HABARI

SIASA

ELIMU

Recent Posts

WIZARA yakutana na Wabunge wa Tanzania EALA: Yasisitiza Kuimarisha Nafasi ya Tanzania Kikanda

April 21, 2026 Add Comment
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki imekutana na kuzungumza na Wabunge wa Tanzania katika Bunge la Afrika Mashariki (EALA) katika Ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam Aprili 21, 2026.

KATIBU MKUU CCM, UJUMBE MTANDAO WA VIONGOZI WANAWAKE AFRIKA WAFANYA MAZUNGUMZO

April 21, 2026 Add Comment
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Ndg. Asha-Rose Migiro, leo tarehe 21 Aprili 2026 amekutana na kufanya mazungumzo na ujumbe wa Mtandao wa Viongozi Wanawake wa Afrika (African Women Leaders Network - AWLN), ulioongozwa na Marais wastaafu wa Jamhuri ya Liberia, Mhe. Ellen Johnson Sirleaf, na Jamhuri ya Shirikisho la Kidemokrasia ya Ethiopia, Mhe. Sahle-Work Zewde, jijini Dar es Salaam.
EWURA YAHAMASISHA UJENZI WA VITUO VIJIJINI CNG WIKI YA NISHATI DODOMA

EWURA YAHAMASISHA UJENZI WA VITUO VIJIJINI CNG WIKI YA NISHATI DODOMA

April 21, 2026 Add Comment

Kaimu Meneja wa Mawasiliano na Uhusiano wa Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA), Bw. Wilfred Mwakalosi,akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) kwenye banda la EWURA wakati wa maonesho ya Wiki ya Nishati yanayoendelea katika viwanja vya bunge jijini Dodoma.

Na.Alex Sonna-Mzalendo blog-DODOMA

Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA), leo 21 Aprili 2026, imetumia fursa ya Wiki ya Nishati kuwahamasisha waheshimiwa wabunge kuwekeza katika ujenzi wa vituo vya mafuta maeneo ya vijijini pamoja na vituo vya CNG ili kuendelea kusogeza huduma kwa wananchi.

Kaimu Meneja wa Mawasiliano na Uhusiano wa EWURA, Bw. Wilfred Mwakalosi, alisema kuwa EWURA inatumia maonesho hayo kutoa elimu kuhusu namna inavyohakikisha upatikanaji wa huduma za nishati na maji kwa wakati na kwa gharama nafuu.

Amebainisha kuwa wabunge ni wawakilishi wa wananchi, hivyo kuwajengea uelewa kuhusu udhibiti, fursa za uwekezaji na utaratibu wa kupokea na kushughulikia migogoro na malalamiko kutawawezesha kuwasilisha taarifa sahihi kwa wananchi kuhusu juhudi za Serikali katika kuhakikisha upatikanaji wa huduma bora za umeme, mafuta na gesi asilia.

Akizungumza katika maonesho hayo, Ofisa Mwandamizi wa Kitengo cha Mafuta, Mhandisi. Ibrahim Kajugusi, amesema elimu inayotolewa pia inalenga kuwafahamisha wananchi jinsi EWURA inavyosimamia upatikanaji wa huduma za mafuta nchini kwa kuzingatia ubora uliopitishwa na gharama sahihi.

Aidha, amewahamasisha wananchi kuchangamkia fursa za uwekezaji katika sekta hiyo, hususan ujenzi wa vituo vya mafuta vya gharama nafuu vijijini na mijini pamoja vituo vya kujazia gesi asilia kwenye magari (CNG).

Kwa upande wake, Mchumi wa EWURA Bi. Achilana Mtingele,amesema  elimu inayotolewa imejikita katika kueleza namna EWURA inavyosimamia upangaji wa viwango vya bei za huduma za umeme, mafuta na gesi asilia. Aliongeza kuwa mamlaka hiyo huweka mizania kati ya maslahi ya watoa huduma na watumiaji, na kwamba wabunge waliopata elimu hiyo wataweza kuiwasilisha ipasavyo kwa wananchi katika maeneo yao.

Akizungumzia sekta ya gesi asilia, Mhandisi Mwandamizi wa Gesi Asilia, Mhandisi Evaline Rweikiza, amesema  EWURA itaendelea kusimamia ubora wa miundombinu ya gesi asilia nchini na kuhamasisha matumizi yake, hususan katika magari.

