HII SI AKAUNTI YA RAIS KARIA

October 31, 2017
Kuna Akaunti mpya wa Twitter inazunguka katika mitandao ya kijamii.
Akaunti hiyo yenye jina la Rais wa Shirikisho l Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), imeanza kutoa taarifa mbalimbali na kuchangia maoni kunakoelezwa kufanywa na Wallace Karia.
TFF tunatangaza kuwa hatuitambui akaunti hiyo. Rais Karia hajafungua akaunti ya Twitter.
Tunaomba wananchi wote hususani wanafamilia wa mpira wa miguu, kutoitambua akaunti hiyo kwa sababu si ridhaa ya Rais Karia wala Kitengo cha Habari TFF kilichofungua akaunti hiyo.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »