HABARI

SIASA

ELIMU

Recent Posts

DC KILWA AIPONGEZA TANESCO KWA KUJIPANGA KUFIKISHA UMEME KATIKA BANDARI YA UVUVI - KILWA

May 07, 2026 Add Comment





📌Asema ni Mradi wa kimkakati wenye fursa za kiuchumi kwa maslahi mapana ya nchi

📌Amtaka Mkandarasi kukamilisha mifumo ya upokeaji umeme kutoka TANESCO

 Mkuu wa Wilaya ya Kilwa, Mhe. Mohamed Nyundo, ameipongeza TANESCO kwa jitihada na utayari wake wa kuhakikisha umeme unafika katika mradi wa ujenzi wa Bandari ya Uvuvi, inayotarajiwa kuwa na mchango mkubwa katika fursa za kiuchumi.

Mhe. Nyundo ameyasema hayo Mei 6, 2026, baada ya ziara ya Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO, Bw. Lazaro Twange, katika mradi huo wa ujenzi wa Bandari ya Uvuvi Kilwa, kwa lengo la kuangalia kama miundombinu ya upokeaji wa umeme imekamilika.
Amesema, licha ya TANESCO kuwa na utayari wa kupeleka umeme katika bandari hiyo, bado mkandarasi hajakamilisha mifumo ya kupokea umeme kutoka TANESCO.

“Nikupongeze sana MD kwa kufika na timu yako ya wataalamu. Mmejionea mahitaji ambayo TANESCO mnapaswa kutoa, na tumeona mkandarasi bado hajakamilisha baadhi ya mifumo katika eneo lake ili kupokea huduma ya umeme kutoka kwenu,” alisema Mhe. Nyundo.
Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO, Bw. Lazaro Twange, amesema TANESCO ina umeme wa kutosha, na tayari kumejengwa njia ya kusafirisha umeme wa msongo wa kilvoti 33 kutoka Somanga ili kupeleka umeme katika bandari hiyo ya uvuvi.
Aidha, ameeleza jitihada zinazoendelea kufanyika za upanuzi wa kituo cha kupokea na kupoza umeme cha Singino, Kilwa, kwa kuongeza transfoma yenye uwezo wa MVA 5 ili kuimarisha hali ya upatikanaji wa umeme katika maeneo hayo.
“Kimsingi, TANESCO tuna umeme wa kutosha kwa ajili ya bandari. Tunafahamu kwamba bandari hii ikiwa inafanya kazi itahitaji takribani megawati 2.5 za umeme. Tutawapa umeme moja kwa moja kutoka katika kituo chetu cha kufua umeme cha Somanga,” alifafanua Bw. Twange.
Ziara ya Mkurugenzi Twange imelenga kukagua miradi ya umeme inayoendelea katika mikoa ya Pwani, Lindi na M Mtwara


RAIS DKT. SAMIA AKUTANA NA UJUMBE WA KAMPUNI YA PERSEUS MINING LIMITED NA SOTTA MININING CORPORATION LIMITED, IKULU CHAMWINO, MKOANI DODOMA

May 06, 2026 Add Comment



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, akiwa kwenye picha na Waziri wa Madini Mhe. Anthony Mavunde, pamoja na Mwenyekiti wa Bodi ya Kampuni ya Perseus Mining Limited Bw. Rick Menell mara baada ya mazungumzo yao, Ikulu ya Chamwino, Dodoma tarehe 06 Mei, 2026.


Perseus Mining Limited ni mwekezaji wa Mgodi wa Dhahabu wa Nyanzaga, Wilayani Sengerema, Mkoani Mwanza kupitia Kampuni ya Sotta Minining Corporation Limited, inayomilikiwa kwa ubia na Serikali ya Tanzania.






Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa na Waziri wa Madini Mhe. Anthony Mavunde kwenye picha na Ujumbe wa Kampuni ya Perseus Mining Limited na Sotta Minining Corporation Limited mara baada ya mazungumzo yao, Ikulu ya Chamwino, Dodoma tarehe 6 Mei, 2026.

Perseus Mining Limited ni mwekezaji wa Mgodi wa Dhahabu wa Nyanzaga, Wilayani Sengerema, Mkoani Mwanza kupitia Kampuni ya Sotta Minining Corporation Limited, inayomilikiwa kwa ubia na Serikali ya Tanzania.



