzo muhimu katika kuongoza uchunguzi huo wa kijinai.
Aidha, Rais Samia ameteua majaji wastaafu watatu wa Mahakama Kuu ya Tanzania kuwa Makamishna wa tume hiyo ili kushirikiana na Mwenyekiti. Makamishna walioteuliwa ni Mhe. Gad John Mjemmas, Mhe. Awadh Mohamed Bawazir, pamoja na Mhe. Aishieli Nelson Sumari. Tume hii inatarajiwa kuanza kazi mara moja ili kuleta majibu na mapendekezo ya kisheria kuhusu ghasia hizo.
BARAZA LA MAWAZIRI LA EAC KUKUTANA KWA DHARURA JIJINI ARUSHA
habari
Maandalizi ya Mkutano wa 60 wa Dharura wa Baraza la Mawaziri la Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), unaotarajiwa kufanyika tarehe 22 Mei 2026, yameanza rasmi kupitia vikao vya ngazi ya wataalamu vinavyoendelea kuanzia tarehe 18 hadi 20 Mei 2026 katika Makao Makuu ya Jumuiya hiyo jijini Arusha.
Kikao hicho cha wataalamu kimepokea na kujadilia taarifa ya Kamati ya Fedha na Utawala kuhusu masuala ya fedha ya Jumuiya, na rasimu ya bajeti ya Sekretarieti ya EAC pamoja na taasisi zake kwa mwaka wa fedha 2026/2027. Mapendekezo yatakayopitishwa katika ngazi hiyo yatawasilishwa kwa Makatibu Wakuu watakaokutana tarehe 21 Mei, 2026 kabla ya kuwasilishwa katika Mkutano wa Baraza la Mawaziri utakaofanyika tarehe 22 Mei, 2026.

Vilevile, mkutano huo wa siku tano kuanzia tarehe 18 hadi 22 Mei, 2026 unalenga kuweka mikakati ya pamoja ya utekelezaji wa maelekezo na maamuzi yaliyotolewa na Mkutano wa 25 wa Wakuu wa Nchi za EAC, hususan katika maeneo ya mipango na fedha
Baraza la Mawaziri la EAC ni chombo kikuu cha maamuzi na kusimamia shughuli za Jumuiya, katika hatua hii ya maandalizi ya bajeti, Baraza hilo lina jukumu la kupokea, kuchambua, kufanya marekebisho na kuidhinisha makadirio ya mapato na matumizi ya Sekretarieti ya EAC kabla ya kuwasilishwa katika Bunge la Afrika Mashariki (EALA) kwa ajili ya kujadiliwa na kupitishwa rasmi.

Ujumbe wa Tanzania katika mkutano huo unajumuisha wajumbe kutoka Wizara ya Fedha, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora pamoja na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, ukionaongozwa na Mkurugenzi wa Sera na Mipango kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Justin Kisoka.



WAZIRI MCHENGERWA ANGOZA UJUMBE WA TZ WHA 79 GENEVA USWISI
afya
Na John Mapepele, Geneva, Uswisi
Waziri wa Afya Nchini, Mheshimiwa Mohamed Mchengerwa ameongoza ujumbe wa Serikali ya Tanzania katika ufunguzi rasmi wa Mkutano Mkuu wa 79 wa Shirika la Afya Duniani (WHA79) ulioanza leo Mei 18, 2026 mjini Geneva, Uswisi.
Mkutano huo mkubwa duniani katika sekta ya afya unashirikisha zaidi ya nchi 180 katika maeneo mbalimbali ulimwengu umefunguliwa na
Tedros Adhanom Ghebreyesus, Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Afya Duniani (WHO).

