HABARI

SIASA

ELIMU

Recent Posts

KIPANGULA ASISITIZA WELEDI WA UANDISHI WA HABARI SABASABA

Kajunason July 03, 2026 Add Comment

 

Na Mwandishi Wetu

Dar es Salaam. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea kutumia Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara (Sabasaba) kutoa elimu kwa wananchi kuhusu majukumu yake, huduma mbalimbali na umuhimu wa ithibati katika kuimarisha taaluma ya uandishi wa habari nchini.

Hatua hiyo imejidhihirisha leo baada ya Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa JAB, Wakili Patrick Kipangula, kuungana na maafisa wa Bodi katika banda la JAB lililopo Kijiji cha Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, kutoa elimu kwa wananchi, kujibu maswali mbalimbali na kuzungumza na waandishi wa habari waliotembelea banda hilo.

Akizungumza katika maonesho hayo, Wakili Kipangula alisema JAB imejipanga kuhakikisha wananchi na wadau wa sekta ya habari wanapata uelewa sahihi kuhusu majukumu ya Bodi pamoja na huduma zinazotolewa kwa mujibu wa Sheria ya Huduma za Habari.

Alisema ushiriki wa JAB katika maonesho ya Sabasaba unalenga kusogeza huduma karibu na wananchi, kuongeza uelewa kuhusu umuhimu wa ithibati kwa waandishi wa habari na kuhamasisha uzingatiaji wa maadili, weledi na uwajibikaji katika taaluma ya uandishi wa habari.

Mbali na kutoa elimu, JAB inaendelea kutoa huduma mbalimbali katika banda lake ikiwemo usajili wa waandishi wa habari, utoaji wa vitambulisho vya ithibati kwa waliokidhi vigezo, marekebisho ya taarifa za usajili pamoja na ushauri kuhusu huduma zinazotolewa na Bodi.

JAB imewahimiza waandishi wa habari, wadau wa sekta hiyo na wananchi kwa ujumla kutumia fursa ya Maonesho ya Sabasaba kutembelea banda lake ili kupata huduma, elimu na ufafanuzi kuhusu shughuli zake, huku ikisisitiza kuwa ithibati ni nyenzo muhimu katika kujenga taaluma ya uandishi wa habari yenye weledi, uwajibikaji na kuaminika.

WAZIRI SANGU: TAASISI ZA DINI NI NGUZO YA AMANI, MAADILI NA MALEZI BORA

July 02, 2026 Add Comment
Na: OWM (KAM), Manyoni - Singida

Serikali imesema inatambua mchango mkubwa wa taasisi za dini katika kuimarisha huduma za kijamii kudumisha amani na kukuza maadili nchini huku ikizitaka viongozi wa dini kuendelea kushirikiana na Serikali katika kukuza malezi bora kwa watoto na vijana ili kujenga taifa lenye ustawi na mshikamano.

BARRICK-TWIGA , SERIKALI WAZINDUA MRADI WA ‘BARRICK FUTURE FORWARD EDUCATION PROGRAM AWAMU YA PILI KIBAIGWA, DODOMA

July 02, 2026 Add Comment
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI), Profesa Riziki Shemdoe akizindua jiwe la msingi la ujenzi wa madarasa sita na mabweni mawili katika Shule ya Sekondari Kibaigwa, mkoani Dodoma. Kushoto ni Meneja wa Fedha wa Barrick nchini, Penina Kituku.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI), Profesa Riziki Shemdoe akizindua jiwe la msingi la ujenzi wa madarasa sita na mabweni mawili katika Shule ya Sekondari Kibaigwa, mkoani Dodoma.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI), Profesa Riziki Shemdoe, akiwa pamoja na ujumbe kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI) na viongozi wa Mkoa wa Dodoma, wakikagua maendeleo ya mradi wa ujenzi wa madarasa na mabweni katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Kibaigwa, mkoani Dodoma.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI), Profesa Riziki Shemdoe, akiwa pamoja na ujumbe kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI) na viongozi wa Mkoa wa Dodoma, wakikagua maendeleo ya mradi wa ujenzi wa madarasa na mabweni katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Kibaigwa, mkoani Dodoma.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI), Profesa Riziki Shemdoe, akiwa pamoja na ujumbe kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI) na viongozi wa Mkoa wa Dodoma, wakikagua maendeleo ya mradi wa ujenzi wa madarasa na mabweni katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Kibaigwa, mkoani Dodoma.
Muonekano wa sehemu ya majengo katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Kibaigwa, mkoani Dodoma.
Muonekano wa sehemu ya majengo katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Kibaigwa, mkoani Dodoma.
Muonekano wa sehemu ya majengo katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Kibaigwa, mkoani Dodoma.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI), Profesa Riziki Shemdoe, akiwa pamoja na ujumbe kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI) na viongozi wa Mkoa wa Dodoma, wakikagua maendeleo ya mradi wa ujenzi wa madarasa na mabweni katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Kibaigwa, mkoani Dodoma.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI), Profesa Riziki Shemdoe akizungumza wakati wa hafla ya uzinduzi wa awamu ya pili ya mpango wa Barrick–Twiga Future Forward Education Program katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Kibaigwa, mkoani Dodoma.
Meneja Mkazi wa Barrick nchini, Dkt. Melkiory Ngido akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya uzinduzi wa awamu ya pili ya mradi wa Barrick–Twiga Future Forward Education Program uliozinduliwa Kibaigwa, mkoani Dodoma, na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI), Profesa Riziki Shemdoe.
Meneja Mkazi wa Barrick nchini, Dkt. Melkiory Ngido (kulia) akipeana mkono na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI), Profesa Riziki Shemdoe, baada ya uzinduzi wa awamu ya pili ya mpango wa Barrick–Twiga Future Forward Education Program unaotekelezwa nchini kote kwa lengo la kuboresha miundombinu katika shule za sekondari zenye madarasa ya Kidato cha Tano na Sita.
Meneja wa Fedha wa Barrick nchini, Penina Kituku, akizungumza wakati wa hafla ya uzinduzi wa awamu ya pili ya mpango wa Barrick–Twiga Future Forward Education Program uliofanyika katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Kibaigwa, mkoani Dodoma.

***
Kampuni ya Barrick, inayofanya shughuli zake kwa ubia na Serikali kupitia Twiga Minerals, imeahidi kwamba kupitia programu yake ya Barrick-Twiga Future Forward Education Program itaendelea kufanya kazi na Serikali ya Awamu ya Sita kwenye sekta ya elimu kwa kuboresha miundombinu ya elimu, kuwezesha mazingira rafiki ya kusomea kwa ajili ya kuchochea maendeleo ya taifa kwenye sekta hiyo.

JAJI MKUU ATOA NENO UTEKELEZAJI WA SHERIA YA USALAMA NA AFYA KAZINI

July 02, 2026 Add Comment
Jaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, George Masaju, akiwasilisha hotuba yake ya ufunguzi wa mafunzo ya usalama na afya kazini ya siku mbili (Julai 2-3, 2026) yanayotolewa na OSHA kwa Majaji wa Mahakama ya Rufani na Viongozi Waandamiziwa Mahakama.

DKT. MAGHEMBE ASHIRIKI MHADHARA KUANDIMISHA MIAKA 51 YA UHURU WA COMORO

July 02, 2026 Add Comment
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Ngwaru Jumanne Maghembe (Mb.), ameshiriki Mhadhara maalum wa kuadhimisha Miaka 51 ya Uhuru wa Muungano wa Visiwa vya Comoro uliofanyika katika Kituo cha Uhusiano wa Kimataifa cha Dkt. Salim Ahmed Salim, jijini Dar es Salaam.

RAIS WA MSUMBIJI AWASILI NCHINI KWA ZIARA YA KIKAZI YA SIKU TATU

July 02, 2026 Add Comment
Rais wa Jamhuri ya Msumbiji Mheshimiwa Daniel Francisco Chapo amewasili nchini kuanza ziara ya kikazi ya siku tatu, kuanzia Julai 2 -4 , 2026.

WIZARA, TAASISI NA UMMA NA BINAFSI NA MASHIRIKA YA KIRAIA YAHIMIZWA KUCHANGAMKIA FURSA MKUTANO WA COP 12

July 02, 2026 Add Comment
Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Mhe. Reuben Kwagilwa akizungumza na waandishi wa vyombo vya habari Julai 2, 2026 Jijini Tanga kuhusu tamko la serikali kuhusiana na maandalizi ya Mkutano wa wa 12 wa Nchi Wanachama wa Mkataba wa Nairobi (COP 12) unaotarajia kufanyika nchini kuanzia tarehe 6-9 Oktoba, 2026.

WATANZANIA SASA KUJIPIMA UTI WAKIWA NYUMBANI

July 02, 2026 Add Comment
…..Ni kwa kutumia kipimo cha Checkfor UTI Test

TANI 22.6 ZA DAWA ZA KULEVYA ZANASWA, WATU 188 WAKAMATWA

July 02, 2026 Add Comment
NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

MAMLAKA ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) imekamata tani 22.6 za dawa za kulevya, lita 30.5 na kilogramu 19.94 za dawa tiba zenye asili ya kulevya katika operesheni zilizofanyika nchini kati ya Mei na Juni mwaka huu, huku watuhumiwa 188 wakitiwa mbaroni na mali mbalimbali zinazohusishwa na biashara hiyo zikikamatwa.

