Showing posts with label siasa. Show all posts
Showing posts with label siasa. Show all posts

DK NCHIMBI ALAKIWA KWA SHANGWE NA MKUTANO MKUBWA UBARUKU, MBARALI

April 19, 2024 Add Comment

 Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi amepokelewa kwa shangwe na nderemo na wananchi wa Mbarali, wakiongozwa na vijana waendesha bodaboda, baada ya kuwasili na msafara wake katika Kata ya Ubaruku, Wilaya ya Mbarali, mkoani Mbeya, leo Aprili 18, 2024, akitokea Mbeya Mjini.


Dk Nchimbi alisimama kuwasalimia wananchi hao wa Ubaruku, akiwa njiani kuelekea Mkoani Njombe ikiwa ni mwendelezo wa ziara yake ya mikoa 6 ya Nyanda za Juu Kusini, ambapo ameambatana na Katibu wa NEC - Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa CCM Taifa Ndg. Amos Makalla pamoja na Katibu wa NEC - Oganaizesheni Ndg. Issa Haji Gavu.







CCM TANGA YADHAMIRIA KUSHINDA VITI VYOTE VYA UDIWANI

CCM TANGA YADHAMIRIA KUSHINDA VITI VYOTE VYA UDIWANI

March 13, 2024 Add Comment

Ndugu Selemani Sankwa – Katibu wa CCM Mkoa wa Tanga.

………………… 

Na: Mwandishi wetu, Tanga.

Chama Cha Mapinduzi (CCM) mkoa wa Tanga kimedhamiria kushinda viti vyote vinne vya udiwani kwenye uchaguzi mdogo utakaofanyika Machi 20 mwaka huu. Kauli hiyo imetolewa na Katibu wa CCM Mkoa wa Tanga Ndugu Selemani Sankwa alipokuwa akitoa mwelekeo wa kampeni kwenye kata nne ndani ya mkoa wa Tanga ambapo uchaguzi utafanyika.

“CCM Mkoa wa Tanga tuna uhakika wa kushinda kata zote nne ambazo ni Mkuzi wilayani Muheza, Boma, Mtimbwani na Mayomboni zilizopo Wilaya ya Mkinga. Ninaposema tuna uhakika wa ushindi si kwamba nabahatisha au najifariji bali ushindi wetu unatokana na utekelezaji wa Ilani ya CCM uliofanywa na serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Dkt. Samia Suluhu Hassan. Katika kata hizo tumeshuhudia ujenzi wa miradi ya Elimu, Afya, Umeme, Maji, Barabara na mingineyo.” amesema Sankwa

Mtendaji huyo Mkuu wa Chama Mkoa wa Tanga aliendelea kusisitiza kuwa “Tunajivunia kazi kubwa iliyofanywa na Viongozi wa Chama Wilaya na Mkoa chini ya Ndugu Rajabu Abdallah (MNEC) ambaye ni Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Tanga ya kuisimamia Serikali katika Miradi ya Maendeleo ambayo ni chachu ya kuchaguliwa kwetu.”

Vilevile, Sankwa amesema CCM inaamini katika kuwatumika wananchi kikamilifu kama siri ya ushindi wake, na ndiyo maana viongozi wa chama na serikali wamejitahidi sana kusikiliza na kutatua kero za wananchi.

Hatua hatua nyingine, Sankwa amesema Chama kimefanikiwa kuendesha vyema uchaguzi wa kura za maoni ambapo wagombea wamepatikana huku umoja na mshikamano wa Wanachama ukibaki imara bila makundi ya aina yeyote. “Niwasihi Wananchi kujitokeza kwa wingi siku ya Uchaguzi ili kutumia haki yao ya kuchagua Viongozi bora wanaotokana na CCM.” amesema Sankwa.

Februari 15, Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) ilitangaza uchaguzi mdogo wa Udiwani katika kata 23 za Tanzania Bara ambapo Uchaguzi utafanyika Machi 20. Kata nne ndani ya Mkoa wa Tanga zitafanya Uchaguzi mdogo huku CCM ikijinadi kushinda kata zote kwa ushindi wa kishindo.

CCM YAUPONGEZA UBALOZI WA UINGEREZA KUHAMIA DODOMA

February 21, 2024 Add Comment

 Chama Cha Mapinduzi kimeumepongeza Ubalozi wa Uingereza nchini kwa kuitikia wito wa Serikali ya Awamu ya Sita wa kuzitaka ofisi za ubalozi mbalimbali zilizopo Tanzania kuhamia Dodoma.


