HABARI

SIASA

ELIMU

Recent Posts

VIJIJI VINNE MBULU VYAANZA KUNUFAIKA NA MRADI WA MAJI WA BILIONI 41

March 13, 2026 Add Comment

Wananchi na wakazi wa Hydom wilayani Mbulu mkoa wa Manyara wamemshukuru Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kufuatia Wizara ya Maji kupitia RUWASA kutekeleza mradi mkubwa wa Majisafi ya bomba wenye thamani ya zaidi ya shilingi bilioni 41 na tayari vijiji vinne vimeshaanza kunufaika na mradi huo.

Wametoa pongezi hizo wakati wa ziara ya kamati ya kudumu ya Bunge ya Maji na Mazingira alipotembelea na kukagua mradi huo ikiongozwa na Mwemyekiti wake Mhe. Jackson Kiswaga (Mb) katika eneo la Hydom lilipo tangi kubwa la ujazo wa lita 2,000,000 la mradi huo.

Mkurugenzi Mkuu wa RUWASA Mha. Wolta Kirita aliieleza Kamati hiyo kuwa tayari wananchi zaidi 800 wameshasajiliwa na kupatiwa kadi za malipo kabla ya matumizi kwani mradi huo unaenda sambamba na ufungaji wa dira za maji za malipo ya kabla, ambapo mwananchi anaweza kuchota maji kwenye kituo muda wowote anapokuwa anahitaji huduma hiyo.

Mkurugenzi Mkuu Kirita alisema mradi huo unatarajiwa kukamilika Novemba 2027.

Kwa mujibu wa Meneja wa RUWASA mkoa wa Manyara Mha. James Kionaumela alisema mradi huo umeshaanza kutoa huduma katika vijiji vinne na ukikamilika utahudumia zaidi ya wakazi 100,000 wa eneo hilo.

Naye Mkuu wa wilaya ya Mbulu Mhe. Michael Semindu akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Manyara Mhe. Queen Sendiga alisema kwa sasa wananchi wa wilaya hiyo wanapata maji kwa saa 12 kwa siku huku akiipongeza RUWASA kwa kazi nzuri katika kutekeleza mradi huo.








KAIMU KAMISHNA WA UHIFADHI TAWA AFUNGUA KIKAO KAZI CHA MAANDALIZI YA BAJETI YA TAWA

KAIMU KAMISHNA WA UHIFADHI TAWA AFUNGUA KIKAO KAZI CHA MAANDALIZI YA BAJETI YA TAWA

March 13, 2026 Add Comment

Na. Joyce Ndunguru, Dodoma.

Kaimu Kamishna wa Uhifadhi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA), Mlage Yussuf Kabange amefungua rasmi kikao kazi cha maandalizi ya bajeti ya TAWA kwa mwaka wa fedha 2026/2027.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa kikao kazi kilichofanyika Machi 13,2026, Jijini Dodoma, Kamishna Kabange amesema Bajeti ya mwaka 2026/27 ni ya kipekee kwa kuzingatia kuwa ni bajeti ya kwanza katika kuchangia utekelezaji wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi 2025 pamoja na Dira ya maendeleo ya Taifa 2050.

“Pia bajeti hii imezingatia kutafsiri Hotuba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan wakati wa kuzindua Bunge la 13, Mkakati wa kuongeza mapato wa TAWA na ni bajeti ya kwanza tangu Bodi ya Nne ya Wakurugenzi ya TAWA iteuliwe”, amesema Kamishna Kabange.

Kamishna Kabange ameongeza kuwa katika bajeti hii TAWA itajielekeza katika vipaumbele mbalimbali ikiwemo kuimarisha ulinzi na usimamizi wa Rasilimali wanyamapori na malikale.

Pia, Kuimarisha shughuli za utalii pamoja na kuongeza idadi ya watalii kwa kuboresha miundombinu ya utalii pamoja na kuongeza vyanzo vipya vya mapato.

Kadhalika, Utatuzi wa migogoro ya mipaka na udhibiti wa wanyamapori wakali na waharibifu pamoja na Kuimarisha mazingira ya utendaji kazi kwa watumishi na uwezo wa Mamlaka katika kutoa huduma.

Vilevile , Kamishna Kabange amewapongeza Makamanda na Askari ambao wamekuwa mstari wa mbele kusimamia utekelezaji wa malengo ya Mamlaka. Aidha, amewaelekeza Makamanda wa vituo kuhakikisha Usimamizi madhubuti wa vitendea kazi yakiwemo magari.

Aidha, Kamishna Kabange amewaelekeza Makamanda kuendelea na utangazaji wa vivutio vya utalii pamoja na kubuni mazao mapya ya utalii.

