HABARI

SIASA

ELIMU

Recent Posts

WATU MILIONI 15.6 WAHAMIA NISHATI SAFI YA KUPIKIA NDANI YA MIAKA MITANO

August 11, 2026 Add Comment




NA MWANDISHI WETU

WATU milioni 15.6 nchini Tanzania wamehama kutoka katika matumizi ya nishati isiyo salama na kuanza kutumia nishati safi ya kupikia ndani ya kipindi cha miaka mitano.

Hayo yameelezwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati (Umeme na Nishati Jadidifu), Mhandisi Felchesmi Mramba, wakati wa Mdahalo wa Nishati Safi uliofanyika Agosti 11, 2026, Kizimkazi, Mkoa wa Kusini Unguja, Zanzibar.

Mhandisi Mramba amesema hatua hiyo imefikiwa kutokana na juhudi mbalimbali zinazotekelezwa na Serikali kuhakikisha Watanzania wanahamia katika matumizi ya nishati safi ya kupikia, ikiwa ni sehemu ya kufikia lengo la asilimia 80 ya Watanzania kutumia nishati hiyo ifikapo mwaka 2034.




Amesisitiza kuwa Serikali inaendelea kuongeza juhudi za kutoa elimu na kuhamasisha wananchi kuhusu umuhimu na manufaa ya kutumia nishati safi ya kupikia.

Vilevile, amesema Serikali inaendelea kuboresha miundombinu ya upatikanaji wa nishati safi ya kupikia ili iweze kupatikana kwa gharama nafuu ambazo wananchi wengi watamudu.




Ameongeza kuwa Serikali inalenga kuhakikisha nishati hiyo inasambaa na kupatikana kwa urahisi katika maeneo yote nchini, kwa kuzingatia aina ya nishati inayopatikana katika eneo husika.

“Serikali inasambaza nishati safi ya kupikia katika maeneo mbalimbali nchini kulingana na mazingira na upatikanaji wa nishati katika eneo husika. Kwa mfano, maeneo ambayo gesi inapatikana kwa wingi yanapelekewa mitungi na majiko ya gesi, huku maeneo yenye umeme yakipelekewa majiko yanayotumia umeme,” amesema Mhandisi Mramba.



Sambamba na hilo, amesema juhudi zaidi zinaendelea kufanyika kuhakikisha wananchi wanapata teknolojia na mifumo rahisi na rafiki ya nishati safi ya kupikia ili kila mwananchi aweze kuitumia.





USIMAMISHWAJI WA MUDA WA UAGIZAJI NA UUZWAJI WA BIDHAA ZA POMBE NCHINI RWANDA

August 11, 2026 Add Comment

WAZIRI NDEJEMBI: MABADILIKO YA MILA, MITAZAMO NI MUHIMU KUFIKIA MALENGO YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA

August 11, 2026 Add Comment



Na Mwandishi Wetu - Zanzibar




Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi amesema juhudi za usambazaji wa teknolojia za nishati safi ya kupikia zinapaswa kwenda sambamba na kuweka mkazo katika mabadiliko ya mila, desturi na mitazamo ambayo inachangia katika kurudisha nyuma juhudi za Serikali za kuhakikisha wananchi wote wanatumia nishati safi ya kupikia.


Mhe. Ndejembi ametoa kauli hiyo Agosti 11, 2026, Kizimkazi Mkoa wa Kusini Unguja, Zanzibar wakati wa Mdahalo wa Nishati Safi ulioandaliwa na Taasisi ya Mwanamke Initiatives Foundation (MIF), uliowakutanisha Serikali, sekta binafsi, washirika wa maendeleo, taasisi za fedha, wanateknolojia, watafiti na asasi za kiraia uliolenga kujadili namna ya kuongeza kasi ya upatikanaji na matumizi ya nishati safi ya kupikia iliyo endelevu na nafuu kwa wananchi na taasisi.


“Licha ya kuwa na mkakati wa nishati safi ya kupikia, tusipowekeza katika kubadili mila na desturi zetu tutajikuta pale pale. Wakati tunasukuma matumizi ya teknolojia, tuwekeze pia katika kubadili mitazamo ya Watanzania kuhusu matumizi ya nishati safi ya kupikia,” amesema Mhe. Ndejembi.


Ameongeza kuwa mabadiliko hayo yanahitaji ushirikiano wa Serikali, taasisi na jamii yenyewe ili kuondoa mitazamo na desturi zinazoweza kuwa kikwazo katika kuhamia kwenye matumizi ya nishati safi ya kupikia.


Aidha, Mhe. Ndejembi amewasisitiza watendaji wa Wizara, Taasisi na sekta binafsi kulipa umuhimu suala la kuweka kipaumbele katika matumizi ya teknolojia mchanganyiko za nishati safi ya kupikia kulingana na rasilimali zinazopatikana katika maeneo husika mfano ni maeneo yenye upatikanaji wa samadi ambayo inaweza kutumika kuzalisha bayogesi ili kuongeza matumizi ya nishati safi ya kupikia.


Mhe. Ndejembi amempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa uwekezaji anaoufanya katika nishati safi ya kupikia ambapo ameiweka Tanzania katika nafasi ya kuonesha kuwa nishati safi ya kupikia si suala la matumizi ya kaya pekee, bali inagusa afya, mazingira, uchumi, usawa wa kijinsia, elimu na maendeleo endelevu.


Amesema tangu kuzinduliwa kwa Mkakati wa Nishati Safi ya Kupikia, Serikali imeongeza uelewa wa wananchi kupitia kampeni na maonesho ya nishati safi, sambamba na kuanzisha na kupanua miradi mbalimbali, ikiwemo utoaji wa ruzuku ya mitungi na majiko kwa kaya zilizopo vijijini na pembezoni mwa miji.


