HABARI

SIASA

ELIMU

Recent Posts

MHANDISI SAMAMBA :HATMA YA SEKTA YA MADINI IKO KWENYE UONGEZAJI THAMANI NDANI YA NCHI

December 17, 2025 Add Comment




✅️ _Asema Ndiyo Mwelekeo Mpya wa Sekta ya Madini_


✅️ _Asisitiza Sekta ya Madini Kutazamwa Kama Injini Mpya ya Uchumi wa Taifa_


✅️ _Ujenzi Jengo la Ghorofa 8 TGC Wafikia Asilimia 10_


📍*Arusha,*


Katibu Mkuu Wizara ya Madini Eng. Yahya Samamba amesisitiza mwelekeo na mkakati wa Serikali ni kuhakikisha madini yanayochimbwa hapa nchini yanaongezewa thamani ndani ya nchi, ikiwa ni nguzo muhimu ya kuongeza Mapato ya Taifa, Mchango wa Sekta katika Pato la Taifa (GDP), ajira na maendeleo ya mnyororo mzima wa thamani katika Sekta ya Madini.

Ametoa kauli hiyo leo Desemba 17, 2025 wakati akizungumza na Watumishi wa Tume ya Madini – Mkoa wa Kimadini Arusha pamoja na Kituo cha Jemolojia Tanzania (TGC) jijini Arusha.

Mhandisi Samamba amesema Serikali ina matarajio makubwa kupitia Sekta ya Madini, hususan katika kuhakikisha madini yanayozalishwa nchini yanaongezewa thamani kabla ya kuuzwa, hatua itakayoongeza mapato, kukuza viwanda vya ndani na kutoa fursa zaidi za ajira kwa Watanzania.

“Maelekezo ya Mhe. Rais Dkt.  Samia Suluhu Hassan ni lazima tuhakikishe value addition na beneficiation vinafanyika ndani ya nchi. Huu ndio mwelekeo wa Serikali katika kuhakikisha Sekta ya Madini inachangia kikamilifu uchumi wa Taifa, hii ni moja ya rasilimali tulizojaaliwa kwa wingi, lazima yachangie kukuza uchumi wetu kama taifa” amesisitiza Samamba.

Katika hatua nyingine, Katibu Mkuu ameeleza kuwa wachimbaji wadogo wataendelea kupewa kipaumbele, akibainisha kuwa kundi hilo ni moja ya mihimili muhimu wa Sekta ya Madini na lina mchango mkubwa katika uzalishaji na ukusanyaji wa maduhuli. Amesema Serikali itaendelea kuweka mazingira rafiki yatakayowawezesha wachimbaji wadogo kuongeza tija, ufanisi na mchango wao katika uchumi.

Akiwahimiza Watumishi wa Tume ya Madini na TGC, Eng. Samamba amesisitiza umuhimu wa utoaji wa huduma bora kwa wateja, akiwataka kuzingatia weledi, maadili ya utumishi wa umma na kuachana kabisa na vitendo vya rushwa. Vilevile amekemea matumizi ya lugha zisizoridhisha kwa wateja, akisisitiza kuwa lugha nzuri ni sehemu ya heshima, uwajibikaji na taswira chanya ya Serikali.

“Huduma bora kwa wateja, kuepuka rushwa na matumizi ya lugha inayojenga heshima ni msingi wa mafanikio ya Taasisi zetu na sekta kwa ujumla,” ameongeza Eng. Samamba.


Amehitimisha kwa kutoa wito kwa watumishi wote kuendelea kufanya kazi kwa bidii, ubunifu na uzalendo, ili Sekta ya Madini iendelee kuwa kichocheo cha maendeleo endelevu na uchumi jumuishi wa Tanzania.

Kwa upande wake Mratibu wa TGC Mhandisi Ally Maganga ameeleza kuwa ujenzi wa jengo la Kituo cha Jemolojia Tanzania (TGC) umefikia asilimia 10, akibainisha kuwa mradi huo ni sehemu ya mkakati wa Serikali wa kuimarisha mafunzo, utafiti na uongezaji thamani wa madini ya vito nchini.


