HABARI

SIASA

ELIMU

Recent Posts

MAADHIMISHO YA IEW 2026 YACHOCHEA UWEKEZAJI WA MAFUTA NCHINI TANZANIA

January 30, 2026 Add Comment



Na Mwandishi Wetu


Wadau na wawekezaji mbalimbali wameonesha nia ya kuwekeza katika sekta ya mafuta nchini Tanzania, uwekezaji ambao utachangia ukuaji wa uchumi wa nchi na kuboresha huduma ya bidhaa za nishati kwa wananchi.


Miongoni mwa wawekezaji hao ni Kampuni ya Mafuta ya India (Indian Oil Corporation Limited), yenye uzoefu mkubwa katika usambazaji wa mafuta na gesi, ambayo imeonesha nia ya kuwekeza nchini Tanzania.

Kampuni hiyo imeonesha nia hiyo katika kikao kilichofanyika kati yao na ujumbe wa Tanzania ukiongozwa na Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba pembezoni mwa Maadhimisho ya Wiki ya Nishati ya India 2026 yanayoendelea Jimbo la Goa, nchini India.

Katika kikao hicho, Mkurugenzi wa Mipango na Biashara wa kampuni hiyo, Suman Kumar, amesema Tanzania ni soko la bidhaa nyingi ikiwemo bidhaa za nishati.

Amesema kutokana na ongezeko la mahitaji ya bidhaa kama mafuta, gesi ya mitungi na nishati linalotokana na ukuaji wa uchumi, idadi ya watu inayoongezeka na miji kukua haraka, inatoa fursa kwa kampuni za nishati kushirikiana katika usambazaji, uchakataji na huduma za nishati.

Kwa upande wake Mhe. Salome amesema “Serikali ya Tanzania inawakaribisha wawekezaji wote na ipo wazi kwa uwekezaji wa kimataifa katika sekta ya nishati, ikiwa ni pamoja na usambazaji wa mafuta na gesi ya mitungi kuendana na msukumo wa Serikali wa kukuza matumizi ya nishati safi ya kupikia."

Aidha Mhe. Salome amewahimiza wawekezaji hao kuona umuhimu wa kufungua matawi nchini Tanzania na kushiriki katika ununuzi wa pamoja wa bidhaa za mafuta ili kuongeza ushindani na uhakika wa upatikanaji wa mafuta ya gharama nafuu nchini.


 "Hivyo tunawakaribisha wadau wote kuja kuwekeza nchini Tanzania kupitia makubaliano ya kibiashara na kampuni zetu za ndani kulingana na sera za Tanzania na mapendekezo ya wawekezaji” amesema Mhe. Salome.


Maadhimisho ya Wiki ya Nishati ya India 2026 yanatarajiwa kuhitimishwa Januari 30, 2026 na yamewakutanisha washiriki kutoka nchi zaidi ya 125, yakivutia wawekezaji wengi wa kigeni katika sekta ya nishati. 


Kupitia Maadhimisho hayo yamefungua fursa mbalimbali za uwekezaji katika sekta ya nishati kwa wadau na wawekezaji kutoka sehemu mbalimbali duniani.


&&&









WAKANDARASI WALIOSHINDA ZABUNI YA UTEKELEZAJI MRADI WA KUSAMBAZA UMEME VITONGOJI 527 MKOANI TANGA WATAMBULISHWA RASMI

January 30, 2026 Add Comment


Wakandarasi walioshinda zabuni ya kutekeleza mradi wa kusambaza umeme katika vitongoji 527 mkoani Tanga kupitia Kampuni ya Giza cable industries pamoja na Energy service Limited ka wametambulishwa rasmi mkoani Tanga kwa ajili ya kuanza utekelezaji wa mradi huo

Mradi huo unatekelezwa na Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) wenye thamani ya shilingi bilioni 73.8 ambao utasaidia kwa kiasi kikubwa kuwezesha vitongoji hivyo kuweza kupata nishati hiyo muhimu

Akizungumza wakati wa halfa ya kuwatambulisha wakandarasi hao Mkurugenzi Mkuu wa REA, Mhandisi. Hassan Saidy wakati wa kuwatambulisha Wakandarasi waliuoshinda zabuni ya kutekeleza mradi huo, Kampuni ya Giza cable industries pamoja na Energy service Limited katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa huo.

