DKT JAKAYA KIKWETE AMPONGEZA MHITIMU UDSM KWA KUVUNJA REKODI YA MIAKA 32 KWA KUPATA DARAJA LA KWANZA LAW SCHOOL

November 20, 2025

Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam Rais Mstaafu Wa Awamu ya Nne Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akimpongeza Mhitimu wa Shahada ya Awali ya Sheria ambaye alivunja rekodi iliyodumu miaka 32 kwa  kupata Daraja la Kwanza katika Taasisi ya Mafunzo ya Uanasheria kwa Vitendo Tanzania (The Law School of Tanzania), rekodi iliyokuwa inashikiliwa na Profesa wa sheria UDSM  Prof. Hamudi Majamba.

Bi Mary Barney Laseko anakuwa mwanamke wa pili kupata daraja la kwanza kutoka Law School of Tanzania, wa kwanza akiwa Katibu Mkuu wa `CCM Dkt. Asha-Rose Migiro. 


Hii imetokea leo wakati wa Mahafali ya 55 (Duru la Tatu) ya Chuo Kikuu cha Dar es salaam yaliyofanyika katika ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es salaam.


Kwenye Mahafali hayo Dkt Kikwete ametunuku Shahada na Stashahada kwa jumla ya wahitimu 2,452 ambapo 1,386 ama asilimia 56.6 ni wanawake. Picha na Issa Michuzi


Ends





 

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »