Showing posts with label siasa. Show all posts
Showing posts with label siasa. Show all posts

KATIBU WA BAVICHA AKANA MADAI YA KUTUHUMIWA KUKIHUJUMU CHAMA

December 06, 2024 Add Comment





Na Oscar Assenga,TANGA.

KATIBU Mstaafu wa Baraza la Vijana wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo Chadema Mkoa wa Tanga (Bavicha) Hemed Said amekana madai ya viongozi wa chama hicho ngazi ya wilaya wanaomtuhumu kukihujumu chama wakati wa uchaguzi wa Serikali za mitaa uliofanyika November 27, 2024.

Tuhuma hizo dhidi yake zinadaiwa ni baada ya Said kushiriki katika kikao cha pamoja na viongozi wa kisiasa wilayani Tanga ambapo Kwa pamoja walipongeza mchakato wa uchaguzi wa viongozi wa Serikali za mitaa , vijiji na vitongoji pamoja na wajumbe ambapo yeye alishiriki kama mgombea licha ya kuwa alienguliwa baada ya kukosa sifa ya kukidhi vigezo.



Akizungumza katika mkutano huo Said alisema kuna sintofahamu kwa chama hicho kumtuhumu kwamba anahusika moja kwa moja katika kuhujumu mipango ya chama jamba ambalo alilipinga kutokuhusika kutokana na kwa sasa amekwisha kustaafu na hawezi kuingia kwenye chama kwa njia yeyote bila kufuata taratibu za kichama"



" Kufuatilia kadhia hii nimekupa nikipata wasiwasi kwa sababu ninapata vitisho kwa baadhi ya wenzangu wakiwemo viongozi na wanachama changu kwamba ninahusika wakati siwezi kuhusika kwa namna yeyote ya kukihujumu chama hivyo naomba nijivue na sihusiki kwa sababu nipo ndani ya chama kwa zaidi ya miaka 15 nafahamu taratibu miongozi na kanuni zinazohusu uendeshaji wa chama" Alisema Said.



Alisema wakati alipokwenda kwenye kikao cha pamoja na viongozi wa kisiasa alikwenda kama mmoja wa wagombea ambaye alienguliwa kwa hiyo maoni aliyoyatoa ni kama mgombea aliyeenguliwa kwenye uchaguzi wa Serikali za mitaa .



“Sasa hapo mimi ninahusikaje na tuhuma za kuuza au kurubuni mipango au kukwamisha shughuli zozote za mafanikio ya chama changu" alihoji Said.

Aidha amesema kuwa licha ya kupokea vitisho kutoka kwa viongozi na wanachama wa chama hicho lakini hakukuwa na utaratibu wowote wa kichama ambao uliofuatwa ikiwemo kumuita kwa nia ya barua.

Kiongozi huyo Mstaafu wa Bavicha Mkoa wa Tanga amesema alishiriki kikamilifu mchakato mzima wa uchaguzi kujisaidia chama chake kusaidia kuwapatia wagombea ambao watakwenda katika uchaguzi wa Serikali za mitaa , vitongoji na vijiji.

“Tofauti zozote zinazozungumzwa kwamba Mimi nimehusika kukirubuni chama hizo sio za kweli kwa sababu nimeshiriki ndani ya chama ngazi ya wilaya kutafuta wagombea na mimi nikiwa ni mgombea wa mtaa ambao ninaoishi sasa nahusikaje kukihujuma chama “Alihoji.

“Haiwezekani nasikia wengine wanasema nimenunuliwa sio kweli nina maisha yangu ninajiendesha kila mtu anafahamu kwa sababu nina uchumi wangu binafsi" alisisitiza mwanachama huyo.

Ameeleza kuwa Chadema wilaya ya Tanga kwenye uchaguzi wa viongozi wa Serikali za mitaa vijiji na vitongoji iliweza kusimamisha wagombea 50 lakini wapo 8 ambao walijitoa wakati mchakato huo ikiendelea licha ya kukidhi vigezo alihoji kuwa wamechukuliwa hatua gani tofauti na yeye ambaye aliyeenguliwa kikanuni.

"Ndani ya chama chetu katika halmashauri ya Jiji la Tanga ambayo tuna mitaa 181 tulikuwa na wagombea 50 lakini 8 katika hao tulikuwa na mawakala 182 , je kwanini hawa 8 na Mimi na Hawa ni nani amerubunika , kama walijitoa chama kimewachukulia hatua gani mpaka mimi nionekane kama ninahusika moja kwa moja? Alihoji.

Alieleza kuwa tangu alipojiunga na chama hicho akiwa shule ya Sekondari na baadye kupata nafasi ya uongozi wa Baraza la vijana Bavicha Mkoa wa Tanga na ni miongoni mwa vijana ambao walisimama imara kukitetea chama hicho hivyo kuhusishwa na tuhuma za kukihujumu chama chake inampa wakati mgumu.


