HABARI

SIASA

ELIMU

Recent Posts

BARA LA AFRIKA: TUNAHITAJI WANAHABARI MAHIRI KUKUZA SAYANSI, TEKNOLOJIA NA UBUNIFU

BARA LA AFRIKA: TUNAHITAJI WANAHABARI MAHIRI KUKUZA SAYANSI, TEKNOLOJIA NA UBUNIFU

December 03, 2025 Add Comment






Na Veronica Mrema – Pretoria

Uandishi wa habari za sayansi kwa umakini na umahiri ni nyenzo muhimu ili kufikisha ujumbe sahihi kwa jamii, kusaidia kukuza maendeleo ya tafiti na vumbuzi mbalimbali.

Bara la Afrika bado lina uhitaji mkubwa wa waandishi wa habari ambao wamejikita na wapo na umahiri katika kuwasilisha masuala ya sayansi kwa lugha rahisi zinazoeleweka kwa jamii.

“Kazi yoyote ile tunayoifanya [katika] sayansi ina maana tu pale inapofahamika vizuri kwa watu na jamii nzima,”.

Waziri wa Sayansi, Teknolojia na Ubunifu wa Afrika Kusini Profesa Blade Nzimande amesema hayo alipokuwa akifungua rasmi Mkutano wa 13 wa Waandishi wa Habari za Sayansi Duniani.

Mkutano huo WCSJ2025 unafanyika Pretoria Afrika Kusini kuanzia Disemba 1-5, 2025 ukiwa na kauli mbiu isemayo ‘Uandishi wa sayansi, unaojenga uelewa na uthabiti wa sayansi na haki za kijamii’.

“Nilipoombwa kuja kufungua mkutano huu nilikubali mara moja kwa sababu ya umuhimu wa nafasi ya waandishi wa habari za sayansi katika kukuza sayansi,” amesema.

Ameongeza “Kwa hiyo waandishi wa habari ni daraja muhimu sana [lakini] hatusemi daraja lisilo na ukosoaji, hapana bali daraja muhimu la kuielimisha jamii kuhusu sayansi.

“Kama bara, tunahitaji waandishi wa habari za sayansi wengi kwa sababu bado tunalo jukumu la kuendeleza sayansi, teknolojia na ubunifu barani Afrika.

“Na mawasiliano ni sehemu muhimu ya hilo. Kwa mfano, tunayo mkakati wa Sayansi, Teknolojia na Ubunifu kwa Afrika [STISA 2034].

“.., ambao unalenga kukuza sayansi, utafiti na maendeleo barani Afrika jambo muhimu sana. Kwa hiyo tunathamini kazi mnayofanya, na ni muhimu sana,” amesema.

Amesema waandishi wa habari wanapaswa kusaidia Bara la Afrika kupambana na dhana potofu na ubaguzi katika namna sayansi inavyowasilishwa.

“Lazima tuwahusishe pia makundi yaliyotengwa wanawake, watu waliodhulumiwa au waliokuwa na historia ya ukandamizaji ili nao wawe sehemu ya mawasiliano ya sayansi.

“Moja ya hatari kubwa inayoweza kuua umuhimu wa sayansi ni kuifanya kuwa mradi wa viongozi au watu wachache.

“Sayansi haipaswi kuwa mradi wa tabaka la juu; lazima iwe mradi unaoeleweka na watu wote. Tunawahimiza kuhakikisha mnazingatia hilo kama waandishi wa sayansi,” amesema.

Prof. Nzimande ameongeza “Waandishi wa habari mnapaswa kukabiliana na changamoto ya taarifa za uongo [fake news].

“Hili ni mojawapo ya mambo hatari sana katika mawasiliano leo, mitandao ya kijamii ina mazuri na mabaya.

“Ni mazuri kwa kuwa kila mtu anaweza kupata taarifa siku hizi karibu kila mtu anasema,” amesema na kuongeza

“Mimi ni mtengeneza maudhui.” Lakini pia mitandao ya kijamii inaweza kusambaza taarifa za uongo haraka sana, jambo ambalo ni hatari.

“Katika sayansi, tunapaswa kupambana na taarifa za uongo, si tu katika jamii kwa ujumla, bali katika sayansi haswa kwa sababu inaweza kusababisha madhara makubwa.

Amesisitiza “Je, mnakumbuka wakati wa COVID jinsi taarifa za uongo zilivyosambaa?

“Leo kuna watu katika nchi kubwa wanaodai kwamba chanjo husababisha autism jambo la uongo kabisa.

“Lakini likirudiwa na watu wenye mamlaka, linakuwa hatari zaidi. Hii ina maana kwamba lazima muwe jasiri kama waandishi.

