HABARI

SIASA

ELIMU

Recent Posts

WAZIRI SANGU: SERIKALI INATHAMINI MCHANGO WA TAASISI ZA DINI KATIKA KUJENGA AMANI NA MAENDELEO YA TAIFA

June 19, 2026 Add Comment
SERIKALI imeendelea kuthamini mchango mkubwa unaotolewa na taasisi za kidini nchini katika kuimarisha amani, mshikamano na maendeleo ya taifa.

RAIS WA NAMIBIA AWASILI KWA ZIARA YA KITAIFA

June 19, 2026 Add Comment
Rais wa Jamhuri ya Namibia, Mhe. Dkt. Netumbo Nandi-Ndaitwah, amewasili nchini kwa Ziara ya Kitaifa ya siku tatu kuanzia tarehe 19 hadi 21 Juni 2026, kwa mwaliko wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan.

PPAA YAJIVUNIA MAFANIKO MODULI YA MALALAMIKO, RUFAA

June 19, 2026 Add Comment



Na Mwandishi Wetu, Dodoma


Mamlaka ya Rufani ya Zabuni za Umma (PPAA) imeendelea kujivunia mafanikio ya matumizi ya Moduli ya kupokea na kushughulikia malalamiko na rufaa kieletroniki kupitia mfumo Mfumo wa Ununuzi wa Umma wa Tanzania (NeST).

Mafanikio hayo yamebainishwa na Katibu Mtendaji wa PPAA, Bw. James Sando alipotembelea banda la Mamlaka hiyo kwenye maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayoendelea katika Viwanja vya Chinangali, Jijini Dodoma.

Bw. Sando amesema kuwa moduli ya kupokea na kushughulikia malalamiko na rufaa ilianzishwa ili kutatua changamoto mbalimbali zilizokuwa zinajitokeza kwenye utatuzi wa migogoro kwenye michakato ya ununuzi wa umma.

“Changamoto tulizoziondoa kwa wazabuni na taasisi nunuzi ni pamoja kuokoa muda, gharama, uwazi na uwajibikaji pamoja na kumbukumbu sahihi za malalamiko na rufaa zinazowasilishwa na wazabuni,” amesema Bw. Sando.

Bw. Sando amebainisha kuwa ili PPAA iweze kufanya maamuzi kuhusu shauri lililowasilishwa kwa Mamlaka hiyo ni lazima kuwa na kumbukumbu sahihi za shauri hilo, hivyo kupitia moduli PPAA imeweza kupata nyaraka mbalimbali zinazohitajika kwa wakati. 

“moduli ya kupokea na kushughulikia malalamiko na rufaa imeziunganisha taasisi nunuzi na PPAA, faida zote hizi zimeletwa na moduli hii,” ameongeza Bw. Sando


“Kwa Mwaka wa fedha 2025/26 hadi sasa malalamiko takribani 157 yamewasilishwa kupitia moduli hiyo kwa taasisi nunuzi, na kati ya malalamiko hayo mashauri 37 yamewasilishwa PPAA na kutolewa uamuzi, hivyo matumizi ya moduli yanaendelea vyema,” ameongeza Bw. Sando

PPAA inampango wa kuunganisha sekta ya utoaji haki katika ununuzi wa umma na mfumo wa utoaji haki wa Mahakama ya Tanzania kwa mwaka wa fedha ujao ili kuongeza uwazi na uwajibikaji zaidi.

MADEREVA WANAOSAFIRISHA KEMIKALI WAZINGATIE MAFUNZO

June 19, 2026 Add Comment
NA Oscar Nkembo

Msimamizi wa Dawati la Ukaguzi wa Kemikali wa Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali Ofisi ya Kanda ya Kati, Suitbert Sinduhije amesema Mamlaka imedhibiti Kemikali ya Sulphur iliyomwagika eneo la Mikumi na amewataka Madereva kuzingatia mafunzo wanayopata huku akiwasihi Wananchi kutoa taarifa kwa Mamlaka pindi ajali za Kemikali zinapotokea.