Hatua nyingine ni kuanzishwa kwa miradi ya kulipia majiko ya umeme kupitia bili za umeme (on-bill financing), ufungwaji wa mifumo ya nishati safi ya kupikia katika taasisi zinazolisha zaidi ya watu 100 kwa siku, pamoja na kupunguza Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) katika gesi, mitungi, matanki, mita janja za LPG na mashine za kutengeneza mkaa mbadala.


Amesema Serikali pia imeimarisha uratibu baina ya wizara na taasisi za Serikali, huku ushiriki wa sekta binafsi, asasi za kiraia na washirika wa maendeleo ukiendelea kuongezeka.


Kwa mujibu wa Waziri Ndejembi, mafanikio hayo yamechangia kuongezeka kwa idadi ya Watanzania wanaotumia nishati safi ya kupikia kutoka asilimia 6.9 mwaka 2021 hadi asilimia 28.6 mwaka 2025.


Ameongeza kuwa miongoni mwa maeneo yanayopewa msisitizo na Serikali ni kuwezesha taasisi zinazolisha zaidi ya watu 100 kwa siku, zikiwemo shule, hospitali, magereza, vyuo na vituo vya mafunzo, kuachana na matumizi ya kuni na mkaa na kuhamia kwenye nishati safi ya kupikia.


Ameeleza kuwa kwa sasa ni taasisi 2,616 pekee kati ya taasisi 31,395 zinazotumia nishati safi ya kupikia hali inayoonesha ukubwa wa kazi iliyopo mbele katika kufikia malengo yaliyowekwa.


Kutokana na ukubwa wa mahitaji hayo, Mhe. Ndejembi amesema mabadiliko hayawezi kufanikishwa kwa kutegemea bajeti ya Serikali pekee, hivyo kuna umuhimu wa kuimarisha ushirikiano na uhamasishaji wa rasilimali fedha (partnerships and resource mobilization).


Hivyo, ametoa wito kwa taasisi za fedha kubuni mikopo nafuu itakayowezesha shule, hospitali na taasisi nyingine kuwekeza katika nishati safi bila kulazimika kulipa gharama zote za awali kwa wakati mmoja.


Pia ameihimiza sekta binafsi kuja na mifumo bunifu ya kifedha, ikiwemo malipo kwa awamu na mikopo yenye masharti nafuu.


Vilevile, ametoa wito kwa washirika wa maendeleo kushirikiana na Serikali kufadhili miradi inayoweza kuzifikia taasisi nyingi zaidi, huku akisisitiza umuhimu wa kuhamisha miradi kutoka hatua za majaribio (pilots) kwenda kwenye uwekezaji wa kiwango kikubwa na wa muda mrefu.


Katika hatua nyingine, Mhe.Ndejembi ameipongeza Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kwa kuendelea na maandalizi ya Mkakati wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia wa Zanzibar akisema hatua hiyo inaonesha dhamira ya kuhakikisha wananchi wanapata nishati safi, salama, nafuu na endelevu ya kupikia.


Amesema Wizara ya Nishati ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania itaendelea kushirikiana kwa karibu na Wizara ya Maji, Nishati na Madini ya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar katika kufikia malengo hayo, ikiwemo kubadilishana uzoefu kuhusu utekelezaji wa mkakati, mifumo ya uratibu, uhamasishaji wa rasilimali, ushirikishwaji wa sekta binafsi, ukusanyaji wa takwimu na ufuatiliaji wa utekelezaji..


Vilevile ameipongeza MIF kwa kuifanya nishati safi ya kupikia kuwa miongoni mwa ajenda zake muhimu na kwa kuandaa mdahalo wenye mafanikio uliowakutanisha wadau muhimu wa nishati safi ya kupikia.






WMA DODOMA YAHAKIKI USAHIHI WA VIPIMO WA VYA MAJI NA VIFAA VYA MAZOEZI (GYM)

August 11, 2026 Add Comment

 

📍Dodoma - WMA

Meneja wa Wakala wa Vipimo (WMA) Mkoa wa Dodoma, Bw. Said Ibrahim, ameendelea na ziara ya kutoa elimu kwa wafanyabiashara pamoja na kukagua vipimo vinavyotumika katika biashara ya kuuza maji ya kunywa mtaani na vile vinavyotumika kwenye kumbi za mazoezi (Gym) jijini Dodoma tarehe 11 Agosti, 2026.

MIAKA 40 YA COSTECH: UTAFITI UNAVYOBADILI MAISHA YA WAFUGAJI

August 11, 2026 Add Comment
Clement akiwa na ng’ombe/eneo la malisho

*******************

MTANANA, KONGWA, DODOMA — Kwa miaka mingi, Clement Alfonce alifuga ng’ombe kwa kutegemea malisho ya asili. Ng’ombe wake walizunguka katika maeneo mbalimbali kutafuta malisho, hali iliyomweka katika migogoro ya mara kwa mara na majirani ambao mazao yao yaliathiriwa na mifugo hiyo.

Clement, mkazi wa Kijiji cha Mtanana katika Wilaya ya Kongwa, Mkoa wa Dodoma, alikuwa na ng’ombe 56. Lakini kuwa na mifugo mingi hakukuwa na maana ya kuwa na ufugaji wenye uhakika.

Wakati wa ukame, malisho yalipungua na hali ya mifugo ilidhoofika. Baadhi ya ng’ombe walikufa kipindi cha ukame. Wakati mwingine mifugo iliingia katika mashamba ya majirani, na Clement alilazimika kulipa faini.