Alisema wakati wanafanya nao majadiliano kuna maagizo mahususi waliwapa na wangependa kama kiongozi wa mkoa waifahamu ikiwemo kuwaelekeza wawe na timu ya kufanya kazi karibu kila Wilaya.

Aidha aliwataka wakandarasi haoa kujiepusha na vitendo vya kutoa lugha chafu, pamoja na vitendo vya rushwa wakati wanatekeleza miradi hiyo kwa wananchi.

Aliongeza kuwa ukifanya kazi kwenye mradi wa Serikali wanatakiwa kufanya kama mtumishi wa umma hivyo lugha chafu hazikubaliki ikiwemo kurubuni wanakijiji ni kitu ambacho kitapelekea kuvunja mkataba wako.

Kwa upande wake Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Dadi Kolimba aliipongeza serikali kwa utekelezaji wa mradi huo na kusema kuwa utakwenda kufungua zaidi fursa za uchumi vijijini.

“Ukiangalia kwa wakandarasi hawa wawili ambao wametambulishwa leo ambao wanaenda kutekeleza mradi wa kupeleka umeme katika vitongoji 527, jumla ya shilingi Bilioni 73.8.

Hata hivyo alisema kwamba wana kila sababu ya kumshukuru Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwezesha kutoa fedha za kuwezesha kutekelezwa kwa mradi huu.

Kolimba aliwataka wakandarasi hao kuhakikisha wanamaliza mradi huo ndani ya muda uliopangwa.

Alitoa wito kwa wananchi kutoa ushirikiano kwa wakandarasi hao pindi watakapoanza kutekeleza mradi huo ili malengo yaliyowekwa na serikali yaweze kufikiwa.

Mwisho.









REA YAMTAKA MKANDARASI NOTHERN ENGINEERING MTWARA KUONGEZA KASI YA UJENZI WA MRADI

January 30, 2026 Add Comment
Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umemtaka Mkandarasi anayetekeleza Mradi wa Kusambaza umeme katika Vitongoji 150 vya Majimbo 10 Mkoani Mtwara kuongeza kasi ya ujenzi ili kukamilisha Mradi kwa wakati.

BIL. 73.8 KUPELEKA UMEME VITONGOJI 527 MKOA WA TANGA

January 30, 2026 Add Comment







Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) inatekeleza mradi wa shilingi bilioni 73.8 wa kusambaza umeme katika vitongoji 527 mkoani Tanga.

Hayo yamebainishwa leo Januari 29, 2026 Jijini Tanga na Mkurugenzi Mkuu wa REA, Mha. Hassan Saidy wakati wa kuwatambulisha Wakandarasi waliuoshinda zabuni ya kutekeleza mradi huo, Kampuni ya Giza cable industries pamoja na Energy service Limited katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa huo.

“Leo tuko hapa kwako kutambulisha Wakandarasi ambao watakuja kutekeleza mradi mkubwa wa kupeleka umeme katika vitongoji 527 katika Mkoa wa Tanga.

Wakati tunafanya nao majadiliano kuna maagizo mahususi tuliwapa na tungependa kama kiongozi wetu wa Mkoa uyafahamu. Moja tumewaelekeza wawe na timu ya kufanya kazi karibu kila Wilaya,” ameainisha Mhandisi Saidy.

Ameongeza pia, Wakandarasi hao wanatakiwa kujiepusha na vitendo vya kutoa lugha chafu, pamoja na vitendo vya rushwa wakati wanatekeleza miradi hiyo kwa wananchi.

