HABARI

SIASA

ELIMU

Recent Posts

MBUNGE MNZAVA AWAKABIDHI WAZEE 300 BIMA ZA AFYA KUPITIA MAKUYUNI FESTIVAL

MBUNGE MNZAVA AWAKABIDHI WAZEE 300 BIMA ZA AFYA KUPITIA MAKUYUNI FESTIVAL

December 26, 2025 Add Comment

MBUNGE wa Jimbo la Korogwe Vijijini, Mhe. Timotheo Mnzava, ameendelea kutekeleza mikakati ya kuboresha huduma za afya kwa wazee kwa kugawa Bima za Afya kwa zaidi ya wazee 300 waliohudhuria Makuyuni Festival, tamasha lililowakutanisha wakazi wa maeneo mbalimbali ya jimbo hilo.

Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Mhe. Mnzava amesema  hatua hiyo inalenga kuhakikisha wazee wanapata huduma bora za matibabu bila vikwazo vya kifedha, huku akisisitiza kuwa afya ya wazee ni sehemu muhimu ya ustawi wa jamii.

 "Bima hizo zitawawezesha wazee kupata matibabu kwa wakati wowote na katika vituo vilivyosajiliwa, hatua inayotafsiriwa kama kupunguza mzigo wa gharama za afya kwa familia nyingi za kipato cha chini."amesema Mhe.Mnzava

Katika tamasha hilo, Mbunge Mnzava pia alipata fursa ya kushiriki chakula cha pamoja na wazee, watu wenye ulemavu, vijana na wananchi wengine waliohudhuria, akisema kitendo hicho ni sehemu ya kuimarisha mshikamano na kuonyesha ushirikiano kwa jamii ya jimbo lake.

Amesema Makuyuni Festival ni jukwaa muhimu katika kuwaunganisha wananchi, kubadilishana mawazo na kuhamasisha vijana kushiriki katika shughuli za kijamii zinazochochea maendeleo ya Korogwe Vijijini.

Hata hivyo ametumia a nafasi hiyo kuwatakia wananchi wa jimbo hilo na Watanzania kwa ujumla heri ya Sikukuu ya Krismasi, akisisitiza umuhimu wa kusherehekea kwa amani, upendo na mshikamano.

Amesema Krismasi ni kipindi cha kutafakari baraka za Mungu na kuonyesha huruma kwa watu wenye uhitaji, akiwahimiza wananchi kuendeleza moyo wa ukaribu na kusaidiana bila kujali tofauti zao.

Mhe. Mnzava amewahimiza vijana na wananchi wote kutumia Sikukuu ya Krismasi kama chanzo cha nguvu mpya na hamasa ya kutekeleza majukumu yao kwa uadilifu, uzalendo na bidii katika kuchochea maendeleo ya jimbo hilo.

Amesema serikali kwa kushirikiana na viongozi wa maeneo mbalimbali itaendelea kusimamia utekelezaji wa miradi ya maendeleo, ikiwemo afya, elimu, maji na barabara ili kuhakikisha ustawi wa wananchi unaongezeka.

Aidha Mnzava amewahimiza wadau wote wa maendeleo wa korogwe ambao wanaishi maeneo mbalimbali nchini, kurudi nyumbani kuja kuwekeza ili kuzidi kuinua maendeleo ya korogwe

Kwa upande wao, baadhi ya wazee walionufaika na bima hizo walimshukuru mbunge kwa kuona umuhimu wa afya zao, wakisema hatua hiyo imewapa faraja na matumaini katika kupata matibabu kwa uhakika.

HOSPITALI YA TEMEKE KUFANYIWA UCHUNGUZI WA UTENDAJI

December 26, 2025 Add Comment
MAVUNDE AMKABIDHI NYUMBA MPYA BIBI ALIYETAKA KUIUZA KWA AJILI YA MATIBABU

MAVUNDE AMKABIDHI NYUMBA MPYA BIBI ALIYETAKA KUIUZA KWA AJILI YA MATIBABU

December 26, 2025 Add Comment

‎Na Edward Winchislaus.