Changamoto hiyo ilikuwa sehemu ya maisha yake ya kila siku.

Leo, hali imebadilika.

Clement amepunguza kwa kiasi kikubwa utegemezi wa ufugaji wa kufuatana na ng’ombe kutafuta malisho. Ameuza ng’ombe wake 50 na kununua ng’ombe 16 wa maziwa anaowafuga kwa mfumo malisho bandani.

Mabadiliko hayo yameambatana na jambo jingine muhimu: sasa Clement analima malisho yake mwenyewe.

Shamba lake la malisho limekuwa sehemu muhimu ya mfumo wake mpya wa ufugaji, na ana matumaini makubwa kwamba uzalishaji huo utampa chakula cha kutosha cha mifugo hata wakati wa ukame.

Mabadiliko hayo yamechochewa kwa kiasi kikubwa na maarifa aliyoyapata kupitia utafiti shirikishi unaofanywa na watafiti wa Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) kwa ufadhili wa Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH).

Utafiti huo, unaoongozwa na Dkt. Dorice Lutatenekwa, unahusisha tathmini ya aina mbalimbali za nyasi kwa lengo la kubaini uwezo wake wa kustahimili ukame na kutoa malisho yanayoweza kusaidia wafugaji katika mazingira yenye changamoto ya mabadiliko ya tabianchi.

Kwa Clement, ushiriki katika utafiti haukuwa suala la kusikia matokeo kutoka kwa wataalamu pekee. Alipata fursa ya kuona aina mbalimbali za malisho zikifanyiwa majaribio na kutathmini matokeo yake katika mazingira yake.

Kadiri alivyopata uelewa kuhusu uzalishaji wa malisho, ndivyo alivyobadilisha mtazamo wake kuhusu ufugaji.

Badala ya kujiuliza ng’ombe wake watapata wapi malisho, alianza kujenga uwezo wa kuzalisha chakula cha mifugo yake mwenyewe.

“Nilikuwa na ng’ombe wengi, lakini changamoto kubwa ilikuwa malisho, hasa wakati wa ukame. Mifugo ilikuwa ikiingia kwenye mashamba ya watu na nililazimika kulipa faini. Nilipojifunza kuhusu uzalishaji wa malisho na kuona matokeo ya utafiti, nikaona umuhimu wa kubadilisha mfumo wangu wa ufugaji.” Clement Alfonce, Mfugaji, Kijiji cha Mtanana B, Kongwa

Uamuzi wa Clement wa kuhamia kwenye ufugaji wa ng’ombe wa maziwa kwa mfumo wa malisho bandani unaonyesha namna utafiti unavyoweza kusaidia katika kufanya maamuzi ya uzalishaji katika ngazi ya kaya.

Badiliko hilo halimaanishi tu kwamba idadi ya ng’ombe wake imeshuka kutoka 56 hadi 16.Maana yake kubwa iko katika mabadiliko ya mfumo wa ufugaji.

Ng’ombe waliokuwa wakitegemea malisho yanayopatikana kwa kutangatanga sasa wana mfumo maalumu wa kulishwa. Clement anaweza kupanga uzalishaji wa malisho, matumizi yake na mahitaji ya mifugo yake.

Hii pia inapunguza utegemezi wa malisho ya asili ambayo hupungua wakati wa ukame.

Utafiti wenye mantiki shambani

Maisha ya Clement inaonyesha changamoto kubwa inayokabili sayansi katika nchi nyingi, na namna ya kuhakikisha kwamba maarifa yanayozalishwa na watafiti yanafika kwa watu wanaohitaji kuyatumia.

Katika utafiti wa Mtanana, wafugaji wameshirikishwa katika mchakato wa kujifunza na kutathmini aina za malisho zinazofanyiwa majaribio.

Katika ziara ya kutathmini maendeleo ya utafiti huo, Dkt. Lutatenekwa alimweleza Mkurugenzi Mkuu wa COSTECH, Dkt. Amos Nungu, matokeo ya awali ya utafiti na namna wafugaji wanavyoshiriki katika mchakato huo.

Ziara hiyo ilitoa picha ya tofauti kati ya utafiti unaobaki kwenye ripoti na utafiti unaoanza kubadili namna watu wanavyozalisha.

Katika eneo la utafiti kulionekana malisho yanayofanyiwa tathmini, mashamba ya wakulima na wafugaji wanaojaribu kutumia maarifa hayo katika mifumo yao ya uzalishaji.

Kwa COSTECH, uzoefu huo unaendana na umuhimu wa kuwekeza katika utafiti unaozalisha maarifa yenye matumizi kwa jamii na uchumi.

Katika mahojiano yake waandishi wa habari wakati wa ziara hiyo, Dkt. Nungu alisisitiza umuhimu wa kuhakikisha kuwa matokeo ya utafiti na teknolojia yanawafikia watumiaji wa mwisho na kusaidia kutatua changamoto halisi zinazowakabili wananchi.

“Tunataka utafiti uzalishe maarifa au utoe teknolojia ambazo zitakuwa suluhui kwa changamoto za watanzania. Mradi huo tumeona unavyobadili maisha ya Mfugaji Bw.Clement Alfonce, tunataka uwe na matokeo makubwa na chanya kwa wafugaji wote zaidi ya 1300 waliopo kwenye kata hii ya Mtanana” Dkt. Amos Nungu, Mkurugenzi Mkuu, COSTECH

Mabadiliko ya tabianchi yanabadilisha namna ya kufuga

Kongwa ni miongoni mwa maeneo ambayo wafugaji wanakabiliwa na changamoto ya upatikanaji wa malisho, hasa katika vipindi vya ukame.

