HABARI MPYA
HABARI
SIASA
ELIMU
Recent Posts
RAIS WA NAMIBIA AWASILI KWA ZIARA YA KITAIFA
habariPPAA YAJIVUNIA MAFANIKO MODULI YA MALALAMIKO, RUFAA
habari
Mamlaka ya Rufani ya Zabuni za Umma (PPAA) imeendelea kujivunia mafanikio ya matumizi ya Moduli ya kupokea na kushughulikia malalamiko na rufaa kieletroniki kupitia mfumo Mfumo wa Ununuzi wa Umma wa Tanzania (NeST).
Mafanikio hayo yamebainishwa na Katibu Mtendaji wa PPAA, Bw. James Sando alipotembelea banda la Mamlaka hiyo kwenye maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayoendelea katika Viwanja vya Chinangali, Jijini Dodoma.
Bw. Sando amesema kuwa moduli ya kupokea na kushughulikia malalamiko na rufaa ilianzishwa ili kutatua changamoto mbalimbali zilizokuwa zinajitokeza kwenye utatuzi wa migogoro kwenye michakato ya ununuzi wa umma.
“Changamoto tulizoziondoa kwa wazabuni na taasisi nunuzi ni pamoja kuokoa muda, gharama, uwazi na uwajibikaji pamoja na kumbukumbu sahihi za malalamiko na rufaa zinazowasilishwa na wazabuni,” amesema Bw. Sando.
Bw. Sando amebainisha kuwa ili PPAA iweze kufanya maamuzi kuhusu shauri lililowasilishwa kwa Mamlaka hiyo ni lazima kuwa na kumbukumbu sahihi za shauri hilo, hivyo kupitia moduli PPAA imeweza kupata nyaraka mbalimbali zinazohitajika kwa wakati.
“Kwa Mwaka wa fedha 2025/26 hadi sasa malalamiko takribani 157 yamewasilishwa kupitia moduli hiyo kwa taasisi nunuzi, na kati ya malalamiko hayo mashauri 37 yamewasilishwa PPAA na kutolewa uamuzi, hivyo matumizi ya moduli yanaendelea vyema,” ameongeza Bw. Sando
PPAA inampango wa kuunganisha sekta ya utoaji haki katika ununuzi wa umma na mfumo wa utoaji haki wa Mahakama ya Tanzania kwa mwaka wa fedha ujao ili kuongeza uwazi na uwajibikaji zaidi.

MADEREVA WANAOSAFIRISHA KEMIKALI WAZINGATIE MAFUNZO
habariNEMC YACHOCHEA UWAJIBIKAJI JUMUISHI: SEKTA YA MAZINGIRA
habariDC NGUBIAGAI AONGOZA VITA DHIDI YA UVUVI HARAMU UKEREWE
habariWALIPAKODI MCHIKICHINI WAPONGEZWA KWA MCHANGO WAO KATIKA MIAKA 30 YA MAFANIKIO YA TRA
habariWAAJIRI WANAOZINGATIA SHERIA ZA KAZI WAPONGEZWA
habari
MKURUGENZI WA UCHAGUZI APONGEZA UFANISI NA UWAZI WA MFUMO WA UAGIZAJI MAFUTA KWA PAMOJA
habari
Na Mwandishi Wetu
Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Bw. Ramadhan Kailima, amepongeza ufanisi na uwazi wa Mfumo wa Uagizaji Mafuta kwa Pamoja unaosimamiwa na Wakala wa Uagizaji Mafuta kwa Pamoja, akieleza kuwa mfumo huo umechangia kuimarisha ukusanyaji wa mapato ya Serikali na kuhakikisha upatikanaji wa mafuta nchini.
Bw. Kailima alitoa pongezi hizo Juni 18, 2026 alipotembelea banda la PBPA katika Maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayoendelea katika viwanja vya Chinangali jijini Dodoma.
Akizungumza baada ya kupata maelezo kuhusu utekelezaji wa mfumo huo, alisema kuwa umejengwa katika misingi ya uwazi na ushindani, jambo linalosaidia kupunguza gharama za uagizaji wa mafuta na kuongeza ufanisi katika usimamizi wa sekta hiyo muhimu kwa uchumi wa nchi.
