HABARI MPYA
HABARI
SIASA
ELIMU
Recent Posts

WADAU:AFRIKA INAPASWA KUJITEGEMEA KATIKA CHAKULA
habari
DAR ES SALAAM:
Mabadiliko yanayoendelea kufanyika katika mpango wa Marekani wa Food for Peace yameibua mjadala muhimu ambao Afrika haiwezi tena kuupuuza: utegemezi wa muda mrefu wa misaada ya chakula kutoka nje ya bara.
Kwa zaidi ya miongo saba, mpango huo umekuwa miongoni mwa vyanzo vikubwa vya msaada wa chakula kwa mataifa yanayokabiliwa na njaa, migogoro na majanga ya kibinadamu. Hata hivyo, taarifa za hivi karibuni zinaonyesha kuwa mwelekeo wa mpango huo unabadilika, huku ukihusishwa zaidi na maslahi ya kilimo na biashara ya Marekani kuliko malengo ya kibinadamu pekee.
Kwa Afrika, suala hili linapaswa kutazamwa kama tahadhari badala ya mgogoro. Linaonesha jinsi usalama wa chakula wa bara unavyoweza kuathiriwa na maamuzi yanayofanyika nje ya mipaka yake.
Kwa miaka mingi, mataifa mengi ya Afrika yamekuwa yakitegemea misaada ya chakula wakati wa ukame, migogoro au misukosuko ya kiuchumi. Ingawa misaada hiyo imeokoa maisha ya mamilioni ya watu, imeacha swali muhimu: Je, usalama wa chakula wa Afrika unaweza kuendelea kutegemea sera zinazobadilika kulingana na vipaumbele vya mataifa wafadhili?
Jibu linaonekana kuwa hapana.
Hoja hii inaendana na mjadala mpana unaoendelea kuhusu uhuru wa kiuchumi wa Afrika. Wanasiasa, wachambuzi na wanazuoni wengi wa Kiafrika wamekuwa wakisisitiza kuwa uhuru wa kisiasa hauwezi kuwa kamili bila uwezo wa bara kujitegemea kiuchumi.
Mgombea urais wa Tanzania kupitia chama cha ADC, Doyo Hassan Doyo, hivi karibuni alieleza kuwa Afrika inapaswa kuimarisha mifumo yake ya ndani badala ya kutegemea sana taasisi za kimataifa. Akizungumzia nafasi ya bara katika mfumo wa dunia, alisema lengo si kujitenga na mataifa mengine bali kuhakikisha usawa katika mahusiano ya kimataifa.
“Lengo si kujitenga, bali ni kuwa na uwiano,” alisema.
Kauli hiyo inaweza kutumika pia katika mjadala wa usalama wa chakula. Kadri nchi za wafadhili zinavyobadilisha sera zao kulingana na mahitaji ya ndani, ndivyo hatari ya Afrika kubaki katika mazingira ya kutegemea maamuzi ya wengine inavyoongezeka.
Wakati huo huo, Afrika ina rasilimali nyingi zinazoweza kuiwezesha kujitosheleza kwa chakula. Bara lina sehemu kubwa ya ardhi inayofaa kwa kilimo ambayo bado haijatumika kikamilifu, vyanzo vikubwa vya maji pamoja na nguvu kazi inayoongezeka kwa kasi.
Hata hivyo, changamoto zinaendelea kujitokeza katika maeneo ya umwagiliaji, uhifadhi wa mazao, usafirishaji na uchakataji wa bidhaa za kilimo. Kiasi kikubwa cha mazao hupotea baada ya kuvunwa huku baadhi ya nchi zikiendelea kuagiza chakula kutoka nje.
Hali hii inaonesha kuwa tatizo si ukosefu wa rasilimali, bali ni namna ya kuzitumia kwa ufanisi.
