HABARI ZETU
Loading...

HABARI

SIASA

ELIMU

Recent Posts

MADIWANI WA MPANDA NA NSIMBO WAIPONGEZA SERIKALI KWA UWEKEZAJI MKUBWA KATIKA KITUO CHA KUFUA UMEME CHA JULIUS NYERERE

MADIWANI WA MPANDA NA NSIMBO WAIPONGEZA SERIKALI KWA UWEKEZAJI MKUBWA KATIKA KITUO CHA KUFUA UMEME CHA JULIUS NYERERE

June 22, 2026 Add Comment





Na Mwandishi wetu,

Rufiji – Pwani

Madiwani wa Halmashauri za Wilaya za Mpanda na Nsimbo mkoani Katavi, wakiongozana na baadhi ya wabunge na viongozi wengine, wamepongeza uwekezaji mkubwa uliofanywa na Serikali katika Kituo cha Kufua Umeme cha Julius Nyerere (JNHPP) baada ya kujionea kwa karibu uendeshaji wa kituo hicho na mchango wake katika maendeleo ya sekta ya nishati nchini.

Viongozi hao walitembelea kituo hicho tarehe 20 Juni 2026 kwa lengo la kujionea uwekezaji mkubwa uliofanywa na Serikali, kufahamu namna kituo kinavyoendeshwa pamoja na kupata uelewa wa mchango wake katika kuimarisha upatikanaji wa umeme nchini. Ziara hiyo ilihusisha madiwani 22 pamoja na baadhi ya wabunge na viongozi wengine kutoka Mkoa wa Katavi.

Akizungumza baada ya ziara hiyo, Mstahiki Meya wa Manispaa ya Mpanda, Charles Philipo, aliishukuru Serikali kwa juhudi kubwa inazoendelea kufanya katika kuimarisha sekta ya nishati na kuipongeza TANESCO kwa kuwapatia viongozi hao fursa ya kujionea kituo hicho.

“Tunaishukuru Serikali yetu kwa namna ambavyo imejikita kutatua changamoto ya umeme. Nipende kuwashukuru TANESCO kwa niaba ya waheshimiwa madiwani wa Mpanda na Nsimbo kwa kuona namna ya sisi kuja hapa na kujionea kituo hiki,” alisema Philipo.

Kwa upande wake, Mbunge wa Jimbo la Nsimbo, Mhe. Anna Mpembe, alisema ameoneshwa kuvutiwa na ukubwa wa kituo hicho na kiwango cha uwekezaji kilichowekwa katika kuhakikisha Tanzania inakuwa na umeme wa kutosha kwa maendeleo ya taifa.

“Leo tunaona maajabu na miujiza kupitia Kituo cha Julius Nyerere. Jinsi kilivyojengwa ni kitu cha thamani kubwa sana katika nchi yetu ya Tanzania,” alisema Mhe. Mpembe.

Naye Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Mpanda, Joseph Lwamba, alisema maendeleo ya sekta ya umeme yameendelea kubadilisha maisha ya wananchi kwa kuongeza fursa za kiuchumi na kijamii katika maeneo mbalimbali ya Mkoa wa Katavi.

“Namshukuru Mwenyezi Mungu kwamba katika wilaya yetu ya Mpanda karibu vijiji vyote sasa vina umeme. Wananchi wanaweza kufanya shughuli zao za maendeleo kupitia umeme huu,” alisema Lwamba.

Akielezea lengo la ziara hiyo, Mhandisi wa Usafirishaji Umeme Mkoa wa Katavi, Victor Ngw’igulu, alisema viongozi hao wameletwa katika kituo hicho ili kujionea kwa macho maendeleo makubwa yanayofanywa na Serikali kupitia sekta ya nishati na kuwa mabalozi wa kueleza wananchi mafanikio hayo.

