HABARI

SIASA

ELIMU

Recent Posts

WANANCHI WAHIMIZWA KUJIUNGA NA HIFADHI SKIMU

March 06, 2026 Add Comment
 

Na: OWM (KAM) - Mwanza

Serikali imehimiza wananchi kujiunga katika na Hifadhi Skimu ili kujihakikishia usalama wa maisha yao ya sasa na baadaye ikiwemo kunufaika na mafao yanayotolewa na Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF).
Akizungumza katika hafla ya uhamasishaji wa kujiunga na hifadhi hiyo, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano Mhe. Deus Sangu amewasihi wananchi kutumia fursa hiyo kujiunga kwa wingi na kuchangia kikamilifu ili wanufaike na mafao mbalimbali yakiwemo ya matibabu pamoja na mafao ya uzeeni.
Aidha, amesema kuwa Serikali kupitia Mfuko wa NSSF imeanzisha Skimu ya Taifa ya Hifadhi ya Jamii kwa wananchi waliojiajiri kwa ajili ya kuhudumia Wananchi waliojiajiri kwenye shughuli za kiuchumi.
Waziri Sangu amebainisha kuwa Hifadhi Skimu ni mpango wa uchangiaji wa hiari unaolenga kuwafikia wananchi waliojiajiri wakiwemo wavuvi, wafanyabiashara, machinga, bodaboda, wakulima, wachimbaji wadogo, wasanii pamoja na makundi mengine  yanayounda sehemu kubwa ya nguvu kazi ya Taifa.
Vilevile, amesema Serikali ya Awamu ya Sita itaendelea kuweka mazingira rafiki ya ajira na kujiajiri sambamba na kuimarisha mifumo ya hifadhi ya jamii ili kuhakikisha hakuna Mtanzania anayebaki nyuma katika kunufaika na huduma hizo muhimu.
“Hifadhi ya jamii ni haki ya msingi inayosaidia wananchi kuwa na maisha yenye heshima hasa wanapofikia umri wa uzee au wanapokumbana na changamoto zisizotarajiwa kama vile maradhi” amesema.
Awali akizungumza Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amewahimiza wananchi wa Mkoa wa huo kuchangamkia fursa ya kujiunga na Hifadhi Skimu, akieleza kuwa ni hatua muhimu ya kuilinda familia dhidi ya majanga ya maisha pamoja na kujihakikishia kipato cha baadaye.
Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii Masha Mshomba amesema Hifadhi Skimu itawasaidia wananchi kuboresha maisha yao kwa kuondokana na utegemezi, hivyo kuwawezesha kujitegemea kiuchumi na kupata usalama wa maisha yao si tu kwa sasa bali pia wanapofikia umri wa uzee.
 
 

VIWANDA MKOANI PWANI VYATAKIWA KUBORESHA MAZINGIRA YA KAZI

March 06, 2026 Add Comment

 

Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu-Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Rahma Kisuo, akizungumza na menejimenti ya Kiwanda cha Keds Tanzania Co. Ltd kinachozalisha bidhaa mbalimbali za usafi katika ziara ya kikazi Mkoani Pwani.
Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu-Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Rahma Kisuo, akitembelea maeneo mbalimbali katika Kiwanda cha Aluminium Trailers Ltd wakati wa ziara yake ya kikazi aliyofanya Wilayani Kibaha Mkoani Pwani Machi 2-3, 2026. Alioambatana nao ni Mtendaji Mkuu wa OSHA, Bi. Khadija Mwenda, Mkurugenziwa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF), Dkt. John Mduma na Watendaji wenginekatika Ofisi ya Waziri Mkuu.
Mtendaji Mkuu wa OSHA, Bi. Khadija Mwenda na Watendaji wengine katika Ofisi yaWaziri Mkuu (Kazi, Ajira na Mahusiano) wakifuatilia maelekezo ya Naibu Waziri waNchi, Ofisi ya Waziri Mkuu-Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Rahma Kisuo (hayupopichani), wakati wa ziara yake ya kikazi aliyofanya katika Wilaya Kibaha Mkoani Pwani Machi 2-3, 2026.
Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu-Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Rahma Kisuo, akiangalia bidhaa zinazozalishwa na Kiwanda cha Aluminium Trailers Ltd wakatiwa ziara yake ya kikazi aliyofanya katika Wilaya ya Kibaha Mkoani Pwani Machi 2-3, 2026.

 NaFredy Mgunda,Pwani

Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Ajira na Mahusiano), Rahma Kisuo, ameziagiza menejimenti za viwanda Mkoani Pwani kuboresha mazingira ya kazi namaslahi ya wafanyakazi ili kuwa na uzalishaji endelevu na wenye tija.

Ametoa agizo hilo katika ziara yake ya kufuatilia utekelezaji wa sheria mbalimbali za kazi ikiwemo Sheria ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi ya mwaka 2003 katikamaeneo mbalimbali ya kazi Wilayani Kibaha, Mkoani Pwani.

Akizungumza kwa nyakati tofauti katika viwanda vilivyotembelewa, Naibu Waziri Kisuoamesema pamoja na viwanda hivyo kufanya kazi nzuri ya uzalishaji na kutekelezasheria za kazi, ziara yake imabaini dosari ndogo ndogo zinazopaswa kurekebishwa nawahusika.

“Tumetembelea baadhi ya maeneo katika viwanda hivi na kujionea hali ilivyo. Kimsingiwanafanya vizuri japokuwa kuna kasoro chache tulizozibaini ikiwemo baadhi yawafanyakazi kutokuwa na mikataba ya ajira pamoja na kutokidhi baadhi ya viwango vyausalama na afya mahali pa kazi,” amesema Naibu Waziri Kisuo.

Amewaagiza watendaji kutoka Ofisi yake na Mamlaka nyingine za udhibiti, kutengamuda maalum wa kufanya ukaguzi wa kina katika viwanda hivyo ili kutoa ushauri stahikiwa maboresho yanayohitajika kwa wawekezaji.

Aidha, amewapongeza wamiliki wa viwanda husika kwa uzalishaji wenye mchangomkubwa katika uchumi wa nchi kupitia kodi inayolipwa serikalini pamoja na kuzalishaajira nyingi kwa Watanzania.

Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Usalama na Afya Mahali pa Kazi (OSHA), Bi. Khadija Mwenda, ambaye aliambatana na Naibu Waziri katika ziara hiyo, ameeleza baadhi yamapungufu yaliyobainika katika mifumo ya usalama na afya ya viwandavilivyotembelewa ikiwa ni pamoja na mazingira ya kazi yenye joto kali, vumbi la makaaya mawe kutapakaa katika mazingira, upungufu wa vifaa kinga na ukosefu wa alama za usalama.

Amemhakikishia Naibu Waziri kuwa watalaam wake watashirikiana na mamlakanyingine kufanya ukaguzi wa kina ambao utawezesha wawekezaji kupata ushauriunaohitajika ili kuboresha mazingira yao ya uzalishaji.

Kwa upande wao, viongozi wa viwanda vilivyotembelewa akiwemo Bw. Jacob Lerise, Msimamizi wa Rasilimali Watu na Utawala katika Kiwanda cha uundaji magari cha GF Vehicle Assemblies Ltd, wamemshukuru Naibu Waziri na watendaji wake na kuahidikutekeleza maagizo mbalimbali yaliyotolewa katika ziara hiyo.

Ziara hiyo ya siku mbili Wilayani Kibaha Mkoani Pwani imefanyika katika kiwanda cha bidhaa za usafi cha Keds Tanzania Co. Ltd, Aluminium Trailers Ltd ambao ni waundajiwa trela za malori, kiwanda cha kuunda magari cha GF Vehicle Assemblies Ltd pamojakiwanda cha sabuni na vipodozi cha Creative Intertraders Ltd.
MASAUNI AITAKA BODI NCMC KUIMARISHA MIFUMO YA UPIMAJI, UTOAJI TAARIFA NA UHAKIKI WA GESIJOTO

MASAUNI AITAKA BODI NCMC KUIMARISHA MIFUMO YA UPIMAJI, UTOAJI TAARIFA NA UHAKIKI WA GESIJOTO

March 06, 2026 Add Comment

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Mhe. Mhandisi Hamad Yussuf Masauni akizungumza wakati akizindua Bodi ya Kituo Taifa cha Kuratibu Kaboni (NCMC), Machi 6, 2026 jijini Dar es Salaam.

Na; Mwandishi Wetu,Dar es Salaam.

Waziri wa nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. Mhandisi Hamad Yussuf Masauni ametoa maagizo matano kwa Bodi ya Kituo Taifa cha Kuratibu Kaboni (NCMC) kilichopo Morogoro mara baada ya kuizindua bodi hiyo.

Waziri Masauni ametoa maagizo hayo Machi 6, 2026 wakati wa uzinduzi wa Bodi hiyo jijini Dar es Salaam akieleza imepaswa kuimarisha mifumo ya kitaifa ya Upimaji, Utoaji Taarifa na Uhakiki wa gesijoto (MRV) ili kuhakikisha kuwa taarifa za kaboni nchini zinakuwa sahihi, za kuaminika na zinazokubalika kimataifa.

Pia ameielekeza Bodi hiyo kuhakikisha Miradi yote ya kaboni inayotekelezwa nchini inasimamiwa kwa ufanisi, uwazi na kwa kuzingatia viwango vya kitaifa na kimataifa pamoja na maslahi mapana ya Taifa. 

Mhe. Masauni ameongeza kuwa bodi inapaswa kuweka Mazingira wezeshi yatakayovutia uwekezaji wa ndani wa kimataifa katika Sekta ya Kaboni huku ikihakikisha kuwa uwekezaji huo unalinda rasilimali za Taifa na kuleta manufaa ya kweli kwa wananchi, kuhakikisha kunakuwepo mfumo wa haki na uwazi wa mgawanyiko wa manufaa ili jamii zinazohifadhi rasilimali za asili zinufaike moja kwa moja na Miradi ya Kaboni inayotekelezwa katika maeneo yao.

“Kuimarisha ushiriki wa Tanzania katika mifumo ya kimataifa ya biashara ya Kaboni hususan chini ya Ibara ya 6 ya Mkataba wa Paris, ikiwemo mifumo ya soko la Kaboni ili kuongeza fursa za kiuchumi kwa Taifa letu.

Aidha, ameisisitiza Bodi hiyo kufanya kazi kwa bidii na kuhakikisha Kituo hicho kinaendeshwa kwa uwajibikaji, uadilifu na weledi wa hali ya juu ili kuhakikisha mifumo ya Usimamizi wa Sekta ya Kaboni inalinda kikamilifu maslahi ya Taifa.

"Ni matarajio ya Serikali kuona kituo hiki kinakuwa kitovu cha ubora katika maswala ya ufuatiliaji wa Kaboni, biadhara ya Kaboni na Tafiti za mabadiliko ya tabianchi katika ukanda wa Afrika. Haya ni matarajio makubwa kwa taifa letu na yanahitaji Usimamizi madhubuti wa taasisi, mifumo imara ya ufuatiliaji pamoja na ushirikiano wa wadau wote.” Amesema Mhe. Masauni.

Ameongeza kuwa matarajio ya Serikali yaliyoainishwa katika Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, na Mpango wa muda mrefu wa Utekelezaji wake, sekta ya Kaboni inauwezo wa kuchangia takribani Dola za kimarekani bilioni mbili kwa Mwaka katika uchumi wa Taifa.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Bodi, Dkt. Albina Chuwa amesema ushirikiano ndio jambo la msingi katika kufikisha lengo na ndoto za watanzania, hivyo watajitahidi kutafuta fursa ili kupata matokeo mazuri.

“Ushirikiano wa kutosha ndio naomba kutoka kwa kila mmoja wetu kwani haya yote tunayoyazungumza tutakuwa tunafanya kazi nyepesi katika kuhakikisha kituo chetu cha Kaboni kinafanya vizuri,” amesema Dkt. Albina.

Amesema Uzinduzi wa Bodi unakuja katika kipindi muhimu ambacho sekta ya biashara ya kaboni inaendelea kukua kwa kasi duniani na hapa nchini, NCMC ina jukumu muhimu la kuhakikisha kuwa rasilimali za kaboni za nchi yetu zinasimamiwa kwa uwazi, weledi na kwa kuzingatia mifumo na viwango vinavyokubalika kimataifa.

