HABARI

SIASA

ELIMU

Recent Posts

SERIKALI YARIDHISHWA NA MAANDALIZI YA NHIF KUELEKEA AFCON

SERIKALI YARIDHISHWA NA MAANDALIZI YA NHIF KUELEKEA AFCON

September 05, 2026 Add Comment

Serikali imeutaka Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) kujipanga kikamilifu katika maandalizi ya mashindano ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) 2027, hususan katika kuhakikisha wageni watakaofika nchini wanapata huduma bora za matibabu bila vikwazo.

Agizo hilo limetolewa l na Naibu Waziri wa Afya Mhe. Dkt. Florence Samizi (Mb.) ambaye amesema NHIF ina jukumu muhimu la kuratibu suala la bima ya afya wakati wa mashindano hayo ili kuhakikisha wageni wanapata huduma za matibabu kwa urahisi pindi wanapohitaji huduma hizo.

“Tuwape uhakika wa huduma bora ili waone fahari kuwapo hapa nchini katika kipindi chote cha mashindano hayo,” amesema Dkt. Samizi.

Amesema maandalizi ya huduma za matibabu yanapaswa kuzingatia pia huduma za dharura pamoja na huduma maalum, ikiwemo za moyo na mifupa, ili kukidhi mahitaji mbalimbali ya afya yatakayoweza kujitokeza wakati wa mashindano.

Aidha alidokeza kuwa tayari Wataalamu kutoka Shirikisho la Soka Afrika (CAF) wamekagua Vituo vya kutolea huduma kwa alengo la kujiridhisha na wamefurahishwa na utayari unaoonyeshwa katika maandalizi ya huduma za matibabu jambo linaloonesha kuwa Tanzania inajiandaa kuhakikisha AFCON 2027 inafanyika katika mazingira salama na yenye huduma bora.

Ameitaka NHIF kushirikiana kwa karibu na Wizara ya Afya, vituo vya kutolea huduma na wadau wengine kuhakikisha mfumo wa huduma za matibabu wakati wa mashindano hayo unakuwa imara, unaopatikana kwa wakati na unaokidhi viwango vinavyohitajika.

Akizungumzia hilo Mkurugenzi Mkuu waa NHIF, Dkt. Irene Isaka alisema kuwa tayari Mfuko umeshajipanga na umeandaa kifurushi maalumu kwa ajili ya wageni wote watakaokuja nchini kwa ajili ya mashindano hayo.

“Tayari tumejipanga na tuna kifurushi ambacho tutakileta Wizarani ili tupate baraka ya Wizara hivyo tunashukuru sana kwa maelekezo haya ambayo yanaboresha na kuhakikisha tunajipanga vyema,” alisema Dkt. Isaka. ‎

NAIBU WAZIRI AVUTIWA NA USAJILI WANACHAMA KIDIGITALI, AITAKA NHIF KUONGEZA KASI YA BIMA YA AFYA KWA WOTE

NAIBU WAZIRI AVUTIWA NA USAJILI WANACHAMA KIDIGITALI, AITAKA NHIF KUONGEZA KASI YA BIMA YA AFYA KWA WOTE

September 05, 2026 Add Comment

‎NAIBU Waziri wa Afya, Mhe Dkt. Florence George Samizi (Mb), amelipongeza Baraza la Wafanyakazi la Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) kwa kuwa moja ya mabaraza bora nchini. Amelitaka baraza kuhakikisha ajenda ya Bima ya Afya kwa wote inawafikia wananchi wengi zaidi.

