HABARI MPYA
HABARI
SIASA
ELIMU
Recent Posts
Dk . Komba: tafiti zitoe majibu ya changamoto za wananchi
habariNAIBU SPIKA SILLO: MICHANGO YA WADAU MUHIMU KUIMARISHA UPANDIKIZAJI FIGO NA ULOTO KWA WATOTO WENYE SICKLE CELL.
afyaNAIBU Spika wa Bunge, Daniel Sillo, ametoa wito kwa wananchi na wadau mbalimbali kushiriki katika kuchangia huduma za matibabu ya upandikizaji Uloto kwa Watoto wenye ugonjwa wa Sicle Cell na upandikizaji figo kwa wenye uhitaji hapa nchini.
Ameyasema hayo wakati wa hafla ya chakula cha jioni tarehe 19 Mei, 2026 katika ukumbi wa Domiya jijini Dodoma, ambapo hafla hiyo imewakutanisha viongozi waandamizi wa mkoa wa Dodoma, wabunge na wadau mbalimbali kwa lengo la kujadili namna ya kuimarisha mfuko wa kusaidia matibabu ya upandikizaji uloto na figo pamoja na huduma nyingine za kibingwa.
Amesema licha ya mafanikio yaliyopatikana ya huduma hizo za upandikizaji uloto na figo kutolewa hapa nchini na hivyo kuokoa fedha nyingi ambazo zingeweza kutumika endapo wananchi wangeenda kutibiwa nje ya nchi.
Alisema kila mwananchi anapaswa kutambua kuwa kuchangia huduma hizo si jukumu la serikali na taasisi pekee, bali ni wajibu wa pamoja kwa kuwa magonjwa ya figo na sickle cell hayachagui mtu kwa nafasi yake, dini wala hali ya maisha.
“Tunaposhiriki katika michango hii si kwa ajili ya taasisi moja, bali tunaunga mkono huduma za kitaifa zinazogusa maisha ya wananchi wengi wanaohitaji matibabu hayo,” alisema Mhe. Sillo.
Alitoa wito kwa wananchi, taasisi na wadau mbalimbali kuendelea kuunga mkono juhudi hizo za BMH ili kuwezesha wagonjwa wanaohitaji huduma za upandikizaji viungo na matibabu mengine maalumu kupata huduma kwa wakati.
Ameeleza kutegemea bajeti ya serikali pekee hakuwezi kukidhi mahitaji yote yanayoongezeka ya huduma za kibingwa, hivyo ushirikishwaji wa wadau ni njia muhimu ya kuimarisha sekta ya afya na kuokoa maisha ya Watanzania wengi.
QWARAY AVUTIWA NA UBUNIFU WA TEHAMA RIDC
habariKatika ziara hiyo iliyofanyika mapema wiki hii, Mhe. Qwaray alipata fursa ya kutembelea na kujionea miradi ya kiteknolojia inayolenga kutoa suluhisho kwa changamoto katika sekta mbalimbali ikiwemo elimu, afya na utawala.
Aidha, miradi hiyo inahusisha matumizi ya teknolojia zinazochipukia kama vile Internet of Things (IoT) na Akili Mnemba (AI), katika kurahisisha utendaji kazi Serikalini na kuongeza ufanisi wa huduma kwa wananchi.
Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Mhe. Qwaray ameipongeza Mamlaka ya Serikali Mtandao (e-GA) kwa juhudi zake za kuibua na kuendeleza vipaji vya vijana, kupitia tafiti na ubunifu wa mifumo mbalimbali ya TEHAMA yenye mchango mkubwa katika maendeleo ya taifa.
“Niwapongeze e-GA kwa kazi kubwa mnayoifanya ya kukuza ubunifu na tafiti za teknolojia. Dunia ya sasa inabadilika kwa kasi kubwa kutokana na maendeleo ya teknolojia, hivyo ni muhimu kuendelea kujifunza, kufanya tafiti na kubuni mifumo mipya itakayokwenda sambamba na mabadiliko hayo,” amesema Mhe. Qwaray.
Amesisitiza kuwa, bunifu zote zinazotengenezwa zinapaswa kuwa na tija kwa jamii na kuchangia moja kwa moja katika kuboresha huduma zinazotolewa kwa wananchi pamoja na kuongeza ufanisi ndani ya taasisi za Serikali.
