HABARI

SIASA

ELIMU

Recent Posts

WAZIRI NDEJEMBI ASISITIZA UTEKELEZAJI WA VIPAUMBELE VYA SERIKALI KUFIKIA 2030

November 19, 2025 Add Comment

 

Waziri wa  Nishati Mhe. Deogratius Ndejembi  amewaagiza Watumishi wa Wizara hiyo kufanya kazi kwa bidii ili kutimiza Vipaumbele vya Serikali katika Sekta ya Nishati ikiwemo kufikia Megawati 8000 ifikapo 2030.

Mhe. Ndejembi ameyasema hayo tarehe 18 Novemba 2025 wakati akizungumza na watumishi wa Wizara mara baada ya kuwasili Katika Wizara  Mji  wa Serikali Mtumba Jijini Dodoma. 

Amesema watumishi wa Wizara ya Nishati ndio watendaji wakuu na wenye dhamana ya kuhakikisha kwamba malengo ya Serikali yaliyowekwa yanatimia kwa kufanya kazi kwa bidii , kuwataka watumishi kuchambua kwa kina  hotuba ya Mhe   Rais ili kuweza kufikia vipaumbele kwa wakati  na kuyoa huduma bora kwa wananchi wa Tanzania.

Pia amesisitiza watumishi kutumia siku mia moja za Mhe. Rais kama kipimo na  kielelezo cha kutathmini uelekeo wa malengo ya Serikali.

“Sisi kama viongozi wenu tunategemea zaidi ushirikano kutoka kwenu ninyi wataalamu wa hapa Wizara ya Nishati  ili tuweze kukamilisha Vipaumbele vya Mhe. Rais alivyoviweka katika sekta yetu  kwasababu tunatakiwa tuanze kwa kukimbia na sio kutembea“ amesema Mhe. Ndejembi.

Nae Naibu Waziri wa  Nishati Mhe. Salome Makamba amewataka watumishi kushirikiana kwa pamoja na viongozi wa Wizara hiyo ili kuendesha Sekta ya Nishati kwa pamoja, na kuongeza kuwa anatambua kwamba maswala mengi ya sekta ya Nishati yameshafanyika tayari mpaka sasa.

Amesema  Serikali imeshafikisha Megawat 4000 za kiwango cha kuzalisha Umeme, hivyo ni jukumu letu kukamilisha miradi iliyokuwa inaendelea na kuongeza vyanzo vingine vya uzalishaji umeme ili kufikia megawati 8,000 ifikapo 2030.

Kwa upande wake Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati Mha. Felchesmi Mramba amewashukuru viongozi hao na amewataka watumishi wa Wizara ya Nishati kutoa ushirikiano kwa viongozi hao sambamba na kutekeleza majukumu yao kwa wakati ili kuweza kutekeleza Vipaumbele vya Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan ifikapo mwaka 2030.











WAANDISHI WA HABARI WAJENGEWA UWEZO WA MASUALA YA FEDHA NA UCHUMI NA BOT

WAANDISHI WA HABARI WAJENGEWA UWEZO WA MASUALA YA FEDHA NA UCHUMI NA BOT

November 19, 2025 Add Comment


Meneja wa Idara ya Uendeshaji, Tawi la Benki Kuu Dodoma, Bw. Nolasco Maluli akizungumza wakati wa ufunguzi wa semina ya waandishi wa habari Jijini Dodoma.

Meneja wa Idara ya Uendeshaji, Tawi la Benki Kuu Dodoma, Bw. Nolasco Maluli akizungumza wakati wa ufunguzi wa semina ya waandishi wa habari Jijini Dodoma.

Meneja msaidizi uchumi wa Benki Kuu Tawi la Dodoma. Bw. Shamy Chamicha akiwasilishamada katika semina ya waandishi wa habari inayofanyika Jijini Dodoma.

Meneja Msaidizi wa Uhusiano wa Umma Benki Kuu ya Tanzania, Bi. Noves Moses akizungumza wakati wa ufunguzi wa semina ya waandishi wa habari inayofanyika Jijini Dodoma.

