HABARI

SIASA

ELIMU

Recent Posts

DKT.MWIGULU : KAZI ZINAZOWEZA KUFANYWA NA WAZAWA ZISIFANYWE NA WAGENI

January 14, 2026 Add Comment



WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba amezitaka wizara zinazohusika na masuala ya ajira zisimamie kikamilifu utekelezaji wa sheria zinazotaka kazi zinazoweza kufanywa na Watanzania zisifanywe na wageni isipokuwa zile zinazohitaji utaalamu ambao nchi inaupungufu.

 

Vilevile, Waziri Mkuu amekemea tabia ya baadhi ya wenye nyumba kumpangisha raia mmoja wa kigeni na kumruhusu mpangaji huyo apangishe watu wengine ndani ya nyumba hiyo jambo ambalo ni hatari kwa usalama na pia halina tija kibiashara.

 

Mheshimiwa Dkt. Mwigulu ametoa agizo hilo leo Jumatano, Januari 14, 2026 alipofungua Kikao cha Mawaziri, Naibu Mawaziri, Makatibu Wakuu na Manaibu Makatibu Wakuu wa Wizara za Kisekta kujadili fursa za ajira ndani na nje ya nchi.


Agizo hilo linalenga kuongeza fursa za ajira kwa Watanzania kufuatia kuwepo kwa wimbi kubwa la wageni kufanya kazi au biashara ambazo zinaweza kufanywa na Watanzania na kuliwezesha Taifa kukabiliana na changamoto ya upungufu wa ajira.


“…Kazi zinazoweza kufanywa na Watanzania ziachwe wafanye, si kuruhusu wageni wafanye. Tusioneane aibu kama tumefungua milango au kulegeza wataalamu wafuatilie. Wageni wafanye kazi za kitaalamu ambazo nchi ina uhaba wa wataalamu.”


Amesema kuwa ni lazima wataalamu wa ndani wasimamie sheria ipasavyo na kama kuna maeneo yanayokwamisha wayabainishe na yafanyiwe marekebisho. “Hatuwezi kuleta watu wanaokuja kufanya kazi ambazo Watazania wanaziweza.”

 

Katika hatua nyingine, Mheshimiwa Dkt. Mwigulu ametoa wito kwa Watanzania kuwa na wivu na nchi yao kwa kutoruhusu baadhi ya vitu kufanyika, ambapo alitolea mfano suala la wenye nyumba kumpangisha raia moja wa kigeni ambaye naye analeta wenzake wengi katika nyumba hiyo hiyo.

 

“Watanzania tuwe na wivu na nchi yetu, mfano mtu anamkodishia nyumba mgeni kwa dola 5,000 kwa mwaka na kisha mgeni huyo anawaleta wenzake 60 na anawakodisha dola 500 hapo Mtanzania anapata hasara, hii si sawa hata kwa usalama.”

 

Waziri Mkuu amewaagiza wahusika wafuatilie suala hilo la makazi ili wakae katika utaratibu ulio rasmi. “Eneo hili liangaliwe wageni wanalundikana na kufanya kazi ambazo Watanzania wangeweza kufanya, hatuwezi kuruhusu hili tunataka wawekezaji.”

 

Hivyo, Waziri Mkuu ameziagiza wizara zinazohusika zifuatilie suala hilo, pamoja na kuwasisitiza wasimamie utekelezwaji wa sheria kwa sababu kila nchi ina sheria zake na Tanzania inatekeleza majukumu yake kwa kufuata sheria.

 

Amesema sheria zimetungwa ili kusaidia kujenga kampuni za Watanzania na kuzikuza, hivyo wizara zinazohusika zihakikishe hazisajili kampuni za kigeni kabla ya kuzifanyia uchunguzi wa kina kwa sababu baadhi ya taarifa zinazowasilishwa si sahihi.

KRETA YA EMPAKAAI (EMPAKAAI CRATER).

