HABARI

SIASA

ELIMU

Recent Posts

UBORESHAJI WA HUDUMA ZA WAZEJA MBUNGE BAGAMOYO AKABIDHI MAGARI TANESCO

March 03, 2026 Add Comment




*📌Lengo ni kupunguza muda wa kushughulikia hitilafu na kuongeza ufanisi katika kuwahudumia wateja*


*📌Asema TANESCO imeimarika, imetoka katika kutengeneza hasara*


📍Bagamoyo, Pwani


Mbunge wa Jimbo la Bagamoyo, Mhe. Subira Mgalu leo Machi 03, 2026 amekabidhi magari mapya kwa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) Wilaya ya Bagamoyo mkoani Pwani kwa lengo la kuimarisha huduma kwa wateja na kuongeza ufanisi wa utendaji kazi katika kuwahudumia Wateja wilayani Bagamoyo.

Akizungumza katika hafla ya makabidhiano iliyofanyika Ofisi ya TANESCO Bagamoyo, Mhe. Mgalu amesema kuwa hatua hiyo ni sehemu ya jitihada za Serikali kuhakikisha wananchi wanapata huduma ya umeme kwa wakati, kwa ubora na kwa uhakika zaidi.

“Magari haya yatawezesha mafundi na wahandisi wa TANESCO kuwafikia wananchi kwa haraka pale panapotokea hitilafu au changamoto za umeme. Tunataka kuona muda wa kushughulikia matatizo unapungua na huduma inaboreshwa,” amesema Mhe. Mgalu.



Amesisitiza kuwa, hivi sasa TANESCO imeimarika katika utoaji wa huduma ikiwa ni pamoja na kutoka katika kutengeneza hasara na linajiendesha bila kupata ruzuku kutoka Serikalini.


Aidha, amesema baada ya kukamilika bwawa la Julius Nyerere linalozalisha megawati 2115 na kupelekea Nchi kuwa na uwezo wa takribani wa megawati 4,000 huku mahitaji yakiwa takribani megawati 2,000 hivyo kuitaka TANESCO kuongeza kasi ya kuwaunganishia wateja.


Mkurugenzi wa TANESCO Kanda ya Mashariki,Mha. Kenneth Boymanda amesema  TANESCO inatekeleza miradi mingi ya maendeleo Wilaya ya Bagamoyo ikiwemo ya umeme Vijijini hivyo upatikanaji wa magari hayo kutarahisisha utekelezaji wa miradi hiyo.


“Bagamoyo tunao mpango mkubwa wa kuhakikisha kila nyumba inafikishiwa nishati ya  umeme nak ama Nchi mpaka mwaka 2030 kuunganisha nyumba milioni nane na laki tatu na nyumba Milioni Moja na Laki Saba kwa mwaka”, amesema Mha. Boymanda



Ameongeza kuwa, majukumu hayo yanahitaji uwepo wa vitendea kazi na kusisitiza kuwa TANESCO itafanya kazi usiku na mchana ili kuhakikisha malengo yaliyowekwa na Serikali kupitia mpango wa mission 300.


Serikali imeendelea kuweka mkazo katika kuboresha miundombinu ya umemme kama msingi wa maendeleo ya viwanda, biashara na ustawi wa jamii.


 Hatua ya TANESCO kununua magari hayo ni sehemu ya juhudi za kuimarisha huduma kwa wateja  na kuongeza ubora wa huduma kwa wananchi.

WAZIRI NDEJEMBI AKUTANA NA TAASISI ZA MAFUTA NA GESI KUIMARISHA USHIRIKIANO KISEKTA

March 03, 2026 Add Comment

Waziri wa Nishati Mhe. Deogratius Ndejembi leo Machi 03, 2026 amekutana na kufanya mazungumzo na taasisi zilizo chini ya Wizara ya Nishati zinazoshughulikia sekta ya mafuta na gesi katika Ofisi Ndogo za Wizara jijini Dar es salaam.


Kikao hicho kimehudhuriwa na Katibu Mkuu Wizara ya Nishati anayeshughulikia Mafuta na Gesi Dkt. James Mataragio, Kamishna wa Mafuta kutoka Wizara ya Nishati Goodluck Shirima, Mkurugenzi Mtendaji wa EWURA James Mwainyekule, Mtendaji Mkuu wa TPDC Mussa Makame  Kaimu Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Uagizaji wa Mafuta kwa Pamoja (PBPA) Bruno Tarimo pamoja na wataalamu wengine kutoka wizarani na Taasisi hizo.

Kikao hicho kinalenga kuimarisha usimamizi, uwazi na ufanisi katika utekelezaji wa majukumu ya Taasisi hizo ili kuimarisha sekta ya mafuta na gesi nchini.





