HABARI

SIASA

ELIMU

Recent Posts

DC NYAMWESE: UWEPO WA BENKI YA NMB NI NYENZO MUHIMU KUCHOCHEA UCHUMI WA WANANCHI

March 31, 2026 Add Comment

Na Oscar Assenga, Handeni

MKUU wa Wilaya ya Handeni, Salum Nyamwese, amesema uwepo wa taasisi za kifedha, ikiwemo Benki ya NMB, ni nyenzo muhimu katika kuchochea na kuimarisha uchumi wa wananchi kupitia sekta mbalimbali kama kilimo, mifugo na biashara ndogondogo.

Amesema Serikali ya Awamu ya Sita inaendelea kutilia mkazo juhudi za kuimarisha uchumi wa wananchi wa vijijini ili waweze kujikwamua kiuchumi na kimaendeleo.

Nyamwese alitoa kauli hiyo leo wakati wa tamasha la “NMB Kijiji Day” lililoandaliwa na Benki ya NMB wilayani Handeni, likihusisha matembezi, mbio fupi na mazoezi, kwa lengo la kuwakutanisha wananchi na kuwahamasisha kushiriki shughuli za maendeleo.

Alisema uwepo wa benki hiyo katika tamasha hilo haujalenga kutangaza huduma zake pekee, bali pia kutoa huduma mbalimbali za kijamii ikiwemo upimaji wa afya na uchangiaji wa damu, jambo ambalo lina manufaa makubwa kwa jamii.

“Ninawahimiza wananchi wa Handeni kutumia fursa hii kujitokeza kwa wingi kupata elimu ya fedha, kufungua akaunti na kujifunza namna bora ya kusimamia mapato yao. Ni muhimu pia kuhakikisha mikopo inayopatikana inatumika kwa malengo yaliyokusudiwa ili kuleta tija kwa familia na jamii kwa ujumla,” alisema Nyamwese.

Aidha, alisema Serikali itaendelea kushirikiana na wadau mbalimbali kuhakikisha huduma za kifedha zinawafikia wananchi wengi zaidi, hususan waliopo maeneo ya pembezoni kupitia mtandao mpana wa matawi na mawakala.

Awali, akizungumza katika tamasha hilo, Mkuu wa Idara ya Mauzo na Mtandao wa Matawi wa Benki ya NMB Makao Makuu, Donatus Richard, alisema “NMB Kijiji Day” ni jukwaa muhimu la kushirikiana na jamii kupitia utoaji wa elimu ya kifedha na huduma za kibenki.


Alisema kupitia tamasha hilo, benki hiyo hutoa elimu ya masuala ya fedha, kufungua akaunti kwa wananchi na kuimarisha mshikamano wa kijamii, sambamba na kuhamasisha afya na ustawi kupitia michezo na burudani.

Donatus alibainisha kuwa hapo awali huduma nyingi za kibenki zilikuwa zinapatikana zaidi mijini, lakini kuanzia mwaka 2024 benki hiyo ilianza mkakati wa kupeleka huduma hizo vijijini.

“Kwa sasa tuna matawi zaidi ya 248 nchini kote, na hata maeneo yasiyo na matawi tunahakikisha huduma zinapatikana kupitia mawakala. Tumeweza kufikia zaidi ya vijiji 3,000 tangu mwaka 2024 ambavyo hapo awali havikuwa na huduma za kibenki,” alisema.

Aliongeza kuwa juhudi hizo zimeongeza idadi ya wateja, ambapo zaidi ya akaunti milioni mbili zimefunguliwa kuanzia mwaka 2024 hadi Januari mwaka huu.

Kwa mwaka 2026, alisema benki hiyo imejipanga kufikisha huduma za kibenki katika vijiji vingine 2,000 ambavyo bado havijafikiwa, sambamba na kuendelea kushiriki katika shughuli za kijamii kama michezo na upandaji miti ili kulinda mazingira.

Aidha, alisema benki hiyo imekuwa mstari wa mbele katika kuhamasisha utunzaji wa mazingira, ikiwemo kuhimiza matumizi ya nishati safi badala ya mkaa.