NEMC YACHOCHEA UWAJIBIKAJI JUMUISHI: SEKTA YA MAZINGIRA

June 19, 2026 Add Comment
Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) linaendelea kuhimiza ushiriki wa wadau mbalimbali katika uhifadhi na usimamizi wa mazingira, likieleza kuwa mafanikio katika sekta hiyo yanategemea ushirikiano wa wananchi, taasisi za umma, sekta binafsi na washirika wa maendeleo.

DC NGUBIAGAI AONGOZA VITA DHIDI YA UVUVI HARAMU UKEREWE

June 19, 2026 Add Comment

  

Mkuu wa Wilaya ya Ukerewe Cde. Christopher Ngubiagai akihutubia wananchi wa Gana katika mkutano
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe Ndg. Vicent Mbua akizungumza na wananchi wa Gana kuachana na uvuvi haramu

Na Mwandishi Wetu - Ukerewe

Mikakati ya Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, ya kuimarisha usimamizi wa rasilimali za taifa na kuhakikisha sekta ya uvuvi inachangia kikamilifu ukuaji wa uchumi inaendelea kuzaa matunda, ambapo Wilaya ya Ukerewe imeendelea kuchukua hatua madhubuti dhidi ya uvuvi haramu.

WALIPAKODI MCHIKICHINI WAPONGEZWA KWA MCHANGO WAO KATIKA MIAKA 30 YA MAFANIKIO YA TRA

June 19, 2026 Add Comment
Kariakoo, 18 Juni, 2026

Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Mkoa wa Kikodi Kariakoo imewapongeza walipakodi wa eneo la Mchikichini kwa mchango wao mkubwa ambao umekuwa sehemu muhimu ya mafanikio ya Mamlaka, katika kipindi cha miaka 30 tangu kuanzishwa kwake.

WAAJIRI WANAOZINGATIA SHERIA ZA KAZI WAPONGEZWA

June 18, 2026 Add Comment
Na OWM-KAM, Mwanza

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Ajira na Mahusiano), Mhe. Deus Sangu, amepongeza waajiri nchini wanaotekeleza wajibu wao kwa kuzingatia sheria za kazi, ikiwemo kuwasilisha michango ya wafanyakazi katika Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) kwa lengo la kulinda maslahi ya wafanyakazi dhidi ya madhara yanayotokana na kazi.
MKURUGENZI WA UCHAGUZI APONGEZA UFANISI NA UWAZI WA MFUMO WA UAGIZAJI MAFUTA KWA PAMOJA

MKURUGENZI WA UCHAGUZI APONGEZA UFANISI NA UWAZI WA MFUMO WA UAGIZAJI MAFUTA KWA PAMOJA

June 18, 2026 Add Comment
 

Na Mwandishi Wetu

Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Bw. Ramadhan Kailima, amepongeza ufanisi na uwazi wa Mfumo wa Uagizaji Mafuta kwa Pamoja unaosimamiwa na Wakala wa Uagizaji Mafuta kwa Pamoja, akieleza kuwa mfumo huo umechangia kuimarisha ukusanyaji wa mapato ya Serikali na kuhakikisha upatikanaji wa mafuta nchini.

Bw. Kailima alitoa pongezi hizo Juni 18, 2026 alipotembelea banda la PBPA katika Maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayoendelea katika viwanja vya Chinangali jijini Dodoma.

Akizungumza baada ya kupata maelezo kuhusu utekelezaji wa mfumo huo, alisema kuwa umejengwa katika misingi ya uwazi na ushindani, jambo linalosaidia kupunguza gharama za uagizaji wa mafuta na kuongeza ufanisi katika usimamizi wa sekta hiyo muhimu kwa uchumi wa nchi.

Akitoa ufafanuzi kwa mgeni huyo, Mkaguzi wa Mafuta wa PBPA, Bw. Issa Mwitazy, alisema kuwa katika mfumo wa uagizaji mafuta kwa pamoja, ushindani hujikita katika gharama za usafirishaji wa mafuta (Premium).

Alieleza kuwa wazabuni hushindanishwa kwa kuwasilisha bei za usafirishaji wa bidhaa za petroli, dizeli na mafuta ya taa, ambapo mzabuni mwenye gharama nafuu zaidi hupatiwa zabuni husika.

