HABARI ZETU
Loading...

HABARI

SIASA

ELIMU

Recent Posts

SERIKALI KUENDELEA KUBORESHA VITUO VYA MAARIFA NCHINI.

May 19, 2026 Add Comment

 

Na, Mwandishi wetu - Pwani


SERIKALI kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu) imeeleza dhamira yake ya kuendelea kuboresha Vituo vya Maarifa nchini, hususan vile vinavyotoa huduma kwa madereva wa malori ya masafa marefu kuhusu masuala ya VVU na UKIMWI.

Kauli hiyo imetolewa na Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo, Dkt. Jim Yonazi mapema mwanzoni mwa wiki mara baada ya kutembelea na kukagua Vituo vya Maarifa vinavyotoa huduma za VVU na UKIMWI kwa madereva wa malori ya masafa marefu vilivyopo eneo la Kurasini  katika wilaya ya Temeke Jijini Dar es Salaam na Mdaula mkoa wa Pwani ambayo Vituo hivyo vipo chini ya Tume ya Kudhibiti UKIMWI Tanzania (TACAIDS).

Dkt. Yonazi amesema Serikali, kupitia Tume ya Kudhibiti UKIMWI Tanzania (TACAIDS), ina jukumu la kusogeza huduma muhimu za VVU na UKIMWI karibu na wananchi.

“Vituo hivi vina mchango mkubwa katika kuwafikia madereva wa masafa marefu ambao mara nyingi hukaa safarini kwa muda mrefu. Serikali itaendelea kuviboresha hususan kwenye miundombinu ya kutolea huduma na kuongeza wataalam wa afya ili viweze kutoa huduma bora Kwa madereva hao wa masafa marefu kwa kujua afya zao dhidi ya maambukizi ya virusi vya UKIMWI,” amesema Dkt. Yonazi.

Kwa upande wao, madereva wa malori ya masafa marefu wanaonufaika na huduma hizo wameeleza kuwa Vituo vya Maarifa ni msaada mkubwa kwao, kwani vinawapa fursa ya kupata elimu na huduma za VVU na UKIMWI kwa urahisi na bila gharama na kuipongeza Serikali kwa namna inavyoendelea kujali na kuwafikia wananchi wake.

=MWISHO=

 JENERALI MKUNDA AKIWASILI BUNGENI KUSHUHUDIA UWASILISHAJI BAJETI YA WIZARA YA ULINZI

JENERALI MKUNDA AKIWASILI BUNGENI KUSHUHUDIA UWASILISHAJI BAJETI YA WIZARA YA ULINZI

May 19, 2026 Add Comment




Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Jacob Mkunda, akiwasili Bungeni jijini Dodoma leo Jumanne Mei 19, 2026, kwa ajili ya kushuhudia uwasilishaji wa bajeti ya Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa kwa mwaka wa fedha 2026/2027

Pichani Jenerali Mkunda akisalimiana na viongozi mbalimbali wa Wizara hiyo wakiongozwa na Waziri Mhe. Dkt. Rhimo Nyansaho

ULINZI WA BOMBA LA GESI WAPEWA KIPAUMBELE MKOA WA PWANI

May 19, 2026 Add Comment
Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) linaendelea kuimarisha ushirikiano na jamii kwa kutoa elimu kwa wananchi kuhusu umuhimu wa kulinda na kuhakikisha usalama wa miundombinu ya bomba la gesi asilia katika vijiji vya Mkwalia Kitumbo na Sunguvuni, wilayani Mkuranga mkoani Pwani.

MAFUNZO YA MAWAKILI YALENGA KUIMARISHA WELEDI NA USULUHISHI

May 19, 2026 Add Comment
WAZIRI wa Katiba na Sheria, Dk Juma Homera amesema watu wanaoitukana Serikali, kufanya uchochezi na vitendo visivyo vya maadili mitandaoni, majina yao yameshakabidhiwa kwa Wizara ya Mambo ya Ndani ili Jeshi la Polisi ili wachukuliwe hatua za kisheria.

