HABARI

SIASA

ELIMU

Recent Posts

MAVUNDE KUANZISHA KIJIJI CHA WANAWAKE DODOMA KUWAKWAMUA KIUCHUMI

MAVUNDE KUANZISHA KIJIJI CHA WANAWAKE DODOMA KUWAKWAMUA KIUCHUMI

January 12, 2026 Add Comment

Waziri wa Madini na Mbunge wa Jimbo la Mtumba, Anthony Mavunde, amesema ana mpango wa kujenga eneo maalumu litakalofanya kazi kama kijiji cha wanawake kwa ajili ya kuwakutanisha wanawake wafanyabiashara katika sehemu moja ili waweze kuuza bidhaa zao kwa pamoja.

Mavunde ametoa kauli hiyo leo Jumatatu, Januari 12, 2025 jijini Dodoma wakati akizungumza na wanawake kwenye hafla ya kukabidhi vitendea kazi kwa wanawake waliohitimu mafunzo ya ufundi stadi kupitia Chuo cha Veta, ikiwa ni sehemu ya juhudi za kuwawezesha wanawake kiuchumi.

Amesema kijiji hicho kitatoa fursa kwa wanawake kufanya biashara katika mazingira rafiki, kubadilishana uzoefu pamoja na kuongeza thamani ya bidhaa zao, hali itakayosaidia kuongeza kipato na kuchangia maendeleo ya familia na taifa kwa ujumla.

“Lengo letu ni kuwawezesha wanawake kiuchumi kwa vitendo, ndiyo maana tunapanga kuwa na eneo maalumu litakalowaunganisha wanawake wote wanaojishughulisha na biashara mbalimbali,” amesema Mavunde.

Aidha, amewataka wanawake wa Jiji la Dodoma kuchangamkia fursa mbalimbali zinazojitokeza ikiwemo mafunzo ya ufundi, mikopo na miradi ya maendeleo ili kujikwamua kiuchumi na kuboresha maisha yao.

Kwa upande wao, wanufaika wa mafunzo hayo wamesema vitendea kazi walivyokabidhiwa vitawawezesha kuanza na kuendeleza shughuli zao za kiuchumi, huku wakimshukuru Mavunde na Serikali kwa kuwapa mafunzo na msaada unaowawezesha kujitegemea.

“Tunashukuru kwa mafunzo na vitendea kazi hivi, sasa tuna uhakika wa kuanza kujipatia kipato na kusaidia familia zetu,” amesema Boke Ramadhan

Naye Sylvia Mpanda amesema kuwa wangetamani eneo watakalojengewa basi liwe la mjini ili wawapate wateja wengi kutoka maeneo mbalimbali kwani wateja wengi wanapatikana maeneo yenye watu wengi

"Sisi tutafanya kazi kwa kikundi hivyo kwenye hichi kijiji atakachoanzisha Mhe Mavunde kitakuwa na wanawake wengi hivyo niwatake wanawake wengine kuacha kulala majumbani na waje kuchangamkia fursa zinazotolewa na serikali yetu." Amesema Sylvia

TANZANIA INA FURSA KUBWA YA KUENDELEZA NISHATI YA JOTOARDHI; WAZIRI NDEJEMBI ALIELEZA BARAZA LA IRENA

TANZANIA INA FURSA KUBWA YA KUENDELEZA NISHATI YA JOTOARDHI; WAZIRI NDEJEMBI ALIELEZA BARAZA LA IRENA

January 12, 2026 Add Comment
 

Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi, amesema kutokana na uwepo wa vyanzo vingi vya nishati ya jotoardhi, Tanzania inayo fursa ya kuviendeleza vyanzo hivyo ili wananchi wapate nishati ya kutosha, nafuu na endelevu ikiwa pia ni sehemu ya kuunga mkono malengo ya dunia ya kuelekea kwenye uzalishaji wa umeme unaotokana na nishati safi.

