HABARI

SIASA

ELIMU

Recent Posts

BARRICK YATOA UFADHILI KWA WANAFUNZI WATANO KUSOMA UTAALAMU WA FANI YA MADINI NJE YA NCHI

January 30, 2026 Add Comment
Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) waliopata ufadhili wa kwenda kusoma nchini Afrika ya Kusini
Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam (UDSM) , Profesa William Anangisye akizungumza na kutoa nasaha zake katika hafla ya kuwaaga wanafunzi wa kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) waliopata ufadhili wa kwenda kusoma shahada ya kwanza ya Jiolojia na Madini
Meneja wa Barrick nchini , Dkt. Melkiory Ngido akizungumza na waandishi wa habari , wanafunzi waliopata udhamini kwa kwenda kusoma nchini , Afrika Kusini na wageni kwenye hafla ya kuwaaga wanafunzi iliyofanyika jijini Dar es Salaam
Meneja Rasilimali watu wa Barrick nchini , Lumbu Kambula akizungumza kwenye hafla ya ufadhili wa wanafunzi watano wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) iliyofanyika jijini Dar es Salaam
Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) waliopata ufadhili wa kwenda kusoma nchini Afrika ya Kusini wakiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa Barrick na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM)

**
-Kuendelea kuwekeza katika kizazi kijacho cha wataalamu wa sekta ya madini

Kampuni ya Barrick nchini inayoendesha shughuli zake kwa ubia na Serikali ya Tanzania kupitia Twiga Minerals imetoa ufadhili kwa wanafunzi watano kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) kwenda kusoma Shahada ya kwanza ya Elimu ya Madini na Jiolojia katika Chuo Kikuu cha Johannesburg Afrika ya Kusini kupitia progamu yake ya kuwezesha wasomi vijana inayotekelezwa kanda ya Afrika na Mashariki ya kati.

Akizungumza kwenye hafla ya kutangaza ufadhili huo na kuwaaga wanafunzi waliofanikiwa kupata fursa hiyo jijini Dar es Salaam , Meneja wa Barrick nchini, Dkt. Melkiory Ngido amesema ufadhili huu ni ushuhuda na uthibitisho kwamba Barrick imelenga kukuza sekta ya madini kupitia uwekezaji wake sambamba na kuhakikisha sekta ya madini inatoa mchango mkubwa katika kukuza uchumi wa nchi.

“Uwajibikaji wetu hauishii kuendesha migodi yetu kwa viwango vya kimataifa bali pia tumejikita kuhakikisha tunawekeza katika kuwapatia watanzania ujuzi hususani kwa vijana ambao watakuwa wataalamu wa siku za usoni,ndio maana kupitia udhamini wa elimu kama huu kunawezesha kuwa na wataalamu wa fani ya madini na wabunifu watakaochangia kuleta maendeleo katika siku za usoni”, amesema Dkt.Ngido.

Amesema Barrick itakuwa karibu na Wanafunzi hao na pindi wakapomaliza masomo yao watapatiwa fursa ya kuwajengea uwezo wa kupata ujuzi zaidi kwa kuwapatia ajira katika migodi yake nchini.

Ameongeza kwamba dhamira ya kampuni ya Barrick ni kuendelea na ushirikiano wenye tija kwa kufanya uwekezaji endelevu wenye tija kwa Tanzania na watu wake kwa kuhakikisha kwamba katika programu hii taifa linaweza kupata wataalamu mbalimbali kwenye fani ya Uinjinia wa madini na Jiolojia hapa nchini.

Pamoja na mambo mengine amefafanua kuwa kupitia programu hiyo kampuni ya Barrick kwa kushirikiana na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) wataendelea na kuhakikisha wanazalisha wataalamu wapya kwenye sekta ya madini hapa nchini.

Kwa upande wake , Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) Profesa William Anangisye ameshukuru kwa kampuni ya Barrick kuwapa ufadhili wanafunzi watano kutoka kwenye Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) baada ya kushindanishwa na wenzao kutoka Vyuo vikuu vingine hapa nchini.

