HABARI

SIASA

ELIMU

Recent Posts

NAIBU KATIBU MKUU CCM BARA AGGREY MWANRI AWA MGENI RASMI MKUTANO WA HADHARA UBUNGO

August 15, 2026 Add Comment

Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara, Ndugu Aggrey Mwanri (MCC), leo Agosti 15, 2026, amekuwa Mgeni Rasmi katika Mkutano wa Hadhara wa Jimbo la Ubungo, ulioandaliwa na Mbunge wa Jimbo hilo, Prof. Kitila Mkumbo, ambaye pia ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji.


Kabla ya kushiriki mkutano huo, Ndugu Mwanri alipokewa katika Ofisi za CCM Mkoa wa Dar es Salaam na Sekretarieti ya CCM Mkoa, chini ya Katibu wa CCM Mkoa, Ndugu Mkandawire.

Aidha, alipokea taarifa fupi kuhusu utendaji wa Chama katika Mkoa huo na kuwashukuru viongozi wa CCM Mkoa wa Dar es Salaam kwa usimamizi mzuri wa Chama na Serikali.

Akizungumza katika mkutano huo, Ndugu Mwanri amesisitiza umuhimu wa Wabunge, Madiwani pamoja na Wenyeviti wa Serikali za Mitaa kufanya mikutano ya hadhara mara kwa mara ili kuwapa wananchi mrejesho kuhusu utekelezaji wa ahadi zilizotolewa na CCM wakati wa Uchaguzi.

Aidha, amewasihi wananchi kumuunga mkono Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, akieleza kuwa Serikali imeendelea kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo katika Mkoa wa Dar es Salaam na maeneo mengine nchini.

Kwa upande wake, Prof. Kitila Mkumbo aliwasilisha taarifa ya utekelezaji wa Ilani ya CCM mbele ya wananchi wa Jimbo la Ubungo, akieleza hatua zilizochukuliwa katika kuboresha miundombinu, hususan sekta ya barabara.

Prof. Kitila amesema ataendelea kushirikiana na Chama Cha Mapinduzi na Serikali katika kuhakikisha wananchi wa Ubungo wanaendelea kupata huduma na maendeleo yanayostahili.




KAZI NA UTU, TUNASONGA MBELE.

KAMATI YA BUNGE YAISHAURI SERIKALI KUIONGEZA WATAALAM OSHA

August 15, 2026 Add Comment
Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ustawi na Maendeleo ya Jamii, Mhe. Hawa Chakoma, akifanya majumuisho ya michango ya Wajumbe wa Kamati katika kikao cha Kamati hiyo kilicholenga kupitia taarifa ya utekelezaji wa Sheria ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi, Sura Namba 297, Toleo ya 2023 katika mwakawa fedha 2025/2026.

RAIS DKT.SAMIA SULUHU HASSAN KUZINDUA RASMI MRADI WA JNHPP AGOSTI 22

August 15, 2026 Add Comment

 

*******

Waziri wa Nishati, Deogratius Ndejembi amesema kuwa, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt.Samia Suluhu Hassan anatarajiwa kuzindua rasmi Kituo cha Kuzalisha Umeme cha Julius Nyerere (JNHPP) chenye uwezo wa kuzalisha Megawati 2,115, tarehe 22 Agosti 2026, katika eneo la mradi lililopo Rufiji, Mkoa wa Pwani.

Amesema hayo tarehe 15 Agosti, 2026 jijini Dar es Salaam  katika ofisi ndogo za Wizara ya Nishati wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu uzinduzi huo utakaohudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Serikali, wageni kutoka ndani na nje ya nchi, wananchi na wadau wa maendeleo.

" Uzinduzi huu wa mradi wa umeme wa  Julius Nyerere ni tukio la kihistoria na hatua muhimu katika safari ya Tanzania ya kujenga mfumo wa nishati ya uhakika nchini, sambamba na kuchochea shughuli za uzalishaji, uwekezaji na ukuaji wa uchumi, huu ni mradi mkubwa zaidi wa kuzalisha umeme kuwahi kutekelezwa nchini kwa kutumia fedha za ndani za Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ukiwa na uwekezaji wa takribani Shilingi trilioni 7.452." Amesema Mhe. Ndejembi

Akifafanua kuhusu mradi huo, amesema JNHPP imeendelea kuongeza kiwango cha umeme kinachoingia katika Gridi ya Taifa na hivyo kusaidia kupunguza changamoto za upungufu wa uzalishaji zilizokuwa zikichangia mgao wa umeme nchini, 

ambapo hadi tarehe 31 Mei 2026, kituo hicho kilikuwa kimezalisha takribani asilimia 44.9  ya umeme wote uliozalishwa na kuingia katika Gridi ya Taifa katika kipindi cha mwaka mmoja

Hivyo kituo hicho kimekuwa kikichangia takribani nusu ya umeme wote unaotumika nchini Tanzania.