Amebainisha kuwa hadi sasa vituo 18 vimepata leseni ya EWURA kutoa huduma ya gesi asilia, huku vituo sita vingine vikiwa katika hatua za mwisho za kupata leseni katika mikoa ya Dar es Salaam na Pwani. Aidha, mipango inaendelea kwa baadhi ya makampuni kusambaza gesi asilia iliyokandamizwa katika mikoa ya Morogoro na Dodoma.

Kwa upande wa sekta ya umeme, Mhandisi Mwandamizi wa Umeme, Lulu Chilumba, amewahamasisha wabunge na wadau wanaotembelea maonesho hayo kutumia mafundi umeme wenye leseni kutoka EWURA ili kuhakikisha usalama wa nyumba na mali zao. Alisema EWURA inaendelea kutoa leseni kwa mafundi umeme wenye sifa stahiki, ambapo zaidi ya leseni 1,000 zilitolewa katika mwaka wa fedha uliopita.

Naye Ofisa Rasilimali Watu Mkuu, Bi. Limi Kahabi, amesema EWURA ni mwajiri anayezingatia misingi ya usawa na haki katika mchakato wa ajira, akisisitiza kuwa taasisi hiyo huajiri kwa kuzingatia sifa, weledi na usawa kwa wote.

Kaimu Meneja wa Mawasiliano na Uhusiano wa Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA), Bw. Wilfred Mwakalosi,akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) kwenye banda la EWURA wakati wa maonesho ya Wiki ya Nishati yanayoendelea katika viwanja vya bunge jijini Dodoma.

Kaimu Meneja wa Mawasiliano na Uhusiano wa Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA), Bw. Wilfred Mwakalosi,akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) kwenye banda la EWURA wakati wa maonesho ya Wiki ya Nishati yanayoendelea katika viwanja vya bunge jijini Dodoma.

Kaimu Meneja wa Mawasiliano na Uhusiano wa Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA), Bw. Wilfred Mwakalosi,akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) kwenye banda la EWURA wakati wa maonesho ya Wiki ya Nishati yanayoendelea katika viwanja vya bunge jijini Dodoma.

Mchumi wa EWURA Bi. Achilana Mtingele,akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) kwenye banda la EWURA wakati wa maonesho ya Wiki ya Nishati yanayoendelea katika viwanja vya bunge jijini Dodoma.

 Ofisa Mkuu, Usimamizi wa Rasilimali Watu,Bi. Limi Kahabi,akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) kwenye banda la EWURA wakati wa maonesho ya Wiki ya Nishati yanayoendelea katika viwanja vya bunge jijini Dodoma.

Mhandisi Mwandamizi wa Umeme, Lulu Chilumba,akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) kwenye banda la EWURA wakati wa maonesho ya Wiki ya Nishati yanayoendelea katika viwanja vya bunge jijini Dodoma.

Ofisa Mwandamizi wa Kitengo cha Mafuta, Mhandisi. Ibrahim Kajugusi,akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) kwenye banda la EWURA wakati wa maonesho ya Wiki ya Nishati yanayoendelea katika viwanja vya bunge jijini Dodoma.

Mhandisi Mwandamizi wa Gesi Asilia, Mhandisi Evaline Rweikiza,akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) kwenye banda la EWURA wakati wa maonesho ya Wiki ya Nishati yanayoendelea katika viwanja vya bunge jijini Dodoma.

Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) wakiwa katika picha ya pamoja siku ya pili ya Maonesho  ya Wiki ya Nishati 2026 yanayofanyikia katika Viwanja vya Bunge Jijini Dodoma

Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) wakiwa katika picha ya pamoja siku ya pili ya Maonesho  ya Wiki ya Nishati 2026 yanayofanyikia katika Viwanja vya Bunge Jijini Dodoma

KATIBU MKUU MAFUTA NA GESI ASILIA AHAMASISHA WANANCHI KUTUMIA NISHATI SAFI YA KUPIKIA

April 21, 2026 Add Comment




📌Asema ni utekelezaji wa Dira ya Taifa ya mwaka 2050


📌Aeleza  miradi ya kimkakati ya umeme inaongeza uzalishaji  wa umeme nchini


Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati anayeshughulikia Mafuta na Gesi asilia, Dkt. James Mataragio, ametoa wito kwa wananchi kutumia nishati safi ya kupikia kama sehemu ya utekelezaji wa Dira ya Taifa ya mwaka 2050 inayolenga kuhamasisha matumizi ya nishati safi ambayo ni  salama na endelevu.


Dkt. Mataragio ametoa kauli hiyo Aprili 21, 2026, alipotembelea banda la TANESCO eneo la nishati safi ya kupikia kwa umeme , katika maonesho ya Wiki ya Nishati yanayoendelea katika viwanja vya Bunge, jijini Dodoma.


