HABARI

SIASA

ELIMU

Recent Posts

FCC YATOA ELIMU YA ULINZI WA MLAJI KWA WANAFUNZI WA SHULE YA SEKONDARI MNAZI MMOJA

FCC YATOA ELIMU YA ULINZI WA MLAJI KWA WANAFUNZI WA SHULE YA SEKONDARI MNAZI MMOJA

March 26, 2026 Add Comment

Afisa Mlinda Mlaji Mwandamizi kutoka FCC, Magdalena Hall,akitoa elimu kuhusiana madhara ya bidhaa bandia katika Shule ya Sekondari Mnazi Mmoja iliyopo jijini Dar es Salaam ikiwa ni sehemu ya kuelekea Maadhimisho ya Wiki ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani.

....

TUME ya Ushindani (FCC) leo Machi 26, 2026 imetoa elimu kwa wanafunzi wa Shule ya Sekondari Mnazi Mmoja iliyopo jijini Dar es Salaam kuhusu kumlinda mlaji, ikiwemo haki na wajibu wa mlaji pamoja na madhara ya matumizi ya bidhaa bandia katika jamii.

Elimu hiyo imelenga kuwajengea wanafunzi uelewa wa awali kuhusu umuhimu wa kuchagua na kutumia bidhaa zilizo salama, huku ikisisitiza kuwa walaji wana nafasi kubwa katika kulinda afya zao na za wengine.

Akizungumza na wanafunzi hao,Afisa Mlinda Mlaji kutoka FCC Bi.Techla Kitosi,amesisitiza umuhimu wa watumiaji kuwa na uelewa wa haki zao wanaponunua bidhaa au huduma. Ameeleza kuwa mlaji ana haki ya kupata bidhaa bora, salama na zenye ubora unaokubalika.

Aidha ameonya dhidi ya ununuzi wa bidhaa bandia ambazo zinaweza kuhatarisha afya na usalama wa mtumiaji.

“Ni muhimu sana kwa kila mmoja wenu kujifunza kutambua bidhaa halisi na bandia. Msikubali kudanganywa na bei ndogo bila kuangalia ubora wa bidhaa,” amesema Bi.Kitosi

Kwa upande wake, Afisa Mlinda Mlaji Mwandamizi, Magdalena Hall, ameeleza wajibu wa mlaji kuwa ni pamoja na kusoma maelekezo ya matumizi ya bidhaa, kuhifadhi stakabadhi za manunuzi na kutoa taarifa pale wanapokutana na bidhaa zisizo na viwango.

Hata hivyo Bi.Hall ,amewahamasisha wanafunzi kuwa mabalozi wa ulinzi wa mlaji katika jamii zao kwa kutoa elimu kwa familia na marafiki kuhusu madhara ya bidhaa bandia.

Wanafunzi walipata fursa ya kuuliza maswali mbalimbali na kupewa majibu ya kina, jambo lililosaidia kuongeza uelewa wao kuhusu masuala ya ulinzi wa mlaji.

Elimu  hiyo ni sehemu ya jitihada za Tume ya Ushindani kuendelea kutoa elimu kwa umma, hususan vijana, ili kujenga jamii yenye uelewa na uwezo wa kufanya maamuzi sahihi wanaponunua bidhaa na huduma.

Mafunzo hayo ni sehemu ya kuelekea Maadhimisho ya Wiki ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani, tukio linaloadhimishwa kila mwaka kwa lengo la kuongeza uelewa kuhusu haki za walaji duniani kote.

Afisa Mlinda Mlaji kutoka FCC ,Thecla Kitosi,akitoa elimu kuhusiana madhara ya bidhaa bandia katika Shule ya Sekondari Mnazi Mmoja iliyopo jijini Dar es Salaam ikiwa ni sehemu ya kuelekea Maadhimisho ya Wiki ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani.

Afisa Mlinda Mlaji kutoka FCC ,Thecla Kitosi,akitoa elimu kuhusiana madhara ya bidhaa bandia katika Shule ya Sekondari Mnazi Mmoja iliyopo jijini Dar es Salaam ikiwa ni sehemu ya kuelekea Maadhimisho ya Wiki ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani.

