HABARI

SIASA

ELIMU

Recent Posts

DKT.MIGIRO AIMARISHA USHIRIKIANO KIMATAIFA NA MABALOZI WA CUBA, VIETNAM, NA UN

May 16, 2026 Add Comment
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi, Dkt. Asha-Rose Migiro, kwa nyakati tofauti amekutana na kufanya mazungumzo na mabalozi wawili wanaoziwakilisha nchi zao katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

KAPINGA: SERIKALI YA RAIS SAMIA INAENDELEA KUBORESHA ELIMU, AFYA NA KILIMO MBINGA VIJIJINI

May 16, 2026 Add Comment
Mbunge wa Jimbo la Mbinga vijijini na Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe. Judith Kapinga amesema Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan, inaendelea kuleta mageuzi makubwa katika sekta za elimu na afya hasa maeneo ya Jimbo hilo kupitia utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo.

BODI YA TVLA YARIDHISHWA NA KASI YA UJENZI WA MAABARA YA KISASA DODOMA

May 16, 2026 Add Comment
Daudi Nyingo – DODOMA

Bodi ya Ushauri ya Wakala ya Maabara ya Veterinari Tanzania (TVLA) imeeleza kuridhishwa kwake na maendeleo ya mradi mkubwa wa ujenzi wa jengo la ofisi na maabara ya kisasa unaotekelezwa katika Kituo cha Kanda ya Kati jijini Dodoma ambapo Mradi huo wenye ghorofa nne unategemewa kuwa mradi kielelezo nchini utakapokamilika.

TBS inaadhimisha nusu karne,Inajivunia mafanikio ya utekelezaji wa majukumu yake kwa ufanisi

May 15, 2026 Add Comment
NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Viwango Tanzania (TBS), Dkt. Ashura Katunzi, amesema katika kipindi cha miaka 50 Shirika hilo limefanikiwa kujenga na kusimamia mifumo ya udhibiti ubora na usalama wa bidhaa nchini hatua iliyosaidia kuongeza tija katika uchumi na sekta ya Viwanda na Biashara kwa ujumla.

SERIKALI YAISIFU CRDB KWA KUKUZA UWEKEZAJI WA VIJANA

May 15, 2026 Add Comment

 



Na Mwandishi Wetu, Arusha.

Serikali imeipongeza Benki ya CRDB Bank Plc kwa juhudi zake za kuhamasisha uwekezaji nchini kupitia elimu ya fedha, uwekezaji wa hisa na uwezeshaji wa kiuchumi unaolenga kuwajenga vijana kuwa wawekezaji wa baadaye.

Pongezi hizo zimetolewa jana jijini Arusha na Waziri wa Fedha, Khamis Mussa Omar wakati akifungua Semina ya Wanahisa wa Benki ya CRDB iliyofanyika sambamba na Mkutano Mkuu wa 31 wa mwaka wa benki hiyo katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Arusha (AICC).

Semina hiyo ilikuwa na kaulimbiu isemayo “Vijana na Uwekezaji kwenye Hisa” na iliwakutanisha viongozi wa serikali, wanahisa, wataalamu wa masoko ya mitaji pamoja na vijana kutoka maeneo mbalimbali nchini.

Akizungumza katika semina hiyo, Waziri Omar alisema vijana wanapaswa kushiriki kikamilifu katika umiliki wa uchumi kupitia uwekezaji badala ya kutegemea ajira pekee.

“Kaulimbiu ya mwaka huu imebeba ujumbe mkubwa wa kimkakati kwa taifa letu. Vijana hawapaswi kuishia kutafuta ajira pekee, bali wanastahili kushiriki katika umiliki wa uchumi kupitia uwekezaji,” alisema Waziri Omar.

Aidha, aliipongeza benki hiyo kwa hatua ya kufungua Ofisi ya Uwakilishi Dubai, akisema hatua hiyo imeongeza hadhi ya Tanzania katika sekta ya fedha na uwekezaji kimataifa.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela alisema benki hiyo itaendelea kuwawezesha vijana kupitia huduma za kifedha, ubunifu na programu za maendeleo ya ujasiriamali.