MAGEREZA MOROGORO YANUFAIKA NA MAPINDUZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA

May 19, 2026 Add Comment


-Magereza 12 Morogoro Yanufaika na Mradi wa Nishati Safi ya Kupikia kutoka REA


Jeshi la Magereza Mkoa wa Morogoro limeendelea kuhamasishwa matumizi ya nishati safi ya kupikia ikiwa ni sehemu ya Mkakati wa Serikali kuhakikisha Asilimia 80 ya wanatumia wahamie kutumia nishati safi ya kupikia ifikapo mwaka 2034.

Akizungumza wakati wa ziara ya kukagua miradi ya nishati safi ya kupikia kwa Jeshi la Magereza mkoani Morogoro, Mwenyekiti wa Bodi ya Nishati Vijijini (REB), Mhe. Balozi Meja Jenerali (Mstaafu), Jacob Kingu amesema kuwa lengo la taifa la kufikia matumizi makubwa ya nishati safi ya kupikia linawezekana kutokana na uwepo wa vyanzo mbalimbali vya nishati hiyo.

Amesema wananchi wana nafasi ya kuchagua aina ya nishati safi kulingana na mazingira wanayoishi, ikiwemo gesi, mkaa mbadala pamoja na matumizi ya umeme kwa ajili ya kupikia.

“Inawezekana ifikapo mwaka 2034 asilimia 80 ya watanzania wanatumia nishati safi za kupikia maana zipo nyingi" amesema Mwenyekiti Kingu.

Aidha, ameeleza kuwa Wakala wa Nishati Vijijini (REA) unaendelea kupeleka huduma ya umeme katika Vijiji na Vitongoji jambo litakalowezesha wananchi wengi zaidi kutumia umeme kama chanzo cha nishati safi ya kupikia.

Kwa upande wake, Mkuu wa Magereza Mkoa wa Morogoro, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza (SACP), Peter Anatory amesema mradi wa majiko ya nishati safi ya kupikia unaotekelezwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umewezesha magereza 12 ya Mkoa wa Morogoro kunufaika na huduma hiyo.

Amesema kupitia mradi huo, magereza hayo yamepata majiko 15 yanayotumia mkaa rafiki kwa mazingira pamoja na tani 236 za mkaa huo, hali iliyosaidia kuongeza matumizi ya nishati safi katika taasisi za magereza.

“Mradi huu umekuwa kichocheo kikubwa kwa magereza katika kuhakikisha tunatumia nishati safi ya kupikia,” amesema Anatory.

Naye Kamishna Msaidizi wa Magereza (ACP) Samuel Aron Mwakatika amesema matumizi ya nishati safi yana mchango mkubwa katika kuboresha maisha ya wananchi, kulinda mazingira pamoja na kukuza uchumi wa taifa.

Amesema katika Chuo cha Udereva KPF Kingolwira, matumizi ya nishati safi yamesaidia kuokoa muda uliokuwa unapotea kwa wanafunzi kwenda kutafuta kuni.

“Katika chuo hiki tuna wanafunzi 381, hivyo zamani ilikuwa lazima kuwe na kundi la wanafunzi wanaokwenda kutafuta kuni jambo lililokuwa linapunguza muda wa kujifunza. Nishati safi imesaidia kuondoa changamoto hiyo,” amesema Mwakatika.

Aidha, Mrakibu Mwandamizi wa Magereza (SSP), Nicostatus Magori amesema gereza hilo liliacha kutumia kuni kwa ajili ya kupikia chakula cha wafungwa tangu Desemba mwaka 2024 baada ya kuanza kutekelezwa kwa mradi huo wa kufungiwa mifumo ya nishati safi ya kupikia katika magereza.






















TANESCO YAANZA UTEKELEZAJI WA MAELEKEZO YA WAZIRI NDEJEMBI, TRANSFOMA KUBWA YAWASILI NGARA

May 19, 2026 Add Comment




 ðŸ“Œ Siku 10’baada ya Mbunge Bahemu kuibua changamoto ya kukatika umeme Ngara.


Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) limeanza kutekeleza maelekezo ya Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi, kwa kuanza kazi ya kufunga transfoma mpya yenye uwezo mkubwa katika Wilaya ya Ngara mkoani Kagera ili kuboresha upatikanaji wa umeme wa uhakika.

