HABARI ZETU
Loading...

HABARI

SIASA

ELIMU

Recent Posts

MKAA MBADALA MKOMBOZI MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA KWA WATANZANIA

February 28, 2026 Add Comment



📌Ni kuelekea asilimia 80 ya Watanzania kutumia nishati safi ya kupikia ifikapo mwaka 2034


📍Morogoro


Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imeendelea kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia kwa kutumia teknolojia mbalimbali ikiwemo matumizi ya mkaa mbadala unaozalishwa nchini ili kuhakikisha asilimia 80 ya Watanzania wanatumia nishati safi ya kupikia ifikapo mwaka 2034 kulingana na Mkakati wa Kitaifa wa Matumizi ya nishati safi hapa nchini. 


Wito huo umetolewa leo Februari 28, 2026 na Mwenyekiti wa Bodi ya Nishati Vijijini (REB), Mhe. Balozi Meja Jenerali Mstaafu Jacob Kingu akiwa ameongoza na Menejimenti ya REA wakati walipotembelea kiwanda cha Shirika la Mzinga kujionea kuhusu uzalishaji wa teknolojia ya mkaa mbadala unaofanywa na Shirika hilo mkoani Morogoro.

Balozi Meja Jenerali Mstaafu Kingu ameeleza kuwa Serikali kupitia REA imehamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia ili kumuunga mkono Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia katika ajenda ya Kitaifa ya nishati safi ya kupikia katika kuwawezesha Watanzania wanatumia nishati hiyo ifikapo mwaka 2034.

"Matumizi ya mkaa mbadala yatatuwezesha kuweza kufikia asilimia 80 ya watanzania kutumia nishati safi ifikapo mwaka 2034. Ni lazima tuipe nguvu ajenda hii kwa kuwa inakwenda kuwa mkombozi kwa nchi yetu, " Ameongeza Balozi Kingu. 

Kwa upande wake, Brigedia Jenerali Seif Hamisi ambaye ni Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Mzinga ameishukuru REA kwa fursa hiyo ya kuwatembelea katika kiwanda chao cha Mzinga na kujionea namna uzalishaji wa mkaa mbadala unavyofanywa na kiwanda hicho mkoani humo. 

Amesema, ni matarajio yao kuwa kiwanda hicho kinakwenda kukidhi mahitaji ya watumiaji wa mkaa mbadala kwa kuwa kwa sasa wanaendelea kufanya tafiti na kuzungumza na wadau mbalimbali ikiwemo REA ili kuhakikisha wanapata teknolojia za kisasa zitakazowezesha kuanza kuzalisha mkaa huo kwa wingi.

Kwa upande wake, Msimamizi wa Mradi wa mkaa mbadala katika kiwanda cha Mzinga Mha. Amiri Msangi, ameeleza kuwa kwa sasa kiwanda kinaendekea kufanya tafiti wa teknolojia  teknolojia bora na rafiki ya uzalishaji wa mkaa mbadala ili uzalishaji utakapoanza na kuwa mkubwa uweze kuleta tija kwa Watanzania na kuongeza kipato kwa shirika. 




Mwisho.

WATU WENYE ULEMAVU WAJIKWAMUA KIUCHUMI KWA MIKOPO YA SERIKALI

February 28, 2026 Add Comment

 


Na Mwandishi wetu Moshi, Kilimanjaro. 


Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera Bunge Uratibu na Wenye Ulemavu Mhe. Ummy Nderiananga, amekutana na kundi la watu wenye ulemavu katika ziara iliyowakutanisha na  wanufaika wa mikopo ya 10% ya mapato ya Halmashauri (2% kwa wenye Ulemavu) na wale ambao wameomba na hawajapata.

WAZIRI NDEJEMBI ASEMA ZAIDI YA TRILIONI 1 ZIMEWEKEZWA MRADI WA GESI MTWARA

February 28, 2026 Add Comment




Mtwara


Waziri wa Nishati Mhe. Deogratius Ndejembi amesema Serikali  imewekeza zaidi ya sh. trilioni moja katika utekelezaji wa miradi ya gesi asilia mkoani Mtwara ili kuongeza uzalishaji, kuboresha miundombinu ya usafirishaji na usambazaji wa gesi asilia.