Naye, Afisa Madini Mkazi wa Mkoa wa Arusha Francis Mihayo amesema kuwa mkoa wa Arusha unaendelea kuchukua hatua madhubuti kutekeleza maelekezo ya Serikali hususan kupitia usimamizi makini wa shughuli za uchimbaji, uchakataji na biashara ya madini. 


Amesema Ofisi ya Afisa Madini Mkazi itaendelea kushirikiana kwa karibu na wachimbaji wadogo, wawekezaji na taasisi za Serikali ikiwemo Tume ya Madini na Kituo cha Jemolojia Tanzania (TGC), ili kuhakikisha mazingira rafiki ya uwekezaji, ufuataji wa sheria na kanuni, pamoja na kukuza mchango wa sekta ya madini katika maendeleo ya kiuchumi ya mkoa na Taifa kwa ujumla.

WAZIRI MCHENGERWA AUONGOZA UJUMBE WA TANZANIA KWENYE UZINDUZI WA MKUTANO WA PILI WA DUNIA WA TIBA ASILI

December 17, 2025 Add Comment

Na John Mapepele, New Delhi

Waziri wa Afya, Mhe. Mohamed Omary Mchengerwa leo ameuongoza ujumbe wa Serikali ya Tanzania katika uzinduzi wa Mkutano wa pili wa dunia wa Tiba Asili unaoratibiwa na Shirika la Afya Duniani (WHO) kwenye ukumbi wa kimataifa wa Bharat Mandapam jijini New Delhi India.
JAFO:TUMUOMBEE RAIS SAMIA NA KULIOMBEA TAIFA LETU

JAFO:TUMUOMBEE RAIS SAMIA NA KULIOMBEA TAIFA LETU

December 17, 2025 Add Comment
 

Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo,akizungumza  na Wajumbe wa  Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kisarawe,kikao kilicholenga kuwashukuru wajumbe kwa mchango wao katika kufanikisha Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kuwashukuru kwa kuchaguliwa tena kuwa Mbunge wa jimbo hilo.

Na.Alex Sonna-KISARAWE

MBUNGE wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo, amewaomba wananchi wa Kisarawe na watanzania kwa ujumla kumuombea Rais, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwa ana maono makubwa ya kuwatumikia Watanzania na kulisukuma Taifa mbele kimaendeleo.

Dkt. Jafo ametoa kauli hiyo alipokuwa akizungumza katika kikao maalum cha Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kisarawe, kilicholenga kuwashukuru wajumbe kwa mchango wao katika kufanikisha Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kuwashukuru kwa kuchaguliwa tena kuwa Mbunge wa jimbo hilo.

“Niwaombe wajumbe wa Halmashauri Kuu kuhakikisha tunamuombea Rais Dkt. Samia kwa kuwa ana kazi kubwa ya kuwaletea maendeleo Watanzania na kuhakikisha Taifa letu linaendelea kusonga mbele,” amesema Dkt.Jafo

Ameongeza kuwa amani na usalama ni nguzo muhimu za maendeleo ya kiuchumi, hivyo ni wajibu wa kila Mtanzania kumuombea Rais na Taifa kwa ujumla.

“Bila amani na usalama, nchi yetu haiwezi kupata mafanikio ya kiuchumi. Nawaomba wananchi wa Kisarawe na Watanzania kwa ujumla tuendelee kumuombea Rais wetu na Taifa letu, kwa sababu kiongozi wetu mwenye maono ni Rais Samia, na lazima tumuombee ili nchi yetu iendelee kusonga mbele,” amesema Dkt. Jafo

Awali, amesema baada ya ushindi huo, chama na serikali vimeanza rasmi awamu mpya ya kazi kwa kipindi cha miaka 5, huku akiendelea na utekelezaji wa majukumu ya maendeleo jimboni kupitia mkakati wao wa ‘Chaka kwa chaka’.

