HABARI

SIASA

ELIMU

Recent Posts

TUFANIKISHE PAMOJA YAUNGA MKONO WATOTO YATIMA TEMEKE

January 18, 2026 Add Comment



DAR ES SALAAM .


 Kikundi cha kijamii cha TUFANIKISHE PAMOJA kimeungana na uongozi wa The Valentine Home Centre kilichopo Kata ya Buza, Wilaya ya Temeke, kusaidia watoto yatima na wenye uhitaji.


Kituo hicho, kinachoendeshwa chini ya Kanisa la Anglikana Tanzania, Dayosisi ya Dar es Salaam, kimekuwa kikitoa huduma za malezi, ulinzi na mahitaji muhimu kwa watoto wanaotoka katika mazingira magumu ya kijamii na kiuchumi.

Akizungumza wakati wa tukio hilo, Mwenyekiti wa TUFANIKISHE PAMOJA, Bw. Daudi Tuli Abdallah, alisema msaada huo ni sehemu ya dhamira ya kikundi kurudisha kwa jamii na kusisitiza kuwa jitihada za kuwasaidia watoto zitakuwa endelevu.


> “Tunaamini kuwa maendeleo ya kweli hayawezi kupatikana bila kuwajali watoto walio katika mazingira hatarishi,” alisema.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa kituo hicho, Bw. Gao John Gao, aliipongeza TUFANIKISHE PAMOJA kwa mchango wao, akisema msaada huo haukidhi tu mahitaji ya kimwili bali pia huleta faraja na matumaini mapya kwa watoto.

Katika tukio hilo, TUFANIKISHE PAMOJA ilishiriki pia katika shughuli za kijamii ikiwemo kilimo na upandaji wa miti, pamoja na kutoa msaada wa vyakula, vifaa vya shule na mahitaji mengine ya uendeshaji wa kituo hicho.

The Valentine Home Centre kilianzishwa mwaka 2015 na kinaendelea kutoa huduma kwa watoto yatima na walio katika mazingira hatarishi Temeke na maeneo jirani.

ENDORO WATER FALLS, MAAJABU MENGINE NGORONGORO

ENDORO WATER FALLS, MAAJABU MENGINE NGORONGORO

January 18, 2026 Add Comment






Mbaraka Mwinshehe aliwahi kuimba akiisifia Morogoro na jinsi maji yanavyotiririka kutoka milimani.

Mwinshehe angekuwa hai pengine angefika maporomoko ya maji Endoro (Endoro Waterfalls) kushuhudia maajabu ya maporomoko hayo yaliyopambwa na msitu uliosheheni sauti za ndege na kupambwa na ulinzi wa Wanyamapori mbalimbali.

Mwinshehe angesema ama kweli Mungu anajua kuumba!!! haya ni maporomoko ya aina yake na hapa hupaswi kuwa na mtazamo wa wahenga kwamba Chema chajiuza na kibaya chajitembeza laah hashaa,

Maporomoko haya ya maji Endoro ni eneo zuri lililopo kusini ndani ya Hifadhi ya Ngorongoro, takribani kilomita 6.5 kutoka mji wa Karatu.

Njia ya kuelekea maporomoko haya hupitia msitu na Mapango ya Tembo (Elephants Caves), na huchukua takribani saa 2–3 za matembezi ya wastani.

Mto Endoro hutiririsha maji mwaka mzima kutoka kwenye kingo za korongo, ukilishwa na chemchem za asili kutoka nyanda za juu za Ngorongoro, na kuanguka kwa urefu wa zaidi ya mita 40.

Naaam, njia ya kuelekea kwenye maporomoko hayo inapita sehemu ya msitu wa nyanda za juu kaskazi katika hifadhi ya Ngorongoro ambapo wapenda ndege na wanyamapori wakubwa kama tembo, nyati na nguruwe pori, Simba na wanyama wengine watakapopanda watakuwa na kumbukumbu isiyosahaulika

Hayo ni maporomoko ya maji ya Endoro ukifika huko utatamani uoge maji hayo na hasa ukiyavulia nguo.