MBUNGE  wa Jimbo la Mtumba na Waziri wa Madini, Mhe. Anthony Mavunde, amemkabidhi nyumba iliyofanyiwa ukarabati Bi. Verian Mlewamwenye umri wa miaka 75, mkazi wa Kata ya Mtumba jijini Dodoma, ambaye alikuwa katika hatua ya kuiuza nyumba yake kwa Shilingi 500,000 ili kupata fedha za matibabu baada ya kuugua uvimbe katika ubavu.

Hatua hiyo imefuatia taarifa za hali ya bibi huyo kuripotiwa kwenye vyombo vya habari, ambapo kwa kushirikiana na Kitengo cha Ustawi wa Jamii, Bi. Verian alipelekwa Hospitali ya Rufaa ya Dodoma na kufanyiwa upasuaji uliomwezesha kurejea katika hali nzuri ya afya.

‎Akizungumza na wananchi wa Mtaa wa Vikonje B, Kata ya Mtumba, wakati wa kukabidhi nyumba hiyo leo, Desemba 26, 2025, Mhe. Mavunde amesema kuwa aliguswa na simulizi ya maisha ya bibi huyo baada ya kuona taarifa zake kwenye vyombo vya habari.

‎“Nimeona nitumie fursa hii kuikabidhi nyumba iliyofanyiwa ukarabati. Nyumba hii ni ya Bi. Verian aliyeijenga mwenyewe. Baada ya kuona taarifa kuwa anaumwa na kukosa fedha za matibabu hadi kufikia hatua ya kutaka kuuza nyumba yake, tulishirikiana na ofisi ya ustawi wa jamii kumpeleka hospitalini, akafanyiwa upasuaji na kupona,” amesema Mhe.Mavunde

Aidha Mavunde ame‎ongeza kuwa baada ya Bi. Verian kupona, waliamua kuikarabati nyumba hiyo ili aishi katika mazingira salama na yenye staha.

“Tuliamua kuikarabati nyumba hii ili bibi aishi maisha bora na ya furaha. Rai yangu ni kuwaona wanajamii wakirejesha tabasamu kwa waliopoteza matumaini, kwani hii ni sadaka kubwa mbele ya Mwenyezi Mungu,” amesisitiza Mhe.Mavunde Katika ukarabati huo, madirisha yaliyokuwa yamezibwa kwa matofali yaliondolewa na kuwekwa madirisha ya kisasa ili kuruhusu mwanga na hewa kuingia ndani. Mbali na ukarabati wa nyumba, Mhe. Mavunde amemkabidhi Bi. Verian msaada wa mahitaji mbalimbali ikiwemo kilo 80 za sukari, mchele, mafuta ya kupikia, maji, pamoja na vitenge na kanga. Aidha, Mhe. Mavunde amebainisha kuwa watamuwezesha Bi. Verian kupata mtaji kwa kumjengea mabanda ya kuku ili afuge kuku wa kienyeji na kujiendeleza kiuchumi.

Kwa upande wake,Afisa Ustawi wa Jamii wa Kata ya Mtumba, Bi. Mela Katamba,amesema kuwa walipokea taarifa za dhamira ya Bi. Verian kuuza nyumba yake na kuchukua hatua za haraka kufanya uchunguzi wa karibu.

“Tulibaini changamoto yake kubwa ilikuwa kupata matibabu. Kwa kuwa alikuwa na zaidi ya miaka 60, alikidhi vigezo vya kupata msamaha wa matibabu, hivyo tulimpeleka hospitalini na akapatiwa huduma stahiki,” amesema

Ameongeza kuwa baada ya matibabu, waliendelea kushirikiana na Mhe. Mavunde ambaye alimhudumia Bi. Verian kwa kumpatia kitanda na godoro kabla ya kutekeleza ahadi ya kukarabati nyumba yake.

Naye Bi. Verian Mlewa amemshukuru Mhe. Mavunde kwa msaada huo akisema umebadilisha maisha yake na kumpa matumaini mapya baada ya kipindi kigumu alichopitia. Awali  Mwanawe, Bi. Abigail Daud (40), amema familia ilikabiliwa na changamoto kubwa ya kugharamia matibabu ya mama yao kutokana na hali duni ya kipato.

