HABARI

SIASA

ELIMU

Recent Posts

WADAU WA BIASHARA WAELIMISHWA NAMNA YA KUPATA HAKI KUPITIA BARAZA LA USHINDANI

WADAU WA BIASHARA WAELIMISHWA NAMNA YA KUPATA HAKI KUPITIA BARAZA LA USHINDANI

February 08, 2026 Add Comment

Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza, Bw. Balandya Elikana,akizungumza wakati akifungua mafunzo ya kuwajengea uwezo wafanyabiashara jijini Mwanza,ili  kuwaongezea uelewa kuhusu masuala ya ushindani wa soko pamoja na taratibu za kupata haki katika shughuli za kibiashara yaliyoandaliwa na Baraza la Ushindani wa Soko (FCT).

Na.Mwandishi Wetu-MWANZA

 BARAZA  la Ushindani wa Soko (FCT)  limetoa mafunzo ya kuwajengea uwezo wafanyabiashara jijini Mwanza, yakilenga kuwaongezea uelewa kuhusu masuala ya ushindani wa soko pamoja na taratibu za kupata haki katika shughuli za kibiashara.

Mafunzo hayo yaliwakutanisha wadau mbalimbali wa sekta ya biashara, ambapo waliipongeza Wizara ya Viwanda na Biashara chini ya Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa juhudi zake za kuweka mazingira bora ya biashara na uwekezaji kupitia uwepo wa chombo huru cha kusimamia na kudhibiti ushindani wa soko.

Akifungua semina hiyo, Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza, Bw. Balandya Elikana, alisema kuwa mafunzo hayo ni muhimu kwa wadau wa sekta ya biashara kwani yanawawezesha kuelewa kwa kina majukumu ya Baraza la Ushindani pamoja na umuhimu wa mshikamano katika utekelezaji wa sheria za ushindani.

“Kupitia semina hii, wadau watapata uelewa mpana kuhusu Baraza la Ushindani na nafasi yake katika kulinda haki za mlaji pamoja na kuendeleza ushindani wa haki katika soko.”Alisema Bw.Elikana

Akizungumza katika mafunzo hayo, Msajili wa Baraza la Ushindani, Bw. Mbegu Kaskasi, alisema kuwa Baraza lipo kwa ajili ya kulinda masuala yote yanayohusu ushindani wa soko na kuchochea maendeleo ya kiuchumi nchini. Alieleza kuwa utekelezaji wa majukumu ya Baraza unalenga kuimarisha misingi ya utawala bora kwa kuhakikisha sheria za ushindani zinatekelezwa kikamilifu, kwa haki na kwa uwazi.

Aidha, aliongeza kuwa Baraza huhakikisha mamlaka za udhibiti zinazingatia taratibu na kanuni za ushindani wakati wa utekelezaji wa majukumu yao, sambamba na kutoa majibu sahihi na ya haraka katika migogoro ya kibiashara. Alibainisha kuwa hatua hiyo inalenga kumlinda mlaji dhidi ya vitendo vinavyodhoofisha ushindani, hivyo kuchangia katika ujenzi wa uchumi shindani, jumuishi na wenye tija kwa Watanzania.

Kwa upande wake, Meneja wa Mkoa wa Chemba ya Wafanyabiashara, Bw. Hassan Karambi, alisema kuwa amepata elimu yenye manufaa makubwa kupitia programu ya Baraza ya kuwajengea uwezo wadau.

Alieleza kuwa mafunzo hayo yamewasaidia wafanyabiashara kufahamu kuwa endapo hawataridhika na maamuzi ya mamlaka za udhibiti kama LATRA, TCRA, TCAA, EWURA, PURA pamoja na Tume ya Ushindani (FCC), wana haki ya kukata rufaa katika Baraza la Ushindani ili kupata haki yao.

Naye Meneja wa Mamlaka ya Mawasiliano Kanda ya Ziwa, Bi. Imelda Salumu, alifafanua utaratibu wa Baraza katika kupokea rufaa kutoka kwa wadau.

