HABARI

SIASA

ELIMU

Recent Posts

TANGA KUWA MWENYEJI MAADHIMISHO YA SIKU YA HAKI ZA MTUMIAJI 2026

TANGA KUWA MWENYEJI MAADHIMISHO YA SIKU YA HAKI ZA MTUMIAJI 2026

March 11, 2026 Add Comment






Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam

Jukwaa la Watumiaji Tanzania (TCF) limetangaza kuwa maadhimisho ya kitaifa ya Siku ya Haki za Mtumiaji Duniani kwa mwaka 2026 yatafanyika jijini Tanga tarehe 15 Machi 2026, yakilenga kuhamasisha ulinzi wa haki, usalama na ustawi wa watumiaji wa bidhaa na huduma nchini.

Akizungumza na vyombo vya habari jijini Dar es Salaam Machi 10, 2026, Mwenyekiti wa Jukwaa hilo, D.G. Daudi, amesema maadhimisho hayo yatatoa fursa kwa wananchi kupata elimu kuhusu haki na wajibu wao kama watumiaji wa huduma mbalimbali zinazodhibitiwa.

Aidha Daudi amesema kuwa, maadhimisho ya mwaka huu yanaongozwa na kaulimbiu isemayo “Bidhaa Salama, Watumiaji Wenye Kujiamini,” inayolenga kuhimiza upatikanaji wa bidhaa na huduma salama zinazokidhi viwango vya ubora ili kuwajengea watumiaji uwezo wa kufanya maamuzi sahihi.

Amesema watumiaji wenye kujiamini ni wale wanaopata bidhaa na huduma salama, wanaofahamu haki na wajibu wao pamoja na kuwa na uwezo wa kuhoji ubora wa huduma wanazotumia.

Daudi ameeleza kuwa katika kuelekea kilele cha maadhimisho hayo, TCF imeandaa shughuli mbalimbali za utoaji elimu kwa umma zitakazoanza Machi 10 hadi 15, 2026 kupitia vipindi vya vyombo vya habari na semina kwa makundi tofauti ya watumiaji.

Amesema maadhimisho ya mwaka huu yataweka msisitizo katika usalama wa huduma na bidhaa katika sekta mbalimbali zinazodhibitiwa, ikiwemo huduma za nishati na maji, usafiri wa anga, usafiri wa nchi kavu pamoja na huduma za mawasiliano.

Kwa upande wake, jukwaa hilo limewahimiza wananchi kushiriki kikamilifu katika shughuli hizo ili kupata elimu kuhusu haki zao na kutumia mifumo iliyopo kuwasilisha maoni au malalamiko kuhusu huduma wanazopokea.

Wananchi wa jijini Tanga na maeneo ya jirani wamekaribishwa kushiriki katika kilele cha maadhimisho kitakachofanyika katika Ukumbi wa Mkurugenzi wa Jiji, ambapo kutakuwa na maonesho, utoaji elimu kwa umma pamoja na fursa ya kujifunza taratibu za kulinda haki zao kama watumiaji.

Jukwaa la Watumiaji Tanzania linaundwa na Mabaraza ya Ushauri ya Watumiaji kutoka mamlaka mbalimbali za udhibiti nchini ikiwemo EWURA CCC, LATRA CCC, TCAA CCC na TCRA CCC, ambayo hushirikiana kulinda na kutetea maslahi ya watumiaji wa huduma hizo.

WANAWAKE WA UWT KIBAHA MJI WAANZA KUTEMA CHECHE BAADA YA USHINDI WA KISHINDO KATIKA UCHAGUZI MKUU

March 11, 2026 Add Comment


NA VICTOR MASANGU,KIBAHA

Jumuiya ya umoja wa wanawake (UWT) Wilaya ya Kibaha mjini katika kukiimarisha chama imeamua kufanya ziara maalumu yenye lengo la kuwashukuru na kuwapongeza wanawake kwa umoja wao na mshikamao waliouonyesha katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2025 na kupelekea chama cha mapinduzi (CCM) kuweza kushinda kwa kishindo katika nafasi za Udiwani, Ubunge pamoja na Urais.