“Ukifanya kazi kwenye mradi wa serikali unatakiwa kufanya kama mtumishi wa umma. Lugha chafu hazikubaliki. Kurubuni wanakijiji ni kitu ambacho kitapelekea kuvunja mkataba wako,” amessisitiza Mhandisi Saidy.

Kwa upande wake Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mhe. Dadi Kolimba ameipongeza serikali kwa utekelezwaji wa mradi huo na kusema kuwa utakwenda kufungua zaidi fursa za uchumi vijijini.

“Ukiangalia kwa wakandarasi hawa wawili ambao wametambulishwa leo ambao wanaenda kutekeleza mradi wa kupeleka umeme katika vitongoji 527, jumla ya shilingi Bilioni 73.8. Tuna kila sababu ya kumshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwezesha kutoa fedha za kuwezesha kutekelezwa kwa mradi huu,” amesema Mhe. Kolimba huku akiwataka Wakandarasi hao kuhakikisha wanamaliza mradi huo ndai ya muda uliopangwa.

Aidha, Mhe. Kolimba ametoa wito kwa wananchi kutoa ushirikiano kwa wakandarasi hao pindi watakapoanza kutekeleza mradi huo ili malengo yaliyowekwa na serikali yaweze kufikiwa.









NLD WAMSIMAMISHA MHAGAMA KUWANIA UBUNGE JIMBO LA PERAMIHO

January 29, 2026 Add Comment


Na Mwandishi Wetu ,RUVUMA.

CHAMA cha National League For Democracy (NLD) kimempitisha Mhagama Hamisi Yusufu kuwania Ubunge Jimbo la Peramiho Mkoani Ruvuma ambayo ataipeperusha Bendera ya chama hicho katika uchaguzi wa mdogo kufuatia Kifo cha aliyekuwa Mbunge wa Jimbo hilo Jenista Mhagama.

Akizungumza na waandishi wa habari mjini hapa,Katibu wa NLD Doyo Hassan Doyo ambapo aliwaambia kwamba siku hiyo ni muhimu kwa wananchi wa Jimbo la Peramiho kufanya maamuzi ya kiongozi wanayemtaka .

Alisema kwamba kiongozi ambaye anaweza kuwaletea maendeleo wananchi wa Jimbo hilo ni mgombea wao kutokana na uongozi uliopita kwa miaka mingi umeshindwa kuwapa maendeleo na mabadiliko katika Jimbo hilo.

Katibu huyo aliwataka wananchi hao kutokufanya makosa katika uchaguzi huo wa marudio kutokana na aliyekuwa Mbunge wa Jimbo hilo kufariki dunia hivyo aliwataka kumchagua mgombea anayetokana na NLD ili aweze kuwapa maendeleo makubwa.

Katika uchaguzi huo Mhagama Hamis Yusuf wa NLD atachuana na wagombea wengine akiwemo Yusuf Rashid Rai wa Chama cha AAFP,Abdallah Boniface Ngonyani wa Chama cha Makini,Hanifa Sembe Mohamed wa Chama cha UMD,Beatrice Omari Muya wa UPDP,Mapunda wa Chama cha DP,Dastan Frolian Pili wa CCK,Morice Thomas Nkongo wa TLP na Mtemi Pachoto wa UDP.


Mwisho.

TANZANIA NA SERBIA ZAJADILI USHIRIKIANO WA AJIRA NA MAENDELEO YA RASILIMALI WATU

TANZANIA NA SERBIA ZAJADILI USHIRIKIANO WA AJIRA NA MAENDELEO YA RASILIMALI WATU

January 29, 2026 Add Comment

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Clement Sangu akizungumza na Waziri wa Kazi, Ajira na Ustawi wa Jamii wa Serbia, Mhe. Milica Djurdjevic, walipo kutana katika kikao cha pembeni (side meeting) kujadili ushirikiano wa masuala ya Kazi na Ajira, Jijini Riyadh, Saudi Arabia.

.....

