HABARI MPYA
HABARI
SIASA
ELIMU
Recent Posts
WAZIRI MKUU APONGEZA TPDC KWA UJENZI WA SHULE YA MSINGI LIKONG'O KUPITIA MRADI WA LNG
habari Nishati📌*Asema ni utimizaji wa majukumu ya kijamii kupitia miradi*
📌*Akumbusha shule kufungwa miundombinu ya Nishati Safi ya Kupikia kuunga mkono jitihada za Rais Samia*
📌*Mhe. Salome asema taasisi 52 zitasambaziwa nishati safi ya kupikia ndani ya siku 100 za uongozi wa Rais Samia*
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.Dkt. Mwigulu Nchemba amepongeza Wizara ya Nishati kupitia Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) kwa ujenzi wa shule bora ya Awali na Msingi katika Kijiji cha Likong'o mkoani Lindi inayojengwa kupitia mradi wa uzalishaji na usindikaji wa Gesi Asilia kuwa kimiminika ( LNG). .
Waziri Mkuu ametoa pongezi hizo tarehe 20 Desemba 2025 wakati akikagua ujenzi wa shule hiyo itakayokuwa na uwezo wa kuhudumia wanafunzi 400 katika Kijiji cha Likong'o, Kata ya Mbanja, Halmashauri ya Manispaa ya Lindi.
" Nawapongeza TPDC kwa hatua hii ya kutekeleza shughuli za uwajibikaji kwa jamii (CSR) kupitia mradi huu wa LNG, shule hii ni bora ya kisasa na imezingatia mahitaji mbalimbali ikiwemo kuwa na miundombinu inayokidhi watu wenye mahitaji maalum na watoto wa kike." Amesema Mhe. Nchemba
Katika hatua nyingine Dkt. Nchemba ametoa msisitizo kwa Wizara ya Nishati kuhakikisha kuwa shule hiyo inafungwa miundombinu ya Nishati Safi ya Kupikia kuunga mkono utekelezaji wa Ajenda ya Nishati Safi ya Kupikia ambayo kinara wake ni Rais, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan.
Kutokana na uwepo wa shule hiyo, Waziri Mkuu amewaasa wananchi kuchangamkia fursa kwa kuwasomesha watoto wao na hivyo kuunga mkono jitihada anazofanya Rais Rais Samia za ujenzi shule katika maeneo mbalimbali nchini ili kuwawezesha watoto wote kupata elimu.
Kwa upande wake Mhe. Salome Makamba ambaye ni Naibu Waziri wa Nishati, amesema mradi wa ujenzi wa Shule ya Msingi Likong'o unatekelezwa kama sehemu ya kurudisha fadhila kwa wananchi waliotoa ardhi kwa ajili ya utekelezaji mradi wa LNG.
Ameeleza kuwa ujenzi wa Shule hiyo ambao umefikia asilimia 70 unaonesha jinsi kaulimbiu ya kazi na utu inavyotekelezwa kwa vitendo na Serikali ya Awamu ya Sita.
Katika hatua nyingine, Mhe. Salome ameeleza kuwa agizo la Waziri Mkuu la shule hiyo kuwekewa miundombinu ya nishati safi ya kupikia litatekelezwa na kuongeza kuwa ndani ya siku 100 za uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan taasisi 52 zitasambaziwa miundombinu ya nishati safi ya kupikia.
Naye, Mbunge wa Lindi, Mohamed Utaly amemshukuru Rais Samia kwa uwekezaji huo wa mradi wa LNG ambao amesema unaleta chachu ya elimu mkoani Lindi.
Amepongeza pia TPDC kwa kuhakikisha kuwa miradi ya uwajibikaji kwa jamii imeanza kutekelezwa mapema kupitia mradi huo wa LNG.
Awali, Mhandisi Msimamizi wa mradi wa shule ya Awali na Msingi Likong'o, Upendo Mahavanu kutoka TPDC alisema mradi huo unagharimu Sh .bilioni 1.27 ambapo shule itakuwa na Madarasa 9; saba yakiwa ni ya shule msingi na mawili ni ya awali. Pia kutakuwa na ofisi na nyumba za walimu.
Utekelezaji wa mradi wa LNG unatarajiwa kuwa na manufaa mbalimbali nchini ikiwemo mapato ya Serikali yatakayotokana na uuzaji wa LNG kwenye soko la kimataifa, fursa za ajira, fursa kwa wazawa kuuza bidhaa, uhaulishaji wa teknolojia mbalimbali ili kuwajengea uwezo wataalam wa ndani n.k
KAMISHNA BADRU AENDELEA KUIMARISHA UHUSIANO NA JAMII INAYOISHI NDANI YA MAMLAKA YA HIFADHI YA NGORONGORO
Mwandishi wetu Endulen Ngorongoro.
Tarehe 20 Desemba, 2025
Uhusiano kati ya Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro (NCAA) na jamii inayoishi ndani ya eneo la hifadhi umeendelea kuimarika kufuatia ziara za Kamishna wa Uhifadhi wa NCAA, Bw. Abdul-Razaq Badru katika vijiji mbalimbali vilivyoko tarafa ya Ngorongoro ambapo leo tarehe 20 Desemba,2025 ametembelea Kata ya Enduleni, wilayani Ngorongoro.
Akiwa ameambatana na baadhi ya wajumbe wa Menejimenti ya Ngorongoro na Diwani wa Kata ya Endulen Mhe. Elias Sakara Nagol, Kamishna Badru ameeleza kuwa, lengo la ziara hiyo ni kuendelea kuimarisha uhusiano kati ya Uongozi wa hifadhi ya Ngorongoro na jamii, pamoja na kukagua maboresho ya miundombinu ya maji inayotumika kwa matumizi ya wananchi, mifugo na wanyamapori.
Katika ziara hiyo Kamishna Badru amewaeleza wananchi wa vijiji vya Kata ya Enduleni kuwa Mamlaka inatekeleza Miradi ya Maji katika kata za Endulen, Kakesio, Olbalbal na maeneo mengine na aliwahimiza wananchi kushiriki kikamilifu katika usimamizi na utunzaji wa miradi hiyo ambayo inagharimu fedha za Serikali.
Kwa upande wake, Diwani wa Kata ya Enduleni, Dkt. Elias Sakara Nagol, amempongeza Kamishna Badru na wasaidizi wake kwa kuendeleza uhusiano ya karibu na jamii inayoishi ndani kwa kuwatembelea mara kwa mara, kusikiliza kero zao na kushirikiana nao katika masuala mbalimbali ya kijamii na kuahidi kuwa wananchi wataendelea kuwa mabalozi wazuri wa kutunza na kulinda hifadhi kupitia programu ya uhifadhi shirikishi.
WAZIRI MKUU APONGEZA TPDC KWA UJENZI WA SHULE YA MSINGI LIKONG'O KUPITIA MRADI WA LNG
habari 

