HABARI MPYA
HABARI
SIASA
ELIMU
Recent Posts
NIT YAJIPANGA KUHUDUMIA MIRADI MIKUBWA YA MAENDELEO
habariWIZARA YA UCHUKUZI YAOMBA BAJETI YA SHILINGI TRILIONI 2.87 KWA MWAKA WA FEDHA 2026/27
habariNa Janeth Raphael MichuziTv -Dodoma
Wizara ya Uchukuzi imewasilisha ombi la kuidhinishiwa bajeti ya jumla ya Shilingi 2,872,738,082,000 kwa mwaka wa fedha 2026/27, ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa mipango ya kuimarisha na kuendeleza sekta ya uchukuzi nchini.
Kwa mujibu wa makadirio hayo, kati ya fedha hizo, Shilingi 126,041,236,000 zimetengwa kwa ajili ya Matumizi ya Kawaida, huku Shilingi 2,746,696,846,000 zikielekezwa katika Miradi ya Maendeleo, ikilenga kuboresha miundombinu ya usafiri wa anga, reli, barabara na huduma nyingine za uchukuzi.
Akizungumza bungeni jijini Dodoma wakati akiwasilisha makadirio ya mapato na matumizi ya wizara hiyo, Waziri wa Uchukuzi, Profesa Makame Mbarawa, amesema kuwa bajeti hiyo imelenga kuharakisha utekelezaji wa miradi ya kimkakati ya sekta ya uchukuzi nchini, sambamba na kuongeza ufanisi wa huduma za usafiri.
Ameeleza kuwa pamoja na hotuba hiyo, wizara imeambatisha majedwali mbalimbali yenye takwimu na taarifa za kina ili kutoa uelewa mpana zaidi kwa Waheshimiwa Wabunge na wananchi kuhusu hali ya utekelezaji wa sekta hiyo.
Aidha, amesema majedwali hayo ni sehemu ya hotuba rasmi ya bajeti na yanapatikana pia kupitia tovuti ya Wizara ya Uchukuzi kwa ajili ya rejea ya umma kupitia www.uchukuzi.go.tz.
Wizara hiyo inaendelea kuweka mkazo katika kuboresha miundombinu ya uchukuzi ili kuchochea ukuaji wa uchumi na kurahisisha usafirishaji wa watu na bidhaa nchini.
NAIBU WAZIRI MMUYA AWASILI ZIMBABWE KUSHIRIKI MKUTANO WA SITA WA MASUALA YA MAAFA
habari.jpeg)
NA MWANDISHIWI WETU – MASVINGO – ZIMBABWE
Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Kaspar Mmuya (Mb), amewasili nchini Zimbabwe kushiriki Mkutano wa Sita (6) wa Kawaida wa Kamati ya Mawaziri Wanaohusika na Usimamizi wa Maafa kwa Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge na Uratibu Mheshimiwa Profesa Palamagamba Kabudi unaofanyika Masvingo, Zimbabwe kuanzia tarehe 11 haadi 14 Mei, 2026.

Mara baada ya kuwasili, Mhe. Mmuya amepokelewa na Balozi wa Tanzania nchini humo, Mhe. Balozi Suzan S. Kaganda na kuipongeza Tanzania kushiriki katika mkutano huo unaolenga kujadili maendeleo yaliyopatikana katika utekelezaji wa programu za kikanda na masuala ya kimkakati katika utekelezaji wa afua mbalimbali katika Usimamizi wa maafa kwa nchi za SADC.
.jpeg)
Masuala mengine yaliyoelezwa na Mheshimiwa Balozi Suzani ni pamoja na Tanzania kuendelea kuzitangaza fursa zilizopo ikiwemo sekta ya utalii, uchukuzi pamoja na kilimo huku akiahidi kuendelea kuimarisha ushirikiano uliopo baina ya Tanzania na Zimbabwe.
.jpeg)
Sambamba na hayo, mkutano huo utahudhuriwa na wadau mbalimbali wa masuala ya Usimamizi wa Maafa kutoka Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) ambapo ni fursa kwa Tanzania kuendelea kujitangaza Kimataifa kwa kuwa na mifumo thabiti ya Usimamizi wa Maafa pamoja na kubadilishana uzoefu kuhusu masuala ya Menejimenti ya maafa.
.jpeg)
Tanzania ni miongoni mwa nchi zilizoshiriki katika Mkutano huo wa siku Nne ambapo umekutanisha wadau wa masuala ya maafa kutoka nchi kumi na sita wakiwemo wataalamu kutoka katika ngazi za Kimataifa pamoja na Mashirika ya Umoja wa Kimataifa.