“Tumeanza kazi kwa mara nyingine katika msimu wa 2025–2030. Tumeendelea na kazi za jimboni, tukikutana na viongozi wa kada mbalimbali wakiwemo viongozi wa kisiasa, watendaji wa halmashauri, madiwani pamoja na wenyeviti wa vijiji na vitongoji vya Wilaya ya Kisarawe,” amesema Dkt. Jafo.

Ameeleza kuwa kikao hicho na wajumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Wilaya ni cha muhimu sana kwa kuwa ni timu inayobeba jukumu la kuimarisha uhai wa chama pamoja na kusimamia utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM.

Aidha, Dkt. Jafo ametumia mkutano huo kueleza mikakati ya maendeleo ndani ya Wilaya ya Kisarawe, ikiwemo kuboresha sekta za afya, elimu, barabara, maji, umeme pamoja na ujenzi wa viwanda vya kati na vikubwa kwa lengo la kuongeza thamani ya mazao na kutoa ajira kwa vijana.

“Wilaya ya Kisarawe ipo na mtazamo mpya wa maendeleo, kuhakikisha tunasonga mbele kwa kasi zaidi katika kuboresha maisha ya wananchi,” amesema.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Kisarawe, Khalfan Sika, amesema jukumu la wanachama wa CCM ni kuipa ushirikiano Serikali ili kuhakikisha Ilani ya Uchaguzi inatekelezwa kikamilifu.

“Ilani tuliyowapa Mhe. Rais, Mbunge na Madiwani ni Ilani ya CCM. Utekelezaji wake ndio mafanikio na suluhisho la kero za wananchi. Huu ni mkataba kati ya wananchi na CCM,” amesema.

Ameongeza kuwa Ilani hiyo ni maelekezo ya chama ambayo Serikali imepewa dhamana ya kuyatekeleza kwa vitendo, huku akimpongeza Rais Samia na Mbunge Jafo kwa maono makubwa waliyonayo ya kuwaletea maendeleo wananchi.

Kadhalika, Mwenyekiti huyo amempongeza Dkt. Jafo kwa uungwana wake wa kukutana na Halmashauri Kuu ya CCM Wilaya mara baada ya kumalizika kwa shughuli za uchaguzi.

“Mara nyingi baada ya uchaguzi, watu waliobeba mzigo mkubwa wa kampeni hawakumbukwi kushukuriwa. Nimpongeze sana Mbunge Jafo kwa kuona umuhimu wa kukutana na wajumbe hawa na kuwashukuru,” amesema.

Amefafanua kuwa katika Wilaya ya Kisarawe, kampeni zilifanyika katika vijiji vyote 84 na mikutano 105 ilifanyika katika ngazi ya vijiji na vitongoji, kwa lengo la kuhakikisha wananchi wanaielewa Ilani ya CCM na sababu za kuchagua chama hicho.

Amesema katika matokeo ya uchaguzi, Rais Samia alipata ushindi wa asilimia 98 huku Mbunge Jafo akipata asilimia 95, hali inayoonesha imani kubwa ya wananchi wa Kisarawe kwa viongozi wao na Chama Cha Mapinduzi.

“Jukumu letu sasa ni kusimamia utekelezaji wa Ilani, kwa sababu uchaguzi mwingine utafanyika mwaka 2030, na wananchi watataka kuona ni kwa kiasi gani tumetekeleza ahadi tulizotoa,” amesema.

Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo,akiwasili katika ukumbi  kwa ajili ya kuzungumza na Wajumbe wa  Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kisarawe kikao kilicholenga kuwashukuru wajumbe kwa mchango wao katika kufanikisha Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kuwashukuru kwa kuchaguliwa tena kuwa Mbunge wa jimbo hilo.

Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo,akizungumza  na Wajumbe wa  Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kisarawe,kikao kilicholenga kuwashukuru wajumbe kwa mchango wao katika kufanikisha Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kuwashukuru kwa kuchaguliwa tena kuwa Mbunge wa jimbo hilo.

Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo,akizungumza  na Wajumbe wa  Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kisarawe,kikao kilicholenga kuwashukuru wajumbe kwa mchango wao katika kufanikisha Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kuwashukuru kwa kuchaguliwa tena kuwa Mbunge wa jimbo hilo.

Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo,akizungumza  na Wajumbe wa  Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kisarawe,kikao kilicholenga kuwashukuru wajumbe kwa mchango wao katika kufanikisha Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kuwashukuru kwa kuchaguliwa tena kuwa Mbunge wa jimbo hilo.

 

Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo,akizungumza  na Wajumbe wa  Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kisarawe,kikao kilicholenga kuwashukuru wajumbe kwa mchango wao katika kufanikisha Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kuwashukuru kwa kuchaguliwa tena kuwa Mbunge wa jimbo hilo.

Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo,akizungumza  na Wajumbe wa  Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kisarawe,kikao kilicholenga kuwashukuru wajumbe kwa mchango wao katika kufanikisha Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kuwashukuru kwa kuchaguliwa tena kuwa Mbunge wa jimbo hilo.

Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo,akizungumza  na Wajumbe wa  Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kisarawe,kikao kilicholenga kuwashukuru wajumbe kwa mchango wao katika kufanikisha Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kuwashukuru kwa kuchaguliwa tena kuwa Mbunge wa jimbo hilo.

Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo akimsikiliza Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Kisarawe Khalfan Sika,wakati ,akizungumza   na Wajumbe wa  Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kisarawe,kikao kilicholenga kuwashukuru wajumbe kwa mchango wao katika kufanikisha Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kuwashukuru kwa kuchaguliwa tena kuwa Mbunge wa jimbo hilo.

Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo akimsikiliza Katibu  wa Chama cha Mapinduzi Wilaya ya Kisarawe Bi.Josephine Mwanga wakati akizungumza  na Wajumbe wa  Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kisarawe,kikao kilicholenga kuwashukuru wajumbe kwa mchango wao katika kufanikisha Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kuwashukuru kwa kuchaguliwa tena kuwa Mbunge wa jimbo hilo.

Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo akimsikiliza Mwenyekiti wa Halmashauri ya Kisarawe, Aidan Kitare wakati akizungumza  na Wajumbe wa  Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kisarawe,kikao kilicholenga kuwashukuru wajumbe kwa mchango wao katika kufanikisha Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kuwashukuru kwa kuchaguliwa tena kuwa Mbunge wa jimbo hilo.

 

Wajumbe wakimsikiliza Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo (hayupo pichani) wakati,akizungumza  na Wajumbe wa  Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kisarawe,kikao kilicholenga kuwashukuru wajumbe kwa mchango wao katika kufanikisha Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kuwashukuru kwa kuchaguliwa tena kuwa Mbunge wa jimbo hilo.

Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo,akiwa katika picha ya pamoja  Wajumbe wa  Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kisarawe,mara baada ya kuzungumza nao kikao  kilicholenga kuwashukuru wajumbe kwa mchango wao katika kufanikisha Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kuwashukuru kwa kuchaguliwa tena kuwa Mbunge wa jimbo hilo.

Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo,akiwa katika picha ya pamoja  Wajumbe wa  Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kisarawe,mara baada ya kuzungumza nao kikao  kilicholenga kuwashukuru wajumbe kwa mchango wao katika kufanikisha Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kuwashukuru kwa kuchaguliwa tena kuwa Mbunge wa jimbo hilo.

Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo,akiwa katika picha ya pamoja  Wajumbe wa  Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kisarawe,mara baada ya kuzungumza nao kikao  kilicholenga kuwashukuru wajumbe kwa mchango wao katika kufanikisha Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kuwashukuru kwa kuchaguliwa tena kuwa Mbunge wa jimbo hilo.

Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo,akiwa katika picha ya pamoja  Wajumbe wa  Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kisarawe,mara baada ya kuzungumza nao kikao  kilicholenga kuwashukuru wajumbe kwa mchango wao katika kufanikisha Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kuwashukuru kwa kuchaguliwa tena kuwa Mbunge wa jimbo hilo.

Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo,akiwa katika picha ya pamoja  Wajumbe wa  Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kisarawe,mara baada ya kuzungumza nao kikao  kilicholenga kuwashukuru wajumbe kwa mchango wao katika kufanikisha Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kuwashukuru kwa kuchaguliwa tena kuwa Mbunge wa jimbo hilo.

Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo,akiwa katika picha ya pamoja  Wajumbe wa  Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kisarawe,mara baada ya kuzungumza nao kikao  kilicholenga kuwashukuru wajumbe kwa mchango wao katika kufanikisha Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kuwashukuru kwa kuchaguliwa tena kuwa Mbunge wa jimbo hilo.

DG EWURA ATAKA WELEDI,UADILIFU KWA WATUMISHI

December 17, 2025 Add Comment


*Singida:* Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA), Dkt. James Mwainyekule, amewataka watumishi wa Ofisi hiyo kutekeleza majukumu yao kwa weledi na uadilifu wa hali ya juu ili kukidhi matarajio ya Watanzania kwa ufanisi na tija zaidi.


Ametoa rai hiyo leo 17 Desemba 2025 wakati wa kikao cha baraza la Wafanyakazi wa EWURA kilichofanyika mkoani Singida.

“ Tufanye kazi kwa ushirikiano, tutoe huduma kwa weledi na tuendelee kuwa waadilifu. Tukumbuke pia sisi ni timu moja, tuepuke majungu na manung’uniko mahali pa kazi kwani husababisha kutokuelewana na hivyo kuathiri utendaji,” alisema Dkt. Mwainyekule.

Aliongeza kuwa wafanyakazi wote wana wajibu wa kutekeleza majukumu yao kwa uwazi, ufanisi na tija ili kuhakikisha ubora na upatikanaji endelevu wa huduma za umeme, mafuta,  gesi asilia na maji na usafi wa mazingira.

“Ifahamike kuwa, baraza la wafanyakazi ni chemchemi ya mawazo mapya.  Tutafanya mabadiliko ya namna tunavyofanya kazi, ili tuendane na wakati wa sasa, hatuwezi kufanya kazi kama ambavyo tulifanya miaka iliyopita,” alisema. 


Naibu Katibu Mkuu TUGHE Taifa, Mha. Amani Msuya, aliipongeza EWURA kwa maandalizi mazuri ya kikao cha baraza la wafanyakazi na kwa kulipa umuhimu  suala la ushirikishwaji wafanyakazi.


Mwisho

NCSS YAFANYA TATHMINI YA MWAKA, YAJIPANGA KUIMARISHA ULINZI WA MTOTO

December 17, 2025 Add Comment
NA EMMANUEL MBATILO, DODOMA 

Umoja wa Kitaifa wa Asasi za Kiraia wa Shule Salama (NCSS), unaoratibiwa na shirika la HakiElimu, umetoa wito kwa wadau kuunga mkono jitihada za pamoja za kumlinda mtoto dhidi ya vitendo vya ukatili.

GEREZA LA KILIMO URAMBO KUNEEMEKA NA MIUNDOMBINU YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA

December 17, 2025 Add Comment


📌*Mkuu wa Gereza Apongeza Juhudi za Serikali*


📌 *Asema Nguvu Kazi Sasa Inaelekezwa Kwenye Shughuli za Kiuchumi*


📍Tabora


Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imepanga kupeleka majiko matatu ya kisasa yanayotumia mkaa mbadala pamoja na sufuria zake katika Gereza la Kilimo Urambo, mkoani Tabora. 


Hatua hiyo ni sehemu ya jitihada za Serikali kuimarisha matumizi ya nishati safi ya kupikia katika taasisi zinazohudumia  watu zaidi ya 100 nchini.