Alisema kupitia CRDB Bank Foundation na programu ya IMBEJU, maelfu ya vijana na wafanyabiashara wadogo wamefikiwa kwa mafunzo, mitaji na ushauri wa biashara.

“Tunaamini vijana wa leo si wateja tu wa benki yetu, bali ni wawekezaji, wabunifu na viongozi wa uchumi wa kesho,” alisema Dkt. Nsekela.

Naye Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya CRDB, Neema Mori alisema uwekezaji katika hisa ni njia muhimu ya kujenga ustawi wa kifedha wa muda mrefu kwa vijana na familia za Kitanzania.

Profesa Mori alisema mafanikio ya Benki ya CRDB yanaonyesha namna uwekezaji wa muda mrefu unavyoweza kuleta matokeo chanya kwa wanahisa.

Alibainisha kuwa ndani ya miaka mitatu iliyopita thamani ya hisa za benki hiyo imeongezeka kwa zaidi ya asilimia 253, huku bei ya hisa ikifikia wastani wa Sh2,800 kutoka Sh460 mwaka 2023.

Aidha, alisema bodi ya wakurugenzi inapendekeza gawio la Sh90 kwa kila hisa kutokana na matokeo mazuri ya kifedha ya mwaka 2025, ikiwa ni ongezeko la asilimia 38 ikilinganishwa na mwaka uliopita.

Profesa Mori aliwahamasisha wazazi kuanza kuwawekezea watoto wao hisa mapema ili kuwajengea msingi imara wa maisha ya kifedha ya baadaye.

Benki ya CRDB ni miongoni mwa taasisi kubwa za kifedha Afrika Mashariki na Kati, ikiwa na zaidi ya wateja milioni sita katika nchi za Tanzania, Burundi na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo pamoja na ofisi ya uwakilishi Dubai, Falme za Kiarabu.
Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), akizungumza wakati akifungua Semina ya Wanahisa wa Benki ya CRDB katika Mkutano Mkuu wa 31 wa Wanahisa, uliobeba kauli mbiu ya “Vijana na Uwekezaji kwenye Hisa”, semina inayofanyika katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Arusha (AICC), ambapo alitoa wito kwa Taasisi za Fedha nchini kupunguza riba na gharama nyingine za mikopo ili kuwawezesha wananchi wakiwemo vijana kupata mitaji ya kuwekeza kwenye shughuli zao za kiuchumi.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dkt. Abdulmajid Nsekela, akizungumza wakati wa hafla ya ufunguzi wa Semina ya Wanahisa wa Benki ya CRDB katika Mkutano Mkuu wa 31 wa Wanahisa hao, uliobeba kauli mbiu ya “Vijana na Uwekezaji kwenye Hisa”, uliofunguliwa na Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb) (hayupo pichani), uliofanyika katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Arusha (AICC).
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya CRDB, Prof. Neema Mori, akizungumza wakati wa hafla ya ufunguzi wa Semina ya Wanahisa wa Benki ya CRDB katika Mkutano Mkuu wa 31 wa Wanahisa hao, uliobeba kauli mbiu ya “Vijana na Uwekezaji kwenye Hisa”, uliofunguliwa na Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb) (hayupo pichani), uliofanyika katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Arusha (AICC).









MRADI WA BARRICK-TWIGA FUTURE FORWARD EDUCATION KUBORESHA SEKTA YA ELIMU TANZANIA

May 15, 2026 Add Comment

Meneja Mkazi wa Barrick nchini Dkt. Melkiory Ngido (kulia) akiweka Jiwe la Msingi la Ujenzi wa Mabweni mawili, vyumba vitano vya madarasa na vyoo matundu nane shule ya sekondari Nyang'hwale
Meneja Mkazi wa Barrick nchini Dkt. Melkiory Ngido (kulia) akiwa na viongozi mbalimbali wakati wa hafla ya uwekaji Jiwe la Msingi la Ujenzi wa Mabweni mawili, vyumba vitano vya madarasa na vyoo matundu nane shule ya sekondari Nyang'hwale.
Muonekano wa sehemu ya madarasa
Muonekano wa sehemu ya vyoo
Meneja Mkazi wa Barrick nchini Dkt. Melkiory Ngido (kulia) akizungumza wakati akiweka Jiwe la Msingi la Ujenzi wa Mabweni mawili, vyumba vitano vya madarasa na vyoo matundu nane shule ya sekondari Nyang'hwale.