CHEVRON YAONESHA NIA YA KUWEKEZA TANZANIA KATIKA SEKTA NDOGO YA MAFUTA NA GESI ASILIA
habari
Kampuni kubwa ya nishati kutoka Marekani, Chevron Corporation imeeleza utayari wake wa kuwekeza nchini Tanzania katika shughuli za utafutaji wa mafuta na gesi asilia, hatua inayodhihirisha kuendelea kuimarika kwa mazingira ya uwekezaji katika sekta ya nishati nchini.
Hayo yameelezwa leo, Mei 12, 2026 jijini London, Uingereza, wakati wa kikao kati ya viongozi wa kampuni hiyo na Mamlaka ya Udhibiti Mkondo wa Juu wa Petroli (PURA), pembeni mwa mkutano wa Africa Energies Summit 2026 unaoendelea nchini humo.
Katika kikao hicho, Makamu wa Rais wa Chevron anayesimamia shughuli za utafutaji wa mafuta na gesi asilia, Bwana Kelvin McLachlan, alisema kampuni hiyo inaendelea kutafuta maeneo mapya ya kimkakati ya uwekezaji barani Afrika, huku Tanzania ikionekana kuwa miongoni mwa nchi zenye fursa kubwa kutokana na utulivu wake wa kisiasa, mazingira rafiki ya biashara na uwepo wa rasilimali kubwa za gesi asilia.
Alieleza kuwa Chevron ina uzoefu mkubwa katika shughuli za utafutaji na uzalishaji wa mafuta na gesi asilia katika nchi mbalimbali za Afrika ikiwemo Nigeria, Angola na Equatorial Guinea na kwamba kampuni hiyo ina nia ya kupanua uwekezaji wake katika ukanda wa Afrika Mashariki.Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa PURA, Mhandisi Charles Sangweni, aliieleza Chevron kuwa Tanzania imeendelea kuweka mazingira bora na thabiti ya uwekezaji katika sekta ya nishati hususani sekta ndogo ya mafuta na gesi asilia kupitia mifumo imara ya kisheria, kisera na kiudhibiti inayolenga kulinda maslahi ya wawekezaji pamoja na nchi kwa ujumla.
Mhandisi Sangweni alibainisha kuwa Tanzania ina fursa nyingi za uwekezaji katika vitalu vya utafutaji wa mafuta na gesi asilia vilivyopo nchi kavu na baharini, huku Serikali ikiendelea kuimarisha usimamizi wa sekta hiyo ili kuongeza ushindani na kuvutia uwekezaji wa kimataifa.Aidha, alieleza kuwa maandalizi ya duru nyingine ya kunadi vitalu vya utafutaji wa mafuta yanaendelea, sambamba na jitihada za kuongeza upatikanaji wa data za petroli kupitia tafiti na uchukuaji wa taarifa za kijiolojia na kijiofizikia hatua zitakazosaidia kuongeza uwezekano wa ugunduzi wa mafuta na gesi asilia zaidi nchini.

Alisisitiza pia kuwa uwepo wa miundombinu ya usafirishaji na uchakataji wa gesi asilia, eneo iliyopo Tanzania kijiografia, utulivu wa kisiasa na mazingira bora ya uwekezaji yanaifanya Tanzania kuwa eneo la kimkakati kwa wawekezaji wakubwa kama Chevron.
Mkurugenzi Mkuu huyo wa PURA aliongeza kuwa Tanzania inaendelea kufungua fursa mpya za uwekezaji kupitia utekelezaji wa miradi mikubwa ya kimkakati ikiwemo mradi wa gesi asilia iliyosindikwa kwa ajili ya kuuza nje ya nchi (LNG) ambao unatarajiwa kuongeza thamani ya sekta ya nishati na kuifanya Tanzania kuwa kitovu muhimu cha biashara ya gesi asilia katika ukanda wa Afrika Mashariki na duniani kwa ujumla.
Katika kikao hicho, pande zote mbili zilisisitiza umuhimu wa kuendelea kwa mazungumzo na ushirikiano wa karibu ili kuchochea uwekezaji, maendeleo ya teknolojia na ukuaji endelevu wa shughuli za utafutaji wa mafuta na gesi asilia nchini Tanzania.

