HABARI

SIASA

ELIMU

Recent Posts

RAIS SAMIA APONGEZWA KWA KUPUNGUZA UHABA WA WATUMISHI HANDENI MJI

RAIS SAMIA APONGEZWA KWA KUPUNGUZA UHABA WA WATUMISHI HANDENI MJI

February 07, 2026 Add Comment

Mwenyekiti wa halmashauri ya Mji Handeni, Amiri Mwaliko,akizungumza katika mkutano wa kupokea na kujadili taarifa za kata za Halmashauri ya Mji Handeni uliofanyika leo Februari 7, 2026.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Handeni, Maryam Ukwaju,akizungumza katika mkutano wa kupokea na kujadili taarifa za kata za Halmashauri ya Mji Handeni uliofanyika leo Februari 7, 2026.

Naibu Waziri wa Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Mhe. Reuben Kwagilwa,akiteta jambo na Mkuu wa Wilaya ya Handeni, Mhe. Salum Nyamwese,wakati wa  mkutano wa kupokea na kujadili taarifa za kata za Halmashauri ya Mji Handeni uliofanyika leo Februari 7, 2026.

Sehemu ya Madiwani wakifuatilia mkutano wa kupokea na kujadili taarifa za kata za Halmashauri ya Mji Handeni uliofanyika leo Februari 7, 2026.

Na Augusta Njoji

MWENYEKITI wa Halmashauri ya Mji Handeni, Mhe. Amiri Mwaliko, amempongeza Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan, kwa kutoa kibali cha ajira kilichowezesha kupatikana kwa watumishi 82 wa kada mbalimbali na hivyo kupunguza uhaba wa watumishi katika halmashauri hiyo.

Akifungua mkutano wa kupokea na kujadili taarifa za kata wa Halmashauri hiyo uliofanyika Februari 7, 2026 mjini hapa, Mhe. Mwaliko amesema serikali imeendelea kuchukua hatua za kutatua changamoto ya upungufu wa watumishi.

“Tunaishukuru serikali kwa kuendelea kutatua changamoto ya watumishi. Tunafurahia hatua hii kwa kuwa lengo la serikali ni kuondoa uhaba wa watumishi na kuboresha utoaji wa huduma kwa wananchi,” amesema.

Aidha, amempongeza Mkuu wa Wilaya ya Handeni, Mhe. Salum Nyamwese, kwa kuhakikisha wilaya hiyo inaendelea kudumisha amani na utulivu.

Mhe. Mwaliko amewataka viongozi na watumishi kushirikiana katika kujenga halmashauri yenye mshikamano na kutatua changamoto zinazojitokeza.

Ameongeza kuwa ni muhimu kusimama pamoja na watumishi na kushughulikia changamoto kwa njia ya mazungumzo ili kujenga timu imara ya utendaji kwa maendeleo ya halmashauri.

Kadhalika, amesisitiza kuendelea kuchukuliwa hatua za kudhibiti utoro wa wanafunzi kwa kushirikiana na madiwani wa maeneo husika.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Handeni, Maryam Ukwaju, amesema katika mwaka wa fedha 2025/26 serikali imeajiri watumishi 82 wakiwemo walimu wa shule za msingi na sekondari pamoja na wauguzi.

Amesema changamoto ya upungufu wa watumishi inaendelea kupatiwa ufumbuzi kadri serikali inavyoendelea kutoa ajira, huku halmashauri ikiendelea kutenga bajeti kupitia mapato ya ndani kwa ajili ya kuchangia maendeleo ya kata, ikiwemo ununuzi wa madawati.

KWAGILWA ABANA UWAJIBIKAJI WA TAASISI ZA UMMA HANDENI MJI

KWAGILWA ABANA UWAJIBIKAJI WA TAASISI ZA UMMA HANDENI MJI

February 07, 2026 Add Comment

Naibu Waziri wa Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Mhe. Reuben Kwagilwa,akizungumza katika mkutano wa kupokea na kujadili taarifa za kata za Halmashauri ya Mji Handeni uliofanyika leo Februari 7, 2026.