Kuhusu gharama za mradi huo, Mhe. Ndejembi amesema fedha iliyotumika kujenga mradi huo ni takriban dola za Marekani Bilioni 3.35 sawa na Shilingi za Tanzania Trilioni 7.452 ambapo pamoja na mradi huo kukusudiwa kuzalisha umeme, utasaidia pia kwenye kudhibiti mafuriko katika mto Rufiji, kilimo cha umwagiliaji, utalii na matumizi ya binadamu.

Ameeleza kuwa ujenzi wa mradi wa JNHPP ulianza Juni 2019 na kukamilika Machi 2025 ambapo uwezo wa Bwawa la kutunza maji ni Mita za ujazo Bilioni 33 (Takribani mara 10 ya Bwawa la Mtera). Bwawa hili ni ziwa la kujenga na linashika nafasi ya nne kwa ukubwa katika maziwa yaliyoko nchini (Baada ya Ziwa Victoria, Ziwa Tanganyika na Ziwa Nyasa) huku kituo cha kuzalisha umeme cha JNHPP kinashika nafasi ya nne kwa ukubwa katika bara la Afrika.

Ameongeza kuwa uwekezaji wa JNHPP unaendana moja kwa moja na malengo ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 ambapo mradi huo  ni sehemu ya hatua zinazoendelea kuchukuliwa na Serikali za kuongeza uzalishaji wa umeme, kuimarisha Gridi ya Taifa na kuweka mazingira bora kwa uchumi kukua kwa kasi.

Katika mkutano huo Waziri Ndejembi amewaalika  Watanzania wote kufuatilia na kushiriki katika tukio hilo ambalo ni kielelezo cha mafanikio  makubwa katika historia ya sekta ya nishati na maendeleo ya Taifa.






DG CHALAMILA: HATUTAMUANGUSHA RAIS DKT .SAMIA SULUHU VITA DHIDI YA RUSHWA

August 15, 2026 Add Comment

 




Na Oscar Assenga, Kilindi

MKURUGENZI Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), Crispian Chalamila amemuahidi Rais Samia Suluhu Hassan kuwa taasisi hiyo itaendelea kufanya kazi kwa bidii na weledi katika kuhakikisha vita dhidi ya rushwa nchini vinafanikiwa.

Chalamila alisema hayo  wakati akizindua jengo jipya la ofisi ya TAKUKURU Wilaya ya Kilindi, mkoani Tanga, akisema Serikali imeendelea kuiwezesha taasisi hiyo kwa rasilimali watu, fedha na vitendea kazi ili kuimarisha mapambano dhidi ya rushwa.

Alisema uwekezaji huo ni ishara ya dhamira ya Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Dkt.Samia Suluhu katika kuhakikisha TAKUKURU inakuwa na uwezo wa kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi.

“Kwa niaba ya menejimenti ya TAKUKURU, nitoe shukrani za dhati kwa Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuiwezesha taasisi hii kwa rasilimali watu, vitendea kazi na fedha,” alisema.

Chalamila alisema uwezeshaji huo umewezesha taasisi kujenga ofisi katika mikoa na wilaya mbalimbali, jambo linalowapa watumishi mazingira bora ya kufanyia kazi na wananchi kupata huduma kwa mazingira rafiki.


Ofisi 93 kufikia 2027

Chalamila alisema TAKUKURU imeweka mkakati wa kutenga bajeti kila mwaka kwa ajili ya ujenzi wa ofisi zake, huku akieleza kuwa taasisi hiyo ina ofisi 145 katika mikoa yote 26, wilaya 111 na vituo maalumu sita.

Alisema kati ya ofisi hizo, majengo 70 yanamilikiwa na TAKUKURU na yanapatikana katika mikoa 23, wilaya 46 na kituo maalumu kimoja.

“Majengo yanayoendelea kujengwa katika mwaka wa fedha 2025/2026 na 2026/2027 ni 23, ambayo yanajumuisha ofisi tatu za mikoa na ofisi 20 za wilaya,” alisema.

