HABARI

SIASA

ELIMU

Recent Posts

SAME UTALII FESTIVAL YAWAINUA WANANCHI KIUCHUMI

April 08, 2026 Add Comment



Wananchi wa wilaya ya Same mkoani Kilimanjaro wamewaomba viongozi kuhakikisha tamasha la utalii la Same Utalii Festival linafanyika kila mwaka kutokana na mchango wake mkubwa katika kukuza uchumi wa jamii.

Wito huo umetolewa leo na kina mama lishe wakati wa joggin ya kuhamasisha tamasha hilo linalotarajiwa kufanyika Aprili 10 hadi 12 mwaka huu, likiwa ni msimu wa tatu tangu kuanzishwa kwake.

Akizungumza katika joggin hiyo, Anna Mzava, ambaye ni mama lishe katika stendi ya mabasi wilayani Same, alisema tamasha hilo limekuwa msaada mkubwa kwao kiuchumi.

Alisema mbali na kuhamasisha utalii, tamasha hilo limeongeza kipato kwa wafanyabiashara wadogo kutokana na ongezeko la watu wanaohudhuria.

“Tunaomba tamasha hili liwe endelevu kwani sisi wananchi wa chini tunafaidika nalo. Biashara zetu zinaenda vizuri na tunapata fedha zaidi. Kwa mfano, badala ya kupika mchele kilo tatu, wakati wa tamasha napika hadi kilo 10 na zote zinaisha,” alisema Mzava.

Kwa upande wake, Jumanne Idd alisema tamasha hilo limekuwa chachu ya kutangaza utalii wa wilaya ya Same pamoja na vyakula vya asili vya kabila la Wapare.

Aliongeza kuwa tukio hilo limechangia kuitangaza wilaya hiyo kitaifa na kuchochea ukuaji wa shughuli za kiuchumi wakati wa msimu wa tamasha.

Akizungumza katika joggin hiyo, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Same, Yusto Mapande, alisema wamejipanga kuhakikisha tamasha hilo linakuwa endelevu ili kuendelea kutangaza vivutio vya utalii vilivyopo wilayani humo.

Alisema halmashauri itaendelea kubuni na kuibua vivutio vipya ili kuongeza fursa za kiuchumi kwa wananchi.

“Faida kubwa tunazotarajia ni za kiuchumi.Panapokusanyika watu wengi ni fursa, kwani wanahitaji huduma mbalimbali na hivyo kuongeza kipato kwa wananchi,” alisema Mapande.

RAIS MHE. DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AWAAPISHA VIONGOZI MBALIMBALI IKULU YA CHAMWINO MKOANI DODOMA

April 08, 2026 Add Comment

 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akimuapisha Mhe. Profesa Palamagamba John Aidan Kabudi kuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu) kwenye hafla iliyofanyika Ikulu ya Chamwino mkoani Dodoma tarehe 08 Aprili, 2026.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akimuapisha Mhe. Profesa Palamagamba John Aidan Kabudi kuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu) kwenye hafla iliyofanyika Ikulu ya Chamwino mkoani Dodoma tarehe 08 Aprili, 2026.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akimuapisha Mhe. Festo John Dugange kuwa Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) kwenye hafla iliyofanyika Ikulu ya Chamwino mkoani Dodoma tarehe 08 Aprili, 2026.



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akimuapisha Mhe. Kwagilwa Reuben Nhamanilo kuwa Naibu Waziri, Ofisi ya Makamu wa Rais, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) kwenye hafla iliyofanyika Ikulu ya Chamwino mkoani Dodoma tarehe 08 Aprili, 2026.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akimuapisha Mhe. Kwagilwa Reuben Nhamanilo kuwa Naibu Waziri, Ofisi ya Makamu wa Rais, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) kwenye hafla iliyofanyika Ikulu ya Chamwino mkoani Dodoma tarehe 08 Aprili, 2026.




Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akimuapisha Mhe. Gerson John Mdemu kuwa Kamishna wa Tume ya Utumishi wa Mahakama kwenye hafla iliyofanyika Ikulu ya Chamwino mkoani Dodoma tarehe 08 Aprili, 2026.
Viongozi wateule wakiapa Kiapo cha Maadili kwenye hafla iliyofanyika Ikulu ya Chamwino mkoani Dodoma tarehe 08 Aprili, 2026

KASULU YAZIDI KUNUFAIKA NA MALIASILI NA UTALII

April 08, 2026 Add Comment


Na Sixmund Begashe, Dodoma
Wananchi wa Jimbo la Kasulu Vijijini wameendelea kunufaika na uwepo wa mwekezaji katika kitalu cha Makere Forest Reserve kwa kupata mgao wa fedha za maendeleo ya jamii zaidi ya Shilingi Milioni 12 kila mwaka kinacholipwa na mwekezaji kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo ya vijiji.