Akizungumza katika ziara yake ya kukagua miradi hiyo, Waziri Ndejembi amesema utekelezaji wa mradi wa uchimbaji wa visima vya gesi Ntorya pamoja na ujenzi wa bomba la kusafirisha gesi kutoka Ntorya hadi Madimba, na uchorongaji wa visima katika Kitalu cha Mnazi Bay utaongeza kiasi kikubwa cha gesi kwa ajili ya uzalishaji wa umeme, matumizi ya viwandani na majumbani.

Amesema mahitaji ya gesi asilia nchini yanaongezeka kwa kasi, hivyo Serikali imeweka kipaumbele katika kuimarisha sekta hiyo ili kukidhi mahitaji ya wateja wanaozidi kuongezeka.


“Miradi hii uwekezaji wake ni mkubwa Serikali imetoa kipaumbele katika eneo la Gesi asilia na sote tunajua mahitaji ya gesi asilia yanakua kwa kasi sana nchini. Wateja wamekuwa wengi hivyo changamoto hii muichukue kama fursa kwa kushirikiana na wabia wenu na Wakandarasi, muitekeleze miradi hii itakayoongeza gesi asilia, kwa kasi na ufanisi mkubwa,"amesisitiza.

Waziri Ndejembi ameelekeza kuanzia Septemba 2026 uzalishaji wa gesi katika eneo la Ntorya uanze rasmi ili kuongeza upatikanaji wa nishati ya uhakika na kuchochea shughuli za kiuchumi hususan katika Ukanda wa Kusini na maeneo mengine ya nchi.

Amebainisha kuwa jitihada hizo ni sehemu ya mkakati wa Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan, ambayo imeendelea kutoa fedha na miongozo madhubuti ili kuhakikisha miradi inatekelezwa kwa ufanisi na kwa kuzingatia thamani ya fedha.

Aidha, Waziri Ndejembi amesisitiza umuhimu wa kuendelea na utafiti pamoja na uchimbaji wa visima vipya ili kuongeza uzalishaji na kuhakikisha nchi inanufaika kikamilifu na rasilimali zake za ndani.

 Pia amelielekeza Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) kuhakikisha linarejesha kwa jamii kwa ajili ya kutekeleza miradi ya maendeleo katika maeneo yanayozunguka miradi ya gesi, ili wananchi wanufaike moja kwa moja na uwekezaji huo kwa kushirikiana na halmashauri husika.



BARRICK YAPONGEZWA KWA KUWEKA MIUNDOMBINU YA KITUO CHA MICHEZO BUZWAGI

February 28, 2026 Add Comment

    

Baadhi ya wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Taifa wa shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) wakiwa katika picha ya pamoja na Rais wa shirikisho hilo Wallace Karia na Meneja wa Ufungaji wa Mgodi wa Barrick Buzwagi, Mhandisi Zonnastraal Mumbi.
Meneja wa Ufungaji wa Mgodi wa Barrick Buzwagi, Mhandisi Zonnastraal Mumbi akitoa maelezo kwa Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) Wallace Karia na ujumbe wake walipotembelea kituo cha michezo cha Buzwagi.

Oryx Gas Tanzania Yatoa Mafunzo ya Nishati Safi kwa Watumishi wa Afya Kwimba

February 28, 2026 Add Comment
Na Mwandishi Wetu,Kwimba

WATUMISHI wa idara ya afya katika Halmashauri ya Wilaya ya Kwimba mkoani Mwanza wamepatiwa mafunzo ya matumizi sahihi na salama ya gesi ya kupikia sambamba ba kuelezea kwa kina madhara yanayotokana na matumizi ya kuni na mkaa kiafya.