Eneo la Biashara Huria la Afrika (AfCFTA) linaweza kuwa sehemu ya suluhisho. Kupitia ushirikiano wa kikanda, nchi za Afrika zinaweza kurahisisha biashara ya mazao ya kilimo na kuhakikisha maeneo yenye ziada ya chakula yanasaidia yale yanayokabiliwa na upungufu.
Lakini mafanikio hayo hayawezi kupatikana bila taasisi imara za ndani.
Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dk. Lupa Ramadhani, anaamini kuwa uimara wa mifumo ya utawala ni msingi muhimu wa kujenga uhuru wa kweli wa Afrika.
“Kushindwa kuchukua hatua ndani ya nchi kunakaribisha uangalizi kutoka nje,” amesema.
Kauli hiyo inaakisi hali ilivyo katika sekta ya chakula. Pale ambapo sera za kilimo hazitekelezwi ipasavyo, uwekezaji ni mdogo au taasisi zinashindwa kutimiza wajibu wake, utegemezi wa misaada kutoka nje huongezeka.
Katika kipindi ambacho dunia inashuhudia mabadiliko ya kisiasa na kiuchumi, pamoja na kuongezeka kwa ushindani wa kijiografia kati ya mataifa makubwa, Afrika inalazimika kufikiria upya mkakati wake wa maendeleo.
Hii haimaanishi kukataa ushirikiano wa kimataifa. Misaada ya kibinadamu itaendelea kuwa muhimu wakati wa majanga na dharura. Hata hivyo, ushirikiano huo unapaswa kuimarisha vipaumbele vya Afrika badala ya kuvibadilisha.
Mustakabali wa usalama wa chakula wa bara hautaamuliwa Washington, Brussels au katika miji mingine ya dunia. Utaamuliwa na maamuzi yatakayofanywa katika miji mikuu ya Afrika kuhusu uwekezaji katika kilimo, miundombinu, biashara ya kikanda na taasisi za umma.
Mjadala kuhusu Food for Peace ni zaidi ya mjadala wa misaada. Ni ukumbusho kwamba uhuru wa kweli unahitaji uwezo wa kulisha wananchi wako mwenyewe. Kwa Afrika, huo si uchaguzi wa kisera pekee, bali ni hitaji la kimkakati kwa mustakabali wa bara.

TAASISI ZA UMMA NA BINAFSI ZAHIMIZWA KUWAJIBIKA KWA JAMII
habari
Mwenza wa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mama Neema Mwigulu Nchemba, amehimiza Taasisi za umma na binafsi kuendelea kuunga mkono juhudi za Serikali katika kuboresha huduma za kijamii kupitia utekelezaji wa programu za uwajibikaji kwa jamii (CSR).
Ameyasema hayo, Juni 16, 2026 katika hafla ya kukabidhi vifaa vya hospitali vilivyotolewa na Shirika la Viwango Tanzania (TBS) katika Hospitali ya Wilaya ya Chamwino, Mkoa wa Dodoma, ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 50 ya Shirika hill.
Aisha, Mama Neema ameishukuru, Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa uwekezaji mkubwa katika sekta ya afya hususani katika ujenzi wa Hospitali, utoaji wa ajira kwa wataalamu wa atya, upatikanaji wa dawa na vifaa tiba pamoja na kuimarisha huduma za kibingwa na ubingwa bobezi ziliOrahisisha upatikanaji wa huduma bora za afya nchini.
Amesema vifaa hivyo vilivyotolewa vinajumuisha vitimwendo 20, vitanda vya kujifungulia vitano, vitanda vya kufanyia uchunguzi vitano, vitanda vitano vya kulaza wagonjwa, machela moja ya kisasa, makabati matatu ya kuhitadhia vitaa tiba pamoja na mabeseni yenye vifaa mbalimbali kwa ajili ya akinamama 30 waliojifungua vitasaidia vitasaidia kuboresha utoaji wa huduma katika Hospitali ya Wilaya ya Chamwino na kuongeza ustawi wa mama na mtoto.
