HABARI

SIASA

ELIMU

Recent Posts

WAZIRI SANGU AHIMIZA DIASPORA KUCHANGIA KIKAMILIFU MAENDELEO YA TAIFA

WAZIRI SANGU AHIMIZA DIASPORA KUCHANGIA KIKAMILIFU MAENDELEO YA TAIFA

January 25, 2026 Add Comment

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Clement Sangu akizungumza na Viongozi wa Watanzania wanaoishi nchini Saudi Arabia (Diaspora), katika hoteli ya Ritz Carlton, Jijini Riyadh, Saudi Arabia tarehe 25 Januari, 2026.

Na: OWM (KAM) – Riyadh, Saudi Arabia

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Masuala ya Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Clement Sangu, amewahimiza Watanzania wanaoishi nje ya nchi (Diaspora) kuitambua na kuielewa kwa kina Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 ili waweze kubaini fursa zilizopo na kuchangia kikamilifu maendeleo ya Taifa.

Amesema Dira hiyo inaeleza mwelekeo wa Taifa ambalo Tanzania inalenga kujenga, hivyo ni muhimu kwa Diaspora kuitumia kama mwongozo wa kutambua na kunufaika na fursa mbalimbali zilizopo katika sekta za uwekezaji, ajira, ujuzi, ubunifu na matumizi ya teknolojia, kwa lengo la kukuza uchumi na kuongeza Pato la Taifa.

Mhe. Sangu ameyasema hayo wakati wa ziara yake ya kikazi nchini Saudi Arabia, ambapo pamoja na mambo mengine, anatarajiwa kushiriki Mkutano wa Mawaziri wa Kazi Duniani (Global Labour Market Conference) unaojadili masuala ya soko la ajira duniani.

Katika ziara hiyo, Waziri Sangu pia amekutana na Watanzania wanaoishi na kufanya kazi nchini Saudi Arabia tarehe 24 Januari, 2026, kwa lengo la kujadiliana, kubadilishana uzoefu na kusikiliza changamoto pamoja na fursa zilizopo kwa Watanzania wanaofanya kazi nje ya nchi.

Alieleza kuwa, Serikali inatambua mchango mkubwa wa Diaspora katika kukuza uchumi wa Taifa kupitia fedha wanazozituma nyumbani (remittances), uwekezaji, pamoja na kuhamasisha maarifa na ujuzi walioupata nje ya nchi.

Aidha, Waziri Sangu amesema Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imeendelea kuchukua hatua madhubuti za kuhakikisha Watanzania wanaofanya kazi nje ya nchi wanalindwa, wanaheshimiwa na wananufaika ipasavyo na fursa za ajira za kimataifa.

“Tumeimarisha ushirikiano na Serikali ya Saudi Arabia kupitia makubaliano ya ajira, kuboresha mifumo ya usimamizi wa mawakala binafsi wa ajira, pamoja na kuanzisha mafunzo ya kabla ya kuondoka nchini ili kuwaandaa Watanzania wetu kikamilifu,” amesema Waziri Sangu

Kadhalika, amewahakikishia Diaspora kuwa Ofisi ya Waziri Mkuu kupitia Kitengo cha Huduma za Ajira itaendelea kuratibu na kusimamia fursa za ajira kwa Watanzania ili kuhakikisha zinakuwa za staha, salama na zenye haki.

Kwa upande mwingine, Waziri Sangu amesema Serikali kupitia Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) imeanzisha mafao yatakayowawezesha Watanzania walioajiriwa katika sekta binafsi pamoja na waliojiajiri kunufaika na huduma za hifadhi ya jamii hata wanapokuwa nje ya nchi.

Pia Waziri Sangu ameipongeza Saudi Arabia kwa mahusiano mazuri na mashirikiano na Tanzania kwani kupitia mkataba wa mashirikiano umewezasha Watanzania 1,049 kupata ajira Nchini Saudi Arabia.