WAZIRI AWESO AMTAKA MKANDARASI MKINGA KUFANYA KAZI USIKU NA MCHANA ILI WANANCHI WAPATE MAJI

January 18, 2026 Add Comment
Na Oscar Assenga, MKINGA


WAZIRI wa Maji Jumaa Aweso amemtaka Mkandarasi anayetekeleza mradi wa Maji Mkinga – Horohoro kuhakikisha wanafanya kazi usiku na mchana kuukamilisha kwa wakati ili wananchi waweze kupata huduma ya maji safi na salama.

Aweso aliyasema hayo leo wakati wa halfa ya Mapokezi ya Vitendea kazi (Mabomba) vitakavyotumika katika utekelezaji wa Mradi wa Maji Mkinga-Horohoro ambao unagharimu kiasi cha Bilioni 35.



Halfa hiyo ilihudhuriwa na viongozi mbalimbali akiwemo Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi Tanga Uwasa,Dkt Ally Fungo,Mkurugenzi wa Tanga Uwasa Mhandisi Geofrey Hilly,Meneja wa Ruwasa Mkoa wa Tanga Mhandisi Upendo Lugongo pamoja na watumishi wa Tanga Uwasa,Ruwasa,Viongozi wa CCM na wananchi wa eneo la Manza.

Alisema kutokana na kwamba mradi huo ni muhimu kwa wananchi ambao wanakabiliwa na changamoto ya maji hivyo wahakikishe unakamalika kwa wakati na ujenzi wake uwe tofauti uende na maji katika maeneo yanayolazwa mabomba nao wapate maji.



“Tunajua tuna miradi mingi sana lakini nikuombe Katibu Mkuu utoe fedha ili mradi huo ukamilike kwa wakati ili wana Mkinga waweze kupata huduma ya maji safi na salama”Alisema



“Kama mnakumbuka tulimleta Rais Dkt Samia Suluhu aliweke kuweka jiwe la msingi kukamilika kwake tumuombe Rais aje kuzindua mradi huu wa Mkinga sababu ndio muasisi na ndio aliyweka jiwe la msingi”Alisema

Waziri Aweso aliwataka wafanye kazi hiyo kwa uadilifu na uaminifu ili kuhakikisha hiyo kazi inakamilika na wana Mkinga waweze kupata maji safi na salama



Hata hivyo Waziri huyo alimuahidi Mbunge wa Jimbo la Mkinga Twaha Mwakiojakwamba watafanya kazi kuhakikisha wanakamilisha mradi huo kutokana na kwamba wapo baadhi ya watumishi wanaishi Tanga kutokana na changamoto ya maji wakikamilisha mradi huo watapata maendeleo makubwa.


Alisema maendeleo hayo yatapatikana kwa wana Mkinga na wawekezaji mbalimbali watakwenda kuwekeza hiyo kazi wameibeba na kufanya kazi usiku na mchana ili kuhakikisha mradi unakamilika.



Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Gilbert Kailima alisema wanaishukuru Serikali kutokana na kwamba mradi huo ni mkombozi mkubwa kwa wananchi wa wilaya ya Mkinga na utaondoa adha kubwa ya Maji.


Alisema wanamshukuru Rais kwa kutoa kipaumbele sana katika mradi huo na ndio maana alikuja kuweka jiwe la Msingi katika mradi huo na kuhaidi watajitahidi kusimamia mradi huo kwa karibu kwa kushirikiana na Tanga Uwasa ili utekelezwe kwa wakati ili uanze kufanya kazi kama Rais anavyotamani iwe pamoja nawe.



Aidha alisema katika wilaya hiyo wana miradi mengine mikubwa iliyopo wilayani humo ikiwemo wa Gombero, Mapatano, Muhinduro na Bamba Mwarongo yote ni mikubwa ambayo Serikali chini ya Wizara ya Maji inaendelea kutenga fedha kwa ajili ya utekelezaji wake na ipo katika hatua mbalimbali.