Awali, akimkaribisha mgeni rasmi kuzungumza katika hafla hiyo, Waziri wa Viwanda na Blashara, Judith Kapinga amesema Serikali itaendelea kuhimiza taasisi zake kutekeleza kwa vitendo sera ya uwajibikaji kwa jamii ili kuchangia kuboresha huduma za kijamii na maisha ya wananchi.
Naye Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Mhe. Rosemary Senyamule, amesema Mkoa wake uko tayari katika kushirikiana na Wizara Pamoja na TBS kwa ujumla katika kuendeleza Sekta ya Viwanda na Biashara na jitihada za uwajibikaji kwa Jamii katika Mkoa wake.
Naye Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya (TBS) Profesa Othman Chande na Mkurugenzi Mkuu wa TBS, Dkt. Ashura Katunzi wamesema TBS itaendelea kutekeleza sera yake ya kuwajibika kwa jamii (CSR Policy) ili kuendelea kuwa karibu na jamii katika kuleta tija na maendeleo.

WAFANYABIASHARA WATAKIWA KUHAKIKI MIZANI KABLA YA KUIUZA SOKONI
habariTANESCO YAKAMILISHA MIRADI YA KUIMARISHA UPATIKANAJI WA UMEME DODOMA
📌 Itanufaisha wilaya za Kongwa,Gairo, Mpwapwa, na Chamwino
📌 Waziri Ndejembi azindua Kituo cha Kubadilishia Njia za Usambazaji Umeme na Transfoma ya Kudhibiti Umeme
📌 Serikali yawekeza zaidi ya Shilingi Bilioni 10.5 kuimarisha huduma ya umeme
Na Mwandishi Wetu, Kongwa
Wananchi wa Wilaya za Gairo, Mpwapwa, Kongwa, Chamwino na Kiteto wanatarajiwa kunufaika na huduma ya umeme wa uhakika zaidi kufuatia kukamilika kwa miradi ya kuimarisha mfumo wa usambazaji wa umeme iliyotekelezwa na Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) kwa gharama ya zaidi ya Shilingi bilioni 10.5.
Miradi hiyo inahusisha Kituo cha Kubadilishia Njia za Usambazaji Umeme (Switching Station), Transfoma ya Kudhibiti Umeme (Automatic Voltage Regulator – AVR) yenye uwezo wa MVA 20 pamoja na njia ya kusafirisha umeme ya msongo wa kilovoti 33 kutoka Kituo cha Kupokea na Kupoza Umeme cha Zuzu hadi Mbande yenye urefu wa kilomita 92.
Akizindua miradi hiyo Juni 16, 2026 katika eneo la Mbande, Wilaya ya Kongwa, Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi, alisema uwekezaji huo ni sehemu ya juhudi za Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, za kuhakikisha wananchi wanapata huduma ya umeme wa uhakika kwa ajili ya shughuli za kijamii na kiuchumi.
Alisema miradi hiyo imeleta maboresho makubwa katika mfumo wa usambazaji wa umeme katika ukanda huo, ambapo hapo awali hitilafu zilizokuwa zikitokea katika eneo moja zilisababisha wananchi wa maeneo mengine kukosa huduma ya umeme kwa muda.
“Kituo hiki kimeimarisha upatikanaji wa umeme wa uhakika. Tunamshukuru sana Mheshimiwa Rais kwa uwekezaji mkubwa uliofanyika. Hapo awali changamoto zilikuwa kubwa, hususan wakati wa mvua ambapo hitilafu katika wilaya moja ziliathiri huduma katika wilaya nyingine. Leo tunashuhudia matokeo ya uwekezaji huu kwa manufaa ya wananchi wetu,” alisema Mhe. Ndejembi.
Waziri huyo alibainisha kuwa Serikali itaendelea kuwekeza katika sekta ya nishati kupitia miradi mbalimbali ya kimkakati inayolenga kuimarisha uzalishaji, usafirishaji na usambazaji wa umeme nchini ili kuendana na kasi ya maendeleo ya Taifa na mahitaji ya wananchi.
