HABARI

SIASA

ELIMU

Recent Posts

KITUO CHA PENINSULA NOBLE: ALAMA MPYA YA JIJI LA DAR ES SALAAM

December 24, 2025 Add Comment

 

Na Mwandishi Wetu - Dar es salaam

Kampuni ya kutoka China ya CRJE (East Africa) Ltd imejivunia uwekezaji wake mkubwa katika Mradi mkubwa wa jengo la kibiashara Peninsula Noble Center, ambapo umekuwa moja ya miradi mikubwa ya maendeleo ya Kampuni hiyo nchini Tanzania.

DKT.MWIGULU : MTENDAJI MKUU WA TEMESA NA MENEJIMENTI YAKE WAFUTWE KAZI

December 24, 2025 Add Comment


_Aagiza uchunguzi ufanyike kubaini sababu za uharibifu wa mara kwa mara wa vivuko_

 


WAZIRI MKUU Dkt. Dkt. Mwigulu Nchemba ameagiza kufutwa kazi na kufikishwa katika vyombo vya sheria kwa aliyekuwa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme Tanzania (TEMESA) pamoja na Menejimenti ya wakala huo kutokana na ubadhilifu wa zaidi ya shilingi bilioni 2.5.


Pia, Waziri Mkuu amemuagiza Waziri wa Ujenzi, Abdallah Ulega kufanya uchunguzi wa vivuko vyote ili kubaini vyanzo vya uharibifu kwa sababu kuna taarifa kwamba vivuko hivyo vinaharibiwa kwa makusudi ili wahusika waweze kujipatia fedha kupitia matengenezo.

Amesema uamuzi huo unatokana na matokeo ya tume maalumu iliyoundwa ndani ya kuchunguza tuhuma za matumizi mabaya ya fedha za umma katika wakala huo. “Vyombo husika vichukue hatua kwa wahusika, haya mambo ya kutoheshimu fedha za umma, kutokuwa na huruma na Watanzania lazima yafike mwisho.”

 

Waziri Mkuu ametoa agizo hilo leo Jumatano, Desemba 24, 2025 akizungumza na viongozi wa mkoa wa Dar es Salaam na wakazi wa Kigamboni akiwa katika ziara ya kukagua hali ya utoaji wa huduma katika kivuko cha Magogoni, Kigamboni jijini Dar es Salaam.



Amesema ubadhilifu uliofanyika ni sawa na watendaji hao kugawana vivuko pamoja na kuiba nauli zinazotolewa na wananchi mambo ambayo yanamkera Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan na amewaagiza wayakomeshe ili wananchi waendelee kupata huduma bora na za uhakika.

 

Pia, Waziri Mkuu amemuagiza Waziri wa Ujenzi, Abdallah Ulega afanye mawasiliano na wizara ya fedha kuhakikisha fedha za malipo ya utengenezaji wa vivuko zinatolewa kwa wakati ili zoezi la ukarabati liweze kukamilika na vivuko hivyo viweze kutoa huduma. Serikali inavivuko vitatu katika eneo la Kivukoni/Kigamboni na kwa sasa kinachonfanyakazi ni kimoja tu.

 


Kwa upande wake, Kaimu Mtendaji Mkuu wa TEMESA, Moses Mabamba amesema Serikali inamiliki vivuko vitatu kwa ajili ya Kivukoni na Kigamboni ambapo kwa sasa kinachotoa huduma ni kimoja tu cha MV. Kazi huku kivuko cha MV. Magogoni kipo kwenye matengenezo Mombasa tangu 2023.

 

Amesema matengenezo hayo ambayo yanagharimu takribani shilingi bilioni 7.5 yamefikia asilimia 70 huku kivuko kingine cha MV. Kigamboni kipo katika matengenezo kwenye kampuni ya Songoro Marine, Kigamboni. “…Kabla ya kuharibika kwa vivuko hivyo tulikuwa na uwezo wa kukusanya shilingi milioni 20 kwa siku ila kwa sasa tunakusanya shilingi milioni 3.61 hadi shilingi milioni nne.”

