Na: OWM (KAM) - Mwanza
HABARI MPYA
HABARI
SIASA
ELIMU
Recent Posts
VIWANDA MKOANI PWANI VYATAKIWA KUBORESHA MAZINGIRA YA KAZI
habari

MASAUNI AITAKA BODI NCMC KUIMARISHA MIFUMO YA UPIMAJI, UTOAJI TAARIFA NA UHAKIKI WA GESIJOTO
habari
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Mhe. Mhandisi Hamad Yussuf Masauni akizungumza wakati akizindua Bodi ya Kituo Taifa cha Kuratibu Kaboni (NCMC), Machi 6, 2026 jijini Dar es Salaam.
Na; Mwandishi Wetu,Dar es Salaam.
Waziri wa nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. Mhandisi Hamad Yussuf Masauni ametoa maagizo matano kwa Bodi ya Kituo Taifa cha Kuratibu Kaboni (NCMC) kilichopo Morogoro mara baada ya kuizindua bodi hiyo.
Waziri Masauni ametoa maagizo hayo Machi 6, 2026 wakati wa uzinduzi wa Bodi hiyo jijini Dar es Salaam akieleza imepaswa kuimarisha mifumo ya kitaifa ya Upimaji, Utoaji Taarifa na Uhakiki wa gesijoto (MRV) ili kuhakikisha kuwa taarifa za kaboni nchini zinakuwa sahihi, za kuaminika na zinazokubalika kimataifa.
Pia ameielekeza Bodi hiyo kuhakikisha Miradi yote ya kaboni inayotekelezwa nchini inasimamiwa kwa ufanisi, uwazi na kwa kuzingatia viwango vya kitaifa na kimataifa pamoja na maslahi mapana ya Taifa.
Mhe. Masauni ameongeza kuwa bodi inapaswa kuweka Mazingira wezeshi yatakayovutia uwekezaji wa ndani wa kimataifa katika Sekta ya Kaboni huku ikihakikisha kuwa uwekezaji huo unalinda rasilimali za Taifa na kuleta manufaa ya kweli kwa wananchi, kuhakikisha kunakuwepo mfumo wa haki na uwazi wa mgawanyiko wa manufaa ili jamii zinazohifadhi rasilimali za asili zinufaike moja kwa moja na Miradi ya Kaboni inayotekelezwa katika maeneo yao.
“Kuimarisha ushiriki wa Tanzania katika mifumo ya kimataifa ya biashara ya Kaboni hususan chini ya Ibara ya 6 ya Mkataba wa Paris, ikiwemo mifumo ya soko la Kaboni ili kuongeza fursa za kiuchumi kwa Taifa letu.
Aidha, ameisisitiza Bodi hiyo kufanya kazi kwa bidii na kuhakikisha Kituo hicho kinaendeshwa kwa uwajibikaji, uadilifu na weledi wa hali ya juu ili kuhakikisha mifumo ya Usimamizi wa Sekta ya Kaboni inalinda kikamilifu maslahi ya Taifa.
"Ni matarajio ya Serikali kuona kituo hiki kinakuwa kitovu cha ubora katika maswala ya ufuatiliaji wa Kaboni, biadhara ya Kaboni na Tafiti za mabadiliko ya tabianchi katika ukanda wa Afrika. Haya ni matarajio makubwa kwa taifa letu na yanahitaji Usimamizi madhubuti wa taasisi, mifumo imara ya ufuatiliaji pamoja na ushirikiano wa wadau wote.” Amesema Mhe. Masauni.
Ameongeza kuwa matarajio ya Serikali yaliyoainishwa katika Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, na Mpango wa muda mrefu wa Utekelezaji wake, sekta ya Kaboni inauwezo wa kuchangia takribani Dola za kimarekani bilioni mbili kwa Mwaka katika uchumi wa Taifa.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Bodi, Dkt. Albina Chuwa amesema ushirikiano ndio jambo la msingi katika kufikisha lengo na ndoto za watanzania, hivyo watajitahidi kutafuta fursa ili kupata matokeo mazuri.
“Ushirikiano wa kutosha ndio naomba kutoka kwa kila mmoja wetu kwani haya yote tunayoyazungumza tutakuwa tunafanya kazi nyepesi katika kuhakikisha kituo chetu cha Kaboni kinafanya vizuri,” amesema Dkt. Albina.