Na.Alex Sonna-DODOMA

Benki Kuu ya Tanzania (BOT) imeanza semina maalum kwa waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali nchini, yenye lengo la kuwajengea uwezo juu ya majukumu, mifumo na huduma za benki hiyo pamoja na masuala mapana ya uchumi na fedha.

Semina hiyo imefunguliwa leo Novemba 19,2025 jjijini Dodoma na Meneja wa Idara ya Uendeshaji, Tawi la Benki Kuu Dodoma, Bw. Nolasco Maluli, amesema  mpango huo ni muhimu katika kuongeza uelewa wa waandishi juu ya masuala ya fedha na uchumi, ili waweze kuandika habari sahihi na zenye weledi zinazowasaidia wananchi.
Bwana Maluli amesema kuwa semina hiyo inalenga kukuza uelewa wa waandishi kuhusu majukumu na huduma zinazotolewa na BOT. Aliongeza kuwa itawapatia waandishi ufahamu wa kina kuhusu masuala ya fedha, ikiwemo sera za fedha na mifumo ya malipo.
"BOT imekuwa ikipata mafanikio kupitia ushirikiano na vyombo vya habari, ikiwamo kuongezeka kwa weledi katika habari na makala za uchumi, upatikanaji wa ufafanuzi sahihi wa masuala ya kifedha kwa umma na kuimarika kwa mahusiano kati ya BOT na wanahabari."amesema Bw.Maluli
Akizungumzia matarajio ya benki hiyo, Bwana Maluli amesema  BOT inatarajia kuona waandishi wa habari wakiandika habari za uchumi na fedha kwa usahihi zaidi, pamoja na kutoa maoni yenye kuchochea maboresho katika mifumo ya fedha na malipo ili kuboresha huduma kwa wananchi.
Miongoni mwa mada zitakazojadiliwa katika semina hiyo ni Muundo na Majukumu ya BOT, Sera ya Fedha Inayotumia Riba, Elimu Kuhusu Hati Fungani, Elimu ya Fedha na Usajili wa Vikundi, Ulinzi na Huduma za Kifedha, Usimamizi wa Mifumo ya Malipo, pamoja na Alama za Usalama katika Noti za Tanzania.
Semina hiyo inaendelea jijini Dodoma na inatarajiwa kuongeza uwezo wa waandishi wa habari katika kuripoti masuala ya uchumi na fedha kwa namna itakayowasaidia wananchi kupata taarifa sahihi na zenye manufaa.

Wapeni watoto wenu mlo wa asubuhi kabla ya kwenda shule

November 19, 2025 Add Comment
Wazazi na walezi wameaswa kuhakikisha wanawapatia watoto wenye umri wa kwenda shule mlo wa asubuhi kabla hawajaenda shule. Rai hiyo imetolewa na Mkurugenzi wa Idara ya Elimu na Mafunzo kutoka Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania (TFNC), Dkt. Eshter Nkuba wakati akizungumza na wazazi na walezi wa shule ya msingi Unubini iliyopo manispaa ya Temeke.

MCHENGERWA AAHIDI KUONGEZA USHIRIKIANO NA TAMISEMI KWENYE AFYA, APEWA MAUA YAKE AKIAGWA LEO

November 18, 2025 Add Comment

Na Mwandishi wetu- Dodoma

Waziri Mteule wa Afya, Mhe. Mohamed Omary Mchengerwa amemhakikishia Waziri wa Ofisi ya Waziri Mkuu- TAMISEMI, Mhe. Prof. Riziki Shemdoe kushirikiana kikamilifu kwenye eneo la Afya ili kutimiza ndoto ya Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan ya kuwaletea tabasamu wananchi wa Tanzania kupitia kauli mbiu ya Serikali ya sasa ya Kazi na Utu Tunasonga Mbele.

MHE. LUKUVI AMSHUKURU RAIS SAMIA KWA KUZIDI KUMUAMINI

November 18, 2025 Add Comment

 



Na. Mwandishi Wetu-DODOMA

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu Mhe. Willium Lukuvi amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kumuamini na kumrudisha kwenye Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu.

