HABARI

SIASA

ELIMU

Recent Posts

SERIKALI KUTEKELEZA MRADI WA UMEME JUA KATIKA VISIWA SABA MUSOMA

July 04, 2026 Add Comment

 


Serikali kupitia Wizara ya Nishati imetenga shilingi milioni 273.6 kwa ajili ya kutekeleza mradi wa kusambaza umeme wa jua katika visiwa saba vya Wilaya ya Musoma ikiwemo Nyasaungu, Muroba, Kagongo, Nyamasanje, Rukuba na Iriga, ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa dhamira ya Rais, Mhe. Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuhakikisha kila Mtanzania anapata huduma ya umeme bila kujali eneo analoishi.

Hayo yameelezwa na Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba, wakati wa ziara ya Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba, ya kutatua kero za wananchi katika Jimbo la Musoma Vijijini.

 Amesema Serikali imepiga hatua kubwa katika upatikanaji wa umeme ambapo vijiji vyote katika jimbo hilo tayari vimefikiwa na huduma hiyo, huku hatua zinazofuata zikielekezwa katika kufikisha umeme kwenye vitongoji vilivyosalia.

 Amebainisha kuwa kati ya vitongoji 374 vilivyopo, takribani 100 pekee ndivyo bado havijafikiwa na umeme huku zaidi ya vitongoji 50 vikiwa katika hatua za utekelezaji wa miradi ya usambazaji wa umeme.

Aidha, amesema Serikali imepokea maombi ya Mbunge wa Musoma Vijijini ya kuhakikisha vitongoji vyote ambavyo havina umeme vinafikiwa na huduma hiyo ifikapo mwaka 2027, akieleza kuwa lengo hilo linaendana na dhamira ya Serikali inayolenga kuhakikisha vitongoji vyote nchini vinaunganishwa na huduma ya umeme ifikapo mwaka 2030.

Sambamba na hilo, Mhe. Salome amesema Wizara ya Nishati imeendelea kuimarisha upatikanaji wa umeme katika maeneo ya uzalishaji mali, ikiwemo maeneo ya wachimbaji wa migodi wilayani Musoma Vijijini.

 Kuhusu  baadhi ya wananchi ambao miundombinu ya umeme imepita karibu na makazi yao lakini hawajaunganishwa na huduma hiyo,  amemuelekeza Meneja wa TANESCO Wilaya ya Musoma kuhakikisha wananchi hao wanaunganishiwa umeme.

Katika hatua nyingine, amewahimiza wananchi wa Musoma Vijijini kutumia nishati safi ya kupikia, akibainisha kuwa Serikali imetoa ruzuku ya zaidi ya asilimia 50 kwenye majiko ya gesi ili kuyawezesha kupatikana kwa gharama nafuu.









SALOME MAKAMBA : WANANCHI WANAOPITIWA NA MIUNDOMBINU YA UMEME WAUNGANISHIWE HUDUMA KWA SH. 27,000

July 04, 2026 Add Comment







Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba, amesema Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, imeelekeza kuwa wananchi wote ambao wamepitiwa na miundombinu ya umeme lakini bado hawajaunganishiwa huduma hiyo waunganishiwe kwa gharama ya Shilingi 27,000 tu.

Mhe. Salome ametoa kauli hiyo leo Julai 3, 2026, katika mkutano wa hadhara uliofanyika wilayani Butiama, mkoani Mara, katika ziara ya Waziri Mkuu, Mhe. Mwigulu Nchemba.

Akizungumza katika mkutano huo, Mhe. Salome amemuelekeza Meneja wa TANESCO Mkoa wa Mara pamoja na Meneja wa TANESCO Wilaya ya Butiama kubaini maeneo yote ambayo nyaya za umeme zimepita juu ya kaya za wananchi lakini bado hawajaunganishwa na huduma husika ili hatua stahiki zichukuliwe, ikiwemo kufunga transfoma katika maeneo yenye uhitaji.

Amesisitiza kuwa umeme ni nguzo muhimu ya maendeleo ya kijamii na kiuchumi, akieleza kuwa unachochea ukuaji wa uchumi, huboresha huduma za afya na kuinua ustawi wa wananchi, hivyo Serikali itaendelea kuhakikisha wananchi wote wanaostahili wanafikiwa na huduma hiyo.

