HABARI MPYA
HABARI
SIASA
ELIMU
Recent Posts
ARBAB VILLAGE IN TANGA KUFANYIWA MABORESHO MAKUBWA, CEO AMTAJA BAKHRESA
habari
Na Oscar Asenga Tanga
Ikiwa ni zaidi ya miezi sita tangu kuzinduliwa rasmi kwa Arbab Village mjini Tanga mnamo Desemba 6, 2025, eneo hilo sasa limeendelea kuwa gumzo kubwa kwa wakazi wa Tanga na wageni kutoka maeneo mbalimbali kutokana na muonekano wake wa kisasa, ubunifu wake wa kipekee na namna lilivyobadilisha kabisa taswira ya eneo hilo.
Mkurugenzi wa Arbab Village, Mbwana Imamu, amesema mafanikio makubwa yaliyopatikana ndani ya muda mfupi ndiyo sababu kubwa iliyowasukuma kuanza mpango wa maboresho makubwa zaidi ili kufanya eneo hilo liendelee kuwa kivutio kikubwa zaidi ndani ya Tanga na nje ya Tanzania 🇹🇿
Kwa sauti yenye kujiamini, Arbab amesema jambo lililompa nguvu zaidi ni namna wananchi wa Tanga walivyoikubali Arbab Village kwa haraka, tofauti na matarajio ya watu wengi waliokuwa hawaamini kama eneo hilo lingeweza kubadilika na kuwa sehemu ya kisasa yenye mvuto mkubwa wa biashara na burudani.
“Watu wengi hawakuwahi kufikiria kama hapa panaweza kuwa sehemu kama hii. Wapo waliowahi kujaribu kufanya uwekezaji lakini walishindwa. Mimi nilikuja na maono tofauti… niliamua kutumia ubunifu mkubwa na kufanya kitu ambacho watu watakikumbuka,” amesema Arbab.
Ameeleza kuwa hakutaka kufanya biashara ya kawaida kama zilivyo sehemu nyingine, bali alitaka kuleta utofauti ambao ungeifanya Arbab Village kuwa na hadhi yake ya kipekee ndani ya jiji la Tanga.
“Biashara kama hizi zipo sehemu nyingi, lakini nilikaa nikafikiria… nifanye nini ambacho kitawafanya watu wajisikie tofauti wakifika hapa? Ndiyo maana nikaja na ubunifu mkubwa ambao leo watu wameukubali na wengine kuvutiwa sana na kuiga”, amesema.
Kutokana na mwitikio mkubwa wa wateja kila siku, Arbab amesema tayari wameanza mipango ya kufanya maboresho makubwa zaidi yatakayoongeza hadhi na ubora wa huduma zinazotolewa katika eneo hilo.
Amesema maboresho hayo hayajasukumwa na malalamiko ya wateja, bali ni sehemu ya maono yangu ya kuhakikisha kila anayefika Arbab Village anapata uzoefu bora na mpya zaidi.
“Sisi hatusubiri kuambiwa na wateja ndipo tubadilike. Tunataka kila siku tuwe bora zaidi kuliko jana,” amesema kwa msisitizo.
Katika mazungumzo yake, Arbab pia alitoa somo kwa vijana wanaotamani kuingia kwenye biashara, akisisitiza kuwa mafanikio hayapatikani kwa mihemko wala kushindana na watu, bali kwa kusikiliza mahitaji ya wateja na kuwa mbunifu.
“Ukitaka kuwa mfanyabiashara mzuri usipoteze muda kushindana na mfanyabiashara mwingine. Angalia wateja wako wanahitaji nini… hakikisha unawapa,” amesema.
Ameongeza kuwa vijana wengi wanaharibu safari zao za biashara kwa kuendeshwa na presha za mitandaoni na kutaka mafanikio ya haraka badala ya kujenga biashara kwa utulivu, ubunifu na uvumilivu, Arbab Village sio night club kwa maana tunapiga disco hapana, Arbab Village ni sehem tulivu yenye music wa wastan sio makelele huku ukipata chakula na vinywaji.
Akizungumzia watu waliompa hamasa katika safari yake ya biashara, Arbab hakusita kumtaja mfanyabiashara maarufu wa Tanzania Said Salim Bakhresa kuwa mmoja wa watu waliomvutia kupitia maneno yake ya motisha.