Hatua hiyo inakuja ikiwa zimepita siku tisa tangu Waziri Ndejembi alipolielekeza shirika hilo kuhakikisha ndani ya mwezi mmoja linapeleka transfoma kubwa kufuatia malalamiko ya kukatika kwa umeme yaliyowasilishwa na Mbunge wa Jimbo la Ngara, Mhe. Dotto Bahemu.

Leo Mei 19, 2026, transfoma hiyo kubwa imewasili katika kituo cha kupozea umeme cha Djululigwa wilayani Ngara huku wataalamu wa TANESCO wakianza kazi ya kuifunga.

Meneja wa TANESCO Wilaya ya Ngara, Eng. Amani Chidundo amethibitisha kuwasili kwa transfoma yenye uwezo wa 5MVA na kueleza kuwa kazi ya kuifunga inatarajiwa kuchukua takribani saa 12 kukamilika.


Eng. Chidundo amesema changamoto ya kukatika kwa umeme wilayani humo ilikuwa ikitokana na transfoma ya awali yenye uwezo wa 3MVA kuzidiwa uwezo kutokana na ongezeko la mahitaji ya umeme.

Akishuhudia kazi ya ufungaji wa transfoma hiyo, Katibu wa Mbunge wa Jimbo la Ngara ameishukuru Serikali kupitia Wizara ya Nishati kwa kusikiliza na kufanyia kazi kwa haraka changamoto ya wananchi wa Ngara.

“Leo tunapokea transfoma kubwa inayoenda kuondoa changamoto ya WanaNgara. Tuombe wananchi mpokee na tutoe shukurani kwa Mheshimiwa Rais, Dkt. Samia Suluhua Hassa, Waziri pamoja na Mbunge kwa kuletewa mtambo mkubwa wa transfoma kuhakikisha zile changamoto tulizokuwa tukizipata, zinakwenda kupungua” amesema Mkubila.

RAIS DKT SAMIA SULUHU AONDOKA NCHINI KUELEKEA NCHINI RWANDA KUSHIRIKI MKUTANO WA WAKUU WA NCHI NA SERIKALI

May 19, 2026 Add Comment

 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiagana na viongozi mbalimbali kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) Jijini Dar es Salaam kabla ya kuondoka nchini, kuelekea Kigali, Rwanda kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali kuhusu Uvumbuzi wa Nishati ya Nyuklia barani Afrika (NEISA) tarehe 19 Mei, 2026.

Mkutano huo wa Kimataifa unawakutanisha pia wataalamu wa nishati, wawekezaji na mashirika ya kimataifa, ambapo utajadili matumizi ya nishati ya nyuklia kwa maendeleo ya Bara la Afrika. Mkutano huo pia unalengakujadili namna bora ya kuongeza upatikanaji wa nishati ya umeme Afrika, kupunguza uchafuzi wa mazingira, kusaidia maendeleo ya viwanda, kukuza ubunifu wa teknolojia za nishati ya nyuklia pamoja na kuvutia wawekezaji katika miradi ya nishati.

NAIBU WAZIRI NISHATI AITAKA TANESCO KUIMARISHA HUDUMA KWA WATEJA KUPITIA MIFUMO YA KIDIGITALI

May 19, 2026 Add Comment

📌 Afungua Mkutano Mkuu wa Mwaka 2026 wa Maafisa Uhusiano na Huduma kwa Wateja TANESCO


📌 Asisitiza utoaji wa taarifa sahihi kwa wateja 


📌 Aagiza kuboreshwa kwa maslahi ya watoa huduma kuongeza ufanisi wa utendaji kazi 


Na Agnes Njaala, Dodoma

Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba, amewataka Maafisa Uhusiano na Huduma kwa Wateja wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) kutumia kwa ufanisi mifumo ya kidigitali na akili mnemba ili kuendana na kasi ya ukuaji wa teknolojia na kuongeza ufanisi wa huduma na mawasiliano kwa wateja.

