
Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Mwanza na Mwenyekiti wa Bodi ya Afya ya Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC) Renatus Nkwande,akizungumza wakati akifungua Mkutano Mkuu wa 88 wa Chama cha Madaktari Tanzania (TCMA) jijini Dodoma.
Na.Alex Sonna-DODOMA
KATIKA kuunga mkono jitihada za serikali kwenye sekta ya afya zaidi ya vituo 900 vya afya nchini ikiwemo hospitali 105, vituo vya afya 134 na zahanati 697 vinaendeshwa na makanisa, mchango unaokadiriwa kufikia asilimia 42 ya huduma za Afya nchini.
Hayo yameelezwa jijini Dodoma na Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Mwanza, Renatus Nkwande, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Bodi ya Afya ya Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC), wakati akifungua Mkutano Mkuu wa 88 wa Chama cha Madaktari Tanzania (TCMA).
Amesema kuwa Kanisa linasimamia hospitali 105, ambapo tatu kati yake ni Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Bugando (Mwanza), Kituo cha Tiba ya Rufaa ya Kanda ya KCMC (Moshi), na Hospitali ya Rufaa ya Kanda Arusha Lutheran Medical Centre (ALMC)—zinatoa huduma za rufaa ngazi ya kanda.
Aidha, hospitali 12 za rufaa za mikoa na hospitali 37 zilizoteuliwa za wilaya (Council Designated Hospitals – CDH) zinaendeshwa kwa makubaliano rasmi na mamlaka za serikali za mitaa.
“Bila shaka mchango huu ni mkubwa na unapaswa kutambuliwa rasmi katika sera ya taifa ya afya,” amesisitiza Askofu Mkuu Renatus Nkwande.
Hata hivyo ameitaka Serikali kuelekeza moja kwa moja mgao wa fedha za basket fund kwenye hospitali za Kanisa badala ya kupitisha fedha hizo kupitia akaunti za halmashauri, akibainisha kuwa ucheleweshaji umekuwa chanzo cha changamoto kubwa za uendeshaji.
“Pia kuna changamoto ya ucheleweshaji wa fedha za mfuko wa pamoja (Basket fund) kunakosababishwa na utaratibu wa serikali kuzipitisha kwenye akaunti ya halmshauri badala ya kuzipeleka moja kwa moja kwenye taasisi za afya za dini kama inavyofanywa kwenye vituo vya serikali.
“Tunaomba uongozi wa makanisa kupitia makatibu wakuu na makatibu wa afya wa majimbo na Dayosisi kwa kushirikiana na Christian Social Services Commission (CSSC) kufuatilia kwa karibu jambo hili kwenye wizara husika,”amesema Askofu Mkuu Nkwande
Aidha, ametoa wito wa kuwepo kwa mgawanyo wa haki wa rasilimali watu, akieleza kuwa hospitali nyingi zinazomilikiwa na taasisi za dini zimekosa wataalamu bingwa, hali inayosababisha kushuka kwa ubora wa huduma.
Kadhalika, alisema hospitlai nyingi za kanisa ni za muda mrefu na nyingine zina zaidi ya miaka 100 miundombinu na vifaa vingi vimechakaa na kupitwa na wakati,
Alisema hali hiyo inachangia huduma duni ambazo zinashindwa kuhimili soko la ushindani.
“Tunashauri kuwepo na mkakati thabiti wa kuzifanyia ukarabati hospitali na vituo vya kutolea huduma ikiwa ni pamoja na uboreshaji wa vifaa tiba ili kuongeza ufanisi na tija katika vituo vya kanisa na hivyo kuhimili ushindani wa soko,”amesema
Kwa upande wake Rais wa Chama cha Madaktari wa Kikristo Tanzania (TCMA) Dk. Gresmus Ssebuyoya amesema vituo vya afya vya makanisa nchini vinakabiliwa na changamoto mbalimbali, ikiwamo uhamishaji wa watumishi kutoka vituo vya kanisa kwenda serikalini bila kufuata utaratibu.