“Niliwahi kumsikia Bakhresa akisema mfanyabiashara lazima ujaribu kila kitu na usikate tamaa. Pia lazima ujitume mwenyewe na upambane binafsi. Yale maneno yalinijenga sana,” amesema.
Arbab amesema leo hii wengi wanashangazwa na namna anavyofanikiwa kufanya mambo makubwa akiwa hana makundi ya vijana wenye mihemko au makelele, bali anaamini katika kazi, nidhamu, ubunifu na kujenga heshima ya biashara yake kupitia matokeo.
Kwa sasa, Arbab Village imeendelea kuwa moja ya sehemu zinazovuta watu wengi zaidi jijini Tanga, huku wengi wakisubiri kwa hamu kuona maboresho mapya yatakayofanyika katika eneo hilo ambalo tayari limeanza kubadilisha sura ya burudani na biashara ndani ya mkoa huo.
TUME YA MADINI YAPATA HATI SAFI YA UKAGUZI, YAKUSANYA MADUHULI TSH. TRILIONI 1.192
habariARUSHA
Tume ya Madini imeendelea kuonesha mafanikio makubwa katika usimamizi wa rasilimali za umma baada ya kupata hati safi ya ukaguzi kwa Hesabu za Mwaka wa Fedha 2024/2025 sambamba na kukusanya maduhuli yaliyofikia Shilingi Trilioni 1.192, sawa na asilimia 99 ya lengo la mwaka.
Akizungumza Mei 19, 2026 mkoani Arusha wakati wa kikao kazi cha wahasibu na wachumi wa Tume, Mkurugenzi wa Fedha na Mipango wa Tume ya Madini, CPA. Idfonce Masoud, amesema hati safi hiyo imetokana na ukaguzi uliokamilika na kuwasilishwa kwa Mheshimiwa Rais na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) mwezi Machi 2026.
CPA. Masoud amesema mafanikio hayo yanatokana na juhudi, nidhamu ya kazi na weledi wa timu ya wahasibu na wachumi waliotekeleza majukumu yao kwa kuzingatia Kanuni za Kimataifa za Uandaaji wa Hesabu za Sekta ya Umma (IPSAS), hatua iliyosaidia kupunguza hoja za ukaguzi na kuimarisha uwazi wa kifedha.
Amezipongeza pia Ofisi za Maafisa Madini Wakazi wa Mikoa kwa mchango wao mkubwa katika ukusanyaji wa maduhuli pamoja na usimamizi madhubuti wa Katibu Mtendaji wa Tume, uliowezesha kufikiwa kwa kiwango kikubwa cha mapato ya Serikali.
“Natumia fursa hii kuwashukuru na kuwapongeza sana kwa juhudi mlizozifanya katika kusimamia ukusanyaji wa maduhuli hadi kufikia kiasi kilichokusanywa kufikia tarehe 15 Mei 2026,” amesema CPA. Masoud.
Aidha, amewataka washiriki wa kikao kazi hicho kutumia ipasavyo mafunzo na mada zitakazowasilishwa ili kuendelea kuimarisha utendaji kazi na kuongeza ufanisi wa Taasisi.
Kwa upande wake, Afisa Madini Mkazi wa Mkoa wa Arusha, Godson Kamihanda, amesema kikao kazi hicho ni jukwaa muhimu la kubadilishana uzoefu, kujadili changamoto za kiutendaji na kuweka mikakati madhubuti ya kuboresha utoaji huduma.
Amesema majadiliano yatakayofanyika yanatarajiwa kuzaa matokeo chanya yatakayochangia maendeleo ya Tume ya Madini na Taifa kwa ujumla.
Kikao kazi hicho kinajumuisha mafunzo katika maeneo mbalimbali ikiwemo matumizi ya Mfumo mpya wa Kodi (IDRAS), uandaaji na utunzaji wa taarifa za madeni ya maduhuli, uandaaji wa hesabu, usimamizi wa bajeti na matumizi ya fedha pamoja na maadili na uwajibikaji mahali pa kazi.
SERIKALI YAFICHUA MIKAKATI YA KULIPA MADENI YA WAKANDARASI NA WAZABUNI
habari
Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Mhandisi Mshamu Ali Munde (Mb), akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalumu, Mhe. Lucy Edward Mwakyembe, aliyetaka kujua mpango wa Serikali wa kulipa madeni ya wakandarasi na wazabuni, bungeni jijini Dodoma.
