HABARI

SIASA

ELIMU

Recent Posts

ROSTAM AZIZI : KENYA -TANZANIA NA KENYA ZIWE NA MFUMO MMOJA WA KIBIASHARA KUPATA MAFANIKIO ZAIDI YA BIASHARA

May 05, 2026 Add Comment

         

Mfanyabiashara mashuhuri na Mwenyekiti wa Taifa Group, Rostam Azizi akiongea katika kongamano hilo
Mwenyekiti wa Taifa Group, Rostam Azizi katika banda la maonesho la kampuni hiyo kwenye kongamano la biashara kati ya Kenya na Tanzania lililofanyika jijini Dar es Salaam ambapo Taifa Group ambayo ni kampuni mama ya Taifa Gas ilkuwa mdhamini mkuu wa kongamano hilo.
Mwenyekiti wa Taifa Group,Rostam Azizi katika picha ya pamoja na Maofisa Waandamizi wa Taifa group na Taifa Gas kwenye banda la maonesho la kampuni hiyo kwenye kongamano la biashara kati ya Kenya na Tanzania lililofanyika jijini Dar es Salaam ambapo Taifa Group ambayo ni kampuni mama ya Taifa Gas ilikuwa mdhamini mkuu wa kongamano hilo.
Muonekano wa banda la maonesho la kampuni ya Taifa Group kwenye kongamano la biashara kati ya Kenya na Tanzania lililofanyika jijini Dar es Salaam ambapo Taifa Group ambayo ni kampuni mama ya Taifa Gas ilkuwa mdhamini mkuu wa kongamano hilo.
#Watanzania wasiwaogope Wakenya katika masuala ya biashara na ajira na Wakenya waache kushabikia matatizo na majanga yanayotokea Tanzania.

 **

Mfanyabiashara mashuhuri na Mwenyekiti wa Taifa Group, Rostam Azizi. ametoa wito wa kuanzishwa kwa mfumo mmoja wa kibiashara ili kuharakisha mtiririko wa uwekezaji, kuhamasisha mitaji, na kufungua fursa zilizopo za biashara kati ya Kenya na Tanzania.

TANZANIA NA KENYA ZASANII MKATABA WA VYETI VYA MABAHARIA NA NA USHIRIKIANO WA USAFIRI WA MAJINI

May 05, 2026 Add Comment

 


SHIRIKA la Uwakala wa Meli Tanzania na Mamlaka ya Udhibiti wa usafiri wa Majini nchini Kenya wamesaini mkataba wa utambuzi wa vyeti vya mabaharia na hati ya makubaliano kuhusu ushirikiano na usimamizi wa sekta ya usafiri wa njia ya maji baina ya nchi hizo mbili.

Mkataba huo umesainiwa na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC) Mohamed Salum na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti wa usafiri wa Majini nchini Kenya CPA Omaye Nyarandi mbele ya Marais, Samia Suluhu Hassan na Rais William Ruto katika Hafla iliyofanyika Mei 4, 2026 Ikulu jijini Dar es Salaam