Tanzania na Jamhuri ya Serbia zimejadili fursa za kuimarisha ushirikiano wa masuala ya kazi, ajira na maendeleo ya rasilimali watu, hususan katika Sekta ya Ujenzi na maeneo mengine muhimu ya kiuchumi.

Hayo yamebainishwa wakati wa kikao cha Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Clement Sangu na Waziri wa Kazi, Ajira na Ustawi wa Jamii wa Serbia, Mhe. Milica Djurdjevic Stamenkovski, walipokutana katika Mkutano wa Mawaziri wa Kazi Duniani (Global Labour Market Conference) uliofanyika Jijini Riyadh, Saudi Arabia.

Akizungumza katika kikao hicho, Waziri Sangu amesema Serikali ya Tanzania imeendelea kufanya mageuzi makubwa yanayolenga kukuza ajira zenye staha, kuongeza ujuzi kwa nguvu kazi na kupanua fursa za ajira kwa wananchi.

Vilevile, Mhe. Sangu alitumia fursa hiyo kueleza wataalamu na uwezo wa wafanyakazi katika nyanja mbalimbali zikiwemo uhandisi, afya, elimu, uhasibu, utawala wa biashara, uchumi, sheria, utalii na ukarimu, kilimo, TEHAMA, biashara ya kilimo na usindikaji wa mazao, anga na usafiri, ufundi mitambo, usafirishaji huduma za majumbani pamoja na fani nyingine nyingi, hivyo amesema Watanzania wanatambulika kwa bidii, unyenyekevu, maadili mema ya kazi na mtazamo chanya kazini.

Kadhalika, Waziri Sangu amemwalika Waziri wa Kazi, Ajira na Ustawi wa Jamii wa Serbia, Mhe. Milica Djurdjevic Stamenkovski kutembelea Tanzania ili kujionea mikakati inayotekelezwa na Serikali katika kuimarisha soko la ajira pamoja na sera za ajira. Pia, amemkaribisha kutembelea vivutio vya utalii nchi ya Tanzania.

Kwa upande wake, Waziri wa Kazi, Ajira na Ustawi wa Jamii wa Serbia, Mhe. Milica Djurdjevic Stamenkovski, amesema nchi ya Serbia ipo katika mchakato wa kufungua ubalozi nchini Tanzania ili kuendelea kukuza ushirikiano kati ya mataifa hayo. Pia alimwalika Waziri Sangu kutembelea nchi ya Serbia ili kujadili kuhusu masuala ya kazi na ajira ikiwemo fursa za ajira zilizopo nchini humo.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Clement Sangu akisalimiana na Waziri wa Kazi, Ajira na Ustawi wa Jamii wa Serbia, Mhe. Milica Djurdjevic, walipo kutana katika kikao cha pembeni (side meeting) kujadili ushirikiano wa masuala ya Kazi na Ajira, Jijini Riyadh, Saudi Arabia.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Clement Sangu akizungumza na Waziri wa Kazi, Ajira na Ustawi wa Jamii wa Serbia, Mhe. Milica Djurdjevic, walipo kutana katika kikao cha pembeni (side meeting) kujadili ushirikiano wa masuala ya Kazi na Ajira, Jijini Riyadh, Saudi Arabia.

Baadhi ya Wajumbe kutoka Tanzania wakifuatilia maelezo ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Clement Sangu alipokutana na kuzungumza na Waziri wa Kazi, Ajira na Ustawi wa Jamii wa Serbia, Mhe. Milica Djurdjevic, katika kikao cha pembeni (side meeting) kujadili ushirikiano wa masuala ya Kazi na Ajira, Jijini Riyadh, Saudi Arabia.

