HABARI

SIASA

ELIMU

Recent Posts

NEMC YAKIJANISHA TANZANIA, YAPANDA MICHE YA MITI ELFU AROBAINI NCHI NZIMA

May 10, 2026 Add Comment
Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) kwa kushirikiana na Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS), Wakuu wa Mikoa, Wakuu wa Wilaya, Halmashauri za Miji, Halmashauri za Wilaya, Shule za msingi, wadau wa mazingira pamoja na Mabalozi wa Mazingira, limepanda miche ya miti elfu arobaini katika maeneo mbalimbali nchini ikiwa ni sehemu ya kuelekea maadhimisho ya miaka 40 tangu kuanzishwa kwa Baraza hilo.

WAZIRI NDEJEMBI ATOA MAELEKEZO MAZITO UTEKELEZAJI MRADI MALAGARASI MW 49.5 KIGOMA

May 10, 2026 Add Comment




📌Hajaridhishwa na kasi ya utekelezaji wa mkandarasi kwenye mradi


📌Aagiza ukaguzi maalum wa matumizi ya dola milioni 20 za malipo ya awali yaliyotolewa kwa mkandarasi kulinganisha na kazi zilizofanyika




📌Aelekeza kuondolewa mara moja kwa meneja wa mradi upande wa mkandarasi


Waziri wa Nishati, Deogratius Ndejembi amesema hajaridhishwa na mwenendo wa utekelezaji wa Mradi wa Kuzalisha Umeme wa Megawati 49.5 katika maporomoko ya Mto Malagarasi mkoani Kigoma unaotekelezwa na Kampuni ya Dongfang Electric kutokana na kuchelewa kwa kazi pamoja na kutotekeleza masharti ya mkataba waliouingia na Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO).

Mhe. Ndejembi ametoa kauli hiyo Mei 10, 2026 wakati wa ziara ya kukagua maendeleo ya mradi huo ambapo alibaini mkandarasi huyo amekuwa akitoa visingizio badala ya kutekeleza majukumu yake kwa wakati kama mkataba unavyoelekeza.

Akizungumza katika ziara hiyo, amesema Serikali tayari imemlipa mkandarasi zaidi ya dola milioni 20 kama malipo ya awali lakini kiwango cha kazi zilizotekelezwa hakionekani kuendana na fedha zilizotolewa.

Baadhi ya kazi zilizochelewa ni pamoja na ujenzi wa makazi ya wafanyakazi na barabara za mradi, hali ambayo imeonesha kusuasua kwa utekelezaji wa mradi huo wa kimkakati.

Aidha, ameielekeza TANESCO pamoja na mshauri mwelekezi kuendelea kumsimamia kwa karibu mkandarasi huyo huku akisisitiza kuwa Serikali haitatoa nyongeza ya fedha wala kuruhusu mabadiliko ya gharama za mradi huo kwani mkandarasi aliwasilisha gharama zake mwenyewe wakati wa zabuni.

Amesema baadhi ya wakandarasi wamekuwa na tabia ya kuomba kazi kwa gharama ndogo ili kupata zabuni na baadaye kuanza kuomba nyongeza ya fedha, jambo ambalo Serikali haitalivumilia.

Katika hatua nyingine, Mhe. Ndejembi ameagiza meneja wa mradi upande wa mkandarasi kuondolewa mara moja kutokana na kile alichokieleza kuwa ni visingizio vinavyochangia kuchelewesha utekelezaji wa kazi. 

Vilevile ameagiza kufanyika kwa ukaguzi maalum wa matumizi ya fedha za malipo ya awali ili kubaini namna fedha hizo zimetumika ukilinganisha na kazi zilizofanyika.


“Mradi huu una umuhimu mkubwa kwa wananchi wa Kigoma, Katavi, Kagera na maeneo ya jirani kwani utaongeza nguvu katika Gridi ya Taifa na kuimarisha upatikanaji wa umeme wa uhakika nchini. Serikali haitakuwa tayari kuvumilia ucheleweshaji unaosababishwa na uzembe wa wakandarasi,” amesema Mhe. Ndejembi.

Ameielekeza TANESCO ndani ya muda wa wiki mbili kukamilisha ukaguzi huo na kuwasilisha taarifa ofisini kwake.

Aidha, amempongeza Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO kwa juhudi za kufanya vikao vya mara kwa mara na mkandarasi huyo pamoja na kuchukua hatua mbalimbali za kutatua changamoto zinazojitokeza katika utekelezaji wa mradi.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa TANESCO Bw, Lazaro Twange amesema TANESCO imepokea maelekezo yote yaliyotolewa na Waziri na itahakikisha yanatekelezwa kwa wakati ili mradi huo ukamilike kama ilivyopangwa.


Mradi wa Malagarasi MW 49.5 unatekelezwa na Kampuni ya Dangfang Electric International Corporation (DEC) kutoka China, ambapo ulianza Aprili 30, 2024 na unatarajiwa kukamilika Oktoba 30, 2027 kwa gharama ya zaidi ya shilingi bilioni 300.


Kukamilika kwake kutaimarisha hali ya upatikanaji wa umeme 

Katika mikoa ya Kigoma, Katavi, Kagera na maeneo ya jirani kwani utaongeza nguvu katika Gridi ya Taifa.

KAFULILA: UJUMBE MAALUM SIKU YA MAMA DUNIANI.

May 10, 2026 Add Comment

Kupitia Ukurasa wake wa Mtandao wa Kijamii wa X (Zamani Twitter) Mwanasiasa na msomi wa masuala ya maendeleo, Mkurugenzi wa kituo cha Ubia kati ya Sekta ya Umma na binafsi (PPPC), David Kafuila ametoa ujumbe maalum wa maadhimisho ya Siku ya Mama Duniani akisisitiza umuhimu wa malezi bora kwa watoto katika siku 1000 kuamzia kutungwa kwa mimba mpk umri wa 2 zina nafasi kubwa kubwa kuamua ubora wa watoto kiafya na zaidi kiakili.
WAMILIKI WA VIWANDA VIPYA WATAKUWA KUAJIRI WAZAWA KUKUZA BIASHARA NA UCHUMI

WAMILIKI WA VIWANDA VIPYA WATAKUWA KUAJIRI WAZAWA KUKUZA BIASHARA NA UCHUMI

May 10, 2026 Add Comment

Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Judith Kapinga, amewashauri Wamiliki wa Viwanda vipya Kutoa kipaumbele kwa wazawa katika ajira ili kukuza uchumi na mapato ya Taifa kwa ujumla.

Akizungumza Mei 09, 2026, wakati wa akifungua wa Kiwanda kipya cha kutengeneza tambi za papo hapo (Instant) cha Kura Food mkoani Pwani, amesema kuwa Serikali inaendelea kuboresha mazingira ya Biashara ikiwemo sera, miundombinu, na mifumo ili kuvutia Wawekezaji na wafanyabiashara na kuongeza ushindani wa bidhaa za Tanzania kimataifa.

Aidha, Wizara imefanya mapitio ya sheria na kanuni ili kuhakikisha zinajielekeza katika kuwezesha biashara na kuondoa vikwazo badala ya kudhibiti pekee. Lengo ni kushirikiana na wadau wa mnyororo wa thamani, kutumia teknolojia za kisasa zinazoongeza tija, uzalishaji, na ufanisi wa biashara nchini.

Naye, Mwenyekiti wa Kura Food, Bw. Wu Yeping, ameipongeza Serikali kwa kuweka mazingira rafiki yanayorahisisha uwekezaji,

Huku Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Mhe. Abubakar Kunenge, akibainisha kuanza kwa uboreshaji wa miundombinu ya barabara na Reli ya Kisasa (SGR) kuanzia mwaka ujao ili kufungua zaidi fursa za kibiashara mkoani humo.

Naye Mbunge wa Kisarawe, Mhe. Selemani Jafo, amemshukuru Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa sera zake thabiti ambazo zimekuwa chachu ya kuvutia wawekezaji. Sera hizi zimesaidia kwa kiasi kikubwa kupunguza changamoto ya ukosefu wa ajira kwa wananchi wa jimbo hilo kupitia kuanzishwa kwa viwanda vipya.

            

COOP BANK YAZINDUA TAWI MTWARA MJINI KUCHOCHEA UCHUMI JUMUISHI

May 10, 2026 Add Comment
Na Mwandishi Wetu

Benki ya Ushirika (Coop Bank) mwishoni mwa wiki ilizindua rasmi tawi lake jipya Mtwara mjini ikiwa ni hatua muhimu katika utekelezaji wa mkakati wa benki hiyo wa kupanua huduma za kifedha na kuimarisha uchumi jumuishi.

KAMATI YA BUNGE YARIDHISHWA NA UWEKEZAJI WA ORYX ENERGIES TANZANIA

May 09, 2026 Add Comment
KAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini imesema kuwa uwekezaji unaofanywa na Oryx Energies Tanzania Limited ni kielelezo cha mafanikio ya juhudi za Serikali katika kuimarisha sekta binafsi na kuongeza mchango wake katika maendeleo ya taifa.

MILIKI UBUNIFU YATAJWA KUINUA TASNIA YA MICHEZO

May 09, 2026 Add Comment
NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

Serikali imewataka wanamichezo na wadau wa sekta ya michezo nchini kutumia mfumo wa miliki ubunifu kulinda vipaji, majina na chapa zao ili kuongeza thamani ya kiuchumi ya shughuli zao na kujijengea maisha bora baada ya michezo.

KONGANI YA VIWANDA VYA DAWA KUPANUA AJIRA NA UWEKEZAJI

May 09, 2026 Add Comment
Serikali imeendelea kuweka mikakati madhubuti ya kuifanya Tanzania kuwa kitovu cha uzalishaji wa dawa na vifaa tiba barani Afrika kupitia uwekezaji mkubwa katika miundombinu ya afya na matumizi ya teknolojia za kisasa.

KITUO CHA UTAMADUNI CHA IRAN CHAZINDUA MASHINDANO YA UCHORAJI TANZANIA.

May 09, 2026 Add Comment
Kituo cha Utamaduni cha Iran nchini Tanzania kimeanzisha mashindano ya uchoraji yanayolenga kuhamasisha jamii, hususan watoto na vijana, kueleza hisia zao kupitia sanaa kufuatia tukio la mlipuko lililotokea nchini Iran mwezi Februari mwaka huu, ambapo Shule ya Msingi ya Minaab ililipuliwa na kusababisha vifo vya wanafunzi 168.

TBS YAKABIDHIWA MAGARI 11 KUFIKIA WADAU KWA WAKATI

May 09, 2026 Add Comment
NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Judith Kapinga, amelielekeza Shirika la Viwango Tanzania (TBS) kuhakikisha linalinda na kuthamini rasilimali za taasisi ili kuongeza ubora na ufanisi katika utoaji wa huduma kwa wananchi.

WAZIRI KAPINGA: SERIKALI KUENDELEA KUWEKA MAZINGIRA BORA YA BIASHARA NA UWEKEZAJI

May 08, 2026 Add Comment
WAZIRI wa Viwanda na Biashara, Judith Kapinga amesema Serikali chini ya uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan itaendelea kulinda ajira zilizopo na kuzalisha ajira mpya kupitia sekta ya viwanda na biashara kwa manufaa ya Watanzania na Taifa kwa ujumla.

JAJI WA MAHAKAMA KUU SHINYANGA AIPONGEZA PSSSF KWA HUDUMA ZA KIDIGITALI

May 08, 2026 Add Comment
Wateja wakipata huduma na elimu mbalimbali katika banda la PSSSF wakati wa Kampeni ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia “Mama Samia Legal Aid” mjini Shinyanga.
Afisa Mfawidhi wa PSSSF Mkoa wa Shinyanga, Nila Magambo (kushoto), akimkabidhi zawadi Jaji wa Mahakama Kuu Kanda ya Shinyanga, Mhe. Ntuli Mwakahesya, alipotembelea banda la PSSSF katika Kampeni ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia “Mama Samia Legal Aid” Awamu ya Pili inayofanyika katika viwanja vya Zimamoto Manispaa ya Shinyanga. Picha na Kadama Malunde – Malunde 1 Blog.
Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Shinyanga, Mhe. Ntuli Mwakahesya, akisikiliza maelezo kutoka kwa Afisa Mfawidhi wa PSSSF Mkoa wa Shinyanga, Nila Magambo  alipotembelea banda la PSSSF.

***

Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Shinyanga, Mhe. Ntuli Mwakahesya, amepongeza Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) kwa hatua kubwa iliyofikiwa katika matumizi ya mifumo ya kidigitali inayorahisisha utoaji wa huduma kwa wanachama na wastaafu.

TANESCO YAZINDUA RASMI ZOEZI LA ULIPWAJI FIDIA KWA WANANCHI LINDI NA MTWARA

May 08, 2026 Add Comment



📌 Lengo ni kupisha Mradi wa ujenzi wa njia ya kusafirisha umeme 220kV Masasi, Mahumbika


📌Zaidi ya Shilingi Bil 5.1 zimetengwa kwa ajili ya zoezi hilo


Shirika la umeme Tanzania ( TANESCO) limezindua rasmi zoezi la ulipaji fidia kwa wananchi wanaopisha mradi wa ujenzi wa njia ya kusafirisha umeme ya msongo wa 220kV kutoka Masasi Mkoani Mtwara hadi Mahumbika Mkoani Lindi.


Akizungumza Mei 7, 2026 katika Kata ya Kiwalala, Halmashauri ya Mtama, Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO, Bw. Lazaro Twange amesema Serikali chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imewekeza fedha nyingi kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya umeme ikiwemo njia za kusafirisha umeme zitakazowezesha mikoa ya kusini kuunganishwa kwenye Gridi ya Taifa.


Amesema zaidi ya shilingi bilioni 5.1 zimetengwa kwa ajili ya kuwalipa takribani wananchi 1,730 katika mikoa ya Lindi na Mtwara watakaopisha mradi wa ujenzi wa njia ya kusafirisha umeme ya msongo wa 220kV kutoka Masasi hadi Mahumbika


Bw. Twange, amesema kaya 78 katika vijiji vya Kiwalala na Mahumbika zitanufaika na zaidi ya shilingi milioni 253 katika awamu ya kwanza ya malipo kisha kuendelea katika vijiji vingine.


Naye Mkuu wa Wilaya ya Lindi Mhe. Victoria Mwanziva amesema ulipaji huo wa fidia unalenga kuhakikisha wananchi wote wanaopitiwa na mradi huo wanalipwa stahiki zao ili kurahisisha utekelezaji wa miradi ya maendeleo hivyo amewataka wananchi kutoa ushirikiano kwa TANESCO


‘’Tunamshukuru sana Mhe. Rais kwa kuidhinisha zaidi ya shilingi bilioni 5.1 zitakazotumika kuwalipa fidia zaidi ya wananchi 1,700 katika maeneo ya Lindi na Mtwara lengo kuu ni kuhakikisha mradi wetu huu wa Masasi hadi Mahumbika unafanikiwa,’’alifafanua Mhe Mwanziva.


Zoezi hilo litaendelea katika vijiji vyote 46 vilivyoguswa na mradi huo katika Wilaya za Lindi, Ruangwa, Newala na Masasi.


Zoezi hilo la malipo linaanza kwa vijiji 14 vya Halmashauri ya Mtama.


Utekelezaji wa mradi huo utasaidia upatikanaji wa umeme wa uhakika kwa wananchi wa kusini, ambao kwa sasa wanategemea umeme unaozalishwa kupitia vituo vya gesi asilia vya Mtwara na kusafirishwa umbali mrefu.







TANZANIA NA ZAMBIA WAAZIMIA KUONDOA VIKWAZO VYA BIASHARA

May 07, 2026 Add Comment
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Jamhuri ya Zambia zimeazimia kuendelea kuchukua hatua katika kuondoa vikwazo vya biashara ili kurahisisha usafirishaji wa bidhaa, huduma na watu, hatua inayolenga kuimarisha zaidi ushirikiano wa kiuchumi, biashara na uwekezaji kati ya mataifa hayo mawili.

CHEM CHEM SAFARI & LODGES WAINGIA UBIA NA AUBERGE COLLECTION

May 07, 2026 Add Comment

    Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa BMG Media. Mawasiliano +255 757 432 694 ama ripotabmg@gmail.com



Kampuni ya Chem Chem Safari, ya Tanzania imeingia katika ushirikiano na Auberge Collection chini ya chapa ya Auberge Safari.

Ushirikiano huu umejengwa juu ya dhamira ya pamoja ya kutoa huduma zinazozingatia mazingira ya eneo husika, zilizoandaliwa mahsusi na zikizingizatia urithi, utamaduni wa maeneo, na uhusiano na
mazingira hayo.

TANZANIA KUSHIRIKIANA NA BARAZA LA UTALII DUNIANI KATIKA MAFUNZO, UWEKEZAJI

May 07, 2026 Add Comment
Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii Dkt. Hassan Abbasi leo Mei 7, 2026, ameongoza ujumbe wa Tanzania kushiriki Mkutano wa Kimataifa unaowakutanisha Wadau wa Utalii Duniani chini ya Baraza la Usafiri na Utalii Duniani (WTTC) unaofanyika ndani ya meli ya Crystal Serenity inayosafiri kutoka bandari ya Sokhna kuelekea Alexandria nchini Misri.

MSSPAT zaunganisha Kampuni nne kwenye madini

May 07, 2026 Add Comment
Na Mwandishi Wetu,Dar.

Kampuni nne za watoa huduma za bidhaa katika migodi ya madini nchini,zimeungana kwa ajili ya kufanya shughuli mbali mbali za utoaji huduma na bidhaa migodini.

