HABARI

SIASA

ELIMU

Recent Posts

NEMC YATAKA UBUNIFU WA MAZINGIRA KUGEUZWA KUWA FURSA

September 16, 2026 Add Comment

NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

BARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) limetoa wito wa kujenga mifumo itakayowezesha ubunifu na fursa za mazingira kugeuzwa kuwa miradi inayotekelezeka, inayoweza kufadhiliwa na kukua.

WADAU WA USAFIRISHAJI WAKUTANA KUIMARISHA BIASHARA YA KIKANDA

September 16, 2026 Add Comment

 

Kigoma, Septemba 16, 2026

Wadau mbalimbali wa sekta ya Uchukuzi na Usafirishaji wamekutana mjini Kigoma katika kikao cha siku moja kilichoandaliwa na Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA), kwa lengo la kujadili fursa na changamoto zinazohusiana na usafirishaji wa mizigo na namna ya kuimarisha biashara katika ukanda wa Magharibi na Maziwa Makuu.

Kikao hicho kimehudhuriwa na wadau mbalimbali kutoka katika sekta ya Uchukuzi na Usafirishaji, ambapo Mgeni Rasmi, Mkuu wa Wilaya ya Kigoma, Dkt. Rashid Chuachua, kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, amesisitiza umuhimu wa ushirikiano miongoni mwa wadau katika kuimarisha ufanisi wa usafirishaji na kukuza biashara ya kikanda.

Kwa upande wa TPA, Naibu Mkurugenzi Mkuu, Mha. Dkt. Baraka Mdima, ameshiriki kikao hicho kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa TPA, akiwakilisha uongozi wa Mamlaka katika majadiliano yaliyolenga kubaini maeneo ya kimkakati ya kuboresha huduma na kuongeza ufanisi wa usafirishaji kupitia Bandari ya Kigoma.

Majadiliano katika kikao hicho yamejikita katika kubaini changamoto zinazokwamisha mtiririko wa mizigo, zikiwemo vikwazo visivyo vya kiforodha, ucheleweshaji na gharama za usafirishaji, pamoja na kutafuta suluhu za pamoja zitakazoboresha mazingira ya biashara na kuongeza ushindani wa njia za usafirishaji.

Aidha, wadau wamejadili umuhimu wa kuimarisha matumizi ya Bandari ya Kigoma kama lango muhimu la biashara katika ukanda wa Maziwa Makuu, hususan kupitia Ushoroba wa Kati (Central Corridor) unaoiunganisha Tanzania na nchi jirani.

Kikao hicho pia kimekuwa fursa ya kuimarisha ushirikiano kati ya Serikali, sekta binafsi na wadau wengine wa mnyororo wa usafirishaji katika kuboresha huduma, kupunguza muda na gharama za usafirishaji, na kuweka mazingira rafiki zaidi kwa biashara ya ndani na ya kikanda.

Kwa ujumla, kikao hicho kimeendelea kuonesha umuhimu wa majadiliano ya pamoja katika kutatua changamoto za usafirishaji na kutumia fursa zilizopo katika ukanda wa Magharibi, huku Bandari ya Kigoma ikiendelea kuwa sehemu muhimu ya kuunganisha biashara ya Tanzania na masoko ya nchi za Maziwa Makuu.











TANZANIA YAWEKA SAUTI YAKE RIYADH, YASISITIZA AI YENYE LUGHA, UTAMADUNI NA MASLAHI YA TAIFA

September 16, 2026 Add Comment


RIYADH, SAUDI ARABIA: 

Tanzania imesisitiza umuhimu wa kujenga na kutumia akili unde (Artificial Intelligence – AI) inayozingatia lugha, utamaduni, mazingira na mahitaji ya jamii, huku ikieleza dhamira ya kuimarisha uwezo wa ndani wa nchi katika teknolojia hiyo na kuongeza nafasi ya Kiswahili katika ulimwengu wa akili unde.

Msisitizo huo umetolewa katika Jukwaa la Nne la Kimataifa la UNESCO la Maadili ya Akili Unde linalofanyika mjini Riyadh, Saudi Arabia, ambapo Tanzania imeshiriki katika mjadala wa kimataifa kuhusu hatua za vitendo zinazoweza kuchukuliwa na nchi ili kuhakikisha maendeleo ya akili unde yanaenda sambamba na maadili, uwajibikaji, usalama na maendeleo jumuishi.

Katika mchango wake kwenye mjadala huo, mwakilishi wa Tanzania aliishukuru UNESCO na Serikali ya Saudi Arabia kwa kuandaa jukwaa hilo, akieleza kuwa majadiliano hayo yana umuhimu mkubwa katika kuzipa nchi nafasi ya kubadilishana uzoefu na kutafuta suluhisho la pamoja kuhusu fursa na changamoto zinazoletwa na maendeleo ya akili unde.

Aidha, Tanzania iliishukuru UNESCO kwa kuiunga mkono Serikali katika kutekeleza Mbinu ya Tathmini ya Utayari wa Akili Unde (Readiness Assessment Methodology – RAM) mwaka 2024, ambayo matokeo yake yalizinduliwa mwaka 2025.

Tathmini hiyo iliisaidia Tanzania kubaini maeneo mbalimbali yanayohitaji kuimarishwa ili kujenga mazingira wezeshi kwa maendeleo na matumizi salama, jumuishi na yenye maadili ya akili unde.

TANZANIA YASISITIZA KUJENGA UWEZO WA NDANI

Akieleza baadhi ya mapengo yaliyobainika, mwakilishi wa Tanzania alitaja umuhimu wa kuhakikisha lugha mbalimbali zinapata nafasi katika mifumo ya akili unde, akisisitiza kuwa nchi zinahitaji kujenga uwezo wa ndani ili teknolojia hiyo iweze kuakisi mazingira na mahitaji ya jamii zao.

Alieleza kuwa utegemezi mkubwa wa mifumo ya akili unde iliyotengenezwa nje unaweza kuibua changamoto zinazohusiana na uwakilishi wa tamaduni, usalama na umiliki wa data, pamoja na ulinganifu wa mifumo hiyo na sheria na maadili ya nchi husika.

Kwa msingi huo, Tanzania imeona umuhimu wa kuwekeza katika uwezo wa ndani wa kutengeneza na kutumia mifumo ya akili unde inayozingatia lugha na mazingira ya Tanzania, sambamba na kuimarisha miundombinu ya data na mifumo ya kitaifa ya usimamizi wa teknolojia hiyo.

Mwelekeo huo unaendana na hatua zinazochukuliwa na Serikali katika kuimarisha mageuzi ya kidijitali nchini. Serikali imetangaza mageuzi ya kidijitali kuwa miongoni mwa vipaumbele katika Bajeti ya mwaka 2026/2027, huku ikiendelea na maandalizi ya Mkakati wa Taifa wa Akili Unde.

KISWAHILI KUPATA NAFASI KATIKA MAPINDUZI YA AI

Moja ya hoja muhimu iliyowasilishwa na Tanzania Riyadh ni umuhimu wa kuendeleza mfumo mkubwa wa lugha (Large Language Model – LLM) wa Kiswahili, ili kuwezesha lugha hiyo kuwa sehemu muhimu ya maendeleo ya teknolojia za akili unde.

Tanzania imeeleza nia ya kushirikiana na wadau mbalimbali, wakiwemo UNESCO, katika kuendeleza mfumo huo, hatua inayolenga kuongeza uwezo wa teknolojia kuelewa na kutumia Kiswahili kwa ufasaha na kwa kuzingatia mazingira ya watumiaji wake.

Kiswahili kinachukua nafasi muhimu katika maisha ya Watanzania na ni miongoni mwa lugha zinazotumika na idadi kubwa ya watu barani Afrika. Kwa hiyo, uwekezaji katika teknolojia inayoweza kuelewa na kutumia Kiswahili una umuhimu katika kupanua ushiriki wa wananchi katika mapinduzi ya kidijitali.

Hatua hii pia inaendana na mwelekeo wa Serikali wa kuendeleza rasilimali na zana za lugha ya Kiswahili kwa ajili ya mifumo ya akili unde na uchakataji wa lugha asilia.

MAGEUZI YA KIDIJITALI KUELEKEA TANZANIA YA MAENDELEO

Mjadala wa Tanzania katika jukwaa hilo unaakisi mwelekeo mpana wa Serikali katika kutumia teknolojia za kisasa kama kichocheo cha maendeleo ya Taifa.

Katika hatua mbalimbali, Serikali imeendelea kuweka mazingira ya matumizi ya akili unde, ikiwemo kuimarisha sera na mifumo ya kidijitali, kulinda taarifa binafsi na kujenga uwezo wa rasilimali watu katika teknolojia zinazochipukia.

Mkakati wa Taifa wa Uchumi wa Kidijitali wa 2024–2034 pamoja na hatua zinazoendelea katika eneo la akili unde vinaweka msingi wa kutumia teknolojia za kisasa katika kuongeza ufanisi wa huduma, kukuza ubunifu na kuchochea shughuli za kiuchumi.

Kwa upande wa elimu, Serikali pia imeendelea kuweka msisitizo katika matumizi sahihi ya teknolojia mpya, ikiwemo akili unde, katika ufundishaji, ujifunzaji, utafiti na ujenzi wa uwezo wa walimu na wanafunzi.

TANZANIA NA AJENDA YA AI BARANI AFRIKA

Katika mjadala huo wa kimataifa, Tanzania imeendelea kuangazia pia nafasi ya Afrika katika mapinduzi ya akili unde, ikisisitiza umuhimu wa bara hilo kuongeza uwezo wake katika sayansi, teknolojia, utafiti, ubunifu na ujuzi wa kidijitali.