“Utaratibu huu umetuwezesha kuhakikisha upatikanaji wa mafuta ya kutosha nchini wakati wote na wakati huohuo kuipa Serikali taarifa sahihi za kiasi cha mafuta na hivyo kuwezesha ukusanyaji wa mapato yatokanayo na biashara ya mafuta,” alisema.

Aliongeza kuwa mikataba ya uagizaji wa mafuta husainiwa mapema kabla ya bidhaa kuwasili nchini, jambo linaloiwezesha Serikali kufanya makadirio sahihi ya mapato yatokanayo na sekta hiyo.

Kwa mujibu wa Mwitazy, mafanikio ya mfumo huo yameifanya PBPA kuwa kitovu cha huduma za uagizaji mafuta kwa nchi kadhaa za ukanda wa Afrika Mashariki na Kati, zikiwemo Malawi, Rwanda, Zambia na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, ambazo huleta mahitaji yao kupitia mfumo wa uagizaji wa mafuta kwa pamoja.

Ziara ya Bw. Kailima katika banda la PBPA ni sehemu ya shughuli za Maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayolenga kuonesha mafanikio, huduma na ubunifu unaotekelezwa na taasisi za umma katika kuwahudumia wananchi na kuchangia maendeleo ya taifa.

Wananchi Dodoma Wajifunza Haki Zao Kupitia Elimu ya Vipimo Sahihi

Kajunason June 18, 2026 Add Comment

 Na Mwandishi Wetu, Dodoma


Wananchi waliotembelea banda la Wakala wa Vipimo (WMA) katika Maonesho ya Kitaifa ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayoendelea katika Viwanja vya Chinangali Park, Dodoma, wameeleza kufurahishwa na elimu wanayoipata kuhusu matumizi sahihi ya vipimo na kuahidi kuwa mabalozi wa kuelimisha jamii kuhusu umuhimu wa kuhakiki vipimo katika shughuli za kila siku.

Siku ya tatu ya maonesho hayo yaliyofunguliwa Juni 16 na yanayotarajiwa kuhitimishwa Juni 23, 2026, banda la WMA limeendelea kuvutia idadi kubwa ya wananchi wanaotaka kujifunza namna Serikali inavyohakikisha vipimo vinavyotumika katika biashara na huduma mbalimbali vinakuwa sahihi na vya kuaminika.

Mmoja wa wananchi hao, Bw. Bilson Vedastus, alisema elimu aliyopata imemsaidia kuelewa mambo muhimu ya kuzingatia anaponunua mafuta, gesi ya kupikia na bidhaa nyingine zinazopimwa.

“Awali sikuwa naelewa mambo haya kwa kina, lakini sasa najua ninachopaswa kuangalia ninapojaza mafuta, kununua sukari au gesi ya kupikia,” alisema.

Kwa upande wake, Bi. Asha Siyaya alisema elimu hiyo imewapa uwezo wa kutambua udanganyifu unaoweza kufanywa kupitia vipimo visivyo sahihi na kuahidi kutoa taarifa pale watakapobaini ukiukwaji.

“Tumeona jinsi pampu za mafuta, mizani na vifaa vingine vinavyohakikiwa ili kuhakikisha vinapima kwa usahihi. Hatuwezi kukaa kimya tukiona mteja anadhulumiwa. Tutawaeleza wengine na kuripoti udanganyifu popote tutakapouona,” alisema.

Wataalamu wa WMA, Albogast Kajungu, Mbwana Amani na Said Ibrahim, waliwaeleza wananchi kuwa huduma za uhakiki wa vipimo zinagusa sekta nyingi zinazohusiana moja kwa moja na maisha ya kila siku ya wananchi.

Walifafanua kuwa pampu za mafuta huhakikiwa na kuwekewa alama za uthibitisho, huku mizani inayotumika sokoni na madukani kupimia bidhaa mbalimbali ikikaguliwa mara kwa mara ili kuhakikisha watumiaji wanapata kiwango stahiki cha bidhaa wanazonunua.

Aidha, mita za maji na umeme zinazotumika majumbani na katika biashara huhakikiwa ili kuhakikisha wateja wanalipia matumizi halisi, huku mitungi ya gesi ya kupikia, bidhaa zilizofungashwa pamoja na mizani za kupimia uzito wa magari barabarani nazo zikiendelea kufanyiwa ukaguzi wa mara kwa mara.