“Chama kinafahamu kuwa katika vijana ambao walisimama na kupambana kwaajili ya kukisimamisha chama Mimi ni mmoja wapo kwa sababu Nina nafasi yangu kuanzia ngazi ya chuo nimehusika kwenye project nyingi mpaka kwenye ushindi wa ubunge ambao tulipata 2015." Alisema.

Kutokana na hali hiyo amesema kwamba atawaandikia barua viongozi wa chama hicho ngazi ya wilaya kisha kupeleka nakala ngazi ya Taifa ili kidai haki yake kama mwanachama halali wa chama hicho.

Alisisitiza kuwa kila mwananchi anauhuru wa kujiunga na chama chochote na kuwa mwanasiasa ambaye anaweza kusimamia maslahi ya wananchi pamoja na Maendeleo ya Taifa kwa ujumla.

"Kuchagua chama chochote cha siasa ni utashi wa mtu binafsi kwa sababu wakati ninajiunga na CHADEMA hakuna mtu ambaye alinilazimisha tupo katika harakati kwaajili ya kuwasaidia wananchi popote pale ambapo upo uweze kupaza   sauti ya wananchi isikike"Alisema 

RC AWAHAKIKISHIA USALAMA WAPIGA KURA

December 05, 2024 Add Comment



Na Paskal Mbunga,Tanga

WAPIGA kura katika uchaguzi wa serikali za mkoani Tanga wamehakikishiwa usalama wa kura zao na kwamba hawana haja ya kukaa vituoni mara baada ya kupiga kura.

Ahadi hiyo imetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Tanga Balozi,Dkt Batilda Burian mara baada ya kupiga kura yake katika kituo cha Raskazone Jijini Tanga ambapo aliwahakikishia wakazi wa mkoa huo usalama wakati wote wa zoezi.

Alisema kwamba kwamba hakuna haja ya kukaa vituoni baada ya kur a, isipokuwa kila mwananchi atakayepiga kura baada ya kumaliza aondoke na kurudi nyumbani wakisubiri matokeo yatakayotangazwa rasmi na wasimamizi wa uchaguzi.

Mkuu huyo wa mkoa alikuwa anajibu swali la mwandishi mmoja aliyetaka kujua kwamba baada ya kupiga kura je kuna uhakika gani wa usalama wa kura hizo ambapo alisema kwamba wananchi wasiwe na wasiwasi wawe na imani na vyombo vilivyowekwa kwa ajili ya usimamizi wa zoezi hilo.

Alisema kwamba mkoa wa Tanga una vituo vya kupigia kura 5460 na kwamba vituo vyote vimewekewa ulinzi na usalama ili watu wapige kura kwa uhuru bila kubuguziwa.

Katika siku hii muhimu kitaifa, viongozi mbalimbali wa kimkoa na taifa walikwenda katika maeneo waliyojiandikisha. Mwenyekiti wa CCM (M), Rajabu Abrahaman alikwenda kupiga kura yake wilayani Pangani,

CCM :TUTASHUGHULIKA NA MATATIZO YA WATU

December 04, 2024 Add Comment

 



Na Mwandishi Maalum , Zanzibar 


Chama cha Mapinduzi (CCM) kimesema hakitaacha kushughulika na changamoto  zinazowakabilii wananchi kwakuwa  hiyo ni moja ya shabaha  ya kuanzishwa CCM  mwaka 1977.


Kimesisitiza kazi ya kupigania haki  za wananchi, uhuru,kuenzi thamani ya utu na heshima ya kila binadamu, majukumu hayo yalianza kutekelezwa na vyama vya TANU na ASP. 


Matamshi hayo yametamkwa na Katibu wa Kamati Maalum ya Nec Zanzibar, Idara ya itikadi, Uenezi na Mafunzo ,Khamis Mbeto  Khamis, wakati  akijibu swali la sababu ipi inayowafanya watanzania kuendelea kuichagua CCM .


Mbeto  akijibu swali hilo, alisema watanzania wataendelea kuiamini CCM  kutokana na kusimamia  malengo  ya kuanzishwa kwake,  sera na siasa yake pia  ni chama kinachoshughilika na matatizo ya wananchi



Alisema CCM haitaacha wala kupuuzia kutafuta majibu  yoyote ya matatizo   yanayowakabili wananchi katika kila Mtaa, Kkijiji, Kitongoji, Wadi/Kata,Wilaya  hadi Mkoa .


