HABARI

SIASA

ELIMU

Recent Posts

BARRICK KUENDELEZA FURSA SAWA KWA WANAWAKE KATIKA SEKTA YA MADINI

March 06, 2026 Add Comment

 

Wahitimu wa Programu ya Mwanamke wa wakati ujao ya ATE (Female Future Programme) kutoka Barrick North Mara katika picha ya pamoja , kuanzia kushoto, Patricia Vulla , Elda Mahenda, Sella Mwaigomole, Edith Dickson Biita na Noela Mataro katika mahafali yaliyofanyika katika ukumbi wa Mlimani City.
Wahitimu wa Programu ya Mwanamke wa wakati ujao ya ATE (Female Future Programme) kutoka Barrick North Mara katika picha ya pamoja , kuanzia kushoto, Patricia Vulla , Elda Mahenda, Sella Mwaigomole, Edith Dickson Biita na Noela Mataro katika mahafali yaliyofanyika katika ukumbi wa Mlimani City.
Wahitimu kutoka Barrick North Mara Noela Mataro na Edith Dickson Biita wakiwa kwenye picha ya pamoja baada ya kuhitimu mafunzo yao ya uongozi
Baadhi ya wahitimu wakifuatilia hotuba mbalimbali katika siku hiyo ya mafahali yaliyofanyika jijini Dar es Salaam
Mgeni rasmi kwenye mahafali hayo , Spika wa Bunge la Tanzania , Musa Hassan Zungu akiwa kwenye picha ya pamoja na viongozi wa Chama cha Waaajiri Tanzania (ATE) na wahitimu wa mafunzo hayo
Mgeni rasmi kwenye mahafali hayo , Spika wa Bunge la Tanzania , Musa Hassan Zungu akiwa kwenye picha ya pamoja na viongozi wa Chama cha Waaajiri Tanzania (ATE) na wahitimu wa mafunzo hayo

**

#Wafanyakazi wake Wanawake wajengewa uwezo kupitia Female Future Programme

Katika kuelekea kilele cha maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani 2026 yakiendelea,kampuni ya Barrick nchini yenye ubia na serikali kupitia Kampuni ya Twiga Minerals, imeendeleza dhamira yake ya kuhakikisha Wanawake wanapewa fursa sawa katika ushiriki wa mnyororo wa sekta ya madini ambapo imewawezesha wafanyakazi wake wanawake watano kupata mafunzo uongozi kupitia programu ya Mwanamke wa Wakati Ujao (Female Future Programme) yanayotolewa na Chama cha Waajiri Tanzania (ATE) inayolenga kuboresha ufanisi wa wafanyakazi wa kike mahali pa kazi.

NAIBU WAZIRI SALOME AZUNGUMZA NA WAFANYAKAZI TANESCO MKOA WA KIGOMA

March 06, 2026 Add Comment


📌 *Awapongeza kwa kazi nzuri*


📌*Ataka waongeze kasi ya kuunganisha wateja na kuhamasisha nishati safi ya kupikia*


Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba amekutana na kufanya mazungumzo na Wafanyakazi wa TANESCO Mkoa wa Kigoma ambapo pamoja na kuwapongeza kwa kazi nzuri wanayofanya amewataka kuongeza nguvu katika utekelezaji wa mipango ya Serikali ya kuboresha huduma za nishati.

Mhe. Salome ametoa pongezi hizo tarehe 6 Machi 2026 wilayani Kigoma, Mkoa wa Kigoma akiwa kwenye ziara ya kikazi ya kukagua miradi mbalimbali ya nishati.


" Waziri wa Nishati pamoja na viongozi wengine wanatambua mchango wenu katka sekta ya umeme,  hata hivyo mnapaswa kuongeza kasi ya kuunganishia umeme wateja ili tuweze kufikia pia lengo la mpango wa misheni 300 linalotutaka kuunganiaha wateja wapya milioni 8 ifikapo 2030." Amesema Mhe.Salome

Aidha, amesema katika kuongeza kasi ya usambazaji wa umeme, TANESCO Kigoma itapokea gari la kunyanyulia mizigo (crane) litakalosaidia katika utekelezaji wa kazi za kiufundi na kuimarisha huduma za umeme.


