HABARI

SIASA

ELIMU

Recent Posts

TUTATOA USHIRIKIANO KWA WIZARA -MNZAVA

January 15, 2026 Add Comment


Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi Maliasili na Utalii imeahidi kutoa ushirikiano kwa Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi wakati wote wa kutekeleza majukumu yake.


Kauli hiyo imetolewa leo tarehe 15 Januari, 2026 na Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mhe. Timetheo Mnzava wakati wa kikao cha Kamati ya Kudumu ya Bunge na Wizara ya Ardhi kilichokuwa na lengo la kuifahamu wizara ya ardhi na taasisi zake.

Pamoja na kuifahamu wizara na taasisi zake, Kamati za Kudumu za Bunge zinatakiwa kufahamu baadhi ya sera na sheria kulingana na majukumu ya kila kamati kama ilivyofafanuliwa kwenye nyongeza ya 8 ya Kanuni za Kudumu za Bunge chini ya Kanuni ya 140 ya Kanuni za Bunge inayoelekeza Kamati kupitishwa kwenye majukumu yake ya msingi na Kamati ya Bajeti kufanya maandalizi ya Hoja zitakazojadiliwa na Bunge.

Mwenyekiti huyo wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi Maliasili na Utalii ambaye ni Mbunge wa jimbo la Korogwe vijijini amesema, kelele ni nyingi katika masuala ya ardhi lakini wao kama kamati wataendelea kuwa pamoja na wizara kuhakikisha migogoro ya ardhi inatatuliwa na kazi ya kushughulikia changamoto za sekta ya ardhi inakuwa nyepesi.

Kwa upande wake Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Dkt Leonard Akwilapo aliwashukuru wajumbe wa kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi Maliasili na Utalii kwa michango yao aliyoieleza kuwa ina lengo la kuboresha sekta ya ardhi nchini.


"Sisi wizara tutahakikisha tunapokea ushauri na maoni yenu na kuyafanyia kazi ili tuwe na matokeo chanya katika sekta ya ardhi" amesema mhe Dkt Akwilapo.

Vikao vya Kamati za Kudumu za Bunge ni kwa ajili ya maandalizi ya Mkutano wa 2 wa Bunge la 13 unaotarajiwa kuanza Jumanne, tarehe 27 Januari, 2026.

Kikao hicho kimehudhuriwa na Naibu Waziri wa Wizara hiyo Mhe. Kaspar Mmuya, Katibu Mkuu Mhandisi Anthony Sanga, Naibu Katibu Mkuu Bi Lucy Kabyemera, wajumbe wa Menejimeti pamoja na Wakuu wa taasisi zilizo chini ya Wizara hiyo.


-----------------mwisho------------

WIZARA YA NISHATI KUSHIRIKIANA NA TBC KUHAMASISHA MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA

January 15, 2026 Add Comment


Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Wizara ya Nishati, Bi. Neema Mbuja  amepokea ujumbe rasmi kutoka Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) wenye lengo la kuimarisha ushirikiano katika kuitangaza Wizara ya nishati hususani katika kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia nchini.

Akizungumza leo Januari 15, 2026 Katika ofisi za Wizara Mtumba Jijini Dodoma, baada ya kupokea ujumbe huo, Bi. Neema Mbuja alimshukuru Mkurugenzi wa Habari na Matukio Shirika la Utangazaji Tanzani (TBC), Bi. Eshe Muhidin pamoja na timu yake kwa kuendelea kuitangaza Wizara ya nishati pamoja na ajenda ya nishati safi ya kupikia kupitia Bongo FM na TBC kwa ujumla.

“Tunashukuru sana juhudi za TBC katika kuelimisha jamii kuhusu nishati safi ya kupikia, kwani kupitia ushirikiano huu tunakusudia kuifanya ajenda hii isambae kwa upana zaidi na kuwafikia wananchi wengi zaidi ili kutimiza azma ya Mhe. Rais ya Kuhakikisha ifikapo 2034 asilimia 80% ya Watanzania wanatumia nishati safi ya kupikia” alisema Bi. Mbuja

Ameongeza kuwa wizara itaendelea kushirikiana kwa karibu na vyombo vya habari katika kuhakikisha taarifa sahihi  za Nishati zinawafikia wananchi kwa wakati.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Habari na Matukio Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC), Bi. Eshe Muhidin ameishukuru Wizara ya Nishati kwa ushirikiano wao wa karibu huku akibainisha kuwa TBC ni wadau wakubwa katika kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia.

“Tunaishukuru Wizara ya Nishati kwa ushirikiano wao, kwani TBC imekuwa mdau mkubwa katika kuhakikisha wananchi wanahamasishwa kutumia nishati safi ya kupikia hivyo tuibebe ajenda hii kwa ukubwa zaidi kwa maslahi mapana ya Taifa lengo likiwa ni kumsaidi Mhe. Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kuifikisha ajenda ya Pika Kijanja kwa wananchi alisema Bi.Muhidin. 