DKT.MWIGULU ATOA WITO KWA VIONGOZI WA DINI KUENDELEA KUTOA ELIMU YA UMOJA NA AMANI

December 25, 2025 Add Comment


_Atoa wito kwa Watanzania kuhimiza umoja na amani_.


Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba ametoa wito kwa viongozi wa dini kuendelea kushirikiana na Serikali katika kutoa elimu ya umoja na amani, kupinga chuki, migawanyiko na vitendo vyovyote vinavyoweza kuvuruga mshikamano waTaifa.


Amesema kuwa vita yoyote inayohusisha wenyewe kwa wenyewe huwa haina mshindi bali ina kupoteza wote na mgawanyiko ndani ya taifa hauna mshindi bali una matokeo ya kushindwa wote kama Taifa.

Ametoa wito huo leo (Alhamisi, Desemba 25, 2026)  aliposhiriki ibada ya Sikukuu ya Krismasi iliyofanyika katika Kanisa Kuu la Kiinjili la Kilutheri la Azani Front jijini Dar es Salaam.


“Manufaa ya amani ni makubwa: huleta maendeleo ya kiuchumi, huimarisha ustawi wa jamii, na huwezesha kila Mtanzania kushiriki kikamilifu katika kujenga Taifa.”

Amesema kuwa Serikali inaendelea kutekeleza wajibu wake wakulinda amani na usalama wa nchi pamoja na kuwajenga Watanzania na hususani vijana kuthamini dhana ya uzalendo kwa nchi yetu.


“Tanzania imeendelea kuwa kielelezo cha umoja, amani, mshikamano na utulivu katika ukanda wetu na barani Afrika. Amani hii imejengwa juu ya misingi imara ya maadili, haki, kuheshimiana, uvumilivu na uzalendo.”

Kadhalika, Mheshimiwa Dkt. Mwigulu ametoa wito kwa wazazi na walezi kuendelea kushirikiana kwa karibu na taasisi za elimu na dini katika kuimarisha malezi ya watoto na vijana kwa kuwajengea misingi imara ya maadili na kuwaongoza kutumia vyema fursa za elimu, teknolojia na utandawazi kwa maendeleo yao na Taifa kwa ujumla.


Aidha, katika Ibada hiyo, Mheshimiwa Dkt. Nchemba ameungana na  Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuwatakia Wakristo na Watanzania wote kwa ujumla, Heri ya Sikukuu ya Krismasi na kuwasishi kusherehekea kwa Amani, Upendo na Utulivu, kudumisha mshikamano wa Kitaifa kwa maslahi ya Taifa la Tanzania.

Kwa upande wake, Mkuu wa Kanisa la Kiinjili na Kilutheri Tanzania (KKKT) na Mkuu wa Dayosisi ya Mashariki na Pwani, Askofu Dkt. Alex Malasusa amekemea tabia za baadhi ya watu za kuchafua taswira za watu wengine, pamoja na kuichonganisha jamii. Kuna watu wakiona  jamii imekaa pamoja kwa amani wao inawakosesha raha”.



KITUO CHA PENINSULA NOBLE: ALAMA MPYA YA JIJI LA DAR ES SALAAM

December 24, 2025 Add Comment

 

Na Mwandishi Wetu - Dar es salaam

Kampuni ya kutoka China ya CRJE (East Africa) Ltd imejivunia uwekezaji wake mkubwa katika Mradi mkubwa wa jengo la kibiashara Peninsula Noble Center, ambapo umekuwa moja ya miradi mikubwa ya maendeleo ya Kampuni hiyo nchini Tanzania.

DKT.MWIGULU : MTENDAJI MKUU WA TEMESA NA MENEJIMENTI YAKE WAFUTWE KAZI

December 24, 2025 Add Comment


_Aagiza uchunguzi ufanyike kubaini sababu za uharibifu wa mara kwa mara wa vivuko_

 


WAZIRI MKUU Dkt. Dkt. Mwigulu Nchemba ameagiza kufutwa kazi na kufikishwa katika vyombo vya sheria kwa aliyekuwa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme Tanzania (TEMESA) pamoja na Menejimenti ya wakala huo kutokana na ubadhilifu wa zaidi ya shilingi bilioni 2.5.