“Mnapaswa kuwa jasiri na msiogope kuuliza maswali makubwa na muhimu,” amesema.

Teknolojia ya Akili Unde [AI] katika sekta ya habari pia si suala la kuliacha nyuma, amesisitiza,

“Tunahitaji kuingiza teknolojia mpya kama akili bandia katika kazi yenu, ili kuimarisha weledi na uwazi katika taaluma yenu.

“Tunapaswa pia kushughulikia tofauti katika namna sayansi inavyoripotiwa. Bara letu bado linatengwa katika mambo mengi.

“Mnachukua jukumu la kuhakikisha masuala ya sayansi yanawafikia Waafrika si hivyo tu.

“Bali pia kuhakikisha ubunifu, uvumbuzi na miradi ya sayansi kutoka Afrika inatambulika ndani na nje ya bara,” amesema Prof Nzimande.

Diplomasia ya sayansi pia waandishi wa habari wanalo jukumu la kusaidia kuikuza ndani ya Bara la Afrika.

“Sayansi haina mipaka, na kwa sababu hiyo ina uwezo mkubwa wa kujenga mahusiano ya kidiplomasia baina ya nchi na mabara.

“Kama Afrika Kusini, tunaamini sana katika sayansi huria kwamba sayansi inapaswa kufikika zaidi na iwe wazi.

“Lakini lazima niseme kwamba waandishi wa habari za sayansi ni sehemu muhimu sana mjue au msijue katika kazi tunazofanya katika sekta ya sayansi.

“Bila ninyi, hatuwezi kuwafikia wale tunaopaswa kuwafikia,” amesema Prof Nzimande.

MBUNGE MAKBEL AWATAKA MADIWANI KUSIMAMIA KWA WALEDI FEDHA ZA MIRADI YA MAENDELEO

December 03, 2025 Add Comment





Na Oscar Assenga, TANGA

Mbunge wa Jimbo la Tanga (CCM) Kassim Amary Mbaraka Makbel amewataka madiwani kuhakikisha wanasimamia kwa waledi halmashauri ikiwemo fedha zote za miradi ya maendeleo zinazotolewa na Serikali ziende kwenye miradi husika.

Makbel aliyasema wakati akizungumza na waandishi wa vyombo vya habari wakati wa mchakato wa kumpitisha Mgombea nafasi ya Umeya na Naibu Meya wa Jiji hilo ambapo alisema kwamba wanawashukuru vongozi wa CCM na kamati kuu kwa kumteua na kumpendekeza kuwa miongoni mwa wagombea.

Alisema kwamba lazima madiwani wahakikishe wanasimamia vema halmashauri kuhakikisha fedha zote za miradi ya maendeleo ya Serikali ziende kwenye miradi husika ikiwemo kutokuwa na ubadhirifu wa aina yote kuhakikisha miradi inakamilika na hilo jambo ambalo watalisimamia kwa ukaribu.

Alisema kwamba hatataka kuona matumizi mabaya ya Fedha za Umma bali ni kuhakikisha kila fedha zinatumika kulingana na taratibu zake ili ziweze kuleta matokeo yaliyokusudiwa

“Katika hili niwaambie Madiwani kwamba sitataka kuona matumizi mabaya ya fedha zaa umma ambazo zinaletwa katika Halmashauri hivyo lazima tuwe makini “Alisema

Awali akizungumza Mbunge wa Viti Maalumu (CCM) Mhandisi Mwanaisha Ulenge alisema kwamba watakwenda bungeni kusukuma kwa nguvu kuhakikisha fedha zinakuja pamoja na kuhakikisha matumizi mazuri ya fedha zinazoletwa kwa ajili ya maendeleo ya watu kama ilivyo dhamira ya Rais Dkt Samia Suluhu ili kupeleka tabasamu kwa wananchi.

Naye kwa upande wake Mstahiki Meya Mteule wa Jiji la Tanga Selebosi Mhina Mustafa amehaidi kusimamia kikamilifu suala la mapato katika Jiji hilo ikiwemo kuzuia mianya ya upotevu wake kwa njia moja ama nyengine ili kuhakikisha halmashauri inakuwa na mafanikio makubwa.

Selebosi aliyasema hayo jana wakati akizungumza na waandishi wa vyombo vya habari ambapo alisema kwamba wanawashukuru vongozi wa CCM na kamati kuu kwa kumteua na kumpendekeza kuwa miongoni mwa wagombea.

Alisema kwamba hiyo ni imani kubwa ambayo walikuwa nayo juu yake huku madiwani wenzake wa Jiji hilo wakimthibitishia kwa kumpitisha kuwa mgombea wa nafasi hiyo na ndio mteule hivyo atakwenda Halmashauri kushirikiana na madiwaniwenzake kuwa chachu ya maendeleo.

