HABARI

SIASA

ELIMU

Recent Posts

RAIS DKT. MWINYI AZINDUA MBIO ZA MWENGE WA UHURU 2026, ASISITIZA AMANI, UZALENDO NA UWAJIBIKAJI

April 02, 2026 Add Comment


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amewataka Watanzania kulinda, kuimarisha na kudumisha Muungano wa Tanzania, amani, utulivu na umoja wa kitaifa kama msingi wa maendeleo endelevu.

Rais Dkt. Mwinyi ameyasema hayo leo tarehe 02 Aprili , 2026 wakati wa uzinduzi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa 2026 uliofanyika Uwanja wa Gombani, Pemba.

Aidha, Rais Mwinyi amesema taasisi zote nchini na wananchi kwa ujumla wana wajibu wa kuheshimu utu, haki, usawa na utawala wa sheria ili kuendeleza mshikamano wa Taifa.

Ameeleza kuwa Mwenge wa Uhuru unaendelea kuwa chombo muhimu cha kuhamasisha uzalendo, uwajibikaji na mapambano dhidi ya maadui wa maendeleo wakiwemo umasikini, ujinga na maradhi.

Vilevile, amewahimiza Watanzania kupinga ubaguzi wa aina yoyote na kuunga mkono juhudi za Serikali katika kupambana na rushwa, dawa za kulevya na magonjwa kama UKIMWI na malaria.

Halikadhalika, Rais Dkt. Mwinyi amebainisha kuwa Serikali inaendelea kuimarisha huduma za afya, kudhibiti matumizi ya dawa za kulevya na kupunguza maambukizi ya malaria, huku akisisitiza umuhimu wa ushirikiano wa wadau wote katika kufanikisha maendeleo ya Taifa.

Mwenge wa Uhuru umeanza mbio zake katika Mkoa wa Kusini Pemba na unatarajiwa kufikia kilele chake Oktoba 14, 2026 mkoani Rukwa, ukiwa na kaulimbiu: “Tanzania ni Yetu Sote, Tushikamane.”































WIZARA YA NISHATI KUWA MFANO WA MATUMIZI BORA YA NISHATI KATIKA MJI WA SERIKALI MTUMBA

WIZARA YA NISHATI KUWA MFANO WA MATUMIZI BORA YA NISHATI KATIKA MJI WA SERIKALI MTUMBA

April 02, 2026 Add Comment






Wizara ya Nishati kwa kushirikiana na Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) inatarajia kutekeleza Mradi wa Matumizi Bora ya Nishati katika Jengo la Wizara ya Nishati na baadaye Mji wote wa Serikali Mtumba.

Hayo yameelezwa na Kamishna wa Umeme na Nishati Jadidifu Wizara ya Nishati, Mhandisi Innocent Luoga wakati akizungumza katika kikao cha kujadili Utekelezaji wa mradi huo na Meneja Miradi wa UNDP, Aaron Cunningham tarehe 1 Aprili, 2026 katika Mji wa serikali Mtumba, Dodoma.

Mhandisi Luoga amesema mradi wa Matumizi Bora ya Nishati utatekelezwa kwa kuanzia katika jengo la Wizara ya Nishati kwa kufunga mitambo midogo ya kuzalisha umeme kwa kutumia Jua, upepo na Miundombinu yenye kutumia umeme kidogo na kwa ufanisi na hivyo kuwezesha Jengo hilo kuwa na umeme safi na wa uhakika.

Vilevile, mradi huo utahusisha pia kufunga mashine za kuchajia magari ya umeme katika viwanja vya jengo hilo na maeneo ya maegesho ya magari.

“ Tutatekeleza mradi huu kwa kuanzia na jengo la Wizara kwakuwa ndiyo wenye dhamana ya kusimamia Sekta ya Nishati ili iwe mfano kwa Taasisi zingine za Serikali na Binafsi, baadaye mradi huu utatekelezwa katika mji wote wa serikali hapa Mtumba. Hii itasaidia kupunguza gharama za kutumia umeme katika majengo hayo na kuwezesha upatikanaji umeme wa uhakika”, alisema Mhandisi Luoga

Kwa upande wake, Meneja Miradi wa UNDP, Aaron Cunningham, amesema UNDP iko tayari kushirikiana na Wizara ya Nishati kutekeleza mradi huo kwa kuwa tayari wamekuwa wakishirikiana katika miradi mbalimbali na inayoleta tija katika jamii na taifa kwa jumla.