Akizungumza na waandishi wa habari, Meneja Mawasiliano wa Wakala wa Vipimo, Bi. Veronica Simba, alisema lengo la WMA ni kuhakikisha kila mwananchi anapata thamani halisi ya fedha anayolipia bidhaa na huduma mbalimbali.

Alitoa wito kwa wananchi kuendelea kutembelea banda la WMA katika maonesho hayo ili kupata elimu zaidi kuhusu haki zao na umuhimu wa matumizi ya vipimo sahihi katika shughuli za kijamii na kiuchumi.


TANZANIA YAIMARISHA UTAYARI WA KUKABILIANA NA TISHIO LA EBOLA

June 18, 2026 Add Comment

NA EMMANUEL MBATILO, DODOMA

SERIKALI imesema Tanzania bado haina mgonjwa wa Ebola na hali ya usalama wa afya nchini inaendelea kuwa nzuri, huku ikieleza kuwa imeimarisha hatua mbalimbali za kuzuia ugonjwa huo kuingia nchini kutokana na mlipuko unaoendelea katika nchi jirani za Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) na Uganda.

WAZIRI RIDHIWANI KIKWETE AFUNGUA RASMI MAADHIMISHO YA WIKI YA UTUMISHI WA UMMA

June 18, 2026 Add Comment
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhwani Jakaya Kikwete (Mb), amefungua rasmi Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma 2026 katika Viwanja vya Chinangali Park jijini Dodoma, yanayofanyika kuanzia Juni 16 hadi 23, 2026 yakibeba kaulimbiu isemayo, "Kuchochea Uwajibikaji Jumuishi kwa Huduma Endelevu."

MTANDAO WATWAA ASILIMIA 44 YA MAWASILISHO YA SAMIA KALAMU

Kajunason June 17, 2026 Add Comment

Dar es Salaam, Juni 17, 2026 – Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), kwa kushirikiana na Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania (TAMWA) na Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), imewahimiza waandishi wa habari na vyombo vya habari nchini kuendelea kuwasilisha kazi zao za kuwania Tuzo za Samia Kalamu 2026 kabla ya kufungwa kwa dirisha la maombi mwishoni mwa mwezi huu.

Taarifa iliyotolewa jijini Dar es Salaam imeeleza kuwa hadi Juni 15, 2026, jumla ya kazi 624 zilikuwa zimewasilishwa kutoka vyombo mbalimbali vya habari nchini, huku vyombo vya habari mtandaoni vikiongoza kwa idadi kubwa ya kazi zilizowasilishwa.

Takwimu zinaonyesha kuwa vyombo vya habari mtandaoni vimewasilisha kazi 276, sawa na asilimia 44 ya kazi zote zilizopokelewa. Magazeti yamewasilisha kazi 178 (asilimia 29), televisheni kazi 102 (asilimia 16), redio kazi 60 (asilimia 10), huku majarida yakichangia kazi nane pekee, sawa na asilimia moja ya jumla ya mawasilisho.

Waandaaji wa tuzo hizo wameeleza kuwa Samia Kalamu Awards zinalenga kuhamasisha ubora, weledi na uwajibikaji katika uandishi wa habari za maendeleo, kwa kutambua mchango wa wanahabari katika kuelimisha na kuhamasisha jamii kuhusu masuala ya maendeleo ya kijamii na kiuchumi.

Kazi zinazostahili kushindanishwa ni zile zilizochapishwa au kurushwa katika vyombo vya habari kati ya Julai 1, 2025 na Juni 30, 2026.

Aidha, waandishi na taasisi za habari zimekumbushwa kuwa dirisha la kuwasilisha kazi litafungwa rasmi Juni 30, 2026 saa 5:59 usiku, hivyo zinapaswa kutumia muda uliobaki kuhakikisha kazi zao zinawasilishwa kwa wakati kupitia tovuti rasmi ya tuzo hizo.

Tuzo za Samia Kalamu zilianzishwa mwaka 2025 na zimekuwa jukwaa muhimu la kutambua na kuenzi mchango wa waandishi wa habari katika kuendeleza taifa kupitia kaulimbiu ya “Kalamu kwa Maendeleo.”