“Kutokana na kwamba umefika leo tunaomba nayo hii miradi waone namna gani inaweza kuisha kwa wakati kama ambavyo wananchi wa Mkinga wanatamani iwe tunaimani sana na utendaji wako na katibu mkuu wa wizara ya Maji “Alisema.


Alitoa wito kwa wananchi wa wilaya hiyo kutoa ushirikiano kwa mkaandarasi ambaye atatoa huduma ya usambazaji wa maji katika mradi huo na kuhakikisha vifaa vyake havihujumiwi badala yake wawe walinzi ili kufanya kazi yake vizuri.

Naye kwa upande wake Mbunge wa Jimbo la Mkinga (CCM) Twaha Mwakioja alisema kwamba katika taifiti iliyofanywa changamoto kubnwa inawakabili zaidi ya wananchi asilimia 80 wamelalamikia hali ya upatikanaji wa maji.



Alisema kwamba mradi huo kabla ya kuanza kutekelezwa wastani wa upatikanaji wa maji katika wilaya ya Mkinga ni asilimia 60 mpaka 69 hivyo wana imani mradi huo utakapokamilika upatinaji wa maji utafika zaidi ya asilimia 88 mradi huo ni mkombozi mkubwa kwao.



Aidha alisema kwamba mradi huo utakakamilika zaidi ya vijiji 37 vinakwenda kupata maji safi na salama ya uhakika na Serikali imeweka fedha nyingi ili kuhakikisha unakamilika ili wananchi waweze kuondokana na adha ya maji.



“Mhe Waziri tunaomba mradi huu kwa maana umesuasua kwa mude mrefu kama unavyotambua upo nyuma zaidi ya miaka miwili na ifikapo julai mradi uwe umekamilika hivyo tunashukuru na wananchi wana mategemeo makubwa sana “Alisema



Mwisho



SERIKALI YATOA TAMKO KIMA CHA CHINI CHA MSHAHARA SEKTA BINAFSI

SERIKALI YATOA TAMKO KIMA CHA CHINI CHA MSHAHARA SEKTA BINAFSI

January 17, 2026 Add Comment

Serikali imetoa onyo kwa waajiri na wafanyakazi wa sekta binafsi kuhakikisha kima cha chini cha mshahara kinatekelezwa ipasavyo.

Hayo yamebainishwa Januari 16, 2025 Jijini Dodoma na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano Mhe. Deus Clement Sangu wakati akitoa ufafanuzi kuhusu Amri ya Kima cha Chini cha Mshahara kwa Sekta Binafsi.

Mhe. Sangu amesema amri ya kima cha chini cha Mshahara kwa Sekta Binafsi imeanza kutumika kuanzia tarehe 1 Januari, 2026 na ilitangazwa kupitia Gazeti la Serikali la tarehe 13 Oktoba, 2025 ambapo kima cha chini cha Mshahara kimeongezeka kwa asilimia 33.4.

Amesema, zoezi la mapitio ya kima cha chini cha Mshahara lilikuwa shirikishi ambapo Serikali kwa kushirikiana na Chama cha Waajiri na Vyama vya Wafanyakazi walikubaliana utekelezaji wake.

“Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan itaendelea kushirikiana na waajiri, wafanyakazi pamoja na Vyama vayo ili kuhakikisha mazingira ya kazi na hali za wafanyakazi zinaboreshwa ili kukuza tija na ustawi wa wafanayakazi,” amesema

Vilevile, Waziri Sangu amewataka Maafisa Kazi pamoja na viongozi wa Vyama vya Wafanyakazi kutoa elimu na ushauri kwa waajiri na wafanyakazi kuhusu utekelezaji wa amri ya kima cha chini cha Mshahara.