“Kwa kweli nawashukuru sana kwa kuniteua kuwa mgombea na nafasi hii lakini niwaambie kwamba kubwa nitakwend kuzuia mianya yote ya upotevu wa mapato kwa njia moja ama nyengine wanaijua ili kuhakikisha halmashauri isimame kama Halamshauri”Alisema

Alisema kwamba katika kufanikisha jambo hilo watahakikisha wanakuwa makini katika suala la ukusanyaji wa mapato huku akiwaomba ushirikiano ili kuweza kutekeleza majukumu yao kwa tija na kufikia malengo waliojiwekea.

Aidha alisema pia atakwenda kusimamia kutekeleza ilani ya CCM na ndio muongozo wao na dira yao ya kwenda kuifanyia pamoja na kuwa wasimamizi wakuu wa fedha za miradi mbalimbali ambazo Mhe Rais Dkt Samia Suluhu amekuwa akizielekeza Tanga kuhakikisha zinatumika kwenye malengo yaliyokusudiwa na sio vyenginevyo.

“Lakini niwaombe wana Tanga ushirikiano,umoja pamoja na ubunifu katika kutekeleza miradi ya maendeleo na kuwa na vyanzo vipya vya mapato ili kuifanya Halmashauri yao iweze kupiga hatua kubwa za kimaendeleo.

“Tanga ni Jiji hivyo kuhakikisha kusimamia Bilioni 22 kwa Jiji la Tanga lenye viwanda karibuni 7 hadi 5 bado kwake ni ni fedha ndogo ipo haja ya kwenda kuzuia mianya yote ambayo kwa njia moja ama nyengine ”Alisema

Katika hatua nyengine Selebosi alizungumzia kuhusu uwepo wa tishio la maandamano Desemba 9 mwaka huu ambako aliwaambia madiwani kwamba wao ndio wanakaa na wananchi lazima viongozi wachukua hatua ikiwemo viongozi wa mitaa na watendaji wa kata ambao ndio walinzi wa amani katika maeneo yao.

“Katika hili lazima kwenye maeneo yenu tuisaidie serikali na kumsaidia Rais kuhakikisha hakutakuwa na maandamano yasiyokuwa rasmi kutokana na kwamba hayana tija kwa maendeleo “Alisema

Alisema kwambaa wanaofanya maandamano hawazuki tu bali wapo kwenye maeneo wanakutana na wana maeneo wanatokea hivyo lazima ifike mahali waisaidie Serikali kuhakikisha viashiria vyovyote vya uvunjifu wa amani hawavipi nafasi.

Awali akizungumza na waandishi wa habari Katibu Itikadi,Mafunzo na Uenezi Mkoa wa Tanga (CCM) Mngazija alisema kwamba alisema kwamba katika mchakato wa nafasi ya Meya na Naibu Meya wamewapitisha Selebosi Mhina Mustapha kuwa mgombea wa CCM baada ya kupata kura 24 kwa 14 dhidi ya mpinzani wake Hamza Bwanga.

Alisema kwamba katika nafasi ya Naibu Meya walimpitisha Khalid Rashid Hamnza kuwania nafasi hiyo baada ya kumgaragaza mpinzani wake Mwanaidi Chombo kwa kura 21 dhidi ya 16 .


Mwisho.

