HABARI

SIASA

ELIMU

Recent Posts

WMA YATOA MSAADA WA VIFAA VYA UJENZI KWA WAHITAJI DODOMA

March 30, 2026 Add Comment

Katika kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia, Wakala wa Vipimo (WMA) imetoa misaada ya vifaa vya ujenzi wa jiko la kisasa katika Kituo cha kulelea watoto wenye mahitaji maalumu Cha RAHMAN ORPHANAGE CENTER kilichopo Chang'ombe jijini Dodoma.

Akizungumza baada ya kutoa misaada hiyo Meneja wa WMA Mkoa wa Dodoma Said Ibrahimu amesema suala la mazingira safi ya kupikia ni haki ya kila mmoja ndio maana wameamua kama Wakala kutoa misaada hiyo itakayowezesha upishi wa kisasa katika mazingira safi na salama ikiwemo usalama wa chakula kwani kituo hicho wamekuwa wakipika kwa kutumia kuni na mazingira ya Nje ambayo sio salama kwa afya ya watoto hao.

"tunamuunga mkono Rais wetu Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuhakikisha nishati safi ya kupikia inakuwa katika mazingira safi na salama ndio maana leo kwa niaba ya wafanyakazi wa WMA tumekabidhi Sementi, Marumaru na vifaa vingine vitakavyosaidia ujenzi wa jiko hilo, "amesema Meneja Said

Kadhalika, Mkurugenzi wa kituo hicho Bi. Rukia Abdallah ameishukuru WMA kwa misaada hiyo itakayokwenda kuboresha mazingira ya mapishi katika Kituo hicho chenye idadi ya watoto 120 huku akiomba wadau wengine kujitokeza kuchangia kituo hicho ikiwemo suala la usafiri ili watoto hao waweze kutembelea maeneo mbalimbali kwa ajili ya kujifunza zaidi.

Mmoja wa watoto wanaolelewa katika Kituo hicho Hazra Ramadhan ameipongeza Wakala wa Vipimo kwa kuona umuhimu wa kuwasaidia na kuwaomba kuendelea kuwakumbuka kila mara ili waweze kutimiza malengo yao.







PPP YAONYESHA NJIA KUFIKIA MALENGO YA UMEME MEGAWATI 70,000 IFIKAPO 2050

March 30, 2026 Add Comment
NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

SEKTA binafsi imeelezwa kuwa nguzo muhimu katika kufanikisha malengo ya Mpango wa Nne wa Maendeleo (FYDP IV), huku Serikali ikisisitiza umuhimu wa kuongeza ushiriki wake katika uwekezaji wa nishati ili kufikia uzalishaji wa megawati 70,000 ifikapo mwaka 2050.

MISA YA KUOMBEA NA KUAGA MWILI WA MAREHEMU MHE.LUKUVI -IRINGA

March 30, 2026 Add Comment

Misa Takatifu ya kuuaga Mwili wa aliyekuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu), na Mbunge wa Jimbo la Isimani, Marehemu Mhe. William Lukuvi, iliyofanyika katika Kanisa Kuu la Moyo Mtakatifu wa Yesu lililopo Kihesa Iringa leo tarehe 30 Machi, 2026 nakuongozwa na Askofu wa Jimbo la iringa Romanus Mihali.


Misa hiyo imehudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Serikali, Viongozi wa Vyama vya Siasa, Viongozi wa dini pamoja na Waombolezaji kutoka maeneo mbalimbali ya mkoa wa Iringa na nje ya mkoa huo.

















Mhe. Lukuvi amefariki dunia tarehe 25 Machi, 2026 katika Hospitali ya Benjamin Mkapa Mkoani Dodoma alipokuwa akipatiwa matibabu.

