HABARI

SIASA

ELIMU

Recent Posts

WATANZANIA KUNUFAIKA NA UMEME WA UHAKIKA; MRADI WA CHALINZE–DODOMA WAFIKIA ASILIMIA 89 YA UTEKELEZAJI

July 01, 2026 Add Comment

 


📌 utaimarisha upatikanaji wa umeme kwa wananchi, viwanda na shughuli za kiuchumi

📌 Wananchi wanatarajiwa kunufaika na huduma ya umeme yenye uhakika zaidi baada ya kukamilika kwa mradi

📌 TANESCO yavunja rekodi kwa kuunganisha zaidi ya wateja laki nane mwaka 2025/26

Na Mwandishi Wetu, Morogoro

Watanzania katika maeneo mbalimbali nchini wanatarajiwa kunufaika na huduma ya umeme yenye uhakika zaidi kutokana na maendeleo makubwa ya ujenzi wa njia ya kusafirisha umeme ya msongo wa kilovoti 400 kutoka Chalinze hadi Dodoma, ambayo sasa imefikia asilimia 89 ya utekelezaji.

Mradi huo wenye urefu wa kilometa 345 unatarajiwa kukamilika Agosti 21, 2026 na utaongeza uwezo wa kusafirisha umeme kutoka vyanzo vikubwa vya uzalishaji kwenda maeneo yenye mahitaji makubwa ya nishati, hatua itakayochochea maendeleo ya kiuchumi na kuboresha maisha ya wananchi.

Akikagua maendeleo ya mradi huo Julai 1, 2026, Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi (Mb), amesema mradi huo ni uwekezaji muhimu unaolenga kuhakikisha wananchi wanapata umeme wa uhakika kwa matumizi ya nyumbani, biashara ndogo na kubwa, pamoja na shughuli za uzalishaji.

Amesema kukamilika kwa mradi huo kutasaidia kuimarisha Gridi ya Taifa na kuwezesha umeme unaozalishwa katika Kituo cha Kufua Umeme cha Julius Nyerere chenye uwezo wa megawati 2,115 kuwafikia wananchi na sekta mbalimbali za uchumi kwa ufanisi zaidi.

“Umeme wa uhakika una maana ya maisha bora zaidi kwa wananchi, biashara kukua, viwanda kufanya kazi bila kukatika kwa huduma na huduma za kijamii kama hospitali na shule kuendelea kutoa huduma kwa ufanisi,” amesema Mhe. Ndejembi.

Aidha, amesema Serikali itaendelea kuwekeza katika miradi ya umeme ili kuhakikisha Watanzania wengi zaidi wanapata huduma ya nishati inayowawezesha kuongeza kipato na kuboresha ustawi wao.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO, Bw. Razalo Twange, amesema ongezeko la uwekezaji katika miundombinu ya umeme limechangia kuongezeka kwa kasi ya uunganishaji wa wateja wapya, jambo linaloonesha namna umeme unavyoendelea kuwa sehemu muhimu ya maisha na maendeleo ya wananchi.

Amesema katika mwaka wa fedha 2025/26, TANESCO imeweka rekodi mpya kwa kuunganisha zaidi ya wateja laki nane, idadi ambayo haijawahi kufikiwa tangu Tanzania ipate uhuru.

“Kila mteja mpya anayepata umeme ni fursa mpya ya biashara, elimu bora kwa watoto, huduma bora za afya na ongezeko la kipato kwa familia. Hii ndiyo maana ya uwekezaji huu mkubwa wa Serikali katika sekta ya umeme,” amesema Bw. Twange.

Awali, Meneja wa Mradi, Mha. Newton Mwakifamba, amesema kazi zinaendelea vizuri na zinatarajiwa kukamilika Agosti 21, 2026 kwa mujibu wa ratiba ya mkataba, na hivyo kufungua ukurasa mpya wa upatikanaji wa umeme wa uhakika kwa Watanzania wengi zaidi.






OFISI YA WAZIRI MKUU NA TAASISI YA CHAKULA NA LISHE TANZANIA KUSHIRIKIANA KUANDAA MPANGO WA LISHE TAIFA

July 01, 2026 Add Comment

 Na Mwandishi wetu- Dodoma 




Na Mwandishi Wetu- Dodoma


Kaimu Mkurugenzi wa Taasisi ya Chakula na  Lishe  Tanzania  (TFNC) Bi. Debora Charwe amesema, Serikali ipo katika mchakato wa kuandaa Mpango wa Muda Mrefu wa Lishe wa Taifa (NN-LTP)  ili kuongeza jitihada za sekta mtambuka  katika kuboresha utekelezaji wa  lishe kwa kipindi cha miaka 25 ijayo.


