HABARI

SIASA

ELIMU

Recent Posts

FCC YAHIMIZA WADAU KUUNGANA KULINDA AFYA NA UCHUMI

FCC YAHIMIZA WADAU KUUNGANA KULINDA AFYA NA UCHUMI

June 26, 2026 Add Comment
 

Serikali imetoa wito kwa wazalishaji, waingizaji bidhaa, wasambazaji, wafanyabiashara, vyombo vya habari, vyombo vya dola, mamlaka za forodha, Taasisi za umma, asasi mbalimbali pamoja na wananchi kwa ujumla kuendelea kushirikiana kwa karibu na Tume ya Ushindani (FCC) katika kubaini na kudhibiti bidhaa bandia.

Vilevile, ameipongeza FCC kwa kuendelea kuimarisha juhudi katika kukabiliana na changamoto ya bidhaa bandia na kulipa uzito unaostahili katika mipango ya baadaye ili kuendelea kuboresha mazingira ya biashara Nchi

Hayo yamesemwa na Mkuu wa Wilaya ya Temeke, Mhe. Sixtus Mapunda, aliyemwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila, katika kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Kudhibiti Bidhaa Bandia Duniani (WACD) 2026.

Aidha, amesema Serikali ya Awamu ya Sita itaendelea kuunga mkono FCC kupitia maboresho ya sera, sheria na mifumo ili kuhakikisha masoko salama na ushindani wa haki ili kukabiliana na athari zake kwa afya za wananchi na uchumi wa taifa.

Mapunda pia amesema FCC inapaswa kupanua matumizi ya teknolojia katika uchunguzi, ufuatiliaji na udhibiti wa bidhaa bandia, hususan katika masoko ya kidijitali na mipaka ya nchi ili kuziba mianya inayotumiwa na wahalifu wa kiuchumi.

Akizungumzia kaulimbiu isemayo, “Linda Maisha na Masoko Dhidi ya Pombe, Vilainishi na Sigara Bandia,” amesema bidhaa bandia zina madhara kwa afya, hupunguza mapato ya Serikali na kudhoofisha biashara halali.

Naye, Kamishna wa Tume Bw. Said Tunda ambaye alimwakilisha Mwenyekiti wa FCC Dkt. Aggrey Mlimuka amesema kampeni za elimu kwa umma na mijadala ya kitaalamu zimeendelea kuongeza uelewa kuhusu athari za bidhaa bandia kwa afya, uchumi na maendeleo ya biashara halali nchini.

Kwa upande wake, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa FCC, Bi. Khadija Ngasongwa, amesema maadhimisho yanalenga kuongeza uelewa wa umma kuhusu madhara ya bidhaa bandia na kuimarisha ushirikiano wa wadau.

FIDIA ZAANZA KUMWAGIKA PANGANI, WANANCHI 474 KUPISHA MRADI WA SUKARI WA DOLA MILIONI 350

June 26, 2026 Add Comment

 




Na Oscar Assenga, Pangani

SERIKALI imeanza rasmi kulipa fidia kwa wananchi 474 wa vijiji vya Mseko na Kigurusimba, Kata ya Masaika, Wilaya ya Pangani mkoani Tanga, kupisha utekelezaji wa mradi mkubwa wa kilimo cha miwa na ujenzi wa kiwanda cha sukari wenye thamani ya dola za Marekani milioni 350.

Hatua hiyo inaashiria mwanzo wa utekelezaji wa moja ya miradi mikubwa ya uwekezaji nchini inayotarajiwa kuzalisha maelfu ya ajira, kuongeza uzalishaji wa sukari na kuchochea ukuaji wa uchumi wa Wilaya ya Pangani na taifa kwa ujumla.

Akizindua rasmi zoezi la ulipaji fidia, Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Dkt. Batilda Burian, alisema Serikali imeanza kuwalipa wananchi wote waliokamilisha taratibu zinazohitajika ili kuondoa vikwazo vya utekelezaji wa mradi huo.

Alisema zaidi ya wananchi 400 tayari wamekamilisha kusaini nyaraka zinazowaruhusu kupokea malipo yao, huku akibainisha kuwa waliojitokeza mapema watapewa kipaumbele na wengine wataendelea kuhudumiwa kadri watakavyokamilisha taratibu.