DAS KIGAMBONI AZINDUA OFISI YA WILAYA YA KITANESCO YA KIMBIJI

May 05, 2026 Add Comment




📌Asema itapunguza adha wananchi kutembea umbali mrefu kufuata huduma

📌Aipongeza TANESCO kwa maboresho yanayoendelea kufanyika kwa wateja wake

Katibu Tawala Wilaya ya Kigamboni Bi. Upendo Mahalu amezindua Ofisi mpya ya Wilaya ya KiTANESCO Kimbiji ikiwa ni mkakati wa Shirika wa kuendelea kuwahudumia na kusogeza huduma zake karibu na wananchi.
Akizungumza Mei 04, 2026 kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni, Katibu Tawala wa Wilaya hiyo, Bi. Upendo Mahalu, amesema uzinduzi wa Ofisi hiyo  umelenga kuboresha utoaji huduma kwa wananchi kadri mahitaji ya nishati ya umeme yanavyozidi kuongezeka.
Ameeleza kuwa hatua hiyo inaakisi maboresho ya kiutendaji yanayolenga kuongeza ufanisi na kupunguza changamoto ya umbali kwa wananchi ambao hapo awali walilazimika kufuata huduma katika ofisi za mkoa zilizopo Tungi Mnadani.
“Lengo la uzinduzi huu ni kuboresha huduma kwa wananchi na kuendana na kasi ya ongezeko la mahitaji ya nishati ya umeme kwa maendeleo ya nchi. Naipongeza Menejimenti ya TANESCO kwa maono ya kusogeza huduma karibu na wananchi,” alisisitiza Bi. Mahalu.
Kwa upande wake, Mbunge wa Jimbo la Kigamboni, Mhe. Haran Sanga, ameipongeza TANESCO kwa maboresho makubwa ya kiutendaji na kimtazamo, huku akiwataka wananchi kuwa mstari wa mbele kulinda miundombinu ya umeme, akisisitiza kuwa serikali inawekeza fedha nyingi katika sekta hiyo.
Akizungumza Kaimu Meneja Huduma kwa Wateja, Bw. Shamu Lameck, amesema TANESCO inaendelea kuimarisha huduma zake kwa wateja kwa kutoa elimu na taarifa sahihi kuhusu matumizi ya umeme na miundombinu yake.
“Dhamira yetu ni mteja kwanza. Tunaendelea kuongeza juhudi kuhakikisha kila mteja anafikiwa na huduma bora ya umeme, tunaishukuru sana Serikali kwa kutaoa ushirikiano katika kufikia malengo yetu ya kumuhudumia mteja kwa ufanisi,” alieleza.
Ofisi ya TANESCO Kimbiji itahudumia kata za Kimbiji, Somangila, Pembamnazi na Kisarawe II. Uzinduzi huo pia uliambatana na kukabidhiwa kwa vitendea kazi, yakiwemo magari na bajaji yatakayosaidia kuwafikia wateja kwa haraka na kwa ufanisi zaidi.


NGORONGORO NGOMA INOGILE

NGORONGORO NGOMA INOGILE

May 05, 2026 Add Comment





Kutoka Pemba, Unguja, Mji mkongwe, Bagamoyo, Kondoa, Magofu ya kilwa, paa la mlima kilimanjaro na maeneo mengine ya Tanzania, wadau wa urithi wa dunia wamekutana katika Makumbusho ya Urithi Geopark Karatu Mkoani Arusha yanayosimamiwa na Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro kwa lengo la kuadhimisha Urithi wa Dunia Afrika yaliyoanza leo tarehe 04/05/2026 hadi tarehe 05/05/2026.

Wakiwa katika jengo la makumbusho ya Urithi Geopark Wadau hao wameelezwa jinsi Ngorongoro ilivyo ni utajiri wa urithi wa dunia kutokana na uumbwaji wake uliotokana na mlipuko wa volcano zaidi ya miaka milioni mbili iliyopita na kutengeneza kasoko iliyokusanya asili, uhai wa binadamu, mifumo ya ikolojia, na ustawi wa viumbe mbalimbali.

Katika taarifa yake kwa vyombo vya habari Kamishna wa Uhifadhi wa Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro Bw. Abdul-Razaq Badru amewashukuru wadau wote hasa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) kwa kuipa fursa Ngorongoro kuandaa na kuwa mwenyeji wa maadhimisho hayo kwa mwaka huu.

Wadau wa urithi wa duania wakiwa katika Makumbusho ya Urithi Geopark walipata fursa ya kuelezewa kuhusu uthibitisho wa wasomi unaoeleza wazi historia ya chimbuko la binadamu wa kale aliyepatikana katika bonde la olduvai takribani milioni 2 iliyopita na ushahidi wa Nyanyo za binadamu wa kale katika eneo la Laetoli takribani miaka 3.6 iliyopiTa ambapo binadamu hao walitembea kwa miguu miwili.

Taasisi zinazoshiriki maadhimisho hayo ambazo zinasimamia maeneo ya urithi wa dunia ni pamoja na Mamlaka ya Hifadhi ya Eneo la Ngorongoro (NCAA), Shirika la hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) Mamlaka ya Uzimamizi wa Wanyamapori (TAWA), Wakala wa Huduma za misitu Tanzania (TFS), pamoja na wawakilishi wa maeneo ya urithi wa dunia kutoka Zanzibar.


TANZANIA NA KENYA ZASAINI MAKUBALIANO YA USHIRIKIANO SEKTA YA NISHATI

May 05, 2026 Add Comment


 📌*Ni kupitia mauziano ya umeme na upembuzi yakinifu mradi wa Bomba la Gesi Dar-es-Salaam- Mombasa*


Waziri wa Nishati Mhe. Deogratius Ndejembi na Waziri wa Nishati na Petroli wa Jamhuri ya Kenya, Mhe. Opiyo Wandayi wamesaini makubaliano ya ushirikiano ya kuanza mauziano ya umeme baina ya Tanzania na Kenya pamoja na upembuzi yakinifu wa mradi wa ujenzi wa bomba la gesi asilia kutoka Dar es Salaam hadi Mombasa.

Makubaliano hayo yamefanyika Mei 04, 2026 Ikulu jijini Dar es Salaam mbele ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan na mgeni wake Rais wa Jamhuri ya Kenya, Mhe. Dkt. William Samoei Ruto ambaye yuko nchini kwa ziara yake ya kitaifa.

TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI YAMKABIDHI RASMI MGOMBEA UBUNGE WA CCM JIMBO LA ISIMANI FOMU ZA KUGOMBEA UBUNGE

May 05, 2026 Add Comment

 

TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) imemkabidhi rasmi fomu za kugombea ubunge wa jimbo la Isimani kwa Emanuela Mtatifikolo Kaganda, kwa ajili ya Uchaguzi Mdogo unaotarajiwa kufanyika Juni 1 mwaka huu.


Zoezi hilo limefanyika katika ofisi za tume zilizopo Ihemi chini ya usimamizi wa Mkurugenzi wa Uchaguzi jimbo la Isimani, Caroline Ang’weni Otieno.

Emanuela alikabidhiwa fomu hizo akisindikizwa na viongozi mbalimbali wa wilaya akiwemo Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wilaya ya Iringa Vijijini, Costantino Kihwele ambapo baada ya kupokea fomu, Emanuela aliwashukuru viongozi na wanachama wote kwa kujitokeza, akisisitiza kuwa ana dhamira ya kutoa mchango chanya kwa maendeleo ya jimbo la Isimani.

Katika hotuba yake, aliwatambua viongozi wa jumuiya zote za chama ikiwemo jumuiya ya wazazi, vijana na UWT, pamoja na madiwani na viongozi wa ngazi mbalimbali.

Aliweka wazi kuwa, licha ya jimbo hilo kupitia kipindi kigumu kutokana na msiba wa aliyekuwa mbunge, wananchi wamethibitisha umoja na mshikamano mkubwa.

Emanuela alitoa shukurani za pekee kwa uongozi wa chama kuanzia ngazi ya shina hadi taifa, kwa kusimamia mchakato wa uteuzi kwa haki na uwazi na alipongeza pia wagombea wenzake walioshiriki mchakato huo na kuonyesha umoja baada ya kukamilika kwa uteuzi.

Aidha, alisisitiza kuwa jimbo la Isimani tangu kuanzishwa kwake limeongozwa na kiongozi mmoja, marehemu William Vangimembe Lukuvi, ambaye alifanya kazi kubwa ya kuliletea maendeleo.

Aliahidi kuendeleza misingi ya maendeleo iliyoachwa na kiongozi huyo.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Iringa Vijijini, Costantino Kihwele, alimpongeza Emanuela kwa kuteuliwa na kamati kuu kuiwakilisha CCM kwenye uchaguzi huo mdogo.

