Picha mbalimbali za matukio ya Mgombea mwenza wa Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Emmanuel John Nchimbi akiwahutubia Wananchi wa jimbo la Lupembe,waliohudhuria mkutano wake mdogo wa hadhara wa kampeni uliofanyika katika uwanja wa mpira wa Ilunda,Lupembe leo Jumatano Septemba 24, 2025 mkoani Njombe.
Pamoja na mambo mengine Dkt. Nchimbi alimnadi Mgombea Ubunge wa jimbo la Lupembe,Ndugu Edwin Enosy Swallel SWALLEL pamoja na Madiwani wa jimbo hilo.
Dkt Nchimbi anaendelea na mikutano yake ya kampeni nchi nzima, kusaka kura za ushindi wa kishindo wa Chama Cha Mapinduzi (CCM),ambapo mpaka sasa amefika mikoa 13.
EmoticonEmoticon