Bi. Debora ameyasema hayo leo tarehe 30 Juni, 2026 wakati akifungua Warsha ya mafunzo kuhusu kuandaa mpango wa muda mrefu wa lishe wa Taifa (National Nutrition Long Term  Plan  2026-2050) ambayo  inafanyika jijini Dodoma kwa siku tatu kuanzia Juni 30 hadi Julai 02, 2026

Amesema, mafunzo hayo yanatolewa kwa Wataalam  kutoka ngazi ya Wizara mbalimbali kwa lengo la kuwajengea uwezo kuhusu uandaaji wa  mipango ya muda mrefu  wa lishe  inayojumuisha sekta mtambuka pamoja na  kubadilishana uzoefu kusaidia katika usanifu, muundo na taratibu za utekelezaji wa Mpango wa muda mrefu wa Lishe wa Taifa.








Vilevile Bi. Debora amefafanua kuwa, mpango huo  unaandaliwa chini ya usimamaizi wa Ofisi ya Waziri  Mkuu  kwa kushirikiana na Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania (TFNC)  na wadau wengine wa maendeleo kwa kuzingatia haja ya  kuifanya lishe kuwa moja ya kichocheo  na kipimo katika  kufikiwa kwa malengo ya Dira  ya Maendeleo ya Tanzania kufikia 2050. 

 Aidha, warsha hiyo imehusisha Afisa viungo wa lishe kutoka Wizara mbalimbali zikiwemo Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, Ofisi ya Rais Maendeleo ya Vijana, Ofisi ya Waziri Mkuu TAMISEMI, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Ajira na Mahusiano) pamoja na  Wizara ya Kilimo, Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Wizara ya Viwanda, Wizara ya Maji na Wizara ya Mambo na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.

==MWISHO==

SAFARI YA UTEKELEZAJI DIRA 2050 YAANZA LEO

July 01, 2026 Add Comment


Baada ya Mheshimiwa Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan kuzindua Dira 2050, Julai 17, 2025 jijini Dodoma, hatimaye leo tarehe 1 Julai, 2026, Tanzania imeanza rasmi utekelezaji wa Dira hiyo.

Kuanza kwa utekelezaji wa Dira 2050 kunahitimisha safari ndefu ya utekelezaji wa DIRA 2025 na kuanza kwa safari nyingine ya robo karne (miaka 25) inayolenga kubadilisha sura ya kiuchumi, kijamii, na kiteknolojia ya taifa letu.

Kwa mujibu wa Katibu Mkuu Ofisi ya Rais-Mipango na Katibu Mtendaji wa Tume ya Taifa ya Mipango Dkt. Tausi M. Kida, Dira ya 2050 imejengwa juu ya misingi ya ushiriki wa moja kwa moja wa mwananchi. Kuanzia kwa mkulima wa kijijini hadi kwa mbunifu wa teknolojia mjini, kila mmoja leo anaanza kuhesabiwa kama injini ya mabadiliko haya.

"Huu ni wakati wa kuangalia jinsi kila sekta, (binafsi na ya umma) inavyoingiza vipaumbele vya Dira 2050 kwenye utendaji wake wa kila siku, kwa kuwa mafanikio ya utekelezaji wake yanategemea ushiriki wa kila mmoja wetu" amesema Dkt. Kida.

Dira hiyo, inatarajiwa kujenga Taifa jumuishi lenye ustawi, haki na linalojitagemea, Taifa litakalokuwa na uchumi imara, jumuishi na wenye Pato la thamani ya dola za Marekani trilioni moja ifikapo 2050.

DKT. HINGORA: MAFANIKIO DHIDI YA EBOLA YANATEGEMEA USHIRIKIANO WA WADAU

July 01, 2026 Add Comment
Wizara ya Afya imewataka waandishi wa habari na wadau wa mitandao ya kijamii kuendelea kutoa taarifa sahihi, kwa wakati na kutoka katika vyanzo rasmi ili kuimarisha uelewa wa wananchi na kuimarisha utayari wa taifa dhidi ya ugonjwa wa Ebola na dharura nyingine za afya ya umma.

BIMA YA AFYA ZA WEZESHWA KWA WANAGENZI

July 01, 2026 Add Comment
-IKUJUMUISHWA NA POSHO YA USAFIRI

SERIKALI YAIMARISHA USHIRIKIANO NA SEKTA BINAFSI KUKUZA UCHUMI

June 30, 2026 Add Comment
Serikali imeahidi kuendelea kufanya mageuzi ya sera, sheria, kanuni na mifumo ya utoaji huduma ili kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji nchini, hatua inayolenga kuiwezesha sekta binafsi kuwa injini ya ukuaji wa uchumi na utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.

TIPER YAANDIKA HISTORIA, YAKABIDHI SERIKALI GAWIO LA SH. BILIONI 15

June 30, 2026 Add Comment
Rais wa Jamhuri ya Muungwana wa Tanzania Dk.Samia Suluhu Hassan (katikati)akikabidhiwa gawio la Sh.bilioni 15 kutoka kwa  Mwenyekiti wa Bodi ya Tiper Balozi Mathias Chikawe(kushoto) na Mkurugenzi Mtendaji wa Tiper  Mohamed Mohamed (kulia) wakati wa hafla ya Siku ya Gawio iliyofanyika Ikulu Dar es Salaam ambapo mashirika na taasisi mbalimbali ambazo Serikali inahisa wamekabidhi gawio serikalini.

UKARABATI WA KITUO CHA KUZALISHA UMEME CHA HALE WAFIKIA ASILIMIA 83 YA UTEKELEZÀJI

June 30, 2026 Add Comment



📌 Waziri Ndejembi amtaka mkandarasi kukamilisha ukarabati kwa wakati bila kuongezewa muda wa mkataba


📌 Kukamilika kwake  kutaongeza ufanisi wa uzalishaji na kuimarisha upatikanaji wa umeme wa uhakika Mkoa wa Tanga na maeneo ya jirani


Na Mwandishi Wetu, Korogwe – Tanga


Serikali imeendelea kusimamia utekelezaji wa miradi ya ukarabati wa miundombinu ya umeme nchini, huku Mradi wa Ukarabati wa Kituo cha Kuzalisha Umeme cha Hale wilayani Korogwe, mkoani Tanga, ukifikia asilimia 83 ya utekelezaji.


Akikagua maendeleo ya Mradi huo tarehe 29 Juni, 2026 Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi (Mb), amemtaka mkandarasi kuhakikisha anakamilisha kazi ndani ya muda uliopangwa, akisisitiza kuwa Serikali haitakuwa tayari kuongeza muda wa mkataba wa utekelezaji wa mradi huo.


Waziri Ndejembi amesema kukamilika kwa ukarabati wa Kituo cha Hale kutaimarisha ufanisi wa uzalishaji wa umeme, kuongeza upatikanaji wa umeme wa uhakika na kuchochea shughuli za kiuchumi katika Mkoa wa Tanga na maeneo ya jirani.


“Mkandarasi ahakikishe anakamilisha mradi huu kwa muda uliopangwa ifikapo Julai 31 mwaka huu, ili wananchi waanze kunufaika na huduma ya umeme wa uhakika pamoja na kuimarisha maendeleo ya kiuchumi,” amesema Mhe. Ndejembi.



Kwa upande wake, Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa Usambazaji Umeme TANESCO, Mhandisi Timoth Mgaya, amesema mradi huo unagharimu dola za Kimarekani milioni 24.81, sawa na takribani shilingi bilioni 64, na hadi sasa umefikia asilimia 83 ya utekelezaji.

“Mradi huu unagharimu dola milioni 24.81 ambazo ni sawa na shilingi bilioni 64. Hadi sasa utekelezaji umefikia asilimia 83, na tunaendelea kushirikiana na mkandarasi kuhakikisha kazi zilizobaki zinakamilika ndani ya muda uliopangwa,” amesisitiza Mhandisi Mgaya



Mradi wa ukarabati wa Kituo cha Kuzalisha Umeme cha Hale unalenga kuongeza ufanisi wa kituo hicho, kuboresha utegemevu wa uzalishaji wa umeme na kuendelea kuimarisha upatikanaji wa huduma ya umeme wa uhakika kwa wananchi.


Kituo cha Kuzalisha Umeme cha Hale ni kituo cha kwanza cha kuzalisha umeme kwa kutumia maji nchini. Kilijengwa kati ya mwaka 1961 na 1964 na kina uwezo wa kuzalisha takribani megawati 21. Ukarabati unaoendelea unalenga kuongeza ufanisi wa kituo hicho ili kiendelee kutoa mchango mkubwa katika Gridi ya Taifa kwa miaka ijayo.