Aidha, amesema Serikali kupitia Wizara ya Nishati imetenga zaidi ya Shilingi bilioni 38 kwa ajili ya utekelezaji wa Awamu ya Pili ya Mradi wa Kusambaza Umeme Vitongojini katika Mkoa wa Mara. Fedha hizo zitawezesha kuendelea kusambaza umeme katika maeneo ambayo bado hayajafikiwa na hivyo kuchochea maendeleo ya kijamii na kiuchumi.

Ameongeza kuwa, kufuatia maelekezo ya Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan, Serikali itahakikisha vitongoji 51 ambavyo havina umeme mkoani Mara vinafikiwa na nishati hiyo.

Kuhusu matumizi ya nishati safi ya kupikia, Mhe.Salome amesema Serikali inaendelea kutekeleza Mkakati wa Taifa wa Nishati Safi ya Kupikia unaolenga kuhakikisha asilimia 80 ya Watanzania wanatumia nishati safi ya kupikia ifikapo mwaka 2034.

Amesema katika Mkoa wa Mara tayari Serikali imesambaza majiko ya gesi zaidi ya 19,000 na majiko banifu zaidi ya 8,000 ili kuongeza matumizi ya nishati safi ya kupikia, kulinda afya za wananchi na kuhifadhi mazingira.

Katika mkutano huo wa hadhara, wananchi waliwasilisha jumla ya kero sita, ambapo kero tatu zilipatiwa ufumbuzi papo hapo, huku hatua za kushughulikia kero zilizobaki zikiendelea kuchukuliwa na Serikali.










DKT. MUNISI: MAHUSIANO MEMA NI NGUZO MUHIMU YA UTEKELEZAJI DIRA YA TAIFA 2050

July 03, 2026 Add Comment
Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Dkt. Evaline Munisi amesema kuwa Mafanikio ya utekelezaji wa Dira 2050 yanategemea Mahusiano mema kwa kuwa ndio matokeo ya Utawala bora, Amani, Usalama na Maendeleo endelevu.

TANZANIA YATAMBULIWA KWA MCHANGO WAKE KATIKA UHURU WA UMOJA WA VISIWA VYA COMORO WAKATI WA MHADHARA MAALUM WA KIDIPLOMASIA

July 03, 2026 Add Comment


.Ubalozi wa Umoja wa Visiwa vya Comoro nchini Tanzania umeandaa mhadhara maalum wa kidiplomasia uliogusia historia ya Comoro, safari yake ya kupata uhuru, pamoja na mchango mkubwa wa Tanzania katika harakati za ukombozi za taifa hilo la visiwa.


Comoro, inayojulikana rasmi kama Umoja wa Visiwa vya Comoro, ni taifa la visiwa lililopo katika Bahari ya Hindi kati ya pwani ya Afrika Mashariki na Madagascar. Nchi hiyo ina urithi wa kipekee ulioathiriwa na ustaarabu wa Kiafrika, Kiarabu na Kiislamu, na inaundwa na visiwa vinne vikuu: Ngazidja (Grande Comore), Ndzuwani (Anjouan), Mwali (Mohéli) na Maore (Mayotte).

Kwa karne nyingi, visiwa hivyo vilikuwa kituo muhimu cha biashara katika Bahari ya Hindi, vikiunganisha wafanyabiashara kutoka Afrika Mashariki, ulimwengu wa Kiarabu na Asia. Hata hivyo, katika karne ya 19, Ufaransa ulipanua ushawishi wake katika visiwa hivyo na hatimaye kuvijumuisha katika himaya yake ya kikoloni.

Harakati za kudai uhuru zilipata nguvu zaidi wakati wa wimbi la ukombozi barani Afrika katika miaka ya 1950 na 1960, ambapo wananchi wa Comoro walizidi kudai haki ya kujitawala chini ya uongozi wa vuguvugu za kitaifa zilizopinga ukoloni.

Tarehe 6 Julai 1975, Comoro ilitangaza rasmi uhuru wake kutoka Ufaransa, hatua iliyofungua ukurasa mpya wa taifa huru lenye mamlaka ya kuamua hatima yake. Hata hivyo, kisiwa cha Mayotte kilibaki chini ya utawala wa Ufaransa kufuatia kura ya maoni, suala ambalo limeendelea kuwa na umuhimu wa kisiasa na kidiplomasia katika masuala ya Comoro.