Wajumbe wanaounda Bodi hiyo ni Bw. Khamis Hamza Khamis, Bi. Amne Sued Kagasheki, Bi. Farhat Mabrouk, Dkt. Ladislaus Kyaruzi, Bw. Rishad Bade pamoja na Dkt.Philipina Fenest Shayo.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Mhe. Mhandisi Hamad Yussuf Masauni akizungumza wakati akizindua Bodi ya Kituo Taifa cha Kuratibu Kaboni (NCMC), Machi 6, 2026 jijini Dar es Salaam.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Mhe. Mhandisi Hamad Yussuf Masauni (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Mwenyekiti wa Bodi ya NCMC, Dkt. Albina Chuwa (kushoto kwake), Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais, Dkt, Festo Dugange, Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Dkt. Richard Muyungi (kulia kwake) na Naibu Katibu Mkuu (Mazingira) Ofisi ya Makamu wa Rais, Balozi Baraka Luvanda, mara baada ya uzinduzi wa Bodi ya Kituo Taifa cha Kuratibu Kaboni (NCMC), Machi 6, 2026 jijini Dar es Salaam.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Mhe. Mhandisi Hamad Yussuf Masauni akimpongeza Mwenyekiti wa Bodi ya Kituo Taifa cha Kuratibu Kaboni (NCMC, Dkt. Albina Chuwa mara baada ya uzinduzi wa Bodi hiyo, Machi 6, 2026 jijini Dar es Salaam

Naibu Waziri, Ofisi ya Makamu wa Rais, Dkt. Festo Dugange akizungumza wakati wa uzinduzi wa Bodi ya Kituo Taifa cha Kuratibu Kaboni (NCMC), Machi 6, 2026 jijini Dar es Salaam.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Mhe. Mhandisi Hamad Yussuf Masauni (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Wajumbe wa Bodi ya Kituo Taifa cha Kuratibu Kaboni (NCMC), mara baada ya uzinduzi wa Bodi hiyo, Machi 6, 2026 jijini Dar es Salaam.

PICHA NA OFISI YA MAKAMU WA RAIS

MAGARI YA UMEME NAFUU KWA ASILIMIA 85 UKILINGANISHWA NA MAFUTA

March 06, 2026 Add Comment




Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam


Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati, Mhandisi Felchesmi Mramba amesema utafiti unaonesha kuwa kuendesha gari la umeme nchini ni nafuu kwa takribani asilimia 85 kwa kila kilomita ikilinganishwa na gari linalotumia petroli au dizeli.

Mramba ameyasema hayo Machi 6, 2026 jijini Dar es Salaam wakati wa uzinduzi rasmi wa matumizi ya magari ya umeme nchini kupitia kampuni ya DOW ELEF AUTO EV (ZERA) Limited.

Amesema kwa wastani gari linalotumia mafuta linaweza kugharimu takribani Sh.200 kwa kilomita moja, wakati gari la umeme linatumia karibu Sh.25 pekee kwa kilomita.

“Gharama hii inaonesha wazi kuwa teknolojia ya magari ya umeme ni nafuu zaidi na inaweza kusaidia wananchi kupunguza matumizi katika sekta ya usafiri,” amesema Mramba.

Ameeleza kuwa uzinduzi huo ni hatua muhimu katika mageuzi ya sekta ya usafiri nchini na unaendana na juhudi za Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Dk. Samia Suluhu Hassan za kukuza uwekezaji na kuhamasisha matumizi ya teknolojia safi ya nishati.

Mramba amesema Serikali tayari imeweka mazingira wezeshi kwa maendeleo ya teknolojia hiyo kwa kupitisha Mfumo wa Kitaifa wa Sera ya Magari ya Umeme (National Electric Vehicles Policy Framework) Desemba 2024.


Amesema sera hiyo inalenga kuhamasisha uzalishaji wa magari ya umeme nchini, kuongeza matumizi yake, kuunganisha sekta hiyo na nishati jadidifu pamoja na kujenga miundombinu ya vituo vya kuchaji magari hayo.

Aidha, amesema Tanzania imeendelea kupiga hatua katika uzalishaji wa umeme ambapo uwezo umeongezeka hadi zaidi ya megawati 4,500, huku upatikanaji wa umeme ukifikia asilimia 85.5 mwaka 2025.

Kwa mujibu wa Mramba, hatua hiyo inalenga kuimarisha sekta mbalimbali za kiuchumi ikiwamo usafiri wa kisasa wenye gharama nafuu na rafiki kwa mazingira.

Kwa sasa Afrika ina zaidi ya magari ya umeme 30,000, huku Afrika Mashariki ikijitokeza kuwa kitovu cha ubunifu katika sekta hiyo.

