HABARI

SIASA

ELIMU

Recent Posts

MLAPONI AUTAKA UDIWANI KATA YA KIMANG'A

June 30, 2025 Add Comment

Joto la uchukuaji fomu kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) linazidi kupamba moto ambapo sasa Ndugu Hamisi Mlaponi amechukua rasmi fomu kwa ajili ya nafasi ya Udiwani katika kata ya Kimang’a, wilayani Pangani, mkoani Tanga.


Mlaponi ni Mwanasayansi katika eneo la Jamii anayejihusisha na masuala ya misaada ya kibinaadamu na kuhamasisha mifumo ya hifadhi ya jamii hususani katika vijiji vilivyopo mkoa wa Tanga.

Pia, kuelekea malengo ya Kidunia ya Maendeleo Endelevu 2030, Mlaponi amadhamiria kutumia ushawishi wa kisiasa katika kuleta mabadiliko chanya kwenye masuala ya Afya, Elimu na Uchumi kwa wakazi wa kata ya Kimang’a 



Mbali na hayo Mlaponi pia ameapa kusimamia kikamilifu utekelezaji wa Ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) 2025-2030 endapo atapata ridhaa ya kuwatumikia wananchi wa Kimang’a na kuwa chachu ya Maendeleo wilayani Pangani.

DKT.BITEKO ASEMA NISHATI ITAKAYOZALISHWA NA NYUKLIA KUJUMUISHWA KWENYE GRIDI YA TAIFA

June 30, 2025 Add Comment



📌 Asema ni Nishati yenye unafuu wa gharama kulinganisha na vyanzo vingine vya nishati, pia isiyochafuzi kwa mazingira.


📌 Asisitiza nyuklia kwa ajili ya kuzalisha umeme ni salama, awatoa hofu jamii kuhusiana na matumizi yake


📌 Akazia kuhusiana na matumizi ya Vinu vidogo vinavyotumia teknolojia ya kisasa ya Small Module na Micro Reactors 


📌 Nyuklia yatajwa kuleta mapinduzi ya kweli ya uchumi na viwanda Afrika


📌 Rais Samia adhamiria Tanzania kuzalisha umeme wa nyuklia


Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati


Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema kuwa Tanzania inatarajia kuzalisha umeme unaotokana na nyuklia utakaojumuishwa katika Gridi ya Taifa ili kukabiliana na ongezeko la mahitaji ya umeme yanayotokana na ongezeko la viwanda.

Dkt. Biteko amesema hayo Juni 30, 2025 Kigali nchini Rwanda wakati akihutubia katika Mkutano kuhusu masuala ya Nyuklia Afrika.


“Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia uongozi wa Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan imeiagiza Wizara ya Nishati chini ya uongozi wangu kuhakikisha kwamba hivi karibuni umeme utakayozalishwa unajumuishwa katika Gridi ya Taifa,” amesema Dkt. Biteko. 

Ameongeza kuwa kupitia agizo hilo Serikali imeendelea kufanya jitihada mbalimbali ikiwemo kuandaa mikakati ya pamoja ya taasisi za Serikali ili kufikia azma ya kuzalisha umeme wa nyuklia kwa kuwa ni nishati yenye unafuu wa gharama kulinganisha na vyanzo vingine vya nishati, pia isiyochafuzi kwa mazingira.

Ametaja baadhi ya jitihada kuwa Juni 2025 Tanzania iliandaa warsha ili kutoa uelewa kwa wadau wa masuala ya nyuklia ikiwa ni pamoja na kuanzisha taasisi itakayoratibu na kusimamia shughuli za nyuklia.


“Serikali yangu itahakikisha inaendeleza mazingira mazuri kwa ajili ya uzalishaji wa nishati kwa kutumia nyuklia kwa kutunga sera thabiti na kuanzisha mifumo ya sheria  na udhibiti kwa ajili ya usimamizi wa raslimali ya nyuklia na uzalishaji wa umeme unaotokana na nyuklia, amesisitiza Dkt. Biteko.

Vilevile amesema Serikali itaongeza raslimali watu wenye ujuzi katika teknolojia za nyuklia ili kutumia kikamilifu raslimali hiyo hususan katika maeneo mengine ikiwemo afya na kilimo.


