HABARI

SIASA

ELIMU

Recent Posts

MFUMO WA PBPA WAWEKA UHAKIKA WA MAFUTA NCHINI

MFUMO WA PBPA WAWEKA UHAKIKA WA MAFUTA NCHINI

August 28, 2026 Add Comment
 

Na Mwandishi Wetu, Morogoro

Wakala wa Uagizaji Mafuta kwa Pamoja (PBPA) umeeleza kuwa Mfumo wa Uagizaji Mafuta kwa Pamoja umeendelea kuhakikisha Tanzania inapata bidhaa za mafuta kwa uhakika, kwa wakati na kwa gharama shindani.

Akizungumza katika Maonesho ya Nne ya Kitaifa ya Utamaduni yanayoendelea mkoani Morogoro, Mchumi wa PBPA, Bw. Henry Kilenga, amesema mfumo huo unahusisha ukusanyaji wa mahitaji ya mafuta kutoka kwa kampuni za uuzaji wa mafuta nchini kabla ya kutangazwa kwa zabuni za kimataifa.

Amesema PBPA hukusanya mahitaji hayo na kuyaunganisha ili mafuta yaagizwe kwa pamoja kwa kiwango kikubwa. Utaratibu huo huiwezesha nchi kunufaika na ununuzi wa pamoja na kupata gharama shindani za uagizaji na usafirishaji.

“PBPA hukusanya mahitaji ya mafuta kutoka kwa kampuni za uuzaji wa mafuta, huandaa zabuni na kuwashindanisha wazabuni waliokidhi vigezo. Utaratibu huu unasaidia kuhakikisha nchi inapata mafuta kwa uhakika na kwa gharama shindani,” amesema Kilenga.

Amefafanua kuwa zabuni hizo hushirikisha kampuni za kimataifa zilizohakikiwa na kukidhi vigezo vilivyowekwa na PBPA. Wazabuni hushindanishwa kwa uwazi, huku tathmini ikizingatia bei zilizowasilishwa, uwezo wa kusambaza mafuta na masharti mengine ya zabuni.

Kwa mujibu wa Kilenga, baada ya kukamilika kwa tathmini, kampuni zilizokidhi vigezo na kuwasilisha bei nzuri huchaguliwa kuleta mafuta nchini kulingana na kiasi na muda uliopangwa.

Kilenga amesema uwazi na ushindani katika uendeshaji wa zabuni unalenga kulinda maslahi ya taifa, kuongeza ufanisi na kuhakikisha bidhaa za mafuta zinaendelea kupatikana kwa ajili ya wananchi na shughuli mbalimbali za kiuchumi.

Amesisitiza kuwa Mfumo wa Uagizaji Mafuta kwa Pamoja una mchango mkubwa katika kuimarisha usalama wa upatikanaji wa nishati na kuchochea maendeleo ya kijamii na kiuchumi nchini.

BUNGE LAMTHIBITISHA NDEJEMBI KWA ASILIMIA 100 UMAKAMU WA RAIS.

August 28, 2026 Add Comment




BUNGE la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania leo (Ijumaa, Agosti 28, 2026) limemthibitisha Mheshimiwa Deogratius Ndejembi kuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.


Mheshimiwa Ndejembi amepitishwa kwa asilimia 100 ya kura zote 324 zilizopigwa na waheshimiwa wabunge, ambapo amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa imani aliyoionesha kwake kwa kumteua kuwa Makamu wa Rais na katika nafasi nyingine mbalimbali za uongozi.


Pia Mheshimiwa Ndejembi amelishukuru Bunge kwa imani kubwa waliyompa kiasi cha kumpigia kura kwa asilimia mia moja.


Mapema akiwasilisha hoja ya kuthibitisha uteuzi wa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba amesema Mheshimiwa Deogratius Ndejembi anatosha na ni mtu sahihi wa kumsaidia Mheshimiwa Rais katika nafasi ya Makamu wa Rais,
akiitaja kuwa ni nafasi yenye dhamana na majukumu makubwa katika uongozi wa nchi.