Alisema kuwa malalamiko huanza kwa mtoa huduma husika, na endapo hayatapatiwa ufumbuzi, hufikishwa katika mamlaka ya udhibiti kama hatua ya kwanza ya rufaa. Aliongeza kuwa iwapo mlalamikaji hataridhishwa na maamuzi ya mamlaka hiyo, utaratibu humruhusu kuwasilisha rufaa katika Baraza la Ushindani kwa hatua zaidi za kisheria.

BARRICK MDAU MUHIMU KUFANIKISHA NDOTO YANGU KUWA MTAALAMU WA MADINI KUANZIA SHULE YA MSINGI BUGARAMA HADI CHUO KIKUU CHA JOHANNESBURG- SAMSON ABEID

February 08, 2026 Add Comment
Samson Abeid akitoa neno la shukrani wakati wa hafla ya kuwaaga wanafunzi wa kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) waliopata ufadhili wa kwenda kusomea taaluma ya madini.
RAIS SAMIA APONGEZWA KWA KUPUNGUZA UHABA WA WATUMISHI HANDENI MJI

RAIS SAMIA APONGEZWA KWA KUPUNGUZA UHABA WA WATUMISHI HANDENI MJI

February 07, 2026 Add Comment

Mwenyekiti wa halmashauri ya Mji Handeni, Amiri Mwaliko,akizungumza katika mkutano wa kupokea na kujadili taarifa za kata za Halmashauri ya Mji Handeni uliofanyika leo Februari 7, 2026.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Handeni, Maryam Ukwaju,akizungumza katika mkutano wa kupokea na kujadili taarifa za kata za Halmashauri ya Mji Handeni uliofanyika leo Februari 7, 2026.

Naibu Waziri wa Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Mhe. Reuben Kwagilwa,akiteta jambo na Mkuu wa Wilaya ya Handeni, Mhe. Salum Nyamwese,wakati wa  mkutano wa kupokea na kujadili taarifa za kata za Halmashauri ya Mji Handeni uliofanyika leo Februari 7, 2026.

Sehemu ya Madiwani wakifuatilia mkutano wa kupokea na kujadili taarifa za kata za Halmashauri ya Mji Handeni uliofanyika leo Februari 7, 2026.

Na Augusta Njoji

MWENYEKITI wa Halmashauri ya Mji Handeni, Mhe. Amiri Mwaliko, amempongeza Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan, kwa kutoa kibali cha ajira kilichowezesha kupatikana kwa watumishi 82 wa kada mbalimbali na hivyo kupunguza uhaba wa watumishi katika halmashauri hiyo.

Akifungua mkutano wa kupokea na kujadili taarifa za kata wa Halmashauri hiyo uliofanyika Februari 7, 2026 mjini hapa, Mhe. Mwaliko amesema serikali imeendelea kuchukua hatua za kutatua changamoto ya upungufu wa watumishi.

“Tunaishukuru serikali kwa kuendelea kutatua changamoto ya watumishi. Tunafurahia hatua hii kwa kuwa lengo la serikali ni kuondoa uhaba wa watumishi na kuboresha utoaji wa huduma kwa wananchi,” amesema.

Aidha, amempongeza Mkuu wa Wilaya ya Handeni, Mhe. Salum Nyamwese, kwa kuhakikisha wilaya hiyo inaendelea kudumisha amani na utulivu.

Mhe. Mwaliko amewataka viongozi na watumishi kushirikiana katika kujenga halmashauri yenye mshikamano na kutatua changamoto zinazojitokeza.

Ameongeza kuwa ni muhimu kusimama pamoja na watumishi na kushughulikia changamoto kwa njia ya mazungumzo ili kujenga timu imara ya utendaji kwa maendeleo ya halmashauri.

Kadhalika, amesisitiza kuendelea kuchukuliwa hatua za kudhibiti utoro wa wanafunzi kwa kushirikiana na madiwani wa maeneo husika.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Handeni, Maryam Ukwaju, amesema katika mwaka wa fedha 2025/26 serikali imeajiri watumishi 82 wakiwemo walimu wa shule za msingi na sekondari pamoja na wauguzi.

Amesema changamoto ya upungufu wa watumishi inaendelea kupatiwa ufumbuzi kadri serikali inavyoendelea kutoa ajira, huku halmashauri ikiendelea kutenga bajeti kupitia mapato ya ndani kwa ajili ya kuchangia maendeleo ya kata, ikiwemo ununuzi wa madawati.

KWAGILWA ABANA UWAJIBIKAJI WA TAASISI ZA UMMA HANDENI MJI

KWAGILWA ABANA UWAJIBIKAJI WA TAASISI ZA UMMA HANDENI MJI

February 07, 2026 Add Comment

Naibu Waziri wa Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Mhe. Reuben Kwagilwa,akizungumza katika mkutano wa kupokea na kujadili taarifa za kata za Halmashauri ya Mji Handeni uliofanyika leo Februari 7, 2026.

Mkuu wa Wilaya ya Handeni, Mhe. Salum Nyamwese,akizungumza katika mkutano wa kupokea na kujadili taarifa za kata za Halmashauri ya Mji Handeni uliofanyika leo Februari 7, 2026.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Handeni, Maryam Ukwaju,akizungumza katika mkutano wa kupokea na kujadili taarifa za kata za Halmashauri ya Mji Handeni uliofanyika leo Februari 7, 2026.

Mwenyekiti wa halmashauri ya Mji Handeni, Amiri Mwaliko,akizungumza katika mkutano wa kupokea na kujadili taarifa za kata za Halmashauri ya Mji Handeni uliofanyika leo Februari 7, 2026.

Naibu Waziri wa Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Mhe. Reuben Kwagilwa,akiteta jambo na Mkuu wa Wilaya ya Handeni, Mhe. Salum Nyamwese,wakati wa  mkutano wa kupokea na kujadili taarifa za kata za Halmashauri ya Mji Handeni uliofanyika leo Februari 7, 2026.

Sehemu ya washiriki wakifatilia hotuba ya Naibu Waziri wa Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Mhe. Reuben Kwagilwa (hayupo pichani) wakati wa mkutano wa kupokea na kujadili taarifa za kata za Halmashauri ya Mji Handeni uliofanyika leo Februari 7, 2026.

Na Augusta Njoji

Naibu Waziri wa Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Mhe. Reuben Kwagilwa, ameelekeza taasisi za serikali zinazohudumia wananchi wilayani Handeni kuwasilisha taarifa za utekelezaji wa majukumu yao katika Baraza la Madiwani ili kuongeza uwazi na kuwafanya wananchi kufahamu kazi zinazofanywa na serikali.

Akizungumza katika mkutano wa kupokea na kujadili taarifa za kata za Halmashauri ya Mji Handeni uliofanyika Februari 7, 2026, Mhe. Kwagilwa amesema ni muhimu kwa wakuu wa taasisi za serikali kuhudhuria vikao vya Baraza la Madiwani na kuwasilisha taarifa zao.

Amezitaja baadhi ya taasisi hizo kuwa ni pamoja na Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS), Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA), Mamlaka ya Maji pamoja na Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), akisisitiza kuwa taasisi hizo zinawajibika moja kwa moja kwa wananchi.

Pamoja na hayo, amempongeza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Handeni, Maryam Ukwaju, pamoja na wataalamu wa halmashauri hiyo kwa mafanikio yaliyopatikana katika utekelezaji wa ilani ya uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) iliyopita na kuendelea kutekeleza ilani ya sasa.

Naye Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo, Mhe. Amiri Mwaliko, amempongeza Naibu Waziri Kwagilwa kwa kuaminiwa na Rais Samia Suluhu Hassan kushika nafasi hiyo, akisema anaamini atatekeleza vyema majukumu yake katika kuisaidia TAMISEMI.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Handeni, Mhe.Salum Nyamwese ameahidi kuwapa ushirikiano Madiwani katika utekelezaji wa majukumu yao.

\
BILIONI 91 KUSAMBAZA UMEME KWENYE VITONGOJI 570 VYA MKOA WA MOROGORO

BILIONI 91 KUSAMBAZA UMEME KWENYE VITONGOJI 570 VYA MKOA WA MOROGORO

February 07, 2026 Add Comment
 

Na.Mwandishi Wetu-Morogoro📍

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Mhe. Adam Malima, tarehe 6 Februari, 2026 amewapokea wakandarasi wawili kutoka Wakala wa Nishati Vijijini (REA); watakaotekeleza Mradi mkubwa wa kusambaza umeme katika vitongoji 570 vya mkoa huo; ikielezwa kuwa Mradi huo una thamani ya shilingi bilioni 91.

Wakandarasi hao ni kampuni ya Sagemcom Energy & Telecom SAS (Italia) na China Railway No. 4 Engineering Group Co. Ltd (China) ambao watasambaza umeme katika vitongoji 570 katika Mradi huo mkubwa kwa gharama ya shilingi bilioni 91.

Akizungumza wakati wa hafla ya kuwatambulisha wakandarasi hao, Mhe. Malima alisema Mradi huo ni utekelezaji wa dhamira ya Serikali ya Awamu ya Sita ya kuhakikisha Watanzania wote wanapata huduma ya umeme wa uhakika hususan maeneo ya vijijini.

Mhe. Malima alisema kuwa Serikali kupitia REA imeleta maendeleo makubwa kwenye Sekta ya Nishati hususan kwenye usambazaji wa umeme vijijini katika kipindi cha miaka 15; akitolea mfano wakati alipokuwa Naibu Waziri wa Nishati mwaka 2008 ambapo bajeti ya REA ilikuwa shilingi bilioni tano pekee.

“Leo hii baada ya miaka 15 mkoa wa Morogoro pekee yake, unatekeleza Miradi ya umeme yenye thamani ya shilingi bilioni 91. Hii inaonesha dhamira ya dhati ya Serikali katika kuhakikisha Wananchi wa vijijini wanapata umeme kwa maendeleo yao ya kiuchumi na kijamii.” alisema Mhe. Malima.

Kwa upande wake, Kaimu Mkurugenzi wa Umeme Vijijini, Mhandisi, Thomas Mmbaga kutoka REA alisema wamewatambulisha rasmi wakandarasi wawili watakaofanya kazi ya kusambaza umeme kwenye vitongoji 570 kwa mgawo wa kampuni ya Sagemcom Energy ambayo itasambaza umeme katika vitongoji 325 na kuunganisha wateja wa awali 11,399 katika wilaya ya Mvomero; Morogoro Vijijini na Gairo kwa gharama ya shilingi bilioni 48.4.

Mkandarasi wa pili ni kampuni ya China Railway No. 4 ambayo itasambaza umeme kwenye vitongoji 245 na kuunganisha wateja wa awali 8,649 katika wilaya ya Kilosa; Malinyi; Kilombero na Ulanga kwa gharama ya shilingi bilioni 42.5 ambapo kipindi cha utekelezaji kwa Mradi huo katika mkoa wa Morogoro ni miaka mitatu.

Naye Meneja wa TANESCO mkoa wa Morogoro, Mhandisi, Zawadi Macha alisema Shirika hilo limejipanga kikamilifu kusimamia utekelezaji wa Mradi huo kwa karibu ili kuhakikisha unatekelezwa kwa ubora unaotakiwa na kwa kuzingatia viwango vilivyowekwa.

Kwa upande wake, Meneja wa Mradi wa Kampuni ya Sagemcom Energy, Bwana Calvin Manase alisema kampuni hiyo ina uzoefu mkubwa katika utekelezaji wa miradi ya umeme na imejipanga kuhakikisha mradi unakamilika ndani ya miezi 34 licha mkataba kuwa miezi 36.