“Tumefurahi na ufadhili huu na ni Imani yangu watakwenda kusoma kwa bidhii na hakuna atayerudishwa kwa kushindwa masomo nawataka muwe mabalozi wazuri kwa Chuo chetu na nchini kwa ujumla,” amesema Profesa Anangisye.

Amesema ufadhili wa wanafunzi hawa umekuwa baada ya mchujo wa wanafunzi kutoka vyuo mbalimbali hapa nchini na hatimaye hawa wameshinda , hawa ni kati ya wanafunzi bora waliopita kwenye mchujo na kupata ufadhili kwa kwenda kusoma shahada ya kwanza kwenye madini,” .

“Ni furaha yangu kuona kwamba kati ya wanafunzi hawa waliopata ufadhili kuna wasichana hii ni moja ya sera ya pale mlimani kuweka uwiano wa jinsia kwenye masomo ili kuhakikisha watoto wa kike na wenye uwezo wanapata fursa za kusonga mbele,” amesisitiza.

Mmoja ya wanafunzi akiongea kwa niaba ya wenzake, Samson Abeid amesema programu hiyo ni fursa ya kipekee kwa wanafunzi wa kitanzania kwa kusoma kwa bidii na kuhakikisha kwamba wanatoa mchango katika maendeleo ya taifa.

“Programu hii itachochea chachu katika sekta ya elimu hapa nchini na kutoa fursa kwa wanafunzi wa kitanzania kupata elimu , maarifa na ujuzi nje ya nchini,” amesema Abeid.
Mmoja wa wanufaika akipokea nyaraka za ufadhili, katika hafla hiyo

WANANCHI MONDULI WAHAMASISHWA KUUNGA MKONO AJENDA YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA

January 30, 2026 Add Comment

 


Na Mwandishi Wetu


Wizara ya Nishati imetoa wito kwa wananchi wa Wilaya ya Monduli  kuachana na matumizi ya kuni na mkaa na badala yake watumie nishati safi ya kupikia, ili  kuunga mkono juhudi za Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan za kuhakikisha ifikapo mwaka 2034, asilimia 80 ya Watanzania wanatumia nishati safi ya kupikia.

Wito huo umetolewa na Mkurugenzi wa Nishati Safi ya Kupikia kutoka Wizara ya Nishati, Nolasco Mlay kwenye ziara ya ukaguzi wa utekelezaji wa maagizo ya Ofisi ya Makamu wa Rais yanayohimiza matumizi ya nishati safi katika taasisi zote zinazohudumia watu zaidi ya 100, Wilaya ya Monduli, Mkoa wa Arusha.

Mlay amesema umefika wakati kwa wananchi kubadili mtazamo na kuachana na jitihada za kutafuta kuni au magunia ya mkaa, na badala yake kuelekeza nguvu katika matumizi ya nishati safi ambayo ni salama kwa afya na mazingira.

“Mazingira ni ajenda ya dunia nzima, na Rais wetu ni kinara wa matumizi ya nishati safi ya kupikia. Hivyo ni wajibu wetu kuunga mkono dhamira yake kwa kukaa pamoja, kujadiliana na kubuni mikakati ya kuwatoa wananchi kwenye matumizi ya nishati zisizo salama na kuwapeleka kwenye matumizi ya nishati safi,” amesisitiza.

Aidha, Mlay amewapongeza viongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Monduli kwa kazi nzuri wanayoifanya ya kutekeleza maagizo ya Serikali kuhusu matumizi ya nishati safi ya kupikia katika taasisi mbalimbali.

Amesema si rahisi kwa Serikali kufahamu changamoto zilizopo katika kila eneo, hivyo mchango wa viongozi wa halmashauri ni muhimu kwani wanajitoa kwa dhati kufichua changamoto zilizopo bila hata kulipwa.


“Serikali inatambua jitihada hizi na inathamini sana taarifa za changamoto zinazowasilishwa, jambo linalowezesha kuchukuliwa kwa hatua stahiki kwa manufaa ya wananchi,” ameongeza.




