HABARI

SIASA

ELIMU

Recent Posts

SERIKALI YAWEKA ADHABU KALI KWA WANAOHARIBU MIUNDOMBINU MUHIMU YA TEHAMA

August 19, 2026 Add Comment
SERIKALI imeonya kuwa mtu au taasisi itakayobainika kuharibu au kutenda kosa dhidi ya Miundombinu Muhimu ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (CII) atakabiliwa na adhabu kali kwa mujibu wa Sheria ya Makosa ya Mtandao ya mwaka 2015.
MAAFISA BIASHARA WAPEWA MBINU ZA KULINDA WALAJI NA USHINDANI

MAAFISA BIASHARA WAPEWA MBINU ZA KULINDA WALAJI NA USHINDANI

August 19, 2026 Add Comment

Kaimu Mkurugenzi wa Udhibiti wa Bidhaa Bandia wa Tume ya Ushindani (FCC), Bw.Salvatory Chuwa, akiwasilisha mada  wakati wa Mkutano wa   Maafisa Biashara katika Kikao cha Tatu cha Wizara ya Viwanda na Biashara na Maafisa Biashara, kilichofanyika kwa siku mbili  jijini Dodoma.

Na Mwandishi Wetu

Tume ya Ushindani (FCC) imetoa elimu  kwa Maafisa Biashara kwa lengo la kuwaongezea uelewa kuhusu masuala ya ushindani katika biashara, udhibiti wa bidhaa bandia pamoja na umuhimu wa kumlinda mlaji dhidi ya bidhaa na huduma zisizokidhi viwango.

Semina hiyo imelenga kuwajengea uwezo Maafisa Biashara ambao wana nafasi muhimu katika kusimamia shughuli za biashara katika maeneo yao, ili waweze kutambua changamoto zinazohusiana na ushindani usio wa haki, bidhaa bandia na vitendo vinavyoweza kuwaathiri walaji.

Akitoa mada kuhusu udhibiti wa bidhaa bandia, wakati wa Mkutano wa  Maafisa Biashara nchini katika Kikao cha Tatu cha Wizara ya Viwanda na Biashara na Maafisa Biashara, kilichofanyika kwa siku mbili  jijini Dodoma.

Kaimu Mkurugenzi wa Udhibiti wa Bidhaa Bandia wa FCC, Bw. Salvatory Chuwa, ameeleza umuhimu wa kuimarisha ushirikiano kati ya FCC na Maafisa Biashara katika kukabiliana na biashara ya bidhaa bandia.

"Bidhaa bandia zina madhara makubwa kwa uchumi, wafanyabiashara wanaofuata sheria na walaji, hivyo ni muhimu kwa Maafisa Biashara kuwa na uelewa wa kutosha kuhusu namna ya kubaini na kutoa taarifa kuhusu bidhaa zinazodhaniwa kuwa bandia."amesema Bw.Chuwa

Amesisitiza kuwa udhibiti wa bidhaa bandia unahitaji ushirikiano wa karibu kati ya taasisi za Serikali, wafanyabiashara na wananchi, huku akiwataka Maafisa Biashara kutumia nafasi zao kuelimisha wafanyabiashara na walaji kuhusu madhara ya bidhaa bandia.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Tafiti, Miungano ya Makampuni na Uraghibishi wa FCC, Bi. Zaytun Kikula, ametoa mada kuhusu masuala ya ushindani, akieleza umuhimu wa kuwepo kwa mazingira ya biashara yenye ushindani wa haki kwa ajili ya kukuza uchumi na kuwapa wafanyabiashara fursa sawa katika soko.

Bi.Kikula amebainisha kuwa ushindani wenye tija husaidia kuongeza ubunifu, kuboresha ubora wa bidhaa na huduma pamoja na kuwapa walaji fursa ya kupata bidhaa bora kwa bei shindani.

Aidha, amewataka Maafisa Biashara kushirikiana na FCC katika kutoa elimu kwa wafanyabiashara kuhusu sheria za ushindani na kuhakikisha kuwa vitendo vinavyoweza kuzuia au kupotosha ushindani vinatambuliwa na kuchukuliwa hatua kwa mujibu wa sheria.

