HABARI

SIASA

ELIMU

Recent Posts

FEDHA ZA CSR ZA BARRICK NORTH ZAENDELEA KUWEZESHA WANANCHI KUPATA HUDUMA BORA ZA AFYA WILAYANI TARIME

December 10, 2025 Add Comment

  

Mgeni rasmi akikata utepea kuashiria uzinduzi wa zahanati hiyo
 **
-Zahanati mpya yazinduliwa katika kijiji cha Mangucha

Wananchi kutoka Mangucha moja ya kijiji kilichopo jirani na mgodi wa dhahabu wa North Mara wilayani Tarime walionekana kuwa na nyuso za furaha na matumaini ya kuondokana na changamoto ya kutembea mwendo mrefu kufuata huduma za afya katika hafla ya Halmashauri ya Wilaya ya Tarime kukabidhiwa zahanati ya kijiji ambayo imejengwa kwa gharama ya shilingi milioni 164 zilizotokana na fedha za uwajibikaji kwa jamii (CSR) zilizotolewa na mgodi wa Barrick North Mara unaoendeshwa na Kampuni ya Barrick kwa ubia na Serikali ya Tanzania kupitia kampuni ya Twiga Minerals.

MIAKA 64 YA UHURU : TBN YASEMA "AMANI KWANZA ,UJENZI WA TAIFA DAIMA "

December 10, 2025 Add Comment

 

Leo Desemba 9, tunapoadhimisha miaka 64 tangu Taifa letu lipate Uhuru, Tanzania Bloggers Network (TBN) inawapongeza Watanzania wote kwa kufikia hatua hii muhimu katika historia ya Taifa letu. Hii ni siku ya kutafakari safari tuliyotoka, mahali tulipo, na mwelekeo tunaoujenga kwa pamoja.

Waasisi wetu walituwachia zawadi kubwa—Uhuru. Lakini walituonya kuwa Uhuru hauwezi kuwa kamili bila kujitegemea. Leo tunakumbusha maneno ya Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, aliyewahi kusisitiza:

"Uhuru hauwezi kukamilika pasipo kujitegemea. Hatuwezi kuitwa huru kama tunategemea wengine kutupatia mahitaji yetu ya kimsingi."

Tujenge Taifa Letu – Tusiibomoe Tanzania

Kama mtandao wa habari za kidijitali, TBN inasisitiza kuwa mafanikio yetu kama Taifa yametokana na utulivu, umoja na mshikamano. Ili kuendelea mbele, tunahitaji kudumisha amani na maridhiano—nguzo muhimu za maendeleo.

Rais mstaafu Benjamin William Mkapa alituasa kwa busara:

"Amani si kitu cha asili; tunahitaji kuilinda na kuitunza kila siku. Bila amani, hakuna maendeleo ya kweli."

Tukikubali kuongozwa na chuki, uchochezi na vurugu, juhudi za waasisi wetu za kupambana na ujinga, umaskini na maradhi zitapotea. Tusiitumie mitandao au uhuru wa maoni kuharibu Taifa letu; tuitumie kulijenga.

Kila Zama na Kiongozi Wake – Tuunge Mkono Mageuzi

Kila kizazi kina wajibu wake. Kama alivyoeleza Rais mstaafu Ali Hassan Mwinyi:

"Kila utawala na zama zake. Kila kiongozi na mchango wake katika ujenzi wa Taifa hili."

Katika awamu ya sasa chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, Tanzania inaendelea na mwelekeo wa 4R: Reconciliation, Resilience, Reforms, and Rebuilding. Huu ni mwaliko kwa Watanzania wote kushiriki katika kujenga Taifa lenye maridhiano, mageuzi chanya na uimara wa kiuchumi na kijamii.

Tuna nafasi ya kuzungumza—basi tuseme kwa njia inayojenga, si inayobomoa. Kuthamini Uhuru ni kufanya kazi kwa bidii, kulinda amani, na kuacha kutumiwa kuharibu misingi ya Taifa letu.

TBN Inawatakia Maadhimisho Mema ya Miaka 64 ya Uhuru!


Tanzania Kwanza — Kazi, Utu na Mshikamano. Tusonge Mbele!


Beda Msimbe

Mwenyekiti, Tanzania Bloggers Network (TBN)

MABORESHO YA BANDARI YA TANGA YAONGEZA UFANISI KATIKA UHUDUMIAJI MELI

December 10, 2025 Add Comment


Na Oscar Assenga, TANGA

MAMLAKA ya Usimamizi wa Bandari nchini (TPA) umesema kwamba maboresho makubwa yaliyofanywa katika Bandari ya Tanga umepelekea wastani wa kuhudumia meli moja kwa siku tatu kutoka siku saba za awali kutokana na kuongezeka kwa ufanisi mkubwa.

Hayo yalisemwa na Mwakilishi wa Meneja wa Bandari ya Tanga Peter Milanzi wakati wa upokeaji aina mpya ya mzigo wa Lami kupitia Kampuni ya Wakala wa Usafirishaji ya Amura unaosafirishwa kwenda nchi jirani ya Malawi ambao wameamua kutumia Bandari hiyo kutokana na ufanisi wake

Alisema kwamba kutokana na ufanisi huo umepelekea kuvutia wateja wengi kuitumia Bandari hiyo kupitisha shehena mbalimbali za mizigo ikiwemo magari na mizigo mbalimbali ambazo zinakwenda nchi mbalimbali.

“Bandari ya Tanga tumeendelea kufanya vizuri kutokana na maboresho yaliyofanywa na Serikali kupitia Rais Dkt Samia Suluhu na hivyo kuvutia wateja wengi na leo tunapokea aina mpya ya mzigo wa Lami kwa wenzao wa Kampuni ya Amoue wameamua kuitumia Bandari ya Tanga kutokana na ufanisi ambao wanao kwa majaribio wameamua kupitisha makontena sita na kila moja lina mapipa 110 inaenda nchi ya Malawi”Alisema

Alisema kwamba hiyo ni ishara kubwa ya kuaminiwa na wafanyabiashara na watu mbalimbali hivyo wanawaambia wateja waendele kuitumia Bandari hiyo kutokana na wao wanaendelea kuwahudumia kwa ufanisi na kutoa huduma bora kama wenzao Amura.