"Chama kinachopigania maslahi  ya umma hakiwezi kunyimwa kura au  kutoaminiwa. Kitaendelea kushinda kwakuwa watanzania  wanaiamini na kuitegemea CCM kwa  kutumikia  kwake wananchi "Alisema mbeto 


Aidha alisema chama kinachohangaikia  shida na  matatizo ya watu , kinachotafuta majibu ya  matatizo  na kuwafikia wananchi  ,kuwasikiliza na kutoa ufumbuzi, lazima kiaminiwe na kushinda .


'Nadhani upinzani  ubadilishe  mtindo  wa siasa zake ili ukubalike katika jamii. Kubeza au kupondoka  kila jema la CCM  si mtaji utakaoufanya upinzami uungwe mkono. Kwa mtindo huo itawachukua miaka mia moja  ijayo hadi uaminike" Alieleza 


Pia alivishauri vyama hivyo  kuungana na kuunda chama kimoja kitakachokuwa na nguvu  za ushindani kwa CCM, kwani kadri unavyooendelea kubaki na utitiri wa vyama, hautakishanda chama tawala.


"kazi ya kushughulika na mataizo ya wananchi  hicho ni kiapo kwetu. Ni jukumu la kufa na kupona .Kinachotuumiza kichwa  CCM usiku na mchana ni kupata maendeleo ya nchi na watu"Alieleza Mbeto

VYAMA VYA SIASA WILAYA YA TANGA VYAPONGEZA MCHAKATO WA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA.

November 30, 2024 Add Comment

Na Oscar Assenga,TANGA

Vyama vya Siasa vilivyoshiriki Uchaguzi wa Serikali za mitaa wa Novemba 27 mwaka huu katika Halmashauri ya Jiji la Tanga, vimetoa tamko la pamoja na kupongeza mchakato wa Uchaguzi huo huku vikitaka dosari chache zinazotakiwa zifanyiwe kazi na Tamisemi.

Vyama hivyo ni pamoja na Chama cha Mapinduzi (CCM),Chama Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) ,vyama vyengine ni (ACT-Wazalendo) CUF, ADC,TLP na NCCR-Mageuzi.


Vyama hivyo vimetoa tamko la pamoja leo Novemba 29 mara baada ya matokeo ya jumla kutangazwa hapo Novemba 28 mwaka huu ambapo CCM katika Jiji la Tanga kimeibuka kidedea kwa kushinda viti vyote vya kuanzia wajumbe na wenyeviti wa mitaa yote.

Wakizungumza na Waandishi wa Habari wakati wa tamko la pamoja,Mussa Mbarouk ambaye ni Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF) wilaya ya Tanga alisema kwamba uchaguzi ulifanyika kwa njia ya amani japo kulikuwa na dosari ndogondogo ambazo wanaamini zitafanyiwe kazi,

"Mchakato wa Uchaguzi huu ulienda vizuri, tulikuwa tukishirikiana na Serikali ya Mkoa na Jiji, kulikuwa na dosari ndogondogo lakini hata sisi vyama vya siasa tunatakiwa tukae na tuungane ili yale maeneo yote yenye Wagombea wanaokubalika tumuunge mkono" Alisema Mbarouk


Mbarouk alisema kwamba chama chake pamoja na vyama vyote shiriki katika Uchaguzi huo vimesikitishwa na matokeo ya jumla ambapo hakuna chama cha upinzani kilichoshinda kiti hata kimoja.

" Uchaguzi wa Serikali za mitaa wa mwaka 2019 tulipata walau viti 61,lakini safari hii haijawahi kutokea kiukweli ni lazima tujipange vizuri Uchaguzi Mkuu Ujao mwaka 2025" Alisisitiza Mbarouk

Naye kwa upande wake Mwenyekiti wa Ngome ya Vijana Chadema Hemed Bakari alisema kuna umuhimu mkubwa kwa vyama vya siasa kuongeza nguvu ya ushawishi kwa wapiga kura,

Kwa upande wake Katibu wa chama cha Mapinduzi (CCM) wilaya ya Tang Shaban Kalaghe alisema mchakato wa Uchaguzi huo ulienda vizuri na kuwashukuru watu wote waliojiandikisha na kupiga kura,

“Kwa kweli niwapongeze wasimamizi wa uchaguzi huu ulienda vizuri tulikuwa na wagombea kwenye mitaa yote na tumeshinda kwa asilimia 100 lakini pia tunawashukuru wenzetu wa vyama vingine kwakukubali matokeo ni jambo zuri na linaonyesha ukomavu mkubwa wa kisiasa”Alisema

Hata hivyo alisema kwamba uchaguzi huu umeisha na sasa wanakwenda kufanya kazi lakini pia kujiandaa na Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025


CCM YATAJA SIRI USHINDI SERIKALI ZA MITAA, YAWAPELEKA UJUMBE UPINZANI

November 29, 2024 Add Comment

 Na Said Mwishehe


CHAMA Cha Mapinduzi(CCM) kimetoa sababu nne ambazo zimefanya Watanzania kuendelea kukiamini na kuchagua wagombea wa Chama hicho katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa na miongoni mwasababu ambazo zimefanya washindi ni uwepo wa migogoro katika vyama vya ipi upinzani.