Mhe. Makamba amesema hayo Mei 18, 2026 wakati akifungua Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Maafisa hao unaofanyika kwa siku tano katika Ukumbi wa Lavenda Hotel jijini Dodoma ukilenga kutathmini utendaji kazi, kutambua changamoto, kujadili mikakati ya kuboresha huduma kwa wateja na kuimarisha mawasiliano ya kimkakati ndani ya Shirika kwa mwaka ujao wa fedha.

“ Sote tunatambua, teknolojia ndiyo msingi wa utoaji huduma wa kisasa hivyo ni wajibu wenu Maafisa Huduma kwa Wateja kuhakikisha mifumo ya kidigitali ikiwemo akili mnemba inatumika kwa ufanisi ili wananchi wapate huduma bora na taarifa sahihi kwa wakati.” amesisita , Mhe. Salome Makamba

Katika hotuba yake, amesema Serikali inatambua jitihada za dhati zinazofanywa na TANESCO katika maboresho yaliyofanyika katika huduma kwa wateja na  mawasiliano ya kimkakati kupitia matumizi ya mitandao ya kijamii, makundi ya WhatsApp pamoja na utoaji wa elimu kuhusu matumizi salama ya umeme na Nishati Safi ya kupikia.

Aidha, ameitaka Menejimenti ya TANESCO kuboresha motisha kwa watoa huduma kwa wateja ili kuongeza ari na ufanisi wao kazini kwa kuzingatia kuwa wao ni watendaji wa mstari wa mbele katika kujenga taswira ya Shirika kwa wateja .

“ Kwa niaba ya Uongozi wa Wizara, nawapongeza watoa huduma kwa kujituma kwenu. Nimuombe Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO kusimamia uboreshaji wa maslahi yao ili waweze kutoa huduma bora na yenye uhakika kwa wateja,” amesema Mhe. Makamba.

Akizungumza kuhusu maboresho ya huduma kwa wateja, amesisitiza umuhimu wa kuongeza ufanisi katika vituo vya huduma kwa wateja (Call Centers) ili kuhakikisha changamoto za wateja zinatatuliwa kwa wakati. 

“Nahimiza ushirikiano madhubuti kati ya TANESCO na wadau mbalimbali ili wateja waweze kupata taarifa sahihi kwa wakati. Aidha, kuna umuhimu mkubwa wa kuimarisha ushirikiano wa ndani kati ya Idara za TEHAMA na Huduma kwa Wateja kwa lengo la kufikia viwango bora zaidi vya utoaji huduma,” ameongeza .

Awali akizungumza kwa niaba ya Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa TANESCO, Dkt. Lucy-Mary Mboma, amesema Bodi inaendelea kuthamini mchango wa Maafisa Huduma kwa Wateja na inatarajia kuona Shirika likiendelea kuimarisha taswira yake kupitia huduma bora na mawasiliano yenye tija.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO, Bw. Lazaro Twange, amesema Shirika limewekeza katika mifumo rasmi itakayowezesha kuhudumia zaidi ya wateja milioni sita kwa ufanisi mkubwa mara itakapoanza kufanya kazi hivi karibuni. Amesema hatua hiyo pia itasaidia kuokoa takribani shilingi milioni 400 zilizokuwa zikitumika kwenye mifumo ya nje.

“ TANESCO itaendelea kuwekeza katika mifumo ya kisasa ya utoaji huduma ili kuongeza ufanisi, kuhudumia kwa uhakika zaidi ya wateja milioni sita na kupunguza gharama za uendeshaji wa mifumo ya nje.” amebainisha, Bw. Twange. 

Mkutano huu wa mwaka wa Maafisa Uhusiano na Huduma kwa Wateja ni muendelezo wa utamaduni wa taratibu za Shirika wenye tija katika kuboresha utendaji kazi kwa maslahi ya Shirika, wateja na nchi kwa ujumla.

DKT. MAGHEMBE AZINDUA KONGAMANO LA TIMUN 2026 ZANZIBAR

May 18, 2026 Add Comment
NAIBU Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Ngwaru Jumanne Maghembe amesisitiza umuhimu wa vijana katika kuleta maendeleo endelevu na mabadiliko chanya kupitia teknolojia, diplomasia na ubunifu katika ngazi ya taifa na kimataifa.

