HABARI

SIASA

ELIMU

Recent Posts

LONDO AFUNGA MBEYA CITY EXPO, AAHIDI MAZINGIRA SALAMA KWA SEKTA BINAFSI KUELEKEA DIRA 2050

May 30, 2026 Add Comment
Serikali imeahidi kuendelea kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji nchini ili kuipa nafasi pana sekta binafsi kushiriki katika ukuaji wa uchumi na uzalishaji wa ajira kuelekea Dira ya Taifa ya Maendeleo ya 2050.

KAPINGA AITAKA TBPL KUONGEZA UZALISHAJI NA KUIMARISHA MIKAKATI YA MASOKO

May 30, 2026 Add Comment
Waziri wa Viwanda na Biashara, Judith Kapinga, ameagiza Menejimenti ya Kiwanda cha Kuzalisha Bidhaa za Kibaolojia Tanzania (TBPL) kinachomilikiwa na Shirika la Taifa la Maendeleo (NDC) kuongeza uzalishaji na kuimarisha mikakati ya masoko ili kunufaika na mahitaji makubwa yaliyopo sokoni, kuhakikisha kiwanda kinaendelea kujiendesha kwa ufanisi wa kibiashara

MRADI WA C- SDTP WALETA HAMASA YA UZALISHAJI MAZIWA UNAOZINGATIA MABADILIKO YA TABIANCHI

May 30, 2026 Add Comment
Sehemu ya Wafanyakazi wa Mradi wa C-SDTP wakiwa kwenye banda la maonesho wakati wa Wiki ya Maziwa Kitaifa Mkoani Iringa.

Na Kadama Malunde - Iringa

Wizara ya Mifugo na Uvuvi kupitia mradi wa Tasnia ya Maziwa na Mabadiliko ya Tabianchi (C-SDTP), kwa kushirikiana na Mfuko wa Kimataifa wa Maendeleo ya Kilimo (IFAD), imeungana na wadau wengine wa kitaifa maadhimisho ya Wiki ya Maziwa kitaifa katika viwanja vya Mwembe Togwa, mkoani Iringa kuanzia 25 Mei hadi 1 Juni 2026 kwa lengo la kuhamasisha ufugaji wa ng'ombe na uzalishaji wa maziwa unaozingatia mabadiliko ya tabianchi.

TADB YAWAWEZESHA WAFUGAJI WADOGO ZAIDI YA 92, 000 KUPITIA MRADI WA MAZIWA WA TI3P

May 30, 2026 Add Comment
Jumla ya wafugaji wadogo 92,831 na wadau wa mnyororo wa thamani wa maziwawa Tanzania Bara na Visiwani-Zanzibar wamenufaika na Mradi Shirikishi waWasindikaji na Wazalishaji wa Maziwa (TI3P) tangu ulipoanzishwa mwezi Machi mwaka 2022, ambapo asilimia 30 ya wanufaika hao ni wanawake.

Mradi huo wa miaka minne unafadhiliwa na Benki ya Maendeleo ya KilimoTanzania - TADB pamoja na Bill & Melinda Gates Foundation huku ukitekelezwakwa kushirikiana na Heifer International, Land O’Lakes Venture37 pamoja naTanager.

Akiongea wakati wa Maonesho ya Wiki ya Maziwa Mkoani Iringa, Mratibu waMradi wa TI3P, Joseph Mabula amesema mradi huo unalenga kutatua changamoto mbalimbali zilizopo kwenye mnyororo wa thamani wa sekta ndogo ya maziwa ilikuongeza uzalishaji, na kuboresha kipato cha wafugaji wadogo wa maziwa nchinihuku akiishukuru serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Dkt. SamiaSuluhu Hassan kwa kuipa uzito mkubwa sekta ndogo ya maziwa.

Mabula amesema tangu kuanza kwake, mradi umewezesha utolewaji wa mikopowa Zaidi ya shilingi bilioni 42 kwenye sekta ndogo ya maziwa ikiwalenga wasindikaji wa maziwa, wafugaji, wasambazaji wa pembejeo, pamoja na wadauwengine kwenye mnyororo wa thamani wa sekta ya maziwa.