TUME YA MADINI YATOA UFAFANUZI KUHUSU AJALI KWENYE MGODI WA MSASA - GEITA

March 30, 2026 Add Comment
Ajali imetokea katika Mgodi wa Dhahabu wa Msasa uliopo Runzewe, Wilaya ya Bukombe mkoani Geita, baada ya sehemu ya eneo la uchimbaji kuporomoka na kufunika madarura manne yenye namba K 46A, 47A, 48A na 49A.

Kwa mujibu wa Ofisi ya Afisa Madini Mkazi – Mbogwe, madarura hayo yalikuwa yamefungwa tangu Machi 27, 2026 kwa ajili ya ukarabati, hata hivyo baadhi ya watu waliingia katika eneo hilo bila kufuata taratibu.

UKiKAMATWA UMEFICHA MAFUTA NI KESI YA UHUJUMU UCHUMI

March 30, 2026 Add Comment

 



📌 EWURA kuendesha operesheni maalum kubaini wanaoficha mafuta.


Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati anayeshughulikia Mafuta na Gesi, Dkt. James Mataragio, ameiagiza Mamlaka ya Udhibiti wa Nishati na Huduma za Maji (EWURA) kuendesha operesheni ya kuwabaini watu wanaojihusisha na vitendo vya kuficha mafuta kwa makusudi ili kusababisha uhaba katika maeneo mbalimbali.


Ameeleza kuwa baadhi ya wafanyabiashara wasio waaminifu wanatumia mwanya wa hali iliyopo kwa kuchukua mafuta kutoka kwenye maghala (depots) kwa kiwango kikubwa kuliko mahitaji yao, kisha kuyahifadhi wakisubiri bei mpya zitangazwe ndipo wayauze kwa bei ya juu.



Amesisitiza kuwa vitendo hivyo ni kosa la uhujumu uchumi, na yeyote atakayebainika atachukuliwa hatua za kisheria. Hivyo, amewaonya wafanyabiashara wanaojihusisha na vitendo hivyo kuacha mara moja kwa kuwa vinachangia kuleta uhaba wa mafuta.


“Nimewaelekeza Ewura kuanzia leo, usimwonee mtu yoyote aibu kama mtu akikamatwa ameficha mafuta, kwakweli sisi hatutamvumilia na Kamshna msimamie hilo mafuta yanayopakiwa hapa Dar es salaam muhakikishe yanafika kwenye vituo kama inavyokuwa imepangwa” amesisitiza Matarajio.


Dkt. Mataragio amefafanua kuwa tayari wameanza kupokea taarifa za baadhi ya vituo kukosa mafuta, hali inayochangiwa na vitendo vya aina hiyo ambapo mafuta yanapochukuliwa Dar es Salaam hayafiki katika vituo kama inavyotakiwa.


Kwa upande wake, Kamishna wa Mafuta na Gesi kutoka Wizara ya Nishati, Bw. Goodluck Shirima, amesema Serikali inaendelea kufuatilia kwa karibu mwenendo wa usafirishaji na uuzaji wa mafuta nchini, ili kuhakikisha mafuta yote yanayopakiwa kutoka kwenye matenki yanafika katika vituo husika na wananchi wanaendelea kupata huduma bila usumbufu wowote.

RAIS MSTAAFU DKT JAKAYA KIKWETE NA RAIS WA MALAWI PROFESQ ARTHUR MUTHARIKA WATETA

March 29, 2026 Add Comment

 


Rais Mstaafu Mhe. Dkt. Jakaya Kikwete, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Jopo la Wazee la Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) (Panel of Elders, POE) akiwa katika picha ya pamoja na Profesa Arthur Peter Mutharika, Rais wa Malawi, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Asasi ya Siasa, Ulinzi na Usalama ya  Jumuiya ya SADC, baada ya kufanya naye mazungumzo jana Ijumaa jijini Lilongwe, Malawi. 