DCEA YAWAWEZESHA WANANCHI KUTAMBUA DAWA ZA KULEVYA KWENYE MAONESHO SABASABA

July 02, 2026 Add Comment
NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

WANANCHI wanaotembelea Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba) mwaka huu watapata fursa ya kujionea kwa mara ya kwanza sampuli za aina mbalimbali za dawa za kulevya pamoja na kemikali zinazotumika kuzitengeneza kupitia mabanda ya Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA), ikiwa ni sehemu ya kampeni ya kuongeza uelewa wa jamii kuhusu madhara ya matumizi na biashara haramu ya dawa hizo.

MKENDA AITAKA COSTECH KUPIMA ATHARI YA MIAKA 40 KATIKA MAENDELEO

July 02, 2026 Add Comment
WAZIRI wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Adolf Mkenda ameutaka uongozi wa Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) kufanya tathmini ya kina ya mchango wake katika kipindi cha miaka 40 iliyopita badala ya kujikita katika kusherehekea mafanikio.

DKT. NCHIMBI: MASLAHI YA TAIFA YATANGULIZWE KATIKA USIMAMIZI WA MAZINGIRA

July 02, 2026 Add Comment
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi akizungumza na Viongozi na Watumishi wa Baraza la Taifala Hifadhi na Usimamizi Mazingira (NEMC) wakati alipofanya ziara MakaoMakuu ya NEMC, Mikocheni Jijini Dar es Salaam leo tarehe 02 Julai 2026.

*************


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi amewasihi watumishi wa Baraza la Taifa la Hifadhi naUsimamizi wa Mazingira (NEMC), kufanya kazi kwa bidii, weledi, ushirikiano nakujiepusha na vitendo vya rushwa ili kuifanya Taasisi hiyo kuwa chachu yauhifadhi wa mazingira na maendeleo ya Taifa.

Makamu wa Rais ametoa wito huo, alipofanya ziara Baraza la Taifa la Hifadhina Usimamizi wa Mazingira (NEMC) Makao Makuu, Mikocheni Jijini Dar es Salaam. Amewataka watumishi kufanya kazi kwa uadilifu na kutokuwakikwazo katika utekelezaji wa miradi mikubwa kwa kutanguliza maslahi yaTaifa mbele.

Makamu wa Rais ameipongeza NEMC kwa kutimiza miaka 40 tangukuanzishwa kwake na kuendelea kuwa chombo kinachohitajika nakutumainiwa nchini.

Aidha, Makamu wa Rais ameipongeza NEMC kwa Mpango Mkakati wa miakaMitano ambao umeanisha vitu mbalimbali vitakavyowezesha usimamizi nautunzanji wa mazingira kwa ufanisi.

Amesema uanzishwaji wa mashindano yauhifadhi wa mazingira ni muhimu kwa kuwa itakua hamasa ya upandaji mitina usafi kitaifa.

Vilevile, Makamu wa Rais amesema ili kudhibiti masuala ya uchafu ni vema pia kuwatambua wanaokuwa wamefanya vibaya katika mashindano ya usafi nakuwataja hadharani ikiwemo kupatiwa vyeti.

Ameiagiza Ofisi ya Makamu waRais, Muungano na Mazingira, kushirikiana na NEMC katika kufanikishamashindano ya usafi na utunzaji mazingira nchini.

Halikadhalika Makamu wa Rais, ameitaka NEMC kutilia mkazo suala la nishatisafi, matumizi ya teknolojia za kisasa katika kulinda mazingira pamoja nakusimamia vema suala la urejerezaji taka.

Makamu wa Rais, amewapongeza Viongozi wa NEMC kwa kuendelea namchakato wa kuifanya NEMC kuwa Mamlaka kamili. Amesema suala hilolinashughulikiwa na katika kipindi cha Serikali ya Awamu ya Sita limepewaumuhimu wa kipekee.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa Baraza la Taifa la Hifadhi naUsimamizi wa Mazingira (NEMC), Dkt. Emmaculate Sware amesema NEMC imeaandaa Mpango Mkakati wa miaka mitano yaani mwaka 2026/2027 – 2030/2031 ambao umelenga kuongeza ufanisi wa usimamizi wa mazingira, kuimarisha matumizi ya teknolojia za kidijitali, kuimarisha ukaguzi nautekelezaji wa sheria pamoja na kuchochea uchumi wa kijani na ustahimilivuwa mabadiliko ya tabianchi.

Ziara hiyo imehudhuriwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais(Muungano na Mazingira) Mhe. Hamad Masauni pamoja na Katibu Mkuu Ofisiya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Dkt. Richard Muyungi.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi akikabidhiwa zawadi na Mkurugenzi Mkuu wa Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) Dkt. Emmaculate Swaremara baada ya kuzungumza na Viongozi na Watumishi wa Baraza hilo,alipofanya ziara Makao Makuu ya NEMC, Mikocheni Jijini Dar es Salaam leotarehe 02 Julai 2026.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi akiwa katika picha ya pamoja na Mkurugenzi Mkuu waBaraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) Dkt. EmmaculateSware pamoja na Watumishi waliofanya kazi pamoja na Makamu wa Raiswakati akifanya kazi Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira(NEMC). Picha hiyo imepigwa mara baada ya Makamu wa Rais kukamilishaziara aliyoifanya Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC), Mikocheni Jijini Dar es Salaam, leo tarehe 02 Julai 2026. 


MTATIFIKOLO ASEMA SABASABA NI JUKWAA LA BIASHARA NA MAENDELEO

Kajunason July 02, 2026 Add Comment

 

Na Mwandishi Wetu

IRINGA – Mbunge wa Jimbo la Ismani, Mhe. Emmanuela Mtatifikolo, amezindua rasmi maonesho na sherehe za Sabasaba zinazofanyika katika Kata ya Ilolo Mpya, Tarafa ya Pawaga, wilayani Ismani, huku akiwataka wananchi kutumia maonesho hayo kujifunza, kufanya biashara na kuimarisha mshikamano wa kijamii.

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Mhe. Mtatifikolo alisema maonesho ya Sabasaba ni fursa muhimu kwa wananchi kukutana, kubadilishana uzoefu, kuuza na kununua bidhaa mbalimbali pamoja na kujifunza fursa za maendeleo kutoka kwa washiriki na wageni wanaotoka maeneo mbalimbali nchini.


Aliwahamasisha wananchi wa Kata ya Ilolo Mpya na Jimbo la Ismani kwa ujumla kushiriki kikamilifu katika shughuli hizo, akieleza kuwa mbali na burudani, maonesho hayo yana mchango mkubwa katika kukuza uchumi wa wananchi na kuimarisha mahusiano ya kijamii.

"Mnatakiwa kutumia maonesho haya kama jukwaa la kujifunza, kufanya biashara na kujenga mahusiano yatakayochochea maendeleo ya Ismani na wananchi wake," alisema Mtatifikolo.

Mbunge huyo pia aliwataka vijana kuendelea kufanya kazi kwa bidii na kujiepusha na vitendo vinavyoweza kuhatarisha amani na utulivu wa nchi, akisisitiza kuwa maendeleo hayawezi kupatikana bila kuwepo kwa mazingira ya amani.



Aidha, aliwahimiza wazazi na walezi kuendelea kuwalea watoto katika misingi ya maadili, uzalendo na uwajibikaji ili kujenga kizazi kitakachochangia maendeleo ya taifa.

"Malezi bora ndiyo msingi wa kujenga taifa lenye vijana wenye nidhamu, uzalendo na uwezo wa kushiriki kikamilifu katika maendeleo ya nchi," alisisitiza.

Maonesho hayo ya Sabasaba yanajumuisha shughuli mbalimbali za kijamii na kiuchumi, zikiwemo maonesho ya bidhaa, michezo ya mpira wa miguu, ngoma za asili pamoja na burudani kutoka kwa wasanii mbalimbali.



Waandaaji wa maonesho hayo wamesema lengo ni kutoa fursa kwa wananchi kuonesha bidhaa na huduma zao, kuhamasisha biashara ndogondogo na kukuza vipaji vya vijana kupitia michezo na sanaa.

Sherehe hizo hufanyika kila mwaka baada ya wananchi kumaliza shughuli za uvunaji, zikiwa sehemu ya kuimarisha mshikamano wa jamii, kuchochea biashara na kutoa burudani kwa wakazi wa Ismani na maeneo jirani.

Wananchi waliohudhuria uzinduzi huo walieleza kufurahishwa na maandalizi ya maonesho hayo, wakisema yameendelea kuwa kichocheo cha maendeleo ya kijamii na kiuchumi katika Jimbo la Ismani.