"Majukumu hayo yanahitaji mtu mwenye uzoefu wa uongozi, uelewa mpana wa shughuli za Serikali, uwezo wa kufanya kazi kwa karibu na Rais, busara katika kushughulikia masuala ya kitaifa, pamoja na uwezo wa kuratibu na kufuatilia utekelezaji wa majukumu mbalimbali ya Serikali," amesema Dkt. Mwigulu.


"Mheshimiwa Rais amemteua Mheshimiwa Deogratius John Pancras Ndejembi kwa kuzingatia, pamoja na mambo mengine, uzoefu alioujenga katika uongozi wa kisiasa na katika nafasi mbalimbali za Serikali," ameongeza Waziri Mkuu.


Dkt. Mwigulu amesisitiza kuwa uzoefu wa uongozi alionao Mheshimiwa Deogratius Ndejembi unadhihirisha kuwa ni mtu sahihi kutumikia wadhifa wa Makamu wa Rais.


"Mheshimiwa Deogratius John Pancras Ndejembi si mgeni katika uongozi wa Umma na katika siasa za nchi yetu. Kabla ya kuwa Mbunge, Mheshimiwa Ndejembi alihudumu kama Mkuu wa Wilaya katika Wilaya ya Kongwa. Mheshimiwa Spika, baada ya kuchaguliwa kuwa Mbunge, Mheshimiwa Ndejembi ameendelea kuaminiwa na Mheshimiwa Rais na kupewa majukumu mbalimbali ndani ya Serikali."


"Amehudumu katika nafasi ya Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora; Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa; Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu; Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, kabla ya kuhudumu kama Waziri wa Nishati," ameongeza Waziri Mkuu.


Dkt. Mwigulu amesema katika kipindi ambacho amehudumu ndani ya Serikali, Mheshimiwa Ndejembi ameonesha uwezo wa kubeba majukumu mbalimbali na kufanya kazi katika sekta zenye mahitaji na changamoto zinazotofautiana, akisisitiza kuwa uzoefu huo ni muhimu kwa Makamu wa Rais ambaye, kwa nafasi yake, anatakiwa kuwa tayari kumsaidia Rais katika masuala mbalimbali ya Jamhuri ya Muungano na kutekeleza majukumu yoyote atakayokabidhiwa kwa mujibu wa Katiba.


"Kwa kuzingatia majukumu ya Kikatiba ya Makamu wa Rais niliyoyaeleza, pamoja na uzoefu wa kisiasa, kiutawala na kiutendaji wa Mheshimiwa Deogratius John Pancras Ndejembi, Serikali inaamini kuwa ana uwezo wa kutekeleza kwa uaminifu na ufanisi majukumu ya nafasi ya Makamu wa Rais na kumsaidia Mheshimiwa Rais katika kuendeleza shughuli za Serikali na maendeleo ya Taifa letu," amefafanua Dkt. Mwigulu.






SERIKALI YAZINDUA 'UGHAIBUNI LOAN'

August 28, 2026 Add Comment
Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Dkt. Evaline Munisi (wa tatu kutoka kushoto) akizindua rasmi Ughaibuni Loan wakati wa hafla ya kuwaaga Watanzania wanaokwenda kufanya kazi nje ya  nchi, wakati wa hafla hiyo iliyofanyika Makao Makuu ya Benki ya CRDB, Palm Beach Jijini Dar es Salaam tarehe 27 Agosti, 2026.
USHIRIKIANO WA NHIF NA ZHSF WAVUTIA KAMATI YA BAJETI YA BARAZA LA WAWAKILISHI

USHIRIKIANO WA NHIF NA ZHSF WAVUTIA KAMATI YA BAJETI YA BARAZA LA WAWAKILISHI

August 28, 2026 Add Comment
 

Na Mwandishi Wetu, Dodoma

Kamati ya Bajeti ya Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar imeupongeza Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) kwa kazi kubwa inayofanya katika kuimarisha mifumo ya utoaji wa huduma za bima ya afya nchini, pamoja na ushirikiano wake na Mfuko wa Huduma za Afya Zanzibar (ZHSF).

Pongezi hizo zimetolewa na Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Bajeti ya Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar, Mhe. Mariam Hamis Said, wakati Kamati hiyo pamoja na Menejimenti za ZHSF na NHIF ilipotembelea Makao Makuu ya NHIF kwa ajili ya kujifunza namna Mfuko huo unavyoendesha na kutoa huduma kwa wanachama.