Aidha Bi. Muhidin aliambatana na Mkurugenzi wa Huduma za Redio TBC, Bi. Anna Kwambaza, pamoja na Mkuu wa Bongo FM, Bi. Anastazia Willherick.


*#KaziNaUtu 

#TunasongaMbele 

#TabasamuLaUtu

#NishatiTupoKazini*

WAZIRI MKUU AONGOZA KIKAO KAZI NA WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA NA TIMU YA WATAALAM

WAZIRI MKUU AONGOZA KIKAO KAZI NA WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA NA TIMU YA WATAALAM

January 15, 2026 Add Comment



Waziri Mkuu, Dkt Mwigulu Nchemba akizungumza katika kikao cha kazi na Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Adolf Mkenda (kushoto) na Timu ya Wataalam kwenye ukumbi wa Ofisi ya Waziri Mkuu, Mlimwa jijini Dodoma, Januari 15, 2026. Kulia ni Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Wanu Hafidh Ameir. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

Waziri Mkuu, Dkt Mwigulu Nchemba akizungumza katika kikao cha kazi na Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Adolf Mkenda na Timu ya Wataalam kwenye ukumbi wa Ofisi ya Waziri Mkuu, Mlimwa jijini Dodoma, Januari 15, 2026. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu).

Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba akiteta na Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Wanu Hafidh Ameir katika kikao cha kazi na Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Adolf Mkenda na Timu ya Wataalam kwenye ukumbi wa Ofisi ya Waziri Mkuu, Mlimwa jijini Dodoma, Januari 15, 2026. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu).

Waziri Mkuu, Dkt.Mwigulu Nchemba akizungumza na Waziri wa Elimu , Sayansi na Teknolojia, Profesa Adolf Mkenda (wa pili kulia), Naibu Waziri wa Elimu , Sayansi na Teknolojia, Wanu Hafidh Ameir (kulia ) na Katibu Mkuu Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia, Profesa Carolyne Nombo katika kikao cha kazi na Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia na Timu ya Wataalam kwenye ukumbi wa Ofisi ya Waziri Mkuu, Mlimwa jijini Dodoma, Januari 15, 2026. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu).

Baadhi ya washiriki wa kikao cha kazi cha Waziri Mkuu na Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia na Timu ya Wataalam wakimsikiliza Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba alipozungumza kwenye ukumbi wa Ofisi ya Waziri Mkuu, Mlimwa jijini Dodoma, Januari 15, 2026. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

SERIKALI KUPITIA REA KUZINDUA MIRADI MIKUBWA YA KIMKAKATI

January 15, 2026 Add Comment




📌Kituo cha Kupoza Umeme Mtera


📌Mradi wa Kusambaza umeme katika vitongoji 9,009


Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) inatarajia kuzindua Kituo cha Kupoza na Kusambaza Umeme cha Mtera na Kusaini Mikataba ya kutekeleza mradi kabambe wa kusambaza umeme kwenye vitongoji 9,009 katika Mikoa yote Tanzania Bara.


Mkurugenzi Mkuu wa REA, Mha. Hassan Saidy amesema hayo Jijini Dodoma Januari 15, 2026 katika mkutano maalum na wanahabari  alipokuwa akitambulisha matukio hayo mawili yatakayoshuhudiwa na Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi ambaye atakuwa mgeni rasmi.


“Tarehe 16 Januari, 2026 Kituo cha Kupoza Umeme cha Mtera kitazinduliwa rasmi na tarehe 17 Januari, 2026 tutasaini mikataba 30 yenye thamani ya shilingi Trilioni 1.2 kwa ajili ya kutekeleza mradi mkubwa wa kusambaza umeme katika vitongoji zaidi ya 9,000,” amefafanua Mha. Saidy


Amebainisha kuwa Kituo cha Mtera kimejengwa kwa gharama ya shilingi bilioni 9.2 na Serikali ya Tanzania kupitia REA kwa ushirikiano na Serikali za Sweden na Norway.


Aidha, Mhandisi Saidy amesema REA itasaini mikataba 30 na Wakandarasi 21 wazawa na wakandarasi 9 kutoka nje ya nchi lakini wamesajiliwa nchini kwa ajili ya kutekeleza mradi huo utakaotekelezwa kwa kipindi cha miaka mitatu ndani ya Mikoa yote Tanzania Bara.


Amewataka wananchi kuchangamkia fursa zitakazopatikana wakati wote wa utekelezaji wake ikiwemo ajira, biashara na huduma mbalimbali zitakazohitajika na pia kuhakikisha wanachangamkia kutumia umeme kuzalisha mali na kuboresha huduma za kijamii.


“Tunatekeleza maono ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan; mradi huu unakwenda kufungua nchi kiuchumi ni wa kipekee na mradi mkubwa kuwahi kutekelezwa na REA kwa viwango vya gharama na idadi ya vitongoji vitakavyofikiwa,” amesema Mha. Saidy.