Asilimia 28 Pekee ya Wanawake Wanamiliki Ardhi Tanzania

February 28, 2026 Add Comment
Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi imetangaza kuanza kwa kampeni maalum ijulikanayo kama “Samia Ardhi Kliniki” itakayofanyika katika mikoa yote 26 ya Tanzania Bara kuanzia tarehe 2 hadi 7 Machi 2026, kuelekea maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani yatakayoadhimishwa tarehe 8 Machi 2026.Akizungumza na waandishi wa habari, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Lucy Kabyemera, amesema kliniki hiyo itaendeshwa na watumishi wanawake kutoka Ofisi za Ardhi za Mikoa yote nchini kwa lengo la kusogeza huduma karibu na wananchi.
“Kupitia Samia Ardhi Kliniki tunalenga kuwafikia wanawake wengi zaidi kwa kuwapatia elimu kuhusu haki zao za umiliki wa ardhi, kuwasaidia kitaalamu na kutoa hati miliki kwa waliokamilisha taratibu,” amesema Kabyemera.
Ameongeza kuwa hatua hiyo ni utekelezaji wa maelekezo ya Samia Suluhu Hassan ya kuwataka watumishi wa umma kuwafuata wananchi na kuwapatia huduma bora kwa kuzingatia utu. “Kauli mbiu ya mwaka huu ni ‘Mwanamke; Haki Yako, Miliki Ardhi Sasa,’ na tunawahimiza wanawake wote kujitokeza kutumia fursa hii muhimu,” amesisitiza.
Kwa mujibu wa Kabyemera, serikali inalenga kuongeza idadi ya wanawake wanaomiliki ardhi kwani kwa sasa ni takribani asilimia 28 tu ya wanawake nchini ndio wanamiliki. “Tunaamini kumwezesha mwanamke kumiliki ardhi ni kuimarisha familia na Taifa kwa ujumla,” amesema.
 
TAWA YAKABIDHI VIFAA VYENYE THAMANI YA SHILINGI MILIONI 362 KWA WILAYA ZA SERENGETI NA BUNDA

TAWA YAKABIDHI VIFAA VYENYE THAMANI YA SHILINGI MILIONI 362 KWA WILAYA ZA SERENGETI NA BUNDA

February 28, 2026 Add Comment

Na. Joyce Ndunguru, Mara.

Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA) kwa kushirikiana na Kampuni ya Grumeti Reserve Ltd imekabidhi vifaa mbalimbali yakiwemo Madawati 3,015, Kompyuta 21, Vitanda vya hospital 24, UPS 8 pamoja na Printa 2 vyenye thamani ya takribani shilingi za kitanzania Milioni 362 kwa Wilaya za Serengeti na Bunda zilizopo Mkoani Mara.

Akizungumza katika hafla ya makabidhiano yaliyofanyika Februari 27,2026, Mwakilishi wa Kamishna wa Uhifadhi ambaye pia ni Kamishna Msaidizi Mwandamizi, Kitengo cha Jamii, Utafiti na Ujirani Mwema, Omary Msangi alisema vifaa hivyo vilivyokabidhiwa ni utekelezaji wa Mkataba wa Uwekezaji Mahiri (SWICA) baina ya TAWA na Kampuni ya Grumeti Reserve Ltd kwa ajili ya shughuli za Uhifadhi katika Hifadhi za Ikorongo na Grumet.

Aidha , Kamishna Msangi aliongeza kuwa miongoni mwa matakwa ya Mkataba huo ni kuongeza mapato na kuhakikisha jamii zinazoishi pembezoni mwa hifadhi hizo zinanufaika na uwepo wa rasilimali Wanyamapori katika maeneo yao.

Sambamba na hilo, Kamishna Msangi, alitoa rai kwa wananchi kuendelea kuunga mkono shughuli za uhifadhi na utalii zinazofanyika sehemu mbalimbali ili kuhakikisha kuwa manufaa yaliyoonekana leo yanaendelea kupatikana.

Naye, Kamanda wa Uhifadhi anayesimamia Kanda ya Ziwa, Mark Chuwa alisema TAWA imekuwa ikishirikiana na wadau mbalimbali katika ulinzi wa maeneo ya hifadhi, Aidha, mashirikiano hayo pia yanajikita katika kuhakikisha wananchi wananufaika na rasimali za Taifa.

Kamanda Chuwa aliongeza kuwa vifaa hivi vilivyokabidhiwa vitaenda kupunguza changamoto za madawati zilizokuwepo katika mashule na kuboresha utendaji kazi katika Zahanati zinazopatikana katika Wilaya za Serengeti na Bunda.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Serengeti, Mhe. Angelina Lubela aliwashukuru TAWA pamoja na Kampuni ya Grumeti kwa kuwakabidhi vifaa hivi ambavyo vitaenda kupunguza changamoto katika Sekta ya Elimu na Afya katika Wilaya ya Serengeti.

Pia, Mhe. Lubela aliongeza kuwa madawati haya yataenda kuweka mazingira mazuri kwa wanafunzi na kuwahamasisha wanafunzi kuhudhuria masomo yao hivyo kuongeza ufaulu wa wanafunzi.