January 14, 2026 Add Comment



 Kasoko ya Empakaai ni mojawapo ya Kasoko za volkano ndani ya Hifadhi ya Ngorongoro, ikiwa na kingo za juu na ziwa zuri linalofunika zaidi ya asilimia 75 ya sakafu ya Kreta/Kasoko. Kivutio kikubwa ndani ya kreta hii ni idadi kubwa ya ndege heroe (flamingo) wanaoonekana kando ya ufukwe wa ziwa, Ndege wanapokuwa wengi hufanya ziwa hilo kuwa na rangi ya pinki.

Kreta hii katika nyanda za juu za Ngorongoro imezungukwa na kuta za misitu yenye mteremko mkali wa takribani mita 300 kwa urefu, zikiwa na uoto wa asili wa kijani kibichi, wanyamapori na aina mbalimbali ya ndege. Eneo lake lina upana wa takribani kilomita 8, huku karibu nusu ya sakafu yake ikifunikwa na ziwa la lenye magadi na kina kirefu, makazi ya heroe (flamingo) na ndege wengine wa majini. 

Kutoka juu ya ukingo wa kreta ya Empakai, wageni wanaweza kuona Mlima Oldoinyo Lengai, Bonde la Ufa na Ziwa Natron kwa mandhari ya kuvutia. Pia wanaweza kufurahia matembezi ya asili kutoka juu ya mlima au kushuka hadi sakafuni kushuhudia vivutio vilivyopo.

Empakaai ina kimo cha takribani mita 3,200 kutoka juu ya usawa wa bahari upande wa magharibi na mita 2,590 upande wa mashariki. Mara nyingi hufunikwa na ukungu kutokana na mwinuko wake ambapo ziwa huonekana la kijani kibichi au buluu ya kina.

Kreta/Kasoko  ya Empakaai ni maarufu kwa safari za kutembea kwa miguu, ambapo watalii hutembea kwa takribani saa mbili na nusu kwenda na kurudi kutegemea na uwezo wa mwili. Wageni wanaweza kuona kwa ukaribu ziwa na msitu mnene uliopo ndani na kuzunguka sakafu ya Kasoko.

 Kivutio cha Empakaai kinaweza kutembelewa wakati wowote wa majira ya mwaka, lakini inapendelewa zaidi kuanzia mwezi Juni hadi Desemba (msimu wa kiangazi).

 _Karibu Ngorongoro 

Tumerithishwa, tuwarithishe_ 






TEKNOLOJIA ZA KIDIJITALI ZATAJWA KUIMARISHA UFANISI WA UFUNDISHIJI NA UJIFUNZAJI

TEKNOLOJIA ZA KIDIJITALI ZATAJWA KUIMARISHA UFANISI WA UFUNDISHIJI NA UJIFUNZAJI

January 14, 2026 Add Comment

Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Carolyne Nombo, akizungumza wakati wa Warsha ya Kujenga Uelewa kwa Wadau  Juu ya  Mkakati na Miongozo ya Kitaifa kuhusu Matumizi ya Teknolojia za Kidijitali kwenye Sekta ya Elimu iliyofanyika leo Januari 14,2026 jijini Dodoma.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Carolyne Nombo, akizungumza wakati wa Warsha ya Kujenga Uelewa kwa Wadau  Juu ya  Mkakati na Miongozo ya Kitaifa kuhusu Matumizi ya Teknolojia za Kidijitali kwenye Sekta ya Elimu iliyofanyika leo Januari 14,2026 jijini Dodoma.

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia (Sekta ya Sayansi), Prof Daniel Mushi, akizungumza wakati wa Warsha ya Kujenga Uelewa kwa Wadau  Juu ya  Mkakati na Miongozo ya Kitaifa kuhusu Matumizi ya Teknolojia za Kidijitali kwenye Sekta ya Elimu iliyofanyika leo Januari 14,2026 jijini Dodoma.

