MINZIRO NGUVU ZOTE SASA KWA AZAM FC.

April 15, 2014
NA SAFARI CHUWA, TANGA.
 KOCHA MKUU wa timu ya JKT Ruvu, Fred Minziro amesema ushindi walioupata wa bao 1-0 dhidi ya wapinzani wao Coastal Union umetokana na mabadiliko makubwa aliyoyafanya kwenye kikosi hicho baada ya kumalizika mechi yao na Yanga.

Minziro aliyasema hayo jana mara baada ya kumalizika kwa mchezo huo ambao ulichezwa kwenye dimba la CCM Mkwakwani kwa kueleza siri hiyo imechangiwa kwa asilimia kubwa na mabadiliko hayo.

Alisema licha ya kupata ushindi huo bado wanakwenda kujipanga kuhakikisha wanacheza vizuri mechi yao inayofuata dhidi ya Azam FC lengo likiwa kupata ushindi ili waweze kusogea katika nafasi za juu kwenye msimamo wa ligi hiyo.

   “Tunajua tunakwenda kucheza na Azam FC hii ni timu nzuri wala sio ya kubeza hivyo nasi tutahakikisha tunajipanga vilivyo ili kuweza kupata matokeo mazuri kwani hilo ndio lengo letu kwa kila mchezo uliopo mbele yetu “Alisema Minziro.

Aidha kocha huyo alisema matokeo hayo waliyoyapata yamewapa nguvu ya kwenda kujipanga wakiamini watafanya vizuri kwenye mechi zao zilizobakia ikiwemo wa Azam FC.

Aliongeza kuwa licha ya Azam watakuwa kwenye uwanja wao wa nyumbani lakini wao watahakikisha wanafanya kazi kubwa ya kucheza kwa umakini mkubwa ili kupata matokeo ya aina yoyote yale ili kupata pointi.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »