HABARI

SIASA

ELIMU

Recent Posts

MENEJA MKUU: HUDUMA BORA KWA MTEJA NDIO KIPAUMBELE CHA SHIRIKA

August 21, 2026 Add Comment

Meneja Mkuu wa Shirika la Masoko ya Kariakoo CPA. Ashraph Abdulkarim amewataka watumishi kuhakikisha kuwa wanakuwa suluhu ya changamoto za wafanyabiashara wa Soko Kuu la Kariakoo kwa kusikiliza, kutoa majawabu ya uhakika kwa wakati na kutoa mrejesho kwa wafanyabiashara hao kwa wakati na kuzingatia mkataba wa huduma kwa mteja.

PROF. NOMBO ATEMBELEA BANDA LA TUME YA TAIFA YA UNESCO TANGA

August 21, 2026 Add Comment



Na: Julitha Mlay
Tanga, 20 Agosti 2026

Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Carolyne Nombo, leo Agosti 20, 2026 ametembelea Banda la Tume ya Taifa ya UNESCO ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika maadhimisho ya Wiki ya Elimu, Ujuzi na Ubunifu Kitaifa yanayoendelea jijini Tanga.

Katika ziara hiyo, Prof. Nombo amepata fursa ya kujionea shughuli na maudhui mbalimbali yanayotolewa na Tume katika kuelimisha umma kuhusu UNESCO, majukumu ya Tume na programu zake katika maeneo ya elimu, sayansi, utamaduni, mawasiliano na taarifa.

Prof. Nombo alikuwa ameambatana na Dkt. Fredrick Salukele, Mkurugenzi wa Elimu ya Ufundi, ambapo walipata fursa ya kufahamu zaidi namna Tume inavyotumia majukwaa ya kitaifa kuwafikia wananchi, wanafunzi, walimu, vijana na wadau wengine kwa taarifa kuhusu UNESCO na fursa zinazopatikana kupitia programu zake.

Ushiriki wa Tume katika Wiki ya Elimu, Ujuzi na Ubunifu Kitaifa ni sehemu ya juhudi za kuimarisha elimu na uelewa wa umma kuhusu UNESCO, pamoja na kuonesha mchango wa elimu, sayansi, utamaduni, mawasiliano na taarifa katika kukuza maarifa, ubunifu na maendeleo endelevu nchini.

Kupitia jukwaa hilo, Tume inaendelea kuwasogezea wananchi taarifa kuhusu kazi za UNESCO na maeneo mbalimbali yanayohusiana na utekelezaji wa programu zake nchini Tanzania, huku ikihamasisha ushiriki wa jamii katika kutumia maarifa na fursa zilizopo kwa maendeleo ya mtu mmoja mmoja na Taifa kwa ujumla.

Maadhimisho ya Wiki ya Elimu, Ujuzi na Ubunifu Kitaifa yanaendelea jijini Tanga yakishirikisha taasisi na wadau mbalimbali wa sekta ya elimu, ujuzi na ubunifu kwa lengo la kuelimisha jamii kuhusu fursa, huduma na jitihada zinazochangia maendeleo ya rasilimali watu nchini.

Kwa habari zaidi kuhusu shughuli, programu, matukio na fursa mbalimbali za Tume ya Taifa ya UNESCO ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, endelea kutufuatilia kupitia kurasa zetu rasmi za mitandao ya kijamii:

Facebook na Instagram: @unesconatcomtz
Tume ya Taifa ya UNESCO — Kuelimisha, Kuhamasisha na Kushirikisha Jamii.






CCM YASISITIZA KUIMARISHA UHUSIANO NA CHAMA CHA KIKOMUNISTI CHA CHINA

August 21, 2026 Add Comment


Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Bara, Ndugu Aggrey Mwanri, amekutana na kufanya mazungumzo na Mwakilishi wa Chama cha Kikomunisti cha China (CPC) nchini Tanzania, Ndugu Xu Sujiang, huku akisisitiza dhamira ya CCM ya kuendelea kuimarisha uhusiano wa kihistoria na wa kimkakati kati ya vyama hivyo viwili.