 


Mhe. Lukuvi ametoa shukrani hizo leo tarehe 18 Novemba, 2025 Jijini Dodoma wakati wa zoezi la kuwapokea Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu na Naibu Waziri wa Ofisi hiyo katika Ofisi za Waziri Mkuu Ngome.

 


“Kwanza ninampongeza Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa ushindi wa kupata kura nyingi, lakini pia ninamshukuru kwa kuniamini na kunirudisha tena kuhudumu katika Ofisi ya Waziri Mkuu ikiwa ni mara ya nne kuhudumu ndani ya ofisi hii” ameeleza Mhe. Lukuvi.

 


Kwa upande wake Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo Dkt. Jim Yonazi amewapongeza kwa uteuzi huo na kusema kuwa ofisi yake ipo tayari kufanya kazi kwa bidii, uaminifu na juhudi ili kuweza kutimiza malengo ya Mhe. Rais.

 


“Nawapongeza kwa kuaminiwa na kuteuliwa tena na Mhe. Rais, tupo tayari kufanya kazi nanyi kwa bidii, uaminifu na juhudi zote ili kuweza kutimiza malengo ya serikali kwa ufanisi” amebainisha Dkt. Yonazi.

 



=MWISHO=

RAS MCHATTA AWAFUNDA WATUMISHI UWEKEZAJI KWENYE MFUKO WA UMOJA WA UTT-AMIS

November 18, 2025 Add Comment

Na Oscar Assenga, TANGA

KATIBU Tawala Mkoa (RAS ) wa Tanga , Rashid Mchatta, amewataka watumishi wa umma kuchangamkia fursa za Mfuko wa Umoja wa Uwekezaji ( UTT-AMIS) kutokana na kwamba kwa uwezo walionao wanaweza kuwekeza na kupata mafanikio makubwa baadae.

Mchatta aliyasema hayo leo wakati akizungumza katika kikao cha utoaji elimu kwa watumishi wa Mkoa huo, kuhusu umuhimu wa uwekezaji kwenye mifuko ya uwekezaji ya pamoja inayoendeshwa na UTT-Amis.

Alisema kwamba hiyo ni fursa nzuri na muhimu kutokana na kwamba mfuko huo una mtaji mzuri wa kutosha, ulioanza na Shilingi bilioni 1, lakini kwa sasa mtaji wao umekuwa na kufikia zaidi ya Shilingi Trilioni 3.6 hivyo wakiwekeza, wanakuwa na uhakika wa kunufaika.

“Nitumie fursa hii kuwahamasisha watumishi wenzangu kuchangamkia fursa za uwepo wa mfuko wa umoja wa Uwekezaji wa UTT-Amis, ukiwekeza unakuwa na uhakika wa kunufaika na uwekezaji tulioufanya,”alisema .

Awali, Afisa Masoko Mwandamizi kutoka Taasisi ya Uwekezaji ya UTT-Amis Oliver Minja, alisema wanakutana na watumishi wa umma wakifanya uhamasishaji kutoa elimu ya uwekezaji kwenye mfuko UTT Amis, ili waweze kuitumia kuweka akiba kwa maisha yao ya sasa na badae.

Oliver alisema kwamba ni muhimu kwa watumishi waanze kuweka akiba, pamoja na na uwekezaji kwa ajili ya kutengeneza kesho yao kutokana na kwamba wanaweza kunufaika na fursa mbalimbali.

Alisema kwamba uwekezaji wa UTT ni huru na unapelekea kurugenzi ya uwekezaji izunguke sokoni kila siku na lazima ichukuliwe iende sokoni kufanya uwekezaji na hawana namna ya kulala na fedha za watu.