Kwa Tanzania, Afrika inapaswa kuwa zaidi ya mtumiaji wa teknolojia hiyo; inahitaji pia kujenga uwezo wa kuzalisha maarifa, data, mifumo na ubunifu unaozingatia mazingira ya Kiafrika.

Hii inamaanisha kuongeza uwekezaji katika wataalamu, taasisi za utafiti, miundombinu ya kidijitali na rasilimali za lugha za Kiafrika ili kuhakikisha maendeleo ya akili unde yanawanufaisha wananchi na kuchangia maendeleo ya bara.

UNESCO NA TANZANIA ZASHIRIKI KUJENGA AI YENYE MAADILI

Ushiriki wa Tanzania katika jukwaa la Riyadh unaendelea kuimarisha ushirikiano kati ya Tanzania na UNESCO katika eneo la teknolojia zinazochipukia na matumizi yake yenye uwajibikaji.

Kupitia Tathmini ya Utayari wa Akili Unde, Tanzania imepata fursa ya kutathmini mazingira yake ya kitaifa na kubaini maeneo yanayohitaji kuimarishwa katika sera, mifumo ya kitaasisi, uwezo wa watu, miundombinu na matumizi ya teknolojia hiyo.

Kwa upande mwingine, ushiriki katika mijadala ya kimataifa kama ya Riyadh unaipa Tanzania nafasi ya kushirikisha uzoefu wake, kujifunza kutoka kwa nchi nyingine na kuendelea kujenga ushirikiano wa kimataifa katika eneo la akili unde.

Hatua hizi zinaendana na dhamira ya Serikali ya kutumia mageuzi ya kidijitali, sayansi, teknolojia na ubunifu kama nyenzo za kuongeza fursa za maendeleo na kujenga Tanzania inayokwenda sambamba na mabadiliko ya kiteknolojia duniani.

TANZANIA YAANGALIA MUSTAKABALI WA TEKNOLOJIA

Kwa ujumla, ujumbe wa Tanzania katika Jukwaa la Nne la Kimataifa la UNESCO la Maadili ya Akili Unde umeweka mkazo katika kujenga teknolojia inayozingatia watu, lugha na mazingira yao.

Kupitia mjadala huo, Tanzania imeendelea kuonyesha umuhimu wa kuunganisha maendeleo ya teknolojia na mahitaji ya jamii, huku ikisisitiza kuwa akili unde inapaswa kutumika kwa kuzingatia maadili, usalama, haki, utofauti wa lugha na tamaduni, pamoja na vipaumbele vya maendeleo ya Taifa.

Ushiriki huo unaendelea kuifanya Tanzania kuwa sehemu ya mjadala wa kimataifa kuhusu mustakabali wa akili unde, wakati Serikali ikiendelea kuchukua hatua za kujenga mazingira wezeshi ya mageuzi ya kidijitali na matumizi ya teknolojia kwa maendeleo ya Taifa.

Jukwaa la Nne la Kimataifa la UNESCO la Maadili ya Akili Unde linaendelea mjini Riyadh, Saudi Arabia, likiwakutanisha viongozi, wataalamu, watafiti, watunga sera na wadau kutoka sehemu mbalimbali duniani kujadili namna ya kuimarisha ushirikiano wa kimataifa na utawala wa akili unde unaozingatia maadili na uwajibikaji.

SIJARIDHISHWA NA KASI YA WAKANDARASI KIKIM NA AMACO YA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA BARABARA, STENDI NA SOKO LINDI - PROF. SHEMDOE

September 16, 2026 Add Comment


Na: OWM – TAMISEMI, Lindi

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM–TAMISEMI), Mhe. Prof. Riziki Shemdoe, amesema hajaridhishwa na kasi ya utekelezaji wa miradi inayotekelezwa na Mkandarasi KIKIM Contractors Limited kwa kushirikiana na mbia wake AMACO Enterprises katika Manispaa ya Lindi.

Miradi hiyo inahusisha ujenzi wa barabara zenye urefu wa kilomita 5.3, Stendi ya Mabasi Mitwero, Soko Kuu la Matopeni na Ofisi ya Mradi, inayotekelezwa na Serikali kupitia Mradi wa Ustawishaji Miji Tanzania (TACTIC).


Prof. Shemdoe ameeleza kutoridhishwa kwake na kasi ya utekelezaji wa miradi hiyo Septemba 15, 2026, mara baada ya kutembelea na kukagua ujenzi wa Stendi ya Mabasi ya Mitwero na Soko Kuu la Matopeni, ambapo alibaini kuwa utekelezaji wake umefikia asilimia 23, huku ikiwa imesalia miezi mitano kabla ya muda wa kukamilisha na kukabidhi miradi hiyo.

Akizungumza baada ya kukagua miradi hiyo, Prof. Shemdoe amemtaka Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Mhe. Adam Kighoma Malima, kuhakikisha suala la utekelezaji wa mikataba hiyo linashughulikiwa kwa mujibu wa masharti ya mikataba, ili kuharakisha utekelezaji na kuhakikisha miradi hiyo inakamilika kwa wakati.


“Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa, hawa wanaotukwamisha ni wakandarasi wazawa ambao usipowapa kazi wanalalamika. Hivyo, Mheshimiwa RC, hawa wana mikataba, shughulikia suala hili kwa mujibu wa mkataba, kwani wakandarasi hawa wanaonekana ni wababaishaji,” amesema Prof. Shemdoe.


Aidha, Prof. Shemdoe amemtaka Mkuu wa Mkoa wa Lindi kukutana na wakandarasi hao ili wampe mpango mkakati wa kukamilisha miradi hiyo haraka iwezekanavyo, na kuwasilisha kwake mpango kazi huo ifikapo Septemba 23, 2026.Vilevile, ameelekeza kuwa kila baada ya wiki mbili apatiwe mrejesho wa utekelezaji wa mpango huo, ili kufahamu hatua zinazochukuliwa na maendeleo ya miradi hiyo.


Akieleza chanzo cha kasi ndogo ya utekelezaji wa miradi hiyo, Mwakilishi wa Mhandisi Mshauri kutoka kampuni ya Interconsult Ltd, ambaye pia ni Mhandisi Mkazi, Mhandisi Rashidi Abdallah, amesema changamoto hiyo imetokana na mkandarasi kutokuwa amejipanga vyema kiutendaji, kutokuwa na rasilimaliwatu ya kutosha na kutumia vibaya fedha za awali alizolipwa kwa ajili ya utekelezaji wa mradi.

Naye mmoja wa Wakurugenzi wa kampuni zilizopewa kandarasi hizo, John Daniel, amekiri kuwa wamechelewa kutekeleza miradi hiyo kutokana na uzembe, huku akieleza kuwa wamejipanga kufanya kazi usiku na mchana baada ya kuzifanyia kazi changamoto zilizokuwa zikikwamisha utekelezaji.


Bw. Daniel ameomba kukutana na Mkuu wa Mkoa wa Lindi ili kuwasilisha mpango kazi wao, huku akimuomba Mkuu wa Mkoa kuwawekea malengo ya muda mfupi yatakayowawezesha kukamilisha kandarasi yao kwa wakati.

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Mhe. Adam Kighoma Malima, amesema atakutana na wakandarasi hao ili wamueleze mkakati wanaokuja nao wa kukamilisha miradi yote ndani ya miezi mitano iliyobaki.


Mhe. Malima amewataka wakandarasi hao, wakati wa kikao hicho, kuwa tayari kuridhia kutoa mkataba mdogo (sub-contract) kwa mkandarasi mwingine kutekeleza sehemu ya mradi endapo wataona hawana uwezo wa kuikamilisha kwa wakati.


Katika ziara yake ya Septemba 15, 2026, Prof. Shemdoe alitembelea na kukagua pia utekelezaji wa miradi ya ujenzi wa Daraja la Ng’uni katika Kata ya Nanganga, ujenzi wa shule mpya ya msingi eneo la Shule ya Sekondari Kitandi, ujenzi wa Kituo cha Afya Chiola Nachingwea, pamoja na kufanya mkutano wa hadhara katika Kijiji cha Mtuha, Nachingwea DC.







DKT. MWIGULU: NDANI YA WIKI MOJA TUTACHUKUA HATUA KUSHUSHA BEI YA SARUJI

September 16, 2026 Add Comment


WAZIRI MKUU Dkt. Mwigulu Nchemba amesema ndani ya wiki moja, Serikali itachukua hatua ya kuhakikisha bei ya saruji inakuwa himilivu kwa wananchi, baada ya kubaini malalamiko ya kupanda kwa bei ya bidhaa hiyo katika mikoa mbalimbali nchini ikiwemo Simiyu.

Ametoa kauli hiyo jana (Jumanne, Septemba 15, 2026) wakati akizungumza na wananchi wa Bariadi Mjini, mkoani Simiyu katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye viwanja vya CCM Saba Saba.

“Serikali tumeliona hilo. Serikali sikivu tumesikia hilo. Nimewatuma wataalamu ndani ya wiki moja wawe wameshapata ufumbuzi. Tutatoa tamko la njia ya kushusha bei ya saruji ili kila Mtanzania aweze kumudu. Katika baadhi ya maeneo bei ya saruji imefikia zaidi ya sh. 26,000 na katika baadhi ya mikoa ya mipakani imefikia sh. 32,000,” amesema na kusisitiza kuwa Serikali inataka wananchi waweze kumudu gharama za ujenzi wa nyumba na miradi mingine ya maendeleo.

Kuhusu zao la pamba, Waziri Mkuu amesema ameielekeza Wizara ya Kilimo ikutane na wadau wa pamba ndani ya mwezi mmoja na ifikapo Oktoba 15, 2026 apelekewe mapendekezo rasmi kuhusu bei na mfumo bora wa ununuzi wa zao hilo ili kuhakikisha wakulima wananufaika zaidi.

“Nimeipokea hoja hii. Nimeelekeza Wizara ya Kilimo ikae na wadau wa pamba ndani ya mwezi mmoja. Ifikapo tarehe 15 mwezi wa 10, niwe nimeshapata mapendekezo rasmi yaliyorejea mifumo ambayo tumeshaitumia na kubaini upi ni mfumo bora ili tuweze kuhakikisha kwamba wakulima wananufaika,” amesema.

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu amesema pia Serikali imebadilisha utaratibu wa kodi kwa wenye biashara mpya, ambapo mfanyabiashara anayeanzisha biashara atapewa muda wa kuimarisha biashara yake kabla ya kuanza kubeba mzigo wa kodi. “Zamani ilikuwa mtu akianzisha tu biashara, siku hiyo hiyo anaanza kudaiwa kodi. Sasa tumefuta, atasubiriwa mwaka mzima ili biashara yake iimarike,” amesema.

Amesema hatua hizo ni sehemu ya utekelezaji wa Dira ya Maendeleo ya 2050 inayolenga kujenga uchumi shirikishi, ambapo sekta binafsi inatarajiwa kutekeleza sehemu kubwa ya shughuli za maendeleo.

Mapema, akizungumza katika mkutano huo, Mbunge wa Bariadi Mjini ambaye pia ni Naibu Waziri wa Maji, Mhandisi Kundo Andrea Mathew, amemshukuru Waziri Mkuu kwa ziara hiyo na kueleza kuwa Serikali imeendelea kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo katika jimbo hilo ikiwemo inayogusa sekta za maji, elimu, afya na barabara.

Mhandisi Kundo amesema mradi mkubwa wa maji kutoka Ziwa Victoria wenye thamani ya sh. bilioni 440 unaendelea kutekelezwa mkoani humo, huku Serikali ikiwa imetoa sh. milioni 460 kupitia TARURA kwa ajili ya ujenzi wa daraja la Majaida–Munambala katika Mto Ndoba.

Kuhusu ujenzi wa soko la kisasa la Bariadi mjini, Mhandisi Kumndo amesema ujenzi wake unaendelea, huku akiomba kasi ya mkandarasi iongezwe ili mradi huo ukamilike kwa wakati.

Akigusia barabara za Bariadi Mjini, Mhandisi Kundo amesema Serikali imeweka mpango wa kuhakikisha kilomita zote 8.6 zilizotengewa ujenzi zinajengwa kwa awamu mbili, ambapo kilomita tano zitajengwa katika awamu ya kwanza.

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Said Mtanda, amesema Serikali ya Mkoa itasimamia na kutekeleza maelekezo yote yaliyotolewa na Waziri Mkuu wakati wa ziara hiyo na kuwasilisha taarifa ya utekelezaji katika Ofisi ya Waziri Mkuu.

“Maagizo na maelekezo yako uliyoyatoa katika ziara yako hii tunayasimamia, tuyatekeleze, na kuleta ripoti ya utekelezaji katika ofisi yako ya Waziri Mkuu,” amesema.




MRADI WA UMEME SIMIYU KUFUNGUA FURSA ZA UWEKEZAJI NA KUCHOCHEA SHUGHULI ZA KIUCHUMI WANANCHI

September 16, 2026 Add Comment






📌 Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Mhe.Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb.) aipongeza TANESCO kwa kutekeleza Mradi kwa kutumia wataalamu wa ndani

📌 MD Twange asema mradi wa ujenzi wa kituo cha kupoza umeme umefikia asilimia 82 ya utekelezaji wake




Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba amekagua ujenzi wa kituo cha kupokea na kupoza umeme cha Imalilo mkoani Simiyu ambapo ameeleza kukamilika kwa mradi huo kutafungua fursa za uwekezaji na kuboresha huduma ya upatikanaji wa umeme kwa wananchi.

Mhe. Mwigulu ameyasema hayo leo Septemba 14, 2026 katika eneo la mradi wa Imalilo wakati akikagua utekelezaji wake.

"Nawapongeza sana Wizara ya Nishati kwa kutekeleza mradi huu kupitia TANESCO kwa kutumia wataalamu wa ndani hongereni sana" amesema Mhe. Dkt. Mwigulu

Dkt. Mwigulu akizungumzia kuhusu ujenzi wa njia ya kusafirisha umeme kutoka Ibadakuli, Shinyanga hadi Imalilo, Simiyu, Dkt. Mwigulu amesema Serikali itatoa fedha kuhakikisha mradi huo unakamalika na kuwa na tija kwa Taifa.

Awali, akitoa taarifa ya utekelezaji wa mradi Mkurugenzi Mtendaji TANESCO Bw. Lazaro Twange amesema mradi umetekelezwa kwa kutumia wataalamu wa ndani na unatarajiwa kukamilika ndani ya mwaka mmoja.