“Wananchi wanapaswa kujua nini kinafanywa na TANESCO kupitia Wizara ya Nishati na hii ni sehemu nzuri ya kuona maendeleo yanayofanywa katika nchi yao. Kupitia Mkoa wa Katavi tumewaleta waheshimiwa hawa ili wajionee kwa macho kile walichokuwa wanakisikia kuhusu Kituo cha Kufua Umeme cha Julius Nyerere, namna kinavyofanya kazi na kuchangia katika uchumi wa taifa,” alisema Ngw’igulu.

Kwa upande wake, Kaimu Mkurugenzi wa Kituo cha Kufua Umeme cha Julius Nyerere, Mhandisi Elinainyi Kalalu, alisema ujio wa viongozi hao una mchango mkubwa katika kuendelea kuhamasisha uelewa wa wananchi kuhusu umuhimu wa kituo hicho na nafasi yake katika maendeleo ya taifa.

“Tumewapitisha katika maeneo mbalimbali na kuwaonyesha miundombinu inayotumika katika uzalishaji wa umeme. Tuna imani kwamba wataichukulia ziara hii kama chachu ya maendeleo na watakuwa wajumbe wazuri huko waendako, hasa katika kuelezea mchango wa Kituo cha Kufua Umeme cha Julius Nyerere katika maendeleo ya taifa,” alisema Kalalu.

Ziara hiyo imewapa madiwani wa Mpanda na Nsimbo pamoja na viongozi wengine kutoka Mkoa wa Katavi fursa ya kujionea kwa karibu uwekezaji mkubwa uliofanywa na Serikali katika sekta ya nishati kupitia Kituo cha Kufua Umeme cha Julius Nyerere. Aidha, viongozi hao wameeleza kuridhishwa na hatua zilizofikiwa na kuahidi kuendelea kuhamasisha wananchi kutambua mchango wa kituo hicho katika kuimarisha upatikanaji wa umeme na kuchochea maendeleo ya kiuchumi na kijamii nchini.

MWENGE WA UHURU KUPITIA MIRADI YA SH.BILIONI 1.5 MUHEZA

June 22, 2026 Add Comment


Na Oscar Assenga, Muheza

MWENGE wa Uhuru 2026 unatarajiwa kuingia Wilaya ya Muheza kesho saa 4:00 asubuhi na kukimbizwa kupitia miradi saba ya maendeleo yenye thamani ya zaidi ya Sh bilioni 1.5, huku viongozi wa wilaya wakitoa wito kwa wananchi kujitokeza kwa wingi kushiriki mbio hizo.

Mwenge huo utapokewa katika eneo la Kilapura, Kijiji cha Muungano, Kata ya Mlingano na utapitia miradi mbalimbali ya kijamii na kiuchumi inayolenga kuboresha maisha ya wananchi wa wilaya hiyo.

Akizungumza kuhusu maandalizi ya ujio wa Mwenge huo, Mkuu wa wilaya ya Muheza Ayoub Sebabili alisema kati ya miradi saba itakayopitiwa, miwili itazinduliwa rasmi, miwili itawekewa mawe ya msingi na mitatu itatembelewa na kukaguliwa.

Alisema mradi wa kwanza ni Zahanati ya Muungano, ikifuatiwa na mradi wa maji wa Kijiji cha Magoda unaolenga kuongeza upatikanaji wa huduma ya maji safi na salama kwa wananchi.

Pia Mwenge wa Uhuru utazindua mabweni ya Shule ya Sekondari Mangenya pamoja na kuweka jiwe la msingi katika darasa jipya linalojengwa kwa ajili ya maandalizi ya kupokea wanafunzi wa kidato cha kwanza mwaka 2027.

Mbali na miradi hiyo, viongozi wa mbio za Mwenge watatembelea Klabu ya Wapinga Rushwa ya wanafunzi ikiwa ni sehemu ya kuhamasisha maadili mema na mapambano dhidi ya vitendo vya rushwa katika jamii.