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini, Mhe. Subira Mgalu, alisema utekelezaji wa miradi ya umeme unaendelea kuleta matokeo chanya kwa wananchi na kuchangia kufanikisha agenda ya maendeleo ya Serikali.
“Tunafarijika kuona kazi kubwa inayofanywa na TANESCO kuhakikisha Watanzania wanapata umeme wa uhakika. Hapo nyuma kulikuwa na changamoto za kukatika kwa umeme mara kwa mara katika maeneo haya, lakini Serikali ya Awamu ya Sita imefanya uwekezaji mkubwa kupitia TANESCO na matokeo yake yanaonekana wazi,” alisema Mhe. Mgalu.
Naye Mkuu wa Wilaya ya Kongwa, Mhe. Mayeka Simon Mayeka, aliwataka wananchi na wawekezaji kutumia fursa ya upatikanaji wa umeme wa uhakika kuanzisha shughuli mbalimbali za uzalishaji mali ikiwemo viwanda vya usindikaji, biashara na shughuli nyingine za kiuchumi zitakazochochea maendeleo ya eneo hilo.
Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO, Bw. Lazaro Twange, alisema kwa muda mrefu wananchi wa Kongwa na maeneo jirani walitegemea njia moja ya umeme ya msongo wa kilovoti 33 kutoka Dodoma Mjini, hali iliyokuwa ikisababisha changamoto za upatikanaji wa umeme wa uhakika kutokana na ongezeko la mahitaji ya huduma hiyo.
Alisema kukamilika kwa miradi hiyo kumeimarisha mfumo wa usambazaji wa umeme katika ukanda huo na kupunguza kwa kiasi kikubwa changamoto zilizokuwa zikiathiri upatikanaji wa huduma.
“Awali kulikuwa na njia moja ya kusambaza umeme inayopita katika wilaya tano tofauti. Kuongezeka kwa mahitaji ya umeme pamoja na fursa za uwekezaji kulianza kuleta changamoto katika utoaji wa huduma. Tangu miradi hii ilipoanza kufanya kazi, tumeshuhudia maboresho makubwa na changamoto zilizokuwa zikiathiri huduma zimepungua kwa zaidi ya asilimia 90,” alisema Bw. Twange.
Kukamilika kwa miradi hiyo kunatarajiwa kuimarisha zaidi upatikanaji wa huduma ya umeme, kuongeza fursa za uwekezaji, kukuza shughuli za kiuchumi na kuboresha utoaji wa huduma za kijamii katika Wilaya za Gairo, Mpwapwa, Kongwa, Chamwino na Kiteto.

EWURA YAFIKIA WANANCHI,MAONESHO YA WIKI YA UTUMISHI WA UMMA 2026
habari

MRADI MPYA WA UMEME KONGWA KULETA AHUENI KWA WAMILIKI WA VIWANDA
Na Mwandishi Wetu
Wamiliki wa viwanda vidogo katika Wilaya ya Kongwa wameeleza matumaini makubwa ya kuondokana na changamoto ya umeme mdogo (low voltage) na mgao wa umeme kufuatia kuzinduliwa kwa mradi mpya wa miundombinu ya umeme utakaoimarisha upatikanaji wa nishati katika eneo hilo.
Mradi huo unahusisha ujenzi wa njia ya kusafirisha umeme ya kilovoti 33 (33kV) kutoka Zuzu hadi Mbande yenye urefu wa kilomita 32 pamoja na kituo cha kubadilisha na kusambaza
umeme chenye uwezo wa MVA 20, kitakachoboresha huduma za umeme katika wilaya za Kongwa, Chamwino na maeneo jirani.
Akizungumza kwa niaba ya wamiliki wa viwanda hivyo wakati wa hafla ya uzinduzi wa mradi huo iliyofanyika leo Juni 16, 2026, Mbande wilayani Kongwa, Mjumbe wa Umoja wa Viwanda Vidogo Wilaya ya Kongwa na mwakilishi wa mwenyekiti wa umoja huo, Nemes Adam Mtei, amesema tatizo la umeme lilikuwa likisababisha hasara kubwa kwa wafanyabiashara.