(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, WF, Dodoma)
Na. Jordan Mbwambo, WF, Dodoma.
Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Mhandisi Mshamu Ali Munde (Mb) amesema kuwa Serikali imejipanga kikamilifu kuendelea kulipa madeni ya wakandarasi, wazabuni, na watumishi nchini ili kulinda mitaji yao na kudhibiti ongezeko la madeni mapya.
Hayo yamebainishwa bungeni jijini Dodoma na Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Mhandisi Mshamu Ali Munde (Mb), alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalumu, Mhe. Lucy Edward Mwakyembe, aliyetaka kujua mpango wa Serikali wa kulipa madeni ya wakandarasi na wazabuni.
Mhe. Munde alisema kuwa Serikali kupitia Wizara ya Fedha imekuwa ikitenga bajeti kila mwaka kwa ajili ya kugharamia ulipaji wa madeni ya wakandarasi, wazabuni na watumishi.
‘‘Katika mwaka 2025/26, shilingi bilioni 700 zilitengwa ambapo, hadi Februari 2026, jumla ya shilingi bilioni 477.6 zimetolewa, pia Serikali imetenga shilingi bilioni 800 katika mwaka wa fedha 2026/27 kwa ajili ya kugharamia ulipaji wa madeni yaliyohakikiwa’’, alisema Mhe. Munde.
Aidha, Mhe. Munde alifafanua kuwa katika kuhakikisha kuwa suala la madeni ya wakandarasi na wazabuni linadhibitiwa, Serikali imeendelea kutoa maelekezo kwa Maafisa Masuuli kupitia Waraka mbalimbali za utekelezaji wa bajeti na Mwongozo wa Maandalizi ya Mpango na Bajeti katika mwaka husika.
Mhe. Munde aliongeza kuwa Serikali imeendelea kutoa maelekezo kwa Mafungu kutenga bajeti kwa ajili ya ulipaji wa madeni ya wakandarasi, wazabuni na watumishi.
Aidha, Serikali imeelekeza Maafisa Masuuli kutumia mifumo ya kudhibiti matumizi pamoja na kuhakikisha kuwa mchakato wowote wa ununuzi unaanzishwa baada ya kujiridhisha uwepo wa bajeti na uhakika wa upatikanaji wa fedha.
MWISHO.
RAIS DKT SAMIA SULUHU ATETA NA MKURUGENZI WA SHIRIKA LA KIMATAIFA LA NISHATI LA ATOMIKI (IAEA), BW. RAFAEL MARIANO GROSSI
habari
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Mkurugenzi wa Shirika la Kimataifa la Nishati la Atomiki (IAEA), Bw. Rafael Mariano Grossi pembezoni mwa Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali kuhusu Uvumbuzi wa Nishati ya Nyuklia barani Afrika (NEISA), Kigali nchini Rwanda tarehe 19 Mei, 2026. Mkutano huo wa Kimataifa unawakutanisha pia wataalamu wa nishati, wawekezaji na mashirika ya kimataifa, ambapo utajadili matumizi ya nishati ya nyuklia kwa maendeleo ya Bara la Afrika. Mkutano huo pia unalenga kujadili namna bora ya kuongeza upatikanaji wa nishati ya umeme Afrika, kupunguza uchafuzi wa mazingira, kusaidia maendeleo ya viwanda, kukuza ubunifu wa teknolojia za nishati ya nyuklia pamoja na kuvutia wawekezaji katika miradi ya nishati, tarehe 19 Mei, 2026.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Mkurugenzi wa Shirika la Kimataifa la Nishati la Atomiki (IAEA), Bw. Rafael Mariano Grossi pembezoni mwa Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali kuhusu Uvumbuzi wa Nishati ya Nyuklia barani Afrika (NEISA), Kigali nchini Rwanda tarehe 19 Mei, 2026. Mkutano huo wa Kimataifa unawakutanisha pia wataalamu wa nishati, wawekezaji na mashirika ya kimataifa, ambapo utajadili matumizi ya nishati ya nyuklia kwa maendeleo ya Bara la Afrika. Mkutano huo pia unalenga kujadili namna bora ya kuongeza upatikanaji wa nishati ya umeme Afrika, kupunguza uchafuzi wa mazingira, kusaidia maendeleo ya viwanda, kukuza ubunifu wa teknolojia za nishati ya nyuklia pamoja na kuvutia wawekezaji katika miradi ya nishati, tarehe 19 Mei, 2026.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Mkurugenzi wa Shirika la Kimataifa la Nishati la Atomiki (IAEA), Bw. Rafael Mariano Grossi mara baada ya kumaliza mazungumzo pembezoni mwa Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali kuhusu Uvumbuzi wa Nishati ya Nyuklia barani Afrika (NEISA), Kigali nchini Rwanda tarehe 19 Mei, 2026. Mkutano huo wa Kimataifa unawakutanisha pia wataalamu wa nishati, wawekezaji na mashirika ya kimataifa, ambapo utajadili matumizi ya nishati ya nyuklia kwa maendeleo ya Bara la Afrika. Mkutano huo pia unalenga kujadili namna bora ya kuongeza upatikanaji wa nishati ya umeme Afrika, kupunguza uchafuzi wa mazingira, kusaidia maendeleo ya viwanda, kukuza ubunifu wa teknolojia za nishati ya nyuklia pamoja na kuvutia wawekezaji katika miradi ya nishati, tarehe 19 Mei, 2026.