Vilevile, Mhe. Salome ameitaka TANESCO  kuhakikisha kuwa wananchi wanaoishi katika maeneo ambayo ni lazima kuvuka kwa kutumia boti iwanafikiwa kwa kutenga bajeti ya kununua boti maalum kwa ajili ya kazi za kufuatilia miradi na usambazaji umeme.

Pia amewahimiza watendaji TANESCO  kuwa wabunifu na  kuendelea kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia kwa wananchi ili kupunguza matumizi ya kuni na mkaa, ikiwa ni pamoja na kupeleka elimu hiyo katika maeneo ya masoko, stendi na maeneo mengine ya mikusanyiko ya watu.


Awali, Meneja wa TANESCO Mkoa wa Kigoma, Mhandisi Hassan Nganjau alisema mkoa huo sasa unapata umeme wa uhakika kupitia gridi ya Taifa ambapo mahitaji ya juu ya umeme ni megawati 27.

Alieleza kuwa, awali mkoa huo ulikuwa ukizalisha umeme kwa kutumia majenereta, hali iliyosababisha kuwepo kwa mgao wa umeme katika baadhi ya nyakati. Hata hivyo, baada ya kuunganishwa na gridi ya Taifa, upatikanaji wa umeme umeimarika na sasa umeme ni wa uhakika.


Alisema uwepo wa umeme wa gridi umepelekea Serikali kuokoa takribani shilingi bilioni 58 kwa mwaka zilizokuwa zikitumika kwa ununuzi wa mafuta na matengenezo ya vipuri vya majenereta.


Vilevile alisema kutokana na upatikanaji huo wa umeme wa uhakika, TANESCO imeweza kuunganisha wateja wengi wakiwemo wa viwanda na pia kuvutia wawekezaji katika sekta mbalimbali.

"Katika  mwaka huu wa fedha, TANESCO Kigoma tumeweza  kuunganisha wateja 23,224 na kuvuka lengo la kuunganisha wateja 16,000." Alisema Mhandisi Nganjau


Kwa upande wa vijiji alisema vijiji vyote 306 vya Mkoa wa Kigoma tayari vina umeme. Aidha, kati ya vitongoji 1,858, vitongoji 1,436 tayari vina umeme huku wakandarasi wakiendelea na kazi ya kusambaza umeme katika vitongoji 316. Lengo ni kuhakikisha ifikapo mwaka 2030 vitongoji vyote vinakuwa vimefikiwa na umeme.

 


Katika ziara yake mkoani Kigoma, Naibu Waziri wa Nishati ameambatana na Mwakilishi wa Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati ( Umeme na Nishati Jadidifu), Mhandisi Edson Ngabo.

NAIBU WAZIRI SALOME AANZA ZIARA YA KIKAZI KIGOMA

March 06, 2026 Add Comment


Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba ameanza ziara ya kikazi ya siku mbili mkoani Kigoma inayolenga kukagua miradi mbalimbali ya umeme ikiwemo mradi wa Malagarasi utakaozalisha megawati 49.5.

Kabla ya kuanza ziara hiyo amekutana Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, Dkt. Rashid  ChuaChua ambapo amepongeza Mkoa wa Kigoma kwa kusimamia miradi ya nishati kwa ufanisi.

Pia ametoa wito kwa viongozi wa Mkoa huo kuendelea kuweka mkazo katika kusukuma ajenda ya nishati safi ya kupikia na nishati safi kwa ujumla.


 Naye, Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, Dkt. Rashid Chuachua amesema mkoa huo unaendelea kusimamia kwa ukaribu miradi ya nishati hususan ya umeme vitongojini.