"Mhe. Waziri Mkuu mradi huu umefikia asilimia 82 ya utekelezaji wake na utakamilkika katika muda ambao tumeupanga" amesema Bw. Twange. Aidha amesema gharama ya utekelezaji wa mradi wa kituo cha kupokea na kupoza umeme umegarimu shilingi bilioni 27, ambapo mpaka sasa Serikali imetumia shilingi bilioni 15 na kazi zote za msingi zimekamilika na ujenzi unaendelea.

Mradi wa kituo cha kupokea na kupoza umeme cha Imalilo unatarajiwa kuboresha upatikanaji wa huduma ya umeme katika mikoa ya Simiyu, Mara na maeneo jirani.


















WATAALAMU NA WATAFITI WAHIMIZWA KUAINISHA VIPAUMBELE VYA KIMKAKATI KUELEKEA MKUTANO WA COP 12

September 15, 2026 Add Comment
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Mazingira Zanzibar (ZEMA) Sheha Mjaja Juma akizungumza na Wataalamu na Watafiti kutoka Wizara, Taasisi za Umma na sekta binafsi wakati wa ufunguzi wa kikao kuhusu maandalizi ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuelekea Mkutano wa 12 wa Nchi Wanachama Zinazotekeleza Mkataba wa Nairobi kuhusu Usimamizi wa Mazingira ya Bahari na Ukanda wa Pwani ya Magharibi ya Bahari ya Hindi. Kikao hicho kimefanyika Septemba 15, 2026 Unguja, Zanzibar.

JUKWAA LA MIFUMO YA CHAKULA LAZINDULIWA DAR

September 15, 2026 Add Comment
NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

JIJI la Dar es Salaam limezindua Jukwaa la Mifumo ya Chakula litakalokuwa chombo cha kuunganisha wadau mbalimbali katika kuboresha upatikanaji wa chakula salama, bora na chenye lishe kwa wakazi wa jiji hilo.
FCC YATAJWA CHACHU YA SOKO HURU NA USHINDANI WA HAKI

FCC YATAJWA CHACHU YA SOKO HURU NA USHINDANI WA HAKI

September 15, 2026 Add Comment

Na.Mwandishi Wetu

Tume ya Ushindani ya Somali  imefanya ziara ya siku moja nchini Tanzania kwa lengo la kujifunza uzoefu na mbinu zinazotumiwa na Tume ya Ushindani Tanzania (FCC) katika kusimamia ushindani wa kibiashara, kudhibiti bidhaa bandia na kulinda maslahi ya walaji.

Ziara hiyo imefanywa na Mkurugenzi wa Masuala ya Uchumi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa ya Jamhuri ya Shirikisho la Somalia na Kamishna wa Mamlaka ya Ushindani ya Afrika Mashariki (EACA), Bw. Ahmed Warsame pamoja na Mkurugenzi wa Biashara na Upatikanaji wa Masoko wa Wizara ya Biashara na Viwanda ya Jamhuri ya Shirikisho la Somalia, Bw. Abdihalim Osman.

Katika ziara hiyo, ujumbe huo umekutana na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa FCC, Bi. Khadija Ngasongwa, pamoja na uongozi wa Tume, ambapo walipata fursa ya kujifunza namna FCC inavyotekeleza majukumu yake ya kukuza na kulinda ushindani, kumlinda mlaji na udhibiti wa bidhaa bandia.

Akizungumza wakati wa ziara hiyo, uongozi wa ujumbe wa Somalia umepongeza utendaji wa FCC, ukieleza kuwa uzoefu wa Tanzania katika kusimamia ushindani na kulinda mlaji ni muhimu kwa Somalia katika kuimarisha mifumo yake ya usimamizi wa soko na kukuza mazingira bora ya biashara.

Ujumbe huo umeeleza kuwa kujifunza kutoka FCC kutasaidia kuongeza uelewa na uwezo wa taasisi za Somalia katika kukabiliana na changamoto zinazohusu ushindani usio wa haki, bidhaa bandia na vitendo vinavyoweza kuwadhuru walaji.

Kwa upande wake,Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa FCC, Bi. Khadija Ngasongwa, amesema  kuwa Tanzania ipo tayari kuendelea kushirikiana na taasisi za Somalia na nchi nyingine katika kubadilishana uzoefu, maarifa na mbinu bora za usimamizi wa ushindani na ulinzi wa walaji.

Ziara hiyo ya siku moja imekuwa fursa muhimu kwa Somalia kujifunza uzoefu wa Tanzania katika eneo la ushindani wa kibiashara, udhibiti wa bidhaa bandia na ulinzi wa mlaji, hatua inayotarajiwa kuimarisha ushirikiano wa kitaasisi na kuchangia katika ujenzi wa masoko yenye ushindani wa haki na biashara endelevu.

WATAALAMU NA WATAFITI WAHIMIZWA KUANISHA VIPAUMBELE VYA KIMKAKATI KUELEKEA MKUTANO WA COP 12.

