HABARI

SIASA

ELIMU

Recent Posts

WAZIRI MAVUNDE AZINDUA HELIKOPTA YA BARRICK KWA UTAFITI WA KISASA WA KIJIOLOJIA

February 01, 2026 Add Comment

Waziri wa Madini, Anthony Mavunde (katikati) akikata utepe ishara ya kuzindua helikopta ya kisasa ya Kampuni ya Barrick kwa ajili ya kufanya utafiti wa kijiolojia wa anga - Picha na Kadama Malunde
Waziri wa Madini, Anthony Mavunde akipata maelezo wakati akizindua helikopta ya kisasa ya Kampuni ya Barrick kwa ajili ya kufanya utafiti wa kijiolojia wa anga 
Helikopta ya kisasa ya Kampuni ya Barrick kwa ajili ya kufanya utafiti wa kijiolojia wa anga 
Waziri wa Madini, Anthony Mavunde na viongozi ,mbalimbali wakishuhudia helikopta ya kisasa ya Kampuni ya Barrick ikiruka angani kwa ajili ya kufanya utafiti wa kijiolojia wa anga 
Helikopta ya kisasa ya Kampuni ya Barrick ikiwa angani 
Waziri wa Madini, Anthony Mavunde akizungumza wakati akizindua helikopta ya kisasa ya Kampuni ya Barrick kwa ajili ya kufanya utafiti wa kijiolojia wa anga 
Meneja wa Barrick nchini , Dkt. Melkiory Ngido akizungumza wakati wa hafla hiyo
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Mboni Mhita akizungumza wakati wa hafla hiyo.
**

Kampuni ya Barrick ambayo inaendesha shughuli zake kwa ubia na serikali kupitia Twiga Minerals leo imezindua helikopta ya kisasa kwa ajili ya kufanya utafiti wa kijiolojia wa anga wenye kupunguza athari za kimazingira na kuboresha shughuli za utafutaji wa madini nchini.

UKIWA NA JANABA USIINGIE PANGO LA FATUMA KATIKA MAPANGO YA AMBONI TANGA

February 01, 2026 Add Comment




Na Kassim Nyaki, Tanga.

Je umewahi kutembelea Mapango ya Amboni na kupata simulizi zake?

Pengine kwa muda mrefu unatafuta mchumba uoe au uolewe lakini mambo kila ukiyapanga hayakai mkao ulionyooka, suluhisho la jambo hili linapatikana kwa kutembelea mapango ya Amboni Tanga ili uweze kufanikisha lengo lako kupitia pango linaloitwa Fatuma.

Hifadhi ya Mapango ya Amboni ambayo inasimamiwa na Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro yana maajabu mengi lakini mojawapo ni uwepo wa pango la Fatuma linalotumiwa na wageni mbalimbali ambao wana shida zinazowatatiza ikiwemo suala zima la mtu kukwama kutokuoa au kuolewa.

Muongoza watalii katika mapango hayo Muhsini Juma anaeleza kuwa watu wengi wamekuwa wakifanikiwa kupata wenza wao wanapofika katika pango la Fatuma ambalo limekuwa likitumika toka enzi za mababu kwa watu mbalimbali kufika na kuomba kupata mume au mke kwa kuishi nae kama mume na mke

“Katika miaka ya hivi karibuni kumekuwa na changamoto sana ya vijana kupata wake au waume wa kuwaoa, lakini wakifika katika pango hili na kusema nia yao na kutambika basi wanafanikiwa na kumekuwa na shuhuda nyingi za wadau ambao wamefanikisha jambo hilo na kurudi kutupa mrejesho”,alisema Muhsin.

Umaarufu wa pango hili umewafanya wageni kwa nyakati tofauti kutembelea na kujifunza jinsi ya kufanya matambiko hayo na baada ya muda si mrefu basi baadhi hurudi kwa ajili ya shukran na inaaminika kwamba si wenyeji tu wa mkoa wa Tanga wanaotembelea mahali hapo bali pia na watu katika maeneo mengine nje ya nchi.