RAIS SAMIA AHUTUBIA MKUTANO WA NISHATI YA NYUKLIA AFRIKA, KIGALI
habari
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akizungumza katika Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali kuhusu Uvumbuzi wa Nishati ya Nyuklia barani Afrika (NEISA), Kigali nchini Rwanda tarehe 19 Mei, 2026. Mkutano huo wa Kimataifa unawakutanisha pia wataalamu wa nishati, wawekezaji na mashirika ya kimataifa, ambapo utajadili matumizi ya nishati ya nyuklia kwa maendeleo ya Bara la Afrika. Mkutano huo pia unalenga kujadili namna bora ya kuongeza upatikanaji wa nishati ya umeme Afrika, kupunguza uchafuzi wa mazingira, kusaidia maendeleo ya viwanda, kukuza ubunifu wa teknolojia za nishati ya nyuklia pamoja na kuvutia wawekezaji katika miradi ya nishati.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan pamoja na Viongozi mbalimbali wakishiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali kuhusu Uvumbuzi wa Nishati ya Nyuklia barani Afrika (NEISA), Kigali nchini Rwanda tarehe 19 Mei, 2026. Mkutano huo wa Kimataifa unawakutanisha pia wataalamu wa nishati, wawekezaji na mashirika ya kimataifa, ambapo utajadili matumizi ya nishati ya nyuklia kwa maendeleo ya Bara la Afrika. Mkutano huo pia unalenga kujadili namna bora ya kuongeza upatikanaji wa nishati ya umeme Afrika, kupunguza uchafuzi wa mazingira, kusaidia maendeleo ya viwanda, kukuza ubunifu wa teknolojia za nishati ya nyuklia pamoja na kuvutia wawekezaji katika miradi ya nishati.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Mkurugenzi wa Shirika la Kimataifa la Nishati la atomiki (IAEA), Bw. Rafael Mariano Grossi pembezoni mwa Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali kuhusu Uvumbuzi wa Nishati ya Nyuklia barani Afrika (NEISA), Kigali nchini Rwanda tarehe 19 Mei, 2026. Mkutano huo wa Kimataifa unawakutanisha pia wataalamu wa nishati, wawekezaji na mashirika ya kimataifa, ambapo utajadili matumizi ya nishati ya nyuklia kwa maendeleo ya Bara la Afrika. Mkutano huo pia unalenga kujadili namna bora ya kuongeza upatikanaji wa nishati ya umeme Afrika, kupunguza uchafuzi wa mazingira, kusaidia maendeleo ya viwanda, kukuza ubunifu wa teknolojia za nishati ya nyuklia pamoja na kuvutia wawekezaji katika miradi ya nishati.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Mkurugenzi wa Shirika la Kimataifa la Nishati la Atomiki (IAEA), Bw. Rafael Mariano Grossi mara baada ya kumaliza mazungumzo pembezoni mwa Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali kuhusu Uvumbuzi wa Nishati ya Nyuklia barani Afrika (NEISA), Kigali nchini Rwanda tarehe 19 Mei, 2026. Mkutano huo wa Kimataifa unawakutanisha pia wataalamu wa nishati, wawekezaji na mashirika ya kimataifa, ambapo utajadili matumizi ya nishati ya nyuklia kwa maendeleo ya Bara la Afrika. Mkutano huo pia unalenga kujadili namna bora ya kuongeza upatikanaji wa nishati ya umeme Afrika, kupunguza uchafuzi wa mazingira, kusaidia maendeleo ya viwanda, kukuza ubunifu wa teknolojia za nishati ya nyuklia pamoja na kuvutia wawekezaji katika miradi ya nishati, tarehe 19 Mei, 2026.