Akizungumza kwenye Baraza la Kimataifa la Nishati Jadidifu (IRENA) katika Mkutano wa Mwaka wa Muungano wa Kimataifa wa Jotoardhi (Global Geothermal Alliance – GGA), unaofanyika Jijini Abu Dhabi, Falme za Kiarabu, Waziri Ndejembi amesema Serikali imeweka mipango ya uzalishaji wa umeme wa jotoardhi katika Dira ya Maendeleo 2050, Sera ya Taifa ya Nishati ya mwaka 2015, Malengo ya Maendeleo Endelevu ya Dunia (SDGs) na Mkataba wa Nchi kuhusu Masuala ya Mabadiliko ya Tabia Nchi (NDCs).

Amesema Tanzania pia kupitia Kampuni ya Uendelezaji wa Jotoardhi (TGDC) inaendeleza maeneo kadhaa ya kipaumbele ya jotoardhi ikiwemo Ngozi (MW 70), Songwe (MW 5–38), Kiejo-Mbaka (MW 60), Natron (MW 60) na Luhoi (MW 5), huku lengo likiwa ni kuwa na mtambo wa kwanza wa kuzalisha umeme wa megawati 130 ifikapo 2030 ambapo mtambo huo utaanza kwa kuzalisha megawati 30.

Katika Mkutano huo, Waziri Ndejembi amealika wawekezaji nchini akieleza kuwa Tanzania inaendelea kuweka mazingira rafiki ya uwekezaji, kuimarisha mifumo ya kisheria na kanuni ili kutoa uhakika wa uwekezaji, kuboresha michakato ya kupata leseni na vibali pamoja na kuboresha mazingira ya upatikanaji wa data za jotoardhi.

Aidha, ili kuweza kuiendeleza ipasavyo nishati ya jotoardhi Ndejembi amesema bado kunahitajika mikopo ya riba nafuu pamoja na kuwa na ushirikiano na Jumuiya za kimataifa pamoja na Sekta binafsi ili kukabiliana na changamoto ya uendelezaji hasa katika hatua za awali za utafiti ambazo zina gharama kubwa.

Ameongeza kuwa, Tanzania pia inakaribisha mataifa yaliyopiga hatua katika uendelezaji wa jotoardhi kuendeleza Wataalam wazawa katika masuala ya Jotoardhi.

Ndejembi amesema kuwa kutokana na uwepo wa Bonde la Ufa, Tanzania imebarikiwa kuwa na vyanzo vingi vya jotoardhi vinavyoweza kuzalisha megawati 5,000 za umeme. Ametaja kuwa kuna maeneo 52 yenye viashiria vya jotoardhi ndani ya mikoa 16.

Akifungua mkutano huo, Naibu Mkurugenzi Mkuu wa IRENA, Gauri Singh amesema kuwa nishati ya jotoardhi ni muhimu duniani katika kutoa hakikisho la usalama wa nishati lakini ameeleza kuwa bado mchango wake bado ni mdogo duniani katika kuzalisha umeme hivyo vyanzo zaidi vinapaswa kuendelezwa.

Katika mkutano wa IRENA, Waziri Ndejembi ameambatana na Kaimu Balozi wa Tanzania katika Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE), Bakari Ameir, Kamishna Msaidizi anayeshughulikia Nishati Jadidifu, Mhandisi Imani Mruma pamoja na wataalamu wengine kutoka Wizara ya Nishati.

SERIKALI YASEMA KONGANI YA BUZWAGI ITACHOCHEA UKUAJI UCHUMI WA NCHI

January 12, 2026 Add Comment

Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Mipango na Uwekezaji, Dkt. Pius Stephen Chaya akiongea na wadau mbalimbali wa kongani ya Buzwagi wakati wa ziara hiyo
Meneja wa ufungaji mgodi wa Barrick Buzwagi-Mhandisi Zonnastraal Mumbi akiongea wakati wa ziara hiyo.
Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Mipango na Uwekezaji, Dkt. Pius Stephen Chaya (Kushoto) akibadilishana mawazo na Mkuu wa wilaya ya Kahama Frank Nkinda (katikati) na Meneja wa ufungaji mgodi wa Barrick Buzwagi-Mhandisi Zonnastraal Mumbi.
Mkuu wa wilaya ya Kahama,Frank Nkinda akiongea wakati wa ziara hiyo.
Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Mipango na Uwekezaji, Dkt. Pius Stephen Chaya akitembezwa katika maeneo mbalimbali ya Kongani ya Buzwagi.
 ****

#Yaipongeza Barrick kwa kufunga mgodi kwa viwango bora

 Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Mipango na Uwekezaji, Dkt. Pius Stephen Chaya, amesema kuwa Kongani ya Viwanda ya Buzwagi Special Economic Zone inatarajiwa kuwa kichocheo kikubwa cha uchumi wa Mkoa wa Shinyanga na Taifa kwa ujumla, kutokana na mpango wake unaotoa fursa mbalimbali za uwekezaji.