Fedha hizo zimewezesha uanzishwaji wa viwanda vipya vya kuchakata maziwapamoja na upanuzi na maboresho kwa jumla ya viwanda 17 vya usindikajivimefikiwa kwa uwekezaji wenye thamani ya shilingi bilioni 22.8.

Aidha, mradi umewezesha ununuzi wa mitamba 3,330 yenye thamani ya zaidi yashilingi bilioni 11.09, hatua iliyochangia kuongeza uzalishaji na tija katika sekta yamaziwa nchini.

Kupitia mradi huo, wafugaji wameendelea kupata huduma za ugani, pembejeobora, masoko, pamoja na huduma za kifedha kwa ajili ya uwekezaji katika sektandogo ya maziwa, jumla ya wasindikaji 19 wa maziwa wamenufaika na programuza kuongeza uwezo, huduma za ugani, na ufanisi katika uzalishaji.

Katika kuhamasisha ushirikishwaji wa kijinsia na ukuaji jumuishi, TADB ilitoaruzuku linganifu yenye thamani ya shilingi bilioni 1.4 kwa wafugaji wadogo 1,216, wakiwemo wanawake 397, ili kupunguza changamoto za upatikanaji wa mitambabora, uzalishaji, uchakataji na uwekezaji katika mnyororo wa thamani wa maziwa.

Vilevile, biashara tano (5) zinazomilikiwa na wanawake zilipatiwa mitambo yakuchemshia maziwa yenye thamani ya shilingi milioni 75 ili kuongeza fursa za masoko kwa wafugaji. Wasindikaji wanawake watano (5) walinufaika na ruzuku za TI3P, huku wasindikaji 12 wakipata ruzuku maalum za kuchochea usawa wakijinsia katika biashara zao.

Katika kuboresha ukusanyaji na kuhakikisha ubora wa maziwa, mradiumefanikiwa kuanzisha na kuimarisha vyama vya ushirikia/msingi 45 pamoja navikundi mbalimbali vya wafugaji na wafanyabiashara kwenye seta ndogo yamaziwa. Vikundi hivyo kwa sasa vinakusanya zaidi ya lita 25,664 za maziwa kwasiku,hivyo kuchochea upatikanaji wa maziwa hususani kwa viwanda nawachakataji wadogo wa maziwa.

Mratibu wa Mradi huo, amesema kuwa mradi umefanikiwa kuanzisha vituo 23 vyaukusanyaji wa maziwa nchini kwa gharama ya zaidi ya shilingi bilioni 1.157 kwakushirikiana na wadau mbalimbali, ikiwemo vyama vya ushirika, wafugaji, wasindikaji wa maziwa, na washirika katika utekelezaji wa mradi.

Mabula amehihimisha kwa kusema kuwa mradi huo unaendelea kushughulikiachangamoto za kisera na kisheria zinazoathiri ukuaji wa sekta ndogo ya maziwasambamba na kuzingatia masuala mtambuka kama usawa wa kijinsia na lishe bora kwa maendeleo endelevu ya sekta hiyo.

Ametoa wito kwa wadau wote kuendelea kushirikiana katika kutatua changamotozinazoikabili sekta ndogo ya maziwa na kutumia kikamilifu fursa zinazotolewakupitia mradi wa TI3P pamoja na huduma za TADB.

SANGU: TUTAENZI MCHANGO WA WAKILI SWAI

May 29, 2026 Add Comment

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Ajira na Mahusiano Mhe. Deus Sangu leo ameongoza watumishi, mawakili na wananchi kumuaga aliyekuwa mtumishi wa Ofisi hiyo, marehemu Wakili Msomi Charles Boaz Swai aliyefariki jana jijini Dodoma.

MIAKA 18 BAADAYE:JK AKUTANA TENA NA CATHERINE,BINTI ALIYEFANYIWA UPASUAJI WA MOYO AKIWA NA MIAKA MINNE

May 29, 2026 Add Comment




Rais mstaafu wa Awamu ya Nne Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, leo Mei 29, 2026 amekutana tena na Bi. Catherine P. Conrad Minja, aliyefanyiwa upasuaji wa moyo kwa mafanikio akiwa na umri wa miaka minne katika taasisi ya  Muhimbili Orthopaedic Institute  (MOI) miaka 18 iliyopita.