TWIGA – BARRICK KINARA KUTOA GAWIO KWA SERIKALI 2026, YATOA KIASI CHA SHILINGI BILIONI 221.9

June 30, 2026 Add Comment

      

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan (katikati), akimkabidhi tuzo Meneja Mkazi wa Barrick nchini Tanzania, Dk. Melkiory Ngido (kulia), kwa kutambua mchango wa kampuni hiyo kupitia utoaji wa gawio kwa Serikali. Kushoto ni Mwenyekiti wa Bodi ya Twiga Minerals Corporation, Bw. Mathias Chanila.
Meneja Mkazi wa Barrick nchini Tanzania, Dk. Melkiory Ngido (kulia), akimkabidhi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan (kushoto), hundi mfano (Dummy Cheque). Katikati ni Mwenyekiti wa Bodi ya Twiga Minerals Corporation, Mathias Chanila.
***

Ubia kati ya kampuni ya Barrick Mining Corporation na Serikali ya Tanzania kupitia kampuni ya Twiga Minerals Corporation unaendelea kujenga thamani katika uchumi wa Tanzania, ambapo leo migodi ya Barrick nchini imetoa gawio la Shilingi 221,907,320,687 kwa Serikali na kutunukiwa tuzo ya nafasi ya kwanza kwa kuongoza kwa kutoa gawio kubwa mwaka huu.

DMG YATUNUKIWA TUZO KWA MAGEUZI YA SEKTA YA MELI

June 30, 2026 Add Comment

    

By Staff Writer

Morogoro, Tanzania – June 27, 2026_ — Dar es Salaam Merchant Group (DMG) has clinched the coveted _Best Maritime Technology Company of the Year_ award at the 2026 Morogoro Business Awards, cementing its position as a leader in Tanzania’s technological transformation of the blue economy.

NAIBU WAZIRI OFISI YA WAZIRI MKUU KAZI,AJIRA NA MAHUSIANO DKT EVELINE MUNISI AKIPATA MAELEKEZO KWA VIJANA WANAOPATA MAFUNZO YA UANAGENZI

June 30, 2026 Add Comment


Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Ajira na Mahusiano Mhe. Dkt. Eveline Munisi akipata maelezo kutoka kwa  vijana wanaopata mafunzo ya Uanagenzi awamu ya 8 ya mwaka 2025/2026 katika ziara yake ya kikazi katika  ufatiliaji wa maendeleo ya Mafunzo ya Uanagenzi Chuo cha Maendeleo ya Vijana Sengerema (FDC) Juni 29, 2026 Wilaya ya Sengerema, Mkoani Mwanza.




DKT. KIJAJI AELEKEZA MAAFISA UHIFADHI KUHAKIKISHA MAENEO YA HIFADHI YANALINDWA NA KUHIFADHIWA

June 30, 2026 Add Comment



Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (Mb) amewaelekeza maafisa uhifadhi nchini kuhakikisha maeneo yote ya hifadhi yanalindwa na kuhifadhiwa kwa manufaa ya vizazi vya sasa na vijavyo.


Dkt. Kijaji ametoa maelekezo hayo leo jijini Dodoma wakati wa kikao kilichowakutanisha Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Mhe. Paul Chacha, Wakuu wa Wilaya wa mkoa huo, watumishi wa Wizara ya Maliasili na Utalii ikiwemo viongozi kutoka  Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS), Mamlaka ya Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) na Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA).

 Kikao hicho kilijadili ongezeko la uvamizi na uharibifu wa misitu unaofanywa na watu mbalimbali katika maeneo ya hifadhi, hali inayohatarisha rasilimali za misitu na wanyamapori pamoja na juhudi za Serikali katika usimamizi endelevu wa maliasili.

Katika kikao hicho, Dkt. Kijaji amesisitiza kuwa maazimio yote yaliyofikiwa katika kikao hicho yanapaswa kutekelezwa kikamilifu na kwa wakati, akieleza kuwa hakuna nafasi ya uzembe katika kulinda maeneo yaliyotengwa kwa ajili ya uhifadhi.

Sambamba na hilo, amewataka watendaji wote wenye dhamana ya usimamizi wa maeneo ya hifadhi kutekeleza majukumu yao kwa weledi na uwajibikaji wa hali ya juu, akionya kuwa watakaoshindwa kutekeleza majukumu yao ipasavyo watachukuliwa hatua kali kwa mujibu wa sheria.

Aidha, Dkt. Kijaji ametumia fursa hiyo kumpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuendelea kuimarisha sekta ya uhifadhi kupitia utoaji wa ajira kwa wahifadhi pamoja na kuongeza bajeti ya sekta hiyo, hatua zinazochangia kuimarisha ulinzi na usimamizi wa maeneo ya hifadhi nchini.