Mhe. Mariam amesema ziara hiyo imekuwa na mafanikio makubwa, kwa kuwa Kamati imepata fursa ya kuelezwa na kujionea kwa vitendo mifumo na huduma zinazotolewa na NHIF, kupitia ziara kwenye Hospitali ya Benjamin Mkapa (BMH).

Pamoja na kutoa pongezi kwa NHIF, Kamati hiyo ilipata fursa ya kutaka kufahamu kwa kina masuala mbalimbali yanayohusu uendeshaji na maendeleo ya Mfuko, ikiwemo namna NHIF inavyopambana na udanganyifu, utekelezaji wa Bima ya Afya kwa Wote, pamoja na hatua zinazochukuliwa kuhakikisha wanachama wanapata huduma bora na kwa wakati.

Aidha, Kamati ilitaka kufahamu namna matumizi ya TEHAMA yameboresha utendaji wa NHIF na kusaidia kupunguza gharama za uendeshaji, pamoja na namna uwekezaji unavyosaidia kuimarisha Mfuko.

Masuala mengine yaliyotiliwa mkazo ni pamoja na vyanzo vya mapato ya Mfuko, viashiria vinavyotumika kupima mafanikio na uendelevu wa NHIF, pamoja na mafunzo na uzoefu ambao Mfuko umeupata katika kipindi cha miaka 25 ya utekelezaji wa majukumu yake.

Amesema ushirikiano kati ya NHIF na ZHSF umeleta matokeo makubwa katika hatua mbalimbali za uanzishaji na uendelezaji wa ZHSF, huku akieleza kuwa uzoefu na msaada uliotolewa na NHIF umeiwezesha Zanzibar kuanza na kuendelea vizuri katika safari ya kuimarisha huduma za bima ya afya.

“Kamati inapongeza NHIF na ZHSF kwa mashirikiano makubwa wanayoyafanya ambayo yamewezesha ZHSF kuanza na kuendelea vizuri,” amesema Mhe. Mariam.

Ameongeza kuwa kazi iliyofanywa na NHIF katika kusaidia uanzishaji wa ZHSF ilihitaji uvumilivu na kujitolea kwa kiwango kikubwa, akieleza kuwa Zanzibar imenufaika na uzoefu wa NHIF katika kujenga mfumo wa bima ya afya.

“Kazi iliyofanywa na NHIF ni kazi iliyofanyika kwa uvumilivu mkubwa, lakini kwa kutubeba Zanzibar katika uanzishaji wa Mfuko wetu,” amesema.

Aidha, Mhe. Mariam ameipongeza Menejimenti ya NHIF kwa kuwawezesha kutembelea Hospitali ya Benjamin Mkapa, ambako wamejionea namna wanachama wa NHIF wanavyopokelewa na kuhudumiwa.

Amesema ziara hiyo imewapa fursa ya kuona kwa vitendo ubora wa huduma zinazotolewa, hususan huduma za kibingwa na kibingwa bobezi, ambayo ni mafanikio ya Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan, katika kuboresha huduma za afya nchini.

“Tumejionea namna wanachama wa NHIF wanavyopokelewa na kuhudumiwa. Hakika kazi hii ni kubwa na nzuri ambayo kwa ujumla tunaipongeza Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Mhe. Samia Suluhu Hassan, ambapo huduma za kibingwa na kibingwa bobezi zinapatikana hapa nchini,” amesema. Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa NHIF, Dkt. Irene Isaka, amesema Mfuko utaendelea kushirikiana kwa karibu na ZHSF ili kuhakikisha wananchi na wanachama wanapata huduma bora za afya kwa wakati na kwa ufanisi.

Dkt. Isaka amesema NHIF itaendelea kutoa ushirikiano unaohitajika kwa ZHSF, hususan katika maeneo ya uzoefu, mifumo ya utoaji huduma na masuala mengine ya kitaalamu, kwa lengo la kuimarisha huduma za bima ya afya kwa wananchi wa Zanzibar.

