HABARI

SIASA

ELIMU

Recent Posts

NEMC, HALMASHAURI YA ILALA NA WADAU WA MAZINGIRA WASAFISHA FUKWE ZA DARAJA LA SALENDER

May 17, 2026 Add Comment
Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) Kanda ya Ilala kwa kushirikiana na Halmashauri ya Wilaya ya Ilala, JUZA, Care and Help, Chuo cha Maji, MUHAS pamoja na wadau mbalimbali wa mazingira wamefanya zoezi la usafi katika fukwe za Daraja la Salender zilizopo Wilaya ya Ilala jijini Dar es Salaam. 

DAS TEMEKE AZINDUA OFISI YA WILAYA YA KITANESCO YA MIKWAMBE

May 17, 2026 Add Comment




Katibu Tawala wa Wilaya ya Temeke Bw. Kimeta Mpui amezindua Ofisi mpya ya Wilaya ya KITANESCO Mikwambe ikiwa ni mkakati wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) wa kuendelea kuwahudumia na kusogeza huduma mbalimbali zinazotolewa na TANESCO karibu na wananchi.


Akizungumza Mei 16, 2026 wakati wa zoezi hilo amesema uzinduzi wa ofisi hiyo umelenga kuboresha utoaji wa huduma kwa wananchi kutokana na mahitaji ya msingi ya Nishati ya umeme kwa wananchi yanavyozidi kuongezeka kila kukicha.




Ameeleza kuwa hatua hiyo inaakisi maboresho ya kiutendaji yanayolenga kuongeza ufanisi na kupunguza changamoto ya umbali kwa wananchi ambao hapo awali walilazimika kufuata huduma katika ofisi za Mkoa wa KITANESCO Kigamboni.


Amesema TANESCO imefanya mabadiliko makubwa ili kuendana na ongezeko la mahitaji ya huduma ya umeme kutoka kwa wananchi hivyo ameipongeza TANESCO kwa kuanzisha ofisi hiyo nakuwataka wafanyakazi kuendelea kuimarisha utoaji wa huduma bora zaidi kwa wananchi.


“Napenda kuupongeza uongozi wa TANESCO kwa kuanzisha ofisi hii kwani ni kielelezo cha maboresho ya kiutendaji inayolenga kuongeza ufanisi na kupunguza kero na kuhakikisha wananchi wanapata huduma kwa wakati”


Akizungumza Kaimu Meneja Huduma kwa Wateja, Bw. Shamu Lameck, amesema TANESCO imejipanga kikamilifu na inaendelea kuimarisha na kusogeza huduma zake kwa wateja ili kuwarahisishia wananchi kupata huduma za umeme.


“Hii ni sehemu mhimu sana, ni ishara kwamba TANESCO tumedhamilia kwamba hali ya upatiakanaji wa umeme Kigamboni unaimarika na huduma yenyewe pia,tumejipanga kuhakikisha kwamba wananchi na wateja wetu tunawahudumia kwa ukaribu na ubora zaidi.


Kwa upande wake, Meneja wa TANESCO Mkoa wa Kigamboni Mhandisi Paschal Luhavi amesema kuwepo kwa ofisi hiyo ya TANESCO Wilaya ya Mikwambe kunakwenda kusogeza huduma zaidi kwa wananchi ndani ya wilaya hiyo hasa maeneo ya kata za Kimbiji, Somangila, Pemba Mnazi na Kisarawe II na maeneo jirani.






SERIKALI KUENDELEA KUIMARISHA UWEZO WA KUZUIA,KUJIANDAA,KUKABILIANA NA MAAFA

May 17, 2026 Add Comment


Na Mwandishi wetu- MBEYA


Serikali imeendelea kuimarisha uwezo wa Kitaifa wa Kuzuia, Kujiandaa, Kukabiliana na Kurejesha hali baada ya maafa ili kuhakikisha wananchi wanaishi katika mazingira salama ya  kuepuka madhara makubwa yatokanayo na maafa.

Kauli hiyo imetolewa na Katibu Tawala Msaidizi Mipango na Uratibu Ofisi ya Mkoa wa Mbeya, Dkt. Noah Sikwese wakati akifunga mafunzo kwa Wajumbe Wateule wa Timu ya Kukabiliana na Dharura (RERT), Waatalamu wa Unendeshaji wa Kituo cha Operesheni na Mawasiliano ya Dharura (REOCC) katika Mkoa huo yaliyoandaliwa na Ofisi ya Waziri Mkuu kupitia Idara ya Menejimenti ya Maafa.

Dkt. Sikwese, amesema timu za kukabiliana na dharura zimejengewa msingi muhimu wa utendaji utakaowezesha Mkoa kuwa na uwezo wa kujiandaa na kukabiliana na matukio ya dharura kwa haraka  na ufanisi mkubwa .

“Timu hizi zitahusika katika kufanya tathmini za awali na za kina wakati wa maafa kubaini mahitaji halisi ya waathirika, pamoja na kuratibu upatikanaji wa rasilimali muhimu kwa ajili ya kukabiliana na athari za maafa,” alisema Dkt. Sikwese.


Pia, aliongeza kwamba mafunzo yamekuwa nyenzo muhimu katika kujenga na kuimarisha uwezo wa kitaalamu na kiutendaji kwa watumishi wanaohusika katika Kituo cha Operesheni na Mawasiliano ya dharura.

“Kuanzishwa kwa Kituo cha Operesheni na Mawasiliano ya Dharura Mkoa wa Mbeya ni hatua muhimu katika kuimarisha uratibu wa shughuli za usimamizi wa maafa. Kituo hiki kitawezesha ufuatiliaji wa matukio  kwa ukaribu, ukusanyaji na uchambuzi wa taarifa kwa wakati, pamoja na kuimarisha mawasiliano miongoni mwa wadau,” alieleza.

Sambamba na hilo Dkt. Sikwese alifafanua kuwa, utekelezaji wa mafunzo hayo ulianza katika Mikoa a Mwanza, Arusha, Dodoma, ambapo hatua za kuanzisha Vituo vya Operesheni na Mawasiliano ya Dharura pamoja na kuimarisha Timu za kukabiliana  na maafa zilianza kutekelezwa.


“Ni matarajio yangu mafunzo haya yataongeza ufanisi, uwajibikaji, ustahimilivu dhidi ya majanga katika Mkoa wetu wa Mbeya,”aliongeza.

Aidha, alitoa wito kwa wataalamu wote waliopatiwa mafunzo kuendelea kuyafanyia kazi maarifa na stadi, kudumisha nidhamu ya kazi na kujenga utamaduani wa ushirikiano wa kitaalamu huku akiwasisitiza kuendelea kufanya mazoezi ya mara kwa mara ya uokoaji na  utoaji wa huduma ya kwanza kwa majeruhi au waliofikwa na maafa.

“Usimamizi wa maafa ni jukumu letu sote, kila mmoja ashiriki sasa na kuchukua hatua katika eneo lake ili kuokoa na kulinda maisha, mali na mazingira,” alisisitiza Dkt. Sikwese.


Ikumbukwe kuwa Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu) kwa mujibu wa Sera ya Taifa ya Usimamizi wa Maafa yam waka 2004 (Toleo la 2025) pamoja na Sheria ya Usimamizi wa Maafa Na. 6 ya mwaka 202 imeipa jukumu la kuratibu masuala yote ya usimamizi wa maafa nchini.






MWISHO

AZZA HILAL AZUNGUMZA NA WANANCHI, AKAGUA MIRADI ITWANGI

May 17, 2026 Add Comment

   Mbunge wa Jimbo la Itwangi mkoani Shinyanga, Mhe. Azza Hilal Hamad akiwashukuru wananchi wa Kijiji cha Igalamya, Kata ya Usule kwa imani yao ya kumchagua yeye kuwa Mbunge, Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwa Rais pamoja na madiwani wao katika uchaguzi mkuu. Picha na Kadama Malunde - Malunde 1 blog

Mbunge wa Jimbo la Itwangi mkoani Shinyanga, Mhe. Azza Hilal Hamad akisalimiana na mkazi wa kijiji cha Bunonga kata ya Mwamala wakati wa ziara yake jimboni
Mbunge wa Jimbo la Itwangi mkoani Shinyanga, Mhe. Azza Hilal Hamad akizungumza katika Zahanati ya  kijiji cha Bunonga kata ya Mwamala ambayo upauaji wake umeanza
Burudani ya ngoma ya Ugoyangi ikiendelea wakati wa ziara ya Mbunge wa Jimbo la Itwangi mkoani Shinyanga, Mhe. Azza Hilal Hamad katika Kijiji cha Igalamya, Kata ya Usule.