Sambamba na hilo, Mhe. Qwaray amesisitiza umuhimu wa kuimarisha ushirikiano kati ya e-GA, vyuo vikuu na sekta binafsi ili kuongeza uwekezaji katika tafiti, ubunifu na maendeleo ya teknolojia zinazoweza kusaidia kutatua changamoto mbalimbali za kijamii na kiuchumi.
Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa e-GA, Mhandisi Benedict Ndomba, amesema kituo hicho kimeendelea kuwa chachu ya mageuzi ya kidijitali Serikalini kupitia ujenzi wa mifumo mbalimbali inayotumika katika taasisi za umma.
Ametaja baadhi ya mifumo hiyo kuwa ni Mfumo wa Uendeshaji wa Vikao vya Bodi na Menejimenti (e-Board) pamoja na Mfumo wa Uendeshaji wa Vikao Kidijitali (e-Mikutano), ambayo imekuwa ikisaidia kuongeza ufanisi katika shughuli za Serikali.
“Kituo hiki kimekuwa na manufaa makubwa kwa taifa kutokana na kazi zake za utafiti, ubunifu na maendeleo ya mifumo ya TEHAMA. Pia, kimefungua fursa kwa wanafunzi na vijana wenye taaluma ya TEHAMA kushiriki katika tafiti na bunifu mbalimbali kwa maslahi ya taifa,” amesema Mha.Ndomba.
Katika kuonesha dhamira ya Serikali kuendelea kuimarisha kituo hicho, Mhe. Qwaray ameahidi kuwa Wizara itaendelea kushirikiana na e-GA kutatua changamoto zinazoikabili RIDC ili kuongeza fursa kwa vijana wengi zaidi wa Kitanzania kupata nafasi ya kujifunza, kufanya tafiti na kushiriki katika ubunifu wa teknolojia mbalimbali za kisasa.








CRDB Yaongeza Ushirikiano na Majeshi Kupitia Mkutano wa Kimataifa
BALOZI MATINYI AWASILI ALGERIA
habari
TANZANIA NA RWANDA ZASAINI MAKUBALIANO YA USHIRIKIANO WA NISHATI MBELE YA RAIS SAMIA NA KAGAME
Zoezi hilo la utiaji saini limefanywa na Waziri wa Nishati wa Tanzania, Mhe. Deogratius Ndejembi na Waziri wa Miundombinu wa Rwanda, Mhe. Dkt. Jimmy Gasore kwenye ukumbi wa mikutano wa Kigali Convention Center (KCC) unapofanyika Mkutano wa Pili wa Uvumbuzi wa Nishati ya Nyuklia barani Afrika (NEISA 2026) unaofanyika jijini Kigali, Rwanda.
Makubaliano hayo yanaangazia maeneo kadhaa ya ushirikiano ikiwemo kubadilishana umeme kati ya Tanzania na Rwanda ili kuimarisha usalama wa nishati, utekelezaji wa miradi ya pamoja ya miundombinu ya umeme, pamoja na kuendeleza biashara ya umeme baina ya nchi hizo mbili.
Aidha maeneo mengine ya ushirikiano ni pamoja na utafutaji na uendelezaji wa mafuta na gesi asilia, usambazaji wa bidhaa za petroli, fursa zilizopo katika miradi ya LNG pamoja na matumizi ya teknolojia za kisasa ikiwemo akili bandia katika Sekta ya Nishati.
Miongoni mwa viongozi waliohudhuria hafla hiyo ni Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Mahmoud Thabit Kombo, Waziri wa Fedha, Mhe Balozi Khamis Omar, Naibu Waziri wa Maji, Nishati na Madini wa Zanzibar, Mhe. Dkt. Seif Pandu, Katibu Mkuu Wizara ya Nishati anayeshughulikia Umeme na Nishati Jadidifu, Mha. Felchesmi Mramba pamoja na wataalamu kutoka serikali zote mbili.