"Tumekuwa na shida kubwa sana ya umeme mdogo usioridhisha, hali iliyosababisha kuungua kwa mota za mashine zetu na kupunguza uzalishaji. Tunamshukuru sana Waziri kwa kutuletea mradi huu ambao tunaamini utabadilisha maisha ya wafanyabiashara na wananchi kwa ujumla," amesema Mtei.
Mtei, ambaye pia ni mkazi wa Kibaigwa, amepongeza Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi, kwa kuzindua mradi huo na kumshukuru Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO, Lazaro Twange, kwa usimamizi uliowezesha kukamilika kwa mradi huo wenye thamani ya Sh.bilioni 10.5.
Amesema mradi huo uliokuwa ukisubiriwa kwa muda mrefu sasa utafungua fursa mpya za uwekezaji, kuongeza uzalishaji wa viwanda vidogo na kukuza uchumi wa wananchi wa Kongwa na maeneo ya jirani.
&&&
DKT .BATILDA BURIAN TANGA IPO TAYARI KUMPOKEA MWENGE WA UHURU 2026
Na Paskal Mbunga,TANGA
Mwenge wa Uhuru 2026 unatarajiwa kuwasili mkoani Tanga Juni 17 mwaka huu, ambapo utakimbizwa katika halmashauri zote 11 za mkoa huo na kukagua, kuzindua pamoja na kuweka mawe ya msingi katika miradi 73 yenye thamani ya zaidi ya Sh bilioni 27.7.
Akizungumza leo na waandishi wa habari kuhusu maandalizi ya Mbio za Mwenge wa Uhuru 2026, Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Balozi Dk. Batilda Burian, alisema Mwenge wa Uhuru utapokelewa katika Viwanja vya Shule ya Msingi Mji Mpya, Kijiji cha Mtoro, Kata ya Tunguli wilayani Kilindi ukitokea Mkoa wa Morogoro.
Alisema baada ya mapokezi hayo, Mwenge utakimbizwa kwa umbali wa kilometa 1,340 kupitia halmashauri zote za Mkoa wa Tanga kabla ya kukabidhiwa Mkoa wa Kilimanjaro Juni 28 mwaka huu katika Uwanja wa Shule ya Msingi Hedaru.
Dk. Burian alisema kati ya miradi 73 itakayofanyiwa kazi na Mwenge wa Uhuru, miradi 34 itawekewa mawe ya msingi, miradi 26 itafunguliwa na kuzinduliwa, miradi 11 ya vijana itakaguliwa pamoja na miradi miwili ya sekta ya maji.
Alifafanua kuwa miradi hiyo ina thamani ya Sh bilioni 27.76, ambapo Sh milioni 300.6 ni nguvu za wananchi, Sh bilioni 1.27 ni michango ya halmashauri, Sh bilioni 10.7 ni fedha za Serikali Kuu na Sh bilioni 15.47 ni mchango wa wahisani.
Akizungumzia kaulimbiu ya Mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka huu inayosema, “Tanzania ni Yetu Sote, Tushikamane kwa Pamoja Kuleta Maendeleo,” Dk. Burian alisema mkoa umejipanga kuhakikisha wananchi wa makundi mbalimbali wanashiriki kikamilifu katika shughuli zote za Mwenge.
Alisema viongozi wa serikali, watumishi wa umma, viongozi wa dini, wanawake, vijana, watu wenye mahitaji maalumu pamoja na makundi mengine wamehamasishwa kushiriki kikamilifu kuanzia mapokezi hadi makabidhiano ya Mwenge wa Uhuru.
Aidha, wananchi watapata fursa ya kuushika na kuukimbiza Mwenge huo kama sehemu ya kuimarisha mshikamano, umoja wa kitaifa na ushiriki wa wananchi katika shughuli za maendeleo.