Afisa Mlinda Mlaji Mwandamizi kutoka FCC, Magdalena Hall,akitoa elimu kuhusiana madhara ya bidhaa bandia katika Shule ya Sekondari Mnazi Mmoja iliyopo jijini Dar es Salaam ikiwa ni sehemu ya kuelekea Maadhimisho ya Wiki ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani.

Afisa Mlinda Mlaji Mwandamizi kutoka FCC, Magdalena Hall,akitoa elimu kuhusiana madhara ya bidhaa bandia katika Shule ya Sekondari Mnazi Mmoja iliyopo jijini Dar es Salaam ikiwa ni sehemu ya kuelekea Maadhimisho ya Wiki ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani.

Sehemu ya wanafunzi wakisikiliza mada mbalimbali wakati wakipata aelimu kuhusiana madhara ya bidhaa bandia katika Shule ya Sekondari Mnazi Mmoja iliyopo jijini Dar es Salaam iliyotolewa na FCC ikiwa ni sehemu ya kuelekea Maadhimisho ya Wiki ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani.

Sehemu ya wanafunzi wakisikiliza mada mbalimbali wakati wakipata aelimu kuhusiana madhara ya bidhaa bandia katika Shule ya Sekondari Mnazi Mmoja iliyopo jijini Dar es Salaam iliyotolewa na FCC ikiwa ni sehemu ya kuelekea Maadhimisho ya Wiki ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani.

Sehemu ya wanafunzi wakisikiliza mada mbalimbali wakati wakipata aelimu kuhusiana madhara ya bidhaa bandia katika Shule ya Sekondari Mnazi Mmoja iliyopo jijini Dar es Salaam iliyotolewa na FCC ikiwa ni sehemu ya kuelekea Maadhimisho ya Wiki ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani.

Wanafunzi Shule ya Sekondari Mnazi Mmoja wakiuliza maswali mbalimbali kuhusu namna ya kutofautisha bidhaa halisi na bandia mara baada ya kupatiwa elimu na FCC  ikiwa ni sehemu ya kuelekea Maadhimisho ya Wiki ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani.

KAMATI YA BUNGE YAPITISHA RANDAMA YA MADINI MWAKA 2026/2027

March 26, 2026 Add Comment



✅️ Madini Yachangia Asilimia 57 ya Mauzo Yote ya Bidhaa Zisizo za Asili Nje ya Nchi


✅️ Makusanyo mpaka Februari 2026 Yafikia Shilingi Bilioni 880


✅️ GST Yakidhi Vigezo Kuendelea Kuwa na Ithibati Mpaka 2029


✅️ Waziri Mavunde Asisitiza Ununuzi wa Helikopta ya Utafiti, Mipango Iko Pale Pale


📍 Dodoma


Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini leo Machi 26, 2026 imepitisha Randama ya Wizara ya Madini kuhusu makadirio ya mapato na matumizi ya kawaida na maendeleo kwa mwaka wa fedha 2026/27 katika kikao kilichofanyika jijini Dodoma, ambacho pia kimepokea taarifa ya utekelezaji wa Wizara kwa kipindi cha Julai 2025 hadi Februari 2026 kwa mwaka 2025/26.


Akizungumza katika kikao hicho, Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Mhe. Subira Mgalu, ameipongeza Wizara kwa namna inavyosimamia utekelezaji wa majukumu yake yaliyopelekea kuongeza mchango wa sekta ya madini kwenye Pato la Taifa kufikia asilimia 12.7 katika robo ya tatu ya Julai hadi Septemba 2025, ikiwemo kuibua miradi mipya na shughuli za utafiti, na kueleza kwamba matokeo ya mchango wa Sekta ya Madini kwenye maendeleo na uchumi wa nchi yanaonekana dhahiri.


Pia ameipongeza Wizara kwa namna inavyodhibiti utoroshaji wa madini na biashara haramu ya madini nchini, hatua ambayo imepelekea kukamatwa kwa madini ya aina mbalimbali yenye thamani ya shilingi trilioni 2.190 katika matukio 41 kwenye mikoa ya kimadini ya Arusha, Chunya, Geita, Dar es Salaam, Mwanza, Iringa, Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere, Kahama, Mahenge, Mbeya, Mbogwe, Mirerani na Songwe.