“Mkutano wa 79 wa Baraza la Afya Duniani (WHA79) unafanyika kuanzia tarehe 18 hadi 23 Mei 2026 mjini Geneva, Uswisi. Mkutano huu unawakutanisha wajumbe kutoka Nchi Wanachama wa WHO ili kushughulikia shinikizo kubwa linaloikabili mifumo ya afya na kuweka sera za afya za kimataifa, huku ukisisitiza sana huduma ya afya kwa wote, afya ya akili, na athari za mabadiliko ya tabianchi kwa afya.” Amefafanua Mheshimiwa Mchengerwa
Kwa mujibu wa Mheshimiwa Mchengerwa, maeneo makuu ya mjadala katika mkutano wa mwaka 2026 ni pamoja na:
Huduma ya Afya kwa Wote (UHC) na Ufadhili ambapo amesema Nchi wanachama na mashirika ya kiraia wanatoa kipaumbele kwa kuharakisha mifumo ya ufadhili wa afya inayoongozwa na nchi husika, mageuzi ya kidijitali katika mifumo ya afya, na kuhakikisha ushiriki wa kijamii ili kuimarisha mamlaka ya afya ya kitaifa.
Aidha amesisitiza eneo jingine linalopewa mkazo ni Afya ya Akili ambapo amesema kufuatia Mkutano wa Ngazi ya Juu wa Umoja wa Mataifa wa mwaka 2025 kuhusu Magonjwa Yasiyoambukiza (NCDs) na afya ya akili, WHA79 ina kampeni kubwa za utetezi na matukio maalum yanayolenga kutafsiri ahadi za kimataifa kuwa mikakati halisi ya kitaifa ya afya ya akili.
Jambo jingine litakalojadiliwa ni Tabianchi na Afya ambapo amefafanua kuwa ingawa si ajenda maalum ya pekee, athari zinazoendelea za mzozo wa tabianchi na matumizi ya mafuta ya kisukuku ni sehemu muhimu ya mijadala inayohusu afya ya uzazi, magonjwa yasiyoambukiza, na usimamizi wa magonjwa.

Amesem WHO pia inazindua mpango wa kimataifa wa utetezi uliokusudiwa kudumisha msukumo kuelekea mkutano ujao wa COP31 kuhusu tabianchi.
Mkakati wa Kimataifa na Uongozi: Wajumbe wanajadili namna ya kuoanisha mageuzi mbalimbali ya afya ya kimataifa ili kuhakikisha matokeo yenye usawa na uwajibikaji.
Aidha, mkutano huu unaweka msingi wa uchaguzi ujao wa Mkurugenzi Mkuu wa WHO, huku wagombea wakianza kutangazwa rasmi na kundi jipya la nchi likichaguliwa kuingia katika Bodi ya Utendaji.

Pia ameongeza kwamba mkutano huu pia utajadili taarifa na Mikakati ya Magonjwa ambapo ajenda ya muda ya mkutano inajumuisha hatua zinazoendelea kwa mpango wa kutokomeza malaria, Ajenda ya Chanjo 2030, na mkakati wa kumaliza ugonjwa wa kifua kikuu (TB).
Ujumbe wa Tanzania katika mkutano huu ulioongozwa na Mheshimiwa Mchengerwa umeshirikisha Mheshimiwa Balozi Abdala Possi, Mwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika Ofisi ya Umoja wa Mataifa na Mashirika Mengine ya Kimataifa Mjini Geneva, Mwenyekiti wa Kamati ya kudumu ya Afya na Ukimwi, Mheshimiwa, Dkt. Johannes Lukumay, Katibu Mkuu Dkt. Seif Shekalaghe, Mganga Mkuu wa Serikali
, Dkt. Grace Magembe na baadhi ya watendaji wa Wizara ya Afya.
Tanzania inatarajia kuwasilisha mawasilisho kadhaa katika mkutano huo na kufanya majadiliano na wadau mbalimbali wa afya pembezoni mwa mkutano huo.