Nimefurahi kusikia kwamba katika kipindi cha mwaka wa fedha 2025/2026 Mfuko umeweza kufikia 10.7% ya Wananchi toka 8% ya wananchi iliyodumu kwa takriban miaka 10. Pamoja na pongezi hizo Mh. NAIBU WAZIRI ameutaka Mfuko kutumia TEHAMA na kusajili wanachama wengi zaidi ili kutimiza ahadi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuwafikishia wananchi wote huduma za bima ya afya. Hii itasaidia wananchi kuondokana na umaskini pale wanapopata maradhi. ‎Dkt. Samizi ametoa maelekezo Hayo wakati wa mkutano wa nne wa wa Baraza la 4 wafanyakazi NHIF, Jijini Arusha, na kusisistiza menejimenti ya wafanyakazi wa NHIF kutekeleza majukumu yao kwa kuzingatia uadilifu, weledi na uwajibikaji, huku wakisikiliza na kutatua kwa wakati kero za wananchi. ‎Aidha, amesisitiza umuhimu wa kutoa elimu kwa wananchi kuhusu umuhimu wa kuwa na bima ya afya. Kutoa huduma bora na kuwa na mfumo wa kupokea mrejesho toka kwa wananchi. ‎Katika kuelekea maadhimisho ya miaka 25 tangu kuanzishwa kwa NHIF, Dkt. Samizi amesema ni muhimu mfuko huo kuonesha mafanikio yaliyopatikana. Kuwepo kwa NHIF kumesaidia kuboresha huduma za Afya kwa kulipa madai na kutoa mikopo kwa vituo vya afya. Ni vema wanachi wakajulishwa hatua kubwa iliyofikiwa katika huduma za Afya na mchango wa NHIFkatika Sekta hii muhimu. Mlianza na vituo vichache sana mwaka 2001 hivi sasa yaani mwaka wa Fedha 2025/26 mmesajili zaidi ya vituo 10,600 nchi nzima. Ni vema kuonesha namna mlivyokabiliana na changamoto za wakati ule na namna zilivyowasaidia kuboresha Mfuko katika utoaji wa huduma. ‎Amesema mafanikio hayo yanadhihirishwa na kujituma, ushirikiano, umoja na mshikamano miongoni mwa watumishi wa NHIF ili kufikia malengo ya mfuko kwa lengo la kutekeleza jitihada za Serikali za kuhakikisha wananchi wanapata bima ya Afya. ‎Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa NHIF, Dkt. Irene Isaka, ameeleza mafanikio yaliyopatikana ikiwa ni pamoja na kupunguza muda wa kilipa madai toka zaidi ya siku 90 hadi wastan wa siku 50 kwa mwaka wa Fedha 2025/2026. Vile vile alieleza kwamba Mfuko umeendelea kuimarika ambapo ziada imeongezeka kwa 57% Mfuko umepunguza matumizi kwa asilimia13% na uwekezaji umeongezeka kwa 106%.

Hii imewezesha Mfuko kuendeleza kifurushi cha wanafunzi, Toto Afya. Mfuko kusajili kifurushi cha tarangire, Mikumi, Ngorongoro, Serengeti Tanzanite na kifurushi cha vikundi yaani Umoja Afya ambacho ni sh. 60, 000 kwa matibabu ya mwaka mzima.

Vile vile alielezea mikakati inayotekelezwa na mfuko huo katika kufikia malengo yake ikiwa ni pamoja na matumizi ya TEHAMA kwenye usajili, uchakataji madai na kupambana na udanganyifu. Mfuko pia unashirikisha Sekta Binafsi katika usajili wa wanachama na katika huduma za matibabu. ‎Mwakilishi wa chama Cha wafanyakazi TUGHE, Bw.Paul wamepongeza baraza Hilo kuzingati misingi ya Kazi stahiki za wafanyakazi kwenye taasisi hiyo. ‎Baadhi ya wafanyakazi walioshiriki semina elekezi ya siku mbili wamesema wamepata maarifa na mwelekeo mpya ambao utawasaidia kuboresha utendaji wao wa kazi na utoaji wa huduma kwa wananchi.

Bima ya Afya kwa wote! Jiunge sasa!

MKENDA: UWEKEZAJI ELIMU YA JUU UENDE SAMBAMBA NA UBORA

MKENDA: UWEKEZAJI ELIMU YA JUU UENDE SAMBAMBA NA UBORA

September 05, 2026 Add Comment
 

Na Alex Sonna, Mzalendo Blog – Dodoma

WAZIRI wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda, ameitaka Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU) kuhakikisha inaweka mfumo bora na wenye ufanisi wa udahili na usajili wa wanafunzi wanaojiunga na elimu ya juu, ili kuepusha vyuo kupokea wanafunzi wanaozidi uwezo wa miundombinu na wakufunzi waliopo na hivyo kulinda ubora wa elimu.

Profesa Mkenda ametoa kauli hiyo leo, Septemba 5, 2026, jijini Dodoma, baada ya kukutana na Makamu Wakuu wa Vyuo Vikuu pamoja na Wenyeviti wa Mabaraza ya vyuo vikuu nchini, katika kikao kilichojadili masuala mbalimbali yanayohusu elimu ya juu, hususan mchakato wa udahili na usajili wa wanafunzi. Amesema lengo ni kuweka utaratibu utakaowawezesha wanafunzi kupata nafasi za masomo kwa haki na kwa ufanisi, huku ukizingatia uwezo halisi wa kila chuo.

“Tumefanya hivyo kwa ajili ya kuhakikisha kwamba tunatengeneza mfumo mzuri ambao hautaleta utata, hautakuwa na kuweka idadi ya wanafunzi kuliko uwezo wa kufundisha,” amesema Prof. Mkenda,

Waziri Mkenda amewahimiza wanafunzi wanaoomba kujiunga na vyuo vikuu kuendelea kufanya maombi yao huku wakisubiri maelekezo zaidi kutoka TCU kuhusu utaratibu wa udahili. Amesema mfumo unaoandaliwa unalenga kulinda maslahi ya wanafunzi na vyuo, sambamba na kuhakikisha mchakato wa udahili unakuwa wa wazi, rahisi na wenye ufanisi.