DCEA YAKAMATA LITA 66,048 ZA KEMIKALI BASHIRIFU DAR
habariWananchi 2,000 wanufaika na huduma za bure Arusha
habariNIT YATIMIZA AZMA YA SERIKALI YA KUANZA MAFUNZO YA URUBANI
habariCHEVRON YATANGAZA NIA YA KUWEKEZA SEKTA YA MAFUTA NA GESI TANZANIA
habariVIONGOZI WA AFRIKA NA UFARANSA WAJADILI UWEKEZAJI NA MAENDELEO
_▪️Dkt. Mwigulu asisitiza matumizi sahihi ya rasilimali ili kujenga uchumi wa Afrika_
_▪️Rais Macron atangaza uwekezaji wa dola bilioni 27 Barani Afrika_
WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba, leo Mei 11, 2026 ameshiriki katika ufunguzi wa Mkutano wa Ushirikiano kati ya Afrika na Ufaransa (Africa Forward: Africa–France Partnership for Innovation and Growth Summit) unaofanyika jijini Nairobi, Kenya.
Mkutano huo umewakutanisha Wakuu wa Nchi na Serikali, viongozi wa sekta binafsi, wadau wa maendeleo pamoja na wawekezaji kwa lengo la kuimarisha ushirikiano kati ya Afrika na Ufaransa katika sekta mbalimbali ikiwemo biashara, teknolojia, nishati, afya, Akili Unde (AI), kilimo, uchumi wa buluu pamoja na viwanda.
Akizungumza baada ya mkutano huo, Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba amesema mkutano huo umekuwa wa manufaa kwa Bara la Afrika na Ufaransa kwa pamoja kwani majadiliano yamegusa namna ya kuzifanya pande hizo mbili ziweze kunufaika na ushirikiano huo.
Amesema rasilimali zinazopatikana barani Afrika zinatosheleza ikiwa zitatumika vizuri katika kujenga uchumi wa Afrika.
“Lengo kubwa la jitihada hizi ni kupambana na umasikini lakini pia na kutengeneza ajira kwa makundi makubwa ikiwemo la vijana pamoja na wanawake,” amesema.
Aidha, Waziri Mkuu amesema maeneo mengi yaliyojadiliwa ni maeneo ambayo yamepewa umuhimu katika Dira ya Taifa ya Maendeleo ya 2050.
“Nguzo zote zilizoongelewa kwenye dira lakini pia na maeneo ya kipaumbele yameguswa katika mijadala ya leo,” amesema.
Akizungumza katika mkutano huo, Rais wa Jamhuri ya Kenya, Mheshimiwa Dkt. William Samoei Ruto, alizitaka nchi za Afrika kutafakari upya mifumo ya kiuchumi kwa kuimarisha ukusanyaji wa rasilimali za ndani, uwekezaji pamoja na ushirikiano wa kikanda ili kuhakikisha kunakuwa na maendeleo ya muda mrefu.
Aidha, Rais Ruto amesema ni wakati wa Afrika kujiweka kama mdau katika uchumi wa kimataifa badala ya kuwa mnufaika wa misaada ya nje pekee.
“Afrika haiwezi tena kubaki kama mshiriki asiyekuwa na sauti katika mifumo ya kimataifa ambapo baadhi ya maamuzi muhimu hufanywa bila sauti ya usawa,” alisema.
Kwa upande wake, Rais wa Jamhuri ya Ufaransa, Mheshimiwa Emmanuel Macron, alisema Bara la Afrika linapiga hatua kubwa za maendeleo na ni bara ambalo halisubiri majawabu ya changamoto bali linatoa majawabu ya changamoto mbalimbali lilazokabiliana nazo.
Katika hatua nyingine, Rais Macron alitangaza uwekezaji wa thamani ya dola za Marekani bilioni 27 barani Afrika katika sekta za nishati, Akili Unde, uchumi wa bahari pamoja na kilimo.
“Mpango huu utasaidia kutengeneza takriban ajira 250,000 barani Afrika na nchini Ufaransa,” alisema.
Aidha, Rais Macron aliwataka wafanyabiashara wa Afrika kuona fursa zilizopo nchini Ufaransa na kwenda kuwekeza.
“Hatuko hapa tu kuja kuwekeza katika Bara la Afrika pamoja nanyi, tunawahitaji viongozi wakubwa wa biashara wa Afrika kuja kuwekeza nchini Ufaransa,” alisema.
Kwa Upande wake Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres alisema watu wa Bara la Afrika wanapaswa kuwa wa kwanza kunufaika na rasilimali za bara hilo.
“Bara hili limebarikiwa rasilimali nyingi, hapa wenyewe ndio wanapaswa wawe wa kwanza kunufaika,” alisema.