Hayo yamesemwa Bungeni Jijini Dodoma na Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji, alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Jimbo hilo Mhe. Edibil Kazala Kinyoma alipotaka kujua "Je, ni kwa kiasi gani wananchi wa Jimbo la Kasulu Vijijini wananufaika na uwepo wa Mwekezaji wa kitalu cha Makere Forest Reserve".

Dkt. Kijaji amesema kuwa kwa kuzingatia vipaumbele vya vijiji husika katika Mwaka wa Fedha 2024/2025 Vijiji vya Kagera Nkanda, Chekenya na Kabulanzwili vililipwa Shilingi 4,356,435.67 kila kimoja.

"Vilevile, mgao wa fedha zinazotokana na asilimia 25 ya ada ya wanyamapori wanaowindwa katika kitalu husika kwa mujibu wa Kifungu cha 137 cha Sheria ya Fedha ya Mwaka 2025 zinalipwa na Serikali kwa Halmashauri husika". Alifafanua Dkt. Kijaji

Ameongeza kuwa asilimia 60 ya fedha hizo hutumika kutekeleza miradi ya maendeleo na asilimia 40 shughuli za uhifadhi katika vijiji vinavyozunguka kitalu husika.

"Sambamba na manufaa yaliyotajwa, katika kipindi cha mwaka 2024/25 na 2025/26 mwekezaji kwa kushirikiana na Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA) wamechangia miradi ya jamii yenye thamani ya shilingi 166,475,000". Aliongeza Dkt. Kijaji

Aidha, Dkt. Kijaji amesema kuwa fedha hizo zimetumika kufadhili kambi ya huduma ya matibabu ya macho katika Halmashauri ya Kasulu, madawati 100 katika Shule za Msingi Chekenya (25), Nyakasanda (25) na Nyantuku (50) na uchimbaji wa visima vya maji sita (6) katika Shule za Msingi Kamganza, Kasasa, Mwitiri, Chekenya na Nyantuki pamoja na Kituo cha Afya cha Kagerankanda.

WATENGENEZA MAUDHUI MTANDAONI WATAKIWA KUWA NGUVU YA KUBADILISHA JAMII KATIKA MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA

April 08, 2026 Add Comment




📌 Kupitia uelimishaji na uhamasishaji wa jamii


Katika mwendelezo wa mafunzo kwa watengeneza maudhui mtandaoni (Content Creators), awamu ya kwanza inayoendelea Jijini Arusha leo Aprili 8, 2026, Wizara ya Nishati imewahimiza washiriki kutumia majukwaa yao ya kidijitali kama chachu ya kuleta mabadiliko chanya katika jamii.


Akitoa wito huo, Mhandisi Benezeth Kabunduguru kutoka Kitengo cha Nishati Safi ya Kupikia amesema watengeneza maudhui wana nafasi kubwa ya kuelimisha umma kuhusu umuhimu wa matumizi ya nishati safi ya kupikia, pamoja na kuhamasisha jamii wanayoizunguka na wafuasi wao kubadili mitazamo na kuanza kutumia nishati hizo.

Akiwasilisha mada yake, Mhandisi Kabunduguru ameeleza kuwa watengeneza maudhui wanaweza kutumia mbinu mbalimbali zenye mvuto kama vile picha za video fupi, vichekesho, hadithi na simulizi za maisha halisi ili kufikisha ujumbe kwa ufanisi na kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia.

Aidha, amesisitiza kuwa nishati safi ya kupikia si aina moja tu, bali ipo katika mfumo mbalimbali ikiwemo gesi, umeme, mkaa mbadala na nyinginezo, ambazo zimeidhinishwa na Shirika la Viwango Tanzania (TBS) kuwa salama kwa afya ya binadamu na rafiki kwa mazingira.