Amesema tayari Tanzania ina nyaraka mbalimbali zinazoiangazia nyuklia kama raslimali ya msingi kwa ajili ya kukidhi mahitaji ya nishati ya baadae kama vile Sera ya Taifa ya Nishati, Mkakati wa Nishati Jadidifu na Sera ya Maendeleo ya Madini.


Hata hivyo amesema Serikali ina lengo la kuimarisha Sera ya Teknolojia ya Nyuklia ya mwaka 2013 ili kiakisi maendeleo ya hivi karibuni sambamba na kufuata viwango vya kimataifa.

Akifungua Mkutano huo Waziri Mkuu wa Rwanda Mhe. Dkt. Edward Ngirente amesema kuwa ili kufikia Mpango wa Maendeleo wa Rwanda wa mwaka 2050 wa kuwa nchi ya kipato cha juu wanahitaji kuwa na uzalishaji wa umeme kwa kiasi kikubwa.


“ Hivyo, Rwanda tumeamua kuzalisha umeme wa nyuklia kwa kuwa ni salama na wa uhakika na hauhitaji mvua ili  kurahisisha maendeleo  kwa kutumia  teknolojia,” amesema Mhe. Ngirente.


Aidha, amesema Mkutano huo wa nyuklia utakuwa na manufaa kwa Afrika katika kusaidia maendeleo. Pia nchi za Afrika kwa pamoja lazima  ziwe kinara katika matumizi ya nishati safi na kuwa muda wa utekelezaji ni sasa ili kukabiliana na uharibifu wa mazingira na ongezeko la idadi ya watu.


Waziri Mkuu wa Niger, Mhe. Ali Mahamane Lamine Zeine amesema kuwa nchi yake ina vyanzo vingi vya nishati ikiwemo maji na sasa imezindua mpango wake wa nyuklia hivyo nyuklia ni nishati safi na ina manufaa makubwa katika uzalishaji wa umeme barani Afrika.


Naye, Mwenyekiti wa Bodi ya Mionzi ya Atomiki Rwanda, Dkt. Lassina Zerbo amesema kuwa Rwanda ipo katika hatua za mwishoni za kuanzisha vinu vya nyuklia vya kuzalisha umeme.


Ameongeza kuwa katika kufikia hatua hiyo ilihitaji dhamira ya viongozi na imani kwa wananchi juu ya umuhimu wa uzalishaji wa umeme wa nyuklia.


Mkutano huo unaofanyika kuanza Juni 30 hadi Julai 1, 2025 nchini humo unajumuisha wadau wa nishati kutoka ndani na nje ya Afrika wenye lengo la kuharakisha matumizi ya nyuklia kwa kutumia teknolojia ya kisasa ili kuleta mabadiliko ya nishati Afrika.


Mwisho

UMMY NDERIANANGA ACHUKUA FOMU UBUNGE VITI MAALUMU WANAWAKE WENYE ULEMAVU

June 30, 2025 Add Comment


Aliyekuwa Mbunge wa Viti Maalum Kundi la Wenye Ulemavu  Ummy Nderiananga  Juni 30,2025 amechukua fomu ya kugombea Ubunge Viti Maalum kundi la Wanawake Wenye Ulemavu.


Nderiananga amekabidhiwa fomu hiyo katika Ofisi ya  Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) na Katibu UWT  Mkoa wa Kilimanjaro  Ndug. Jane Chatanda.


KADA WA CCM MARIAM WAJIKA AJITOSA UBUNGE VITI MAALUMU SONGEA

June 30, 2025 Add Comment

 





Kada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM)  Mariam wajika amechukua Fomu ya kugombea ubunge viti maalumu songea



WATAALAM SADC WAKUTANA ZIMBABWE KUJADILI SEKTA YA NISHATI NA MAJI

June 30, 2025 Add Comment


📌 *Miundombinu ya usafirishaji umeme kikanda kujadiliwa*


📌 *Nishati Safi ya kupikia kupewa kipaumbele*


📌 *Mkakati mahsusi wa kuongeza watumiaji wa umeme Afrika (M300) kuwa moja ya Ajenda*


📌 *Maendeleo ya Sekta ndogo ya Mafuta na Gesi pamoja na umeme vijijini kujadiliwa*



Wataalam wa Wizara ya Nishati pamoja na taasisi zake  leo wameshiriki katika Mkutano wa ngazi ya  Makatibu Wakuu na Watalaam wanaoshughulikia masuala ya Nishati na Maji unaofanyika katika Jiji la Harare nchini Zimbabwe. 