Nchini Tanzania, inakadiriwa kuwa tayari kuna zaidi ya magari ya umeme 10,000 yakiwemo pikipiki pamoja na vyombo vingine vya usafiri vya magurudumu mawili na matatu.


Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Kampuni ya DOW ELEF AUTO EV (ZERA) Limited, Emmanuel Kazimoto, amesema kampuni hiyo imeanza na mpango wa kuagiza magari kamili ya umeme, kabla ya kuanza kuleta magari ya kuunganishwa hapa nchini.

Ameongeza kuwa lengo la baadaye ni kuanzisha kiwanda cha kuunganisha magari ya umeme nchini, hatua itakayochochea ajira na kuwajengea vijana wa Kitanzania ujuzi katika teknolojia ya kisasa.

NINA IMANI KUBWA NA UTENDAJI KAZI WA OFISI YA MWANDISHI MKUU WA SHERIA -MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI

March 06, 2026 Add Comment

Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Mhe. Hamza S. Johari amewataka  Watumishi wa Ofisi ya Mwandishi Mkuu wa Sheria kufanya kazi kwa Weledi na Ufanisi ili kufikia malengo ya Ofisi kwani ana Imani kubwa na utendaji kazi wa OFISI ya Mwandishi Mkuu wa Sheria.


Mhe. Johari amesema hayo alipofungua kikao cha kwanza cha Baraza la Wafanyakazi la Ofisi ya Mwandishi Mkuu wa Sheria tarehe 6 Machi, 2026 jijini Dar es Salaam.

*"Niwaombe muendelee kutekeleza majukumu ya Ofisi hii kwa Weledi na Ufanisi ili kufikia malengo ya Ofisi na nina imani kubwa na utendaji kazi wa Ofisi ya Mwandishi Mkuu wa Sheria”* amesema Mhe. Johari 

Aidha Mhe. Johari ameendelea kwa kuwataka watumishi wa  Ofisi ya Mwandishi Mkuu wa Sheria kuzingatia kanuni na Sheria za Utumishi wa Umma ili kutoathiri utendaji kazi wa Serikali.


*"Utumishi wa Umma unaongozwa na Sheria pamoja na Kanuni, hivyo natoa rai kwa watumishi wote tuzingatie Miongozo ya Utumishi wa Umma ili tusiathiri utendaji kazi wa Serikali,"* ameongeza Mhe. Mwanasheria Mkuu wa Serikali.

Vilevile Mhe. Johari ameitaka Ofisi ya Mwandishi Mkuu wa Sheria kuboresha matumizi ya mifumo ya TEHAMA ili kufanya kazi kwa ufanisi zaidi.


*"Naomba nisisitize matumizi ya mifumo ya TEHAMA ili kurahisisha utendaji kazi na kutoa kazi zenye ufanisi kwa matumizi ya Serikali na jamii kwa ujumla,"* ameeleza Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mhe. Hamza Johari.


Awali, akimkaribisha Mgeni Rasmi, Mwandishi Mkuu wa Sheria, Bw. Onorius Njole, amesema Ofisi ya Mwandishi Mkuu wa Sheria imewekeza nguvu kubwa kwenye mifumo ya TEHAMA ili kuendelea kuimarisha utendaji kazi.


*"Katika kuendelea kuimarisha  utekelezaji wa Uandishi wa Sheria tumeamua kuweka nguvu kubwa kwenye mifumo ya Tehama kwa kuanzisha e-drafting, e-translation na e-revision na kwa usaidizi wako Mwanasheria Mkuu wa Serikali tutaweza kufanikisha hili.* amesema.


Pia, Mwandishi Mkuu wa Sheria Bw. Njole amemshukuru Mwanasheria Mkuu wa Serikali kwa kuendelea kuwa kiongozi bora na mwenye msaada mkubwa kwa Ofisi ya Mwandishi Mkuu wa Sheria.



*"Kwa niaba ya menejimenti ya Ofisi ya Mwandishi Mkuu wa Sheria na Wafanyakazi wote, tunamshukuru Sana Mhe. Johari kwa kuwa kiongozi bora kwa Ofisi yetu, na kutupa ushirikiano kila tunapohitaji”* Amesema.


Miongoni mwa Wageni waalikwa katika Baraza la Wafanyakazi wa Ofisi ya Mwandishi Mkuu wa Sheria ni Mkurugenzi wa Mashtaka, Bw. Sylvester Mwakitalu. 