AFUA ZA UKIMWI KUBORESHWA MKOA WA PWANI
habari 
Na, Mwandishi wetu – Pwani
Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Mhe. Abubakar Kunenge, amekutana na Katibu Mkuu wa Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu, Dkt. Jim Yonazi, katika ziara maalum ya kutembelea, kukagua na kutoa elimu katika Kituo cha Maarifa cha Mdaula kilichopo Chalinze, Mkoa wa Pwani.
Ziara hiyo imefanyika leo tarehe 18 Mei, 2026 ambapo Dkt. Yonazi alipata fursa ya kupokea taarifa ya maendeleo ya Mkoa wa Pwani, hususan katika utekelezaji wa Afua za masuala ya UKIMWI hasa huduma na mipango inayohusu WAVIU (Watu Wanaoishi na Virusi vya UKIMWI).
Taarifa hiyo ilieleza hatua mbalimbali zinazochukuliwa na Serikali pamoja na wadau wa maendeleo katika kuboresha huduma za afya na ustawi wa jamii kwa wananchi wa mkoa huo.
Aidha kwa upande wake amesema Serikali kwa sasa imeongeza bajeti katika hutuma za VVU na UKIMWI ii kungeza ufanisi zaidi katika kuwahudumia wananchi.
Zahanati ya Mdaula ilianza kutoa huduma za afya mwezi Oktoba mwaka 2022, ikiwa ni pamoja na huduma za wagonjwa wa nje, huduma za mama na mtoto, uzazi pamoja na huduma za chanjo kupitia kliniki tembezi. Kwa sasa, zahanati hiyo ina tawi dogo lililopo kandokando ya barabara ambalo linatoa huduma za maarifa ya jamii kwa wananchi na wasafiri wanaopita katika eneo hilo.
Tawi hilo lilifanyiwa maboresho na Tume ya Kudhibiti UKIMWI Tanzania (TACAIDS) kupitia Mradi wa SATTF uliokuwa unasimamiwa na TANROADS wakati wa utekelezaji wa ujenzi wake. Maboresho hayo yamelenga kuongeza ufanisi wa utoaji wa elimu na huduma zinazohusiana na mapambano dhidi ya maambukizi ya Virusi vya UKIMWI pamoja na huduma nyingine za afya ya jamii. 
TANESCO YATAKIWA KUBUNI TEKNOLOJIA MPYA KUBORESHA HUDUMA KWA WATEJA
NishatiNaibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba, ameielekeza TANESCO kuendelea kufanya tafiti na kubuni teknolojia mpya zitakazorahisisha utoaji wa huduma kwa wateja nchini.
Amesema dunia inabadilika kwa kasi kubwa hivyo Shirika hilo linapaswa kuendana na mabadiliko ya teknolojia ili kuongeza ufanisi na kuwafikia wananchi wengi zaidi kwa urahisi.
Akifungua mkutano wa mwaka wa Maafisa Uhusiano na Huduma kwa Wateja wa TANESCO unaofanyika mkoani Dodoma, Mhe. Salome amesema matumizi makubwa ya mifumo ya kidijitali pamoja na akili mnemba yatasaidia kuboresha mawasiliano na kupunguza changamoto zinazowakabili wananchi wanapohitaji huduma za umeme.
Aidha, ameagiza kufanyika kwa maboresho katika manunuzi ya vifaa pamoja na kuongeza uwezo wa vituo vya huduma kwa wateja ili kupunguza ucheleweshaji wa huduma.
Amesema hatua hizo zitasaidia kuongeza ufanisi wa kiutendaji na kuweka tabasamu kwa wananchi wanaotegemea huduma za TANESCO kila siku.
Mhe. Salome pia amesisitiza umuhimu wa ushirikiano kati ya idara mbalimbali ndani ya Shirika ikiwemo TEHAMA, usambazaji na huduma kwa wateja. Amesema huduma bora hutokana na ushirikiano mzuri wa watumishi wote katika kuhakikisha changamoto za wananchi zinatatuliwa kwa wakati.
Sambamba na hilo, amewataka maafisa hao kuendelea kuhamasisha matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia kwa kutumia majukwaa ya kidijitali na makundi ya kijamii kuwafikia wananchi wengi zaidi. Amesema matumizi ya umeme kama nishati safi ni salama, nafuu na yenye mchango mkubwa katika maendeleo ya taifa.
Career Guidance na mentorship kupewa nguvu mpya kupitia DUCE na GEL
habariMBUNGE AZZA HILLAL ATANGAZA MAKAO MAKUU YA OFISI YA MBUNGE ITWANGI, AKAGUA SHULE YA SEKONDARI NHUMBILI
habari
Mbunge wa Jimbo jipya la Itwangi Mhe. Azza Hillal Hamad akikagua ujenzi wa shule ya Sekondari Nhumbili katika kata ya Tinde Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga.