September 15, 2026 Add Comment
 Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Mazingira Zanzibar (ZEMA) Sheha Mjaja Juma akizungumza na Wataalamu na Watafiti kutoka Wizara, Taasisi za Umma na sekta binafsi wakati wa ufunguzi wa kikao kuhusu maandalizi ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuelekea Mkutano wa 12 wa Nchi Wanachama Zinazotekeleza Mkataba wa Nairobi kuhusu Usimamizi wa Mazingira ya Bahari na Ukanda wa Pwani ya Magharibi ya Bahari ya Hindi. Kikao hicho kimefanyika Septemba 15, 2026 Unguja, Zanzibar.
Mkurugenzi Msaidizi wa Mazingira, Ofisi ya Makamu wa Rais, Dkt. Paul Deogratius akizungumza na Wataalamu na Watafiti kutoka Wizara, Taasisi za Umma na sekta binafsi wakati wa ufunguzi wa kikao kuhusu maandalizi ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuelekea Mkutano wa 12 wa Nchi Wanachama Zinazotekeleza Mkataba wa Nairobi kuhusu Usimamizi wa Mazingira ya Bahari na Ukanda wa Pwani ya Magharibi ya Bahari ya Hindi. Kikao hicho kimefanyika Septemba 15, 2026 Unguja, Zanzibar.
Wakili Mkuu wa Serikali Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Bi. Vaileth Machary akizungumza jambo wakati wa kikao cha Wataalamu na Watafiti kutoka Wizara, Taasisi za Umma na sekta binafsi kuhusu maandalizi ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuelekea Mkutano wa 12 wa Nchi Wanachama Zinazotekeleza Mkataba wa Nairobi kuhusu Usimamizi wa Mazingira ya Bahari na Ukanda wa Pwani ya Magharibi ya Bahari ya Hindi. Kikao hicho kimefanyika Septemba 15, 2026 Unguja, Zanzibar.
Kaimu Mkurugenzi Maendeleo ya Uchumi wa Buluu Ofisi ya Makamu wa Rais, Bi. Magdalena Ngotolainyo akizungumza na Wataalamu na Watafiti kutoka Wizara, Taasisi za Umma na sekta binafsi wakati wa ufunguzi wa kikao kuhusu maandalizi ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuelekea Mkutano wa 12 wa Nchi Wanachama Zinazotekeleza Mkataba wa Nairobi kuhusu Usimamizi wa Mazingira ya Bahari na Ukanda wa Pwani ya Magharibi ya Bahari ya Hindi. Kikao hicho kimefanyika Septemba 15, 2026 Unguja, Zanzibar.
Afisa Takwimu Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Bi. Caroline Gweso akizungumza jambo wakati wa kikao cha Wataalamu na Watafiti kutoka Wizara, Taasisi za Umma na sekta binafsi kuhusu maandalizi ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuelekea Mkutano wa 12 wa Nchi Wanachama Zinazotekeleza Mkataba wa Nairobi kuhusu Usimamizi wa Mazingira ya Bahari na Ukanda wa Pwani ya Magharibi ya Bahari ya Hindi. Kikao hicho kimefanyika Septemba 15, 2026 Unguja, Zanzibar.
Mratibu wa Mipango ya Bahari kutoka Shirika la Uhifadhi wa Maizngira Duniani (WWF) Dkt. Modesta Medard akizungumza jambo wakati wa kikao cha Wataalamu na Watafiti kutoka Wizara, Taasisi za Umma na sekta binafsi kuhusu maandalizi ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuelekea Mkutano wa 12 wa Nchi Wanachama Zinazotekeleza Mkataba wa Nairobi kuhusu Usimamizi wa Mazingira ya Bahari na Ukanda wa Pwani ya Magharibi ya Bahari ya Hindi. Kikao hicho kimefanyika Septemba 15, 2026 Unguja, Zanzibar.

Watendaji Waandamizi kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Bi. Sophia Kivina na Zahara Suleiman wakifuatilia kikao cha Wataalamu na Watafiti kutoka Wizara, Taasisi za Umma na sekta binafsi kuhusu maandalizi ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuelekea Mkutano wa 12 wa Nchi Wanachama Zinazotekeleza Mkataba wa Nairobi kuhusu Usimamizi wa Mazingira ya Bahari na Ukanda wa Pwani ya Magharibi ya Bahari ya Hindi. Kikao hicho kimefanyika Septemba 15, 2026 Unguja, Zanzibar.

Wataalamu na watafiti kutoka Wizara, Taasisi za Umma na sekta binafsi wamehimizwa kubainisha vipaumbele vya kimkakati ili kuhakikisha Tanzania inanufaika vyema na Mkutano wa 12 wa Mkataba wa Nairobi unaotarajia kufanyika nchini kuanzia tarehe 6-9 Oktoba, mwaka huu.


Maafisa Waandamizi kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Bi. Salome Musangile na Bi. Vaileth Machary wakijadialiana jambo wakati wa wa kikao cha Wataalamu na Watafiti kutoka Wizara, Taasisi za Umma na sekta binafsi kuhusu maandalizi ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuelekea Mkutano wa 12 wa Nchi Wanachama Zinazotekeleza Mkataba wa Nairobi kuhusu Usimamizi wa Mazingira ya Bahari na Ukanda wa Pwani ya Magharibi ya Bahari ya Hindi. Kikao hicho kimefanyika Septemba 15, 2026 Unguja, Zanzibar.