Awali, akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa bajeti ya Wizara ya Madini kwa mwaka 2025/26, Mkurugenzi wa Sera na Mipango, Wizara ya Madini, Augustino Olal, ameieleza kamati kuwa thamani ya mauzo ya madini na bidhaa za madini nje ya nchi mwaka 2024 ilikuwa dola za Marekani milioni 4,119.9 ikilinganishwa na dola za Marekani milioni 3,551.4 mwaka 2023, sawa na ongezeko la asilimia 16.0, na kueleza kuwa “mauzo hayo yamechangia asilimia 57.0 ya mauzo yote ya bidhaa zisizo za asili nje ya nchi.”

Pia ameieleza kamati hiyo kuwa makusanyo ya maduhuli yaliyokusanywa na kuwasilishwa Hazina kwa kipindi cha Julai 2025 hadi Februari 2026 yameongezeka hadi kufikia shilingi 880,711,819,180.04 ikilinganishwa na shilingi 690,757,642,936.80 katika kipindi kama hicho mwaka 2024/25, sawa na ongezeko la asilimia 27.50. Mwaka 2025/26 Wizara imepangiwa kukusanya shilingi trilioni 1.2.

Akizungumzia mafanikio yaliyopatikana kwa Shirika la Madini la Taifa (STAMICO), amesema limesaini mkataba wa kuendeleza leseni za madini ya dhahabu zilizopo eneo la Kigosi, wilayani Bukombe mkoani Geita, na Kampuni ya Plantcor Mining and Plant Hire (PTY) Ltd ya nchini Afrika Kusini. Ameongeza kuwa STAMICO imepata mikataba ya uchorongaji katika Kampuni ya GFX yenye thamani ya shilingi bilioni 3.8 na Shanta Buhemba yenye thamani ya shilingi bilioni 1.4.

“Mhe. Mwenyekiti, katika kipindi husika jumla ya leseni 9,802 zilitolewa, ikiwa ni zaidi ya lengo la leseni 6,687 zilizopangwa kutolewa, sawa na asilimia 146.58,” amesema Olal.

Akizungumzia mafanikio ya Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini Tanzania (GST), ameyataja baadhi, ikiwemo maabara ya taasisi hiyo kukidhi vigezo vya kuendelea kuwa na ithibati (maintained accreditation status) kwa kipindi kingine cha miaka mitano (5) mpaka Oktoba 2029, baada ya ukaguzi wa nje kupitia Shirika linalodhibiti ubora wa huduma za maabara katika nchi zilizopo Kusini mwa Bara la Afrika (SADCAS) uliofanyika Februari 24, 2026.

Kwa upande wake, Waziri wa Madini, Mhe. Anthony Mavunde, akitoa ufafanuzi wa masuala mbalimbali katika kikao hicho, ameihakikishia kamati kuhusu kutekelezwa kwa mipango yote iliyopangwa na Wizara, ikiwemo ununuzi wa helikopta kwa ajili ya shughuli za utafiti, na kuishukuru kwa namna inavyoisimamia Wizara, akieleza kuwa mafanikio hayo yametokana na maelekezo na usimamizi mzuri wa kamati hiyo. 




*Vision2030:*

#MadiniNiMaisha

#MadiniNiUtajiri

DKT. MWIGULU: TUENDELEE KUMUOMBEA MHE. LUKUVI

DKT. MWIGULU: TUENDELEE KUMUOMBEA MHE. LUKUVI

March 26, 2026 Add Comment

Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba akimfariji, Germina Lukuvi, mjane wa aliyekuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu, William Lukuvi alipokwenda nyumbani kwa marehemu Area D jijini Dodoma kuhani, Machi 26, 2026. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba akimfariji, Germina Lukuvi (wa tatu kushoto), mjane wa aliyekuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu, William Lukuvi alipokwenda nyumbani kwa marehemu Area D jijini Dodoma kuhani, Machi 26, 2026. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba akizungumza wakati alipokwenda nyumbani kwa aliyekuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu, marehemu William Lukuvi, Area D jijini Dodoma, Machi 26, 2026. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba akitia saini kitabu cha maombolezo ya kifo cha aliyekuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu, William Lukuvi, nyumbani kwa marehemu Area D jijini Dodoma, Machi 26, 2026. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)


Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba akiwafariji watoto wa aliyekua Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge na Uratibu, na Wenye Ulemavu, William Lukuvi, Mossy Lukuvi (wa pili kulia na Brown Lukuvi (kulia) nyumbani kwa marehemu Area D jijini Dodoma alipokwenda kuhani, Machi 26, 2026. Kulia ni Katibu Tawala wa Mkoa wa Arusha, Dkt. Toba Nguvila. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)


Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba akizungumza na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Ridhiwani Kikwete, Naibu Spika Daniel Sillo (kulia) na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule, wakati alikokwenda kuhani msiba nyumbani kwa aliyekuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu, marehemu William Lukuvi, Area D jijini Dodoma, Machi 26, 2026. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)


WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba amewaomba Watanzania waendelee kumuombea kwa Mwenyezi Mungu aliyekuwa Waziri Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu, marehemu William Lukuvi aliyefariki jana Machi 25, 2026 katika Hospitali ya Benjamin Mkapa, jijini Dodoma.


Akiongea kwa niaba ya Serikali nyumbani kwa marehemu Area D, jijini Dodoma leo, Alhamisi, Machi 26, 2026, Waziri Mkuu amesema: “Kwa niaba ya Serikali natoa pole kwa familia, ndugu, jamaa. Jambo hili zito, gumu kulielewa, gumu kulipokea.”


…Lakini ndio limeshatufika na sote hatukutarajia maana Mheshimiwa Waziri alikuwa kazini. Tuendelee kumuombea kwa Mwenyezi Mungu na kuifariji familia. Mwenyezi Mungu awaimarishe kwa sababu yeyé ndio mfariji mkuu,” amesisitiza.


Vilevile, Mheshimiwa Dkt. Mwigulu ametumia fursa hiyo kuihakikishia familia kwamba Serikali itaendelea kuwa pamoja nayo katika kipindi hiki chote cha majonzi.


Viongozi wengine waliokuwepo msibani hapo ni pamoja na Naibu Spika, Daniel Siro, Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais, (Muungano na Mazingira), Mhandisi Hamad Masauni, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Menejimenti ya Utumisi wa Umma na Utawala Bora), Ridhiwani Kikwete, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule na Katibu Tawala wa Mkoa wa Arusha, Dkt. Toba Nguvila.

TRANSFORMA MPYA MAHUMBIKA YAIMARISHA UPATIKANAJI UMEME MIKOA YA LINDI NA MTWARA

March 26, 2026 Add Comment




Serikali kupitia Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) imekamilisha kwa asilimia 99 mradi wa kufunga transfoma ya ziada ya MVA 15 katika kituo cha kupokea na kupoza umeme cha Mahumbika, mkoani Lindi, uliogharimu shilingi milioni 702.


Mradi huu umeimarisha kwa kiasi kikubwa upatikanaji wa umeme katika Mkoa wa Lindi na wilaya za Masasi, Newala na Nanyumbu mkoani Mtwara.



Akiwa katika ziara ya kukagua utekelezaji wa mradi wa ufungaji transfoma hiyo, Mkuu wa Wilaya ya Lindi, Mhe. Victoria Mwanziva, ameipongeza  Serikali 

kwa uwekezaji mkubwa katika sekta ya nishati unaoendelea kuimarisha upatikanaji wa umeme mkoani Lindi na maeneo jirani.



"Ufungwaji wa transfoma hii umeboresha upatikanaji wa umeme na kuchochea maendeleo ya wananchi na Taifa kwa ujumla". Amesema Mhe. Victoria. 



Aidha, viongozi wa Serikali  wameahidi kuendelea kushirikiana na TANESCO katika kuhakikisha huduma bora zaidi ya

 umeme inapatikana kwa wananchi.