Katika hatua nyingine muhimu, tarehe 12 Novemba 1975, Comoro ilikubaliwa kuwa mwanachama kamili wa Umoja wa Mataifa, hatua iliyothibitisha hadhi yake kama taifa huru na mwanachama muhimu wa jumuiya ya kimataifa.

Mhadhara huo maalum wa kidiplomasia ulifanyika tarehe 2 Julai 2026 jijini Dar es Salaam katika Kituo cha Mahusiano ya Kigeni. Tukio hilo liliwakutanisha wajumbe wa kidiplomasia, mabalozi waliokubaliwa nchini Tanzania, wawakilishi wa mashirika ya kimataifa, wanafunzi wa Kituo cha Mahusiano ya Kigeni, maafisa wakuu wa serikali pamoja na wageni wengine mashuhuri. Mkutano huo ulitoa jukwaa muhimu la kutafakari uhusiano wa kihistoria kati ya Tanzania na Umoja wa Visiwa vya Comoro, huku ukisisitiza umuhimu wa diplomasia, majadiliano na mshikamano wa Kiafrika katika kuhifadhi urithi wa pamoja wa historia ya bara la Afrika.

Akifungua rasmi mhadhara huo, Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wa Tanzania, Mheshimiwa Ngwaru Maghembe, alisema uhusiano kati ya Tanzania na Umoja wa Visiwa vya Comoro ni wa kihistoria, kindugu na uliojengwa juu ya ukaribu wa kijiografia, urithi wa kitamaduni na maono ya pamoja ya amani, mshikamano na maendeleo katika eneo la Bahari ya Hindi.

Alibainisha kuwa Tanzania imeendelea kusimamia kwa uthabiti misingi ya mshikamano wa Kiafrika na haki ya wananchi kujitawala, hali inayofafanua uungaji mkono wake wa muda mrefu kwa harakati za ukombozi za Comoro na mataifa mengine ya Afrika.

Maghembe aliongeza kuwa uhusiano kati ya nchi hizo mbili umeendelea kukua katika maeneo kama diplomasia, biashara, elimu, usafiri wa baharini, usalama, utalii na ushirikiano wa kikanda.

Aidha alisema katika miaka ya hivi karibuni, Tanzania na Umoja wa Visiwa vya Comoro zimeongeza mawasiliano ya ngazi ya juu na kuimarisha diplomasia ya kiuchumi katika sekta mbalimbali, jambo linaloonesha dhamira ya pamoja ya kujenga mustakabali wenye mafanikio kwa wananchi wao.

Akizungumza katika hafla hiyo, Balozi wa Umoja wa Visiwa vya Comoro nchini Tanzania na Dean wa Mabalozi, Ahmada El Badaoui, aliwasilisha maelezo ya kina kuhusu safari ndefu ya nchi yake kuelekea uhuru pamoja na changamoto zilizokabili kabla na baada ya kupata mamlaka kamili.

Alitoa heshima kwa viongozi mbalimbali wa Afrika waliounga mkono harakati za ukombozi wa Comoro, akimtaja kwa namna ya pekee Rais wa kwanza wa Tanzania Julius Nyerere, kwa mchango wake muhimu katika kuendeleza matarajio ya wananchi wa Comoro ya kujitawala na kuimarisha juhudi za kidiplomasia zilizochangia uhuru huo.

Balozi huyo alieleza kuwa msaada wa Tanzania chini ya uongozi wa Mwalimu Nyerere uliakisi sera ya muda mrefu ya nchi hiyo ya kuunga mkono ukombozi wa Afrika, mshikamano wa bara, na kuheshimu haki ya mataifa kujitawala.

Alisisitiza kuwa historia ya Comoro haiwezi kusimuliwa kikamilifu bila kuitambua Tanzania kama mshirika wa karibu na rafiki wa kweli katika harakati zake za uhuru.

Mhadhara huo ulikuwa na ujumbe mzito wa kihistoria na kidiplomasia, ukionesha kuwa uhusiano kati ya Tanzania na Umoja wa Visiwa vya Comoro haujajengwa tu juu ya ukaribu wa kijiografia, bali pia juu ya misingi imara ya mshikamano, urafiki wa kweli, ushirikiano wa kimkakati na historia ya pamoja ya mapambano ya uhuru, heshima na maendeleo ya Waafrika.