Kwa mujibu wa waandaaji, waandishi na vyombo vya habari vinakaribishwa kuendelea kushiriki ili kuhamasisha uandishi wenye tija kwa maendeleo ya Tanzania.

UKEREWE YAWEKA KIPAUMBELE KWA WENYE ULEMAVU, VIJANA NA WANAWAKE KUPITIA MIKOPO YA MAENDELEO

June 17, 2026 Add Comment
Mkuu wa wilaya ya Ukerewe Cde. Christopher Ngubiagai
Dhamira ya Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, ya kuwawezesha wananchi kiuchumi kupitia mikopo ya asilimia 10 ya mapato ya ndani inaendelea kuzaa matunda, huku Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe ikitekeleza kwa vitendo maelekezo hayo kwa kutoa mikopo yenye thamani ya Shilingi milioni 586.5 kwa vikundi 57 vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu.

SANGU :MAHUSIANO MEMA NI MSINGI WA KUIMARISHA UMOJA NA DEMOKRASIA NCHINI

June 17, 2026 Add Comment
Na. OWM (KAM), Morogoro

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano Deus Sangu amesema mahusiano mema, mazungumzo ya kujenga na mshikamano wa kitaifa ni nguzo muhimu katika kuimarisha demokrasia, amani na maendeleo endelevu nchini.

WADAU WA MADINI WAKUMBUSHWA KUZINGATIA SHERIA KUONGEZA MANUFAA KWA TAIFA

June 17, 2026 Add Comment
-DODOMA

Wadau wa Sekta ya Madini wamehimizwa kuzingatia sheria, kanuni na taratibu zinazosimamia shughuli za madini ili kuhakikisha rasilimali hizo zinaendelea kuchangia maendeleo ya taifa na kunufaisha wananchi.
TBS KUADHIMISHA MIAKA 50, KUZINDUA KITABU CHA HISTORIA YAKE DODOMA

TBS KUADHIMISHA MIAKA 50, KUZINDUA KITABU CHA HISTORIA YAKE DODOMA

June 17, 2026 Add Comment

Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Viwango Tanzania (TBS), Dkt. Ashura Katunzi,akitoa taarifa kwa umma kuelekea kuhitimisha maadhimisho ya miaka 50 tangu kuanzishwa kwake Juni 19,2026 jijini Dodoma.

...

Shirika la Viwango Tanzania (TBS) linatarajia kuandika historia mpya Juni 19, 2026 kwa kuhitimisha maadhimisho ya miaka 50 tangu kuanzishwa kwake, huku likitarajia kuzindua kitabu maalumu kitakachobeba historia, mafanikio na mchango wake katika maendeleo ya viwanda, biashara na ustawi wa Watanzania.

Akizungumza jijini Dodoma kuhusu maandalizi ya kilele cha maadhimisho hayo, Mkurugenzi Mkuu wa TBS, Dkt. Ashura Katunzi, amesema hafla hiyo itafanyika katika ofisi za shirika hilo na inatarajiwa kuhudhuriwa na wadau mbalimbali kutoka sekta za umma na binafsi.

Dkt. Katunzi amesema mgeni rasmi katika kilele cha maadhimisho hayo anatarajiwa kuwa Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Judith Salvio Kapinga (Mb), ambaye ataungana na viongozi, wadau na wananchi kusherehekea mafanikio ya nusu karne ya taasisi hiyo muhimu nchini.

Amesema sambamba na sherehe hizo, TBS itazindua kitabu maalumu cha miaka 50 kitakachoelezea safari ya shirika hilo tangu kuanzishwa kwake, hatua mbalimbali za maendeleo iliyopitia pamoja na mchango wake katika kuhakikisha bidhaa na huduma zinazotolewa nchini zinazingatia viwango vinavyotakiwa.

“Kitabu hiki kitakuwa sehemu ya kumbukumbu muhimu ya taifa. Kitaelezea historia ya TBS, mafanikio yaliyopatikana katika kipindi cha miaka 50 na kitakuwa rejea kwa vizazi vya sasa na vijavyo ili kuelewa mchango wa shirika katika maendeleo ya nchi,” amesema Dkt. Katunzi.