Kwa upande wake,  Katibu Tawala wa Wilaya ya Kigoma, Mganwa Nzota  amesema Mkoa wa Kigoma imekuwa ni mnufaika mkubwa wa mageuzi ya kinishati yanayoendelea kufanyika hasa baada ya mkoa huo kupata umeme wa gridi ambao umefanya umeme kuwa wa uhakika.



DC NYAMWESE AWAPA SOMO WANAWAKE HANDENI MJI MATUMIZI YA SIMU JANJA KIBIASHARA

DC NYAMWESE AWAPA SOMO WANAWAKE HANDENI MJI MATUMIZI YA SIMU JANJA KIBIASHARA

March 06, 2026 Add Comment
 

Na Mwandishi Wetu, Handeni

Wanawake katika Halmashauri ya Mji Handeni wametakiwa kutumia simu janja na teknolojia ya kidijitali kwa kuwa ni nyenzo muhimu ya kukuza biashara na kujikwamua kiuchumi kupitia fursa mbalimbali zinazopatikana mtandaoni.

 Mkuu wa Wilaya ya Handeni, Mhe. Salum Nyamwese ameyasema hayo wakati akizindua Jukwaa la Uwezeshaji Wanawake Kiuchumi katika kongamano la wanawake lililofanyika mjini Handeni.

Amesema matumizi sahihi ya simu janja yanaweza kuwasaidia wanawake kupanua masoko ya biashara zao kupitia mitandao ya kijamii pamoja na kupata taarifa muhimu za fursa za kiuchumi zinazotolewa na serikali.

Nyamwese amesema jukwaa hilo limekuja wakati muafaka kutokana na juhudi za serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan katika kuwawezesha kiuchumi wanawake na wasichana.

“Jukwaa hili litawawezesha kupata fursa na kujadiliana namna ya kujikwamua. Mtapata mbinu mbalimbali za kuongeza thamani ya biashara zenu na namna ya kuzifikia fursa zinazotolewa na serikali ikiwamo mikopo ya asilimia 10 inayotolewa na halmashauri,” amesema.

Aidha, amewasisitiza wanawake kuwa wabunifu katika biashara zao na kutumia kikamilifu teknolojia pamoja na mikopo inayotolewa na halmashauri ili kujiongezea kipato.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Handeni, Maryam Ukwaju amesema halmashauri imeandaa mkakati wa kusaidia vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu kujiunga kwenye mfumo wa ununuzi wa umma wa NeST ili viweze kunufaika na fursa ya asilimia 30 ya zabuni zinazotolewa kwa makundi hayo.

Amesema kupitia mfumo huo vikundi vitapata nafasi ya kushiriki kikamilifu katika zabuni zinazotangazwa na halmashauri na hivyo kuongeza kipato na kukuza uchumi wao.

Akizungumza kuhusu kongamano hilo, Mkurugenzi huyo amesema katika kongamano hilo wanawake walipata elimu mbalimbali ikiwamo masuala ya fedha, msaada wa kisheria, umiliki wa ardhi pamoja na masuala ya ndoa ili kuwajengea uelewa na kuwasaidia kuwa chachu ya maendeleo ya Handeni.

Aliongeza kuwa elimu hiyo pia inalenga kuwawezesha wanawake kushiriki kikamilifu katika kufikia malengo ya maendeleo ya Taifa yaliyowekwa katika Dira ya Maendeleo ya mwaka 2050.

Akisoma taarifa ya uendeshaji wa shughuli za majukwaa ya uwezeshaji wananchi kiuchumi, Mratibu wa majukwaa hayo, Carin Umwambe amesema jukwaa hilo linalenga kuwaunganisha wanawake wajasiriamali na watoa huduma katika sekta za umma na binafsi ili waweze kupata fursa mbalimbali za kiuchumi na kibiashara.