Mkutano huo wa awali ni sehemu ya maandalizi kuelekea katika Mkutano wa pamoja wa Kamati ya Mawaziri wanaoshughulikia masuala ya Nishati na Maji wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC). 


Mkutano huo pamoja na kujadili masuala ya Nishati na Maji, umekuwa ni fursa pia kwa Tanzania  kuendeleza diplomasia ya kiuchumi pamoja na kuwasilisha mafanikio ya nchi katika kuboresha huduma za nishati vijijini kupitia miradi inayotekelezwa na Wakala wa Nishati Vijijjni (REA). 

Aidha, Mkutano huo umeangazia maendeleo ya Sekta ndogo ya Mafuta na Gesi, pamoja na ujenzi wa miundombinu ya kikanda ya Mafuta na gesi inayohusu nchi wanachama wa SADC. 

Wataalam kutoka Wizara ya Nishati na taasisi zake waliohudhuria mkutano huo ni Kamishna Msaidizi wa Maendeleo ya Umeme, Mha. Styden Rwebangila, Mkurugenzi Mkuu wa REA, Mha. Hassan Saidy, Mkurugenzi wa  Mipango na Uwekezaji (TPDC), Derick Moshi, Mkurugenzi wa Mifumo ya Udhibiti Umeme (TANESCO) , Mha. Deogratius Mariwa, Mkurugenzi wa Udhibiti Uchumi (EWURA), Msafiri Mtepa na  Wataalam kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.

DKT.KAZUNGU AKUTANA NA WAWEKEZAJI KUTOKA JAPAN,WAAHIDI KUWEKEZA KWENYE MIRADI YA UMEME

June 30, 2025 Add Comment


📌Pia kuwekeza kwenye miundombinu ya usafirishaji umeme nchini


📌Waialika Tanzania kushiriki mkutano wa Tisa wa maendeleo kati ya Japan na Afrika


📌 Waupongeza mpango mahsusi wa Nishati wa Taifa kuwa bora na wa mfano kwa nchi za Afrika


Naibu katibu Mkuu Wizara ya Nishati, anayeshughulikia umeme na nishati jadidifu  Dkt Khatibu Kazungu, leo amekutana na kuzungumza na ujumbe wa wawekezaji kutoka nchini Japan kupitia kampuni ya Toyota Tshusho Cooperation, uliolenga kufanya mazungumzo kuhusu uwekezaji wa miradi mbalimbali kwenye sekta ya umeme hususan umeme wa jua, upepo na njia za kusafirisha umeme pamoja na ujenzi wa vituo vya kupoza umeme chini ya mpango mahsusi wa Nishati wa Taifa ujulikanao kama Energy Compact. 


Kupitia serikali ya Japan chini ya Japan International Banking Corporation, Japan imeonesha nia yake ya kuwekeza kwenye maeneo hayo na kwa sasa wapo kwenye mazungumzo na Serikali ya Tanzania  ili kuainisha maeneo hayo ya uwekezaji. 

Dkt Kazungu amesema Japan imeonesha nia hiyo ya kuwekeza chini ya mpango huo mahsusi kutokana na Tanzania kuwa na mpango mzuri wa ajenda ya Compact ambao umekuwa wa mfano kwa nchi za Afrika hususan kwenye mafanikio kuunganisha umeme kwa wateja, na nchi nyingi za Afrika zimekuwa zikijifunza kutoka mpango wa Tanzania.


Mpango mahususi wa Nishati wa Taifa ulibuniwa na Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) na Benki ya Dunia kwa lengo la kuzisaidia nchi za Afrika kutekeleza miradi mbalimbali ya nishati wakati wa mkutano wa wakuu wa nchi uliofanyika jijini Dar es salaam wa Mission 300 uliobeba ajenda ya kuhakikisha waafrika milioni 300 wanafikiwa na umeme ifikapo mwaka 2030.


Katika hatua nyingine Serikali ya Japan imeialika Tanzania kushiriki kwenye mkutano wa tisa wa masuala ya maendeleo kwa nchi za Afrika utakaofanyika nchini Japan mwezi Agosti, 2025 kwa lengo la kuzikutanisha nchi za Afrika kujadili masuala ya maendeleo kwenye sekta mbalimbali.