Semina hiyo ni sehemu ya jitihada za FCC za kuimarisha uelewa wa wadau kuhusu wajibu wa kulinda ushindani katika soko, kudhibiti bidhaa bandia na kuhakikisha haki za walaji zinalindwa.

FCC imeendelea kusisitiza kuwa ushirikiano wa wadau mbalimbali, hususan Maafisa Biashara, ni muhimu katika kujenga soko lenye ushindani wa haki, bidhaa salama na mazingira bora ya biashara kwa manufaa ya wafanyabiashara, walaji na uchumi kwa ujumla.

Kaimu Mkurugenzi wa Udhibiti wa Bidhaa Bandia wa Tume ya Ushindani (FCC), Bw.Salvatory Chuwa, akiwasilisha mada  wakati wa Mkutano wa   Maafisa Biashara katika Kikao cha Tatu cha Wizara ya Viwanda na Biashara na Maafisa Biashara, kilichofanyika kwa siku mbili  jijini Dodoma.

Mkurugenzi wa Tafiti, Miungano ya Makampuni na Uraghibishi wa FCC, Bi. Zaytun Kikula, akiwasilisha mada  wakati wa Mkutano wa   Maafisa Biashara katika Kikao cha Tatu cha Wizara ya Viwanda na Biashara na Maafisa Biashara, kilichofanyika kwa siku mbili  jijini Dodoma.

 Maafisa Biashara nchini wakifatilia mada mbalimbali kutoka kwa wataalamu wa Tume ya Ushindani (FCC) katika Kikao cha Tatu cha Wizara ya Viwanda na Biashara na Maafisa Biashara, kilichofanyika kwa siku mbili  jijini Dodoma.

 Maafisa Biashara nchini wakifatilia mada mbalimbali kutoka kwa wataalamu wa Tume ya Ushindani (FCC) katika Kikao cha Tatu cha Wizara ya Viwanda na Biashara na Maafisa Biashara, kilichofanyika kwa siku mbili  jijini Dodoma.

TANZANITE ROYAL GIN YASOGEZA MBELE MANYARA TANZANITE MARATHON 2026, WASANII KUTUMBUIZA

August 19, 2026 Add Comment

 

Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Queen Sendiga, amekabidhi wasanii hao T-shirt rasmi za Manyara Tanzanite Marathon, ikiwa ni sehemu ya maandalizi kuelekea tukio hilo ambalo limeendelea kupata mwitikio kutoka kwa wadau mbalimbali.
Na Mwandishi Wetu, Manyara

Manyara Tanzanite Marathon 2026 inatarajiwa kuwa na burudani ya aina yake baada ya wasanii maarufu nchini, Dully Sykes, Banana Zoro na Mr Blue, kuthibitisha kushiriki na kutumbuiza katika tukio hilo litakalofanyika Agosti 22, 2026 mjini Babati, mkoani Manyara.

Ushiriki wa wasanii hao umewezeshwa na kampuni ya Mati Super Brands Ltd kupitia kinywaji chake cha Tanzanite Royal Gin, hatua inayoongeza ushiriki wa sekta binafsi katika kufanikisha mbio hizo zinazolenga kuunganisha michezo, burudani na shughuli za kijamii.
Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Queen Sendiga, amekabidhi wasanii hao T-shirt rasmi za Manyara Tanzanite Marathon, ikiwa ni sehemu ya maandalizi kuelekea tukio hilo ambalo limeendelea kupata mwitikio kutoka kwa wadau mbalimbali.

Manyara Tanzanite Marathon 2026 imebeba kaulimbiu “Hatua Moja Okoa Maisha”, ikiwa na lengo la kukusanya Shilingi bilioni 1.5 kwa ajili ya ujenzi wa wodi maalumu ya kuwahudumia watoto njiti wanaozaliwa kabla ya wakati.
Ujio wa Dully Sykes, Banana Zoro na Mr Blue unatarajiwa kuongeza hamasa kwa wanariadha, vikundi vya jogging na wananchi watakaoshiriki au kujitokeza kushuhudia mbio hizo. Burudani hiyo pia inalenga kuwapa washiriki na watazamaji uzoefu wa kipekee huku ikihamasisha jamii kuunga mkono kampeni ya kuokoa maisha ya watoto njiti..
Mchango wa Mati Super Brands Ltd kupitia Tanzanite Royal Gin unaendelea kuonesha nafasi ya sekta binafsi katika kusaidia shughuli zenye manufaa kwa jamii. Ushiriki huo unatarajiwa kuongeza mvuto wa marathon na kuwafikia watu wengi zaidi kupitia michezo na burudani.