“Bandari ya Tanga ni salama na itaendelea kuwa samana na kutoa huduma ya ushushaji wa mizigo na kwa wale waliokwama kwenye Bandari nyengine njooni Tanga mtahudumiwa kwa ufanisi mkubwa na kwa muda mfupi”Alisema Milanzi.

Hata hivyo alisema kwamba kuanzia mwezi Julai mwaka huu wa Fedha 2025/2026 walipangiwa kuhudumia Tani milioni 1.6 ,sasa wastani wa kuhudumia tani laki 137,000 lakini tokea mwezi Julai mwaka huu wamekuwa wakivuka malengo walianza na tani laki 152,000 na baadae wakapanda tani 157,000 na mwezi Septemba –Octoba wamefikisha tani 200,000 kila mwezi.

Alieleza kwamba wanaona malengo ambao wamewekewa watayafikia hayo yote yamekua kutokana na ufanisi wao kwenye kazi na hivyo wateja wameongezeka hatua inayoonyesha watavuta malengo waliopangiwa kutokana na m.

Awali akizungumza mara baada ya mara baada ya kushushwa kwa Shehena hiyo ya Lami –Mwakilishi wa Kampuni ya  Amura ya Dar ,Zakaria Mohamed Nanimuka alisema kwamba kutokana na ufanisi wa Bandari ya Tanga wanategemea kuingiza kontena nyengine 20 zitazohudumiwa kwenye Bandari hiyo.

“Sisi kama Kampuni Amura tumefurahishwa na ufanisi wa Bandari ya Tanga na hakuna malalamiko wala changamoto zozote zile tunashukuru Serikali kwa kuwekeza hapa na sasa sisi wasafirishaji tutaendelea kuitumia katika kuingiza shehena mbalimbali”Alisema

Zakari alisema kwamba wamekuja Tanga kupokea shehena ya mzigo wa Lami kutoka Iran na kushukia Bandari ya Tanga kontena sita zenye tani 125 na kilo 430 ambapo kontena moja lina kuwa na pipa 110 kwa kontena

Alisema kwamba wanashukuru kwa namna walivyohudumiwa wamefanya kazi vizuri na wala hakukuwa na changamoto za aina yoyote ile mzigo wao umeweza kushughulikiwa wamepita scana kwa wakati hivyo wanamshukuru Rais Dkt Samia Suluhu kwa maboresho makubwa yaliyosaidia kuongeza ufanisi.

WAZIRI NDEJEMBI KUSHIRIKI KONGAMANO LA MAWAZIRI WA NISHATI WA AU NCHINI ETHIOPIA

December 09, 2025 Add Comment


📌*Kujadiliana mikakati ya kuendeleza matumizi bora ya Nishati*


📌*Mkakati na Mpango Kazi wa Matumizi Bora ya Nishati barani Afrika kuzinduliwa*


Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi leo Disemba 09, 2025 amewasili jijini Addis Ababa, Ethiopia kwa ajili ya kushiriki Kongamano la Mawaziri wa Sekta ya Nishati wa Nchi Wanachama wa Umoja wa Afrika (AU) wenye lengo la kujadili na kuweka mikakati ya kuendeleza matumizi bora ya nishati kwa Bara la Afrika. 


Kongamano hilo litafanyika kwa siku mbili  ambapo nchi wanachama wa AU watabadilishana uzoefu katika mikakati, mipango, changamoto na upatikanaji wa fedha kwa ajili ya kutekeleza ya miradi ya kuongeza ufanisi wa nishati katika bara la Afrika 

Katika kongamano hilo pia Mkakati na Mpango Kazi wa Matumizi Bora ya Nishati barani Afrika utazinduliwa ambao unaendana na malengo ya Mpango wa Afrika wa Mwaka 1963. 


Aidha kongamano hilo la siku mbili limetanguliwa na mafunzo kwa wataalamu wa sekta ya Nishati katika kuwajengea uzoefu kwenye maeneo ya kupunguza Matumizi ya umeme katika sekta za majengo, viwanda, usafiri pamoja na majumbani.

Katika kongamano hilo Waziri Ndejembi ameongozana na Kamishna wa Umeme na Nishati Jadidifu, Mhandisi Innocent Luoga.


Nchini Ethiopia Waziri Ndejembi amepokelewa na Balozi na Mwakilishi wa Kudumu wa Umoja wa Afrika (AU) na Kamisheni ya Uchumi Afrika (UNECA), Mhe. Innocent Shiyo.

SQF Zanzibar Cleft Marathon Yarejea Kwa Msimu wa 7, Yazidi Kutoa Matumaini kwa Watoto

December 09, 2025 Add Comment

 


Na Mwandishi Wetu


Mashabiki wa michezo na wakimbiaji nchini wanatarajiwa kujitokeza kwa wingi kwenye The SQF Zanzibar Cleft Marathon – Season 7, mbio maalum zinazolenga kuchangisha fedha kwa ajili ya watoto waliozaliwa na tatizo la mdomo na taya wazi (cleft).


Mbio hizo zimepangwa kufanyika Desemba 21, 2025 katika viwanja vya New Aman Complex visiwani Zanzibar, na zimekuwa kivutio kikubwa kwa wanamichezo, wadau wa afya, pamoja na wananchi wanaoguswa na masuala ya kijamii.


Kwa mujibu wa waandaaji, The Same Qualities Foundation (SQF), usajili kwa ajili ya mbio za mwaka huu umeshaanza katika maeneo mbalimbali ikiwemo New Aman Complex, Michenzani Mall, Forodhani, Masomo Bookshop, pamoja na Hospitali ya Edward Michaud jijini Dar es Salaam. Ada ya usajili ni shilingi 35,000 kwa washiriki wa mbio za 21KM, 10KM na 5KM.


Tukio hili ni zaidi ya mashindano, wamesema waandaaji. “Kila hatua unayokimbia ni sehemu ya kubadilisha maisha ya mtoto mmoja—kutoa tabasamu jipya, kuondoa unyanyapaa, na kurejesha matumaini kwa familia nzima.”


Mbio hizi zimepata pia heshima ya kuhudhuriwa na Mgeni Rasmi, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, hatua inayoongeza uzito na hamasa kwa washiriki.


Kwa upande wao, wadau wa michezo wamepongeza juhudi za SQF kwa kuunganisha michezo na huduma za kijamii, wakisema mbio hizi zimekuwa mfano bora wa jinsi nguvu ya umoja inaweza kubadili maisha ya watu wanaohitaji msaada.


Waandaaji wametoa wito kwa wakimbiaji, klabu za michezo, mashirika na familia kujitokeza kwa wingi kushiriki na kuchangia. Washiriki wanaweza pia kulipia kupitia M-Pesa kwa namba 5427230 (The Same Qualities Foundation).


Mbio hizi zinatarajiwa kuwa miongoni mwa matukio makubwa ya michezo ya kijamii mwaka 2025 nchini, yakileta pamoja wanamichezo, wafadhili na watu wa kada mbalimbali kwa lengo moja—kupigania tabasamu la mtoto.

MIAKA 64 YA UHURU: TBN YASEMA "AMANI KWANZA,UJENZI WA TAIFA DAIMA

December 09, 2025 Add Comment


Leo Desemba 9, tunapoadhimisha miaka 64 tangu Taifa letu lipate Uhuru, Tanzania Bloggers Network (TBN) inawapongeza Watanzania wote kwa kufikia hatua hii muhimu katika historia ya Taifa letu. Hii ni siku ya kutafakari safari tuliyotoka, mahali tulipo, na mwelekeo tunaoujenga kwa pamoja.


Waasisi wetu walituwachia zawadi kubwa—Uhuru. Lakini walituonya kuwa Uhuru hauwezi kuwa kamili bila kujitegemea. Leo tunakumbusha maneno ya Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, aliyewahi kusisitiza:


"Uhuru hauwezi kukamilika pasipo kujitegemea. Hatuwezi kuitwa huru kama tunategemea wengine kutupatia mahitaji yetu ya kimsingi."

 

Tujenge Taifa Letu – Tusiibomoe Tanzania


Kama mtandao wa habari za kidijitali, TBN inasisitiza kuwa mafanikio yetu kama Taifa yametokana na utulivu, umoja na mshikamano. Ili kuendelea mbele, tunahitaji kudumisha amani na maridhiano—nguzo muhimu za maendeleo.


Rais mstaafu Benjamin William Mkapa alituasa kwa busara:


"Amani si kitu cha asili; tunahitaji kuilinda na kuitunza kila siku. Bila amani, hakuna maendeleo ya kweli."


Tukikubali kuongozwa na chuki, uchochezi na vurugu, juhudi za waasisi wetu za kupambana na ujinga, umaskini na maradhi zitapotea. Tusiitumie mitandao au uhuru wa maoni kuharibu Taifa letu; tuitumie kulijenga.

Kila Zama na Kiongozi Wake – Tuunge Mkono Mageuzi


Kila kizazi kina wajibu wake. Kama alivyoeleza Rais mstaafu Ali Hassan Mwinyi:


"Kila utawala na zama zake. Kila kiongozi na mchango wake katika ujenzi wa Taifa hili."


Katika awamu ya sasa chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, Tanzania inaendelea na mwelekeo wa 4R: Reconciliation, Resilience, Reforms, and Rebuilding. Huu ni mwaliko kwa Watanzania wote kushiriki katika kujenga Taifa lenye maridhiano, mageuzi chanya na uimara wa kiuchumi na kijamii.


Tuna nafasi ya kuzungumza—basi tuseme kwa njia inayojenga, si inayobomoa. Kuthamini Uhuru ni kufanya kazi kwa bidii, kulinda amani, na kuacha kutumiwa kuharibu misingi ya Taifa letu.

 

TBN Inawatakia Maadhimisho Mema ya Miaka 64 ya Uhuru!


Tanzania Kwanza — Kazi, Utu na Mshikamano. Tusonge Mbele!


Beda Msimbe

Mwenyekiti, Tanzania Bloggers Network (TBN)

KAMISHNA BADRU AWATAKA WATUMISHI KUCHAPA KAZI KWA BIDII KUENZI MIAKA 64 YA UHURU

December 09, 2025 Add Comment


 Na Mwandishi Wetu, Ngorongoro.


Kamishna wa Uhifadhi Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro (NCAA) Bw. Abdul-Razaq Badru amewataka watumishi wa mamlaka hiyo kufanya kazi kwa bidii, weledi, uaminifu, ubunifu na ushirikiano katika ulinzi wa rasilimali za Wanyamapori na misitu ili kuenzi uhuru wa Tanzania Bara kwa vitendo.

Katika salamu zake za kuadhimisha miaka 64 ya Uhuru wa Tanzania Bara kamishna Badru amesema hifadhi ya Ngorongoro imedhamiria kuendelea kuwa eneo muhimu la uhifadhi na utalii duniani na kusisitiza kila mtumishi kutimiza majukumu yake kwa malengo ya kimkakati na kutekeleza dira ya nchi ya 2050.

“Dhamira yetu kwa Ngorongoro ni kuendelea kuifanya kuwa Premium Safari Destination hivyo hatutomwacha mtu nyuma wala kukata tamaa katika kutimiza malengo hayo na tutahakikisha tunalinda rasilimali za Wanyamapori, misitu na malikale zilizopo Ngorongoro kwa wivu mkubwa kama ambayo mwasisi wa Taifa letu Mwalimu Julius Nyerere alituachia,”alisema Kamishna Badru.

Ameeleza kuwa katika maadhimisho haya ya miaka 64 ya uhuru wa Tanzania bara njia pekee ya Ngorongoro kuyaenzi ni kuongeza ufanisi katika nyanja zote za uhifadhi,utalii na kudumisha mahusiano thabiti kwa maendeleo ya jamii.

Katika kuadhimisha siku ya uhuru wa Tanzania Bara Maafisa na askari wa Jeshi wa Uhifadhi Ngorongoro wametumia siku hiyo kufanya usafi katika maeneo mbalimbali yaliyopo eneo la hifadhi ya Ngorongoro ili kuendelea kuweka mandhari ya kuvutia kwa wageni wanaotembelea hifadhi hiyo.

Tanzania bara inaadhimisha miaka 64 ya uhuru uliopatikana tarehe 09 Desemba mwaka 1961 chini ya uongozi thabiti wa baba wa Taifa hayati Julius Kambarage Nyerere.









OUT TRAINS 24 IRINGA STEM TEACHERS IN COMPETENCY-BASED DIGITAL SKILLS

December 09, 2025 Add Comment
The Open University of Tanzania (OUT), through its UNESCO Chair on Teacher Education and Curriculum, has completed a dissemination and certificate award workshop for 24 STEM teachers from Iringa District Council who were trained under the CL4STEM digital skills programme.

TANZANIA NA MAREKANI ZASONGA MBELE KUKAMILISHA MAKUBALIANO MAKUBWA YA UWEKEZAJI

December 08, 2025 Add Comment


Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, leo amefanya mazungumzo na Kaimu Balozi wa Marekani nchini Tanzania, Andrew Lentz, katika Ikulu ya Chamwino, kujadili maeneo muhimu ya ushirikiano na kuimarisha dhamira ya pamoja ya kujenga ushirikiano wa kisasa na wenye manufaa kwa pande zote mbili.


Balozi Lentz—aliyefuatana na Mshauri wa Masuala ya Kisiasa na Uchumi—amesisitiza dhamira ya Washington kuhuisha mahusiano na kuongeza kina la ushirikiano wa kiuchumi, kisiasa na kiusalama kati ya mataifa haya mawili.

“Marekani imejitolea kujenga ushirikiano usiotegemea misaada, bali unaojengwa juu ya ustawi wa pamoja,” alisema Balozi Lentz.


Mazungumzo yamejikita katika hatua za majadiliano ya miradi mikubwa inayoongozwa na kampuni za Marekani. Pande zote mbili zimekubaliana kuwa majadiliano ya miradi miwili ya kimkakati—Mradi wa LNG na Mradi wa Tembo Nickel—yamefikia hatua za mwisho kabla ya kutiwa saini rasmi. Uwekezaji wa tatu, Mradi wa Mahenge Graphite, unaendelea kufanyiwa uchambuzi wa kiufundi.

Rais Samia ameukaribisha upya msimamo wa Marekani na kuhakikishia ujumbe huo kuwa Tanzania itaendelea kusimamia hatua zote zilizobaki ili kukamilisha taratibu na kufungua njia ya utekelezaji wa miradi hiyo.


“Kama taifa lisilofungamana na upande wowote, Tanzania iko wazi, tayari na imejitoa kufanya kazi na washirika wote wanaoheshimu uhuru wetu na kushiriki katika dira yetu ya maendeleo,” alisema Rais.

“Miradi hii ni ya umuhimu mkubwa kwa taifa, na tumejidhatiti kuikamilisha ili iweze kufungua ajira, uwekezaji, na ustawi endelevu kwa wananchi wetu.”


Rais pia alibainisha kuwa zaidi ya kampuni 400 za Marekani kwa sasa zinafanya shughuli zao nchini Tanzania—kiashiria cha uthabiti wa nchi, mazingira mazuri ya uwekezaji na historia ya muda mrefu ya ushirikiano wa kiuchumi kati ya mataifa haya mawili.


Mbali na uwekezaji, mazungumzo yamegusa maeneo mapana ya ushirikiano ikiwemo utulivu wa kisiasa, usalama wa kikanda, mageuzi ya kiuchumi, ukuaji wa sekta binafsi, ushirikiano katika afya na programu za kubadilishana uzoefu kati ya wananchi wa nchi hizi mbili.


Balozi Lentz amempongeza Rais Samia kwa maono na mipango madhubuti ya muda mrefu kupitia Vision 2050, na kusisitiza kuwa Serikali ya Marekani iko tayari kuunga mkono utekelezaji wake pamoja na kuimarisha falsafa ya 4R ya Rais—maridhiano, ustahimilivu, mageuzi na kujenga upya imani katika utawala.


Pande zote zimekubaliana kuwa mawasiliano ya karibu, ushirikiano wa mara kwa mara, na hatua za haraka katika kukamilisha makubaliano yaliyosalia ni muhimu katika kufungua uwezo kamili wa uhusiano kati ya Tanzania na Marekani.


Kikao hiki kinawakilisha hatua muhimu katika kufafanua upya na kuhuisha mahusiano kati ya Tanzania na Marekani. Dhamira ya pamoja iliyothibitishwa na serikali zote mbili inaashiria mwanzo wa ushirikiano wa kisasa, wazi, unaoongozwa na sekta binafsi—ukijengwa juu ya ustawi wa pamoja, kuheshimiana na ushirikiano wa muda mrefu wa kimkakati.


Miradi Mikuu ya Kimkakati


1. Mradi wa LNG — Thamani Inayokadiriwa: Dola Bilioni 42


Mradi mkubwa wa kugundua na kuchakata gesi asilia unaohusisha kampuni kubwa za kimataifa za nishati. Mradi huu unalenga kufungua hazina kubwa ya gesi iliyopo baharini, kuongeza mapato ya taifa, kuunda maelfu ya ajira na kuiweka Tanzania katika ramani ya dunia kama mchezaji muhimu wa LNG.


2. Mradi wa Tembo Nickel — Thamani: Dola Milioni 942


Uwekezaji mkubwa wa madini muhimu eneo la Ngara unaolenga nikeli—kiungo muhimu katika utengenezaji wa betri za magari yanayotumia umeme. Mradi huu utaimarisha minyororo ya kimataifa ya nishati safi, kuchochea viwanda na kuongeza pato la mauzo ya nje.


3. Mradi wa Mahenge Graphite — Thamani: Dola Milioni 300


Chanzo kikubwa duniani cha madini ya graphite yenye ubora wa juu, yenye umuhimu katika uzalishaji wa betri na teknolojia za nishati jadidifu. Mradi huu utaimarisha nafasi ya Tanzania kama mtoa huduma mkuu wa malighafi muhimu za viwanda vya kisasa vya betri.

TPDC NA PURA HAKIKISHENI WA TANZANIA WANANUFAIKA NA RASILIMALI ZA MAFUTA NA GESI-MHE.SALOME

December 08, 2025 Add Comment


📌*Awekea mkazo upatikanaji wa ajira, huduma za kijamii na nishati nafuu*


📌*Apongeza PURA na TPDC kwa jitihada wanazofanya katika utafiti na uendelezaji wa Mafuta na Gesi Asilia*


📌*Asisitiza mazingira rafiki ya uwekezaji*


Naibu Waziri wa Nishati Mhe. Salome Makamba amefanya ziara katika  Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) pamoja na Mamlaka ya Udhibiti wa Mkondo wa Juu wa Petroli (PURA) kwa lengo la kuzungumza na Watendaji taasisi hizo mara baada ya kuteuliwa na Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan kushika nyadhifa hiyo  ambapo amewataka watendaji kuhakikisha  Watanzania wananufaika moja kwa moja na uwepo wa rasilimali za mafuta na gesi.


Katika mazungumzo hayo yaliyofanyika jijini Dar es Salaam, Mhe. Salome ameweka mkazo kuhusu upatikanaji wa ajira kwa Watanzania, huduma za kijamii na upatikanaji wa nishati kwa gharama nafuu. 

Mhe. Salome pia ameielekeza Menejimenti ya TPDC kuongeza kasi ya usambazaji wa gesi asilia majumbani ili Watanzania waendelee kunufaika zaidi na rasilimali hiyo muhimu.

Vilevile  ameipongeza TPDC kwa jitihada wanazoendelea kufanya katika utafutaji na uendelezaji wa rasilimali za mafuta na gesi asilia nchini kwani uboreshaji huo umeanza kuleta matokeo chanya katika upatikanaji wa nishati hiyo katika maeneo mbalimbali nchini huku akiwataka kuhakikisha jitihada hizo zinawanufaisha wananchi wengi zaidi.

Katika hatua nyingine, Mhe. Salome amewapongeza PURA kwa kazi nzuri wanazozifanya katika kuhakikisha sekta ya mafuta inakua nchini huku akiwahimiza kuhakikisha mazingira ya uwekezaji yanakuwa rafiki kwa wawekezaji wapya ili kuongeza ajira na kuhakikisha wananchi wanapata manufaa ya moja kwa moja kutokana na rasilimali na uwekezaji uliopo nchini.  

Aidha, amesisitiza kuwa miradi ya utafiti na uendelezaji wa gesi asilia, ikiwemo mradi wa LNG, ipewe kipaumbele ili kuongeza tija katika uwekezaji na kuhakikisha nchi inanufaika kikamilifu na rasilimali zake huku akisisitiza kuwa taasisi zote zilizo chini ya Wizara lazima ziweke mbele maslahi ya wananchi wakati wa kusimamia miradi ya kimkakati ya nishati lakini pia kufuatilia utekelezaji wa maagizo ya Serikali kuhusu usimamizi, matumizi na faida za rasilimali za gesi asilia.


Kwa upande wake, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati, Dkt. James Mataragio amewasisitiza TPDC kuongeza kasi ya uzalishaji na upatikanaji wa  gesi ili nishati hiyo iwe ya kutosha na inawafikia wananchi huku akiisisitiza PURA kuhakikisha wanawapa wawekezaji kipaumbele katika kuwekeza katika fursa za mafuta na gesi kwa lengo la kuhakikisha Serikali inapata mapato na wananchi wananufaika na miradi hiyo.



Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa TPDC Mussa Makame amesema shirika linaendelea kuimarisha miundombinu ya kuhifadhi na kusafirisha nishati ya mafuta na gesi, huku likiandaa vizuri upande wa maboresho ya masoko ili kuongeza ufanisi na upatikanaji wa bidhaa hizo nchini na kueleza kuwa kampuni ipo kwenye hatua za kufanya upanuzi wa miradi ya gesi, ikiwemo utekelezaji wa miradi midogo ya LNG itakayowezesha kusafirisha gesi hiyo katika mikoa mbalimbali kwa gharama nafuu na kwa wakati.

Naye Mkurugenzi Mkuu wa PURA, Eng. Charles Sangweni amesema PURA itaendelea kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi huku ikichangia kufanikisha malengo ya sekta kwa mujibu wa Dira ya Taifa 2050.

#Siku100ZaMhe.RaisNishatiTunatekeza.

#NishatiTupoKazini.

NAIBU WAZIRI WA NISHATI APONGEZA TPDC KWA JITIHADA ZA UENDELEZAJI WA NISHATI YA MAFUTA NA GESI ASILIA

December 08, 2025 Add Comment
Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba, amekutana na Uongozi wa Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) na kuwapongeza kwa jitihada wanazoendelea kufanya katika utafutaji na uendelezaji wa rasilimali za mafuta na gesi asilia nchini.