TADB yaadhimisha miaka 10 kwa mafanikio makubwa ya kifedha

January 29, 2026 Add Comment
Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) imeendelea kuimarisha uwezo wake wa kifedha baada ya mali zake kuongezeka na kufikia shilingi trilioni 1.3, hatua inayotokana na mafanikio ya utoaji mikopo katika mnyororo wa thamani wa sekta ya kilimo.
DK.JAFO AIBANA WIZARA YA UJENZI KUTENGA BAJETI YA BARABARA YA LAMI MLANDIZI-MZENGA-BOGA

DK.JAFO AIBANA WIZARA YA UJENZI KUTENGA BAJETI YA BARABARA YA LAMI MLANDIZI-MZENGA-BOGA

January 29, 2026 Add Comment

Mbunge wa Jimbo la  Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo,akiuliza swali la nyongeza leo Januari 29,2026 bungeni jijini Dodoma.

Na.Alex Sonna, Dodoma

Mbunge wa Jimbo la  Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo, amehoji mpango wa Serikali wa kutenga bajeti ya kutosha kwa ajili ya ujenzi wa Barabara ya Mlandizi–Mzenga–Maneromango kwa kiwango cha lami, akisisitiza kuwa ni barabara muhimu kwa shughuli za kiuchumi na kijamii.

Akiuliza swali la nyongeza Bungeni, Dkt. Jafo amesema barabara hiyo yenye urefu wa kilometa 70.2 inaanzia Mlandizi kupitia Mzenga hadi Maneromango, na kwamba tayari upembuzi yakinifu umekamilika.

Ameeleza kuwa kwa sasa mkandarasi ameanza kazi katika kipande cha Mzenga chenye urefu wa mita 300, hali iliyomfanya kuihoji Serikali kuhusu mpango wake wa kuongeza fedha katika bajeti ya mwaka huu ili kufungua kipande cha Mlandizi hadi Mzenga.

“Nini mpango wa Serikali katika bajeti ya mwaka huu kuongeza fedha ili kuhakikisha barabara hii muhimu inaanza kujengwa kuanzia Mlandizi hadi Mzenga?” amehoji Dkt. Jafo.

Akijibu swali hilo, Naibu Waziri wa Ujenzi, Mhandisi Godfrey Kasekenya, amesema Serikali tayari imeonesha nia ya dhati ya kuijenga barabara hiyo, akibainisha kuwa kutokana na ukubwa na umuhimu wake, lazima ijengwe kwa kiwango cha lami.

Ameongeza kuwa Serikali itaendelea kutenga na kuongeza fedha kadri zinavyopatikana, ili kuhakikisha ujenzi wa barabara hiyo unaendelea hadi kukamilika kwa kiwango kilichokusudiwa.

BILIONI 151 RUWASA MWANZA KUNG’ARISHA HUDUMA YA MAJI VIJIJINI

January 29, 2026 Add Comment


Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) mkoa wa Mwanza unaendelea na utekelezaji wa miradi 71 inayoendelea kujengwa katika wilaya mbalimbali ambapo ikikamilika inatarajiwa kupandisha wastani wa huduma ya maji vijijini mkoani humo kutoka wastani wa asilimia 73 ya sasa hadi kufikia asilimia 88 hivyo kuendelea kuimarisha uchumi wa mtu mmoja na jamii kwa ujumla.

Miradi hiyo inatekelezwa kwa gharama ya shilingi bilioni 151 kutoka vyanzo mbalimbali vya fedha ikiwemo Serikali Kuu, Programu ya lipa kwa matokeo (PforR) na Mfuko wa Taifa wa Maji.

Hayo yameelezwa na Meneja wa RUWASA mkoa wa Mwanza Mha. Godfrey Sanga wakati wa ziara ya timu ya Menejimenti ya taasisi hiyo kutoka Makao Makuu inayofanya tathimini ya uendeshaji wa huduma ya maji vijijini inayotolewa na Vyombo vya Utoaji Huduma ya Maji Ngazi ya Jamii (CBWSOs) kote nchini.