Amesema Uzinduzi wa Bodi unakuja katika kipindi muhimu ambacho sekta ya biashara ya kaboni inaendelea kukua kwa kasi duniani na hapa nchini, NCMC ina jukumu muhimu la kuhakikisha kuwa rasilimali za kaboni za nchi yetu zinasimamiwa kwa uwazi, weledi na kwa kuzingatia mifumo na viwango vinavyokubalika kimataifa.
Wajumbe wanaounda Bodi hiyo ni Bw. Khamis Hamza Khamis, Bi. Amne Sued Kagasheki, Bi. Farhat Mabrouk, Dkt. Ladislaus Kyaruzi, Bw. Rishad Bade pamoja na Dkt.Philipina Fenest Shayo.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Mhe. Mhandisi Hamad Yussuf Masauni akizungumza wakati akizindua Bodi ya Kituo Taifa cha Kuratibu Kaboni (NCMC), Machi 6, 2026 jijini Dar es Salaam.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Mhe. Mhandisi Hamad Yussuf Masauni (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Mwenyekiti wa Bodi ya NCMC, Dkt. Albina Chuwa (kushoto kwake), Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais, Dkt, Festo Dugange, Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Dkt. Richard Muyungi (kulia kwake) na Naibu Katibu Mkuu (Mazingira) Ofisi ya Makamu wa Rais, Balozi Baraka Luvanda, mara baada ya uzinduzi wa Bodi ya Kituo Taifa cha Kuratibu Kaboni (NCMC), Machi 6, 2026 jijini Dar es Salaam.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Mhe. Mhandisi Hamad Yussuf Masauni akimpongeza Mwenyekiti wa Bodi ya Kituo Taifa cha Kuratibu Kaboni (NCMC, Dkt. Albina Chuwa mara baada ya uzinduzi wa Bodi hiyo, Machi 6, 2026 jijini Dar es Salaam

Naibu Waziri, Ofisi ya Makamu wa Rais, Dkt. Festo Dugange akizungumza wakati wa uzinduzi wa Bodi ya Kituo Taifa cha Kuratibu Kaboni (NCMC), Machi 6, 2026 jijini Dar es Salaam.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Mhe. Mhandisi Hamad Yussuf Masauni (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Wajumbe wa Bodi ya Kituo Taifa cha Kuratibu Kaboni (NCMC), mara baada ya uzinduzi wa Bodi hiyo, Machi 6, 2026 jijini Dar es Salaam.
PICHA NA OFISI YA MAKAMU WA RAIS
MAGARI YA UMEME NAFUU KWA ASILIMIA 85 UKILINGANISHWA NA MAFUTA
NishatiNa Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati, Mhandisi Felchesmi Mramba amesema utafiti unaonesha kuwa kuendesha gari la umeme nchini ni nafuu kwa takribani asilimia 85 kwa kila kilomita ikilinganishwa na gari linalotumia petroli au dizeli.
Mramba ameyasema hayo Machi 6, 2026 jijini Dar es Salaam wakati wa uzinduzi rasmi wa matumizi ya magari ya umeme nchini kupitia kampuni ya DOW ELEF AUTO EV (ZERA) Limited.
Amesema kwa wastani gari linalotumia mafuta linaweza kugharimu takribani Sh.200 kwa kilomita moja, wakati gari la umeme linatumia karibu Sh.25 pekee kwa kilomita.
“Gharama hii inaonesha wazi kuwa teknolojia ya magari ya umeme ni nafuu zaidi na inaweza kusaidia wananchi kupunguza matumizi katika sekta ya usafiri,” amesema Mramba.
Ameeleza kuwa uzinduzi huo ni hatua muhimu katika mageuzi ya sekta ya usafiri nchini na unaendana na juhudi za Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Dk. Samia Suluhu Hassan za kukuza uwekezaji na kuhamasisha matumizi ya teknolojia safi ya nishati.
Mramba amesema Serikali tayari imeweka mazingira wezeshi kwa maendeleo ya teknolojia hiyo kwa kupitisha Mfumo wa Kitaifa wa Sera ya Magari ya Umeme (National Electric Vehicles Policy Framework) Desemba 2024.