"Tunataka zoezi hili lifanyike kwa uwazi, haki na kwa wakati. Serikali imejipanga kuhakikisha kila mwananchi aliyestahili analipwa fidia yake bila kuchelewa," alisema Dkt. Burian.

Aidha, aliwataka wananchi kuendelea kushirikiana na mamlaka zinazoratibu zoezi hilo ili kuhakikisha mradi unaanza kwa wakati na kuleta manufaa yaliyokusudiwa kwa jamii na taifa.

Awali, akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Uwekezaji na Maeneo Maalumu ya Kiuchumi Tanzania (TISEZA), Remigius Reverius alisema malipo yanafanyika moja kwa moja kupitia akaunti za benki za wanufaika waliokamilisha uhakiki wa nyaraka zao.

Alisema zoezi hilo limeanza katika Kijiji cha Kigurusimba na litaendelea kwa awamu hadi wananchi wote waliothibitishwa kulipwa fidia watakapopokea stahiki zao.

"Tunawashukuru wananchi kwa ushirikiano wao. Serikali kupitia TISEZA imejipanga kuhakikisha kila aliyefanyiwa tathmini analipwa haki yake. Zoezi hili litaendelea hadi Juni 30 mwaka huu," alisema Reverius.

Aliongeza kuwa wataalamu wanaendelea kuhakiki taarifa za akaunti za benki pamoja na nyaraka mbalimbali ili kuhakikisha malipo yote yanafanyika kwa usahihi na bila dosari.

Mwakilishi wa wakulima wa Kigurusimba, Biligita Batilimeo, alisema kuanza kwa ulipaji wa fidia ni hatua muhimu inayoonyesha dhamira ya Serikali ya kutekeleza mradi huo huku ikilinda maslahi ya wananchi.

Alisema pamoja na fidia, mradi huo unatarajiwa kufungua fursa nyingi za ajira na biashara ambazo zitainua uchumi wa wakazi wa Pangani.

Naye mkazi wa Kigurusimba, Benard Mhagama, aliwasihi wananchi watakaopokea fidia kutumia fedha hizo kwa busara kwa kuwekeza katika shughuli za maendeleo zitakazowanufaisha wao na familia zao kwa muda mrefu.

Kwa upande wake, Diwani wa Kata ya Masaika, George Mariano, alisema uwekezaji huo utabadilisha sura ya uchumi wa Pangani kwa kuongeza ajira, kuchochea shughuli za biashara na kuongeza mapato ya Serikali.

Mradi huo wa kilimo cha miwa na ujenzi wa kiwanda cha sukari unatekelezwa na TISEZA katika eneo la ekari 22,000 kwa gharama ya dola za Marekani milioni 350, na unatarajiwa kuwa miongoni mwa miradi mikubwa itakayochangia kuongeza uzalishaji wa sukari nchini pamoja na kuharakisha maendeleo ya kiuchumi katika Mkoa wa Tanga.

Mwisho.


MBARAWA AFUNGUA MILANGO YA AJIRA ZA BAHARINI KWA VIJANA WASIOSOMA SAYANSI

Kajunason June 25, 2026 Add Comment

Uchumi wa Bluu Kunufaika na Elimu ya Ubaharia

Na Mwandishi Wetu, Kigoma

Waziri wa Uchukuzi, Profesa Makame Mnyaa Mbarawa, amesema Serikali itaendelea kukiunga mkono Chuo cha Bahari Dar es Salaam (DMI) katika jitihada zake za kuanzisha kozi ya awali ya ubaharia itakayowawezesha vijana wengi zaidi wa Kitanzania kupata elimu ya sekta hiyo na kushiriki kikamilifu katika kukuza uchumi wa bluu.

Profesa Mbarawa ametoa kauli hiyo alipotembelea banda la DMI katika kilele cha Maadhimisho ya 16 ya Siku ya Mabaharia Duniani yaliyofanyika mkoani Kigoma, ambapo alieleza kuwa kozi hiyo ni suluhisho kwa vijana wengi wenye ndoto za kuwa mabaharia lakini ambao hawakupata nafasi ya kusoma masomo ya sayansi yanayohitajika kujiunga na taaluma hiyo.

Alisema DMI imebuni mpango huo mahsusi ili kuwapa vijana hao fursa ya kupata msingi wa masomo muhimu yatakayowawezesha kuendelea na mafunzo ya ubaharia na hatimaye kuingia katika soko la ajira la sekta ya usafiri wa majini.

“DMI inafanya kazi kubwa ya kuangalia namna ya kuwawezesha vijana wengi zaidi kupata fursa za elimu ya ubaharia. Kozi hii ya awali itawasaidia wale ambao hawakusoma masomo ya sayansi kupata msingi unaohitajika na hatimaye kujiunga na mafunzo ya ubaharia,” alisema Profesa Mbarawa.
Alibainisha kuwa hatua hiyo ni sehemu ya mkakati wa Serikali wa kuongeza idadi ya mabaharia wenye ujuzi na sifa zinazotambulika kitaifa na kimataifa, huku ikilenga kuongeza ushiriki wa Watanzania katika ajira za sekta ya bahari na usafiri wa majini duniani.

Waziri huyo pia alimpongeza Mkuu wa Chuo cha DMI, Profesa Tumaini Gurumo, kwa ubunifu na juhudi zake za kuendeleza programu mbalimbali za mafunzo zinazowawezesha mabaharia wa Tanzania kufikia viwango vya kimataifa vinavyohitajika katika sekta ya usafiri wa majini.

“Tunakipongeza DMI kwa juhudi zake za kubuni na kuendeleza mafunzo yanayowawezesha mabaharia wetu kuwa na sifa zinazokubalika kimataifa. Mabaharia wanazunguka dunia nzima, hivyo ni lazima waandaliwe kwa viwango vinavyokidhi mahitaji ya sekta ya kimataifa,” alisema Profesa Mbarawa.
Kwa upande wake, Mkuu wa Chuo cha DMI, Profesa Tumaini Gurumo, ameishukuru Serikali kupitia Wizara ya Uchukuzi kwa kuendelea kukiunga mkono chuo hicho katika kuzalisha wataalamu wenye tija na ushindani katika soko la ajira la ndani na nje ya nchi.

Profesa Gurumo alisema kutokana na asili ya kazi ya ubaharia inayowafanya mabaharia kufanya kazi na kusafiri katika mataifa mbalimbali duniani, ni muhimu kwao kupata elimu na stadi zinazotambulika kimataifa ili waweze kushindana kwa ufanisi katika soko la ajira la dunia.

Aliongeza kuwa DMI itaendelea kupanua na kuboresha mafunzo ya bahari ili kuhakikisha vijana wengi zaidi wanapata elimu na ujuzi unaohitajika kwa taifa kunufaika na fursa zilizopo katika uchumi wa bluu na sekta ya usafiri wa majini.

Maadhimisho ya 16 ya Siku ya Mabaharia Duniani yamewakutanisha wadau mbalimbali wa sekta ya bahari na usafiri wa majini kwa lengo la kutambua na kuthamini mchango mkubwa wa mabaharia katika kukuza biashara, uchumi na maendeleo ya jamii duniani.

MHE.SALOME AZINDUA MFUMO WA KUAGIZA GESI YA KUPIKIA KIDIJITALI

June 25, 2026 Add Comment



📌*Unalenga kurahisisha upatikanaji wa nishati safi ya kupikia kwa wananchi*



Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba, amezindua mfumo wa kidijitali wa kuagiza gesi ya kupikia uitwao Orion Gas, unaomilikiwa na kampuni ya Hygge, utakaowezesha wateja kuagiza mitungi ya gesi mtandaoni na kufikishiwa bila gharama za usafirishaji. 


Mfumo huo utaanza kutumika katika mkoa wa Dar es Salaam kama sehemu ya kurahisisha upatikanaji wa nishati safi ya kupikia kwa wananchi.