MATUMIZI YA NISHATI SAFI YAPUNGUZA UKATAJI WA MITI MVOMERO

March 05, 2026 Add Comment




Na Mwandishi Wetu,


Wananchi wa Mvomero wamesema kuwa utekelezaji wa agizo la Serikali la kuhamasisha matumizi ya nishati safi umeanza kuleta matokeo chanya, ikiwemo kupungua kwa ukataji wa miti na uchomaji wa mkaa katika baadhi ya maeneo.


Hayo yameelezwa na baadhi ya wananchi wa Wilaya ya Mvomero wakati wa ziara ya timu kutoka Wizara ya Nishati kwa kushirikiana na Mfuko wa Maendeleo ya Mitaji wa Umoja wa Mataifa (UNCDF), iliyofika wilayani humo kutoa elimu kuhusu umuhimu wa matumizi ya nishati safi ya kupikia. 

Kampeni hiyo imefanyika katika maeneo mbalimbali ya Mkoa wa Morogoro kwa lengo la kuhamasisha matumizi ya nishati salama.

Wameeleza kuwa wananchi wengi sasa wameanza kuhamia katika matumizi ya gesi na umeme kwa ajili ya kupikia, jambo linalowasaidia kuokoa muda katika shughuli zao za kila siku pamoja na kujikinga na madhara ya kiafya yanayotokana na moshi wa kuni na mkaa.

Katika kampeni hiyo, wananchi wamepata fursa ya kushuhudia maonesho ya matumizi ya majiko ya gesi na umeme, ambapo walioneshwa jinsi yanavyoweza kupika chakula kwa haraka, kwa gharama nafuu na kuhifadhi ubora pamoja na ladha ya chakula. Hali hiyo imeongeza mwitikio wa wananchi wengi kuanza kutumia nishati safi ya kupikia.



TBA YASHIRIKI KLINIKI YA KUTATUA KERO ZA WANANCHI DODOMA

TBA YASHIRIKI KLINIKI YA KUTATUA KERO ZA WANANCHI DODOMA

March 05, 2026 Add Comment

Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) Mkoa wa Dodoma unashiriki katika Kliniki maalum ya kutatua kero na changamoto mbalimbali za wananchi iliyoandaliwa na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, inayofanyika tarehe 3 hadi 6 Machi, 2026 katika viwanja vya Nyerere Square jijini Dodoma.

Kupitia kliniki hiyo, TBA inakutana na wateja wake ambao ni wapangaji wa nyumba zake kwa lengo la kusikiliza na kutatua changamoto pamoja na kero mbalimbali zinazojitokeza katika maeneo wanayoishi.

Aidha, kliniki hiyo imekuwa fursa kwa taasisi mbalimbali za Serikali kutoa elimu kwa wananchi pamoja na kueleza mafanikio yaliyopatikana katika utekelezaji wa majukumu yao ndani ya siku 100 za Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan tangu kuingia madarakani.

Katika kliniki hiyo, TBA kama zilivyo taasisi nyingine za Serikali imeweka banda maalum kwa ajili ya kutoa elimu kwa wananchi kuhusu majukumu yake pamoja na kueleza miradi mbalimbali iliyotekelezwa na wakala huo katika kipindi hicho.

Akitembelea mabanda ya taasisi mbalimbali katika viwanja hivyo leo Machi 5, 2026, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Mhe. Rosemary Senyamule, ameipongeza TBA kwa kutekeleza miradi mikubwa ya Serikali katika mkoa wa Dodoma, ikiwemo ujenzi wa Mji wa Serikali Mtumba pamoja na mradi wa ujenzi wa nyumba 3,500 za makazi ya watumishi wa umma katika eneo la Nzuguni.

Kwa upande wao, wananchi waliotembelea banda la TBA wamepongeza utekelezaji wa mradi wa nyumba za makazi katika eneo la Nzuguni, wakisema umechangia kusogeza huduma za kijamii na biashara karibu na wananchi pamoja na kuimarisha hali ya ulinzi na usalama katika eneo hilo.