“Nitoe rai kwenu kuendelea kuwa wabunifu na kutangaza maeneo mnayoyasimamia,” amesema Kamishna Kabange 

Sambamba na hilo, Kamishna Kabange amewaelekeza Makamanda kuendelea kusimamia askari kutekeleza majukumu yao kwa weledi na kwa kuzingatia haki, sheria na miongozo iliyowekwa.

Kikao kazi cha maandalizi ya bajeti kimehudhuriwa na viongozi wa TAWA kwa ngazi ya Makao Makuu, Kanda na Vituo.

KAMATI YA BUNGE YARIDHISHWA NA MABORESHO YA BANDARI YA TANGA

March 13, 2026 Add Comment





Na Oscar Assenga,TANGA

Kamati ya kudumu ya Bunge ya miundombinu leo imefanya ziara ya kutembelea Bandari ya Tanga huku ikiridhinshwa na uboreshaji wa miundombinu katika Bandari ya Tanga hatua inayoonesha mabadiliko ya kiutendaji ikiwemo ongezeko la shehena za mizigo.

Hayo yalisemwa leo na Mwenyekiti wa Kamati hiyo Profesa Joyce Ndalichako wakati wa ziara hiyo katika Bandari ya Tanga ambapo alisema maono ya Serikali yameleta mapinduzi katika Bandari ya Tanga na wao kama wasimamizi wataendelea kuisimamia Serikali katika utekelezaji wa mradi huo



Uboresho huo wa Bandari ya Tanga umepelekea kuvuka lengo la upokeaji wa shehena za mizigo kutoka mataifa mbalimbali kutoka tani 137,000 mwezi Oktoba hadi kufikia tani zaidi ya 200,000 mwezi Novemba mwaka 2025.



Alisema kutokana na maboresho hayo wana kila sababu ya kuipongeza Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Raisi Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa uboreshaji wa Bandari ya Tanga hatua inayochagiza kuinua uchumi wa mkoa wa Tanga kwa kiasi kikubwa.




Profesa Ndalichako alisema kwamba uwekezaji huo wa shilingi bilioni 429.1 uliofanywa na Serikali katika Bandari ya Tanga umewezesha uchimbwaji wa kina na ujenzi wa gati hatua iliyoiongezea ufanisi wa utendaji na hivyo kuwezesha meli kubwa kutia nanga na kurahisisha shughuli za upakiaji na upakuaji wa mizigo.

Aliongeza Serikali ina maono ya kuunganisha Bandari na reli ambapo mpango uliopo ni kujenga reli ya kisasa ya SGR kutoka Tanga hadi Musoma hatua itakayochochea maendeleo ya mkoa wa Tanga na kuzalisha ajira kwa vijana.



Kamati ya kudumu ya Bunge ya miundombinu imeipongeza Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Raisi Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa uboreshaji wa Bandari ya Tanga hatua inayochagiza kuinua uchumi wa mkoa wa Tanga kwa kiasi kikubwa.

Uwekezaji wa shilingi bilioni 429.1 uliofanywa na Serikali katika Bandari ya Tanga zimewezesha uchimbwaji wa kina na ujenzi wa gati na hatimaye kuleta ufanisi wa utendaji katika Bandari hiyo hatua inayowezesha Meli kubwa kutia nanga na kurahisusha shughuli za upakiaji na upakuaji wa mizigo.



Aidha katika hatua nyengine Profesa Ndalichako amesema Serikali ina maono ya kuunganisha Bandari na reli ambapo mpango uliopo ni kujenga reli ya kisasa ya SGR kutoka Tanga hadi Musoma hatua itakayochagiza maendeleo ya mkoa wa Tanga hususani kwa vijana kupata ajira.



Kwa upande wake, Naibu Waziri wa Uchukuzi, David Kihenzile, alisema Serikali inaendelea na mpango wa kuunganisha bandari hiyo na mtandao wa reli wa kilomita 248 (Tanga–Mruazi–Ruvu) na hatimaye kufika Arusha.



Alisema pamoja na kuwa na reli ya SGR kupitia Minjingu na Engaruka hadi Musoma itakuwa kiunganishi muhimu cha kiuchumi.

Naye kwa upande wake ,Meneja wa Bandari ya Tanga, Salehe Mbega alisema maboresho hayo yameongeza kina cha maji kufikia mita 12 hali inayoruhusu meli kubwa zenye urefu wa hadi mita 200 kutia nanga gatini tofauti na hapo awali.


