HABARI MPYA
HABARI
SIASA
ELIMU
Recent Posts
WAZIRI NDEJEMBI ATOA MAELEKEZO MAZITO UTEKELEZAJI MRADI MALAGARASI MW 49.5 KIGOMA
📌Hajaridhishwa na kasi ya utekelezaji wa mkandarasi kwenye mradi
📌Aagiza ukaguzi maalum wa matumizi ya dola milioni 20 za malipo ya awali yaliyotolewa kwa mkandarasi kulinganisha na kazi zilizofanyika
📌Aelekeza kuondolewa mara moja kwa meneja wa mradi upande wa mkandarasi
Waziri wa Nishati, Deogratius Ndejembi amesema hajaridhishwa na mwenendo wa utekelezaji wa Mradi wa Kuzalisha Umeme wa Megawati 49.5 katika maporomoko ya Mto Malagarasi mkoani Kigoma unaotekelezwa na Kampuni ya Dongfang Electric kutokana na kuchelewa kwa kazi pamoja na kutotekeleza masharti ya mkataba waliouingia na Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO).
Mhe. Ndejembi ametoa kauli hiyo Mei 10, 2026 wakati wa ziara ya kukagua maendeleo ya mradi huo ambapo alibaini mkandarasi huyo amekuwa akitoa visingizio badala ya kutekeleza majukumu yake kwa wakati kama mkataba unavyoelekeza.
Akizungumza katika ziara hiyo, amesema Serikali tayari imemlipa mkandarasi zaidi ya dola milioni 20 kama malipo ya awali lakini kiwango cha kazi zilizotekelezwa hakionekani kuendana na fedha zilizotolewa.
Baadhi ya kazi zilizochelewa ni pamoja na ujenzi wa makazi ya wafanyakazi na barabara za mradi, hali ambayo imeonesha kusuasua kwa utekelezaji wa mradi huo wa kimkakati.
Aidha, ameielekeza TANESCO pamoja na mshauri mwelekezi kuendelea kumsimamia kwa karibu mkandarasi huyo huku akisisitiza kuwa Serikali haitatoa nyongeza ya fedha wala kuruhusu mabadiliko ya gharama za mradi huo kwani mkandarasi aliwasilisha gharama zake mwenyewe wakati wa zabuni.
Amesema baadhi ya wakandarasi wamekuwa na tabia ya kuomba kazi kwa gharama ndogo ili kupata zabuni na baadaye kuanza kuomba nyongeza ya fedha, jambo ambalo Serikali haitalivumilia.
Katika hatua nyingine, Mhe. Ndejembi ameagiza meneja wa mradi upande wa mkandarasi kuondolewa mara moja kutokana na kile alichokieleza kuwa ni visingizio vinavyochangia kuchelewesha utekelezaji wa kazi.
Vilevile ameagiza kufanyika kwa ukaguzi maalum wa matumizi ya fedha za malipo ya awali ili kubaini namna fedha hizo zimetumika ukilinganisha na kazi zilizofanyika.
“Mradi huu una umuhimu mkubwa kwa wananchi wa Kigoma, Katavi, Kagera na maeneo ya jirani kwani utaongeza nguvu katika Gridi ya Taifa na kuimarisha upatikanaji wa umeme wa uhakika nchini. Serikali haitakuwa tayari kuvumilia ucheleweshaji unaosababishwa na uzembe wa wakandarasi,” amesema Mhe. Ndejembi.
Ameielekeza TANESCO ndani ya muda wa wiki mbili kukamilisha ukaguzi huo na kuwasilisha taarifa ofisini kwake.
Aidha, amempongeza Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO kwa juhudi za kufanya vikao vya mara kwa mara na mkandarasi huyo pamoja na kuchukua hatua mbalimbali za kutatua changamoto zinazojitokeza katika utekelezaji wa mradi.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa TANESCO Bw, Lazaro Twange amesema TANESCO imepokea maelekezo yote yaliyotolewa na Waziri na itahakikisha yanatekelezwa kwa wakati ili mradi huo ukamilike kama ilivyopangwa.
Mradi wa Malagarasi MW 49.5 unatekelezwa na Kampuni ya Dangfang Electric International Corporation (DEC) kutoka China, ambapo ulianza Aprili 30, 2024 na unatarajiwa kukamilika Oktoba 30, 2027 kwa gharama ya zaidi ya shilingi bilioni 300.
Kukamilika kwake kutaimarisha hali ya upatikanaji wa umeme
Katika mikoa ya Kigoma, Katavi, Kagera na maeneo ya jirani kwani utaongeza nguvu katika Gridi ya Taifa.