RAS TANGA AHAKIKISHA UTAYARI WA WIKI YA FEDHA

January 15, 2026 Add Comment

                  

                 Na Chedaiwe Msuya na Eva Ngowi, WF, Tanga


Katibu Tawala wa Mkoa wa Tanga (RAS), Bw. Rashid Mchatta, amewahakikishia wadau wa sekta ya fedha kuwa maadhimisho ya Wiki ya Huduma za Fedha yatakayofanyika jijini Tanga yatakuwa na mafanikio makubwa kutokana na maandalizi madhubuti na ushirikiano wa karibu kati ya Serikali na wadau husika.

Bw. Mchatta alitoa kauli hiyo ofisini kwake jijini Tanga wakati alipokutana na wataalamu kutoka Wizara ya Fedha kwa kushirikiana na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, waliowasili mkoani humo kwa ajili ya maandalizi ya maadhimisho hayo yanayotarajiwa kufanyika kuanzia Januari 19 hadi 26, 2026, katika Viwanja vya Usagara.

Akizungumza katika kikao hicho, Bw. Mchatta alisema Serikali ya Mkoa imejipanga kikamilifu kuhakikisha maadhimisho hayo yanawafikia wananchi wengi iwezekanavyo, akibainisha kuwa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Halmashauri na Taasisi nyingine za Serikali zitatumika kuhamasisha ushiriki wa wananchi.

“Tutahakikisha uhamasishaji unafanyika vya kutosha ili wananchi wa makundi yote wakiwemo watumishi wa umma, wajasiriamali, vikundi mbalimbali, waendesha bodaboda na wakazi wote wa Jiji la Tanga wanashiriki kikamilifu,” alisema Bw. Mchatta.

Kwa upande wao, wataalamu kutoka Wizara ya Fedha walieleza kuwa lengo kuu la maadhimisho hayo ni kuwawezesha wananchi kupata elimu sahihi ya fedha, ili waweze kutumia huduma za kifedha kwa tija na hatimaye kujikwamua kiuchumi.

Walifafanua kuwa licha ya wananchi wengi kupata mikopo, ruzuku na fursa mbalimbali za uwezeshaji, changamoto ya uelewa mdogo wa elimu ya fedha imekuwa ikiwafanya washindwe kufikia matokeo yaliyokusudiwa, hali inayochangia kushindwa kwa miradi mingi ya kiuchumi.

Katika kuimarisha maandalizi, Bw. Mchatta aliomba Wizara ya Fedha kuendelea kushirikiana kwa karibu na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa pamoja na Halmashauri, huku akiahidi ushirikiano wa dhati na utatuzi wa changamoto zozote zitakazojitokeza kabla na wakati wa maadhimisho.

Naye Mchumi Mkuu, kutoka Idara ya Uendelezaji wa Sekta ya Fedha, Wizara ya Fedha Bw. Thobias Kanyoki, kwa niaba ya Timu ya Wizara ya Fedha, alimshukuru Bw. Mchatta na uongozi wa Mkoa wa Tanga kwa ushirikiano mkubwa waliouonesha tangu kuwasili kwao mkoani humo.

Alisema ushiriki wa Serikali ya Mkoa ni muhimu sana, hasa katika kuhakikisha wananchi wengi wanapata elimu ya fedha, kwani taasisi zote za kifedha zinatarajiwa kushiriki na kutoa huduma pamoja na elimu katika Viwanja vya Usagara wakati wa maadhimisho hayo.

“Wananchi wa Jiji la Tanga wanahimizwa kujitokeza kwa wingi kushiriki katika Maadhimisho ya Wiki ya Huduma za Fedha ili kupata elimu ya fedha kwa maendeleo endelevu ya kiuchumi. Hudhuria Wiki ya Huduma za Fedha – Jifunze, Jiwezeshe, Jikwamue Kiuchumi.” Alisema Bw. Kanyoki.


Katibu Tawala Mkoa wa Tanga (RAS), Rashid Mchatta, akizungumza na Timu ya Uratibu ya Maadhimisho ya Wiki ya Huduma za Fedha kutoka Wizara ya Fedha katika Ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Jiji la Tanga kuhusu maandalizi ya maonyesho hayo, yanayotarajia kufanyika katika Viwanja vya Usagara jijini Tanga.
Afisa Msimamizi wa Fedha Mkuu, kutoka Idara ya Uendelezaji wa Sekta ya Fedha, Wizara ya Fedha Bw. Salim Kimaro, akifafanua jambo kwa Katibu Tawala Mkoa wa Tanga (RAS), Rashid Mchatta, katika Ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Jiji la Tanga kuhusu maandalizi ya maonyesho hayo, yanayotarajia kufanyika katika Viwanja vya Usagara jijini Tanga.
 Picha ya Pamoja ya Katibu Tawala Mkoa wa Tanga (RAS), Rashid Mchatta,(katikati) akiwa na Timu ya Uratibu kutoka Wizara ya katika Ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Jiji la Tanga kuhusu maandalizi ya maonyesho hayo, yanayotarajia kufanyika katika Viwanja vya Usagara jijini Tanga. (Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Tanga) 