Wakati dunia ikiendelea kukabiliana na changamoto mpya za kisiasa, kiuchumi na kiusalama, Tanzania na Umoja wa Visiwa vya Comoro zimeendelea kuwa mfano wa jinsi diplomasia, historia ya pamoja na ushirikiano wa kindugu vinavyoweza kuwa nguzo muhimu za kuimarisha amani, kukuza ushirikiano wa kikanda na kuendeleza dira ya Afrika yenye umoja, ustawi na ushawishi katika jukwaa la kimataifa.



 

WAANDISHI WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KUHUSU DAWA ZA KULEVYA

July 03, 2026 Add Comment
Na Mwandishi Wetu

MAMLAKA ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) imebainisha kuwa mwaka 2025 ilikamata tani 31.76 na lita 183,500 za kemikali bashirifu, huku ikizuia tani 734 kuingia nchini kinyume cha sheria, ikisema waandishi wa habari wanapaswa kuwa sehemu ya mapambano dhidi ya uhalifu huo kupitia utoaji wa taarifa sahihi kwa umma.

NEMC YAJA NA KIJIJI CHA MAZINGIRA MAONESHO SABASABA

July 03, 2026 Add Comment
Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) linashiriki Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam (Sabasaba) kwa kuanzisha Kijiji cha Mazingira, jukwaa maalum linalowakutanisha wananchi, wadau wa mazingira na taasisi mbalimbali kwa lengo la kutoa elimu, kuonesha ubunifu na teknolojia rafiki kwa mazingira, pamoja na kuhamasisha uhifadhi na usimamizi endelevu wa mazingira.

TANZANIA IPO TAYARI KUELEKEA AFCON 2027

July 03, 2026 Add Comment
Na. Mwandishi Wetu - Arusha

Tanzania ipo tayari kwa mashindano ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON 2027) ikiwa mwenyeji kwa kushirikiana na Kenya na Uganda ambapo maandalizi yamefikia hatua nzuri kwa kuzingatia viwango vya Shirikisho la Mpira wa Miguu Barani Afrika (CAF) vinavyotakiwa.

KIPANGULA ASISITIZA WELEDI WA UANDISHI WA HABARI SABASABA

Kajunason July 03, 2026 Add Comment

 

Na Mwandishi Wetu

Dar es Salaam. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea kutumia Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara (Sabasaba) kutoa elimu kwa wananchi kuhusu majukumu yake, huduma mbalimbali na umuhimu wa ithibati katika kuimarisha taaluma ya uandishi wa habari nchini.

Hatua hiyo imejidhihirisha leo baada ya Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa JAB, Wakili Patrick Kipangula, kuungana na maafisa wa Bodi katika banda la JAB lililopo Kijiji cha Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, kutoa elimu kwa wananchi, kujibu maswali mbalimbali na kuzungumza na waandishi wa habari waliotembelea banda hilo.

Akizungumza katika maonesho hayo, Wakili Kipangula alisema JAB imejipanga kuhakikisha wananchi na wadau wa sekta ya habari wanapata uelewa sahihi kuhusu majukumu ya Bodi pamoja na huduma zinazotolewa kwa mujibu wa Sheria ya Huduma za Habari.

Alisema ushiriki wa JAB katika maonesho ya Sabasaba unalenga kusogeza huduma karibu na wananchi, kuongeza uelewa kuhusu umuhimu wa ithibati kwa waandishi wa habari na kuhamasisha uzingatiaji wa maadili, weledi na uwajibikaji katika taaluma ya uandishi wa habari.

Mbali na kutoa elimu, JAB inaendelea kutoa huduma mbalimbali katika banda lake ikiwemo usajili wa waandishi wa habari, utoaji wa vitambulisho vya ithibati kwa waliokidhi vigezo, marekebisho ya taarifa za usajili pamoja na ushauri kuhusu huduma zinazotolewa na Bodi.

JAB imewahimiza waandishi wa habari, wadau wa sekta hiyo na wananchi kwa ujumla kutumia fursa ya Maonesho ya Sabasaba kutembelea banda lake ili kupata huduma, elimu na ufafanuzi kuhusu shughuli zake, huku ikisisitiza kuwa ithibati ni nyenzo muhimu katika kujenga taaluma ya uandishi wa habari yenye weledi, uwajibikaji na kuaminika.