Dkt. Mwigulu amemuwakilisha Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mkutano
FCC, BRELA WATOA MAFUNZO YA MILIKI UBUNIFU KWA MAJAJI WA MAHAKAMA KUU
habariWAZIRI NDEJEMBI,BALOZI WA SWEDEN NA UJERUMANI WAJADILI FURSA ZA USHIRIKIANO SEKTA YA NISHATI
Waziri wa Nishati Mhe. Deogratius Ndejembi leo Mei 12, 2026 amekutana na kufanya mazungumzo na Wawakilishi kutoka Ubalozi wa Sweden, Ujerumani na kampuni ya Siemens Energy kwa lengo la kujadili fursa za uwekezaji na ushirikiano katika sekta ya nishati nchini.
Mazungumzo hayo yalihusisha pia Taasisi ya kifedha ya KfW IPEX ya Ujerumani na EKN ya Sweden ambazo zimekuwa zikishiriki katika kufadhili miradi mbalimbali ya maendeleo ya nishati.
Katika kikao hicho, ujumbe kutoka Siemens Energy uliwasilisha maeneo mbalimbali ambayo wameonesha nia ya kuwekeza ikiwemo uzalishaji wa umeme kwa kutumia gesi asilia, ufadhili na usambazaji wa mitambo ya kuzalisha umeme ambapo ilieleza uzoefu na uwezo wa kampuni hiyo katika teknolojia za mitambo ya kuzalisha umeme.
Katika kikao hicho Waziri Deogratius Ndejembi alieleza kufurahishwa kwake na ujio wa ujumbe huo katika wakati ambao Serikali inaendelea kutekeleza miradi mikubwa ya kimkakati ya nishati nchini.
Aidha, aliipongeza kampuni ya Siemens Energy kwa kupata kandarasi ya kusambaza mitambo ya kuzalisha umeme katika mradi wa kuzalisha umeme kwa kutumia gesi asilia wa Mkuranga wenye uwezo wa kuzalisha megawati 177, akisema hatua hiyo inaonesha imani waliyonayo wawekezaji wa kimataifa kwa Tanzania.
Sambamba na hilo, Mhe. Deogratius Ndejembi alizihimiza kampuni hizo kuangalia fursa za kuwekeza katika vyanzo vingine vya uzalishaji umeme ikiwemo umeme wa jua, upepo na jotoardhi ili kuunga mkono jitihada za Serikali za kufikia lengo la kuzalisha megawati 8,000 ifikapo mwaka 2030.
Nao Wawakilishi wa mabalozi pamoja na kampuni hizo waliishukuru Serikali ya Tanzania kwa kuendelea kuamini teknolojia ya Siemens Energy na ushirikiano wa kifedha kutoka katika nchi zao huku wakiahidi kuendelea kushirikiana na Serikali kuhakikisha upatikanaji wa mitambo na fedha za utekelezaji wa miradi hiyo kwa wakati.
Kikao hicho kilihudhuriwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati anayeshughulikia Mafuta na Gesi Asilia, Dkt. James Mataragio, Kamishna Msaidizi wa Umeme Mha. Styden Rwebangira, Kaimu Kamishna wa Petroli, Mha. Petro Marwa pamoja na wataalam kutoka Wizara ya Nishati.
MDEMU AWATAKA WANAWAKE KUJIKWAMUA KIUCHUMI NA KUDUMISHA MALEZI BORA
habari
Na Saidi Saidi, WMJJWM – Iringa
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Makundi Maalum, Felister Mdemu, amewataka wanawake kushirikiana katika kujikwamua kiuchumi huku wakiendelea kuthamini familia, malezi bora, kuwaheshimu waume zao na kuhakikisha watoto wanapata malezi yenye maadili mema.
Mdemu amesema hayo mkoani Iringa, wakati wa mafunzo ya mwongozo wa uanzishwaji na uwezeshaji wa majukwaa ya wanawake kiuchumi yaliyofanyika katika Kijiji cha Kipaduka, Kata ya Uhambingeto, wilayani Kilolo. Mafunzo hayo yalihusisha madiwani pamoja na viongozi wa majukwaa ya uwezeshaji wanawake kiuchumi kutoka kata mbalimbali za mkoa huo.

Akizungumzia umuhimu wa majukwaa hayo, Mdemu amesema ni maono ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, yenye lengo la kuwainua wanawake kiuchumi kupitia elimu ya fedha, ujasiriamali, matumizi ya teknolojia pamoja na upatikanaji wa mikopo na masoko.