“Benki yetu inatambua umuhimu wa kuhifadhi mazingira na tunatambulika kimataifa kwa uwajibikaji wa kijamii. Fedha za wateja wetu ziko salama na wanapata huduma bora kwa wakati,” alisema.

Alibainisha kuwa mwaka 2026 benki hiyo imetambuliwa kwa ubora katika masuala ya uendelevu nchini, ikiwa na zaidi ya matawi 248, mashine za ATM zaidi ya 700, mawakala 73,000 na wateja zaidi ya milioni 10.

Mwisho, alitoa wito kwa wananchi ambao bado hawajafungua akaunti kufanya hivyo ili waweze kunufaika na huduma mbalimbali zinazotolewa na benki hiyo.

Mwisho.

WANANCHI IDODI WAMLILIA LUKUVI

March 31, 2026 Add Comment



NA. MWANDISHI WETU – IDODI IRINGA

Wananchi wamlilia aliyekuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera Bunge Uratibu na Wenye Ulemavu na Mbunge wa Jimbo la Isimani Marehemu William Lukuvi kwa kazi nzuri alizozifanya wakati akitekeleza majukumu yake katika sekta mbalimbali serikalini na kuwaletea maendeleo katika nyanja mbalimbali.


Hayo yamelezwa kwa wakati tofauti hii leo 30 Machi, 2026 wakati mwili wa marehemu Lukuvi ulipowasili Kijijini Kwake Kata ya Idodi, Wilaya ya Iringa Vijijini ambapo ndipo kunatarajiwa kuwa makazi yake ya milele mara baada ya ibada ya mazishi kijijini hapo.

Wananchi hao wameonesha simanzi kubwa na kumkumbuka kama kiongozi shupavu, na mtetezi wa wanyonge hususan kwa wakazi wa Jimbo Lake la Isimani mkoani Iringa.

Akizungumza na waandishi wa habari Mmoja wa waombolezaji Bw. Kombo  Jumbe amesema Marehemu William Lukuvi aliasisi utaratibu wa kliniki za ardhi wakati akiwa anahudumu kama Waziri wa Ardhi na hivyo kuwezesha wananchi kuhudumiwa kwa  urahisi na kwa haraka.


“Marehemu Lukuvi alituwezesha sisi hupata huduma kwa haraka hasa zilizohusu masuala ya migogoro ya ardhi na kufanya kufikiwa kwa urahisi na watoa huduma katika wizara ya ardhi  na yeye ndiye aliyezindua upatikanaji wa hati za ardhi na kufanya zoezi lile kuwa endelevu” alieleza

Kwa upande wake Bw. Frank Mbindile Mkazi wa Kijiji cha Magozi Wilaya ya Iringa amesema Marehemu William Lukuvi alikuwa ni mtu anayependa kusikiliza shida za watu kwa makundi na hata shida za mwananchi mmoja mmoja na kukiri kuwa wamepoteza mtu muhimu na Lulu kwa Taifa. 


“Ni aina ya kiongozi anayeamini katika kusimamia mambo ya msingi kwa ajili ya maslahi mapana ya wananchi na akizungumza jambo alikuwa anauwezo wa kulisimamia, hivyo wanaisimani tumepoteza kiongozi mkubwa,” alieleza.

=MWISHO=

KILIMANJARO MARATHON 2026: ZAIDI YA MBIO, NI FAHARI YA TAIFA

March 31, 2026 Add Comment

   

 Moshi ilichangamka kwa mara nyingine tena wakati maelfu ya wakimbiaji, mashabiki na wageni walipokusanyika kushiriki Kilimanjaro Marathon 2026. Tukio hili limeendelea kukua na kuwa zaidi ya mbio, likiunganisha michezo, utalii na jamii katika jukwaa moja.

ADEM NA TET KUIMARISHA MISINGI YA UJENZI WA UWEZO KWA WALIMU

March 31, 2026 Add Comment
WAKALA wa Maendeleo ya Uongozi wa Elimu nchini (ADEM) kwa kushirikiana na Taasisi ya Elimu Tanzania (TET) wamefanya warsha maalumu ya kuhakiki Matini ya uendeshaji wa Jumuiya za Kujifunza za walimu na viongozi wa elimu (JzK), ikiwa ni hatua muhimu ya kukusanya maoni ya wadau kwa ajili ya kuboresha nyenzo hiyo.

WMA YATOA MSAADA WA VIFAA VYA UJENZI KWA WAHITAJI DODOMA

March 30, 2026 Add Comment

Katika kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia, Wakala wa Vipimo (WMA) imetoa misaada ya vifaa vya ujenzi wa jiko la kisasa katika Kituo cha kulelea watoto wenye mahitaji maalumu Cha RAHMAN ORPHANAGE CENTER kilichopo Chang'ombe jijini Dodoma.

Akizungumza baada ya kutoa misaada hiyo Meneja wa WMA Mkoa wa Dodoma Said Ibrahimu amesema suala la mazingira safi ya kupikia ni haki ya kila mmoja ndio maana wameamua kama Wakala kutoa misaada hiyo itakayowezesha upishi wa kisasa katika mazingira safi na salama ikiwemo usalama wa chakula kwani kituo hicho wamekuwa wakipika kwa kutumia kuni na mazingira ya Nje ambayo sio salama kwa afya ya watoto hao.

"tunamuunga mkono Rais wetu Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuhakikisha nishati safi ya kupikia inakuwa katika mazingira safi na salama ndio maana leo kwa niaba ya wafanyakazi wa WMA tumekabidhi Sementi, Marumaru na vifaa vingine vitakavyosaidia ujenzi wa jiko hilo, "amesema Meneja Said

Kadhalika, Mkurugenzi wa kituo hicho Bi. Rukia Abdallah ameishukuru WMA kwa misaada hiyo itakayokwenda kuboresha mazingira ya mapishi katika Kituo hicho chenye idadi ya watoto 120 huku akiomba wadau wengine kujitokeza kuchangia kituo hicho ikiwemo suala la usafiri ili watoto hao waweze kutembelea maeneo mbalimbali kwa ajili ya kujifunza zaidi.

Mmoja wa watoto wanaolelewa katika Kituo hicho Hazra Ramadhan ameipongeza Wakala wa Vipimo kwa kuona umuhimu wa kuwasaidia na kuwaomba kuendelea kuwakumbuka kila mara ili waweze kutimiza malengo yao.







PPP YAONYESHA NJIA KUFIKIA MALENGO YA UMEME MEGAWATI 70,000 IFIKAPO 2050

March 30, 2026 Add Comment
NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

SEKTA binafsi imeelezwa kuwa nguzo muhimu katika kufanikisha malengo ya Mpango wa Nne wa Maendeleo (FYDP IV), huku Serikali ikisisitiza umuhimu wa kuongeza ushiriki wake katika uwekezaji wa nishati ili kufikia uzalishaji wa megawati 70,000 ifikapo mwaka 2050.

MISA YA KUOMBEA NA KUAGA MWILI WA MAREHEMU MHE.LUKUVI -IRINGA

March 30, 2026 Add Comment

Misa Takatifu ya kuuaga Mwili wa aliyekuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu), na Mbunge wa Jimbo la Isimani, Marehemu Mhe. William Lukuvi, iliyofanyika katika Kanisa Kuu la Moyo Mtakatifu wa Yesu lililopo Kihesa Iringa leo tarehe 30 Machi, 2026 nakuongozwa na Askofu wa Jimbo la iringa Romanus Mihali.


Misa hiyo imehudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Serikali, Viongozi wa Vyama vya Siasa, Viongozi wa dini pamoja na Waombolezaji kutoka maeneo mbalimbali ya mkoa wa Iringa na nje ya mkoa huo.

















Mhe. Lukuvi amefariki dunia tarehe 25 Machi, 2026 katika Hospitali ya Benjamin Mkapa Mkoani Dodoma alipokuwa akipatiwa matibabu.

TUME YA MADINI YATOA UFAFANUZI KUHUSU AJALI KWENYE MGODI WA MSASA - GEITA

March 30, 2026 Add Comment
Ajali imetokea katika Mgodi wa Dhahabu wa Msasa uliopo Runzewe, Wilaya ya Bukombe mkoani Geita, baada ya sehemu ya eneo la uchimbaji kuporomoka na kufunika madarura manne yenye namba K 46A, 47A, 48A na 49A.

