HABARI MPYA
HABARI
SIASA
ELIMU
Recent Posts
WAKENYA WAASWA KUACHA KUWADHARAU WATANZANIA NA WATANZANIA KUACHA KUWAOGOPA WAKENYA
habari
Mfanyabiashara nguli na Mwenyekiti wa Taifa Group , Rostam Azizi akizungumza kwenye mkutano wa Biashara kati ya Kenya na Tanzania uliyofanyika jijini Dar es Salaam.
MABILIONI YA CSR KUTOKA BARRICK BULYANHULU KUTEKELEZA MIRADI YA KIJAMII HALMASHAURI YA MSALALA 2026
habari
HISA STAHIKI MCB ZAFUNGUA FURSA MPYA ZA UWEKEZAJI NA MIKOPO
habariRAIS DKT. WILLIAM RUTO AIPONGEZA NSSF TANZANIA KWA UWEKEZAJI WA DOLA ZAIDI YA MILIONI 51 NAIROBI
habariRais wa Kenya, Mhe. Dkt. William Ruto, ameusifu uwekezaji wa Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) wa Tanzania unaoendelea jijini Nairobi, akisema ni mfano bora wa matumizi sahihi ya akiba za wanachama katika kukuza uchumi na maendeleo ya kikanda.
Akizungumza Mei 5, 2026 wakati akihutubia Bunge jijini Dodoma, Mhe. Dkt. Ruto alimpongeza Mkurugenzi Mkuu wa NSSF Tanzania, Bw. Masha Mshomba, kwa usimamizi thabiti wa uwekezaji huo, akibainisha kuwa unaonesha namna bora ya kugeuza akiba za wanachama kuwa miradi yenye tija.
Alisema mradi huo uliopo eneo la Upper Hill, jijini Nairobi, unahusisha ujenzi wa majengo pacha yenye ghorofa 22, unaogharimu takribani dola za Marekani zaidi ya Milioni 51. Mradi huo unatekelezwa kwa kutumia akiba za wanachama wa NSSF Tanzania na unatarajiwa kukamilika ndani ya kipindi cha miaka miwili.
Mhe. Dkt. Ruto alieleza kuwa uwekezaji huo ni somo muhimu kwa Kenya na mataifa mengine ya Afrika Mashariki kuhusu umuhimu wa kukuza utamaduni wa akiba na uwekezaji kwa maendeleo ya muda mrefu.
“Uwekezaji ni zao la akiba. Huwezi kuwekeza kama huna akiba,” alisisitiza Dkt. Ruto, akihimiza wananchi na taasisi kuzingatia nidhamu ya kuchangia katika mifuko ya hifadhi ya jamii kwa mustakabali wa baadaye.
Aidha, alibainisha kuwa nchini Kenya wamefanya maboresho ya mfumo wa hifadhi ya jamii mwaka 2023 baada ya kujifunza kutoka mifumo bora ikiwemo ya Tanzania.
Alieleza kuwa mfumo huo unahitaji mwajiri na mwajiriwa kuchangia kwa pamoja hadi asilimia 20 ya mapato ili kuimarisha usalama wa kifedha kwa wafanyakazi wanapostaafu.
Mhe. Dkt. Ruto alisisitiza kuwa utamaduni wa kujiwekea akiba unapaswa kuendelezwa ndani ya jamii, akieleza kuwa hatua hiyo ni muhimu katika kujenga mifumo imara ya hifadhi ya jamii.
Rais Dkt. Ruto pia alisifu mafanikio ya Tanzania katika sekta ya hifadhi ya jamii, akieleza kuwa Kenya inaendelea kujifunza na kuchukua mifano bora kutoka kwa majirani zake.
Katika kuimarisha ushirikiano wa kikanda, alisema anajivunia uhusiano mzuri uliopo kati ya Kenya na Tanzania chini ya uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, akibainisha kuwa huu ni wakati muhimu katika historia ya mataifa hayo mawili.
Akihitimisha, Dkt. Ruto amesema kuwa kwa sasa kuna hatua kubwa ya kihistoria katika uhusiano wa Kenya na Tanzania, akieleza furaha yake kwa ushirikiano wa karibu kati yake na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan.
Amesema viongozi hao wanafanya kazi kwa pamoja kuwaleta karibu wananchi wa Afrika Mashariki na kuondoa changamoto zilizodumaza maendeleo kwa muda mrefu.
Kauli hiyo inaakisi mwelekeo wa mataifa ya Afrika Mashariki katika kutumia rasilimali zao za ndani kama kichocheo cha ukuaji wa uchumi na ustawi wa wananchi.
Rais Dkt. William Ruto anahitimisha ziara rasmi ya siku mbili nchini Tanzania, iliyoanza Mei 4 hadi 5, 2026.
CRDB BENKI YATOA BILIONI 2.7 KUWASAIDIA ELIMU NA UWEZESHWAJI WANANCHI KIUCHUMI
habariNa Oscar Assenga,LUSHOTO
