JESHI LA POLISI NCHINI RWANDA LAWATIA MBARONI WATATU WANAOTISHIA USALAMA WA NCHI HIYO.

April 15, 2014
NA MWANDISHI WETU,KIGALI.
 Jeshi la Polisi nchini Rwanda limewakamata watu watatu wanaotuhumiwa kutishia usalama wa taifa. 

Miongoni mwa waliokamatwa ni mtangazaji wa redio, ambaye awali aliripoti kuhusu kutoweka kwake pamoja na mwanamuziki aliye  mwanaharakati wa amani.


Katika taarifa yake leo, jeshi hilo limesema watuhumiwa hao wana uhusiano na chama cha upinzani cha Rwanda National Congress-RNC, chenye mafungamano na Patrick Karegeya afisa wa zamani wa ujasusi wa Rwanda aliyeuawa nchini Afrika Kusini mwanzoni mwa mwaka huu.


Watu hao pia wanatuhumiwa mara nyingine kufanya kazi na kundi la waasi la FDLR, linalojumuisha maafisa waliohusika na mauaji ya kimbari ya mwaka 1994 ambao wako kwenye misitu ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo.


Taarifa hiyo imeeleza kuwa Cassien Ntamuhanga, mtangazaji wa Redio Amazing Grace amekamatwa leo, mwanamuziki Kizito Mihigo alikamatwa Ijumaa iliyopita na askari aliyefukuzwa jeshini Jean Paul Dukuzumuremyi alikamatwa mwishoni mwa wiki iliyopita.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »