HABARI

SIASA

ELIMU

Recent Posts

RAIS KAGAME ATUA TANZANIA,KUKUTANA NA RAIS DKT.SAMIA IKULU JIJINI DAR ES SALAAM

May 03, 2026 Add Comment



Rais wa Jamhuri ya Rwanda, Mhe. Paul Kagame amewasili nchini kwa Ziara ya Kikazi ya siku moja yenye lengo la kuimarisha uhusiano wa uwili kati ya Tanzania na Rwanda.

Mhe. Rais Kagame anatarajia kukutana na kufanya mazungumzo na mwenyeji wake, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Ikulu jijini Dar es Salaam.

Inategemewa kwamba Ziara hii itadumisha mahusiano mazuri na ya kihistoria kati ya majirani hawa wawili. Ushirikiano huu umezidi kuimarika katika miaka ya hivi karibuni kwa kupitia Tume ya Kudumu ya Pamoja (JPC), ambapo Tanzania imeendelea kuwa miongoni mwa washirika wakuu watatu wa biashara wa Rwanda duniani, huku kiwango cha biashara kati ya nchi hizi kikiongezeka kila mwaka.
 

Aidha, katika uwekezaji, kuanzia mwaka 1990 hadi Machi 2026, Tanzania imesajili miradi 42 ya uwekezaji kutoka Rwanda yenye thamani ya dola za Marekani milioni 325.53 na kuunda ajira 2,225 katika sekta mbalimbali ikiwemo viwanda, usafirishaji, huduma za kifedha, maliasili na utalii.

Vilevile, wawekezaji wa Tanzania pia wamewekeza nchini Rwanda kupitia kampuni mbalimbali zikiwemo Bakhresa Group, Magodoro Dodoma, Discount Center, Jambo Plastic, Sagar Enterprises, Buffalo Travelling Tours, Maxcom Africa, Gasabo Grain Milling Company, LCM Delta Company na Metrex Integrated Consultancy.























CHUO KIKUU CHA HARVARD CHA MAREKANI KUINGIA USHIRIKIANO WA MATUMIZI YA AKILI MNEMBA (AI) NA CHUO KIKUU CHA DAR ES SALAAM

May 03, 2026 Add Comment

 



Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) kimeingia katika mazungumzo ya ushirikiano wa kimkakati na Chuo Kikuu cha Harvard, Marekani, yakilenga kuimarisha matumizi ya Akili Mnemba (AI) katika elimu, utafiti na uchambuzi wa taarifa.


Mazungumzo hayo yalianzishwa na Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Rais Mstaafu Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, alipokuwa katika ziara ya kikazi nchini Marekani.

Ushirikiano huo unalenga kujenga uwezo wa kutumia AI kwa ufanisi katika kufundishia, kuongeza kasi ya tafiti, na kurahisisha uchakataji wa taarifa nyingi kwa wakati mfupi, eneo ambalo linazidi kuwa muhimu katika vyuo vikuu duniani.

Katika kipindi ambacho taasisi za elimu ya juu zinakabiliana na changamoto na fursa zinazotokana na AI, hatua ya UDSM kuingia katika mazungumzo na Harvard inaonekana kama mkakati wa mapema wa kuhakikisha Tanzania haiwi nyuma katika mapinduzi ya teknolojia.

Akizungumza katika kikao hicho, Dkt. Kikwete alisisitiza umuhimu wa matumizi sahihi na yenye uwajibikaji ya AI, akibainisha kuwa teknolojia hiyo inaweza kuwa nyenzo muhimu ya kuboresha ubora wa elimu na utafiti iwapo itasimamiwa vyema.

Kwa upande wa Harvard, majadiliano yalihusisha viongozi na wataalamu waandamizi, akiwemo Mkuu wa Harvard Kennedy School, Prof. Jeremy M. Weinstein, pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Maendeleo ya Kimataifa (CID), Dkt. Fatema Sumar.

Aidha, timu ya wataalamu wa AI kutoka Harvard ilishiriki majadiliano hayo, wakiongozwa na Prof. Sharad Goel, akishirikiana na Dkt. Dan Levy na Dkt. Teddy Svoronos—wote wakiwa na uzoefu mkubwa katika matumizi ya AI katika sera za umma na uchambuzi wa data.

Mazungumzo haya yatafuatiwa na ushirikiano wa karibu wa Wahusika katika Vyuo Vikuu hivi viwili. Chuo Kikuu cha Harvard cha Harvard kimeahidi kusaidiakatika kukijengea uwezo Chuo Kikuu cha Dar esSalaam kwenye eneo hili.

Ushirikiano huu unatarajiwa kufungua ukurasa mpya katika sekta ya elimu ya juu nchini, kwa kuunganisha utaalamu wa ndani na uzoefu wa kimataifa katika matumizi ya teknolojia ya kisasa.

 Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam Rais Mstaafu Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na Mkuu wa Harvard Kennedy School, Prof. Jeremy M. Weinstein baada ya mazungumzo yao huko Marekani


TANGA YAZIDI KUFUNGUKA KIUCHUMI, WAWEKEZAJI WAMIMINIKA

May 03, 2026 Add Comment


Na Oscar Assenga, Tanga

Mkoa wa Tanga unaendelea kuandika historia mpya ya kiuchumi kufuatia kuongezeka kwa kasi kwa wawekezaji na kuimarika kwa miundombinu, hatua inayotajwa kuwa kichocheo kikubwa cha ukuaji wa biashara na mapato ya serikali.

Akifungua kikao cha Baraza la Biashara la Mkoa huo, Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Balozi Batilda Burian, alisema lengo la kikao hicho ni kujadili kwa kina namna ya kuboresha mazingira ya biashara ili yawe rafiki na wezeshi zaidi, pamoja na kuibua fursa za uwekezaji na kutafuta suluhisho la changamoto zinazoikabili sekta hiyo.

Alisema serikali inaendelea kuchukua hatua mbalimbali kuboresha mfumo wa kodi, akieleza kuwa tayari Rais aliunda tume maalum iliyopitia kodi mbalimbali na kutoa mapendekezo.

Alibainisha kuwa mkoa unasubiri utekelezaji wa mapendekezo hayo ili kusaidia kuondoa migongano ya kodi, hususan zile za halmashauri zilizokuwa zikilalamikiwa na wafanyabiashara.

Katika hatua nyingine, Balozi Burian alisema Tanga imekuwa kivutio kikubwa cha uwekezaji, huku Jiji la Tanga likiongoza kwa kupokea wawekezaji wengi zaidi.
 

Aliongeza kuwa uwekezaji huo sasa umeanza kusambaa hadi wilaya za Muheza na Korogwe, ambako kunatarajiwa kujengwa kiwanda kikubwa cha sukari pamoja na kuanzishwa kwa bandari kavu.

Akizungumzia mafanikio ya Bandari ya Tanga, alisema kumekuwa na ongezeko kubwa la shehena ya mizigo kutoka tani 470,000 sasa wanapokea zaidi ya tani milioni 1.3, jambo linalochochea ukuaji wa uchumi.

Alifafanua kuwa kwa sasa takriban meli 60 huingia bandarini kila mwezi, ikilinganishwa na meli 18 hapo awali, huku kila meli ikiingiza Bandarini wastani wa shilingi bilioni 2 kwa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA).

“Tunafanya jitihada kuhakikisha ufanisi wa bandari unaongezeka zaidi kwa kupunguza muda wa kuhudumia meli na kuondoa msongamano, ili kuongeza tija kwa sekta binafsi na serikali kwa ujumla,” alisema.

Kuhusu miradi ya kimkakati, Balozi Burian alisema mradi wa bomba la mafuta wa EACOP umefikia hatua za mwisho, huku ukitarajiwa kuanza rasmi kupitisha mafuta kati ya mwezi Juni na Julai.

