Na Mwandishi Wetu,TANGA.
KADA wa Chama cha Mapinduzi CCM Mkoa wa Tanga Macrina Clemens amechukua fomu ya kuomba ridhaa ya kuteuliwa kugombea Ubunge wa viti Maalumu Mkoa huku akihaidi kushirikiana na wananchi katika kuleta maendeleo.

Akizungumza mara baada ya kuchukua fomu alisema ameamua kuchukua fomu ili kuweza kutoa mchango wake kwa wananchi hususani Jumuiya wa Wanawake wa Chama cha Mapinduzi (UWT) Mkoa wa Tanga.
Zoezi la kuchukua fomu limeanza katika ofisi za Chama cha Mapinduzi linaendelea nchi nzima ambapo watia nia tofauti wameendelea kujitokeza kwa ajili ya kuchukua fomu za Ubunge na Udiwani.
EmoticonEmoticon