Katika kuunga mkono juhudi za serikali za matumizi ya nishati safi, Mwenge wa Uhuru pia utashuhudia utoaji wa mitungi ya gesi kwa wananchi ili kuhamasisha matumizi ya nishati mbadala na kulinda mazingira.

Ratiba hiyo itahusisha pia uzinduzi wa boksi kalavati katika Kijiji cha Tongwe, Kata ya Tongwe, kabla ya kutembelea kikundi cha vijana wa Kijiji cha Magila, Kata ya Genge, waliopata mkopo wa asilimia 10 kutoka mapato ya halmashauri kwa ajili ya shughuli za maendeleo.

Aidha, Mwenge huo utafungua rasmi Hoteli ya Harvest Inn, mradi wa uwekezaji wa mwananchi wenye thamani ya Sh milioni 950, unaotarajiwa kuongeza fursa za ajira na kuchochea ukuaji wa sekta ya utalii na huduma wilayani Muheza.

Baada ya shughuli za miradi kukamilika, mbio za Mwenge wa Uhuru zitahitimishwa katika viwanja vya Mkesha Jitegemee, ambapo kutafanyika maonesho mbalimbali ya utalii, biashara za wajasiriamali, burudani kutoka kwa wasanii wa ndani na nje ya wilaya pamoja na maonesho ya vipaji vya vijana.

Vilevile, wananchi watapata fursa ya kupatiwa elimu kuhusu mapambano dhidi ya rushwa, matumizi ya dawa za kulevya, maambukizi ya UKIMWI, malaria na masuala mengine ya kijamii yanayogusa maendeleo ya taifa.

Wananchi wa Muheza wametakiwa kujitokeza kwa wingi kushiriki mbio hizo za Mwenge wa Uhuru, zinazobeba kaulimbiu ya kuhamasisha uzalendo, uwajibikaji na maendeleo ya wananchi.

LINDI,MTWARA,KAGERA NA RUKWA KUPATA UMEME WA GRIDI NDANI YA MWAKA WA FEDHA 2026/2027

June 22, 2026 Add Comment




Serikali imesema katika mwaka wa fedha 2026/2027 itatekeleza miradi mbalimbali ya umeme ikiwemo kuunganisha mikoa ya Lindi, Mtwara, Kagera na Rukwa kwenye gridi ya taifa ya umeme ili kuhakikisha wananchi wengi zaidi wanapata huduma hiyo nchini.


Akichangia makadirio ya mapato na matumizi ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2026/2027 bungeni jijini Dodoma  Juni 22, 2026, Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi amesema umeme si anasa tena bali ni hitaji la msingi kwa maisha ya wananchi jambo linaloiifanya Serikali kuendelea kuwekeza fedha nyingi katika sekta hiyo.



Amesema Serikali imeendelea kuimarisha miundombinu ya uzalishaji, usafirishaji na usambazaji wa umeme nchini ili kuhakikisha nishati hiyo inawafikia wananchi katika maeneo mbalimbali.


Waziri  Ndejembi ameeleza kuwa umeme unaozalishwa katika Bwawa la Julius Nyerere unasafirishwa kupitia Chalinze kuelekea Morogoro na Dodoma, huku pia ukiunganishwa kwenye njia ya usafirishaji umeme ya Zuzu ili uweze kufika mikoa ya Singida, Tabora, Shinyanga, Simiyu, Geita na Mwanza.


Ameongeza  kuwa katika bajeti ya mwaka wa fedha 2026/2027 Serikali itahakikisha mkandarasi anayetekeleza mradi wa njia ya umeme ya Songea–Tunduru–Masasi–Mahumbika anatekeleza kazi kwa wakati huku Serikali ikiendelea kutoa malipo  yatakayomwezesha mkandarasi huyo kufanya kazi bila kukwama na hivyo kuwezesha mikoa ya Lindi na Mtwara kupata umeme kutoka gridi ya taifa.


