DKT.NCHIMBI AOMBA KURA ZA KISHINDO ZA CCM,AAHIDI NEEMA KWA WANA NJOMBE

September 23, 2025

MGOMBEA mwenza wa Urais kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Emmanuel  John Nchimbi amewahutubia Wananchi  wa Mjini Njombe,waliohudhuria mkutano wake wa hadhara wa kampeni huku akiwaomba ifikapo Oktoba 29 mwaka huu wakipigie kura Chama hicho ili kishinde kwa kishindo.




Dk.Nchimbi ameyasema hayo leo Septemba 23,2025 alipokuwa katika uwanja wa Stendi ya zamani, mkoani Njombe ambapo ametumia nafasi hiyo kutoa ahadi kwa wananchi wa Njombe  endapo wataichaguwa CCM basi Ilani ya chama chake imepanga kufanya mipango mingi ya maendeleo mkoani humo.

Maendeleo hayo ni katika maeneo mbalimbali yakiwemo katika sekta ya afya, elimu, kilimo, maji  pamoja na kuinua biashara mbalimbali.

Pia Dkt.Nchimbi alitumia nafasi hiyo ya kumnadi Mgombea Ubunge wa jimbo la Jombe Mjini,Ndugu Deodatus Philip Mwanyika pamoja na Madiwani wa jimbo hilo.

Dkt Nchimbi anaendelea na mikutano yake ya kampeni nchi nzima, kusaka kura za ushindi wa kishindo wa Chama Cha Mapinduzi (CCM),ambapo mpaka sasa amefika mikoa  13.















Share this

Related Posts

Latest
Previous
Next Post »