Alisema kukamilika kwa miradi hiyo kutafanya hadi mwaka 2027 TAKUKURU kuwa na majengo 93 yanayomilikiwa na taasisi hiyo.

Hata hivyo, alisema bado kuna ofisi 52 ambazo hazijafikiwa na mpango huo wa ujenzi, zikiwa katika mikoa miwili, wilaya 45 na vituo maalumu vitano.

Kwa upande wa jengo la TAKUKURU Kilindi, Chalamila alisema limegharimu Sh450.7 milioni hadi kukamilika, ikiwa ni ongezeko la Sh3.1 milioni, sawa na asilimia 0.7 ya bajeti ya awali.

Alisema ongezeko hilo lilitokana na changamoto mbalimbali zilizojitokeza wakati wa utekelezaji wa mradi.

Aliwapongeza wataalamu wa TAKUKURU, Mkoa wa Tanga na Wilaya ya Kilindi kwa kuhakikisha ujenzi wa jengo hilo unakamilika kwa wakati.

Pia aliwataka watumishi wa TAKUKURU katika wilaya ya  Kilindi na maeneo mengine yenye majengo mapya kuyatunza pamoja na vitendea kazi walivyopewa ili yaweze kutumika kwa muda mrefu.

“Serikali imewawezesha kwa kiwango kikubwa. Hilo ni deni ambalo tunapaswa kulilipa kwa kufanya kazi kwa bidii na weledi zaidi ili dhamira ya Serikali ya kuitokomeza rushwa nchini itimie,” alisema.

DC aomba jenereta

Mkuu wa Wilaya ya Kilindi, Hashim Mgandilwa, aliishukuru Serikali kwa kuendelea kuziwezesha taasisi zake kuwa na miundombinu bora inayorahisisha utoaji wa huduma kwa wananchi.

Mgandilwa alisema ujenzi wa jengo hilo ni hatua muhimu kwa wilaya hiyo, ambayo tangu kuanzishwa kwake mwaka 2002 imekuwa ikikabiliwa na changamoto ya upungufu wa miundombinu ya ofisi.

Hata hivyo, aliomba TAKUKURU kuangalia uwezekano wa kuiwezesha ofisi hiyo kupata jenereta kutokana na changamoto ya kukatika kwa umeme katika eneo hilo.

“Jengo ni zuri, lakini haitakuwa na maana kama mwananchi akija kupata huduma anaambiwa umeme umekatika. Tunaomba muone namna ya kupata jenereta ili huduma ziendelee muda wote,” alisema.

Alisema Serikali tayari imeweka mpango wa kuimarisha umeme katika eneo hilo na imetenga Sh98 milioni kwa ajili ya ujenzi wa kituo kidogo cha kupoza umeme.

TAKUKURU Kilindi yapata ofisi baada ya miaka 20

Kwa upande wake, Kamanda wa TAKUKURU Mkoa wa Tanga, Ramadhan Ndwatah, alisema kabla ya kupata jengo hilo, taasisi hiyo ilifanya kazi katika majengo ya kupanga kwa takribani miaka 20.

Alisema kuanzia mwaka 2005 hadi 2010 walikuwa katika majengo ya kupanga Kata ya Songe, kabla ya kuhamia Kata ya Bokwa, Kijiji cha Legeza Mwendo, ambako walikaa hadi mwaka 2026.

Ndwatah alisema hali hiyo ilisababisha changamoto mbalimbali, ikiwamo majengo kutokidhi mahitaji ya kisasa ya ofisi, changamoto za mawasiliano na ulazima wa kufanya ukarabati mara kwa mara.

Alisema pia kuwepo kwa ofisi katika majengo ya makazi ya watu kulikuwa kunawafanya baadhi ya wananchi kukosa uhuru wa kufika kutoa taarifa za vitendo vya rushwa kwa utulivu.

“Tunamshukuru Mkurugenzi Mkuu kwa uamuzi wa kutujengea jengo hili la kisasa. Litasaidia wananchi wa Kilindi kufika kwa uhuru na kupata huduma katika mazingira bora,” alisema.

Jengo hilo jipya linatarajiwa kuongeza ufanisi wa TAKUKURU Wilaya ya Kilindi katika kutekeleza majukumu yake, ikiwamo kupokea taarifa na malalamiko ya wananchi kuhusu vitendo vya rushwa.