Wakati huo madaktari bingwa wa Moyo wa Taasisi ya Moyo ya JKCI walikuwa wakitumia majengo ya MOI kabla jengo lao halijakamilika.


Mara ya kwanza wawili hao walikutana Novemba 14, 2008 wakati Dkt. Kikwete akiwa Rais alipokwenda kumjulia hali Catherine  hapo MOI baada ya kufanyiwa upasuaji wa moyo mapema wiki hiyo. Wakati huo Catherine alikuwa mmoja wa wagonjwa wa mwanzo kufanyiwa upasuaji huo katika taasisi hiyo.


Miaka 18 baadaye, Catherine amekua na sasa ni mwanafunzi wa mwaka wa kwanza wa Shahada ya Udaktari katika Chuo Kikuu cha Kairuki  jijini Dar es salaam.


Alifika ofisini kwa Rais Mstaafu kumsabahi na kumshukuru kwa mchango wake katika kuanzisha na kuimarisha huduma za matibabu ya magonjwa ya moyo nchini.


Dkt. Kikwete alimpongeza Catherine kwa kutimiza ndoto yake ya kusomea udaktari, jambo ambalo aliahidi kulifanya alipokuwa mtoto. Alisema amefurahishwa kumuona akiwa mwenye afya njema na akijiandaa kulitumikia taifa kupitia taaluma ya tiba.


Kwa upande wake, Catherine alisema anatamani kuwa Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Moyo ili kuwasaidia wagonjwa wenye changamoto kama aliyowahi kupitia yeye mwenyewe, akieleza kuwa hiyo itakuwa ni moja ya njia ya kumshukuru Mungu kwa zawadi ya maisha na afya njema.

Kipangula Asisitiza Weledi Katika Uandishi wa Habari

May 29, 2026 Add Comment

 

Na Mwandishi Wetu

DAR ES SALAAM — Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema uhuru wa uhariri ni nguzo muhimu katika taaluma ya habari na unapaswa kulindwa ili vyombo vya habari viweze kutekeleza majukumu yake kwa weledi, uwajibikaji na kwa maslahi ya umma.

Akizungumza Mei 26, 2026 katika mahojiano maalum yaliyofanyika katika Ofisi za JAB jijini Dar es Salaam, Wakili Kipangula alisema hakuna mtu anayepaswa kuingilia maamuzi ya uhariri wa chombo cha habari, awe ni chanzo cha taarifa, mmiliki wa chombo, mwanasiasa au mtu mwingine yeyote mwenye maslahi binafsi.

Alisema uhuru huo unapaswa kuendana sambamba na uwajibikaji wa kitaaluma, huku akisisitiza kuwa maadili ya taaluma ya habari yanamtaka mwandishi kufanya kazi kwa uadilifu, bila upendeleo na kuhakikisha taarifa zote zinathibitishwa kabla ya kuchapishwa au kurushwa.

“Ukweli ndio mlinzi wa taaluma ya habari. Mwandishi anatakiwa kutoa taarifa ambazo amezithibitisha na ana uhakika nazo kwa sababu jamii inategemea kupata taarifa sahihi na kwa wakati ili iweze kufanya maamuzi sahihi kuhusu masuala mbalimbali ya maendeleo,” amesema Wakili Kipangula.

Aidha, alisema waandishi wa habari wana nafasi kubwa katika kujenga jamii yenye uelewa, mshikamano na maendeleo, hivyo ni muhimu kutumia uhuru wa habari kwa kuzingatia sheria, maadili ya taaluma pamoja na kuheshimu haki na uhuru wa wengine kwa mujibu wa Katiba na sheria za nchi.

Kwa upande wake, Mhariri Mtendaji wa Gazeti la Jamhuri, Bw. Deodatus Balile, alisema uhuru wa vyombo vya habari utakuwa na maana halisi pale vyombo hivyo vitakapokuwa na uwezo wa kiuchumi wa kujiendesha bila kutegemea ushawishi wa nje.

“Uhuru wa vyombo vya habari utakuwa uhuru wa kweli pale vyombo vya habari vitakapokuwa na nguvu ya kiuchumi,” amesema Balile.

TBS YAFUNGUA MILANGO YA MASOKO KWA VIJANA WABUNIFU

May 29, 2026 Add Comment

Shirika la Viwango Tanzania (TBS) limeendelea kuonesha nafasi yake katika kuchochea maendeleo ya viwanda na kukuza ubunifu wa vijana kwa kutoa elimu ya viwango na ubora wa bidhaa katika Maonesho ya Fursa za Kazi na Ubunifu kwa Vijana (Career Fair 2026), hatua inayolenga kuwajengea vijana uwezo wa kuzalisha bidhaa zenye ushindani katika soko la ndani na kimataifa.

KABUDI AIPONGEZA MAMLAKA YA KUDHIBITI DAWA ZA KULEVYA KWA MAFANIKIO YA 2025

May 29, 2026 Add Comment
WAZIRI wa Nchi,Ofisi ya Waziri Mkuu(Sera,Bunge,Uratibu na Wenye Ulemavu) Profesa Palamagamba Kabudi ameta taarifa ya hali ya dawa za kulevya kwa mwaka 2025 ambapo inaonesha namna Serikali ya Awamu ya Sita, chini ya uongozi wa Dkt. Samia Suluhu Hassan, ilivyowekeza na kuweka nguvu kubwa katika mapambano dhidi ya dawa za kulevya.

ORXY YAFUNGUA FURSA MPYA ZA KIUCHUMI KARATU

May 29, 2026 Add Comment
UWEKEZAJI wa ndani umeendelea kupewa msukumo nchini kufuatia juhudi za Serikali za kuboresha mazingira ya biashara, huku uzinduzi wa kituo cha mafuta cha Orxy Karatu ukitajwa kuwa sehemu ya utekelezaji wa maono ya kukuza uchumi jumuishi chini ya uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan.

RAIS SAMIA APOKEA TAARIFA YA SENSA YA WANYAMAPORI ILIYOFANYIKA NCHI NZIMA MWAKA 2024 – 2025

May 29, 2026 Add Comment

 




Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akizungumza wakati wa kikao cha kupokea Taarifa ya Sensa ya Wanyamapori iliyofanyika nchi nzima mwaka 2024 – 2025 iliyowasilishwa na Waziri wa Maliasili na Utalii Dkt. Ashatu Kijaji, tarehe 29 Mei, 2026 Ikulu Dar es Salaam.



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye kikao cha kupokea Taarifa ya Sensa ya Wanyamapori iliyofanyika nchi nzima mwaka 2024 – 2025 iliyowasilishwa na Waziri ya Maliasili na Utalii Dkt. Ashatu Kijaji kupitia Taasisi ya Utafiti wa Wanyamapori Tanzania (TAWIRI), tarehe 29 Mei, 2026 Ikulu Dar es Salaam.




CAREER FAIR 2026 YATUMIKA KUWAKUTANISHA VIJANA NA FURSA ZA AJIRA NA BIASHARA

May 29, 2026 Add Comment
NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

SERIKALI imewataka vijana nchini kutumia ubunifu, ujuzi na teknolojia kama nyenzo muhimu za kuchochea ukuaji wa biashara, viwanda na ajira, ikisisitiza kuwa maendeleo ya uchumi wa taifa yanategemea uwekezaji katika rasilimali watu wenye maarifa ya vitendo na uwezo wa kuzalisha thamani.
MAKAMU WA RAIS AONGOZA WAOMBOLEZAJI MAZISHI YA MAREHEMU BI SUZANA MAGUFULI

MAKAMU WA RAIS AONGOZA WAOMBOLEZAJI MAZISHI YA MAREHEMU BI SUZANA MAGUFULI

May 29, 2026 Add Comment




Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi, amemwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika Mazishi ya Marehemu Bi. Suzana Ngolo Magufuli, ambaye ni Mama wa aliyekuwa Rais wa Awamu ya Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Hayati Dkt. John Pombe Magufuli, yaliyofanyika Kilimani, Chato mkoani Geita.

Akitoa salamu za rambirambi mara baada ya kumalizika kwa Ibada ya kumuombea Marehemu Bi. Suzana Ngolo Magufuli, Makamu wa Rais amesema Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ameguswa na msiba huo na anatoa salamu za pole kwa familia, ndugu jamaa na marafiki na wote walioguswa na msiba huo.