Na Kadama Malunde - Malunde 1 blog

Mbunge wa Jimbo la Itwangi mkoani Shinyanga, Mhe. Azza Hilal Hamad ameanza ziara maalum ya kuwashukuru wananchi kwa imani kubwa waliyoionesha kwa kumchagua kuwa Mbunge wa jimbo hilo pamoja na kumchagua Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan na madiwani wa Chama Cha Mapinduzi (CCM).

MWENGE WAPITA NYASA,MRADI WA REA WA BILIONI 4 WAZINDULIWA

May 16, 2026 Add Comment


*📌Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa aridhishwa na miradi ya REA*


📍Nyasa - Ruvuma


Wananchi wa Kitongoji cha Ndecha Wilaya ya Nyasa mkoani Ruvuma wameanza kushuhudia mwanga wa matumaini baada ya kuzinduliwa rasmi kwa mradi wa REA kwa gharama ya zaidi ya shilingi bilioni 4.17 wa kusambaza umeme unaotekelezwa kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA), mradi ambao unatarajiwa kuleta mageuzi makubwa ya kiuchumi na kijamii kwa wananchi wa eneo hilo.


Mradi huo umezinduliwa leo tarehe 16 Mei, 2026 na Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa, Ndugu  Wazo Michael Mwang’onda, ambaye amesema kuwa dhamira ya Serikali ni kuhakikisha wananchi wa vijijini wanapata huduma bora za nishati ili kuboresha maisha yao na kuchochea maendeleo ya Taifa.


Halikadhalika Bw. Mwang'onda  amewataka wananchi kutumia nafasi hiyo ya mradi kulipa shilingi 27,000 tu ili waweze kuwekewa umeme huo. 


“Tunataka kuona wananchi wanalipia 27,000 ili wawekewe umeme hata ukiuza kuku mmoja 27,000 unaenda kuweka umeme kwenye nyumba yako sio 300,000 kama ilivyokuwa hapo zamani'' amesema Kiongozi wa Mwenge kitaifa. 

Kwa upande wake, Msimamizi wa Miradi ya REA Mkoa wa Ruvuma, Mha. Hamisi  Mrope, amesema mradi wa kusambaza umeme vijijini (REDP2C) katika Wilaya ya Nyasa unalenga kufikisha huduma ya umeme katika vitongoji vyote ili kuinua maisha ya wananchi na kuchochea maendeleo ya kiuchumi na kijamii.

Aidha, Mha. Mrope amesema mradi huo ulianza rasmi tarehe 16 Novemba 2023 na unatarajiwa kukamilika  ifikapo mwezi Oktoba, 2026, huku ukihusisha vitongoji 30, mashine umba 30 pamoja na wateja 1,247 kwa gharama ya zaidi ya shilingi bilioni 4.17.

Katika Kitongoji cha Ndecha pekee, mradi umehusisha ujenzi wa kilomita 8.43 za njia ya umeme, ufungaji wa mashine umba mbili pamoja na kuunganisha wateja 94 kwa gharama ya zaidi ya shilingi milioni 307.6. Hadi sasa, miundombinu imekamilika kwa asilimia 100 huku wananchi 56 tayari wakiwa wameunganishiwa huduma ya umeme kwa gharama nafuu ya shilingi 27,000 kwa kila mteja.


Mradi huo unatekelezwa na Mkandarasi mzawa MF Electrical Engineering Ltd chini ya usimamizi wa TANESCO.

Naye, Mbunge wa jimbo  la Nyasa Mhe. John Nchimbi amesema miradi ya REA imesaidia kwa sasa vijiji vyote 84 vya wilaya Nyasa kupata huduma ya umeme huku Tanzana ikijivunia kuwa ya pili Afrika Mashariki kwa kusambaza umeme.