Akizungumza katika ziara hiyo ambayo imefanyika katika Kata mbili za Visiga pamoja na Misugusugu Mwenyekiti wa (UWT) Wilaya ya Kibaha Elina Mgonja amesema kwamba wameamua kufanya ziara hiyo ambayo itaweza kuwapa fursa ya kukutana na wanawake hao ambao ndio walikuwa mstari wa mbele katika kukipigania chama kiweze kushinda na kupata viongozi wa CCM katika nafasi mbali mbali.'

Katika ziara hiyo ambayo imeongozwa na Mwenyekiti wa UWT Wilaya ya Kibaha pamoja na baadhi ya wajumbe wa kamati ya utekelezaji ambapo pia wametumia fursa ya kutembelea zahanati ya Misusugu pamoja na kuendesha zoezi la upandaji wa miti.

Mwenyekiti huyo amebainisha kwamba wameamua kufanya ziara hiyo kwa lengo la kuweza kutoa shukrani kwa wanawake ikiwa pamoja na kuhamasiha viongozi wa matawi mbali mbali kuwezaa kushikamana kwa pamoja ili kuimalisha uwahi wa jumuiya pamoja na chama kuanzia ngazi za chini.

"Tumeanza ziara yetu ya jumuiya ya wanawake Wilayaa ya Kibaha ambapo tumetembeleakata mbili za visiga pamoja na kata ya Misugusugu lakini kitu kikubwa ni kwa ajili ya kuwashukuru wanawake wote wa chama cha mapinduzi pamoja na jumuiya wa UWT kwa kuweza kuwachagua viongozi kwa kura nyingi za kishindo katika nafasi ya Udiwani, Ubunge, pamoja na nafasi ya Urais,"amebainisha Elina

Kadhalika Mwenyekiti huyo amempongeza kwa dhati Rais wa awamu ya sita kwa kuweza kutekeleza ilani ya cchama kwa vitendo ikiwemo kutenga fedha nyingi ambazo zimekwenda kutekeleza miradi mbali mbali ya maendeleo ikiwemo sekta ya afya, eilimu, maji, nishati ya umeme pamoja na huduma za kijamii.

Kwa upande wake Katibu wa UWT Wilaya ya Kibaha Cesilia Ndalu amesema kuwa ziara hiyo pia imelenga kuanzisha vikundi vya uchumi ambavyo vitaweza kuwasaidia kwa kiasi kukubwa kupambana na wimbii la umasikini.

Diwani wa kata ya Misugusugu Ally Simba amewahimiza wanawake wa UWT kuhakikisha wanachangamkia fursa za mikopo mbali mbali ambayo inatolewa na Halmashauri kwa lengo la kuweza kujikwamua kiuchumi pamoja na kuleta mabadiliko chanya ya kimaendeleo katika nyanja tofauti.

RAIS SAMIA AMUASILI MTOTO MCHANGA ALIYETELEKEZWA NZEGA

March 11, 2026 Add Comment



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, amemuasili mtoto mchanga wa kike leo tarehe 11 Machi, 2026, katika makazi yake, Ikulu Chamwino, mkoani Dodoma.

Mtoto huyo aliyepewa jina la Grace Samia Suluhu, alitelekezwa mjini Nzega, mkoani Tabora, na amekabidhiwa kwa Rais Dkt. Samia na Mkuu wa Wilaya ya Nzega, Mhe. Naitapwaki Tukai. 



Akizungumza wakati wa kumkabidhi mtoto huyo, Mkuu wa Wilaya Tukai alisema mtoto huyo aliokotwa tarehe 17 Januari, 2026 akiwa ametelekezwa katika eneo jirani na nyumba ya wageni ya Kasulu, Nzega Mjini.

Alieleza kuwa baada ya kupokea taarifa hizo, alishirikiana na Jeshi la Polisi kumchukua mtoto huyo na kumpeleka hospitalini kwa uchunguzi na uangalizi, huku juhudi za kumtafuta mama yake zikiendelea bila mafanikio.

Rais Dkt. Samia amemkaribisha mtoto huyo katika familia yake na kuahidi kumpatia malezi, ulinzi na huduma zote muhimu ili akue katika mazingira salama na yenye upendo.