BARRICK NORTH MARA KUENDELEA KUSHIRIKIANA NA SERIKALI, WADAU KUTOKOMEZA UKIMWI

December 02, 2025 Add Comment
Katibu Tawala wa Wilaya ya Tarime, Mwl. Saul Mwaisenye, akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya viongozi na wafanyakazi wa Mgodi wa North Mara, Halmashauri ya Wilaya ya Tarime na Kampuni ya RIN kwenye maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani yaliyofanyika Nyamongo.
Meneja wa Afya na Usalama katika Mgodi wa Dhahabu wa North Mara, Dkt. Nicholas Mboya, akizungumza wakati wa maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani yaliyofanyika Nyamongo, Halmashauri ya Wilaya ya Tarime
Katibu Tawala wa Wilaya ya Tarime, Mwl. Saul Mwaisenye (katikati), akikagua moja ya mabanda ya huduma za afya na ushauri katika maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani yaliyofanyika Nyamongo, Halmashauri ya Wilaya ya Tarime.
Katibu Tawala wa Wilaya ya Tarime, Mwl. Saul Mwaisenye, akikabidhi kadi ya Bima ya Afya kwa mmoja wa akina mama wazee wakati wa maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani yaliyofanyika Nyamongo, Halmashauri ya Wilaya ya Tarime
8
Katibu Tawala wa Wilaya ya Tarime, Mwl. Saul Mwaisenye, akikabidhi kadi ya Bima ya Afya kwa mmoja wa wazee wakati wa maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani yaliyofanyika Nyamongo, Halmashauri ya Wilaya ya Tarime
Wananchi wakipata ushauri wa kitaalamu kuhusu masuala ya afya wakati wa maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani yaliyofanyika Nyamongo, Halmashauri ya Wilaya ya Tarime.
Wazee wakiwa wamejipanga mstari kwa ajili ya kupokea kadi za Bima ya Afya kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Tarime wakati wa maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani yaliyofanyika Nyamongo, Halmashauri ya Wilaya ya Tarime.
Katibu Tawala wa Wilaya ya Tarime, Mwl. Saul Mwaisenye (katikati mbele), akiongozwa kukagua mabanda ya huduma za afya na ushauri katika maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani yaliyofanyika Nyamongo, Halmashauri ya Wilaya ya Tarime.

**
Katika dhamira yake ya kuendelea kuunga mkono jitihada za Serikali za kuboresha huduma katika sekta ya afya nchini, Mgodi wa Barrick North Mara uliopo wilayani Tarime mkoani Mara, umewezesha na kuungana na Halmashauri ya Wilaya ya Tarime, Ofisi ya Mganga Mkuu wa Wilaya na wadau wengine kuadhimisha Siku ya UKIMWI Duniani mwaka huu wa 2025.
WATENDAJI WA MITAA HANDENI MJI WANOLEWA USIMAMIZI WA MIRADI YA MAENDELEO

WATENDAJI WA MITAA HANDENI MJI WANOLEWA USIMAMIZI WA MIRADI YA MAENDELEO

December 02, 2025 Add Comment

Na Mwandishi Wetu, Handeni TC

Wenyeviti wa Serikali za Mitaa pamoja na Watendaji wa Mitaa katika Halmashauri ya Mji Handeni wamepatiwa mafunzo maalum ya uongozi na utawala bora, yanayolenga kuongeza ufanisi katika utekelezaji wa majukumu yao, hususan usimamizi wa miradi ya maendeleo na utoaji wa huduma bora kwa wananchi.

Akizungumza wakati wa mafunzo hayo yaliyofanyika Desemba 1, 2025, Mkuu wa Wilaya ya Handeni, Mhe. Salum Nyamwese, amewataka viongozi hao kutumia kikamilifu ujuzi walioupata ili kuboresha utendaji katika maeneo wanayosimamia.

Amesema viongozi wa mitaa wana nafasi muhimu katika kuhakikisha miradi ya maendeleo inatekelezwa kwa ubora unaotakiwa, kwa kuzingatia maslahi mapana ya wananchi na matumizi sahihi ya rasilimali.

Mhe. Nyamwese amesisitiza pia umuhimu wa kudumisha amani ya nchi, akibainisha kuwa ni urithi wenye thamani mkubwa uliopatikana kupitia juhudi za viongozi wa kizazi kilichotangulia, hivyo ni wajibu wa kizazi cha sasa kuithamini, kuilinda na kuikuza kwa ustawi wa taifa.

Awali, akifunga mafunzo hayo, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Handeni, Maryam Ukwaju, amewataka Wenyeviti na Watendaji wa Mitaa kutumia mafunzo hayo kuongeza ufanisi na kuleta matokeo yenye tija katika maeneo yao ya kazi.

Aidha, amewahimiza kuzingatia weledi, uwajibikaji na uadilifu katika usimamizi wa miradi ya maendeleo, akisisitiza kuwa wananchi wana matarajio makubwa kutoka kwao katika kusukuma agenda za ustawi wa jamii.

DC NYAMWESE: JIUNGENI NA BIMA YA AFYA KUPUNGUZA GHARAMA ZA MATIBABU

DC NYAMWESE: JIUNGENI NA BIMA YA AFYA KUPUNGUZA GHARAMA ZA MATIBABU

December 02, 2025 Add Comment

Na Mwandishi Wetu, Handeni TC

Mkuu wa Wilaya ya Handeni, Mhe. Salum Nyamwese, amewataka wananchi wa wilaya hiyo kujiunga na Mfuko wa Afya ya Jamii Ulioboreshwa (iCHF) ili kunufaika na matibabu nafuu na kupunguza mzigo wa gharama za huduma za afya katika ngazi ya familia.