Pongezi hizo, zimetolewa leo, tarehe 21/2/2024, jijini Dodoma na Katibu wa NEC wa Idara ya Mambo ya Siasa na Uhusiano wa Kimataifa, Ndg. Rabia Abdalla Hamid, wakati akizungumza na ujumbe wa Maafisa wa Ubalozi wa Uingereza, katika Ofisi za Makao Makuu ya CCM, Dodoma.

Ujumbe wa Maafisa wa Ubalozi wa Uingereza, ukiongozwa na Mkuu wa Ofisi ya Dodoma, Bi. Godfrida Magubo, mapema leo, umetembelea Ofisi za Makao Makuu ya CCM, Dodoma kwa ajili ya kujitambulisha na kuitambulisha Ofisi ya Ubalozi huo, iliyopo Dodoma, ambayo ilifunguliwa Januari 2024.

‘’Chama Cha Mapinduzi kinawashukuru na kuwapongeza sana kwa kuunga mkono juhudi za kuhamia Makao Makuu ya Nchi hapa Dodoma,’’ Rabia alisema akiwapongeza.

Aidha, ameutaka Ubalozi wa Uingereza wawe mabalozi wa kuhamasisha ofisi zingine za ubalozi mbalimbali nchini kuhamia Dodoma.

Ndg. Rabia ameongeza kusema, ‘’ Chama na Serikali tumehamia Dodoma moja kwa moja, na hatukusudii kurudi nyuma, hivyo natoa wito kwa ofisi zingine za ubalozi wa nchi mbalimbali kuhamia Dodoma kama ninyi mlivyofanya’’.

Katibu wa NEC Mambo ya Siasa na Uhusiano wa Kimataifa na ujumbe wa Maafisa wa Ubalozi wa Uingereza wamezungumza na kujadiliana mambo mbalimbali ya kuimarisha uhusiano kati ya Tanzania na Uingereza.





CCM WAMPA KONGOLE RAIS SAMIA KWA KUIMARISHA DEMOKRASIA

February 21, 2024 Add Comment

 NA MWANDISHI WETU,ZANZIBAR.

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar kimempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu Hassan,kwa juhudi zake za kuimarisha diplomasia inayoongeza fursa za kiuchumi zinazoleta tija na mafanikio kwa pande zote za Muungano.

Kauli hiyo imetolewa na Katibu wa Kamati Maalum ya NEC,Idara Idara ya Itikadi,Uenezi na Mafunzo CCM Zanzibar Khamis Mbeto Khamis,wakati akitoa tathimini na uchambuzi wa fursa na mafanikio ya Tanzania Kimataifa kupitia mahojiano yaliyofanyika katika Kituo cha Radio ya Bahari FM,kilichopo Migombani Zanzibar.

Mbeto,alifafanua kuwa Rais Dkt.Samia,ameendelea kuipaisha Tanzania kiuchumi ili ifike katika kilele cha maendeleo endelevu sambamba na kupata hadhi ya nchi iliyoendelea kiuchumi Barani Afrika.

Alisema Chama Cha Mapinduzi kwa upande wa Zanzibar kinapongeza kwa dhati juhudi,maarifa,ubunifu na uchapakazi wa Rais wa Dkt.Samia na kwamba utendaji huo uliotuka ndio kibali cha Wananchi kumpa ridhaa ya kushinda kwa kishindo Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025.

Katika maelezo yake Katibu huyo wa NEC,aliwasihi Wananchi bila kujali tofauti za kisiasa,kidini na kikabila kumuunga mkono kwa kila hatua anayopiga katika kutafuta fursa mbalimbali kupitia ziara,makongamano na mikutano ya kimataifa.

Katibu huyo mwenezi alisema kupitia ziara zake amekuwa akitangaza fursa za Utalii kupitia dhana za Royal Tour na Uchumi wa Buluu zinazofafanua kwa kina rasilimali zilizopo nchini zikiwemo mbuga za wanyama,Bahari,mito,maziwa,vivutio vya mambo ya kale ili raia wa kigeni waje kwa wingi nchini kwa ajili ya Uwekezaji na utalii.

