HABARI

SIASA

ELIMU

Recent Posts

DKT. YONAZI AKUTANA NA KUFANYA MAZUNGUMZO NA MKURUGENZI MTENDAJI MPYA WA TACAIDS DKT. MRISHO

March 23, 2026 Add Comment



Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu Dkt. Jim Yonazi amekutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi Mtendaji mpya wa Tume ya Kudhibiti UKIMWI Tanzania (TACAIDS) Dkt. Adam Joseph Mrisho ambaye amefika kujitambulisha baada ya kuteuliwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.


Kikao hicho kimefanyika tarehe 23 Machi, 2026 katika Ofisi ya Waziri Mkuu iliyopo mtaa wa Reli jijini Dodoma na kudhuriwa na Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu) Dkt. James Kilabuko pamoja na Mratibu wa Masuala ya UKIMWI Bi. Adela Mpina.


Dkt.Yonazi ameahidi kumpa ushirikiano katika utekelezaji wa majukumu yake ya kila siku.
(PICHA ZOTE NA OFISI YA WAZIRI MKUU)




WAZIRI NDEJEMBI AITAKA EWURA KUKAGUA MAGHALA YA MAFUTA KUHAKIKISHA HAKUNA MAFUTA YANAYOFICHWA

March 23, 2026 Add Comment

 



📌*Asema nchi ina usalama mkubwa wa mafuta hivyo wananchi waendelee kupata huduma muda wote*


📌*Timu maalum kuundwa kufuatilia uingizaji wa mafuta nchini*


Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi ameitaka Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) kuhakikisha kuwa, hakuna mfanyabiashara anayeficha mafuta kwa kisingizio cha kusubiri bei za mafuta zipande kutokana na mgogoro unaoendelea katika eneo la Mashariki ya Kati ambao umepelekea baadhi ya nchi kukumbana na changamoto za upatikanaji wa mafuta.

Akizungumza jijini Dodoma katika kikao na Taasisi za Wizara zinazosimamia Sekta ya Mafuta, Mhe. Ndejembi ameeleza kuwa nchi ina usalama mkubwa wa mafuta na kwamba Serikali imejipanga vizuri kuhakikisha  wananchi katika maeneo yote wanapata huduma bila vikwazo hivyo EWURA anapaswa kuhakikisha hakuna mafuta yanayofichwa katika maghala ya kuhifadhi Mafuta.

Aidha, ili kuhakikisha mafuta yote yaliyoagizwa nje ya nchi yanafika nchini kwa mujibu wa mkataba, Mhe. Ndejembi ameelekeza kuundwa kwa timu maalum kufuatilia mwenendo wa uingizaji wa Mafuta nchini ambayo itahusisha Wataalam kutoka Wakala wa Uagizaji wa Mafuta kwa Pamoja (PBPA),  EWURA, Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) pamoja na Ulinzi na Usalama.

 " Timu hii itakuwa na jukumu la kufuatilia hatua kwa hatua  na kuhakikisha kuwa mafuta yote yaliyoagizwa ambayo yako njiani  kuja nchini yanafika kwa wakati bila kikwazo wala changamoto yoyote. Hali ya biashara ya mafuta huko duniani si ya kuridhisha, baadhi ya nchi bei ya mafuta imepanda maradufu na wafanyabiashara wengine wanaweza kuingia tamaa na kupeleka mafuta huko, katika hili sitarajii kuona mikataba tuliyoingia na waagizaji wa mafuta ikikiukwa." Amesisitiza Mhe. Ndejembi


Kwa upande wake, Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati anayeshughulikia Mafuta na Gesi Asilia, Dkt. James Mataragio, amewahakikishia Watanzania kuwa nchi ina akiba ya kutosha ya mafuta hadi mwezi Julai 2026. 


Amesema Serikali ilichukua hatua za mapema kwa kushirikiana na taasisi zake, ili kuhakikisha kunakuwa na uhakika wa upatikanaji wa mafuta na kwa gharama himilivu. 




Ameongeza kuwa Wizara itaendelea kusimamia Taasisi zake ili kuhakikisha mafuta yaliyopo njiani yanafika kwa wakati, pamoja na kuwadhibiti wauzaji ili wasitumie changamoto iliyopo kama fursa ya kupandisha bei.