WANAFUNZI 500 JIJINI TANGA WASHIRIKI BONANZA LA MICHEZO LA MICHEZO PLUS .

January 30, 2026 Add Comment



Na Oscar Assenga, TANGA



BONANZA la Michezo maarufu kama Michezo Plus limekuwa na mvuto wa aina yake huku likifanyika kwenye viwanja vya Shule ya Sekondari Tanga Ufundi kwa kushirkisha wanafunzi zaidi ya 500.


Wanafunzi hao kutoka shule 50 Jijini Tanga ambao walishiriki katika Michezo ya Mpira wa Miguu,Pete na Wavu huku wakionyesha vipaji vya hali ya juu hatua iliyoshangiliwa na wadau wa michezo ambao walijitokeza kushuhudia bonanza hilo


Akizungumza baada ya kumalizika kwa Bonanza hilo Afisa Michezo wa Jiji la Tanga na Mratibu wa Michezo Plus katika mradi unaotekelezwa na Jiji hilo ukifadhiliwa nan a Botnar Foundation chini ya Programu ya Tanga Yetu Lucy Michael alisema kwamba waliliandaamaalumu kwa ajili ya kujenga mahusiano na kuwajenga kiakili.

Alisema kwamba bonanza hilo litakuwa linafanyika kila mwaka mara mbili ambapo hilo limeanza kwa kufungua mwaka na kukaribisha wanafunzi na watafanya bonanza la vijana.



Awali akizungumza Mratibu wa Bonanza hilo Haji Milao alisema kwamba nia na madhumuni yake ni kuwaweka watoto sawa kwa ajili ya michezo ya Umistashumta mwaka huu 2026 ikiwemo kutengeneza afya za watoto ili waweze kuwa sawa na watoto wakiwa vizuri kwenye michezo hata darasani watakuwa vizuri.



Naye kwa upande wake Mwanafunzi wa Shule ya Msingi Makorora Zuhuru Ally alisema michezo hiyo ina faida kubwa sana kwao kutokana na kwamba inawafanya wakutana na wenzao na kubadilisha mawazo jambo ambalo linawapa fursa.


RAIS DKT.SAMIA AMEJIPANGA KUFIKISHA UMEME VITONGOJI VYOTE

January 30, 2026 Add Comment


*📌Bilioni 24.9 kupeleka umeme vitongoji 218 Njomb*


📍Njombe


Imeelezwa kuwa, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameelekeza Wakala wa Nishati Vijijini (REA), kufikisha umeme kwenye vitongoji vyote vilivyobakia nchini ambavyo bado havina huduma ya umeme ifikapo mwaka 2030.


Hayo yamebainishwa leo Januari 30, 2026 na Bw. Frank Mugogo kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa REA, Mha. Hassan Saidy wakati wa hafla fupi ya kumtambulisha mkandarasi kutoka kampuni ya Central Electricals International Ltd katika Mradi wa HEP 2B ambaye anaenda kutekeleza kwenye vitongoji 218 mkoani Njombe.

"Jumla ya vitongoji vyote mkoa wa Njombe ni 1,833 na vitongoji vyenye umeme ni 1,276. Vilevile vitongoji ambavyo havina umeme ni 557. Hivyo mradi huu unakwenda kupeleka umeme kwenye vitongoji 218 katika mkoa huu na vitabakia vitongoji 339 ambavyo havina umeme navyo vitakamilika, " Amesema Bw. Mugogo.

Ameongeza kuwa, gharama za kuunganisha umeme huo ni shilingi 27,000 tu na kuwataka wananchi wa mkoa huo kutumia fursa ya kuunganisha umeme kwa gharama nafuu iliyowezeshwa na Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mhe.Rais Samia.

Akizungumza mara baada ya kupokea taarifa ya utekelezaji wa miradi hiyo mkoani Njombe, Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa Bw. Lewisi Mnyambwa amemshukuru Rais Samia kwa kuleta fedha nyingi zaidi ya bilioni 24 ili kupeleka umeme kwenye vitongoji vya mkoa wa Njombe.