Muhsin anaeleza kuwa ukifika katika pango la Fatuma kama una mtu ambaye unataka kumuoa au kukuoa basi unataja jina lake na kumuita na haitochukua muda mrefu mtu huyo mwenyewe ataanza kukutafuta kwa lengo la kutaka kuoa au kuolewa.

Na kwa wale ambao hawana mtu kabisa wakifika katika mapango hayo wanachotakiwa kusema ni kwamba mimi mwaka huu nataka kuoa au kuolewa na namkusudia mtu flani, mwenye sifa Fulani... haichukui muda mrefu wanapata wenza wa kufunga nao ndoa.

Pango hili la Fatuma ambalo ni miongoni mwa mapango yaliyopo Amboni pia linatumika kwa kufanya matambiko yanayohusu masuala mbalimbali ya kijamii ikiwemo kupata mtoto, kuombea mvua inyeshe, kupata kazi na mambo mengine na ndiyo maana ukifika katika pango hilo watu kadhaa wa kadhaa hufanya maombi yao na mara nyingi hawataki waonekane zaidi ya kufuata taratibu za wenyeji wao kw autulivu na faragha.

Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro imeweka utaratibu mahsusi wa kuhakikisha kuwa jamii ya mkoa wa Tanga na wale ambao bado wanaamini mambo hayo wanapata wasaa wa kufanya matambiko yao bila kuathiri utamaduni huo uliopo miaka na miaka.



Hayo ndiyo maajabu ya pango la Fatuma na hii inadhihirisha kwamba mwenda tezi na omo marejeo ngamani, Amboni ndiyo ngama yako ya kupata mume au mke ,usidharau mila kwani mdharau mila ni mtumwa.

FEZA BOYS YAFAULISHA KWA ALAMA A; WANAFUNZI WOTE WAPATA MATOKEO MAZURI KIDATO CHA NNE

February 01, 2026 Add Comment

 

Baraza la Mitihani la Taifa (NECTA) limetangaza matokeo ya Mtihani wa Kidato cha Nne, huku baadhi ya wanafunzi wakifutiwa matokeo yao kutokana na makosa ya utovu wa nidhamu, ikiwemo kuandika matusi katika karatasi za mitihani.

Wakati baadhi ya wanafunzi wakikumbana na adhabu hiyo, hali imekuwa tofauti kabisa kwa wanafunzi wa Shule ya Sekondari FEZA Boys, ambapo matokeo yao yameleta furaha kubwa.

Kwa mujibu wa matokeo yaliyotangazwa, jumla ya wanafunzi 71 walifanya mtihani wa Kidato cha Nne katika shule hiyo. Kati yao, wanafunzi 69 wamepata ufaulu wa Daraja la Kwanza (Division I), huku wanafunzi wawili pekee wakipata Daraja la Pili (Division II).

Akizungumza mara baada ya kutangazwa kwa matokeo hayo, Mwalimu wa Taaluma wa shule hiyo, Said Hassan, aliwaeleza waandishi wa habari kuwa siri ya mafanikio hayo ni ushirikiano wa pamoja kati ya wazazi, walimu na wanafunzi, mkakati wanaouita “Utatu Mtakatifu (W3)”.

Alisema kuwa kwa upande wa shule, walimu hutimiza wajibu wao kwa kufundisha kwa bidii, huku wazazi wakipewa jukumu la kuhakikisha mahitaji muhimu ya wanafunzi yanapatikana kwa wakati, hali hiyo humwezesha mwanafunzi kupata muda wa ziada wa kujisomea.

Aidha, shule hiyo ina utaratibu wa kukaa na wanafunzi mmoja mmoja ili kufahamu changamoto zao, jambo linalosaidia kujenga urafiki kati ya mwalimu na mwanafunzi na hivyo kuongeza hamasa ya kupenda masomo.
Pia, shule hufanya mitihani ya mara kwa mara, ikiwemo kwa kushirikiana na shule jirani, hali inayowasaidia wanafunzi kuzoea mitihani na kuichukulia kama jambo la kawaida.