Kwa mifugo inayotegemea malisho ya asili, ukame unaweza kumaanisha kupungua kwa chakula, kudhoofika kwa mifugo na hata vifo.

Katika mazingira hayo, uwezo wa mfugaji kuzalisha malisho yanayostahimili ukame unaweza kuwa sehemu ya mkakati mpana wa kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi.

Ndiyo maana utafiti wa aina hii una umuhimu zaidi ya kutafuta aina nzuri ya nyasi. Unahusu usalama wa chakula cha mifugo, ustahimilivu wa mifumo ya uzalishaji na uwezo wa kaya za wafugaji kukabiliana na mabadiliko ya mazingira.

Kwa Clement, mwanga umeanza kuonekana.

Shamba lake la malisho linampa nafasi ya kupanga zaidi kuhusu chakula cha mifugo yake. Mfumo wa malisho bandani unapunguza hitaji la ng’ombe kuzunguka kutafuta malisho na hivyo kupunguza uwezekano wa migogoro inayotokana na mifugo kuingia kwenye mashamba ya wakulima.

Na muhimu zaidi, Clement sasa anaona ufugaji kama mfumo wa uzalishaji unaoweza kupangwa na kusimamiwa, badala ya kutegemea upatikanaji wa malisho ya asili.

Miaka 40 ya COSTECH: kipimo ni maisha yanayobadilika

Tanzania inapoadhimisha miaka 40 ya COSTECH, hadithi ya Clement inaibua swali muhimu kuhusu maana ya uwekezaji katika sayansi, teknolojia na ubunifu.

Matokeo ya utafiti hayaishii katika maabara, ripoti au machapisho ya kitaalamu.Thamani yake inaonekana zaidi pale ambapo maarifa yanatumiwa kufanya uamuzi mpya.

Kwa Clement, uamuzi huo ulikuwa kubadilisha mfumo wa ufugaji. Kutoka kuwa na ng’ombe 56 wanaozunguka kutafuta malisho, sasa ana ng’ombe 16 wa maziwa wanaofugwa ndani.Kutoka kutegemea zaidi malisho yanayopatikana kwenye nyanda za malisho, sasa analima malisho kwa ajili ya mifugo yake. Kutoka kukabiliana mara kwa mara na migogoro ya mifugo na wakulima, sasa ana mfumo wa ufugaji unaomruhusu kudhibiti zaidi mahitaji ya mifugo yake.

Na kutoka kukabili ukame bila uhakika wa chakula cha mifugo, sasa anajenga msingi wa uzalishaji wa malisho unaoweza kumsaidia kukabiliana na changamoto hiyo.

Hii ndiyo picha pana ya miaka 40 ya COSTECH: sayansi inapokuwa na maana pale inapobadilisha uwezo wa Mtanzania kutatua changamoto yake mwenyewe.

Katika Mtanana, mabadiliko hayo hayajaandikwa tu kwenye ripoti. Yanaonekana kwenye shamba.Yanaonekana kwenye malisho. Yanaonekana kwenye banda la ng’ombe. Na yanaonekana katika uamuzi wa mfugaji mmoja kubadilisha kabisa namna anavyofuga.

Clement hakubadilisha tu idadi ya ng’ombe alionao. Alibadilisha mfumo wa maisha unaowaendesha. Kutoka ng’ombe wa kuzunguka kutafuta malisho hadi ng’ombe wa kufugia ndani.Kutoka kutegemea malisho asili hadi kuanza kuzalisha chakula cha mifugo yake.

Na nyuma ya mabadiliko hayo kuna jambo moja: maarifa yaliyotokana na utafiti.

MIAKA 40 YA COSTECH: MKURUGENZI MKUU AKAGUA MIRADI YA UTAFITI KUKABILIANA NA MABADILIKO YA TABIANCHI

August 11, 2026 Add Comment
Clement Alfonce akizungumza na ITV akiwa shambani

TUME YABAINISHA MATAMANIO YA SERIKALI KULINDA AFYA NA USALAMA WA WATUMISHI WA UMMA

August 11, 2026 Add Comment
Katibu wa Tume ya Utumishi wa Umma, Nolasco Kipanda, akifungua mafunzo ya usalama na afya mahali pa kazi kwa wakaguzi wa Tume hiyo yaliyoandaliwa na Wakala wa Usalama naAfya Mahali pa Kazi (OSHA) kwa lengo la kuwajengea uelewa wakaguzi hao wenye jukumu la kukagua uzingatiaji wa sheria na miongozo mbalimbali katika sekta ya umma.

KAPINGA ABAINISHA KUUZA MAZAO GHAFI NI HASARA

August 10, 2026 Add Comment
Serikali imekusudia kukomesha uuzaji wa mazao ghafi kwani mfumo huo unamnyima mkulima zaidi ya nusu ya faida halisi na kubainisha kuwa mkakati uliopo ni kuongeza thamani ya mazao kama korosho kabla ya kuyaweka sokoni, hatua itakayoinua kipato cha wajasiriamali na wakulima wadogo mkoani humo.

WAZIRI KAPINGA AAGIZA MIRADI YOTE YA MAENDELEO KUKAMILIKA KWA WAKATI

August 10, 2026 Add Comment
Serikali imetoa agizo kwa wakandarasi na wasimamizi wa miradi ya maendeleo katika Halmashauri ya Mji wa Masasi kuhakikisha miradi yote inakamilika ndani ya muda uliopangwa, na kusisitiza kuwa utamaduni wa kuongeza muda wa utekelezaji (extension) hauleti tija wala maendeleo kwa Taifa.