RAIS DKT.SAMIA AZUNGUMZA NA MABALOZI KATIKA SHEREHE YA MWAKA MPYA KWA MABALOZI

January 15, 2026 Add Comment





Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Mabalozi wanaowakilisha nchi zao Tanzania, Wawakilishi wa Mashirika ya Kimataifa, pamoja na Wawakilishi wa Heshima katika sherehe ya Mwaka Mpya kwa Mabalozi (Diplomatic Sherry Party) iliyofanyika kwa mara ya kwanza Ikulu ya Chamwino, Dodoma tarehe 15 Januari, 2026.


Mabalozi wanaowakilisha nchi zao Tanzania, Wawakilishi wa Mashirika ya Kimataifa, pamoja na Wawakilishi wa Heshima wakiwa kwenye sherehe ya Mwaka Mpya kwa Mabalozi (Diplomatic Sherry Party) iliyofanyika kwa mara ya kwanza, Ikulu ya Chamwino, Dodoma tarehe 15 Januari, 2026.

Amidi wa Mabalozi ambaye pia ni Balozi wa Comoro nchini Tanzania Mhe. Ahmada El Badaoui Mohamed Fakih, akizungumza kwenye sherehe ya Mwaka Mpya kwa Mabalozi (Diplomatic Sherry Party) iliyofanyika kwa mara ya kwanza, Ikulu ya Chamwino, Dodoma tarehe 15 Januari, 2026.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye sherehe ya Mwaka Mpya kwa Mabalozi (Diplomatic Sherry Party) iliyofanyika kwa mara ya kwanza, Ikulu ya Chamwino, Dodoma tarehe 15 Januari, 2026.



Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Thabit Kombo akizungumza kwenye sherehe ya Mwaka Mpya kwa Mabalozi (Diplomatic Sherry Party) iliyofanyika kwa mara ya kwanza, Ikulu ya Chamwino, Dodoma tarehe 15 Januari, 2026.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa na Amidi wa Mabalozi ambaye pia ni Balozi wa Comoro nchini Tanzania Mhe. Ahmada El Badaoui Mohamed Fakih, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Thabit Kombo, Katibu Mkuu Kiongozi Mhe. Balozi Dkt. Moses Kusiluka, Katibu Mkuu Ikulu Ndugu Mululi Majula Mahendeka kwenye picha ya pamoja na Mabalozi wanaowakilisha nchi zao Tanzania katika sherehe ya Mwaka Mpya kwa Mabalozi (Diplomatic Sherry Party), Ikulu ya Chamwino, Dodoma tarehe 15 Januari, 2026.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa na Amidi wa Mabalozi ambaye pia ni Balozi wa Comoro nchini Tanzania Mhe. Ahmada El Badaoui Mohamed Fakih, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Thabit Kombo, Katibu Mkuu Kiongozi Mhe. Balozi Dkt. Moses Kusiluka, Katibu Mkuu Ikulu Ndugu. Mululi Majula Mahendeka kwenye picha ya pamoja na Wawakilishi wa Heshima na Kaimu Mabalozi katika sherehe ya Mwaka Mpya kwa Mabalozi (Diplomatic Sherry Party), Ikulu ya Chamwino, Dodoma tarehe 15 Januari, 2026.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa na Amidi wa Mabalozi ambaye pia ni Balozi wa Comoro nchini Tanzania Mhe. Ahmada El Badaoui Mohamed Fakih, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Thabit Kombo, Katibu Mkuu Kiongozi Mhe. Balozi Dkt. Moses Kusiluka, Katibu Mkuu Ikulu Ndugu. Mululi Majula Mahendeka kwenye picha ya pamoja na Wakuu wa Mashirika ya Kimataifa katika sherehe ya Mwaka 

USISHANGAE MATAA MJINI,TEMBEA UONE MCHANGA UNAOHAMA ( SHIFTING SANDS) NGORONGORO

January 15, 2026 Add Comment




Waswahili husema tembea uone na Mwenda bure si mkaa bure huenda ataokota.


Ukitaka kujaribu kuuokota mchanga unaohama njoo jirani na bonde la Olduvai ndani ya hifadhi ya Ngorongoro ushangae.


Jirani na bonde hili la Olduvai kuna mchanga unaohama  ambao huwavutia mealfu ya watalii kuja kujionea maajabu hayo.


Mchanga huu upo katika umbo la nusu mwezi na upo  karibu na Bonde la Olduvai ndani ya Hifadhi ya Ngorongoro. 

Mchanga huu wenye rangi nyeusi umetokana na madini ya chuma na majivu yaliyotokana na mlipuko wa Volcano kutoka Mlima Oldoinyo Lengai.