TUZO ZA KARIAKOO BUSINESS AWARDS KUCHOCHEA UKUAJI WA BIASHARA
habariNEMC, HALMASHAURI YA ILALA NA WADAU WA MAZINGIRA WASAFISHA FUKWE ZA DARAJA LA SALENDER
habariDAS TEMEKE AZINDUA OFISI YA WILAYA YA KITANESCO YA MIKWAMBE
Nishati
Katibu Tawala wa Wilaya ya Temeke Bw. Kimeta Mpui amezindua Ofisi mpya ya Wilaya ya KITANESCO Mikwambe ikiwa ni mkakati wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) wa kuendelea kuwahudumia na kusogeza huduma mbalimbali zinazotolewa na TANESCO karibu na wananchi.
Akizungumza Mei 16, 2026 wakati wa zoezi hilo amesema uzinduzi wa ofisi hiyo umelenga kuboresha utoaji wa huduma kwa wananchi kutokana na mahitaji ya msingi ya Nishati ya umeme kwa wananchi yanavyozidi kuongezeka kila kukicha.
Ameeleza kuwa hatua hiyo inaakisi maboresho ya kiutendaji yanayolenga kuongeza ufanisi na kupunguza changamoto ya umbali kwa wananchi ambao hapo awali walilazimika kufuata huduma katika ofisi za Mkoa wa KITANESCO Kigamboni.
Amesema TANESCO imefanya mabadiliko makubwa ili kuendana na ongezeko la mahitaji ya huduma ya umeme kutoka kwa wananchi hivyo ameipongeza TANESCO kwa kuanzisha ofisi hiyo nakuwataka wafanyakazi kuendelea kuimarisha utoaji wa huduma bora zaidi kwa wananchi.
“Napenda kuupongeza uongozi wa TANESCO kwa kuanzisha ofisi hii kwani ni kielelezo cha maboresho ya kiutendaji inayolenga kuongeza ufanisi na kupunguza kero na kuhakikisha wananchi wanapata huduma kwa wakati”
Akizungumza Kaimu Meneja Huduma kwa Wateja, Bw. Shamu Lameck, amesema TANESCO imejipanga kikamilifu na inaendelea kuimarisha na kusogeza huduma zake kwa wateja ili kuwarahisishia wananchi kupata huduma za umeme.
“Hii ni sehemu mhimu sana, ni ishara kwamba TANESCO tumedhamilia kwamba hali ya upatiakanaji wa umeme Kigamboni unaimarika na huduma yenyewe pia,tumejipanga kuhakikisha kwamba wananchi na wateja wetu tunawahudumia kwa ukaribu na ubora zaidi.
Kwa upande wake, Meneja wa TANESCO Mkoa wa Kigamboni Mhandisi Paschal Luhavi amesema kuwepo kwa ofisi hiyo ya TANESCO Wilaya ya Mikwambe kunakwenda kusogeza huduma zaidi kwa wananchi ndani ya wilaya hiyo hasa maeneo ya kata za Kimbiji, Somangila, Pemba Mnazi na Kisarawe II na maeneo jirani.