Akizungumza wakati wa maadhimisho ya Siku ya Ukimwi Duniani yaliyofanyika katika Kata ya Msasa, Mhe. Nyamwese amesema kujiunga na bima hiyo ni sehemu ya utekelezaji wa mpango wa Bima ya Afya kwa Wote, ambao ni miongoni mwa ahadi alizoahidi kuzitekeleza Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ndani ya siku 100 baada ya kuchaguliwa kwake.

Amesema iCHF imeendelea kuwa mkombozi kwa wananchi wengi kutokana na kuwezesha upatikanaji wa huduma bora kwa gharama nafuu, hivyo kutoa nafasi kwa familia kupanga matumizi mengine ya kimaendeleo.

“Afya bora ni nguzo muhimu ya uzalishaji. Kila kaya inapaswa kuwa na bima ili huduma za matibabu zipatikane kwa wakati bila kuathiri uchumi wa familia,” amesema.

Awali, akiwasilisha taarifa ya mapambano dhidi ya Ukimwi wilayani humo, Mratibu wa Ukimwi wa Halmashauri ya Mji Handeni, Joyce Gideon, amesema halmashauri inaendelea kufanya vizuri katika kuwafikia wananchi wanaoishi na VVU.

Amesema watu 205 waliobainika kuwa na maambukizi wameanza dawa za kufubaza virusi, huku asilimia 99 ya watu wanaoishi na VVU wakijua hali zao. Aidha, aliongeza kuwa asilimia 98 ya wanaotumia dawa hizo wana kiwango kidogo sana cha virusi mwilini, ishara ya mafanikio makubwa ya matibabu.

Maadhimisho ya Siku ya Ukimwi Duniani 2025 yamefanyika yakiwa na kaulimbiu: “Imarisha Mwitikio, Tokomeza UKIMWI”.

KARNE YA AI: 'SADC BADO KUNA PENGO LA MAWASILIANO YA SAYANSI'

December 02, 2025 Add Comment




Na Veronica Mrema - Pretoria 

Ulimwengu wa sayansi na teknolojia unasonga kwa kasi ya ajabu. Mataifa makubwa duniani yanawekeza kwenye ubunifu, utafiti wa kisayansi, na teknolojia za kisasa.

Teknolojia kama akili unde, kilimo cha kisasa na tiba za kibunifu zaidi zinabadilisha maisha katika mataifa makubwa duniani.

Karne ya akili unde [AI], roketi zinavuka anga, kuna uvumbuzi na gunduzi nyingi katika teknolojia mpya kwa kasi ambayo dunia haijawahi kushuhudia.

Mataifa makubwa yanawekeza, yanashirikiana, na yanapasha habari za sayansi kwa umma wao kwa kasi.

Lakini upande mwingine wa dunia, ndani ya Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika [SADC], bado kuna pengo kubwa katika mawasiliano ya sayansi. 

Watafiti wanagundua, Serikali zinafanya miradi, taasisi zinavumbua, lakini taarifa 'hazitembei' kwa kasi inayohitajika.

Bado haziwafikii vema wananchi wake, hazijengi uelewa na hazifanyi sayansi kuwa sehemu ya maisha ya kila siku.

Ndani ya SADC, bado kuna pengo kubwa kati ya maendeleo ya ki-sayansi na jinsi ambavyo taarifa hizo zinavyowafikia wananchi.

"Kwa sababu nchi nyingi za SADC bado hazina mkakati wa mawasiliano katika masuala ya sayansi,".

Yameelezwa hayo na Mkurugenzi Mkuu wa Ushirikiano wa Kimataifa na Afrika, Wizara ya Sayansi, Teknolojia na Ubunifu (DSTI), Afrika Kusini Mwampei Chaba.

Ni wakati alipokuwa akifungua mdahalo wa siku moja wa waandishi wa masuala ya sayansi kutoka nchi 18 wanachama wa SADC.

Amesema kutokana na pengo lililopo katika upashanaji habari kuhusu maendeleo ya sayansi katika nchi hizo, ndiyo maana DSTI iliona vema kuwaleta pamoja waandishi wa habari na kufanya mdahalo huo.

Ni katika mkutano wa kimataifa wa waandishi wa habari za masuala ya sayansi [WCSJ2025] unaofanyika Pretoria nchini Afrika Kusini.

Akifungua mjadala huo, aliweka wazi changamoto kubwa wanazokutana nazo waandishi wa sayansi katika ukanda huu.

“Nchi nyingi katika SADC bado hazina mkakati wa ushirikiano katika mawasiliano kuhusu sayansi. Hiyo ndiyo sababu upashanaji habari za sayansi unakumbwa na changamoto nyingi.”

Ameongeza "Ukosefu wa mkakati huo unawafanya waandishi wengi kukosa ushirikiano wanaohitaji kutoka kwa Serikali zao.