Naye, Mkuu wa Wilaya ya Bunda, Mhe. Aswege Kaminyonge aliipongeza Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuweka mazingira mazuri kwa wawekezaji ambazo faida za wawekezaji hao zinagusa jamii moja kwa moja.

Kadhalika, Mhe.Kaminyonge aliishukuru TAWA pamoja na Kampuni ya Grumeti kwa vifaa hivyo yakiwemo madawati kwani yataenda kupunguza upungufu wa madawati kwa wanafunzi takribani 4,600 wa Wilaya ya Bunda.

Kwa upande wake, Mwakilishi kutoka Kampuni ya Grumeti Reserve Ltd, Frida Mollel alisema , Grumeti wataendelea kuhakikisha jamii zinazoishi pembezoni mwa Hifadhi ya Ikorongo na Grumet wanafaidika na uwepo wao kama wawekezaji.

Aidha, alisema kuwa vifaa hivi vilivyotolewa kwa wananchi vikawe chachu katika kuendelea kuhamasisha wananchi kutunza maeneo ya hifadhi.

SERIKALI YAFANYA UKAGUZI WA KIZIMBA NA KITUO CHA ASKARI KUKABILIANA NA WANYAMAPORI WAKALI NA WAHARIBIFU

February 28, 2026 Add Comment

 Ruvuma

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Wizara ya Maliasili na Utalii imefanya ukaguzi wa kizimba cha mamba katika Kijiji cha Mtonya na  Kituo  cha askari katika Kijiji cha Nambecha, Wilaya ya Namtumbo, Mkoa wa Ruvuma ikiwa ni miongoni mwa mikakati inayotekelezwa na serikali katika kukabiliana na wanyamapori wakali na waharibifu. 

Ukaguzi huo umefanyika tarehe 27 Februari 2026, ambapo watumishi kutoka Wizara ya Maliasili na Utalii, hususan Idara ya Wanyamapori kwa kushirikiana na Halmashauri ya Wilaya husika walitembelea maeneo hayo kwa lengo la kuona maendeleo ya miundombinu hiyo.

Kwa upande wa wananchi ambao ni  wakazi wa maeneo husika walionesha furaha yao na kuipongeza serikali kwa juhudi za kuweka vizimba hivyo, ambavyo vimewasaidia kujikinga na madhara ya mamba pindi wanapotumia maji ya mto Mtonya kwa matumizi ya nyumbani. Aidha, wamekuwa wenye furaha, amani na kuona usalama wao kuimarishwa zaidi. Wananchi wameipongeza serikali kwa jitihada zinazofanyika.

USHAHIDI WA TUNDA LA MTI WA KATI KULIWA NGORONGORO HUU HAPA

February 28, 2026 Add Comment






Mwaka 1976, Mtafiti wa masuala ya Akiolojia Dr. Mary Leakey aligundua nyayo za zamadamu eneo la Laetoli zilizohifadhika katika mwamba wa jivu la volcano iliyolipuka kwenye milima ya Ngorongoro zaidi ya miaka milion 3.6 iliyopita. Wataalamu wanaamini kuwa nyayo hizo ziliachwa na jamii ya watu wa kale waitwao _Australopithecus Afarensis._

Nyayo za Zamadamu Laetoli Ngorongoro ni ushahidi usiopingika kuwa zamadamu (Hominin) wa umri wa miaka milioni 3.66 iliyopita walitembea wima kwa miguu miwili eneo la Laetoli Tanzania.

Kutembea wima kwa miguu miwili kunatutofautisha wanadamu na wanyama kama Sokwe na Nyani waliotokana na babu/bibi mmoja miaka takribani millioni 7 iliyopita.

Uwepo wa Nyayo na masalia ya binadamu, ndege na wanyama, urithi wa utamaduni, mambo kale, mimea, maji, matunda na kila kitu kinachomfanya binadamu kuishi ni kiashiria kuwa pengine bustani ya Eden ni Ngorongoro ni mahali ambapo tunda la mti wa katikati lililiwa.

KITETO WAAHIDIWA KUPATIWA MWENYEKITI WA BARAZA LA ARDHI NA NYUMBA LA WILAYA

February 28, 2026 Add Comment
 

Na Munir Shemweta, KITETO

Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Dkt Leonard Akwilapo ameahidi kupelewa kwa Mwenyekiti wa Baraza la Ardhi na Nyumba la wilaya ya Kiteto mkoani Manyara.