Alisema urahisi wa kuwekeza UTT-Amis ni mkubwa kutokana na kwamba wanaweza kupitia mabenki yaliyopo kwenye maeneo mbalimbali nchini, na hivyo kutoa urahisi wa kuwekeza na kuyafikia masoko ambayo wasingeweza kuyafikia

“Watumishi wenzangu hii ni fursa nzuri itakayotuwezesha kukidhi mahitaji yetu ya sasa na baadae hivyo hakikisheni kwenye mishahara yenu mnatoa asilimia 10 wekezeni kwa kutengeneza kesho yenu ”Alisema

MADINI YAIBUKA KAMA NGUZO YA MAENDELEO MOROGORO

November 18, 2025 Add Comment


🔶 Sekta yaongezeka kwa kasi, yajenga miundombinu na kuinua wananchi


Morogoro


Mauzo ya madini ya dhahabu mkoani Morogoro yamefikia Shilingi bilioni 16.51 katika kipindi cha Julai 2023 hadi Septemba 2025, yakionesha kasi kubwa ya ukuaji wa sekta ya madini na mchango wake katika uchumi wa mkoa.


Mapato ya Serikali kupitia sekta hiyo pia yameendelea kupanda kutoka Shilingi bilioni 2.67 mwaka 2021/2022 hadi Shilingi bilioni 4.9 mwaka 2023/2024, huku Morogoro ikitarajia kukusanya Shilingi bilioni 6.5 katika mwaka wa fedha 2025/2026.

Ofisi ya Madini ya Mkoa wa Morogoro inasimamia shughuli za madini katika wilaya za Gairo, Kilosa, Mvomero na Morogoro.

Akizungumza katika mahojiano maalum, hivi karibuni Afisa Madini Mkazi wa Mkoa wa Morogoro, Zabibu Napacho, alisema kuwa mkoa huo umebarikiwa na aina nyingi za madini ikiwemo Feldspar, Rhodolite Amethyst, Green Garnet, Dhahabu, Kaolin, Shaba, Ruby, Spinel, Marble, Graphite, REE na Quartz.

Alifafanua kuwa jumla ya leseni za uchimbaji mdogo zilizotolewa ni 2,413, za uchimbaji wa kati 205, wakati leseni za uchimbaji mkubwa ni 10 na leseni za utafiti mkubwa zikiwa 61, hatua inayolenga kuimarisha shughuli za madini na kuvutia uwekezaji zaidi mkoani humo.

Kwa upande wa sekta binafsi, Meneja wa Mgodi wa Yusra A. Yusuph, Isack Mushi, alisema mgodi huo unazalisha Dolomitic Marble kwa ajili ya kutengeneza tiles, rangi na bidhaa nyingine, sambamba na kuchangia maendeleo ya jamii.

Alibainisha kuwa mgodi huo umejenga ofisi ya kijiji yenye thamani ya Shilingi milioni 28, umenunua kiwanja cha ofisi kwa Shilingi milioni 4, umeunganisha umeme, kuboresha barabara, kuchimba kisima pamoja na kutoa ajira 65.

Naye Mkurugenzi wa Mangiolin Gems Limited, Shamaina Bashir, alisema kuwa kampuni yake imejikita katika biashara ya vito na uongezaji thamani, huku ikitoa ajira kwa wanawake na vijana ili kuwawezesha kujitegemea na kurejea shule kupitia akaunti za malengo.


“Tangu kuanza Julai 2024, vijana 10 wamerudi shule na wengine 10 wapo katika maandalizi ya kujiendeleza mwakani,” alisema.

Bashir alisisitiza kuwa dhamira ya kampuni hiyo ni kuifanya sekta ya madini Morogoro kuwa chanzo thabiti cha mapato na kichocheo cha maendeleo ya kijamii na kiuchumi.



Uhamasishaji wa Tuzo za Serengeti kwa wadau washika kasi Kanda ya Kaskazini

November 18, 2025 Add Comment
Wajumbe wa Kamati Kuu ya Kitaifa ya Tuzo za Uhifadhi na Utalii 2025 wakiongozwa na Mkurugenzi Msaidizi Utalii Richie Wandwi wameendelea na zoezi la uhamasishaji na utoaji elimu kwa wadau wa utalii na uhifadhi juu ya tuzo za Serengeti zinazotarajiwa kufanyika mwezi Desemba 2025.

Zoezi hilo linalolenga kuwajengea uelewa wadau juu mambo muhimu ikiwemo, kategoria za tuzo na namna ya kujisajili na kuwa mshiriki wa tuzo hizo limefanyika Jumatatu Novemba 17 Jijini Arusha kwa Kanda ya Kaskazini.