NAIBU WAZIRI SALOME AKUTANA NA MKURUGENZI WA Go PLANT TANZANIA

March 03, 2026 Add Comment

 


Dodoma


Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba amekutana na Mkurugenzi wa Go Plant Tanzania Bw. Emmanuel Likida kwa lengo la kujadili namna ya kushirikiana katika maandalizi ya Mjadala (Debate) wa Clean Cooking Solutions utakaowahusisha wanafunzi wa shule za Sekondari katika Halmashauri za Mkoa wa Dodoma. 


Katika kikao hicho, pande zote mbili zimejadili umuhimu wa kuwajengea vijana uelewa wa mapema kuhusu matumizi ya nishati safi ya kupikia, athari za matumizi ya nishati zisizo safi kwa afya na mazingira, pamoja na fursa zilizopo katika ubunifu na ujasiriamali wa suluhisho za upishi safi.

Mjadala huo unatarajiwa kuwa jukwaa la kielimu na kimkakati la kukuza uelewa, kuchochea fikra bunifu, na kuibua mabalozi vijana wa Nishati Safi katika jamii.

Kikao hicho kimefanyika leo Machi 03,2026 katika Ofisi za Wizara ya Nishati zilizopo Mtumba, jijini Dodoma.



EXPERIENCE THE WONDERS INAANZIA GETI LA NGORONGORO KUELEKEA BUSTANI YA EDEN

March 03, 2026 Add Comment


Wadigo wana msemo usemao " baraka hubarikiwa waliobarikiwa hata kama si majaaliwa" Naam, ukisikia Ngorongoro ni eneo pekee unaloweza kuona Wanyama wakubwa watano (The Big 5) si hadithi za kusadikika wala Ndoto za alinacha, ni dhahiri inayothibitishwa na nuru ya upeo wa macho yako

Fikiria unaingia tu getini, umbali wa nusu kilomita upande wako wa kushoto unashuhudia mti mkubwa umepambwa na mnyama adimu sana kuonekana nyakati za mchana, huyu si mwingine ni Anko Chui.

Sasa wakati Unamshangaa Chui inakulazimu ukimbizane na muda maana Big Five wengine kama Simba, Tembo, Faru na Nyati wanakusubiri Kasoko ya Ngorongoro wakiwa wamezungungukwa na makundi ya Pundamilia, swala, Pofu, viboko, Kasongo ndege aina Falamingo, Yangeyange, ndege karani na wengine wengi.

Ngorongoro ni hifadhi ya maajabu yenye Hadhi ya kimataifa, Destination ya maajabu, Bustani ya Eden, Nyayo za Laetoli, Tamaduni hai, Bonde la Olduvai na Mazalia ya Nyumbu.


RAIS SAMIA AWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI WA MATANKI YA KUPOKELEA MAFUTA KIGAMBONI

RAIS SAMIA AWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI WA MATANKI YA KUPOKELEA MAFUTA KIGAMBONI

March 03, 2026 Add Comment

 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akivuta kitambaa kuashiria uwekaji wa jiwe la msingi Mradi wa ujenzi wa Matanki ya kupokea mafuta katika Bandari ya Dar es Salaam katika eneo la Kigamboni Jijini Dar es Salaam, tarehe 03 Machi, 2026.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akisikiliza maelezo ya Mradi wa ujenzi wa Matanki ya kupokea Mafuta katika Bandari ya Dar es Salaam, Kigamboni Jijini Dar es Salaam, tarehe 03 Machi, 2026. Ujenzi wa Matanki hayo utasaidia kupunguza uhaba wa mafuta nchini, kupunguza muda wa meli kusubiri nangani kutoka wastani wa siku 22 hadi siku 7, kupunguza muda wa kushusha shehena ya mafuta kutoka siku 7 hadi siku 1, kuongeza mapato ya Taifa pamoja na kutoa ajira kwa Watanzania.

 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan mara baada ya kuweka jiwe la msingi Mradi wa Ujenzi wa Matanki ya kupokea Mafuta katika Bandari ya Dar es Salaam, Kigamboni, Jijini Dar es Salaam, tarehe 03 Machi, 2026.

Muonekano wa eneo la Mradi wa ujenzi wa Matanki ya kupokea mafuta katika Bandari ya Dar es Salaam, Kigamboni Jijini Dar es Salaam. Ujenzi wa Matanki hayo utasaidia kupunguza au kuondoa kabisa uhaba wa mafuta Nchini, kuimarisha usalama wa nishati hiyo, kupunguza muda wa meli kusubiri nangani kutoka wastani wa siku 22 hadi siku 7, kupunguza muda wa kushusha shehena ya mafuta kutoka siku 7 hadi siku 1, kuongeza mapato ya Taifa kupitia makusanyo ya kodi na tozo mbalimbali zitakazo kusanywa na Mamlaka husika pamoja na kutoa ajira kwa Watanzania.