Mkuu wa Wilaya ya Handeni, Mhe. Salum Nyamwese,akizungumza katika mkutano wa kupokea na kujadili taarifa za kata za Halmashauri ya Mji Handeni uliofanyika leo Februari 7, 2026.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Handeni, Maryam Ukwaju,akizungumza katika mkutano wa kupokea na kujadili taarifa za kata za Halmashauri ya Mji Handeni uliofanyika leo Februari 7, 2026.

Mwenyekiti wa halmashauri ya Mji Handeni, Amiri Mwaliko,akizungumza katika mkutano wa kupokea na kujadili taarifa za kata za Halmashauri ya Mji Handeni uliofanyika leo Februari 7, 2026.

Naibu Waziri wa Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Mhe. Reuben Kwagilwa,akiteta jambo na Mkuu wa Wilaya ya Handeni, Mhe. Salum Nyamwese,wakati wa  mkutano wa kupokea na kujadili taarifa za kata za Halmashauri ya Mji Handeni uliofanyika leo Februari 7, 2026.

Sehemu ya washiriki wakifatilia hotuba ya Naibu Waziri wa Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Mhe. Reuben Kwagilwa (hayupo pichani) wakati wa mkutano wa kupokea na kujadili taarifa za kata za Halmashauri ya Mji Handeni uliofanyika leo Februari 7, 2026.

Na Augusta Njoji

Naibu Waziri wa Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Mhe. Reuben Kwagilwa, ameelekeza taasisi za serikali zinazohudumia wananchi wilayani Handeni kuwasilisha taarifa za utekelezaji wa majukumu yao katika Baraza la Madiwani ili kuongeza uwazi na kuwafanya wananchi kufahamu kazi zinazofanywa na serikali.

Akizungumza katika mkutano wa kupokea na kujadili taarifa za kata za Halmashauri ya Mji Handeni uliofanyika Februari 7, 2026, Mhe. Kwagilwa amesema ni muhimu kwa wakuu wa taasisi za serikali kuhudhuria vikao vya Baraza la Madiwani na kuwasilisha taarifa zao.

Amezitaja baadhi ya taasisi hizo kuwa ni pamoja na Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS), Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA), Mamlaka ya Maji pamoja na Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), akisisitiza kuwa taasisi hizo zinawajibika moja kwa moja kwa wananchi.

Pamoja na hayo, amempongeza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Handeni, Maryam Ukwaju, pamoja na wataalamu wa halmashauri hiyo kwa mafanikio yaliyopatikana katika utekelezaji wa ilani ya uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) iliyopita na kuendelea kutekeleza ilani ya sasa.

Naye Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo, Mhe. Amiri Mwaliko, amempongeza Naibu Waziri Kwagilwa kwa kuaminiwa na Rais Samia Suluhu Hassan kushika nafasi hiyo, akisema anaamini atatekeleza vyema majukumu yake katika kuisaidia TAMISEMI.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Handeni, Mhe.Salum Nyamwese ameahidi kuwapa ushirikiano Madiwani katika utekelezaji wa majukumu yao.

\
BILIONI 91 KUSAMBAZA UMEME KWENYE VITONGOJI 570 VYA MKOA WA MOROGORO

BILIONI 91 KUSAMBAZA UMEME KWENYE VITONGOJI 570 VYA MKOA WA MOROGORO

February 07, 2026 Add Comment
 

Na.Mwandishi Wetu-Morogoro📍

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Mhe. Adam Malima, tarehe 6 Februari, 2026 amewapokea wakandarasi wawili kutoka Wakala wa Nishati Vijijini (REA); watakaotekeleza Mradi mkubwa wa kusambaza umeme katika vitongoji 570 vya mkoa huo; ikielezwa kuwa Mradi huo una thamani ya shilingi bilioni 91.

Wakandarasi hao ni kampuni ya Sagemcom Energy & Telecom SAS (Italia) na China Railway No. 4 Engineering Group Co. Ltd (China) ambao watasambaza umeme katika vitongoji 570 katika Mradi huo mkubwa kwa gharama ya shilingi bilioni 91.

Akizungumza wakati wa hafla ya kuwatambulisha wakandarasi hao, Mhe. Malima alisema Mradi huo ni utekelezaji wa dhamira ya Serikali ya Awamu ya Sita ya kuhakikisha Watanzania wote wanapata huduma ya umeme wa uhakika hususan maeneo ya vijijini.

Mhe. Malima alisema kuwa Serikali kupitia REA imeleta maendeleo makubwa kwenye Sekta ya Nishati hususan kwenye usambazaji wa umeme vijijini katika kipindi cha miaka 15; akitolea mfano wakati alipokuwa Naibu Waziri wa Nishati mwaka 2008 ambapo bajeti ya REA ilikuwa shilingi bilioni tano pekee.

“Leo hii baada ya miaka 15 mkoa wa Morogoro pekee yake, unatekeleza Miradi ya umeme yenye thamani ya shilingi bilioni 91. Hii inaonesha dhamira ya dhati ya Serikali katika kuhakikisha Wananchi wa vijijini wanapata umeme kwa maendeleo yao ya kiuchumi na kijamii.” alisema Mhe. Malima.

Kwa upande wake, Kaimu Mkurugenzi wa Umeme Vijijini, Mhandisi, Thomas Mmbaga kutoka REA alisema wamewatambulisha rasmi wakandarasi wawili watakaofanya kazi ya kusambaza umeme kwenye vitongoji 570 kwa mgawo wa kampuni ya Sagemcom Energy ambayo itasambaza umeme katika vitongoji 325 na kuunganisha wateja wa awali 11,399 katika wilaya ya Mvomero; Morogoro Vijijini na Gairo kwa gharama ya shilingi bilioni 48.4.

Mkandarasi wa pili ni kampuni ya China Railway No. 4 ambayo itasambaza umeme kwenye vitongoji 245 na kuunganisha wateja wa awali 8,649 katika wilaya ya Kilosa; Malinyi; Kilombero na Ulanga kwa gharama ya shilingi bilioni 42.5 ambapo kipindi cha utekelezaji kwa Mradi huo katika mkoa wa Morogoro ni miaka mitatu.

Naye Meneja wa TANESCO mkoa wa Morogoro, Mhandisi, Zawadi Macha alisema Shirika hilo limejipanga kikamilifu kusimamia utekelezaji wa Mradi huo kwa karibu ili kuhakikisha unatekelezwa kwa ubora unaotakiwa na kwa kuzingatia viwango vilivyowekwa.

Kwa upande wake, Meneja wa Mradi wa Kampuni ya Sagemcom Energy, Bwana Calvin Manase alisema kampuni hiyo ina uzoefu mkubwa katika utekelezaji wa miradi ya umeme na imejipanga kuhakikisha mradi unakamilika ndani ya miezi 34 licha mkataba kuwa miezi 36.

Manase aliongeza kuwa kampuni hiyo itatoa ajira kwa Wananchi (Wazawa) wa maeneo husika ili wanufaike moja kwa moja wakati wa utekelezaji wa Mradi huo. Aidha, ameipongeza REA kwa mpango wake wa kulipa malipo ya awali kwa wakandarasi akisema hatua hiyo itasaidia kupunguza changamoto ya upatikanaji wa vifaa vya ujenzi wa Mradi huo.

         
UMEME VITONGOJINI KUINUA UCHUMI WA WANANCHI – RC  SENDIGA

UMEME VITONGOJINI KUINUA UCHUMI WA WANANCHI – RC SENDIGA

February 07, 2026 Add Comment

Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Mhe. Queen Sendiga amesema kuwa utekelezaji wa mradi wa umeme kwenye vitongoji ni chachu ya kuinua uchumi wa wananchi vijijini.