Sehemu ya washiriki wakimsikiliza Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Carolyne Nombo (hayupo pichani),wakati wa Warsha ya Kujenga Uelewa kwa Wadau  Juu ya  Mkakati na Miongozo ya Kitaifa kuhusu Matumizi ya Teknolojia za Kidijitali kwenye Sekta ya Elimu iliyofanyika leo Januari 14,2026 jijini Dodoma.

Sehemu ya washiriki wakimsikiliza Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Carolyne Nombo (hayupo pichani),wakati wa Warsha ya Kujenga Uelewa kwa Wadau  Juu ya  Mkakati na Miongozo ya Kitaifa kuhusu Matumizi ya Teknolojia za Kidijitali kwenye Sekta ya Elimu iliyofanyika leo Januari 14,2026 jijini Dodoma.

 

Wadau  wakichangia mada mbalimbali wakati wa Warsha ya Kujenga Uelewa kwa Wadau  Juu ya  Mkakati na Miongozo ya Kitaifa kuhusu Matumizi ya Teknolojia za Kidijitali kwenye Sekta ya Elimu iliyofanyika leo Januari 14,2026 jijini Dodoma.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Carolyne Nombo,akiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kufungua  Warsha ya Kujenga Uelewa kwa Wadau  Juu ya  Mkakati na Miongozo ya Kitaifa kuhusu Matumizi ya Teknolojia za Kidijitali kwenye Sekta ya Elimu iliyofanyika leo Januari 14,2026 jijini Dodoma.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Carolyne Nombo,akiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kufungua  Warsha ya Kujenga Uelewa kwa Wadau  Juu ya  Mkakati na Miongozo ya Kitaifa kuhusu Matumizi ya Teknolojia za Kidijitali kwenye Sekta ya Elimu iliyofanyika leo Januari 14,2026 jijini Dodoma.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Carolyne Nombo,akiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kufungua  Warsha ya Kujenga Uelewa kwa Wadau  Juu ya  Mkakati na Miongozo ya Kitaifa kuhusu Matumizi ya Teknolojia za Kidijitali kwenye Sekta ya Elimu iliyofanyika leo Januari 14,2026 jijini Dodoma.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Carolyne Nombo,akiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kufungua  Warsha ya Kujenga Uelewa kwa Wadau  Juu ya  Mkakati na Miongozo ya Kitaifa kuhusu Matumizi ya Teknolojia za Kidijitali kwenye Sekta ya Elimu iliyofanyika leo Januari 14,2026 jijini Dodoma.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Carolyne Nombo,akiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kufungua  Warsha ya Kujenga Uelewa kwa Wadau  Juu ya  Mkakati na Miongozo ya Kitaifa kuhusu Matumizi ya Teknolojia za Kidijitali kwenye Sekta ya Elimu iliyofanyika leo Januari 14,2026 jijini Dodoma.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Carolyne Nombo,akiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kufungua  Warsha ya Kujenga Uelewa kwa Wadau  Juu ya  Mkakati na Miongozo ya Kitaifa kuhusu Matumizi ya Teknolojia za Kidijitali kwenye Sekta ya Elimu iliyofanyika leo Januari 14,2026 jijini Dodoma.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Carolyne Nombo,akiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kufungua  Warsha ya Kujenga Uelewa kwa Wadau  Juu ya  Mkakati na Miongozo ya Kitaifa kuhusu Matumizi ya Teknolojia za Kidijitali kwenye Sekta ya Elimu iliyofanyika leo Januari 14,2026 jijini Dodoma.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Carolyne Nombo,akiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kufungua  Warsha ya Kujenga Uelewa kwa Wadau  Juu ya  Mkakati na Miongozo ya Kitaifa kuhusu Matumizi ya Teknolojia za Kidijitali kwenye Sekta ya Elimu iliyofanyika leo Januari 14,2026 jijini Dodoma.

Na.Alex Sonna-DODOMA

Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia imezitaka taasisi zote za elimu nchini kuongeza ubunifu na ufanisi katika ufundishaji na ujifunzaji kupitia matumizi bora, salama, na yenye uwajibikaji wa teknolojia za kidijitali.

