HABARI

SIASA

ELIMU

Recent Posts

DG RUWASA AWAELEKEZA MAMENEJA WA MIKOA NA WILAYA KUZISHIRIKISHA CBWSOs KATIKA PROGRAMU ZOTE

July 13, 2026 Add Comment


Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA), Mha. Wolta Kirita, amesisitiza umuhimu wa kushirikisha Vyombo vya Utoaji wa Huduma ya Maji Ngazi ya Jamii (CBWSOs) katika mipango na programu zote zinazolenga kuboresha huduma za maji vijijini ili kuhakikisha huduma hizo zinakuwa endelevu na wananchi wanaendelea kunufaika na uwekezaji mkubwa unaofanywa na Serikali.

REA YANG'ARA SABASABA 2026

July 13, 2026 Add Comment




🏆 *RAIS MWINYI ASHUHUDIA REA IKITWAA TUZO YA MUONESHAJI BORA WA TAASISI ZA SERIKALI*


🤝 *REA YAWASHUKURU WADAU KWA MCHANGO WAO KATIKA MAFANIKIO HAYO*


📍 Dar es Salaam


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, ameshuhudia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) ukitwaa Tuzo ya Muoneshaji Bora wa Taasisi za Serikali (*Government Institutions Exhibitor*) katika kilele cha Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba) 2026.


Tuzo hiyo imepokelewa na Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano na Mawasiliano kwa Umma wa REA, Bi. Martha Chassama, kwa niaba ya Wakala.


REA inawashukuru wadau wote waliotembelea banda lake, kujionea mafanikio na utekelezaji wa miradi ya nishati vijijini, pamoja na kuendelea kuunga mkono jitihada za Wakala za kupeleka nishati ya umeme kwenye vitongoji. 


Mwisho

NEEC YALETA ELIMU YA MITAJI KARIBU NA WANANCHI RUKWA

July 13, 2026 Add Comment
Mafunzo ya utoaji wa elimu kuhusu fursa za mitaji kupitia mifuko na programu mbalimbali za uwezeshaji wananchi kiuchumi yanaendelea kufanyika katika Manispaa ya Sumbawanga, mkoani Rukwa, yakilenga kuwaongezea wananchi uelewa kuhusu fursa za kupata mitaji na huduma za maendeleo ya biashara ili kukuza shughuli za kiuchumi.

MHANDISI MRAMBA ATEMBELEA BANDA LA TANESCO SABASABA

July 13, 2026 Add Comment




Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati (Umeme na Nishati Jadidifu), Mhandisi Felchesmi Mramba, ametembelea Banda la Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), na kampuni zake Tanzu katika Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam (Sabasaba), ambayo leo yanafikia kilele katika Viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere, jijini Dar es Salaam.

Mha.Mramba ametembelea banda hilo ili kuona huduma mbalimbali zinazotolewa kwa wananchi  wanaotembelea banda hilo.



RAIS MWINYI ATEMBELEA BANDA LA NISHATI SABASABA

July 13, 2026 Add Comment

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, akisalimiana na Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati, Mhandisi Felchesmi Mramba mara baada ya kufika  katika Banda la Wizara ya Nishati katika kilele cha  Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam (Sabasaba), yanayofanyika katika Viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere, jijini Dar es Salaam. 

Kushoto kwa Katibu Mkuu ni Mkurugezi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania ( TANESCO), Lazaro Twange.




MHANDISI MRAMBA ATEMBELEA BANDA LA WIZARA YA NISHATI SABASABA

July 13, 2026 Add Comment


Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati (Umeme na Nishati Jadidifu), Mhandisi Felchesmi Mramba, ametembelea Banda la Wizara ya Nishati katika Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam (Sabasaba), ambayo leo yanafikia kilele katika Viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere, jijini Dar es Salaam.

Akiwa katika banda la Wizara, Mhandisi Mramba amepata maelezo kutoka kwa wataalam wa Wizara ya Nishati kuhusu elimu inayoendelea kutolewa kwa wananchi wanaotembelea maonesho hayo. 