Kuelekea maadhimisho ya miaka 50 ya Shirika la Viwango TBS yawakaribisha wadau Viwango Marathon

May 18, 2026 Add Comment
NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

SHIRIKA la Viwango Tanzania (TBS) limeandaa mbio za marathon zijulikanazo kama ‘Viwango Marathon’ ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 50 tangu kuanzishwa kwa shirika hilo, huku likihamasisha matumizi ya bidhaa zilizothibitishwa na TBS pamoja na kuimarisha afya kwa jamii kupitia michezo.

RAIS SAMIA AUNDA TUME YA UCHUNGUZI WA KIJINAI VURUGU UCHAGUZI MKUU 2025 KUONGOZWA NA JAJI SHABANI LILA

May 18, 2026 Add Comment

 

Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameunda Tume ya Uchunguzi wa Kijinai wa Matukio ya Ghasia ya Wakati na Baada ya Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025. 

Hatua hiyo imechukuliwa katika kutekeleza mapendekezo ya Tume ya Rais ya Kuchunguza Matukio ya Uvunjifu wa Amani yaliyotokea katika kipindi hicho cha uchaguzi.  

Katika taarifa rasmi iliyotolewa leo tarehe 18 Mei, 2026 na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Dkt. Moses M. Kusiluka, Rais ameteua viongozi na wajumbe wa tume hiyo kwa kuzingatia mamlaka aliyonayo chini ya Sheria ya Tume za Uchunguzi, Sura ya 32.  

Katika uteuzi huo, Jaji wa Mahakama ya Rufani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Shabani Ally Lila, ameteuliwa kuwa Kamishna na Mwenyekiti wa Tume hiyo. 

Uzoefu wake katika mambo ya kisheria unatajwa kuwa nguzo muhimu katika kuongoza uchunguzi huo wa kijinai. 

 Aidha, Rais Samia ameteua majaji wastaafu watatu wa Mahakama Kuu ya Tanzania kuwa Makamishna wa tume hiyo ili kushirikiana na Mwenyekiti. Makamishna walioteuliwa ni Mhe. Gad John Mjemmas, Mhe. Awadh Mohamed Bawazir, pamoja na Mhe. Aishieli Nelson Sumari. Tume hii inatarajiwa kuanza kazi mara moja ili kuleta majibu na mapendekezo ya kisheria kuhusu ghasia hizo.

BARAZA LA MAWAZIRI LA EAC KUKUTANA KWA DHARURA JIJINI ARUSHA

May 18, 2026 Add Comment





Maandalizi ya Mkutano wa 60 wa Dharura wa Baraza la Mawaziri la Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), unaotarajiwa kufanyika tarehe 22 Mei 2026, yameanza rasmi kupitia vikao vya ngazi ya wataalamu vinavyoendelea kuanzia tarehe 18 hadi 20 Mei 2026 katika Makao Makuu ya Jumuiya hiyo jijini Arusha.

Kikao hicho cha wataalamu kimepokea na kujadilia taarifa ya Kamati ya Fedha na Utawala kuhusu masuala ya fedha ya Jumuiya, na rasimu ya bajeti ya Sekretarieti ya EAC pamoja na taasisi zake kwa mwaka wa fedha 2026/2027. Mapendekezo yatakayopitishwa katika ngazi hiyo yatawasilishwa kwa Makatibu Wakuu watakaokutana tarehe 21 Mei, 2026 kabla ya kuwasilishwa katika Mkutano wa Baraza la Mawaziri utakaofanyika tarehe 22 Mei, 2026.