Aidha, amesema Serikali inaendelea kuongeza uwezo wa vyuo vikuu nchini kupitia ujenzi na upanuzi wa kampasi katika mikoa mbalimbali, hatua inayolenga kuongeza nafasi za wanafunzi kupata elimu ya juu. Amesema uwekezaji huo utawezesha kuongeza idadi ya wanafunzi wanaopata fursa za elimu ya juu bila kushusha viwango vya elimu vinavyotolewa.

Profesa Mkenda amesema Tanzania bado haijafikia kiwango cha uandikishaji wa wanafunzi katika elimu ya juu kinacholengwa, hivyo Serikali itaendelea kushirikiana na vyuo vikuu kuongeza nafasi za masomo huku ikihakikisha ubora unaendelea kuwa kipaumbele. Amesema Serikali inalenga kuwa na mfumo wa elimu ya juu unaoweza kutoa fursa zaidi kwa vijana sambamba na kuwaandaa kwa mahitaji ya soko la ajira.

Ameongeza kuwa Wizara imepanga kufanya kikao kama hicho na viongozi wa vyuo vya kati vilivyo chini ya Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi na Mafunzo ya Ufundi Stadi (NACTVET), kwa ajili ya kujadili masuala ya ubora wa elimu, udahili na mifumo ya uongozi katika sekta hiyo. Amesema ushirikiano kati ya Serikali, vyuo na wadau wengine ni muhimu katika kuhakikisha uwekezaji unaofanywa katika elimu unazaa matokeo yanayotarajiwa.

Kwa upande wake, Katibu Mtendaji wa TCU, Profesa Charles Kihampa, amesema kikao hicho kimejadili masuala mbalimbali yanayohusu udahili wa wanafunzi katika vyuo vya elimu ya juu, ubora wa elimu pamoja na hatua zinazochukuliwa na Serikali katika kuendeleza sekta hiyo.

Amesema wadau hao wamekubaliana kuendelea kushirikiana katika kuboresha mifumo ya udahili, huku wakizingatia mahitaji na mabadiliko yanayoendelea katika sekta ya elimu.

Prof. Kihampa amesema ongezeko linalotarajiwa la wanafunzi kutokana na mabadiliko mbalimbali ya sera linahitaji Serikali, TCU na vyuo vikuu kujiandaa mapema ili kuongeza uwezo wa kutoa elimu bora kwa idadi kubwa ya wanafunzi.

Naye Mwenyekiti wa Baraza la Chuo Kikuu cha Teolojia cha Lweru, Aggrey Mlimuka, amesisitiza umuhimu wa vyuo vikuu nchini kusimamia ubora wa elimu ili kuhakikisha wahitimu wanakuwa na uwezo na weledi unaokidhi mahitaji ya soko la ajira.

Amesema vyuo vina wajibu wa kuhakikisha kila taaluma inazalisha wataalamu wenye uwezo, huku akibainisha kuwa endapo vyuo vitashindwa kusimamia ubora, soko la ajira lenyewe litachuja wahitimu kulingana na uwezo wao.

Awali Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Ushirika Moshi (MoCU), Prof. Alfred Sife, amesema vyuo vikuu nchini vimekubaliana kuendelea kuboresha mchakato wa udahili wa wanafunzi kwa mwaka wa masomo 2026/2027 ili kuhakikisha wanafunzi wanaopokelewa wanakidhi vigezo na kujiunga na programu zinazolingana na taratibu, kanuni na sheria zilizowekwa.

Amesema mjadala mkubwa katika kikao hicho ulihusu mwenendo wa udahili unaoendelea kwa sasa, ambapo dirisha la kwanza la maombi limekamilika na kinatarajiwa kufunguliwa dirisha la pili wiki ijayo.

Kwa mujibu wa Profesa Sife, lengo ni kuhakikisha mfumo wa udahili unaendelea kuimarishwa ili kupata wanafunzi wenye sifa na kuwawezesha kujiunga na programu na vyuo vinavyokidhi mahitaji yao, huku taratibu, kanuni na sheria za udahili zikizingatiwa.

Aidha, Profesa Sife amesema ushirikiano huo ni muhimu katika kuhakikisha vyuo vikuu vinaendelea kuboresha ubora wa elimu katika programu mbalimbali na kutoa wahitimu wenye uwezo unaokidhi mahitaji ya taifa na soko la ajira.

NAIBU WAZIRI DKT. PIUS CHAYA ATEMBELEA KIWANDA CHA DAWA NCHINI CHINA

September 05, 2026 Add Comment


Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Mipango na Uwekezaji, Mheshimiwa Dkt. Pius Stephen Chaya  ameanza ziara ya kikazi nchini China yenye lengo la kuvutia wawekezaji wa China kuwekeza nchini Tanzania. Dkt Chaya ameambatana na Mkuu wa Mkoa wa Tanga Mhe.Balozi.Dkt. Batilda Buriani.