WAZIRI SANGU: TAASISI ZA DINI NI NGUZO YA AMANI, MAADILI NA MALEZI BORA

July 02, 2026 Add Comment
Na: OWM (KAM), Manyoni - Singida

Serikali imesema inatambua mchango mkubwa wa taasisi za dini katika kuimarisha huduma za kijamii kudumisha amani na kukuza maadili nchini huku ikizitaka viongozi wa dini kuendelea kushirikiana na Serikali katika kukuza malezi bora kwa watoto na vijana ili kujenga taifa lenye ustawi na mshikamano.

BARRICK-TWIGA , SERIKALI WAZINDUA MRADI WA ‘BARRICK FUTURE FORWARD EDUCATION PROGRAM AWAMU YA PILI KIBAIGWA, DODOMA

July 02, 2026 Add Comment
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI), Profesa Riziki Shemdoe akizindua jiwe la msingi la ujenzi wa madarasa sita na mabweni mawili katika Shule ya Sekondari Kibaigwa, mkoani Dodoma. Kushoto ni Meneja wa Fedha wa Barrick nchini, Penina Kituku.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI), Profesa Riziki Shemdoe akizindua jiwe la msingi la ujenzi wa madarasa sita na mabweni mawili katika Shule ya Sekondari Kibaigwa, mkoani Dodoma.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI), Profesa Riziki Shemdoe, akiwa pamoja na ujumbe kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI) na viongozi wa Mkoa wa Dodoma, wakikagua maendeleo ya mradi wa ujenzi wa madarasa na mabweni katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Kibaigwa, mkoani Dodoma.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI), Profesa Riziki Shemdoe, akiwa pamoja na ujumbe kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI) na viongozi wa Mkoa wa Dodoma, wakikagua maendeleo ya mradi wa ujenzi wa madarasa na mabweni katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Kibaigwa, mkoani Dodoma.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI), Profesa Riziki Shemdoe, akiwa pamoja na ujumbe kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI) na viongozi wa Mkoa wa Dodoma, wakikagua maendeleo ya mradi wa ujenzi wa madarasa na mabweni katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Kibaigwa, mkoani Dodoma.
Muonekano wa sehemu ya majengo katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Kibaigwa, mkoani Dodoma.
Muonekano wa sehemu ya majengo katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Kibaigwa, mkoani Dodoma.
Muonekano wa sehemu ya majengo katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Kibaigwa, mkoani Dodoma.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI), Profesa Riziki Shemdoe, akiwa pamoja na ujumbe kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI) na viongozi wa Mkoa wa Dodoma, wakikagua maendeleo ya mradi wa ujenzi wa madarasa na mabweni katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Kibaigwa, mkoani Dodoma.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI), Profesa Riziki Shemdoe akizungumza wakati wa hafla ya uzinduzi wa awamu ya pili ya mpango wa Barrick–Twiga Future Forward Education Program katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Kibaigwa, mkoani Dodoma.
Meneja Mkazi wa Barrick nchini, Dkt. Melkiory Ngido akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya uzinduzi wa awamu ya pili ya mradi wa Barrick–Twiga Future Forward Education Program uliozinduliwa Kibaigwa, mkoani Dodoma, na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI), Profesa Riziki Shemdoe.
Meneja Mkazi wa Barrick nchini, Dkt. Melkiory Ngido (kulia) akipeana mkono na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI), Profesa Riziki Shemdoe, baada ya uzinduzi wa awamu ya pili ya mpango wa Barrick–Twiga Future Forward Education Program unaotekelezwa nchini kote kwa lengo la kuboresha miundombinu katika shule za sekondari zenye madarasa ya Kidato cha Tano na Sita.
Meneja wa Fedha wa Barrick nchini, Penina Kituku, akizungumza wakati wa hafla ya uzinduzi wa awamu ya pili ya mpango wa Barrick–Twiga Future Forward Education Program uliofanyika katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Kibaigwa, mkoani Dodoma.