Pamoja nao ni Mama Joyce Banda, Rais Mstaafu wa Malawi, ambaye ni Mjumbe wa Jopo hilo la Wazee. Katika mazungumzo yao, pamoja na mambo mengine, Viongozi hao walipata fursa ya kumweleza Rais Mutharika kuhusu kazi zilizofanywa na zinazoeandelea kufanywa na POE katika kusuluhisha migogoro katika nchi za Ufalme wa Lesotho, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Malawi na kwa sasa Madagascar. 

Kimuundo, POE ni moja ya vyombo vya kuzuia migogoro na kurejesha amani katika nchi za SADC ambacho kinaripoti moja kwa moja kwenye Asasi ya SADC Troika, ambayo nchi ya Malawi ndiyo Mwenyekiti wake kwa sasa.



SERIKALI YAONGEZA NGUVU KATIKA MIKAKATI YA KUHAKIKISHA UPATIKANAJI ENDELEVU WA MAFUTA NCHINI

March 28, 2026 Add Comment

Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratias Ndejembi amekutana na kufanya mazungumzo na Wakuu wa Taasisi zilizo chini ya Wizara ya Nishati  zinashughuliki mafuta na gesi nchini katika Ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es salaam.


Kikao hicho kilichofanyika leo, tarehe 28 Machi 2026, ni sehemu ya juhudi za Serikali kuendelea kuweka mikakati madhubuti ya kuhakikisha usalama na upatikanaji wa mafuta.

Uhaba wa mafuta unaoshuhudiwa unatokana na changamoto za usambazaji katika soko la kimataifa, zilizochochewa na vita inayoendelea katika ukanda wa Mashariki ya Kati. 

Hali hiyo imeathiri njia muhimu za usafirishaji wa mafuta, ikiwemo kupungua kwa upitishaji wa shehena kupitia Mlango wa Bahari wa Hormuz, jambo lililosababisha kucheleweshwa kwa usafirishaji na hatimaye kupungua kwa upatikanaji wa mafuta katika baadhi ya maeneo.

Kikao hicho kimehudhuriwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati anayeshughulikia Mafuta na Gesi, Dkt. James Mataragio, Kamishna wa Mafuta na Gesi, Bw. Goodluck Shirima, Mkurugenzi Mkuu wa EWURA, Dkt. James Mwainyekule, Mkurugenzi Mtendaji wa TPDC Bw. Musa Makame, Mtendaji Mkuu wa PBPA Bw. Erasto Simon na wataalamu kutoka Wizara ya Nishati kwa lengo la kupokea taarifa ya hali ya upatikanaji wa mafuta nchini.

TANZANIA YANG’ARA KIMATAIFA KWA USIMAMIZI BORA WA DENI LA SERIKALI

March 28, 2026 Add Comment

  Na Joseph Mahumi, WF


Serikali ya Tanzania imeendelea kung’ara katika jukwaa la kimataifa baada ya kuibuka mshindi wa jumla wa mwaka katika Tuzo za Usimamizi wa Deni la Umma za Jumuiya ya Madola na tuzo ya Ofisi Bora Kanda ya Afrika kupitia Idara ya Usimamizi wa Deni la Serikali, Wizara ya Fedha (Debt Management Division), ambazo zilitangazwa tarehe 26 Machi 2026 wakati wa Mkutano wa Jukwaa la Jumuiya ya Madola kuhusu Usimamizi wa Deni la Umma, uliofanyika jijini London, nchini Uingereza.

Ushindi huo mkubwa unatokana na juhudi za Serikali katika kuimarisha mifumo ya usimamizi wa deni la umma, ikiwemo kuunganisha vyema mifumo ya kifedha ya Serikali na kuboresha upatikanaji wa rasilimali fedha kwa ajili ya maendeleo, ambapo Jopo huru la wataalamu lililochambua mawasilisho kutoka nchi mbalimbali za Jumuiya ya Madola lilizingatia vigezo vya ubunifu, uimara na uendelevu katika kutoa tuzo hizo.

Akifungua hafla ya utoaji tuzo hizo, Naibu Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Madola, Bw. Tanmaya Lal, alisisitiza umuhimu wa nchi wanachama kuendelea kubuni mbinu madhubuti za kusimamia deni la umma ili kulinda uchumi dhidi ya misukosuko ya kifedha duniani.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu Mwandamizi wa Idara ya Uchumi, Maendeleo, Biashara na Uwekezaji wa Sekretarieti ya Jumuiya ya Madola, Bi. Ruth Kattumuri, aliipongeza Tanzania kwa mageuzi makubwa iliyoyafanya katika kuimarisha usimamizi wa deni la umma.

Alieleza kuwa mafanikio hayo ni kielelezo cha dhamira ya dhati ya nchi katika kujenga uchumi imara na unaostahimili mishtuko ya kiuchumi.

Aidha, Bi. Kattumuri, alisema kuwa Sekretarieti ya Jumuiya ya Madola itaendelea kuisaidia Tanzania katika juhudi zake za kuboresha sera na mifumo ya usimamizi wa deni, sambamba na utekelezaji wa maazimio ya Kikao cha 72 cha Kundi la Mawaziri wa Jumuiya ya Madola.

Mkutano huo wa Jukwaa la Jumuiya ya Madola uliofanyika kwa muda wa wiki moja uliwakutanisha wataalamu wa usimamizi wa deni kutoka nchi wanachama wa Jumuiya ya Madola kwa lengo la kubadilishana uzoefu, kujifunza na kujadili mbinu bora za kukopa, kusimamia na kulipa deni la umma, na umeandaliwa ikiwa ni sehemu ya Maadhimisho ya Mwaka wa Jumuiya ya Madola wa Deni Imara, Bunifu na Endelevu, ambapo Tanzania imejitokeza kama kinara na mfano wa kuigwa barani Afrika na katika Jumuiya nzima ya Madola.
Kamishna Msaidizi Idara ya Usimamizi wa Deni la Serikali, Wizara ya Fedha, Bw. Omary Khama (Katikati) akiwa ameshika tuzo mbili ambazo Tanzania imepata kwa kuibuka Mshindi wa jumla wa mwaka katika Tuzo za Usimamizi wa Deni la Umma za Jumuiya ya Madola na Tuzo ya Ofisi bora Kanda ya Afrika kupitia Idara ya Usimamizi wa Deni la Serikali, Wizara ya Fedha (Debt Management Division), ambazo zilitangazwa tarehe 26 Machi 2026 wakati wa Mkutano wa Jukwaa la Jumuiya ya Madola kuhusu Usimamizi wa Deni la Umma, uliofanyika jijini London, nchini Uingereza. Wengine katika picha ni Naibu Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Madola, Bw. Tanmaya Lal (kushoto) na  Mkurugenzi Mkuu Mwandamizi wa Idara ya Uchumi, Maendeleo, Biashara na Uwekezaji wa Sekretarieti ya Jumuiya hiyo, Bi. Ruth Kattumuri.
Kamishna Msaidizi Idara ya Usimamizi wa Deni la Serikali, Wizara ya Fedha, Bw. Omary Khama, akionesha tuzo mbili ambazo Tanzania imepata kwa kuibuka Mshindi wa jumla wa mwaka katika Tuzo za Usimamizi wa Deni la Umma za Jumuiya ya Madola na Tuzo ya Ofisi bora Kanda ya Afrika kupitia Idara ya Usimamizi wa Deni la Serikali, Wizara ya Fedha (Debt Management Division), ambazo zilitangazwa tarehe 26 Machi 2026 wakati wa Mkutano wa Jukwaa la Jumuiya ya Madola kuhusu Usimamizi wa Deni la Umma, uliofanyika jijini London, nchini Uingereza.
Kamishna Msaidizi Idara ya Usimamizi wa Deni la Serikali, Wizara ya Fedha, Bw. Omary Khama (Katikati) Aakiwa ameshika tuzo mbili ambazo Tanzania imepata kwa kuibuka Mshindi wa jumla wa mwaka katika Tuzo za Usimamizi wa Deni la Umma za Jumuiya ya Madola na Tuzo ya Ofisi Bora Kanda ya Afrika kupitia Idara ya Usimamizi wa Deni la Serikali, Wizara ya Fedha (Debt Management Division), ambazo zilitangazwa tarehe 26 Machi 2026 wakati wa Mkutano wa Jukwaa la Jumuiya ya Madola kuhusu Usimamizi wa Deni la Umma, uliofanyika jijini London, nchini Uingereza. Wengine katika picha ni washindi wenngine wa tuzo hizo kutoka nchi ya Barbados ambayo iliibuka mshindi wa Msimamizi bora wa deni katika ukanda wa nchi za Caribbean na Sri Lanka Msimamizi bora wa deni katika ukanda wa nchi za Asia.