Kwa upande wake, Mkandarasi wa mradi huo MF Electrical Engineering Ltd mhandisi Mussa David amesema mradi huo kwa kitongoji cha Ndecha 1 wameshafikisha umeme na wameshawasha nyumba 56.

Wananchi wa Ndecha wameeleza furaha yao kutokana na ujio wa umeme ambapo mwenyekiti wa kijiji cha Linda Antony Nkoma amesema  sasa wataweza kufanya shughuli zao za kiuchumi kwa ufanisi zaidi tofauti na zamani walipotegemea taa za vibatari na vyanzo vya nishati visivyo salama.


Uzinduzi wa mradi huo umeonekana kuwa hatua muhimu katika safari ya kuwaletea wananchi maendeleo endelevu huku ukiunga mkono kaulimbiu ya Mwenge wa Uhuru 2026 isemayo:


“Tanzania ni Yetu Sote, Tushikamane kwa Pamoja Kuleta Maendeleo.”


Mwisho

SERIKALI KUIMARISHA NISHATI YA UMEME WILAYANI KONDOA

May 16, 2026 Add Comment




Katika jitihada za kuendeleza ustawi wa wananchi na kuchochea uchumi wa maeneo ya vijijni na vitongojini, Serikali inaendelea kuimarisha upatikanaji wa umeme wilayani Kondoa kupitia mpango wa kusambaza umeme katika vitongoji vyote vya wilaya hiyo.


 Mpaka sasa vitongoji 113 vina umeme huku kukiwa na mradi unaoendelea wa kupeleka umeme katika vitongoji 60.


Hayo yameelezwa leo Mei 16, 2026 na Naibu Waziri wa Nishati Mhe. Salome Makamba wakati wa ziara ya kikazi ya Waziri Mkuu Mhe. Dkt Mwigulu Nchemba wilayani Kondoa, Dodoma.

Mhe. Salome ameeleza kwamba katika mradi wa umeme unaotekelezwa sasa wa kusambaza umeme katika vitongoji 60 zaidi ya shilingi billion 21 imetengwa kuhakikisha mradi huo unakamilika ambapo kukamilika kwake kutafanya  Kondoa kubakiwa na vitongoji 88 tu ambavyo havina umeme  vitakavyofikiwa na huduma hiyo ifikapo mwaka 2030.


Pia Mhe Salome ameeleza kwamba Serikali imetenga zaidi ya shilingi milioni 752 kwa ajili ya  kuhakikisha wananchi ambao miradi ya umeme inapita karibu na nyumba zao  wanafikiwa na huduma ya umeme katika kaya zao.


Ameongeza kuwa katika Wilaya ya Kondoa,  Wizara ya Nishati ina mpango wa kubadilisha nguzo zote chakavu na kupeleka nguzo za zege ili kuhakikisha wilaya hiyo inakuwa na nishati ya umeme ya uhakika ili wananchi waendelee kufanya shughuli zao za kiuchumi kama vile uendeshaji wa viwanda vidogo na shughuli za kijamii.

Vilevile amesema Serikali ina mpango mahsusi kujenga laini kubwa ya umeme ili kuimarisha na kutatua changamoto ya nguvu ya umeme (Low Voltage katika Jimbo la Kondoa).


Katika hatua nyingine, Mhe. Salome amewaasa wananchi kuendelea kutumia nishati safi ya kupikia akieleza kuwa pamoja na jitihada zinazofanywa na Wananchi Kondoa  kutunza misitu bado wanatakiwa kuilinda kwa kuachana na matumizi ya Kuni na mkaa na kuhamia katika matumizi ya nishati safi ya kupikia kama vile gesi, umeme na mkaa mbadala 


“Niwahakikishie wanakondoa sasa hivi Serikali imeweka ruzuku katika mitungi ya gesi, hivyo niwaombee sana tuanze kutumia Nishati safi kwa ajili ya kulinda  afya, mazingira na kuokoa muda wa kukaa jikoni ili tuweze kujiendeleza kiuchumi lakini pia tutumie nishati nyingine kama mkaa mbadala usiotoa moshi ambapo utatumia mkaa kidogo kupika chakula kingi na katika hali iliyo bora zaidi." Amesisitiza  Mhe Salome.