Kwa upande mwengine, Mhe. Sangu amesema Ofisi ya Waziri Mkuu itafuatilia utekelezaji wa suala hilo katika maeneo yote ya kazi, hivyo Serikali itawachukulia hatua waajiri ambao hawatatekeleza agizo hilo. Pia, ametoa wito kwa Waajiri na Wafanyakazi wa Sekta Binafsi kuelewa viwango vya kima cha chini vilivyoainishwa katika sekta mbalimbali ikiwemo kilimo, afya, mawasiliano, usafirishaji, hoteli, madini, biashara na viwanda, shule binafsi, huduma za ulinzi binafsi, nishati, uvuvi na huduma ya baharini, michezo na utamaduni pamoja na huduma nyingine.

“Hatutapenda kuona migogoro inatokea katika maeneo ya kazi kwa sababu ya ucheleweshaji wa utekelezaji wa amri ya kima cha chini cha Mshahara,"

WAZIRI MKUU AONGOZA KIKAO KAZI KUHUSU UJENZI WA MIRADI YA BARABARA ZA HARAKA KWA UBIA WA MFUMO WA PPP

January 17, 2026 Add Comment
Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba leo Januari 17, 2026 ameongoza kikao cha kazi kuhusu ujenzi wa miradi ya barabara za haraka (Express Ways) kwa ubia kupitia mfumo wa PPP.

REA YASAINI MIKATABA YA TRILIONI 1.2 KUSAMBAZA UMEME KATIKA VITONGOJI 9,009

January 17, 2026 Add Comment


📌*Wakandarasi wazawa wapewa kipaumbele*


*📌Wakandarasi watakiwa kufanya kazi kwa weledi, ubora na kasi*


*📌Watakiwa kuepukana na vitendo vya rushwa*


*📌Wahimizwa kufuata Sheria, Kanuni na Taratibu za Nchi*


📍Dodoma


Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imesaini mikataba 30 yenye thamani ya shilingi Trilioni 1.2 kwa ajili ya kutekeleza Mradi wa Kusambaza Umeme katika Vitongoji 9,009 utakaonufaisha Wateja wa awali 290,300  katika mikoa 25 ya Tanzania Bara.


Akizungumza katika hafla hiyo leo, Januari 17, 2026 Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi amesema kusaini kwa mikataba ya Mradi huo ni utekelezaji wa maelekezo ya Serikali ya Awamu ya Sita, inayoongozwa na Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuhakikisha ifikapo 2030 vitongoji vyote nchini viwe vimefikishiwa nishati ya umeme.

“Serikali imedhamiria kuhakikisha hakuna Mtanzania atakayebaki bila umeme. Tumekamilisha vijijini na sasa ni zamu ya vitongoji na kwa mikataba hii iliyosainiwa hivi leo ni ushahidi wa dhamira hiyo ya Serikali,” amesema Mhe. Ndejembi.

Amebainisha kuwa kati ya mikataba 30 iliyosainiwa, mikataba 21 ni ya kampuni za Wazawa na mikataba mingine tisa ni ya kampuni kutoka Nje ya nchi ambazo zimesajiliwa hapa nchini.

Serikali ya Rais Samia inatambua Sekta ya Nishati ni injini ya kuchochea maendeleo na amekuwa akitoa fedha nyingi ili kuboresha maisha ya Wananchi wa vijijini.

Ameipongeza REA kwa kuendelea kuwa chombo imara cha Serikali kwa utekelezaji wa Miradi mbalimbali ya kusimamia na kupeleka nishati bora kwa Wananchi na ameendelea kuhakikisha kuwa Taasisi zote za Umma ziunganishwe na umeme zikiwemo shule za msingi, sekondari na vituo vya afya.

Kwa upande wake, Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba amesema Serikali itaendelea na kasi yake ya kusambaza umeme ili kuleta tija inayokusudiwa.

Naye, Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini, Mhe. Subira Mgalu amepongeza jitihada za REA katika kutimiza azma ya Serikali ya kuhakikisha nishati ya umeme inasambaa kote nchini.