Mha. Sanga alisema miradi hiyo ipo katika hatua tofauti za ujenzi ikiwemo mradi wa maji wa Ukiriguru wenye vijiji 19, na Ilujamahate-Buhingo utakaohudumia vijiji 16, na kwamba itakapokamilika itainua huduma kufikia vijiji vingi zaidi mkoani humo na kuendelea kukamilisha dhamira ya serikali ya kumtua mama wa kijijini ndoo kichwani.
Katika siku ya kwanza mkoani Mwanza, timu ya Menejimenti ya ukaguzi na tathimini ya kazi za CBWSO ilitembelea Chombo cha Nyamwaki kilichopo wilayani Magu na Miswaso kilichopo wilaya ya Kwimba ambapo zoezi hilo litaendelea katika wilaya za Misungwi na Segerema.





RC IRINGA ASISITIZA WANANCHI KUWALINDA WAKANDARASI NA VIFAA VYA UJENZI

January 29, 2026 Add Comment


*📌Mradi wa bilioni 32.3 kusambaza umeme kwenye vitongoji 214 vya mkoa wa Iringa*


*📌Mkandarasi M/s Silo Power atakiwa kumaliza kazi kwa wakati*


*📌Wateja 7,500 wataunganishiwa huduma ya umeme*


*📌Asema umeme ni maendeleo, uchumi, huduma na biashara*


📍Iringa


Mkuu wa Mkoa wa Iringa Mhe. Kheri James, amewataka wananchi wa Mkoa huo kutoa ushirikiano kwa Wakandarasi wa miradi ya Wakala wa Nishati Vijijini (REA), ikiwemo kulinda miundombinu na vifaa vya ujenzi ili miradi hiyo ikamilike kwa wakati na iweze kuleta tija na kuchochea maendeleo nchini. 

RC James amebainisha hayo leo Januari 29, 2026 wakati Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) ikimtambulisha rasmi mkandarasi; kampuni ya M/s Silo Power itakayotekeleza Mradi wa Kusambaza Umeme kwenye vitongoji 214 vya mkoa wa Iringa  ambapo mradi huo unatarajiwa kutekelezwa katika kipindi cha miaka mitatu, kuanzia sasa.

Vile vile, RC James amesema mkoa wa Iringa unamahitaji makubwa ya umeme kutokana na kuongezeka kwa viwanda vidogo na vya kati na kwamba hiyo ni fursa kwa Wananchi kukuza uchumi na maendeleo kwa ujumla.


“Namshukuru sana Rais wa Jamhuri ya Muungano wanna Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kutoa kipaumbele kwenye Sekta ya Nishati hususan katika Sekta ya nishati; nikitoa mfano kwenye usambazaji wa umeme kwenye vijiji, Iringa vijiji vyote 360 vilishaunganishwa na huduma ya umeme na sasa tunapokea Mradi wenye thamani ya shilingi bilioni 32.3 na  wananchi zaidi ya 7,500 watanufaika”. Amesema RC James. 

Katika hatua nyingine, RC James amemtaka na kumsisitiza mkandarasi wa mradi huo kuhakikisha anatoa kipaumbele cha ajira kwa wazawa wanaozunguka eneo la mradi ili wananchi hao pia waweze kunufaika na miradi hiyo na kuchochea shughuli za kijamii na kiuchumi mkoani Iringa. 

Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa REA, Bw. Frank Mugogo amesema kuwa vitongoji 1,458 tayari vimefikiwa na huduma ya umeme mkoani Iringa na ambavyo havina umeme ni vitongoji 382. Ameongeza kuwa REA itaendelea kusimamia miradi yote inayotekelezwa nchini kwa weledi ili iweze kukamilika kwa wakati na kuwaomba vingozi wa Serikali ya kijiji na wananchi walioshiriki katika kikao hicho kutoa ushirikiano kwa wakandarasi ili miradi hiyo ikamilike kwa wakati. 

Kwa upande wake,  Mha. Mmbalo Msuya kutoka kampuni ya M/s Silo Power amesema kampuni yao, imejipanga ili kukamilisha Mradi wa kusambaza umeme kwenye vitongoji 214 vya mkoa wa Iringa kwa wakati na kuongeza kuwa maelekezo ya RC James ya kutoa ajira kwa wazawa yatapewa kipaumbele ili wananchi wanaozunguka miradi hiyo waweze kunufaika. 