TANZANIA NI NCHI YA PILI AFRIKA KUWA NA HADHI YA UTALII WA JIOLOJIA (GEOPARK MUSEUM)

May 16, 2026 Add Comment
-Ni kutokana na kuwa na hadhi ya Ngorongoro Lengai UNESCO Global Geopark;

DKT. KOMBA: TEHAMA NI MSINGI WA ELIMU YA KISASA

May 16, 2026 Add Comment
NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

TAASISI ya Elimu Tanzania (TET) imezindua maabara za kompyuta katika Shule ya Sekondari Kimara pamoja na Shule ya Msingi Mkwawa jijini Dar es Salaam ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 50 ya taasisi hiyo na jitihada za kuimarisha matumizi ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) katika sekta ya elimu.

DKT.MIGIRO AIMARISHA USHIRIKIANO KIMATAIFA NA MABALOZI WA CUBA, VIETNAM, NA UN

May 16, 2026 Add Comment
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi, Dkt. Asha-Rose Migiro, kwa nyakati tofauti amekutana na kufanya mazungumzo na mabalozi wawili wanaoziwakilisha nchi zao katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

KAPINGA: SERIKALI YA RAIS SAMIA INAENDELEA KUBORESHA ELIMU, AFYA NA KILIMO MBINGA VIJIJINI

May 16, 2026 Add Comment
Mbunge wa Jimbo la Mbinga vijijini na Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe. Judith Kapinga amesema Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan, inaendelea kuleta mageuzi makubwa katika sekta za elimu na afya hasa maeneo ya Jimbo hilo kupitia utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo.

BODI YA TVLA YARIDHISHWA NA KASI YA UJENZI WA MAABARA YA KISASA DODOMA

May 16, 2026 Add Comment
Daudi Nyingo – DODOMA

Bodi ya Ushauri ya Wakala ya Maabara ya Veterinari Tanzania (TVLA) imeeleza kuridhishwa kwake na maendeleo ya mradi mkubwa wa ujenzi wa jengo la ofisi na maabara ya kisasa unaotekelezwa katika Kituo cha Kanda ya Kati jijini Dodoma ambapo Mradi huo wenye ghorofa nne unategemewa kuwa mradi kielelezo nchini utakapokamilika.

TBS inaadhimisha nusu karne,Inajivunia mafanikio ya utekelezaji wa majukumu yake kwa ufanisi

May 15, 2026 Add Comment
NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Viwango Tanzania (TBS), Dkt. Ashura Katunzi, amesema katika kipindi cha miaka 50 Shirika hilo limefanikiwa kujenga na kusimamia mifumo ya udhibiti ubora na usalama wa bidhaa nchini hatua iliyosaidia kuongeza tija katika uchumi na sekta ya Viwanda na Biashara kwa ujumla.

SERIKALI YAISIFU CRDB KWA KUKUZA UWEKEZAJI WA VIJANA

May 15, 2026 Add Comment

 



Na Mwandishi Wetu, Arusha.

Serikali imeipongeza Benki ya CRDB Bank Plc kwa juhudi zake za kuhamasisha uwekezaji nchini kupitia elimu ya fedha, uwekezaji wa hisa na uwezeshaji wa kiuchumi unaolenga kuwajenga vijana kuwa wawekezaji wa baadaye.

Pongezi hizo zimetolewa jana jijini Arusha na Waziri wa Fedha, Khamis Mussa Omar wakati akifungua Semina ya Wanahisa wa Benki ya CRDB iliyofanyika sambamba na Mkutano Mkuu wa 31 wa mwaka wa benki hiyo katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Arusha (AICC).

Semina hiyo ilikuwa na kaulimbiu isemayo “Vijana na Uwekezaji kwenye Hisa” na iliwakutanisha viongozi wa serikali, wanahisa, wataalamu wa masoko ya mitaji pamoja na vijana kutoka maeneo mbalimbali nchini.