Hayo yamesemwa   na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Prof. Carolyne Nombo,wakati wa Warsha ya Kujenga Uelewa kwa Wadau  Juu ya  Mkakati na Miongozo ya Kitaifa kuhusu Matumizi ya Teknolojia za Kidijitali kwenye Sekta ya Elimu iliyofanyika leo Januari 14,2026 jijini Dodoma.

Prof. Nombo amewataka wadau wa elimu kuzingatia mabadiliko ya kidijitali kama hitaji la lazima, huku akisisitiza kwamba ustawi wa baadaye wa Tanzania unategemea nguvu kazi yenye ujuzi wa kidijitali na ubunifu, kama inavyobainishwa katika Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.

“Mkakati huu unalenga kuweka mfumo wa kitaifa wa kuratibu na kuongoza mageuzi ya kidijitali katika ngazi zote za elimu kuanzia shule, vyuo vya ualimu, taasisi za TVET, vyuo vikuu, hadi ujifunzaji wa mtandaoni,” amesema Prof. Nombo.

Aidha, Prof. Nombo amesisitiza umuhimu wa ufundishaji wa kidijitali na ujumuishaji wa TEHAMA, pamoja na uelewa wa Akili Unde  (AI) na stadi za data katika mafunzo ya walimu. Ameeleza kuwa maendeleo endelevu ya kitaaluma kupitia majukwaa ya kidijitali ni muhimu ili kuwawezesha walimu kutumia teknolojia kwa ubunifu na uwajibikaji.

“Nafasi ya walimu ni nguzo kuu ya mageuzi kidijitali. Teknolojia peke yake haiwezi kuleta mabadiliko bila walimu wenye ujuzi na utayari wa kutumia teknolojia za kufundishia na kujifunzia,” amefafanua.

Prof. Nombo pia amesisitiza umuhimu wa Miongozo ya Kitaifa ya Elimu ya Kidijitali na Mwongozo wa Matumizi ya Akili Unde  katika Elimu, ambayo inalenga kuhakikisha matumizi ya teknolojia hayaingilii maadili, ulinzi wa data, ujumuishi, na ubora wa kitaaluma. Vyuo vikuu na taasisi za utafiti wanahimizwa kuongeza ubunifu na utafiti unaozingatia AI na teknolojia nyingine zinazochipuka.

Aidha,ametoa wito kwa taasisi za udhibiti na uthibitishaji ubora kama TCU, NACTVET, COSTECH, TCRA na ICTC kushirikiana na wizara na kutoa elimu ili kuhakikisha mshikamano wa kisera, ulinganifu, na muingiliano wa mifumo sambamba na sera na miongozo ya kitaifa.

Prof. Nombo amewahimiza kutoa  ushirikiano na washirika wa maendeleo na sekta binafsi, wakihimizwa kuunda suluhisho zinazolingana na muktadha wa Tanzania na kuunga mkono ukuaji wa stadi, ubunifu, na uendelevu wa elimu ya kidijitali.


“Usambazaji ni hatua ya kwanza tu. Utekelezaji unahitaji uongozi, uratibu, rasilimali na uwajibikaji. Naomba taasisi zote kuingiza Mkakati wa Kitaifa wa Elimu ya Kidijitali na Miongozo yake katika mipango yao, kuteua waratibu, kutenga rasilimali, na kushiriki kikamilifu katika ufuatiliaji, tathmini na kujifunza kwa pamoja.”amesema Prof. Nombo

Kwa upande wake,Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia (Sekta ya Sayansi), Prof Daniel Mushi, amepongeza hatua ya Serikali kuandaa Mkakati na Miongozo ya Kitaifa ya Matumizi ya Teknolojia za Kidijitali katika Elimu, akisema juhudi hizo zinaweka msingi madhubuti wa mageuzi ya elimu yanayoendana na kasi ya dunia ya sasa.