TADB YATOA GAWIO LA BILIONI 8.38 KWA SERIKALI

May 15, 2026 Add Comment
Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) imetoa gawio la shilingi Bilioni 8.38 kwa serikali ikiwa ni ongezeko la Asilimia 50 kutoka shilingi Bilioni 5.58 ya mwaka 2024, katika Mkutano Mkuu wa wanahisa kwa mwaka ulioishia 31 Desemba 2025.

TBS YASHIRIKI MKUTANO WA 28 WA VIWANGO AFRIKA MASHARIKI

May 15, 2026 Add Comment
Shirika la Viwango Tanzania (TBS) limeshiriki Mkutano wa 28 wa Kamati ya Viwango Afrika Mashariki (EASC) uliofanyika Makao Makuu ya Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) jijini Arusha kuanzia Mei 12 hadi 14, 2026, kwa lengo la kutekeleza mpango kazi wa viwango, upimaji, metrolojia na ubora wa bidhaa (SQMT).

NAIBU KATIBU MKUU FEDHA AAGIZA UJENZI WA MCHAKATO WA UTEKELEZAJI WA MAJUKUMU (BUSINESS PROCESSES) ZA KIDIGITALI

May 15, 2026 Add Comment

Mkurugenzi wa Idara ya Usimamizi wa Mali za Serikali, Wizara ya Fedha, Bw. Chotto Sendo, akizungumza kwa niaba ya Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Fedha, Bw. Nsubili Joshua, wakati akifungua mafunzo kwa Menejimenti ya Wizara kuhusu Mwongozo wa Udhibiti wa Ndani wa Wizara ya Fedha, yaliyofanyika katika Hotel ya Morena mkoani Morogoro.

Meza Kuu ikiongozwa na Mkurugenzi wa Idara ya Usimamizi wa Mali za Serikali, Wizara ya Fedha, Bw. Chotto Sendo (katikati), Kaimu Mkaguzi wa Ndani Mkuu wa Serikali, Wizara ya Fedha, Bw. Kenneth Nindie (kushoto), na Mhasibu Mkuu Wizara ya Fedha Fungu 21 CPA. Sostheness Mafuru (kulia) wakifuatilia mawasilisho mbalimbali yaliyotolewa na Wawezeshaji kutoka Kampuni ya Ushauri (KPMG) wakati wa mafunzo ya Mwongozo wa Udhibiti wa Ndani wa Wizara ya Fedha, yaliyohusisha Menejimenti ya Wizara ya Fedha na Watumishi wa Wizara hiyo yaliyofanyika katika Hotel ya Morena mkoani Morogoro.

Mkaguzi Mkuu wa Ndani wa Wizara ya Fedha CPA, Evalisto Mwalongo, akitoa utambulisho wakati wa mafunzo ya Mwongozo wa Udhibiti wa Ndani wa Wizara ya Fedha, yaliyohusisha Menejimenti ya Wizara ya Fedha na Watumishi wa Wizara hiyo yaliyofanyika katika Hotel ya Morena mkoani Morogoro.

Baadhi ya viongozi wa Idara, Vitengo na Watumishi wa Wizara ya Fedha, wakifuatilia hotuba ya mgeni rasmi (hayupo pichani), wakati wa mafunzo ya Mwongozo wa Udhibiti wa Ndani wa Wizara ya Fedha, yaliyohusisha Menejimenti ya Wizara ya Fedha na Watumishi wa Wizara hiyo yaliyofanyika katika Hotel ya Morena mkoani Morogoro.