Kwa upande wa wanafunzi bora, Baraka Yunus, aliyepata alama A katika masomo yote, alisema mafanikio hayo yametokana na juhudi za pamoja kati ya shule na wazazi, aliongeza kuwa alipata muda wa kutosha wa kusoma akiwa shuleni na anatarajia kuwa mfanyabiashara baada ya kumaliza masomo yake.

Naye Chriss Mwingila, ambaye pia alipata alama A katika masomo yote, aliwashukuru walimu na wazazi kwa kuwawekea mazingira rafiki ya masomo yaliyowasaidia kupata muda wa kutosha wa kujifunza

Waalimu na wanafunzi wa shule ya Feza Boyz wakishangilia mara baada ya kupata matokeo ya kidato cha nne na kupata ufaulu wa alama A kwa darasa zima

Mwalimu wa taaluma wa shule ya Feza Boyz ,Said Hasan akizungumza na Waandishi wa Habari mara baada ya kutangazwa kwa matokeo ya kidato cha nne jijini Dar es salaam.
Wanafunzi wa shule ya Feza Boyz wakishangilia kwa kuwabeba wanafunzi waliofanya vizuri katika matokeo ya kidato cha nne na kupata ufaulu wa alama A kwa darasa zima

RC SENDIGA, SEKTA BINAFSI WASHIRIKIANA KUWAWEZESHA WAATHIRIKA WA MAJANGA

February 01, 2026 Add Comment

 

Na Mwandishi Wetu, Manyara

Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Mhe. Queen Sendiga, amekabidhi pikipiki ya umeme ya magurudumu matatu iliyotolewa na Mati Foundation kwa binti mwenye ulemavu, Bertina Francis, aliyepoteza wazazi wake wote wawili kufuatia maporomoko ya tope yaliyotokea Wilaya ya Hanang’ mwezi Desemba 2023.

Bertina Francis, ambaye kwa sasa anaishi katika moja ya nyumba zilizojengwa na Serikali kwa ajili ya waathirika wa maporomoko hayo katika eneo la Waret wilayani Hanang’, ameelezwa kuwa anajishughulisha na biashara ndogo ya uuzaji wa vitafunwa. Kupatikana kwa pikipiki hiyo ya umeme kunatarajiwa kumrahisishia shughuli zake za kiuchumi hususan katika usambazaji wa bidhaa zake na hivyo kuongeza kipato na kujitegemea.
Akizungumza wakati wa hafla ya makabidhiano, Mhe. Sendiga amesema msaada huo ni matokeo ya ushirikiano mzuri uliopo kati ya Serikali na sekta binafsi, akisisitiza kuwa ushirikiano huo una mchango mkubwa katika kugusa maisha ya wananchi wenye uhitaji. Amempongeza mwekezaji David Mulokozi kupitia taasisi yake ya Mati Foundation kwa moyo wa kujitolea na kusaidia makundi maalum katika jamii.

“Serikali inaendelea kuhamasisha wawekezaji na taasisi binafsi kushiriki katika maendeleo ya jamii. Msaada huu ni mfano mzuri wa namna sekta binafsi inavyoweza kushirikiana na Serikali kuwainua wananchi walioko katika mazingira magumu,” amesema RC Sendiga.
Kwa upande wake, Bertina Francis ameishukuru Serikali pamoja na Mati Foundation kwa msaada huo, akieleza kuwa pikipiki hiyo itamfungulia fursa zaidi za kiuchumi na kumpa matumaini mapya ya maisha. Ameiomba taasisi hiyo kuendelea kuwasaidia watu wenye uhitaji ili nao wajisikie kuwa sehemu ya jamii na kuchangia katika maendeleo yao binafsi na ya Taifa.

Pikipiki hiyo ya umeme ni sehemu ya mpango unaoendelea wa kampuni ya Mati Super Brands Ltd kupitia taasisi yake ya Mati Foundation wa kugawa pikipiki za magurudumu matatu kwa watu wenye ulemavu zaidi ya 2,000 kote nchini. Mpango huo ulianza rasmi mwezi Septemba 2025 ukiwa na lengo la kuwawezesha watu wenye ulemavu kushiriki kikamilifu katika shughuli za kiuchumi na kijamii.