 


Naye, Mkurugenzi wa Uhusiano na Mawasiliano wa Bakhresa Group, ambao wameingia ubia na Serikali kutoa hutua ya vivuko, Hussein Sufian amesema walianza kutoa huduma mwanzoni mwa mwaka huu baada ya vivuko vya Serikali kupata hitilafu na walianza na vivuko vinne na sasa wanavivuko nane ambavyo kila kimoja kinauwezo wa kubeba watu 200.

 

Amesema awali walikuwa wanasafirisha watu 20,000 kwa siku na sasa wanasafirisha watu 50,000 hadi 100,000, kutokana na wingi wa abiria wanakusudia kuongeza kivuko kingine ili waweze kukidhi mahitaji. Vivuko hivyo vinatumia muda wa dakika tano hadi 10 ikitegemea na hali ya bahari.

MAHAFALI YA 6 YA LAVENDER DAY CARE CENTER YAFANA KITUNDA MASAI

December 24, 2025 Add Comment

 


Na. Mwandishi Wetu, Dar

Mahafali ya sita (6) kwa Watoto wa darasa la Awali ya Kituo cha Lavender Day Care Center kilichopo Kitunda Masai, yameweza kukonga nyoyo Wazazi na viongozi waliofika kushuhudia tukio hilo la kipekee katika kuhitimisha Wanafunzi hao.




Katika mahafali hayo yaliyofanyika hivi karibuni Disemba 2025, Wahitimu hao wa darasa la awali wameweza kuonesha uwezo wao mkubwa wa yale waliofundishwa darasani kama masomo na michezo mbali mbali.




Awali mgeni rasmi katika mahafali hayo, Mdau wa Elimu Bi. Elly Kitaly ambaye ni Mkurugenzi wa taasisi ya Chadron's Hope Foundation amepongeza uongozi wa shule, Walimu pamoja kwa namna ya kipekee katika kumsaidia Mtoto kitaaluma sambamba na wazazi kwa kuichagua Lavender Day Care tawi la Kitunda Masai.




Amesema uwezo wa watoto hao ni mkubwa hivyo wanatakiwa kuendelea kusimamiwa katika malezi sahihi ya kielimu na kuendelea kujengwa katika mambo mema katika hatua ya Elimu ya Msingi.

Bi.Elly Kitaly amesema kuwa, Elimu ni muhimu lakini pia vitu vingine vya Msingi kabisa vinapaswa kufundishwa Watoto ilikuwajenga zaidi.

"Nimeona kuna watu wana elimu kubwa lakini hawafanyi mambo makubwa.Elimu ni pamoja na mambo ya msingi ni kwa kujifunza Hutu, kujifunza kuwa mkweli na kujifunza kusimama kwenye haki." Amesema Bi. Elly Kitaly.

Aidha, katika risala ya Kituo hicho, juu ya kuongeza majengo mengine, Bi. Elly Kitaly amesema kuwa anaamini Wazazi wanaweza kuchangia chochote ilikufanikisha ujenzi huo kwani itasaidia maendeleo ya watoto wengi.

"Nimesikia tunataka kujenga majengo mengine, moja ya changamoto ya kuendeshea shughuli kama hizi za taasisi za shule ni suala la kifedha, na nafahamu pesa ni changamoto hivyo tuungane kusaidia kituo cha Levender ili kiendelee kusaidia watoto wetu, Mimi na wewe tuungane tukatoa kilichopo mifuko ya cement, au matofali au hata kuchangia elfu moja (Tsh 1,000) inaweza kubadilisha mazingira ya Lavender.

Ameongeza "Utakuja hapa utakuta mazingira safi yame boreshwa, madarasa yame ongezeka, sehemu ya michezo ya watoto imeboreshwa hata utakuta na eneo la kuogelea (swimming pool) ya watoto.

Aidha amesema kuwa, 

Elimu ni muhimu, lakini pia lazima tujifunze mengine kama fani ya muziki, kuogelea na mengine katika vipaji ili kukabiliana na soko la ajira.

"Nimeona watoto wamefanya mambo makubwa hapa, niwapongeze Uongozi wa Lavender, na Walimu kwa kuwalea vyema watoto hawa, na wakawe mfano huko katika ngazi inayofuata.

Nae Mkurugenzi wa kituo cha Lavender Day Care, Bi.Vida Andrew Ngowi amewashukuru Wazazi na Walezi kwa kuendelea kuwaunga mkono na kwa sasa wanaendelea kuongeza majengo mengine ya Kituo hicho cha eneo la Kitunda Masai.

Aidha, kupitia risala ya msimamizi wa kituo hicho, amesema Lavender Day Care Center kilichopo Kitunda Masai ilianzishwa mwaka 2019 kwa lengo la kutoa huduma bora ya malezi, makuzi na maendeleo ya awali ya watoto. 

"Kituo kilianza na watoto wachache mwaka 2019 na hadi kufikia sasa tuna watoto wengi, tuna washukuru Wazazi na Walezi kutukimbilia Lavender kwa hapa eneo la Kitunda Masai, kwani kituo chetu "Mtoto ndiye kiini cha ujifunzaji ", lakini pia falsafa yetu kuu inasema"Tunajifunza kupitia michezo".

Kituo cha Lavender pia kina tawi katika eneo la Bunju A ambacho nacho kinafanya vizuri sana ikiwemo watoto wanajifunza kifaransa, kuogolea na muziki kama chaguo kwa wale wanaopenda. 












MKURUGENZI MKUU TUME YA TAIFA YA UMWAGILIAJI AKAGUA BWAWA LA UJENZI MKOMAZI.

December 24, 2025 Add Comment

 -Ujenzi wafikia asilimia 85,


-Asisitiza kuzingatia muda na ubora wa ujenzi



Na MWANDISHI WETU

Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji(NIRC), Bw. Raymond Mndolwa, amefanya ziara ya kikazi katika bwawa la kilimo cha Umwagiliaji la Mkomazi lililopo kijiji cha Manga Mtindiro, Wilaya ya Korogwe, mkoani Tanga, kwa lengo la kukagua na kujionea maendeleo ya ujenzi wa bwawa hilo.

Katika ziara hiyo, Bw. Mndolwa alipata fursa ya kutembelea eneo la mradi na kujionea hatua mbalimbali za utekelezaji wake, huku akisisitiza umuhimu wa kuhakikisha mradi huo unakamilika kwa wakati na kwa viwango vinavyotakiwa ili kuwanufaisha wakulima wa eneo hilo na wilaya na Mkoa wa Tanga kwa ujumla.

Mkurugenzi Mndolwa, amekagua eneo hilo la mradi na kujiridhisha na hatua ya ujenzi iliyofikiwa huku akisisitiza haja ya usimamizi wenye kuzingatia ubora.

Bw. Mndolwa, amesema lengo kuu la ziara hiyo ni kukagua maendeleo ya mradi, kusikiliza changamoto zinazojitokeza pamoja na kuhakikisha kuwa mradi unatekelezwa kwa mujibu wa mpango kazi na fedha zilizotengwa.

“Dhamira ya Tume ni kuona mradi huu unakamilika kwa wakati uliopangwa, niwahakikishie wananchi wa Wilaya ya Korogwe kuwa serikali kupitia Tume ya Taifa ya Umwagiliaji itaendelea kusimamia mradi huu kwa karibu hadi utakapokamilika na kuanza kuleta manufaa yaliyokusudiwa,”amesema.

Amesema mbali na mradi huo Tume inaendelea kutekeleza miradi mingine ya Umwagiliaji katika maeneo mbalimbali nchini, ikiwa ni sehemu ya mkakati wa Serikali wa kuboresha sekta ya kilimo na kuondokana na kilimo kinachotegemea mvua.