"Serikali kupitia REA imefanya kazi kubwa. Tunasisitiza miradi hii ikamilike kwa muda uliopangwa na tutaendelea kuusimamia ipasavyo ili mkandarasi aweze kutekeleza majukumu yake pasipo changamoto yeyote katika kipindi chote cha utekelezaji wa mradi," Amesema Mnyambwa. 

Aidha, ametoa rai kwa wananchi wanaozunguka eneo la mradi kumpatia ushirikiano mkandarasi huyo na ametakiwa kutoa kipaumbele cha ajira kwa wazawa ili kufanya shughuli mbalimbali katika mradi huo ili uchumi wa wananchi uongezeke na wanufaike na uwepo wa miradi hiyo katika mazingira yao.


Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Miradi kutoka kampuni ya Central Electricals International Ltd, Bw. Zameer Meghji ameishukuru Serikali kupitia REA kwa kupewa fursa ya kutekeleza mradi huo mkubwa. Amesema watahakikisha miradi hiyo inakamilika kwa wakati, watashirikiana na wananchi na kutoa kipaumbele cha ajira kwa wazawa ili miradi hiyo ilete tija kwa wananchi na nchi kwa ujumla.


Mwisho

MAADHIMISHO YA IEW 2026 YACHOCHEA UWEKEZAJI WA MAFUTA NCHINI TANZANIA

January 30, 2026 Add Comment



Na Mwandishi Wetu


Wadau na wawekezaji mbalimbali wameonesha nia ya kuwekeza katika sekta ya mafuta nchini Tanzania, uwekezaji ambao utachangia ukuaji wa uchumi wa nchi na kuboresha huduma ya bidhaa za nishati kwa wananchi.


Miongoni mwa wawekezaji hao ni Kampuni ya Mafuta ya India (Indian Oil Corporation Limited), yenye uzoefu mkubwa katika usambazaji wa mafuta na gesi, ambayo imeonesha nia ya kuwekeza nchini Tanzania.

Kampuni hiyo imeonesha nia hiyo katika kikao kilichofanyika kati yao na ujumbe wa Tanzania ukiongozwa na Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba pembezoni mwa Maadhimisho ya Wiki ya Nishati ya India 2026 yanayoendelea Jimbo la Goa, nchini India.

Katika kikao hicho, Mkurugenzi wa Mipango na Biashara wa kampuni hiyo, Suman Kumar, amesema Tanzania ni soko la bidhaa nyingi ikiwemo bidhaa za nishati.

Amesema kutokana na ongezeko la mahitaji ya bidhaa kama mafuta, gesi ya mitungi na nishati linalotokana na ukuaji wa uchumi, idadi ya watu inayoongezeka na miji kukua haraka, inatoa fursa kwa kampuni za nishati kushirikiana katika usambazaji, uchakataji na huduma za nishati.

Kwa upande wake Mhe. Salome amesema “Serikali ya Tanzania inawakaribisha wawekezaji wote na ipo wazi kwa uwekezaji wa kimataifa katika sekta ya nishati, ikiwa ni pamoja na usambazaji wa mafuta na gesi ya mitungi kuendana na msukumo wa Serikali wa kukuza matumizi ya nishati safi ya kupikia."

Aidha Mhe. Salome amewahimiza wawekezaji hao kuona umuhimu wa kufungua matawi nchini Tanzania na kushiriki katika ununuzi wa pamoja wa bidhaa za mafuta ili kuongeza ushindani na uhakika wa upatikanaji wa mafuta ya gharama nafuu nchini.


 "Hivyo tunawakaribisha wadau wote kuja kuwekeza nchini Tanzania kupitia makubaliano ya kibiashara na kampuni zetu za ndani kulingana na sera za Tanzania na mapendekezo ya wawekezaji” amesema Mhe. Salome.


Maadhimisho ya Wiki ya Nishati ya India 2026 yanatarajiwa kuhitimishwa Januari 30, 2026 na yamewakutanisha washiriki kutoka nchi zaidi ya 125, yakivutia wawekezaji wengi wa kigeni katika sekta ya nishati. 