Akizungumza Juni 25, 2026 wakati akifunga Maonesho na Kongamano la Nishati Safi ya Kupikia yaliyofanyika katika Ukumbi wa EACLC, Ubungo jijini Dar es Salaam, Mhe. Salome  amesema Serikali chini ya uongozi wa Rais, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, imeweka mkazo mkubwa katika utekelezaji wa Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia wa mwaka 2024–2034 unaolenga kuhakikisha asilimia 80 ya Watanzania wanatumia nishati safi ya kupikia ifikapo mwaka 2034.


Amesema Serikali imeendelea kuchukua hatua mbalimbali za kukabiliana na changamoto zinazoikabili sekta hiyo, ikiwemo kuondoa baadhi ya kodi na ushuru kwenye vifaa vya nishati safi ya kupikia ili kupunguza gharama kwa watumiaji. 

Amesema juhudi mbalimbali zinazochukuliwa na Serikali pamoja na wadau zimeanza kuzaa matunda ambapo matumizi ya nishati safi ya kupikia yameongezeka kutoka asilimia 6.9 mwaka 2021 hadi asilimia 28.9 kwa sasa.

Mhe. Salome ametoa wito kwa sekta binafsi kuongeza uwekezaji katika uzalishaji na usambazaji wa teknolojia za nishati safi, taasisi za fedha kuweka mifumo rafiki ya mikopo kwa wafanyabiashara na wananchi, pamoja na vyombo vya habari kuendelea kutoa elimu kwa umma.


Ameeleza kuwa mwitikio mkubwa wa wadau wa ndani na nje ya nchi katika Maonesho na Kongamano la Nishati Safi ya Kupikia unaonesha kuwa ajenda hiyo sasa imekuwa kipaumbele muhimu cha kitaifa. Amesema kongamano hilo limefanikiwa kuikutanisha Serikali, sekta binafsi na washirika wa maendeleo katika jukwaa moja la kujadili suluhisho za kuharakisha matumizi ya nishati safi ya kupikia nchini.


Katika hatua nyingine Mhe. Salome ametoa wito kwa wananchi na wadau mbalimbali kushiriki  Mbio za Kitaifa za Nishati Safi ya Kupikia (Clean Cooking Marathon) zitakazofanyika Juni 27, 2026 jijini Dar es Salaam  ili kuendelea kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia kwa ajili ya kulinda afya, mazingira na ustawi wa jamii.


SALOME MAKAMBA AFUNGA MAONYESHO YA NISHATI EXPO 2026

June 25, 2026 Add Comment

 



📌*Apongeza juhudi za REA kusambaza Nishati Safi ya kupikia vijijini*


📍Dar es Salaam


Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba leo tarehe 25 Juni, 2026 amefunga rasmi Maonesho na Kongamano la Nishati Safi Expo 2026  yaliyofanyika katika ukumbi wa EACLC jijini Dar es Salaam


Akiwa katika banda la Wakala wa Nishati Vijijini (REA), ameipongeza REA kwa kuendelea kusambaza na kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia hususan katika maeneo ya vijijini na pembezoni mwa miji. 

"Naipongeza REA kwa kazi kubwa mnayoifanya katika kuimarisha upatikanaji wa nishati safi ya kupikia na naendelea kuwahimiza wananchi kuendelea kutumia teknolojia mpya za nishati safi ili kulinda afya, mazingira na kuboresha ustawi wa jamii, " Ameongeza Mhe. Makamba. 


Amesisitiza kuwa Serikali itaendelea kuwekeza na kushirikiana na wadau mbalimbali ili kuhakikisha malengo ya Taifa ya matumizi ya nishati safi ya kupikia yanafikiwa kwa manufaa ya Watanzania wote.

Aidha, Mhe. Makamba ameelezwa hatua mbalimbali zinazochukuliwa na Serikali katika kuhakikisha wananchi wanahama kutoka katika matumizi ya nishati zisizo safi na zisizo salama kwenda kwenye teknolojia bora za nishati safi ya kupikia.



Vilevile, Mha wa miradi Francis Manyama amemfafanulia  kuwa kupitia maonesho hayo, REA imeendelea kutoa elimu kwa wananchi kuhusu matumizi ya nishati safi ya kupikia pamoja na kuonesha teknolojia mbalimbali ikiwemo matumizi ya kuni mbadala, majiko banifu, majiko ya umeme na teknolojia nyingine rafiki kwa mazingira.