Manase aliongeza kuwa kampuni hiyo itatoa ajira kwa Wananchi (Wazawa) wa maeneo husika ili wanufaike moja kwa moja wakati wa utekelezaji wa Mradi huo. Aidha, ameipongeza REA kwa mpango wake wa kulipa malipo ya awali kwa wakandarasi akisema hatua hiyo itasaidia kupunguza changamoto ya upatikanaji wa vifaa vya ujenzi wa Mradi huo.

         
UMEME VITONGOJINI KUINUA UCHUMI WA WANANCHI – RC  SENDIGA

UMEME VITONGOJINI KUINUA UCHUMI WA WANANCHI – RC SENDIGA

February 07, 2026 Add Comment

Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Mhe. Queen Sendiga amesema kuwa utekelezaji wa mradi wa umeme kwenye vitongoji ni chachu ya kuinua uchumi wa wananchi vijijini.

Mhe. Sendiga ameyabainisha hayo leo Mkoani Manyara wakati wa kikao na Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kilicholenga kumtambulisha Mkandarasi Mzawa aliyeshinda zabuni ya kutekeleza mradi wa kupeleka umeme katika vitongoji 267 kwa mkoa huo, Kampuni ya SAGEM COM ENERGY.

Mradi huo unaogharimu zaidi ya shilingi bilioni 45.8 unatarajiwa kutekelezwa katika kipindi cha miaka mitatu ambapo Vitongoji katika Wilaya za Babati, Hanang, Mbulu, Kiteto, na Simanjiro vitanufaika na mradi huo.

“Tunamshkuru sana Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha hizo zinazowezesha kutekelezwa kwa mradi huu muhimu unaokwenda kuendelea kuinua uchumi wa maisha wa wananchi wetu hasa wa vijijini,” amesema Mhe. Sendiga.

Mkuu huyo wa Mkoa pia amewataka wakandarasi kufanya kazia kwa bidii na weledi na kuhakikisha mradi huo unakamilika ndani ya muda uliopangwa huku akitoa rai kwa viongozi wa serikali pamoja na wananchi kutoka ushirikiano kwa mkandarasi wakati wa utekelezaji wa mradi huo.

“Nikiwa kama Mkuu wa Mkoa natoa maelekezo kwa Waheshimiwa Wakuu wa Wilaya kuhakikisha kuwa wanashirikiana na wanaenda kumtambulisha mkandarasi kwa wananchi. Lakini pia nitoe rai kwa wananchi, miradi hii ya kijamii ambayo inakwenda kutupatia faida kubwa tuipokee, tupunguze vikwazo,” amesisitiza Mhe. Sendiga.

Awali akizungumza kuhusu utekelezwaji wa mradi huo, Mwakilishi wa Mkurugenzi Mkuu wa REA, Mhandisi Herini Mhina amesema kuwa Mkoa wa Manyara unajumla ya Vitongoji 1946 na vitongoji 1113 tayari vimefikishiwa umeme.

Mhandisi Mhina ameongeza kuwa dhamira ya Serikali ni kuhakikisha ifikapo mwaka 2030 vitongoji vyote nchini viwe vimefikishiwa nishati ya umeme na kwamba REA ikiwa na dhamana hiyo imejipanga kikamilifu kupitia miradi mbalimbali ya kimkakati kufikia dhamira hiyo.

RAIS SAMIA AFANYA MABADILIKO OFISI YA RAIS – MIPANGO, DKT. TAUSI KIDA ATEULIWA KATIBU MKUU

February 07, 2026 Add Comment

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, amefanya mabadiliko ya muundo wa Ofisi ya Rais - Mipango na Uwekezaji ambapo amemteua Dkt. Tausi Mbaga Kida kuwa Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais - Mipango na Katibu Mtendaji wa Tume ya Taifa ya Mipango.

WiLDAF HONORS 16 CHAMPIONS IN THE FIGHT AGAINST GENDER-BASED VIOLENCE, CALLS FOR STRENGTHENED COLLECTIVE ACTION

February 06, 2026 Add Comment

        

The Women in Law and Development in Africa (WiLDAF Tanzania), in partnership with the Gender-Based Violence Network (Mkuki) and other development stakeholders, has recognized and awarded 16 outstanding champions for their commitment to combating gender-based violence and advancing human rights.