Akitoa ufafanuzi kwa mgeni huyo, Mkaguzi wa Mafuta wa PBPA, Bw. Issa Mwitazy, alisema kuwa katika mfumo wa uagizaji mafuta kwa pamoja, ushindani hujikita katika gharama za usafirishaji wa mafuta (Premium).
Alieleza kuwa wazabuni hushindanishwa kwa kuwasilisha bei za usafirishaji wa bidhaa za petroli, dizeli na mafuta ya taa, ambapo mzabuni mwenye gharama nafuu zaidi hupatiwa zabuni husika.
“Utaratibu huu umetuwezesha kuhakikisha upatikanaji wa mafuta ya kutosha nchini wakati wote na wakati huohuo kuipa Serikali taarifa sahihi za kiasi cha mafuta na hivyo kuwezesha ukusanyaji wa mapato yatokanayo na biashara ya mafuta,” alisema.
Aliongeza kuwa mikataba ya uagizaji wa mafuta husainiwa mapema kabla ya bidhaa kuwasili nchini, jambo linaloiwezesha Serikali kufanya makadirio sahihi ya mapato yatokanayo na sekta hiyo.
Kwa mujibu wa Mwitazy, mafanikio ya mfumo huo yameifanya PBPA kuwa kitovu cha huduma za uagizaji mafuta kwa nchi kadhaa za ukanda wa Afrika Mashariki na Kati, zikiwemo Malawi, Rwanda, Zambia na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, ambazo huleta mahitaji yao kupitia mfumo wa uagizaji wa mafuta kwa pamoja.
Ziara ya Bw. Kailima katika banda la PBPA ni sehemu ya shughuli za Maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayolenga kuonesha mafanikio, huduma na ubunifu unaotekelezwa na taasisi za umma katika kuwahudumia wananchi na kuchangia maendeleo ya taifa.

Wananchi Dodoma Wajifunza Haki Zao Kupitia Elimu ya Vipimo Sahihi
habariTANZANIA YAIMARISHA UTAYARI WA KUKABILIANA NA TISHIO LA EBOLA
habariNA EMMANUEL MBATILO, DODOMA
SERIKALI imesema Tanzania bado haina mgonjwa wa Ebola na hali ya usalama wa afya nchini inaendelea kuwa nzuri, huku ikieleza kuwa imeimarisha hatua mbalimbali za kuzuia ugonjwa huo kuingia nchini kutokana na mlipuko unaoendelea katika nchi jirani za Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) na Uganda.
WAZIRI RIDHIWANI KIKWETE AFUNGUA RASMI MAADHIMISHO YA WIKI YA UTUMISHI WA UMMA
habariMTANDAO WATWAA ASILIMIA 44 YA MAWASILISHO YA SAMIA KALAMU
habari
UKEREWE YAWEKA KIPAUMBELE KWA WENYE ULEMAVU, VIJANA NA WANAWAKE KUPITIA MIKOPO YA MAENDELEO
habariSANGU :MAHUSIANO MEMA NI MSINGI WA KUIMARISHA UMOJA NA DEMOKRASIA NCHINI
habariWADAU WA MADINI WAKUMBUSHWA KUZINGATIA SHERIA KUONGEZA MANUFAA KWA TAIFA
habari
TBS KUADHIMISHA MIAKA 50, KUZINDUA KITABU CHA HISTORIA YAKE DODOMA
habari
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Viwango Tanzania (TBS), Dkt. Ashura Katunzi,akitoa taarifa kwa umma kuelekea kuhitimisha maadhimisho ya miaka 50 tangu kuanzishwa kwake Juni 19,2026 jijini Dodoma.
...
Shirika la Viwango Tanzania (TBS) linatarajia kuandika historia mpya Juni 19, 2026 kwa kuhitimisha maadhimisho ya miaka 50 tangu kuanzishwa kwake, huku likitarajia kuzindua kitabu maalumu kitakachobeba historia, mafanikio na mchango wake katika maendeleo ya viwanda, biashara na ustawi wa Watanzania.
Akizungumza jijini Dodoma kuhusu maandalizi ya kilele cha maadhimisho hayo, Mkurugenzi Mkuu wa TBS, Dkt. Ashura Katunzi, amesema hafla hiyo itafanyika katika ofisi za shirika hilo na inatarajiwa kuhudhuriwa na wadau mbalimbali kutoka sekta za umma na binafsi.
