HABARI

SIASA

ELIMU

Recent Posts

SERIKALI IMETOA BIL 424.6 UTEKELEZAJI MIRADI YA TANRODS RUKWA-ENG MWANGA

October 20, 2025 Add Comment
Katika kipindi cha miaka minne ya Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan imetoa zaidi ya shilingi bilioni 424.6 kwa ajili ya kutekeleza miradi mbalimbali ya Kitaifa ikiwemo Ukarabati wa uwanja wa Ndege Sumbawanga na ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami.

DAKIKA ZA LALA SALAMA,DKT NCHIMBI ATUA KILWA KUSAKA KURA ZA USHINDI WA CCM

October 20, 2025 Add Comment


Mgombea mwenza wa Urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi mapema leo Oktoba 20, 2025 amewasili katika uwanja wa ndege wa Kilwa mkoani  Lindi,ikiwa ni muendelezo wa mikutano ya Kampeni ya kusaka kura za ushindi wa kishindo kwa Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Dkt.Samia Suluhu Hassan,Wabunge na Madiwani.

Ikiwa zimebaki siku 9  za lala salama kufikia uchaguzi mkuu,Dkt. Nchimbi anatarajia kufanya mkutano wake wa hadhara wa kampeni wa kunadi Sera na Ilani ya CCM (2025-2030) katika kata ya Tingi, jimbo la Kilwa  Kaskazini na kuomba  ridhaa ya wananchi kukipigia kura za ndio chama hicho kupitia wagombea wake katika nafasi zote kwenye uchaguzi mkuu unaotarajia kufanyika Oktoba 29, 2025.



NEWALA WAIPA KONGOLE REA MRADI WA KUSAMBAZA UMEME VITONGOJINI

October 19, 2025 Add Comment
-Waeleza kuridhishwa na kasi ya utekelezaji wake

DKT.NCHIMBI ATIKISA TUNDURU,AMUOMBEA KURA DKT.SAMIA

October 19, 2025 Add Comment

PICHA mbalimbali za Mgombea mwenza wa Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) Dkt. Emmanuel John Nchimbi akiwa katika mkutano wake wa hadhara wa kampeni uliofanyika kata ya Nalasi,Jimbo la Tunduru Kusini,mkoa wa Ruvuma, leo Oktoba 19,2025, katika mwendelezo wa mikutano yake ya hadhara ya kampeni nchi nzima kusaka kura za ushindi wa kishindo za mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Dkt.Samia Suluhu Hassan,Wabunge na Madiwani.

Akiwa katika mkutano huo wa kampeni pamoja na kunadi sera na Ilani ya CCM ya 2025-30 ,Dkt.Nchimbi aliwashukuru wananchi wa Tunduru kwa kujitokeza kwa wingi kwenye mkutano wake huku akiwaomba kujitokeza kwa wingi ifikapo Octoba 29,2025 kuwapigia kura  za kishindo Wagombea wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) .

Katika hatua nyingine Dkt.Nchimbi alitumia nafasi hiyo kuwanadi wagombea Ubunge wa mkoa huo,akiwemo mgombea Ubunge wa jimbo la Tunduru Kusini,Mhandisi Fadhili Sandali CHILOMBE na Mgombea Ubunge wa Jimbo la Tunduru Kaskazini Ndugu Sikudhani Yassin CHIKAMBO pamoja na Madiwani







PIGENI KURA ZA MAENDELEO- MHE. WANU

October 19, 2025 Add Comment

Na Yohana Kidaga- Rufiji

Mlezi wa Umoja wa Wanawake wa CCM Tanzania( UWT) Wilaya ya Rufiji, na Mgombea wa Ubunge kwa jimbo la Makunduchi, Mhe. Wanu Hafidh ametoa wito kwa wanarufiji na watanzania kwa ujumla kukipigia kura CCM kwenye uchaguzi mkuu ili kupata maendeleo ya kweli.
TAMISEMI  YAAHIDI KUSHIRIKIANA NA TEMDO KUTUMIA BIDHAA ZA NDANI

TAMISEMI YAAHIDI KUSHIRIKIANA NA TEMDO KUTUMIA BIDHAA ZA NDANI

October 19, 2025 Add Comment

Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Bw Adolf Ndunguru,akipata maelezo  wakati akikagua  bidhaa mbalimbali zinazozalishwa na Taasisi ya Uhandisi na Usanifu Mitambo Tanzania (TEMDO) katika Makao Makuu ya taasisi hiyo leo  Oktoba 19, 2025,  jijini Arusha.