***
Kampuni ya Barrick, inayofanya shughuli zake kwa ubia na Serikali kupitia Twiga Minerals, imeahidi kwamba kupitia programu yake ya Barrick-Twiga Future Forward Education Program itaendelea kufanya kazi na Serikali ya Awamu ya Sita kwenye sekta ya elimu kwa kuboresha miundombinu ya elimu, kuwezesha mazingira rafiki ya kusomea kwa ajili ya kuchochea maendeleo ya taifa kwenye sekta hiyo.

JAJI MKUU ATOA NENO UTEKELEZAJI WA SHERIA YA USALAMA NA AFYA KAZINI

July 02, 2026 Add Comment
Jaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, George Masaju, akiwasilisha hotuba yake ya ufunguzi wa mafunzo ya usalama na afya kazini ya siku mbili (Julai 2-3, 2026) yanayotolewa na OSHA kwa Majaji wa Mahakama ya Rufani na Viongozi Waandamiziwa Mahakama.

DKT. MAGHEMBE ASHIRIKI MHADHARA KUANDIMISHA MIAKA 51 YA UHURU WA COMORO

July 02, 2026 Add Comment
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Ngwaru Jumanne Maghembe (Mb.), ameshiriki Mhadhara maalum wa kuadhimisha Miaka 51 ya Uhuru wa Muungano wa Visiwa vya Comoro uliofanyika katika Kituo cha Uhusiano wa Kimataifa cha Dkt. Salim Ahmed Salim, jijini Dar es Salaam.

RAIS WA MSUMBIJI AWASILI NCHINI KWA ZIARA YA KIKAZI YA SIKU TATU

July 02, 2026 Add Comment
Rais wa Jamhuri ya Msumbiji Mheshimiwa Daniel Francisco Chapo amewasili nchini kuanza ziara ya kikazi ya siku tatu, kuanzia Julai 2 -4 , 2026.

WIZARA, TAASISI NA UMMA NA BINAFSI NA MASHIRIKA YA KIRAIA YAHIMIZWA KUCHANGAMKIA FURSA MKUTANO WA COP 12

July 02, 2026 Add Comment
Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Mhe. Reuben Kwagilwa akizungumza na waandishi wa vyombo vya habari Julai 2, 2026 Jijini Tanga kuhusu tamko la serikali kuhusiana na maandalizi ya Mkutano wa wa 12 wa Nchi Wanachama wa Mkataba wa Nairobi (COP 12) unaotarajia kufanyika nchini kuanzia tarehe 6-9 Oktoba, 2026.

WATANZANIA SASA KUJIPIMA UTI WAKIWA NYUMBANI

July 02, 2026 Add Comment
…..Ni kwa kutumia kipimo cha Checkfor UTI Test

TANI 22.6 ZA DAWA ZA KULEVYA ZANASWA, WATU 188 WAKAMATWA

July 02, 2026 Add Comment
NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

MAMLAKA ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) imekamata tani 22.6 za dawa za kulevya, lita 30.5 na kilogramu 19.94 za dawa tiba zenye asili ya kulevya katika operesheni zilizofanyika nchini kati ya Mei na Juni mwaka huu, huku watuhumiwa 188 wakitiwa mbaroni na mali mbalimbali zinazohusishwa na biashara hiyo zikikamatwa.

DCEA YAWAWEZESHA WANANCHI KUTAMBUA DAWA ZA KULEVYA KWENYE MAONESHO SABASABA

July 02, 2026 Add Comment
NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

WANANCHI wanaotembelea Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba) mwaka huu watapata fursa ya kujionea kwa mara ya kwanza sampuli za aina mbalimbali za dawa za kulevya pamoja na kemikali zinazotumika kuzitengeneza kupitia mabanda ya Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA), ikiwa ni sehemu ya kampeni ya kuongeza uelewa wa jamii kuhusu madhara ya matumizi na biashara haramu ya dawa hizo.

MKENDA AITAKA COSTECH KUPIMA ATHARI YA MIAKA 40 KATIKA MAENDELEO

July 02, 2026 Add Comment
WAZIRI wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Adolf Mkenda ameutaka uongozi wa Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) kufanya tathmini ya kina ya mchango wake katika kipindi cha miaka 40 iliyopita badala ya kujikita katika kusherehekea mafanikio.