Kwa ujumla, Manyara Tanzanite Marathon 2026 inatarajiwa kuwa jukwaa linalounganisha michezo, burudani, utalii na uwajibikaji kwa jamii, huku kila hatua ya washiriki ikilenga kuchangia upatikanaji wa huduma bora kwa watoto njiti mkoani Manyara.

SENDIGA AZINDUA KIT YA MANYARA TANZANITE MARATHON 2026

August 19, 2026 Add Comment

 

Na Mwandishi Wetu.

Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Queen Sendiga, amezindua rasmi vifaa maalum (KIT) vitakavyotumiwa na washiriki wa Manyara Tanzanite Marathon 2026, huku idadi ya watu waliojiandikisha kushiriki mbio hizo za hisani ikifikia 2,200.

Uzinduzi wa KIT hiyo, inayojumuisha T-shirt, kofia na namba za washiriki, umefanyika Agosti 17, 2026, mjini Babati, ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya mwisho kuelekea mbio hizo zinazotarajiwa kufanyika Agosti 22, 2026.

Manyara Tanzanite Marathon 2026 imeandaliwa ikiwa na lengo la kuchangisha fedha zitakazosaidia kuboresha huduma za afya kwa watoto njiti katika Mkoa wa Manyara, hususan katika maeneo yanayohitaji miundombinu na huduma bora zaidi kwa watoto wanaozaliwa kabla ya muda.

Kaulimbiu ya mbio hizo mwaka huu ni “Hatua Moja, Okoa Maisha ya Mtoto,” inayolenga kuhamasisha wananchi, taasisi, kampuni na wadau mbalimbali kushiriki katika tukio hilo huku wakitoa mchango wa moja kwa moja katika kuboresha maisha ya watoto njiti.

Akizungumza katika uzinduzi huo, RC Sendiga amehimiza wananchi na wadau mbalimbali kuendelea kujitokeza kwa wingi kushiriki mbio hizo, akieleza kuwa mwitikio wa watu 2,200 waliojisajili hadi sasa ni ishara ya namna jamii inavyoguswa na ajenda ya kuboresha afya na ustawi wa watoto.

Idadi hiyo ya washiriki inatarajiwa kuongezeka kadri siku ya mbio inavyokaribia, huku waandaaji wakiendelea kutoa wito kwa watu ambao bado hawajajisajili kutumia fursa hiyo kushiriki katika tukio lenye lengo la kuchangia ustawi wa watoto na maendeleo ya afya mkoani Manyara.

Mbali na kushiriki katika mbio hizo, tukio hilo limeandaliwa pia kwa namna inayolenga kukuza utalii wa ndani na kuifanya Manyara kuwa sehemu ya kuvutia kwa wageni kutoka ndani na nje ya Tanzania. Washiriki watakaokuwa wamechagua kifurushi kinachojumuisha ziara ya utalii watapata fursa ya kutembelea Hifadhi ya Taifa ya Tarangire baada ya kumalizika kwa mbio.

Uhusiano kati ya mbio hizo na utalii unalenga kuwapa washiriki uzoefu mpana zaidi, huku ukiendelea kutangaza vivutio vya utalii vilivyopo mkoani Manyara na kuchochea shughuli za kiuchumi zinazotokana na utalii.

Manyara Tanzanite Marathon imeendelea kujijenga kama moja ya matukio yanayounganisha michezo, afya, utalii na uwajibikaji kwa jamii. Kupitia mbio hizo, waandaaji wanatarajia kuhamasisha watu kutoka makundi mbalimbali kushiriki katika jitihada za kuchangia huduma za afya kwa watoto njiti.