Ameeleza kuwa kwa kipindi cha miaka 50, TBS imeendelea kuwa mhimili muhimu katika kulinda afya na usalama wa watumiaji wa bidhaa mbalimbali, huku ikichochea ukuaji wa viwanda kwa kuhakikisha bidhaa zinazozalishwa nchini zinakuwa bora na zenye ushindani katika masoko ya ndani na nje ya nchi.

Kwa mujibu wa Dkt. Katunzi, mafanikio yaliyofikiwa na TBS katika kipindi hicho si ya shirika pekee bali ni matokeo ya ushirikiano mkubwa kati ya taasisi hiyo, wadau wa maendeleo, sekta binafsi na wananchi kwa ujumla.

“Miaka 50 ya TBS ni mafanikio ya wadau wetu na jamii kwa ujumla. Tunawakaribisha wananchi na wadau wote kushiriki katika kilele cha maadhimisho haya ili kwa pamoja tuadhimishe safari hii ya mafanikio,” amesema.

Maadhimisho hayo yanatarajiwa kuwa fursa ya kutafakari mchango wa TBS katika maendeleo ya taifa, huku yakitoa mwanga wa matarajio na mwelekeo wa shirika hilo katika kuendelea kuimarisha ubora wa bidhaa na huduma kwa manufaa ya Watanzania na uchumi wa nchi.

TANESCO MUONGEZE VITUO VYA KUCHAJIA VYOMBO VYA USAFIRI VINAVYOTUMIA UMEME-WAZIRI RIDHIWANI

June 17, 2026 Add Comment


Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete amelitaka Shirika la umeme Tanzania ( TANESCO) kuongeza vituo vya kuchajia vyombo vya usafiri vinavyotumia nishati ya  umeme ili kuongeza wigo wa utoaji huduma hiyo ambayo imeonekana kuleta mageuzi katika matumizi ya nishati safi.


Mhe. Ridhiwani ameyasema hayo Juni 17, 2026 alipotembelea Banda la TANESCO katika Maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayoendelea kufanyika katika Viwanja vya Chinangali Mkoani Dodoma.

Waziri huyo mwenye dhamana ya Utumishi ametumia nafasi hiyo kuipongeza TANESCO kwa kuendelea kuhamasisha matumizi ya Nishati safi kwa ajili ya  kupikia na katika vyombo vya usafiri.


‘’ TANESCO mnafanya kazi kubwa nawapongeza kwa mageuzi ya matumizi ya nishati ya umeme katika vyombo vya usafiri, natoa rai muongeze Vituo vya kuchajia vyombo hivyo ili kuongeza wigo wa utoaji huduma,’’ alisisitiza Mhe. Ridhiwani

Naye Meneja Masoko Bw. Fredrick Kalinga amesema TANESCO inashiriki katika Maonesho hayo ili kutoa elimu kwa wananchi juu ya huduma na bidhaa zinazotolewa na Shirika ikiwemo maendeleo ya miradi ya uzalishaji, usafirishaji na usambazaji umeme, maboresho makubwa yaliyofanywa na Shirika kwenye mifumo ya kidigitali ya utoaji huduma kwa wateja pamoja na kuhamasisha jamii kutumia nishati safi ya umeme kupikia na katika vyombo vya usafiri kama magari, bajaji, guta, na pikipiki.

Maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma kwa mwaka 2026  yenye kauli mbiu isemayo ‘’Kuchochea Uwajibikaji Jumuishi kwa huduma Endelevu’’ yameanza rasmi Juni 16, 2026 na yanatarajiwa kuhitimishwa Juni 23, 2026





KUELEKEA MAADHIMISHO YA MIAKA 30,TRA YAFANYA KONGAMANO LA MAADILI NA VIONGOZI WA DINI

June 17, 2026 Add Comment

 



Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), kupitia Idara ya Mambo ya Ndani (INAD), leo Juni 17, 2026 imeandaa Kongamano la Maadili lililowakutanisha viongozi wa dini mbalimbali kujadili nafasi ya maadili katika kuimarisha ukusanyaji wa kodi na kujenga utamaduni wa ulipaji kodi kwa hiari. Kongamano hilo ni sehemu ya maandalizi ya Maadhimisho ya Miaka 30 ya TRA yatakayofanyika Julai 1, 2026.

