JOHN MNYIKA AMLILIA GURUMO

April 15, 2014


Mbunge wa Ubungo na Mkurugenzi wa Mawasiliano wa chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), John Mnyika amuelezea Gwiji la muziki wa Dans nchini, "Baba ya Muziki", Muhidin Maalim Gurumo aliyefariki dunia juzi kama "Mbuyu" uliodondoka katika tasnia hiyo.
 
Mnyika amesema amepokea kwa masikitiko makubwa kifo cha Mwanamuziki huyo mkongwe ambaye alifariki duni juzi baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Alisema, amekwishawasiliana na Shirikisho la Wasanii kwa ajili ya kuwasilisha rambirambi zake na kutoa pole kwa Chama cha Muziki wa Dansi Tanzania (Chamudata), kwa kupoteza mshauri na mkuu wake wa Idara ya Fedha.
 
“Aidha natoa wito kwa wananchi wa Ubungo na Jiji la Dar es Salaam kwa ujumla, kushiriki katika kumuaga kesho (leo), nyumbani kwake Mabibo External katika Kata ya Makuburi kabla ya kwenda kuzikwa kwao Kisarawe Kijiji cha Masaki. Kwa kuwa niko katika Bunge la Katiba, nitawakilishwa katika kutoa heshima za mwisho na Diwani wa Kata ya Makuburi alipoishi marehemu,” alisema Mnyika na kuongeza. 
 
Nichukue fursa hii kutoa pole kwa mashabiki wenzangu wa nyimbo zake kuanzia akiwa Kilimanjaro, Chacha, Rufiji Jazz, Kilwa Jazz, Sikinde na Msondo Ngoma kuanzia wakati wa Nuta, Juwata mpaka Ottu".

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »