HABARI

SIASA

ELIMU

Recent Posts

DKT.AKWILAPO KUSHIRIKI KONGAMANO LA MIJI AFRIKA NAIROBI

April 07, 2026 Add Comment


Nairobi

Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. Dkt Leonard Akwilapo, anatarajiwa kuongoza ujumbe wa Tanzania kushiriki Kongamano la Pili la Jukwaa la Miji Afrika (2nd African Urban Forum) litakalofanyika kuanzia tarehe 8 hadi 10 Aprili 2026 katika jiji la Nairobi nchini Kenya.

Kongamano hilo linaongozwa na kauli mbiu isemayo “Adequate Housing for All: Advancing Socio-Economic and Environmental Transformation Towards the Realization of Agenda 2063,” linalenga kuhamasisha mijadala itakayotoa fursa kwa washiriki kutoka nchi mbalimbali za Afrika kubadilishana uzoefu na suluhisho bunifu katika kukabiliana na changamoto za maendeleo ya miji na makazi.

Kupitia kongamano hilo, Tanzania inatarajiwa kutoa tamko la nchi litakaloeleza jitihada za Serikali katika kuchochea maendeleo endelevu ya miji na makazi, ikiwa ni pamoja na sera, mipango na mikakati inayotekelezwa kuboresha makazi na upangaji wa miji.

Aidha, Mhe. Dkt Akwilapo atashiriki katika mijadala ya ngazi ya juu itakayowahusisha mawaziri, mameya na wataalamu mbalimbali, kwa lengo la kuimarisha ushirikiano wa kikanda na kimataifa katika sekta ya maendeleo ya miji.

Awali Dkt Akwilapo aliongoza kikao cha maandalizi kwa ujumbe wa Tanzania utakaoshiriki kongamano hilo katika ubalozi wa Tanzania nchini Kenya tarehe 7 April, 2026 ambapo masuala mbalimbali ya uwakilishi wa nchi yalijadiliwa.


Dkt Akwilapo ameambatana na Mkurugenzi wa Maendeleo ya Makazi Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Bw. Deogratias Kalimenze, Mkurugenzi Msaidizi Uzingatiaji Mipango ya Matumizi ya Ardhi kutoka Tume ya Taifa ya Matumizi ya Ardhi Bi. Rehema Kishoa, Maafisa kutoka Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makazi pamoja na taasisi binafsi.

WAZIRI NDEJEMBI AFANYA KIKAO KAZI CHA PAMOJA NA TAASISI ZILIZO CHINI YA WIZARA YA NISHATI

April 07, 2026 Add Comment

 


Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi amekutana na kufanya kikao kazi cha pamoja na Taasisi zilizo chini ya Wizara ya Nishati zinazoshughulikia mafuta leo Aprili 07, 2026 jijini Dodoma.


Lengo la kikao hicho ni kupitia na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini kuhusu hali ya upatikanaji na bei za bidhaa za mafuta nchini itakayowasilishwa mbele ya kamati hiyo Aprili 08, 2026.

Kikao hicho kinatokana na agizo la Spika wa Bunge, Mhe. Mussa Zungu alilolitoa Aprili 01, 2026 kwa Waziri wa Nishati akielekeza kukutana na Kamati ya Nishati na Madini ili kujadili hali na mwenendo wa kupanda kwa bei ya mafuta nchini.

Kikao hicho kimehudhuriwa na Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba, Katibu Mkuu Wizara ya Nishati anayeshughulikia Mafuta na Gesi, Dkt. James Mataragio, Wataalamu kutoka wizarani pamoja na Wakuu wa Taasisi zilizo chini ya wizara zinazoshughulikia mafuta na gesi.



BARRICK NORTH MARA YAWEZESHA VIJANA TARIME KUANZISHA MIRADI YA KIUCHUMI

April 07, 2026 Add Comment

Vijana wakiwezeshwa kuendesha miradi mbalimbali ikiwemo ya kilimo wataweza kujikwamua kiuchumi kama wanavyoonekana vijana wakiwa shambani kwenye mradi wa kilimo cha mboga wa Matongo unaofadhiliwa na Barrick North Mara (Picha kutoka maktaba)
Mgodi wa Barrick North Mara uliopo wilayani Tarime katika mkoa wa Mara umeendelea kutekeleza moja ya sera ya mkakati endelevu wa kampuni ya kuwezesha wananchi wanaoishi jirani na migodi yake kuwa na maisha bora ambapo kupitia fedha za uwajibikaji kwa jamii (CSR) umetoa shilingi milioni 220 kwa vikundi 13 vya vijana ili kuanzisha miradi ya kiuchumi katika vijiji vyote 11 vinavyozunguka mgodi huo.

DC MPOGOLO AWAPONGEZA VIONGOZI WA DINI KWA KUIMARISHA AMANI NA MAENDELEO.

April 07, 2026 Add Comment

 




Mkuu wa wilaya ya Ilala, Mheshimiwa Edward Mpogolo, ambaye amemuwakilisha Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Mheshimiwa Albert Chalamila, amepongeza na kuwashukuru viongozi wa dini kwa mchango wao mkubwa wa kuimarisha na kudumisha amani lengo kuleta maendeleo katika jamii.

Akizungumza katika maadhimisho ya kumbukumbu ya miaka 19 ya kanisa la WRC Kivule tarehe,6 April, DC Mpogolo alisema licha ya changamoto mbalimbali viongozi wa dini wameendelea kujitoa na kushirikiana na serikali pale wanapohitajika.

Aidha alimpongeza mgeni rasmi, Deus Sangu, Waziri wa nchi ofisi ya waziri mkuu kazi na ajira , ambaye alimuwakilisha makamu wa raisi Mheshimiwa Emmanuel Nchimbi kwa kushiriki katika maadhimisho hayo.

DC Mpongolo ameipongeza serikali chini ya Mheshimiwa raisi Dkt Samia Suluhu Hassan kwa juhudi zake za kuleta maendeleo kwa utoaji wa fedha katika mkoa huo na kusisitiza kuwa mafanikio hayo yasingewezekana bila uwepo wa amani, maadili na mchango wa viongozi wa dini.

Aliongeza kuwa viongozi wa dini wamekuwa nguzo muhimu katika kuleta amani, utulivu, upendo na mshikamano miongoni mwa wananchi na kujenga jamii kupitia hofu ya Mungu hali inayochangia kwa kiasi kikubwa utekelezaji wa malengo ya serikali.

“Mgeni rasmi kwa niaba ya mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam tufikishie salamu kwa raisi wetu amekuwa na mafanikio makubwa lakini mafanikio haya ni kutokana na maombi ya viongozi wetu na waumini”

Mheshimiwa Mpogolo aliwataka waumini na wananchi kwa ujumla kuendelea kumuombea Rais pamoja na kudumisha amani, akibainisha kuwa mafanikio ya Taifa yanatokana na ushirikiano wa viongozi wa dini na wananchi kwa ujumla.














RAIS DKT SAMIA SULUHU HASSAN ASHIRIKI DUA MAALUMU YA KUMUOMBEA ALIYEKUWA RAIS WA KWANZA WA ZANZIBAR HAYATI ABEID AMANI KARUME KATIKA MAADHIMISHO YA SIKU YA KUMBUKUMBU YA KARUME (KARUME DAY) ZANZIBAR

April 07, 2026 Add Comment


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akishiriki Dua maalum ya kumuombea aliyekuwa Rais wa kwanza wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Hayati Abeid Amani Karume ikiwa ni miaka 54 tangu kuuawa kwake.
Dua hiyo maalum imefanyika Afisi Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Kisiwandui, Zanzibar tarehe 7 Aprili, 2026.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akishiriki Dua maalum ya kumuombea aliyekuwa Rais wa kwanza wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Hayati Abeid Amani Karume ikiwa ni miaka 54 tangu kuuawa kwake.
Dua hiyo maalum imefanyika Afisi Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Kisiwandui, Zanzibar tarehe 7 Aprili, 2026.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan akiwa pamoja na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mheshimiwa Dkt. Hussein Ali Mwinyi wakati wa kuweka Shada la Maua katika Kaburi la Rais wa Kwanza wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Hayati Abeid Amani Karume mara baada ya Dua iliyofanyika katika Afisi Kuu ya Chama cha Mapinduzi (CCM) Kisiwandui Zanzibar leo tarehe 07 Aprili 2026, katika Siku ya Kumbukumbu ya (Karume Day).

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akishiriki Dua maalum ya kumuombea aliyekuwa Rais wa kwanza wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Hayati Abeid Amani Karume ikiwa ni miaka 54 tangu kuuawa kwake.
Dua hiyo maalum imefanyika Afisi Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Kisiwandui, Zanzibar tarehe 7 Aprili, 2026.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan akiweka Shada la Maua katika Kaburi la Rais wa Kwanza wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Hayati Abeid Amani Karume mara baada ya Dua iliyofanyika katika Afisi Kuu ya Chama cha Mapinduzi (CCM) Kisiwandui Zanzibar leo tarehe 07 Aprili 2026, katika Siku ya Kumbukumbu ya (Karume Day).

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan akiweka Shada la Maua katika Kaburi la Rais wa Kwanza wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Hayati Abeid Amani Karume mara baada ya Dua iliyofanyika katika Afisi Kuu ya Chama cha Mapinduzi (CCM) Kisiwandui Zanzibar leo tarehe 07 Aprili 2026, katika Siku ya Kumbukumbu ya (Karume Day).

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan akiweka Shada la Maua katika Kaburi la Rais wa Kwanza wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Hayati Abeid Amani Karume mara baada ya Dua iliyofanyika katika Afisi Kuu ya Chama cha Mapinduzi (CCM) Kisiwandui Zanzibar leo tarehe 07 Aprili 2026, katika Siku ya Kumbukumbu ya (Karume Day).
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan akiwa pamoja na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mheshimiwa Dkt. Hussein Ali Mwinyi wakati wa kuweka Shada la Maua katika Kaburi la Rais wa Kwanza wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Hayati Abeid Amani Karume mara baada ya Dua iliyofanyika katika Afisi Kuu ya Chama cha Mapinduzi (CCM) Kisiwandui Zanzibar leo tarehe 07 Aprili 2026, katika Siku ya Kumbukumbu ya (Karume Day).





MWAKITINYA AKATA UTEPE MASHINDANO YA AWESO VIJANA CUP PANGANI

April 07, 2026 Add Comment




Na: Mwandishi Wetu, Pangani

Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Bara na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa (MNEC), Mussa Mwakitinya, amezindua rasmi mashindano ya mpira wa miguu yaliyopewa jina la "Aweso Vijana Cup," wilayani Pangani mkoani Tanga.

Uzinduzi huo umefanyika Aprili 4, 2026, katika uwanja wa Kata ya Mwera. Katika hotuba yake fupi ya ufunguzi, Mwakitinya ameupongeza uongozi wa UVCCM wa wilayani humo kufuatilia uratibu mzuri wa mashindano hayo huku akisisitiza umuhimu wa vijana kushiriki kikamilifu ili kukuza vipaji vyao.

"Vijana wetu wana uwezo mkubwa, kupitia Aweso Vijana Cup tunafungua jukwaa la wao kuonyesha vipaji vyao na kujijengea mustakabali bora," amesema Mwakitinya.


Sambamba na hilo, Mwakitinya amesema serikali ipo pamoja na wadau wote wa michezo ili kuhakikisha sekta ya michezo inakua na inachangia maendeleo ya nchi.

Kwa upande wa Mwenyekiti wa UVCCM mkoa wa Tanga, Ramadhani Omary, amesema vijana ni wadau muhimu kwa uhai wa Chama na maendeleo ya nchi, hivyo wanapaswa kutumia fursa zilizopo katika mazingira yao ikiwemo suala la michezo.

Katika mechi ya ufunguzi wa mashindano hayo, timu ya Tungamaa ilipata ushindi wa (1-0) dhidi ya Mwera. Tungamaa ilipata goli la ushindi katika dakika 87, kupitia kwa mchezaji wake Said Mandera, na hivyo kuchukua alama tatu muhimu.

Mashindano hayo yanahusisha timu kutoka Kata zote 14 za wilaya ya Pangani huku mfadhili wa mashindano hayo akiwa ni Mbunge wa Jimbo la Pangani na Waziri wa Maji, Jumaa Aweso.