RIDHIWANI AWASHA MOTO AAPAM, AIPA HONGERA TEMESA KWA BOSI MPYA

May 06, 2026 Add Comment




Meneja Masoko na Uhusiano kwa Umma TEMESA Bi Martha Joachim akimkabidhi zawadi Waziri
wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (Mb)

Waziri wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (Mb), leo tarehe 6 Mei, 2026 amefungua rasmi Mkutano Mkuu wa Pili wa Mwaka wa Jumuiya ya Wataalamu wa Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu katika Utumishi wa Umma (AAPAM), unaowakutanisha wadau mbalimbali wa sekta hiyo.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mkutano huo uliofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Arusha (AICC), Waziri Ridhiwani alisisitiza umuhimu wa wataalamu wa Rasilimali watu katika kuimarisha utendaji na ufanisi wa taasisi za umma ambapo alibainisha kuwa mchango wao ni muhimu katika kufanikisha utoaji wa huduma bora ili kuendana na kasi ya mabadiliko ya kiutawala na kiteknolojia.

Aidha, alieleza kuwa Serikali inaendelea kuweka mazingira rafiki kwa wataalamu hao ili waweze kutekeleza majukumu yao kwa weledi.


Katika ziara yake katika mabanda ya maonesho yanayoambatana na mkutano huo, Mhe. Ridhiwani alitembelea banda la Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA), ambapo alipata fursa ya kujionea shughuli mbalimbali zinazotekelezwa na taasisi hiyo pamoja na maboresho ya huduma zake.

Akiwa katika banda hilo, aliipongeza TEMESA kwa kumpata Mtendaji Mkuu mpya, nakusema hatua hiyo imeashiria fursa ya kuimarisha zaidi uongozi, kuongeza ubunifu na kuleta matokeo chanya katika utoaji wa huduma kwa umma.


“TEMESA kwanza nawapongeza kwa kupata mtendaji mpya naamini mabadiliko haya yataleta chachu ya kiutendaji na utoaji wa huduma bora hongereni sana.” Amesema Mhe. Ridhiwani.


Mkutano huo wa siku nne umebeba kaulimbiu isemayo: “Kufikiri upya utoaji wa huduma kwa umma: Jinsi Serikali inavyoweza kutumia teknolojia kuanzisha huduma bora na zinazomlenga mwananchi, kukabiliana na ukosefu wa ajira kwa vijana pamoja na changamoto za mazingira.”

TRA KARIAKOO YATEMBELEA KIJIWE CHA RAHA SQUARE NA KUSIKILIZA CHANGAMOTO ZA WALIPAKODI

May 06, 2026 Add Comment
Wafanyabiashara Wa Kijiwe cha Raha Square Wamepata Fursa Ya Kukutana Na Kaimu Meneja Wa Kariakoo Bw.Edson Issanya, ambapo waliwasilisha changamoto mbalimbali wanazokutana nazo katika utekelezaji wa majukumu yao ya kikodi, ikiwemo uelewa mdogo wa masuala ya kodi.

LALJI FOUNDATION YAWAINUA WAJANE KIGOMA KUPITIA UFUGAJI NYUKI

May 06, 2026 Add Comment
Uongozi wa Taasisi ya LALJI FOUNDATION ukiwa katika picha ya pamoja na wanachama wa Chama cha Wanawake Wajane Tanzania (CCWWT) mkoani Kigoma mara baada ya kukabidhi mizinga 50 ya nyuki, ikiwa ni sehemu ya jitihada za kuwawezesha wajane kiuchumi kupitia ufugaji nyuki.

WAKENYA WAASWA KUACHA KUWADHARAU WATANZANIA NA WATANZANIA KUACHA KUWAOGOPA WAKENYA

May 06, 2026 Add Comment

 


Mfanyabiashara nguli na Mwenyekiti wa Taifa Group , Rostam Azizi akizungumza kwenye mkutano wa Biashara kati ya Kenya na Tanzania uliyofanyika jijini Dar es Salaam.


***

Mkutano wa siku moja wa biashara kati ya Tanzania na Kenya uliofanyika Jumatatu wiki hii jijini Dar es Salaam ulikuwa na mambo mengi na mikakati ya kuimarisha umoja baina ya wananchi wa nchi hizi mbili.

MABILIONI YA CSR KUTOKA BARRICK BULYANHULU KUTEKELEZA MIRADI YA KIJAMII HALMASHAURI YA MSALALA 2026

May 06, 2026 Add Comment

         


Meneja Mahusiano ya Jamii wa Mgodi wa Barrick Bulyanhulu, Bw. Agapith Paul wa pili kushoto akibadilishana hati ya mkataba na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Msalala , Bw. Mibako Mabubu na wa kwanza kushoto ni Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Msalala, Nico Kayange.
Meneja Mahusiano ya Jamii wa Mgodi wa Barrick Bulyanhulu, Bw. Agapith Paul wa pili kushoto akibadilishana hati ya mkataba na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Msalala , Bw. Mibako Mabubu na wa kwanza kushoto ni Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Msalala, Nico Kayange.
Meneja Mahusiano ya Jamii wa Mgodi wa Barrick Bulyanhulu, Bw.  Agapith Paul akisaini mkataba wa makubaliano ya kutekeleza miradi ya maendeleo kupitia sheria , kanuni za Uwajibikaji kwa Jamii (CSR) kwa ajili ya miradi ya maendeleo ya Halmashauri ya Wilaya ya Msalala.

Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Msalala, Nico Kayange akiweka saini kwenye makubaliano hayo , katikati ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Msalala , Bw. Mibako Mabubu akishuhudia.
Afisa Mahusiano ya Jamii Mwandamizi wa Mgodi wa Barrick Bulyanhulu , Zuwena Senkondo akitia saini kwenye mkataba huo.
Afisa Mahusiano ya Jamii Mwandamizi wa Mgodi wa Barrick Bulyanhulu , Zuwena Senkondo akizungumza kwenye halfa hiyo.

***
Uwekezaji wa kampuni ya Barrick nchini yenye ubia na Serikali kupitia kampuni ya Twiga unazidi kuleta manufaa ambapo mwaka huu mgodi wa Barrick Bulyanhulu umetoa kiasi cha shilingi bilioni 1.8 za uwajibikaji kwa jamii kwa Halmashauri ya wilaya ya Msalala kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mbalimbali 26 ya maendeleo kwa wananchi.

HISA STAHIKI MCB ZAFUNGUA FURSA MPYA ZA UWEKEZAJI NA MIKOPO

May 06, 2026 Add Comment
NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

Hatua ya Benki ya Biashara ya Mwalimu (MCB) kuuza hisa stahiki imeelezwa kuwa chachu ya kuimarisha mtaji na kupanua wigo wa utoaji wa mikopo nafuu kwa walimu pamoja na wafanyabiashara wadogo nchini.

RAIS DKT. WILLIAM RUTO AIPONGEZA NSSF TANZANIA KWA UWEKEZAJI WA DOLA ZAIDI YA MILIONI 51 NAIROBI

May 06, 2026 Add Comment


Rais wa Kenya, Mhe. Dkt. William Ruto, ameusifu uwekezaji wa Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) wa Tanzania unaoendelea jijini Nairobi, akisema ni mfano bora wa matumizi sahihi ya akiba za wanachama katika kukuza uchumi na maendeleo ya kikanda.

Akizungumza Mei 5, 2026 wakati akihutubia Bunge jijini Dodoma, Mhe. Dkt. Ruto alimpongeza Mkurugenzi Mkuu wa NSSF Tanzania, Bw. Masha Mshomba, kwa usimamizi thabiti wa uwekezaji huo, akibainisha kuwa unaonesha namna bora ya kugeuza akiba za wanachama kuwa miradi yenye tija.

Alisema mradi huo uliopo eneo la Upper Hill, jijini Nairobi, unahusisha ujenzi wa majengo pacha yenye ghorofa 22, unaogharimu takribani dola za Marekani zaidi ya Milioni 51. Mradi huo unatekelezwa kwa kutumia akiba za wanachama wa NSSF Tanzania na unatarajiwa kukamilika ndani ya kipindi cha miaka miwili.

Mhe. Dkt. Ruto alieleza kuwa uwekezaji huo ni somo muhimu kwa Kenya na mataifa mengine ya Afrika Mashariki kuhusu umuhimu wa kukuza utamaduni wa akiba na uwekezaji kwa maendeleo ya muda mrefu.

“Uwekezaji ni zao la akiba. Huwezi kuwekeza kama huna akiba,” alisisitiza Dkt. Ruto, akihimiza wananchi na taasisi kuzingatia nidhamu ya kuchangia katika mifuko ya hifadhi ya jamii kwa mustakabali wa baadaye.

Aidha, alibainisha kuwa nchini Kenya wamefanya maboresho ya mfumo wa hifadhi ya jamii mwaka 2023 baada ya kujifunza kutoka mifumo bora ikiwemo ya Tanzania.

Alieleza kuwa mfumo huo unahitaji mwajiri na mwajiriwa kuchangia kwa pamoja hadi asilimia 20 ya mapato ili kuimarisha usalama wa kifedha kwa wafanyakazi wanapostaafu.

Mhe. Dkt. Ruto alisisitiza kuwa utamaduni wa kujiwekea akiba unapaswa kuendelezwa ndani ya jamii, akieleza kuwa hatua hiyo ni muhimu katika kujenga mifumo imara ya hifadhi ya jamii.

Rais Dkt. Ruto pia alisifu mafanikio ya Tanzania katika sekta ya hifadhi ya jamii, akieleza kuwa Kenya inaendelea kujifunza na kuchukua mifano bora kutoka kwa majirani zake.

Katika kuimarisha ushirikiano wa kikanda, alisema anajivunia uhusiano mzuri uliopo kati ya Kenya na Tanzania chini ya uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, akibainisha kuwa huu ni wakati muhimu katika historia ya mataifa hayo mawili.

Akihitimisha, Dkt. Ruto amesema kuwa kwa sasa kuna hatua kubwa ya kihistoria katika uhusiano wa Kenya na Tanzania, akieleza furaha yake kwa ushirikiano wa karibu kati yake na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Amesema viongozi hao wanafanya kazi kwa pamoja kuwaleta karibu wananchi wa Afrika Mashariki na kuondoa changamoto zilizodumaza maendeleo kwa muda mrefu.

Kauli hiyo inaakisi mwelekeo wa mataifa ya Afrika Mashariki katika kutumia rasilimali zao za ndani kama kichocheo cha ukuaji wa uchumi na ustawi wa wananchi.

Rais Dkt. William Ruto anahitimisha ziara rasmi ya siku mbili nchini Tanzania, iliyoanza Mei 4 hadi 5, 2026.
















CRDB BENKI YATOA BILIONI 2.7 KUWASAIDIA ELIMU NA UWEZESHWAJI WANANCHI KIUCHUMI

May 06, 2026 Add Comment

Na Oscar Assenga,LUSHOTO

Benki ya CRDB imeendelea kudhihirisha dhamira yake ya kuchangia maendeleo ya jamii kwa kutoa zaidi ya shilingi bilioni 2.7 katika mwaka uliopita, fedha ambazo zimeelekezwa kwa kiasi kikubwa katika sekta ya elimu na uwezeshaji wa wananchi kiuchumi.

Akizungumza katika hafla ya kukabidhi vyumba viwili vya madarasa pamoja na ofisi ya walimu katika Shule ya Msingi Kwendoghohi, iliyopo Kata ya Usambara wilayani Lushoto, Mjumbe wa Bodi ya Wakurugenzi Taasisi ya CRDB Bank Foundation, Marian Balampama, alisema kati ya fedha hizo, shilingi bilioni 1 zimetumika kuboresha elimu.

Alieleza kuwa uwekezaji huo umejumuisha ujenzi wa madarasa, ununuzi wa madawati, pamoja na upatikanaji wa vifaa vya kufundishia na kujifunzia, ikiwemo maabara. Alisisitiza kuwa benki hiyo haijikita tu katika miundombinu, bali pia inahakikisha mwanafunzi anapata mazingira salama na bora ya kujifunzia.

Mbali na elimu, CRDB pia imewekeza katika kuwawezesha wananchi kiuchumi kupitia programu mbalimbali. Balampana alisema benki hiyo inaamini kuwa kumwezesha mtu mmoja ni sawa na kuinua familia na jamii kwa ujumla.

Kupitia kampuni tanzu ya CRDB Bank Foundation na programu ya Embeju, zaidi ya wanufaika 500,000 pamoja na vikundi mbalimbali wamenufaika. Alifafanua kuwa uwezeshaji huo hauishii kwenye utoaji wa fedha pekee, bali pia unahusisha mafunzo ya ujuzi na mbinu za kutambua masoko ili kuongeza tija na faida.

Aidha, alibainisha kuwa benki hiyo imekuwa ikiangalia pia changamoto nyingine za kijamii, ikiwemo upatikanaji wa huduma za afya, kwa lengo la kuboresha ustawi wa wananchi kwa ujumla.

“Sisi tunajisikia fahari kushirikiana na Serikali, hususan katika kusimamia mikopo ya asilimia 10 katika baadhi ya mikoa, ili kuhakikisha fedha zinawafikia walengwa na kuleta matokeo chanya,” alisema Balampana.

Aliongeza kuwa CRDB inaendelea kushirikiana kwa karibu na viongozi wa Wilaya ya Lushoto pamoja na Mkoa wa Tanga katika kutekeleza miradi ya maendeleo.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Lushoto, Zephania Sumaye, aliishukuru benki hiyo kwa mchango huo, akisema ujenzi wa madarasa hayo utasaidia kupunguza msongamano wa wanafunzi na kuboresha mazingira ya kujifunzia.

Alieleza kuwa shule hiyo, iliyoanzishwa mwaka 1965, ilikuwa na miundombinu iliyochakaa, hivyo msaada huo unaleta matumaini mapya katika kuinua ubora wa elimu katika eneo hilo.

Kwa ujumla, hatua ya CRDB inaonesha namna taasisi za kifedha zinavyoweza kuwa chachu ya maendeleo kwa kurejesha kwa jamii sehemu ya mapato yao, sambamba na kuunga mkono juhudi za Serikali kufikia dira ya maendeleo ya Taifa ya mwaka 2050.








STARTUPS ZAASWA KUONGEZA UBORA WA BIDHAA ILI KUCHOCHEA UCHUMI WA TAIFA

May 06, 2026 Add Comment
Dar es Salaam, Mei 5, 2026

Kampuni changa (startups) nchini waaswa kuongeza juhudi katika kukuza ubunifu na kuugeuza kuwa bidhaa ama huduma zenye ushindani, hatua iliyotajwa kuwa mhimili muhimu wa kukuza uchumi wa taifa na kuimarisha ajira kwa vijana.

Mzumbe yaandaa Siku ya Mzumbe na Kambi ya Wajasiriamali kwa mara ya kumi

May 05, 2026 Add Comment
Chuo Kikuu Mzumbe kupitia Shule yake ya Biashara kimeandaa tukio la Siku ya Mzumbe na Kambi ya Wajasiriamali, litakalofanyika kwa mara ya kumi mfululizo katika Kampasi Kuu Morogoro, kuanzia Mei 6 hadi 8, 2026.

UNESCO NA NACTVET WAZINDUA KOZI MTANDAO YA ELIMU YA STADI ZA MAISHA NA AFYA YA UZAZI KWA WANAFUNZI TVET

May 05, 2026 Add Comment
Tanzania imepiga hatua muhimu katika kuboresha afya na ustawi wa vijana kwa uzinduzi rasmiwa Kozi Mtandao ya Elimu ya Stadi za Maisha na Afya ya Uzazi (CSE) chini ya mradi wa“Maisha yetu, Haki Zetu, Mustakabali wetu”- (O3 Plus). 

SANLAM ALLIANZ YAFADHILI MRADI WA PAZA SAUTI+ KUIMARISHA MAPAMBANO DHIDI YA UKATILI WA KIJINSIA NA WATOTO

May 05, 2026 Add Comment

Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa ya Kahama, Stephen Magalla, akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo kwa watoa huduma za afya yaliyoandaliwa kupitia Mradi wa Paza Sauti+, kwa lengo la kuimarisha mapambano dhidi ya ukatili wa kijinsia (GBV) na ukatili dhidi ya watoto (VAC) katika Halmashauri ya Manispaa ya Kahama, mkoani Shinyanga. Picha na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Afisa Sheria kutoka Ofisi ya Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali (GCLA), Mohamed Mdemu, akizungumza wakati wa mafunzo kwa watoa huduma za afya yaliyoandaliwa kupitia Mradi wa Paza Sauti+, yenye lengo la kuimarisha mapambano dhidi ya ukatili wa kijinsia (GBV) na ukatili dhidi ya watoto (VAC) katika Halmashauri ya Manispaa ya Kahama, mkoani Shinyanga.
Mkuu wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (OC-CID) Kahama, SP Maro Kenyunko, akizungumza wakati wa mafunzo kwa watoa huduma za afya yaliyoandaliwa kupitia Mradi wa Paza Sauti+, yenye lengo la kuimarisha mapambano dhidi ya ukatili wa kijinsia (GBV) na ukatili dhidi ya watoto (VAC) katika Halmashauri ya  Manispaa ya Kahama, mkoani Shinyanga.

**
Na Mwandishi Wetu, Kahama

Kampuni ya bima ya Sanlam Allianz imefadhili Mradi wa Paza Sauti+, unaotekelezwa na Shirika la Tanzania Health Promotion Support (THPS) kwa kushirikiana na Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali (GCLA), ukiwa na lengo la kuimarisha mapambano dhidi ya ukatili wa kijinsia (GBV) na ukatili dhidi ya watoto (VAC) katika Halmashauri ya Manispaa ya Kahama, mkoani Shinyanga.