Amesema sera hiyo inalenga kuhamasisha uzalishaji wa magari ya umeme nchini, kuongeza matumizi yake, kuunganisha sekta hiyo na nishati jadidifu pamoja na kujenga miundombinu ya vituo vya kuchaji magari hayo.
Aidha, amesema Tanzania imeendelea kupiga hatua katika uzalishaji wa umeme ambapo uwezo umeongezeka hadi zaidi ya megawati 4,500, huku upatikanaji wa umeme ukifikia asilimia 85.5 mwaka 2025.
Kwa mujibu wa Mramba, hatua hiyo inalenga kuimarisha sekta mbalimbali za kiuchumi ikiwamo usafiri wa kisasa wenye gharama nafuu na rafiki kwa mazingira.
Kwa sasa Afrika ina zaidi ya magari ya umeme 30,000, huku Afrika Mashariki ikijitokeza kuwa kitovu cha ubunifu katika sekta hiyo.
Nchini Tanzania, inakadiriwa kuwa tayari kuna zaidi ya magari ya umeme 10,000 yakiwemo pikipiki pamoja na vyombo vingine vya usafiri vya magurudumu mawili na matatu.
Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Kampuni ya DOW ELEF AUTO EV (ZERA) Limited, Emmanuel Kazimoto, amesema kampuni hiyo imeanza na mpango wa kuagiza magari kamili ya umeme, kabla ya kuanza kuleta magari ya kuunganishwa hapa nchini.
Ameongeza kuwa lengo la baadaye ni kuanzisha kiwanda cha kuunganisha magari ya umeme nchini, hatua itakayochochea ajira na kuwajengea vijana wa Kitanzania ujuzi katika teknolojia ya kisasa.
NINA IMANI KUBWA NA UTENDAJI KAZI WA OFISI YA MWANDISHI MKUU WA SHERIA -MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI
Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Mhe. Hamza S. Johari amewataka Watumishi wa Ofisi ya Mwandishi Mkuu wa Sheria kufanya kazi kwa Weledi na Ufanisi ili kufikia malengo ya Ofisi kwani ana Imani kubwa na utendaji kazi wa OFISI ya Mwandishi Mkuu wa Sheria.
Mhe. Johari amesema hayo alipofungua kikao cha kwanza cha Baraza la Wafanyakazi la Ofisi ya Mwandishi Mkuu wa Sheria tarehe 6 Machi, 2026 jijini Dar es Salaam.
*"Niwaombe muendelee kutekeleza majukumu ya Ofisi hii kwa Weledi na Ufanisi ili kufikia malengo ya Ofisi na nina imani kubwa na utendaji kazi wa Ofisi ya Mwandishi Mkuu wa Sheria”* amesema Mhe. Johari
Aidha Mhe. Johari ameendelea kwa kuwataka watumishi wa Ofisi ya Mwandishi Mkuu wa Sheria kuzingatia kanuni na Sheria za Utumishi wa Umma ili kutoathiri utendaji kazi wa Serikali.
*"Utumishi wa Umma unaongozwa na Sheria pamoja na Kanuni, hivyo natoa rai kwa watumishi wote tuzingatie Miongozo ya Utumishi wa Umma ili tusiathiri utendaji kazi wa Serikali,"* ameongeza Mhe. Mwanasheria Mkuu wa Serikali.
Vilevile Mhe. Johari ameitaka Ofisi ya Mwandishi Mkuu wa Sheria kuboresha matumizi ya mifumo ya TEHAMA ili kufanya kazi kwa ufanisi zaidi.
*"Naomba nisisitize matumizi ya mifumo ya TEHAMA ili kurahisisha utendaji kazi na kutoa kazi zenye ufanisi kwa matumizi ya Serikali na jamii kwa ujumla,"* ameeleza Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mhe. Hamza Johari.
Awali, akimkaribisha Mgeni Rasmi, Mwandishi Mkuu wa Sheria, Bw. Onorius Njole, amesema Ofisi ya Mwandishi Mkuu wa Sheria imewekeza nguvu kubwa kwenye mifumo ya TEHAMA ili kuendelea kuimarisha utendaji kazi.
*"Katika kuendelea kuimarisha utekelezaji wa Uandishi wa Sheria tumeamua kuweka nguvu kubwa kwenye mifumo ya Tehama kwa kuanzisha e-drafting, e-translation na e-revision na kwa usaidizi wako Mwanasheria Mkuu wa Serikali tutaweza kufanikisha hili.* amesema.