MAAFISA UHUSIANO NA HUDUMA KWA WATEJA TANESCO WAPEWA MAFUNZO YA KITAALAMU JIJINI DODOMA
NishatiMaafisa wa Uhusiano na Huduma kwa Wateja wa TANESCO wakiendelea kupewa mafunzo na makuzi ya kitaalamu kupitia mada mbalimbali zinazohusiana moja kwa moja na utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku, katika Mkutano Mkuu wa Mwaka unaoendelea kufanyika katika Hoteli ya Lavenda, jijini Dodoma.
Mkutano huo ulifunguliwa rasmi tarehe 18 Mei, 2026 na Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba, ambapo unalenga kuimarisha utoaji wa huduma bora kwa wateja pamoja na kuongeza ufanisi katika utendaji kazi wa maafisa hao.
#MkutanoMkuuWaMaafisaUhusianoNaHudumaKwaWateja2026#TupoKazini
WATAALAM WAONYA HATARI YA MASALIA YA DAWA KWENYE MAZIWA, WADAU WAPEWA MAFUNZO MBEYA
habari
RAIS DKT. SAMIA AWASILI KIGALI NCHINI RWANDA
habari
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Kigali ambapo atashiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali kuhusu Uvumbuzi wa Nishati ya Nyuklia barani Afrika (NEISA), Kigali nchini Rwanda tarehe 19 Mei, 2026. Mkutano huo wa Kimataifa unawakutanisha pia wataalamu wa nishati, wawekezaji na mashirika ya kimataifa, ambapo utajadili matumizi ya nishati ya nyuklia kwa maendeleo ya Bara la Afrika.

SERIKALI KUENDELEA KUBORESHA VITUO VYA MAARIFA NCHINI.
habariNa, Mwandishi wetu - Pwani
SERIKALI kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu) imeeleza dhamira yake ya kuendelea kuboresha Vituo vya Maarifa nchini, hususan vile vinavyotoa huduma kwa madereva wa malori ya masafa marefu kuhusu masuala ya VVU na UKIMWI.
Kauli hiyo imetolewa na Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo, Dkt. Jim Yonazi mapema mwanzoni mwa wiki mara baada ya kutembelea na kukagua Vituo vya Maarifa vinavyotoa huduma za VVU na UKIMWI kwa madereva wa malori ya masafa marefu vilivyopo eneo la Kurasini katika wilaya ya Temeke Jijini Dar es Salaam na Mdaula mkoa wa Pwani ambayo Vituo hivyo vipo chini ya Tume ya Kudhibiti UKIMWI Tanzania (TACAIDS).
Dkt. Yonazi amesema Serikali, kupitia Tume ya Kudhibiti UKIMWI Tanzania (TACAIDS), ina jukumu la kusogeza huduma muhimu za VVU na UKIMWI karibu na wananchi.
“Vituo hivi vina mchango mkubwa katika kuwafikia madereva wa masafa marefu ambao mara nyingi hukaa safarini kwa muda mrefu. Serikali itaendelea kuviboresha hususan kwenye miundombinu ya kutolea huduma na kuongeza wataalam wa afya ili viweze kutoa huduma bora Kwa madereva hao wa masafa marefu kwa kujua afya zao dhidi ya maambukizi ya virusi vya UKIMWI,” amesema Dkt. Yonazi.
Kwa upande wao, madereva wa malori ya masafa marefu wanaonufaika na huduma hizo wameeleza kuwa Vituo vya Maarifa ni msaada mkubwa kwao, kwani vinawapa fursa ya kupata elimu na huduma za VVU na UKIMWI kwa urahisi na bila gharama na kuipongeza Serikali kwa namna inavyoendelea kujali na kuwafikia wananchi wake.



.jpeg)

.jpeg)


.jpeg)

.jpeg)





.jpeg)




.jpeg)