ZAHARA MICHUZI ,ALIYEKUWA DED MEATU,IFAKARA NA GEITA AJITOSA MBIO ZA UBUNGE VITI MAALUMu UWT TABORA

June 30, 2025 Add Comment


Zahara Michuzi, mmoja wa watumishi wa umma waliopitia majukumu makubwa serikalini kwa miaka kadhaa, amejiunga rasmi katika kinyang’anyiro cha ubunge wa Viti Maalum kupitia Umoja wa Wanawake wa CCM (UWT) Mkoa wa Tabora.


Katika tukio lililosubiriwa kwa bashasha na matumaini makubwa, Zahara alipokea rasmi fomu ya kugombea kutoka kwa Katibu wa UWT wa Mkoa, Bi. Rhoda Sanga. Tukio hilo limezua msisimko miongoni mwa wanachama wa UWT, huku wengi wakimtaja Zahara kama mwanamke shupavu na mchapakazi mwenye historia isiyo na doa katika utumishi wa umma.

Zahara, ambaye amewahi kuwa Mkurugenzi Mtendaji (DED) katika Halmashauri tatu tofauti — Meatu (Simiyu), Ifakara (Morogoro), na Geita (Geita Mjini) — anajivunia rekodi ya uongozi ulioleta mabadiliko halisi katika maeneo aliyohudumu. Kabla ya kupandishwa cheo kuwa DED, aliwahi pia kuwa Katibu Tawala wa Wilaya (DAS) katika Wilaya ya Chemba mkoani Dodoma, nafasi aliyoitumikia kwa weledi na kujenga imani kwa viongozi na wananchi.


Kwa kuingia kwake kwenye siasa, hasa katika nafasi ya uwakilishi wa wanawake kupitia UWT, Zahara analeta pamoja uzoefu wa kiutawala, usimamizi wa miradi ya maendeleo, na uelewa wa changamoto halisi zinazowakabili wanawake na jamii kwa ujumla katika mkoa wa Tabora na Tanzania nzima.



Wadadisi wa siasa wanaona uamuzi wa Zahara kama hatua ya kuhamasisha wanawake waliobobea katika sekta ya umma kushiriki moja kwa moja katika uundaji wa sera, hasa zile zinazolenga ustawi wa wanawake, vijana, na makundi maalum.

SALEHE MHANDO ACHUKUA FOMU KUGOMBEA JIMBO LA KILINDI MKOANI TANGA

June 30, 2025 Add Comment


 Aliyewahi kuwa Mkuu wa Wilaya ya Tanganyika na Mkuu wa Utawala Ofisi ndogo ya CCM Makao Makuu Lumumba jijini Dar Es Salaam, Ndugu Salehe Mbwana Muhando, leo Jumatatu Juni 30,2025 amechukua fomu ya kugombea Ubunge wa Jimbo la Kilindi,mkoani Tanga,kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika uchaguzi mkuu ujao.





MCHENGERWA AOMBA RIDHAA KWA CCM KUGOMBEA UBUNGE WA RUFIJI

June 30, 2025 Add Comment

Na Mwandishi Wetu - Rufiji

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais- TAMISEMI na aliyekuwa Mbunge wa Rufiji Mhe. Mohamed Mchengerwa leo Juni 30, amejitokeza kuomba ridhaa kwa Chama chake- Chama cha Mapinduzi (CCM) kuchaguliwa kuwa mgombea ubunge wa jimbo hilo katika Uchaguzi Mkuu wa Mwezi Oktoba mwaka huu.

MJUE MTOTO WA MFANYABIASHARA MAARUFU SEIF SAID MWERA ANAYETAJWA KUGOMBEA JIMBO LA TEMEKE

June 29, 2025 Add Comment


Seif Said Mwera alikuwa ni miongoni mwa waasisi wa Biashara ya Usafirisha wa Abiria kusini Mwa Tanzania ambapo Ma BUS yake yalikuwa yakisafiri kutoka Dar Es Salaam kuelekea Mloka kwa Kipindi cha Takriban miongo 4 toka miaka ya Sabini. 

Pamoja na Mwera, majina mengine maarufu ya wakati ule katika sekta ya usafirisha yalikuwa Akida, Manitu na Born Coast, hawa ni miongoni mwa Matajiri wa Kwanza kutokea katika eneo la Temeke na Ukanda Wa Kusini Mwa Tanzania. 