Awali, Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Uagizaji wa Mafuta kwa Pamoja (PBPA) Bw. Erasto Simon alieleza kuwa hali ya upatikanaji wa mafuta nchini iko salama  ambapo ameeleza kuwa ukijumuisha mafuta yaliyopo nchini na yaliyopo njiani kuna petroli lita milioni 474 inayotosheleza siku 78, dizeli  lita milioni 392 inayotosheleza siku 50 pamoja na lita milioni 55 za mafuta ya ndege zinazotosheleza siku 91.


Naye, Mkurugenzi Mtendaji Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) Bw.Mussa Makame ameeleza kuwa kuna mafuta ya kutosha ndani ya nchi na ambayo yako safarini kwani Serikali ilishasaini mikataba na wazabuni mapema kwa ajili ya uingizaji wa mafuta.

Kwa upande wake,  Mkurugenzi Mkuu wa EWURA, Dkt. James Andilile ameeleza kuwa kwa sasa soko liko sawa hakuna mfumuko wa bei hivyo  EWURA itahakikisha watu hawafichi mafuta kusubiri mfumuko wa bei katika soko la dunia.


Amesema EWURA imeendela kushirikiana na wadau wa mafuta wakiwemo waagizaji na wauzaji ili kuhakikisha kama kuna changamoto zozote  zinatatuliwa kwa haraka ili wananchi wapate huduma kwa uhakika.

UJENZI WA BARABARA YA KAHAMA - BULYANHULU JCT - KAKOLA KWA UWEZESHAJI WA MIGODI YA BARRICK NI UWEKEZAJI ENDELEVU UTAKAOACHA ALAMA YA KUDUMU NCHINI

March 23, 2026 Add Comment

Mchakato wa kumwaga lami katika barabara ya Kahama-Kakola inayojengwa kwa uwezeshaji wa kampuni ya Barrick nchini ukiendelea
Mchakato wa kumwaga lami na kuisambaza ukiendelea
Msimamizi wa Ujenzi wa barabara ya Kahama-Kakola kutoka Wakala wa Barabara nchini (TANROADS) Mhandisi Marco Bee, akiongea kuhusu maendeleo ya ujenzi huo unaotekelezwa kwa ufadhili wa kampuni ya Barrick nchini.
Msimamizi Msaidizi kutoka kampuni ya Barrick, Mhandisi Ibahim Paul akielezea maendeleo ya ujenzi wa barabara hiyo.
**
#Wafikia hatua ya barabara kuwekwa lami

Mradi wa ujenzi wa barabara ya Kahama-Bulyanhulu JCT- Kakola kwa kiwango cha lami yenye kilomita 73 kwa uwezeshaji wa migodi ya Barrick nchini ya Bulyanhulu na North Mara yenye ubia na Serikali kupitia kampuni ya Twiga Minerals kwa gharama ya shilingi bilioni 101.2 umefikia hatua ya kuwekwa lami na kudhihirisha dhamira ya kampuni ya uwekezaji unaoenda sambamba na kufanikisha miradi mikubwa endelevu inayobadilisha maisha ya wananchi kuwa bora na itakayoacha alama ya kudumu hadi kwa vizazi vijavyo.

THPS YAKABIDHI KLINIKI YA MAT SHINYANGA KUIMARISHA MAPAMBANO DHIDI YA MATUMIZI YA DAWA ZA KULEVYA

March 23, 2026 Add Comment

  


MAHITAJi YA UMEME YAONGEZEKA KWA WASTANI WA ASILIMIA 10-15 KILA MWAKA

March 22, 2026 Add Comment


ONGEZEKO la idadi ya watu pamoja na kuimarika kwa shughuli za viwanda na biashara limeendelea kuchochea kasi ya mahitaji ya umeme nchini kwa wastani wa asilimia 10 hadi 15 kila mwaka.


Kutokana na mwenendo huo, Serikali imejipanga kuongeza jitihada za kuhakikisha upatikanaji wa umeme wa uhakika kwa wananchi wote, sambamba na kuimarisha miundombinu ya nishati.

Akizungumza katika mkutano wa Powering Africa Summit uliofanyika jijini Washington, DC, Machi 20, 2025, Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba, amesema kuwa ongezeko hilo la mahitaji linachochea uwekezaji mkubwa katika sekta ya nishati, ambayo ni mhimili muhimu wa ukuaji wa uchumi.