FCC YANG’ARA KATIKA KONGAMANO LA 16 LA WATAALAMU WA MANUNUZI NA UGAVI
habari
Naibu Waziri wa Fedha, Mhe.Mshamu Munde,akimkabidhi tuzo Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano cha FCC, Bi. Roberta Feruzi kwa niaba ya Waziri wa Fedha tuzo hiyo imetolewa kwa Tume ya Ushindani (FCC) kutambua mchango wake katika maendeleo ya Sekta ya Manunuzi na Ugavi nchini.Hafla ya utoaji wa tuzo hiyo ilifanyika katika Kongamano la 16 la Wataalamu wa Manunuzi na Ugavi,lililoandaliwa na Bodi ya Wataalamu na Mafundi wa Ununuzi na Ugavi (PSPTB) jijini Arusha.
....
TUME ya Ushindani (FCC) imetunukiwa tuzo maalum ya kutambua mchango wake katika maendeleo ya Sekta ya Manunuzi na Ugavi nchini.
Tuzo hiyo imekabidhiwa na Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Mshamu Munde, kwa niaba ya Waziri wa Fedha, na kupokelewa na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano cha FCC, Bi. Roberta Feruzi.
Hafla ya utoaji wa tuzo hiyo ilifanyika katika Kongamano la 16 la Wataalamu wa Manunuzi na Ugavi, lililofanyika katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Arusha (AICC), jijini Arusha lililoandaliwa na Bodi ya Wataalamu na Mafundi wa Ununuzi na Ugavi (PSPTB).
FCC imeshiriki kongamano hilo kama mdau muhimu wa sekta ya manunuzi na ugavi, ambapo iliwasilisha mada kuhusu umuhimu wa ushindani wa haki katika masuala ya manunuzi na ugavi, hususan katika kulinda mnyororo wa thamani.
Kupitia kongamano hilo, Tume pia ilitoa elimu kwa wadau mbalimbali kuhusu majukumu na kazi zake, ikisisitiza nafasi yake katika kuhakikisha mazingira ya ushindani yanayochochea uwazi, ufanisi na maendeleo endelevu ya sekta ya manunuzi na ugavi nchini.