Kupitia Maadhimisho hayo yamefungua fursa mbalimbali za uwekezaji katika sekta ya nishati kwa wadau na wawekezaji kutoka sehemu mbalimbali duniani.


&&&









WAKANDARASI WALIOSHINDA ZABUNI YA UTEKELEZAJI MRADI WA KUSAMBAZA UMEME VITONGOJI 527 MKOANI TANGA WATAMBULISHWA RASMI

January 30, 2026 Add Comment


Wakandarasi walioshinda zabuni ya kutekeleza mradi wa kusambaza umeme katika vitongoji 527 mkoani Tanga kupitia Kampuni ya Giza cable industries pamoja na Energy service Limited ka wametambulishwa rasmi mkoani Tanga kwa ajili ya kuanza utekelezaji wa mradi huo

Mradi huo unatekelezwa na Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) wenye thamani ya shilingi bilioni 73.8 ambao utasaidia kwa kiasi kikubwa kuwezesha vitongoji hivyo kuweza kupata nishati hiyo muhimu

Akizungumza wakati wa halfa ya kuwatambulisha wakandarasi hao Mkurugenzi Mkuu wa REA, Mhandisi. Hassan Saidy wakati wa kuwatambulisha Wakandarasi waliuoshinda zabuni ya kutekeleza mradi huo, Kampuni ya Giza cable industries pamoja na Energy service Limited katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa huo.

Alisema wakati wanafanya nao majadiliano kuna maagizo mahususi waliwapa na wangependa kama kiongozi wa mkoa waifahamu ikiwemo kuwaelekeza wawe na timu ya kufanya kazi karibu kila Wilaya.

Aidha aliwataka wakandarasi haoa kujiepusha na vitendo vya kutoa lugha chafu, pamoja na vitendo vya rushwa wakati wanatekeleza miradi hiyo kwa wananchi.

Aliongeza kuwa ukifanya kazi kwenye mradi wa Serikali wanatakiwa kufanya kama mtumishi wa umma hivyo lugha chafu hazikubaliki ikiwemo kurubuni wanakijiji ni kitu ambacho kitapelekea kuvunja mkataba wako.

Kwa upande wake Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Dadi Kolimba aliipongeza serikali kwa utekelezaji wa mradi huo na kusema kuwa utakwenda kufungua zaidi fursa za uchumi vijijini.

“Ukiangalia kwa wakandarasi hawa wawili ambao wametambulishwa leo ambao wanaenda kutekeleza mradi wa kupeleka umeme katika vitongoji 527, jumla ya shilingi Bilioni 73.8.

Hata hivyo alisema kwamba wana kila sababu ya kumshukuru Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwezesha kutoa fedha za kuwezesha kutekelezwa kwa mradi huu.

Kolimba aliwataka wakandarasi hao kuhakikisha wanamaliza mradi huo ndani ya muda uliopangwa.

Alitoa wito kwa wananchi kutoa ushirikiano kwa wakandarasi hao pindi watakapoanza kutekeleza mradi huo ili malengo yaliyowekwa na serikali yaweze kufikiwa.

Mwisho.









REA YAMTAKA MKANDARASI NOTHERN ENGINEERING MTWARA KUONGEZA KASI YA UJENZI WA MRADI

January 30, 2026 Add Comment
Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umemtaka Mkandarasi anayetekeleza Mradi wa Kusambaza umeme katika Vitongoji 150 vya Majimbo 10 Mkoani Mtwara kuongeza kasi ya ujenzi ili kukamilisha Mradi kwa wakati.

BIL. 73.8 KUPELEKA UMEME VITONGOJI 527 MKOA WA TANGA

January 30, 2026 Add Comment







Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) inatekeleza mradi wa shilingi bilioni 73.8 wa kusambaza umeme katika vitongoji 527 mkoani Tanga.

Hayo yamebainishwa leo Januari 29, 2026 Jijini Tanga na Mkurugenzi Mkuu wa REA, Mha. Hassan Saidy wakati wa kuwatambulisha Wakandarasi waliuoshinda zabuni ya kutekeleza mradi huo, Kampuni ya Giza cable industries pamoja na Energy service Limited katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa huo.