Baraza la kwanza la Wafanyakazi wa Ofisi ya Mwandishi Mkuu wa Sheria, limefanyika tarehe 6 Machi, 2026 katika ukumbi wa Mikutano wa Julius Nyerere (JNICC) jijini, Dar es salaam.

UMEME WA GRIDI YA KIGOMA UMEOKOA BILIONI 58 ZA MAFUTA NA MATENGENEZO -NAIBU WAZIRI MHE. SALOME

March 06, 2026 Add Comment


Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba amelipongeza Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) kwa kusimamia na kukamilisha mradi wa kupeleka umeme wa gridi mkoani Kigoma na hivyo kuokoa takribani shilingi bilioni 58 zilizokuwa zikitumika kila mwaka kwa ajili ya ununuzi wa mafuta na matengenezo ya vipuri vya majenereta ya kuzalisha umeme.

Mhe. Salome ametoa pongezi hizo tarehe 6 Machi 2026 mara baada ya kutembelea mradi wa ujenzi wa kituo kikubwa cha Kupoza umeme cha Kidahwe kilichopo mkoani Kigoma pamoja na kituo cha kupoza umeme cha kigoma mjini na kituo cha muda cha Kidahwe.

“Niwapongeze TANESCO kwa kufikisha umeme wa gridi Kigoma hasa baada ya kukamilisha mradi  kutoka Nyakanazi hadi Kigoma na kwa kuamua kutumia fedha zenu za ndani shilingi bilioni tano kukamilisha kituo cha muda cha Kidahwe ambacho kwa sasa kinapeleka umeme Kigoma wakati ujenzi wa kituo kikubwa cha umeme Kidahwe ukiendelea,” amesema Mhe. Salome

Amesema kituo kipya cha umeme cha Kidahwe kitakuwa na uwezo wa megawati 192 na hivyo kitaimarisha zaidi hali ya upatikanaji wa umeme katika Mkoa wa Kigoma ambao kwa sasa unapata takribani megawati 30.

Ameongeza kuwa kituo hicho kinatarajiwa kukamilika mwezi Novemba mwaka huu na kitasaidia pia kuimarisha hali ya umeme katika mikoa ya Magharibi, kuendesha Treni ya Mwendo Kasi (SGR) pamoja na kuchochea biashara ya umeme na nchi jirani za Magharibi mwa Tanzania.

Kutokana na uwepo wa umeme wa kutosha mkoani Kigoma, Mhe. Salome amewakaribisha wawekezaji wa ndani na nje ya nchi kuwekeza katika mkoa huo.

 Aidha, amewaasa wananchi kulinda miundombinu ya umeme akieleza kuwa Rais, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan anaendelea kutoa fedha nyingi kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya nishati nchini hivyo wananchi wanao wajibu wa kuilinda na kuithamini.

Awali, Mratibu wa Mradi wa Kusafirisha umeme wa msongo wa kilovolti 400 kutoka Nyakanazi hadi Kigoma, Mhandisi Ramadhan Uwessu, alisema kuwa ujenzi wa kituo kipya cha Kidahwe unaenda sambamba na upanuzi wa kituo cha Nyakanazi ili kukiwezesha kusafirisha umeme wa msongo wa kV 400 kutoka Nyakanazi hadi Kidahwe.

Ameongeza kuwa kituo hicho pia kitapokea umeme kutoka njia ya Tabora kwa msongo wa kV 132, kutoka Sumbawanga kwa msongo wa kV 400 pamoja na umeme utakaozalishwa kutoka mradi wa Malagarasi.

Amesema mradi huo umefikia asilimia 47 ya utekelezaji na unagharimu takribani shilingi bilioni 434 zilizotolewa na Serikali ya Tanzania, Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) pamoja na Mfuko wa Maendeleo wa Watu wa Korea Kusini (EDCF).

EWURA YAFUTA LESENI YA IYAN ENERGY,YASITISHA YA CRESCENT ENERGY KWA MIEZI SITA

EWURA YAFUTA LESENI YA IYAN ENERGY,YASITISHA YA CRESCENT ENERGY KWA MIEZI SITA

March 06, 2026 Add Comment
 

Na Mwandishi Wetu

Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) imetangaza kufuta leseni ya rejareja ya bidhaa za mafuta ya petroli ya kampuni ya Iyan Energy Limited na kusitisha kwa muda wa miezi sita leseni ya kampuni ya Crescent Energy Tanzania Limited, baada ya kubaini ukiukwaji wa sheria na masharti ya leseni.