"Hongereni REA mnafanya kazi kubwa, leo hii tumefurahi kushuhudia tukio la kihistoria la kusaini mikataba ya kusambaza umeme vitongojini," amepongeza.


Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Bodi ya Nishati Vijijini (REB), Meja Jenerali Mstaafu, Mhe. Balozi Jacob Kingu aliwasisitiza Wakandarasi kuzingatia thamani ya fedha za umma zilizotolewa kutekeleza Miradi sambamba kujifunza kutoka kwenye Miradi iliyokamilika ili kutekeleza kwa ufanisi na kwa ubora unaotakiwa.


Akizungumzia utekelezaji wa Miradi mbalimbali, Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mha. Hassan Saidy amesema REA inatekeleza azma ya Serikali ya kuhakikisha umeme unawafikia Wananchi kwa vitendo.


"Hadi kufikia mwishoni mwa mwaka 2025, Serikali imefanikiwa kufikisha umeme katika vijiji vyote 12,318 vya Tanzania Bara. Hatua hii imeleta mapinduzi ya kweli ya kiuchumi na kijamii, ikichangia kuboresha maisha ya Wananchi wanaoishi vijijini," amefafanua.



Amesema mwaka 2021 kati ya vitongoji 64,359 vilivyopo Tanzania Bara, vitongoji 28,258 pekee vilikuwa na umeme wakati vitongoji 36,101 vilikosa huduma hiyo muhimu.


Amefafanua kuwa kupitia utekelezaji wa Miradi mbalimbali kuanzia mwaka 2021 hadi Desemba 2025, Serikali imeunganisha umeme katika vitongoji 10,745, na hivyo kuongeza idadi ya vitongoji vyenye umeme kufikia 39,003.


Aidha, amesema vitongoji 2,435 vipo katika hatua za utekelezaji wa miradi inayoendelea na hivyo kufanya jumla ya vitongoji 41,438

kuwa tayari vimeunganishwa au vipo katika utekelezaji.


"Utekelezaji wa miradi hii ni utekelezaji wa maelekezo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuhakikisha vitongoji vyote vinasambaziwa umeme," amefafanua.


Amesema Mradi utatekelezwa kwa kipindi cha miaka mitatu na aliwasisitiza Wakandarasi kuhakikisha wanafanya kazi kwa weledi na kujiepusha na vitendo vya rushwa na tabia zisizo na maadili.


"Mradi huu utahusisha ujenzi wa kilomita 13,180 za njia za msongo wa kilovolti 33, kilomita 14,016 za njia za msongo wa volti 415,

pamoja na ujenzi wa mashineumba 9,009 na utatekelezwa kupitia mafungu 30 ambapo mafungu 21 yakitekelezwa na kampuni za ndani, na mafungu 9 na kampuni za nje zilizosajiliwa nchini," amefafanua.


Amebainisha kwamba kwa kuzingatia gharama na idadi ya vitongoji vitakavyofikiwa, Mradi huo, ndiyo mkubwa zaidi kwa usambazaji umeme kuwahi kutekelezwa nchini.


MWISHO!!!

KAMATI YA BUNGE YAPONGEZA UTENDAJI KAZI WA BRELA

KAMATI YA BUNGE YAPONGEZA UTENDAJI KAZI WA BRELA

January 17, 2026 Add Comment

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara, Kilimo na Mifugo imeipongeza Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) kwa utendaji kazi mzuri, maendeleo na mabadiliko makubwa yanayoonekana katika utoaji wa huduma kwa wananchi.

Pongezi hizo zimetolewa leo tarehe 16 Januari, 2026, katika Ofisi za Bunge jijini Dodoma na Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Mhe. Deodatus Mwanyika (Mb), baada ya Kamati kupokea Taarifa ya Muundo na Majukumu ya BRELA iliyowasilishwa na Afisa Mtendaji Mkuu wa BRELA, Bw. Godfrey Nyaisa.