Elimu hiyo inahusu  huduma zinazotolewa na Wizara na Taasisi zake pamoja na fursa mbalimbali zilizopo katika sekta ya nishati, ikiwemo umeme, mafuta, gesi asilia, nishati jadidifu na nishati safi ya kupikia, sambamba na hatua zinazochukuliwa na Serikali kuboresha upatikanaji wa huduma za nishati nchini.



MHANDISI MRAMBA AVUTIWA NA KASI YA REA KUSAMBAZA UMEME KWENYE VITONGOJI

July 13, 2026 Add Comment

Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati (Umeme na Nishati Jadidifu) Mha. Felchesmi Mramba ameipongeza Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa utekelezaji wa miradi ya umeme vijijini pamoja na mafanikio ya usambazaji umeme kwenye vitongoji.

Mha. Mramba amesema hayo leo Julai 13, 2026 alipotembelea banda la REA kwenye Kilele cha  maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba)




ELIMU YA UTOAJI WA MIKOPO KWA MAKUNDI MAALUM IONGEZEKE - RABIA

July 13, 2026 Add Comment

 

Viongozi wa Serikali wameshauriwa kuongeza Elimu ya utoaji na urejeshaji wa mikopo ya asilimia 10, ambayo katika bajeti ya mwaka 2026/2027 itakuwa asilimia 15.

Hayo yameelezwa leo Julai 12,2026 na Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, Idara ya Mambo ya Siasa na Uhusiano wa Kimataifa Ndg Rabia Abdalla Hamid katika muendelezo wa ziara yake ya Kusikiliza na kutatua changamoto za Makundi mbalimbali ya kijamii mkoani Rukwa.

“Nitoe rai kwa Viongozi wa serikali kuhakikisha Elimu ya utoaji na urejeshaji wa mikopo ya asilimia 10,ambayo katika bajeti ya mwaka 2026/2027 itakuwa asilimia 15 inatolewa kwa kasi  ili wananchi wawe na uelewa mpana katika masuala ya fedha na walengwa waendelee kunufaika ”,amesema Ndugu Rabia.
















AJIRA ZA WAZAWA ZILINDWE : CI NYAKUNGA

July 12, 2026 Add Comment
Na. OWM (KAM), Dar es Salaam

Kamishna wa Uhamiaji wa Divisheni ya Usimamizi na Udhibiti wa Mipaka, CI Fakih Nyakunga, ameiomba Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Ajira na Mahusiano) kupitia Idara ya Kazi kuhakikisha vibali vya kazi vinatolewa kwa raia wa kigeni wenye ujuzi ambao haupatikani nchini Tanzania ili kulinda ajira za wazawa.

DKT. BATILDA BURIAN ATOA WITO WA KUTEMBELEA BANDA LA OFISI YA WAZIRI MKUU

Kajunason July 12, 2026 Add Comment

Na Mwandishi Wetu - Dar es Salaam

Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mhe. Balozi Dkt. Batilda Burian ametoa wito kwa wananchi kuendelea kujitokeza kupata elimu ya masuala mbalimbali katika Banda Jumuishi la Ofisi ya Waziri Mkuu na Taasisi zake katika Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara (Sabasaba 2026) yanayoendelea katika Viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere, jijini Dar es Salaam. 

Ametoa wito huo hii leo (12 Julai, 2026)
alipotembelea na kujionea namna ofisi hiyo inavyoendelea kutoa huduma kwa wananchi na kuwasihi waendelee kujitokeza kwa wingi na kupata taarifa na huduma zinazotolewa na Ofisi ya Waziri Mkuu pamoja na taasisi zake.
Dkt. Batilda amepongeza namna Ofisi ya Waziri Mkuu ilivyojipanga na kuhakikisha inawafikia wananchi kwa utoaji wa huduma bora na kuzingatia viwango huku wakiendelea kutatua changamoto mbalimbali kwa jamii kupitia maonesho hayo.

Aidha amewakumbusha watumishi wa ofisi hiyo kuendelea kuwa na program mbalimbali za elimu kwa umma ili kuifikia jamii kwa ukumbwa wake na kuendelea kutangaza huduma zinazotolewa.
Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam yanaendelea katika viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere chini ya kaulimbiu isemayo, "Maonesho ya Biashara ya Kimataifa ya Sabasaba ni Fahari ya Tanzania," yakilenga kukuza biashara, uwekezaji na ubunifu, nchini.