REA YAANZA USAMBAZAJI WA MAJIKO BANIFU 8,424 KIGOMA

March 13, 2026 Add Comment







Na Mwandishi Wetu Kibondo - Kigoma


Wakala wa Nishati Vijijini imeanza utekelezaji wa mpango mkakati wa kitaifa wa nishati safi ya kupikia ili kufikia lengo la zaidi ya asilimia themanini 80% ya watanzania ifikapo mwaka 2034 wawe wanatumia nishati safi ya kupikia nishati ambayo ni salama kwa mtumiaji na rafiki kwa mazingira.

Akizungumza wakati wa ugawaji wa majiko katika Wilaya Kibondo mkoani Kigoma Mhandisi Ramadhan Mganga amesema kuwa Wakala ya Nishati Vijijini-REA mkoa huo umeanza usambazaji wa majiko banifu 8,424.

Mhandisi Mganga amesema kuwa mradi huo unahusisha usambazaji wa majiko banifu yanayotumia kuni na mkaa kidogo ili kupunguza matumizi ya vyanzo hivyo vya nishati pamoja na athari za moshi zitokanazo na matumizi katika majiko ya kawaida. Katika mkakati huo Wakala wa Nishati Vijijini umeandaa mpango wa uuzwaji wa majiko banifu 200,000 kwa bei ya ruzuku yenye ufanisi mkubwa katika utumiaji wake.

"Mikataba hii imesainiwa tarehe 09 Mei, 2025 na itatekelezwa ndani ya miezi 15. Gharama ya mradi kwa mkoa wa Kigoma ni TZS 429,539,760.00 ambapo Serikali imeroa ruzuku ya TZS 365,108,796.00," Amesema Mha. Mganga

Mtoa huduma ni Envotec Services ambapo jumla ya majiko banifu 8,424 yatauzwa kwa wananchi kwa bei ya ruzuku. Gharama ya jiko moja ni TZS 50,990 lakini serikali imetoa ruzuku ya asilimia 85.

Akizindua rasmi majiko hayo, Mkuu wa Wilaya ya Kibondo, Mhe. Aggrey Magwaza, amesema majiko hayo yaliyotolewa kwa awamu hii yataleta manufaa makubwa kwa wananchi na kusisitiza kuwa waliopata fursa ya kuyapata wayatumie kwa matumizi ya nyumbani badala ya kuyafanya biashara.

"Wilaya ya kibondo itanufaika na majiko banifu 1404 ambapo kila kaya itanufaika kwa kununua jiko moja kwa gharama ya shiringi 7,649 punguzo la asilimia 85% kutoka kwenye bei harisia ya shilingi 50,990," Amesema DC Magwaza.

Kwa upande wao wananchi ambao wamenufaika na majiko hayo wamempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kuamua kutoa majiko bunifu kwa bei ya ruzuku ambayo itawanufaisha wananchi wote.






ELIMU YA UVUNAJI WA MAJI YA MVUA YAWAFIKIA WENYE ULEMAVU SINGIDA

ELIMU YA UVUNAJI WA MAJI YA MVUA YAWAFIKIA WENYE ULEMAVU SINGIDA

March 13, 2026 Add Comment

Mhandisi wa Maji na Usafi wa Mazingira wa EWURA Kanda ya Kati, Saidi Mwangalo,akiwasilisha mada kuhusu uvunaji na uhifadhi wa maji ya mvua kwa wadau mbalimbali mkoani Singida,wakati wa semina iliyotolewa leo Machi 13,2026 kwa wanachama wa Chama cha Watu Wenye Ulemavu, viongozi kutoka wilaya ya Singida pamoja na wajumbe wa Kamati ya Ushauri ya Watumiaji wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA CCC).

Na.Mwandishi Wetu-SINGIDA

Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) imetoa elimu ya uvunaji na uhifadhi wa maji ya mvua kwa wadau mbalimbali mkoani Singida, wakiwemo wanachama wa Chama cha Watu Wenye Ulemavu, viongozi kutoka wilaya ya Singida pamoja na wajumbe wa Kamati ya Ushauri ya Watumiaji wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA CCC), leo tarehe 13 Machi 2026.

Akiwasilisha mada kuhusu uvunaji wa maji ya mvua, Mhandisi wa Maji na Usafi wa Mazingira wa EWURA Kanda ya Kati, Saidi Mwangalo, alieleza mbinu mbalimbali za kuvuna na kuhifadhi maji ya mvua ili yaweze kutumika kwa muda mrefu na bila kuharibika.

Alisema uvunaji wa maji ya mvua ni njia muhimu ya kuongeza upatikanaji wa maji, hususan wakati wa ukame au pale kunapotokea changamoto katika huduma ya maji. Alisisitiza kuwa mvua ni rasilimali inayopatikana bure, hivyo ni muhimu kutunza na kutumia kila tone la maji ipasavyo ili kukabiliana na changamoto za upatikanaji wa maji.