IPTL EMERGES VICTORIOUS IN LONG-RUNNING BATTLE AGAINST STANDARD CHARTERED BANK

January 12, 2026 Add Comment

  

By Staff Writer

Independent Power Tanzania Limited (IPTL) has won an appeal filed by Standard Chartered Bank Hong Kong in the Court of Appeal of Tanzania   which is Civil Appeal No. 386 of 2022. IPTL challenged in the High Court of Tanzania - commercial division in Commercial Application No. 67 and 75 of  2017.

RIPOTI YA BENKI YA DUNIA YATHIBITISHA MAFANIKIO YA MAGEUZI YA TEHAMA SERIKALINI 11:15

January 11, 2026 Add Comment



Na Mwandishi Wetu 


Tanzania imeendelea kung’ara kimataifa baada ya Benki ya Dunia (World Bank - WB) kuitaja kuwa miongoni mwa nchi zilizo na ukomavu wa juu wa matumizi ya TEHAMA katika sekta ya umma, hatua inayothibitisha mafanikio ya mageuzi ya kidijitali yanayoendelea kutekelezwa na Serikali.


Kwa mujibu wa Ripoti ya Ukomavu wa Matumizi ya Teknolojia Duniani katika Utoaji wa Huduma za Serikali na Ushirikishwaji wa Wananchi ‘GovTech Maturity Index - GTMI’ ya Benki ya Dunia mwaka 2025, Tanzania imeorodheshwa katika Kundi A - Ukomavu wa Juu wa matumizi ya TEHAMA (Extensive GovTech Maturity), kundi linalojumuisha nchi zinazoongoza duniani katika matumizi ya teknolojia katika kuboresha utoaji wa huduma za serikali na ushirikishwaji wa wananchi.

Ripoti hiyo hutathmini kiwango cha ukomavu wa TEHAMA serikalini takriban katika nchi zote duniani, kwa kuzingatia maeneo mbalimbali yakiwemo sera, sheria, miongozo, mifumo, na utekelezaji wake ambapo, katika mwaka uliopita ripoti hiyo ilitolewa mwezi Desemba, 2025.


Hii ni mara ya pili kwa Tanzania kutambuliwa na Benki ya Dunia (WB) katika kupiga hatua ya ukomavu wa TEHAMA, ambapo mwaka 2022 Tanzania ilitajwa kuwa miongoni mwa nchi zilizofanya vizuri zaidi duniani katika GovTech Maturity Index. Katika utafiti huo uliohusisha nchi 198, Tanzania ilipanda kutoka nafasi ya 90 mwaka 2021 hadi nafasi ya 26 mwaka 2022 na kutoka kundi B hadi kundi A. Barani Afrika, Tanzania ilishika nafasi ya pili baada ya Mauritius na kuwa kinara wa ukanda wa Afrika Mashariki.

Kuimarika kwa Nafasi ya Tanzania Kimataifa
Mafanikio haya ni mwendelezo wa safari ya Tanzania ya kupanda ngazi katika ukomavu wa TEHAMA serikalini, na kuendelea kujijengea taswira chanya kimataifa na kikanda.

Tanzania imeendelea kuonesha uthabiti katika matumizi ya teknolojia kama nyenzo ya kuboresha ufanisi wa taasisi za umma, kuongeza uwazi na kuimarisha uwajibikaji katika utoaji wa huduma kwa wananchi.