WANAFUNZI 32 KUSOMA IRELAND KUPITIA UFADHILI WA SAMIA SCHOLARSHIP

March 26, 2026 Add Comment
NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

Serikali ya Tanzania kwa kushirikiana na Chuo Kikuu cha Limerick cha nchini Ireland wamesaini hati ya makubaliano ya utekelezaji wa ufadhili wa Samia Scholarship Extended, utakaowawezesha wanafunzi 32 kusoma katika chuo hicho.

WATENGENEZAJI MAUDHUI WAHAMASHWA KUTUMIA FURA ZA NISHATI SAFI YA KUPIKIA KUELIMISHA JAMII NA KUJIPATIA KIPATO

March 26, 2026 Add Comment


Mkurugenzi wa Nishati Safi ya Kupikia, Nolasco Mlay, amewahimiza watengeneza maudhui nchini kutumia ubunifu wao kuelimisha jamii kuhusu matumizi ya nishati safi ya kupikia, huku wakitumia fursa hiyo kujiongezea kipato. 

Ameyabainisha  hayo leo Machi 25, 2026, jijini Dar es Salaam wakati akizungumza kwenye mafunzo kwa watengeneza maudhui (content creators), yaliyoandaliwa na Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa kushirikiana na Mfuko wa Utamaduni na Sanaa Tanzania, huku Wizara ya Nishati ikiwa miongoni mwa wawezeshaji wakuu.

Akizungumza katika mafunzo hayo  ameeleza kuwa Serikali imeweka mkakati wa kuhakikisha ifikapo mwaka 2034, angalau asilimia 80 ya Watanzania wawe wanatumia nishati safi ya kupikia ambapo amebainisha kuwa suluhisho za nishati safi ya kupikia  zipo na zinaendelea kuwafikia wananchi, kilichobaki ni kuhakikisha taarifa sahihi zinawafikia watu wengi zaidi ili kuchochea mabadiliko ya matumizi.

Amesema licha ya hatua iliyofikiwa, bado kuna changamoto ya uelewa mdogo kwa wananchi kuhusu nishati safi ya kupikia, ambapo wengi hudhani kuwa ni matumizi ya gesi pekee. hivyo amefafanua kuwa nishati safi ya kupikia inajumuisha pia matumizi ya umeme, gesi asilia, biyogasi, mkaa mbadala na teknolojia nyingine mbadala ambazo husaidia kupunguza athari za kiafya na kimazingira.

Bw. Mlay amesisitiza kuwa watengeneza maudhui wana nafasi kubwa ya kubadilisha mtazamo wa jamii kwa kutengeneza video za elimu, vichekesho, hadithi na kampeni mbalimbali zitakazowafikia wananchi kwa urahisi ambapo amesisitiza kuwa maudhui hayo yakifanyika kwa ubunifu na ubora, yanaweza kununuliwa na kuwapatia kipato watayarishaji wake huku yakisaidia kusambaza ujumbe muhimu kwa jamii.

Ametoa wito kwa watengeneza maudhui hao  kuchangamkia fursa hiyo kwa kuandaa kazi zenye kuelimisha kuhusu faida za nishati safi ya kupikia pamoja na madhara ya kutumia nishati zisizo safi, akisisitiza kuwa jamii ikipata taarifa sahihi, itafanya mabadiliko chanya yatakayoboreshwa maisha na kulinda afya za Watanzania.



CHIEF WA KIBONDO MWANAMVUA RAJAB RUHAGA NYAMALIZA AFARIKI DUNIA GHALFA AKIWA MSIBANI MALINYI ,MOROGORO

March 25, 2026 Add Comment




Chief wa Kibondo mkoani Kigoma  Mama Mwamvua Rajab Ruhaga Nyamaliza amefariki dunia ghafla asubuhi ya tarehe 24 Machi 2026 akiwa msibani Malinyi, mkoani Morogoro.


Taarifa za kifamilia zinaeleza kuwa marehemu alikuwa amesafiri kwenda Malinyi kuhudhuria mazishi ya binti yake, Zubeda Juma Ruhaga, kabla ya kifo chake hicho cha kushtukiza kutokea.