Baadhi ya Watumishi wa Wizara ya Fedha wakifuatilia hotuba ya mgeni rasmi (hayupo pichani), wakati wa mafunzo ya Mwongozo wa Udhibiti wa Ndani wa Wizara ya Fedha, yaliyohusisha Menejimenti ya Wizara ya Fedha na Watumishi wa Wizara hiyo yaliyofanyika katika Hotel ya Morena mkoani Morogoro.

Meza kuu ikiongozwa na Mkurugenzi wa Idara ya Usimamizi wa Mali za Serikali, Wizara ya Fedha, Bw. Chotto Sendo (katikati), Kaimu Mkaguzi wa Ndani Mkuu wa Serikali, Wizara ya Fedha, Bw. Kenneth Nindie (kulia), na Mhasibu Mkuu Fungu 21 Wizara ya Fedha, CPA. Sostheness Mafuru (kushoto) wakiwa katika picha ya pamoja na Menejimenti ya Wizara ya Fedha baada ya kumalizika kwa mafunzo ya Mwongozo wa Udhibiti wa Ndani wa Wizara ya Fedha, yaliyohusisha Menejimenti ya Wizara ya Fedha na Watumishi wa Wizara hiyo yaliyofanyika katika Hotel ya Morena mkoani Morogoro.

Meza kuu ikiongozwa na Mkurugenzi wa Idara ya Usimamizi wa Mali za Serikali, Wizara ya Fedha, Bw. Chotto Sendo (katikati), Kaimu Mkaguzi wa Ndani Mkuu wa Serikali, Wizara ya Fedha, Bw. Kenneth Nindie (kulia), na Mhasibu Mkuu Fungu 21, Wizara ya Fedha CPA. Sostheness Mafuru (kushoto) wakiwa katika picha ya pamoja na Watumishi wa Wizara ya Fedha baada ya kumalizika kwa mafunzo ya Mwongozo wa Udhibiti wa Ndani wa Wizara ya Fedha, yaliyohusisha Menejimenti ya Wizara ya Fedha na Watumishi wa Wizara hiyo yaliyofanyika katika Hotel ya Morena mkoani Morogoro.

Meza kuu ikiongozwa na Mkurugenzi wa Idara ya Usimamizi wa Mali za Serikali, Wizara ya Fedha, Bw. Chotto Sendo (katikati), Kaimu Mkaguzi wa Ndani Mkuu wa Serikali, Wizara ya Fedha Bw. Kenneth Nindie (kulia), na Mhasibu Mkuu Fungu 21 Wizara ya Fedha CPA. Sostheness Mafuru (kushoto) wakiwa katika picha ya pamoja na Sekretarieti ya maandalizi, baada ya kumalizika kwa mafunzo ya Mwongozo wa Udhibiti wa Ndani wa Wizara ya Fedha, yaliyohusisha Menejimenti ya Wizara ya Fedha na Watumishi wa Wizara hiyo yaliyofanyika katika Hotel ya Morena mkoani Morogoro.

(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, WF, Morogoro)


Na. Chedaiwe Msuya, WF, Morogoro


Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Fedha, Bw. Nsubili Joshua, amekiagiza Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini cha Wizara ya Fedha kuratibu ujenzi wa mchakato wa utekelezaji wa majukumu (business processes) za kidigitali ili kuongeza ufanisi wa utekelezaji wa majukumu ya Wizara.

Maagizo hayo yametolewa kwa niaba yake na Mkurugenzi wa Idara ya Usimamizi wa Mali za Serikali, Wizara ya Fedha, Bw. Chotto Sendo, wakati akifungua mafunzo mafunzo ya Mwongozo wa Udhibiti wa Ndani wa Wizara ya Fedha, kwa
Menejimenti ya Wizara hiyo, yaliyofanyika katika Hotel ya Morena mkoani Morogoro.

Alisema business processes mpya zinazotakiwa ni pamoja na ufuatiliaji wa Mfumo wa Ununuzi (NeST), ufuatiliaji na udhibiti wa mapato kupitia big data analysis, ufuatiliaji wa miradi ya PPP, miradi ya alternative financing, ulipaji wa michango ya Serikali kwenye taasisi za kimataifa, na ufuatiliaji wa mapato yasiyo ya kodi.