KAPINGA: ZAMA ZAKUFUNGIA BIASHARA ZIMEPITWA NA WAKATI.

August 10, 2026 Add Comment
Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Judith Kapinga (Mb), amewataka watendaji wa Serikali na taasisi za udhibiti kuwa wawezeshaji wa biashara badala ya kufungia biashara, akisema hatua hiyo ni muhimu katika kulinda mitaji na maslahi ya wananchi.

WADAU WA SEKTA YA FEDHA WAJADILI MUSTAKABALI WA BENKI ZA KIDIJITALI

Kajunason August 10, 2026 Add Comment

 

EY Tanzania imezindua kwa mafanikio Ripoti ya Sekta Ndogo ya Benki Tanzania 2025, tukio lililowakutanisha viongozi wa sekta ya fedha, wadhibiti na wataalamu wa benki kujadili mwelekeo wa sekta hiyo katika mazingira yanayobadilika kwa kasi. Mada kuu ya mwaka huu ilikuwa“Akili Mnemba katika Sekta ya Benki: Faida ya Ushindani Ijayo”, ikilenga kuonesha jinsi Akili Mnemba (AI) inavyobadilisha ushindani katika huduma za kifedha.
Majadiliano hayo yaliongozwa na Bi. Irene Morris (EY) ambapo aligusia safari ya mageuzi ya sekta ya benki kutoka mifumo ya jadi inayotegemea mahusiano ya karibu na wateja (relationship banking) hadi benki za kidijitali, majukwaa ya kifedha (platform banking) na mifumo ya ikolojia ya huduma za kifedha (ecosystem banking). Washiriki walijadili namna AI, data na teknolojia vinavyoboresha uzoefu wa wateja, kuimarisha usimamizi wa hatari, kuongeza ufanisi wa shughuli za benki na kuibua fursa mpya za ukuaji wa biashara.

Tukio hilo pia liliangazia mwenendo muhimu unaoendelea kuunda sekta ya benki nchini Tanzania, ikiwemo ukuaji endelevu wa sekta, kuongezeka kwa ujumuishaji wa kifedha, matumizi yanayoongezeka ya huduma za kifedha za kidijitali, pamoja na umuhimu wa ubunifu katika kujenga taasisi za kifedha zilizo imara na zenye uwezo wa kukabiliana na mahitaji ya siku zijazo.
Aidha, washiriki walipata fursa ya kujadili kiwango kipya cha utoaji taarifa za kifedha (IFRS 18) na athari zake kwa sekta ya benki. Majadiliano yalioongozwa na Bw. Joshua Luoga (EY) ambapo alitoa ufahamu kuhusu mabadiliko yajayo katika uwasilishaji wa taarifa za kifedha, upimaji wa utendaji wa kifedha pamoja na kuongeza uwazi kwa wadau wa sekta ya fedha.
EY Tanzania inawashukuru kwa dhati wazungumzaji, (Bw. Rweyemamu Barongo, Kiongozi wa Kitengo cha Ubunifu wa Akili Mnemba (AI) na Data katika Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Dkt. Tobias Swai, Mhadhiri Mwandamizi na Mkuu wa Idara ya Fedha katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) Pamoja na Bw. Robert Bwana, Mwanasayansi Mwandamizi wa Data katika Benki ya NMB) washiriki na wadau wote waliochangia mjadala wenye tija kuhusu mustakabali wa sekta ya benki nchini Tanzania na nafasi ya teknolojia na ubunifu katika kuendeleza ukuaji wa sekta hiyo.

ZOEZI LA UVUTAJI NYAYA AWAMU YA PILI ENEO LA KIKOMBO NA MKONZE KATIKA MRADI WA CHALINZE-DODOMA KUANZA KESHO

August 10, 2026 Add Comment




📌TANESCO yasema baadhi ya Mikoa ya Kanda ya Kati, Kanda ya Magharibi, Kanda ya Kaskazini, Kanda ya Kusini Magharibi na Kanda ya ziwa kupata umeme kwa ratiba maalumu


📌Lengo ni kumpisha Mkandarasi kuendelea na utekelezaji wa Mradi huo wa kusafirisha umeme Msongo wa Kilovolti 400  ambao uko mbioni kukamilika.


Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) limewakumbusha wananchi kuwa, kuanzia Agosti 11 hadi 17, 2026, mkandarasi anayetekeleza Mradi wa Kusafirisha Umeme wa Msongo wa Kilovolti 400 Chalinze–Dodoma ataendelea na zoezi la uvutaji wa nyaya kwa awamu ya pili katika eneo la Kikombo na Mkonze, Dodoma, katika mradi huo ambao uko mbioni kukamilika.


Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano na Huduma kwa Wateja, Bi. Irene Gowelle, amesema hatua hiyo imekuja baada ya awamu ya kwanza ya uvutaji wa nyaya kutoka Chalinze hadi Mkambarani, Morogoro, kufanyika kwa mafanikio makubwa.


Amesema kutokana na kazi hiyo, baadhi ya mikoa itapata umeme kwa ratiba maalumu. Mikoa hiyo ni ile inayopatikana katika Kanda ya Kati, Kanda ya Magharibi, Kanda ya Kaskazini, Kanda ya Kusini Magharibi na Kanda ya Ziwa. Aidha, amesisitiza kuwa mikoa ambayo haitaathirika katika kanda hizo ni pamoja na Morogoro na Tanga.