Amefafanua kuwa hadi kufikia Machi 2026, uwezo wa uzalishaji wa umeme nchini umefikia megawati 4,383, wakati kiwango cha juu cha mahitaji kikiwa takribani megawati 2,100.


Hata hivyo, ameonya kuwa kasi ya ongezeko la mahitaji inahitaji uwekezaji zaidi katika uzalishaji, usafirishaji na usambazaji wa umeme ili kuendana na mahitaji ya sasa na ya baadaye.

Kuhusu upatikanaji wa huduma hiyo, amesema Serikali imefanikiwa kufikisha miundombinu ya umeme katika vijiji vyote vya Tanzania Bara, ingawa kiwango cha uunganishaji wa umeme katika kaya bado ni cha chini, hali inayoonesha changamoto ya kuwafikia wananchi wote.


Mhe. Salome amesisitiza kuwa Serikali imelenga kufikia asilimia 100 ya upatikanaji wa umeme ifikapo mwaka 2030, huku ikikusudia kuongeza kiwango cha uunganishaji wa kaya hadi asilimia 75 ili kuchochea maendeleo ya kijamii na kiuchumi.

Aidha, ameeleza kuwa Tanzania ina vyanzo mbalimbali vya nishati ikiwemo gesi asilia, maji, jua, upepo na jotoardhi, ambavyo vina uwezo mkubwa wa kukidhi mahitaji yanayoongezeka.


Ameongeza kuwa Serikali itaendelea kuhimiza matumizi ya nishati jadidifu ili kuhakikisha upatikanaji endelevu wa umeme, huku ikiendeleza juhudi za kuhamasisha uwekezaji katika sekta hiyo.


Hatua hizo zinatarajiwa kusaidia kukidhi mahitaji ya nishati yanayoongezeka na kuiwezesha Tanzania kuwa kitovu cha nishati katika ukanda wa Afrika.

MAENEO YA UWEKEZAJI SEKTA YA NISHATI YATAJWA NCHINI INDIA

March 22, 2026 Add Comment


📌*Mhandisi Mramba asema Tanzania ina fursa nyingi na mazingira ya uwekezaji ni rafiki*


New Delhi, India


Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati anayeshughulikia Umeme na Nishati Jadidifu,  Mhandisi Felchesmi Mramba, ametangaza fursa mbalimbali za uwekezaji zilizopo katika sekta ya nishati nchini, akizialika kampuni na wawekezaji wa kimataifa kuchangamkia nafasi hizo ili kuchochea ukuaji wa sekta hiyo.


Akizungumza katika kikao maalum cha India–Africa Partnership kilichofanyika wakati wa mkutano wa Bharat Electricity 2026 unaoendelea nchini India, Mhandisi Mramba amesema Tanzania ina mazingira rafiki ya uwekezaji na inaendelea kujipambanua kama moja ya maeneo yenye fursa kubwa katika sekta ya nishati barani Afrika.


Ameeleza kuwa fursa hizo zinapatikana katika maeneo mbalimbali ikiwemo miradi ya kuzalisha umeme, kusafirisha na kusambaza umeme, pamoja na uwekezaji katika nishati jadidifu kama jua, upepo, jotoardhi na umeme wa maji. Aidha, ametaja pia uwekezaji katika nishati safi ya kupikia kuwa ni eneo muhimu linalopewa kipaumbele na Serikali. 


Mhandisi Mramba ameeleza kuwa Tanzania inaendelea kukuza sekta ya umeme ili kukidhi ongezeko la mahitaji linalochochewa na ukuaji wa viwanda na ongezeko la matumizi ya umeme mijini na vijijini, akibainisha kuwa uwezo wa uzalishaji umefikia takribani megawati 4,500 na unatarajiwa kufikia megawati 8,000 ifikapo mwaka 2030. 


Ameongeza kuwa Serikali kupitia Mpango wa Taifa wa Nishati ( National Energy Compact) inalenga kuongeza upatikanaji wa umeme, kuimarisha matumizi ya nishati jadidifu na kufikia matumizi ya nishati safi ya kupikia kwa asilimia 75 ifikapo mwaka 2030 hatua inayofungua zaidi fursa kwa wawekezaji kushiriki katika miradi yenye tija. 