FCC, TBS wakutana na wadau wa Pombe kutatua changamoto bidhaa hafifu na bandia

March 28, 2026 Add Comment
NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

SHIRIKA la Viwango Tanzania (TBS) kwa kushirikiana na Tume ya Ushindani (FCC) wamekutana na wadau wa bidhaa za pombe nchini kwa lengo la kuwajengea uelewa juu ya matakwa ya sheria, kanuni na viwango vinavyosimamia sekta hiyo.

WAZIRI WA NISHATI AKABIDHI VITENDEA KAZI KWA TANESCO MKOA WA SHINYANGA

March 28, 2026 Add Comment



Na Mwandishi Wetu, Kahama


Naibu Waziri wa Nishati Mh. Salome Makamba amekabidhi vitendea kazi vya usafiri kwa TANESCO Mkoa wa Shinyanga kwa lengo la kuimarisha utoaji wa huduma kwa wananchi na kutatua changamoto zao kwa haraka.

Akizungumza tarehe 27, Machi 2026 wakati wa hafla ya kukakabidhi vitendea kazi hivyo iliyofanyika katika Manispaa ya Kahama Mkaoni Shinyaga Mhe. Salome amesema hatua hiyo ya kukabidhi vitendea kazi hivyo ni kuyaishi maono ya Mhe Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuhakikisha wananchi wanapata huduma za Umeme wa uhakika.

WAZIRI NDEJEMBI NA WAZIRI CHIKOTE WA ZAMBIA WAJADILI USHIRIKIANO SEKTA YA NISHATI

March 27, 2026 Add Comment


Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi, amekutana na kufanya mazungumzo na Waziri wa Nishati wa Zambia, Mhe. Makozo Chikote, leo tarehe 27 Machi 2026 katika Jiji la Lusaka, Zambia.

Katika kikao hicho kilichowashirikisha wataalam kutoka nchi hizo mbili, Viongozi hao wamejadili masuala mbalimbali yaliyolenga kuimarisha na kuendeleza ushirikiano katika sekta ya nishati, hususan sekta ndogo ya mafuta na gesi.

Kikao hicho kimehudhuriwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati anayeshughulikia Mafuta na Gesi, Dkt. James Mataragio, Balozi wa Tanzania nchini Zambia, Luteni Jeneral Mathew Edward Mkingule pamoja na wataalam kutoka Wizara ya Nishati na taasisi zilizo chini yake.

Tanzania na Zambia zimekuwa na historia ya ushirikiano wa karibu katika sekta ya nishati, ikiwemo usimamizi na matumizi ya Bomba la Mafuta la TAZAMA, ambalo ni kiungo muhimu katika usafirishaji wa mafuta kutoka Bandari ya Dar es Salaam kwenda Zambia.


Ushirikiano huo umeendelea kuchangia kuimarika kwa usalama wa nishati na kukuza uchumi wa nchi zote mbili.