Alisema mradi huo tayari umetoa fidia ya zaidi ya shilingi bilioni 10 kwa wananchi na kutoa ajira kwa zaidi ya watu 1,700.

Katika sekta ya miundombinu, ujenzi wa barabara ya Tanga–Pangani unaendelea, licha ya changamoto za mvua, huku serikali ikiahidi kuhakikisha shughuli za biashara haziathiriki.

Aidha, uwanja wa ndege wa Tanga unaendelea kuboreshwa kwa gharama ya shilingi bilioni 63, ikiwa ni pamoja na ujenzi wa jengo la abiria, uzio na upanuzi wa njia ya kurukia ndege ili kuruhusu ndege kubwa kutua.

Kwa upande wa viwanda, serikali ya mkoa kwa kushirikiana na Wizara ya Viwanda na Biashara inaendelea kufuatlia viwanda vilivyokuwa vimekufa na kuvifufua viwanda vilivyokufa na kuvutia uwekezaji mpya.

Ikiwemo kutaka Maeneo ya uwekezaji yaliyotengwa kupitia TISEZA sasa yanasimamiwa kwa karibu zaidi na kuwekwa alama ili wawekezaji wanapokwenda waweze kuwekeza na tayari mwekezaji mmoja ameonyesha nia ya kujenga kiwanda cha nondo.

Sekta ya utalii nayo imeelezwa kuwa na fursa kubwa, hususan katika maeneo ya fukwe za Pangani na Mking ambapo alisema kwamba Pangani wana maeneo ya Kipumbwi wanayagawa kwa ajili ya uwekezaji kwenye fukwe na Mkinga katika maeneo ya Kwale na maeneo mengine ya Fukwe .


Aliongeza pia kwamba kuna uwekezaji mkubwa katika soko la Samaki na ni juzi tu Rais alizindua Meli kubwa ya Uvuvi wa Bahari ya Kuu na Meli hiyo itavua mpaka Tanga lakini katika meli nne zitakapotimia nadhani moja itakuja kufanya shughuli zake hapa Tanga .


Akisisitiza wana imani wataanza kutumia rasilimali za bahari kwa ufanisi na itakuwa na mchango mkubwa kutokana na kwamba kuwepo na masoko ya Samaki ikiwemo ,Mkinga,Tanga eneo la Deepsea na soko la Samaki la Kimataifa la Kipumbwi.

Sambamba na hilo, uwekezaji katika uvuvi wa bahari kuu unatarajiwa kuongeza upatikanaji wa samaki na kuimarisha masoko, ikiwemo soko la kimataifa la samaki la Kipumbwi.

Awali, Katibu Tawala wa Mkoa wa Tanga, Rashid Mchatta, alisema Baraza la Biashara ni jukwaa muhimu linaloleta pamoja sekta ya umma na binafsi kwa lengo la kujenga mazingira bora ya biashara, kuimarisha uaminifu na kuhakikisha sekta binafsi inakuwa endelevu.


SERIKALI KUONGEZA UPATIKANAJI WA MAKAZI NAFUU KWA VIJANA NCHINI

May 03, 2026 Add Comment
-Ulega asema ni mkakati endelevu

BARRICK BULYANHULU SPORTS CLUB YATWAA UBINGWA WA BONANZA LA MEI MOSI SHINYANGA

May 03, 2026 Add Comment
Nahodha wa Timu ya Mpira wa Miguu ya Barrick Bulyanhulu Sports Club akipokea zawadi kutoka kwa Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Mboni Mhita, baada ya timu hiyo kutwaa ubingwa wa Bonanza la Mei Mosi.
Nahodha wa Timu ya Mpira wa Miguu ya Barrick Bulyanhulu Sports Club akipokea zawadi kutoka kwa Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Mboni Mhita, baada ya timu hiyo kutwaa ubingwa wa Bonanza la Mei Mosi.
Nahodha wa Timu ya Mpira wa Miguu ya Barrick Bulyanhulu Sports Club akipokea zawadi kutoka kwa Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Mboni Mhita, baada ya timu hiyo kutwaa ubingwa wa Bonanza la Mei Mosi.

MIGODI YA BARRICK YASHINDA TUZO 11 ZA OSHA 2026

May 03, 2026 Add Comment

        

Naibu Katibu Mkuu-Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi,Ajira na Mahusiano, Zuhura Yunus (kushoto) akimkabidhi tuzo ya ushindi wa kwanza katika kipengele cha usambazaji maji na udhibiti wa Maji taka na shughuli za urekebishaji, Afisa Rasilimali Mwandamizi wa Mgodi wa Barrick Bulyanhulu, Renatus Malawa wakati wa hafla ya tuzo za OSHA 2026 zilizofanyika mjini Njombe. Migodi ya Barrick nchini ilishinda tuzo 11.

WIZARA YA MALIASILI NA UTALII MGUU SAWA KUWASILISHA BAJETI YAKE BUNGENI KWA MWAKA WA FEDHA 2026/2027.

May 02, 2026 Add Comment
Waziri wa Maliasili na Utalii, Ashatu Kijaji (Mb), ameongoza kikao kazi cha maandalizi ya bajeti ya Wizara hiyo inayotarajiwa kuwasilishwa katika Bunge la bajeti la mwaka wa fedha 2026/2027 linaloendelea Jijini Dodoma.

WAFANYAKAZI FCC WASHIRIKI MAADHIMISHO YA MEI MOSI JIJINI DAR

May 02, 2026 Add Comment
Wafanyakazi wa Tume ya Ushindani (FCC) wameshiriki kikamilifu katika Maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani (Mei Mosi) yaliyofanyika Leo tarehe 1 Mei, 2026 katika Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.

NPCC YATOA ELIMU YA UDHIBITI WA SUMU KUVU KITETO

May 01, 2026 Add Comment
Mkuu wa Kituo cha Taifa cha Kudhibiti Matukio ya Sumu, Yohana Goshashy, akizungumza wakati akifungua mafunzo ya kudhibiti matukio ya sumu kuvu kwa wananchi wa Kata ya Kibaya wilaya ya Kiteto, Mkoa wa manyara (hawapo pichani), mafunzo hayo yamefanyika katika Ukumbi wa Maktaba, mkoani Manyara, Aprili 29, 2026.

WATAALAMU WA MAZINGIRA WATAJWA KUWA NGUZO MUHIMU KUFANIKISHA DIRA YA TAIFA 2050 NA KUCHOCHEA USHIRIKIANO WA KIKANDA**

May 01, 2026 Add Comment
Na Grace Msungu Dar es Salaam

Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais – Muungano na Mazingira, Mheshimiwa Kwagilwa Reuben Nhamanilo, amesema kuwa kufikiwa kwa malengo ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 kunategemea kwa kiwango kikubwa uwekezaji wa kimkakati katika usimamizi endelevu wa mazingira pamoja na uwezeshaji wa wataalamu wazawa.

WATAALAMU KWENYE MAFUNZO YA KUKABILIANA NA MAAFA WATAKIWA KUYATUMIA KUKABILIANA NA MAAFA.

May 01, 2026 Add Comment






Na Mwandishi wetu- Dodoma

Mkurugenzi wa Idara ya Menejimenti ya Maafa Ofisi ya Waziri Mkuu Brigedia Jenerali Hosea Ndagala amewataka wataalamu ambao wamepatiwa mafunzo ya kukabiliana na maafa kuyatumia vyema katika  kuzuia, kujiandaa na kukabiliana na kurejesha hali baada ya maafa.
Ameyasema hayo jijini Dodoma wakati akifunga mafunzo ya siku nne  ya kujiandaa na kukabiliana na maafa  kwa  Kamati ya wataalamu , Timu ya kukabiliana na maafa na watumishi wa Kituo cha Operesheni na Mawasiliano ya dharura  (REOCC) Mkoa wa Dodoma.