DKT. NCHIMBI: MASLAHI YA TAIFA YATANGULIZWE KATIKA USIMAMIZI WA MAZINGIRA

July 02, 2026 Add Comment
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi akizungumza na Viongozi na Watumishi wa Baraza la Taifala Hifadhi na Usimamizi Mazingira (NEMC) wakati alipofanya ziara MakaoMakuu ya NEMC, Mikocheni Jijini Dar es Salaam leo tarehe 02 Julai 2026.

*************


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi amewasihi watumishi wa Baraza la Taifa la Hifadhi naUsimamizi wa Mazingira (NEMC), kufanya kazi kwa bidii, weledi, ushirikiano nakujiepusha na vitendo vya rushwa ili kuifanya Taasisi hiyo kuwa chachu yauhifadhi wa mazingira na maendeleo ya Taifa.

Makamu wa Rais ametoa wito huo, alipofanya ziara Baraza la Taifa la Hifadhina Usimamizi wa Mazingira (NEMC) Makao Makuu, Mikocheni Jijini Dar es Salaam. Amewataka watumishi kufanya kazi kwa uadilifu na kutokuwakikwazo katika utekelezaji wa miradi mikubwa kwa kutanguliza maslahi yaTaifa mbele.

Makamu wa Rais ameipongeza NEMC kwa kutimiza miaka 40 tangukuanzishwa kwake na kuendelea kuwa chombo kinachohitajika nakutumainiwa nchini.

Aidha, Makamu wa Rais ameipongeza NEMC kwa Mpango Mkakati wa miakaMitano ambao umeanisha vitu mbalimbali vitakavyowezesha usimamizi nautunzanji wa mazingira kwa ufanisi.

Amesema uanzishwaji wa mashindano yauhifadhi wa mazingira ni muhimu kwa kuwa itakua hamasa ya upandaji mitina usafi kitaifa.

Vilevile, Makamu wa Rais amesema ili kudhibiti masuala ya uchafu ni vema pia kuwatambua wanaokuwa wamefanya vibaya katika mashindano ya usafi nakuwataja hadharani ikiwemo kupatiwa vyeti.

Ameiagiza Ofisi ya Makamu waRais, Muungano na Mazingira, kushirikiana na NEMC katika kufanikishamashindano ya usafi na utunzaji mazingira nchini.

Halikadhalika Makamu wa Rais, ameitaka NEMC kutilia mkazo suala la nishatisafi, matumizi ya teknolojia za kisasa katika kulinda mazingira pamoja nakusimamia vema suala la urejerezaji taka.

Makamu wa Rais, amewapongeza Viongozi wa NEMC kwa kuendelea namchakato wa kuifanya NEMC kuwa Mamlaka kamili. Amesema suala hilolinashughulikiwa na katika kipindi cha Serikali ya Awamu ya Sita limepewaumuhimu wa kipekee.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa Baraza la Taifa la Hifadhi naUsimamizi wa Mazingira (NEMC), Dkt. Emmaculate Sware amesema NEMC imeaandaa Mpango Mkakati wa miaka mitano yaani mwaka 2026/2027 – 2030/2031 ambao umelenga kuongeza ufanisi wa usimamizi wa mazingira, kuimarisha matumizi ya teknolojia za kidijitali, kuimarisha ukaguzi nautekelezaji wa sheria pamoja na kuchochea uchumi wa kijani na ustahimilivuwa mabadiliko ya tabianchi.

Ziara hiyo imehudhuriwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais(Muungano na Mazingira) Mhe. Hamad Masauni pamoja na Katibu Mkuu Ofisiya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Dkt. Richard Muyungi.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi akikabidhiwa zawadi na Mkurugenzi Mkuu wa Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) Dkt. Emmaculate Swaremara baada ya kuzungumza na Viongozi na Watumishi wa Baraza hilo,alipofanya ziara Makao Makuu ya NEMC, Mikocheni Jijini Dar es Salaam leotarehe 02 Julai 2026.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi akiwa katika picha ya pamoja na Mkurugenzi Mkuu waBaraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) Dkt. EmmaculateSware pamoja na Watumishi waliofanya kazi pamoja na Makamu wa Raiswakati akifanya kazi Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira(NEMC). Picha hiyo imepigwa mara baada ya Makamu wa Rais kukamilishaziara aliyoifanya Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC), Mikocheni Jijini Dar es Salaam, leo tarehe 02 Julai 2026.