Mradi huo utakuwa na ufanisi mkubwa kwa katika kupunguza gharama za umeme katika taasisi za serikali.

Ametaja baadhi ya miradi ambayo wameshirikiana na Wizara kuwa ni pamoja na mradi wa Matumizi bora ya Nishati ambapo Mkakati wake wa Miaka 10 ulizinduliwa Desemba, 2024

FURAHA YA PASAKA KUTIKISA DAR TAMASHA LA MTOKO NA SHUSHO KUFANYIKA MLIMANI CITY

FURAHA YA PASAKA KUTIKISA DAR TAMASHA LA MTOKO NA SHUSHO KUFANYIKA MLIMANI CITY

April 01, 2026 Add Comment

Tamasha la Pasaka ‘Mtoko na Christina Shusho

Na Mwandishi Wetu

WAZIRI Mkuu wa Tanzania, Dkt. Mwigulu Nchemba, anatarajiwa kuwa mgeni rasmi Aprili 5, 2026, siku ya Jumapili ya Pasaka, katika tamasha la ‘Mtoko na Christina Shusho Pasaka’ litakalofanyika katika Ukumbi wa Mlimani City, jijini Dar es Salaam ambapo wananchi wataruhusiwa kuingia bure.

Kauli mbiu ya tamasha hilo ni “Ushindi wa Milele.”

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam Machi 30, 2026, Meneja wa msanii wa muziki wa injili Christina Shusho, Humphrey Gatimu, amesema maandalizi ya tamasha hilo yamekamilika kwa asilimia 100 na kusisitiza kuwa wananchi wote wanakaribishwa kushiriki bila malipo yoyote.

Amesema tamasha hilo litawakutanisha waimbaji mbalimbali wa muziki wa injili akiwemo Rose Muhando, Joel Lwaga, The Voice, Bella Kombo, Ambwene Mwasongwe, Neema Gospel Choir, Paul Clement na wengine wengi.
“Milango ya ukumbi itafunguliwa rasmi saa nane mchana, hivyo tunawaomba wananchi kujitokeza kwa wingi na kuwahi mapema ili kuepuka changamoto ya kukosa nafasi ndani,” amesema Gatimu.
Aidha, Gatimu amebainisha kuwa matarajio ya waandaaji ni kupanua wigo wa tamasha hilo mwakani kwa kulipeleka katika mikoa mitatu tofauti, huku wakiahidi kuweka wazi maeneo hayo wakati utakapofika.
Kwa upande wake, mwimbaji wa nyimbo za injili, Shusho amesema tamasha hilo ambalo hufanyika kila mwaka kipindi cha Pasaka, limekuwa jukwaa muhimu la kuwakutanisha wasanii wa muziki wa injili, waumini pamoja na familia kwa lengo la kusherehekea sikukuu hiyo na kuinua vipaji vipya.
Amesema mafanikio ya tamasha hilo yanatokana na amani iliyopo nchini Tanzania, akimshukuru Mungu kwa kumpatia kibali cha kufanya tamasha pamoja na viongozi wa serikali kwa kuendelea kudumisha utulivu na maendeleo ya taifa.
“Tunawahimiza watu kufika mapema ili waweze kushiriki kikamilifu ibada ya sifa na kuabudu pamoja nasi, kwani kuna mambo mengi mazuri yameandaliwa kwa ajili ya kumtukuza Mungu,” amesema Shusho.
Naye mwimbaji kutoka kundi la The Voice, Obedi Mark amesema tamasha hilo limekuwa chachu kwa wasanii wengi kukuza vipaji vyao sambamba na kueneza ujumbe wa injili kupitia muziki.
Kwa upande wake mwanakwaya wa kwaya ya Mt Cecilia Makuburi, Joseph Atanasi amesema wao kama kwaya watashiriki kikamilifu katika tamasha hilo wakiwa wamejiandaa vyema kuendelea kumsifu Mungu kupitia uimbaji.
WIKI YA HAKI ZA MLAJI YAADHIMISHWA KWA MSAADA WA VIFAA TIBA HOSPITALI YA RUFAA MBEYA

WIKI YA HAKI ZA MLAJI YAADHIMISHWA KWA MSAADA WA VIFAA TIBA HOSPITALI YA RUFAA MBEYA

April 01, 2026 Add Comment
 

Na.Mwandishi Wetu

TUME ya Ushindani (FCC) Kanda ya Nyanda za Juu Kusini imeadhimisha Wiki ya Haki za Mlaji Duniani kwa kutoa msaada wa vifaa tiba katika Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya, ikiwa ni sehemu ya kuunga mkono juhudi za kuboresha huduma za afya kwa wananchi.

Shughuli hiyo imefanyika tarehe 31 Machi, 2026 ambapo FCC imekabidhi vifaa tiba vinne vya Oxygen Flow Meter vitakavyosaidia wagonjwa wanaohitaji huduma ya hewa tiba, hususan wale wanaopata changamoto ya kupumua.

Akizungumza wakati wa hafla ya makabidhiano hayo, Mkuu wa FCC Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, Bw.Dickson Mbanga, amesema kuwa tukio hilo ni sehemu ya kuadhimisha Wiki ya Haki za Mlaji Duniani pamoja na kutimiza miaka mitatu tangu kuanzishwa kwa ofisi hiyo katika ukanda huo.

Mbanga ameeleza kuwa FCC imeona ni vyema kutumia maadhimisho hayo kwa kutoa mchango wa kijamii utakaoleta tija moja kwa moja kwa wananchi, hasa katika sekta ya afya ambayo ni nyeti na muhimu kwa ustawi wa jamii.

 "Vifaa hivyo vitasaidia kuongeza uwezo wa hospitali katika kuhudumia wagonjwa wanaohitaji msaada wa hewa tiba, hivyo kupunguza changamoto zinazoweza kujitokeza wakati wa utoaji wa huduma hizo."amesema Bw.Mbanga

Kwa upande wake, akipokea vifaa hivyo kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya, Muuguzi Kiongozi Ndg. Petro Seme ametoa shukrani za dhati kwa FCC kwa msaada huo muhimu.

Seme amesema kuwa vifaa hivyo ni vya kisasa na vina uwezo wa kuhudumia wagonjwa wawili kwa wakati mmoja, jambo ambalo litarahisisha upatikanaji wa huduma ya hewa tiba na kuongeza ufanisi katika utoaji wa huduma kwa wagonjwa.

‎WAFANYAKAZI WA TUME YA TAIFA YA MIPANGO WATAKIWA KUWA WABUNIFU NA WELEDI

April 01, 2026 Add Comment

Katibu Mkuu-Mipango na Katibu Mtendaji wa Tume ya Taifa ya Mipango Dkt Tausi M. Kida ametoa wito kwa watendaji wa Tume hiyo kufanya kazi kwa weledi, ubunifu na ushirikiano ili kuishi dhana ya kufanya kazi isivyokawaida ili kuyafikia matarajio ya Taifa jumuishi, lenye ustawi, haki na linalojitegemea.

‎Dkt Kida ametoa wito huo leo jijini Dar es Salaam wakati akifungua Mkutano wa Baraza la Wafanyakazi wa Tume ya Taifa ya Mipango.

Aidha, amesisitiza ‎kuwa Serikali ya awamu ya sita chini ya Mheshimiwa Rais Dkt Samia Suluhu Hassan inayo matarajio makubwa kwa Tume ya kuhakikisha inatekeleza ipasavyo majukumu yake kwa weledi, ari na kuzingatia utu.

‎Mkutano huo, umeongozwa na kauli mbiu isemayo: Utumishi Imara ni Msingi wa Utekelezaji wa Dira 2050.





RAIS DKT. SAMIA SULUHU AKUTANA NA KUFANYA MAZUNGUMZO NA WAGOMBEA WA NAFASI YA URAIS WALIOSHIRIKI UCHAGUZI MKUU OKTOBA, 2025

April 01, 2026 Add Comment


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye mazungumzo na Wagombea wa Nafasi ya Urais na Wagombea Wenza kutoka vyama vya Siasa 16 vilivyoshiriki Uchaguzi Mkuu uliofanyika mwezi Oktoba, 2025. Mazungumzo hayo yalifanyika Ikulu jijini Dar es Salaam tarehe 31 Machi, 2026.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye mazungumzo na Wagombea wa Nafasi ya Urais na Wagombea Wenza kutoka vyama vya Siasa 16 vilivyoshiriki Uchaguzi Mkuu uliofanyika mwezi Oktoba, 2025. Mazungumzo hayo yalifanyika Ikulu jijini Dar es Salaam tarehe 31 Machi, 2026.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye mazungumzo na Wagombea wa Nafasi ya Urais na Wagombea Wenza kutoka vyama vya Siasa 16 vilivyoshiriki Uchaguzi Mkuu uliofanyika mwezi Oktoba, 2025. Mazungumzo hayo yalifanyika Ikulu jijini Dar es Salaam tarehe 31 Machi, 2026.