Hatua hiyo imeelezwa kuwa ni mchango muhimu katika juhudi za Serikali za kuhakikisha makundi maalum yanapata fursa sawa za maendeleo na kujitegemea kiuchumi, hususan kwa waathirika wa majanga mbalimbali nchini.
DC NYAMWESE: MADIWANI MSITANGULIZE MASLAHI BINAFSI KWENYE HALMASHAURI

DC NYAMWESE: MADIWANI MSITANGULIZE MASLAHI BINAFSI KWENYE HALMASHAURI

February 01, 2026 Add Comment

MKUU wa Wilaya ya Handeni, Mhe. Salum Nyamwese,akizungumza wakati akifunga mafunzo ya kuwajengea uwezo madiwani wa Halmashauri ya Mji Handeni, Halmashauri ya Wilaya ya Handeni na Halmashauri ya Wilaya ya Kilindi yaliyolenga kuwaimarisha katika masuala ya utawala bora, ufuatiliaji wa mapato na uelewa wa mipaka ya majukumu yao katika uendeshaji wa halmashauri.

Na Augusta Njoji

MKUU wa Wilaya ya Handeni, Mhe. Salum Nyamwese, amewataka madiwani wa Halmashauri ya Mji Handeni, Halmashauri ya Wilaya ya Handeni na Halmashauri ya Wilaya ya Kilindi kuacha kutanguliza maslahi binafsi au ya kisiasa wanapotekeleza majukumu yao, na badala yake kuweka mbele maslahi ya wananchi na maendeleo ya halmashauri.

Nyamwese ametoa wito huo mjini Handeni wakati akifunga mafunzo ya kuwajengea uwezo madiwani, yaliyolenga kuwaimarisha katika masuala ya utawala bora, ufuatiliaji wa mapato na uelewa wa mipaka ya majukumu yao katika uendeshaji wa halmashauri.

Amesisitiza kuwa serikali haitavumilia uzembe, hujuma wala vitendo vyovyote vinavyozorotesha maendeleo ya halmashauri, akiwataka madiwani kuwa macho na kutoa taarifa kwa wakati pindi wanapobaini mianya ya upotevu wa mapato.

“Tunaomba mkawe wabunifu na mzishauri halmashauri namna bora ya kuboresha na kusimamia vyanzo vya mapato. Nyie ndio mnaoishi na wananchi; mnapobaini kapu linavuja, tuambieni linavuja wapi na nani analivujisha ili hatua stahiki zichukuliwe,” amesema Nyamwese.

Ameongeza kuwa madiwani ni macho na masikio ya serikali katika maeneo yao, hivyo wanapaswa kusimamia nidhamu ya watumishi, kuacha kufanya kazi kwa mazoea na kuchochea ushiriki wa wananchi katika shughuli za maendeleo.

Kwa upande wake, Katibu Tawala wa Wilaya ya Handeni, Margareth Killo, amesema mafunzo hayo yataongeza ufanisi na uwajibikaji wa madiwani katika kuwahudumia wananchi.

Naye, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Handeni, Amiri Mwaliko, pamoja na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilindi, Michael Chabai, wamesema mafunzo hayo yamewawezesha madiwani kufahamu vyema wajibu na mipaka yao, hali itakayopunguza migongano na kuongeza tija katika utendaji wa halmashauri.

TISEZA YATOA VIVUTIO KWA UPANUZI WA MRADI WA HOSPITALI MWANZA

January 31, 2026 Add Comment
Mamlaka ya Uwekezaji na Maeneo Maalumu ya Kiuchumi Tanzania (TISEZA) imetembelea mradi wa Hospitali ya Kamanga Medics (Kamanga Medics Hospital) iliyopo eneo la Nyegezi jijini Mwanza, ambao kwa sasa uko katika hatua ya upanuzi.