Awali akizungumza na waandishi wa habari wakati wa ziara hiyo, Meneja wa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji Mkoa wa Tanga, Mhandisi Leonard Someke, amesema kuwa utekelezaji wa mradi wa bwawa la Mkomazi unaendelea vizuri na kwa kasi ambapo ujenzi wake umefikia asilimia 85.

Ameeleza kuwa mradi huo unatarajiwa kukamilika ifikapo tarehe 04 Februari 2026, huku akibainisha kuwa bwawa hilo lina uwezo mkubwa wa kuhifadhi maji ya kutosha kwa ajili ya kilimo cha umwagiliaji katika msimu wote wa mwaka, jambo litakalosaidia kuongeza uzalishaji wa mazao kwa wakulima wa eneo hilo.

Kwa upande wa Wananchi wa kijiji cha Manga Mtindiro na Wilaya ya Korogwe kwa ujumla wamempongeza Mheshimiwa Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa juhudi zake za kuendeleza sekta ya kilimo kupitia uwekezaji mkubwa katika miradi ya Umwagiliaji nchini.

Aidha, wametoa pongezi kwa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji chini ya uongozi wa Mkurugenzi Mkuu wake, Bw. Raymond Mndolwa, kwa kupeleka na kusimamia utekelezaji wa mradi wa bwawa la Mkomazi, wakisema kuwa mradi huo utaleta mabadiliko makubwa ya kiuchumi, kuongeza uzalishaji wa mazao na kuboresha maisha ya wakulima wa eneo hilo.






NAIBU WAZIRI OWM-TAMISEMI MHE REUBEN KWAGILWA AENDELEA NA ZIARA UBUNGO

NAIBU WAZIRI OWM-TAMISEMI MHE REUBEN KWAGILWA AENDELEA NA ZIARA UBUNGO

December 24, 2025 Add Comment





Naibu Waziri wa nchi ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serilali za mitaa TAMISEMI Mhe Reuben Kwagilwa amemtaka katibu Mkuu wa wizara hiyo kuunda timu maalumu ya wataalamu kushughulikia changamoto zilizopo kwenye kituo cha Mabasi cha Magufuli ili kiwe na tija kwa wananchi, wafanyabiashara, Serikali na wadau wengine

Ametoa maelekezo hayo leo Disemba 23,2025 alipofanya ziara kwa niaba ya Waziri wa TAMISEMI kwenye kituo cha Mabasi cha Magufuli kilichopo Mbezi Luis Wilayani Ubungo jijini Dar es salaam ambapo amesema miongoni mwa mambo ya kufuatilia ni pamoja na mapato na matumizi ya kituo hicho kero za wananchi,wafanuabiashara wadogo na wadau wengine

Aidha amesema timu hiyo ijimuishe wataalamu kutoka ofisi ua Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam na wadau wengine lengo likiwa ni kuhakikisha makusidio ya Serikali kutumia fedha nyingi kujenga kituo hicho cha mabasi cha Magufuli linatimia

Akizungimzia suala la mikopo ya asilimia kumi wa vijana wanawake na watu wenye ulemavu jambo ambalo ni miongoni mwa vitu vilivyolalamikiwa na wananchi wa eneo hilo Kwagilwa amewatoa shaka wananchi kuwa Rais Dkt Samia ameshatoa maelekezo hivyo watapata mikopo hiyo

Awali kabla ya kumkaribisha Naibu Waziri wa TAMISEMI kuongea Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Wakili Albert Msando amesema Wilaya hiyo iko shwari na wananchi wanaendelea na shughuli zao

Kwa upande wao baadhi ya wananchi na wadau mbalimbali wamelalamikia suala la mabasi ya mikoani na nchi jirani kutopaki kwenye kituo hicho huku pia wakilalamikia kuchelewa kwa mikopo ya halmashairi