Katika kuanza kwa ziara hiyo leo, tarehe 5 Septemba 2026, Dkt. Chaya ametembelea kiwanda cha kutengeneza dawa cha Yiling Pharmaceutical Co., Ltd., ambapo amepata fursa ya kujifunza kuhusu shughuli za uzalishaji wa dawa na teknolojia zinazotumika katika kiwanda hicho.


Akizungumza na uongozi wa kampuni hiyo, Dkt. Chaya amewaalika wawekezaji hao kuangalia fursa za kuwekeza nchini Tanzania, akieleza kuwa Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan imeweka mazingira na sera rafiki kwa wawekezaji, hususan katika sekta ya uzalishaji wa dawa na vifaa tiba.


Dkt. Chaya ameeleza kuwa Serikali, kupitia utekelezaji wa Dira ya Maendeleo ya Taifa 2050, inalenga kuimarisha uzalishaji wa dawa na vifaa tiba nchini.

TANESCO YABORESHA MAISHA YA WAFANYAKAZI NYUMBA YA MUNGU

September 05, 2026 Add Comment



*📌 Nyumba za wafanyakazi zakarabatiwa, kuboresha utendaji wa kazi*


*📌 Mtambo wa kisasa wa kuchakata maji wazinduliwa*


📍 MWANGA, KILIMANJARO | Septemba 2, 2026

Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) limezindua na kukabidhi nyumba zilizokarabatiwa kwa wafanyakazi wa Kituo cha Kuzalisha Umeme kwa Maji cha Nyumba ya Mungu, Wilaya ya Mwanga, mkoani Kilimanjaro.


Nyumba hizo, zilizojengwa tangu mwaka 1969, wakati Kituo cha Nyumba ya Mungu kilipoanza kufanya kazi, zimefanyiwa ukarabati mkubwa hatua inayolenga kuboresha mazingira ya makazi na ustawi wa wafanyakazi.

Akizungumza wakati wa uzinduzi na makabidhiano hayo, Afisa Rasilimali Watu wa Kituo cha Nyumba ya Mungu, Bi. Neema Mwaisaka, amewataka wafanyakazi waliokabidhiwa nyumba hizo kuzitunza ili ziendelee kuwa na thamani na kutumika kwa muda mrefu.


“Natoa rai kwa wafanyakazi ambao tumewakabidhi nyumba hizi wazitunze, kwani Shirika limetumia fedha nyingi katika kuzikarabati,” amesema Bi. Neema.

Kwa upande wao, wafanyakazi waliokabidhiwa nyumba hizo, kupitia mwakilishi wao Masasi Maduka, wameipongeza Menejimenti ya TANESCO kwa kuboresha mazingira yao ya kuishi, wakieleza kuwa mazingira bora ya makazi yataongeza morali, ufanisi na kujituma katika kutekeleza majukumu yao.


“Kuboresha mazingira yetu ya kuishi kutatuongezea morali ya kufanya kazi na kutuwezesha kujituma zaidi katika kutekeleza majukumu yetu,” amesema Masasi.

Katika hatua nyingine, Kituo cha Nyumba ya Mungu kimezindua mtambo wa kisasa wa kuchakata maji kwa ajili ya matumizi ya binadamu pamoja na matumizi katika mitambo ya kituo.


Akizungumza wakati wa uzinduzi wa mtambo huo, Mkuu wa Kitengo wa Kituo cha Nyumba ya Mungu, Mha. Andrea Shio, amesema TANESCO imefanya ukarabati na uboreshaji wa mtambo huo ili kuufanya kuwa wa kisasa na kuongeza ufanisi wake.


“Naipongeza Menejimenti ya Shirika kwa ukarabati wa mtambo huu. Maji haya yanatumika kwa matumizi ya binadamu pamoja na kwenye mitambo,” amesema Mha. Shio.


Ukarabati wa nyumba za wafanyakazi pamoja na kuboresha miundombinu muhimu kama mtambo wa kuchakata maji ni sehemu ya jitihada za TANESCO za kuimarisha mazingira ya kazi na makazi, kuongeza ufanisi na kuhakikisha huduma za uzalishaji umeme zinaendelea kutolewa kwa uhakika.

Masauni atoa wito kusimamia agizo la usafi wa mazingira

September 05, 2026 Add Comment
Na; Mwandishi Wetu, Dar es Salaam

Serikali inatoa wito kwa Wakuu wa Mikoa, Wakuu wa Wilaya, Wakurugenzi wa Halmashauri, Wenyeviti wa Serikali za Mitaa, Vijiji na Vitongoji kuhakikisha kuwa wanaweka utaratibu wa kusimamia utekelezaji wa maelekezo ya kila Jumamosi ya mwisho wa mwezi kuwa siku ya usafi wa Mazingira Kitaifa kwa kuzingatia maslahi ya makundi mbalimbali.