Kifo hicho kimeacha simanzi kubwa kwa familia, ndugu, jamaa na wakazi wa Kibondo, ambako marehemu alikuwa akihudumu kama kiongozi wa kimila na mshauri muhimu wa jamii.


Kwa sasa, familia ipo katika maandalizi ya kusafirisha mwili wa marehemu kutoka Morogoro kuelekea Kibondo, Kigoma, kwa ajili ya mazishi yatakayofanyika nyumbani kwake.


Taarifa zaidi kuhusu taratibu za mazishi zinatarajiwa kutolewa na familia kadri mipango inavyoendelea.

TUME YA UMOJA WA AFRIKA YAMTEUA RAIS MSTAAFU DKT JAKAYA MRISHO KIKWETE KUWA MWAKILISHI WAKE MAALUM KWA UKANDA WA PEMBE YA AFRIKA NÀ BAHARI NYEKUNDU

March 25, 2026 Add Comment





Na Mwandishi Maalum




Rais Mstaafu Dkt, Jakaya Mrisho Kikwete ameteuliwa kuwa Mwakilishi Maalum wa Umoja wa Afrika kwa Ukanda wa Pembe ya Afrika na Bahari Nyekundu, jukumu linalomrejesha katika mstari wa mbele wa diplomasia ya bara Afrika.



Uteuzi huo ulitangazwa leo mjini Addis Ababa Ethiopia na Mahmoud Ali Youssouf, Mwenyekiti wa Tume ya Umoja wa Afrika, ambaye alionesha imani kubwa katika uzoefu na uongozi wa Kikwete kushughulikia changamoto tata za kisiasa, amani na usalama katika ukanda huo.



Ukanda huo unaendelea kuwa na changamoto nyingi, kuanzia migogoro ya kisiasa hadi maslahi ya kimkakati ya kimataifa, hasa kutokana na umuhimu wa Bahari Nyekundu katika biashara ya dunia.



Ni eneo ambalo si tu linahusu nchi za Afrika, bali pia lina mvuto wa nguvu za kimataifa.



Katika nafasi hiyo mpya, Kikwete anatarajiwa kusaidia Tume hiyo kuimarisha juhudi za kuleta amani kupitia diplomasia ya kuzuia migogoro, kukuza mazungumzo jumuishi, na kujenga uaminifu miongoni mwa wadau mbalimbali.



Aidha, alikabidhiwa jukumu la kuratibu juhudi za taasisi mbalimbali, ikiwa ni pamoja na Intergovernmental Authority on Development, East African Community, League of Arab States pamoja na United Nations, ili kuhakikisha juhudi za kuleta amani zinakuwa na mshikamano na ufanisi.



Hili linaonekana kuwa jukumu nyeti zaidi, kwani ukanda huo kwa muda mrefu umekuwa ukivutia maslahi yanayokinzana kutoka kwa mataifa na taasisi mbalimbali. Kuleta mwelekeo mmoja kunahitaji busara, uvumilivu na ustadi wa hali ya juu wa kidiplomasia.



Na wengi wanaamini kwamba hapo ndipo nguvu ya Dkt. Kikwete ilipo.



Siku zote amejulikana kwa mtindo wa uongozi wa mazungumzo badala ya mabavu, ushawishi badala ya shinikizo. Katika ukanda ambao mara nyingi nguvu za kijeshi hazijaleta suluhu ya kudumu, mtazamo huu unaweza kuwa wa faida kubwa.



Kwa Tanzania, uteuzi huu uliibua hisia za fahari ya kimya. Kwa miaka mingi, nchi imejijengea sifa ya kuwa na mchango mkubwa katika diplomasia ya bara—kuanzia enzi za Mwalimu Nyerere hadi viongozi waliomfuata



Uteuzi wa Dkt Kikwete umetajwa kuwa ni ukumbusho kwamba uongozi hauishii madarakani. Mara nyingi, viongozi wastaafu hupata nafasi ya kutumia uzoefu wao kwa uhuru zaidi katika jukwaa la kimataifa, na wakati mwingine kwa mafanikio makubwa zaidi.



Mwenyekiti wa Tume ya Umoja wa Afrika alieleza imani yake kwamba hekima na uzoefu wa Kikwete vitachangia kwa kiasi kikubwa katika kutafuta suluhu za kudumu za amani na ustawi katika ukanda huo.



Kwa Pembe ya Afrika, safari bado ni ndefu na yenye changamoto. Lakini diplomasia ni mchakato wa hatua kwa hatua, na si wa matokeo ya haraka. Na kwa kumteua Jakaya Kikwete, Umoja wa Afrika unaonekana kuchagua si tu kiongozi mwenye uzoefu, bali pia mtazamo wa subira, mazungumzo na matumaini ya suluhu ya kudumu.


Rais Mstaafu Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akipeana mkono na Mwenyekiti wa tume ya Umoja wa Afrika Bw. Mahamoud Ali Youssouf baada ya kuteuliwa kuwa Mwakilishi Maalumu wa Umoja wa Afrika kwa Ukanda wa Pembe ya Afrika na Bahari Nyekundu leo Mjini Addis Ababa,Ethiopia




UONGOZI ADEM WAHIMIZA USHIRIKIANO KAZINI

March 25, 2026 Add Comment
Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Maendeleo ya Uongozi wa Elimu (ADEM), Dkt. Maulid J. Maulid, amefanya kikao kazi na watumishi wa taasisi hiyo kutoka kampasi zote, akisisitiza umuhimu wa uwajibikaji, umoja na mshikamano katika kufanikisha malengo ya taasisi.
MKUU WA KANDA YA ZIWA FCC ASISITIZA ULINZI WA HAKI ZA WALAJI MARA

MKUU WA KANDA YA ZIWA FCC ASISITIZA ULINZI WA HAKI ZA WALAJI MARA

March 25, 2026 Add Comment

WATUMISHI  wa Tume ya Ushindani Ofisi ya Kanda ya Ziwa wametoa elimu kwa wadau mbalimbali, wakiwemo wanafunzi, waandishi wa habari na wafanyabiashara, walipotembelea Banda la Kliniki ya Walaji katika Manispaa ya Musoma Mkoani Mara.

Banda hilo limegeuka kuwa kitovu cha maarifa, likiwavutia wengi waliotaka kuelewa kwa undani haki zao kama walaji pamoja na namna bora ya kushiriki katika soko kwa uadilifu na uelewa mpana.

Akitoa elimu hiyo, Mkuu wa Kanda ya Ziwa FCC, Bw. Mdimi, amesisitiza umuhimu wa walaji kuwa na uelewa wa haki zao ili kujilinda dhidi ya bidhaa duni, huduma zisizo na viwango na vitendo vya udanganyifu vinavyoweza kujitokeza sokoni.

"Amebainisha kuwa elimu kwa walaji ni silaha muhimu katika kujenga uchumi imara unaozingatia haki na usawa kwa wote."amesema Bw.Mdimi

Kwa upande wa wafanyabiashara, wamekumbushwa umuhimu wa kuendesha shughuli zao kwa kuzingatia sheria za ushindani wa haki, wakielezwa kuwa uaminifu kwa wateja ni msingi wa mafanikio ya biashara yoyote endelevu.

Elimu hiyo imewajengea uelewa mpya kuhusu wajibu wao katika kulinda maslahi ya walaji.

Wanafunzi  wameahidi kuwa mabalozi wa elimu hiyo katika jamii zao, huku waandishi wa habari wakiahidi kueneza ujumbe huo kwa umma kupitia vyombo vyao.

Elimu hiyo  ni sehemu ya maandalizi kuelekea Maadhimisho ya Wiki ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani 2026, yakilenga kuendelea kuhamasisha jamii kuhusu umuhimu wa kulinda haki za walaji na kuimarisha ushindani wa haki sokoni.

Kwa ujumla, juhudi hizi zinaakisi dhamira ya Tume ya Ushindani kuhakikisha kuwa kila mlaji anakuwa na sauti, analindwa na anapata huduma bora, huku biashara zikikua katika mazingira ya haki na uwazi.