Amesisitiza kuwa Tanzania iko tayari kushirikiana na wadau wa kimataifa katika kuendeleza miradi ya kimkakati kupitia ubia kati ya sekta ya umma na binafsi (PPP), akiwahakikishia wawekezaji uwepo wa mazingira wezeshi, sera thabiti na dhamira ya dhati ya Serikali katika kusimamia na kutekeleza miradi ya nishati.

EID AL-FITR AND THE NGORONGO CRATER REFLECTED IN THE HOLY QUR'AN ( SURAH 99 -AL-ZALZALAH

March 22, 2026 Add Comment




As Muslims and Tanzanians at large celebrate Eid al-Fitr, marking the end of the holy month of Ramadan, it is a fitting moment to reflect on the deeper spiritual truths that connect faith, nature, and existence. For those open to belief, there will come a final day when the earth is shaken and gathered together, and mountains are reduced to dust.


This philosophy, described in sacred teachings, mirrors what unfolded at the Ngorongoro Crater approximately 2.5 million years ago.


In the Holy Qur’an, Surah 99—Al-Zalzalah (The Earthquake), which consists of eight verses, vividly describes the events of the Day of Judgement. The earth will shake violently and release its burdens, and humanity will witness every deed: good or bad, even those as small as a particle.


These verses find a powerful parallel in the history and present state of the Ngorongoro Crater.


Scientists explain that over 2.5 million years ago, a massive volcanic mountain: believed to have been larger than Mount Kilimanjaro, erupted within what is now the Ngorongoro area. A series of intense eruptions destabilized the structure, and the volcanic cone could no longer support its own weight. It collapsed inward, forming the vast caldera we now know as the Ngorongoro Crater, one of the largest intact volcanic calderas in the world.


Today, the crater spans roughly 20 kilometers in diameter and reaches a depth of about 610 meters, forming a natural basin of extraordinary scale and beauty.


This geological event took place during the Pleistocene epoch, a time marked by significant volcanic activity across the Eastern Rift Valley, as the Great Rift itself continued to expand.


Over time, nature shaped this landscape into a self-contained ecosystem of remarkable diversity. The crater floor hosts a mosaic of habitats: freshwater and soda lakes, forests, open grasslands, rivers, springs, rocky outcrops, and rolling hills. These environments support an abundance of wildlife, with populations exceeding 25,000 animals throughout the year.


When you consider the formation of the Ngorongoro Crater alongside insights drawn from sacred texts and blend them with the region’s rich culture, traditions, and natural heritage, a profound narrative emerges. Ngorongoro reveals itself as a living testament often described as a “Garden of Eden” where humanity, nature, and the Creator’s design converge, and where every layer of its story continues to unfold.

RC BATILDA AWATAKA WAZAZI KUWA MAKINI NA WATOTO

March 22, 2026 Add Comment




Na Oscar Assenga, TANGA



MKUU wa Mkoa wa Tanga Balozi,Dkt Batilda Burian ametoa salamu za sikuu ya Eid El Fitri kwa wakazi wa mkoa huo huku akiwataka wazazi na walezi kuwa makini na watoto wanapotoka kwenda kutembea.



Dkt Batilda aliyasema hayo jana mara baada ya kumalizika kwa Swala ya Eid El Fitri iliyofanyika kwenye msikiti wa Ijumaa Jijini Tanga ambapo alisema ni muhimu wakati wa sikuuu wahakikishe watoto wanapokwenda kutembea wanakuwa na uangalizi.



Alisema kwamba kufanya hivyo kutawasadia kwenda kutembelea salama na kuweza kusheherekea sikuuu salama bila kadhia ambayo inaweza kuleta madhara mbalimbali ikiwemo majozi na msiba.



“Wazazi na walezi niwaombe Shehere ya Eid watoto wanakwenda kutembelea tuwe makini wawe na mtu mzima hata njiani wawe makini kuna vyombo vya usafiri bodabodoa na magari tuhakikishe tunakula sikuuu salama bila kadhia ambayo italeta msiba na majonzi”Alisema



Aidha aliwataka wakazi wa mkoa huo kuendelea kudumisha amani na utulivu kuendeleza mshikamano kwa upendo pamoja na kuendelea kumuombea Rais wetu Dkt Samia Suluhu .