 Prof Mushi amesema  hatua hiyo inalenga kuboresha ubora wa ufundishaji na ujifunzaji, kukuza ubunifu, na kuwaandaa walimu na wanafunzi kukidhi mahitaji ya zama za kidijitali.

Warsha hiyo ya siku mbili, inayofanyika Januari 14–15, 2026, inawakutanisha wataalam na viongozi mbalimbali wakiwemo makatibu wakuu, wakuu wa vyuo vikuu, viongozi wa VETA, wakuu wa vyuo vya ualimu, taasisi za maendeleo pamoja na wadau wengine wa elimu kutoka sekta za umma na binafsi.

“Huu ni mwendelezo wa jitihada za Serikali kujenga mfumo mmoja na shirikishi wa matumizi ya teknolojia za kidijitali kwenye elimu. Ushiriki wenu unaonesha dhamira ya dhati ya kuijenga Tanzania yenye elimu bora, jumuishi na inayoshindana kikanda na kimataifa,” amesema Prof Mushi.

WAZIRI MAKONDA AAHIDI BILIONI MOJA KWA WAANDISHI WA MITANDAONI

January 13, 2026 Add Comment

 

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Paul Makonda, ameahidi kuomba Serikali kutenga kiasi cha shilingi bilioni moja hadi bilioni mbili kwa ajili ya kuwawezesha waandishi wa habari za mitandaoni nchini kukopeshwa fedha zitakazowawezesha kununua vifaa vya kisasa vya kufanyia kazi, kwa lengo la kuboresha ubora wa maudhui na kuitangaza Tanzania kimataifa.

Waziri Makonda ametoa ahadi hiyo Januari 13, 2026, wakati akizungumza na watumishi wa Wizara hiyo katika Ofisi za Wizara zilizopo Mji wa Serikali Mtumba, sambamba na hafla ya makabidhiano ya Ofisi kati yake na aliyekuwa Waziri wa Wizara hiyo, Mheshimiwa Profesa Palamagamba Kabudi.

Amesema Serikali inatambua mchango mkubwa wa vijana waliojiajiri kupitia vyombo vya habari vya mtandaoni, hususan televisheni za mtandaoni (Online TV) na mitandao ya kijamii, hivyo kuna haja ya kuwawezesha ili wafanye kazi zao kwa viwango vinavyokubalika kimataifa.

“Mungu akituwezesha, vijana wengi wamejiajiri kwenye habari, hasa kupitia televisheni za mtandaoni na mitandao ya kijamii. Tutaomba mamlaka husika, na mtakumbuka Mheshimiwa Rais anapenda sana mitandao ya kijamii, hata alipoingia madarakani alihakikisha vijana wanapata ajira,” amesema Mhe. Makonda.

Ameongeza kuwa atamwomba Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kutenga fedha hizo ili ziwe mikopo kwa waandishi wa mitandaoni, akisisitiza kuwa lengo ni kuboresha ubora wa kazi zao.

“Nitaenda kumlilia Dkt. Samia ili atupatie fedha kiasi cha shilingi bilioni moja hadi bilioni mbili ili tuwakopeshe vijana wa mitandaoni wawe na vifaa vyao wenyewe. Lengo ni kuhakikisha hawarekodi kwa simu pekee, bali wanatumia kamera za kisasa, wanakuwa na kompyuta bora na kutengeneza maudhui ambayo dunia itayaona na kuiona Tanzania katika uzuri wake,” ameeleza.

Katika hatua nyingine, Waziri Makonda amesema Wizara hiyo ina mpango wa kuanzisha Kitengo maalum cha Mawasiliano ya Lugha za Kimataifa kitakachohusika na kuandaa na kusambaza habari za matukio muhimu ya kitaifa kwa vyombo vya habari vya kimataifa.


RAIS SAMIA :MAHAKAMA HURU NI NGUZO YA UTAWALA BORA NA MAENDELEO YA TAIFA

January 13, 2026 Add Comment

 


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amesema hakuna taifa linaloweza kufikia maendeleo endelevu na ustawi wa wananchi wake bila kuwepo kwa usimamizi mzuri wa haki unaosimamiwa na Mahakama huru, yenye uwezo na uadilifu.