Dkt Akwilapo alitoa ahadi hiyo leo tarehe 26 Februari 2026 kufuatia kuwasilishwa kwa malalamiko na mwananchi mmoja aliyemueleza Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt Mwigulu Nchemba aliyeko katika ziara mkoani Manyara kuwa, katika wilaya ya kiteto wananchi wamekuwa wakipata shida ya kushughulikiwa mashauri yao ya ardhi kupitia Baraza la Ardhi kutokana na kukosekana kwa mwenyekiti wa Baraza.

Kwa sasa Baraza la Ardhi na Nyumba la Wilaya ya Kiteto linahudumiwa na Mwenyekiti wa Baraza la Ardhi na Nyumba kutoka Dodoma jambo lililoelezwa kuwa limechangia mashauri kuchukua muda mrefu.

Dkt Akwilapo amesema, suala la Mwenyekiti wa Baraza la Ardhi na Nyumba Wilaya katika wilaya ya Kiteto tayari limeshamfikia na analifanyia kazi na muda wowote mwenyeikiti atapatikana ndani ya muda mfupi.

‘’Nimemuagiza katibu mkuu aliyefanyie kazi na muda wowote tutapata mwenyekiti mahsusi kwa ajili ya eneo hili’’. Amesema Dkt Akwilapo

Akigeukia suala la migogoro ya ardhi katika wilaya ya Kiteto, Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi amesema, migogoro mingi katika wilaya ya Kiteto imesababishwa na ukosefu wa mipango ya matumizi ya ardhi.

Kwa mujibu wa Dkt Akwilapo, wilaya ya Kiteto ina jumla ya vijiji 63 na kati ya hivyo vijiji 33 ndivyo vilivyofanyiwa mpango wa matumizi ya ardhi huku vijiji 22 mpango wake ukiwa umeisha muda wake jambo alilolieleza kuwa, sasa jumla ya vijiji 52 vinahitaji kufanyiwa mpango wa matumizi ya ardhi.

Amesema, Wizara yake inalifanyia kazi suala hilo na katika mpango wa Bajeti ijayo ya 2026/2026 wameomba fedha na itakapofanikiwa Wizara yake itatekeleza mpango huo kwa kushirikiana na Jumuiya ya Hifadhi ya Wanyamapori (WMA). Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Dkt Leonard Akwilapo akizungumza katika mkutano wa hadhara wakati wa ziara ya Waziri Mkuu Mhe. Dkt Mwigulu Nchemba wilayani Kiteto mkoani Manyara tarehe 26 Februari 2026. Waziri Mkuu Mhe. Dkt Mwigulu Nchemba akiwa pamoja na viongozi wengine wakati wa ziara yake mkoani Manyara tarehe 26 Februari 2026. Wa pili kulia ni Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Dkt Leonard Akwilapo. Sehemu ya wananchi waliohudhuria mkutano wa hadhara katika ziara ya Waziri Mkuu Wilayani Kiteto mkoani Manyara tarehe 26 Februari 2026. Waziri Mkuu Mhe. Dkt Mwigulu Nchemba akisalimiana na viongozi mbalimbali wakiwemo Mawaziri alipowasili wilayani Kiteto wakati wa ziara yake mkoani Manyara tarehe 26 Februari 2026. (PICHA ZOTE NA WIZARA YA ARDHI)

TANZANIA YAPEWA PONGEZI UUNDWAJI WA TUME YA UCHUNGUZI

February 28, 2026 Add Comment


Pongezi hizo zimetolewa katika taarifa ya Kamishna Mkuu wa Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa Volker Turk wakati wakutoa taarifa inayoangazia maeneo yaliyokumbwa na changamoto ya vita na migogoro duniani katika kikao cha 61 cha Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa kilichofanyika Geneva, Uswisi.

Akizungumza katika kikao hicho,
Kamishna Turk alisema hatua iliyochukuliwa na Tanzania kuanzisha Tume ya kuchunguza kilichojiri Oktoba 29, kama hatua muhimu inayojali haki za binadamu


Tume ya kuchunguza matukio ya uvunjifu wa amani yaliyotokea Oktoba, 2025 ilianza rasmi majukumu yake Desemba 2025, kwa mujibu wa Sheria ya Tume za Uchunguzi, Sura ya 32.