Mkuu huyo wa Mkoa alisisitiza wana Tanga kuendelea kuwaombea waliotangulia mbele za haki na waliojaliwa kuendelea kumshukuru Mwenyezi Mungu ikiwemo kuwaombea viongozi wa dini.



“Nitoe mkono wa Eid Fitri kwa wana Tanga na watanzania tuendelee kama tulivelekezwa tuwatembelee wagonjwa ndugu na jamaa na tuzuru makaburi na tufanye amali njema na tuendelee kupendana na kutenda mema”Alisema



Akizungumza Mbunge wa Jimbo la Tanga Kassim Amary Makubel aliwatakia heri ya sikuu ya Eid El Fitri wakazi wa Jiji hilo huku akieleza kwamba hivi sasa Tanga imefunguka kimaendeleo na itaendelea kufunguka zaidi kutokana na uwekezaji mkubwa uliofanywa na Serikali.



Mbunge huyo aliwashauri watu wa Tanga wasiwe wepesi wa kuunza nyumba zao hata kama ni za urithi na kama ikitokea anataka kuja Mwekezaji kuwekeza ingieni ubia kwa miaka fulani kwani watakapouza wanaweza kuwa nje ya mji.



Awali akizungumza Diwani wa Kata ya Ngamiani Kaskazini, Fahadi Rished amesema umoja ulioonyeshwa wakati wa swala ya Eid uendelee kushikamana na waendelee kuwasaidia ndugu na jamaa wasiojiweze.



Alisema kwamba kata yao ipo salama kwa wananchi kusheherekea sikuu ya Eid hivyo wananchi washeherekee kwa salama .


Mwisho.








TANESCO YAGUSA MIOYO YA WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUMU

March 21, 2026 Add Comment




📌Ni sehemu ya uwajibikaji wake kwa jamii 


📌Yatoa misaada mbalimbali kwa vituo vitatu Dar es Salaam.


Katika kuendeleza dhamira ya uwajibikaji kwa jamii, Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), tarehe 19 Machi 2026, lilifanya ziara ya kutembelea vituo vitatu vya watoto wenye mahitaji maalum jijini Dar es Salaam, na kutoa misaada mbalimbali kwa lengo la kuleta faraja na matumaini.


Akizungumza wakati wa ziara hiyo kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji ,Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano na Huduma kwa Wateja wa TANESCO, Bi. Irene Gowelle, alisema kuwa lengo la ziara hiyo ni kushirikiana na jamii kwa vitendo kwa kutoa misaada hususan kwa makundi ya watoto yenye uhitaji .

Alieleza kuwa msaada huo haujalenga tu kukidhi mahitaji ya msingi, bali pia kuwajengea watoto hao imani, matumaini na ujasiri wa kuendelea kuamini katika ndoto zao licha ya changamoto wanazokabiliana nazo.


“Leo TANESCO tumeshiriki na watoto hawa wenye mahitaji maalum kwa kutoa misaada mbalimbali, ikiwa ni sehemu ya kurejesha kwa jamii na kuendeleza uwajibikaji wetu wa kijamii,” alisema Bi. Irene.

Aidha, alisisitiza kuwa TANESCO itaendelea kushirikiana na jamii inayowazunguka kama sehemu ya mchango wake katika kujenga taifa lenye mshikamano, upendo na ustawi wa pamoja.


Kwa upande wake, Mwanzilishi wa Kituo cha Umra Orphanage Center, Bi. Rahma Juma, aliipongeza TANESCO kwa hatua hiyo, akisema msaada uliotolewa umefika kwa wakati muafaka na umeleta faraja kubwa kwa watoto pamoja na walezi wao.


Alibainisha kuwa ujio wa TANESCO umeongeza furaha na kuwapa watoto motisha mpya, huku akieleza kuwa vituo vya aina hiyo bado vinakabiliwa na changamoto mbalimbali zinazohitaji ushirikiano wa wadau.



“Kazi hii iliyofanywa na TANESCO ni mfano wa kuigwa. Msaada huu umekuja kwa wakati mwafaka na utatusaidia sana katika malezi ya watoto tulionao hapa kituoni,” alisema Bi. Rahma.