Katika hatua nyingine, alibainisha kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan ni kinara wa ajenda ya nishati safi ya kupikia barani Afrika. Hivyo amewataka watengeneza maudhui kumuunga mkono kwa vitendo ili kufanikisha lengo la kitaifa la kufikia asilimia 80 ya matumizi ya nishati safi ya kupikia ifikapo mwaka 2034.

Ameongeza kuwa watengeneza maudhui wanapaswa kutumia ushawishi wao kubadilisha mitazamo hasi ya jamii kwa kutumia lugha sahihi, ubunifu na maudhui yenye kugusa maisha ya watu.

Kwa mujibu wa takwimu, takribani vifo 33,000 hutokea kila mwaka kutokana na matumizi ya nishati isiyo safi ya kupikia. Hivyo, kuna umuhimu mkubwa wa kuifikisha elimu hii kwa wananchi wengi zaidi kupitia majukwaa ya kidijitali yanayotumiwa na watengeneza maudhui.

Mafunzo hayo yameandaliwa na Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa kushirikiana na Mfuko wa Utamaduni na Sanaa Tanzania, huku Wizara ya Nishati ikiwa miongoni mwa wadhamini wakuu.



BARRICK YAPOKEA UAMUZI WA MAHAKAMA YA RUFAA YA ONTARIO WA KUTUPILIA MBALI RUFAA KUHUSU MGODI WA NORTH MARA

April 08, 2026 Add Comment

Kampuni ya Barrick Mining Corporation imepokea uamuzi wa Mahakama ya Rufaa ya Ontario kutupilia mbali rufaa ya baadhi ya wakazi wa Tanzania wanaodai kuwepo ukiukwaji wa haki za binadamu unaofanywa na askari wa Jeshi la Polisi la Tanzania karibu na mgodi wa dhahabu wa Kampuni ya North Mara. 

MAFUNZO YA WAKAGUZI WA UVUVI KUCHOCHEA MAPINDUZI YA UBORA

MAFUNZO YA WAKAGUZI WA UVUVI KUCHOCHEA MAPINDUZI YA UBORA

April 08, 2026 Add Comment

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi anayeshughulikia Uvuvi Prof. Mohammed Sheikh,akizungumza leo Aprili 8,2026 wakati akizindua mafunzo ya siku tano kwa maafisa wakaguzi wa mazao ya uvuvi 25 yaliyoandaliwa na Wakala ya Elimu na Mafunzo ya Uvuvi (FETA) kwa kushirikiana na Shirika la Kilimo na Chakula Duniani (FAO).

.....

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi anayeshughulikia Uvuvi Prof. Mohammed Sheikh amewataka wakaguzi wa mazao ya uvuvi kufanya kazi zao kwa ubora ili kulisaidia Taifa kuongeza kiwango cha mazao ya uvuvi yanayosafirishwa nje ya nchi.

Prof Sheikh ametoa kauli hiyo 8 April, 2026 wakati akizindua mafunzo ya siku tano kwa maafisa wakaguzi wa mazao ya uvuvi 25 yaliyoandaliwa na Wakala ya Elimu na Mafunzo ya Uvuvi (FETA) kwa kushirikiana na Shirika la Kilimo na Chakula Duniani (FAO).

"Takwimu zinaonesha kwasasa tunasafirisha tani 60,000 pekee za samaki kwenda nje ya nchi hivyo uwepo wa mafunzo haya uwe chachu ya kuongeza ubora utakaosaidia Taifa kuongeza kiasi cha samaki kinachopelekwa nje ya nchi" Amesema Prof. Sheikh

Kwa uoande wake Mtendaji Mkuu wa Wakala ya Elimu na Mafunzo ya Uvuvi (FETA) Dkt Semvua Mzighani amesema Mafunzo haya yamelenga kuwajengea uwezo maafisa ukaguzi wa mazao ya uvuvi juu ya taratibu za ukaguzi wa mazao ya uvuvi pamoja na viwango vya ubora vya kitaifa,kikanda na kimataifa.

Pia amewasihi washiriki wa mafunzo kuzingatia mafunzo watakayopatiwa na elimu watakayoipata kupitia mafunzo hayo ikawasaidie wananchi katika maeneo yao.

Awali Mratibu wa mafunzo hayo Mkufunzi Anold Mbunda amesema hii ni awamu ya kwanza ya mafunzo ambapo imejumuisha washiriki toka ukanda wa pwani, awamu ya pili ya mafunzo haya itafanyika mkoani Kigoma ambapo itahusisha washiriki kutoka kanda ya ziwa.