Washiriki pia walipatiwa elimu na Ofisa Huduma kwa Wateja, Bw. Juma Singano, kuhusu utaratibu wa kushughulikia malalamiko na kutatua migogoro kati ya watoa huduma na wateja wa sekta zinazodhibitiwa na EWURA

Mada nyingine zilizowasilishwa ni pamoja na utaratibu wa utoaji vibali vya ujenzi wa vituo vya mafuta mijini na vijijini, iliyowasilishwa na Mhandisi wa Petroli Kanda ya Kati, Bi. Roselyne Mndeme, pamoja na matumizi sahihi na salama ya gesi ya kupikia majumbani, iliyowasilishwa na Ofisa Uhusiano Mwandamizi wa EWURA, Bi. Tobietha Makafu.

Akitoa neno la shukrani baada ya semina hiyo, Mkurugenzi wa Chama cha PPD, Bw. Ramadhan Mrisho aliishukuru EWURA kwa kuwafikia wanachama wao kwa elimu hiyo muhimu.

Pia aliishauri EWURA kuendelea kutoa elimu kwa jamii, hususan katika maeneo yenye changamoto ya upatikanaji wa maji, ili wananchi waweze kutumia misimu ya mvua kuvuna na kuhifadhi maji kwa matumizi ya baadaye.

Mhandisi wa Maji na Usafi wa Mazingira wa EWURA Kanda ya Kati, Saidi Mwangalo,akiwasilisha mada kuhusu uvunaji na uhifadhi wa maji ya mvua kwa wadau mbalimbali mkoani Singida,wakati wa semina iliyotolewa leo Machi 13,2026 kwa wanachama wa Chama cha Watu Wenye Ulemavu, viongozi kutoka wilaya ya Singida pamoja na wajumbe wa Kamati ya Ushauri ya Watumiaji wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA CCC).

 Ofisa Huduma kwa Wateja, Bw. Juma Singano, akitoa mada kuhusu utaratibu wa kushughulikia malalamiko na kutatua migogoro kati ya watoa huduma na wateja wa sekta zinazodhibitiwa na EWURA wakati wa semina iliyotolewa leo Machi 13,2026 kwa wanachama wa Chama cha Watu Wenye Ulemavu, viongozi kutoka wilaya ya Singida pamoja na wajumbe wa Kamati ya Ushauri ya Watumiaji wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA CCC).

 

Mhandisi wa Petroli Kanda ya Kati, Bi. Roselyne Mndeme,akitoa mada wakati wa semina iliyotolewa na EWURA leo Machi 13,2026 kwa wanachama wa Chama cha Watu Wenye Ulemavu, viongozi kutoka wilaya ya Singida pamoja na wajumbe wa Kamati ya Ushauri ya Watumiaji wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA CCC) iliyofanyika Mkoani Singida.

Ofisa Uhusiano Mwandamizi EWURA, Bi. Tobietha Makafu,akitoa mada  wakati wa semina iliyotolewa na EWURA leo Machi 13,2026 kwa wanachama wa Chama cha Watu Wenye Ulemavu, viongozi kutoka wilaya ya Singida pamoja na wajumbe wa Kamati ya Ushauri ya Watumiaji wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA CCC) iliyofanyika Mkoani Singida.

Mkurugenzi wa Chama cha Walemavu (PPD), Bw. Ramadhan Mrisho,akitoa neno la shukrani baada ya kupatiwa elimu na EWURA  kuhusu uvunaji na uhifadhi wa maji ya mvua kwa wadau mbalimbali mkoani Singida, iliyotolewa leo Machi 13,2026 kwa wanachama wa Chama cha Watu Wenye Ulemavu, viongozi kutoka wilaya ya Singida pamoja na wajumbe wa Kamati ya Ushauri ya Watumiaji wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA CCC).

Sehemu ya washiriki wakifuatilia mada mbalimbali wakati wa semina iliyotolewa na EWURA  kuhusu uvunaji na uhifadhi wa maji ya mvua kwa wadau mbalimbali mkoani Singida.

Sehemu ya washiriki wakifuatilia mada mbalimbali wakati wa semina iliyotolewa na EWURA  kuhusu uvunaji na uhifadhi wa maji ya mvua kwa wadau mbalimbali mkoani Singida.

Sehemu ya washiriki wakifuatilia mada mbalimbali wakati wa semina iliyotolewa na EWURA  kuhusu uvunaji na uhifadhi wa maji ya mvua kwa wadau mbalimbali mkoani Singida.

Sehemu ya washiriki wakifuatilia mada mbalimbali wakati wa semina iliyotolewa na EWURA  kuhusu uvunaji na uhifadhi wa maji ya mvua kwa wadau mbalimbali mkoani Singida.