Aidha, amesema Serikali inaendelea kukamilisha miradi ya njia za kusafirisha umeme kutoka Iringa kwenda Mbeya, Songwe na Rukwa pamoja na mradi wa Benako–Kyaka ambao unalenga kuimarisha upatikanaji wa umeme katika maeneo husika.


Kwa upande wa usambazaji wa umeme vijijini, Mhe.Ndejembi amesema Serikali imepanga kupeleka umeme katika vitongoji 9,009  huku idadi ya vitongoji vitakavyofikiwa na huduma hiyo ikiendelea kuongezeka katika miaka inayofuata.


Amesema lengo la Serikali ni kuhakikisha ifikapo mwaka 2030 vitongoji vyote nchini vinafikiwa na huduma ya umeme, hatua itakayochochea maendeleo ya kiuchumi na kijamii kwa wananchi.


“Ni kazi kubwa ambayo inakwenda kufanywa, lakini Serikali imejipanga kuhakikisha wananchi wengi zaidi wanapata huduma ya umeme wa uhakika." Amesisitiza Waziri Ndejembi

MAFANIKIO YA USAMBAZAJI UMEME -MHANDISi MRAMBA AIPONGEZA REA NA TANESCO

June 22, 2026 Add Comment




📌*Wakandarasi wa umeme wakaribishwa Zambia kutekeleza miradi*


Dar es Salaam


Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati, Mhandisi Felchesmi Mramba, amesema Tanzania imepiga hatua kubwa katika upatikanaji wa huduma ya umeme, kutoka hatua ya kusambaza umeme kwenye mikoa hadi kufikia ngazi ya  vitongoji, ambapo  amewapongeza Wakala wa Nishati Vijijini (REA) na Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) kwa mchango wao katika mafanikio hayo.


Mhandisi Mramba ametoa pongezi hizo  leo Juni 22, 2026, jijini Dar es Salaam wakati wa hafla ya utoaji wa tuzo na vyeti kwa wasimamizi wa miradi kutoka REA na wakandarasi waliotekeleza   miradi ya umeme vijijini na vitongojini na kuikamilisha kwa wakati.


Amesema hadi sasa asilimia 62 ya vitongoji nchini vimefikiwa na huduma ya umeme, huku Serikali ikilenga kuhakikisha vitongoji vyote vinaunganishwa na umeme ifikapo mwaka 2030 kupitia mpango wa kuunganisha wateja wa mwisho (Last Mile Household Electrification).



Katika hafla hiyo, Mhandisi Mramba amewataka wakandarasi wote wanaotekeleza miradi ya umeme nchini kuhakikisha wanazingatia muda, ubora na gharama, akisisitiza kuwa Wizara itaendelea kufuatilia kwa karibu utendaji wao. 


Amesema Serikali haitaacha kujadiliana na wakandarasi pale changamoto zinapotokea lakini kwa watakaoshindwa kutekeleza majukumu yao ipasavyo hawatapewa fursa ya kushiriki miradi mingine ya Serikali.


Katika kikao hicho, Mhandisi Mramba pia alimkaribisha  Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati ya Zambia anayeshughulikia masuala ya umeme, Mhandisi Arnold Simwaba ambaye yupo nchini  pamoja na ujumbe wake  kwa ziara ya kikazi katika miradi ya umeme.

Katibu Mkuu huyo wa Wizara ya Nishati nchini Zambia amesema wakandarasi walioonyesha uwezo mkubwa katika utekelezaji wa miradi ya umeme nchini Tanzania wanakaribishwa pia kushiriki katika utekelezaji wa miradi ya umeme nchini Zambia.



Kwa upande wake, mwakilishi wa wakandarasi ambaye kampuni yake ya Derm Electric imefanya vizuri katika miradi ya umeme vijijini na vitongojini, Ridhuani  Mringo  amesema wakandarasi wazawa wanapaswa kuendelea kutekeleza miradi kwa uadilifu, weledi na uaminifu ili kuendelea kujenga imani ya Serikali na kuongeza nafasi ya kampuni za ndani kushiriki katika utekelezaji wa miradi mikubwa na ya kimkakati.



