Showing posts with label magazeti. Show all posts
Showing posts with label magazeti. Show all posts

TANESCO YAANZA KAMPENI YA KUTOA ELIMU YA USALAMA KWENYE MATUMIZI YA UMEME MIKOA YA KANDA YA ZIWA

March 29, 2025 Add Comment


📌Kampeni inalenga kuelimisha watoto kuzingatia usalama kwanza watumiapo umeme. 


📌Itasaidia Kupunguza athari na ajali zitokanazo na majanga ya umeme kwenye Mikoa hiyo.

Shirika la Umeme Tanzania  (TANESCO) Machi 27 limeanza kampeni maalumu ya kuelimisha juu ya kuzingatia usalama kwanza kwenye matumizi ya Umeme kwa Makundi ya watoto katika shule mbalimbali za msingi zilizopo kwenye mikoa ya Mara, Kagera, Mwanza, Geita na Simiyu.

Kampeni hiyo inayoitwa " Zingatia Usalama Kwanza Utumiapo Umeme" inalenga kuwafikia wanafunzi wa shule za msingi na kuwapa elimu inayowawezesha kugundua vihatarishi vinavyoweza kusababisha ajali zinazotokana na majanga ya umeme na kuepuka  athari zitokanazo na majanga hayo.

Akizungumza katika moja ya Shule zilizotembelewa Kaimu Meneja Masoko kutoka TANESCO Bwana Sylvester Matiku amesema elimu hiyo ni muhimu kuwalinda watoto na majanga ya umeme kutokana na kuwa kati ya makundi yanayopata athari zaidi na ajali za umeme.

''Shirika limeona lianze kampeni hii hasa kwenye mikoa ya Kanda ya Ziwa kutokana na hivi karibuni kuwa na matukio ya ajali zitokanazo na umeme zinazoathiri zaidi watoto na hivyo tukaona tuje kuwaelimisha ili kusaidia kupunguza na kuondoa madhara ya ajali zitokanazo na umeme''.

Wanafunzi hao wamepatiwa elimu kuhusu Matumizi Sahihi ya Umeme ili kuokoa gharama pamoja na kuitambulisha namba mpya ya ya huduma kwa wateja bila malipo ya Mchongo 180.

Katika kampeni hiyo Wanafunzi katika  shule mbalimbali wamepata fursa ya kuhoji maswali kuhusu umeme na athari za umeme na jinsi ya kumsaidia muathirika wa ajali za umeme.

Wanafunzi hao wameahidi kufikisha elimu waliyoipata kuhusu Umeme na Usalama katika Kampeni ya hiyo kwa familia zao, ndugu, jamaa na marafiki na wameomba elimu hiyo pia ifikishwe kwa Wanafunzi Wenye Mahitaji Maalum.

Kampeni hii muhimu inaendelea kwenye mikoa yote Kwenye Kanda ya Ziwa.



Barrick yatunukiwa Tuzo ya mdhamini mkuu wa Mkutano wa Kimataifa wa Madini Tanzania 2024

November 19, 2024 Add Comment

 

Waziri Mkuu Mh.Kassim Majaliwa akikabidhi cheti cha tuzo ya udhamini mkuu wa mkutano wa kimataifa wa sekta ya madini kwa Meneja wa Barrick nchini, Melkiory Ngido.
Baadhi ya wafanyakazi wa Barrick wakifurahia tuzo ya udhamini wa mkutano wa kimataifa wa sekta ya madini unaoendelea nchini.
Mmoja wa washiriki wa mkutano wa sekta ya madini nchini akipata maelezo ya shughuli za Barrick kwenye banda la maonesho la kampuni hiyo lililopo katika ukumbi wa kimataifa wa Mwalimu Nyerere, Dar es Salaam.

Na Mwandishi Wetu.

Kampuni ya Dhahabu ya Barrick inayoendesha shughuli zake nchini kwa ubia na Serikali ya Tanzania kupitia kampuni ya Twiga Minerals, imetunikiwa tuzo ya udhamini mkuu wa mkutano wa uwekezaji katika sekta ya Madini Tanzania unaoendelea katika ukumbi wa mikutano wa Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam.

Tuzo hizo kwa makampuni yaliyodhamini mkutano huu mkubwa wa kimataifa wa sekta ya madini zimekabidhiwa na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, ambaye alikuwa mgeni rasmi akimwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano, Dkt.Samia Suluhu Hassan, baada ya ufunguzi wa mkutano huo

Mkutano huo mkubwa wa kimataifa unawakutanisha wadau wa madini wanaojishughulisha na utafutaji, uchimbaji, uchenjuaji, uongezaji thamani madini, wasimamizi wa Sekta kutoka Serikalini, watoa huduma migodini na wafanyabiashara na kauli mbiu yake mwaka huu ni “Uongezaji wa Thamani ya Madini kwa Maendeleo ya Kiuchumi”.

Akiongea katika mkutano huo kabla ya kukabidhiwa tuzo hizo, Meneja wa Barrick nchini, Melkiory Ngido, amewaeleza wajumbe wa mkutano huo jinsi ubia wa Barrick na Twiga unavyoendelea kupata mafanikio makubwa na kuwa mfano wa kimataifa unaodhihirisha kuwa Serikali inaweza kushirikiana na sekta binafsi na kuleta mapinduzi makubwa ya kiuchumi.

Ngido, ameeleza kuwa katika kipindi kifupi kupitia ubia huu, umeweza kuchangia pato la taifa kwa kiasi kikubwa kupitia kodi na tozo mbalimbali za Serikali, kuongeza ajira kwa watanzania, kufanikisha miradi mikubwa ya kijamii hususani katika sekta ya barabara, afya, maji, na elimu pia umefanikisha kuinua uchumi wa wazabuni wa kitanzania wanaouza bidhaa mbalimbali kwenye migodi yake ya North Mara, Bulyanhulu na Buzwagi