Rais Samia ametoa kauli hiyo leo Jumanne Januari 13, 2025 jijini Dodoma wakati akifungua Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Chama cha Mahakimu na Majaji Tanzania (TMJA), unaoongozwa na kauli mbiu “Jukumu la Mahakama Huru Katika Utoaji Haki.”

Dkt. Samia amesema uwepo wa Mahakama huru ni nguzo muhimu ya utawala bora na ni msingi wa upatikanaji wa haki kwa wananchi, akisisitiza kuwa uhuru wa Mahakama lazima uende sambamba na uwajibikaji, uadilifu, nidhamu, utii wa sheria na uzalendo kwa taifa.

“Serikali itaendelea kuulinda na kuheshimu uhuru wa Mahakama, lakini uhuru huo hauna budi kuenda sambamba na uwajibikaji na maadili ya kazi."

Aidha, Rais Samia amesema Dira ya Taifa ya 2025–2050 imejengwa juu ya misingi ya utawala bora, amani, usalama na utulivu, akibainisha kuwa mhimili wa Mahakama una nafasi muhimu katika kujenga taifa lenye haki na ustawi wa kudumu.

Mkutano huo wa TMJA unawakutanisha majaji na mahakimu kutoka maeneo mbalimbali nchini kwa lengo la kujadili masuala ya uboreshaji wa utoaji haki na kuimarisha utendaji wa Mahakama.









RAIS DKT. SAMIA AWAAPISHA VIONGOZI MBALIMBALI ALIOWATEUA IKULU CHAMWINO

RAIS DKT. SAMIA AWAAPISHA VIONGOZI MBALIMBALI ALIOWATEUA IKULU CHAMWINO

January 13, 2026 Add Comment



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akimuapisha Profesa Palamagamba John Adan Kabudi kuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Ikulu (Kazi Maalum) kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Chamwino mkoani Dodoma tarehe 13 Januari,2026.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akimuapisha Mhe. Paul Christian Makonda kuwa Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Chamwino mkoani Dodoma tarehe 13 Januari,2026.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akimuapisha Mhe. Patrobas Paschal Katambi kuwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Chamwino mkoani Dodoma tarehe 13 Januari,2026.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akimuapisha Mhe. Dennis Lazaro Londo kuwa Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Chamwino mkoani Dodoma tarehe 13 Januari,2026.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akimuapisha Mhe. Ayoub Mohamed Mahmoud kuwa Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Chamwino mkoani Dodoma tarehe 13 Januari,2026.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akimuapisha Dkt. Richard Stanslaus Muyungi kuwa Katibu Mkuu, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Chamwino mkoani Dodoma tarehe 13 Januari,2026.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akimuapisha Mhandisi Zena Ahmed Said kuwa Balozi kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Chamwino mkoani Dodoma tarehe 13 Januari,2026.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akimuapisha Mhandisi Cyprian John Luhemeja kuwa Balozi kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Chamwino mkoani Dodoma tarehe 13 Januari,2026.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akimuapisha Ndugu Waziri Rajab Salum kuwa Balozi kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Chamwino mkoani Dodoma tarehe 13 Januari,2026.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akimuapisha Meja Jenerali Mbaraka Naziad Mkeremy kuwa Balozi kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Chamwino mkoani Dodoma tarehe 13 Januari,2026.

Viongozi Wateule wakiapa Kiapo cha Maadili kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Chamwino mkoani Dodoma tarehe 13 Januari,2026

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Balozi Dkt. Emanuel John Nchimbi akiwa pamoja na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba katika hafla ya uapisho wa viongozi mbalimbali, Ikulu Mkoani Dodoma tarehe 13 Januari, 2026

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akizungumza mara baada ya kuwaapisha Viongozi mbalimbali, Ikulu Chamwino Mkoani Dodoma tarehe 13 Januari,2026.