Jina la Mwera ni jina Maarufu katika Wilaya ya Temeke na Kusini na Mwa Tanzania.Mwera, alikuwa Mzalendo mwenye kupenda Nchi yake na watu wa Nyumbani kwake, kiasi cha kuita Ma BUS yake kuyaita MZALENDO BUS SERVICE. 



Uzalendo wake ulidhihirika zaidi pale wakati wa Vita vya Tanzania na Uganda ambapo alijitolea Bus lake kwenda kusaidia katika Vita vya Tanzania na Uganda Mwaka 1979.



Sambamba na hilo, Mwera ndie aliyekuwa MKANDARASI wa Ujenzi wa Shule zote za Rufiji, wakati wa utengenezaji wa Vijiji vya Ujamaa Mwaka 1972, ambapo Watu wa Rufiji walihama kutoka katika Vijiji vya Mabondeni kuja katika Vijiji vya Juu. 



Mwera pia alikuwa, mdau Mkubwa wa Maendeleo katika Wilaya ya Rufiji na Temeke Dar Es Salaam ambako alikuwa akiishi katika maisha yake yote.



Mwera, amechangia uimara, uanzishwaji na Ustawi wa Umoja wa Maendeleo Rufiji kwa kifupi (UMAKURU).



Umoja ambao ulileta mwamko katika Ujenzi wa Shule za Secondary ndani ya Wilaya ya Rufiji, ambapo vijana wengi walipata nafasi ya kusoma katika shule hizo.



Kwa ujumla alikuwa Mdau Mkubwa wa Maendeleo katika maeneo mbali mbali alichangia ujenzi wa Misikiti, ukiwemo Msikiti wa Temeke Mwisho, alichangia Ujenzi wa Ofisi za CCM ikiwemo ujenzi wa Ofisi ya CCM Kata ya Miburani kabla ya kuzaliwa kwa  Kata ya Mtoni.



Seif Said Mwera,  alizaliwa Mwaka 1934 katika Kijiji cha Mgoholi ambacho kwa sasa kinaitwa Kipo katika Wilaya ya Rufiji, na kufariki Mwaka 2001 jijini Dar Es Salaam.



Allah aendelee kumpuzisha kwa amani Mwanawe Tano Seif Mwera anayetajwa kugombea Ubunge katika Jimbo la Temeke amewahi kuwa Mkuu wa Wilaya ya Busega na Kalambo kwa nyakati tofauti. 


Ametumikia nafasi ya Ukuu wa Wilaya kwa miaka Saba. Aidha Tano anafahamika kwa utendaji mahili ulitukuka ambapo alipokuwa Mkuu wa Wilaya ya Busega aliweza kusimamia utekelezaji wa miradi mbali mbali kwa ufanisi mkubwa.



Msimamizi wa Ujenzi wa Vituo vya Afya Nasa, Igalukilo na Hospital ya Wilaya ya Busega. Miradi ya Maji, Lamadi, Nyashimo na Kiloleli.



Alifanya Harambee kubwa uliyo wezesha ujenzi wa Shule Tatu mpya za secondary, Shule ya Secondary Dr Chegeni, Antony Mtaka na Nyamikoma.



Alisimamia kikamilifu mapambano dhidi ya Uvivu haramu. Alisimamia kikamilifu shughuli za Kilimo na Utalii kutaja kwa Uchache. 



Alipokuwa katika Wilaya ya Kalambo alileta mapinduzi makubwa ya Ujenzi wa Miradi ya maendeleo kama Vituo vya Afya, madarasa n.k. Tano alipiga marufuku ujenzi wa kutumia matofali ya kuchoma na matope badala yake matumizi ya tofauli za Block kuimarishwa na kuleta mapinduzi makubwa katika Ujenzi wa Vyumba vya Madarasa. 



Tano pia anafahamika kwa umahili wake wa kupenda Maendeleo ya Wanawake ambapo ameanzisha Taasisi ya Wanawake Lakimoja yenye lengo la kuunganisha Wanawake kupinga ukatili wa Kijinsia na Umasikini.