Naye, Mwenyekiti wa Diaspora nchini Saudi Arabia, Dkt. Zidikheri Msechu, amesema Diaspora wako tayari kushirikiana na Serikali katika utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo. Pia amewahimiza Watanzania wanaopata fursa za ajira nje ya nchi kufuata taratibu rasmi na kutumia mawakala wanaotambulika na Serikali kabla ya kwenda kufanya kazi nje ya nchi.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Clement Sangu akizungumza na Viongozi wa Watanzania wanaoishi nchini Saudi Arabia (Diaspora), katika hoteli ya Ritz Carlton, Jijini Riyadh, Saudi Arabia tarehe 25 Januari, 2026.

 Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Clement Sangu akipokea taarifa kutoka kwa Mwenyekiti wa Watanzania wanaofanya kazi nchini Saudi Arabia (Diaspora), Dkt. Zidikheri Msechu walipokutana katika hotrli ya Ritz Carlton, Jijini Riyadh, Saudi Arabia. Kushoto ni Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Ajira na Mahusiano, Zuhura Yunus.

 

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Clement Sangu,akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi wa Watanzania wanaoishi nchini Saudi Arabia (Diaspora), katika hoteli ya Ritz Carlton, Jijini Riyadh, Saudi Arabia tarehe 25 Januari, 2026.

MABILIONI YA MRABAHA KUTOKA BARRICK NORTH MARA YAANZA KUTEKELEZA MIRADI YA MAENDELEO KWA KASI TARIME VIJIJINI

January 25, 2026 Add Comment

   

Wenyeviti wa vijiji vya Kewanja, Kerende, Genkuru, Nyamwaga na Nyangoto wakiwa katika mojawapo ya matukio ya kupokea gawio la mrahaba kutoka Mgodi wa Dhahabu wa Barrick North Mara mwaka 2025.

Miradi mipya ya kijamii imeanza kutekelezwa kwa kasi katika vijiji vitano kutokana na fedha za gawio wa mrabaha zilizotolewa na Mgodi wa Dhahabu wa North Mara katika miaka ya hivi karibuni ambazo zimekuwa zinawekwa kwenye akaunti za benki kwa muda mrefu bila matumizi yoyote ya miradi ya kuwaletea maendeleo wananchi wa vijiji hivyo.

WATENDAJI WA UCHAGUZI PERAMIHO WATAKIWA KUVISHIRIKISHA VYAMA VYA SIASA

January 25, 2026 Add Comment

 

Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Mahakama ya Rufaa, Jacobs Mwambegele akizungumza leo tarehe 24 Januari, 2026 mkoani Iringa wakati akifungua mafunzo ya watendaji wa uchaguzi kutoka Halmashauri za Wilaya ya Songea, mkoani Ruvuma na Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi, mkoani Songwe.
Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Mahakama ya Rufaa, Jacobs Mwambegele akizungumza leo tarehe 24 Januari, 2026 mkoani Iringa wakati akifungua mafunzo ya watendaji wa uchaguzi kutoka Halmashauri za Wilaya ya Songea, mkoani Ruvuma na Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi, mkoani Songwe.

Washiriki wa mafunzo 
ya watendaji wa uchaguzi kutoka Halmashauri za Wilaya ya Songea, mkoani Ruvuma na Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi, mkoani Songwe wakifuatilia hotuba ya ufunguzi ya Mwemyekiti wa Tume.
Washiriki wa mafunzo ya watendaji wa uchaguzi kutoka Halmashauri za Wilaya ya Songea, mkoani Ruvuma na Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi, mkoani Songwe wakifuatilia hotuba ya ufunguzi ya Mwemyekiti wa Tume.
Meza Kuu ikiwa katika mafunzo hayo.
Viongozi kutoka Managementi ya Tume wakiwa katika mkutano huo.