Benki ya CRDB imeendelea kudhihirisha dhamira yake ya kuchangia maendeleo ya jamii kwa kutoa zaidi ya shilingi bilioni 2.7 katika mwaka uliopita, fedha ambazo zimeelekezwa kwa kiasi kikubwa katika sekta ya elimu na uwezeshaji wa wananchi kiuchumi.
Akizungumza katika hafla ya kukabidhi vyumba viwili vya madarasa pamoja na ofisi ya walimu katika Shule ya Msingi Kwendoghohi, iliyopo Kata ya Usambara wilayani Lushoto, Mjumbe wa Bodi ya Wakurugenzi Taasisi ya CRDB Bank Foundation, Marian Balampama, alisema kati ya fedha hizo, shilingi bilioni 1 zimetumika kuboresha elimu.
Alieleza kuwa uwekezaji huo umejumuisha ujenzi wa madarasa, ununuzi wa madawati, pamoja na upatikanaji wa vifaa vya kufundishia na kujifunzia, ikiwemo maabara. Alisisitiza kuwa benki hiyo haijikita tu katika miundombinu, bali pia inahakikisha mwanafunzi anapata mazingira salama na bora ya kujifunzia.
Mbali na elimu, CRDB pia imewekeza katika kuwawezesha wananchi kiuchumi kupitia programu mbalimbali. Balampana alisema benki hiyo inaamini kuwa kumwezesha mtu mmoja ni sawa na kuinua familia na jamii kwa ujumla.
Kupitia kampuni tanzu ya CRDB Bank Foundation na programu ya Embeju, zaidi ya wanufaika 500,000 pamoja na vikundi mbalimbali wamenufaika. Alifafanua kuwa uwezeshaji huo hauishii kwenye utoaji wa fedha pekee, bali pia unahusisha mafunzo ya ujuzi na mbinu za kutambua masoko ili kuongeza tija na faida.
Aidha, alibainisha kuwa benki hiyo imekuwa ikiangalia pia changamoto nyingine za kijamii, ikiwemo upatikanaji wa huduma za afya, kwa lengo la kuboresha ustawi wa wananchi kwa ujumla.
“Sisi tunajisikia fahari kushirikiana na Serikali, hususan katika kusimamia mikopo ya asilimia 10 katika baadhi ya mikoa, ili kuhakikisha fedha zinawafikia walengwa na kuleta matokeo chanya,” alisema Balampana.
Aliongeza kuwa CRDB inaendelea kushirikiana kwa karibu na viongozi wa Wilaya ya Lushoto pamoja na Mkoa wa Tanga katika kutekeleza miradi ya maendeleo.
Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Lushoto, Zephania Sumaye, aliishukuru benki hiyo kwa mchango huo, akisema ujenzi wa madarasa hayo utasaidia kupunguza msongamano wa wanafunzi na kuboresha mazingira ya kujifunzia.
Alieleza kuwa shule hiyo, iliyoanzishwa mwaka 1965, ilikuwa na miundombinu iliyochakaa, hivyo msaada huo unaleta matumaini mapya katika kuinua ubora wa elimu katika eneo hilo.
Kwa ujumla, hatua ya CRDB inaonesha namna taasisi za kifedha zinavyoweza kuwa chachu ya maendeleo kwa kurejesha kwa jamii sehemu ya mapato yao, sambamba na kuunga mkono juhudi za Serikali kufikia dira ya maendeleo ya Taifa ya mwaka 2050.
STARTUPS ZAASWA KUONGEZA UBORA WA BIDHAA ILI KUCHOCHEA UCHUMI WA TAIFA
habariMzumbe yaandaa Siku ya Mzumbe na Kambi ya Wajasiriamali kwa mara ya kumi
habariUNESCO NA NACTVET WAZINDUA KOZI MTANDAO YA ELIMU YA STADI ZA MAISHA NA AFYA YA UZAZI KWA WANAFUNZI TVET
habariSANLAM ALLIANZ YAFADHILI MRADI WA PAZA SAUTI+ KUIMARISHA MAPAMBANO DHIDI YA UKATILI WA KIJINSIA NA WATOTO
habari
ROSTAM AZIZI : TANZANIA NA KENYA ZIWE NA MFUMO MMOJA WA KIBIASHARA KUPATA MAFANIKIO ZAIDI YA BIASHARA
habari

TANZANIA NA KENYA ZASANII MKATABA WA VYETI VYA MABAHARIA NA NA USHIRIKIANO WA USAFIRI WA MAJINI
habari .jpeg)
SHIRIKA la Uwakala wa Meli Tanzania na Mamlaka ya Udhibiti wa usafiri wa Majini nchini Kenya wamesaini mkataba wa utambuzi wa vyeti vya mabaharia na hati ya makubaliano kuhusu ushirikiano na usimamizi wa sekta ya usafiri wa njia ya maji baina ya nchi hizo mbili.
DAS KIGAMBONI AZINDUA OFISI YA WILAYA YA KITANESCO YA KIMBIJI
Nishati
Asema itapunguza adha wananchi kutembea umbali mrefu kufuata huduma
Aipongeza TANESCO kwa maboresho yanayoendelea kufanyika kwa wateja wake







.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)






.jpeg)






.jpg)