Makamu wa Rais amewasihi Watanzania kumtumia marehemu Bi. Suzana Ngolo Magufuli kama kielelezo cha malezi ya watoto, malezi ya maadili na uzalendo kwa kuwafanya watoto kutanguliza maslahi ya Taifa mbele na kuwa tayari kutumikia Taifa kwa nafasi yeyote wanayopewa. Ameongeza kwamba namna bora ya kumuenzi marehemu Bi. Suzana Ngolo Magufuli ni kuiga mfano wa malezi bora na mema ya watoto.

Amesema msiba wa Bi. Suzana Ngolo Magufuli unafundisha kuwa alikuwa sehemu kuu ya malezi ya Hayati Rais Dkt. John Magufuli ambaye alitoa mchango mkubwa katika utumishi wa nchi yetu. Amesema kitendo cha wananchi wengi kutoa salamu za rambirambi kupitia mitandao ya kijamii ni ishara ya Watanzania kuguswa na Maisha ya Hayati Magufuli ambaye alitumikia nchi kwa uzalendo wa hali ya juu.

Halikadhilika, Makamu wa Rais amemuelezea hayati Dkt. John Pombe Magufuli, kama kiongozi aliyejitoa kutetea nchi pamoja na kuwa na utashi wa kujua wajibu wa kulea watu wengine na kuwafanya kuwa Viongozi wa Taifa baadaye. Ameongeza kwamba kujitoa na kufanya matendo mema kwaajili ya wengine ni matunda ya baadaye kwa mtu na familia yake.

Akitoa salamu za shukrani kwa niaba ya familia Bw. Simon Nyahinga amesema familia hiyo inamshukuru kwa dhati kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa upendo mkubwa, huruma, faraja na mchango wake mkubwa aliyouonesha wakati wa kuugua kwa Bi Suzana Magufuli. Amesema tangu kufariki kwa Hayati Dkt. John Magufuli, Rais Samia ameendelea kusimama pamoja na familia katika kipindi chote cha matibabu.

Aidha, amewashukuru Viongozi wakuu wa Kitaifa na Viongozi wakuu wastaafu kwa msaada waliyotoa na kuifariji familia wakati wa matibabu ya Bi Suzana Magufuli pamoja na wakati wa msiba. Pia ameishukuru Serikali kwa kubeba jukumu ya kugharamia shughuli zote za msiba huo.

Ibada ya kumuaga na kumuombea Marehemu Bi. Suzana Magufuli imeongozwa na Askofu Mkuu wa Jimbo Katoliki Mwanza Mhashamu Renatus Nkwande na kuhudhuriwa na Maaskofu mbalimbali, Mapadre, Viongozi mbalimbali, Viongozi Wakuu wastaafu, pamoja na wananchi mbalimbali.

Bi Suzana Magufuli amezikwa katika makaburi ya familia ya Magufuli , Kilimani Wilayani Chato.





TBS YATAKIWA KUSHIRIKIANA NA TRA KUONDOA KERO ZA MIFUMO YA VIBALI KWA SHEHENA ZINAZOINGIA NCHINI

TBS YATAKIWA KUSHIRIKIANA NA TRA KUONDOA KERO ZA MIFUMO YA VIBALI KWA SHEHENA ZINAZOINGIA NCHINI

May 29, 2026 Add Comment

Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe. Judith  Kapinga (Mb), ameliagiza Shirika la Viwango Tanzania (TBS) kushirikiana kikamilifu na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) pamoja na Taasisi nyingine husika katika kushughulikia na kuondoa kero zote zinazosababishwa na mifumo ya utoaji vibali kwa shehena zinazoingia nchini.

Waziri Kapinga ametoa agizo hilo akiwa ameambatana na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Balozi Waziri Salum alipokutana na Mkurugenzi Mkuu wa TBS, Dkt. Ashura Katunzi na ujumbe wake Mei 29, 2026 katika ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam, kufuatia kuibuka kwa changamoto zilizojitokeza wakati wa kuunganisha mfumo wa TANeSW wa TRA na mfumo wa OAS wa TBS na kusababisha usumbufu kwa baadhi ya wafanyabiashara.