Alieleza kuwa washiriki mbalimbali wakiwemo baba lishe, mama lishe, washiriki kutoka asasi za kirai, na mashirika ya binafisi, walimu na wadau wengine walitembelea banda la REA na kupata elimu pamoja na kujionea teknolojia hizo zinazochochea matumizi ya nishati safi nchini.


Aidha, Mha. Manyama alimueleza Mhe. Makamba kuwa REA inaendelea kutekeleza miradi mbalimbali ya kimkakati ikiwemo usambazaji wa majiko banifu 200,000 katika mikoa 25 ya Tanzania Bara pamoja na usambazaji wa mitungi ya gesi ya LPG ya kilo sita ipatayo 3,255 kwa kila Wilaya kwa lengo la kurahisisha upatikanaji na matumizi ya nishati safi ya kupikia kwa wananchi.

Vilevile, alibainisha kuwa Wakala unatekeleza mradi wa kuhamasisha matumizi ya nishati safi katika taasisi zinazohudumia watu zaidi ya 100 kwa siku, ambapo utekelezaji wake unafanyika kwa ushirikiano na Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) pamoja na Jeshi la Magereza.


Katika hatua nyingine, alieleza kuwa REA kupitia TPDC imetekeleza mradi wa kusambaza gesi asilia ya kupikia katika kaya zilizopo mikoa ya Lindi na Pwani, hatua inayolenga kuongeza upatikanaji wa nishati safi na salama kwa wananchi wa maeneo hayo. Pia alieleza kua Wakala kupitia STAMICO utawezesha usimikaji wa mashine ya kuzalisha mkaa mbadala katika mkoa wa Geita ili kurahisha upatikanaji endelevu wa nishati ya kupikia kwa wingi na wakati.


Mwisho

MTAKUWWA YAANZA OPERESHENI YA MALEZI BORA NA ULINZI WA WATOTO MWANZA

June 25, 2026 Add Comment


Kamati ya Ulinzi na Usalama wa Wanawake na Watoto Mkoa wa Mwanza (MTAKUWWA) imezindua kampeni ya “Amsha Ari” yenye lengo la kuhamasisha malezi bora, kuzuia mmomonyoko wa maadili na kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake na watoto mkoani Mwanza.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa kampeni hiyo uliofanyika katika Soko la Milongo, Mwenyekiti Mwenza wa MTAKUWWA Mkoa wa Mwanza, Yassin Ally, amesema kampeni hiyo itatekelezwa kwa mfumo wa nyumba kwa nyumba, mtaa kwa mtaa na pango kwa pango ili kuwafikia wananchi wengi zaidi.

Amesema baadhi ya maeneo hayo yamekuwa hatarishi kwa malezi ya watoto, hivyo kampeni hiyo imelenga kufikia makundi mbalimbali ya jamii kupitia mbinu tofauti za utoaji elimu na uhamasishaji.

Kwa upande wao, wajumbe wa MTAKUWWA Mkoa wa Mwanza ambao ni viongozi wa dini, wameitaka jamii, hususan waumini wao, kuzingatia malezi bora ya watoto na kujiepusha na vitendo vya ukatili wa kijinsia dhidi ya wanawake na watoto.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti, wafanyabiashara wa Soko la Milongo lililopo Kata ya Milongo, Wilaya ya Nyamagana mkoani Mwanza, wameipongeza kampeni hiyo kwa kutoa elimu inayopinga vitendo vya ukatili dhidi ya wanawake na watoto pamoja na kuhamasisha jamii kuendelea kudumisha amani nchini




 

KCMC YAPATA TIBA MIONZI: SERIKALI YAWEKEZA BILIONI 5.5 KUSOGEZA HUDUMA ZA SARATANI KARIBU NA WANANCHI

June 24, 2026 Add Comment

Na John Mapepele, WAF – Kilimanjaro

Tanzania imeandika ukurasa mpya katika mapambano dhidi ya saratani baada ya Serikali kuzindua rasmi Jengo la Tiba Mionzi katika Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Kilimanjaro Christian Medical Centre (KCMC), hatua inayotarajiwa kuwanufaisha maelfu ya wagonjwa wa Kanda ya Kaskazini na nchi jirani.