BARRICK NORTH MARA YAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE KATIKA MADINI KWA KUTOA MSAADA GEREZA LA TARIME NA KWENYE JAMII

June 22, 2026 Add Comment


Mkuu wa Wilaya, Meja Edward Gowele (aliyevaa shati la bluu), viongozi wa Gereza la Tarime na wafanyakazi wanawake kutoka Barrick North Mara wakiwa katika hafla ya kukabidhi misaada gerezani hapo.

ABBASI AONGOZA KIKAO CHA PILI CHA BODI YA USIMAMIZI WA MRADI WA FORLAND

June 22, 2026 Add Comment
Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Dkt. Hassan Abbasi akiwa na Mwenyekiti mwenza ambaye ni Naibu Balozi wa Finland Bw. Tomi Lounio, wameongoza Kikao cha Pili cha Bodi ya Usimamizi wa Mradi wa Maendeleo ya Matumizi ya Ardhi, Misitu na Mnyororo wa Thamani(FORLAND).

MWENYEKITI MPYA WA BODI YA USHAURI ADEM DKT. DACHI AONGOZA KIKAO CHAKE CHA KWANZA,

June 22, 2026 Add Comment
📍Bagamoyo, Tanzania

Mwenyekiti mpya wa Bodi ya Ushauri ya ADEM, Dkt. Hillary A. Dachi, amewasili rasmi chuoni hapo na kuongoza kikao chake cha kwanza tangu alipoteuliwa kushika nafasi hiyo, ambapo Bodi ilikutana kujadili masuala mbalimbali ya kimkakati yanayolenga kuimarisha utendaji wa taasisi na kuchangia maendeleo ya sekta ya elimu nchini.
RAIS DKT. SAMIA AMUAGA RAIS WA NAMIBIA DKT. NETUMBO NDAITWAH

RAIS DKT. SAMIA AMUAGA RAIS WA NAMIBIA DKT. NETUMBO NDAITWAH

June 22, 2026 Add Comment

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiagana na mgeni wake Rais wa Jamhuri ya Namibia Mhe. Dkt, Netumbo Nandi-Ndaitwah katika viwanja vya Ikulu Jijini Dar es Salaam, tarehe 22 Juni, 2026. Rais Mhe. Dkt. Ndaitwah amehitimisha Ziara yake ya Kitaifa ya siku 4 nchini Tanzania ambapo pamoja na kufanya mazungumzo na Rais Mhe. Dkt. Samia pia alitembelea Kambi ya Kihistoria ya Wapigania Uhuru wa nchi yake, Kongwa mkoani Dodoma.        

WATALAAM WA REA ZAMBIA KUJIFUNZA MAFANIKIO YA TANZANIA KATIKA USAMBAZAJI UMEME VIJIJINI

June 22, 2026 Add Comment

Viongozi wa Mamlaka ya Nishati Vijijini (REA) kutoka nchini Zambia wamewasili nchini kwa ajili ya ziara ya kujifunza na kubadilishana ujuzi na Wakala wa Nishati Vijijini (REA).


REA Zambia ambao wameongozwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati Zambia anayeshughulikia Umeme, Mhandisi Arnold Simwaba wamewasili leo Juni 21, 2026 katika Uwanja wa Kimataifa wa Julius Nyerere na kupokelewa na Mwakilishi wa Katibu Mkuu Wizara ya Nishati Tanzania, Wilson Nyamanga pamoja na Mkurugenzi wa Umeme Vijijini kiutoka REA Tanzania, Mhandisi Jones Olotu, Mkurugenzi wa Rasilimali Watu na Utawala wa REA Tanzania, Renatus Msangira.

Uongozi wa REA Zambia utakuwa nchini kwa ziara ya kikazi ya Siku 7 ambapo pamoja na vikao vya kubadilishana ujuzi, wajumbe hao wanatarajiwa kutembelea miradi mbalimbali ya umeme vijijini inayotekelezwa na Wakala wa Nishati Vijijini.