Aidha, Waziri Kapinga amepongeza jitihada zinazoendelea kuchukuliwa baina ya TBS pamoja na TRA katika kuunganisha mifumo ya kielektroniki ili kurahisisha taratibu na kuongeza ufanisi wa utoaji wa vibali kwa shehena za mizigo inayoingia nchini.

DKT. MWIGULU AIPONGEZA TADB KWA KUINUA WAKULIMA, WAFUGAJI NA WAVUVI

May 28, 2026 Add Comment
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba ameipongeza Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) kwa mchango wake katika kuwawezesha wakulima, wafugaji na wavuvi kupitia utoaji na usimamizi wa mikopo, hatua aliyoeleza kuwa inaendelea kuchochea maendeleo ya sekta za uzalishaji na ukuaji endelevu wa uchumi wa Taifa.
 MAKAMU WA RAIS AWASILI CHATO – KUMWAKILISHA RAIS MAZISHI YA BI SUZANA MAGUFULI

MAKAMU WA RAIS AWASILI CHATO – KUMWAKILISHA RAIS MAZISHI YA BI SUZANA MAGUFULI

May 28, 2026 Add Comment




Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi akisaini kitabu cha maombolezo kufuatia kifo cha Bi. Suzana Magufuli ambaye ni Mama wa aliyekuwa Rais wa Awamu ya Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Hayati Dkt. John Pombe Magufuli, wakati alipowasili Kilimani Wilayani Chato leo tarehe 29 Mei 2026 Wilayani Chato.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi akiwafariji wa watoto wa marehemu Bi. Suzana Magufuli ambaye ni Mama wa aliyekuwa Rais wa Awamu ya Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Hayati Dkt. John Pombe Magufuli, wakati alipowasili Kilimani Wilayani Chato leo tarehe 29 Mei 2026 Wilayani Chato.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi akimfariji Mama Janeth Magufuli, kufuatia kifo cha marehemu Bi. Suzana Magufuli ambaye ni Mama wa aliyekuwa Rais wa Awamu ya Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Hayati Dkt. John Pombe Magufuli, wakati alipowasili Kilimani Wilayani Chato leo tarehe 29 Mei 2026 Wilayani Chato.



Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi akizungumza na Waziri Mkuu Mstaafu Mhe. Kassim Majaliwa, wakati alipowasili Kilimani Wilayani Chato, katika msiba wa marehemu Bi. Suzana Magufuli ambaye ni Mama wa aliyekuwa Rais wa Awamu ya Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Hayati Dkt. John Pombe Magufuli, leo tarehe 29 Mei 2026 Wilayani Chato.



Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi akiwasili katika Uwanja wa Ndege wa Geita, Wilayani Chato leo tarehe 28 Mei 2026. Makamu wa Rais anatarajiwa kumwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Mazishi ya Marehemu Bi. Suzana Magufuli ambaye ni Mama wa aliyekuwa Rais wa Awamu ya Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Hayati Dkt. John Pombe Magufuli, yatakayofanyika tarehe 29 Mei 2026 Wilayani Chato.

…………

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi amewasili Chato Mkoani Geita, ambapo anatarajiwa kumwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika Mazishi ya Marehemu Bi. Suzana Magufuli ambaye ni Mama wa aliyekuwa Rais wa Awamu ya Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Hayati Dkt. John Pombe Magufuli, yatakayofanyika tarehe 29 Mei 2026 Wilayani Chato.

Makamu wa Rais amepokelewa katika Uwanja wa Ndege Geita, Wilayani Chato, Mapokezi yaliyoongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhe. Martin Shigela, Viongozi wa Kamati ya Ulinzi na Usalama, Viongozi wa Chama Cha Mapinduzi pamoja na Viongozi mbalimbali Waandamizi.

Pia Makamu wa Rais, amefika nyumbani kwa marehemu, Kilimani Chato kusaini kitabu cha maombolezo pamoja na kuwafariji wafiwa kufuatia msiba huo.

Imetolewa na
Ofisi ya Makamu wa Rais
28 Mei 2026
Chato, Geita.