Mhe. Sendiga ameyabainisha hayo leo Mkoani Manyara wakati wa kikao na Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kilicholenga kumtambulisha Mkandarasi Mzawa aliyeshinda zabuni ya kutekeleza mradi wa kupeleka umeme katika vitongoji 267 kwa mkoa huo, Kampuni ya SAGEM COM ENERGY.

Mradi huo unaogharimu zaidi ya shilingi bilioni 45.8 unatarajiwa kutekelezwa katika kipindi cha miaka mitatu ambapo Vitongoji katika Wilaya za Babati, Hanang, Mbulu, Kiteto, na Simanjiro vitanufaika na mradi huo.

“Tunamshkuru sana Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha hizo zinazowezesha kutekelezwa kwa mradi huu muhimu unaokwenda kuendelea kuinua uchumi wa maisha wa wananchi wetu hasa wa vijijini,” amesema Mhe. Sendiga.

Mkuu huyo wa Mkoa pia amewataka wakandarasi kufanya kazia kwa bidii na weledi na kuhakikisha mradi huo unakamilika ndani ya muda uliopangwa huku akitoa rai kwa viongozi wa serikali pamoja na wananchi kutoka ushirikiano kwa mkandarasi wakati wa utekelezaji wa mradi huo.

“Nikiwa kama Mkuu wa Mkoa natoa maelekezo kwa Waheshimiwa Wakuu wa Wilaya kuhakikisha kuwa wanashirikiana na wanaenda kumtambulisha mkandarasi kwa wananchi. Lakini pia nitoe rai kwa wananchi, miradi hii ya kijamii ambayo inakwenda kutupatia faida kubwa tuipokee, tupunguze vikwazo,” amesisitiza Mhe. Sendiga.

Awali akizungumza kuhusu utekelezwaji wa mradi huo, Mwakilishi wa Mkurugenzi Mkuu wa REA, Mhandisi Herini Mhina amesema kuwa Mkoa wa Manyara unajumla ya Vitongoji 1946 na vitongoji 1113 tayari vimefikishiwa umeme.

Mhandisi Mhina ameongeza kuwa dhamira ya Serikali ni kuhakikisha ifikapo mwaka 2030 vitongoji vyote nchini viwe vimefikishiwa nishati ya umeme na kwamba REA ikiwa na dhamana hiyo imejipanga kikamilifu kupitia miradi mbalimbali ya kimkakati kufikia dhamira hiyo.

RAIS SAMIA AFANYA MABADILIKO OFISI YA RAIS – MIPANGO, DKT. TAUSI KIDA ATEULIWA KATIBU MKUU

February 07, 2026 Add Comment

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, amefanya mabadiliko ya muundo wa Ofisi ya Rais - Mipango na Uwekezaji ambapo amemteua Dkt. Tausi Mbaga Kida kuwa Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais - Mipango na Katibu Mtendaji wa Tume ya Taifa ya Mipango.

WiLDAF HONORS 16 CHAMPIONS IN THE FIGHT AGAINST GENDER-BASED VIOLENCE, CALLS FOR STRENGTHENED COLLECTIVE ACTION

February 06, 2026 Add Comment

        

The Women in Law and Development in Africa (WiLDAF Tanzania), in partnership with the Gender-Based Violence Network (Mkuki) and other development stakeholders, has recognized and awarded 16 outstanding champions for their commitment to combating gender-based violence and advancing human rights.

TUZO ZA MAPAMBANO DHIDI YA UKATILI WA KIJINSIA ZATOLEWA

February 06, 2026 Add Comment

      

Shirika la Wanawake katika Sheria na Maendeleo Barani Afrika (WiLDAF Tanzania), kwa kushirikiana na mtandao wa kupambana na ukatili wa kijinsia (Mkuki) na wadau wengine wa maendeleo, wameandaa na kugawa tuzo kwa vinara 16 wa kupinga vitendo vya ukatili wa kijinsia na utetezi wa haki za binadamu.
WAFANYABIASHARA KARIAKOO WAPO TAYARI KWA MFUMO WA IDRAS

WAFANYABIASHARA KARIAKOO WAPO TAYARI KWA MFUMO WA IDRAS

February 06, 2026 Add Comment

Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wafanyabiashara wa Kariakoo (JWK) Bw. Severin Mushi,akizungumza wakati wa mafunzo ya mfumo mpya kwa wafanyabiashara wa Kariakoo.

