HABARI MPYA
HABARI
SIASA
ELIMU
Recent Posts
PSSSF YAFIKIA WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM TANGA
elimu habari
Tanga, Julai 28, 2026
Katika kuendeleza dhamira yake ya kuchangia maendeleo ya jamii kupitia mpango wa Uwajibikaji kwa Jamii (CSI) chini ya kampeni yake ya #PSSSFKaribuNaJamii, Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) umekabidhi rasmi mradi wa miundombinu wenye thamani ya Shilingi milioni 25 katika Shule ya Msingi Majani Mapana iliyopo mkoani Tanga.
Mradi huo unahusisha ujenzi wa chumba cha darasa, chumba cha mapumziko pamoja na vifaa mbalimbali vya michezo kwa ajili ya watoto wenye mahitaji maalum.

Akizungumza wakati wa makabidhiano hayo, Bw. Kwame Temu alieleza kuwa msaada huo unalenga kuunga mkono juhudi za Serikali kwa kuhakikisha watoto wenye mahitaji maalum wanapata haki yao ya msingi ya elimu.
Alisisitiza kuwa hatua hiyo itawasaidia wanafunzi hao kujifunza katika mazingira yanayowawezesha kujifunza kwa ufanisi, kushiriki katika michezo na kukuza vipaji vyao mbalimbali.
MANYARA YAWEKA REKODI MPYA YA HISANI, SHILINGI BILIONI 1.3 ZATIKISA DAR
habari
Kajunason
Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
Dar es Salaam imeandika historia mpya katika harakati za kuboresha huduma za afya baada ya Mkoa wa Manyara kufanikisha zoezi kubwa la kuchangisha fedha lililowezesha kupatikana kwa zaidi ya Shilingi bilioni 1.3 kwa ajili ya kuokoa maisha ya watoto wanaozaliwa njiti na kuimarisha huduma za afya katika mkoa huo.
Fedha hizo zilikusanywa kupitia hafla maalumu ya chakula cha jioni cha hisani (Manyara Tanzanite Marathon Dinner Gala) iliyofanyika Julai 24, 2026 katika Hoteli ya Serena, Dar es Salaam, ikiwa ni sehemu ya kampeni ya Hatua Moja Okoa Maisha ya Mtoto, ambayo inalenga kuongeza upatikanaji wa vifaa tiba vya kisasa, kuboresha huduma za watoto wachanga na kupunguza vifo vinavyotokana na kuzaliwa njiti.
Jumla ya Shilingi 1,356,900,000 zilipatikana kupitia ahadi za michango na fedha taslimu kutoka kwa wadau mbalimbali wa maendeleo, taasisi za fedha, makampuni binafsi, viongozi wa Serikali, wabunge, wafanyabiashara na wananchi waliojitokeza kuunga mkono kampeni hiyo.
Hafla hiyo ilihudhuriwa na viongozi wa kitaifa na kikanda pamoja na wadau wa sekta ya afya, ambapo mshikamano mkubwa ulionekana katika jitihada za kuhakikisha watoto wanaozaliwa njiti wanapata huduma bora na salama.
Akizungumza baada ya harambee hiyo, Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mbunge wa Babati Vijijini, Mhe. Daniel Baran Sillo, aliyekuwa mgeni rasmi, alisema mafanikio hayo yanaonesha moyo wa uzalendo na mshikamano wa Watanzania katika kusaidia sekta ya afya.
Alisema lengo la kampeni hiyo ni kufikisha zaidi ya Shilingi bilioni 1.5, huku akiwakaribisha Watanzania kushiriki Manyara Tanzanite Marathon itakayofanyika Agosti 22, 2026 mkoani Manyara.
“Tunawashukuru wadau wote waliojitokeza na kuchangia. Kila mchango una maana kubwa katika kuokoa maisha ya watoto wetu. Tunataka kuhakikisha hospitali zetu zinakuwa na vifaa vinavyohitajika kuwahudumia watoto njiti kwa kiwango cha kisasa,” alisema Mhe. Sillo.
Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Mhe. Queen Sendiga, alisema kampeni hiyo imeibuka kuwa jukwaa muhimu la kuunganisha nguvu za Serikali na sekta binafsi katika kuboresha huduma za afya kwa mama na mtoto.
Aliwataka wananchi, taasisi na wadau mbalimbali kuendelea kujitokeza kuchangia ili kufanikisha lengo lililowekwa, akisisitiza kuwa uwekezaji katika afya ya watoto ni uwekezaji katika mustakabali wa taifa.
“Kila mtoto ana haki ya kuishi. Tunapowekeza katika vifaa tiba na huduma za watoto njiti, tunaokoa familia, tunaimarisha jamii na tunajenga taifa lenye nguvu,” alisema Mhe. Sendiga.
Naye Mganga Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Dkt. Andrew Method, alieleza kuwa mkoa huo unakabiliwa na changamoto kubwa ya watoto wanaozaliwa njiti, ambapo kati ya watoto 3,000 hadi 3,200 huzaliwa njiti kila mwaka.
Alisema idadi hiyo inaweka shinikizo kubwa katika vituo vya kutolea huduma za afya, hasa katika upatikanaji wa mashine za kusaidia watoto kupumua, incubators, vifaa vya ufuatiliaji wa afya za watoto wachanga na miundombinu ya huduma maalumu.