“Leo tuko hapa kwako kutambulisha Wakandarasi ambao watakuja kutekeleza mradi mkubwa wa kupeleka umeme katika vitongoji 527 katika Mkoa wa Tanga.

Wakati tunafanya nao majadiliano kuna maagizo mahususi tuliwapa na tungependa kama kiongozi wetu wa Mkoa uyafahamu. Moja tumewaelekeza wawe na timu ya kufanya kazi karibu kila Wilaya,” ameainisha Mhandisi Saidy.

Ameongeza pia, Wakandarasi hao wanatakiwa kujiepusha na vitendo vya kutoa lugha chafu, pamoja na vitendo vya rushwa wakati wanatekeleza miradi hiyo kwa wananchi.

“Ukifanya kazi kwenye mradi wa serikali unatakiwa kufanya kama mtumishi wa umma. Lugha chafu hazikubaliki. Kurubuni wanakijiji ni kitu ambacho kitapelekea kuvunja mkataba wako,” amessisitiza Mhandisi Saidy.

Kwa upande wake Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mhe. Dadi Kolimba ameipongeza serikali kwa utekelezwaji wa mradi huo na kusema kuwa utakwenda kufungua zaidi fursa za uchumi vijijini.

“Ukiangalia kwa wakandarasi hawa wawili ambao wametambulishwa leo ambao wanaenda kutekeleza mradi wa kupeleka umeme katika vitongoji 527, jumla ya shilingi Bilioni 73.8. Tuna kila sababu ya kumshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwezesha kutoa fedha za kuwezesha kutekelezwa kwa mradi huu,” amesema Mhe. Kolimba huku akiwataka Wakandarasi hao kuhakikisha wanamaliza mradi huo ndai ya muda uliopangwa.

Aidha, Mhe. Kolimba ametoa wito kwa wananchi kutoa ushirikiano kwa wakandarasi hao pindi watakapoanza kutekeleza mradi huo ili malengo yaliyowekwa na serikali yaweze kufikiwa.









NLD WAMSIMAMISHA MHAGAMA KUWANIA UBUNGE JIMBO LA PERAMIHO

January 29, 2026 Add Comment


Na Mwandishi Wetu ,RUVUMA.

CHAMA cha National League For Democracy (NLD) kimempitisha Mhagama Hamisi Yusufu kuwania Ubunge Jimbo la Peramiho Mkoani Ruvuma ambayo ataipeperusha Bendera ya chama hicho katika uchaguzi wa mdogo kufuatia Kifo cha aliyekuwa Mbunge wa Jimbo hilo Jenista Mhagama.

Akizungumza na waandishi wa habari mjini hapa,Katibu wa NLD Doyo Hassan Doyo ambapo aliwaambia kwamba siku hiyo ni muhimu kwa wananchi wa Jimbo la Peramiho kufanya maamuzi ya kiongozi wanayemtaka .

Alisema kwamba kiongozi ambaye anaweza kuwaletea maendeleo wananchi wa Jimbo hilo ni mgombea wao kutokana na uongozi uliopita kwa miaka mingi umeshindwa kuwapa maendeleo na mabadiliko katika Jimbo hilo.

Katibu huyo aliwataka wananchi hao kutokufanya makosa katika uchaguzi huo wa marudio kutokana na aliyekuwa Mbunge wa Jimbo hilo kufariki dunia hivyo aliwataka kumchagua mgombea anayetokana na NLD ili aweze kuwapa maendeleo makubwa.

Katika uchaguzi huo Mhagama Hamis Yusuf wa NLD atachuana na wagombea wengine akiwemo Yusuf Rashid Rai wa Chama cha AAFP,Abdallah Boniface Ngonyani wa Chama cha Makini,Hanifa Sembe Mohamed wa Chama cha UMD,Beatrice Omari Muya wa UPDP,Mapunda wa Chama cha DP,Dastan Frolian Pili wa CCK,Morice Thomas Nkongo wa TLP na Mtemi Pachoto wa UDP.


Mwisho.