Kwa upande wa bara la Afrika, Tanzania imeendelea kuwa miongoni mwa nchi vinara wa mageuzi ya kidijitali serikalini, ikilinganishwa na mataifa mengine yaliyofanyiwa tathmini katika ripoti hiyo. Tanzania ni moja kati ya nchi tano tu katika bara la Afrika ambazo zimeingia kwenye kundi la juu la ukomavu wa TEHAMA Serikalini, nchi nyingine ni Kenya, Misri, Uganda na Rwanda.

Ripoti ya GovTech Maturity Index (GTMI) 2025 imeangazia maeneo makuu manne ya TEHAMA:
Mifumo ya Mikuu ya Serikali (Core Government Systems)
Huduma Zinazotolewa Mtandaoni (Online Public Service Delivery)
Jukwaa la Ushirikishwaji Wananchi Kidijitali (Digital Citizen Engagement)
Mazingira Wezeshi (GovTech Enablers).

Mifumo ya Mikuu ya Serikali Yachochea Mafanikio
Ripoti ya Benki ya Dunia inaonesha kuwa, mafanikio ya Tanzania yametokana kwa kiasi kikubwa na uwepo na matumizi ya Mifumo ya Mikuu ya Serikali (Core Government Systems).

Mifumo hiyo imejumuisha mifumo ya usimamizi wa rasilimaliwatu kama vile (Mfumo wa Taarifa za Watumishi na Mishahara - ‘Human Capital Information Management System’ - HCIMS’), mifumo ya ajira (Ajira Portal), pamoja na mifumo ya kuunganisha na kubadilishana taarifa kati ya taasisi za umma (interoperability).

Mfumo Mkuu wa Ubadilishanaji Taarifa Serikalini (Government Enterprise Service Bus – GovESB) umetajwa kuwa mhimili muhimu unaowezesha mifumo ya taasisi mbalimbali za umma kusomana na kubadilishana taarifa kwa usalama na ufanisi zaidi. Hatua hii imepunguza urudufu wa taarifa, kuharakisha utoaji wa huduma na kuongeza uwajibikaji.

Ushirikishwaji wa Wananchi Kidijitali

Katika eneo la Ushirikishwaji wa Wananchi Kidijitali (Digital Citizen Engagement), Tanzania imetajwa kuwa miongoni mwa nchi zinazochukua hatua madhubuti katika kujenga mifumo inayowawezesha wananchi kushiriki kikamilifu katika masuala ya utawala.

Mfumo wa e-Mrejesho umekuwa ni nyenzo muhimu inayowaunganisha wananchi na Serikali, kwa kuwezesha utoaji wa maoni, malalamiko, ushauri na pongezi, pamoja na kupata mrejesho kwa wakati. Mfumo huu umechangia kuimarisha uwazi, uwajibikaji na imani ya wananchi kwa Serikali.

Mazingira Wezeshi (GovTech Enablers)

Ripoti hiyo pia inaonesha kuwa Sera, Sheria, Kanuni, Viwango na Miongozo ya Serikali Mtandao (GovTech Enablers) vimekuwa chachu ya mafanikio ya Tanzania katika mageuzi ya kidijitali.

Mazingira haya rafiki yameiwezesha Serikali kuwekeza na kusimamia miradi ya TEHAMA kwa mwelekeo mmoja wa kitaifa.

Utoaji wa Huduma Mtandaoni (Online Public Service Delivery)

Aidha, utoaji wa huduma za serikali kwa njia ya mtandao (Public Service Delivery) kupitia mifumo mbalimbali ikiwemo Mfumo Mkuu wa Malipo Serikalini (GePG), Mfumo wa Kitaifa wa Manunuzi ya Kielektroniki (NeST) na mifumo ya huduma za Serikali za Mitaa (TAUSI), umeongeza upatikanaji wa huduma kwa wananchi kwa ufanisi na kwa gharama nafuu.

Mtazamo wa e-GA

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Serikali Mtandao (e-GA), Mhandisi Benedict Ndomba, amesema kuwa mafanikio hayo ni ushahidi wa mwelekeo sahihi wa taifa katika kujenga Serikali ya kidijitali.

“World Bank imefanya utafiti huu kwa takriban mwaka mmoja huku ikikusanya uthibitisho na taarifa mbalimbali kwenye matumizi ya TEHAMA Serikalini (Evidence-based GovTech Maturity Index Survey) katika nchi mbalimbali duniani”, amefafanua Ndomba.