MWENGE UHURU WARIDHISHWA NA MRADI WA MAJI WA SH.MILIONI 233.4 TANGA

June 22, 2026 Add Comment




Na Oscar Assenga,TANGA.

Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa, Wazo Michael Mwang’onda, amepongeza utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa miundombinu ya kuboresha upatikanaji wa maji safi katika eneo la Mzizima hadi Mikocheni, akisema unadhihirisha dhamira ya Serikali ya Awamu ya Sita ya kusogeza huduma muhimu karibu na wananchi.

Mwenge wa Uhuru 2026 umetembelea na kukagua mradi huo unaotekelezwa na Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Tanga (Tanga UWASA) katika Kata ya Mzizima, ambapo viongozi wa mbio hizo walieleza kuridhishwa na kasi ya utekelezaji wake.


Akizungumza baada ya ukaguzi huo na kushiriki katika zoezi la kumuunganishia mteja mpya huduma ya maji safi, Mwang’onda alisema Serikali chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan inaendelea kutekeleza mkakati wa kuboresha huduma za maji nchini ili kumtua mama ndoo kichwani.

Alisema dhamira hiyo inaonekana kupitia miradi mbalimbali ya kimkakati inayotekelezwa katika sekta ya maji nchini, huku akiipongeza Tanga UWASA kwa usimamizi mzuri wa mradi huo ambao unalenga kuongeza upatikanaji wa huduma ya maji kwa wananchi.

Kwa upande wake, Msimamizi wa Mradi, Mhandisi Aaron Chanimbaga, akisoma taarifa ya utekelezaji alisema mradi huo wenye thamani ya Shilingi milioni 233.4 umefikia asilimia 50 ya utekelezaji.

Alieleza kuwa mradi huo unatarajiwa kukamilika ifikapo Septemba mwaka huu na unalenga kunufaisha zaidi ya wananchi 4,780 kwa kuwapatia huduma ya maji safi na salama kwa uhakika.

Mbio za Mwenge wa Uhuru 2026 zinaongozwa na kauli mbiu isemayo: “Tanzania ni yetu sote, tushirikiane kwa pamoja kuleta maendeleo.”








WAZIRI AWESO ATOA MAAGIZO KWA RUWASA PANGANI

June 21, 2026 Add Comment
Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa, Wazo Mwang'onda (wa pili kushoto) akizungumza kwenye mradi wa maji wa Mikocheni/Mkwaja. Kushoto kwake ni Waziri wa Maji, Mhe Jumaa Aweso na kulia kwake ni Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Pangani, Mhe Ayubu Sebabili


Na Mwandishi Wetu, PANGANI


WAZIRI wa Maji, Mhe. Jumaa Aweso, ameagizi Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) katika Wilaya ya Pangani mkoani Tanga, kuunganisha mtandao wa majisafi na salama kwenye makazi ya watu katika kijiji cha Mkwaja.


Mhe. Aweso ambaye pia ni Mbunge wa Pangani, ameyasema hayo leo Juni 20, 2026 kijijini hapo, alipokaribishwa na Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa, Wazo Mwang’onda, kabla ya kuweka jiwe la msingi kwenye mradi wa upanuzi mtandao wa maji kutoka ‘mradi mama’ uliopo kijiji cha Mikocheni.
Mkimbiza Mwenge wa Uhuru Kitaifa, Raiyan Mohamed Rashid, akimtishwa ndoo ya maji mmoja wa wakazi wa kijiji cha Mkwaja wilayani Pangani,  Mkoa wa Tanga kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji uliofika kijijini hapo kutokea kijiji jirani cha Mikocheni.



Mwenge wa Uhuru wenye kauli mbiu inayosema, “Tanzania ni yetu sote tushikamane kwa pamoja kuleta maendeleo” ulifika kwenye mradi huo wa kwanza baada ya kuingia katika Halmashauri ya Pangani kutokea Handeni.