Katika hatua nyingime Naibu Waziri wa TAMISEMI Reuben Kwagilwa ametembelea ujenzi wa daraja na barabara inayoendelea na ujenzi goba mpakani kwa mkorea hadi madale na kumtaka mkandarasi kuongeza kasi ya ujenzi ili ujenzi huo usiathiriwe na mvua

DC NYAMWESE AONGOZA UKAGUZI WA KUSHTUKIZA BARABARANI, ATOA ONYO KALI KWA MADEREVA

DC NYAMWESE AONGOZA UKAGUZI WA KUSHTUKIZA BARABARANI, ATOA ONYO KALI KWA MADEREVA

December 24, 2025 Add Comment

Mkuu wa Wilaya ya Handeni, Mhe. Salum Nyamwese, akiwa ameongoza na Kikosi cha Usalama Barabarani wilayani humo kufanya ukaguzi wa kushtukiza katika barabara kuu ya Dar es Salaam–Tanga, eneo la Segera, ambapo jumla ya madereva 60 walibainika kukiuka makosa mbalimbali ya usalama barabarani.

Na Mwandishi Wetu, Handeni

Mkuu wa Wilaya ya Handeni, Mhe. Salum Nyamwese, ameongoza Kikosi cha Usalama Barabarani wilayani humo kufanya ukaguzi wa kushtukiza katika barabara kuu ya Dar es Salaam–Tanga, eneo la Segera, ambapo jumla ya madereva 60 walibainika kukiuka makosa mbalimbali ya usalama barabarani.

Akizungumza wakati wa ukaguzi huo, Mhe. Nyamwese amesisitiza umuhimu wa madereva kuzingatia sheria na kanuni za usalama barabarani, hususan katika kipindi hiki cha msimu wa sikukuu, ili kuepusha ajali na kulinda maisha ya abiria pamoja na watumiaji wengine wa barabara.

“Ninatoa wito kwa madereva wote; huu ni msimu wa sikukuu, tafadhali epukeni kabisa matumizi ya vilevi mnapokuwa barabarani. Tuko macho saa 24. Dereva yeyote atakayekamatwa akiendesha gari akiwa amelewa katika barabara yetu hatapata msamaha, leseni yake itafutwa,” amesema Mhe. Nyamwese.

Ameeleza kuwa ukaguzi huo ni sehemu ya jitihada za Serikali ya Wilaya ya Handeni katika kuhakikisha usalama wa wananchi unaimarishwa na ajali za barabarani zinapungua, hasa katika kipindi cha sikukuu.

NGORONGORO YATANGAZA VIVUTIO VYA UTALII KWA WASHIRIKI WA ROMBO MARATHON

December 24, 2025 Add Comment


Na Mwandishi Wetu, Rombo.


Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro (NCAA) imeshiriki katika tamasha la _Rombo _Marathon_ lililofanyika leo tarehe 23 Desemba 2025,  Rombo Mkoani Kilimanjaro na kuvutia wageni kutoka maeneo mbalimbali ya ndani na nje ya nchi. 


Ushiriki wa Ngorongoro Rombo Marathon ambayo pia watumishi wa Mamlaka hiyo wameshiriki mbio za umbali tofauti inadhihirisha jitihada za  mamlaka hiyo  kuunga mkono sekta ya michezo,  kutangaza vivutio vya utalii  kupitia utalii wa michezo, kujenga uhusiano na wadau kupitia matukio ya kijamii na kitaifa na kimataifa.

Sambamba na kushiriki katika tamasha hilo, wananchi waliohudhuria mashindano hayo walipata fursa ya kutembelea banda la Ngorongoro lililowekwa mahsusi kwa ajili ya kutoa elimu kwa washiriki na wananchi kwa ujumla kuhusu shughuli za Uhifadhi na utalii pamoja  na mchango wa hifadhi ya Ngorongoro katika kulinda urithi wa asili na wa kitamaduni.