Ameongeza kuwa mikoa inayotoka katika  Kanda hizo  zitakosa umeme kuanzia saa 12:00 asubuhi hadi saa 11:00 jioni. Hatua hiyo ni sehemu ya jitihada za kukamilisha mradi huo, ambao unatarajiwa kuwa na mchango chanya katika kuimarisha mfumo wa usafirishaji na upatikanaji wa umeme nchini.


‘’Hii ni awamu ya pili ya zoezi la uvutaji wa nyaya katika eneo la Kikombo na Mkonze Mkoani Dodoma, niwaondoe hofu wananchi kwamba tutaendelea kutoa ratiba za upatikanaji wa umeme kupitia mitandao yake ya kijamii, ili kuwawezesha wananchi kupanga shughuli zao kulingana na ratiba hiyo’’alisisitiza Bi. Gowelle.



Mradi wa Njia ya Kusafirisha Umeme wa Msongo wa Kilovolti 400 kutoka Chalinze hadi Dodoma unatarajiwa kukamilika Agosti 21, 2026. Kukamilika kwake kutaongeza uwezo wa mfumo wa usafirishaji wa umeme nchini na kuimarisha upatikanaji wa huduma ya umeme yenye ubora na uhakika kwa wananchi.

NDEJEMBI AWASHA UMEME MWANUBI, ASEMA UMEME NI HITAJI LA MSINGI KWA WATANZANIA

August 10, 2026 Add Comment

 


📌 Ahimiza wananchi kuunganishiwa huduma ya umeme na kuitumia kuongeza tija

📌 Shule, zahanati na maeneo mengine ya huduma za kijamii kupewa kipaumbele

Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi, amewasha umeme katika Kitongoji cha Mwanubi mkoani Shinyanga na kusema kuwa huduma ya umeme ni hitaji la msingi kwa Watanzania na nyenzo muhimu katika kuchochea maendeleo ya kiuchumi na kijamii.

Akizungumza wakati wa hafla ya kuwasha umeme katika kitongoji hicho, Mhe. Ndejembi amesema kufikishwa kwa umeme vijijini kunapaswa kwenda sambamba na matumizi yenye tija, ikiwemo kuongeza thamani ya mazao, kuendeleza biashara na shughuli za uzalishaji pamoja na kuboresha utoaji wa huduma za kijamii.

Amesema Serikali inaendelea kuhakikisha wananchi wengi zaidi wanafikiwa na huduma ya umeme, hususan katika maeneo ya vijijini, ili nishati hiyo iwe kichocheo cha uzalishaji, ongezeko la kipato na uboreshaji wa maisha ya wananchi.

Mhe. Ndejembi amewahimiza wananchi ambao miundombinu ya umeme imewafikia kuchangamkia fursa hiyo kwa kuunganishiwa huduma kwa gharama nafuu ya shilingi 27,000, na kutumia umeme katika shughuli mbalimbali za uzalishaji na kujiletea maendeleo.

Aidha, ameiagiza Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kufanya tathmini ya maeneo ambayo bado hayajafikiwa na miundombinu ya umeme ili yaingizwe katika mipango ya utekelezaji na kufikishiwa huduma hiyo.

Pia, amewataka wakandarasi wanaotekeleza miradi ya umeme kuongeza kasi ya kusimika nguzo na kujenga miundombinu katika maeneo yaliyosalia ili wananchi wengi zaidi waweze kufikiwa na kuunganishiwa huduma ya umeme.

Amesisitiza kuwa shule, zahanati na maeneo mengine muhimu ya kutolea huduma za kijamii yanapaswa kupewa kipaumbele katika kufikishiwa umeme ili kuongeza ufanisi na kuboresha huduma zinazotolewa kwa wananchi.

Aidha Serikali chini ya uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, inaendelea kutekeleza miradi mbalimbali ya uzalishaji, usafirishaji na usambazaji wa umeme katika maeneo mbalimbali nchini kwa lengo la kuhakikisha Watanzania wanapata nishati ya uhakika.

Ameeleza kuwa uwekezaji huo unalenga kuwezesha wananchi kutumia umeme katika shughuli za uzalishaji, kuongeza thamani ya mazao, kukuza biashara, kuongeza fursa za ajira na kuboresha huduma za kijamii.

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Mboni Mhita ameishukuru Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kufikisha huduma ya umeme katika vijiji vyote vya Mkoa wa Shinyanga, akieleza kuwa hatua hiyo imefungua fursa mbalimbali za maendeleo kwa wananchi.

Amesema upatikanaji wa umeme katika maeneo ya vijijini umeendelea kubadilisha maisha ya wananchi kwa kuchochea shughuli za kiuchumi, kuongeza fursa za uzalishaji na ajira pamoja na kuboresha upatikanaji wa huduma muhimu za kijamii.

Naye, Mwakilishi wa Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mha. Herini Mhina, amesema Wakala unaendelea kutekeleza miradi ya kufikisha huduma ya umeme katika vitongoji mbalimbali nchini ili kuhakikisha wananchi wengi zaidi, hususan katika maeneo ya vijijini, wanapata huduma hiyo.

Mha. Mhina amesema REA itaendelea kusimamia kwa karibu utekelezaji wa miradi hiyo ili kupanua wigo wa upatikanaji wa umeme na kuwawezesha wananchi kutumia nishati hiyo katika shughuli za kiuchumi, uzalishaji na utoaji wa huduma za kijamii.

Nao wananchi wa Kitongoji cha Mwanubi wameishukuru Serikali kwa kuwafikishia huduma ya umeme katika kitongoji chao, wakieleza kuwa hatua hiyo itachochea shughuli za kiuchumi na kijamii na kuboresha maisha yao.

Wamesema ujio wa umeme utafungua fursa mpya za biashara na uzalishaji, kuongeza thamani ya mazao pamoja na kuboresha upatikanaji wa huduma muhimu katika eneo hilo.