“Wanaotupa watoto hawajui wanalolifanya. Kuliko kumtupa mtoto ni afadhali ukamkabidhi katika mamlaka za kisheria au kituo cha kulelea watoto


WAZIRI KATAMBI MBELE YA KAMATI YA MAMBO YA NJE,ULINZI NA USALAMA

March 11, 2026 Add Comment


Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,Patrobas Katambi akiwasilisha Taarifa ya Utekelezaji wa Miradi iliyopo katika Vyombo vya Usalama vilivyopo chini ya wizara yake kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje,Ulinzi na Usalama.

Amewasilisha Taarifa hizo leo jijini Dodoma ikiwa ni utaratibu wa kamati hiyo kupokea Taarifa za Utekelezaji wa Miradi iliyotolewa fedha za Serikali.



VIGEZO VINNE VYA KUMPATA MREMBO WA KIHADZABE,KARIBU JIOPAKI YA NGORONGORO

March 11, 2026 Add Comment




Wahadzabe ni kabila linalopatikana pembezoni mwa ziwa Eyasi na habari za maisha yao zimehifadhiwa makumbusho ya Urithi Jiopaki liyopo Karatu.


Baadhi ya vidume vinatamani kuwaoa wasichana wa kihadzabe  lakini kuwapata si kazi rahisi, lazima utumize vigezo vinne kama ifuatavyo; 


Kwanza *Usitahiriwe* , Kabila hili linaamini kwamba mwanaume kutahiriwa hupunguza utaalam wa mambo na kufanya  mwili wako kuwa legelege.


Pili, uwezo wa *kula Mizizi , matunda na nyama pori,* wakiamini kuwa vitu hivyo hukupa nguvu ya kutosha na Jembe la kazi wakati wa tendo la ndoa na huitaji kutafuta Vumbi la Congo kama wala Chipsi mjini.


Tatu uwezo wa *kulenga shabaha,* wakiamini kwamba hutamlaza njaa  kila siku utarudi na nyama pori ambayo ni chakula hapo nyumbani.


Nne *usiwe na mchepuko* , wakiamini mtu anayechepuka anaweza kuuawa wakati wowote akifumaniwa kwa kuzini na pia kuleta maradhi nyumbani.


Karibuni makumbusho ya  Jiopaki na eneo la  ziwa Eyasi kwa wahadzabe ujue kuwa mcheza kwao hutuzwa

DKT.MAGEMBE ATAKA KILA MWAJIRI AHAKIKISHE MTUMISHI WAKE ANAKUWA NA UHAKIKA WA MATIBABU KUELEKEA BIMA YA AFYA KWA WOTE

March 10, 2026 Add Comment




Na Hassan Kimweri, WAF - Dar es Salaam


Mganga Mkuu wa Serikali Dkt. Grace Magembe amewataka waajiri kuhakikisha kila muajiriwa anakuwa na uhakika wa matibabu kuelekea utekelezaji wa Bima ya Afya kwa Wote na Dira ya Maendeleo ya Taifa ya mwaka 2050. 


Dkt. Magembe amesema hayo leo Machi 10, 2026 baada ya wasilisho la maandalizi ya Bima ya Afya kwa Wote kwenye mkutano na Wakurugenzi Wakuu wa Makampuni ya Tanzania (CEO Roundtable of Tanzania – CEOrt) uliofanyika jijini Dar es Salaam na kuwakutanisha viongozi kutoka serikalini, sekta binafsi na washirika wa maendeleo. 



"Serikali inaendelea kuimarisha utekelezaji wa mpango wa Bima ya Afya kwa Wote kwa kuwa na ubunifu wa vyanzo vya fedha pamoja na kuanzisha kitita muhimu kitakachohakikisha kila mwananchi anapata huduma muhimu za afya katika vituo vyote vya kutolea huduma nchini," amesema Dkt. Magembe

Aidha, Dkt. Magembe amesema Serikali imeanza utekelezaji wa Sheria ya Bima ya Afya kwa Wote ambapo utekelezaji wake unafanyika kwa awamu, awamu ya kwanza ilianza Januari 6, 2025 kwa kuwatambua zaidi ya familia milioni 3.6 kidijitali kwa kushirikiana na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) pamoja na Mamlaka za Serikali za Mitaa," amesema Dkt. Magembe

Katika hatua nyingine, Dkt. Magembe amesema Serikali imeanzisha Mfuko wa kugharamia huduma za Afya (Health Equity Fund) utakaosaidia kugharamia huduma za afya kwa wananchi wasio na uwezo wa kumudu gharama za matibabu kupitia vyanzo mbalimbali.