Vilevile, mkutano huo wa siku tano kuanzia tarehe 18 hadi 22 Mei, 2026 unalenga kuweka mikakati ya pamoja ya utekelezaji wa maelekezo na maamuzi yaliyotolewa na Mkutano wa 25 wa Wakuu wa Nchi za EAC, hususan katika maeneo ya mipango na fedha

Baraza la Mawaziri la EAC ni chombo kikuu cha maamuzi na kusimamia shughuli za Jumuiya, katika hatua hii ya maandalizi ya bajeti, Baraza hilo lina jukumu la kupokea, kuchambua, kufanya marekebisho na kuidhinisha makadirio ya mapato na matumizi ya Sekretarieti ya EAC kabla ya kuwasilishwa katika Bunge la Afrika Mashariki (EALA) kwa ajili ya kujadiliwa na kupitishwa rasmi.



Ujumbe wa Tanzania katika mkutano huo unajumuisha wajumbe kutoka Wizara ya Fedha, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora pamoja na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, ukionaongozwa na Mkurugenzi wa Sera na Mipango kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Justin Kisoka.



WATATU ZAIDI WAPITISHWA NA TUME KUWANIA UDIWANI KATA YA BWONGERA -CHATO MKOANI GEITA

May 18, 2026 Add Comment

 

 

WAZIRI MCHENGERWA ANGOZA UJUMBE WA TZ WHA 79 GENEVA USWISI

WAZIRI MCHENGERWA ANGOZA UJUMBE WA TZ WHA 79 GENEVA USWISI

May 18, 2026 Add Comment






Na John Mapepele, Geneva, Uswisi

Waziri wa Afya Nchini, Mheshimiwa Mohamed Mchengerwa ameongoza ujumbe wa Serikali ya Tanzania katika ufunguzi rasmi wa Mkutano Mkuu wa 79 wa Shirika la Afya Duniani (WHA79) ulioanza leo Mei 18, 2026 mjini Geneva, Uswisi.

Mkutano huo mkubwa duniani katika sekta ya afya unashirikisha zaidi ya nchi 180 katika maeneo mbalimbali ulimwengu umefunguliwa na
Tedros Adhanom Ghebreyesus, Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Afya Duniani (WHO).

“Mkutano wa 79 wa Baraza la Afya Duniani (WHA79) unafanyika kuanzia tarehe 18 hadi 23 Mei 2026 mjini Geneva, Uswisi. Mkutano huu unawakutanisha wajumbe kutoka Nchi Wanachama wa WHO ili kushughulikia shinikizo kubwa linaloikabili mifumo ya afya na kuweka sera za afya za kimataifa, huku ukisisitiza sana huduma ya afya kwa wote, afya ya akili, na athari za mabadiliko ya tabianchi kwa afya.” Amefafanua Mheshimiwa Mchengerwa

Kwa mujibu wa Mheshimiwa Mchengerwa, maeneo makuu ya mjadala katika mkutano wa mwaka 2026 ni pamoja na:
Huduma ya Afya kwa Wote (UHC) na Ufadhili ambapo amesema Nchi wanachama na mashirika ya kiraia wanatoa kipaumbele kwa kuharakisha mifumo ya ufadhili wa afya inayoongozwa na nchi husika, mageuzi ya kidijitali katika mifumo ya afya, na kuhakikisha ushiriki wa kijamii ili kuimarisha mamlaka ya afya ya kitaifa.

Aidha amesisitiza eneo jingine linalopewa mkazo ni Afya ya Akili ambapo amesema kufuatia Mkutano wa Ngazi ya Juu wa Umoja wa Mataifa wa mwaka 2025 kuhusu Magonjwa Yasiyoambukiza (NCDs) na afya ya akili, WHA79 ina kampeni kubwa za utetezi na matukio maalum yanayolenga kutafsiri ahadi za kimataifa kuwa mikakati halisi ya kitaifa ya afya ya akili.

Jambo jingine litakalojadiliwa ni Tabianchi na Afya ambapo amefafanua kuwa ingawa si ajenda maalum ya pekee, athari zinazoendelea za mzozo wa tabianchi na matumizi ya mafuta ya kisukuku ni sehemu muhimu ya mijadala inayohusu afya ya uzazi, magonjwa yasiyoambukiza, na usimamizi wa magonjwa.