Kwa mujibu wa Ofisi ya Afisa Madini Mkazi – Mbogwe, madarura hayo yalikuwa yamefungwa tangu Machi 27, 2026 kwa ajili ya ukarabati, hata hivyo baadhi ya watu waliingia katika eneo hilo bila kufuata taratibu.

UKiKAMATWA UMEFICHA MAFUTA NI KESI YA UHUJUMU UCHUMI

March 30, 2026 Add Comment

 



📌 EWURA kuendesha operesheni maalum kubaini wanaoficha mafuta.


Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati anayeshughulikia Mafuta na Gesi, Dkt. James Mataragio, ameiagiza Mamlaka ya Udhibiti wa Nishati na Huduma za Maji (EWURA) kuendesha operesheni ya kuwabaini watu wanaojihusisha na vitendo vya kuficha mafuta kwa makusudi ili kusababisha uhaba katika maeneo mbalimbali.


Ameeleza kuwa baadhi ya wafanyabiashara wasio waaminifu wanatumia mwanya wa hali iliyopo kwa kuchukua mafuta kutoka kwenye maghala (depots) kwa kiwango kikubwa kuliko mahitaji yao, kisha kuyahifadhi wakisubiri bei mpya zitangazwe ndipo wayauze kwa bei ya juu.



Amesisitiza kuwa vitendo hivyo ni kosa la uhujumu uchumi, na yeyote atakayebainika atachukuliwa hatua za kisheria. Hivyo, amewaonya wafanyabiashara wanaojihusisha na vitendo hivyo kuacha mara moja kwa kuwa vinachangia kuleta uhaba wa mafuta.


“Nimewaelekeza Ewura kuanzia leo, usimwonee mtu yoyote aibu kama mtu akikamatwa ameficha mafuta, kwakweli sisi hatutamvumilia na Kamshna msimamie hilo mafuta yanayopakiwa hapa Dar es salaam muhakikishe yanafika kwenye vituo kama inavyokuwa imepangwa” amesisitiza Matarajio.


Dkt. Mataragio amefafanua kuwa tayari wameanza kupokea taarifa za baadhi ya vituo kukosa mafuta, hali inayochangiwa na vitendo vya aina hiyo ambapo mafuta yanapochukuliwa Dar es Salaam hayafiki katika vituo kama inavyotakiwa.


Kwa upande wake, Kamishna wa Mafuta na Gesi kutoka Wizara ya Nishati, Bw. Goodluck Shirima, amesema Serikali inaendelea kufuatilia kwa karibu mwenendo wa usafirishaji na uuzaji wa mafuta nchini, ili kuhakikisha mafuta yote yanayopakiwa kutoka kwenye matenki yanafika katika vituo husika na wananchi wanaendelea kupata huduma bila usumbufu wowote.

RAIS MSTAAFU DKT JAKAYA KIKWETE NA RAIS WA MALAWI PROFESQ ARTHUR MUTHARIKA WATETA

March 29, 2026 Add Comment

 


Rais Mstaafu Mhe. Dkt. Jakaya Kikwete, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Jopo la Wazee la Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) (Panel of Elders, POE) akiwa katika picha ya pamoja na Profesa Arthur Peter Mutharika, Rais wa Malawi, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Asasi ya Siasa, Ulinzi na Usalama ya  Jumuiya ya SADC, baada ya kufanya naye mazungumzo jana Ijumaa jijini Lilongwe, Malawi. 

Pamoja nao ni Mama Joyce Banda, Rais Mstaafu wa Malawi, ambaye ni Mjumbe wa Jopo hilo la Wazee. Katika mazungumzo yao, pamoja na mambo mengine, Viongozi hao walipata fursa ya kumweleza Rais Mutharika kuhusu kazi zilizofanywa na zinazoeandelea kufanywa na POE katika kusuluhisha migogoro katika nchi za Ufalme wa Lesotho, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Malawi na kwa sasa Madagascar. 

Kimuundo, POE ni moja ya vyombo vya kuzuia migogoro na kurejesha amani katika nchi za SADC ambacho kinaripoti moja kwa moja kwenye Asasi ya SADC Troika, ambayo nchi ya Malawi ndiyo Mwenyekiti wake kwa sasa.