Pia, Waziri Mkuu amemuagiza Waziri wa Ujenzi, Abdallah Ulega kufanya uchunguzi wa vivuko vyote ili kubaini vyanzo vya uharibifu kwa sababu kuna taarifa kwamba vivuko hivyo vinaharibiwa kwa makusudi ili wahusika waweze kujipatia fedha kupitia matengenezo.

Amesema uamuzi huo unatokana na matokeo ya tume maalumu iliyoundwa ndani ya kuchunguza tuhuma za matumizi mabaya ya fedha za umma katika wakala huo. “Vyombo husika vichukue hatua kwa wahusika, haya mambo ya kutoheshimu fedha za umma, kutokuwa na huruma na Watanzania lazima yafike mwisho.”

 

Waziri Mkuu ametoa agizo hilo leo Jumatano, Desemba 24, 2025 akizungumza na viongozi wa mkoa wa Dar es Salaam na wakazi wa Kigamboni akiwa katika ziara ya kukagua hali ya utoaji wa huduma katika kivuko cha Magogoni, Kigamboni jijini Dar es Salaam.



Amesema ubadhilifu uliofanyika ni sawa na watendaji hao kugawana vivuko pamoja na kuiba nauli zinazotolewa na wananchi mambo ambayo yanamkera Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan na amewaagiza wayakomeshe ili wananchi waendelee kupata huduma bora na za uhakika.

 

Pia, Waziri Mkuu amemuagiza Waziri wa Ujenzi, Abdallah Ulega afanye mawasiliano na wizara ya fedha kuhakikisha fedha za malipo ya utengenezaji wa vivuko zinatolewa kwa wakati ili zoezi la ukarabati liweze kukamilika na vivuko hivyo viweze kutoa huduma. Serikali inavivuko vitatu katika eneo la Kivukoni/Kigamboni na kwa sasa kinachonfanyakazi ni kimoja tu.

 


Kwa upande wake, Kaimu Mtendaji Mkuu wa TEMESA, Moses Mabamba amesema Serikali inamiliki vivuko vitatu kwa ajili ya Kivukoni na Kigamboni ambapo kwa sasa kinachotoa huduma ni kimoja tu cha MV. Kazi huku kivuko cha MV. Magogoni kipo kwenye matengenezo Mombasa tangu 2023.

 

Amesema matengenezo hayo ambayo yanagharimu takribani shilingi bilioni 7.5 yamefikia asilimia 70 huku kivuko kingine cha MV. Kigamboni kipo katika matengenezo kwenye kampuni ya Songoro Marine, Kigamboni. “…Kabla ya kuharibika kwa vivuko hivyo tulikuwa na uwezo wa kukusanya shilingi milioni 20 kwa siku ila kwa sasa tunakusanya shilingi milioni 3.61 hadi shilingi milioni nne.”

 


Naye, Mkurugenzi wa Uhusiano na Mawasiliano wa Bakhresa Group, ambao wameingia ubia na Serikali kutoa hutua ya vivuko, Hussein Sufian amesema walianza kutoa huduma mwanzoni mwa mwaka huu baada ya vivuko vya Serikali kupata hitilafu na walianza na vivuko vinne na sasa wanavivuko nane ambavyo kila kimoja kinauwezo wa kubeba watu 200.

 

Amesema awali walikuwa wanasafirisha watu 20,000 kwa siku na sasa wanasafirisha watu 50,000 hadi 100,000, kutokana na wingi wa abiria wanakusudia kuongeza kivuko kingine ili waweze kukidhi mahitaji. Vivuko hivyo vinatumia muda wa dakika tano hadi 10 ikitegemea na hali ya bahari.

MAHAFALI YA 6 YA LAVENDER DAY CARE CENTER YAFANA KITUNDA MASAI

December 24, 2025 Add Comment

 


Na. Mwandishi Wetu, Dar

Mahafali ya sita (6) kwa Watoto wa darasa la Awali ya Kituo cha Lavender Day Care Center kilichopo Kitunda Masai, yameweza kukonga nyoyo Wazazi na viongozi waliofika kushuhudia tukio hilo la kipekee katika kuhitimisha Wanafunzi hao.