Mhe. Mwanyika amesema kuwa, licha ya kazi nzuri inayoendelea kufanywa na BRELA, bado kuna changamoto ya wafanyabiashara na wamiliki wa kampuni wengi kutohuisha taarifa za kampuni zao kupitia mfumo wa BRELA. Ameeleza kuwa tatizo hilo ni kubwa, lakini wananchi wengi hawalitambui ipasavyo.

“Hili tatizo ni kubwa lakini wengi hawalielewi; wengi wana kampuni lakini hawajahuisha taarifa za kampuni hizo,” amesema Mhe. Mwanyika.

Kutokana na hali hiyo, Mhe. Mwanyika ameielekeza Wizara ya Viwanda na Biashara kufanya utafiti na kutathmini namna ya kuboresha mfumo wa uhuishaji wa taarifa za biashara na kampuni, ili kuja na mfumo wezeshi, unaoongeza ufanisi na kuharakisha utoaji wa huduma.

Aidha, Mwenyekiti huyo amesisitiza umuhimu wa kuhuisha taarifa za biashara na kampuni, akitoa wito kwa wafanyabiashara kuchukua hatua hiyo kwa hiari na kwa wakati.

“Kuhuisha taarifa ni jambo jema, na ni muhimu tukalifanye,” amesisitiza.

Kwa upande wake, Afisa Mtendaji Mkuu wa BRELA, Bw. Godfrey Nyaisa, amesema kuwa Wakala itaendelea kutoa elimu kwa Waheshimiwa Wabunge kupitia Kamati hiyo ili kuwajengea uelewa mpana kuhusu majukumu ya BRELA pamoja na mifumo ya kidijitali inayotumika katika utoaji wa huduma.

Bw. Nyaisa ameeleza kuwa, pamoja na mafanikio yaliyopatikana, uelewa mdogo wa wananchi kuhusu matumizi ya mifumo ya kidijitali bado ni miongoni mwa changamoto zinazokwamisha urasimishaji wa biashara na utoaji wa leseni.

Amefafanua kuwa mfumo wa BRELA ni rafiki kwa mtumiaji na unajieleza wenyewe, hivyo kumwezesha mwananchi kujisajili moja kwa moja bila usumbufu.

“Mfumo wa BRELA ni rafiki kwa mtumiaji na unajieleza wenyewe, hivyo humwezesha mtu kuingia moja kwa moja na kusajili kampuni yake bila usumbufu,” amesema Bw. Nyaisa.

Ameongeza kuwa BRELA inaendelea kutoa elimu kwa wananchi ili kuwahamasisha kufahamu kuwa mchakato wa usajili wa biashara, kampuni na utoaji wa leseni si mgumu kama inavyodhaniwa.

Amebainisha kuwa katika mapitio ya sheria yanayoendelea, BRELA inapendekeza kutambuliwa rasmi kwa Mawakala wa Usajili wa Kampuni, ili kusaidia wananchi wanaokutana na changamoto wakati wa usajili.

“Lengo ni kuhakikisha mwananchi akikwama, anapata msaada kutoka kwa watu wanaotambulika na kuaminika,” amesisitiza Bw. Nyaisa.

CCM YAKEMEA SIASA ZA JAZBA, CHUKI NA MIGAWANYIKO

CCM YAKEMEA SIASA ZA JAZBA, CHUKI NA MIGAWANYIKO

January 17, 2026 Add Comment

Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa CCM, Kenani Kihongosi, akizungumza na waandishi wa habari leo Januari 17,2026  jijini Dodoma

Na.Alex Sonna-DODOMA

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) kimempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan, kwa kukutana na Mabalozi wa Tanzania Januari 15, 2026 katika kikao cha ufunguzi wa mwaka, hatua iliyotajwa kuongeza hadhi ya nchi kimataifa na kuonyesha mwelekeo chanya wa diplomasia ya taifa.

Pongezi hizo zimetolewa leo Januari  17, 2026 na Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa CCM, Kenani Kihongosi, wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini Dodoma.
 "Mkutano huo kati ya Rais Samia na mabalozi umeonyesha dhamira ya Serikali kuendelea kuimarisha ushirikiano wa kimataifa huku ukaleta taswira nzuri ya Tanzania katika medani za diplomasia na uchumi."amesema Kihongosi
Aidha, Kihongosi ametoa pongezi kwa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kwa kuimarisha mifumo ya ukusanyaji kodi, ambapo makusanyo yamefikia shilingi trilioni 3.1 na mwezi Desemba pekee kuvuka zaidi ya shilingi trilioni 4, akisema hatua hiyo inaonyesha ufanisi mkubwa katika usimamizi wa mapato ya Serikali.
Katika masuala ya kijamii, Kihongosi amesema Serikali inaendelea na maandalizi ya uzinduzi wa Bima ya Afya kwa Wote, sambamba na kuchukua hatua za kuondoa utaratibu wa kuzuiliwa kwa maiti pale wagonjwa wanaposhindwa kulipia gharama za matibabu.
Ameongeza kuwa Serikali imetekeleza ahadi ya ajira kwa kutoa zaidi ya ajira 12,000 katika sekta mbalimbali, huku mpango wa kutoa shilingi bilioni 2 kwa ajili ya kuwawezesha vijana kiuchumi ukiendelea kutekelezwa.
Katika hatua nyingine Kihongosi,ametoa onyo  vikali dhidi ya kauli na mienendo inayopotosha ukweli, kuchafua historia ya taifa na kuhujumu amani kwa maslahi binafsi, kikisisitiza kuwa hakitaruhusu siasa za jazba, chuki na migawanyiko.
Kihongosi amesema CCM ni chama kinachojengwa juu ya misingi ya maridhiano umoja na kuheshimiana hivyo hakitovumilia juhudi zozote za kupotosha ukweli au kueneza chuki zisizo na tija kwa Taifa. 
Amesema CCM inamheshimu Waziri Mkuu na Jaji Mkuu Mstaafu Joseph Warioba kwa mchango wake mkubwa alioutoa kwa Taifa lakini ikamtaka kuendelea kufurahia maisha ya kustaafu kwa utulivu bila kutoa malalamiko. 
"Ni jambo la kawaida kwa viongozi waliotumikia Taifa kuheshimiwa lakini wastaafu wanapaswa kutoa nafasi kwa viongozi waliopo kuendelea na majukumu yao Kihongosi, "amesema
Ameongeza kuwa "Licha ya Jaji Warioba kukutana  na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan bado alionekana mitandaoni akitoa kauli zenye malalamiko hali aliyoitaja kuwa haina tija kwa maendeleo ya Taifa, ". 
Kuhusu ziara ya kitaifa Kihongosi amesema kuanzia Januari 18 2026 ataanza ziara ya kichama itakayohusisha mikoa yote ya Tanzania kuanzia mkoani Singida Ziara hiyo inalenga kusikiliza na kutatua kero za wananchi kuimarisha chama na kufuatilia utekelezaji wa ahadi za Rais Samia
" Ziara hii ni jukwaa la wananchi kama kuna anayehisi kuonewa au kunyanyaswa tunawakaribisha waje ili tusikilize na kutatua changamoto zao, "Kihongosi 

DKT. MAULID AKUTANA NA KUFANYA MAZUNGUMZO NA DC MAGOTI

January 17, 2026 Add Comment
Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe, Mheshimiwa Petro Magoti akiwa kwenye picha ya pamoja na Mtendaji Mkuu wa ADEM, Dkt. Maulid J. Maulid, Katibu Tawala wa Wilaya ya Kisarawe pamoja na Mwakilishi wa Madiwani wa Mkoa wa Pwani, mara baada ya kufunga mafunzo kwa Waheshimiwa Madiwani.