Amesema ushirikiano huo ni sehemu ya dhamira ya NHIF ya kuhakikisha huduma za afya zinapatikana kwa wananchi popote walipo nchini, huku mifuko hiyo ikiendelea kujifunza na kubadilishana uzoefu katika kuboresha huduma kwa wanachama.

Ziara hiyo imefanyika ikiwa ni sehemu ya juhudi za kuimarisha ushirikiano na kubadilishana uzoefu baina ya taasisi zinazohusika na utoaji wa huduma za bima ya afya Tanzania Bara na Zanzibar.

Bima ya Afya kwa Wote, Jiunge Sasa!

GCLA ENDELEENI KUWAJENGEA UWEZO WADAU WA TIBA ASILI

August 28, 2026 Add Comment
Na Mwanaheri Jazza

Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Dkt. Elizabeth Myema, ameipongeza Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali kwa kutoa huduma bora kwa jamii huku akiitaka Mamlaka kuendelea kuwajengea uwezo wadau wanaojihusisha na Tiba Asili kwa kuzalisha dawa zenye ubora kwa kuwa sehemu kubwa ya watanzania wanatumia dawa hizo.

DG NEMC ATUNUKIWA TUZO YA HESHIMA–USIMAMIZI WA MAZINGIRA

August 28, 2026 Add Comment
-Ni katika hitimisho la Kongamano la FARViBE 2026,lililofanyika Jijini Dar es salaam

TFS YATOA ELIMU KWA WAFANYABIASHARA WA MAZAO YA MISITU

August 27, 2026 Add Comment
Na Mwandishi Wetu – Dar es Salaam

Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) umetoa elimu kwa wafanyabiashara wa mazao ya misitu katika eneo la Mbezi Kwa Msuguli, jijini Dar es Salaam, kuhusu sheria na taratibu zinazopaswa kuzingatiwa katika shughuli hizo.

WAZIRI KIKWETE: SOMALIA IMEKUJA KUJIFUNZA MAFANIKIO YA MATUMIZI YA MIFUMO YA KIDIJITARI KATIKA UTUMISHI WA UMMA NCHINI TANZANIA

August 27, 2026 Add Comment


Na Lusungu Helela, Dodoma


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhwani Kikwete, amesema uamuzi wa Serikali ya Somalia kumtuma Waziri mwenye dhamana ya Utumishi wa Umma nchini Tanzania ni ishara ya kutambua mafanikio yaliyofikiwa na Tanzania katika eneo la matumizi ya mifumo katika masuala ya Utumishi wa Umma nchini.

Mhe. Kikwete amesema hayo leo jijini Dodoma wakati akizungumza na ujumbe wa Serikali ya Somalia unaoongozwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Masuala ya Utumishi wa Umma, Hirsi Jama Ganni, uliofika nchini kwa ziara ya kikazi ya siku tatu.

Amesema ujio wa ujumbe huo unaonyesha kuwa Somalia inatambua na kuthamini uzoefu wa Tanzania katika uendeshaji wa Serikali, utumishi wa umma na matumizi ya mifumo ya kidijitali katika utoaji wa huduma kwa wananchi.

“Ukiona wenzako wanakufuata hasa katika eneo hili ambalo sisi ni watoa huduma, ni wazi kuwa huduma tunayotoa wapo wenzetu wanatambua na kuthamini tunachokifanya na ndiyo maana wameamua kuja kujifunza na kupata uzoefu,” amesema Mhe. Kikwete

Amesema anaamini uzoefu ambao Somalia itaupata kupitia ziara hiyo utasaidia kuboresha zaidi masuala ya utumishi wa umma nchini humo.

Mhe. Kikwete amesema ujumbe huo unapata fursa ya kujifunza maeneo mbalimbali, ikiwemo namna Serikali inavyohusiana na wananchi, uratibu wa masuala ya kazi na ajira, usalama wa wafanyakazi mahali pa kazi pamoja na mifumo ya pensheni kwa watumishi wanaostaafu katika taasisi za Serikali na sekta binafsi.