WANANCHI WAHIMIZWA KUTUMIA LANDMAX KUEPUKA UTAPELI WA ARDHI

June 24, 2026 Add Comment

Na Hamida Ramadhan,Dodoma

MBUNGE wa Jimbo la Mbozi, Onesmo Mnkondya, amewataka wananchi na madalali wanaohusika na biashara ya ardhi kutumia huduma za Landmax Real Estate Company Limited ili kufanya uwekezaji kwa usalama na kuondokana na migogoro inayotokana na mauzo au ununuzi usio rasmi wa ardhi.

Mnkondya, ambaye pia ni Mkurugenzi wa Landmax Real Estate Company Limited, amesema hayo Juni 24, 2026 jijini Dodoma wakati wa hafla ya uzinduzi wa ofisi za kampuni hiyo.

Amesema Landmax imeanzishwa kwa lengo la kuwasaidia wananchi kupata ardhi salama na makazi bora huku ikichangia kupunguza migogoro ya ardhi.

Aidha, amebainisha kuwa kampuni hiyo inatoa huduma mbalimbali ikiwemo uuzaji na ununuzi wa ardhi na mali isiyohamishika, ushauri wa uwekezaji wa ardhi, usimamizi wa mali, urasimishaji wa nyaraka za ardhi, uendelezaji wa miradi, tafiti za soko pamoja na ushirikiano katika miradi ya maendeleo.

“Tunawaalika wananchi na madalali wote wanaotaka kununua au kuuza ardhi kufika ofisini kwetu ili wapate huduma bora na salama,” amesema Mnkondya.

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule, amezitaka Halmashauri zote za Mkoa huo kufanya kazi kwa kasi na ufanisi ili kuendana na kasi ya wawekezaji wa sekta binafsi.

Amesema ucheleweshaji wa huduma kwa wawekezaji unaweza kudhoofisha maendeleo ya uchumi wa Taifa na kuathiri mchango wa sekta binafsi katika maendeleo ya nchi.

“Ukiichelewesha sekta binafsi, unakuwa unadhoofisha mchango wao katika ujenzi wa Taifa ni muhimu Halmashauri na taasisi nyingine za umma kufanya kazi kwa kasi inayolingana na wawekezaji,” amesema Senyamule.

Naye Mbunge wa Jimbo la Kigoma Mjini, Clayton Chipando, amewataka wananchi kutumia huduma za Landmax Real Estate Company Limited ili kujiepusha na matapeli wanaojihusisha na biashara za ardhi na mali isiyohamishika.

Amesema matukio ya utapeli yamekuwa yakiongezeka kutokana na baadhi ya watu kutumia njia zisizo rasmi katika miamala ya ardhi, hivyo ni muhimu wananchi kutumia kampuni zinazotoa huduma za kitaalamu na zinazofuata taratibu za kisheria.

“Ndugu zangu kama mnavyojua matapeli siku hizi wamekuwa wengi na wajanja, hivyo ili kuwa salama tumieni kampuni ya Landmax,” amesema Baba Levo

Ameongeza kuwa" Kupitia huduma za kitaalamu zinazotolewa na kampuni hiyo, wananchi watapata uhakika wa umiliki wa ardhi na kufanya uwekezaji wao kwa kujiamini zaidi, " Amesema.








 

YOGE TO CONVENE A REGION POLICY SUMMIT ON INCLUSIVE FRESHWATER GOVERNANCE IN RUVUMA, TANZANIA

June 24, 2026 Add Comment

 

The Youth Environmental Justice and Gender Equality (YOGE), with support from IUCNs BRIDGE Women Leadership Grants, will on June 25th, 2026 convene a one‑day Region Policy Summit on Inclusive Water Governance in Ruvuma Basin, Tanzania.
WRRB YAANZA KUTEKELEZA MAAGIZO YA WAZIRI MKUU KUONGEZA UFANISI WA STAKABADHI ZA GHALA

WRRB YAANZA KUTEKELEZA MAAGIZO YA WAZIRI MKUU KUONGEZA UFANISI WA STAKABADHI ZA GHALA

June 24, 2026 Add Comment

Bodi ya Usimamizi wa Mfumo wa Stakabadhi za Ghala (WRRB) imeanza rasmi utekelezaji wa maagizo yaliyotolewa na Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba, ya kuimarisha usimamizi wa Mfumo wa Stakabadhi za Ghala na kuhakikisha changamoto zinazojitokeza katika utekelezaji wake zinatatuliwa bila kurudi kwenye biashara holela ya mazao.