KAFULILA: UJUMBE MAALUM SIKU YA MAMA DUNIANI.
habari
WAMILIKI WA VIWANDA VIPYA WATAKUWA KUAJIRI WAZAWA KUKUZA BIASHARA NA UCHUMI
habari
Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Judith Kapinga, amewashauri Wamiliki wa Viwanda vipya Kutoa kipaumbele kwa wazawa katika ajira ili kukuza uchumi na mapato ya Taifa kwa ujumla.
Akizungumza Mei 09, 2026, wakati wa akifungua wa Kiwanda kipya cha kutengeneza tambi za papo hapo (Instant) cha Kura Food mkoani Pwani, amesema kuwa Serikali inaendelea kuboresha mazingira ya Biashara ikiwemo sera, miundombinu, na mifumo ili kuvutia Wawekezaji na wafanyabiashara na kuongeza ushindani wa bidhaa za Tanzania kimataifa.
Aidha, Wizara imefanya mapitio ya sheria na kanuni ili kuhakikisha zinajielekeza katika kuwezesha biashara na kuondoa vikwazo badala ya kudhibiti pekee. Lengo ni kushirikiana na wadau wa mnyororo wa thamani, kutumia teknolojia za kisasa zinazoongeza tija, uzalishaji, na ufanisi wa biashara nchini.
Naye, Mwenyekiti wa Kura Food, Bw. Wu Yeping, ameipongeza Serikali kwa kuweka mazingira rafiki yanayorahisisha uwekezaji,
Huku Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Mhe. Abubakar Kunenge, akibainisha kuanza kwa uboreshaji wa miundombinu ya barabara na Reli ya Kisasa (SGR) kuanzia mwaka ujao ili kufungua zaidi fursa za kibiashara mkoani humo.
Naye Mbunge wa Kisarawe, Mhe. Selemani Jafo, amemshukuru Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa sera zake thabiti ambazo zimekuwa chachu ya kuvutia wawekezaji. Sera hizi zimesaidia kwa kiasi kikubwa kupunguza changamoto ya ukosefu wa ajira kwa wananchi wa jimbo hilo kupitia kuanzishwa kwa viwanda vipya.

COOP BANK YAZINDUA TAWI MTWARA MJINI KUCHOCHEA UCHUMI JUMUISHI
habariKAMATI YA BUNGE YARIDHISHWA NA UWEKEZAJI WA ORYX ENERGIES TANZANIA
habariMILIKI UBUNIFU YATAJWA KUINUA TASNIA YA MICHEZO
habariKONGANI YA VIWANDA VYA DAWA KUPANUA AJIRA NA UWEKEZAJI
habariKITUO CHA UTAMADUNI CHA IRAN CHAZINDUA MASHINDANO YA UCHORAJI TANZANIA.
habariTBS YAKABIDHIWA MAGARI 11 KUFIKIA WADAU KWA WAKATI
habariWAZIRI KAPINGA: SERIKALI KUENDELEA KUWEKA MAZINGIRA BORA YA BIASHARA NA UWEKEZAJI
habariJAJI WA MAHAKAMA KUU SHINYANGA AIPONGEZA PSSSF KWA HUDUMA ZA KIDIGITALI
habari

Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Shinyanga, Mhe. Ntuli Mwakahesya, amepongeza Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) kwa hatua kubwa iliyofikiwa katika matumizi ya mifumo ya kidigitali inayorahisisha utoaji wa huduma kwa wanachama na wastaafu.
TANESCO YAZINDUA RASMI ZOEZI LA ULIPWAJI FIDIA KWA WANANCHI LINDI NA MTWARA
📌 Lengo ni kupisha Mradi wa ujenzi wa njia ya kusafirisha umeme 220kV Masasi, Mahumbika
📌Zaidi ya Shilingi Bil 5.1 zimetengwa kwa ajili ya zoezi hilo
Shirika la umeme Tanzania ( TANESCO) limezindua rasmi zoezi la ulipaji fidia kwa wananchi wanaopisha mradi wa ujenzi wa njia ya kusafirisha umeme ya msongo wa 220kV kutoka Masasi Mkoani Mtwara hadi Mahumbika Mkoani Lindi.
Akizungumza Mei 7, 2026 katika Kata ya Kiwalala, Halmashauri ya Mtama, Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO, Bw. Lazaro Twange amesema Serikali chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imewekeza fedha nyingi kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya umeme ikiwemo njia za kusafirisha umeme zitakazowezesha mikoa ya kusini kuunganishwa kwenye Gridi ya Taifa.
