Nahodha wa Timu ya Mpira wa Miguu ya Barrick Bulyanhulu Sports Club akipokea zawadi kutoka kwa Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Mboni Mhita, baada ya timu hiyo kutwaa ubingwa wa Bonanza la Mei Mosi.
HABARI NA MATUKIO MBALIMBALI
Nahodha wa Timu ya Mpira wa Miguu ya Barrick Bulyanhulu Sports Club akipokea zawadi kutoka kwa Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Mboni Mhita, baada ya timu hiyo kutwaa ubingwa wa Bonanza la Mei Mosi.










Wafanyakazi wa EWURA wakishiriki maandamano ya Mei Mosi mbele ya Rais, Mhe. Samia Suluhu Hassan.
...
Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) leo, Mei 1, 2026, imeungana na wafanyakazi wengine duniani kuadhimisha Siku ya Wafanyakazi Duniani (Mei Mosi), maadhimisho yaliyofanyika kitaifa mkoani Njombe.
Sherehe hizo zilihudhuriwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, ambaye alikuwa mgeni rasmi. Katika hotuba yake, Rais Samia amewahimiza waajiri na waajiriwa kote nchini kuendeleza ushirikiano, kuaminiana, na kutanguliza maslahi ya taifa katika utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku.
Amesisitiza kuwa Serikali itaendelea kuboresha mazingira na ustawi wa wafanyakazi, huku akiwataka kuongeza bidii na ufanisi kazini. Aidha, alibainisha wazi kuwa Serikali inathamini mchango wa wafanyakazi na itaendelea kuwaunga mkono katika juhudi za maendeleo ya nchi.
Katika maadhimisho hayo, EWURA imewakilishwa na wafanyakazi wake bora kutoka idara na vitengo mbalimbali. Wafanyakazi hao walichaguliwa kwa kura za wenzao kwa kuzingatia vigezo muhimu kama vile utendaji uliotukuka, nidhamu ya kazi, ubunifu pamoja na kujituma kazini.
Wawakilishi hao walishiriki katika maandamano rasmi yaliyopita mbele ya mgeni rasmi, wakibeba mabango yenye ujumbe wa kuhamasisha mshikamano na uwajibikaji kazini.
Ushiriki wao umeonesha dhamira ya EWURA kuendelea kutoa huduma bora kwa wananchi na kuchangia maendeleo ya taifa kwa ujumla.

Wafanyakazi wa EWURA wakishiriki maandamano ya Mei Mosi mbele ya Rais, Mhe. Samia Suluhu Hassan.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwapungia mkono wafanyakazi wa EWURA, wakati wa maandamano ya Maadhimisho ya Sherehe za Meimosi leo.
NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM
Wahitimu 12 wa Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT) wamehitimu mafunzo ya awali ya lugha ya Kijapani, hatua inayolenga kuongeza ujuzi na ushindani wao katika soko la ajira la ndani na kimataifa.








Ushirikiano kati ya Tanzania na Japan katika sekta ya nishati unaingia hatua mpya, huku juhudi zikielekezwa zaidi katika kuvutia uwekezaji wa sekta binafsi na teknolojia za kisasa za uzalishaji umeme.
Hatua hiyo imebainishwa jijini Dar es Salaam leo tarehe 30 Aprili,2026 wakati Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati anayeshughulikia Mafuta na Gesi Asilia,Dkt. James Mataragio alipokutana na Mwakilishi Mkuu mpya wa Japan International Cooperation Agency, Dkt. Kuge Katsuya.
Katika kikao hicho Dkt. Mataragio ameweka wazi Mkakati wa Serikali kuifanya sekta ya nishati kuwa kivutio kikubwa cha mitaji ya kimataifa hususan kutoka Japan.
Amesema kuwa pamoja na historia ndefu ya ushirikiano kati ya nchi hizo mbili, hatua inayofuata inapaswa kulenga uwekezaji mkubwa zaidi unaoweza kuongeza uzalishaji na upatikanaji wa nishati nchini.
“Huu ni wakati wa kuhamasisha kampuni binafsi na taasisi za kifedha kutoka Japan kuja kuwekeza moja kwa moja katika miradi ya nishati Tanzania,” amesisitiza.
Akizungumzia ushirikiano wa Tanzania na Japan Dkt. Mataragio amesema JICA imekuwa mdau wa muda mrefu katika sekta ya nishati nchini na wameshiriki katika miradi ya Uandaaji wa Mpango kabambe wa Matumizi ya Gesi Asilia Nchini (Natural Gas Utilization Master Plan -NGUMP), wametoa fursa za kuwajengea uwezo wataalamu katika Matumizi ya gesi asili pamoja na utekelezaji wa Miradi mbalimbali ya umeme.
Aidha Dkt. Mataragio amembushia ahadi ya muda mrefu ya Japan ya kuwezesha Mradi wa umeme wa megawati 300 mkoani Mtwara.
Kwa upande wake, Dkt. Kuge ameashiria mwelekeo mpya wa ushirikiano utakaojikita katika Mafunzo ya teknolojia ya nishati ya nyuklia, Uzalishaji wa umeme kupitia gesi asilia kwa ufanisi mkubwa zaidi na Kuunganisha Tanzania na wawekezaji binafsi kutoka Japan
Ahadi hiyo inaashiria uwezekano wa Tanzania kunufaika na teknolojia za kisasa zaidi za nishati kutoka Japan, moja ya nchi zinazoongoza duniani katika ubunifu wa nishati.
Mkutano huo umeonesha wazi kuwa ushirikiano kati ya Tanzania na Japan hauishii katika misaada, bali sasa unaelekea kwenye uwekezaji mkubwa na ubadilishanaji wa teknolojia hatua inayoweza kubadilisha kabisa sekta ya nishati nchini