FCC KUADHIMISHA SIKU YA HAKI YA MLAJI KWA KUTOA ELIMU KWA UMMA

March 03, 2026 Add Comment
Na Emmanuel Mbatilo, Dar es Salaam

Tume ya Ushindani (FCC) imetangaza kuadhimisha Siku ya Kimataifa ya Haki ya Mlaji Duniani kwa kuendesha kampeni maalum ya utoaji elimu kwa walaji na wafanyabiashara ili kuongeza uelewa wa haki na wajibu wao katika soko.

SERIKALI YAWEKA UWAJIBAKAJI SEKTA YA ARDHI

March 02, 2026 Add Comment
 

 Na Munir Shemweta, WANMM

 Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. Dkt. Leonard Akwilapo, ameutumia uzinduzi wa “Samia Ardhi Kliniki” jijini Dar es Salaam kutangaza msimamo mkali wa Wizara dhidi ya vitendo vya uzembe na ucheleweshaji wa huduma kwa wananchi.

 

Katika hafla hiyo, Waziri Akwilapo amesema Wizara imeamua “kujivua gamba” na kuanza ukurasa mpya wa uwajibikaji, akisisitiza kuwa kauli za watumishi kudai mafaili kupotea au kutoonekana hazitavumiliwa tena.

 

“Hakuna kitu kama faili kupotea. Ofisi zetu zina mifumo thabiti, na mafaili hayana miguu ya kutoroka. Kauli hizi nimezipiga marufuku rasmi,” alisisitiza.

 

Waziri huyo alieleza kuwa hatua hiyo ni sehemu ya mageuzi yanayolenga kurejesha imani ya wananchi kwa sekta ya ardhi, ambayo imekuwa ikikabiliwa na malalamiko ya muda mrefu kuhusu urasimu na usumbufu usio wa lazima.

 

Alisema Wizara haitasita kuchukua hatua kali za kinidhamu kwa watumishi watakaobainika kukwamisha huduma kwa maslahi binafsi, akisisitiza kuwa ardhi ni rasilimali ya Taifa na watumishi ni wasimamizi tu, si wamiliki.

 

Uzinduzi wa “Samia Ardhi Kliniki” umefanyika ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani, chini ya uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan. Kliniki hiyo itafanyika nchi nzima kuanzia Machi 2 hadi 7, 2026, ikitoa huduma za msaada wa kisheria, utoaji wa hatimiliki na elimu ya taratibu za umilikishwaji wa ardhi.

 

Mbali na kuhimiza wanawake kujitokeza kunufaika na huduma hizo, Waziri Akwilapo aliwataka wanaume na viongozi wa kaya kuachana na mila potofu zinazowanyima wanawake haki ya kumiliki ardhi.

 

Kwa mujibu wa Waziri, idadi ya wanawake wenye hatimiliki imeongezeka hadi wastani wa asilimia 28 kutoka chini ya asilimia 10 miaka ya nyuma, hatua aliyoitaja kuwa ni mafanikio makubwa ya Serikali ya Awamu ya Sita.

 

Kauli mbiu ya zoezi hilo ni: “Mwanamke; Haki Yako, Miliki Ardhi Sasa,” ikiwa ni sehemu ya mkakati mpana wa kuhakikisha usawa wa kijinsia na kuimarisha uchumi wa familia na Taifa kwa ujumla.

Awali Mkuu wa Wilaya ya Ilala Bw Edward Mpogolo akimuwakilisha Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Bw. Albert Chalamila mbali na kuipongeza Wizara ya Ardhi kwa kuanzisha Samia Ardhi Kliniki amesema, kuna baadhi ya changamoto zilizoanza kujitokeza kwa wale wanaopata hati miliki za ardhi kufunga barabara zinazotumika kwa jamii.

 

Ameomba utaratibu wa fomu za kuthibitishwa na majirani katika maeneo yaliyorasimishwa kuzingaitiwa kwa kupitishwa katika ngazi husika na kusimamiwa ili kuepuka changamoto kama hizo.

 

Kwa upande wake Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Bi. Lucy Kabyemnera amesema huduma kubwa zinazotolewa kupitia Samia Ardhi Kliniki ni elimu hususan ya haki za umiliki kwa wanawake, ushauri wa mambo mbalimbali ya sekta ya ardhi, utoaji hati kwa waliokamilisha taratibu pamoja na huduma nyingine. 

 Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Dkt Leonard Akwilapo akizungumza wakati wa Kuzindua Samia Ardhi Kliniki jijini Dar es Salaam tarehe 2 Machi 2026
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Dkt Leonard Akwilapo akimkabidhi hati milki ya ardhi mmoja wa wakazi wa jiji la Dar es Salaam wakati wa Samia Ardhi Kliniki tarehe 2 Machi 2026.
Naibu Katibu Mkuu Bi. Lucy Kabyemera akimkabidhi hati Miliki ya Ardhi Mkuu wa Wilaya ya Ilala Bw. Edrward Mpogolo katika tukio la uzinduzi wa Samia Ardhi Kliniki jijini Dar es Salaam tarehe 2 Machi 2026. Kushoto ni Mkurugenzi wa Kitengo cha Milki Wizara ya Ardhi Dkt Upendo Matotola.
Sehemu ya wakazi wa jiji la Dar es Salaam wakipata huduma kupitia Samia Ardhi Kliniki inayoendelea jijini Dar es Salaam
Sehemu ya watumishi wa sekta ya ardhi wanawake wakitoa huduma katika Samia Ardhi Kliniki inayofanyika jijini Dar es Salaam
 
Mkurugenzi wa Kitengo cha Milki Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt. Upendo Matotola akimkabidhi mwanamama mkazi wa jiji la Dar es Salaam  Hati Milki ya ardhi katika Samia Ardhi Kliniki inayoendelea jijini Dar es Salaam.Katikati ni Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi Bi. Lucy Kabyemera (PICHA ZOTE NA EMMANUEL MASSAKA, MICHUZI TV)
 
 
 
 
 
SERIKALI YASISITIZA ULINZI WA AJIRA NA UKUAJI WA UCHUMI KUPITIA VIWANDA

SERIKALI YASISITIZA ULINZI WA AJIRA NA UKUAJI WA UCHUMI KUPITIA VIWANDA

March 02, 2026 Add Comment

Serikali kuendelea kuweka mazingira salama kwa wenye Viwanda vinavyofanya kazi na kutatua changamoto kwa wakati ili kuendelea kulinda ajira za Watanzania na kuongeza mzunguko wa fedha kwa jamii na wananchi kwa ujumla.

Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Denis Londo (Mb) wakati wa ziara ya kikazi Machi 2, 2026 mkoani Morogoro.

Londo amemshauri Katibu Tawala mkoani Morogoro kuweka utaratibu kwa mikopo ya asilimia 10 kuwafikia walengwa kupitia Shirika la Maendeleo ya Viwanda vidogo (SIDO) ili kuleta maana ya utoaji wa mikopo kwa jamii nchini.

Londo ametembelea viwanda vinne katika Manispaa ya Morogoro ikiwemo SIDO, Mkwawa, Cotex na Mazava katika ziara yake ya siku moja mkoani hapa.

Pia amesema ikiwa wajasiliamali hao watapata mikopo wakiwa hapo ambako wamezungukwa na aina mbalimbali za ujasiriamali itawasaidia kupata namna ya kujengwa na kuwa wajasiriamali wazuri na hivyo kuwa na uhakika wa kurejesha mikopo hiyo.

Uwepo wa gundi inayozalishwa kwenye viwanda hivyo vidogo vilivyopo kwenye eneo la viwanda SIDO Morogoro ambapo ameiomba serikali ya mkoa kusimamia uzalishaji huo na kufanya masoko makubwa ya gundi kuanzia ndani ya mkoa na kisha nje ya mkoa Taifa hadi nje ya nchi.

Naye Mkurugenzi Mkuu wa SIDO, Mhandisi Profesa Sylvester Mpanduji anasema wanajipanga kuhakikisha wanaboresha eneo la viwanda la SIDO Morogoro ili kufanya wajasiriamali kulitumia kama kongani la viwanda na kuleta maana

Hata hivyo, Meneja wa SIDO Morogoro, Bi.Joan Nangawe anasema wametengeneza ajira zaidi ya 115 baada ya kutoa elimu, kuwakusanya wajasiriamali kwenye eneo la viwanda na kutoa mikopo ya shilingi Milioni 62.5.

Anasema katika siku 100 za Rais Samia Suluhu Hassan jumla ya wajasiriamali ambao ni vijana wanatarajia kupata mikopo ya shilingi Milioni 250 kupitia mikopo ya asilimia 10 inayotolewa na Halmashauri.

Mmoja wa wajasiriamali anayetengeneza Gundi kwenye eneo la viwanda SIDO Marry Hassan anasema licha ya kuwa na uhakika wa soko la ndani kwa mikoa ya Morogoro na Dar es salaam lakini bado wanakabiliwa na changamoto ya ukosefu wa masoko ya nje ambayo yanaweza kuwapa nafasi kubwa katika kuongeza uzalishaji na kukua kiuchumi.