Amesisitiza kuwa, uwepo wa mifumo mbalimbali ya TEHAMA serikalini unaonesha usimamizi mzuri wa rasilimali za TEHAMA, na kutoa wito kwa taasisi za umma kuendelea kuzingatia Sheria, Kanuni, Viwango na Miongozo ya Serikali Mtandao katika utekelezaji wa miradi ya TEHAMA. Pia amehimiza matumizi ya mifumo ya ushirikishwaji wa wananchi na kuunganisha mifumo ya taasisi na GovESB.

Mafanikio haya yanaifanya Tanzania kuwa kielelezo cha mageuzi ya kidijitali barani Afrika, na kuweka msingi imara wa kuendelea kuboresha utoaji wa huduma za umma, kukuza uwazi na kuimarisha uchumi wa kidijitali kwa maendeleo endelevu ya taifa.



TANZANIA YATAJA MAFANIKIO YAKE YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA KATIKA JUKWAA LA KIMATAIFA LA IRENA -ABU DHABI

January 11, 2026 Add Comment





ABU DHABI, UAE


Imeelezwa kuwa, Tanzania inaendelea kufanya jitihada mbalimbali ili kuhakikisha wananchi wanaendelea kupata nishati safi, salama na nafuu ya kupikia, kwa kuhakikisha fedha za kuwezesha miradi ya nishati safi ya kupikia zinapatikana kutoka Serikalini, Sekta Binafsi, Wadau na Mashirika ya Kimataifa yanayounga mkono jitihada za matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia duniani.

Akizungumza katika Mkutano wa pembeni wa Baraza la Kimataifa Nishati Jadidifu (IRENA), uliohusu suala la upatikanaji wa fedha kwa ajili ya miradi ya Nishati Safi ya Kupikia, Abu Dhabi katika Falme za Kiarabu, Mhandisi Anita Ringia kutoka Wizara ya Nishati, amesema Tanzania imeendeelea kutenga na kutafuta fedha kwa ajili ya utekelezaji wa Ajenda ya Nishati Safi ya Kupikia na matokeo yake yanaonekana kupitia upatikanaji wa nishati safi ya kupikia.

Amesema.upatikanaji wa Nishati Safi ya Kupikia umeongezeka kutoka asilimia 6.9 mwaka 2021 hadi asilimia 23.2 mwaka 2025, ikiwa ni zaidi ya mara tatu ndani ya kipindi cha miaka minne pekee.

Amesema mafanikio hayo yametokana na uongozi thabiti wa Serikali chini ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, ambaye ameifanya nishati safi ya kupikia kuwa kipaumbele cha kitaifa na nguzo muhimu ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.

Katika hatua nyingine, Ringia amesema Tanzania katika mwaka wa fedha 2025/26 inaendelea na miradi mbalimbali ikiwemo usambazaji wa majiko banifu 200,000 yenye ruzuku, kulipia majiko ya umeme 480 kupitia bili ya umeme kwa kushirikiana na TANESCO katika mradi wa majaribio, na kusambaza mitungi zaidi ya 450,000 ya gesi ya LPG kwa bei ya ruzuku.

Ameongeza kuwa Serikali pia imepiga marufuku matumizi ya kuni na mkaa katika taasisi zinazohudumia zaidi ya watu 100 kwa siku, hatua iliyolenga kuhamasisha matumizi ya nishati safi katika zaidi ya taasisi za umma 31,000 uwekezaji unaohitaji zaidi ya bilioni 1 za kimarekani, sambamba na kuimarisha kampeni za uhamasishaji na kusaidia biashara ndogo na za kati katika sekta hiyo.

Mhandisi Ringia amebainisha kuwa mafanikio hayo yameungwa mkono pia Sekta binafsi nchini kupitia ongezeko la uwekezaji wa taasisi za kifedha za ndani, zikiwemo Benki ya NMB na CRDB, ambazo zimeanza kutoa mikopo kwa riba nafuu kwa wajasiriamali wa nishati safi ya kupikia ili kupanua mitandao ya usambazaji nchi nzima.