EWURA, TRA kuimarisha ushirikiano

December 23, 2025 Add Comment

Watendaji wa Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) na wenzao wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), leo 23 Desemba 2025, wamekutana na kujadili namna ya kuimarisha ushirikiano wa utendaji hususani katika usimamizi wa masuala ya kikodi yanayotokana na huduma zinazodhibitiwa na EWURA.

NANAUKA AWATAKA VIONGOZI WASHUKE CHINI, WAFIKIE VIJANA KWA FURSA ZA SERIKALI

December 23, 2025 Add Comment

 

 


Na Ashrack Miraji

Waziri wa Maendeleo ya Vijana, Joel Nanauka, amewataka viongozi wa Mikoa, Wilaya, Halmashauri na Kata kuacha tabia ya kukaa ofisini na badala yake kushuka chini kuwafuata vijana ili kuwaeleza fursa mbalimbali za kimaendeleo zinazotolewa na Serikali kwa ajili ya kuwainua kiuchumi.

Akizungumza na vijana wa Jimbo la Same Mashariki mkoani Kilimanjaro, Waziri Nanauka alisema viongozi hao wana wajibu wa kuwafikia vijana moja kwa moja kwenye maeneo yao na kuwapatia taarifa sahihi kuhusu fursa za mikopo, mafunzo, ajira na miradi mbalimbali ya kiuchumi inayotolewa na Serikali.

Alisema katika ziara zake tangu ateuliwe kuwa Waziri wa wizara hiyo, amebaini kuwa idadi kubwa ya vijana hawana taarifa za fursa za maendeleo zinazotolewa na Serikali, hali inayosababisha fursa hizo kuwafikia vijana wachache huku wengi wakibaki nyuma kwa kukosa taarifa.


“Nimegundua taarifa nyingi za fursa za vijana hubaki kwa makundi machache. Serikali ya Awamu ya Sita inataka kila kijana, bila kujali itikadi au eneo alipo, apate taarifa na kunufaika na fursa hizi,” alisema Waziri Nanauka.

Aliongeza kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameagiza fursa zote zinazohusu vijana zitolewe kwa uwazi na usawa, huku viongozi wa ngazi zote wakihamasishwa kuhakikisha vijana wanapata elimu ya namna ya kuzitumia fursa hizo kwa maendeleo yao binafsi na Taifa kwa ujumla.


Kwa upande wake, Mbunge wa Jimbo la Same Mashariki, Anne Kilango, alisema kundi la vijana ni kubwa kuanzia ngazi ya dunia, Taifa hadi jimbo lake, akieleza kuwa takribani asilimia 64 ya wakazi wa jimbo hilo ni vijana, hivyo linahitaji mikakati madhubuti ya kuwawezesha kiuchumi.

Kilango alisema miradi mikubwa ya maendeleo inayotekelezwa ndani ya jimbo hilo imeongeza imani ya vijana kwa Serikali, ikiwemo mradi wa ujenzi wa barabara ya Mkomazi–Kisiwani Same yenye urefu wa kilomita 101 inayojengwa kwa kiwango cha lami, ambayo imefungua fursa za kiuchumi na kijamii kwa vijana wa eneo hilo.

Naye Waziri Nanauka aliahidi kushughulikia changamoto zilizowasilishwa na vijana, hususan miundombinu ya umwagiliaji, akisema Serikali inaendelea kutenga rasilimali ili kuboresha kilimo cha umwagiliaji kwa mazao ya kimkakati yanayolimwa na vijana ili kuongeza tija na kipato.

Kwa upande wao, vijana waliohudhuria mkutano huo, wakati wakiwasilisha risala yao kwa Waziri, walisema wanakabiliwa na changamoto ya miundombinu ya umwagiliaji katika kilimo cha tangawizi kwenye kata za milimani pamoja na kilimo cha mpunga katika kata za tambarare, wakiiomba Serikali kuharakisha upatikanaji wa miradi ya maji kwa ajili ya kilimo.