Akizungumza katika semina hiyo, Waziri Omar alisema vijana wanapaswa kushiriki kikamilifu katika umiliki wa uchumi kupitia uwekezaji badala ya kutegemea ajira pekee.

“Kaulimbiu ya mwaka huu imebeba ujumbe mkubwa wa kimkakati kwa taifa letu. Vijana hawapaswi kuishia kutafuta ajira pekee, bali wanastahili kushiriki katika umiliki wa uchumi kupitia uwekezaji,” alisema Waziri Omar.

Aidha, aliipongeza benki hiyo kwa hatua ya kufungua Ofisi ya Uwakilishi Dubai, akisema hatua hiyo imeongeza hadhi ya Tanzania katika sekta ya fedha na uwekezaji kimataifa.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela alisema benki hiyo itaendelea kuwawezesha vijana kupitia huduma za kifedha, ubunifu na programu za maendeleo ya ujasiriamali.

Alisema kupitia CRDB Bank Foundation na programu ya IMBEJU, maelfu ya vijana na wafanyabiashara wadogo wamefikiwa kwa mafunzo, mitaji na ushauri wa biashara.

“Tunaamini vijana wa leo si wateja tu wa benki yetu, bali ni wawekezaji, wabunifu na viongozi wa uchumi wa kesho,” alisema Dkt. Nsekela.

Naye Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya CRDB, Neema Mori alisema uwekezaji katika hisa ni njia muhimu ya kujenga ustawi wa kifedha wa muda mrefu kwa vijana na familia za Kitanzania.

Profesa Mori alisema mafanikio ya Benki ya CRDB yanaonyesha namna uwekezaji wa muda mrefu unavyoweza kuleta matokeo chanya kwa wanahisa.

Alibainisha kuwa ndani ya miaka mitatu iliyopita thamani ya hisa za benki hiyo imeongezeka kwa zaidi ya asilimia 253, huku bei ya hisa ikifikia wastani wa Sh2,800 kutoka Sh460 mwaka 2023.

Aidha, alisema bodi ya wakurugenzi inapendekeza gawio la Sh90 kwa kila hisa kutokana na matokeo mazuri ya kifedha ya mwaka 2025, ikiwa ni ongezeko la asilimia 38 ikilinganishwa na mwaka uliopita.

Profesa Mori aliwahamasisha wazazi kuanza kuwawekezea watoto wao hisa mapema ili kuwajengea msingi imara wa maisha ya kifedha ya baadaye.

Benki ya CRDB ni miongoni mwa taasisi kubwa za kifedha Afrika Mashariki na Kati, ikiwa na zaidi ya wateja milioni sita katika nchi za Tanzania, Burundi na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo pamoja na ofisi ya uwakilishi Dubai, Falme za Kiarabu.
Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), akizungumza wakati akifungua Semina ya Wanahisa wa Benki ya CRDB katika Mkutano Mkuu wa 31 wa Wanahisa, uliobeba kauli mbiu ya “Vijana na Uwekezaji kwenye Hisa”, semina inayofanyika katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Arusha (AICC), ambapo alitoa wito kwa Taasisi za Fedha nchini kupunguza riba na gharama nyingine za mikopo ili kuwawezesha wananchi wakiwemo vijana kupata mitaji ya kuwekeza kwenye shughuli zao za kiuchumi.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dkt. Abdulmajid Nsekela, akizungumza wakati wa hafla ya ufunguzi wa Semina ya Wanahisa wa Benki ya CRDB katika Mkutano Mkuu wa 31 wa Wanahisa hao, uliobeba kauli mbiu ya “Vijana na Uwekezaji kwenye Hisa”, uliofunguliwa na Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb) (hayupo pichani), uliofanyika katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Arusha (AICC).
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya CRDB, Prof. Neema Mori, akizungumza wakati wa hafla ya ufunguzi wa Semina ya Wanahisa wa Benki ya CRDB katika Mkutano Mkuu wa 31 wa Wanahisa hao, uliobeba kauli mbiu ya “Vijana na Uwekezaji kwenye Hisa”, uliofunguliwa na Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb) (hayupo pichani), uliofanyika katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Arusha (AICC).