Mhe. Aweso amesema, kwa vile Mwenge umechagiza maendeleo wilayani humo kwa vipindi tofauti, ipo haja ya kuendeleza hali hiyo kwa kuingiza maji kwenye makazi ya watu, badala ya kuishia kwenye vituo 12 vya kuchotea maji (DPs) vilivyopo Mkwaja.


Amesema, usambazaji majisafi na salama ni utekelezaji wa ahadi za Mhe Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kumtua ndo mama kichwani.


Kwa mujibu wa Mhe. Aweso, kati ya vijiji 12,333 vilivyopo nchini, 10,758 vimefikiwa na huduma ya majisafi na salama wakati 1,575 vitafikiwa ifikapo 2030.


Meneja wa RUWASA wa Wilaya ya Pangani, Mhandisi Rajab Hussein, amesema upanuzi wa mradi wa Mikocheni ni matokeo ya upatikanaji maji kwa wastani wa lita 480,000 kwa siku, wakati mahitaji ya Mikocheni pekee ni lita 40,000.


Kwa mujibu wa Mhandisi Hussein, mahitaji yaliyobainika kwa matumizi katika kijiji cha Mkwaja ni lita 65,000 kwa siku na kufanya jumla yake kuwa lita 105, hivyo kuwa na lita 375,000 za ziada.

Ni picha ya uzinduzi wa mradi wa maji.

Amesema kupitia upanuzi wa mradi huo, RUWASA imejenga tenki lenye uwezo wa kuchukua lita 90,000 na kuwekwa kwenye mnara wa urefu wa mita sita, hivyo kuwa na uwezo wa kusambaza maji kijijini Mkwaji kupitia DPs zilizopo.


Naye Mwang’onda amesema agizo la Mhe. Aweso kwa RUWASA kuunganisha mtandao wa maji kwenye makazi ya watu ni kuuheshimisha Mwenge na kwa Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan.


Mwang’onda amesema historia imeandikwa kwa Mhe. Rais Dkt Samia kuboresha huduma za kijamii ikiwemo upatikanaji majisafi na salama sehemu kubwa ya nchi.


Kwa hali, Mwang’onda, amehimiza wananchi kuwekeza zaidi katika amani, umoja na mshikamano, ili kufikia maono ya Mhe. Rais Dkt Samia kuwa na maendeleo endelevu.


MWISHO.





WANANCHI WAHOJI UHAKIKI MFUMO WA VIPIMO VYA DATA: “TUNACHOLIPIA HAKITOSHI”

June 21, 2026 Add Comment


Na Okuly Julius, OKULY BLOG, DODOMA


Wakazi wa Jiji la Dodoma wameiomba Serikali kupitia Wakala wa Vipimo (WMA) kuingilia kati na kusimamia ipasavyo matumizi sahihi ya vipimo vya vifurushi vya intaneti “bando” pamoja na muda wa maongezi wakidai kupoteza data zao kwa haraka na bila uwazi.

Wananchi hao wametoa wito wa kuwepo kwa uwazi na ukomo sahihi wa muda wa matumizi ya data, wakisema ni haki yao kupata kile wanacholipia.

Baadhi ya wakazi waliozungumza jijini hapa wameeleza kusikitishwa na namna megabytes (MBs) au gigabytes (GBs) wanazonunua zinavyoisha kwa muda mfupi hata pale wanapokuwa hawatumii simu zao kikamilifu, jambo linaloashiria kasoro kwenye usahihi wa vipimo hivyo

Meneja wa Wakala wa vipimo mkoa wa Dodoma Said Ibrahim, anasema wakala umepokea maoni hayo ya wadau na kuongeza kuwa umeshaanza mchakato wa kusimamia uhakiki ikiwemo katika vifurushi vya intaneti (Bando) na muda wa maongezi.