JK AENDELEA KUWA KINARA WA ELIMU DUNIANI

December 08, 2025 Add Comment


Rais Mstaafu Jakaya Dkt. Mrisho Kikwete, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Bodi ya Taasisi ya Kimataifa inayoshughulikia Masuala ya Elimu Duniani (Global Partnership for Education - GPE) akiongea na wajumbe wa Bodi ya GPE baada ya kumalizika kwa mkutano huo mjini Brussels, Ubelgiji. Pamoja naye ni Afisa Mtengaji Mkuu wa GPE, Bi Laura Frigenti


Rais Mstaafu Jakaya Dkt. Mrisho Kikwete, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Bodi ya Taasisi ya Kimataifa inayoshughulikia Masuala ya Elimu Duniani (Global Partnership for Education - GPE) ameendelea na jitihada za kukuza elimu duniani.

Kwa nafasi yake ya Mwenyekiti wa Bodi ya GPE alisimamia Mkutano wa mwisho wa Bodi hiyo wa kuhitimisha Mpango wa 4 wa Miaka 5 wa Mzunguko wa Ufadhili wa GPE (4th financing campaign 2021 - 2025) ambao ulifanikiwa kukusanya takriban Dola za Kimarekeni bilioni 4.1 kwa ajili ya kugharamia uboreshaji wa elimu ya awali na ya msingi kwa watoto wanaoishi katika nchi za kipato cha chini na zinazoendelea, hususan watoto wa kike na wale wanaojikuta kwenye mazingira magumu kama vile ya vita, ukame, mafuriko, nk.

Pamoja na mambo mengine, Mkutano huo uliofanyika wiki hii huko Brussels, Ubelgiji ulitathmini mkakati wa kukusanya fedha uliofanyika kwa mafanikio katika kukusanya fedha kupitia utaratibu wa misaada (grants) na ufadhili wa pamoja (co - financing) ambapo nchi zinazonufaika na miradi ya GPE huchangia kiasi cha fedha kwenye sekta ya elimu na GPE huongezea kiasi kinachobakia kwa makubaliano maalumu.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na GPE, kiasi hicho cha Dola za Marekani milioni 4.7 kilichopatikana kimesaidia kuboresha elimu kwa watoto takriban milioni 372 duniani kote huku watoto milioni 10 zaidi wakiandikishwa shule. Aidha, kupitia ufadhili wa GPE, walimu milioni 4.7 kote duniani walipatiwa mafunzo ya kuwaongezea ujuzi.

Aidha, Mkutano huo ulipokea taarifa ya mkakati wa utekelezaji wa mpango mpya wa 5 wa kampeni ya ufadhili wa GPE utakaoanza mwaka 2026 hadi 2030. Kampeni hiyo imelenga kukusanya Dola za Marekani milioni 5 na itaongozwa kwa pamoja kati ya Rais Bola Tinubu wa Nigeria na Waziri Mkuu Giorgia Meloni wa Italia. Fedha zitakazopatokana kutokana na kampeni hiyo zitaongeza wigo wa GPE kuhudumia watoto takriban milioni 750 kote duniani kwa kuwapatia elimu bora zaidi inayoendana na mahitaji ya karne ya 21.

Vilevile, Mkutano huo ulishukuru baadhi ya nchi ambazo zimeahidi kuendeleza ushirikiano na GPE kama vile Ujerumani ambayo tayari imeahidi kuchangia kampeni hii mpya ya GPE kiasi cha Dola za Marekani milioni 320 kwa kipindi cha miaka 6 ijayo.

Kwa kuzingatia mabadiliko ya sasa ya hali ya kifedha duniani ambapo wafadhili mbalimbali, hususan nchi zilizoendelea, zinabadilisha vipaumbele vyao vya maeneo ya kuelekeza ufadhili, Taasisi ya GPE imelenga kuendelea kuhakikisha inasimamia na kutumia vizuri fedha zinazotolewa na wafadhili ili kuwanufaisha watoto wengi zaidi duniani. Vilevile, GPE imepanga kuendelea kuzishawishi nchi ambazo siyo wafadhili waliozoeleka wa GPE (non traditional donors) kama vile nchi za mashariki ya kati ili ziweze kuoanisha programu zao za kusaidia elimu duniani na zile za GPE, na kuongeza fedha zaidi wanazochangia kwa GPE.

Kama sehemu ya kutekeleza mkakati huo, Mwenyekiti huyo wa Bodi ya GPE Dkt. Kikwete leo amepata fursa ya kushiriki Mkutano wa 23 wa Kimataifa wa Qatar ambapo ametumia nafasi hiyo kueleza utayari wa GPE kuendelea kushirikiana na Serikali ya Qatar katika jitihada zake za kusaidia watoto wenye mahitaji mbalimbali ya kielimu kote duniani.

Aidha, katika mazungumzo yake na Viongozi mbalimbali wa Taifa la Qatar pambezoni mwa Mkutano huo ameeleza nia ya GPE amepongeza mchango mkubwa wa Qatar katika elimu duniani na kuihakikishia utayari wa GPE kuendelea kushirikiana na Serikali ya Qatar na Shirika la Qatar la Education Above All Foundation.

GPE ni Taasisi iliyoanzishwa na Kundi la Nchi zenye Uchumi na Utajiri Mkubwa Duniani (G7) mwaka 2002 ili kuharakisha ufikiwaji wa lengo la elimu la kuhakikisha kila mtu, bila kujali umri, jinsia au hali ya kijamii, anapata elimu ya msingi bila malipo na kwa usawa. Tanzania ni moja ya nchi 90 zinazonufaika na miradi inayotekelezwa na GPE ambapo tangu ilipojiunga mwaka 2013 imeshapokea zaidi ya misaada yenye thamani ya Dola za Marekani milioni 344 kusaidia jitihada zinazofanywa na Serikali kuendeleza elimu ya awali na ya msingi.