"Napenda kuwashukuru TANESCO  kwa ujio wao kwetu tunashukuru

kwa sadaka ambazo wameleta hasa katika msimu huu  wa  sikukuu zimekuja  kwa wakati sahihi wametuletea  vitu ambavyo  ni mahitaji yetu ya kila siku "  Amesema Bi. Nuru Mwegoha

Aidha, alitoa wito kwa taasisi, makampuni na watu binafsi kujitokeza kusaidia makundi yenye mahitaji maalum ili kuhakikisha wanapata huduma bora na kuishi maisha yenye matumaini.



Vituo vilivyofikiwa katika ziara hiyo ni Umra Orphanage Center kilichopo Magomeni, Kituo cha Watoto Yatima cha CHAKUWAMA kilichopo Sinza Mori, pamoja na New Hope for Girls Organization kilichopo Kimara.

FCC YASISITIZA UMUHIMU WA KUJUA HAKI NA WAJIBU WA MLAJI

FCC YASISITIZA UMUHIMU WA KUJUA HAKI NA WAJIBU WA MLAJI

March 20, 2026 Add Comment

Mkuu wa Kanda ya Tume ya Ushindani (FCC) - Nyanda ya Juu Kusini, Bw. Dickson Mbanga,akitoa elimu kuhusiana madhara ya bidhaa bandia kwa wanafunzi wa Chuo cha Maendeleo ya Wananchi Njombe (FDC) ikiwa ni sehemu ya kuelekea Maadhimisho ya Wiki ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani 2026.

....

TUME ya Ushindani (FCC) kanda ya Nyanda za Juu Kusini  imetoa elimu kwa wanafunzi wa Chuo cha Maendeleo ya Wananchi Njombe (FDC) kuhusu masuala ya kumlinda mlaji, ikiwemo haki na wajibu wa mlaji pamoja na madhara ya matumizi ya bidhaa bandia katika jamii.

Elimu hiyo imelenga kuwajengea wanafunzi uelewa mpana ili waweze kufanya maamuzi sahihi wanaponunua na kutumia bidhaa mbalimbali  ikiwa ni sehemu ya maandalizi kuelekea kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani 2026.

Akitoa elimu hiyo Mkoani Njombe, Mkuu wa Kanda ya Tume ya Ushindani (FCC) Nyanda za Juu Kusini, Bw. Dickson Mbanga, amesisitiza umuhimu wa kila mlaji kufahamu haki zake za msingi.alieza kuwa haki hizo ni pamoja na kupata bidhaa bora, kupata taarifa sahihi kuhusu bidhaa, pamoja na haki ya kulalamika pale mlaji anapodhulumiwa.

Aidha, Bw. Mbanga ameeleza madhara makubwa yatokanayo na matumizi ya bidhaa bandia, akibainisha kuwa bidhaa hizo zinaweza kusababisha athari za kiafya, kupoteza fedha, na kudhoofisha uchumi wa nchi. Amewataka wanafunzi kuwa mabalozi wa kuelimisha jamii zao ili kupunguza matumizi ya bidhaa hizo hatarishi.

“FCC imesisitiza kuwa elimu hii ni endelevu na inalenga kuwafikia makundi mbalimbali ya jamii ili kujenga taifa lenye walaji wenye uelewa na uwezo wa kufanya maamuzi sahihi.”amesema Bw. Mbanga

Kwa ujumla, mafunzo hayo yameacha alama chanya kwa wanafunzi wa FDC Njombe, ambapo wengi wao wameeleza kuwa elimu hiyo imewafungua macho na kuwapa nguvu ya kusimamia haki zao kama walaji, huku wakiahidi kushiriki kikamilifu katika mapambano dhidi ya bidhaa bandia nchini.

Kupitia mafunzo hayo, walikumbushwa kuwa mlaji ana nafasi kubwa katika kulinda afya yake na uchumi wa taifa kwa kuchagua bidhaa zilizo salama na zenye ubora unaokubalika.

Mkuu wa Kanda ya Tume ya Ushindani (FCC) - Nyanda ya Juu Kusini, Bw. Dickson Mbanga,akitoa elimu kuhusiana madhara ya bidhaa bandia kwa wanafunzi wa Chuo cha Maendeleo ya Wananchi Njombe (FDC) ikiwa ni sehemu ya kuelekea Maadhimisho ya Wiki ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani 2026.