Aidha, Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini (M&E) kimetakiwa kuhakikisha kuwa business processes hizo zinajengwa kwa mfumo wa kielektroniki ili kurahisisha ufuatiliaji na tathmini ya utekelezaji wa majukumu ya Wizara ili kuimarisha uwajibikaji, uwazi na ufanisi wa mifumo ya kiutendaji.

Bw. Sendo, alifafanua kuwa mafunzo hayo yataiwezesha Menejimenti na Watumishi wa Wizara kuelewa dhana na mbinu za udhibiti wa ndani, kujifunza namna ya kuchambua viashiria hatarishi, na kuimarisha business processes zilizopo.

“Mwongozo huu utakuwa na manufaa makubwa ikiwemo kuimarisha mifumo ya ufuatiliaji na tathmini kwa njia za kidigitali, kuwezesha Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani kufanya tathmini kwa mujibu wa Mwongozo wa Kimataifa wa Ukaguzi wa Ndani wa mwaka 2024, na kuweka vigezo vya kupima ufanisi wa mifumo ya kiutendaji”, alisisitiza Bw. Sendo.

Aliwasisitiza washiriki wa mafunzo hayo kufuatilia kwa umakini ili kuutumia Mwongozo huo kuboresha mfumo wa udhibiti wa ndani katika maeneo yao ya kazi ili kuimarisha uchumi wa taifa kupitia usimamizi bora wa rasilimali za umma.

Naye Kaimu Mkaguzi wa Ndani Mkuu wa Serikali, Wizara ya Fedha, Bw. Kenneth Nindie, alitoa rai kwa Idara zote za Serikali kuhakikisha wanatumia vizuri Mwongozo huo ili uweze kuwasaidia kuweka taratibu vizuri na malengo ya Wizara yanafikiwa kwa ufasaha.

Kwa upande wake, Mkaguzi Mkuu wa Ndani wa Serikali Msaidizi Bw. Abraham Msechu, amesema kuwa mafunzo yatasaidia Menejimenti ya Wizara kupata uelewa wa Mwongozo wa Udhibiti wa Ndani na kuimarisha mifumo ya udhibiti wa ndani.

Akizungumzia mafunzo hayo mmoja wa washiriki, Kamishna Msaidizi Idara ya Usimamizi wa Madeni, Wizara ya Fedha, Bw. Omary Khama, aliahidi kuyafanyia kazi mafunzo yote waliyopata katika Idara na Vitengo ili kufikia malengo ya Serikali katika udhibiti wa ndani.


Mafunzo hayo yamewajumuisha Menejimenti ya Wizara ya Fedha pamoja na Watumishi wa Wizara na Wawezeshaji kutoka Kampuni ya Ushauri (KPMG).

JUMUIYA YA UMOJA WA ULAYA (EU) YASHIRIKIANA NA SERIKALI KUKABILIANA NA MABADILIKO YA TABIA NCHI KIGOMA

May 15, 2026 Add Comment

       

Na Mwandishi Wetu, Dodoma.

Ofisi ya Waziri Mkuu-Sera, Bunge na Uratibu na wenye Ulemavu kupitia Idara ya Menejimenti ya Maafa kwa kushirikiana na Umoja wa Ulaya (EU) imeanza utekelezaji wa mradi wa Mwitikio wa Kikanda dhidi ya Uhamaji Unaotokana na Mabadiliko ya Tabia nchi  (Regional Responses to Climate Displacement in Subsaharan Africa- RE2CLID) unaolenga kujenga uhimilivu wa jamii zinazoishi maeneo yanayozunguka Ziwa Tanganyika mkoani Kigoma dhidi ya athari za mabadiliko ya tabia nchi.
MHE. MMUYA AONGOZA UJUMBE WA TANZANIA KWENYE MKUTANO WA MAWAZIRI WA MAAFA SADC ZIMBABWE

MHE. MMUYA AONGOZA UJUMBE WA TANZANIA KWENYE MKUTANO WA MAWAZIRI WA MAAFA SADC ZIMBABWE

May 15, 2026 Add Comment






MASVINGO – ZIMBABWE

Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Kaspar Mmuya ameongoza ujumbe wa Tanzania katika Mkutano wa Sita (6) wa Kawaida wa Kamati ya Mawaziri Wanaohusika na Usimamizi wa Maafa kwa Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge na Uratibu Mheshimiwa Profesa Palamagamba Kabudi unaofanyika Masvingo, Zimbabwe.