Amesema pia ni wajibu wa viongozi wa Wizara na wa Mkoa kuhakikisha sheria zinasimamiwa kikamilifu ili kulinda rasilimali za taifa zilizopo katika maeneo ya hifadhi.

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Mhe. Paulo Chacha, amesema kikao hicho kimekuwa na manufaa makubwa katika kuweka mikakati madhubuti ya kukabiliana na uvamizi wa maeneo ya hifadhi na kuimarisha ushirikiano kati ya Wizara na viongozi wa mkoa.

Naye Kaimu Mkurugenzi wa Misitu kutoka Wizara ya Maliasili na Utalii, Daniel Pancras, amesema watahakikisha maeneo yote ya misitu yanalindwa na kuhifadhiwa ipasavyo, huku akiahidi kuwa maazimio na maelekezo yote yaliyotolewa katika kikao hicho yatafanyiwa kazi kwa ufanisi.

Aidha, Dkt. Kijaji amesisitiza kuwa maelekezo yaliyotolewa na Mawaziri wanane wa kisekta kuhusu ulinzi wa maeneo ya hifadhi yatekelezwe kikamilifu katika mikoa yote nchini ili kuimarisha uhifadhi wa rasilimali za taifa na kuhakikisha sheria zinafuatwa bila upendeleo.






 

DKT MUNISI: PROGRAMU YA TAIFA YA UKUZAJI UJUZI YAENDELEA KUWAJENGA VIJANA

June 30, 2026 Add Comment


✅VIJANA 5,746 WANUFAIKA NCHINI

Na: Mwandishi Wetu - Mwanza

Serikali imeendelea kudhihirisha dhamira thabiti ya kuwawezesha vijana kiujuzi kupitia Programu ya Taifa ya Ukuzaji Ujuzi.

Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Ajira na Mahusiano, Dkt. Evaline Munisi amesema hayo leo Juni 29, 2026 Mwanza alipotembelea Chuo cha Maendeleo ya Wananchi Sengerema FDC kwa lengo la kukagua maendeleo ya mafunzo ya Uanagenzi yanayotolewa kupitia programu hiyo.

Amesema, Serikali inalenga kujenga nguvukazi yenye ujuzi, maarifa na ubunifu ili kukidhi mahitaji ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 na kuongeza ushindani katika soko la ajira la ndani na nje ya nchi.

Dkt. Munisi alisema Serikali kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano inaendelea kutekeleza Programu ya Taifa ya Kukuza Ujuzi kwa kushirikiana na sekta binafsi kupitia mfumo wa ubia (PPP), huku mafunzo ya uanagenzi yakichukua nafasi muhimu katika kuziba pengo la ujuzi kwa vijana. 

Vile vile, amesema kuwa mfumo huo unamwezesha mwanagenzi kutumia asilimia 40 ya muda kujifunza nadharia darasani na zaidi ya asilimia 60 kupata uzoefu wa vitendo sehemu za kazi, huku Serikali ikigharamia ada zote za mafunzo hayo kwa asilimia 100.

Kadhalika, Mhe. Munisi alisema katika awamu ya nane ya programu hiyo, Serikali imeboresha mazingira ya mafunzo kwa kuwapatia wanagenzi 5,746 bima ya afya pamoja na posho ya usafiri ya shilingi 100,000 kwa mwezi kwa kipindi cha miezi miwili watakapokuwa kwenye mafunzo ya vitendo. Aliwataka viongozi wa vyuo kuendelea kuwajengea vijana kimaadili, nidhamu, uzalendo na uwajibikaji pamoja na kuimarisha ushauri nasaha na ushirikiano na waajiri ili kuhakikisha wanagenzi wanapata mafunzo yenye tija.

Kwa upande wake, Kaimu Mkurugenzi Idara ya Ajira na Ukuzaji Ujuzi, Bi. Alana Nchimbi, alisema Programu ya Taifa ya Kukuza Ujuzi ilianzishwa mwaka 2016/17 ikiwa na lengo la kuongeza ujuzi wa nguvukazi na kukuza ajira nchini. Alibainisha kuwa hadi sasa jumla ya Watanzania 168,657 wamenufaika na programu hiyo kupitia maeneo manne ya utekelezaji ambayo ni mafunzo ya uanagenzi, uzoefu wa kazi kwa wahitimu, urasimishaji wa ujuzi uliopatikana nje ya mfumo rasmi wa elimu na kuongeza ujuzi kwa wafanyakazi.