Na.Mwandishi Wetu- KARIAKOO

Wafanyabiashara wameukubali mfumo wa Usimamizi wa Kodi za ndani (IDRAS) ,huku wakijiandaa kuupokea Jumatatu ya tarehe 9 Februari mwaka huu.

Akizungumza leo 6.2.2026 jijini Dar es salaam katika mafunzo ya mfumo mpya kwa wafanyabiashara wa Kariakoo Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wafanyabiashara wa Kariakoo (JWK) Bw. Severin Mushi amesema wapo tayari kuanza kuutumia mfumo huo kwa ushirikiano wa karibu na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA).

Mwenyekiti huyo amesema kupitia mafunzo ambayo wamepatiwa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) wanaamini mfumo utakuwa msaada kwao na kuondoa changamoto mbalimbali ambazo zilikuwepo.

Amesema mafunzo hayo yamekuwa msaada mkubwa kwa wafanyabiashara kwa kuwa yameondoa hofu iliyokuwepo awali na kuwapa uelewa wa pamoja kuhusu matumizi ya mfumo huo.

Bw. Mushi amesema wamejiandaa kuupokea mfumo wa IDRAS, akieleza kuwa jambo lolote jipya huwa linaogopesha kwa wanaolipokea.

Amebainisha kuwa mabadiliko ya kiteknolojia hayaepukiki katika dunia ya sasa, hivyo wafanyabiashara wanapaswa kuendana nayo ili kuboresha ufanisi wa ulipajikodi.

Hata hivyo, Mushi ametoa rai kwa TRA kushirikiana na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) kutatua changamoto ya mtandao katika baadhi ya maeneo ya biashara, hususani Kariakoo ili kuleta ufanisi wa matumizi mazuri ya mfumo mpya wa IDRAS kwa walipakodi.

Aidha, ametoa wito kwa wafanyabiashara wote kuwa tayari kuupokea mfumo wa IDRAS na kushirikiana na Serikali pamoja na TRA kwa karibu, akisisitiza kuwa lengo kubwa ni kuhakikisha ulipaji wa kodi unakuwa rahisi na wenye tija.

“Tumejiandaa kuupokea mfumo kuanzia Jumatatu ya tarehe 9 mwezi huu Kikubwa ni kushirikiana na Serikali kuhakikisha tunalipa kodi na mifumo ya ulipaji iwe rahisi,” amesema Bw. Mushi.

Aidha,Mwenyekiti huyo amependekeza kuwepo kwa kipindi cha mpito cha mafunzo ili kuwapa wafanyabiashara nafasi ya kuuelewa mfumo huo Zaidi na kuleta ufanisi sahihi wa utekelezaji wake.

“Angalau miezi mitatu ya mwanzo iwe ni ya mafunzo na kuwaelimisha watu namna ya kutumia mfumo, watakapokuwa wameuelewa, tutakwenda pamoja,”- Bw. Mushi.

INDIA YAELEZWA TUNDA LA MTI WA KATI LILILIWA NGORONGORO

February 06, 2026 Add Comment


India imefikiwa na Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro kupata simulizi nzuri ya Eden inayosimuliwa kwenye vitabu vya dini inayoelezwa kwamba Adam na Eva walikula tunda la Mti wa kati.


Katika maonesho ya kimataifa ya utalii yanayofanyika  India tarehe 6-7 Januari, 2026 Afisa Masoko Mkuu Michael Makombe anatoa elimu kwa washiriki kuhusu kasoko ya Ngorongoro kuwa ni Eden inayozungumzwa kwenye vitabu vya dini.