Kikao hicho kimefanyika leo Agosti 20,2026 katika Makao Makuu ya CCM, Dodoma, ambapo Ndugu Xu ametumia nafasi hiyo kuaga rasmi kabla ya kuhitimisha majukumu yake nchini Tanzania

WRS KUONGEZA TIJA KWA WAKULIMA WA PARACHICHI, WRRB YATAKIWA KUHARAKISHA

WRS KUONGEZA TIJA KWA WAKULIMA WA PARACHICHI, WRRB YATAKIWA KUHARAKISHA

August 20, 2026 Add Comment

Na.Mwandishi Wetu- Dodoma

KAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara, Kilimo na Mifugo imeipongeza Bodi ya Usimamizi wa Stakabadhi za Ghala (WRRB) kwa utekelezaji mzuri wa majukumu yake na kuitaka kuharakisha matumizi ya Mfumo wa Stakabadhi za Ghala (WRS) katika zao la parachichi ili kuongeza tija kwa wakulima.

Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Mhe. Deodatus Mwanyika, ametoa pongezi hizo leo Agosti 20, 2026 jijini Dodoma baada ya Kamati hiyo kupokea na kujadili taarifa ya utekelezaji wa majukumu ya WRRB kwa mwaka 2025/26.

Mhe. Mwanyika amesema Kamati imeridhishwa na utendaji kazi wa WRRB, hasa katika kushughulikia changamoto za wananchi, na kuitaka Bodi hiyo iongeze kasi katika utoaji elimu ili kuchochea matumizi ya mfumo huo katika maeneo mengine.

Akitoa ufafanuzi wa hoja za wajumbe, Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Judith Kapinga, ameahidi kufanyia kazi maelekezo ya Kamati hiyo na kuihakikishia kuwa ataendelea kulinda majukumu ya taasisi zilizo chini yake kwa mujibu wa sheria.

Awali, akiwasilisha taarifa kwa Kamati hiyo, Mkurugenzi Mtendaji wa WRRB, Bw. Asangye Bangu, amesema kwa mwaka 2025/26, WRRB imetoa leseni kwa waendesha ghala 235, kusajili ghala 951, wanunuzi 390, waweka mali 2,667 na kutoa stakabadhi za ghala 214,170.

TACAIDS YAWEKA MIKAKATI MADHUBUTI KATIKA MAPAMBANO DHIDI YA UKIMWI

August 20, 2026 Add Comment


Dodoma

Tume ya Kudhibiti UKIMWI Tanzania (TACAIDS) inaendelea kuimarisha mikakati madhubuti ya kupambana na VVU na UKIMWI kupitia ushirikiano wa kisekta, kuhamasisha vyanzo vya fedha vya ndani, kusogeza huduma karibu na jamii ikiwemo Vituo vya Maarifa kwa madereva wa malori na kuwajengea uwezo vijana na wanawake ili kufikia lengo la kutokomeza kabisa janga hili ifikapo mwaka 2030.

Hayo yamebainishwa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu) Mhe. Profesa Palamagamba Kabudi wakati wa kikao cha Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Afya na Masuala ya UKIMWI ilipokutana kwa lengo la kupokea taarifa ya wasilisho la hali ya Maambukizi ya VVU na UKIMWI kwa Vijana na Mkakati wa Kupunguza Maambukizi Mapya kwa Vijana, kilichofanyika tarehe 20 Agosti, 2026 Bungeni Jijini Dodoma.


Waziri Kabudi ameipongeza Kamati kwa namna ilivyoshauri na kupendekeza  uboreshwaji wa masuala  mbalimbali ikiwemo matumizi ya teknolojia katika utoaji wa huduma, kuongeza nguvu kufikia vijana hasa walioko vijijini, elimu zaidi katika maeneo ya starehe ikiwemo kumbi za miziki na makongamano ya vijana lengo ni kuhakikisha jamii inafikiwa kwa ukubwa wake.

Naye Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Afya na Masuala ya UKIMWI Mhe. Dkt. Johannes Lumbulung Lukumay ameipongeza Ofisi ya Waziri Mkuu kwa namna inavyoratibu masuala ya Afua za UKIMWI nchini huku akieleza jitihada zinazofanywa na Serikali ya Awamu ya Sita kuhakikisha Utekelezaji wa Afua hizo unafanikiwa bila mkwamo wowote.