Akifungua kongamano hilo kwa niaba ya Kamishna Mkuu wa TRA, Naibu Kamishna wa TRA, Bw. Mcha Hassan Mcha, amesema kuwa katika kipindi cha miaka 30 tangu kuanzishwa kwa TRA, taasisi hiyo imepiga hatua kubwa katika kuimarisha mifumo ya ukusanyaji wa mapato, huku maadili yakiendelea kuwa nguzo muhimu katika utekelezaji wa majukumu yake.

Bw. Mcha amesema TRA inaendelea kuwekeza katika mifumo na mikakati mbalimbali ya kuimarisha maadili kwa watumishi wake na walipakodi ili kujenga uaminifu, uwajibikaji na kuongeza kiwango cha ulipaji kodi kwa hiari.

“Maadili hujenga imani, na imani hujenga ulipaji wa kodi kwa hiari,” alisema Bw. Mcha.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Jumuiya ya Maridhiano Tanzania (JMAT), Sheikh Alhad Mussa Salum, ameipongeza TRA kwa kuandaa kongamano hilo na kueleza kuwa maadili ni msingi muhimu wa maendeleo ya jamii na taifa. Amesema mafundisho ya dini yanasisitiza uadilifu, uwajibikaji na kufanya mema, huku ulipaji wa kodi ukiwa sehemu ya wajibu unaochangia ustawi wa wananchi na maendeleo ya nchi.

Naye Mkuu wa Evangelical Fellowship Church Tanzania, Askofu Charles Asher Howard, amesema maandiko matakatifu yanaelekeza waumini kutimiza wajibu wao kwa mamlaka halali, ikiwemo kulipa kodi. Amebainisha kuwa maendeleo ya Tanzania yanategemea mchango wa kila mwananchi, hivyo ulipaji wa kodi ni jukumu la pamoja linalopaswa kutekelezwa kwa uaminifu na uzalendo.

Viongozi hao wa dini wamepongeza hatua ya TRA ya kuwashirikisha katika mijadala ya maadili na ukusanyaji wa mapato, wakisisitiza kuwa ushirikiano kati ya taasisi za umma na viongozi wa dini una nafasi muhimu katika kuhamasisha wananchi kulipa kodi kwa hiari na kujenga taifa lenye uwajibikaji, uadilifu na maendeleo endelevu.


















WAZIRI KIKWETE AVUTIWA NA MFUMO WA KUPANGA NA KUSIMAMIA MIRADI YA REA

June 17, 2026 Add Comment

 



*📌Asema REA Digital Platform ni mfumo wa kisasa kueleza miradi*


📍Chinangali Park - Dodoma


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete, amevutiwa na mfumo wa Kupanga na Kusimamia miradi ya Wakala wa Nishati Vijijini (REA). 


Mhe. Kikwete ameipongeza REA kwa kuja na mfumo huo mara baada ya kutembelea banda hilo kwenye ufunguzi wa Maadhimiaho ya Wiki ya Utumishi kwa Umma 2026 yanayofanyika katika viwanja vya Chinangali Park jijini Dodoma. 

Mfumo huo (*REA DIGITAL PLATFORM*) unaonyesha miradi yote inayotekelezwa na REA na kuweza kuisimamia kidijitali na kuwapa taarifa wadau popote walipo duniani kuhusiana na miradi ya Nishati vijijini.

Akimueleza Mhe. Kikwete, Afisa Upimaji Mwandamizi wa REA, Bw. Hussein Shamdas ameeleza kuwa kupitia mfumo huo mwananchi anaweza kujua mipango ya Wakala kwenye eneo lake na kufuatilia miradi inayotekelezwa na Wakala katika eneo husika.



Mwisho

UMEME UPO WA KUTOSHA :MNAANGAZA MAISHA YA WANANCHI-MHE.KIKWETE

June 17, 2026 Add Comment


Waziri wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwan Kikwete ameipongeza Wizara ya Nishati na Taasisi zake kwa kuendelea kuhamasisha Matumizi ya Nishati Safi kwa Wananchi pamoja na kuimarika kwa upatikanaji wa huduma za nishati nchini.


Kikwete amesema hayo Juni 17, 2026  alipotembelea Banda la Wizara ya Nishati na Taasisi zake wakati wa maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayofanyika Katika viwanja vya Chinangali jijini   Dodoma.