Pia, Mwandishi Mkuu wa Sheria Bw. Njole amemshukuru Mwanasheria Mkuu wa Serikali kwa kuendelea kuwa kiongozi bora na mwenye msaada mkubwa kwa Ofisi ya Mwandishi Mkuu wa Sheria.
*"Kwa niaba ya menejimenti ya Ofisi ya Mwandishi Mkuu wa Sheria na Wafanyakazi wote, tunamshukuru Sana Mhe. Johari kwa kuwa kiongozi bora kwa Ofisi yetu, na kutupa ushirikiano kila tunapohitaji”* Amesema.
Miongoni mwa Wageni waalikwa katika Baraza la Wafanyakazi wa Ofisi ya Mwandishi Mkuu wa Sheria ni Mkurugenzi wa Mashtaka, Bw. Sylvester Mwakitalu.
Baraza la kwanza la Wafanyakazi wa Ofisi ya Mwandishi Mkuu wa Sheria, limefanyika tarehe 6 Machi, 2026 katika ukumbi wa Mikutano wa Julius Nyerere (JNICC) jijini, Dar es salaam.
UMEME WA GRIDI YA KIGOMA UMEOKOA BILIONI 58 ZA MAFUTA NA MATENGENEZO -NAIBU WAZIRI MHE. SALOME
Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba amelipongeza Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) kwa kusimamia na kukamilisha mradi wa kupeleka umeme wa gridi mkoani Kigoma na hivyo kuokoa takribani shilingi bilioni 58 zilizokuwa zikitumika kila mwaka kwa ajili ya ununuzi wa mafuta na matengenezo ya vipuri vya majenereta ya kuzalisha umeme.
Mhe. Salome ametoa pongezi hizo tarehe 6 Machi 2026 mara baada ya kutembelea mradi wa ujenzi wa kituo kikubwa cha Kupoza umeme cha Kidahwe kilichopo mkoani Kigoma pamoja na kituo cha kupoza umeme cha kigoma mjini na kituo cha muda cha Kidahwe.
“Niwapongeze TANESCO kwa kufikisha umeme wa gridi Kigoma hasa baada ya kukamilisha mradi kutoka Nyakanazi hadi Kigoma na kwa kuamua kutumia fedha zenu za ndani shilingi bilioni tano kukamilisha kituo cha muda cha Kidahwe ambacho kwa sasa kinapeleka umeme Kigoma wakati ujenzi wa kituo kikubwa cha umeme Kidahwe ukiendelea,” amesema Mhe. Salome
Amesema kituo kipya cha umeme cha Kidahwe kitakuwa na uwezo wa megawati 192 na hivyo kitaimarisha zaidi hali ya upatikanaji wa umeme katika Mkoa wa Kigoma ambao kwa sasa unapata takribani megawati 30.
Ameongeza kuwa kituo hicho kinatarajiwa kukamilika mwezi Novemba mwaka huu na kitasaidia pia kuimarisha hali ya umeme katika mikoa ya Magharibi, kuendesha Treni ya Mwendo Kasi (SGR) pamoja na kuchochea biashara ya umeme na nchi jirani za Magharibi mwa Tanzania.
Kutokana na uwepo wa umeme wa kutosha mkoani Kigoma, Mhe. Salome amewakaribisha wawekezaji wa ndani na nje ya nchi kuwekeza katika mkoa huo.
Aidha, amewaasa wananchi kulinda miundombinu ya umeme akieleza kuwa Rais, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan anaendelea kutoa fedha nyingi kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya nishati nchini hivyo wananchi wanao wajibu wa kuilinda na kuithamini.
Awali, Mratibu wa Mradi wa Kusafirisha umeme wa msongo wa kilovolti 400 kutoka Nyakanazi hadi Kigoma, Mhandisi Ramadhan Uwessu, alisema kuwa ujenzi wa kituo kipya cha Kidahwe unaenda sambamba na upanuzi wa kituo cha Nyakanazi ili kukiwezesha kusafirisha umeme wa msongo wa kV 400 kutoka Nyakanazi hadi Kidahwe.
Ameongeza kuwa kituo hicho pia kitapokea umeme kutoka njia ya Tabora kwa msongo wa kV 132, kutoka Sumbawanga kwa msongo wa kV 400 pamoja na umeme utakaozalishwa kutoka mradi wa Malagarasi.