“Ni vyema sasa kuendelea kuwajengea uwezo vijana katika mikoa yenye ushamiri mkubwa wa maambukizi na kuratibu utoaji wa elimu na upimaji wa hiari katika maeneo ya kazi na sekta ya usafirishaji hususan kwa madereva wa malori wa masafa marefu," alisema Dkt. Lukumay

Vilevile ameipongeza Serikali kwa namna ilivyowekeza nguvu kuhakikisha janga hili linatokomezwa pamoja na kubuni program na miradi mbalimbali ikiwemo ya TIMIZA Malengo Awamu ya Tatu, inayoendeshwa na kauli mbiu isemayo; "Tusonge na Samia kutokomeza UKIMWI, ambavyo vinaleta mwamko wa jamii kujitokeza kupima afya zao na kuendelea kuchukua tahadhari juu ya maambukizi mapya ya VVU.


Pia wajumbe wa kamati hiyo  wamepongeza na kuishukuru Serikali katika kuhakikisha upatikanaji wa Dawa za kufubaza makali ya Virusi vya UKIMWI (ARVs) zinazosaidia kuimarisha kinga ya mwili, kuzuika VVU kujizalisha mwilini na kushusha kiwango cha Virusi hadi kutokuonekana ili kuzuia maambukizi mapya kwa jamii.

Akifafanua hoja za wajumbe wa kamati hiyo Mkurugenzi Mtendaji wa Tume ya Kudhibiti UKIMWI Tanzania (TACAIDS) Dkt. Adam Mrisho amesema, ofisi yake imeendelea kuweka mikakati madhubuti na hatua za makusudi katika kuhakikisha utekelezaji wa Afua za UKIMWI unafanyuka vyema na kuyafikia makundi yote hususan vijana.

“Tume imejipanga kuhakikisha elimu inaendelea kuifikia jamii ili kuwa na utayari wa kupima na kuhamasisha matumizi ya dawa kwa watakao gundulika kuwa na maambukizi ya VVU pamoja na kuimarisha mashirikiano na sekta binafsi” alieleza Dkt. Mrisho

Jitihada zingine ni kuwezesha wahudumu ngazi ya jamii wapatao elfu tisini kwa kuwapatia elimu ya kutoa huduma za kinga na huduma za JIPIME, hivyo kusaidia kuwafikia vijana waliopo vijijini na kuongeza mwitikio wa masuala ya UKIMWI.

Pia mikakati mingine ni kuviwezesha na kuboresha vituo 32 vya maarifa vinavyotoa elimu ya kinga, huduma za ARVs, upimaji na kuhakikisha vijana wanapewa elimu za masuala ya UKIMWI hususani madereva wa malori ya masafa marefu kupitia vituo hivyo vilivyopo nchini. 





 

KAMATI YA BUNGE YAIPONGEZA WIZARA YA VIWANDA NA TAASISI ZAKE KWA UFANISI

August 20, 2026 Add Comment
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara, Kilimo na Mifugo, kupitia Mwenyekiti wake Mhe.Deodatus Mwanyika, ameipongeza Wizara ya Viwanda na Biashara pamoja na taasisi zake kwa utekelezaji mzuri wa majukumu yake ya udhibiti ubora kwa ufanisi .
TBS YAPONGEZWA KWA KUIMARISHA UDHIBITI  WA UBORA WA BIDHAA

TBS YAPONGEZWA KWA KUIMARISHA UDHIBITI WA UBORA WA BIDHAA

August 20, 2026 Add Comment

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda,Biashara,Kilimo na Mifugo imeipongeza TBS kwa kutekeleza majukumu yake ya udhibiti ubora kwa ufanisi.

Pongezi hizo zimetolewa na Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mhe.Deogratias Mwanyika kwaniaba ya kamati wakati wa kikao cha Kamati cha kupokea taarifa ya utekelezaji wa majukumu,katika, ofisi za Bunge Jijini Dodoma mapema leo.

Mhe.Mwanyika amesema juhudi zinazofanywa na TBS katika kuhakikisha usalama na ubora wa bidhaa zinazotumiwa na Watanzania zinaonekana hata hivyo ametoa rai kwa TBS kuendelea kutoa elimu na kuongeza jitihada sambambana na kuwa na programu maalum za kushughulikia bidhaa zinazoingizwa nchini kwa njia zisizo rasmi.

Naye Mhe. Waziri wa Wizara ya Viwanda na Biashara Mhe. Judith Kapinga(Mb) ameishukuru kamati hiyo na kuahidi kuyafanyia kazi maelekezo na ushauri uliotolewa na kamati hiyo ili kuendelea kurahisisha utendaji kazi wa TBS.

Vile vile Mhe.Kapinga amesema lengo la Wizara kupitia TBS ni kuhakikisha kunakuwa na bidhaa zenye ubora na usalama katika soko zinazozalishwa ndani na zinazotoka nje ya nchi.

KAMATI YA KUDUMU YA BARAZA LA WAWAKILISHI ZANZIBAR YAZURU NEMC

August 20, 2026 Add Comment
-Yafurahishwa na Mradi wa Kituo cha Gesi Asilia kwa matumizi ya Nishati Safi

MWENGE WA UHURU WAZINDUA TAWI LA CRDB TINDE

August 20, 2026 Add Comment

    

Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa, Wazo Michael Mwang’onda, akikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa Tawi la Benki ya CRDB Tinde mkoani Shinyanga.
Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa, Wazo Michael Mwang’onda, akiwa pamoja na viongozi mbalimbali wakifurahia wakati wa uzinduzi wa Tawi la Benki ya CRDB Tinde mkoani Shinyanga.
Mwenge wa Uhuru ukiwa katika Tawi la Benki ya CRDB Tinde mkoani Shinyanga wakati wa uzinduzi rasmi wa tawi hilo.
Mwenge wa Uhuru ukiwa katika Tawi la Benki ya CRDB Tinde mkoani Shinyanga wakati wa uzinduzi rasmi wa tawi hilo.
Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa, Wazo Michael Mwang’onda, akitembelea Tawi la Benki ya CRDB Tinde mkoani Shinyanga wakati wa uzinduzi rasmi wa tawi hilo.
Mkurugenzi wa Mikopo wa Benki ya CRDB, Xavery Makwi, akiimba shairi wakati wa uzinduzi wa Tawi la Benki ya CRDB Tinde mkoani Shinyanga.
Mkurugenzi wa Mikopo wa Benki ya CRDB, Xavery Makwi, akiwa ameshika Mwenge wa Uhuru wakati wa uzinduzi wa Tawi la Benki ya CRDB Tinde mkoani Shinyanga.
Meneja wa CRDB Kanda ya Magharibi, Jumanne Wagana, akiwa ameshika Mwenge wa Uhuru wakati wa uzinduzi wa Tawi la Benki ya CRDB Tinde mkoani Shinyanga.
Mbunge wa Jimbo la Itwangi, Azza Hillal Hamad, akiwa ameshika Mwenge wa Uhuru wakati wa uzinduzi wa Tawi la Benki ya CRDB Tinde mkoani Shinyanga.
Mwenge wa Uhuru ukiondoka katika Tawi la Benki ya CRDB Tinde mkoani Shinyanga baada ya kukamilika kwa shughuli za uzinduzi wa tawi hilo.


Mwenge wa Uhuru ukiondoka katika Tawi la Benki ya CRDB Tinde mkoani Shinyanga baada ya kukamilika kwa shughuli za uzinduzi wa tawi hilo.
Wafanyakazi wa Tawi la Benki ya CRDB Tinde mkoani Shinyanga.

Na Elizabeth Cosmas na Kadama Malunde - Shinyanga

Mwenge wa Uhuru umezindua rasmi Tawi la Benki ya CRDB Tinde mkoani Shinyanga, huku Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa, Wazo Michael Mwang’onda, akiipongeza benki hiyo kwa kuendelea kupanua wigo wa huduma za kifedha na kuzisogeza karibu na wananchi.

RUWASA na wadau waja na mkakati wa kuboresha usafi wa mazingira vijijini

August 20, 2026 Add Comment

Morogoro

Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA), kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wa Sekta ya Maji, Afya na Usafi wa Mazingira, umeanza rasmi mchakato wa kuandaa Mkakati wa RUWASA wa Menejimenti ya Tope Kinyesi (Faecal Sludge Management Strategy), unaolenga kuweka mfumo madhubuti, salama na endelevu wa menejimenti ya tope kinyesi katika maeneo ya vijijini.