Dkt. Katunzi amesema mgeni rasmi katika kilele cha maadhimisho hayo anatarajiwa kuwa Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Judith Salvio Kapinga (Mb), ambaye ataungana na viongozi, wadau na wananchi kusherehekea mafanikio ya nusu karne ya taasisi hiyo muhimu nchini.
Amesema sambamba na sherehe hizo, TBS itazindua kitabu maalumu cha miaka 50 kitakachoelezea safari ya shirika hilo tangu kuanzishwa kwake, hatua mbalimbali za maendeleo iliyopitia pamoja na mchango wake katika kuhakikisha bidhaa na huduma zinazotolewa nchini zinazingatia viwango vinavyotakiwa.
“Kitabu hiki kitakuwa sehemu ya kumbukumbu muhimu ya taifa. Kitaelezea historia ya TBS, mafanikio yaliyopatikana katika kipindi cha miaka 50 na kitakuwa rejea kwa vizazi vya sasa na vijavyo ili kuelewa mchango wa shirika katika maendeleo ya nchi,” amesema Dkt. Katunzi.
Ameeleza kuwa kwa kipindi cha miaka 50, TBS imeendelea kuwa mhimili muhimu katika kulinda afya na usalama wa watumiaji wa bidhaa mbalimbali, huku ikichochea ukuaji wa viwanda kwa kuhakikisha bidhaa zinazozalishwa nchini zinakuwa bora na zenye ushindani katika masoko ya ndani na nje ya nchi.
Kwa mujibu wa Dkt. Katunzi, mafanikio yaliyofikiwa na TBS katika kipindi hicho si ya shirika pekee bali ni matokeo ya ushirikiano mkubwa kati ya taasisi hiyo, wadau wa maendeleo, sekta binafsi na wananchi kwa ujumla.
“Miaka 50 ya TBS ni mafanikio ya wadau wetu na jamii kwa ujumla. Tunawakaribisha wananchi na wadau wote kushiriki katika kilele cha maadhimisho haya ili kwa pamoja tuadhimishe safari hii ya mafanikio,” amesema.
Maadhimisho hayo yanatarajiwa kuwa fursa ya kutafakari mchango wa TBS katika maendeleo ya taifa, huku yakitoa mwanga wa matarajio na mwelekeo wa shirika hilo katika kuendelea kuimarisha ubora wa bidhaa na huduma kwa manufaa ya Watanzania na uchumi wa nchi.
TANESCO MUONGEZE VITUO VYA KUCHAJIA VYOMBO VYA USAFIRI VINAVYOTUMIA UMEME-WAZIRI RIDHIWANI
habariWaziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete amelitaka Shirika la umeme Tanzania ( TANESCO) kuongeza vituo vya kuchajia vyombo vya usafiri vinavyotumia nishati ya umeme ili kuongeza wigo wa utoaji huduma hiyo ambayo imeonekana kuleta mageuzi katika matumizi ya nishati safi.
Mhe. Ridhiwani ameyasema hayo Juni 17, 2026 alipotembelea Banda la TANESCO katika Maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayoendelea kufanyika katika Viwanja vya Chinangali Mkoani Dodoma.
Waziri huyo mwenye dhamana ya Utumishi ametumia nafasi hiyo kuipongeza TANESCO kwa kuendelea kuhamasisha matumizi ya Nishati safi kwa ajili ya kupikia na katika vyombo vya usafiri.
‘’ TANESCO mnafanya kazi kubwa nawapongeza kwa mageuzi ya matumizi ya nishati ya umeme katika vyombo vya usafiri, natoa rai muongeze Vituo vya kuchajia vyombo hivyo ili kuongeza wigo wa utoaji huduma,’’ alisisitiza Mhe. Ridhiwani
Naye Meneja Masoko Bw. Fredrick Kalinga amesema TANESCO inashiriki katika Maonesho hayo ili kutoa elimu kwa wananchi juu ya huduma na bidhaa zinazotolewa na Shirika ikiwemo maendeleo ya miradi ya uzalishaji, usafirishaji na usambazaji umeme, maboresho makubwa yaliyofanywa na Shirika kwenye mifumo ya kidigitali ya utoaji huduma kwa wateja pamoja na kuhamasisha jamii kutumia nishati safi ya umeme kupikia na katika vyombo vya usafiri kama magari, bajaji, guta, na pikipiki.
Maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma kwa mwaka 2026 yenye kauli mbiu isemayo ‘’Kuchochea Uwajibikaji Jumuishi kwa huduma Endelevu’’ yameanza rasmi Juni 16, 2026 na yanatarajiwa kuhitimishwa Juni 23, 2026
KUELEKEA MAADHIMISHO YA MIAKA 30,TRA YAFANYA KONGAMANO LA MAADILI NA VIONGOZI WA DINI
Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), kupitia Idara ya Mambo ya Ndani (INAD), leo Juni 17, 2026 imeandaa Kongamano la Maadili lililowakutanisha viongozi wa dini mbalimbali kujadili nafasi ya maadili katika kuimarisha ukusanyaji wa kodi na kujenga utamaduni wa ulipaji kodi kwa hiari. Kongamano hilo ni sehemu ya maandalizi ya Maadhimisho ya Miaka 30 ya TRA yatakayofanyika Julai 1, 2026.
Akifungua kongamano hilo kwa niaba ya Kamishna Mkuu wa TRA, Naibu Kamishna wa TRA, Bw. Mcha Hassan Mcha, amesema kuwa katika kipindi cha miaka 30 tangu kuanzishwa kwa TRA, taasisi hiyo imepiga hatua kubwa katika kuimarisha mifumo ya ukusanyaji wa mapato, huku maadili yakiendelea kuwa nguzo muhimu katika utekelezaji wa majukumu yake.
Bw. Mcha amesema TRA inaendelea kuwekeza katika mifumo na mikakati mbalimbali ya kuimarisha maadili kwa watumishi wake na walipakodi ili kujenga uaminifu, uwajibikaji na kuongeza kiwango cha ulipaji kodi kwa hiari.
“Maadili hujenga imani, na imani hujenga ulipaji wa kodi kwa hiari,” alisema Bw. Mcha.
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Jumuiya ya Maridhiano Tanzania (JMAT), Sheikh Alhad Mussa Salum, ameipongeza TRA kwa kuandaa kongamano hilo na kueleza kuwa maadili ni msingi muhimu wa maendeleo ya jamii na taifa. Amesema mafundisho ya dini yanasisitiza uadilifu, uwajibikaji na kufanya mema, huku ulipaji wa kodi ukiwa sehemu ya wajibu unaochangia ustawi wa wananchi na maendeleo ya nchi.
Naye Mkuu wa Evangelical Fellowship Church Tanzania, Askofu Charles Asher Howard, amesema maandiko matakatifu yanaelekeza waumini kutimiza wajibu wao kwa mamlaka halali, ikiwemo kulipa kodi. Amebainisha kuwa maendeleo ya Tanzania yanategemea mchango wa kila mwananchi, hivyo ulipaji wa kodi ni jukumu la pamoja linalopaswa kutekelezwa kwa uaminifu na uzalendo.
Viongozi hao wa dini wamepongeza hatua ya TRA ya kuwashirikisha katika mijadala ya maadili na ukusanyaji wa mapato, wakisisitiza kuwa ushirikiano kati ya taasisi za umma na viongozi wa dini una nafasi muhimu katika kuhamasisha wananchi kulipa kodi kwa hiari na kujenga taifa lenye uwajibikaji, uadilifu na maendeleo endelevu.

.jpeg)

.jpeg)

.jpeg)

.jpeg)



.jpeg)
WAZIRI KIKWETE AVUTIWA NA MFUMO WA KUPANGA NA KUSIMAMIA MIRADI YA REA
Nishati
*📌Asema REA Digital Platform ni mfumo wa kisasa kueleza miradi*
📍Chinangali Park - Dodoma
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete, amevutiwa na mfumo wa Kupanga na Kusimamia miradi ya Wakala wa Nishati Vijijini (REA).
Mhe. Kikwete ameipongeza REA kwa kuja na mfumo huo mara baada ya kutembelea banda hilo kwenye ufunguzi wa Maadhimiaho ya Wiki ya Utumishi kwa Umma 2026 yanayofanyika katika viwanja vya Chinangali Park jijini Dodoma.
Mfumo huo (*REA DIGITAL PLATFORM*) unaonyesha miradi yote inayotekelezwa na REA na kuweza kuisimamia kidijitali na kuwapa taarifa wadau popote walipo duniani kuhusiana na miradi ya Nishati vijijini.