Aidha, Mkutano huo pamoja na masuala mengine umejadili maendeleo yaliyopatikana katika utekelezaji wa programu za kikanda na masuala ya kimkakati katika utekelezaji wa afua mbalimbali katika Usimamizi wa maafa,pia mkutano huo utatumika kama jukwaa kwa Mawaziri kuimarisha ushirikiano na Washirika wa Maendeleo wa Kimataifa na Jumuiya ya Wafadhili kuhusu uwekezaji katika Usimamizi wa Maafa ili kujenga ustahimilivu wa kikanda.

Naibu Waziri Ameongozana na mwenyeji wake ambaye ni Balozi wa Tanzania nchini Zimbabwe Mhe. CP-Suzan Kaganda, Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu, Dkt. Jim Yonazi, Mkurugenzi wa Idara ya Usimamizi wa Maafa Ofisi ya Waziri Mkuu Brig.Jenerali Hosea Ndagala, Mkurugenzi Msaidizi Urasimishaji Makazi kutoka ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Bw. Nicholaus Mwakasege, Mratibu wa Maafa Dkt. Baltazar Leba, Bw. Abubakar Juma kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,Msaidizi wa naibu waziri Bw. Blastus Kahemela, Msaidizi wa katibu mkuu Bw. Januari Kitunsi, pamoja na afisa habari Ofisi ya Waziri Mkuu, Bi. Nyamagory Kitwara.


MBEYA YANUFAIKA MAFUNZO KUJIANDAA KUKABILIANA NA MAAFA

May 15, 2026 Add Comment


Na Mwandishi wetu- MBEYA

Mkurugenzi msaidizi wa Kituo cha Taifa cha Operesheni na Mawasiliano  ya Dharura kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu Bi. Jane Kikunya amewataka Wajumbe wa Timu  ya kukabiliana na Dharura na Uendeshaji  wa Kitio  cha Operesheni  na Mawasiliano  ya Dharura ya  Mkoa wa  Mbeya kufanya kazi kwa ushirikiano, mshikamano na mawasiliano ya karibu ili kutekeleza wajibu wao kwa weledi na ufanisi unaotakiwa.

Mkurugenzi huyo, ameyasema hayo wakati akifungua mafunzo ya siku tano yanayolenga kuziandaa timu za kukabiliana na Maafa za Mkoa huo.

Aidha, mafunzo hayo  ambayo yaliyoandaliwa na Ofisi ya Waziri Mkuu yanatolewa kwa Wajumbe wa Kamati ya Wataalamu ya Usimamizi  wa Maafa, Wajumbe wateule wa Timu ya kukabiliana na Dharura ya Mkoa na wataalamu wa Kituo cha Operesheni na Mawasiliano ya Dharura, Waratibu wa Maafa Mkoa na Halmashauri.

Vilevile, Bi. Jane amesema mafunzo hayo yatakuwa mhimili muhimu katika kuhakikisha Mkoa unajiandaa vyema ili kukabiliana na matukio ya dharura kwa haraka hivyo ni lazima timu lengwa ifanye kazi kwa mshikamano ili kuleta ufanisi unaohitajika.

Kwa upande wao  wanufaika wa mafunzo hayo wameishukuru Serikali kwa namna inavyofanya jitihada kuhakikisha wananchi wanaishi katika mazingira salama.

Hivyo, wameahidi kutumia elimu hiyo ya kukabiliana na maafa pindi yanapotokea kuokoa maisha ya watu, mali zao  na kurejesha hali.




*MWISHO*