Pia, amesema Serikali imeanza kuchukua hatua za kupunguza utegemezi wa misaada ya wahisani katika sekta ya afya kwa kuimarisha zaidi vyanzo vya ndani vya fedha na kutafuta mbinu mpya za ubunifu zitakazochangia kugharamia huduma za afya nchini.

Hata hivyo, ameeleza dhamira ya Serikali kuimarisha viwanda vya ndani vya dawa na bidhaa za afya ili kuhakikisha upatikanaji wa dawa unakuwa wa uhakika, kuongeza ajira na kukuza sekta binafsi kuelekea utekelezaji wa bima ya afya kwa wote. 

Mwisho, Serikali imewahimiza wawekezaji kutumia fursa zilizopo katika sekta hiyo, huku ikiendelea kukuza ushirikiano kati ya sekta ya umma na binafsi katika uzalishaji wa dawa na vifaa tiba nchini. 



MCHAWI WA MWANAMKE SI MWANAMKE

March 10, 2026 Add Comment


Wanawake watumishi wa Mamlaka  Hifadhi ya Ngorongoro katika muendelezo wa  kuadhimisha Siku ya Wanawake Duniani, wamedhihirisha kwamba mchawi wa mwanamke si mwanamke  kwa kutembelea  shule ya Sekondari ya wasichana Ngorongoro na kuwapa tabasamu la  msaada wa vifaa mbalimbali


Akiongea kwa Niaba ya Kamishna wa Uhifadhi, Afisa Uhifadhi Mkuu Sarah Lushu ameeleza kuwa vitu ambavyo Mamlaka vinajumuisha vyakula, Sabuni, vifaa vya kujifunzia, taulo la kike, Vyombo vya kuogea, kupikia na kufulia na mahitaji mbalimbali mahususi kwa wanafunzi wanawake ilo kuwaongezea tabasabu na kuonyesha nguvu ya mwanamke katika Jamii.

"Msaada huu ni sehemu ya jitihada za Shirika kupitia kamishna wa Uhifadhi kuimarisha uhusiano na jamii iliyopo ndani ya Hifadhi na kuhakikisha kuwa wanafunzi hasa wa kike wanapata mahitaji muhimu ya kuwapa utulivu wa kusoma na kupata ufaulu mzuri" alifafanua PCO Sarah.

Msaada huu unadhihirisha wazi kuwa wanawake ni watu wa kusaidiana na mchawi wa mwanamke sio Mwanamke.

KAMATI YA BUNGE YAAGIZA UDHIBITI WA USAHIHI WA VIPIMO UONGEZEWE NGUVU

KAMATI YA BUNGE YAAGIZA UDHIBITI WA USAHIHI WA VIPIMO UONGEZEWE NGUVU

March 10, 2026 Add Comment

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara, Kilimo na Mifugo imeiagiza Wakala wa Vipimo (WMA) kuongeza nguvu katika kudhibiti usahihi wa vipimo ili kuhakikisha huduma wanazopata wananchi zinaendana na thamani halisi ya fedha wanayotumia

Hayo yamesemwa na Mwenyekiti wa Kamati ya kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara, Kilimo na Mifugo Mhe. Deodatus Mwanyika (Mb), Wakati Kamati hiyo ili pokea Taarifa ya Wizara ya Viwanda na Biashara kuhusu utekelezaji ya Miradi ya Maendeleo kwa mwaka 2025/26 kutoka Wakala wa Vipimo (WMA) na Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE) Taasisi zake yake Machi 10, 2026 , Bungeni jijini Dodoma.

Mwanyika amesisitiza kuwa vita dhidi ya lumbesa haipaswi kuachiwa WMA pekee, bali inahitaji nguvu ya pamoja kati ya Halmashauri, Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), na Serikali Kuu ili kufanya oparesheni za nchi nzima.

