HABARI

SIASA

ELIMU

Recent Posts

USHIRIKIANO WA ADEM NA PROJECT ZAWADI KUINUA UONGOZI NA USIMAMIZI WA ELIMU MKOANI MARA

February 02, 2026 Add Comment
Katika jitihada za kuboresha sekta ya elimu nchini Tanzania, ADEM na Taasisi ya Project Zawadi wameingia makubaliano ya ushirikiano utakaowezesha kuendesha mafunzo ya muda mfupi kuhusu uongozi, usimamizi na uendeshaji wa elimu kwa viongozi wa Mkoani Mara.

DC NYAMWESE ATAKA MASHAURI YA ARDHI YASIKILIZWE HARAKA KUCHOCHEA MAENDELEO HANDENI

DC NYAMWESE ATAKA MASHAURI YA ARDHI YASIKILIZWE HARAKA KUCHOCHEA MAENDELEO HANDENI

February 02, 2026 Add Comment

Mkuu wa Wilaya ya Handeni, Mhe. Salum Nyamwese,akizungumza wakati wa maadhimisho ya Siku ya Sheria yaliyofanyika katika Mahakama ya Wilaya ya Handeni leo Februari 2,2026.

Na Augusta Njoji

Mkuu wa Wilaya ya Handeni, Mhe. Salum Nyamwese, ametoa rai kwa Mahakama ya Wilaya ya Handeni kutoa kipaumbele katika usikilizwaji wa mashauri yanayohusu ardhi ili yahitimishwe kwa wakati na kuchochea maendeleo ya wananchi.

Akizungumza wakati wa maadhimisho ya Siku ya Sheria yaliyofanyika katika Mahakama ya Wilaya ya Handeni, Mhe. Nyamwese amesema migogoro ya ardhi imekuwa ikichukua muda mrefu kusikilizwa pindi inapofikishwa mahakamani, hali inayosababisha kucheleweshwa kwa utekelezaji wa shughuli za maendeleo.

Amesema ardhi ni rasilimali muhimu katika Wilaya ya Handeni, lakini imeendelea kukumbwa na migogoro mingi, ambayo baadhi yake haina tija kwa maendeleo ya jamii.

Amesisitiza kuwa haki inapocheleweshwa, maendeleo nayo hucheleweshwa, hususan pale wananchi wanapokusudia kutumia ardhi kwa uwekezaji au shughuli za uzalishaji.

“Sisi kama Wilaya tumekuwa na migogoro ya ardhi, lakini inapofika mahakamani mashauri haya huchukua muda mrefu kusikilizwa. Hali hii inawaathiri wananchi na kudumaza maendeleo kwa ujumla,” amesema Mhe. Nyamwese.

Aidha, amepongeza hatua zilizochukuliwa na Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kuboresha utendaji wa Mahakama, ikiwemo ujenzi wa miundombinu ya mahakama karibu na wananchi pamoja na matumizi ya teknolojia, hatua zinazoongeza imani ya wananchi katika mfumo wa utoaji haki.

Kwa upande wake, Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Wilaya ya Handeni, Joseph Waruku, amesema Mahakama imeendelea kusogeza huduma karibu na wananchi kwa kuanzisha Mahakama za Mwanzo 12 mwaka 2025 katika maeneo yenye msongamano wa mashauri, ikiwemo Mahakama ya Mwanzo Msomera.

Naye, Mwakilishi wa Mwanasheria wa Halmashauri ya Mji Handeni, Regina Pangah, amesema Mahakama zina mchango mkubwa katika ustawi wa jamii na ukuaji wa uchumi kwa kuhakikisha haki inapatikana kwa wakati, huku akiahidi kuendeleza ushirikiano katika kutoa elimu ya sheria kwa wananchi.

RC MAKAME AIPONGEZA REA KUWAPELEKEA UMEME WATEJA 6,135 SONGWE

February 02, 2026 Add Comment



📌Vitongoji 173 kupelekewa umeme kwa bilioni 28.3

📌Mkandarasi atakiwa kutekeleza mradi kwa kasi

📍Songwe

Mkuu wa Mkoa wa Songwe, Mhe. Jabiri Makame ameishukuru Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA), kwa kutoa kiasi cha shilingi bilioni 28.3 kupeleka umeme kwa wateja 6,135   waliopo kwenye vitongoji 173 mkoani humo.

RC Makame ametoa pongezi hizo leo Februari 2, 2026 mara baada ya kukutana na Wataalam kutoka REA waliofika kumtambulisha mkandarasi wa mradi wa HEP 2B kampuni ya M/s Jaitech Company Ltd atakayetekeleza mradi wa kupeleka umeme vitongojini.

"Namshukuru sana Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kutuletea fedha hizi ili kupeleka umeme kwa wananchi wapatao 6,135 wa mkoa huu ili watumie nishati ya umeme," Amesema RC Makame.

Vilevile, amemtaka mkandarasi wa mradi kutekeleza mradi huo kwa kasi na weledi kwa kuwa wananchi wanamatumaini ya kuwashiwa umeme huo mapema ili waendelee na shughuli za kiuchumi na kuwaletea maendeleo.

Kwa upande wake, Mwakilishi wa Mkurugenzi Mkuu wa REA, Bw. Frank Mugogo ameeleza kuwa REA itaendelea kutekeleza miradi ya nishati ya umeme vijijini kwa ubora na uhakika ili wananchi wapate umeme wa uhakika. 


TUIBADILISHE HOFU YA WANANCHI KUWA UELEWA – WAZIRI MCHENGERWA

February 02, 2026 Add Comment

Na WAF, Dar es Salaam

Waziri wa Afya, Mhe. Mohamed Mchengerwa, amesema wahariri wa vyombo vya habari wana jukumu muhimu la kubadilisha hofu ya wananchi kuwa uelewa sahihi kuhusu Bima ya Afya kwa Wote, ili waweze kunufaika kikamilifu na huduma za afya.

WAKANDARASI WA KUSAMBAZA UMEME WATAKIWA KWENDA NA KASI YA SERIKALI

February 02, 2026 Add Comment
-Lengo ni kufikisha umeme kwenye vitongoji vyote nchini ifikapo 2030

MRADI WA KUPELEKA UMEME KWENYE VITONGOJI KUCHOCHEA UCHUMI, VIWANDA NA BIASHARA

February 02, 2026 Add Comment

    

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Mboni Mhita akizungumza wakati wa utambulisho wa mkandarasi kampuni ya Derm Group Ltd atakayetekeleza mradi wa kupeleka umeme kwenye vitongoji 581 kwa gharama ya shilingi bilioni 60.9 mkoani Shinyanga

  

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Mboni Mhita akizungumza wakati wa utambulisho wa mkandarasi kampuni ya Derm Group Ltd atakayetekeleza mradi wa kupeleka umeme kwenye vitongoji 581 kwa gharama ya shilingi bilioni 60.9 mkoani Shinyanga
Msimamizi wa Miradi ya REA Kanda ya Magharibi Mhandisi Robert Dulle akizungumza wakati wa utambulisho wa mkandarasi kampuni ya Derm Group Ltd atakayetekeleza mradi wa kupeleka umeme kwenye vitongoji 581 kwa gharama ya shilingi bilioni 60.9 mkoani Shinyanga
Msimamizi wa Miradi ya REA Kanda ya Magharibi Mhandisi Robert Dulle akizungumza wakati wa utambulisho wa mkandarasi kampuni ya Derm Group Ltd atakayetekeleza mradi wa kupeleka umeme kwenye vitongoji 581 kwa gharama ya shilingi bilioni 60.9 mkoani Shinyanga
Meneja wa Kampuni ya Derm Group (T) LTD Mhandisi Musa Abdallah akizungumza wakati wa utambulisho huo
Meneja wa TANESCO Mkoa wa Shinyanga Mhandisi Hadija Mbaruku akizungumza wakati wa utambulisho huo

***
📌Bilioni 60.9 kupeleka umeme kwenye vitongoji 581 Shinyanga

📍Shinyanga

Imeelezwa kuwa Mradi wa kupeleka umeme kwenye vitongoji 9,009 Awamu ya Pili B (HEP 2B), utakaonufaisha Wateja wa awali 290,300 katika mikoa 25 ya Tanzania Bara nchini unakwenda kuchochea shughuli za kiuchumi, Biashara na Viwanda na kuongeza Pato la Taifa.

Hayo yameelezwa leo Februari 2, 2026 na Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Mboni Mhita wakati akitambulishwa mkandarasi kampuni ya Derm Group Ltd atakayetekeleza mradi huo wa kupeleka umeme kwenye vitongoji 581 kwa gharama ya shilingi bilioni 60.9 mkoani Shinyanga.

"Nimeelezwa kuwa, mradi wa HEP 2B unakwenda kuunganisha wateja wapatao 20,421. Hii inakwenda kuchochea maendeleo ya wakazi wa mkoa huu kuweza kufanya shughuli mbalimbali za kiuchumi ikiwemo kufungua Viwanda na Biashara, " amesema RC Mhita.

Halikadhalika, RC Mhita amemtaka mkandarasi kuhakikisha anamaliza mradi huo wa kupeleka umeme kwenye vitongoji kwa muda uliopangwa ili wananchi wa mkoa huo waweze kunufaika na mradi ikiwemo kufungua shughuli za kibiashara.