Amesema, hali hiyo inasababisha uhaba wa watumishi unaochangia kuzorota kwa huduma katika vituo husika.
“Kama tulivyotangulia kusema, hospitali na vituo vingi vya kanisa hufanya kazi na serikali kupitia mikataba na halmshauri husika. Pamoja na nia njema ya serikali ya kufanya kazi na taasisi kupitia mpango wa PPP, utekelezajia wa mikataba hii umekuwa na changamoto kadhaa ikiwemo baadhi ya halmshauri kusita kuendelea kusaini mikataba inapoisha hata kama vituo husika vinaendelea kutumia rasamimali za serikali na kutoa huduma kama awali,”amesema Dk. Ssebuyoya
Amesema, hali hiyo inasabaisha uwapo wa hoja za kiukaguzi kutoka Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi (CAG) zinazohitaji vituo vya kanisa kutoa ufafanuzi.
Aidha, alisema vituo vingi vya kutolea huduma za afya vya makanisa vipo vijijini sehemu ambazo ndiko waliko wananchi wengi na walio na uwezo mdogo wa kumudu hali ya maisha.
“Hadi mwishoni mwa mwaka jana, makanisa kwa pamoja yanaendesha vituo takriban 900 vya huduma za afya zikiwamo hospitali 105 ambapo hospitali tatu ni za rufaani ngazi ya kanda , ambazo ni Bugando Medical Center (BMC) ya Mwanza, Kilimanjaro Christian Medical Center (KCMC) ya Moshi na Arusha Lutheran Medical Center (ALMC) ya Arusha na hospili 12 zikiwa na huduma za rufaa ngazi ya mkoa,”alisisitiza
Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Mwanza na Mwenyekiti wa Bodi ya Afya ya Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC) Renatus Nkwande,akizungumza wakati akifungua Mkutano Mkuu wa 88 wa Chama cha Madaktari Tanzania (TCMA) jijini Dodoma.
Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Mwanza na Mwenyekiti wa Bodi ya Afya ya Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC) Renatus Nkwande,akizungumza wakati akifungua Mkutano Mkuu wa 88 wa Chama cha Madaktari Tanzania (TCMA) jijini Dodoma.
Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Mwanza na Mwenyekiti wa Bodi ya Afya ya Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC) Renatus Nkwande,akizungumza wakati akifungua Mkutano Mkuu wa 88 wa Chama cha Madaktari Tanzania (TCMA) jijini Dodoma.
Rais wa Chama cha Madaktari wa Kikristo Tanzania (TCMA) Dk. Gresmus Ssebuyoya,akizungumza wakati akifungua Mkutano Mkuu wa 88 wa Chama cha Madaktari Tanzania (TCMA) jijini Dodoma.
Sehemu ya washiriki wakimsikiliza Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Mwanza na Mwenyekiti wa Bodi ya Afya ya Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC) Renatus Nkwande (hayupo pichani) wakati akifungua Mkutano Mkuu wa 88 wa Chama cha Madaktari Tanzania (TCMA) jijini Dodoma.
Sehemu ya washiriki wakimsikiliza Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Mwanza na Mwenyekiti wa Bodi ya Afya ya Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC) Renatus Nkwande (hayupo pichani) wakati akifungua Mkutano Mkuu wa 88 wa Chama cha Madaktari Tanzania (TCMA) jijini Dodoma.
Sehemu ya washiriki wakimsikiliza Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Mwanza na Mwenyekiti wa Bodi ya Afya ya Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC) Renatus Nkwande (hayupo pichani) wakati akifungua Mkutano Mkuu wa 88 wa Chama cha Madaktari Tanzania (TCMA) jijini Dodoma.
Sehemu ya washiriki wakimsikiliza Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Mwanza na Mwenyekiti wa Bodi ya Afya ya Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC) Renatus Nkwande (hayupo pichani) wakati akifungua Mkutano Mkuu wa 88 wa Chama cha Madaktari Tanzania (TCMA) jijini Dodoma.









EmoticonEmoticon