"Mnashindwa kuwa karibu na watafiti, mnakosa mazingira rafiki ya kupata habari, pamoja na fursa za ufadhili au mwaliko kwenye matukio muhimu yanayohusu sayansi na uvumbuzi.

Amesisitiza "Kwa hivyo, katika nchi yako na unataka kupata ushirikiano kutoka Serikali [kuandika kuhusu habari fulani inayohusu sayansi] au unataka watambue kazi yako.

"Unataka kufadhiliwa kwa baadhi ya kazi zako. Unataka kualikwa kwenye matukio [kwa wengi wenu], itakuwa ngumu kwa kuwa hawana mkakati wa ushirikiano kuhusu hilo," amesema.

"Mkirudi nchini mwenu kafuatilieni hili kwa undani, nendeni mkaulize wizara [zinazohusika na masuala ya] sayansi, wizara za mawasiliano [iwapo] wameandaa mkakati?.

Hii ni mara ya kwanza kwa Bara la Afrika kuwa mwenyeji wa mkutano wa kimataifa wa waandishi wa habari za sayansi, afya, mazingira na mambo mengine yanayohusiana na hayo.

Mdahalo huo kwa ajili ya waandishi wa habari kutoka SADC ulilenga kuwaleta pamoja kujadiliana namna gani watasukuma mbele masuala ya sayansi ndani ya nchi zao kwa upashanaji habari.

"Hii ni warsha ya mafunzo yenye umuhimu mkubwa kwetu. wazo hili lilikuja kwetu mwaka 2022 tulipoandaa Mkutano wa Sayansi Duniani (World Science Forum).

"..,, ambao ulikuwa wa kwanza kuandaliwa barani Afrika. Kwa hivyo, tulitengeneza historia mwaka 2022 kwa kuandaa mkutano wa Sayansi Duniani barani Afrika. 

"Kisha tukaamua kuwa kuleta fursa kama hii barani Afrika bila waandishi, waandishi wa sayansi kuwa kwenye chumba, kungekuwa kupoteza. 

Ameongeza "Tunawezaje kuwasilisha kile tunachofanya katika mkutano, kama idara, kama serikali barani Afrika, kama taasisi zinazofanya utafiti, ikiwa hatuna uandishi wa sayansi kwenye chumba?

"Pia tuligundua kuwa waandishi wa sayansi bado hawana uwezo wa kutosha kuhusiana na uandishi na kuandika makala za sayansi. 

"Hivyo basi, tuliona hitaji la kuunda ushirikiano. Na Stellenbosch alishirikiana nasi kwa kiwango kikubwa. 

Amesema walianza kupanga warsha ya mafunzo, yenye vipengele vingi, ambayo itasaidia kujenga uwezo wa waandishi wa habari katika kuwasilisha kazi tunazofanya kwa ufanisi zaidi. 

"UNESCO ilifadhili baadhi ya wajumbe mwaka 2022, na imeendelea kuwa mshirika wetu tangu wakati huo. 

"Sekretari ya SADC pia imekuwa mshirika wetu, na tunashukuru sana michango waliyotoa kwa waandishi wa SADC kuungana nasi. 

"Chama cha Waandishi wa Sayansi wa Afrika Kusini (SASJA) pia kimeungana nasi, na sisi pia tuko kwenye mshirika mkubwa katika mkutano mwingine wa kihistoria," amebainisha,

Amesema mkutano wa WCSJ2025 walioandaa mwaka huu unatengeneza historia mpya nyingine na walitaka kuwa sehemu ya historia hiyo.

Amesema Afrika Kusini waliunda mkakati wa mawasiliano na ushirikiano katika masuala ya sayansi tangu mwaka 2015 na kwamba walichelewa mno kuunda.

"Taasisi yetu ilianzishwa Juni 2004, hivyo karibu miaka 11 baadaye, tu wakati huo tu tulikuwa na mkakati wa ushirikiano wa sayansi unaotekelezwa kwa sasa, na mchakato wa ukaguzi upo.

Amebainisha "Mwaka huu SADC ilishiriki katika G20. Tulikuwa Rais wa G20 na GSTI ilipanga kile kinachoitwa Wiki ya Utafiti na Ubunifu [Research and Innovation Week]. 

"Pia tulipitisha hati maalumu inayoitwa Azimio la Ushirikiano wa Sayansi wa G20 (G20 Science Engagement Resolutions). 

"Hati hiyo inahimiza nchi za G20 kuweka sayansi kati-kati ya jamii inahimiza kuongeza ufahamu katika jamii zetu kuhusu thamani ya sayansi, na kuwasilisha sayansi kwa njia jamii zinaweza kuelewa.