WIZARA YA NISHATI YAPONGEZWA KUTEKELEZA MAAGIZO YA KAMATI

September 05, 2026 Add Comment

Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini, Mhe. Subira Mgalu, ameipongeza Wizara ya Nishati na Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) kwa kutekeleza maagizo ya Kamati hiyo ya kuwataka Wizara ya Nishati na Wizara ya Madini kushirikiana katika kutatua changamoto za upatikanaji wa nishati katika sekta ya madini.


Mhe. Mgalu ameyasema hayo Septemba 3, 2026, jijini Dodoma, wakati wa hafla ya utiaji saini mkataba wa ujenzi wa njia ya kusafirisha umeme ya Mponvu–GGM ya msongo wa kilovolti 220 (kV) pamoja na Kituo cha Kupoza Umeme kitakachojengwa katika eneo la GGM, Geita.

Amesema anafurahishwa na hatua zilizochukuliwa na Wizara ya Nishati na Wizara ya Madini katika kutekeleza maelekezo yaliyotolewa na Kamati hiyo, hususan kuwezesha upatikanaji wa umeme wa uhakika kwa migodi ya wachimbaji wadogo, wa kati na wakubwa.


“Tunafarijika kuona maelekezo tuliyoyatoa katika kikao cha Kamati yakitekelezwa. Ushirikiano kati ya Wizara ya Nishati na Wizara ya Madini umewezesha kufikiwa kwa hatua hii kubwa ya kupeleka umeme wa uhakika katika maeneo ya migodi kupitia mradi wenye thamani ya zaidi ya shilingi bilioni 63,” amesema Mhe. Mgalu.


Aidha, amekumbusha ziara ya Kamati hiyo iliyofanyika Machi 15, 2026, katika Kituo cha Mponvu, Geita, ambapo pamoja na Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba, walijionea uwekezaji wa zaidi ya shilingi bilioni 50 uliofanywa na Serikali ya Awamu ya Sita katika miundombinu ya umeme.


Amesema ujenzi wa njia mpya ya kusafirisha umeme ya msongo wa kV 220 utakaoiwezesha migodi ya GGM kupata umeme wa uhakika ni hatua muhimu katika kuhakikisha shughuli za uchimbaji zinafanyika kwa ufanisi na tija zaidi.


“Upatikanaji wa umeme wa uhakika utasaidia migodi kufanya kazi kwa ufanisi, kuongeza uzalishaji na hatimaye kuchangia katika kukuza pato la Taifa kupitia sekta ya madini,” amesema.


Mhe. Mgalu pia ameipongeza TANESCO pamoja na Bodi ya Wakurugenzi kwa kazi nzuri wanayoifanya katika kuboresha huduma ya umeme nchini, akihusisha jitihada hizo na kauli mbiu ya Shirika isemayo “Tunaangaza Maisha Yako.”


Amesema jitihada za kuimarisha upatikanaji wa umeme wa uhakika ni sehemu muhimu ya kujenga uchumi wa kisasa na kufikia malengo ya maendeleo ya Taifa kuelekea Dira ya Maendeleo ya Tanzania 2050.

WAKULIMA BABATI WANUFAIKA NA PROGRAMU YA KUENDELEZA KILIMO NA UVUVI (AFDP)

September 05, 2026 Add Comment
Na; Mwandishi wetu – Babati

Wakulima wa vijiji vya Endakiso na Orng'adida vilivyopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Babati Mkoani Manyara wameeleza kunufaika na Programu ya kuendeleza Kilimo na Uvuvi (AFDP) inayofadhiliwa na Shirika la Kimataifa la Maendeleo ya Kilimo (IFAD) kwa kushirikina na Serikali na kuratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Uratibu, na wenye Ulemavu.

WAKULIMA BABATI WANUFAIKA NA PROGRAMU YA KUENDELEZA KILIMO NA UVUVI (AFDP)

September 05, 2026 Add Comment




Na; Mwandishi wetu – Babati


Wakulima wa vijiji vya Endakiso na Orng'adida vilivyopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Babati Mkoani Manyara wameeleza kunufaika na Programu ya kuendeleza Kilimo na Uvuvi (AFDP) inayofadhiliwa na Shirika la Kimataifa la Maendeleo ya Kilimo (IFAD) kwa kushirikina na Serikali na kuratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Uratibu, na wenye Ulemavu.



Kwa nyakati Tofauti wakulima kutoka vijiji hivyo wameyasema hayo tarehe 4 Septemba wakati wa ziara ya timu kutoka IFAD inayotathimini maendeleo ya utekelezaji  Programu ya  muda wa kati  (MTR).

Wakulima hao waliweka bayana kuwa, Programu hiyo imeweza kuwaletea teknolojia ya kisasa ya Kilimo Mseto kwa kutumia Mbegu himilivu zinazoweza kuhimili athari zitokanazo na mabadiliko ya tabia nchi.



Akizungumza wakati wa Ziara hiyo Bw. Ramadhani Iddi Mfumbilo mkulima kutoka katika kijiji cha Mkombozi Kata ya Endasiko alisema, kupitia Programu hii wakulima wameweza kupata mbegu za mahindi aina ya situka na mbegu za lishe ambazo zimepandwa mashambani pamoja na mazao mengine kama vile labulabu ambayo yanaweza kurutubisha ardhi na kuzuia Mmomonyoko wa udongo.

“Majani hayo pia siyo rafiki kwa mifugo kama vile ng’ombe hivyo mifugo itakapovamia shamba la Mkulima si rahisi kuweza kula au kuharibu mazao, na yanakimbiza wadudu waharibifu wa mazao.” Aliendekea kufafanua.

Alibainisha kuwa, Mbegu hizi za Lishe zina uwezo mkubwa wa Kurutubisha Afya ya Familia hasa kwa watoto, kinamama wajazito, wazazi na wazee na pia zimesaidia kupunguza magonjwa ya Utapiamlo kwa watoto.

Aidha, Akiongelea mbegu za Jamii ya Mikunde yaani Maharage aina ya Jesca, alisema, Mbegu hizo zina virutubisho muhimu na vya kipekee hasa kwa watoto.



Kwa upande wake Bi Naseriani Joseph kutoka katika Kijiji cha Orng'adida Kata ya Qash mkulima wa mazao ya Lishe yanayolimwa katika bustani nyumbani maarufu kama '_Kitchen gardens_', alisema kuwa, kupitia Programu ya AFDP wakulima hao waliweza kupata Elimu na Mbegu bora za mazao ya lishe ambayo wanalima Nyumbani na wamepata manufaa mengi kama vile kuwepo kwa mboga nyumbani pamoja na kuwasaidia watoto shule na familia kwa ujumla pamoja na kuimarisha Afya ya familia na kuongeza kipato

“Wanawake tunapata mahitaji yetu muhimu kupitia kilimo hiki kwa upande wa mboga mboga na mazao ya mikunde, tumepata elimu ya maharage lishe tumepata mbegu na tumeyatumia, Maharage yale yameboreshwa yana viini lishe na madini chuma, hivyo afya za familia zinaimarika, natoa tuu wito kwa serikali kuongeza mbegu hizi maana ni adimu na zinazalishwa kwa uchache katika kata yetu. Alisema”


Wataalam hao wanaendelea na ziara hiyo kwa kutembela maeneo tofauti yanayotekeleza programu nchini katika sekta za Kilimo na Uvuvi.

TANZANIA, MAREKANI KUIUNGANISHA AFRIKA KWENYE SEKTA YA AFYA

September 04, 2026 Add Comment

Na John Mapepele – WAF

Washington, D.C.

Serikali ya Tanzania imekubaliana na Chama cha Wafanyabiashara cha Marekani (U.S. Chamber of Commerce) mjini Washington, D.C na Serikali ya Marekani kufanya utekelezaji wa kimkakati wa mkataba wa sekta ya afya ulioingiwa hivi karibuni ili kuzinufaisha pande zote mbili,huku wakiifanya Tanzania kuwa muhimili wa uzalishaji na usambazaji dawa na vifaa tiba katika bara la Afrika.

SHANGWE CHEM CHEM SAFARI LODGE WAKISHINDA TENA TUZO HOTEL BORA YA KIFAHARI AFRIKA

September 04, 2026 Add Comment

Na Mwandishi wetu

Kwa mwaka wa pili mfululizo, hoteli ya kitalii ya Chem Chem Safari Lodge imeshinda tuzo ya hotel Bora ya kifahari barani Afrika katika tuzo ambazo ziliandaliwa na shirika la kimataifa la Utalii, World Travel Awards (WTA).

TCAA NA UMOJA WA ULAYA WATHIBITISHA DHAMIRA YA KUIMARISHA USIMAMIZI WA USALAMA WA USAFIRI WA ANGA

September 04, 2026 Add Comment

 


Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA), Dkt. Jabiri K. Bakari akizungumza wakati wa kikao cha kuhitimisha ujumbe wa timu wataalam kutoka Shirika la Usalama wa Anga la Umoja wa Ulaya (EASA).
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA), Dkt. Jabiri K. Bakari akizungumza wakati wa kikao cha kuhitimisha ujumbe wa timu wataalam kutoka Shirika la Usalama wa Anga la Umoja wa Ulaya (EASA).
Kiongozi wa Ujumbe wa EASA Bw. Jose Miguel Manso Angulo akizungumza wakati wa kikao hicho.