Mchanga huu ambao husogea kwa kasi ya takribani mita 15–29 kwa mwaka tuta lake lina urefu wa mita 5 na upana wa mita 100.


Hayo ndiyo maajabu ya Hifadhi ya Ngorongoro ukitaka kujua zaidi kuhusu mchanga huu tembea uone kwani fahari ya macho ni kuona  na fahari ya macho haifilisi duka.


 _Tumerithishwa, Tuwarithishe_

NGORONGORO YANADI UTALII MKUTANO WA MAHAKIMU NA MAJAJI DODOMA

January 15, 2026 Add Comment


Na Mwandishi wetu, Dodoma.


Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro (NCAA) imeshiriki mkutano mkuu wa Chama cha Mahakimu na Majaji Tanzania kwa lengo la kunadi vivutio vya utalii na kuimarisha ushirikiano kati ya Ngorongoro na Mahakama. 


Mkutano huo uliofunguliwa  tarehe 13 januari, 2026 na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan unaendelea hadi tarehe 16 Januari, 2026 ambapo wadau mbalimbali wa sekta ya sheria kutoka maeneo tofauti ya nchi wanashiriki kujadili masuala mbalimbali yanayohusu haki, utawala wa sheria na maendeleo ya mfumo wa utoaji haki nchini.

Ujumbe wa Ngorongoro uliongozwa na Kamishna msaidizi mwandamizi wa Uhifadhi anayesimamia idara ya utalii na Masoko Mariam Kobelo pamoja na Afisa Uhifadhi mwandamizi-Sheria Usaje Mwambene ambapo mada mbalimbali kuhusu vivutio vya utalii, fursa za uwekezaji, huduma zinazotolewa na upekee wa Ngorongoro kama kivutio bora cha utalii barani afrika kwa mwaka 2023 na 2025. 

Aidha, NCAA imetumia mkutano huo kujenga uelewa kwa wadau wa sheria kuhusu misingi ya kisheria inayosimamia uhifadhi wa rasilimali za asili ili kutangaza vivutio mbalimbali vya utalii vinavyopatikana katika hifadhi hiyo ikiwemo Kreta za Ngorongoro, Empakai, Olmoti, maporomoko yaa maji endoro, Ndutu ambalo ni maarufu kwa mazalia ya nyumbu wanaaohama, mchanga unaohama, makumbusho ya olduvai, makumbusho na jiopaki na vingine vingi.


MAAFISA MAWASILIANO WAANDALIWA KUKABILIANA NA MABADILIKO YA TEKNOLOJIA

January 15, 2026 Add Comment
Chama Cha Maafisa Mawasiliqno wa Serikali Tanzania (TAGCO) kimeendelea kutoa mafunzo mbalimbali ikiwemo matumizi ya teknolojia ya Akili unde (Artificial Intelligence – AI) kwa Maafisa Mawasiliano wa serikali kwa lengo la kuhakikisha wanafanya kazi kuendana na mabadiliko ya teknolojia.

DKT.MWIGULU : KAZI ZINAZOWEZA KUFANYWA NA WAZAWA ZISIFANYWE NA WAGENI

January 14, 2026 Add Comment



WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba amezitaka wizara zinazohusika na masuala ya ajira zisimamie kikamilifu utekelezaji wa sheria zinazotaka kazi zinazoweza kufanywa na Watanzania zisifanywe na wageni isipokuwa zile zinazohitaji utaalamu ambao nchi inaupungufu.

 

Vilevile, Waziri Mkuu amekemea tabia ya baadhi ya wenye nyumba kumpangisha raia mmoja wa kigeni na kumruhusu mpangaji huyo apangishe watu wengine ndani ya nyumba hiyo jambo ambalo ni hatari kwa usalama na pia halina tija kibiashara.

 

Mheshimiwa Dkt. Mwigulu ametoa agizo hilo leo Jumatano, Januari 14, 2026 alipofungua Kikao cha Mawaziri, Naibu Mawaziri, Makatibu Wakuu na Manaibu Makatibu Wakuu wa Wizara za Kisekta kujadili fursa za ajira ndani na nje ya nchi.


Agizo hilo linalenga kuongeza fursa za ajira kwa Watanzania kufuatia kuwepo kwa wimbi kubwa la wageni kufanya kazi au biashara ambazo zinaweza kufanywa na Watanzania na kuliwezesha Taifa kukabiliana na changamoto ya upungufu wa ajira.


“…Kazi zinazoweza kufanywa na Watanzania ziachwe wafanye, si kuruhusu wageni wafanye. Tusioneane aibu kama tumefungua milango au kulegeza wataalamu wafuatilie. Wageni wafanye kazi za kitaalamu ambazo nchi ina uhaba wa wataalamu.”


Amesema kuwa ni lazima wataalamu wa ndani wasimamie sheria ipasavyo na kama kuna maeneo yanayokwamisha wayabainishe na yafanyiwe marekebisho. “Hatuwezi kuleta watu wanaokuja kufanya kazi ambazo Watazania wanaziweza.”

 

Katika hatua nyingine, Mheshimiwa Dkt. Mwigulu ametoa wito kwa Watanzania kuwa na wivu na nchi yao kwa kutoruhusu baadhi ya vitu kufanyika, ambapo alitolea mfano suala la wenye nyumba kumpangisha raia moja wa kigeni ambaye naye analeta wenzake wengi katika nyumba hiyo hiyo.

 

“Watanzania tuwe na wivu na nchi yetu, mfano mtu anamkodishia nyumba mgeni kwa dola 5,000 kwa mwaka na kisha mgeni huyo anawaleta wenzake 60 na anawakodisha dola 500 hapo Mtanzania anapata hasara, hii si sawa hata kwa usalama.”

 

Waziri Mkuu amewaagiza wahusika wafuatilie suala hilo la makazi ili wakae katika utaratibu ulio rasmi. “Eneo hili liangaliwe wageni wanalundikana na kufanya kazi ambazo Watanzania wangeweza kufanya, hatuwezi kuruhusu hili tunataka wawekezaji.”

 

Hivyo, Waziri Mkuu ameziagiza wizara zinazohusika zifuatilie suala hilo, pamoja na kuwasisitiza wasimamie utekelezwaji wa sheria kwa sababu kila nchi ina sheria zake na Tanzania inatekeleza majukumu yake kwa kufuata sheria.

 

Amesema sheria zimetungwa ili kusaidia kujenga kampuni za Watanzania na kuzikuza, hivyo wizara zinazohusika zihakikishe hazisajili kampuni za kigeni kabla ya kuzifanyia uchunguzi wa kina kwa sababu baadhi ya taarifa zinazowasilishwa si sahihi.

KRETA YA EMPAKAAI (EMPAKAAI CRATER).

January 14, 2026 Add Comment



 Kasoko ya Empakaai ni mojawapo ya Kasoko za volkano ndani ya Hifadhi ya Ngorongoro, ikiwa na kingo za juu na ziwa zuri linalofunika zaidi ya asilimia 75 ya sakafu ya Kreta/Kasoko. Kivutio kikubwa ndani ya kreta hii ni idadi kubwa ya ndege heroe (flamingo) wanaoonekana kando ya ufukwe wa ziwa, Ndege wanapokuwa wengi hufanya ziwa hilo kuwa na rangi ya pinki.

Kreta hii katika nyanda za juu za Ngorongoro imezungukwa na kuta za misitu yenye mteremko mkali wa takribani mita 300 kwa urefu, zikiwa na uoto wa asili wa kijani kibichi, wanyamapori na aina mbalimbali ya ndege. Eneo lake lina upana wa takribani kilomita 8, huku karibu nusu ya sakafu yake ikifunikwa na ziwa la lenye magadi na kina kirefu, makazi ya heroe (flamingo) na ndege wengine wa majini. 

Kutoka juu ya ukingo wa kreta ya Empakai, wageni wanaweza kuona Mlima Oldoinyo Lengai, Bonde la Ufa na Ziwa Natron kwa mandhari ya kuvutia. Pia wanaweza kufurahia matembezi ya asili kutoka juu ya mlima au kushuka hadi sakafuni kushuhudia vivutio vilivyopo.

Empakaai ina kimo cha takribani mita 3,200 kutoka juu ya usawa wa bahari upande wa magharibi na mita 2,590 upande wa mashariki. Mara nyingi hufunikwa na ukungu kutokana na mwinuko wake ambapo ziwa huonekana la kijani kibichi au buluu ya kina.

Kreta/Kasoko  ya Empakaai ni maarufu kwa safari za kutembea kwa miguu, ambapo watalii hutembea kwa takribani saa mbili na nusu kwenda na kurudi kutegemea na uwezo wa mwili. Wageni wanaweza kuona kwa ukaribu ziwa na msitu mnene uliopo ndani na kuzunguka sakafu ya Kasoko.

 Kivutio cha Empakaai kinaweza kutembelewa wakati wowote wa majira ya mwaka, lakini inapendelewa zaidi kuanzia mwezi Juni hadi Desemba (msimu wa kiangazi).

 _Karibu Ngorongoro 

Tumerithishwa, tuwarithishe_ 






TEKNOLOJIA ZA KIDIJITALI ZATAJWA KUIMARISHA UFANISI WA UFUNDISHIJI NA UJIFUNZAJI

TEKNOLOJIA ZA KIDIJITALI ZATAJWA KUIMARISHA UFANISI WA UFUNDISHIJI NA UJIFUNZAJI

January 14, 2026 Add Comment

Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Carolyne Nombo, akizungumza wakati wa Warsha ya Kujenga Uelewa kwa Wadau  Juu ya  Mkakati na Miongozo ya Kitaifa kuhusu Matumizi ya Teknolojia za Kidijitali kwenye Sekta ya Elimu iliyofanyika leo Januari 14,2026 jijini Dodoma.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Carolyne Nombo, akizungumza wakati wa Warsha ya Kujenga Uelewa kwa Wadau  Juu ya  Mkakati na Miongozo ya Kitaifa kuhusu Matumizi ya Teknolojia za Kidijitali kwenye Sekta ya Elimu iliyofanyika leo Januari 14,2026 jijini Dodoma.