Mbali na kuhamasisha maendeleo, Mwenge wa Uhuru utaendelea kutoa elimu kuhusu mapambano dhidi ya rushwa, malaria, VVU/UKIMWI, matumizi ya dawa za kulevya pamoja na umuhimu wa lishe bora kwa jamii.
Dk. Burian aliwataka wananchi wa Mkoa wa Tanga kujitokeza kwa wingi katika maeneo ya mapokezi, miradi na mikesha mbalimbali ili kushiriki shughuli za Mwenge wa Uhuru na kufaidika na ujumbe wake.
Alisema mkoa umejipanga kikamilifu kuhakikisha wananchi wanapata burudani na hamasa kupitia ushiriki wa wasanii na vikundi vya sanaa vitakavyoshiriki katika maeneo yote ambayo Mwenge wa Uhuru utakesha.
Kwa ujumla, alisema maandalizi ya kuupokea Mwenge wa Uhuru wa mwaka 2026 yamekamilika kwa kiwango cha kuridhisha na Mkoa wa Tanga uko tayari kwa shughuli zote za mbio hizo.
TRAMEPRO: TUTAENDELEA KUWA SAUTI YA WATU WENYE UALBINO
habariAidha limewataka ndugu wote wenye ualbino nchini Tanzania na duniani kote, wasikate tamaa na kuwakumbusha waendelee kuamini katika uwezo wao,kushiriki kikamilifu katika maendeleo ya jamii na kutimiza ndoto zao na kwamba Dunia inahitaji mchango, vipaji na uwezo wenu.
Hayo yamesemwa na Boniventura Mwalongo ambaye ni Katibu Mkuu wa Shirika la Dawa Asilia na Ulinzi wa Mazingira (TRAMEPRO)
na Mjumbe wa Kamati Maalumu ya Pamoja ya Kushughulikia Changamoto za Watu Wenye Ualbino nchini alipokuwa akitoa salamu katika Maadhimisho ya kimataifa ya kuongeza uelewa kuhusu Ualbino yaliyofanyika Juni 13,2026.
“TRAMEPRO inapenda kuwahakikishia watu wote wenye ualbino kwamba itaendelea kuwa sauti yao na mshirika wao katika kutetea haki, usawa, heshima na maendeleo yao. Ahadi yetu ni kwamba kamwe hatutawasaliti katika kusimamia haki zenu na haki za binadamu kwa ujumla.
“Tutaendelea kushirikiana na Serikali, Bunge, taasisi mbalimbali, wadau wa maendeleo na jamii kwa ujumla katika kuhakikisha kuwa watu wenye ualbino wanapata ulinzi, heshima, fursa na haki zote wanazostahili kama raia wengine,”amesema na kuongeza "Utu, usawa, upendo na uhifadhi wa mazingira ni msingi wa maendeleo endelevu na jamii yenye amani kwa wote."
Akieleza zaidi kuhusu maadhimisho hayo amesema TRAMEPRO inaamini siku hiyo ni fursa muhimu ya kuendelea kuelimisha jamii kuhusu haki, usawa, usalama, afya na ustawi wa watu wenye ualbino, pamoja na kupinga ubaguzi, unyanyapaa na vitendo vyote vya ukatili vinavyokiuka haki zao za msingi.
Pia maadhimisho hayo yanakumbusha wajibu wa pamoja wa kujenga jamii inayoheshimu utu, usawa na haki za kila mwanadamu bila kujali tofauti zake za kimaumbile.
“TRAMEPRO inatoa pongezi kwa Chama cha Watu Wenye Ualbino Tanzania (TAS), Albinism Sports Club, Serikali, Bunge, wataalamu wa tiba asili, wadau wa afya, elimu, michezo na mazingira pamoja na wanachama wote wa TRAMEPRO kwa mchango wao katika kuimarisha ustawi, usalama na maendeleo ya watu wenye ualbino nchini.”