Amesema kuwa Serikali inaendelea kuweka mkazo katika kuhamasisha matumizi ya nishati safi, ikiwa ni pamoja na umeme, ili kulinda afya za wananchi na mazingira kwa ujumla, Aidha, ameipongeza TANESCO kwa juhudi zake za kuelimisha na kuhamasisha wananchi kutumia umeme kupikia.



‘’ Bajeti ya Nishati inatarajiwa kusomwa Bungeni, miongoni mwa mambo tunayotekeleza katika Bajeti yetu ni Dira ya Taifa ya mwaka 2050 ,hapo kuna kipengele cha nishati safi ya kupikia na kwa ujumla Taasisi zetu ikiwemo TANESCO  zinahamasisha matumizi ya nishati  safi ya  kupika kwa umeme,’’alifafanua Dkt Mataragio.


Kwa upande wake, Mbunge kutoka  Manyara, Mhe. Justina Rahhi, amesifu teknolojia ya majiko ya umeme yanayotumia nishati kidogo, akieleza kuwa yana uwezo wa kupunguza matumizi ya mkaa na kuni.

“Nimejifunza kuwa majiko haya yanatumia umeme kidogo sana ukilinganisha na mkaa. Ni muhimu teknolojia hii iwafikie wananchi wa vijijini ili waweze kunufaika na matumizi ya nishati safi,” amesema Mhe. Rahhi

Naye Mbunge wa Viti Maalum kutoka mkoa wa Ruvuma, Mhe. Mariam Nyoka, amepongeza kuimarika kwa huduma ya umeme katika mikoa ya Nyanda za Juu Kusini, akieleza kuwa hali hiyo itasaidia kuongeza matumizi ya nishati safi.



Katika maonesho hayo ya Wiki ya Nishati, TANESCO pia imewasilisha teknolojia mpya ya magari yanayotumia umeme, ambayo yanaelezwa kuwa na gharama nafuu zaidi kwa matumizi ikilinganishwa na magari yanayotumia nishati nyingine.

EWURA YAENDELEA KUBORESHA HUDUMA ZA UMEME NA GESI ASILIA

EWURA YAENDELEA KUBORESHA HUDUMA ZA UMEME NA GESI ASILIA

April 21, 2026 Add Comment

Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati anayeshughulikia mafuta na gesi asilia, Dkt. James Mataragio,akipata maelezo kutoka kwa Kaimu Meneja wa Mawasiliano na Uhusiano wa EWURA, Bw.Wilfred Mwakalosi,alipotembelea banda la EWURA  katika  maonesho ya Wiki ya Nishati 2026 yanayoendelea katika viwanja vya Bunge jijini Dodoma.

.....

Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati anayeshughulikia mafuta na gesi asilia, Dkt. James Mataragio, amewaomba waheshimiwa wabunge na wadau mbalimbali kuendelea kutembelea maonesho ya Wiki ya Nishati 2026 yanayoendelea katika viwanja vya Bunge jijini Dodoma, ili kupata elimu juu ya shughuli za kimkakati zinazotekelezwa na taasisi zilizo chini ya wizara hiyo pamoja na kubaini fursa za uwekezaji zinazopatikana.

Akiwa akiwa katika banda la Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA), Dkt. Mataragio amesema mamlaka hiyo imeendelea kuwa nguzo muhimu katika kuhakikisha uwiano kati ya maslahi ya watoa huduma na watumiaji wa huduma zinazodhibitiwa, ikiwemo mafuta, gesi asilia na umeme.

“Tumeshuhudia jitihada kubwa zinazofanywa na EWURA katika kusimamia ubora wa huduma na bei stahiki, jambo ambalo linachangia kukuza uchumi na kulinda wananchi,” amesema Dkt. Mataragio.

Ameongeza kuwa uwepo wa EWURA katika maonesho hayo unatoa fursa kwa wananchi kupata elimu kuhusu haki na wajibu wao katika matumizi ya nishati, sambamba na kuelewa mifumo ya udhibiti inayolenga kuboresha huduma na fursa mbalimbali za uwekezaji.

Kwa upande wao, baadhi ya wabunge waliotembelea banda hilo pia waliipongeza EWURA kwa uwajibikaji wake, wakisema imekuwa mstari wa mbele kusikiliza na kushughulikia changamoto zinazowakabili wananchi katika sekta ya nishati pamoja na kuhakilisha upatikanaji wa huduma bora kwa wananchi.