SERIKALI KUENDELEA KUIMARISHA UWEZO WA KUZUIA,KUJIANDAA,KUKABILIANA NA MAAFA
Na Mwandishi wetu- MBEYA
Serikali imeendelea kuimarisha uwezo wa Kitaifa wa Kuzuia, Kujiandaa, Kukabiliana na Kurejesha hali baada ya maafa ili kuhakikisha wananchi wanaishi katika mazingira salama ya kuepuka madhara makubwa yatokanayo na maafa.
Kauli hiyo imetolewa na Katibu Tawala Msaidizi Mipango na Uratibu Ofisi ya Mkoa wa Mbeya, Dkt. Noah Sikwese wakati akifunga mafunzo kwa Wajumbe Wateule wa Timu ya Kukabiliana na Dharura (RERT), Waatalamu wa Unendeshaji wa Kituo cha Operesheni na Mawasiliano ya Dharura (REOCC) katika Mkoa huo yaliyoandaliwa na Ofisi ya Waziri Mkuu kupitia Idara ya Menejimenti ya Maafa.
Dkt. Sikwese, amesema timu za kukabiliana na dharura zimejengewa msingi muhimu wa utendaji utakaowezesha Mkoa kuwa na uwezo wa kujiandaa na kukabiliana na matukio ya dharura kwa haraka na ufanisi mkubwa .
“Timu hizi zitahusika katika kufanya tathmini za awali na za kina wakati wa maafa kubaini mahitaji halisi ya waathirika, pamoja na kuratibu upatikanaji wa rasilimali muhimu kwa ajili ya kukabiliana na athari za maafa,” alisema Dkt. Sikwese.
Pia, aliongeza kwamba mafunzo yamekuwa nyenzo muhimu katika kujenga na kuimarisha uwezo wa kitaalamu na kiutendaji kwa watumishi wanaohusika katika Kituo cha Operesheni na Mawasiliano ya dharura.
“Kuanzishwa kwa Kituo cha Operesheni na Mawasiliano ya Dharura Mkoa wa Mbeya ni hatua muhimu katika kuimarisha uratibu wa shughuli za usimamizi wa maafa. Kituo hiki kitawezesha ufuatiliaji wa matukio kwa ukaribu, ukusanyaji na uchambuzi wa taarifa kwa wakati, pamoja na kuimarisha mawasiliano miongoni mwa wadau,” alieleza.
Sambamba na hilo Dkt. Sikwese alifafanua kuwa, utekelezaji wa mafunzo hayo ulianza katika Mikoa a Mwanza, Arusha, Dodoma, ambapo hatua za kuanzisha Vituo vya Operesheni na Mawasiliano ya Dharura pamoja na kuimarisha Timu za kukabiliana na maafa zilianza kutekelezwa.
“Ni matarajio yangu mafunzo haya yataongeza ufanisi, uwajibikaji, ustahimilivu dhidi ya majanga katika Mkoa wetu wa Mbeya,”aliongeza.
Aidha, alitoa wito kwa wataalamu wote waliopatiwa mafunzo kuendelea kuyafanyia kazi maarifa na stadi, kudumisha nidhamu ya kazi na kujenga utamaduani wa ushirikiano wa kitaalamu huku akiwasisitiza kuendelea kufanya mazoezi ya mara kwa mara ya uokoaji na utoaji wa huduma ya kwanza kwa majeruhi au waliofikwa na maafa.
“Usimamizi wa maafa ni jukumu letu sote, kila mmoja ashiriki sasa na kuchukua hatua katika eneo lake ili kuokoa na kulinda maisha, mali na mazingira,” alisisitiza Dkt. Sikwese.
Ikumbukwe kuwa Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu) kwa mujibu wa Sera ya Taifa ya Usimamizi wa Maafa yam waka 2004 (Toleo la 2025) pamoja na Sheria ya Usimamizi wa Maafa Na. 6 ya mwaka 202 imeipa jukumu la kuratibu masuala yote ya usimamizi wa maafa nchini.
MWISHO

