Washiriki wa mafunzo ya watendaji wa uchaguzi kutoka Halmashauri za Wilaya ya Songea, mkoani Ruvuma na Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi, mkoani Songwe wakifuatilia hotuba ya ufunguzi ya Mwemyekiti wa Tume.
Washiriki wa mafunzo ya watendaji wa uchaguzi kutoka Halmashauri za Wilaya ya Songea, mkoani Ruvuma na Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi, mkoani Songwe wakifuatilia hotuba ya ufunguzi ya Mwemyekiti wa Tume.
****************
Na. Mwandishi Wetu, Iringa
Watendaji wa uchaguzi wametakiwa kuvishirikisha kwa ukaribu vyama vya siasa vyenye usajili kamili katika hatua zote za mchakato wa uchaguzi katika maeneo yao ili kurahisisha utekelezaji wa majukumu.

Hayo yamesemwa na Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Mahakama ya Rufaa, Jacobs Mwambegele leo tarehe 24 Januari, 2026 mkoani Iringa wakati akifungua mafunzo ya watendaji wa uchaguzi kutoka Halmashauri za Wilaya ya Songea, mkoani Ruvuma na Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi, mkoani Songwe.

Mafunzo hayo ni sehemu ya maandalizi ya uchaguzi mdogo wa ubunge kwenye Jimbo la Peramiho lililopo Halmashauri ya Wilaya ya Songea, mkoani Ruvuma na Kata ya Shiwinga iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi, mkoani Songwe unaotarajiwa kufanyika tarehe 26 Februari, 2026.

“Wakati wote wa mchakato wa uchaguzi huu, ni vema mkavishirikisha kwa karibu vyama vyote vya siasa vyenye usajili kamili na wadau wengine wa uchaguzi katika maeneo yenu kuhusu masuala ya kiuchaguzi ambayo wanastahili kushirikishwa kwani jambo hilo litawarahisishia utekelezaji wa majukumu yenu,” amesema Jaji Mwambegele.

Ameongeza kuwa watendaji hao wa uchaguzi wanapaswa kuzingatia sheria, kanuni na maelekezo watakayopewa na Tume badala ya kufanya kazi kwa mazoea.

“Nachukua nafasi hii kuwaasa kuwa, pamoja na uzoefu ambao baadhi yenu mnao katika uendeshaji wa uchaguzi, mhakikishe mnazingatia maelekezo mtakayopewa na Tume badala ya kufanya kazi kwa mazoea. Kwani kila uchaguzi unatofautiana na uchaguzi mwingine,” amesema.

Amewataka watendaji hao kufanya utambuzi wa vituo vya kupigia kura mapema ili kubaini mahitaji maalum ya vituo husika na kuhakikisha kunakuwa na mpangilio mzuri ambao utaruhusu uchaguzi kufanyika kwa utulivu na amani.

Jaji Mwambegele amewasisitiza watendaji hao kuhakikisha wanaajiri watendaji wa vituo wenye sifa, weledi, wanaojitambua na kuachana na upendeleo kwa ndugu na jamaa ambao hawana sifa za kufanya shughuli za uchaguzi.

“Mhakiki vifaa vya uchaguzi mnavyopokea kutoka Tume na kuhakikisha kila mkuu wa kituo anapata vifaa vyote vya uchaguzi vinavyohitajika mapema na muweke utaratibu utakaowezesha kila kituo cha kupigia kura kufunguliwa saa 1:00 asubuhi,” amesema.

Aidha, washiriki wa mafunzo hayo kutoka Halmashauri za Wilaya ya Songea, mkoani Ruvuma na Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi, mkoani Songwe walikula viapo vya kujitoa uanachama wa vyama vya siasa na kile cha kutunza siri mbele ya Hakimu Mkazi wa Mkoa wa Iringa, Mhe. Rehema Mayagilo. 

Mafunzo hayo ya siku tatu yamewahusisha Waratibu wa Uchaguzi wa Mikoa ya Songwe na Ruvuma, Wasimamizi wa Uchaguzi, Wasimamizi Wasaidizi wa Uchaguzi Ngazi ya Jimbo, Wasimamizi wa Uchaguzi Ngazi ya Kata, Maafisa Uchaguzi, Maafisa Ununuzi na Wahasibu.
Hakimu Mkazi Mkoa wa Iringa, Mhe. Rehema Mayagilo akiongoza viapo vya kujitoa uanachama wa vyama vya siasa na Kiapo cha kutunza siri kwa washiriki wa mafunzo hayo. 