"Kwa nini tunapaswa kufanya hivyo? Ni kwa nini hii ni muhimu? Sayansi haifadhiliwi vya kutosha, na hili ni changamoto katika jamii nzima.

Amesisitiza "Ikiwa thamani ya sayansi haifahamiki, ikiwa athari ya sayansi haijulikani kwa serikali zetu, jamii zetu, wafadhili wetu na wachangiaji.

"Basi mpango wa kufafanua ni ninyi walioko hapa. Ninyi ndio midomo yetu. Ninyi ndio mabalozi wetu wa kuwasilisha sayansi kwa jamii. 

"Mara sayansi itakapofahamika, mara thamani ya sayansi itakapothibitishwa kwenye hatua za vitendo, kwenye jamii, kwenye vijiji.

"Basi mna nafasi nzuri ya kupata ufadhili kutoka Serikalini, ufadhili kutoka kwa wafadhili na kadhalika. 

"Kwa hivyo, jukumu lenu ni muhimu sana, na tunategemea ninyi kusaidia kuunganisha pengo," amesema na kuongeza, 

"Napenda kuwahimiza kwamba katika wiki hii, mchukue fursa ya warsha nyingi zinazofanyika kuhamasisha sayansi. 

"Matumizi ya data, sita-sita kusema kwamba sayansi inapaswa kuwa kati-kati ya jamii, elimu, viwanda, ili kuendesha maendeleo kwa ujumla. 

"Na haiwezi kuwa katikati ikiwa ninyi hufahami jinsi ya kuwasilisha sayansi. Nami naamini hatuhitaji kuwa wanasayansi ili kuelewa sayansi. 

"Sayansi inapaswa kufafanuliwa kwa mtu wa miaka 85 na mtoto wa miaka 5. Bila kutumia maneno magumu. 

Amesisitiza "Ikiwa mtu hawezi kueleza, ikiwa mwanasayansi unayemhoji hawezi kueleza sayansi yao kwa njia unayoielewa, basi hawafanyi kazi nzuri. 

"Na pia unapaswa kuwa na uwezo wa kuhimiza wanasayansi kuzungumza na kuwasilisha sayansi kwa njia kila mtu anaweza kuelewa.

Amehoji "Je, unajua waandishi mashuhuri wa sayansi barani Afrika? Kwa nini haingewezekana iwe wewe?

"Kwa nini haingewezekana iwe wewe?” aliuliza, akiwahimiza washiriki kuwa wao wenyewe wanaweza kuwa waandishi mashuhuri wa sayansi Barani Afrika. 

“Kuna waandishi wa sayansi mashuhuri duniani kote, lakini sio barani Afrika. Afrika inahitaji sayansi kwa maendeleo zaidi kuliko kanda nyingine yoyote duniani. 

"Hivyo basi, tufanye lengo letu kuwa na waandishi mashuhuri wa sayansi katika jamii zetu, nchi zetu, ndani ya SADC na barani kote. 

Amesisitiza "Vinginevyo, mbona mko hapa? Kwa nini mko hapa ikiwa hatutumiwe kile tulicho nacho kuwasilisha sayansi na kuifanya iwe ‘fashionable’?”

Amehimiza waandishi wa habari kutumia vema majukwaa ya kidigitali kama fursa ya kufikisha taarifa muhimu zinazohusu sayansi kwa kundi la vijana ambalo kubwa lipo kwenye majukwaa hayo.

"Kila mtu yupo TikTok, kila mtu yupo YouTube, lakini lazima tuone maudhui ya sayansi pia kwenye TikTok au YouTube. 

"Tumia majukwaa haya maarufu kuwasilisha sayansi. Tuwafikie vijana walipo kwenye YouTube, Instagram na mitandao mingine na kuwapa elimu ya sayansi kwa njia wanayoielewa.”

Picha zote kwa hisani ya DSTI

WATAKA UVUVI WA KOKORO UDHIBITIWE UNAATHIRI VIUMBE WA BAHARINI

December 02, 2025 Add Comment


Na Oscar Assenga,MKINGA

WAKULIMA wa Mwani Katika Maeneo ya Boma Subutini Kata ya Boma wilayani Mkinga mkoani Tanga wameitaka Serikali kuona namna ya kuzibiti uvuvi wa kokoro ambao ndio chanzo kikubwa cha kuathiri viumbe hai wa bahari na mazao ya mwani.

Walitoa wito huo mwishoni mwa wiki katika mdahalo wa wavuvi na wakulima wa mwani katika Kata ya Boma wilayani Mkinga ikiwa ni muendelezo wa mradi wa kujenga uwezo kwa matumizi ya rasilimali za bahari ngazi ya kata.