Hayo yameelezwa na Mkurugenzi wa Nishati Safi ya Kupikia, Bw. Nolasco Mlay, wakati wa ziara yake ya kikazi katika  Gereza la Kilimo Urambo ambapo alijionea utekelezaji wa agizo la Serikali la matumizi ya nishati safi ya kupikia.

 Mlay amesema Serikali kupitia REA inaendelea kuchukua hatua mbalimbali za kuongeza matumizi ya nishati safi ya kupikia kwa taasisi mbalimbali nchini, ikiwa ni pamoja na kuziimarisha kwa miundombinu ya kisasa inayotumia teknolojia rafiki kwa mazingira kama majiko banifu na mifumo ya gesi.

Aidha, Bw. Mlay amesema Gereza la Mahabusu Urambo tayari limefungiwa mfumo mmoja wa gesi na kwa sasa linasubiri kupatiwa majiko manne ya gesi, Sambamba na hilo, gereza hilo pia litapatiwa majiko matatu yanayotumia mkaa mbadala  ili kuendelea kuimarisha matumizi ya nishati safi ya kupikia katika magereza nchini.


Akizungumza katika ziara hiyo, Mkuu wa Gereza la Kilimo Urambo, Bw. Joseph Mzumara  amepongeza juhudi za Serikali katika kuhakikisha taasisi na jamii kwa ujumla zinaachana na matumizi ya nishati zisizo salama kama kuni, ambazo zinaathiri afya na mazingira.

“Hapo awali tulikuwa tunakabiliwa na changamoto kubwa za kutafuta kuni maeneo ya mbali, lakini kwa sasa tunatumia mkaa mbadala. Hali hii imesaidia kupunguza muda unaotumika kutafuta nishati zisizo salama na badala yake nguvu kazi inaelekezwa kwenye shughuli nyingine za kiuchumi," amesema Mzumara


Aidha,  ameishukuru Wizara ya Nishati kupitia Kitengo cha Nishati Safi ya Kupikia kwa kuhakikisha nishati safi ya kupikia inawafikia pia watumishi wa Jeshi la Magereza.

"Watumishi wote tumepatiwa majiko ya gesi yanayotuwezesha kupika kwa haraka na kutekeleza majukumu yetu mengine kwa ufanisi zaidi badala ya kutumia muda mwingi kutafuta nishati zisizo salama,"  amesema.



Ameongeza kuwa Gereza la Kilimo Urambo lina mifugo ya kutosha, na kwa siku zijazo linajipanga kuanza kuzalisha gesi vunde (biogas) ili kujiongezea vyanzo endelevu vya nishati safi ya kupikia.

MWENYEKITI WA BODI YA WAKURUGENZI TANESCO AKABIDHIWA RASMI OFISI

December 17, 2025 Add Comment




📌Asema TANESCO imepiga hatua kubwa katika utekelezaji wa miradi ya umeme


📌Apongeza jitihada zinazoendelea za  kuimarisha eneo la huduma kwa wateja 


📌Aahidi kutoa ushirikiano na kuendeleza alipoishia mtangulizi wake


Mwenyekiti  wa Bodi ya Wakurugenzi wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), Bw. Plasduce Mbossa, leo Desemba 16, 2025 amekabidhiwa rasmi ofisi na aliyekuwa Mwenyekiti wa Bodi hiyo,  Mhe. Dkt. Rhimo Nyansaho, ambaye kwa sasa ni Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa.


Hafla hiyo ya makabidhiano imefanyika jijini Dar es Salaam na kuhudhuriwa na wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi pamoja na Menejimenti ya TANESCO.

Akizungumza katika hafla hiyo, Bw. Mbossa amesema Mheshimiwa Nyansaho ameondoka akiiacha  TANESCO katika mwelekeo mzuri  na usimamizi mzuri baada ya miradi mingi mikubwa ya umeme kukamilika ikiwemo miradi ya kimkakati kama Bwawa la Kuzalisha Umeme la Julius Nyerere ambalo limechangia kwa kiasi kikubwa kuimarisha uzalishaji na upatikanaji wa umeme nchini.