TRAMEPRO: VIJANA WALINDE MAZINGIRA, WAJENGE UCHUMI WA KIJANI

Kajunason August 15, 2026 Add Comment

 

Na Mwandishi Wetu

Dar es Salaam. Shirika la Dawa Asilia na Ulinzi wa Mazingira Tanzania (TRAMEPRO) limewataka vijana kutumia ubunifu, sayansi na teknolojia kama nyenzo za kujenga uchumi, kuzalisha ajira na kulinda mazingira, likisisitiza kuwa wao ndiyo nguvu ya mabadiliko ya sasa na si viongozi wa kesho pekee.

Wito huo umetolewa na Katibu Mkuu wa TRAMEPRO, Boniventura Ferdinand Mwalongo, katika maadhimisho ya Siku ya Vijana Duniani yaliyofanyika Agosti 15, 2026. Amesema Tanzania ina takribani vijana milioni 20.6 wenye umri wa miaka 15 hadi 35, sawa na asilimia 34.4 ya wananchi wote kwa mujibu wa Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2022, hivyo ni muhimu kuwawezesha kushiriki kikamilifu katika maendeleo ya taifa.

Mwalongo amesema dunia inaingia kwa kasi katika matumizi ya akili mnemba (AI), teknolojia za kidijitali, bioteknolojia na nishati jadidifu, hali inayowalazimu vijana kujikita katika maarifa, utafiti na ubunifu ili wawe wabunifu wa teknolojia badala ya kuwa watumiaji pekee wa teknolojia zinazobuniwa na wengine.

Ameeleza kuwa licha ya changamoto zinazowakabili vijana, zikiwemo ukosefu wa ajira, mitaji, ujuzi unaoendana na mahitaji ya soko, taarifa potofu na athari za mabadiliko ya tabianchi, bado wana nafasi kubwa ya kubadilisha changamoto hizo kuwa fursa kupitia ujasiriamali, matumizi sahihi ya teknolojia na uwekezaji katika sekta mbalimbali za uzalishaji.

Kwa mujibu wa TRAMEPRO, ulinzi wa mazingira unapaswa kuwa sehemu ya maisha ya kila kijana kwani maendeleo endelevu hayawezi kupatikana bila kuhifadhi udongo, maji, misitu, hewa na bioanuwai. Shirika hilo limesisitiza kuwa vijana wanapaswa kuwa walinzi wa rasilimali za asili huku wakizitumia kwa busara ili kunufaisha kizazi cha sasa na kijacho.

Aidha, Mwalongo amesema Tanzania ina utajiri mkubwa wa mimea tiba na maarifa ya jadi ambayo yanaweza kuwa chanzo cha ajira, utafiti na uchumi wa kijani iwapo yataendelezwa kwa kuzingatia misingi ya kisayansi, ubora na sheria. Amewahimiza vijana kujitokeza kuwekeza katika kilimo cha mimea tiba, uchakataji, uzalishaji wa bidhaa zenye thamani, teknolojia na biashara zinazohusiana na sekta hiyo.

TRAMEPRO pia imeiomba Serikali na wadau wa maendeleo kuendelea kuwekeza katika elimu, tafiti, vituo vya ubunifu, mitaji, viwanda na masoko ili kuwajengea vijana uwezo wa kujitegemea na kuzalisha ajira. Shirika hilo limehimiza familia, viongozi wa dini, wazee wa mila, mashirika ya kiraia na sekta binafsi kushiriki katika malezi na uwezeshaji wa vijana wenye maadili, maarifa na uwezo wa kushindana katika uchumi wa dunia.

Akihitimisha ujumbe wake, Mwalongo amewataka vijana kutambuliwa kwa kazi, ubunifu, uadilifu na mchango wao katika maendeleo ya taifa badala ya idadi yao, akisisitiza kuwa uwekezaji kwa vijana wa leo ndiyo msingi wa kujenga Tanzania na Afrika yenye uchumi shindani, mazingira salama na maendeleo endelevu.

DKT.SAMIA SULUHU HASSAN KUZINDUA RASMI MRADI WA JNHPP AGOSTI 22

August 15, 2026 Add Comment



Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi amesema kuwa, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt.Samia Suluhu Hassan anatarajiwa kuzindua rasmi Kituo cha Kuzalisha Umeme cha Julius Nyerere (JNHPP) chenye uwezo wa kuzalisha Megawati 2,115, tarehe 22 Agosti 2026, katika eneo la mradi lililopo Rufiji, Mkoa wa Pwani.


Amesema hayo tarehe 15 Agosti, 2026 jijini Dar es Salaam katika ofisi ndogo za Wizara ya Nishati wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu uzinduzi huo utakaohudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Serikali, wageni kutoka ndani na nje ya nchi, wananchi na wadau wa maendeleo.


" Uzinduzi huu wa mradi wa umeme wa Julius Nyerere ni tukio la kihistoria na hatua muhimu katika safari ya Tanzania ya kujenga mfumo wa nishati ya uhakika nchini, sambamba na kuchochea shughuli za uzalishaji, uwekezaji na ukuaji wa uchumi, huu ni mradi mkubwa zaidi wa kuzalisha umeme kuwahi kutekelezwa nchini kwa kutumia fedha za ndani za Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ukiwa na uwekezaji wa takribani Shilingi trilioni 7.452." Amesema Mhe. Ndejembi


Akifafanua kuhusu mradi huo, amesema JNHPP imeendelea kuongeza kiwango cha umeme kinachoingia katika Gridi ya Taifa na hivyo kusaidia kupunguza changamoto za upungufu wa uzalishaji zilizokuwa zikichangia mgao wa umeme nchini,
ambapo hadi tarehe 31 Mei 2026, kituo hicho kilikuwa kimezalisha takribani asilimia 44.9 ya umeme wote uliozalishwa na kuingia katika Gridi ya Taifa katika kipindi cha mwaka mmoja
Hivyo kituo hicho kimekuwa kikichangia takribani nusu ya umeme wote unaotumika nchini Tanzania.


Kuhusu gharama za mradi huo, Mhe. Ndejembi amesema fedha iliyotumika kujenga mradi huo ni takriban dola za Marekani Bilioni 3.35 sawa na Shilingi za Tanzania Trilioni 7.452 ambapo pamoja na mradi huo kukusudiwa kuzalisha umeme, utasaidia pia kwenye kudhibiti mafuriko katika mto Rufiji, kilimo cha umwagiliaji, utalii na matumizi ya binadamu.


Ameeleza kuwa ujenzi wa mradi wa JNHPP ulianza Juni 2019 na kukamilika Machi 2025 ambapo uwezo wa Bwawa la kutunza maji ni Mita za ujazo Bilioni 33 (Takribani mara 10 ya Bwawa la Mtera). Bwawa hili ni ziwa la kujenga na linashika nafasi ya nne kwa ukubwa katika maziwa yaliyoko nchini (Baada ya Ziwa Victoria, Ziwa Tanganyika na Ziwa Nyasa) huku kituo cha kuzalisha umeme cha JNHPP kinashika nafasi ya nne kwa ukubwa katika bara la Afrika.


Ameongeza kuwa uwekezaji wa JNHPP unaendana moja kwa moja na malengo ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 ambapo mradi huo ni sehemu ya hatua zinazoendelea kuchukuliwa na Serikali za kuongeza uzalishaji wa umeme, kuimarisha Gridi ya Taifa na kuweka mazingira bora kwa uchumi kukua kwa kasi.


Katika mkutano huo Waziri Ndejembi amewaalika Watanzania wote kufuatilia na kushiriki katika tukio hilo ambalo ni kielelezo cha mafanikio makubwa katika historia ya sekta ya nishati na maendeleo ya Taifa.

SERIKALI YAWEKA MKAKATI WA KUPUNGUZA MUDA WA MELI ZA MAFUTA BANDARINI

August 15, 2026 Add Comment




DAR ES SALAAM. 


Serikali imeweka mkakati wa kupunguza muda ambao meli za mafuta hutumia bandarini, ikiwa ni sehemu ya juhudi za kuongeza ufanisi katika upokeaji, uhifadhi na usambazaji wa bidhaa za mafuta nchini.


Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati, anayeshughulikia Mafuta na Gesi Dkt. James Mataragio, amesema hayo wakati wa ziara ya kukagua miundombinu ya mafuta katika eneo la Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) na Tanzania International Petroleum Reserves Limited (TIPER), Leo Augosti 14,2026 Jijini Dar es Salaam.

Dkt. Mataragio amesema Serikali inalenga kuhakikisha meli zinazowasili nchini zinapata huduma kwa wakati, zinashusha mafuta kwa ufanisi na kuondoka bandarini bila ucheleweshaji usio wa lazima.