Aidha, amesisitiza umuhimu wa wanawake kupata taarifa sahihi, kuunganishwa katika vikundi na kushiriki kikamilifu katika majukwaa hayo ili wasiachwe nyuma kutokana na ukosefu wa taarifa au usimamizi hafifu. Pia amewataka madiwani kushirikiana na taasisi za fedha, sekta binafsi pamoja na wataalam ili kuongeza fursa za kiuchumi kwa wanawake katika maeneo yao.

Naye Diwani wa Viti Maalum kutoka Tarafa ya Kilolo, Mheshimiwa Julieth Mkolongo, akizungumza kwa niaba ya madiwani na viongozi wa majukwaa hayo, amesema wako tayari kutekeleza maelekezo yaliyotolewa ili kuhakikisha wanawake wanapata fursa za kiuchumi kwa maendeleo ya jamii na Taifa kwa ujumla.

Kwa upande wao, baadhi ya wanawake walioshiriki mafunzo hayo wamesema elimu waliyoipata itawasaidia kuendesha vikundi vyao kwa ufanisi, kuongeza kipato pamoja na kuimarisha ustawi wa familia zao.
RAIS DKT SAMIA AWASILI NCHINI UGANDA KWA AJILI YA KUHUDHURIA SHEREHE ZA UAPISHO WA RAIS MTEULE WA NCHI HIYO YOWERI MUSEVENI
habariRAIS SAMIA AONDOKA NCHINI KUELEKEA UGANDA KUHUDHURIA SHEREHE ZA UAPISHO WA RAIS MUSEVENI
habariGPE, EP4R WARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA ELIMU BUSWELU
habari
Ujumbe wa wadau wa maendeleo ya elimu ukiwemo Global Partnership for Education (GPE) pamoja na Education Program for Results (EP4R) ukiongozwa na Morten Sigsgaard Mratibu wa Ushirika wa Nchi (GPE) umeridhishwa na utekelezaji wa miradi mbalimbali ya elimu inayotekelezwa katika Shule ya Msingi na Sekondari Buswelu, Manispaa ya Ilemela mkoani Mwanza.

Akizungumza wakati wa ziara ya ukaguzi wa miradi hiyo Mei 11, 2026, Morten amesema miradi hiyo imeendelea kuboresha mazingira ya kufundishia na kujifunzia, hususan kwa wanafunzi wa elimu jumuishi.
Katika Shule ya Msingi Buswelu, inayohudumia wanafunzi 1,211 wakiwemo 176 wenye mahitaji maalumu, imefanikiwa kujenga bweni la wasichana wenye mahitaji maalumu kupitia ufadhili wa Serikali na GPE-LANES II.
Mradi huo9 umewezesha wanafunzi 80 kupata makazi salama ya bweni, huku huduma za bweni zikianza rasmi Mei 8, 2026 baada ya Serikali kuanza kutoa fedha za chakula.
Aidha, walimu na wanafunzi wameeleza mabadiliko chanya yaliyotokana na miradi hiyo, wakisema awali wanafunzi walikuwa wakisoma katika mazingira ya msongamano wa madarasa, lakini sasa wanapata nafasi ya kusoma katika mazingira bora na yenye nafasi ya kutosha, jambo lililoongeza umakini na ushiriki darasani.
Katika Shule ya Sekondari Buswelu, kupitia Programu ya EP4R, shule imepokea Shilingi milioni 50 kwa ajili ya ujenzi wa vyumba viwili vya madarasa vyenye viti na meza 100, mradi ambao tayari umekamilika na unatumika.
Baadhi ya wanafunzi wa shule hiyo wanasema awali walikuwa wakisoma wakiwa wamebanana kutokana na upungufu wa madarasa, hali iliyokuwa ikichangia usumbufu wakati wa masomo, lakini kwa sasa wanafurahia kusoma katika madarasa mapya yenye nafasi kubwa na mazingira rafiki ya kujifunzia.
Uongozi wa shule ulieleza kuwa miradi hiyo imechangia kuboresha ufaulu pamoja na kuongeza hamasa ya kujifunza.
Wadua wa maendeleo walitoa pongezi kwa Serikali kwa kuendelea kuwekeza katika sekta ya elimu na kuahidi kuendelea kushirikiana katika kuboresha mazingira ya kujifunzia nchini.


































.jpeg)