Amesem WHO pia inazindua mpango wa kimataifa wa utetezi uliokusudiwa kudumisha msukumo kuelekea mkutano ujao wa COP31 kuhusu tabianchi.
Mkakati wa Kimataifa na Uongozi: Wajumbe wanajadili namna ya kuoanisha mageuzi mbalimbali ya afya ya kimataifa ili kuhakikisha matokeo yenye usawa na uwajibikaji.

Aidha, mkutano huu unaweka msingi wa uchaguzi ujao wa Mkurugenzi Mkuu wa WHO, huku wagombea wakianza kutangazwa rasmi na kundi jipya la nchi likichaguliwa kuingia katika Bodi ya Utendaji.

Pia ameongeza kwamba mkutano huu pia utajadili taarifa na Mikakati ya Magonjwa ambapo ajenda ya muda ya mkutano inajumuisha hatua zinazoendelea kwa mpango wa kutokomeza malaria, Ajenda ya Chanjo 2030, na mkakati wa kumaliza ugonjwa wa kifua kikuu (TB).

Ujumbe wa Tanzania katika mkutano huu ulioongozwa na Mheshimiwa Mchengerwa umeshirikisha Mheshimiwa Balozi Abdala Possi, Mwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika Ofisi ya Umoja wa Mataifa na Mashirika Mengine ya Kimataifa Mjini Geneva, Mwenyekiti wa Kamati ya kudumu ya Afya na Ukimwi, Mheshimiwa, Dkt. Johannes Lukumay, Katibu Mkuu Dkt. Seif Shekalaghe, Mganga Mkuu wa Serikali
, Dkt. Grace Magembe na baadhi ya watendaji wa Wizara ya Afya.

Tanzania inatarajia kuwasilisha mawasilisho kadhaa katika mkutano huo na kufanya majadiliano na wadau mbalimbali wa afya pembezoni mwa mkutano huo.
AFUA ZA UKIMWI KUBORESHWA MKOA WA PWANI

AFUA ZA UKIMWI KUBORESHWA MKOA WA PWANI

May 18, 2026 Add Comment

 




Na, Mwandishi wetu – Pwani

Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Mhe. Abubakar Kunenge, amekutana na Katibu Mkuu wa Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu, Dkt. Jim Yonazi, katika ziara maalum ya kutembelea, kukagua na kutoa elimu katika Kituo cha Maarifa cha Mdaula kilichopo Chalinze, Mkoa wa Pwani.

Ziara hiyo imefanyika leo tarehe 18 Mei, 2026 ambapo Dkt. Yonazi alipata fursa ya kupokea taarifa ya maendeleo ya Mkoa wa Pwani, hususan katika utekelezaji wa Afua za masuala ya UKIMWI hasa huduma na mipango inayohusu WAVIU (Watu Wanaoishi na Virusi vya UKIMWI).

Taarifa hiyo ilieleza hatua mbalimbali zinazochukuliwa na Serikali pamoja na wadau wa maendeleo katika kuboresha huduma za afya na ustawi wa jamii kwa wananchi wa mkoa huo.

Aidha kwa upande wake amesema Serikali kwa sasa imeongeza bajeti katika hutuma za VVU na UKIMWI ii kungeza ufanisi zaidi katika kuwahudumia wananchi.

Zahanati ya Mdaula ilianza kutoa huduma za afya mwezi Oktoba mwaka 2022, ikiwa ni pamoja na huduma za wagonjwa wa nje, huduma za mama na mtoto, uzazi pamoja na huduma za chanjo kupitia kliniki tembezi. Kwa sasa, zahanati hiyo ina tawi dogo lililopo kandokando ya barabara ambalo linatoa huduma za maarifa ya jamii kwa wananchi na wasafiri wanaopita katika eneo hilo.

Tawi hilo lilifanyiwa maboresho na Tume ya Kudhibiti UKIMWI Tanzania (TACAIDS) kupitia Mradi wa SATTF uliokuwa unasimamiwa na TANROADS wakati wa utekelezaji wa ujenzi wake. Maboresho hayo yamelenga kuongeza ufanisi wa utoaji wa elimu na huduma zinazohusiana na mapambano dhidi ya maambukizi ya Virusi vya UKIMWI pamoja na huduma nyingine za afya ya jamii.