Akimueleza Mhe. Kikwete, Afisa Upimaji Mwandamizi wa REA, Bw. Hussein Shamdas ameeleza kuwa kupitia mfumo huo mwananchi anaweza kujua mipango ya Wakala kwenye eneo lake na kufuatilia miradi inayotekelezwa na Wakala katika eneo husika.
Mwisho
UMEME UPO WA KUTOSHA :MNAANGAZA MAISHA YA WANANCHI-MHE.KIKWETE
habariWaziri wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwan Kikwete ameipongeza Wizara ya Nishati na Taasisi zake kwa kuendelea kuhamasisha Matumizi ya Nishati Safi kwa Wananchi pamoja na kuimarika kwa upatikanaji wa huduma za nishati nchini.
Kikwete amesema hayo Juni 17, 2026 alipotembelea Banda la Wizara ya Nishati na Taasisi zake wakati wa maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayofanyika Katika viwanja vya Chinangali jijini Dodoma.
Aidha, amesisitiza Wizara pamoja na Taasisi zake kuendelea kutoa elimu kwa wananchi kuhusu Matumizi ya Nishati Safi ili Kila mmoja aifahamu kwa kina kwa manufaa ya kulinda Afya na mazingira.
" Hongerani Sana Nishati kwa kuendelea kuwasha Umeme na kuangaza Maisha ya Wananchi, tunaona Umeme upo wa kutosha" Alisema Kikwete
Sambamba na hilo amesisitiza kuendelea kutangaza fursa zilizopo katika Sekta ya Nishati nchini kwa wananchi.
Ametembelea Taasisi zilizo chini ya Wizara ya Nishati ambazo ni TANESCO, REA, TPDC, EWURA, PURA,PBPA na EWURA CCC ambapo alipata fursa ya kujionea huduma zinazotolewa na taasisi hizo pamoja na mafanikio ya miradi mbalimbali inayotekelezwa.
NEMC YASISITIZA MASHIRIKIANO KATIKA UHIFADHI NA USIMAMIZI WA MAZINGIRA
Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) limesisitiza ushirikiano wa wadau wote wakiwemo Serikali, Sekta binafsi, taasisi za umma, jamii na wananchi katika kusimamia na kuhifadhi mazingira kwa maendeleo endelevu.
Akizungumza na waandishi wa habari tarehe 17 Juni, 2026 katika ukumbi wa mikutano wa NEMC Jijini Dar es salaam, Kaimu Meneja Uhusiano na Mawasiliano kwa Umma NEMC, Bi. Martha Kawishe, amesema mazingira ni suala mtambuka linalohitaji kila mdau kutimiza wajibu wake kwa kuzingatia Sheria na Miongozo ya Mazingira iliyowekwa.
Ameeleza kuwa NEMC inaendelea kusimamia utekelezaji wa Sheria kupitia ukaguzi wa miradi, utoaji wa elimu kwa umma katika masuala mazima ya udhibiti wa kelele chafuzi za mazingira, uharibifu wa vyanzo vya maji, utupaji holela wa taka, kutiririsha maji taka msimu wa mvua, ukataji hovyo wa miti na kuhakikisha miradi yote inazingatia Tathmini ya Athari kwa Mazingira (TAM) kabla ya kuanza.
Aidha, amewataka wananchi kuwa makini na watu wanaojifanya maafisa wa NEMC kwa lengo la udanganyifu, akisisitiza kuwa malipo yote hufanyika kwa utaratibu wa kiserakili na ukaguzi hufanywa na maafisa kisheria wakiwa na vithibitsho vifuatavyo: vitambulisho vya ukaguzi, vitambulisho vya kazi pamoja na nyaraka zinazompa mamlaka kisheria ya kufanya ukaguzi, na hasa ikizingatiwa ukaguzi hufanywa kidigitali ambapo mteja hupokea ujumbe mara baada ya ukaguzi.
NEMC pia imehimiza wananchi kutumia huduma rasmi ya kituo cha huduma kwa mteja kwa kupiga namba ya bure 0800110115 na kutumia mfumo wa e-mrejesho kwa kufuata menyu ya *152*00# na kufuata maelekezo ili kutoa ushauri, taarifa au changamoto za kimazingira.
RC MBONI MHITA AWEKA JIWE LA MSINGI JENGO LA KISASA LA BILIONI 5.3 USHETU,
habari





