Bi. Nchimbi alisema katika mwaka wa fedha 2025/26, mafunzo ya uanagenzi yanatekelezwa katika vyuo na taasisi 46 zilizopo katika mikoa 25 ya Tanzania Bara, yakihusisha vijana 5,746 katika fani mbalimbali. Mkoa wa Mwanza unashiriki kupitia vyuo vitatu ambavyo ni Chuo cha Maendeleo ya Wananchi Sengerema, Chuo cha Maendeleo ya Wananchi Malya na Pine College, vyenye jumla ya wanagenzi 339.

Mmoja wa Wanagenzi  alimshkuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, pamoja na Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano kwa kuwezesha mafunzo hayo kwa kugharamia ada kwa asilimia 100 na kuwapatia bima ya afya. 

Walisema tangu kuanza kwa mafunzo Januari 2026 wamepata ujuzi wa kitaaluma, uwezo wa kujitegemea, kujenga mahusiano ya kikazi na mbinu za kupata wateja, huku baadhi yao tayari wakianza kujipatia kipato kupitia ujuzi walioupata.

Hata hivyo, wanagenzi hao waliiomba Serikali kuendelea kushirikiana na waajiri ili kuongeza nafasi za mafunzo kwa vitendo, wakieleza kuwa baadhi ya taasisi na waajiri bado wanatoza fedha ili kutoa nafasi za mafunzo. Walisisitiza kuwa mafunzo ya uanagenzi yamewapa msingi imara wa kujiajiri na kuajiriwa, na kuahidi kutumia ujuzi walioupata kuchangia maendeleo ya Taifa kupitia uzalishaji, ubunifu na utoaji wa huduma bora.


Aidha, amesema Programu hiyo inalenga kuwajengea vijana stadi zinazokidhi mahitaji ya soko la ajira, kuongeza fursa za kujiajiri na kuimarisha mchango wao katika maendeleo ya uchumi wa taifa.

MWISHO




 

MANISPAA YA MOSHI YAKANUSHA KUBADILI MATUMIZI YA ENEO LA UHURU PARK..

June 29, 2026 Add Comment

Moshi.

Halmashauri ya Manispaa ya Moshi imesema haijabadilisha matumizi ya eneo lolote la wazi, ikieleza kuwa kinachoendelea katika eneo la Uhuru Park ni utekelezaji wa mpango wa muda mrefu wa kuboresha eneo hilo bila kuathiri matumizi yake ya awali.

Hayo yamebainishwa jana na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Manispaa ya Moshi, Mwajuma Nasombe, alipozunguma kuhusiana na tetesi za kubadilishwa kwa matumizi ya eneo hilo.

Alisema kuwa, ofisi yake haijabadilisha matumizi ya ardhi katika eneo lolote na kudai  baada ya Waziri Mkuu kuagiza Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro kufuatilia suala hilo, Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa ilitembelea eneo husika na taarifa ya uchunguzi itawasilishwa serikalini.
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Kamati ya Mipango Miji ya Halmashauri ya Manispaa ya Moshi, Francis Shio, alisema eneo la Uhuru Park lina hati miliki ya halmashauri na tangu awali lilipangwa kutumika kama eneo la wananchi kupumzika na kufanyia shughuli mbalimbali za kijamii.

Alisema ujenzi unaoendelea wa vibanda vinavyozunguka eneo hilo ni sehemu ya mpango wa kulijengea uzio, kuweka mageti ya kuingilia na kutokea pamoja na kuimarisha usalama na mazingira ya bustani hiyo.

"Mpango huu si wa leo, miaka ya nyuma tayari halmashauri ilijenga vibanda takribani 39 katika eneo hilo. Sasa tunaendelea na hatua nyingine za utekelezaji wa mpango huo," alisema Shio.

Alieleza kuwa baada ya kukamilika kwa uzio, eneo hilo litaboreshwa kwa ndani kwa kuweka sehemu za watoto kuchezea, maeneo ya mapumziko na huduma nyingine zitakazowezesha wananchi kulitumia kwa usalama zaidi.

"Lengo letu si kubadilisha matumizi ya eneo hili, bali kulifanya liwe salama na lenye huduma bora. Mzazi atakapomleta mtoto wake atakuwa na uhakika wa usalama kutokana na uwepo wa uzio," alifafanua.




 

THBUB YAWAFIKIA ZAIDI YA WANANCHI 89,000 KUPITIA ELIMU YA HAKI ZA BINADAMU

June 29, 2026 Add Comment

 


Na Mwandishi Wetu- Dar es Salaam


Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB) imeendelea kuimarisha uelewa wa wananchi kuhusu haki za binadamu na misingi ya utawala bora kwa kuwafikia zaidi ya wananchi 89,000 kupitia njia mbalimbali za utoaji elimu katika mwaka wa fedha 2025/2026.