“Ni matarajio ya Serikali kuona meli zikifika, zinashusha mafuta na kuondoka. Kila taasisi inapaswa kufahamu jukumu lake na kujipanga ipasavyo,” amesema.


Ameeleza kuwa moja ya changamoto zinazochangia meli kukaa bandarini kwa muda mrefu ni kasi ndogo ya upokeaji na uondoshwaji wa mafuta katika baadhi ya maghala binafsi. Hali hiyo husababisha meli kusubiri na kuongeza msongamano bandarini.

Kutokana na changamoto hiyo, Dkt. Mataragio ameutaka Wakala wa Uagizaji wa Mafuta kwa Pamoja (PBPA) kuimarisha usimamizi wa wamiliki wa maghala binafsi na kuhakikisha wanaweka miundombinu inayokidhi mahitaji ya uendeshaji.


Amesema wamiliki wa maghala wanapaswa kuboresha pampu na vifaa vingine vinavyotumika kupokea mafuta, hasa vinapokuwa vimechakaa au havina uwezo unaohitajika.



Kwa mujibu wa Dkt. Mataragio, ucheleweshaji wa meli bandarini huongeza gharama za uendeshaji, zikiwemo gharama za meli kusubiri, ambazo hatimaye zinaweza kuathiri bei ya mafuta kwa mwananchi.


Kwa upande wake, Mtendaji Mkuu wa PBPA, Bw. Erasto Simon, amesema taasisi hiyo itakutana na wadau muhimu katika sekta ya mafuta, wakiwemo kampuni za uuzaji wa mafuta (OMCs) na TPA, kwa ajili ya kupitia na kuboresha Mwongozo wa Taratibu za Uendeshaji (Standard Operating Procedure Manual).


Amesema mapitio hayo yanalenga kuweka wazi majukumu, muda wa utekelezaji na uwajibikaji wa kila mdau katika mchakato wa upokeaji na uhamishaji wa mafuta.


Hatua hiyo inatarajiwa kuimarisha uratibu kati ya meli na maghala ya kupokea mafuta, kupunguza muda wa meli kukaa bandarini na kudhibiti gharama zinazotokana na ucheleweshaji.


Katika ziara hiyo, Dkt. Mataragio aliambatana na Kamishna wa Mafuta kutoka Wizara ya Nishati, Bw. Goodluck Shirima; Mtendaji Mkuu wa PBPA, Bw. Erasto Simon; Meneja wa Bandari ya Dar es Salaam, Bw. Abed Gallus Abed; pamoja, Meneja wa Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) Kanda ya Mashariki, Mhandisi Lorivii Long’idu na wataalam kutoka Wizara ya Nishati.

TAASISI ZAIDI YA 300 KUSHIRIKI WIKI YA ELIMU, UBUNIFU NA UJUZI TANGA

August 14, 2026 Add Comment
Wananchi wa Mkoa wa Tanga na mikoa jirani wanahamasishwa kushiriki katika Wiki ya Kitaifa ya Elimu, Ubunifu na Ujuzi, itakayofanyika kuanzia tarehe 15 - 24 Agosti 2026 katika viwanja vya Shule ya Sekondari Usagara, jijini Tanga, ili kujifunza, kubadilishana maarifa na kutumia fursa mbalimbali za elimu, ujuzi na ubunifu.

ORYX GAS ZANZIBAR YANOGESHA TAMASHA LA KIZIMKAZI,YAKABIDHI MITUNGI YA GESI 200

August 14, 2026 Add Comment
Na Mwandishi Wetu ,Zanzibar

ORYX Gas Zanzibar imeeleza hatua mbalimbali inazochukua kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia na katika Tamasha la Kizimkazi kampuni hiyo imetoa mitungi ya gesi 200 huku mkakati kwasasa ni kutoa majenerata yanatotumia gesi ya LPG katika hoteli na viwanda visiwani Zanzibar.
TANGA YAWAITA WANANCHI KUTUMIA FURSA ZA ELIMU, UJUZI NA TEKNOLOJIA

TANGA YAWAITA WANANCHI KUTUMIA FURSA ZA ELIMU, UJUZI NA TEKNOLOJIA

August 14, 2026 Add Comment

Wananchi wa Mkoa wa Tanga na mikoa jirani wanahamasishwa kushiriki katika Wiki ya Kitaifa ya Elimu, Ubunifu na Ujuzi, itakayofanyika kuanzia tarehe 15 - 24 Agosti 2026 katika viwanja vya Shule ya Sekondari Usagara, jijini Tanga, ili kujifunza, kubadilishana maarifa na kutumia fursa mbalimbali za elimu, ujuzi na ubunifu.