Naibu Waziri wa Fedha, Mhe.Mshamu Munde,akimkabidhi tuzo Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano cha FCC, Bi. Roberta Feruzi kwa niaba ya Waziri wa Fedha tuzo hiyo imetolewa kwa Tume ya Ushindani (FCC) kutambua mchango wake katika maendeleo ya Sekta ya Manunuzi na Ugavi nchini.Hafla ya utoaji wa tuzo hiyo ilifanyika katika Kongamano la 16 la Wataalamu wa Manunuzi na Ugavi,lililoandaliwa na Bodi ya Wataalamu na Mafundi wa Ununuzi na Ugavi (PSPTB) jijini Arusha.

Naibu Waziri wa Fedha, Mhe.Mshamu Munde,akimkabidhi tuzo Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano cha FCC, Bi. Roberta Feruzi kwa niaba ya Waziri wa Fedha tuzo hiyo imetolewa kwa Tume ya Ushindani (FCC) kutambua mchango wake katika maendeleo ya Sekta ya Manunuzi na Ugavi nchini.Hafla ya utoaji wa tuzo hiyo ilifanyika katika Kongamano la 16 la Wataalamu wa Manunuzi na Ugavi,lililoandaliwa na Bodi ya Wataalamu na Mafundi wa Ununuzi na Ugavi (PSPTB) jijini Arusha.

Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Ushindani (FCC) Bi. Khadija Ngasongwa,akizungumza katika Kongamano la 16 la Wataalamu wa Manunuzi na Ugavi, lililoandaliwa na Bodi ya Wataalamu na Mafundi wa Ununuzi na Ugavi (PSPTB) jijini Arusha.

Meneja Huduma za Sheria FCC Bw. Josephat Mkizungo, akitoa mada katika Kongamano la 16 la Wataalamu wa Manunuzi na Ugavi,lililoandaliwa na Bodi ya Wataalamu na Mafundi wa Ununuzi na Ugavi (PSPTB) jijini Arusha.

Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Ushindani (FCC) Bi. Khadija Ngasongwa,akifuatilia mada mbalimbali wakati wa Kongamano la 16 la Wataalamu wa Manunuzi na Ugavi,lililoandaliwa na Bodi ya Wataalamu na Mafundi wa Ununuzi na Ugavi (PSPTB) jijini Arusha.

Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Ushindani (FCC) Bi. Khadija Ngasongwa (kushoto),akifuatilia mada mbalimbali wakati wa Kongamano la 16 la Wataalamu wa Manunuzi na Ugavi, lililofanyika jijini Arusha .Katikati ni Afisa Mtendaji Mkuu wa BRELA, Bw. Godfrey Nyaisa na Kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Missenyi Bw. John Paul Wanga.lililoandaliwa na Bodi ya Wataalamu na Mafundi wa Ununuzi na Ugavi (PSPTB) .

Naibu Waziri wa Fedha, Mhe.Mshamu Munde,akiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kukabidhi tuzo kwa Tume ya Ushindani (FCC) ya kutambua mchango wake katika maendeleo ya Sekta ya Manunuzi na Ugavi nchini.Hafla ilifanyika katika Kongamano la 16 la Wataalamu wa Manunuzi na Ugavi, lililoandaliwa na Bodi ya Wataalamu na Mafundi wa Ununuzi na Ugavi (PSPTB) jijini Arusha.
NSIMBO WACHANGAMKIA MAJIKO YA RUZUKU

HANDENI TUPO MGUU SAWA UTEKELEZAJI BIMA YA AFYA KWA WOTE
habari
Na Mwandishi Wetu, Handeni TC
Mkuu wa Wilaya ya Handeni, Mhe. Salum Nyamwese, amesema wilaya hiyo imejipanga kikamilifu kuhakikisha wananchi wanahamasika kujiunga na Bima ya Afya kwa Wote ili kuwa na uhakika wa kupata huduma bora za matibabu.
Akizungumza mjini Handeni, Mhe. Nyamwese amesema kuwa katika wilaya hiyo yenye Halmashauri ya Mji Handeni na Halmashauri ya Wilaya ya Handeni, Serikali imewekeza kwa kiasi kikubwa katika ujenzi wa miundombinu ya kisasa ya kutolea huduma za afya.
Amesema kuwa katika kuhakikisha wananchi wananufaika na bima ya afya kwa wote, wilaya imejiandaa kikamilifu kwa kuweka mazingira wezeshi ya utoaji huduma ikiwemo upatikanaji wa vituo vya afya, vifaa tiba, dawa pamoja na rasilimali watu.
“Wilaya yetu tumejipanga na tuna mikakati madhubuti ya kuhakikisha tunamsaidia Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan, kutimiza ahadi yake kwa Watanzania ya kuhakikisha wanapata huduma bora za afya kupitia bima ya afya kwa wote,” amesema Mhe. Nyamwese.
Amebainisha kuwa ndani ya wilaya ya Handeni kuna jumla ya vituo 84 vya kutolea huduma za afya ambavyo vimepatiwa vifaa tiba kulingana na ngazi ya utoaji huduma.
Aidha amesema huduma za kibingwa zinatolewa katika hospitali za wilaya kwa kushirikiana na wataalamu kutoka hospitali za rufaa za kikanda, hatua inayolenga kuhakikisha wananchi wanapata huduma karibu na maeneo yao.
Kuhusu upatikanaji wa dawa, Mkuu wa Wilaya amesema kuwa kwa sasa hali ni nzuri kwani zaidi ya asilimia 90 ya dawa zinapatikana katika hospitali zote za wilaya.
Ameongeza kuwa wilaya inatarajia kupokea wataalamu zaidi wa afya ili kuimarisha utoaji wa huduma, kutokana na Serikali tayari kuwekeza katika miundombinu na vitendea kazi.
“Nitoe wito kwa wananchi kutumia fursa ya bima ya afya kwa wote. Tusiiache itupite. Tutatangaziwa utaratibu wa kujiunga nayo na ni muhimu sisi wananchi kuwa mstari wa mbele kunufaika na fursa hii, kwani ina faida kubwa katika kupanua wigo wa upatikanaji wa huduma za afya,” amesisitiza Mhe. Nyamwese.