TUZO ZA MAPAMBANO DHIDI YA UKATILI WA KIJINSIA ZATOLEWA

February 06, 2026 Add Comment

      

Shirika la Wanawake katika Sheria na Maendeleo Barani Afrika (WiLDAF Tanzania), kwa kushirikiana na mtandao wa kupambana na ukatili wa kijinsia (Mkuki) na wadau wengine wa maendeleo, wameandaa na kugawa tuzo kwa vinara 16 wa kupinga vitendo vya ukatili wa kijinsia na utetezi wa haki za binadamu.
WAFANYABIASHARA KARIAKOO WAPO TAYARI KWA MFUMO WA IDRAS

WAFANYABIASHARA KARIAKOO WAPO TAYARI KWA MFUMO WA IDRAS

February 06, 2026 Add Comment

Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wafanyabiashara wa Kariakoo (JWK) Bw. Severin Mushi,akizungumza wakati wa mafunzo ya mfumo mpya kwa wafanyabiashara wa Kariakoo.

Na.Mwandishi Wetu- KARIAKOO

Wafanyabiashara wameukubali mfumo wa Usimamizi wa Kodi za ndani (IDRAS) ,huku wakijiandaa kuupokea Jumatatu ya tarehe 9 Februari mwaka huu.

Akizungumza leo 6.2.2026 jijini Dar es salaam katika mafunzo ya mfumo mpya kwa wafanyabiashara wa Kariakoo Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wafanyabiashara wa Kariakoo (JWK) Bw. Severin Mushi amesema wapo tayari kuanza kuutumia mfumo huo kwa ushirikiano wa karibu na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA).

Mwenyekiti huyo amesema kupitia mafunzo ambayo wamepatiwa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) wanaamini mfumo utakuwa msaada kwao na kuondoa changamoto mbalimbali ambazo zilikuwepo.

Amesema mafunzo hayo yamekuwa msaada mkubwa kwa wafanyabiashara kwa kuwa yameondoa hofu iliyokuwepo awali na kuwapa uelewa wa pamoja kuhusu matumizi ya mfumo huo.

Bw. Mushi amesema wamejiandaa kuupokea mfumo wa IDRAS, akieleza kuwa jambo lolote jipya huwa linaogopesha kwa wanaolipokea.

Amebainisha kuwa mabadiliko ya kiteknolojia hayaepukiki katika dunia ya sasa, hivyo wafanyabiashara wanapaswa kuendana nayo ili kuboresha ufanisi wa ulipajikodi.

Hata hivyo, Mushi ametoa rai kwa TRA kushirikiana na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) kutatua changamoto ya mtandao katika baadhi ya maeneo ya biashara, hususani Kariakoo ili kuleta ufanisi wa matumizi mazuri ya mfumo mpya wa IDRAS kwa walipakodi.

Aidha, ametoa wito kwa wafanyabiashara wote kuwa tayari kuupokea mfumo wa IDRAS na kushirikiana na Serikali pamoja na TRA kwa karibu, akisisitiza kuwa lengo kubwa ni kuhakikisha ulipaji wa kodi unakuwa rahisi na wenye tija.

“Tumejiandaa kuupokea mfumo kuanzia Jumatatu ya tarehe 9 mwezi huu Kikubwa ni kushirikiana na Serikali kuhakikisha tunalipa kodi na mifumo ya ulipaji iwe rahisi,” amesema Bw. Mushi.

Aidha,Mwenyekiti huyo amependekeza kuwepo kwa kipindi cha mpito cha mafunzo ili kuwapa wafanyabiashara nafasi ya kuuelewa mfumo huo Zaidi na kuleta ufanisi sahihi wa utekelezaji wake.

“Angalau miezi mitatu ya mwanzo iwe ni ya mafunzo na kuwaelimisha watu namna ya kutumia mfumo, watakapokuwa wameuelewa, tutakwenda pamoja,”- Bw. Mushi.