“Ngorongoro tuna amini kuwa ndiyo Eden kutokana na kuwa na vitu vyote ambavyo Mungu amevitaja katika sifa za Bustani ya Eden.

Amevitaja vitu hivyo kuwa ni mandhari ya kuvutia,wanyama na ndege, matunda ya aina zote,misitu na mimea,wadudu,maji na miamba yenye mapango yenye muundo unaomfanya binadamu aweze kuwasiliana na Mungu.

Ngorongoro yenye utajiri wa Vivutio imetambuliwa na mtandao wa World Travel Awards kama kivutio bora cha utalii kwa mwaka 2023 na 2025 vivutio ambavyo  vipo sehemu moja na hivyo kudhihirisha Eden iliyotajwa kwenye vitabu vya dini

UMEME VITONGOJINI WACHOCHEA UCHAKATAJI MAZAO KATAVI

UMEME VITONGOJINI WACHOCHEA UCHAKATAJI MAZAO KATAVI

February 06, 2026 Add Comment






*Wakandarasi watakiwa kuacha maneno, ahadi na michakato wamalize mradi kwa wakati

*Bilioni 57.3 kupeleka umeme vitongoji 358 mkoani Katavi

*Ajira kupewa kipaumbele

Katavi

Imeelezwa kuwa mradi wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Awamu ya Pili B (HEP 2B) unakwenda kuongeza na kuchocchea uchakataji wa mazao ambayo kwa kiasi kikubwa wananchi wa mkoa wa Katavi wanazalisha mazao katika mkoa huo.

Hayo yamebainishwa na Mkuu wa Mkoa wa Katavi, Mhe. Mwanamvua Mrindoto leo tarehe 6 Februari, 2026 mara baada ya kutambulishwa kwake mkandarasi Kampuni ya M/s ETDCO Ltd atakayetekeleza mradi wa HEP 2B wa kupeleka umeme kwenye vitongoji 358 kwa wakazi zaidi ya 11,536 mkoani Katavi.

“Kwa sasa badala ya kuuza mazao ghafi tutaiza bidhaa, suala hili la kupatikana kwa umeme litakwenda kuipandisha bei za mazao kwa sababu yatachakatwa katika hali nzuri na zitauzwa bidhaa badala ya kuuza malighafi,” Amesema RC. Mrindoto.

Vilevile, ameongeza kuwa upatikanaji wa umeme wa uhakika kupitia mradi wa HEP 2B utakwenda kukuza uchumi, kukuza uwekezaji na kuleta ajira kwa vijana, wanawake, wazee na makundi mbalimbali katika mkoa huo.

“Nimsisitize mkandarasi kujipanga sawasawa uingie kazini kwa miguu yote miwili ukiwa na kasi kubwa kwa sababu wanachohitaji wananchi ni umeme wala sio maneno au ahadi, sio ratiba, sio michakato,” Amesema RC Mrindoto.

Kwa upande wake, Mwakilishi wa Mkurugenzi Mkuu wa REA, Bw. Mussa Muze amesema lengo kuu la utekelezaji wa mradi wa HEP 2B ni kuongeza upatikanaji wa umeme kwa wananchi katika vitongoji vya mkoa wa Katavi na kusaidia maendeleo jumuishi ya kijamii na kiuchumi.

Naye, Msimamizi wa Miradi ya REA mkoa wa Katavi, Mha. Gilbert Furia amesema, Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imetoa rai kwa wananchi wa mkoa wa Katavi kushiriki vema katika utekelezaji wa mradi, na kutumia fursa ya kuletewa umeme kuweza kujiinua kiuchumi.

Pia, Mkandarasi kutoka Kampuni ya M/s ETDCO Ltd, Mha. Abdalah Mitenda amemueleza RC Mrindoto kuwa katika mradi huo wakandarasi watapewa kipaumbele kufanya shughuli mbalimbali zitakazokuwa zinafanyika katika mradi huo na kuwataka kuchangamkia fursa.