Elimu hiyo ilitolewa kupitia mafunzo kwa makundi mbalimbali ya jamii, vipindi vya redio na televisheni, mitandao ya kijamii, huduma ya ujumbe mfupi wa simu (Bulk SMS) pamoja na usambazaji wa vipeperushi na machapisho ya elimu.


Taarifa hiyo imetolewa na Msemaji wa Tume hiyo ambaye pia ni Mkurugenzi wa Elimu kwa Umma, Mawasiliano,Utafiti na Nyaraka wakati akiongea na vyombo vya habari katika viwanja vya Maonesho ya Kimataifa ya Biashara saba saba leo Juni 29,2029


Bi. Mnanka amesema katika kipindi hicho, wananchi zaidi ya 80,000 walifikishiwa ujumbe wa elimu kupitia simu za mkononi, huku vipeperushi 39,129 na vitabu 200 vya elimu vikisambazwa kwa wananchi ili kuongeza uelewa kuhusu haki za binadamu, utawala bora na namna ya kuwasilisha malalamiko THBUB.


Aidha, Tume ilirusha vipindi 79 vya elimu kupitia redio na televisheni, hatua iliyochangia kuwafikia wananchi wengi zaidi nchini.


THBUB imesema itaendelea kutumia teknolojia na majukwaa mbalimbali kuhakikisha elimu ya haki za binadamu inawafikia Watanzania wengi zaidi.


Pia, Bi. Mnanka amesema THBUB imeendelea kuwekeza katika elimu ya haki za binadamu kwa kutoa mafunzo kwa zaidi ya washiriki 9,300 kutoka makundi mbalimbali ya jamii nchini katika mwaka wa fedha 2025/2026.


Akitoa takwimu ya walionufaika na mafunzo hayo, Bi. Mnanka ametaja makundi hayo kuwa ni pamoja na askari wa Jeshi la Polisi 827, waandishi wa habari 324, madiwani 60, wanafunzi zaidi ya 8,000 na walimu 121 kutoka vyuo vikuu tisa pamoja na taasisi nyingine za elimu.


Mafunzo hayo yalilenga kuongeza uelewa kuhusu haki za binadamu, misingi ya utawala bora na wajibu wa kila mmoja katika kulinda na kuheshimu haki hizo.


“…..kuwajengea uwezo makundi mbalimbali katika jamii ni hatua muhimu ya kuimarisha utamaduni wa kuheshimu haki za binadamu na kuzuia vitendo vya uvunjifu wa haki na ukiukwaji wa misingi ya utawala bora…..” amesema Bi.Mnanka.

IRELAND YAHAKIKISHA KUENDELEA KUFADHILI MIRADI YA USAWA WA KIJINSIA VYUONI

June 29, 2026 Add Comment
NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

Serikali ya Ireland imesisitiza kuendelea kuunga mkono juhudi za kukuza usawa wa kijinsia na uwezeshaji wa wanawake katika taasisi za elimu ya juu nchini Tanzania, ikieleza kuwa elimu jumuishi ni msingi wa maendeleo endelevu na jamii yenye usawa.

WAZIRI NDEJEMBI -MRADI WA EACOP WAELEKEA UKINGONI MELI YA KWANZA KUBEBA MAFUTA JANUARI 2027

June 29, 2026 Add Comment




Na Oscar Assenga, Tanga

WAZIRI wa Nishati, Dkt. Deogratius Ndejembi, amesema ujenzi wa Mradi wa Bomba la Kusafirisha Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki (EACOP) umefikia asilimia  86, huku mafuta ya kwanza yakitarajiwa kupokelewa katika Kituo cha Chongoleani, Tanga, na kusafirishwa Januari mwaka 2027.

Dkt. Ndejembi alisema hayo leo baada ya kutembelea eneo la mradi Chongoleani, mkoani Tanga, kujionea maendeleo ya utekelezaji wake, ambapo alieleza kuwa matarajio ni kukamilisha ujenzi huo ifikapo mwisho wa Agosti mwaka huu.

Alisema kazi nyingi muhimu zimekamilika na kilichobaki ni hatua za mwisho ikiwemo kukamilisha miundombinu ya umeme ili kuwezesha mitambo ya kusukuma mafuta kufanya kazi.