Aidha, Bw. Mbossa  amepongeza jitihada zinazofanywa katika kuboresha huduma kwa wateja, ambazo zimeongeza ufanisi na kumfanya mteja kuwa kipaumbele.

‘’TANESCO ipo katika mweleko mzuri miradi mingi ya umeme imekamilika na kupelekea nchi kuwa na umeme wa kutosha. Tutaendelea kufanya jitihada za kuongeza uzalishaji wa umeme ili kuendana na kasi ya ongezeko la mahitaji ya umeme,‘’ alifafanua Bw. Mbossa.


Kwa upande wake, Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kulinda Taifa ambaye ni Mwenyekiti wa Bodi aliyemaliza muda wake, Mhe. Dkt. Rhimo Nyansaho, amewashukuru wajumbe wa Bodi na Menejimenti ya TANESCO kwa ushirikiano waliouonesha katika kipindi chote cha uongozi wake ambapo pia amemuahakikisha Mwenyekiti wa Bodi kuwa Bodi  iko imara na anaimani ataendeleza pale alipoishia.

‘’Kwa dhati naishukuru sana Bodi ya Wakurugenzi na Menejimenti ya TANESCO kwa ushirikiano mlionipatia katika kipindi chote tulichokuwa pamoja. Tulishirikiana kwa karibu kutatua changamoto na kuhakikisha Shirika linasonga mbele katika kuwahudumia wananchi,’’ alisema Dkt Nyansaho.


Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO, Naibu Mkurugenzi Mtendaji (Uzalishaji), Mhandisi Antony Mbushi, amemshukuru Mwenyekiti  wa bodi aliyemaliza muda wake kwa uongozi na ushirikiano wake mzuri, na kusisitiza kuwa Menejimenti itaendelea kusikiliza na kutekeleza maelekezo ya Mwenyekiti  wa Bodi wa sasa kwa maslahi ya Shirika na Taifa kwa ujumla.


Wakati wa uongozi wake Mhe. Nyansaho alisimamia utekelezaji wa miradi mingi ya umeme na kuhakikisha imekamilika, ikiwemo Miradi ya Bwawa la kufua umeme la Julius Nyerere, Rusumo, Mradi wa kusafirisha umeme wa Lemuguru, Miradi mbalimbali ya Gridi imara, Kuingiza mikoa ya Kigoma na Katavi kwenye Gridi ya taifa na huku akiicha miradi mingine ikiwa katika hatua nzuri za utekelezaji kama Mradi Umeme wa Jua wa Kishapu, ambao mpaka sasa umefikia zaidi ya asilimia 84 ya utekelezaji.


Pia katika kipindi chake, TANESCO imefanikiwa kuboresha mazingira ya kazi kwa wafanyakazi wake jambo lililochangia kuongeza ufanisi katika utekelezaji wa majukumu ya Shirika pamoja na maboresho makubwa ya eneo la huduma kwa wateja ikiwemo maboresho ya kituo cha miito ya simu, uwepo wa namba 180 ya huduma kwa wateja na mfumo wa Jisoti kuimarisha mawasiliano.

WAZIRI MCHENGERWA KUSHIRIKI MKUTANO WA DUNIA KUHUSU TIBA ASILI, KUFANYA MAZUNGUMZO NA MAWAZIRI WA AFYA

December 17, 2025 Add Comment

Na John Mapepele, New Delhi

Waziri wa Afya wa Tanzania, Mhe. Mohamed Omary Mchengerwa amewasili New Delhi, nchini India, tayari leo kushiriki Mkutano wa pili wa Kimataifa wa Shirika la Afya Duniani (WHO) kuhusu tiba asili ikiwa ni mkakati wa Serikali ya Tanzania katika kushirikiana na mataifa mbalimbali kwenye kuboresha huduma ya afya kwa wananchi ambapo amepokelewa na ujumbe wa ubalozi wa Tanzania India ukiongozwa na Mhe. Balozi, Anisa Mbega.