Katika Mkutano huo, Mhandisi Ringia ametangaza fursa mbalimbali za uwekezaji katika ujenzi wa miundombinu ya kupokea, kuhifadhi na kusambaza nishati safi ya kupikia, ujenzi wa viwanda vya ndani vya kutengeneza majiko, vifaa, na mitungi na uwepo wa fursa bunifu za kuwezesha wananchi kulipia nishati kupitia mifumo ya kulipia kidogo kidogo (PAYGO), kulipia kwa riba nafuu na kulipia kupitia bili za umeme.

Akizungumza kuhusu suala la mchango wa kimataifa katika kuwezesha fedha za kutekeleza Ajenda ya Nishati Safi ya Kupikia, Mhandisi Anita amesema Tanzania inaunga mkono wito wa kuimarisha ushirikiano kati ya Serikali, sekta binafsi, taasisi za kifedha, na washirika wa maendeleo ili kuziba pengo la ufadhili wa nishati safi ya kupikia, hususan barani Afrika ambako karibu watu bilioni moja bado hawana huduma hiyo.

Wataalam wengine wakiongozwa na Kamishna Msaidizi anayeshughulikia Nishati Jadidifu, Imani Mruma walishiriki vikao vya awali vilivyohusu masuala ya utungaji wa sheria, udhibiti, uandaaji wa mipango na uwekezaji wa miradi ya Nishati Jadidifu.

Katika vikao hivyo Tanzania ilieleza kuhusu juhudi inazochukua katika kuhakikisha Nishati Jadidifu inakuwa na mchango wa kutosha katika gridi ya Taifa ili kuendana na maendeleo endelevu ya matumizi ya nishati jadidifu duniani (SDG 7) .

Katika Nishati Jadidifu Tanzania imeeleza kuwa inazidi kupiga hatua ambapo mchango wake unaoingizwa kwenye gridi ya taifa ni asilimia 68 huku juhudi nyingine zikiendelea.ikiwemo ya ujenzi wa mradi wa umeme Jua wa Kishapu wa MW 150 ambao ifikapo Februari mwaka huu utakuwa umeanza kuzalisha umeme kiasi cha MW 50.

Aidha vyanzo vingine vya Nishati Jadidifu vinavyoendelezwa ni pamoja na vyanzo vya Jotoardhi katika ziwa Ngozi (70MW) Songwe (5MW) kiejombaka (60MW), Natron (60MW) na Luhoi (5MW).

Akifungua Mkutano wa IRENA katika siku yake ya kwanza, Naibu Mkurugenzi Mkuu wa IRENA, Gaun Singh amehimiza kila nchi wanachama kuzidi kuwekeza kwenye miradi ya nishati jadidifu ambapo lengo la kidunia ni kuwa na umeme wa GW 11,000 zinazotokana na nishati jadidifu ifikapo 2030.


Mkutano wa IRENA 2026 unaongozwa na kaulimbiu ya “Matumizi ya Nishati Jadidifu kwa manufaa ya pamoja kwa kila binadamu” yaani “Powering Humanity: Renewable Energy for Shared Prosperity”.

     

MRADI WA UMEME JUA KISHAPU UKO MBIONI KUKAMILIKA- MHE SALOME MAKAMBA

MRADI WA UMEME JUA KISHAPU UKO MBIONI KUKAMILIKA- MHE SALOME MAKAMBA

January 10, 2026 Add Comment

Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba, amesema Mradi wa Umeme unaozalishwa kwa nguvu ya Jua uliopo Kishapu, Mkoani Shinyanga, uko mbioni kukamilika ambapo jumla ya megawati 50 zinatarajiwa kuingizwa kwenye Gridi ya Taifa ili kuimarisha upatikanaji wa umeme katika Mkoa wa Shinyanga na mikoa jirani.

Mhe. Salome ameyasema hayo Januari 9, 2026, wakati wa ziara yake ya kukagua miradi ya umeme mkoani Shinyanga, ukiwemo Mradi wa Umeme wa Jua Kishapu, Mradi wa upanuzi wa Kituo cha Kupoza Umeme cha Ibadakuli pamoja na Mradi wa ujenzi wa njia ya kusafirisha umeme kutoka Ibadakuli kwenda Mkoa wa Simiyu.