HAYAWI HAYAWI PUNDE YATAKUWA
*Macho na masikio tuyaelekeze ndani ya Hifadhi ya Taifa ya tano kwa ukubwa Tanzania.*
Tukio lililosubiriwa kwa hamu na bashasha tele la uzinduzi wa Kampeni yetu ya *“Shangwe la Sikukuu na TANAPA”* msimu wa pili linazinduliwa rasmi leo Desemba 20, 2025 ndani ya Hifadhi ya Taifa Katavi iliyopo mkoani Katavi.
Shangwe hilo mbali na uzinduzi rasmi pia litajumuisha utalii wa ndani wa kutembelea vivutio vya utalii, burudani kedekede na milindimo ya Wagongwe na wabembe sanjali na nyamachoma usiku!
Hii ni kali ya kufungia mwaka 2025 na kufungulia mwaka 2026. Ni ruksa kuja na umpendaye.
*“Asiye na mwana aeleke jiwe”.*
*Tukutane tambarare ya Katsunga ndani ya Hifadhi ya Taifa Katavi*

FCT YAELIMISHA WADAU KUHUSU HUDUMA NA MAJUKUMU YAKE
habari
BARAZA la Ushindani (FCT) jana Desemba 18, 2025, limeendesha semina ya elimu kwa wadau mkoani Mbeya kwa lengo la kuongeza uelewa kuhusu majukumu na huduma zinazotolewa na Baraza hilo.
Semina hiyo ilifanyika katika Ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mbeya na kufunguliwa na Katibu Tawala Msaidizi – Viwanda, Biashara na Uwekezaji Mkoa wa Mbeya, Bi Anna Mwambene, ambaye aliwahimiza wadau kutumia ipasavyo mifumo ya kisheria iliyopo na kuwa mabalozi wa kuitangaza huduma za Baraza la Ushindani.
Bi Mwambene alisema uelewa wa sheria na taratibu za ushindani ni muhimu katika kukuza mazingira bora ya biashara na uwekezaji, akisisitiza umuhimu wa wadau kushiriki kikamilifu katika kulinda haki zao kwa kutumia mifumo rasmi iliyowekwa na Serikali.
Katika semina hiyo, Baraza la Ushindani liliwapatia washiriki elimu kuhusu matumizi ya mfumo wa kidijitali wa kuwasilisha rufaa zinazotokana na maamuzi ya Tume ya Ushindani (FCC) pamoja na mamlaka mbalimbali za udhibiti, zikiwemo LATRA, EWURA, TCRA, TCAA na PURA.
Akizungumza wakati wa mafunzo hayo, Afisa TEAMA wa Baraza la Ushindani, Bw Athuman Kanyegezi, alisema mfumo huo unamwezesha mtumiaji kuanzisha akaunti, kuwasilisha rufaa kwa njia ya mtandao, kupakia nyaraka husika, kulipa ada na kufuatilia hatua za mwenendo wa kesi bila kulazimika kufika ofisini.
Aliongeza kuwa matumizi ya mfumo wa kidijitali yanalenga kurahisisha upatikanaji wa haki, kuongeza uwazi na kupunguza gharama na muda kwa wadau wanaohitaji huduma za Baraza hilo.
Semina hiyo iliwahusisha wafanyabiashara, wajasiriamali na wawakilishi wa taasisi mbalimbali, ambapo washiriki walipata fursa ya kuuliza maswali na kupata ufafanuzi kuhusu taratibu za rufaa na utoaji wa haki kwa njia ya kidijitali.











.jpg)