UKAGUZI WA VIBALI VYA ARDHI WAWANASA WAWEKEZAJI WANAOKWEPA KODI ZANZIBAR

July 02, 2026 Add Comment


📌_*Kamisheni ya Ardhi, ZRA na ZAECA yaweka kambi Nungwi kubaini ukiukwaji wa masharti ya umiliki wa ardhi katika mahoteli.*_


📌_*Ukaguzi waongeza ukusanyaji wa mapato na kuwezesha utoaji wa mikataba ya ardhi kwa wawekezaji.*_


Kamisheni ya Ardhi Zanzibar kwa kushirikiana na Mamlaka ya Mapato Zanzibar (ZRA) na Mamlaka ya Kuzuia Rushwa na Uhujumu Uchumi Zanzibar (ZAECA), imefanya ziara maalumu ya ukaguzi wa vibali vya ardhi kwa wawekezaji wa mahoteli katika Shehia ya Banda Kuu, Nungwi, Wilaya ya Kaskazini A, Mkoa wa Kaskazini Unguja, ikiwa ni sehemu ya juhudi za kubaini ukiukwaji wa masharti ya umiliki wa ardhi na kuhakikisha ukusanyaji wa kodi ya ardhi unaimarishwa.

Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Katibu Tawala wa Wilaya ya Kaskazini A, Dkt. Farid Mohammed Haji @faridhaji_ , aliyemwakilisha Mkuu wa Wilaya Laila Burhan Ngozi, amesema ukaguzi huo umelenga kubaini wawekezaji wanaokiuka masharti ya umiliki wa ardhi, ikiwemo kutolipa kodi ya ardhi kwa Serikali.

Amesema ukaguzi huo umezaa matokeo chanya baada ya kuwabaini baadhi ya wawekezaji ambao hawakuwa wametekeleza wajibu wao wa kulipa kodi ya ardhi, hatua iliyowezesha mamlaka husika kuchukua hatua stahiki kwa mujibu wa sheria.

Kwa upande wake, Katibu Mtendaji wa Kamisheni ya Ardhi Zanzibar, Mussa Kombo, amesema ukaguzi huo ni sehemu ya mkakati wa Kamisheni wa kuhakikisha wawekezaji wote wanatekeleza wajibu wao wa kulipa kodi ya ardhi kwa wakati na kuzingatia masharti ya umiliki wa ardhi. Ameeleza kuwa zoezi hilo pia limechangia kuongeza mapato ya Serikali kupitia malipo ya kodi ya ardhi, sambamba na utoaji wa mikataba ya ardhi kwa baadhi ya wawekezaji ambao hapo awali hawakuwa na mikataba hiyo.


Amesisitiza kuwa utoaji wa mikataba hiyo utaimarisha uwazi na uhalali wa umiliki wa ardhi, huku ukichangia usimamizi bora wa rasilimali za ardhi Zanzibar na kuhakikisha sheria za ardhi zinaendelea kuheshimiwa na kutekelezwa ipasavyo.

TAASISI 300 KUFUNGIWA MIFUMO YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA 2026/2027

July 02, 2026 Add Comment



Katika juhudi za kuhakikisha kuwa Tanzania inafikia asilimia 80 ya matumizi ya nishati safi ya kupikia ifikapo 2034, Serikali katika mwaka wa fedha 2026/2027 itasambaza mifumo ya nishati safi ya kupikia katika taasisi 300 zinazolisha watu zaidi ya 100.


Hayo yamesemwa na Mtaalam kutoka Kitengo cha Nishati Safi ya Kupikia, Wizara ya Nishati, Bw. Omari Khalifa wakati wa Maonesho ya Kimataifa ya Biashara (SabaSaba) yanayoendelea katika Viwanja vya Mwl.Nyerere jijini Dar es Salaam.


Khalifa amesema mpango huo utatekelezwa katika bajeti ya mwaka huu wa fedha kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) ambapo jumla ya shilingi bilioni 15 ambazo ni fedha za ndani zimetengwa kwa ajili ya utekelezaji wa mpango huo.


Ameeleza kuwa mifumo itakayofungwa inajumuisha gesi ya LPG, majiko banifu, mkaa mbadala pamoja na majiko ya umeme kwa lengo la kuboresha huduma za upishi, kulinda mazingira na kuimarisha afya ya watumiaji.


Katika utekelezaji wa mpango huo kampuni mbalimbali zinazotoa huduma ya mifumo ya nishati safi ya kupikia zitafaidika kupitia fursa zitakazotangazwa na REA huku taasisi hiyo ikisimamia usimikaji wa mifumo hiyo katika taasisi zitakazokidhi vigezo vilivyowekwa.