TET KUSHIRIKIANA NA DUCE KUIMARISHA ELIMU KUPITIA TAFITI
habariARBAB VILLAGE IN TANGA KUFANYIWA MABORESHO MAKUBWA, CEO AMTAJA BAKHRESA
habari
Na Oscar Asenga Tanga
Ikiwa ni zaidi ya miezi sita tangu kuzinduliwa rasmi kwa Arbab Village mjini Tanga mnamo Desemba 6, 2025, eneo hilo sasa limeendelea kuwa gumzo kubwa kwa wakazi wa Tanga na wageni kutoka maeneo mbalimbali kutokana na muonekano wake wa kisasa, ubunifu wake wa kipekee na namna lilivyobadilisha kabisa taswira ya eneo hilo.
Mkurugenzi wa Arbab Village, Mbwana Imamu, amesema mafanikio makubwa yaliyopatikana ndani ya muda mfupi ndiyo sababu kubwa iliyowasukuma kuanza mpango wa maboresho makubwa zaidi ili kufanya eneo hilo liendelee kuwa kivutio kikubwa zaidi ndani ya Tanga na nje ya Tanzania 🇹🇿
Kwa sauti yenye kujiamini, Arbab amesema jambo lililompa nguvu zaidi ni namna wananchi wa Tanga walivyoikubali Arbab Village kwa haraka, tofauti na matarajio ya watu wengi waliokuwa hawaamini kama eneo hilo lingeweza kubadilika na kuwa sehemu ya kisasa yenye mvuto mkubwa wa biashara na burudani.
“Watu wengi hawakuwahi kufikiria kama hapa panaweza kuwa sehemu kama hii. Wapo waliowahi kujaribu kufanya uwekezaji lakini walishindwa. Mimi nilikuja na maono tofauti… niliamua kutumia ubunifu mkubwa na kufanya kitu ambacho watu watakikumbuka,” amesema Arbab.
Ameeleza kuwa hakutaka kufanya biashara ya kawaida kama zilivyo sehemu nyingine, bali alitaka kuleta utofauti ambao ungeifanya Arbab Village kuwa na hadhi yake ya kipekee ndani ya jiji la Tanga.
“Biashara kama hizi zipo sehemu nyingi, lakini nilikaa nikafikiria… nifanye nini ambacho kitawafanya watu wajisikie tofauti wakifika hapa? Ndiyo maana nikaja na ubunifu mkubwa ambao leo watu wameukubali na wengine kuvutiwa sana na kuiga”, amesema.
Kutokana na mwitikio mkubwa wa wateja kila siku, Arbab amesema tayari wameanza mipango ya kufanya maboresho makubwa zaidi yatakayoongeza hadhi na ubora wa huduma zinazotolewa katika eneo hilo.
Amesema maboresho hayo hayajasukumwa na malalamiko ya wateja, bali ni sehemu ya maono yangu ya kuhakikisha kila anayefika Arbab Village anapata uzoefu bora na mpya zaidi.
“Sisi hatusubiri kuambiwa na wateja ndipo tubadilike. Tunataka kila siku tuwe bora zaidi kuliko jana,” amesema kwa msisitizo.
Katika mazungumzo yake, Arbab pia alitoa somo kwa vijana wanaotamani kuingia kwenye biashara, akisisitiza kuwa mafanikio hayapatikani kwa mihemko wala kushindana na watu, bali kwa kusikiliza mahitaji ya wateja na kuwa mbunifu.
“Ukitaka kuwa mfanyabiashara mzuri usipoteze muda kushindana na mfanyabiashara mwingine. Angalia wateja wako wanahitaji nini… hakikisha unawapa,” amesema.
Ameongeza kuwa vijana wengi wanaharibu safari zao za biashara kwa kuendeshwa na presha za mitandaoni na kutaka mafanikio ya haraka badala ya kujenga biashara kwa utulivu, ubunifu na uvumilivu, Arbab Village sio night club kwa maana tunapiga disco hapana, Arbab Village ni sehem tulivu yenye music wa wastan sio makelele huku ukipata chakula na vinywaji.
Akizungumzia watu waliompa hamasa katika safari yake ya biashara, Arbab hakusita kumtaja mfanyabiashara maarufu wa Tanzania Said Salim Bakhresa kuwa mmoja wa watu waliomvutia kupitia maneno yake ya motisha.