Kwa mwaka 2026, msisitizo umewekwa katika kaulimbiu “Hatua Moja, Okoa Maisha ya Mtoto,” huku fedha zitakazopatikana kupitia mbio hizo zikilenga kusaidia ujenzi na uboreshaji wa huduma kwa watoto njiti katika Mkoa wa Manyara.

Uzinduzi wa KIT hiyo umeongeza hamasa kuelekea Agosti 22, ambapo Babati inatarajiwa kuwa kitovu cha tukio hilo litakalowakutanisha washiriki, wadau wa afya, taasisi, wafanyabiashara, watalii na wananchi kwa ujumla katika hatua ya pamoja ya kuokoa maisha ya watoto njiti.

EADB Yamwaga Ufadhili wa Mil 240 Michezo ya FEASSA, Tanzania Yakamia Kufanya Vizuri.

August 19, 2026 Add Comment

 

Mashindano ya 23 ya Shirikisho la Michezo ya Shule za Sekondari Afrika Mashariki (FEASSA) yamepata msukumo mkubwa baada ya Benki ya Maendeleo ya Afrika Mashariki (EADB) kutoa udhamini wa Dola za Marekani 90,000, (takribani mil 240) katika kuunga mkono maandalizi na uendeshaji wa mashindano ya shirikisho hilo yanayoendelea mkoani Morogoro.

Mashindano hayo makubwa zaidi ya michezo ya shule katika ukanda wa Afrika Mashariki yamezikutanisha timu 413 na washiriki 5,548 kutoka nchi mbalimbali za Afrika Mashariki, zinazoshindana katika aina 51 za michezo. Mashindano hayo yanatarajiwa kuhitimishwa Agosti 22, 2026.

Akizungumza katika hafla rasmi ya ufunguzi wa mashindano hayo, Meneja wa EADB nchini Tanzania, Bw. Stephen Wambura, alisema ushirikiano wa Benki hiyo na FEASSA unaakisi dhamira ya EADB ya kuwekeza kwa vijana na kuunga mkono mipango inayochangia maendeleo endelevu katika Afrika Mashariki.

“Ingawa jukumu letu kuu ni kufadhili miradi ya maendeleo katika sekta mbalimbali muhimu za uchumi, tunatambua kuwa maendeleo endelevu hayaishii kwenye miundombinu na shughuli za biashara. Pia yanahusisha kuwawezesha watu, hususan vijana, ambao ndio msingi wa mustakabali wa ukanda wetu,” alisema Bw. Wambura.

Alisema dhamira hiyo ndiyo iliyochochea uamuzi wa EADB kuwa mdhamini mkuu wa Mashindano ya 23 ya FEASSA, kwa kutoa mchango wa Dola za Marekani 90,000 kwa ajili ya kuwezesha mashindano hayo kufanyika kwa mafanikio.

“Udhamini wa michezo ni mojawapo ya nguzo muhimu katika ajenda yetu ya Mipango ya Uwajibikaji wa Kijamii wa Kampuni (CSI), kwa sababu tunaelewa uwezo mkubwa wa michezo katika kujenga tabia, kuhamasisha mtindo bora wa maisha na kufungua fursa kwa vijana katika ukanda wetu,” aliongeza.

“Kupitia udhamini huu, hatuwekezi tu katika mashindano haya, bali pia tunawekeza katika kuwaandaa kizazi kijacho cha viongozi wa Afrika Mashariki.”

Kwa mujibu wa makubaliano ya udhamini, EADB inasaidia utengenezaji wa medali na vikombe kwa ajili ya washindi, pamoja na upatikanaji wa sare za michezo kwa washiriki watakaoshiriki katika hatua za fainali.

Ikiwa mwenyeji wa mashindano ya mwaka huu, Tanzania imetuma moja ya vikosi vikubwa zaidi, ikiwa na timu 127 na washiriki 1,704 wanaoshiriki katika michezo mbalimbali.

Katika mpira wa miguu kwa wavulana, Tanzania inawakilishwa na Shule za Sekondari Nsumba, Mbeya Day, Morogoro na Urambo Day, ambazo zitakuwa na jukumu la kutetea heshima ya nchi katika mashindano hayo.