Amesema mradi huo umefikia asilimia 47 ya utekelezaji na unagharimu takribani shilingi bilioni 434 zilizotolewa na Serikali ya Tanzania, Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) pamoja na Mfuko wa Maendeleo wa Watu wa Korea Kusini (EDCF).

EWURA YAFUTA LESENI YA IYAN ENERGY,YASITISHA YA CRESCENT ENERGY KWA MIEZI SITA
habari
Na Mwandishi Wetu
Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) imetangaza kufuta leseni ya rejareja ya bidhaa za mafuta ya petroli ya kampuni ya Iyan Energy Limited na kusitisha kwa muda wa miezi sita leseni ya kampuni ya Crescent Energy Tanzania Limited, baada ya kubaini ukiukwaji wa sheria na masharti ya leseni.
Kwa mujibu wa taarifa ya EWURA, uamuzi huo umefanyika kufuatia maamuzi yaliyotolewa na Bodi ya Wakurugenzi wakati wa vikao vyake vya hivi karibuni.
EWURA imesema leseni iliyofutwa ni Petroleum Retail Licence Na. PRL-2018-269, iliyokuwa ikimilikiwa na Iyan Energy Limited kwa ajili ya kuendesha biashara ya rejareja ya mafuta katika Kiwanja Na. 26 na 27, Barabara ya Pangani, Jiji la Tanga.
Wakati huohuo, Bodi imesitisha kwa muda wa miezi sita leseni ya rejareja ya bidhaa za mafuta ya petroli Namba PRL-2022-296 ya Crescent Energy Tanzania Limited, iliyotolewa kwa ajili ya kuendesha biashara ya rejareja katika Kiwanja Na. 5, Kitalu “N”, Eneo la Chamakweza, Wilaya ya Chalinze, Mkoa wa Pwani.
Taarifa hiyo imeeleza kuwa maamuzi hayo yamefanyika baada ya EWURA kujiridhisha kuwa kampuni hizo zilikuwa zikijihusisha na shughuli zinazofanana na biashara ya uuzaji wa bidhaa za mafuta kwa jumla, hali ambayo haikuruhusiwa chini ya leseni za rejareja walizokuwa nazo.
EWURA imeeleza kuwa hatua hizo zinakiuka Kifungu Na. 131 cha Sheria ya Petroli, Sura ya 392, pamoja na Kanuni ya 9 na 11 za Kanuni za Mafuta (Biashara ya Jumla, Uhifadhi, Rejareja na Matumizi Binafsi), Tangazo la Serikali Na. 150/2022.
Onyo kwa umma
Katika taarifa yake, EWURA imeutaarifu umma kuwa kujihusisha kwa namna yoyote na kampuni hizo katika biashara ya usambazaji wa bidhaa za mafuta ya petroli kutakuwa kinyume cha sheria, na kwamba hatua stahiki za kisheria zitachukuliwa dhidi ya watakaokiuka.
Mamlaka hiyo imeongeza kuwa itaendelea kusimamia sekta ya mafuta kwa kuhakikisha kunakuwa na mazingira ya ushindani wa haki na upatikanaji wa uhakika wa bidhaa za mafuta nchini, kwa kudumisha “uwanja ulio sawa” kwa wadau wote.
CCM NA FRELIMO KUIMARISHA USHIRIKIANO WA KIUCHUMI
siasaKatibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dkt. Asha-Rose Migiro, amekutana na kufanya mazungumzo na Katibu Mkuu wa Chama cha FRELIMO, (Msumbiji), Ndugu Chakil Felizardo Passadas Aboobacar, ambaye ameanza ziara rasmi ya kikazi kwa siku mbili nchini.
Katika mazungumzo hayo yaliyofanyika leo tarehe 6 Machi 2026, katika Ofisi Ndogo za Makao Makuu ya CCM, Dar Es Salaam, vyama hivyo viwili ambavyo vina urafiki na udugu wa kihistoria, vimekubaliana kuendelea kuimarisha uhusiano uliopo kati ya pande hizo mbili, hasa kushirikiana kiuchumi.
.jpeg)

.jpeg)



