Mwisho

REA WAMTAMBULISHA MKANDARASI ATAKAYEFIKISHA UMEME VITONGOJI 175 MTWARW

January 29, 2026 Add Comment


Katika kutekeleza kauli mbiu ya “Vitongojini kama Mjini”, Wakala wa Nishati Vijijini (REA) wamefika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mtwara kumtambulisha mkandarasi wa atakaesambaza umeme kwenye vitongoji 175 mkoa wa Mtwara.


Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, Mhe. Kanali Patrick Sawala amewataka REA kumsimamia vema mkandarasi ili aweze kukamilisha kwa wakati huku akiwahakikishia ushirikiano.

“Nahitaji Ofisi ya Mkoa ipatiwe mpango kazi wa mkandarasi ili tuweze kufuatilia mwenendo wa utekezwaji wa mradi. Kwa ile miradi iliyokamilika, REA toeni taarifa ili izinduliwe wananchi waweze kuanza kuitumia. Umeme ni uchumi, unachochea ajira na uwekezaji.” Alieleza Kanali Sawala

Meneja Usimamizi  wa miradi REA, Mha. Deogratius Nagu ameeleza kuwa mradi huo wa kusambaza umeme kwa ngazi ya vitongoji kwa Mkoa wa Mtwara itatekelezwa kwa miaka mitatu kuanzia Januari 2026 mpaka Januari 2029 ukitarajiwa kunufaisha wananchi 5,646

Kwa upande wake Meneja wa kampuni ya Dieynem inayotekeleza mradi huo, Mha. Novatus Lyimo ameishukuru Serikali kwa kuendelea kuwapa kipaumbele wakandarasi wazawa huku akiahidi kutekeleza maradi ndani ya kipindi tarajiwa.



TANZANIA NA OMAN KUIMARISHA USHIRIKIANO MASUALA YA KAZI NA AJIRA

TANZANIA NA OMAN KUIMARISHA USHIRIKIANO MASUALA YA KAZI NA AJIRA

January 28, 2026 Add Comment

Tanzania na Oman zimeendelea kuonyesha dhamira ya kuendelea kuimarisha ushirikiano katika masuala ya kazi na ajira ili kuongeza ajira zenye staha, kulinda haki za wafanyakazi na kukuza uchumi wa mataifa yote mawili.

Hayo yamebainishwa wakati wa kikao cha Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Clement Sangu na Waziri wa Kazi wa Oman, Dkt. Mahad bin Said bin Ali Baawain walipokutana katika Mkutano wa Mawaziri wa Kazi Duniani (Global Labour Market Conference) uliofanyika Jijini Riyadh, Saudi Arabia.

Aidha, katika kikao hicho Waziri Sangu alielezea umuhimu wa kukamilishwa na kutiwa saini kwa Hati ya Makubaliano ya Ushirikiano wa masuala ya Kazi na Ajira (MoU) kati ya nchi hizo mbili, ili kuweka mfumo rasmi na endelevu wa usimamizi wa masuala ya ajira, ulinzi wa haki za wafanyakazi na utatuzi wa changamoto za kiutendaji zinazojitokeza.

Vilevile, Waziri Sangu ameishukuru Serikali ya Oman kwa kuendelea kutoa fursa za ajira kwa Watanzania katika sekta mbalimbali. Pia, amesema idadi ya Watanzania wanaofanya kazi nchini Oman imeendelea kuongezeka , jambo linaloonesha kuimarika kwa mahusiano ya ajira kati ya mataifa hayo mawili.

Kwa upande mwingine, nchi hizo zimekubaliana kuendeleza ushirikiano kwa kuendelea kupanua wigo wa ajira zenye staha, kulinda haki za wafanyakazi na kuimarisha mahusiano ya kiuchumi na kijamii kati ya mataifa yetu mawili.