Wakati huo huo Mwalongo ametumia maadhimisho hayo kueleza wanatambua na kupongeza mechi ya kirafiki iliyochezwa Juni 6,2026 kati ya Bunge Sports Club na Albinism Sports Club, ambayo imeendelea kuwa mfano bora wa matumizi ya michezo katika kuhamasisha ushirikishwaji, mshikamano, uelewa na mapambano dhidi ya ubaguzi kwa watu wenye ualbino.
Tukio hilo limeonesha michezo ni nyenzo muhimu ya kuunganisha jamii na kuimarisha mshikamano wa kitaifa.Tunatoa shukrani za dhati kwa viongozi wa Bunge Sports Club, Waheshimiwa Wabunge na wadau wote walioshiriki kufanikisha tukio hilo muhimu.
Aidha, wanaguswa na moyo wa upendo, utu na kujali uliooneshwa na Salma Kikwete, ambaye baada ya kuguswa na hali halisi ya baadhi ya wachezaji wa Albinism Sports Club alionesha moyo wa kuwafariji na kuwasaidia. Kitendo hicho ni mfano wa kuigwa katika kujenga jamii yenye huruma, mshikamano na usawa.
“Pia tunatoa shukrani kwa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania(TFS)kwa kuwezesha upatikanaji wa miche iliyotumika katika zoezi hilo. Mchango huo unaonesha umuhimu wa ushirikiano kati ya taasisi za Serikali, mashirika ya kiraia na wananchi katika kulinda mazingira kwa manufaa ya kizazi cha sasa na kijacho.”
NEMC YAVIFUNGIA VIWANDA VIWILI MKURANGA KWA UCHAFUZI WA MAZINGIRA
habariTANGA KUPOKEA MWENGE WA UHURU JUNI 17, MIRADI YA BIL. 27.7 KUKAGULIWA
habariNa Oscar Assenga, Tanga
Mkoa wa Tanga unatarajia kuupokea Mwenge wa Uhuru Juni 17, mwaka huu, ambapo utakimbizwa katika halmashauri zote 11 za mkoa huo na kukagua, kuzindua pamoja na kuweka mawe ya msingi katika miradi 73 yenye thamani ya zaidi ya Sh bilioni 27.7.
Hayo yalisemwa leo na Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Balozi Dk. Batilda Burian, wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu maandalizi ya mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka 2026.
Dk. Burian alisema Mwenge wa Uhuru utapokelewa katika Viwanja vya Shule ya Msingi Mji Mpya, Kijiji cha Mtoro, Kata ya Tunguli wilayani Kilindi ukitokea Mkoa wa Morogoro, kabla ya kukimbizwa kwa umbali wa kilometa 1,340 katika halmashauri zote za mkoa huo.
Alisema Juni 28, mwaka huu, Mwenge huo utakabidhiwa Mkoa wa Kilimanjaro katika Uwanja wa Shule ya Msingi Hedaru.
Kwa mujibu wa Mkuu huyo wa Mkoa, kati ya miradi 73 itakayofanyiwa kazi na Mwenge wa Uhuru, miradi 34 itawekewa mawe ya msingi, 26 itafunguliwa na kuzinduliwa, huku miradi 11 ya vijana na miradi miwili ya sekta ya maji ikikaguliwa.

Alifafanua kuwa miradi hiyo ina thamani ya Sh bilioni 27.76, ambapo Sh milioni 300.6 ni nguvu za wananchi, Sh bilioni 1.27 ni michango ya halmashauri, Sh bilioni 10.7 ni fedha za Serikali Kuu na Sh bilioni 15.47 ni kutoka kwa wahisani.
Akizungumzia kaulimbiu ya mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka huu inayosema, “Tanzania ni Yetu Sote, Tushikamane kwa Pamoja Kuleta Maendeleo,” Dk. Burian alisema mkoa umejipanga kuhakikisha wananchi wa makundi mbalimbali wanashiriki kikamilifu katika shughuli zote za Mwenge.