WAZIRI NDEJEMBI AKUTANA NA CHAMA CHA WAAGIZAJI NA WASAMBAZAJI WA MAFUTA TAOMAC

March 05, 2026 Add Comment


Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi, amekutana na kufanya mazungumzo na Chama cha Waagizaji na Wasambazaji wa Mafuta Tanzania (TAOMAC) kwa lengo la kuboresha na kukuza sekta ya mafuta nchini pamoja na kuimarisha ushirikiano kati ya Serikali na wadau wa sekta hiyo.

Kikao hicho kimefanyika leo, Machi 5, katika Ofisi Ndogo za Wizara ya Nishati zilizopo jijini Dar es Salaam.


Katika Kikao hicho wamejadili masuala mbalimbali yanayolenga kuimarisha usimamizi, ufanisi na maendeleo ya sekta ya mafuta nchini kwa manufaa ya uchumi na wananchi kwa ujumla.

Kikao hicho kimehudhuriwa na Kamishna wa Mafuta kutoka Wizara ya Nishati, Bw. Goodluck Shirima; Mtendaji Mkuu wa PBPA, Bw. Erasto Simon; Mkurugenzi Mkuu wa EWURA, Dkt. James Mwainyekule; pamoja na viongozi na wanachama wa TAOMAC.






MAKATIBU WAKUU VYAMA VYA UKOMBOZI WAJADILI HALI YA KISIASA KUSINI MWA AFRIKA

March 05, 2026 Add Comment


Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimeongoza Kikao cha 12 cha Makatibu Wakuu wa Vyama vya Ukombozi Kusini mwa Afrika, ambapo, pamoja na mambo mengine, vimejadili hali ya siasa, ukombozi wa kiuchumi na kuboresha hali za wananchi katika nchi zao. 

Kikao hicho kilichofanyika leo tarehe 5 Machi 2026, Kibaha, mkoani Pwani, kilihusisha Makatibu Wakuu wa Vyama 6 vya Ukombozi Kusini mwa Afrika, ambavyo ni ANC (Afrika Kusini), CCM (Tanzania), FRELIMO (Msumbiji), SWAPO (Namibia), ZANU-PF (Zimbabwe) na MPLA (Angola).

Akizungumza na vyombo vya habari baada ya mkutano huo, Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi, Asha-Rose Migiro, amesema kuwa katika kikao hicho wamepitia maazimio ya Mkutano Mkuu wa Wakuu wa Vyama hivyo uliofanyika mwaka jana, nchini Afrika ya Kusini. 

Alisema mijadala ilijikita kuangalia hali ya kisiasa katika ukanda wa Kusini mwa Afrika, hususan kulinda uhuru wa kisiasa na kiuchumi, kutathmini malengo ya harakati za ukombozi pamoja na kuendelea kulinda na kuimarisha uhuru uliopatikana.


Dkt. Migiro amesema jukumu kubwa la vyama hivyo ni kuimarisha mshikamano na umoja wao pamoja na kujadili changamoto mbalimbali zinazoikabili kanda hiyo ikiwemo mabadiliko ya tabianchi. Aidha, walijadili namna ya kutatua migogoro katika nchi wanachama na kuchochea maendeleo ya kiuchumi, kisiasa na kijamii.


Katika kikao hicho pia walifanya mapitio ya maendeleo yaliyopatikana katika nchi zao, ikiwa ni pamoja na kuimarisha huduma za jamii, kuboresha miundombinu pamoja na kuweka mikakati ya kujenga uchumi stahimilivu na kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi.

Masuala mengine yaliyojadiliwa ni pamoja na umuhimu wa kuongeza ajira kwa vijana, kuwawezesha wanawake pamoja na kujenga uchumi jumuishi na stahimilivu kwa maendeleo ya Ukanda wa Kusini mwa Afrika.


#Ends