Kwa upande wa mpira wa miguu kwa wasichana, Tanzania inawakilishwa na Shule za Sekondari Ziba, Fountain Gate na Kilombero, ambazo zinatarajiwa kutumia vyema fursa ya kucheza mbele ya mashabiki wa nyumbani katika kuwania nafasi za juu.

Tanzania pia inalenga kufanya vizuri katika mpira wa wavu. Katika upande wa wavulana, Shule za Sekondari Lumala, Kaliua na Kajunjumele ndizo zinazobeba matumaini ya Tanzania, huku Mengele, Lumala na Mwanhuzi zikiiwakilisha nchi katika mashindano ya wasichana.

Mpira wa kikapu ni miongoni mwa michezo ambayo Tanzania inalenga kutumia vizuri fursa ya kucheza nyumbani. Katika mashindano ya wavulana ya 5x5, Tanzania inawakilishwa na Shule za Sekondari Nsumba, St Jude na Juhudi.

Kwa upande wa wasichana wa 5x5, Shule za Sekondari Orkeeswa, Uru Community na Rungwa ndizo zitakazobeba matumaini ya Tanzania.

Tanzania pia inatarajia kupata matokeo mazuri katika netiboli, mchezo ambao kwa muda mrefu umekuwa miongoni mwa michezo ambayo Tanzania imekuwa ikitoa timu zenye ushindani mkubwa. Shule za Sekondari Mkolani, Vwawa na Mbeya ni miongoni mwa timu zinazotarajiwa kuongoza kinyang’anyiro cha Tanzania katika mchezo huo.

Kwa kuwakutanisha maelfu ya vijana kutoka nchi mbalimbali za Afrika Mashariki, Michezo ya FEASSA haitoi tu jukwaa la ushindani wa kimichezo, bali pia inawapa vijana fursa ya kukuza vipaji, nidhamu, mshikamano, uwezo wa kufanya kazi kwa pamoja na uongozi, huku ikichangia kuimarisha mshikamano na ushirikiano wa kikanda kupitia michezo.

Kadiri mashindano yanavyoelekea kileleni kuelekea tarehe 22 Agosti, Tanzania inalenga kutumia vyema faida ya kuwa mwenyeji ili kujinyakulia medali katika michezo mbalimbali. Kwa upande wake, udhamini wa EADB unaendelea kusisitiza dhamira ya Benki hiyo ya kuunga mkono mipango inayowekeza katika vijana na kuchangia maendeleo ya muda mrefu ya Afrika Mashariki.

Meneja wa Benki ya Maendeleo ya Afrika Mashariki (EADB), Bw. Stephen Wambura (kulia), akikabidhi rasmi sare za michezo kwa Rais wa Shirikisho la Michezo ya Shule za Sekondari Afrika Mashariki (FEASSA), Bw. Justus Mugisha, kwa ajili ya kutumiwa na timu zinazoshiriki katika hatua za fainali za Michezo ya FEASSA zinazoendelea Morogoro, Tanzania. Sare hizo ni sehemu ya udhamini wa Dola za Marekani 90,000 ( takribani mil 240) kutoka EADB kwa ajili ya kufanikisha toleo la 23 la mashindano hayo ya michezo ya shule katika ukanda wa Afrika Mashariki, ambayo yamewakutanisha timu 413 na washiriki 5,548 kutoka nchi mbalimbali za Afrika Mashariki.



TANZANITE ROYAL GIN YAZIDI KUPAMBA MANYARA TANZANITE MARATHON 2026

Kajunason August 18, 2026 Add Comment

 

Na Mwandishi Wetu, Manyara

Manyara Tanzanite Marathon 2026 inatarajiwa kuwa na burudani ya aina yake baada ya wasanii maarufu nchini, Dully Sykes, Banana Zoro na Mr Blue, kuthibitisha kushiriki na kutumbuiza katika tukio hilo litakalofanyika Agosti 22, 2026 mjini Babati, mkoani Manyara.