Amesema kuwa hadi sasa mradi wa Umeme wa Jua Kishapu umefikia zaidi ya asilimia 89 ya utekelezaji wake na unatarajiwa kukamilika mwishoni mwa mwezi huu, ikiwa ni jitihada kubwa zinazofanywa na Serikali za kuhakikisha nchi inakuwa na umeme wa kutosha kwa ajili ya kukuza fursa kiuchumi na maendeleo endelevu.

“Mradi huu umefikia zaidi ya asilimia 89 ya utekelezaji wake, na tunatarajia kwamba ifikapo mwishoni mwa mwezi huu tutaingiza megawati 50 kwenye Gridi ya Taifa. Huu ni muendelezo wa juhudi za Serikali kuhakikisha Tanzania inakuwa na umeme wa kutosha na mtandao imara wa kusafirisha na kusambaza umeme,” alisisitiza Mhe. Salome.

Akizungumza katika Mradi wa Upanuzi wa Kituo cha Kupoza Umeme cha Ibadakuli, ambao umefikia asilimia 44.32 , Naibu Waziri huyo wa Nishati amesema mradi huo una umuhimu mkubwa kwa kuwa utakuwa na uwezo wa kupeleka umeme katika reli ya kisasa ya SGR pamoja na nchi jirani za Kenya na Uganda.

“Tunamshukuru na kumpongeza Mhe. Rais kwa kutoa fedha kwa ajili ya upanuzi wa Kituo cha Kupoza Umeme cha Ibadakuli. Kwetu sisi ni heshima kubwa kwa kuwa kituo hiki kitahudumia mradi mkubwa wa kimkakati wa SGR, sambamba na kupeleka umeme katika nchi jirani za Kenya na Uganda,” alifafanua Naibu Waziri Salome.

Akizungumzia Mradi wa ujenzi wa njia ya kusafirisha umeme wa msongo wa kilovoti 220 kutoka Ibadakuli hadi Simiyu, Kaimu Mkurugenzi wa Miradi TANESCO, Mhandisi Frank Mashalo, amesema lengo la mradi huo ni kuimarisha upatikanaji wa umeme katika Mkoa wa Simiyu na mikoa Jirani ambapo hadi sasa mradi umefikia asilimia 53 na unatarajiwa kukamilika mwezi Juni mwaka huu.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Kishapu, Mhe. Peter Masindi, amesema kukamilika kwa mradi huo kutachochea shughuli za uzalishaji na uchumi kwa wananchi wa Kishapu, wengi wao wanajishughulisha na kilimo cha pamba, ambacho kinahitaji nishati ya umeme kwa ajili ya uzalishaji.

Mradi wa Umeme wa Jua Kishapu unatekelezwa kwa gharama ya shilingi bilioni 323 kwa awamu zote mbili. Mradi huo ulianza rasmi mwezi Desemba 2023 na unatarajiwa kukamilika mwishoni mwa mwezi Januari 2026.
MFUMO WA SIS MWAROBAINI WA UTORO SHULE ZA HANDENI MJI

MFUMO WA SIS MWAROBAINI WA UTORO SHULE ZA HANDENI MJI

January 09, 2026 Add Comment

Na Mwandishi Wetu

Halmashauri ya Mji Handeni imetoa mafunzo maalum ya Mfumo wa Kidigitali wa Taarifa za Shule (School Information System – SIS) kwa Walimu Wakuu wa Shule za Msingi, Wakuu wa Shule za Sekondari pamoja na baadhi ya walimu, huku ikielezwa kuwa mfumo huo utasaidia kuongeza uwajibikaji kwa walimu na kudhibiti tatizo la utoro shuleni.

Akizungumza wakati wa mafunzo hayo yaliyofanyika Januari 9, 2026, mjini Handeni, Kaimu Afisa Elimu Idara ya Sekondari ambaye pia ni Afisa Elimu Vifaa na Takwimu wa Halmashauri ya Mji Handeni, Montan Mathew, amesema mafunzo hayo yamelenga kuwajengea uwezo Walimu Wakuu wa Shule za Msingi, Wakuu wa Shule za Sekondari pamoja na mwalimu mmoja kutoka kila shule ili waweze kutumia mfumo huo kwa ufanisi.