Amesema zaidi ya shilingi bilioni 5.1 zimetengwa kwa ajili ya kuwalipa takribani wananchi 1,730 katika mikoa ya Lindi na Mtwara watakaopisha mradi wa ujenzi wa njia ya kusafirisha umeme ya msongo wa 220kV kutoka Masasi hadi Mahumbika
Bw. Twange, amesema kaya 78 katika vijiji vya Kiwalala na Mahumbika zitanufaika na zaidi ya shilingi milioni 253 katika awamu ya kwanza ya malipo kisha kuendelea katika vijiji vingine.
Naye Mkuu wa Wilaya ya Lindi Mhe. Victoria Mwanziva amesema ulipaji huo wa fidia unalenga kuhakikisha wananchi wote wanaopitiwa na mradi huo wanalipwa stahiki zao ili kurahisisha utekelezaji wa miradi ya maendeleo hivyo amewataka wananchi kutoa ushirikiano kwa TANESCO
‘’Tunamshukuru sana Mhe. Rais kwa kuidhinisha zaidi ya shilingi bilioni 5.1 zitakazotumika kuwalipa fidia zaidi ya wananchi 1,700 katika maeneo ya Lindi na Mtwara lengo kuu ni kuhakikisha mradi wetu huu wa Masasi hadi Mahumbika unafanikiwa,’’alifafanua Mhe Mwanziva.
Zoezi hilo litaendelea katika vijiji vyote 46 vilivyoguswa na mradi huo katika Wilaya za Lindi, Ruangwa, Newala na Masasi.
Zoezi hilo la malipo linaanza kwa vijiji 14 vya Halmashauri ya Mtama.
Utekelezaji wa mradi huo utasaidia upatikanaji wa umeme wa uhakika kwa wananchi wa kusini, ambao kwa sasa wanategemea umeme unaozalishwa kupitia vituo vya gesi asilia vya Mtwara na kusafirishwa umbali mrefu.
![]() |
TANZANIA NA ZAMBIA WAAZIMIA KUONDOA VIKWAZO VYA BIASHARA
habariCHEM CHEM SAFARI & LODGES WAINGIA UBIA NA AUBERGE COLLECTION
habariYaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa BMG Media. Mawasiliano +255 757 432 694 ama ripotabmg@gmail.com

TANZANIA KUSHIRIKIANA NA BARAZA LA UTALII DUNIANI KATIKA MAFUNZO, UWEKEZAJI
habariMSSPAT zaunganisha Kampuni nne kwenye madini
habariMkoa wa Dodoma kusafirisha walimu wake 40 Korea Kusini
habariDC KILWA AIPONGEZA TANESCO KWA KUJIPANGA KUFIKISHA UMEME KATIKA BANDARI YA UVUVI - KILWA
habari
Asema ni Mradi wa kimkakati wenye fursa za kiuchumi kwa maslahi mapana ya nchi
Amtaka Mkandarasi kukamilisha mifumo ya upokeaji umeme kutoka TANESCORAIS DKT. SAMIA AKUTANA NA UJUMBE WA KAMPUNI YA PERSEUS MINING LIMITED NA SOTTA MININING CORPORATION LIMITED, IKULU CHAMWINO, MKOANI DODOMA
habari
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, akiwa kwenye picha na Waziri wa Madini Mhe. Anthony Mavunde, pamoja na Mwenyekiti wa Bodi ya Kampuni ya Perseus Mining Limited Bw. Rick Menell mara baada ya mazungumzo yao, Ikulu ya Chamwino, Dodoma tarehe 06 Mei, 2026.
Perseus Mining Limited ni mwekezaji wa Mgodi wa Dhahabu wa Nyanzaga, Wilayani Sengerema, Mkoani Mwanza kupitia Kampuni ya Sotta Minining Corporation Limited, inayomilikiwa kwa ubia na Serikali ya Tanzania.



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa na Waziri wa Madini Mhe. Anthony Mavunde kwenye picha na Ujumbe wa Kampuni ya Perseus Mining Limited na Sotta Minining Corporation Limited mara baada ya mazungumzo yao, Ikulu ya Chamwino, Dodoma tarehe 6 Mei, 2026.
Perseus Mining Limited ni mwekezaji wa Mgodi wa Dhahabu wa Nyanzaga, Wilayani Sengerema, Mkoani Mwanza kupitia Kampuni ya Sotta Minining Corporation Limited, inayomilikiwa kwa ubia na Serikali ya Tanzania.





