Washiriki wa mafunzo ya watendaji wa uchaguzi kutoka Halmashauri za Wilaya ya Songea, mkoani Ruvuma na Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi, mkoani Songwe wakila viapo vya kujitoa uanachama wa vyama vya siasa na kile cha kutunza siri mbele ya Hakimu Mkazi wa Mkoa wa Iringa, Mhe. Rehema Mayagilo. 

Washiriki wa mafunzo ya watendaji wa uchaguzi kutoka Halmashauri za Wilaya ya Songea, mkoani Ruvuma na Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi, mkoani Songwe wakila viapo vya kujitoa uanachama wa vyama vya siasa na kile cha kutunza siri mbele ya Hakimu Mkazi wa Mkoa wa Iringa, Mhe. Rehema Mayagilo. 
Washiriki wa mafunzo ya watendaji wa uchaguzi kutoka Halmashauri za Wilaya ya Songea, mkoani Ruvuma na Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi, mkoani Songwe wakila viapo vya kujitoa uanachama wa vyama vya siasa na kile cha kutunza siri mbele ya Hakimu Mkazi wa Mkoa wa Iringa, Mhe. Rehema Mayagilo. 

MHE. MILLYA ATEMBELEA KITUO CHA UTOAJI HUDUMA KWA PAMOJA CHA NAMANGA

January 25, 2026 Add Comment
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje anayeshughulikia masuala ya Afrika Mashariki Mhe. James Kinyasi Millya (Mb.) ametembelea Kituo cha Utoaji Huduma kwa Pamoja Mpakani ( One Stop Boarder Post-OSBP ) cha Namanga kilichopo mkoani Arusha Januari 24,2026.

Akitembelea kituoni hapo, Mhe Millya alipokelewa na Meneja wa Mamlaka ya Mapato mkoa wa Arusha Bw. Deogratius Shuma na wawakilishi kutoka Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Longido na watumishi wa taasisi 18 za Serikali zinazotoa huduma katima kituo hicho.

Mhe Waziri Milya pia alikutana na viongozi wa Jumuiya ya Wafanyabiashara mpakani ikiwemo TAFFA, CHAWAMATA, TCCIA, na Wanawake Wajasiliamali Mpakani.

Ziara hiyo ililenga kujionea hali halisi ya utendaji kazi wa Kituo cha Namanga kwa upande wa Tanzania, kukagua miundombinu ya Kituo na utoaji wa huduma hususan katika uendeshaji wa shughuli za pamoja za Forodha katika mwamvuli wa Mtangamano wa Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Akizungumza na wadau kituoni hapo Mhe. Millya amesema mpaka wa Namanga ni moja kati ya vituo vikubwa na kitovu cha kiuchumi kati ya Tanzania na Kenya kutokana na usafirishaji wa bidhaa za viwandani, mazao ya kilimo, huduma za utalii na muingiliano wa wananchi ki fursa kati ya nchi mbili.

Katika mazungumzo na wadau, Mhe Millya amepokea changamoto zinazokabili ufanisi wa Kituo cha Namanga, aidha wadau wameishukuru Serikali kwa kutembelea kituo hicho na kuonesha imani kubwa katika kutatua changamoto mbalimbali zilizopo na kuboresha miundombinu ili kuleta tija na kuimarisha ushirikiano kati ya Tanzania na Kenya.

MCC RAJAB AWAKABIDHI AFRICAN SPORTS BASI JIPYA, AHAIDI KUENDELEA KUISAPOTI IREJEE LIGI KUU

January 25, 2026 Add Comment


Na Oscar Assenga,TANGA

MJUMBE wa Kamati Kuu ya CCM Taifa na Mwenyekiti wa  Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Tanga  Rajabu Abdurhaman amesema ana dhamira ya dhati kurejesha timu ya mpira wa miguu, African Spots ya jijini humo ili kurejesha heshima ya timu hiyo kongwe pamoja na Daby ya Tanga iliyokuwa na upinzani mkubwa hapa nchini.