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia (Sekta ya Sayansi), Prof Daniel Mushi, akizungumza wakati wa Warsha ya Kujenga Uelewa kwa Wadau  Juu ya  Mkakati na Miongozo ya Kitaifa kuhusu Matumizi ya Teknolojia za Kidijitali kwenye Sekta ya Elimu iliyofanyika leo Januari 14,2026 jijini Dodoma.

Sehemu ya washiriki wakimsikiliza Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Carolyne Nombo (hayupo pichani),wakati wa Warsha ya Kujenga Uelewa kwa Wadau  Juu ya  Mkakati na Miongozo ya Kitaifa kuhusu Matumizi ya Teknolojia za Kidijitali kwenye Sekta ya Elimu iliyofanyika leo Januari 14,2026 jijini Dodoma.

Sehemu ya washiriki wakimsikiliza Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Carolyne Nombo (hayupo pichani),wakati wa Warsha ya Kujenga Uelewa kwa Wadau  Juu ya  Mkakati na Miongozo ya Kitaifa kuhusu Matumizi ya Teknolojia za Kidijitali kwenye Sekta ya Elimu iliyofanyika leo Januari 14,2026 jijini Dodoma.

 

Wadau  wakichangia mada mbalimbali wakati wa Warsha ya Kujenga Uelewa kwa Wadau  Juu ya  Mkakati na Miongozo ya Kitaifa kuhusu Matumizi ya Teknolojia za Kidijitali kwenye Sekta ya Elimu iliyofanyika leo Januari 14,2026 jijini Dodoma.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Carolyne Nombo,akiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kufungua  Warsha ya Kujenga Uelewa kwa Wadau  Juu ya  Mkakati na Miongozo ya Kitaifa kuhusu Matumizi ya Teknolojia za Kidijitali kwenye Sekta ya Elimu iliyofanyika leo Januari 14,2026 jijini Dodoma.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Carolyne Nombo,akiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kufungua  Warsha ya Kujenga Uelewa kwa Wadau  Juu ya  Mkakati na Miongozo ya Kitaifa kuhusu Matumizi ya Teknolojia za Kidijitali kwenye Sekta ya Elimu iliyofanyika leo Januari 14,2026 jijini Dodoma.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Carolyne Nombo,akiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kufungua  Warsha ya Kujenga Uelewa kwa Wadau  Juu ya  Mkakati na Miongozo ya Kitaifa kuhusu Matumizi ya Teknolojia za Kidijitali kwenye Sekta ya Elimu iliyofanyika leo Januari 14,2026 jijini Dodoma.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Carolyne Nombo,akiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kufungua  Warsha ya Kujenga Uelewa kwa Wadau  Juu ya  Mkakati na Miongozo ya Kitaifa kuhusu Matumizi ya Teknolojia za Kidijitali kwenye Sekta ya Elimu iliyofanyika leo Januari 14,2026 jijini Dodoma.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Carolyne Nombo,akiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kufungua  Warsha ya Kujenga Uelewa kwa Wadau  Juu ya  Mkakati na Miongozo ya Kitaifa kuhusu Matumizi ya Teknolojia za Kidijitali kwenye Sekta ya Elimu iliyofanyika leo Januari 14,2026 jijini Dodoma.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Carolyne Nombo,akiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kufungua  Warsha ya Kujenga Uelewa kwa Wadau  Juu ya  Mkakati na Miongozo ya Kitaifa kuhusu Matumizi ya Teknolojia za Kidijitali kwenye Sekta ya Elimu iliyofanyika leo Januari 14,2026 jijini Dodoma.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Carolyne Nombo,akiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kufungua  Warsha ya Kujenga Uelewa kwa Wadau  Juu ya  Mkakati na Miongozo ya Kitaifa kuhusu Matumizi ya Teknolojia za Kidijitali kwenye Sekta ya Elimu iliyofanyika leo Januari 14,2026 jijini Dodoma.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Carolyne Nombo,akiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kufungua  Warsha ya Kujenga Uelewa kwa Wadau  Juu ya  Mkakati na Miongozo ya Kitaifa kuhusu Matumizi ya Teknolojia za Kidijitali kwenye Sekta ya Elimu iliyofanyika leo Januari 14,2026 jijini Dodoma.

Na.Alex Sonna-DODOMA

Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia imezitaka taasisi zote za elimu nchini kuongeza ubunifu na ufanisi katika ufundishaji na ujifunzaji kupitia matumizi bora, salama, na yenye uwajibikaji wa teknolojia za kidijitali.