***
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA), Dkt. Jabiri K. Bakari, amethibitisha dhamira ya Mamlaka hiyo ya kujenga Mamlaka ya Usafiri wa Anga ya kiwango cha kimataifa barani Afrika, yenye matarajio ya kufikia viwango vinavyolingana na mamlaka za usafiri wa anga za Ulaya katika ubora wa udhibiti, umahiri wa kitaalamu, ufanisi wa kiutendaji na usimamizi wa usalama wa anga.

WALIMU KUTUMIA TEHAMA KUBORESHA UFUNDISHAJI NA UJIFUNZAJI

September 04, 2026 Add Comment


ARUSHA, Septemba 4, 2026 — Mafunzo ya siku nne ya Umahiri wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano kwa Walimu Tanzania (ICT Competency Standards for Teachers in Tanzania - ICT CSTT) yameahirishwa leo jijini Arusha, huku walimu wakihimizwa kutumia maarifa na stadi walizojifunza kuboresha ufundishaji, ujifunzaji, tathmini pamoja na kuwawezesha waalimu wenzao.
Mafunzo hayo yaliyofanyika Gold Crest Hotel kuanzia Septemba 1 hadi 4, 2026, yamewajengea washiriki uwezo wa kutumia Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA), Akili Bandia (AI), rasilimali za kidijitali na mifumo ya kujifunzia kwa njia ya mtandao katika kazi za kila siku za mwalimu.
Akifunga mafunzo hayo, Mkurugenzi Msaidizi wa Elimu, Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia, Bw. Mathias Innocent Mvula, amebainisha kuwa kukamilika kwa mafunzo hayo kunapaswa kuwa mwanzo wa utekelezaji wa maarifa na stadi hizo katika shule za na za jirani.


Kwa mtazamo wake, thamani ya uwekezaji huo itaonekana kupitia mabadiliko katika ufundishaji na ujifunzaji, badala ya kuishia kwenye vyeti. Amewataka washiriki kutekeleza mipango kazi waliyoandaa wakati wa mafunzo na kuonesha hatua watakazochukua katika utekelezaji wanaporejea shuleni.
Akieleza mazingira mapya ya utekelezaji wa Sera ya Elimu na Mafunzo ya mwaka 2014 Toleo la mwaka 2023, Bw. Mvula amebainisha kuwa maendeleo ya teknolojia, hususan Akili Unde, yamebadilisha namna watu wanavyopata taarifa na maarifa, hali inayohitaji walimu kuongeza uwezo wa kutumia zana hizo kwa malengo ya kuinua ubora wa elimu.


Amebainisha pia kuwa simu za mkononi na vifaa vingine vya kidijiti vinaweza kuwa nyenzo muhimu za kujifunzia na kufundishia vinapotumiwa kwa usahihi. Hata hivyo, matumizi ya teknolojia yanapaswa kwenda sambamba na mabadiliko ya sera na mitaala yanayolenga kujenga umahiri wa mwanafunzi.
Kwa mujibu wa Bw. Mvula, elimu ya sasa inalenga kumwandaa mwanafunzi kutumia maarifa na stadi katika maisha halisi, kukabiliana na changamoto na kutumia fursa za kiuchumi, badala ya kutegemea ajira pekee. Ameeleza kuwa kuimarishwa kwa mikondo ya amali ni miongoni mwa hatua zinazolenga kuongeza uwezo huo.
Katika kuendana na mabadiliko hayo, Bw. Mvula ametoa wito kwa walimu kuendelea kutumia fursa za Mafunzo Endelevu ya Walimu Kazini (MEWAKA), akibainisha kuwa ujifunzaji kwa njia ya mtandao unawapa nafasi ya kuongeza uwezo kitaaluma na kitaalamu bila kulazimika kurejea chuoni mara kwa mara.


Ameongeza kuwa Serikali inaendelea kuweka mifumo endelevu ya kuimarisha umahiri wa walimu, ikiwemo utaratibu wa kutambua mafunzo kabilishi mbalimbali ya kuwajengea uwezo walimu ili kuboresha elimu nchini. 
MKOA WATAKA UJUZI UONEKANE SHULENI
Akizungumza katika hafla hiyo, Afisa Elimu Mkoa wa Arusha, Bw. Vicent Boniface Kayombo, amewataka walimu walioshiriki katika mafunzo hayo kuwa kiungo cha kusambaza maarifa kwa walimu wenzao na kuhakikisha ujuzi walioupata unatafsirika katika vitendo vya ufundishaji na ujifunzaji shuleni.
Kayombo ameeleza kuwa Mkoa wa Arusha una mpango wa utekelezaji wa MEWAKA katika shule za msingi na sekondari, hivyo walimu walioshiriki katika mafunzo hayo wana nafasi muhimu ya kusaidia kufanikisha mpango huo kwa kushirikisha wenzao na kuchochea matumizi yenye tija ya TEHAMA katika shule zao.
VETA YAPANIA KUIMARISHA UJUZI KUPITIA USHIRIKIANO NA WAAJIRI