Akizungumza na Waandishi wa habari leo Jijini Dar es Salaam Katibu wa Halmashauri Kuu(NEC) ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Itikadi,Uenezi na Mafunzo CPA Amoss Makalla amesema wamekuwa katika kampeni kwa siku saba kuanzia Novemba 20 mpaka Novemba 26 na Novemba 27 uchaguzi umefanyika na kupiga kura.

“Ahadi yetu wakati wa kampeni ni kwamba CCM imeongozwa na 4R za Rais Samia Samia Suluhu Hassan za uvumilivu, ustahimili, kuheshimiana lakini pia kuhakikisha tunaendelea kujenga nchi yetu.CCM imeonesha kuheshimu kwa kufanya kampeni za kistaarab, kuheshimu ratiba wakati wa kampeni,”amesema.

Akitaja sababu za Chama hicho kushinda katika uchaguzi huo wa Serikali wa Serikali za mitaa ni kwamba wanaamini wamepewa imani hiyo ambayo wamepewa CCM imetokana na sababu mbalimbali na sababu ya kwanza wananchi wameridhika na utekelezaji mzuri wa Ilani ,miradi ya maendeleo, utatuzi wa kero mbalimbali.

“Hii imejenga imani kwa Watanzania kukiamini Chama Cha Mapinduzi lakini kikubwa miradi mbalimbali inayotekelezwa iko katika mitaa,Vitongoji,vijiji, kwa hiyo tunaamini mafanikio yaliyopatikana yalijenga imani kwa wananachi.”

CPA Makalla amesema sababu ya pili ni maandalizi ya Chama cha Mapinduzi kwa kuwa walijua kutakuwa na Uchaguzi wa Serikali za mitaa , hivyo walifanya na maandalizi ya kutosha kwa kuanza kwa kufanya tathimini ya viongozi waliopo katika mitaa , vijiji na vitongoji.

“Kwahiyo kila eneo kila wilaya tuliwafanyia tathimini viongozi walioko madarakani lakini na kutambua changamoto na maoni ya wananchi.CCM haikukosea kuteua wagombea safi ambao wabakubalika na hiyo imekuwa siri ya ushindi lakini nyie ni mashuhuda kuanzia ngazi ya kitaifa mpaka ngazi ya Mashina uchaguzi huu tuliuchukulia kwa uzito mkubwa , hivyo maandalizi ya kuandaa wananchi yalikuwa makubwa na tunaamini tulikuwa na maandalizi mazuri.”

CPA Makalla amesema hatarajii mtu akaja akahoji CCM imeshindaje kwani Watanzania ni mashuhuda vyama vingine havikuwa na maandalizi,vyama vingine havijaonekana kwa wananchi miezi Saba ,wengine wamewekeza katika maandamano .

“Unafanya maandalizi kwa siku tatu unatarajia unaweza kushinda? CCM imefanya maandalizi ya kutosha kupitia viongozi wake.Changamoto ambayo wapinzani wameipata ni kutokana na kutakuwa na maandalizi ya uchaguzi.Tusitafute sababu yoyote.Sababu hakukuwa na maandalizi.”

Pia amesema sababu ya Tatu CCM imefanya kampeni zake kisayansi kuanzia uzinduzi ,kufunga kampeni pamoja uratibu na ushirikishwaji kwa viongozi wa Chama kuanzia ngazi ya Taifa mpaka ngazi ya shina.

Sababu ya nne iliyowafanya CCM kushinda,CPA Makalla amesema imechangiwa vizuri na migogoro ya vyama vya siasa na kuelez adui yako muombee njaa.Kwahiyo katika vyama vya siasa migogoro imefanya CCM kushinda ingawa kuna sababu nyingine nyingi.

Ametumia nafasi hiyo kuvitaka vyama vya upinzani kuendelea kuvumiliana na kujiepusha na migogoro kwani Chama chenye Mgogoro ni ngumu kushinda katika uchaguzi akitolea mfano CHADEMA ambayo kwa sasa kuna Mgogoro mkubwa na wameshuhudia Arusha wanachama wakivurugana na kupigana wakati wakielekea uchaguzi wa Serikali za mitaa.

“Najua vyama vya upinzani leo vinaongea lakini watakachoweza ni kutoa propaganda tu kwa kuituhumu TAMISEMI na CCM lakini ukweli wameshindwa uchaguzi kwasababu ya kutakuwa na maandalizi na migogoro kwa viongozi wao.Mengine yote watakayosema hayana ukweli.”