Mtandao ambao umeleta hamasa kubwa kwa Wanawake kushiriki shughuli za kiuchumi na kuepuka ukatili wa Kijinsia.Kikubwa Tano, anachojivunia ni huasisi wa Ujenzi  wa Shule ya Secondary Bi Titi Mohammed iliyopo Rufiji katika Kijiji cha Kilimani ambayo kwa sasa inaitwa shule ya Secondary Ujamaa.



Tano alifanya Harambee kubwa katika Ukumbi wa PTA kuhakikisha shule hiyo inapata michango na msukumo  wa kujengwa.



Kwa ujumla Tano ni Kiongozi mkweli, mwaminifu, mpenda maendeleo, mbunifu, hodari wa kazi, ana elimu nzuri, uzoefu wa uongozi , ana upeo mkubwa kuhusu maendeleo ya uchumi, jamii na ujenzi wa Taifa kwa ujumla. 

Karibu Temeke Tano Seif Mwera.

DKT.BITEKO AWASILI RWANDA KUSHIRIKI MKUTANO WA NYUKLIA AFRIKA

June 29, 2025 Add Comment


Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati


Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt Doto Biteko Juni 29, 2025 amewasili Kigali nchini Rwanda kwa ajili ya kushiriki katika Mkutano unaohusu masuala ya nyuklia Afrika.

Katika Mkutano huo unaotarajiwa kuanza Juni 30 hadi Julai 1, 2025  nchini humo unajumuisha wadau wa nishati kutoka ndani na nje ya Afrika wenye lengo la  kuharakisha  matumizi ya nyuklia kwa kutumia teknolojia ya kisasa ili kuleta mabadiliko ya nishati Afrika.

Pamoja na ushiriki wake katika Mkutano huo Dkt. Biteko anatarajiwa kufungua mjadala wenye mada kuhusu nishati Afrika na utashi wa kisiasa.


Aidha, katika Mkutano huo Dkt. Biteko ameambatana na Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Cosato Chumi, Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati, Mhandisi Felchesmi Mramba na Mkurugenzi wa Tume ya Mionzi ya Atomiki, Prof. Najat Mohamed.




Mwisho

JESCA MBOGO ACHUKUA FOMU YA KUWANIA UBUNGE VITI MAALUMU MKOA WA DODOMA

June 29, 2025 Add Comment


 Aliyekuwa Naibu Katibu mkuu UWT  Taifa Bi.Jesca Mbogo leo amechukua fomu ya kuwania ubunge wa viti maalumu mkoa wa Dodoma, Bi.Jesca amekabidhiwa fomu leo na katibu wa UWT Mkoa wa Dodoma Bi. Irimina Mushongi.

KIMWANGA ACHUKUA NA KURUDISHA FOMU KUTETEA UDIWANI MAKURUMLA

June 29, 2025 Add Comment

Akabidhi fomu kwa Katibu wa Kata wa CCM Makurumla, Omari Suleiman Bakari


Akizungumza baada ya kukabidhi fomu hiyo, Kimwanga ambaye pia ni mwanahabari alisema kuwa anajivunia kazi kubwa aliyoifanya kwa miaka mitano na sasa anaomba fursa kwenye kukamilisha maeneo yaliyobaki ili kujenga jamii yenye ustawi.

"Ninamaliza miaka mitano ya mafanikio ambapo sisi Makurumla tumefanikiwa kutekeleza miradi ya zaidi ya bilioni 18 ikiwamo barabara, kituo cha afya na elimu.



"Miaka mitano ijayo tunakwenda kujenga kata yenye kasi zaidi na muonekano mkubwa wa maendeleo kwa jamii, wana Makurumla na wana CCM ni watu wema sana nyakati zote tumekuwa pamoja na Mungu akipenda ikiwa chama itawapendeza jina likarudi kwenye uteuzi sina shaka na maamuzi yao kwangu na chama chetu ni ushindi," amesema Kimwanga

Subira Mgalu Aonyesha Nia ya Kuliongoza Jimbo la Bagamoyo

June 29, 2025 Add Comment
Aliyekuwa mbunge wa viti maalum mkoani Pwani, Subira Khamis Mgalu, leo June 29,2025 amechukua fomu ya kuwania nafasi ya ubunge katika Jimbo la Bagamoyo mkoani Pwani.