Naye, Msimamizi wa Miradi ya REA Kanda ya Magharibi Mhandisi Robert Dulle ameeleza kuwa, kwa mkoa wa Shinyanga jumla una vijiji 509 ambavyo vyote vina huduma ya umeme, vitongoji vyenye umeme ni 2,704 na ambavyo havina umeme ni vitongoji vyenye 1,205.
Aidha, Mha. Dulle ameongeza kuwa katika mradi wa HEP 2B unakwenda kufikisha umeme kwenye vitongoji 581 kwa gharama ya shilingi bilioni 60.9 na vitakavyosalia ni vitongoji 918 tu.

Kwa upande wake, Meneja wa Kampuni ya Derm Group (T) Ltd, Mhandisi Musa Abdallah ameishukuru Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA), kwa kupewa fursa ya kutekeleza mradi huo mkoani humo. 

Ameihakikishia Serikali kuwa mradi huo utataekelezwa kwa wakati kama ilivyopangwa kwenye mkataba na mradi unakwenda kuwa nyenzo ya uchumi katika mkoa huo.
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Mboni Mhita akizungumza wakati wa utambulisho wa mkandarasi kampuni ya Derm Group Ltd atakayetekeleza mradi wa kupeleka umeme kwenye vitongoji 581 kwa gharama ya shilingi bilioni 60.9 mkoani Shinyanga

KAMPASI MPYA ZA VYUO VIKUU KUFUNGUA MILANGO YA UBIA RASMI NA SEKTA BINAFSI

KAMPASI MPYA ZA VYUO VIKUU KUFUNGUA MILANGO YA UBIA RASMI NA SEKTA BINAFSI

February 02, 2026 Add Comment

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Daniel Mushi,akizungumza na wadau leo Februari 02, 2026 jijini Dodoma.

....

Serikali imeelekeza wadau kuhakikisha uwekezaji unaofanyika karibu na kampasi mpya 16 za vyuo vikuu unazingatia mpangilio wa miji, usalama na viwango vya kitaifa ili kuzuia ujenzi holela na kuhakikisha huduma zinazotolewa zinakidhi mahitaji ya wanafunzi, watumishi na jamii jirani.

Akizungumza Februari 02, 2026 jijini Dodoma, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Daniel Mushi,amesema kuwa halmashauri na serikali za mitaa zinapaswa kutenga ardhi na kuandaa mpango wa matumizi ya ardhi kwa kushirikiana na vyuo husika.

Prof. Mushi amesisitiza kuwa mipango hiyo lazima izingatie viwango vya kitaifa vya upangaji miji na kuondoa migongano ya matumizi ya ardhi.

Profesa Mushi pia amevielekeza vyuo vikuu kufungua milango ya ushirikiano na sekta binafsi kupitia ubia rasmi (PPP) katika ujenzi wa hosteli, vituo vya biashara na miundombinu maalum.

Amesema mashauriano ya mara kwa mara kati ya vyuo na serikali za mitaa ni muhimu ili kuoanisha mipango ya maendeleo na kuimarisha mazingira rafiki kwa uwekezaji.

Aidha, sekta binafsi imetakiwa kuhakikisha huduma wanazotoa zinajibu mahitaji halisi ya jamii kwa kuzingatia usalama, ubora na uwajibikaji wa kijamii.

Mratibu wa Mradi wa HEET Taifa, Dkt. Kenneth Hosea, amesema kuwa mbali na kutoa mafunzo ya programu za Shahada ya Kwanza na Shahada ya Pili, kampasi mpya pia zitalenga kutoa ujuzi wa vitendo kwa vijana, wanawake na makundi maalum. Hatua hii inalenga kuchochea maendeleo ya kijamii na kiuchumi katika maeneo ya pembezoni kupitia ujenzi wa miundombinu, upatikanaji wa huduma za msingi pamoja na fursa za ajira.

Aidha, Dkt. Hosea ameongeza kuwa kila kampasi inatarajiwa kudahili zaidi ya wanafunzi 1,000 mwanzoni, na idadi hiyo inatarajiwa kuongezeka hadi kufikia takribani wanafunzi 7,000 kadri muda unavyosonga.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mkinga, Rashid Karim Gembe, amesema kuwa kuanzishwa kwa kampasi mpya za elimu ya juu katika maeneo ya pembezoni kumeleta manufaa makubwa ya kiuchumi na kijamii

Amesema kuwa kutachochea ujenzi wa miundombinu kama barabara, maji na umeme, kuongeza upatikanaji wa huduma za msingi, pamoja na kutoa fursa za ajira kwa wananchi kupitia mahitaji ya walimu, wanafunzi na sekta binafsi, hivyo kuchangia kwa kiasi kikubwa ustawi wa jamii na maendeleo ya uchumi wa eneo husika.