Mkuu wa Kanda ya Tume ya Ushindani (FCC) - Nyanda ya Juu Kusini, Bw. Dickson Mbanga,akitoa elimu kuhusiana madhara ya bidhaa bandia kwa wanafunzi wa Chuo cha Maendeleo ya Wananchi Njombe (FDC) ikiwa ni sehemu ya kuelekea Maadhimisho ya Wiki ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani 2026.

Mkuu wa Kanda ya Tume ya Ushindani (FCC) - Nyanda ya Juu Kusini, Bw. Dickson Mbanga,akitoa elimu kuhusiana madhara ya bidhaa bandia kwa wanafunzi wa Chuo cha Maendeleo ya Wananchi Njombe (FDC) ikiwa ni sehemu ya kuelekea Maadhimisho ya Wiki ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani 2026.

  Afisa Mlinda Mlaji kutoka FCC Bw.Anderson Lwiza,akitoa elimu kuhusiana madhara ya bidhaa bandia kwa wanafunzi wa Chuo cha Maendeleo ya Wananchi Njombe (FDC) ikiwa ni sehemu ya kuelekea Maadhimisho ya Wiki ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani 2026.

  Afisa Mlinda Mlaji kutoka FCC Bw.Anderson Lwiza,akitoa elimu kuhusiana madhara ya bidhaa bandia kwa wanafunzi wa Chuo cha Maendeleo ya Wananchi Njombe (FDC) ikiwa ni sehemu ya kuelekea Maadhimisho ya Wiki ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani 2026.

Sehemu ya wanafunzi wa Chuo cha Maendeleo ya Wananchi Njombe (FDC) Mkoani Njombe wakisikiliza mada mbalimbali wakati wakipata aelimu kuhusiana madhara ya bidhaa bandia yaliyotolewa  na FCC ikiwa ni sehemu ya kuelekea Maadhimisho ya Wiki ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani.

KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE AFYA NA MASUALA YA UKIMWI YAIPONGEZA SERIKALI KUWAWEZESHA KIUCHUMI WAISHIO NA VVU

March 20, 2026 Add Comment





Na Mwandishi wetu- DAR ES SALAAM


Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu  ya Bunge ya Afya na Masuala ya UKIMWI ambaye pia ni Mbunge wa

Arumeru Magharibi Mhe. Johannes Lukumay ameipongeza  Serikali kuendelea kusaidia kundi la Watu waishio na Maamubikizi Virusi vya 

UKIMWI kupitia shughuli mbalimbali za kiuchumi ili kujikwamua kiuchumi.


Mhe. Lukumay ameyasema  hayo tarehe 19 Machi 2026 mara baada ya ziara ya kutembelea Baraza la Watu waishio na maambukizi ya Virusi vya  UKIMWI akiwa ameambatana na Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Afya na Masuala ya UKIMWI katika ( Konga ya Jiji) iliyofanyika   katika Viwanja vya Pugu Mnadani Jijini Dar es Salaam.

 Amesema kuwa watu waishio na maambukizi ya Virusi vya UKIMWI ni sawa na watu wengine hivyo yapaswa kuwapa kipaumbele katika fursa mbalimbali za kimaendeleo.



Pia Mwenyekiti huyo amelipongeza kundi hilo kwa namna

wanavyojituma katika kuhakikisha wanajikwamua kiuchumi na kuondokana na umasikini hivyo  kuziagiza  sekta husika kusaidia katika kuwatafutia masoko kwa ajili ya bidhaa zao.




Kwa upande wake Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu Mhe. Ummy Nderiananga amesema kuwa Serikali chini ya uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan wataendelea kuunga mkono jitihada zao kwa kuongeza nguvu zaidi kwa Wanakonga ili waweze kujikwamua kiuchumi.



Mhe. Nderiananga amempongeza Mkurugenzi wa Jiji, Mkuu wa Wilaya pamoja na Katibu Tawala wa Halmashauri ya Jiji la Dar es salaam na timu nzima kwa kuwawezesha Wanakonga katika fursa mbalimbali na kuwataka kuendelea na desturi hiyo ya kuwawezesha kwani mwaka huu wa fedha bado haujamalizika.



Aidha  Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dar es salaam Elihuruma Mabelya amesema kuwa moja ya eneo waliloliwekea nguvu ni Konga hiyo kwa kuunga mkono shughuli zao za  kiuchumi ili kuhakikisha

wanainuka na kufanikiwa katika nyanja mbalimbali za maendeleo.





N