Wiki ya Nishati 2026 imewakutanisha wadau mbalimbali wa sekta ya nishati, zikiwemo taasisi zote zilizo chini ya Wizara ya Nishati kwa lengo la kuonesha maendeleo na fursa zilizopo katika sekta hiyo muhimu kwa ustawi wa uchumi wa taifa.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati anayeshughulikia mafuta na gesi asilia, Dkt. James Mataragio,akipata maelezo kutoka kwa Kaimu Meneja wa Mawasiliano na Uhusiano wa EWURA, Bw.Wilfred Mwakalosi,alipotembelea banda la EWURA  katika  maonesho ya Wiki ya Nishati 2026 yanayoendelea katika viwanja vya Bunge jijini Dodoma.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati anayeshughulikia mafuta na gesi asilia, Dkt. James Mataragio,akipata maelezo kutoka kwa Kaimu Meneja wa Mawasiliano na Uhusiano wa EWURA, Bw.Wilfred Mwakalosi,alipotembelea banda la EWURA  katika  maonesho ya Wiki ya Nishati 2026 yanayoendelea katika viwanja vya Bunge jijini Dodoma.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati anayeshughulikia mafuta na gesi asilia, Dkt. James Mataragio,akisisitiza jambo kwa watumishi wa EWURA alipotembelea banda la EWURA  katika  maonesho ya Wiki ya Nishati 2026 yanayoendelea katika viwanja vya Bunge jijini Dodoma.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati anayeshughulikia Mafuta na Gesi, Dkt. James Mataragio akisaini kitabu cha wageni mara baada ya kutembelea Banda la EWURA kwenye Maonesho ya Wiki ya Nishati 2026 yanayoendelea katika Viwanja vya Bunge Jijini Dodoma

Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati anayeshughulikia Mafuta na Gesi, Dkt. James Mataragio akipokea zawadi kutoka kwa Kaimu Meneja wa Mawasiliano na Uhusiano wa EWURA, Bw.Wilfred Mwakalosi, mara baada ya kutembelea Banda la EWURA kwenye Maonesho ya Wiki ya Nishati 2026 yanayoendelea katika Viwanja vya Bunge Jijini Dodoma

Wabunge mbalimbali wakipata elimu walipotembelea banda la EWURA  katika  maonesho ya Wiki ya Nishati 2026 yanayoendelea katika viwanja vya Bunge jijini Dodoma.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati anayeshughulikia mafuta na gesi asilia, Dkt. James Mataragio,akizungumza mara baada ya kutembelea mabanda ya taasisi zilizo chini ya Wizara ya Nishati  katika  maonesho ya Wiki ya Nishati 2026 yanayoendelea katika viwanja vya Bunge jijini Dodoma.

KATIBU MKUU MATARAGIO AIPONGEZA PBPA KWA KUHAKIKISHA UWEPO WA MAFUTA YA KUTOSHA NCHINI

April 21, 2026 Add Comment
Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati (anayeshughulikia mafuta na gesi),Dkt. James Mataragio ameipongeza Wakala wa Uagizaji Mafuta kwa Pamoja (PBPA) kwa kuhakikisha nchi inakuwa na mafuta ya kutosha wakati wote.

DAWASA YAWAUNGANISHIA MAJI KWA MKOPO WAKAZI WA KIBOSHA

April 21, 2026 Add Comment
Wakazi zaidi ya 100 wa Kitongoji cha Kibosha Mji Mpya wamejitokeza kuomba kuunganishiwa huduma ya majisafi na salama, wakati mradi wa maji wa Kibosha Mnarani ukiendelea kukamilishwa na Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA).

TIRDO IJE NA TEKNOLOJIA RAHISI KWENYE NISHATI SAFI- MHE. RAIS

April 21, 2026 Add Comment
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan ameitaka TIRDO kushirikiana na Taasisi zingine kuhakikisha watanzania wanapata nishati safi rafiki na Kwa bei rahisi .

TANZANIA YAIMARISHA DIPLOMASIA YA ELIMU KUPITIA KONGAMANO LA 3 LA MARAIS WA VYUO VIKUU CHINA–AFRIKA

April 21, 2026 Add Comment
Na Mwandishi Wetu

JINHUA, CHINA — Taasisi za elimu ya juu kutoka Tanzania zikiwemo ADEM, MUCE, TIA, SUZA na UDSM zimeshiriki Kongamano la 3 la Marais wa Vyuo Vikuu kati ya China na Afrika lililofanyika jijini Jinhua kuanzia Aprili 14 hadi 20, 2026.