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Wagombea wa nafasi ya Urais wa Vyama vya Siasa 16 vilivyoshiriki Uchaguzi Mkuu uliofanyika mwezi Oktoba, 2025 mara baada ya mazungumzo yao, Ikulu jijini Dar es Salaam tarehe 31 Machi, 2026.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Wagombea wa nafasi ya Urais wa Vyama vya Siasa 16 vilivyoshiriki Uchaguzi Mkuu uliofanyika mwezi Oktoba, 2025 mara baada ya mazungumzo yao, Ikulu jijini Dar es Salaam tarehe 31 Machi, 2026.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Wagombea wa nafasi ya Urais wa Vyama vya Siasa 16 vilivyoshiriki Uchaguzi Mkuu uliofanyika mwezi Oktoba, 2025 mara baada ya mazungumzo yao, Ikulu jijini Dar es Salaam tarehe 31 Machi, 2026.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Wagombea wa nafasi ya Urais pamoja na Wagombea Wenza wa Vyama vya Siasa 16 vilivyoshiriki Uchaguzi Mkuu uliofanyika mwezi Oktoba, 2025 mara baada ya mazungumzo yao, Ikulu jijini Dar es Salaam tarehe 31 Machi, 2026.







RAIS MSTAAFU DKT JAKAYA MRISHO KIKWETE AHANI MSIBA WA RAIS WA ZAMANI WA ALGERIA JENERALI MSTAAFU LIAMINE ZEROUL

April 01, 2026 Add Comment


Rais Mstaafu Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete leo April 1, 2026 akitia saini kitabu cha maombolezo kufuatia kifo cha Rais wa zamani wa Algeria, Jenerali Mstaafu Liamine Zeroual,  aliyefariki dunia mnamo Machi 28, 2026 akiwa na umri wa miaka 84 baada ya kuugua kwa muda mrefu. Pamoja naye ni Balozi wa Algeria nchini Mheshimiwa Ghalib Zermane.  Kitabu hicho kimefunguliwa nyumbani kwa Balozi Oysterbay jijini Dar es salaam.

Rais Mstaafu Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete leo April 1, 2026 ametia saini kitabu cha maombolezo kufuatia kifo cha Rais wa zamani wa Algeria, Jenerali Mstaafu Liamine Zeroual,  aliyefariki dunia mnamo Machi 28, 2026 akiwa na umri wa miaka 84 baada ya kuugua kwa muda mrefu.


Jenerali Zeroual, aliyependwa na kuheshimikka sana, alichaguliwa kuwa rais mwaka 1995 katika kipindi kigumu cha vita vya wenyewe kwa wenyewe nchini Algeria. Alianzisha mageuzi ya kisiasa, ikiwa ni pamoja na kuratibu uchaguzi wa kwanza wa vyama vingi.

Rais Mstaafu Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete leo April 1, 2026 akitia saini kitabu cha maombolezo kufuatia kifo cha Rais wa zamani wa Algeria, Jenerali Mstaafu Liamine Zeroual,  aliyefariki dunia mnamo Machi 28, 2026 akiwa na umri wa miaka 84 baada ya kuugua kwa muda mrefu. Pamoja naye ni Balozi wa Algeria nchini Mheshimiwa Ghalib Zermane.  Kitabu hicho kimefunguliwa nyumbani kwa Balozi Oysterbay jijini Dar es salaam.

Hata hivyo alijiuzulu mapema mwaka 1998 kabla ya kumaliza muhula wake wa miaka mitano ili kutoa nafasi kwa mpito wa kisiasa, na tangu hapo aliishi maisha ya faragha bila kujihusisha sana na siasa.

Hadi leo anakumbukwa kama kiongozi aliyetoa mchango muhimu katika kuiongoza Algeria katika kipindi cha mpito na changamoto kubwa za kisiasa na kiusalama.

Akiongea na Balozi wa Algeria nchini Mheshimiwa Ghalib Zermane, Dkt Kikwete alisema Algeria na Tanzania imekuwa rafiki wa karibu kwa muda mrefu, na kwamba viongozi wake wote waliopita wamefanya kazi kwa karibu na viongozi wa Tanzania kuanzia Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, hususan hususan katika  ukombozi wa bara la Afrika, akiwataja wataja viongozi hao kama Ahmed Ben Bella, Houari Boumédiène, Chadli Bendjedid,  Liamine Zéroual na Abdelaziz Bouteflika