Amesema mfumo wa SIS utatumika kukusanya, kuhifadhi na kuchambua taarifa zote muhimu za shule na kwamba Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEMI imeelekeza mfumo huo kuanza kutumika rasmi mara shule zitakapofunguliwa Januari 13, 2026.

“Walimu hawa wanapaswa kuanza kutumia mfumo huu mara moja ili kuweka taarifa za shule zao. Sisi kama Halmashauri ya Mji Handeni tuna wajibu wa kuhakikisha mfumo unatumika kama ilivyoelekezwa, na tutafanya ufuatiliaji wa mara kwa mara,” amesema Mathew.

Kwa upande wake, Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Mshikamano, Beatrice Chaeka, amesema mfumo huo utasaidia kuwa na takwimu zenye mpangilio mzuri ikilinganishwa na awali walipokuwa wakitumia karatasi ambazo wakati mwingine zilipotea au kuharibika.

Ameongeza kuwa mfumo wa SIS utakuwa suluhisho la changamoto mbalimbali ikiwemo utoro wa wanafunzi na walimu.

“Katika mfumo huu, mwanafunzi anapowekewa alama ya hayupo mara tatu mfululizo, ujumbe hutumwa moja kwa moja kwa mzazi. Hii itawasaidia wazazi kufuatilia mahudhurio na maendeleo ya watoto wao, kwani kuna baadhi ya wanafunzi wanatoka nyumbani lakini hawafiki shuleni,” amesema Chaika.

Naye, Mkuu wa Shule ya Sekondari Kwenjugo, John Rajabu, amesema hapo awali kulikuwa na changamoto katika mipangilio ya taarifa za shule, lakini ujio wa mfumo wa SIS utaboresha usimamizi wa shule kwa ujumla.

Amesema mfumo huo utaongeza uwajibikaji kwa walimu katika ufundishaji pamoja na kuwahusisha wazazi kikamilifu katika kufuatilia maendeleo ya watoto wao kielimu.

DC NYAMWESE AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA SOKO LA CHOGO- HANDENI, ATOA MAAGIZO

DC NYAMWESE AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA SOKO LA CHOGO- HANDENI, ATOA MAAGIZO

January 09, 2026 Add Comment

Na Mwandishi Wetu, Handeni

Mkuu wa Wilaya ya Handeni, Mhe. Salum Nyamwese, ametoa wiki tatu kwa Halmashauri ya Mji Handeni kufanya maboresho mbalimbali katika Soko la Chogo, ikiwamo kurekebisha mageti ya kuingilia sokoni, ili kudhibiti tatizo la wizi wa bidhaa za wafanyabiashara.

Mhe. Nyamwese ametoa agizo hilo Januari 9, 2026, baada ya kufanya ziara ya kushtukiza katika soko hilo na kusikiliza changamoto zinazowakabili wafanyabiashara wanaofanya shughuli zao katika eneo hilo.

Amesema dhamira ya Serikali ni kuhakikisha wafanyabiashara wanafanya shughuli zao katika mazingira safi, salama na rafiki, ili waweze kutoa huduma bora kwa wananchi bila hofu ya usalama wa mali zao.

Aidha, katika ziara hiyo, Mhe. Nyamwese ameelekeza Halmashauri ya Mji Handeni kufanya marekebisho ya haraka ya mageti ya kuingilia sokoni hapo ili kudhibiti wizi wa mara kwa mara wa bidhaa za wafanyabiashara, jambo ambalo limekuwa likisababisha hasara kwao.

“Hali ya usafi katika lile dampo hairidhishi. Mrundikano wa taka uliopo unahatarisha afya za wananchi na wafanyabiashara. Naiagiza Halmashauri kwa kushirikiana na viongozi wa soko kuangalia namna bora ya kuhakikisha taka zinaondolewa kwa haraka pindi zinapokusanywa,” ameagiza.

Naye, Afisa Biashara wa Halmashauri wa Mji Handeni, Paul Lusinde, ameahidi kufanyia kazi maagizo ya Mkuu huyo.