Mradi huo unaendeshwa na Shirika la Umoja wa Wasaidizi wa Sheria wilayani Mkinga (Uwashem) ukifadhiliwa na Shirika la  4H Tanzania pamoja na We World ambapo kwa sasa utasaidia kuwaweka kwenye hali ya amani ili waweze kushirikiana kwa pamoja kufanya kazi bila kuwepo mvutano wowote.

Akizungumza katika mdahalo huo Mwaita Miraji alisema kwamba uvuvi wa kutumia kokoro umekuwa kikwazo kikubwa kwa ustawi wa viumbe vya baharini lakini pia kuharibu zao la mwani  jambo ambalo linapelekea kuwarudisha nyuma kimaendeleo.

Alisema kwamba wanaishukuru Serikali kwa kuzibiti na kutokomeza uvuvi haramu katika maeneo mbalimbali hapa nchini lakini hivi sasa wanawaomba waelekeze nguvu kwenye kutekeleza uvuvi wa kokoro ambao nao umekuwa ukileta athari kubwa.

“Tunaiomba Serikali itumie mbinu walizotumia kutokomeza uvuvi haramu wautumie kutokomeza wa Kokoro ambao umekuwa ukileta athari kubwa hususani katika mazao ya mwani yaliyopo baharini”Alisema

Aidha alisema kwamba uvuvi wa kokoro sio mzuri kutokana na kwamba unachangia kuharibu mazalia ya bahari pamoja na kuadhimia kwa pamoja uvuvi huo unaathiri ustawi wa viumbe wa bahari na hivyo kupelekea mazao ya bahari kuadimika .

“Tunaomba ikiwezekana uvuvi wa kokoro ubadilishwe jina na kuitwa uhalifu wa Kokoro lengo likiwa kuhakikisha unatokomezwa kwenye jamii lakini Serikali iwekeze nguvu zake katika mapambano ya kutokomeza uvuvi huo “Alisema

Naye kwa upande Gonda Mwaita ambaye ni mkulima wa mwani alitaka Serikali iweke sheria kali za kuwadhibiti wavuvi wanaokamatwa wakivua kupitia kokoro kutokana na kwamba umekuwa ukichangia kuharibu mazalia ya bahari ikiwemo mashamba ya mwani na hivyo kurudisha nyuma juhudi za wakulima hao.

“Lakini pia kuwepo na faini kubwa mtu akikamatwa analipa laki tano kama faini wakati huo tayari unakuwa umeshaharibu mashamba ya mwani baharini huo ni uhalifu hivyo iongezwe kwa lengo la kudhibiti uendelee”Alisema

Awali akizungumza katika mdahalo huo Afisa Mtendaji wa Kata ya Boma Hadija Mganga alisema uwepo wa elimu hiyo itawasaidia  wakulima wa mwani kwani wamekuwa hawana amani na ukulima wao unakuwa wa kuzorota kutokana na kuathiriwa na uvuvi wa kokoro na kupelekea mtu mmoja moja kushindwa kujimudu katika uchumi.

Alisema kwamba jambo hilo wakishirikiana na watendaji wa vijiji na kata kusimamia kwa kupewa nguvu ili kuweza kuwatoa kwenye hilo jambo kwa sababu Kata ya Boma ndio kitovu cha shughuli za Mwani na uwepo wa kiwanda kidogo cha ukaushaji wa mwani ili kudhalisha.

Hadija alisema kwamba kwa kuharibu mazao hayo kunarudisha nyuma na kuwavunja moyo hivyo wanalishukuru shirika la uwashem kutoa elimu na wananchi wametoa mapendekezo ya Kamati za BMU zijengewe uwezo na zisimamie hasa majukumu yao.

Alisema mwingiliano wa wavuvi na wakulima wa mwani yakitokea wakibishana na kugombana mwisho wa siku wanaumizani na mwisho wa wiku sio jambo nzuri kwa Taifa na Kamati ngazi ya kata wapo tayari kushirikiana na vyombo vya ulinzi kuweza ktoa taarifa za kina kuhusu hali hiyo chanzo ni nini  na wanaamini wakishirikiana kwa pamaoja na kuwa agenda yao kubwa kwenye vikao vyao na hivyo kuweza kupiga vita vitendo hivyo.

Hata hivyo alisema kwa upande wake Mratibu wa Uwashemu Salehe Sokoro alisema kwamba anaamini changamoto ambazo zimeelezwa katika mdahalo huo zimechukuliwa na zitakwenda kufanyiwa kazi ili kukomesha vitendo vya namna hiyo kwenye maeneo husika