Aliwahimiza wanachama kuendelea na umoja na maandalizi ya kampeni, akieleza kuwa chama kitafanya kampeni za kidiplomasia na za ushahidi wa kazi zilizofanyika.

Kihwele pia aliwapongeza wagombea wengine waliokuwa kwenye mchakato wa awali kwa kuonyesha uzalendo na kukubali matokeo, akiahidi kuwa watashirikishwa kikamilifu katika kampeni zitakapoanza rasmi.

Viongozi na washiriki wa mkutano huo walionyesha hamasa ya pamoja, huku wakiahidi kumpa mgombea wao ushindi wa kishindo katika uchaguzi wa Juni 1.






MBUNGE MWAKIOJA ATANGAZA NEEMA YA SOKA WILAYA MKINGA,AGAWA VIFAA VYA MICHEZO KWA TIMU ZINAZOSHIRIKI LIGI YA WILAYA

May 04, 2026 Add Comment


>Agawa vifaa vya michezo kwa timu zote zinazoshiriki Ligi ya wilaya ya Mkinga

Na Oscar Assenga, MKINGA

Mbunge wa Jimbo la Mkinga mkoani Tanga (CCM), Twaha Mwakioja, ameahidi kushirikiana na wadau mbalimbali wa michezo kuinua kiwango cha soka wilayani humo kwa kuwekeza katika elimu na maendeleo ya waamuzi pamoja na makocha.

Akizungumza wakati wa mchezo wa Ngao ya Jamii uliokwenda sambamba na uzinduzi wa Ligi ya Wilaya ya Mkinga, uliofanyika katika Uwanja wa Chamazi, Kata ya Matamba, Mwakioja alisema lengo lao ni kuwekeza katika michezo kwa vijana ili kuwapatia ajira, kuboresha afya zao, pamoja na kuimarisha amani, mahusiano mema na ushirikiano miongoni mwao.

Alieleza kuwa dhamira yao ni kuwashika mkono vijana ili waweze kupiga hatua kutoka ngazi ya wilaya, kwenda mkoa, kanda na hatimaye ligi za juu, huku yeye akiwa bega kwa bega nao kuhakikisha wanafikia malengo yao.

Mbunge huyo alibainisha kuwa wamepata taarifa ya kuwepo kwa changamoto mbalimbali, ikiwemo uhaba wa makocha na waamuzi wenye sifa. Hivyo, wamejipanga kuwekeza katika mafunzo ya makocha ili kila kata iwe na angalau kocha mmoja mwenye ujuzi na mafunzo rasmi, pamoja na kuandaa waamuzi wenye vyeti ili kuboresha usimamizi wa michezo.

Alisisitiza kuwa uwekezaji huo utaenda sambamba na ushirikiano na Chama cha Soka Wilaya ya Mkinga katika kukuza na kuendeleza vipaji vya vijana.

Aidha, alisema mpango wao ni kuhakikisha kila kata na kijiji kinakuwa na timu ya mpira wa miguu inayoshiriki ligi ya wilaya. Aliongeza kuwa watawekeza zaidi ili kuibua timu imara zitakazoweza kushiriki ligi za ngazi ya mkoa, kanda na hatimaye Ligi Kuu, hatua itakayosaidia kuitangaza Mkinga katika ramani ya soka nchini.

Katika kuonyesha dhamira hiyo, Mwakioja alikabidhi jezi na mipira kwa timu zinazoshiriki ligi hiyo, ikiwa ni sehemu ya kuhamasisha na kusaidia maendeleo ya michezo wilayani humo.

Kwa upande wake, Katibu wa Chama cha Soka Wilaya ya Mkinga, Fadhili Habibu, alisema ratiba ya ligi hiyo imeanza Mei 4 katika kituo cha Mkinga, huku kituo cha Maramba kikitarajiwa kuanza Mei 6 (Jumatano), ambapo kutakuwa na vituo vinne vitakavyochezwa katika Kijiji cha Maramba, ikiwa ni pamoja na mechi kati ya Viva Dynamo na Maramba FC.