“Watoto njiti wanahitaji uangalizi wa karibu na vifaa maalumu. Bila uwekezaji wa kutosha, tunakuwa katika hatari ya kupoteza maisha ambayo yangeweza kuokolewa,” alisema Dkt. Method.
Kwa mujibu wa wataalamu wa afya, kuzaliwa njiti ni miongoni mwa sababu kuu zinazochangia vifo vya watoto wachanga duniani, na huduma bora katika saa na siku za mwanzo baada ya kuzaliwa ndiyo huamua kwa kiasi kikubwa uwezekano wa mtoto kuendelea kuishi.
Wadau waliohudhuria hafla hiyo walieleza kuwa kampeni hiyo imeonesha mfano wa namna matukio ya michezo yanaweza kutumika kama nyenzo ya kuchangisha fedha kwa ajili ya miradi ya kijamii na maendeleo.
Mbio za Manyara Tanzanite Marathon zimekuwa zikikua kwa kasi na sasa zinatajwa kuwa moja ya matukio makubwa ya michezo na hisani nchini Tanzania, yakilenga kuhamasisha afya, utalii na maendeleo ya jamii kwa wakati mmoja.
Waandaaji wa marathon hiyo walisema fedha zitakazopatikana zitaelekezwa katika ununuzi wa vifaa tiba, uboreshaji wa huduma za watoto wachanga na kuimarisha uwezo wa hospitali za Mkoa wa Manyara kuhudumia watoto njiti kwa ufanisi zaidi.
Kampeni hiyo pia inaunga mkono juhudi za Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, ambazo zimekuwa zikilenga kuboresha huduma za afya, kupunguza vifo vya mama na mtoto, kuimarisha ustawi wa jamii na kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora katika maeneo yote ya nchi.
Waandaaji wameendelea kutoa wito kwa Watanzania kushiriki mbio hizo au kuchangia kupitia akaunti maalumu za kampeni, wakisisitiza kuwa kila mchango ni hatua muhimu katika kuokoa maisha ya mtoto mmoja au zaidi.
Michango inaendelea kupokelewa kupitia CRDB Lipa Namba 113069180 na CRDB Account No. 10401215064 (Manyara Tanzania Marathon).
Kwa mafanikio yaliyopatikana katika usiku huo wa kihistoria, Mkoa wa Manyara umeonesha kuwa mshikamano wa jamii unaweza kuwa nguvu kubwa ya kuokoa maisha, huku kampeni ya Hatua Moja Okoa Maisha ya Mtoto ikiendelea kuwa mwanga wa matumaini kwa maelfu ya watoto wanaozaliwa njiti kila mwaka nchini Tanzania.
RAIS MUSEVENI ABARIKI KUREJEA KWA SHUGHULI ZA NATION MEDIA GROUP NCHINI UGANDA
habari

Kampuni ya Taifa Group leo Julai 28,2026 imetangaza kurejea kwa shughuli za kampuni yake tanzu ya Nation Media Group nchini Uganda kufuatia idhini iliyotolewa na Mheshimiwa Rais Yoweri Kaguta Museveni.
MRADI WA NJIA YA KUSAFIRISHA UMEME WA MSONGO WA KILOVOLTI 400 CHALINZE–DODOMA MBIONI KUKAMILIKA
Nishati
Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) limesema Mradi wa Njia ya Kusafirisha Umeme ya Msongo wa Kilovolti 400 kutoka Chalinze hadi Dodoma uko kwenye hatua za mwisho za utekelezaji wake, huku ujenzi ukiwa umekamilika kwa asilimia 94 na unatarajiwa kukamilika ifikapo Agosti 21, 2026.
Akizungumza na waandishi wa habari leo Julai 28, 2026, Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano na Huduma kwa Wateja wa TANESCO, Bi. Irene Gowelle, amesema ili kuwezesha ukamilishaji wa kazi za mradi huo kutakuwepo na katizo la muda la umeme katika baadhi ya maeneo nchini kwa ratiba maalumu kwa awamu mbili ambapo awamu ya kwanza itakua Julai 30 hadi Agosti 4 na ya pili itaanza Agosti 11 hadi 17, 2026.