Mkoa wa Dodoma kusafirisha walimu wake 40 Korea Kusini

May 07, 2026 Add Comment
Na Mwandishi Wetu, Dodoma

WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu TAMISEMI, Profesa Riziki Shemdoe, ameipongeza Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma kwa kuandaa mpango wa kuwapeleka walimu 40 kwenda kusoma Korea Kusini, akieleza kuwa ni hatua muhimu ya kuimarisha ubora wa elimu nchini.

DC KILWA AIPONGEZA TANESCO KWA KUJIPANGA KUFIKISHA UMEME KATIKA BANDARI YA UVUVI - KILWA

May 07, 2026 Add Comment





📌Asema ni Mradi wa kimkakati wenye fursa za kiuchumi kwa maslahi mapana ya nchi

📌Amtaka Mkandarasi kukamilisha mifumo ya upokeaji umeme kutoka TANESCO

 Mkuu wa Wilaya ya Kilwa, Mhe. Mohamed Nyundo, ameipongeza TANESCO kwa jitihada na utayari wake wa kuhakikisha umeme unafika katika mradi wa ujenzi wa Bandari ya Uvuvi, inayotarajiwa kuwa na mchango mkubwa katika fursa za kiuchumi.

Mhe. Nyundo ameyasema hayo Mei 6, 2026, baada ya ziara ya Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO, Bw. Lazaro Twange, katika mradi huo wa ujenzi wa Bandari ya Uvuvi Kilwa, kwa lengo la kuangalia kama miundombinu ya upokeaji wa umeme imekamilika.
Amesema, licha ya TANESCO kuwa na utayari wa kupeleka umeme katika bandari hiyo, bado mkandarasi hajakamilisha mifumo ya kupokea umeme kutoka TANESCO.

“Nikupongeze sana MD kwa kufika na timu yako ya wataalamu. Mmejionea mahitaji ambayo TANESCO mnapaswa kutoa, na tumeona mkandarasi bado hajakamilisha baadhi ya mifumo katika eneo lake ili kupokea huduma ya umeme kutoka kwenu,” alisema Mhe. Nyundo.
Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO, Bw. Lazaro Twange, amesema TANESCO ina umeme wa kutosha, na tayari kumejengwa njia ya kusafirisha umeme wa msongo wa kilvoti 33 kutoka Somanga ili kupeleka umeme katika bandari hiyo ya uvuvi.
Aidha, ameeleza jitihada zinazoendelea kufanyika za upanuzi wa kituo cha kupokea na kupoza umeme cha Singino, Kilwa, kwa kuongeza transfoma yenye uwezo wa MVA 5 ili kuimarisha hali ya upatikanaji wa umeme katika maeneo hayo.
“Kimsingi, TANESCO tuna umeme wa kutosha kwa ajili ya bandari. Tunafahamu kwamba bandari hii ikiwa inafanya kazi itahitaji takribani megawati 2.5 za umeme. Tutawapa umeme moja kwa moja kutoka katika kituo chetu cha kufua umeme cha Somanga,” alifafanua Bw. Twange.
Ziara ya Mkurugenzi Twange imelenga kukagua miradi ya umeme inayoendelea katika mikoa ya Pwani, Lindi na M Mtwara


RAIS DKT. SAMIA AKUTANA NA UJUMBE WA KAMPUNI YA PERSEUS MINING LIMITED NA SOTTA MININING CORPORATION LIMITED, IKULU CHAMWINO, MKOANI DODOMA

May 06, 2026 Add Comment



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, akiwa kwenye picha na Waziri wa Madini Mhe. Anthony Mavunde, pamoja na Mwenyekiti wa Bodi ya Kampuni ya Perseus Mining Limited Bw. Rick Menell mara baada ya mazungumzo yao, Ikulu ya Chamwino, Dodoma tarehe 06 Mei, 2026.


Perseus Mining Limited ni mwekezaji wa Mgodi wa Dhahabu wa Nyanzaga, Wilayani Sengerema, Mkoani Mwanza kupitia Kampuni ya Sotta Minining Corporation Limited, inayomilikiwa kwa ubia na Serikali ya Tanzania.






Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa na Waziri wa Madini Mhe. Anthony Mavunde kwenye picha na Ujumbe wa Kampuni ya Perseus Mining Limited na Sotta Minining Corporation Limited mara baada ya mazungumzo yao, Ikulu ya Chamwino, Dodoma tarehe 6 Mei, 2026.

Perseus Mining Limited ni mwekezaji wa Mgodi wa Dhahabu wa Nyanzaga, Wilayani Sengerema, Mkoani Mwanza kupitia Kampuni ya Sotta Minining Corporation Limited, inayomilikiwa kwa ubia na Serikali ya Tanzania.