Katika mahafali hayo yaliyofanyika hivi karibuni Disemba 2025, Wahitimu hao wa darasa la awali wameweza kuonesha uwezo wao mkubwa wa yale waliofundishwa darasani kama masomo na michezo mbali mbali.




Awali mgeni rasmi katika mahafali hayo, Mdau wa Elimu Bi. Elly Kitaly ambaye ni Mkurugenzi wa taasisi ya Chadron's Hope Foundation amepongeza uongozi wa shule, Walimu pamoja kwa namna ya kipekee katika kumsaidia Mtoto kitaaluma sambamba na wazazi kwa kuichagua Lavender Day Care tawi la Kitunda Masai.




Amesema uwezo wa watoto hao ni mkubwa hivyo wanatakiwa kuendelea kusimamiwa katika malezi sahihi ya kielimu na kuendelea kujengwa katika mambo mema katika hatua ya Elimu ya Msingi.

Bi.Elly Kitaly amesema kuwa, Elimu ni muhimu lakini pia vitu vingine vya Msingi kabisa vinapaswa kufundishwa Watoto ilikuwajenga zaidi.

"Nimeona kuna watu wana elimu kubwa lakini hawafanyi mambo makubwa.Elimu ni pamoja na mambo ya msingi ni kwa kujifunza Hutu, kujifunza kuwa mkweli na kujifunza kusimama kwenye haki." Amesema Bi. Elly Kitaly.

Aidha, katika risala ya Kituo hicho, juu ya kuongeza majengo mengine, Bi. Elly Kitaly amesema kuwa anaamini Wazazi wanaweza kuchangia chochote ilikufanikisha ujenzi huo kwani itasaidia maendeleo ya watoto wengi.

"Nimesikia tunataka kujenga majengo mengine, moja ya changamoto ya kuendeshea shughuli kama hizi za taasisi za shule ni suala la kifedha, na nafahamu pesa ni changamoto hivyo tuungane kusaidia kituo cha Levender ili kiendelee kusaidia watoto wetu, Mimi na wewe tuungane tukatoa kilichopo mifuko ya cement, au matofali au hata kuchangia elfu moja (Tsh 1,000) inaweza kubadilisha mazingira ya Lavender.

Ameongeza "Utakuja hapa utakuta mazingira safi yame boreshwa, madarasa yame ongezeka, sehemu ya michezo ya watoto imeboreshwa hata utakuta na eneo la kuogelea (swimming pool) ya watoto.

Aidha amesema kuwa, 

Elimu ni muhimu, lakini pia lazima tujifunze mengine kama fani ya muziki, kuogelea na mengine katika vipaji ili kukabiliana na soko la ajira.

"Nimeona watoto wamefanya mambo makubwa hapa, niwapongeze Uongozi wa Lavender, na Walimu kwa kuwalea vyema watoto hawa, na wakawe mfano huko katika ngazi inayofuata.

Nae Mkurugenzi wa kituo cha Lavender Day Care, Bi.Vida Andrew Ngowi amewashukuru Wazazi na Walezi kwa kuendelea kuwaunga mkono na kwa sasa wanaendelea kuongeza majengo mengine ya Kituo hicho cha eneo la Kitunda Masai.

Aidha, kupitia risala ya msimamizi wa kituo hicho, amesema Lavender Day Care Center kilichopo Kitunda Masai ilianzishwa mwaka 2019 kwa lengo la kutoa huduma bora ya malezi, makuzi na maendeleo ya awali ya watoto. 

"Kituo kilianza na watoto wachache mwaka 2019 na hadi kufikia sasa tuna watoto wengi, tuna washukuru Wazazi na Walezi kutukimbilia Lavender kwa hapa eneo la Kitunda Masai, kwani kituo chetu "Mtoto ndiye kiini cha ujifunzaji ", lakini pia falsafa yetu kuu inasema"Tunajifunza kupitia michezo".

Kituo cha Lavender pia kina tawi katika eneo la Bunju A ambacho nacho kinafanya vizuri sana ikiwemo watoto wanajifunza kifaransa, kuogolea na muziki kama chaguo kwa wale wanaopenda.