Nao, Wajumbe wa Kamati hiyo walizipongeza WMA na CBE kwa utekelezaji wa miradi mbalimbali na kutoa maoni na mapendekezo mbalimbali yaliyolenga kuboresha utekelezaji wa Miradi hiyo kwa ufanisi.

Naye, Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Dennis Londo (Mb), alifafanua kuwa msingi wa Tanzania ya Viwanda ni kilimo ambapo WMA inatekeleza jukumu la kumlinda mkulima, huku akibainisha kuwa idadi kubwa ya watumishi wa Wakala huyo wanazalishwa na Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE), jambo linaloashiria kuwepo kwa uhusiano mkubwa wa kikazi baina ya taasisi hizo mbili.

Naye Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Vipimo (WMA), Bw. Alban Kihulla, amesema kuwa taasisi hiyo, kwa wakishirikiana na mamlaka nyingine za Serikali pamoja na sekta binafsi, wanaenda kupata suluhisho la kudumu la malalamiko ya wananchi ambayo yamekuwa yakiwasilishwa kwa muda mrefu kuhusu ukosefu wa usahihi wa vipimo katika maeneo mbalimbali ikiwemo lumbesa.

Kwa upande wake Mkuu wa Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE), Prof. Edda Lwoga amesema miradi ya majengo inayojengwa kwenye Kampasi mbalimbali za Chuo hicho mara itakapokamilika itaboresha mazingira ya kujifunzia na kuongeza udahili wa wanafunzi katika chuo hicho.

WIZARA YA NISHATI YAPOKEA TRIL.1 ZA MIRADI YA MAENDELEO

March 10, 2026 Add Comment




 ðŸ“ŒNi asilimia 61 ya bajeti ya 2025/26


Na Mwandishi Wetu, Dodoma


WIZARA ya Nishati imepokea Sh. trilioni 1.150 kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika kipindi cha Julai 2025 hadi Februari 2026, sawa na asilimia 61 ya bajeti ya maendeleo iliyoidhinishwa kwa mwaka wa fedha 2025/26.


Taarifa hiyo imetolewa Machi 10, 2026 na Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi, wakati akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa miradi ya sekta ya nishati kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini inayoongozwa na Mwenyekiti wake, Mhe. Subira Mgalu, katika Ukumbi wa Bunge jijini Dodoma.

Mhe.Ndejembi amesema katika mwaka wa fedha 2025/26 wizara imeendelea kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo inayolenga kuimarisha uzalishaji, usafirishaji na usambazaji wa umeme nchini.

Amesema katika fedha zilizopokelewa hadi sasa, Sh. bilioni 410.04 ni fedha za ndani na Sh. bilioni 740.30 ni fedha za nje ambazo zimeendelea kusaidia utekelezaji wa miradi mbalimbali ya sekta ya nishati.

Ameongeza kuwa miradi hiyo inajumuisha upelekaji wa umeme vijijini na vitongojini, utafutaji na uendelezaji wa mafuta na gesi asilia, ujenzi wa miundombinu ya usafirishaji na uhifadhi wa bidhaa za mafuta ya petroli pamoja na kukuza matumizi ya nishati safi ya kupikia.

Kwa mujibu wa Ndejembi, katika mwaka wa fedha 2025/26 Wizara ya Nishati iliidhinishiwa kutumia jumla ya Sh trilioni 1.965, ambapo Sh trilioni 1.886 sawa na asilimia 95.97 zilitengwa kwa ajili ya miradi ya maendeleo huku Sh bilioni 79.23 sawa na asilimia 4.03 zikiwa kwa matumizi ya kawaida.

Amefafanua kuwa kati ya fedha za maendeleo zilizoidhinishwa, Sh trilioni 1.466 ni fedha za ndani na Sh bilioni 420.49 ni fedha za nje.

Ndejembi ameishukuru Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini kwa miongozo na maelekezo ambayo imekuwa ikitoa na kuchangia mafanikio katika utekelezaji wa miradi hiyo.

Amesisitiza kuwa wizara itaendelea kupokea ushauri na maoni ya kamati hiyo pamoja na kutoa ushirikiano unaostahili ili kuimarisha maendeleo ya sekta ya nishati nchini.