"Nimefurahishwa na maendeleo ya mradi. Kazi kubwa imefanyika na tunaamini ifikapo mwisho wa Agosti ujenzi utakuwa umekamilika. Ratiba inaonyesha kuwa meli ya kwanza itachukua mafuta ghafi kutoka Chongoleani mwezi Januari, 2027," alisema.

Hata hivyo, alisema changamoto iliyobaki ni kukamilika kwa njia ya umeme kutoka Majani Mapana kuelekea eneo la mradi, huku akiutaka mkandarasi anayetekeleza kazi hiyo chini ya Tanesco kuhakikisha anakamilisha mradi huo kwa wakati.

Alionya kuwa mkandarasi atakayeshindwa kutekeleza kazi hiyo ndani ya muda uliopangwa atachukuliwa hatua, ikiwemo kuondolewa katika orodha ya wakandarasi wanaofanya kazi na Tanesco.

Dkt. Ndejembi alisema EACOP ni mradi wa kimkakati kwa Tanzania, Uganda na ukanda mzima wa Afrika Mashariki, akibainisha kuwa bomba hilo lenye urefu wa zaidi ya kilomita 1,400 ni la kwanza duniani lenye mfumo wa kupashwa joto katika urefu wake wote.

Alisema Serikali ya Tanzania imewekeza zaidi ya Sh bilioni 973 kupitia Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC), ambalo linamiliki asilimia 15 ya hisa za mradi huo kwa kushirikiana na kampuni za UNOC, TotalEnergies na CNOOC.

Aidha, aliwataka Watanzania kuendelea kutumia fursa zinazotokana na mradi huo, akieleza kuwa zaidi ya Watanzania 3,000 wamepata ajira za moja kwa moja, huku vijana wengine zaidi ya 100 wakipelekwa Madimba kwa mafunzo ya kuongeza ujuzi kabla ya kuajiriwa.

Aliongeza kuwa zaidi ya vijana 400 kutoka Chongoleani wamepatiwa mafunzo na kuajiriwa katika maeneo mbalimbali ya mradi huo, huku fursa nyingine nyingi zikiendelea kujitokeza.

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Balozi Dkt. Batilda Burian, alisema mradi huo umeendelea kuleta manufaa makubwa kwa mkoa huo kupitia ongezeko la shughuli za Bandari ya Tanga, mapato ya Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na fursa za ajira kwa wananchi.

Alisema vifaa vingi vya mradi vimepitia Bandari ya Tanga kabla ya kusafirishwa katika maeneo mbalimbali ya utekelezaji wa bomba hilo, jambo lililochochea ukuaji wa shughuli za kiuchumi.

Balozi Burian alisema pia mradi huo umezingatia viwango vya kimataifa vya utunzaji wa mazingira, akieleza kuwa shughuli za uvuvi zinaendelea kama kawaida na hakuna viumbe hai walioathirika kutokana na ujenzi wa gati na miundombinu mingine.

Aliongeza kuwa kupitia mradi huo, Halmashauri na jamii zinazozunguka eneo la mradi zimenufaika na miradi mbalimbali ya maendeleo, ikiwemo ujenzi wa uwanja wa mpira unaotumiwa na klabu ya Coastal Union.

Naye Mkurugenzi wa Rasilimali Watu na Huduma za Mradi wa EACOP, Jofrey Mponda, ambaye pia alizungumza kwa niaba ya uongozi wa EACOP Tanzania, alisema mradi umefikia hatua za mwisho za utekelezaji, huku zaidi ya asilimia 90 ya kazi ikiwa imekamilika.

Alisema mradi huo unaounganisha mikoa 18 ya Tanzania na wilaya 27 umeingia katika hatua ya ukaguzi na makabidhiano ya mifumo mbalimbali, ikiwemo vituo vya kusukuma mafuta, matenki ya kuhifadhi mafuta na miundombinu mingine muhimu.

Mponda alisema pampu sita za kusukuma mafuta zimejengwa, mbili zikiwa nchini Uganda na nne nchini Tanzania, huku pampu mbili za kupunguza shinikizo la mafuta zikiwa Chongoleani.

Alibainisha kuwa matenki manne ya kupokelea mafuta tayari yamekamilika, huku kazi iliyobaki ikiwa ni kuunganisha mfumo wa umeme ili kuwezesha mitambo yote kuanza kufanya kazi kwa wakati.

Alisema EACOP inaendelea kushirikiana kwa karibu na Tanesco kuhakikisha miundombinu ya umeme inakamilika ifikapo Septemba mwaka huu, hatua itakayowezesha maandalizi ya kupokea mafuta ya kwanza mwezi Januari, 2027.