Akitoa taarifa baada ya kutembelea mikoa ya Pwani, Lindi, Mtwara, Ruvuma, Morogoro na Iringa ikiwa ni utekelezaji wa maagizo hayo aliyoyatoa kwenye maadhimisho ya miaka 20 ya Bodi hiyo Mei 19, 2026 jijini Dodoma, Mkurugenzi Mtendaji wa WRRB, Bw. Asangye Bangu, amesema katika ziara hiyo amekutana na viongozi wa mikoa, wilaya na Kamati za Usimamizi wa Mfumo wa Stakabadhi za Ghala na kujionea namna mfumo huo unavyotekelezwa kwenye zao la ufuta.

“Nimeridhishwa na namna serikali za mikoa zinavyoendelea kushirikiana na WRRB katika kuhakikisha mfumo unasimamiwa vizuri. Viongozi wote tuliokutana nao wameonesha utayari mkubwa wa kusimamia utekelezaji wa mfumo huu na kushughulikia changamoto zinazojitokeza,” amesema.

Amesema moja ya maelekezo makubwa yaliyotolewa na Waziri Mkuu ni kuhakikisha changamoto zinazojitokeza katika mfumo huo hazitumiki kama sababu ya kurejea katika biashara holela ya mazao, bali zitafutiwe ufumbuzi kwa wakati.

Kwa mujibu wa Bw. Bangu, changamoto zilizotajwa na Waziri Mkuu zinahusisha miundombinu ikiwamo ujenzi wa maghala, matengenezo ya barabara na uwepo wa mazingira bora ya kurahisisha usafirishaji wa mazao yanayopitia katika mfumo huo. Amesema WRRB imeweka mikakati mahsusi ya kuhakikisha ubora wa mazao unaimarishwa kwa kushirikiana na wakuu wa mikoa na wilaya ili bidhaa zote zinazopelekwa maghalani zikidhi viwango vinavyotakiwa.

“Tumewaelekeza waendesha maghala kuzingatia kikamilifu miongozo iliyotolewa na taasisi husika. Kwa sasa zao lililo sokoni ni ufuta na tayari miongozo ya utekelezaji imetolewa na COPRA,” amesema.

Kuhusu upungufu wa maghala, Bw. Bangu amesema tayari WRRB imeanza mazungumzo na halmashauri mbalimbali ili kuona namna ya kutumia fursa ya uwekezaji katika miundombinu ya maghala ambayo itaongeza ufanisi wa mfumo huo na kuwafikisha wakulima karibu zaidi na minada.

Kadhalika, amesema WRRB kwa kushirikiana na COPRA pia imeanza kuangalia uwezekano wa kuongeza mazao mengine kwenye mfumo ikiwamo karanga, njugu mawe na choroko ili kuongeza idadi ya wanufaika.

Akizungumzia changamoto ya mdororo wa bei, Bangu amesema wananchi wamekuwa wakilinganisha bei za sasa na zile za miaka mitatu iliyopita bila kuzingatia mabadiliko ya soko la dunia, hivyo WRRB imeendelea kutoa elimu kuhusu mwenendo wa bei katika masoko ya kimataifa.

Pia amesema baadhi ya maeneo yamekumbwa na upungufu wa uzalishaji kutokana na mabadiliko ya hali ya hewa na ukosefu wa mbegu bora, na kwamba WRRB imeanza mazungumzo na Jeshi la Magereza ili kutumia mashamba yake kuongeza uzalishaji wa mbegu.

“Niwahakikishie wananchi kuwa mfumo huu ni imara na tunaendelea kutatua changamoto zote zinazojitokeza. Tukishirikiana na wadau wote, tutamkomboa mkulima wa Tanzania na kuhakikisha anapata thamani halisi ya mazao yake,” alisema.