Gowelle amesema hatua hiyo ni sehemu ya maandalizi ya ombi la Mkandarasi anayetekeleza mradi huo kampuni ya TBEA ambayo inalenga kuhakikisha kazi zinafanyika kwa hali ya usalama .
“Mradi huu umefikia hatua muhimu sana ya utekelezaji ambapo kipindi hiki, baadhi ya njia za kusafirisha umeme za kilovolti 220 na 132 zitalazimika kuzimwa kwa muda ili kuruhusu kazi za kuvuta na kuunganisha nyaya mpya kufanyika kwa usalama. Hii ni hatua ya kawaida katika utekelezaji wa miradi mikubwa ya miundombinu ya kusafirisha umeme na inalenga kukamilisha mradi huu wenye manufaa makubwa kwa Taifa,” amesema Bi. Gowelle.

Amefafanua kuwa baadhi ya maeneo katika mikoa iliyoko Kanda ya Kati, Kanda ya Ziwa, Kanda ya Kaskazini, Kanda ya Magharibi na Kanda ya Kusini Magharibi inaweza kuathiriwa kwa nyakati tofauti kulingana na ratiba za utekelezaji wa kazi hizo.
Bi. Gowelle amesema TANESCO itaendelea kutoa taarifa kwa wananchi kupitia vyombo vya habari, mitandao ya kijamii na majukwaa mbalimbali ya mawasiliano ili kuwawezesha wateja kupanga matumizi yao ya umeme kwa kuzingatia ratiba zitakazotolewa.

Aidha, amesisitiza kuwa Tanzania ina umeme wa kutosha na kwamba katizo hilo ni la muda, likiwa ni sehemu ya kukamilisha mradi huo wa kimkakati unaolenga kuimarisha uwezo wa usafirishaji wa umeme nchini. Ameongeza kuwa mikoa ya Dar es Salaam, Pwani, Lindi na Mtwara haitahusika katika ratiba hiyo ya katizo.
Kwa upande wake, Meneja wa Mradi wa Njia ya Kusafirisha Umeme ya Kilovolti 400 Chalinze–Dodoma, Mhandisi Newton Mwakifwamba, amesema mradi huo wenye urefu wa kilomita 345 na thamani ya takribani shilingi bilioni 514 umefadhiliwa kwa asilimia 100 na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Amesema mradi unahusisha ujenzi wa njia mpya ya kusafirisha umeme pamoja na upanuzi wa vituo vya kupokea na kusambaza umeme vya Chalinze na Dodoma.
“Katika hatua hizi za mwisho, tutafanya kazi za kuvusha na kuunganisha njia mpya ya umeme katika maeneo ya Mkambarani, Kikombo na Mkonze. Hatua hizi ni muhimu ili kuhakikisha mradi unaanza kufanya kazi kwa ufanisi na usalama,” amesema Mhandisi Mwakifwamba.
Ameongeza kuwa kukamilika kwa mradi huo kutaimarisha uwezo wa mfumo wa taifa wa usafirishaji umeme na kuwezesha usafirishaji wa umeme unaozalishwa katika Bwawa la Kufua Umeme la Julius Nyerere kwenda maeneo mbalimbali ya nchi, hatua itakayoimarisha uhakika wa upatikanaji wa umeme na kuchochea maendeleo ya kiuchumi na kijamii.