Ushiriki wa wasanii hao umewezeshwa na kampuni ya Mati Super Brands Ltd kupitia kinywaji chake cha Tanzanite Royal Gin, hatua inayoongeza ushiriki wa sekta binafsi katika kufanikisha mbio hizo zinazolenga kuunganisha michezo, burudani na shughuli za kijamii.
Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Queen Sendiga, amekabidhi wasanii hao T-shirt rasmi za Manyara Tanzanite Marathon, ikiwa ni sehemu ya maandalizi kuelekea tukio hilo ambalo limeendelea kupata mwitikio kutoka kwa wadau mbalimbali.

Manyara Tanzanite Marathon 2026 imebeba kaulimbiu “Hatua Moja Okoa Maisha”, ikiwa na lengo la kukusanya Shilingi bilioni 1.5 kwa ajili ya ujenzi wa wodi maalumu ya kuwahudumia watoto njiti wanaozaliwa kabla ya wakati.
Ujio wa Dully Sykes, Banana Zoro na Mr Blue unatarajiwa kuongeza hamasa kwa wanariadha, vikundi vya jogging na wananchi watakaoshiriki au kujitokeza kushuhudia mbio hizo. Burudani hiyo pia inalenga kuwapa washiriki na watazamaji uzoefu wa kipekee huku ikihamasisha jamii kuunga mkono kampeni ya kuokoa maisha ya watoto njiti..
Mchango wa Mati Super Brands Ltd kupitia Tanzanite Royal Gin unaendelea kuonesha nafasi ya sekta binafsi katika kusaidia shughuli zenye manufaa kwa jamii. Ushiriki huo unatarajiwa kuongeza mvuto wa marathon na kuwafikia watu wengi zaidi kupitia michezo na burudani.

Kwa ujumla, Manyara Tanzanite Marathon 2026 inatarajiwa kuwa jukwaa linalounganisha michezo, burudani, utalii na uwajibikaji kwa jamii, huku kila hatua ya washiriki ikilenga kuchangia upatikanaji wa huduma bora kwa watoto njiti mkoani Manyara.

MWENGE WA UHURU WAZINDUA TAWI LA CRDB MAGANZO, SHINYANGA

August 18, 2026 Add Comment

 

Mkurugenzi wa Mikopo wa Benki ya CRDB, Xavery Makwi, akitoa taarifa kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dkt. Abdulmajid Mussa Nsekela, wakati wa uzinduzi wa Tawi la CRDB Maganzo, Wilaya ya Kishapu mkoani Shinyanga, Agosti 18, 2026.
Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa 2026, Wazo Michael Mwang’onda (kulia) baada ya kufungua rasmi Tawi la Benki ya CRDB Maganzo, Wilaya ya Kishapu mkoani Shinyanga, Agosti 18, 2026.
Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa 2026, Wazo Michael Mwang’onda akikata keki wakati akifungua rasmi Tawi la Benki ya CRDB Maganzo, Wilaya ya Kishapu mkoani Shinyanga, Agosti 18, 2026.
Mwenge wa Uhuru Kitaifa 2026 ukiwa katika Benki ya CRDB Maganzo, Wilaya ya Kishapu mkoani Shinyanga, wakati wa uzinduzi wa tawi hilo, Agosti 18, 2026.
Wafanyakazi wa Benki ya CRDB wakifurahia wakati wa uzinduzi wa Tawi la CRDB Maganzo, Wilaya ya Kishapu mkoani Shinyanga.
Mwenge wa Uhuru Kitaifa 2026 ukiondoka katika Tawi la Benki ya CRDB Maganzo, Wilaya ya Kishapu mkoani Shinyanga, baada ya uzinduzi wa tawi hilo, Agosti 18, 2026.

Na Kadama Malunde & Elizabeth Cosmas Shinyanga

Mwenge wa Uhuru Kitaifa 2026 umezindua rasmi Tawi la Benki ya CRDB Maganzo, Wilaya ya Kishapu mkoani Shinyanga, huku benki hiyo ikiahidi kuongeza fursa za huduma za kifedha kwa wakulima, wafugaji, wafanyabiashara, wastaafu, vijana na wananchi wengine katika eneo hilo.