" Najua wapo baadhi ya watu wachache wanakosoa na kubeza juhudi hizi za Rais Dkt.Samia,wakidai anafanya ziara nyingi nchi za nje lakini tukumbuke kuwa ziara hizo sio za kifamilia bali anaenda kutafuta fursa za kiuchumi na kuimarisha mahusiano mema ya kidiplomasia yakiambatana kuingia na mikataba mikubwa yenye tija kwa nchi.

Alisema bajeti Kuu ya Tanzania kwa mara ya kwanza imefikia kiasi cha zaidi ya Trioni 41 ambapo asilimia 35 imeelekezwa katika miradi ya maendeleo inayowanufaisha Wananchi.

Mbeto,akizungumzia ziara za Rais Dkt.Samia,Makao Makuu ya dhehebu la dini ya Kikiristo Vatican,amesema imejenga mahusiano makubwa na kudhihirisha kuwa kiongozi huyo hana ubaguzi anajali imani za dini za wananchi wote.

Alieleza kuwa pamoja na hayo ziara hiyo ya kukutana na Papa Francisko wamekubaliana kuongeza miundombinu ya kijamii na kiuchumi ikiwemo ujenzi wa skuli,vyuo vikuu,hoteli kubwa za kitalii na viwanda vitakavyowanufaisha wananchi wote.

Pia ziara nyingine ya nchini Norway imeendelea kufungua fursa mpya za kiuchumi zikiwemo Uwekezaji katika Sekta za uvuvi pamoja na kuingia mikataba ya kushirikiana katika teknolojia ya masuala ya Gesi na Mafuta nchini.

Mafanikio hayo yanatokana na utekelezaji wa makubaliano na Wananchi kupitia Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2020/2025 ibara ya 132 (a)-(e) imeelekeza katika kipindi Cha miaka mitano ijayo,CCM itahakikisha kuwa mahusiano ya nchi kikanda na kimataifa yanaendelea kuimarishwa lengo Kuu ni kuhakikisha Tanzania inaendelea kuwa mstari wa mbele katika kuimarisha Amani,uhuru na maslahi ya Taifa katika nyanja za kimataifa.
Katibu wa Kamati Maalum ya NEC,Idara ya Itikadi,Uenezi na Mafunzo CCM Zanzibar Khamis Mbeto Khamis.
MAKONDA AWASILIANA  WAZIRI BASHUNGWA AKIMTAKA KUONGEZA NGUVU UJENZI WA BARABARA YA KAKONKO

MAKONDA AWASILIANA WAZIRI BASHUNGWA AKIMTAKA KUONGEZA NGUVU UJENZI WA BARABARA YA KAKONKO

February 02, 2024 Add Comment



Katibu wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi Taifa, Itikadi, Uenezi na Mafunzo Ndugu. Paul Makonda amempigia simu Waziri wa Ujenzi Ndugu. Innocent Bashungwa na kumtaka kuongeza nguvu katika kukamilisha ujenzi wa Barabara ya Kakonko kuelekea Halmashauri ya Kakonko yenye urefu wa Kilomita 3 kwa kiwango cha lami ambapo Waziri Bashungwa ameahidi kutekeleza ili wananchi kuondokana na changamoto hiyo ya mawasiliano.

Akiwa Wilayani Kakonko, Mwenezi Makonda amepokea changamoto hiyo ambapo aliwataka TANROADS na TARURA kutekeleza ujenzi wa miundombinu ya barabara kwa kuzingatia muda ilikusudi Watanzania kunufaika na urahisi wa mawasiliano ya barabara kutoka sehemu moja kwenda sehemu nyingine kwa haraka.

Pia, Amewasihi watendaji kuongeza nguvu ya ushawishi ili kupata fedha za kutekeleza miradi kwa haraka.

“Ahadi za Rais ni ahadi ya upendeleo na sio maana kwamba mipango iliyopo inaachwa..Hapana, ndio maana tunatekeleza Bajeti kwa kutekeleza Ilani ya CCM na maelekezo ya Viongozi wakuu” Alisema Mwenezi Makonda.
“Kwenye Maendeleo kazi kubwa tuliyonayo ni uwezo wa ushawishi, Keki inaweza kuwa ndogo lakini ni nyinyi namna gani ya kuipambania, Wataalam ongezeni namna ya ushawishi kutekeleza na kukamilisha miradi ya maendeleo Nchini” Amesema Makonda.