MTENDAJI MKUU ADEM AMKABIDHI CHA USHIRIKI WA MAFUNZO MWENYEKITI WA TAHOSSA

February 27, 2026 Add Comment

Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Maendeleo ya Uongozi wa Elimu (ADEM), Dkt. Maulid J. Maulid, akimkabidhi cheti cha ushiriki wa Mafunzo ya Usimamizi wa Kimkakati wa Elimu Mwalimu Dennis John Otieno, ambaye ni Mwenyekiti wa Umoja wa Wakuu wa Shule za Sekondari Tanzania (TAHOSSA) na pia Mkuu wa Shule ya Sekondari Ilboru mkoani Arusha.

HAKUNA MGONJWA WA UVIKO- 19, MAFUA MAKALI NA KIPINDUPINDU TANZANIA- MHE. MCHENGERWA

February 27, 2026 Add Comment

Na Mwandishi wetu– WAF, Dar es Salaam.

Wizara ya Afya imewataka wananchi kuendela kuchukua tahadhari na kufuatilia ushauri wa kitaalam ili kujikinga dhidi ya magonjwa mbalimbali kama ilivyoelezwa katika taarifa kwa umma ya Mganga Mkuu wa Serikali hivi karibuni.

SERIKALI YADHAMIRIA KUMALIZA CHANGAMOTO YA USAFIRI DAR ES SALAAM

February 27, 2026 Add Comment




NA. MWANDISHI WETU – Dar es Salaam


KATIBU Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu, Dkt. Jim Yonazi ambaye pia ni mwenyekiti wa Kamati ya Usimamizi wa Mradi wa DART amesema Serikali imejipanga kikamilifu kuhakikisha inamaliza changamoto ya usafiri katika Jiji la Dar es Salaam, ili wananchi waweze kupata huduma bora, ya haraka na yenye uhakika.

Akizungumza hii leo 27 Februari, 2026 mara baada ya Kamati hiyo kufanya ziara ya kukagua miundombinu ya usafirishaji jijini humo, Dkt. Yonazi amesema Serikali imewekeza kwa kiwango kikubwa katika kuboresha sekta ya usafiri wa umma.

Alisema katika ziara hiyo, kamati ilitembelea Wakala wa Mabasi Yaendayo Haraka Dar es Salaam (DART) pamoja na Kampuni ya Uendeshaji wa Mabasi Yaendayo Haraka (UDART) na kujionea maendeleo ya uwekezaji uliofanywa.

“Ni dhamira ya Serikali kuhakikisha usafiri wa Dar es Salaam unakuwa bora, wa kisasa na unaokidhi mahitaji ya wananchi. Tumejionea miundombinu iliyowekwa na jitihada zinazoendelea kuboresha huduma,” alisema.

Dkt. Yonazi alibainisha kuwa tayari kampuni zimeanza kuleta mabasi mapya, hatua itakayoliwezesha jiji hilo kuwa miongoni mwa majiji yenye usafiri wa kisasa barani Afrika. Aliongeza kuwa mabasi mengi yatatumia gesi asilia, huku Serikali ikiwa imejenga miundombinu ya vituo vya gesi ili kuhakikisha huduma hiyo inapatikana kwa urahisi.

Aidha, alisema Serikali imewekeza katika mifumo ya TEHAMA itakayomwezesha mwananchi kutumia kadi maalumu kulipia nauli bila kulazimika kupanga foleni, jambo litakaloongeza ufanisi na kupunguza usumbufu.

Katika hatua nyingine, aliwahakikishia wananchi kuwa mabasi yote yaliyoharibika yatafanyiwa ukarabati na kurejea barabarani ili kuimarisha upatikanaji wa huduma.

Kwa upande wake, Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Mabasi Yaendayo Haraka Bw. Said Tunda alisema lengo kuu ni kurejesha furaha kwa wananchi wa Dar es Salaam kwa kuwapatia usafiri wa uhakika.

Pia aliwataka waendesha daladala kuendelea kutoa huduma huku Serikali ikiendelea kufanya mazungumzo nao ili kupata utaratibu bora wa ushirikiano, hususan kwa zile zilizopewa kibali cha kutumia barabara ya mwendokasi.

Hatua hizo zinaonesha dhamira ya dhati ya Serikali ya Awamu ya Sita ya inayoongozwa na Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kuboresha maisha ya wananchi kupitia miundombinu imara na huduma bora za kijamii.


=MWISHO=