Brigedia Jenerali Ndagala ameeleza kuwa Awamu ya kwanza ya utekelezaji ilianza katika Mkoa wa Mwanza na Arusha, ambapo hatua za kuanzisha Kituo cha Operesheni na Mawasiliano ya Dharura pamoja na kuimarisha Timu ya kukabiliana na Maafa ilianza kutekelezwa Mikoay a Mwanza na Arusha huku akiongeza kuwa mafunzo hayo yataendelea katika Mikoa yote Nchini.

Sambamba na hilo amebainisha kuwa mafunzo hayo ni  nyenzo muhimu katika kujenga na kuimarisha uwezo wa kitaalamu na kiutendaji kwa watumishi wanaohusika na uendeshaji wa kituo cha Operesheni na Mawasiliano ya Dharura.
Pia ameeleza  kuwa Uanzishwaji wa kituo hicho katika Mkoa wa Dodoma ni hatua muhimu  kwani kitawezeshaufuatiliaji  wa matukio kwa ukaribu, ukusanyaji na uchambuzi wa taarifa kwa wakati, pamoja na kuimarisha mawasiliano kati ya wadau mbalimbali ndani na nje ya Mkoa wa Dodoma na Taifa kwa ujumla ili kuokoa maisha ya watu na mali zao.
Aidha Brigedia Jenerali Ndagala amemshukuru Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Bi. Rosemary Senyamule kwa kukubali mafunzo hayo kutolewa katika timu hizo na kuanzisha Kituo  cha Operesheni na Mawasiliano ya Dharura cha Mkoa ambacho kitaunganishwa na Kituo cha Taifa akisema uamuzi huo unaonyesha dhamira thabiti ya uongozi wa Mkoa wa  kuimarisha utayari, mwitikio wa haraka na uratibu madhubuti wakati wa dharura.

DCEA YATEKETEZA EKARI 68 ZA MASHAMBA YA BANGI TABORA

May 01, 2026 Add Comment
Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) kwa kushirikiana na Wakala wa Huduma za Misitu (TFS) pamoja na kamati ya ulinzi na usalama mkoa wa Tabora, imefanya operesheni maalum katika hifadhi ya msitu wa Igombe river iliyopo wilaya ya Uyui na katika hifadhi ya msitu wa Nyahua iliyopo wilaya ya Skonge mkoani Tabora na kufanikiwa kuteketeza ekari 68 za mashamba ya bangi, kukamata gunia 133 za bangi huku watu saba (7) wakikamatwa katika operesheni hiyo.

UTT AMIS YASHIRIKI MEI MOSI, YAHAMASISHA WANANCHI KUWEKEZA MIFUKO YA PAMOJA

May 01, 2026 Add Comment
NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

Mfuko wa uwekezaji nchini, UTT AMIS, umehimiza wananchi kutumia fursa ya kuwekeza katika mifuko mbalimbali ya uwekezaji wa pamoja ili kuongeza thamani ya fedha zao na kupata faida shindani.

DKT.SAMIA ASISITIZA HAKI NA MASLAHI YA WAFANYAKAZI .

May 01, 2026 Add Comment



Na Mwandishi Wetu, Njombe.




Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesisitiza umuhimu wa kulinda haki za wafanyakazi na kuboresha maslahi yao ili kuongeza tija na maendeleo ya taifa.


Akihutubia katika maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani (Mei Mosi) yaliyofanyika kitaifa mkoani Njombe leo Mei Mosi, Rais Samia amesema Serikali itaendelea kuweka mazingira bora ya kazi pamoja na kuhakikisha mishahara na stahiki za wafanyakazi zinazingatia hali halisi ya uchumi.