Kwa mujibu wa taarifa ya EWURA, uamuzi huo umefanyika kufuatia maamuzi yaliyotolewa na Bodi ya Wakurugenzi wakati wa vikao vyake vya hivi karibuni.

EWURA imesema leseni iliyofutwa ni Petroleum Retail Licence Na. PRL-2018-269, iliyokuwa ikimilikiwa na Iyan Energy Limited kwa ajili ya kuendesha biashara ya rejareja ya mafuta katika Kiwanja Na. 26 na 27, Barabara ya Pangani, Jiji la Tanga.

Wakati huohuo, Bodi imesitisha kwa muda wa miezi sita leseni ya rejareja ya bidhaa za mafuta ya petroli Namba PRL-2022-296 ya Crescent Energy Tanzania Limited, iliyotolewa kwa ajili ya kuendesha biashara ya rejareja katika Kiwanja Na. 5, Kitalu “N”, Eneo la Chamakweza, Wilaya ya Chalinze, Mkoa wa Pwani.

Taarifa hiyo imeeleza kuwa maamuzi hayo yamefanyika baada ya EWURA kujiridhisha kuwa kampuni hizo zilikuwa zikijihusisha na shughuli zinazofanana na biashara ya uuzaji wa bidhaa za mafuta kwa jumla, hali ambayo haikuruhusiwa chini ya leseni za rejareja walizokuwa nazo.

EWURA imeeleza kuwa hatua hizo zinakiuka Kifungu Na. 131 cha Sheria ya Petroli, Sura ya 392, pamoja na Kanuni ya 9 na 11 za Kanuni za Mafuta (Biashara ya Jumla, Uhifadhi, Rejareja na Matumizi Binafsi), Tangazo la Serikali Na. 150/2022.

Onyo kwa umma

Katika taarifa yake, EWURA imeutaarifu umma kuwa kujihusisha kwa namna yoyote na kampuni hizo katika biashara ya usambazaji wa bidhaa za mafuta ya petroli kutakuwa kinyume cha sheria, na kwamba hatua stahiki za kisheria zitachukuliwa dhidi ya watakaokiuka.

Mamlaka hiyo imeongeza kuwa itaendelea kusimamia sekta ya mafuta kwa kuhakikisha kunakuwa na mazingira ya ushindani wa haki na upatikanaji wa uhakika wa bidhaa za mafuta nchini, kwa kudumisha “uwanja ulio sawa” kwa wadau wote.

CCM NA FRELIMO KUIMARISHA USHIRIKIANO WA KIUCHUMI

March 06, 2026 Add Comment


Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dkt. Asha-Rose Migiro, amekutana na kufanya mazungumzo na Katibu Mkuu wa Chama cha FRELIMO, (Msumbiji), Ndugu Chakil Felizardo Passadas Aboobacar, ambaye ameanza ziara rasmi ya kikazi kwa siku mbili nchini. 

Katika mazungumzo hayo yaliyofanyika leo tarehe 6 Machi 2026, katika Ofisi Ndogo za Makao Makuu ya CCM, Dar Es Salaam, vyama hivyo viwili ambavyo vina urafiki na udugu wa kihistoria, vimekubaliana kuendelea kuimarisha uhusiano uliopo kati ya pande hizo mbili, hasa kushirikiana kiuchumi.



BARRICK KUENDELEZA FURSA SAWA KWA WANAWAKE KATIKA SEKTA YA MADINI

March 06, 2026 Add Comment

Wahitimu wa Programu ya Mwanamke wa wakati ujao ya ATE (Female Future Programme) kutoka Barrick North Mara katika picha ya pamoja , kuanzia kushoto, Patricia Vulla , Elda Mahenda, Sella Mwaigomole, Edith Dickson Biita na Noela Mataro katika mahafali yaliyofanyika katika ukumbi wa Mlimani City.
Wahitimu wa Programu ya Mwanamke wa wakati ujao ya ATE (Female Future Programme) kutoka Barrick North Mara katika picha ya pamoja , kuanzia kushoto, Patricia Vulla , Elda Mahenda, Sella Mwaigomole, Edith Dickson Biita na Noela Mataro katika mahafali yaliyofanyika katika ukumbi wa Mlimani City.