WAZIRI NDEJEMBI AWAKARIBISHA WABUNGE KUTEMBELEA KITUO CHA KUFUA UMEME CHA JULIUS NYERERE KIDIGITALI

April 21, 2026 Add Comment


📌Awakaribisha kujionea kazi kubwa inayofanyika katika uzalishaji wa umeme


📌Ni katika maonesho ya wiki ya nishati yanayoendelea Bungeni Dodoma



Waziri wa Nishati Mhe. Deogratius Ndejembi amewakaribisha wabunge kutembelea Kituo cha kufua umeme cha Julius Nyerere ambacho kinazalisha jumla ya megawati 2115 za umeme kupitia kifaa maalumu cha uhalisia pepe. 


Mhe Ndejembi ameyasema hayo Aprili 20, 2026  wakati akikagua mabanda ya maonesho ya wiki ya nishati  yanayofanyika katika viwanja vya Bunge jijini Dodoma yenye lengo la kuonesha shughuli mbalimbali zinazofanywa  na taasisi chini ya Wizara ya Wizara ya nishati.

“Kupitia maonesho haya, wabunge watapata nafasi ya kujionea kazi mbalimbali zinazofanywa na Wizara ya Nishati kupitia taasisi zake. Hata ambaye hajawahi kufika katika Bwawa la Julius Nyerere ataweza kuliona kupitia teknolojia ya uhalisia pepe na kushuhudia juhudi kubwa zinazofanyika za kuzalisha umeme nchini,” alifafanua Mhe. Ndejembi.

Aidha, amewafahamisha wabunge kuwa wataalamu wa TANESCO kutoka mikoa mbalimbali wapo tayari kupokea na kushughulikia kero pamoja na changamoto zinazowakabili wananchi katika majimbo yao, ili kuzitatua kwa haraka.

Katika hatua nyingine, Mhe. Ndejembi ameelezea juhudi za Serikali katika kuhakikisha wananchi wanapata nishati ya umeme kwa lengo la kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia. Amebainisha kuwa katika maonesho hayo, kuna majiko yanayotumia umeme kidogo ambayo yanaweza kupika chakula kwa ufanisi mkubwa.

“Katika maonesho haya, watu wataona jitihada zinazofanyika katika matumizi ya nishati safi ya kupikia. Hapa kuna vyakula vinapikwa kwa kutumia nishati safi, mtajionea pia majiko ya kisasa yanayotumia umeme kidogo lakini yanapika kwa ufanisi ,” alisisitiza.



Maonesho ya Wiki ya Nishati yanafanyika kwa siku nne, huku bajeti ya Wizara ya Nishati ikitarajiwa kuwasilishwa bungeni Aprili 22, 2026.

BARRICK YADHAMINI KONGAMANO LA AIESEC 2026

April 20, 2026 Add Comment

  

Afisa Rasilimali Mwandamizi wa Barrick Tanzania, Elibramack Joel akiongea na Wanafunzi wa Vyuo vikuu vilivyopo jijini Dar es Salaam wakati wa uzinduzi wa kongamano la AIESEC 2026 lililofanyika katika Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam (UDSM) kampasi ya Mlimani kwa udhamini wa Barrick
Afisa Mafunzo kutoka Barrick Sundi Isandiko akigawa vipeperushi kuhusiana shughuli za kampuni wakati wa kongamano hilo
Watoa mada kutoka makampuni na taasisi mbalimbali wakati wa kongamano la AIESEC lililofanyika katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam
Afisa Mafunzo kutoka Barrick nchini Mwita Matiko akiongea na Wanafunzi katika kongamano hilo
Wanafunzi na wafanyakazi wa Barrick wakifuatilia matukio mbalimbali wakati wa uzinduzi wa kongamano hilo.
Wanafunzi na wafanyakazi wa Barrick wakifuatilia matukio mbalimbali wakati wa uzinduzi wa kongamano hilo.
Wanafunzi kutoka vyuo vikuu mbalimbali walipata fursa za kupiga picha za ukumbusho wakati wa kongamano hilo
Wanafunzi kutoka vyuo vikuu mbalimbali walipata fursa za kupiga picha za ukumbusho wakati wa kongamano hilo

***
Kampuni ya Barrick nchini, imeendeleza dhamira yake ya kuibua na kukuza vipaji vya vijana wasomi wa vyuo vya elimu ya juu na kati nchini ili waweze kukabiliana na mabadiliko yanayoendelea kutokea duniani na kuhimili ushindani katika soko la ajira sambamba na kuweza kujiamini kutumia ujuzi na taaluma zao kujiajiri kwa ajili ya kujenga mustakabali endelevu.