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi anayeshughulikia Uvuvi Prof. Mohammed Sheikh,akizungumza leo Aprili 8,2026 wakati akizindua mafunzo ya siku tano kwa maafisa wakaguzi wa mazao ya uvuvi 25 yaliyoandaliwa na Wakala ya Elimu na Mafunzo ya Uvuvi (FETA) kwa kushirikiana na Shirika la Kilimo na Chakula Duniani (FAO).

Mtendaji Mkuu wa Wakala ya Elimu na Mafunzo ya Uvuvi (FETA) Dkt Semvua Mzighani,akizungumza  wakati wa mafunzo ya siku tano kwa maafisa wakaguzi wa mazao ya uvuvi 25 yaliyoandaliwa na Wakala ya Elimu na Mafunzo ya Uvuvi (FETA) kwa kushirikiana na Shirika la Kilimo na Chakula Duniani (FAO).

Sehemu ya washiriki wakifatilia hotuba ya Mgeni rasmi Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi anayeshughulikia Uvuvi Prof. Mohammed Sheikh (hayupo pichani) ,wakati akizindua mafunzo ya siku tano kwa maafisa wakaguzi wa mazao ya uvuvi 25 yaliyoandaliwa na Wakala ya Elimu na Mafunzo ya Uvuvi (FETA) kwa kushirikiana na Shirika la Kilimo na Chakula Duniani (FAO). 

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi anayeshughulikia Uvuvi Prof. Mohammed Sheikh,akiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kuzindua  mafunzo ya siku tano kwa maafisa wakaguzi wa mazao ya uvuvi 25 yaliyoandaliwa na Wakala ya Elimu na Mafunzo ya Uvuvi (FETA) kwa kushirikiana na Shirika la Kilimo na Chakula Duniani (FAO).

TRA TANGA YAKUSANYA BILIONI 406.17 KWA MIEZI 9,YAVUKA LENGO KWA ASILIMIA 137

April 08, 2026 Add Comment



Na Oscar Assenga,TANGA


MAMLAKA ya Mapato Tanzania (TRA) Mkoa wa Tanga imefanikiwa kukusanya kiasi cha shilingi bilioni 406.17 katika kipindi cha miezi tisa kuanzia Julai 2025 hadi Machi 2026, ikilinganishwa na lengo la bilioni 296.3 ukiwa ni ufanisi wa asilimia 137.


Akizungumza kuhusu mafanikio hayo leo  Meneja wa TRA Mkoa wa Tanga, Casto John, alisema kuwa matokeo hayo makubwa yametokana na mchango na ushirikiano mzuri wa wadau mbalimbali, ikiwemo Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Wakuu wa Wilaya, pamoja na vyombo vingine vya serikali ambavyo vimekuwa mstari wa mbele kuhakikisha ukusanyaji wa kodi unafanyika katika mazingira salama na tulivu.


Aidha, aliwashukuru walipa kodi wote kwa mchango wao mkubwa akisisitiza kuwa mafanikio hayo ni matokeo ya wananchi kujitokeza kwa hiari kulipa kodi zao  



Pia alipongeza ushirikiano kutoka kwa vyama vya wafanyabiashara kama JW na TCCIA, pamoja na taasisi za serikali na binafsi ambazo zimekuwa zikifanya kazi kwa pamoja kama timu.


Katika hatua nyingine, Meneja huyo alisisitiza umuhimu wa kipindi cha makadirio ya kodi (Januari hadi Machi) kwa wafanyabiashara kuhakikisha wanajitokeza kwa wingi huku akiwashukuru walipa kodi waliojitokeza kukadiriwa na kulipa kodi zao.



 Hata hivyo, aliwataka wale ambao bado hawajafika kujitokeza haraka kwani ofisi za TRA ziko wazi kwa huduma hiyo.


Alionya kuwa kutakuwa na zoezi la kuwafuatilia wadaiwa wa kodi, likiwemo ukaguzi wa barabarani kwa magari na wafanyabiashara wasiolipa kodi, hivyo ni vyema wakazingatia sheria mapema.



Kuhusu matumizi ya mashine za kielektroniki za kutoa risiti (EFD), amesema bado kuna changamoto katika baadhi ya maeneo kutokana na baadhi ya wafanyabiashara kutokutoa hivyo niwatake 


Aliwataka wafanyabiashara kuhakikisha wanatoa risiti kwa kila huduma au bidhaa wanayouza, huku akiwahimiza wananchi kudai risiti wanaponunua bidhaa au kupata huduma.