VETA YAPANIA KUIMARISHA UJUZI KUPITIA USHIRIKIANO NA WAAJIRI

September 04, 2026 Add Comment
 

Na Mwandishi Wetu, Dodoma

MAMLAKA ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) imewaalika waajiri na wamiliki wa viwanda nchini kuendelea kushirikiana na mamlaka hiyo katika kuandaa na kuendeleza wataalamu wenye ujuzi unaokidhi mahitaji ya soko la ajira na kuchochea maendeleo ya Taifa.

Mkurugenzi Mkuu wa VETA, CPA Anthony Kasore, alitoa kauli hiyo jana jijini Dodoma wakati wa hafla ya kusaini Hati ya Makubaliano (MoU) kati ya VETA na Kampuni ya Van Mo, inayolenga kuimarisha ushirikiano katika kuwaendeleza vijana wenye ujuzi na kuwawezesha kupata ajira mara baada ya kuhitimu mafunzo yao.

Makubaliano hayo yaliyosainiwa katika Ukumbi wa Mikutano wa VETA Makao Makuu yalihusisha CPA Kasore kwa upande wa VETA na Meneja Mkuu wa Van Mo, Fathi Ahmed Ally. Kampuni hiyo inajihusisha na shughuli mbalimbali zikiwemo usafirishaji, uchukuzi, uuzaji wa mafuta, umiliki wa majengo na ardhi, kilimo, utalii pamoja na shughuli za uzalishaji viwandani.

Kwa mujibu wa makubaliano hayo, pande hizo zinalenga kuongeza upatikanaji wa wahitimu wenye umahiri, tija, ubunifu, maadili na wanaozingatia usalama kazini, huku Van Mo ikitoa fursa za ajira kwa wahitimu wa VETA wenye sifa zinazohitajika.

Aidha, ushirikiano huo utasaidia kuoanisha programu za mafunzo ya ufundi stadi na mahitaji halisi ya sekta ya viwanda na biashara pamoja na kuwawezesha wanafunzi kupata mafunzo kwa vitendo katika maeneo ya kazi.

Maeneo ya ushirikiano yaliyoainishwa katika MoU hiyo ni pamoja na mafunzo ya udereva wa magari makubwa, usimamizi wa vyombo vya usafiri, uchukuzi na uhifadhi wa mizigo, usimamizi wa mnyororo wa ugavi, ukaguzi na ukarabati wa magari pamoja na mifumo ya umeme na elektroniki ya magari. Maeneo mengine ni uendeshaji wa maghala na usimamizi wa stoo, uendeshaji wa vituo vya mafuta, ujenzi, usimamizi wa majengo na miundombinu, utalii na ukarimu pamoja na kilimo na uhifadhi wa mazao.

Akizungumza baada ya kusainiwa kwa makubaliano hayo, Kasore alisema ushirikiano huo pia utasaidia kuwajengea uwezo wakufunzi na kuhakikisha mafunzo yanayotolewa na VETA yanaendana na mahitaji ya soko la ajira.

Alisema VETA itaendelea kushirikiana na waajiri na wamiliki wa viwanda ili kutambua fursa zilizopo na kuhakikisha wahitimu wanapata nafasi za ajira katika viwanda na maeneo mengine yenye uhitaji wa wataalamu wenye ujuzi.

“Tutahakikisha pia wenzetu wa Van Mo wanapohitaji wataalamu wenye ujuzi mbalimbali, sisi VETA tuweze kusaidia kuwapata. Sambamba na hilo, ushirikiano huu una maslahi mapana kwa wananchi katika kupata fursa za ajira,” alisema Kasore.

Kwa upande wake, Meneja Mkuu wa Van Mo, Fathi Ahmed Ally, alisema kampuni hiyo imelenga kutoa ajira kwa takribani vijana 500 wenye ujuzi mbalimbali waliohitimu katika vyuo vya VETA.

Alisema kampuni hiyo imeamua kushirikiana na VETA kutokana na ubora wa ujuzi unaopatikana kwa wahitimu wake, hususan katika fani zinazohusiana na shughuli za usafirishaji ambazo ni muhimu katika utekelezaji wa shughuli za kampuni hiyo.

“Kilichotuvutia kuja VETA ni kutokana na wahitimu kutoka katika vyuo hivi kuwa na ujuzi ambao sisi tunauhitaji katika kampuni yetu, hususan shughuli za usafirishaji. Hivyo tumeona hapa ndipo mahali sahihi pa kuwapata vijana wenye ujuzi huo,” alisema Fathi.