 Aidha, amesisitiza Wizara pamoja na Taasisi zake kuendelea kutoa elimu kwa wananchi kuhusu Matumizi ya Nishati Safi ili Kila mmoja aifahamu kwa kina kwa manufaa  ya kulinda Afya na mazingira.

" Hongerani Sana Nishati kwa kuendelea kuwasha Umeme na kuangaza Maisha ya Wananchi, tunaona Umeme upo wa kutosha" Alisema Kikwete 


Sambamba na hilo amesisitiza  kuendelea kutangaza fursa zilizopo katika Sekta ya Nishati nchini kwa wananchi.

Ametembelea Taasisi  zilizo chini ya Wizara ya Nishati ambazo ni TANESCO, REA, TPDC, EWURA, PURA,PBPA na EWURA CCC ambapo alipata fursa ya kujionea huduma zinazotolewa na taasisi hizo pamoja na mafanikio ya miradi mbalimbali inayotekelezwa.

NEMC YASISITIZA MASHIRIKIANO KATIKA UHIFADHI NA USIMAMIZI WA MAZINGIRA

June 17, 2026 Add Comment

Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) limesisitiza ushirikiano wa wadau wote wakiwemo Serikali, Sekta binafsi, taasisi za umma, jamii na wananchi katika  kusimamia na kuhifadhi mazingira kwa maendeleo endelevu.


Akizungumza na waandishi wa habari tarehe 17 Juni, 2026 katika ukumbi wa mikutano wa NEMC Jijini Dar es salaam, Kaimu Meneja Uhusiano na Mawasiliano kwa Umma NEMC, Bi. Martha Kawishe, amesema mazingira ni suala mtambuka linalohitaji kila mdau kutimiza wajibu wake kwa kuzingatia Sheria na Miongozo ya Mazingira iliyowekwa.

Ameeleza kuwa NEMC inaendelea kusimamia utekelezaji wa Sheria kupitia ukaguzi wa miradi, utoaji wa elimu kwa umma katika masuala mazima ya udhibiti wa kelele chafuzi za mazingira, uharibifu wa vyanzo vya maji, utupaji holela wa taka, kutiririsha maji taka msimu wa mvua, ukataji hovyo wa miti na kuhakikisha miradi yote inazingatia Tathmini ya Athari kwa Mazingira (TAM) kabla ya kuanza.


Aidha, amewataka wananchi kuwa makini na watu wanaojifanya maafisa wa NEMC kwa lengo la udanganyifu, akisisitiza kuwa malipo yote hufanyika kwa utaratibu wa kiserakili na ukaguzi hufanywa na maafisa kisheria wakiwa na vithibitsho vifuatavyo: vitambulisho vya ukaguzi, vitambulisho vya kazi pamoja na nyaraka zinazompa mamlaka kisheria ya kufanya ukaguzi, na hasa ikizingatiwa ukaguzi hufanywa kidigitali ambapo mteja hupokea ujumbe mara baada ya ukaguzi.

NEMC pia imehimiza wananchi kutumia huduma rasmi ya kituo cha huduma kwa mteja kwa kupiga namba ya  bure 0800110115 na kutumia mfumo wa e-mrejesho kwa kufuata menyu ya *152*00# na kufuata maelekezo ili kutoa ushauri, taarifa au changamoto za kimazingira.

RC MBONI MHITA AWEKA JIWE LA MSINGI JENGO LA KISASA LA BILIONI 5.3 USHETU,

June 17, 2026 Add Comment

 

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Mboni Mhita, akiwa pamoja na Mbunge wa Jimbo la Ushetu, Mhe. Emmanuel Cherehani na viongozi mbalimbali wa Serikali, wakipanda lift ndani ya Jengo jipya la Utawala la Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu. Picha na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Mboni Mhita (kulia), akiweka jiwe la msingi wa Jengo jipya la Utawala la Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu lililopo Nyamilangano, wilayani Kahama.
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Mboni Mhita, akifungua mlango na kuingia rasmi ndani ya Jengo jipya la Utawala la Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu mara baada ya kuweka jiwe la msingi la mradi huo wa kimkakati uliopo Nyamilangano.