“Tumewaandaa viongozi wa serikali, watumishi wa umma, viongozi wa dini, wanawake, vijana, watu wenye mahitaji maalumu pamoja na makundi mengine kushiriki kikamilifu kuanzia mapokezi hadi makabidhiano ya Mwenge wa Uhuru,” alisema.
Aliongeza kuwa wananchi watapata fursa ya kuushika na kuukimbiza Mwenge huo kama sehemu ya kuimarisha mshikamano na umoja wa kitaifa unaosisitizwa katika kaulimbiu ya mwaka huu.
Mbali na kuhamasisha maendeleo, alisema Mwenge wa Uhuru utaendelea kutoa elimu kuhusu mapambano dhidi ya rushwa, malaria, VVU/UKIMWI, matumizi ya dawa za kulevya na umuhimu wa lishe bora.
Dk. Burian aliwataka wananchi wa Mkoa wa Tanga kujitokeza kwa wingi katika maeneo ya mapokezi, miradi na mikesha mbalimbali ili kushiriki shughuli za Mwenge wa Uhuru.
“Mkoa umejipanga kikamilifu kuhakikisha wananchi wanapata burudani na hamasa kupitia ushiriki wa wasanii na vikundi mbalimbali vya sanaa katika maeneo yote ambayo Mwenge wa Uhuru utakesha,” alisema.
Alisema kwa ujumla maandalizi ya kuupokea Mwenge wa Uhuru wa mwaka 2026 yamekamilika kwa kiwango cha kuridhisha na mkoa uko tayari kwa shughuli zote za mbio hizo.
ORYX YAZINDUA KITUO KIPYA CHA MAFUTA WAZO, YAAHIDI KUSOGEZA HUDUMA ZA NISHATI KARIBU NA WANANCHI
habariSERIKALI YAHAKIKISHA MAZINGIRA BORA KWA SHULE BINAFSI
habariCBE YAONGEZA KOZI ZENYE MAHITAJI MAKUBWA KATIKA SOKO LA AJIRA
habariPHD YA DKT. NSEKELA YAFICHUA SIRI YA MAGEUZI NA MAFANIKIO YA CRDB
habari

RAIS DKT. MWINYI AJUMUIKA KATIKA MAZISHI YA MSANII MKONGWE, MAREHEMU MZEE ONYANGO
habari.jpeg)
.jpeg)
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, leo tarehe 13 Juni 2026, amejumuika na wanafamilia, ndugu, jamaa, wasanii, na mamia ya waombolezaji katika mazishi ya msanii mkongwe, marehemu Issa Joseph Mohamed, maarufu kwa jina la Mzee Onyango, yaliyofanyika Kawe , Wilaya ya Kinondoni, Jijini Dar es Salaam.
Mazishi hayo yamehudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, akiwemo Naibu Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Hamis Mwinjuma, pamoja na wasanii wa fani mbalimbali na wananchi waliofika kutoa heshima zao za mwisho kwa marehemu.
Mara baada ya kuwasili, Rais Dkt. Mwinyi alisaini kitabu cha maombolezo na kutoa mkono wa pole kwa wanafamilia.
Marehemu Issa Joseph Mohamed alizaliwa tarehe 14 Aprili 1950 na kufariki dunia tarehe 11 Juni 2026, akiwa anapatiwa matibabu katika Hospitali ya Jeshi ya Lugalo, Jijini Dar es Salaam.
Wakati wa uhai wake, marehemu alipata umaarufu mkubwa kupitia kazi zake za filamu na maigizo na kujizolea heshima kubwa miongoni mwa Watanzania kwa jina la Mzee Onyango.
Marehemu amezikwa katika Makaburi ya Kondo, Ununio, Wilaya ya Kinondoni, Jijini Dar es Salaam.
Bwana ametoa na Bwana ametwaa; jina la Bwana lihimidiwe. Amina.

.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)
