Hafla ya kuwasha umeme katika Kitongoji cha Mwanubi ni sehemu ya jitihada za Serikali kupitia REA za kupanua wigo wa upatikanaji wa umeme vitongojini na kuhakikisha nishati hiyo inakuwa kichocheo cha maendeleo endelevu ya wananchi.

WANDONDI, WANDWEWE WATOA WITO WA KULINDA MAISHA NA AMANI

Kajunason August 10, 2026 Add Comment


Na Mwandishi Wetu.

JAMII ya Wandondi na Wandwewe, imetoa mwito wa kitaifa na kimataifa kwa watu wote wenye nia njema kuungana katika Dua Maalum kwa ajili ya Amani, Umoja, Maridhiano, Mshikamano na Ulinzi wa Maisha ya Binadamu.

Dua hiyo ni mwito wa pamoja unaolenga kuwakutanisha watu wa imani, mila, tamaduni na mitazamo mbalimbali katika kusimama kwa pamoja kutetea amani, utu, uhai, mshikamano na heshima kwa mwanadamu, bila kujali tofauti za dini, kabila, rangi, taifa, utamaduni, itikadi au hali ya kijamii.

Taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari na Chifu Felix G. L. Mfunda, kwa niaba ya jamii ya Wandondi na Wandwewe amesema dua hiyo itafanyika  Agosti 12, 2026,  ambapo Misa Maalumu ya Kikatoliki itafanyika katika Kanisa Katoliki, Kigango cha Mhangazi, Parokia ya Kitanda, Namtumbo, Ruvuma. huku akitoa  mwito wa amani na maridhiano.

Aidha, kuanzia jioni ya Agosti 13 hadi mchana wa Agosti 14, 2026, kutafanyika dua, na shughuli za jadi zitakazoambatana na ngoma na sanaa mbalimbali za asili za Wandwele na Wandondi.

Jamii mbalimbali za Mkoa wa Ruvuma, zikiwemo Makumbo, Lizombe na Makiwa, zinatarajiwa kushiriki katika shughuli hizo zinazolenga kuenzi urithi wa tamaduni, kuimarisha undugu na mshikamano, pamoja na kukuza amani kati ya jamii.

Mfululizo huo utakamilishwa Agosti 16, 2026, kwa Dua Maalumu ya Kiislamu itakayofanyika jioni kwa ajili ya kuiombea Tanzania, Afrika na dunia nzima.
Ambapo  amesema Dunia ya leo inakabiliwa na changamoto mbalimbali zikiwemo migogoro, vita, chuki, migawanyiko ya kijamii, changamoto za kiuchumi, ukosefu wa usawa na athari za mabadiliko ya tabianchi.

“Katika mazingira haya, tunapaswa kutambua kwamba amani si wajibu wa Serikali pekee; ni wajibu wa kila mwanadamu.Tunatoa mwito kwa viongozi wa kitaifa na kimataifa, viongozi wa dini, viongozi wa kimila, wasomi, vijana, wanawake, mashirika ya kiraia na wananchi wote kutumia nafasi zao kujenga madaraja ya maelewano badala ya kuta za migawanyiko.

“Tunasisitiza umuhimu wa mazungumzo, kusikilizana, kusameheana, kuheshimiana na kutafuta suluhu za amani katika kila tofauti inayojitokeza.”

Aidha amesema ulinzi wa maisha ni wajibu wa pamoja akifafanua maisha ya mwanadamu ni tunu kubwa na hayapaswi kuwekwa rehani kwa sababu ya tofauti za kisiasa, kidini, kikabila, kiuchumi, kijamii au kiitikadi.

Ameongeza kwa msingi huo, wanatoa mwito wa kuheshimiwa kwa utu wa binadamu, haki ya kuishi, usalama wa raia na ulinzi wa watoto, wanawake, wazee na makundi yote yaliyo katika mazingira hatarishi.

“Tunasisitiza tofauti zetu zisigeuke kuwa sababu ya kupoteza maisha ya watu.Kila jamii ina wajibu wa kulinda maisha na kujenga mazingira ambayo kila mwanadamu anaweza kuishi kwa usalama.

Pia amesema kuhusu amani, afya na ulinzi wa mazingira ni kwamba amani ya kweli haiwezi kutenganishwa na afya ya jamii, usalama wa chakula, maji safi, mazingira salama na matumizi endelevu ya rasilimali za asili.

“Uharibifu wa mazingira, ukataji wa misitu, uharibifu wa vyanzo vya maji, upotevu wa bayoanuai na athari za mabadiliko ya tabianchi vinaweza kuongeza changamoto za kijamii na kiuchumi na kuhatarisha maisha ya watu.

“Kwa hiyo, tunatoa mwito wa kuunganisha juhudi za amani, afya, mazingira na maendeleo endelevu kwa ajili ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo.

Akieleza zaidi amesema katika dua kwa Watanzania ,Afrika na Dunia amefafanua Tanzania iendelee kuwa taifa la amani, umoja, mshikamano na utulivu na kwa Afrika ipate amani na utulivu wa kudumu.

Pia migogoro na vita duniani zipungue na hatimaye kumalizika na kuongeza viongozi wapate hekima, busara, uadilifu na moyo wa kuhudumia watu.Vijana wapate fursa za elimu, ajira, ubunifu, ujasiriamali na maendeleo.

Kwa watoto walindwe dhidi ya ukatili, unyanyasaji na mazingira yanayohatarisha maisha yao. Wanawake, wazee na makundi yaliyo katika mazingira magumu walindwe na kuheshimiwa.Wagonjwa na wote wanaokabiliwa na changamoto mbalimbali wapate faraja, matumaini na huduma stahiki na mazingira.