Habibu alisema lengo la ligi hiyo ni kusimamia na kuibua vipaji vya vijana, pamoja na kuwapa mwelekeo wa maendeleo yao kisoka. Alimshukuru mbunge kwa kujitoa na kushirikiana nao katika kufanikisha malengo hayo.

Naye Mwenyekiti wa Chama cha Soka Wilaya ya Mkinga, Hassan Zumo, alimpongeza mbunge kwa juhudi zake za kuendeleza michezo wilayani humo, akieleza kuwa hatua hiyo imeongeza hamasa na matarajio ya ushindani mkubwa katika ligi hiyo, hasa baada ya timu kukabidhiwa vifaa.

Zumo aliongeza kuwa tangu kuanzishwa kwa chama hicho mwaka 2008, wamekuwa wakipeleka vilabu katika mashindano ya ngazi ya mkoa lakini wamekuwa wakikwama kutokana na changamoto za kifedha. Hata hivyo, alisema kupitia uongozi wa Mbunge Mwakioja, wana matumaini ya kupata timu itakayoweza kufika hadi Ligi Kuu.

Aidha, timu zinazoshiriki mashindano hayo zimeahidi kujituma na kupambana kwa juhudi zote ili kuhakikisha ligi hiyo inaleta mafanikio na tija kwa vijana wa Wilaya ya Mkinga.




WANANCHI WA DODOMA WAPONGEZA JUHUDI ZA SERIKALI MKAKATI WA MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA

May 04, 2026 Add Comment

 



Na Mwandishi Wetu, Dodoma.

Wananchi wa Dodoma wamepongeza juhudi za Serikali kupitia mkakati wa kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia, wakieleza kuwa mkakati huo unasaidia kuboresha afya, kuokoa muda na kulinda mazingira.
Hayo yamejiri leo tarehe 4 Mei 2026 katika Soko la Mavunde, Chang’ombe, ambapo wananchi wamepata elimu ya nishati safi ya kupikia kwa nadharia na vitendo, ikiwemo mafunzo ya jinsi ya kutumia nishati hizo kwa usahihi na kwa ufanisi zaidi katika shughuli za upishi wa kila siku.
Baadhi ya wananchi waliohudhuria wamesema kuwa elimu hiyo ya vitendo imewasaidia kuelewa kwa urahisi faida za nishati safi, hususan kupunguza moshi majumbani unaochangia magonjwa ya njia ya hewa na kurahisisha shughuli za upishi.
Aisha Ramadhani, mmoja wa wananchi waliohudhuria na ni mkazi wa Kata ya Chang’ombe, amesema amefurahishwa na kampeni hiyo inayoendelea jijini Dodoma, akibainisha kuwa elimu aliyoipata imemsaidia kubadili mtazamo wake kuhusu matumizi ya nishati, na sasa anaelewa vizuri faida za kutumia nishati safi kama vile kupunguza matumizi ya kuni na mkaa, kuokoa muda pamoja na kuboresha afya ya familia.
Akizungumza katika eneo hilo, mtaalamu kutoka Wizara ya Nishati, Kitengo cha Nishati Safi ya Kupikia, Nsajigwa Maclean, amesema Serikali inaendelea kutekeleza mkakati kwa kuhakikisha nishati safi ya kupikia inapatikana kwa urahisi, kwa gharama nafuu na kuwafikia wananchi wa makundi yote bila kujali kipato au eneo wanaloishi.
Aidha, amefafanua kuwa serikali imeweka juhudi katika kutoa elimu endelevu kwa jamii kupitia mafunzo ya vitendo, ili kuhakikisha wananchi wanapata uelewa wa kina kuhusu matumizi salama ya nishati safi, pamoja na kuhimiza mabadiliko ya tabia kutoka matumizi ya kuni na mkaa kwenda nishati mbadala inayolinda afya na mazingira.
Wananchi waliohudhuria wameeleza kuridhishwa na juhudi hizo za Serikali na kuahidi kuendelea kuhamasishana juu ya matumizi ya nishati safi ya kupikia katika maeneo yao wanayoishi.