REA YAMTAKA MKANDARASI CCC INTERNATIONAL MKOANI RUVUMA KUONGEZA KASI YA UJENZI WA MRADI

January 31, 2026 Add Comment
Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umemtaka Mkandarasi Kampuni ya CCC International Engineering Nigeria Ltd anayetekeleza Mradi wa Kusambaza umeme katika Vitongoji 135 vya Majimbo 9 ya uchaguzi Mkoani Ruvuma kuongeza kasi ya ujenzi ili kukamilisha Mradi huo kwa wakati.
WAZIRI MAVUNDE AKABIDHI MAJIKO YA GESI 1,000 KWA MAMA NA BABA LISHE DODOMA

WAZIRI MAVUNDE AKABIDHI MAJIKO YA GESI 1,000 KWA MAMA NA BABA LISHE DODOMA

January 31, 2026 Add Comment

Waziri wa Madini na Mbunge wa Jimbo la Mtumba, Antony Mavunde, amekabidhi jumla ya majiko 1,000 ya gesi kwa mama lishe na baba lishe wa Jimbo la Mtumba, ikiwa ni sehemu ya jitihada za Serikali katika kukuza matumizi ya nishati safi ya kupikia.

Akizungumza wakati wa hafla ya makabidhiano hayo, Mavunde amesema mpango huo unalenga kuboresha afya za mama na baba lishe, kuongeza ufanisi katika shughuli zao za kila siku pamoja na kulinda mazingira kwa kupunguza matumizi ya mkaa na kuni.

Amesema kuwa Serikali itaendelea kuweka mazingira rafiki kwa wajasiriamali wadogo ambapo ameahidi kuanzisha klabu za mama lishe katika kila kata za Jimbo la Mtumba zitakazosaidia kuwaunganisha mama lishe na kuwapatia elimu ya ujasiriamali, usimamizi wa fedha pamoja na kuwawezesha kupata mikopo kwa urahisi ili waondokane na mikopo kandamizi maarufu kama kausha damu.

Kwa upande wake, Mkuu wa Idara ya Mafunzo kutoka kampuni ya Oryx Gas, Peter Ndomba, amewataka mama lishe na baba lishe kuacha kabisa matumizi ya mkaa na kuni akisema nishati hizo zimekuwa zikisababisha madhara makubwa ya kiafya ikiwemo magonjwa ya mfumo wa hewa, macho na moyo kutokana na moshi unaotokana na matumizi yake.

Kwa upande wao, mama lishe na baba lishe waliopokea majiko hayo wameishukuru Mbunge wao Antony Mavunde pamoja kwa msaada huo wakisema utawapunguzia adha ya kuni na mkaa, kuboresha mazingira ya kazi na kuongeza ufanisi katika shughuli zao za kila siku.

VITONGOJI VYOTE MKOA WA KILIMANJARO SASA KUWA NA UMEME

January 31, 2026 Add Comment

 📌 Wananchi wahamasishwa kuanza kufanya wiring kupokea mradi wa vitongojini

📌 Wananchi watakiwa kulinda miundombinu ya umeme

📌 Bilioni 33.5 kupeleka umeme vitongoji 186 Kilimanjaro


Wananchi katika vitongoji 186 ambavyo vinatarajiwa kupelekewa umeme Mkoani Kilimanjaro wamehamasishwa kuanza kufanya maandalizi ya kuupokea mradi huo kwa kuanza kutandaza nyaya ndani ya nyumba zao (wiring).

Rai hiyo imetolewa leo na Mkuu wa Mkoa wa Kilimnajrao, Mhe. Nurdin Babu wakati wa kikao cha kumtambulisha mkandarasi, Derm Group (T) Limited alieshinda zabuni ya kupeleka umeme kwenye vitongoji 186 vya Mkoa huo katika kipindi cha miaka mitatu.

Mradi huo wa kupeleka umeme katika vitongoji unatekelezwa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) utagharimu zaidi ya shilingi bilioni 33.5.