Pia alibainisha kuwa changamoto zozote zinazohusiana na EFD zinapaswa kuripotiwa ili zipatiwe ufumbuzi.


Akizungumzia suala la magendo, alisema Mkoa wa Tanga unapakana na nchi jirani akionya baadhi ya wafanyabiashara wanaotumia njia zisizo rasmi kuingiza bidhaa nchini .huku akiwataka kutumia mipaka rasmi ili kuhakikisha bidhaa zinakaguliwa na taasisi husika kama TBS kwa ajili ya kulinda afya za wananchi.


Alisisitiza kuwa magendo yana madhara makubwa kwa uchumi wa nchi, kwani husababisha kukosekana kwa takwimu sahihi za biashara, kupunguza mapato ya serikali, na kuathiri wafanyabiashara halali pamoja na wananchi kwa ujumla.


MH. LUSWETULA: TRA IHARAKISHE TATHMINI YA MAHITAJI YA VITUO VYA FORODHA.

April 08, 2026 Add Comment


Na. Saidina Msangi, WF, Dodoma.

Serikali imesema kuwa kupitia Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) inaendelea kufanya tathmini ya mahitaji ya ujenzi wa Kituo cha Forodha katika Jimbo la Momba, ikiwemo upembuzi yakinifu, upatikanaji na utambuzi wa eneo, gharama za mradi na utayari wa nchi jirani.

Hayo yalisemwa bungeni jijini Dodoma na Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Laurent Deogratius Luswetula (Mb), alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Momba, Mhe. Condester Michael Sichalwe, aliyetaka kujua wakati ambao Serikali itajenga kituo cha forodha katika Jimbo la Momba mkoa wa Songwe.

Alisema eneo hilo linaangaliwa kwa kuzingatia ongezeko la shughuli za biashara na umuhimu wake katika kuongeza ufanisi wa ukusanyaji wa mapato na udhibiti wa biashara mipakani.

’’Ujenzi wa vituo vya forodha, ikiwemo katika Jimbo la Momba, hufanyika kwa kuzingatia vipaumbele vya Serikali, ukamilifu wa taratibu na kanuni za kiforodha, utayari wa nchi jirani tunazopakana nazo, masuala ya kiusalama, upatikanaji wa rasilimali fedha, pamoja na tathmini ya umuhimu wa eneo husika katika shughuli za biashara za mipakani,’’ alifafanua Mhe. Luswetula.

Aliongeza kuwa ujenzi wa kituo hicho utaanza mara baada ya kukamilika kwa maandalizi yote muhimu, ikiwa ni pamoja na kupatikana kwa fedha za utekelezaji wa mradi katika bajeti ya Serikali na kutangazwa kwenye Gazeti la Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Aidha, Mhe. Luswetula alieleza kuwa TRA inaendelea na maandalizi na itatoa taarifa rasmi pindi ratiba ya utekelezaji wa ujenzi itakapokamilika na kuielekeza TRA kuharakisha tathmini hiyo ambayo iko katika hatua za mwisho.

RAIS WA UGANDA MHE YOWERI MUSEVENI AKUTANA NA DKT JAKAYA MRISHO KIKWETE, RAIS MSTAAFU WA TANZANIA NA MWAKIKLISHI MAALUMU WA UMOJA WA AFRIKA KWA UKANDA WA PEMBE YA AFRIKA NA BAHARI YA SHAMU

April 08, 2026 Add Comment


Rais wa Uganda, Mheshimiwa Yoweri Kaguta Museveni, amekutana na kufanya mazungumzo na Rais mstaafu wa Tanzania na Mwakilishi Maalum wa Umoja wa Afrika (AU) kwa Ukanda wa Pembe ya Afrika na Bahari ya Shamu, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, katika Ikulu ndogo ya Nakasero jijini Kampala, Jumanne tarehe 7 Aprili 2027.

Katika mazungumzo yao, viongozi hao wawili walijadili hali ya kisiasa na kiusalama nchini Sudan Kusini, wakisisitiza umuhimu wa mazungumzo ya amani na maridhiano kati ya pande husika ili kurejesha utulivu wa kudumu.