Akizungumza Agosti 14, 2026, Katibu Tawala wa Mkoa wa Tanga, Rashid Kassim Mchata, amesema maonyesho hayo yatashirikisha taasisi zaidi ya 300 pamoja na wadau wa sekta ya elimu, sayansi na teknolojia. Aidha, kutakuwa na mashindano ya ubunifu na ujuzi katika fani mbalimbali ikiwemo ushonaji, ususi, umeme na mengineyo, ambapo washindi wa kitaifa watapata nafasi ya kushiriki mashindano ya kimataifa.

Mchata ameongeza kuwa wadhamini mbalimbali wakiwemo mabenki wamejitokeza kudhamini miradi ya ubunifu na kuunga mkono wajasiriamali chipukizi.

Kwa upande wake, Prof. Ladislaus Mnyone, Mkurugenzi wa Idara ya Sayansi, Teknolojia na Ubunifu, alisema lengo kuu la wiki hiyo ni kuwaleta pamoja wadau kujadili na kuweka mikakati ya pamoja kuhusu elimu, ujuzi na ubunifu.

Amebainisha kuwa matukio makuu yatakuwa ni maonesho ya teknolojia yanayoonyesha mchango wa sayansi katika sekta mbalimbali, pamoja na kongamano la elimu na ubunifu litakalojadili utekelezaji wa Dira 2050.

Prof. Mnyone amefafanua kuwa kongamano hilo litaangazia nyenzo tano kuu: utafiti na maendeleo, sayansi na ubunifu, teknolojia za kidijitali, nishati, na usafirishaji funganishi.

Kupitia mijadala na maonesho hayo, Wizara inalenga kufanikisha malengo ya taifa ikiwemo kufikia uchumi wa dola trilioni 1 ifikapo mwaka 2050, kipato cha wastani cha mtu mmoja kati ya Dola za Marekani 7,000 - 12,000, na ajira zenye staha kwa angalau asilimia 50 ya Watanzania.

WATUMISHI WA WIZARA WATEMBELEA OFISI ZA UBALOZI WA TANZANIA NCHINI INDIA

August 14, 2026 Add Comment
Watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wanaohudhuria mafunzo maalum ya diplomasia nchini India wametembelea Ofisi za Ubalozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania jijini New Delhi.

KIRITA AAGIZA KASI MRADI WA MAJI KAHAMA–USHETU: “TUTEMBEE NA MAJI”

August 13, 2026 Add Comment

 

Mkurugenzi Mkuu wa RUWASA, Mhandisi Wolta Kirita, akizungumza katika moja ya matanki ya maji, Kata ya Ulowa, Halmashauri ya Ushetu.  Picha na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Mkurugenzi Mkuu wa RUWASA, Mhandisi Wolta Kirita, akiwa ameambatana na wataalamu mbalimbali katika moja ya matanki ya maji, Kata ya Ulowa, Halmashauri ya Ushetu.
Mkurugenzi Mkuu wa RUWASA, Mhandisi Wolta Kirita, akiwa ameambatana na wataalamu mbalimbali katika moja ya matanki ya maji wakati wa ziara yake ya kukagua utekelezaji wa mradi wa maji Kahama - Ushetu. 
Meneja Mradi kutoka RUWASA, John Msengi akieleza kuhusu utekelezaji wa mradi wa maji Kahama–Ushetu.
Muonekano wa sehemu ya mabomba katika mradi wa maji Kahama–Ushetu
Mkurugenzi Mkuu wa RUWASA, Mhandisi Wolta Kirita, akizungumza wakati wa ziara katika Mradi wa Maji Kahama - Ushetu.

Na Kadama Malunde – Malunde 1 Blog

Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA), Mhandisi Wolta Kirita, amewataka Mameneja wa RUWASA ngazi ya mikoa na wilaya kuhakikisha utekelezaji wa miradi ya maji unaenda sambamba na upatikanaji wa huduma, akisisitiza falsafa ya “kutembea na maji” kuwa kipaumbele katika utekelezaji wa miradi hiyo.