Hayo yamesemwa   na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Prof. Carolyne Nombo,wakati wa Warsha ya Kujenga Uelewa kwa Wadau  Juu ya  Mkakati na Miongozo ya Kitaifa kuhusu Matumizi ya Teknolojia za Kidijitali kwenye Sekta ya Elimu iliyofanyika leo Januari 14,2026 jijini Dodoma.

Prof. Nombo amewataka wadau wa elimu kuzingatia mabadiliko ya kidijitali kama hitaji la lazima, huku akisisitiza kwamba ustawi wa baadaye wa Tanzania unategemea nguvu kazi yenye ujuzi wa kidijitali na ubunifu, kama inavyobainishwa katika Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.

“Mkakati huu unalenga kuweka mfumo wa kitaifa wa kuratibu na kuongoza mageuzi ya kidijitali katika ngazi zote za elimu kuanzia shule, vyuo vya ualimu, taasisi za TVET, vyuo vikuu, hadi ujifunzaji wa mtandaoni,” amesema Prof. Nombo.

Aidha, Prof. Nombo amesisitiza umuhimu wa ufundishaji wa kidijitali na ujumuishaji wa TEHAMA, pamoja na uelewa wa Akili Unde  (AI) na stadi za data katika mafunzo ya walimu. Ameeleza kuwa maendeleo endelevu ya kitaaluma kupitia majukwaa ya kidijitali ni muhimu ili kuwawezesha walimu kutumia teknolojia kwa ubunifu na uwajibikaji.

“Nafasi ya walimu ni nguzo kuu ya mageuzi kidijitali. Teknolojia peke yake haiwezi kuleta mabadiliko bila walimu wenye ujuzi na utayari wa kutumia teknolojia za kufundishia na kujifunzia,” amefafanua.

Prof. Nombo pia amesisitiza umuhimu wa Miongozo ya Kitaifa ya Elimu ya Kidijitali na Mwongozo wa Matumizi ya Akili Unde  katika Elimu, ambayo inalenga kuhakikisha matumizi ya teknolojia hayaingilii maadili, ulinzi wa data, ujumuishi, na ubora wa kitaaluma. Vyuo vikuu na taasisi za utafiti wanahimizwa kuongeza ubunifu na utafiti unaozingatia AI na teknolojia nyingine zinazochipuka.

Aidha,ametoa wito kwa taasisi za udhibiti na uthibitishaji ubora kama TCU, NACTVET, COSTECH, TCRA na ICTC kushirikiana na wizara na kutoa elimu ili kuhakikisha mshikamano wa kisera, ulinganifu, na muingiliano wa mifumo sambamba na sera na miongozo ya kitaifa.

Prof. Nombo amewahimiza kutoa  ushirikiano na washirika wa maendeleo na sekta binafsi, wakihimizwa kuunda suluhisho zinazolingana na muktadha wa Tanzania na kuunga mkono ukuaji wa stadi, ubunifu, na uendelevu wa elimu ya kidijitali.


“Usambazaji ni hatua ya kwanza tu. Utekelezaji unahitaji uongozi, uratibu, rasilimali na uwajibikaji. Naomba taasisi zote kuingiza Mkakati wa Kitaifa wa Elimu ya Kidijitali na Miongozo yake katika mipango yao, kuteua waratibu, kutenga rasilimali, na kushiriki kikamilifu katika ufuatiliaji, tathmini na kujifunza kwa pamoja.”amesema Prof. Nombo

Kwa upande wake,Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia (Sekta ya Sayansi), Prof Daniel Mushi, amepongeza hatua ya Serikali kuandaa Mkakati na Miongozo ya Kitaifa ya Matumizi ya Teknolojia za Kidijitali katika Elimu, akisema juhudi hizo zinaweka msingi madhubuti wa mageuzi ya elimu yanayoendana na kasi ya dunia ya sasa.

 Prof Mushi amesema  hatua hiyo inalenga kuboresha ubora wa ufundishaji na ujifunzaji, kukuza ubunifu, na kuwaandaa walimu na wanafunzi kukidhi mahitaji ya zama za kidijitali.

Warsha hiyo ya siku mbili, inayofanyika Januari 14–15, 2026, inawakutanisha wataalam na viongozi mbalimbali wakiwemo makatibu wakuu, wakuu wa vyuo vikuu, viongozi wa VETA, wakuu wa vyuo vya ualimu, taasisi za maendeleo pamoja na wadau wengine wa elimu kutoka sekta za umma na binafsi.

“Huu ni mwendelezo wa jitihada za Serikali kujenga mfumo mmoja na shirikishi wa matumizi ya teknolojia za kidijitali kwenye elimu. Ushiriki wenu unaonesha dhamira ya dhati ya kuijenga Tanzania yenye elimu bora, jumuishi na inayoshindana kikanda na kimataifa,” amesema Prof Mushi.