

HABARI NA MATUKIO MBALIMBALI


Meneja Mkazi wa Barrick nchini, Dkt. Melkiory Ngido akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya uzinduzi wa awamu ya pili ya mradi wa Barrick–Twiga Future Forward Education Program uliozinduliwa Kibaigwa, mkoani Dodoma, na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI), Profesa Riziki Shemdoe.*************
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi akiwa katika picha ya pamoja na Mkurugenzi Mkuu waBaraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) Dkt. EmmaculateSware pamoja na Watumishi waliofanya kazi pamoja na Makamu wa Raiswakati akifanya kazi Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira(NEMC). Picha hiyo imepigwa mara baada ya Makamu wa Rais kukamilishaziara aliyoifanya Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC), Mikocheni Jijini Dar es Salaam, leo tarehe 02 Julai 2026. 









📌_*Kamisheni ya Ardhi, ZRA na ZAECA yaweka kambi Nungwi kubaini ukiukwaji wa masharti ya umiliki wa ardhi katika mahoteli.*_
📌_*Ukaguzi waongeza ukusanyaji wa mapato na kuwezesha utoaji wa mikataba ya ardhi kwa wawekezaji.*_
Kamisheni ya Ardhi Zanzibar kwa kushirikiana na Mamlaka ya Mapato Zanzibar (ZRA) na Mamlaka ya Kuzuia Rushwa na Uhujumu Uchumi Zanzibar (ZAECA), imefanya ziara maalumu ya ukaguzi wa vibali vya ardhi kwa wawekezaji wa mahoteli katika Shehia ya Banda Kuu, Nungwi, Wilaya ya Kaskazini A, Mkoa wa Kaskazini Unguja, ikiwa ni sehemu ya juhudi za kubaini ukiukwaji wa masharti ya umiliki wa ardhi na kuhakikisha ukusanyaji wa kodi ya ardhi unaimarishwa.
Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Katibu Tawala wa Wilaya ya Kaskazini A, Dkt. Farid Mohammed Haji @faridhaji_ , aliyemwakilisha Mkuu wa Wilaya Laila Burhan Ngozi, amesema ukaguzi huo umelenga kubaini wawekezaji wanaokiuka masharti ya umiliki wa ardhi, ikiwemo kutolipa kodi ya ardhi kwa Serikali.
Amesema ukaguzi huo umezaa matokeo chanya baada ya kuwabaini baadhi ya wawekezaji ambao hawakuwa wametekeleza wajibu wao wa kulipa kodi ya ardhi, hatua iliyowezesha mamlaka husika kuchukua hatua stahiki kwa mujibu wa sheria.
Kwa upande wake, Katibu Mtendaji wa Kamisheni ya Ardhi Zanzibar, Mussa Kombo, amesema ukaguzi huo ni sehemu ya mkakati wa Kamisheni wa kuhakikisha wawekezaji wote wanatekeleza wajibu wao wa kulipa kodi ya ardhi kwa wakati na kuzingatia masharti ya umiliki wa ardhi. Ameeleza kuwa zoezi hilo pia limechangia kuongeza mapato ya Serikali kupitia malipo ya kodi ya ardhi, sambamba na utoaji wa mikataba ya ardhi kwa baadhi ya wawekezaji ambao hapo awali hawakuwa na mikataba hiyo.
Amesisitiza kuwa utoaji wa mikataba hiyo utaimarisha uwazi na uhalali wa umiliki wa ardhi, huku ukichangia usimamizi bora wa rasilimali za ardhi Zanzibar na kuhakikisha sheria za ardhi zinaendelea kuheshimiwa na kutekelezwa ipasavyo.




