ALIYEKUWA MENEJA WA KANDA YA MASHARIKI TMDA DAR ES SALAAM AMWANGUSHA MWIJAGE KURA ZA MAONI MULEBA KASKAZINI

August 05, 2025




Na Mariam Kaagenda _Kagera 

Adonis Bitegeko aliyekuwa Meneja  wa  TMDA  Kanda ya Mashariki ameshinda Uchaguzi wa Kura za maoni Jimbo la Muleba Kasikazini katika Uchaguzi wa ndani wa chama cha Mapinduzi (CCM) kwa nafasi ya Ubunge  kwa kupata Kura 4392 na kumshinda aliyekuwa Mbunge wa Jimbo hilo  Charles Mwijage ambaye amepata Kura 2320 


Wakati akitangaza matokeo ya Uchaguzi huo mkurugenzi wa Uchaguzi wilaya ya Muleba Agnes Kasera amesema kuwa Kura zilizotarajiwa kupigwa ni 8637,Kura zilizopigwa ni 7252,zilizoharibika ni 92 na Kura halali ni 7160 


Ambapo Adonis Bitegeko ameibuka kidedea kwa kupata Kura 4392 ambapo wengine waliogombea katika Uchaguzi huo Jimbo la Muleba Kasikazini ni Fortunatus Muhalila aliyepata Kura 248 ,Edward Mujungi Kura 157,Danstan Mutagaywa Kura 53 

Adonis amewashukuru Wajumbe kwa kumuamini na kumpatia Kura nyingi ambapo amesema kuwa Chama chake cha Mapinduzi kikimteua hatowaangusha Wajumbe waliomchagua   kwani atawalipa uwajibikaji katika swala la Maendeleo ya Jimbo la Muleba Kasikazini .

Share this

Related Posts

Latest
Previous
Next Post »