“Hii ziara ni kielelezo tosha kuwa Somalia imedhamiria, ndiyo maana haijaweza kutuma maafisa pekee, lakini Waziri mwenye dhamana ya Utumishi wa Umma ameamua kuja mwenyewe na timu yake kwa lengo la kujifunza na kuja kuona kwa macho yake kazi kubwa iliyofanyika Tanzania,” amesisitiza Mhe. Kikwete

Kwa upande wake, Mhe. Ganni amesema ujumbe wake umefika Tanzania kujifunza namna Tanzania ilivyofanikiwa katika masuala ya utumishi wa umma, hususan matumizi ya mifumo ya kidijitali katika kuboresha utoaji wa huduma.

Amesema Tanzania imekuwa ikifanya vizuri katika utoaji wa huduma kwa wananchi, huku watumishi wa umma wakitumia mifumo ya kidijitali kuwahudumia wananchi na kuhakikisha wanapata haki zao.

Mhe. Ganni amesema ujio wao ni muhimu kutokana na hatua ambazo Tanzania imepiga katika kuboresha utendaji wa Serikali na utoaji wa huduma kwa wananchi.

Amesema wamevutiwa pia na namna mifumo ya Serikali inavyowawezesha watumishi kuwahudumia wananchi kwa ufanisi.

Akizungumzia mfumo wa e-Mrejesho, Mhe.Ganni amesema ni miongoni mwa mifumo waliyoona ina umuhimu katika kuimarisha mawasiliano kati ya Serikali na wananchi, hivyo wanatarajia kujifunza namna unavyofanya kazi na uwezekano wa kutumia uzoefu huo katika kuboresha huduma nchini Somalia.

Ziara hiyo ya ujumbe wa Somalia inalenga pia kujifunza kuhusu mifumo ya Baraza la Mawaziri, usimamizi wa rasilimali watu, uajiri kwa kuzingatia sifa, Serikali mtandao, usimamizi wa ajira na mifumo ya taarifa za soko la ajira.

Ujumbe huo pia unatarajiwa kutembelea Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Ajira na Mahusiano pamoja na Mji wa Serikali Mtumba jijini Dodoma, kwa ajili ya kujionea namna shughuli za Serikali zinavyoratibiwa na kutekelezwa.








TANZANIA YAUNGA MKONO TEKNOLOJIA BUNIFU ZA NYUKLIA KUPITIA MPANGO WA ATLAS

August 27, 2026 Add Comment




Washington Dc,


Waziri wa Nishati na Makamu wa Rais Mteule, Mhe. Deogratius Ndejembi, amelipongeza Shirika la Kimataifa la Nishati ya Atomiki (IAEA) kwa juhudi zake za kuwezesha uzinduzi wa Mpango wa Teknolojia za Atomiki Zilizopewa Leseni ya Matumizi ya Baharini (ATLAS), akieleza kuwa mpango huo ni hatua muhimu katika kuendeleza teknolojia bunifu za nyuklia na kuongeza matumizi ya nishati ya nyuklia duniani.

Mhe. Ndejembi ameyasema hayo wakati akizungumza katika Mkutano wa Ngazi ya Juu wa Uzinduzi wa ATLAS unaofanyika tarehe 26–27 Agosti 2026 jijini Washington, D.C., Marekani.

Amesema mabadiliko makubwa yanayoendelea katika sekta ya nishati duniani yanazilazimu nchi kushirikiana katika kutafuta suluhisho zitakazowezesha kuimarisha usalama wa nishati, kukuza uchumi wa viwanda, kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi na kuhakikisha wananchi wanapata nishati ya uhakika, nafuu na endelevu.

Akieleza hatua zinazochukuliwa na Tanzania katika kuimarisha upatikanaji wa nishati, Mhe. Ndejembi amesema Serikali inaendelea kutekeleza mkakati wa kutumia mchanganyiko wa vyanzo mbalimbali vya nishati, ikiwemo umeme wa maji, gesi asilia, jua, upepo na vyanzo vingine vya nishati jadidifu.

Ameongeza kuwa Tanzania inaendelea kufuatilia kwa karibu maendeleo ya teknolojia bunifu za nishati, ikiwemo teknolojia za nyuklia, kwa lengo la kuongeza fursa za upatikanaji wa nishati salama, ya uhakika na endelevu pamoja na kuchochea maendeleo ya kiuchumi na kijamii.