Kuhusu ujumbe kwa Watanzania amesema wanawakumbusha Umoja wetu ni nguvu yetu, amani yetu ni utajiri wetu, na maisha ya kila Mtanzania ni sehemu ya thamani ya Taifa letu.

“Tunapaswa kukataa chuki, uchochezi, ubaguzi, vurugu na lugha zinazogawa jamii. Badala yake, tujenge utamaduni wa kusikilizana, kuheshimiana, kusameheana, kusaidiana na kutatua tofauti zetu kwa njia za amani.

“Tanzania yenye amani na mshikamano ni msingi muhimu wa maendeleo ya watu wake na mchango mkubwa kwa amani ya Afrika na dunia.”

SERIKALI YAMTAKA MKANDARASI KUONGEZA KASI UJENZI WA BARABARA YA KAHAMA-KAKOLA UNAOWEZESHWA NA MIGODI YA BARRICK NCHINI

August 10, 2026 Add Comment

  

Waziri wa Nishati na Mlezi wa Mkoa wa Shinyanga Kiserikali, Mhe. Deogratius Ndejembi akiongozana na Mkuu wa mkoa wa Shinyanga, Mhe. Mboni Mhita na viongozi wengine wa serikali kukagua mradi wa barabara ya Kahama–Bulyanhulu Jct–Kakola unaowezeshwa na migodi ya Barrick-Twiga nchini.
Sehemu ya barabara iliyowekwa lami katika Mradi wa Barabara ya Kahama–Bulyanhulu Jct–Kakola, unaowezeshwa na migodi ya Barrick-Twiga nchini Tanzania.

MAHAKAMA YA RUFAA YAIPA USHINDI IPTL, PAP KATIKA USD 168M MGOGORO DHIDI YA STANDARD CHARTERED

August 10, 2026 Add Comment

  


Na Mwandishi Wetu

Mahakama ya Rufani ya Tanzania imezipa gharama za kisheria Kampuni ya Independent Power Tanzania Limited - IPTL na Pan Africa Power Solutions (T) Limited ya Dola za Kimarekani 8,000,000 kufuatia kufanikiwa kupinga rufaa iliyokatwa na Benki ya Standard Chartered kuhusu mgogoro wa kibiashara wa muda mrefu wa dola za Marekani 168,000,000.

SERIKALI KUJA NA MRADI MAALUMU WA KUSAMBAZA UMEME KWENYE MAENEO YA UZALISHAJI

August 10, 2026 Add Comment




KAHAMA, SHINYANGA


Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi, Serikali inaandaa mradi maalumu wa kusambaza umeme katika maeneo ya uzalishaji, hususan maeneo yenye shughuli za uchimbaji wa madini, kwa lengo la kuwawezesha wazalishaji kutumia nishati ya uhakika na kupunguza utegemezi wa dizeli.


Mhe. Ndejembi ameyasema hayo wakati akijibu swali la Mbunge wa Jimbo la Msalala, Mhe. Mabula Magangila, aliyeomba Serikali kupeleka umeme katika maeneo ya uzalishaji, akieleza kuwa baadhi ya wachimbaji madini katika jimbo hilo bado wanatumia dizeli kuendesha shughuli zao za uzalishaji.


Mbunge huyo pia ameieleza Serikali kuwa vitongoji 98 katika Jimbo la Msalala bado havijaunganishwa na huduma ya umeme.

Akijibu hoja hiyo, Mhe. Ndejembi amesema Serikali tayari imeanza maandalizi ya utekelezaji wa mradi huo maalumu kwa kushirikiana na Wizara ya Madini, ambao utalenga kusogeza huduma ya umeme moja kwa moja kwenye maeneo yenye shughuli za uzalishaji, hususan maeneo ya migodi.


Amesema hatua hiyo inalenga kuongeza tija katika uzalishaji, kupunguza gharama zinazotokana na matumizi ya dizeli pamoja na kuwawezesha wachimbaji na wazalishaji kutumia nishati ya umeme iliyo nafuu, ya uhakika na endelevu.

Kuhusu upatikanaji wa umeme vijijini katika Jimbo la Msalala, Mhe. Ndejembi amesema vijiji vyote tayari vimefikiwa na huduma ya umeme, huku Serikali ikiendelea na jitihada za kuwafikishia huduma hiyo wananchi waliopo katika vitongoji ambavyo bado havijaunganishwa, ikiwemo vitongoji 98 vilivyotajwa.


Aidha, akizungumzia upatikanaji wa umeme katika Jimbo la Kahama Mjini, Mhe. Ndejembi amesema tayari amefanya mazungumzo na Mbunge wa Jimbo hilo, Mhe. Benjamini Ngaiwa, kwa lengo la kubainisha maeneo yaliyopo ndani ya Manispaa ya Kahama ambayo, licha ya kuwa ndani ya eneo la mjini, yana sifa na taswira za maeneo ya vijijini.

Amesema maeneo hayo yataangaliwa ili yaweze kunufaika na utaratibu wa Serikali wa kuunganishiwa umeme kwa gharama ya Shilingi 27,000 kwa mteja, kama ilivyoelekezwa.

Mhe. Ndejembi amesema Serikali itaendelea kuweka kipaumbele katika upanuzi wa miundombinu ya umeme na kuhakikisha nishati inafika katika maeneo yenye shughuli za kiuchumi na uzalishaji, ili kuongeza tija, kuchochea uwekezaji na kuboresha maisha ya wananchi.