Na.Mwandishi Wetu

Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Bw Adolf Ndunguru amesema TAMISEMI itaendelea kushirikiana na Taasisi ya Uhandisi na Usanifu Mitambo Tanzania (TEMDO) kwa kuzihamasisha Halmashauri zote nchini kuanza kutumia bidhaa na vifaa tiba vinavyozalishwa na Shirika hilo katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo, hususan kwenye sekta za afya, elimu na kilimo.

Bw. Ndunguru ameyasema hayo leo  Oktoba 19, 2025, alipotembelea makao makuu ya TEMDO jijini Arusha, ambako alipata fursa ya kujionea namna bidhaa mbalimbali zinavyozalishwa na kujadili jinsi taasisi zilizo chini ya TAMISEMI zinavyoweza kushirikiana na TEMDO katika miradi ya maendeleo na kimkakati.

Amesema Serikali, kupitia dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, inaendelea kuimarisha sekta ya afya kwa kuhakikisha upatikanaji wa vifaa tiba bora, imara na vyenye gharama nafuu ili wananchi wapate huduma bora za afya katika vituo vyao.

Aidha, Bw. Ndunguru ameisisitiza TEMDO kuendeleza ubunifu katika bidhaa zake ili ziweze kushindana katika soko na kutumika zaidi na hospitali pamoja na vituo vya afya nchini.

Kwa upande wake, Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda na Biashara, Dkt. Hashil Abdallah, ameihakikishia TAMISEMI kuwa TEMDO ina uwezo mkubwa wa kutengeneza vifaa tiba kwa viwango vya kimataifa vilivyothibitishwa na Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba (TMDA) pamoja na Bohari ya Dawa (MSD), na kwamba taasisi hiyo iko tayari kutoa huduma kwa halmashauri zote nchini.

Naye Kaimu Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa TEMDO, Profesa Lazaro Busagala, amesema kuwa taasisi hiyo inazalisha zaidi ya bidhaa 16 zikiwemo vifaa tiba vya hospitali kama majokofu ya kuhifadhia maiti, vichomea taka hatarishi, na vitanda vya aina mbalimbali.

Aidha amesisitiza kuwa bidhaa hizo zinapaswa kufika hadi Zanzibar ili kuongeza pato la taifa, kukuza uchumi na kupunguza uagizaji wa bidhaa kutoka nje ya nchi.

Awali, Mkurugenzi Mkuu wa TEMDO, Profesa Frederick Kahimba, amebainisha kuwa tangu mwaka 2022 hadi sasa taasisi hiyo imetengeneza zaidi ya vifaa tiba 1,000 vyenye thamani ya shilingi 2,335,133,622/= na wateja wa TEMDO kuwa ni pamoja na MSD, Hospitali ya Bugando-ZRH, Uhuru Hospital, Hospitali za Kanda za Wizara ya Ulinzi, JKT, Jeshi la Polisi, Hospitali ya Wilaya ya Maswa na Hospitali ya Jiji la Arusha (CSR).

Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Bw Adolf Ndunguru,akizungumza wakati wa ziara ya kukagua bidhaa mbalimbali zinazozalishwa na Taasisi ya Uhandisi na Usanifu Mitambo Tanzania (TEMDO) katika Makao Makuu ya taasisi hiyo leo  Oktoba 19, 2025,  jijini Arusha.

 Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda na Biashara, Dkt. Hashil Abdallah,akizungumza wakati wa ziara ya kukagua bidhaa mbalimbali zinazozalishwa na Taasisi ya Uhandisi na Usanifu Mitambo Tanzania (TEMDO) katika Makao Makuu ya taasisi hiyo leo  Oktoba 19, 2025,  jijini Arusha.

Kaimu Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa TEMDO, Profesa Lazaro Busagala,akielezea  bidhaa zinazozalishwa katika Taasisi ya Uhandisi na Usanifu Mitambo Tanzania (TEMDO)  iliyopo   jijini Arusha.

Mkurugenzi Mkuu wa TEMDO, Profesa Frederick Kahimba,akitoa taarifa za  bidhaa zinazozalishwa katika Taasisi ya Uhandisi na Usanifu Mitambo Tanzania (TEMDO)  iliyopo   jijini Arusha.

Wakimsikiliza Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Bw Adolf Ndunguru,(hayupo pichani) akizungumza wakati wa ziara ya kukagua bidhaa mbalimbali zinazozalishwa na Taasisi ya Uhandisi na Usanifu Mitambo Tanzania (TEMDO) katika Makao Makuu ya taasisi hiyo leo  Oktoba 19, 2025,  jijini Arusha.

Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Bw Adolf Ndunguru,akikagua  bidhaa mbalimbali zinazozalishwa na Taasisi ya Uhandisi na Usanifu Mitambo Tanzania (TEMDO) katika Makao Makuu ya taasisi hiyo leo  Oktoba 19, 2025,  jijini Arusha.

Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Bw Adolf Ndunguru,akipata maelezo wakati akikagua  bidhaa mbalimbali zinazozalishwa na Taasisi ya Uhandisi na Usanifu Mitambo Tanzania (TEMDO) katika Makao Makuu ya taasisi hiyo leo  Oktoba 19, 2025,  jijini Arusha.

Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Bw Adolf Ndunguru,akipata maelezo i wakati akikagua  bidhaa mbalimbali zinazozalishwa na Taasisi ya Uhandisi na Usanifu Mitambo Tanzania (TEMDO) katika Makao Makuu ya taasisi hiyo leo  Oktoba 19, 2025,  jijini Arusha.

DKT.NCHIMBI "SITAWAANGUSHA WANA NYASA" ATAKA DKT.SAMIA AUNGWE MKONO OCTOBA 29.

October 19, 2025 Add Comment

Wakati ikiwa imesalia takribani siku 1O kabla ya Kufanyika kwa Uchaguzi mkuu wa Oktoba 29, Mgombea mwenza wa Kiti cha Urais kupitia CCM, Balozi Dkt Emmanuel Nchimbi ametoa rai kwa Wakazi wa Lituhi, Jimbo la Nyasa mkoani Ruvuma kutunza Vitambulisho vya kupigia kura kwa ajili ya kutimiza Wajibu wa kikatiba na Msingi ili kuchagua Viongozi watakaounda Serikali ijayo, ambayo itakuwa Chini ya Dkt Samia Suluhu Hassan.

Dkt Nchimbi ametoa rai hiyo leo Oktoba 19, 2025 akiwa katika  muendelezo wa Kampeni za Kusaka Kura za Ushindi wa Dkt Samia Suluhu Hassan pamoja na Kunadi Ilani ya Uchaguzi ya CCM na Sera zake ambazo pia zimelenga Kuboresha maisha ya Watanzania.

"Ndugu zangu Wana nyasa, nimekuja hapa kwa ajili ya Kuwahakikishia kwamba sitawaangusha, nitakuwa Msaidizi mzuri wa Dkt Samia Suluhu Hassan, kwa hiyo nami niwaombe msiniangushe Ifikapo Oktoba 29, mjitokeze kwa Wingi kwenda kupiga kura na Kumchagua Dkt Samia Suluhu Hassan ili aweze kuongoza Serikali ijayo kwa Muhula wa miaka mingine mitano" amesema Dkt Nchimbi.