Rais Mstaafu Jakaya Dkt. Mrisho Kikwete, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Bodi ya Taasisi ya Kimataifa inayoshughulikia Masuala ya Elimu Duniani (Global Partnership for Education - GPE) akiteta jambo na Bi. Christine nHogan, Makama mwenyekiti wa GPE wakati wa mkutano wao mjini Brussels, Ubelgiji.
Rais Mstaafu Jakaya Dkt. Mrisho Kikwete, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Bodi ya Taasisi ya Kimataifa inayoshughulikia Masuala ya Elimu Duniani (Global Partnership for Education - GPE) akishiriki Mkutano wa 23 wa Kimataifa wa Qatar mjini Doha

Rais Mstaafu Jakaya Dkt. Mrisho Kikwete, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Bodi ya Taasisi ya Kimataifa inayoshughulikia Masuala ya Elimu Duniani (Global Partnership for Education - GPE) akiteta jambo na Dkt Hamad bin Abdulaziz Al Kawari, Waziri wa Nchi na Naibu Waziri Mkuu wa Qatar, mjini Doha leo. Kulia ni Balozi wa Tanzania nchini Qatar, Mhe Habib Awesi Mohamed.



VIKUNDI 29 VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU VYALAMBA MILIONI 250 HALMASHAURI MUHEZA

December 08, 2025 Add Comment




Na Oscar Assenga, MUHEZA

VIKUNDI 29 vya Wanawake,Vijana na Watu Wenye ulemavu wamekabidhiwa Milioni 250 zinazotokana na mikopo asilimia 10 kutoka katika Halmashauri ya wilaya ya Muheza ikiwa ni kuwawezesha kujikwamua kiuchumi wao na jamii zao.

Makabidhiano ya Hundi ya Fedha hizo ilitolewa na Mkuu wa Mkoa wa Tanga Dkt,Balozi Batilda Burian na kushuhudiwa na viongozi mbalimbali wa wilaya ya Muheza akiwemo Mkuu wa wilaya,Mkurugenzi wa Halmashauri,Mwenyekiti wa Halamshauri na Madiwani wa Halmshauri hiyo.

Akizungumza baada ya kukabidhi mikopo hiyo ,Mkuu huyo wa Mkoa aliwaasa wanufaika wa mikopo ya asilimia 10 ya Halmashauri kuitumia kwa uangalifu ili kuweza kujikwamua kiuchumi pamoja na kuhakikisha wengine nao wananufaika na fursa hizo.

Alisema kwamba dhamira ya Rais Dkt Samia Suluhu ni kuona mikopo hiyo inawafikia wahitaji bila kuwepo kwa vikwazo vya aina yoyote kupitia mfumo wa mtandao bila kuhitaji kumjua mtu .

Aidha alitoa wito kwa vijana kujitokeza kwa wingi kuchangamkia fursa za uwepo wa mikopo hiyo ili waweze kujikwamua kiuchumi.

“Tumekubaliana kuandaa kongamano la vijana litakalowakutanisha maafisa maendeleo ya jamii na wadau wa mikopo kwa lengo la kuwaelimisha juu ya mchakato mzima wa kuipata na jinsi ya kuunda vikundi imara”Alisema

Mkuu huyo wa mkoa alisema lengo ni kuhakikisha kila kijana anakuwa na uelewa hatua za kuomba mikopo na kutumia fursa zilizopo.

Awali akizungumza Mkuu wa wilaya ya Muheza Ayoub Sebabili alisema kwamba mikopo iliyozinduliwa ya asilimia 10 ,wanawake asilimia 4,vijana 4 na walemavu 2 huku akimpongeza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Muheza Dkt Jumaa Mhina na menejimentii ya halmshauri kwa kuratibu vizuri mikopo na kuwafikia walengwa.

Aliwaomba wanufaika wa mikopo hiyo watoa ushirikiano kwenye marejesho ili kuweza kutoa nafasi watu wengine kupata mikopo kwa lengo la kukuza kipato na kujikwamua kiuchumi.





“Tunaopokea mikopo hii tutoe ushirikiano wakati wa marejesho kwa sababu utapelekea mfuko wa mikopo uweze kuwa endelevu na kuwafikia watu wengine na hivyo kuondoa umaskini kwa mtu mmoja mmoja na wengine kunufika nayo”Alisisitiza



Naye kwa upande wake Mkurugenzi wa Halmshauri ya Muheza Dkt Jumaa Mhina alimpongeza Mkuu huyo wa wilaya akieleza kwamba ndio muhimili wa halmashauri kuhakikisha asilimia 10 inatoka na kufikia vikundi hivyo.


Dkt Jumaa alisema kwamba wameweka mkazo kwa vikundi vyote lakini hususani kwa vijana ambao siku za nyuma walikwa wanawatafuta kwa tochi hivyo sasa watawafuata vijana walipo ili kuwaibua waweze kuunda vikundi na hivyo kunufaika na mikopo asilimia 10 ikiwa ni sehemu ya kutengeneza ajira .



Imbeju: Programu Inayozalisha Fursa na Kuunganisha Watanzania na Huduma za Kifedha

December 08, 2025 Add Comment

 

  
Dar es Salaam – Katika hafla ya Marketers Night Out iliyofanyika jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB Bank Foundation, Tully Esther Mwambapa, aliwasilisha mada iliyoangazia kwa kina mchango wa programu ya Imbeju katika kubadilisha maisha ya wananchi, hasa wanawake na vijana, kupitia uwezeshaji wa kiuchumi na kukuza ujumuishi wa kifedha nchini.

Akizungumza mbele ya wataalamu wa masoko, viongozi wa taasisi, wajasiriamali na wadau wa maendeleo, Mwambapa alisema Imbeju ni zaidi ya mpango wa kutoa mikopo pekee bali ni programu jumuishi inayolenga kujenga msingi imara wa ujasiriamali. Alieleza kuwa programu hiyo imejengwa juu ya nguzo tatu kuu; elimu ya ujasiriamali na uongozi, upatikanaji wa mitaji rafiki, pamoja na uunganishaji wa wajasiriamali na masoko pamoja na huduma rasmi za kifedha.
 