KADA WA CCM MACRINA AJITOSA UBUNGE VITI MAALUMU MKOA WA TANGA

June 29, 2025 Add Comment

 

KADA wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Tanga Macrina Clemens (kulia ) akikabidhiwa fomu na Katibu wa UWT Mkoa wa Tanga Anastazia Aman

Na Mwandishi Wetu,TANGA.

KADA wa Chama cha Mapinduzi CCM Mkoa wa Tanga Macrina Clemens amechukua fomu ya kuomba ridhaa ya kuteuliwa kugombea Ubunge wa viti Maalumu Mkoa huku akihaidi kushirikiana na wananchi katika kuleta maendeleo.

Akizungumza mara baada ya kuchukua fomu alisema ameamua kuchukua fomu ili kuweza kutoa mchango wake kwa wananchi hususani Jumuiya wa Wanawake wa Chama cha Mapinduzi  (UWT) Mkoa wa Tanga.

Zoezi la kuchukua fomu limeanza katika ofisi za Chama cha Mapinduzi linaendelea nchi nzima ambapo watia nia tofauti wameendelea kujitokeza kwa ajili ya kuchukua fomu za Ubunge na Udiwani.




DKT.DOTO MASHAKA BITEKO ACHUKUA FOMU JIMBO LA BUKOMBE

June 29, 2025 Add Comment


Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dkt. Doto Mashaka Biteko aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Bukombe amechukua fomu ya kuomba ridhaa ya kutetea Ubunge katika Jimbo la Bukombe.

Dkt. Biteko amechukua fomu hiyo na kuirejesha kwa Katibu wa Chama Cha Mapinduzi Wilaya ya Bukombe, Ndugu. Leonard Yesaya Mwakalukwa mapema leo Juni 29, 2025.


Zoezi la uchukuaji fomu katika ofisi za Chama Cha Mapinduzi (CCM) linaendelea nchi nzima ambapo watia nia tofauti wameendelea kujitokeza kwa ajili ya kuchukua fomu za Ubunge na Udiwani.

MHASIBU SUA AJITOSA UBUNGE JIMBO LA SAME MASHARIKI

June 29, 2025 Add Comment

 

Kada wa Chama cha Mapinduzi, CPA (T) Ruth Hassani akisaini kitabu.
Kada wa Chama cha Mapinduzi, CPA (T) Ruth Hassani  ametia nia ya kuwania kuteuliwa na Chama chake kuwania Ubunge katika Jimbo la Same Mashariki, Wilaya ya Same Mkoani Kilimanjaro.

Akiwa ameambatana na Mumewe Bw. Banyinga Majeshi, CPA Ruth ambaye ni Mhasibu wa Chuo Kikuu cha Sokoine (SUA) mkoani Moprogoro alichukua fomu hiyo katika Ofisi za CCM Wilaya ya Same  na kukabidhiwa na Katibu wa CCM Wilaya, Ndg.
Amos Kusakula leo Juni 29,2025.

Ruth amesema nia yake si kutafuta nafasi ya uongozi katika jimbo la Same Mashariki bali kuwasemea Wanasame Mashariki na kusaidiana nao kutatua kero mbalimbali zinazowakabili katika jimbo hilo na Same kwa ujumla akiangazia masuala ya elimu, huduma za Afya, Maji na nisshati safi. 

Katika kuwania uteuzi ndani ya Chama pia Mbunge anayemaliza muda wake Bi. Anne Kilango Malecela na Kada mwingine Bi. Miriam Mjema ni mingoni mwa wana CCM waliochukua fomu kuomba kuteuliwa kugombea Ubge katika jimbo la Same Mashariki.

Jimbo la Same Mashariki lilianzishwa mnamo mwaka 1995 ambapo lilizaliwa kutoka Jimbo la Same hivyo ni moja ya majimbo mawili yanayoiunda Wilaya ya Same na ni moja ya majimbo tisa yanayounda mkoa wa Kilimanjaro.
Jimbo hilo linaundwa na Kata 14 ambapo Kata 5 ziko ukanda wa Tambarare na Kata 9 ziko ukanda wa milimani aidha lina vijiji 49 vyenye kaya 131350.

Wananchi wa Jimbo hilo kwa kiasi kikubwa wanajishughulisha na shughuli za kilimo cha Mpunga, Tangawizi, Mahindi, Maharagwe, Karanga, Ndizi, Kahawa, matunda na miti kwa ajili ya mbao.