“Niliwahi kumsikia Bakhresa akisema mfanyabiashara lazima ujaribu kila kitu na usikate tamaa. Pia lazima ujitume mwenyewe na upambane binafsi. Yale maneno yalinijenga sana,” amesema.
Arbab amesema leo hii wengi wanashangazwa na namna anavyofanikiwa kufanya mambo makubwa akiwa hana makundi ya vijana wenye mihemko au makelele, bali anaamini katika kazi, nidhamu, ubunifu na kujenga heshima ya biashara yake kupitia matokeo.
Kwa sasa, Arbab Village imeendelea kuwa moja ya sehemu zinazovuta watu wengi zaidi jijini Tanga, huku wengi wakisubiri kwa hamu kuona maboresho mapya yatakayofanyika katika eneo hilo ambalo tayari limeanza kubadilisha sura ya burudani na biashara ndani ya mkoa huo.
TUME YA MADINI YAPATA HATI SAFI YA UKAGUZI, YAKUSANYA MADUHULI TSH. TRILIONI 1.192
habariARUSHA
Tume ya Madini imeendelea kuonesha mafanikio makubwa katika usimamizi wa rasilimali za umma baada ya kupata hati safi ya ukaguzi kwa Hesabu za Mwaka wa Fedha 2024/2025 sambamba na kukusanya maduhuli yaliyofikia Shilingi Trilioni 1.192, sawa na asilimia 99 ya lengo la mwaka.
Akizungumza Mei 19, 2026 mkoani Arusha wakati wa kikao kazi cha wahasibu na wachumi wa Tume, Mkurugenzi wa Fedha na Mipango wa Tume ya Madini, CPA. Idfonce Masoud, amesema hati safi hiyo imetokana na ukaguzi uliokamilika na kuwasilishwa kwa Mheshimiwa Rais na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) mwezi Machi 2026.
CPA. Masoud amesema mafanikio hayo yanatokana na juhudi, nidhamu ya kazi na weledi wa timu ya wahasibu na wachumi waliotekeleza majukumu yao kwa kuzingatia Kanuni za Kimataifa za Uandaaji wa Hesabu za Sekta ya Umma (IPSAS), hatua iliyosaidia kupunguza hoja za ukaguzi na kuimarisha uwazi wa kifedha.
Amezipongeza pia Ofisi za Maafisa Madini Wakazi wa Mikoa kwa mchango wao mkubwa katika ukusanyaji wa maduhuli pamoja na usimamizi madhubuti wa Katibu Mtendaji wa Tume, uliowezesha kufikiwa kwa kiwango kikubwa cha mapato ya Serikali.
“Natumia fursa hii kuwashukuru na kuwapongeza sana kwa juhudi mlizozifanya katika kusimamia ukusanyaji wa maduhuli hadi kufikia kiasi kilichokusanywa kufikia tarehe 15 Mei 2026,” amesema CPA. Masoud.
Aidha, amewataka washiriki wa kikao kazi hicho kutumia ipasavyo mafunzo na mada zitakazowasilishwa ili kuendelea kuimarisha utendaji kazi na kuongeza ufanisi wa Taasisi.
Kwa upande wake, Afisa Madini Mkazi wa Mkoa wa Arusha, Godson Kamihanda, amesema kikao kazi hicho ni jukwaa muhimu la kubadilishana uzoefu, kujadili changamoto za kiutendaji na kuweka mikakati madhubuti ya kuboresha utoaji huduma.
Amesema majadiliano yatakayofanyika yanatarajiwa kuzaa matokeo chanya yatakayochangia maendeleo ya Tume ya Madini na Taifa kwa ujumla.
Kikao kazi hicho kinajumuisha mafunzo katika maeneo mbalimbali ikiwemo matumizi ya Mfumo mpya wa Kodi (IDRAS), uandaaji na utunzaji wa taarifa za madeni ya maduhuli, uandaaji wa hesabu, usimamizi wa bajeti na matumizi ya fedha pamoja na maadili na uwajibikaji mahali pa kazi.

.jpeg)




























.jpeg)

.jpeg)


.jpeg)

.jpeg)