Hayo yamesemwa Septemba 15, 2026 Mjini Zanzibar na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Mazingira Zanzibar (ZEMA) Sheha Mjaja Juma wakati akifungua kikao cha wataalamu kuhusu Maandalizi ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuelekea Mkutano wa 12 wa Nchi Wanachama zinazotekeleza Mkataba wa Nairobi (COP 12).

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Mazingira Zanzibar (ZEMA) Sheha Mjaja Juma (waliokaa katikati) akiwa katika picha ya pamoja na watumishi wa Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) na Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais Zanzibar muda mfupi baada ya kufungua kikao cha Watalaamu na  Watafiti kutoka Wizara, Taasisi za Umma na sekta binafsi kuhusu maandalizi ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuelekea Mkutano wa 12 wa Nchi Wanachama Zinazotekeleza Mkatab awa Nairobi kuhusu Usimamizi wa Mazingira ya Bahari na Ukanda wa Pwani ya Magharibi ya Bahari ya Hindi. Kikao hicho kimefanyika Septemba 15, 2026 Unguja, Zanzibar.

Mjaja amesema Mkutano wa COP 12 unafanyika katika kipindi muhimu ambapo Tanzania Bara na Zanzibar zinatekeleza ajenda za maendeleo za muda mrefdu kupitia Dira ya Maendeleo ya Zanzibar 2050 na Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.


“Dira hizi zinatambua umuhimu wa matumizi endelevu ya rasilimali za asili, ulinzi wa mazingira na kujenga uchumi unaostahimili mabadiliko ya tabianchi, hivyo ni fursa muhimu kuainisha mijadala ya kikanda na mikakati ya uchumi wa buluu” amesema Mjaja.

Kwa mujibu wa Mjaja amewataka wataalamu hao kuhakikisha changamoto kuhusiana na uchafuzi wa bahari, taka za plastiki, uharibifu wa matumbawe, uvuvi usio endelevu zinapata majibu ya pamoja na kuweza kufanyiwa kazi.

Mjaja amebainisha masuala muhimu ya wataalamu hao yanayopaswa kuzingatiwa ni mbinu za kuimarisha uchumi wa buluu endelevu, uhifadhi wa mifumo ikolojia ikiwemo mikoko, matumbawe na maeneo oevu.

Amesema afya ya bahari na ukanda wa pwani ni msingi wa afya ya jamii, usalama wa chakula, ajira, kipato na ustawi wa wananchi ambao unabeba mustakabali endelevu wa maisha na ustawi wa jamii.

Kwa upande wake Mkurugenzi Msaidizi wa Mazingira Ofisi ya Makamu wa Rais, Dkt. Paul Deogratius amesema malengo ya mkutano huo ni pamoja na kupokea taarifa ya utekelezaji wa Mkataba wa Nairobi na pamoja na kupokea taarifa ya mapato na matumizi ya fedha.

Dkt. Paul piua amebainisha manufaa ya Mkutano wa COP 12 ni pamoja na kuiwezesha Tanzania kuimarisha diplomasia ya mazingira katika majukwaa ya kikanda na kimataifa, kuvutia uwekezaji katika sekta za uvuvi, utalii, nishati na usafiri.

“Tanzania imeendelea kuweka mkazo katika masuala ya uhifadhi wa mazingira na kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi sambamba na matumizi endelevu ya rasilimali na kukuza uchumi wa Buluu” amesema Dkt. Deogratius.

Naye Mkuu wa Sekretarieti ya Mkataba wa Nairobi, Dkt. Jaredi Bosire ameipongeza maandalizi ya Serikali ya Tanzania kuelekea Mkutano wa COP 12 na kuzitaka Nchi wanachama kuiga mfano huo kuelekea mikutano ijayo.

Amesema mkutano wa COP 12 umeweza kuvutia idadi kubwa ya washiriki ambapo hadi kufikia sasa jumla ya washiriki 800 wameweza kujisajili katika tovuti ya Shirika la Mazingira la Umoja wa Mataifa (UNEP).

Dkt. Bosire amesema katika Mkutano huo pia umepanga kuwa na jumla ya mikutano ya pembezoni takribani 50 ikilinganisha na mikutano 40 ya aina hiyo iliyofanyika katika mkutano uliofanyika Madagascar mwaka 2024.

Mkataba wa Nairobi kuhusu Usimamizi na Uendelezaji wa Mazingira ya Bahari na Ukanda wa Pwani ya Magharibi ya Bahari ya Hindi unatekelezwa na Nchi Wanachama 10 ambazo ni Tanzania, Komoro, Kenya, Somalia, Madagascar, Mauritius, Msumbiji, Shelisheli na Ufaransa.