Kuanza kwa mradi huo wa kupeleka umeme katika vitongoji 186, kutaufanya Mkoa wa Kilimanjaro kuwa na umeme katika vitongoji vyake vyote 2,258.

“Tunamshkuru sana Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa dhamira yake njema ya kutaka kuhakikisha kwamba wananchi wa Tanzania wote wanapata nishati ya umeme mpaka kwenye ngazi ya kitongoji.

Mkoa wa Kilimanjaro tunaenda kuandika historia kuwa miongoni mwa mikoa 3 inayokwenda kufikisha umeme katika vitongoji vyake vyote. Hii ni heshima kubwa sana. Nitumie fursa hii kuwahamasisha wananchi kuanza kufanya maandalizi ya kupokea umeme pindi mkandarasi atakapoanza kazi rasmi kwa kufanya wiring kwenye nyumba zao,” amesema Mhe. Babu.

Mkuu huyo wa Mkoa pia ametoa rai kwa wananchi kuchangamkia fursa ya uwepo wa umeme kwa kuanzisha biashara mbalimbali ili lengo la serikali la kuboresha maisha ya wananchi wa vijijini kupitia upatikanaji wa nishati ya umeme liweze kutimia.

Kwa upande wake Mwakilishi wa Mkurugenzi Mkuu wa REA ambaye pia ni Mkurugenzi wa Fedha, CPA. Daniel Mungure ametoa wito kwa wananchi kumpa ushirikiano mkandarasi pindi atakapoanza kutekeleza mradi lakini pia kulinda miundombinu ya umeme ambayo imejengwa kwa gharama kubwa.

Kwa upande wake Meneja wa kampuni ya Derm Group, Mhandisi Musa Abdallah ameahidi kukamilisha mradi huo ndani ya muda uliopangwa kimkataba na kwamba atashirikiana karibu na viongozi na wananchi wa maeneo ya mradi.



MBEYA WAPOKEA BILIONI 42.6, KUPELEKA UMEME VITONGOJI 318

January 31, 2026 Add Comment




*📌Idadi ya vitongoji vyenye umeme Mbeya ni 1,970 sawa na asilimia 67%*


*📌Mkandarasi atakiwa kutekeleza mradi huo kulingana Taratibu zilizowekwa*


📍Mbeya


Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Mhe. Beno Malisa ameishukuru Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA), kwa kupeleka kiasi cha shilingi bilioni 42.6 mkoani Mbeya ili kupeleka umeme kwenye vitongoji 316 kupitia mradi wa HEP 2B unaotekelezwa mkoani humo ili wananchi wanufaike na nishati hiyo. 


RC Malisa amesema mradi huo unakwenda kuleta tija na kuchochea maendeleo ya wananchi wa mkoa huo ambao wataunganishiwa umeme huo kuwawezesha kuendesha shughuli zao za kiuchumi. 

"Gharama ya kuunganisha umeme ni shilingi 27,000 tu. Nawaomba wananchi wa mkoa huu mtumie fursa hii ya kuunganisha umeme iliyoletwa na Serikali kupitia REA.," Amesema RC Malisa. 


Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa REA, Bw. Frank Mugogo amesema jumla ya Vitongoji mkoa wa Mbeya ni 2,951 ambapo vitongoji vyenye umeme ni 1,970 sawa na asilimia 67%. 

Ameongeza kuwa vitongoji ambavyo havina umeme ni 1,981 na vitongoji vilivyopo kwenye mradi huo wa HEP 2B uliotambulishwa mkoani Mbeya ni 316 na vitongoji vitakavyosalia ni 665.

Kwa upande wake, Meneja wa Miradi kutoka kampuni ya White City International Contractors Ltd, Mha.Baraka Mungai ambaye atatekelesa mradi huo ameishukuru Serikali kupitia REA kwa kupewa fursa ya kutekeleza mradi huo. Ameuhakikishia uongozi wa mkoa wa Mbeya kuwa mradi huo utakamilika kwa wakati ili uweze kuleta tija kwa wananchi wa mkoa huo.