Rais Museveni alimweleza Dkt. Kikwete kuwa Uganda itaendelea kuunga mkono juhudi zote za kuleta amani nchini humo, akibainisha kuwa utulivu wa Sudan Kusini, hasa katika eneo la Equatoria ambako kuna idadi kubwa ya raia wa Uganda, ni muhimu kwa usalama wa kikanda na ustawi wa kiuchumi.

Dkt. Kikwete, mwenye uzoefu mkubwa wa kidiplomasia katika masuala ya amani barani Afrika, hivi karibuni aliteuliwa na Mwenyekiti wa Umoja wa Afrika kuwa Mwakilishi Maalum kwa Ukanda wa Pembe ya Afrika na Bahari ya Shamu, jukumu linalolenga kuimarisha juhudi za upatanishi, ushirikiano wa kikanda na utatuzi wa migogoro katika eneo hilo lenye changamoto za kiusalama na kisiasa.



DKT.AKWILAPO KUSHIRIKI KONGAMANO LA MIJI AFRIKA NAIROBI

April 07, 2026 Add Comment


Nairobi

Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. Dkt Leonard Akwilapo, anatarajiwa kuongoza ujumbe wa Tanzania kushiriki Kongamano la Pili la Jukwaa la Miji Afrika (2nd African Urban Forum) litakalofanyika kuanzia tarehe 8 hadi 10 Aprili 2026 katika jiji la Nairobi nchini Kenya.

Kongamano hilo linaongozwa na kauli mbiu isemayo “Adequate Housing for All: Advancing Socio-Economic and Environmental Transformation Towards the Realization of Agenda 2063,” linalenga kuhamasisha mijadala itakayotoa fursa kwa washiriki kutoka nchi mbalimbali za Afrika kubadilishana uzoefu na suluhisho bunifu katika kukabiliana na changamoto za maendeleo ya miji na makazi.

Kupitia kongamano hilo, Tanzania inatarajiwa kutoa tamko la nchi litakaloeleza jitihada za Serikali katika kuchochea maendeleo endelevu ya miji na makazi, ikiwa ni pamoja na sera, mipango na mikakati inayotekelezwa kuboresha makazi na upangaji wa miji.

Aidha, Mhe. Dkt Akwilapo atashiriki katika mijadala ya ngazi ya juu itakayowahusisha mawaziri, mameya na wataalamu mbalimbali, kwa lengo la kuimarisha ushirikiano wa kikanda na kimataifa katika sekta ya maendeleo ya miji.

Awali Dkt Akwilapo aliongoza kikao cha maandalizi kwa ujumbe wa Tanzania utakaoshiriki kongamano hilo katika ubalozi wa Tanzania nchini Kenya tarehe 7 April, 2026 ambapo masuala mbalimbali ya uwakilishi wa nchi yalijadiliwa.


Dkt Akwilapo ameambatana na Mkurugenzi wa Maendeleo ya Makazi Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Bw. Deogratias Kalimenze, Mkurugenzi Msaidizi Uzingatiaji Mipango ya Matumizi ya Ardhi kutoka Tume ya Taifa ya Matumizi ya Ardhi Bi. Rehema Kishoa, Maafisa kutoka Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makazi pamoja na taasisi binafsi.

WAZIRI NDEJEMBI AFANYA KIKAO KAZI CHA PAMOJA NA TAASISI ZILIZO CHINI YA WIZARA YA NISHATI

April 07, 2026 Add Comment

 


Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi amekutana na kufanya kikao kazi cha pamoja na Taasisi zilizo chini ya Wizara ya Nishati zinazoshughulikia mafuta leo Aprili 07, 2026 jijini Dodoma.


Lengo la kikao hicho ni kupitia na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini kuhusu hali ya upatikanaji na bei za bidhaa za mafuta nchini itakayowasilishwa mbele ya kamati hiyo Aprili 08, 2026.

Kikao hicho kinatokana na agizo la Spika wa Bunge, Mhe. Mussa Zungu alilolitoa Aprili 01, 2026 kwa Waziri wa Nishati akielekeza kukutana na Kamati ya Nishati na Madini ili kujadili hali na mwenendo wa kupanda kwa bei ya mafuta nchini.

Kikao hicho kimehudhuriwa na Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba, Katibu Mkuu Wizara ya Nishati anayeshughulikia Mafuta na Gesi, Dkt. James Mataragio, Wataalamu kutoka wizarani pamoja na Wakuu wa Taasisi zilizo chini ya wizara zinazoshughulikia mafuta na gesi.