JAJI MWAMBEGELE AWAPA NENO MAKARANI WA UCHAGUZI ISIMANI

May 28, 2026 Add Comment



Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Jaji wa Mahakama ya Rufaa Mhe.Jacobs Mwambegele akizungumza wakati alipotembelea mafunzo ya siku moja kwa Makarani waogozaji Wapiga Kura katika Jimbo la Isimani yaliyofanyika katika Shule Sekondari Ufundi Ifunda mkoani Iringa ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya Uchaguzi huo utakaofanyika Jumatatu ya Juni 1, 2026.





Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Jaji wa Mahakama ya Rufaa Mhe.Jacobs Mwambegele akizungumza wakati alipotembelea mafunzo ya siku moja kwa Makarani waogozaji Wapiga Kura katika Jimbo la Isimani yaliyofanyika katika Shule Sekondari Ufundi Ifunda mkoani Iringa ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya Uchaguzi huo utakaofanyika Jumatatu ya Juni 1, 2026.


Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Jaji wa Mahakama ya Rufaa Mhe.Jacobs Mwambegele amewataka watendaji wa uchaguzi ambao ni Makarani waongozaji Wapiga kura kufanya kazi yao kwa kufuata Sheria, Kanuni na utaratibu wakati wa uchaguzi Mdogo wa Ubunge katika Jimbo la Isimani Mkoani Iringa na Kata 12 za Tanzania Bara.

Jaji Mwambegele ameyasema hayo wakati akitembelea mafunzo ya siku moja kwa Makarani hao waogozaji katika Jimbo la Isimani yaliyofanyika katika Shule Sekondari Ufundi Ifunda mkoani Iringa ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya Uchaguzi huo utakaofanyika Jumatatu ya Juni 1, 2026.

Jaji Mwambegele pia amewasisistiza watendaji hao kuishi kwenye viapo vyao wakati wa utekelezaji majukumu yao ya Uchaguzi ili kujiepusha na upendeleo wa aina yoyote.

Kwa upande wake mwenyekiti wa Mafunzo hayo ya Makarani Waongozaji Wapiga Kura Vituoni Bw. Baraka Matonya amemuhakikishia Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi kwamba watafuata sheria, kanuni, miongozo na maelekezo ya Tume wakati wote wa Utekelezaji wa majukumu yao ya Uchaguzi .

Naye Msimamizi wa Uchaguzi wa Jimbo la Isimani,Bi. Caroline Otieno amesema maandalizi ya uchaguzi huo Mdogo wa Jimbo hilo, yamekamilika kwa asilimia 100 ambapo vifaa vyote vimepokelewa.

Uchaguzi huo utafanyika sambamba na uchaguzi mdogo katika kata 12 za Tanzania Bara ambazo ni Mzimuni iliyopo Manispaa ya Kinondoni; Zongomera, Manispaa ya Kahama; Itilo, Halmashauri ya Mji wa Nzega; Ketare, Halmashauri ya Mji wa Tarime na Nyumbigwa, Halmashauri ya Mji wa Kasulu.

Nyingine ni kata ya Kala iliyoko Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi; Ziba, Halmashauri ya Wilaya Igunga; Kamsisi, Halmashauri ya Wilaya ya Mlele; Nyamugali, Halmashauri ya wilaya ya Buhigwe; Namasakata Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru; Bwongera, Halmashauri ya Wilaya ya Chato na Kibiti Halmashauri ya Wilaya ya Kibiti.





Sehemu ya washiriki wa mafunzo hayo wakimsikiliza Mwenyekiti wa Tume.

Mratibu wa Uchaguzi Mkoa wa Iringa Bi. Nuru Sovella akizungumza wakati wa mafunzo hayo.
Sehemu ya washiriki wa mafunzo hayo wakimsikiliza Mwenyekiti wa Tume.

Sehemu ya washiriki wa mafunzo hayo wakimsikiliza Mwenyekiti wa Tume.

Msimamizi wa Uchaguzi wa Jimbo la Isimani,Bi. Caroline Otieno akizungumza na kusema kua maandalizi ya uchaguzi huo Mdogo wa Jimbo hilo, yamekamilika kwa asilimia 100 ambapo vifaa vyote vimepokelewa.