“Wafanyakazi ni muhimili muhimu wa uchumi wetu. Serikali yangu itaendelea kusimamia maslahi yenu, ikiwa ni pamoja na kuboresha mazingira ya kazi na kuhakikisha haki zenu zinalindwa,” amesema Rais Samia.


Aidha, ameeleza kuwa serikali itaendelea kufanya maboresho katika sekta mbalimbali ikiwemo afya, elimu na miundombinu, hatua ambayo inalenga kurahisisha utendaji kazi na kuongeza ufanisi kwa wafanyakazi.


Katika hotuba yake, Rais Samia amewataka waajiri kuzingatia sheria za kazi, kutoa mikataba halali na kuhakikisha usalama wa wafanyakazi mahali pa kazi unazingatiwa ipasavyo.


Kwa upande wao, viongozi wa vyama vya wafanyakazi walitumia fursa hiyo kuwasilisha changamoto mbalimbali ikiwemo gharama ya maisha, mishahara midogo na ukosefu wa ajira kwa vijana, wakiiomba serikali kuendelea kuchukua hatua za kuboresha hali hiyo.


Maadhimisho ya Mei Mosi mwaka huu yamebeba kaulimbiu isemayo: “Ulinzi wa Haki za Wafanyakazi, Chachu ya Maendeleo ya Taifa,” yakilenga kuhamasisha usawa, haki na ustawi wa wafanyakazi nchini.


Sherehe hizo zilihudhuriwa na viongozi mbalimbali wa serikali, vyama vya wafanyakazi pamoja na wadau wa sekta ya ajira kutoka maeneo mbalimbali nchini.







EWURA YADHIHIRISHA NIDHAMU NA BIDII KATIKA SIKU YA WAFANYAKAZI DUNIANI

EWURA YADHIHIRISHA NIDHAMU NA BIDII KATIKA SIKU YA WAFANYAKAZI DUNIANI

May 01, 2026 Add Comment

Wafanyakazi wa EWURA wakishiriki maandamano ya Mei Mosi mbele ya Rais, Mhe. Samia Suluhu Hassan.

...

Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) leo, Mei 1, 2026, imeungana na wafanyakazi wengine duniani kuadhimisha Siku ya Wafanyakazi Duniani (Mei Mosi), maadhimisho yaliyofanyika kitaifa mkoani Njombe.

Sherehe hizo zilihudhuriwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, ambaye alikuwa mgeni rasmi. Katika hotuba yake, Rais Samia amewahimiza waajiri na waajiriwa kote nchini kuendeleza ushirikiano, kuaminiana, na kutanguliza maslahi ya taifa katika utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku.

Amesisitiza kuwa Serikali itaendelea kuboresha mazingira na ustawi wa wafanyakazi, huku akiwataka kuongeza bidii na ufanisi kazini. Aidha, alibainisha wazi kuwa Serikali inathamini mchango wa wafanyakazi na itaendelea kuwaunga mkono katika juhudi za maendeleo ya nchi.

Katika maadhimisho hayo, EWURA imewakilishwa na wafanyakazi wake bora kutoka idara na vitengo mbalimbali. Wafanyakazi hao walichaguliwa kwa kura za wenzao kwa kuzingatia vigezo muhimu kama vile utendaji uliotukuka, nidhamu ya kazi, ubunifu pamoja na kujituma kazini.

Wawakilishi hao walishiriki katika maandamano rasmi yaliyopita mbele ya mgeni rasmi, wakibeba mabango yenye ujumbe wa kuhamasisha mshikamano na uwajibikaji kazini.

Ushiriki wao umeonesha dhamira ya EWURA kuendelea kutoa huduma bora kwa wananchi na kuchangia maendeleo ya taifa kwa ujumla.

Wafanyakazi wa EWURA wakishiriki maandamano ya Mei Mosi mbele ya Rais, Mhe. Samia Suluhu Hassan.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwapungia mkono wafanyakazi wa EWURA, wakati wa maandamano ya Maadhimisho ya Sherehe za Meimosi leo.