“Kupitia mafunzo ya vitendo, washiriki huwezeshwa kuendesha biashara zao kwa ufanisi zaidi, kutumia fursa za teknolojia, kufuatilia mapato na faida kwa weledi na kufanya maamuzi sahihi ya uwekezaji. mbinu hiyo imewezesha wajasiriamali wengi kuimarisha biashara zao na kuongeza ajira katika jamii”, alisema Mwambapa

Akizungumzia wanawake, Mwambapa alieleza kuwa wamekuwa walengwa muhimu wa programu kwani ndio mhimili wa ustawi wa familia na jamii. Wanawake wengi waliokuwa wakikabiliwa na changamoto za mtaji na elimu ya ujasiriamali sasa wameweza kuanzisha au kupanua biashara zao kupitia Imbeju, jambo lililosababisha kuongezeka kwa uzalishaji, kuboreshwa kwa kipato cha kaya na kuinuka kwa hali ya maisha ya familia zao. Alisisitiza kuwa uwekezaji kwa mwanamke mmoja hupelekea kuleta mafanikio kwa kizazi kizima.

Kwa upande wa vijana, alisema programu hiyo imekuwa chachu ya kubadilisha fikra bunifu kuwa miradi halisi katika maeneo ya teknolojia, kilimo-biashara, sanaa na biashara mtandao. Kupitia ushauri wa kitaalmu, mafunzo na ufadhili wa mawazo bunifu, vijana wengi wamepata uwezo wa kuzifikisha bidhaa zao katika masoko mengi zaidi kupitia majukwaa ya kidijitali, hivyo kuongeza ushindani na kupanua wigo wa biashara zao.
Mwambapa pia aligusia mchango wa Imbeju katika kukuza ujumuishi wa kifedha nchini kwa kuwawezesha wananchi waliokuwa nje ya mfumo rasmi wa benki kufungua akaunti, kujiwekea akiba, kukopa na kufanya miamala kwa urahisi zaidi baada ya kupata elimu ya kifedha. Kupitia ushirikiano wa CRDB Bank Foundation na Benki ya CRDB, huduma hizi sasa zimefika hata maeneo ya vijijini ambako upatikanaji wa huduma za kifedha ulikuwa mdogo awali.

Alisema hatua hiyo imeimarisha uthabiti wa biashara ndogondogo, kuongeza uwezo wa kujitegemea kwa wananchi na kuongeza mchango wa sekta hiyo katika ukuaji wa uchumi wa taifa.

Akihitimisha mada yake, Mwambapa alitoa wito kwa wadau wote kuendelea kuwekeza katika mipango inayowawezesha wanawake na vijana, akisisitiza kuwa mafanikio ya Imbeju ni ushahidi kuwa uwekezaji katika watu ndiyo msingi wa kujenga uchumi jumuishi, thabiti na wenye tija kwa kizazi cha sasa na kijacho.

WANANCHI VUO WAPATIWA FEDHA KUNUSURU RASILIMALI BAHARI

December 07, 2025 Add Comment


‎Na Boniface Gideon,TANGA

‎Wakazi wa kijiji cha vuo wilayani Mkinga mkoani Tanga,wamepatiwa mafunzo ya usimamizi wa mazingira ya Bahari na usimamizi wa fedha ikiwa ni juhudi za kunusuru viumbe Bahari ikiwemo makazi ya samaki ( matumbawe) ,kulinda uvuvi haramu,kutunza fukwe ,upandaji miti ya mikoko pamoja na kulima kilimo cha mwani.

‎Sambamba na mafunzo hayo,wakazi wamepatiwa fedha Sh.10.5 Mil.kwaajili ya kuendesha biashara ili kupunguza utegemezi wa shughuli za baharini,


Fedha hizo ni sehemu ya mradi wa pwani yetu unaosimamiwa na Shirika la Maendeleo la GIZ kwakushirikiana na Shirika la Mwambao Coastal Community Network Tanzania.

‎Akizungumza ,wakati wa hafla ya kukabidhi fedha  kwa Wakazi wa kijiji hicho,Mratibu wa mipango kutoka Shirika la Mwambao Coastal Community Network Tanzania,Abubakar Masoud,alisema fedha hizo zimetolewa kwenye vikundi 5 vyenye wanachama 150 ,kwaajili yakuwasaidia kujikwamua kiuchumi kupitia biashara ili kupunguza utegemezi wa shughuli za kibinadamu baharini,

‎"fedha hizi ,ni sehemu ya mkakati wetu wa kupunguza shughuli za kibinadamu baharini na kuongeza kipato kwa wakazi ,tunatarajia kuona matokeo chanya ya fedha hizi,niwaombe Watu wote mnaokwenda kunufaika na fedha hizi ,mkazitumie kwenye malengo yaliyokusudiwa ili yalete matokeo chanya yaliyokusudiwa "Alisisitiza Masoud


‎Kwaupande wake ,mratibu wa Shirika la Mwambao Coastal Community Network Tanzania mkoa wa Tanga ,Ahmad Salim ,alisema ,kabla ya kutolewa kwa fedha hizo,wakazi wa kijiji hicho walipatiwa mafunzo maalumu ya kuwajengea uwezo kwenye nyanja mbalimbali ikiwamo utunzaji wa mazingira na usimamizi wa fedha,


‎"Kabla ya hatujatoa fedha hizi,tulianza kuwajengea uwezo wa kiuchumi,usimamizi wa mazingira na fedha ,lengo ni kuwafanya wakazi hawa waweze kujisimamia hata sisi tukiwa hatupo,tunaamini Elimu waliyoipata itawasaidia kusimamia utunzaji wa mazingira na fedha,na kila mmoja atakuwa balozi wa mazingira,hivyo niwaombe kila aliyepata Elimu hii akawe balozi wa mazingira ili tutimize lengo" aliongeza Ahmad


‎ MWISHO