Alisema timu hiyo imekuwa ikisuasua kupanda daraja kwa muda mrefu kutokana na changamoto mbali mbali ikiwemo basi la kuwasafirisha wachezaji pamoja na benchi la ufundi hivyo uwepo wa basi hilo utasaidia kuwawezesha kuondokana nazo


Aliyasema hayo Januari 24 mwaka huu katika hafla ya kuukabidhi uongozi wa timu hiyo gari Jipya aina ya TATA lililogarimu takribani shilingi Milioni 170, katika hafla iliyofanyika Makao Makuu ya Klabu hiyo barabara 12 Jijini Tanga .

Rajabu ambaye  pia ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Taifa (MCC) alisema kwamba kurudi kwa timu hiyo  kongwe hapa nchini ambayo ilianzishwa mwaka 1936 kutarejesha heshima ya Mkoa wa Tanga kutokana na kwamba bila African Spots hakuna Coastal Union inayochangiwa na utani wa  jadi timu hizo kama ilivyokuwa Simba na Yanga za Jijini Dar es Salaam.


Mbali ya kununua basi na kukabidhi, Mwenyekiti ameahidi kusaidia timu hiyo na kuiinua hadi kufikia kucheza ligi kuu ambapo ataipambania na kujenga Jengo la Ofisi la Gorofa tatu ikiwa ni pamoja na kununua gari kubwa zaidi wakati gari iliyokabidhiwa kubaki kuwa ya kuwapeleka wachezaji mazoezini.


Sambamba na kukabidhi gari hilo mwenyekiti huyo pia alitoa kiasi cha shilingi Milioni 30 na kukabidhi kwa uongozi wa timu ya Coastal Union kwa ajili ya kutatua changamoto kadhaa zinazowakabili.


Awali akizungumza katika Halfa hiyo Rais wa TFF  Walles Karia aliwasihi wanachama kushirikiana na vionhozi ili kufanya maamuzi pamoja na kujitokeza uwanjani pindi timu zitakapokuwq zancheza kwani ndio jambo sahihi la kuvuta wawekezaji.


Lakini pia aliwasihi viwanja vya michezo vilivyopo Myanjani Technically Center, "kile kituo kipo na kinafanya vizuri sana lakini kinanufaisha vijana walioko nje ya Tanga, niwasiji kwamba mpeleke vijana pale ili timu zetu zipate wachezaji bora" alisema Karia.

Katika hafla hiyo alikuwepo Naibu Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Hamisi Mwinjuma (Mwana FA) ambaye alisisitiza suala la wanachama kushirikiana na vionhozi wa timu hiyo na kuchangia kipato kwenye timu matokeo yataonekana.

"Kama tutakuwa na timu mbili (2) zinazoenda ligi kuu, hata uchumi wa Tanga utaimarika kupitia michezo, tuchangie timu kwa kwenda uwanjani na hata kununua jezi, kwa kufanya hivyo kutaimarisha timu zetu na wachezaji kuwa na ari uwanjani" alisema.

Katika kuinua timu hizo Naibu Waziri Mwana FA alitoa kiasi cha shilingi Milioni 10 ambapo kila timu imekabidhiwa kwa vionhozi wa timu zote mbili kiasi cha shilingi Milioni 5.

Rais Karia amewahakikishia Watanzania kwamba timu ya African Spots ikismama imara kama awali na Coastal Union ndiyo timu pekee ambazo zina uwezo wa kusimamishana na Simba na Yanga na siyo timu nyingine.

Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Balozi, Dk. Batilda Buriani aliwataka vionhozi wa timu za mipira na wanamichezo wote kutumia fursa ambazo zipo mkoani humo katika kuimarisha timu na kuleta manufaa katika Mkoa.

"Mradi wa Bomba la mafuta nao una fursa katika michezo, kule Uganda wamesaidia kujenga uwanja wa mpira, na hata timu yetu ya Coastal Union imeshapeleka maombi yake tunasubiri utekelezaji mwengine uendelee" alisema