RAIS MUSEVENI ABARIKI KUREJEA KWA SHUGHULI ZA NATION MEDIA GROUP NCHINI UGANDA
habari
Kampuni ya Taifa Group leo imetangaza kurejea kwa shughuli za kampuni yake tanzu ya Nation Media Group nchini Uganda kufuatia idhini iliyotolewa na Mheshimiwa Rais Yoweri Kaguta Museveni.
Uamuzi huu ni hatua muhimu katika uwekezaji wa kikanda, maendeleo ya sekta ya habari na ustawi wa ushirikiano wa Afrika Mashariki. Kupitia kampuni tanzu yake, Taarifa Limited, Taifa Group ndiyo mbia mkuu wa Nation Media Group na inaendelea kujitolea katika uwekezaji wenye uwajibikaji, utawala bora wa kampuni na maendeleo endelevu kote katika kanda hii.
Akizungumzia hatua hiyo, Mwenyekiti wa Taifa Group, Bw. Rostam Azizi, alitoa shukrani zake za dhati kwa Mheshimiwa Rais Yoweri Kaguta Museveni kwa kuruhusu kurejea kwa shughuli za Nation Media Group nchini Uganda. Pia alitoa shukrani kwa Jenerali Muhoozi Kainerugaba, Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi ya Uganda (UPDF), kwa uungaji mkono wake katika mchakato mzima uliopelekea matokeo haya chanya akisema,
“Ningependa kutoa shukrani zangu za dhati kwa Mheshimiwa Rais Yoweri Kaguta Museveni kwa uamuzi huu muhimu, na kwa Jenerali Muhoozi Kainerugaba kwa uungaji mkono wake katika mchakato mzima uliopelekea matokeo haya chanya.
Tunajivunia uamuzi huu na tunadumisha azma yetu thabiti ya kuchangia maendeleo ya kijamii na kiuchumi ya Uganda kupitia uwekezaji wenye uwajibikaji, ushirikiano wa muda mrefu na ujenzi wa thamani endelevu.
Kama mbia mkuu wa Nation Media Group, tunaunga mkono kikamilifu dhamira ya Kampuni hiyo ya kufuata misingi ya uandishi wa habari wa haki, uwiano, uhuru na uwajibikaji, unaotoa taarifa, kuelimisha na kuchangia vyema katika mijadala ya umma. Tunashiriki dhima kuu ya Kampuni hiyo ya kuleta athari chanya katika jamii, na tunaamini kuwa vyombo vya habari imara, vya kitaalamu na vinavyozingatia uwajibikaji vina jukumu muhimu katika kusaidia maendeleo ya taifa, utawala bora na ushirikiano wa kikanda.”
"Uamuzi huu unaonyesha thamani ya mazungumzo, kuheshimiana na ushirikiano wa kikanda. Taifa Group itaendelea kuwekeza katika fursa zinazozalisha ajira, kuimarisha taasisi na kuendeleza ustawi wa pamoja katika Afrika Mashariki."
Mwenyekiti wa Nation Media Group, Bw Joe Muganda, alisema Kundi hilo sasa litazingatia kujenga upya uwepo wake, kuungana tena na watazamaji na kuimarisha mchango wake katika sekta ya vyombo vya habari nchini Uganda.
"Tunakaribisha fursa ya kurejesha shughuli nchini Uganda na kuunganishwa tena na watazamaji wetu, wafanyakazi, washirika wa kibiashara na jumuiya.
"Kipaumbele chetu cha haraka kitakuwa kurejesha majukwaa yetu kwa uwajibikaji, kuimarisha maudhui ya ndani na kuwapa Waganda uandishi wa habari wa kuaminika, muhimu na wa ubunifu katika magazeti, matangazo na njia za digital.
"Nation Media Group itatumia uwezo wake wa kikanda na uzoefu ili kusaidia tasnia ya habari yenye uthabiti, yenye mtazamo wa mbele nchini Uganda, huku ikitengeneza fursa za talanta, biashara na ushiriki wa umma."
Kurejeshwa kwa shughuli hizo kunaonyesha uhusiano wa kudumu kati ya Uganda na Tanzania na dhamira pana ya serikali za Afrika Mashariki na sekta binafsi ya kukuza utangamano wa kikanda, uwekezaji wa mipakani na ushirikiano wa kiuchumi.
Nation Media Group inapojenga upya shughuli zake nchini Uganda, itaendelea kutumia uwepo wake kote nchini Kenya, Uganda, Tanzania na Rwanda ili kuunganisha watazamaji, kuimarisha mazungumzo ya kikanda na kusaidia maendeleo ya kijamii na kiuchumi ya Afrika Mashariki. Taifa Group itaendelea kushirikiana na serikali, taasisi, wafanyabiashara na jumuiya kote kanda ili kupanua fursa za kiuchumi endelevu na kusaidia ustawi wa muda mrefu wa Afrika Mashariki.
Subscribe to:
Posts (Atom)



































